Title August 2023

Fahamu maana ya Zaburi 125:3 “ Kwa maana fimbo ya udhalimu Haitakaa juu ya fungu la wenye haki.

SWALI: Nini maana ya Zaburi 125:3 “ Kwa maana fimbo ya udhalimu Haitakaa juu ya fungu la wenye haki; Wenye haki wasije wakainyosha Mikono yao kwenye upotovu”.


JIBU: Mstari huo unatuonyesha jinsi Mungu anavyowatenga watu wake na adhabu ambazo zinawahusu waovu. Kwamba kamwe fimbo ya adhabu haiwezi kuwahusu watu wa Mungu, Ndio maana ya hilo neno ‘Kwa maana fimbo ya udhalimu Haitakaa juu ya fungu la wenye haki;.. Ni mfano tu wa wana wa Israeli wakati ule walipokuwa Misri, Mungu aliwatenga na wamisri na kuwaweka kule Gosheni, na mpigo yote yalipokuja hayakuwakuta wana wa Israeli, bali wamisri tu. Hata baadaye alipotaka kuliadhibu taifa zima, bado aliwaficha  watu wake ndani ya nyumba, na Yule malaika aliyeshushwa kuwauwa watu, hakupita katika nyumba zao. Kuonyesha kuwa fimbo za makosa Mungu hana desturi ya kuzijumuisha na watu wake, isipokuwa tu wamekataa wenyewe. Ndivyo ilivyokuwa kwa Nuhu, na Lutu.

Na anafanya hivyo kwasababu gani? Ndio hapo anasema ili “Wenye haki wasije wakainyosha Mikono yao kwenye upotovu”. Kwamba anawataadharisha watu wake wasidiriki kufanya makosa kama hayo hayo ya waovu kwasababu na wenyewe adhabu inaweza kuwakuta vilevile. Na kweli ndivyo ilivyokuwa kwa wana wa Israeli baadaye, walimwacha Mungu wakaanza kuitumikia miungu, na matokeo yake Mungu akawarudisha tena utumwani, na miji yao kubomolewa.

Hivyo, ni kutuonya kuwa sisi tuliokoka, kamwe tusijichanganye na maovu kwasababu adhabu ya makosa yaweza kutupata na sisi pia, kwasababu Mungu hatazami uso wa mwanadamu, bali ulekevu wako kwake.

Shalom.

Kwa maana nyingine ya mistari mbalimbali ya biblia tembelea website yetu hii >>> www.wingulamashahidi.org.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Kulabu ni nini katika biblia?(2Wafalme 19:27)

Miimo ni nini na kizingiti ni nini?

Tirshatha ni nini? (Ezra 2:63)

Naye atawachunga kwa fimbo ya chuma.

TUNAHESABIWA HAKI BURE KWA NJIA YA IMANI.

Je Bwana Yesu aliruhusu wanafunzi wake kubeba Fimbo au hakuwaruhusu? (Marko 6:8 na Mathayo 10:10).

Tofauti kati ya zaka na sadaka ni ipi?

UTARATIBU WA KUTOA FUNGU LA 10 UPOJE?.

Rudi nyumbani

Print this post

DHABIHU ZA ROHO NI ZIPI? (1Petro 2:5)

SWALI: Dhabibu za roho ni zipi, zinazotajwa kwenye maandiko haya?

1Petro 2:5  “Ninyi nanyi, kama mawe yaliyo hai, mmejengwa mwe nyumba ya Roho, ukuhani mtakatifu, mtoe dhabihu za roho, zinazokubaliwa na Mungu, kwa njia ya Yesu Kristo”.

Dhabihu ni sadaka za kuteketezwa zilizokuwa zinatolewa katika agano la kale. Hizi zilikuwa na lengo la kufanya upatanisho wa makosa ya watu, kwamfano  alipochinjwa mwanakondoo, au ng’ombe au mbuzi, au njiwa (Walawi 1:3-16) na kuteketezwa kisha ule moshi wake ukapanda juu basi huo ndio unakuwa  uthibitisho wa sadaka yake kukubaliwa. Na mtu huyo makosa yake yanakuwa yamefunikwa kwa muda.

Hivyo katika agano jipya pia tunayo dhabihu yetu, ambayo kwa kupitia hiyo tunapokea upatanisho wa makosa yetu, na dhabihu yenyewe ni YESU KRISTO mwokozi wetu ambaye yeye kama mwanakondoo alichinjwa kwa ajili yetu ili sisi tupokee ondoleo la dhambi, hivyo yoyote ambaye yupo sasa ndani ya Kristo Yesu tayari ameshamtolea Mungu dhabihu ya upatanisho wake.

Lakini tunapokuwa ndani ya Kristo, hatuna budi kuonyesha kuwa tumekombolewa na yeye, kwa matendo yetu. Hivyo ni lazima tutaonyesha tabia kama za mtu anayekwenda kutoa dhabihu mbele za Bwana, na sio kama za mtu aliyejiamulia tu. Na tabia zenyewe ndio hizo zinazojulikana  kama dhabihu za roho ambazo sisi tunazitoa.

Zifuatazo ndio dhabihu za roho  zenyewe.

1) Shukrani

Zaburi 50:14 Mtolee Mungu dhabihu za kushukuru; Mtimizie Aliye juu nadhiri zako.

Zaburi 50:23 Atoaye dhabihu za kushukuru, Ndiye anayenitukuza. Naye autengenezaye mwenendo wake, Nitamwonyesha wokovu wa Mungu.

Ukiwa mtu wa shukrani kwa Mungu, Ni kuonyesha kuwa umetambua kazi ya msalaba ndani yako. Na shukrani hizi ni lazima ziwe katika Sifa za kinywa chako, pamoja na matoleo kwa kile Mungu anachokubariki. Ni muhimu sana wewe kama mkristo kuwa mtu na namna hii. Wote waliokwenda kutoa sadaka za namna hii mioyo yao ilijaa shukrani kwa Mungu wao, hawakwenda hivi hivi tu.

2) Moyo uliopondeka

Zaburi 51:16 Maana hupendezwi na dhabihu, au ningeitoa, Wewe huridhii sadaka ya kuteketezwa.  17 Dhabihu za Mungu ni roho iliyovunjika; Moyo uliovunjika na kupondeka, Ee Mungu, hutaudharau.

Moyo uliopondeka ni moyo wa toba, wa majuto ya dhambi, ambao unakufanya utaabike moyoni mwako kwasababu ya makosa yaliyotendeka, na hivyo unakufanya uwe mnyenyekevu sana mbele za Mungu.

Mtu mwenye moyo huu, mbele za Mungu anaonekana kama amejitambua yeye ni mkosaji, na hivyo Yesu amefanyika upatanisho kwa ajili yake, tofauti na mtu ambaye mambo yote kwake ni sawa, hata baada ya kuona kosa bado anaukaza moyo wake, kujifanya kama hana hatia yoyote mbele za Mungu. Yatupasa wakati wote tuwe watu wa kujinyenyekeza mbele za Mungu. Watu wa kutaka rehema zake.

3) Kuitoa miili yetu;

Warumi 12:1  “Basi, ndugu zangu, nawasihi, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, ya kumpendeza Mungu, ndiyo ibada yenu yenye maana. 2  Wala msiifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu.

Unapoutunza mwili wako mbali na mambo ya kidunia, kisha ukaufanya utumike kwa ajili ya kazi ya Mungu, hapo ni sawa na unamtolea Mungu dhabihu yenye kupendeza, yaani unaenda mbele za Mungu na badiliko, unasema msalaba mbele, udunia nyuma. Lakini ukiwa unavaa ovyo ovyo, unazini, unatumia mikorogo, unajichora mwili wako, unakunywa pombe, unavuta sigara, unatoa mimba, hapo hufanyi ibada yoyote mbele za Mungu. Kwasababu lazima ufahamu kuwa miili yetu ni hekalu la Roho Mtakatifu (1Wakorintho 3:16).

Hivyo, wewe ambaye umeokoka, zangatia mambo hayo matatu, SHUKRANI, MOYO ULIOPONDEKA, NA KUUTOA MWILI WAKO. Wokovu wako utakuwa na maana sana mbele za Mungu.

Bwana akubariki.

Je! Umeshaokoka?. Kama bado wasubiri nini? Unatambua kuwa haya ni majira ya siku za mwisho, na Kristo amekaribia kurudi?.  Dalili zote zimeshatimia, Embu tubu sasa mgeukie Kristo akuokoe uwe upande salama. Ikiwa upo tayari kufanya hivyo, basi waweza fungua hapa kwa ajili ya mwongozo was ala hiyo.>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Dhabihu ni nini?

KUTII NI BORA KULIKO DHABIHU.

Mahali pa juu palikuwa ni wapi kama tunavyosoma katika biblia?

Swali: Kurushwa upesi kunakozungumziwa katika Danieli 9:21 ndio kupi?

Mnanaa, Bizari na Jira ni viungo gani? (Mathayo 23:23)

Sadaka ya Moyo ipoje? (Walawi 22:21).

Kwanini samaki wasio na mapezi na magamba hawakuruhusiwa kuliwa?

Rudi nyumbani

Print this post

NIFANYE NINI ILI NISILALE NINAPOSOMA BIBLIA.

Mara nyingi tunapojikuta tumelala tunaposoma biblia, huwa moja kwa moja tunamsingizia shetani. Lakini ukweli ni kwamba shetani anahusika kwa sehemu ndogo, sehemu kubwa ni hali zetu za kimwili ndio zinakuwa adui katika jambo hili. Mazingira ambayo ni mashambulizi kutoka kwa adui mfano wake yanakuwa ni  kama haya; pengine mtu akianza tu kusoma biblia anasikia maumivu makali kwenye kichwa, au mwili, lakini akiacha tu kusoma hali yake inarudia kama kawaida, au anaona giza au vitu kama mianga mianga kwenye macho na hivyo inamfanya asiweze kuisoma biblia, au kila anapotaka kusoma anapoteza hapo hapo kumbukumbu zote kwamba alikuwa anasoma biblia, na hatimaye anajikuta yupo usingizini, au anafanya mambo mengine kabisa, hiyo ndio mfano ya mashambulizi.. Na inahitaji kuombewa, au kushindana na hiyo roho hadi ikutoke.

Lakini ukijiona unaposoma biblia usingizi mzito umekukamata, unasinzia sinzia, unapiga piga miayo, huyo sio adui huo ni mwili wako, usiopenda mambo ya rohoni. Hivyo ni lazima uushinde huo.

Wagalatia 5:17  “Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka”

Hivyo hizi ni njia ambazo zitakusaidia usilale pale unaposoma biblia.

1) Omba kabla ya kusoma biblia

Usipende kufungua biblia kama kitabu cha riwaya, unasoma tu utakavyo. Kumbuka yale ni maneno ya ROHO, na hivyo inahitaji umkaribishe Roho akusaidie. Hivyo  usiwe mvivu wa kuomba, pata dakika, kadhaa za kufanya hivyo. Ni jambo ambalo nimejifunza sana, wakati nasoma biblia bila kuomba, na pale ninapoomba kisha nikaisoma, kuna tofauti kubwa sana ya kiuelewa na kiutulivu. Maombi pia yanasaidia kama kuna mashambulizi yoyote, basi yanatowekea hapo.

2) Pata muda wa kupumzika.

Ikiwa umechoka sana, si lazima usome biblia muda huo huo. Pendelea kuruhusu mwili wako upumzike vizuri, kwamfano umetoka kazini, umeshughulika kutwa nzima, ni rahisi sana kukabwa na usingizi muda huo huo usomapo biblia peke yako. Hivyo tumia busara, wahi kulala, kisha amka usiku. Ukilala hata masaa 3, mwili unapokea taarifa kuwa huyu mtu tayari alishapumzika. Hivyo ukiamka ukajimwagia maji, ukaketi utajiona unafuu mkubwa, na utapata kitu kikubwa kuliko kulizimisha mwili wakati umechoka.

3) Usipende kusomea biblia kitandani:

Tafuta meza ukae, mwili wako uwe kama mtu aliye darasani, sio kama aliye hospitalini mgonjwa unasubiriwa kuhudumiwa. Kaa kwenye meza, kisha ndio usome biblia yako

Luka 12:35  Viuno vyenu na viwe vimefungwa, na taa zenu ziwe zinawaka

4) Kuwa na daftari na kalamu.

Kusoma kwa kuandika na kwa sauti, huwa kuna matokeo makubwa kuliko, kutumia tu macho yako. Hivyo andiko vifungu unavyovisoma, na ufunuo unaopata, itakuongezea umakini katika usomaji wako, na hivyo Roho Mtakatifu atapata nafasi ya kukufindisha kwa urahisi zaidi.

5) Soma na wengine.

Ukiona huwezi kujiwekea ustaarabu wa kuzingatia ratiba yako ya usomaji, pendelea kujifunza na wengine. Kaa na familia yako, au ndugu zako, au rafiki yako katika Bwana jiwekeeni ratiba ya usomaji wa biblia pamoja, kisha mnachambua kile mlichojifunza, kwa namna hiyo itakusaidia sana kuielewa ..

Mathayo 18:20  “Kwa kuwa walipo wawili watatu wamekusanyika kwa jina langu, nami nipo papo hapo katikati yao”

 6) Soma kwa vituo.

Kusoma biblia sio mashindano kwamba ni lazima uimalize yote kwa siku moja, soma vifungu kadhaa, kisha tumia muda mwingi, kuvitafakari hivyo vilimaanisha nini. Roho Mtakatifu anapenda kutufundisha taratibu sana, hataki tuvuke madarasa ya juu wakati ya chini bado hatujayamaliza. Hivyo zingatia kusoma kwa muktadha wa kuelemishwa na Roho Mtakatifu, sio kumaliza silabasi. Kusoma vifungu vitano kwa dakika mbili, kisha ukavifakari kwa masaa 2, ni bora kuliko kusoma vifungu elfu kwa saa2, halafu hakuna tafakari yoyote.

7) Mifungo

Mfungo ni jambo zuri ambalo huupa mwili wepesi, kwasababu mwili unapotaabika kwa kunyimwa haja zake kwa kawaida roho yako huwa inakuja juu. Hivyo ukiwa katika kipindi cha mfungo, utaona wepesi Fulani wa kuisoma biblia kwa masafa marefu kidogo, kuliko kipindi kingine. Fungu mara kwa mara, au ukiwa unatamani wiki hiyo kuitumia vizuri usiku katika kusoma Biblia, basi hakikisha wiki hiyo yote unafunga, utajiona mwepesi sana hususani wakati wa usiku unapotulia.

8) Mshirikishe mkufunzi wako

Si kila jambo utaweza kulitatua tu peke yako mengine, utahitaji msaada, hivyo hakikisha maendeleo yako ya kiusomaji, kiongozi wako anayafahamu, hatua zako unamshirikisha mchungaji wako, itakusaidia sana, kupata ushauri au maombi , au ushuhuda kwa yale ambayo pengine usingeyafahamu uwapo peke yako. Na hiyo itakupa hamasa zaidi na shauku ya kusoma.

Bwana akubariki.

Hakikisha unasoma BIBLIA kila siku.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Jinsi ya kuandaa Somo la kufundisha

JINSI YA KUSOMA BIBLIA.

Tirshatha ni nini? (Ezra 2:63)

HEKIMA YA KIMUNGU, INAINGIAJE MIOYONI MWETU?

UFUNUO NI NINI, NA NITAPOKEAJE UFUNUO KUTOKA KWA MUNGU?

Biblia inamaana gani inaposema tutoapo unabii tutoe kwa kadiri ya imani?

Rudi nyumbani

Print this post

JINSI YA KUSIMAMA NA KUFUNDISHA/ KUHUBIRI

Ni kanuni gani ya kuzingatia wakati wa kuhubiri/kufundisha ili usimzimishe Roho?.

Kuna vita vikubwa sana vya kiroho vinavyoinuka muda mchache kabla ya kusimama kufundisha/kuhubiri ambavyo ni lazima mkristo avijue na ajue jinsi ya kuvishinda ili injili ya Bwana isizuilike.

Baada ya kuandaa somo kwa kuongozwa na Roho Mtakatifu, hatua inayofuata ni wewe kwenda kuwasilisha ujumbe ulioupokea mbele ya mtu au watu. Sasa ni muhimu kujua kanuni za kuwasilisha ujumbe ili usije ukamzimisha Roho, kwasababu Roho Mtakatifu pia anaweza kuzimishwa ndani ya mtu na mtu mwenyewe, na shetani ndicho anachokitafuta hicho, lengo lake Injili isiwafikie wengine.

(Kumbuka shetani mwenyewe hawezi kumzimisha Roho Mtakatifu, kwasababu Roho Mtakatifu ana nguvu kuliko yeye), anachokifanya shetani ni kuzikoroga hisia za mtu ili zisiruhusu Roho Mtakatifu kufanya kazi ndani yake. Na neno linatuambia kuwa “tusimzimishe Roho”

1Wathesalonike 5:19  “Msimzimishe Roho”.

Wengi huwa wanamzimisha Roho Mtakatifu wakati wa kusimama kufundisha/kuhubiri pasipo wao kujijua..unakuta wakati wanaandaa somo/mahubiri wanakuwa katika uwepo mkubwa sana lakini wakati wa kufundisha au kuhubiri ule uwepo au ile hali ya kutiririka inapotea, na hivyo kumfanya huyu mtu ajihisi Mungu hayupo naye au kamwacha.

Kiuhalisia huyu mtu hajaachwa na Roho Mtakatifu, isipokuwa hali yake ya ndani imezuia utendaji kazi wa Roho Mtakatifu.

Sasa yafuatayo ni mambo ya kuzingatia ili Roho asizime ndani yako, (kule kutiririka kusikome), na ule ujumbe wa Roho Mtakatifu ulioupokea ufike kwa walengwa kama Roho alivyokufunulia.

1.Usijipange kwa maneno mengi.

Epuka kujipanga kwa maneno mengi;  Maneno mengi yanazuia kutiririka kwa Roho Mtakatifu, wengi wanadhani kuwa na maneno mengi ndiko kueleweka, pasipo kujua kuwa anayewagusa watu na kuwafanya waelewe ni Roho Mtakatifu, hivyo ukifuata kanuni ya Roho Mtakatifu utaeleweka tu na utakuwa na matunda.

Unapojiandaa kwa maneno mengi, utajikuta unategemea yale maneno yako, na hivyo wakati Roho Mtakatifu anataka kuingiza mada nyingine katika akili yako wakati wa kufundisha ule ukuta wa maneno uliojiwekea unazuia kinywa cha Roho Mtakatifu kifanye kazi, na hivyo utajikuta unafundisha kwa akili zako, na yale maneno uliyoyaandaa yanapokwisha unajikuta na wewe umekauka, huna cha kusema Zaidi.

Kwahiyo jiandae kwa maneno machache tu!, hata kama unaona somo litakuwa ni fupi sana, Roho Mtakatifu ndio anataka iwe hivyo, ili hayo maneno mengine ayajazie yeye, ukiweka desturi hiyo siku zote utaona muda hautoshi, utaona daftari lako lina maneno machache uliyoyaandaa, lakini muda uliofundisha ni madakika mengi au masaa mengi, ukiona hiyo hali imekutokea jua sio wewe uliyekuwa unafundisha bali ni Roho Mtakatifu ndani yako.

2. Usifikiri fikiri.

Kufikikri fikiri ni nini utaenda kusema au kuhubiri, kunazima kinywa cha Roho Mtakatifu. Unapofika wakati wa kwenda kufundisha wengi huwa wanapaniki na kuwaza mara nyingi nyingi ni nini wataenda kusema, na hivyo kujikuta kulazimisha kupanga maneno ya kuzungumza kuanzia mwanzo hadi mwisho. Ukiona hiyo hali inakujua ndani yako dakika chache kabla ya kusimama kufundisha au kuhubiri ikatae!. Kwani ni adui anataka kutumia fikra zako kumzimisha Roho ndani yako.

Siku zote usijiangalie hali uliyonayo kifikra wakati wa kwenda kufundisha, hata kama hukumbuki chochote, wewe tulia mpaka wakati utakapofika wa kusimama, funga fikra zako kufikiri ni nini utaenda kufundisha au kuhubiri, ukiona mawazo hayo yanakujia hamisha fikra zako kwa kutafakari mambo mengine ya kiMungu au soma Neno, kwasababu wakati huo ndio wakati wa vita vikali, shetani anatumia nguvu kubwa sana kumshambulia mtu katika hii hatua.

Hivyo funga fikra zako na subiri ule wakati wa kufundisha Roho Mtakatifu atakupa cha kusema wakati ule ule utakaposimama kufundisha.

Kanuni kama hii Bwana Yesu aliwafundisha wanafunzi wake wakati wakipelekwa mbele ya watu wa Mataifa, akawaambia wasifikiri fikiri watakavyojibu kwani watapewa kinywa saa ile ile watakaposimamishwa.

Mathayo 10:19 “ Lakini hapo watakapowapeleka, msifikiri-fikiri jinsi mtakavyosema; maana mtapewa saa ile mtakayosema

20  Kwa kuwa si ninyi msemao, bali ni Roho wa Baba yenu asemaye ndani yenu”.

Kwahiyo na wewe usiwe mtu wa kufikiri fikiri utakavyosema, subiri ule muda utakapofika utapewa kinywa cha kusema, ambacho hata wewe mwenyewe utajishangaa.

3. Usijiangalie udhaifu wako na Jiachilie

Usijipime kwa kujiangalia udhaifu wako, kama unajua kuhubiri au la!, kama una kigugumizi au la!, kama una uzoefu au la!..Kwani kinywa chochote kilichovuviwa na Roho Mtakatifu kina nguvu kwasababu kimebeba ujumbe wa Roho Mtakatifu.

Hivyo kabla ya kwenda kufundisha weka kando udhaifu wako, weka kando kumbukumbu za nyuma ambazo unahisi uliwahi kukosea, weka kando hisia kwamba husikilizwi au hueleweki, au unapotezea watu muda.

Zungumza kile kinachokuja kinywani mwako muda ule kwa ujasiri wote, (achilia moyo wako na fikra zako), wala usijilinganishe na yeyote wala usitafute kufundisha kama mtu Fulani unayemjua, hapo utaona Roho Mtakatifua atakavyokutumia na utakavyomhisi akitenda kazi ndani yako kwa viwango vingine.

4. Usiongozwe na  muda.

Ukiona hofu ya kuwahi kumaliza inaingia ndani yako, ikatae hiyo hali!.. Kwasababu ni mbinu nyingine ya shetani kumzimisha Roho Mtakatifu ndani yako (Kumbuka tena shetani mwenyewe hawezi kumzimisha Roho Mtakatifu, kwasababu Roho Mtakatifu ana nguvu kuliko yeye), anachokifanya shetani ni kuzikoroga hisia zako ili zisiruhusu Roho Mtakatifu kufanya kazi ndani yako.

Kwahiyo  hofu ya muda ikatae. Kama umepewa lisaa la kufundisha, usianze kuwaza utasema nini kwenye hilo lisaa lote (hiyo sio kazi yako) ni kazi ya Roho Mtakatifu, ukianza kuwaza utasema nini muda wote huo wakati utakapofika hofu iliyopo ndani yako itamzuia Roho Mtakatifu kusema kupitia wewe. Wewe anza kufundisha kana kwamba utamaliza dakika tano zijazo, na utaona Roho Mtakatifu atakachokifanya!.. Kama atapenda umalize ujumbe kwa dakika hizo hizo tano, wala usiogope!, ndivyo alivyotaka yeye, na kama atakusudia ufundishe kwa kwa lisaa au masaa mawili, atakupa maneno na utashangaa yametoka wapi.. Kwahiyo ondoa hofu ya muda!.

5. Wahusishe watu katika kufundisha kwako

Hii ni njia nyingine ya kuendeleza uwepo uwepo wa Roho Mtakatifu usikatike ndani yako, tumia muda kuwauliza maswali unaowafundisha kama unaweza kufanya hivyo, au kuwapa jukumu la kusoma mistari ya biblia n.k

Hizi ni baadhi ya njia chache utakazoweza kuzitumia ili Kile Roho Mtakatifu alichokufunulia kiweze kuwafikia walengwa.

Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba kabla ya kwenda kusimama kufundisha ZILINDE SANA FIKRA ZAKO!.. Kwasababu hizo ndizo shetani anashughulika nazo kuharibu mambo.

Bwana akubariki.

Ikiwa hukupata somo la “Jinsi ya kuandaa somo basi wasiliana nasi kwa njia ya inbox”

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Jinsi ya kuandaa Somo la kufundisha

Wanikolai ni watu gani? Katika biblia?

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

Roho Mtakatifu ni nani?.

MASOMO MAALUMU KWA WANAWAKE.

Rudi nyumbani

Print this post

Tirshatha ni nini? (Ezra 2:63)

Neno hili utalipata katika vifungu hivi kwenye biblia.

Ezra 2:63 Na huyo Tirshatha akawaambia wasile katika vitu vitakatifu sana ,hata atakaposimama kuhani mwenye urimu na Thumimu.

Nehemia 8:9 Naye Nehemia, ndiye aliyekuwa Tirshatha, na Ezra kuhani, mwandishi, na Walawi waliowafundisha watu, wakawaambia watu wote, Siku hii ni takatifu kwa Bwana, Mungu wenu; msiomboleze wala msilie. Maana watu wote walilia, walipoyasikia maneno ya torati

Nehemia 10: 1 Basi hawa ndio waliotia muhuri; Nehemia, ndiye Tirshatha, mwana wa Hakalia, na Sedekia;

Soma pia Nehemia 7:65

Tirshatha ni neno la kiajemi, ambalo linamaanisha mtawala aliyeteuliwa kuongoza uyahudi chini ya ufalme wa uajemi. Kwa jina lingine ni gavana/ liwali, Katika vifungu hivyo vinamwonyesha Nehemia alikuwa kama Tirshatha/Mtawala. Soma pia (Nehemia 5:18).

Lakini pia Zerubabeli, alipewa nafasi hii kama tunavyosoma hapo kwenye Ezra 2:63, Hivyo wote hawa walisimama kama wakuu wa majimbo hayo wayaangalie, na kusimamia kazi zote walizoagizwa na mfalme.

Bwana akubariki.

Tazama pia maana ya maneno mengine ya kibiblia chini.

Je! Umeokoka? Je, unatambua kuwa Kristo anakaribia kurudi? Umejiandaaje? Tubu dhambi zako ukabatizwe upokee Roho Mtakatifu uwe salama zizini mwa Bwana. Muda ni mfupi sana tuliobakiwa nao, huu si wakati wa kubembelezewa wokovu, ni wewe mwenyewe kuona na kugeuka upesi. Ikiwa upo tayari kuyakabidhi maisha yako kwa Bwana basi fungua hapa ili upate mwongozo wa sala ya toba >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Maana Ya Maneno Katika Biblia.

Ayari ni nini kama tunavyosoma katika biblia?

Jabari ni nini, kama linavyotumika kwenye biblia?

Kisima cha joka na lango la jaa ni nini?(Nehemia 2:13)

HAPAKUWA NA NAFASI YA KUPITA KWA YULE MNYAMA ALIYEKUWA CHINI YANGU.

NI MAONO YAPI HAYO UNAYOSUBIRIA?

FUMBO ZA SHETANI.

Rudi nyumbani

Print this post

Je! Wamwona mtu mwenye bidii katika kazi zake?

SWALI: Nini maana ya Neno hili; Mithali 22:29 “Je! Wamwona mtu mwenye bidii katika kazi zake? Huyo atasimama mbele ya wafalme; Hatasimama mbele ya watu wasio na cheo”.


JIBU: Neno la Mungu linatuonyesha kuwa ‘bidii’ humkweza mtu. Na bidii inayozungumziwa kibiblia ni zaidi ile inayodhaniwa kufanya tu kazi sana kwa muda mrefu, hapana, bali ni pamoja na kutumia ujuzi wako wote na ufanisi ili kutimiza kusudi ulilowekewa ndani ya muda. Watu wa namna hii mara nyingi huwa wanateka macho ya  watu wenye vyeo au wakuu wa nchi.

Kwamfano Wafanyakazi wanaoonyesha ufanisi katika utendaji kazi, na kutimiza malengo ya shirika lao ndani ya wakati waliowekewa, huwa wanapendwa na ma-boss wao, na mara nyingi hupandishwa vyeo kama sio kupewa zawadi. Wagunduzi wa mipango ambayo inaleta mabadiliko chanya kwenye jamii, huwa wanaalikwa na viongozi wakubwa na maraisi kupongezwa na wakati mwingine kufanywa washauri wao.

Vivyo hivyo kiroho pia, ili tupate kibali kwa aliye Mfalme wa wafalme, na Bwana wa mabwana, zaidi ya wakuu wote duniani (yaani YESU KRISTO), hatuna budi kuwa na bidii katika kumtumikia yeye, na kuyafanya mapenzi yake.

Anasema,..

Kumbukumbu 28:1 Itakuwa utakaposikia sauti ya Bwana, Mungu wako, KWA BIDII, kutunza kuyafanya maagizo yake yote nikuagizayo leo, ndipo Bwana, Mungu wako, atakapokutukuza juu ya mataifa yote ya duniani; 

Umeona? Tusipokuwa walegevu, Bwana atatunyanyua juu sana tena sana kwasababu ni ahadi yake na haiwezi kutanguka..

Warumi 12:11  ‘kwa bidii, si walegevu; mkiwa na juhudi katika roho zenu; mkimtumikia Bwana;’

Hivyo, hakikisha, kile  ulichopewa na Bwana unakitendea kazi, zaidi sana angalia ni kwa namna gani utakiweka ili kilete matokeo mazuri katika ufalme wa Bwana, usikifanye bila maarifa, hakikisha unatumia vyote yaani; nguvu zake zote, akili zako zote, roho yako yote, na moyo wako wote kwa pamoja bila kusahau kimoja wapo, ndani ya muda huu mchache uliopewa na Mungu hapa duniani. Na hakika kitakapochipuka kama Bwana alivyokusudia, Bwana atakutukuza sana.

Bwana akubariki.

Lakini ikiwa upo nje ya Kristo, tambua kuwa bado huwezi kumtumikia Bwana, na hata ukifa sasa ni moja kwa moja unaenda katika jehanamu ya moto. Kwanini usiyapange upya maisha yako leo kwa kufanya uamuzi wa busara wa kumkabidhi Kristo maisha yako?

Ikiwa upo tayari kufanya hivyo sasa, basi fungua hapa kwa mwongozo huo wa sala.>>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya Mithali 27:21  inaposema “mtu hujaribiwa kwa sifa zake?”

Nini maana ya Mithali 5:15-18 anaposema Unywe maji ya birika lako mwenyewe?

USINIPE UMASKINI WALA UTAJIRI. (Mithali 30)

Je! Wamwona mtu mwenye bidii katika kazi zake?

TULITAFUTE KWA BIDII TUNDA LA ROHO.

HAKUVAA NGUO SIKU NYINGI.

KUWA MAKINI, HATUA ZA UNYAKUO ZINAENDELEA.

Rudi nyumbani

Print this post

Jinsi ya kuandaa Somo la kufundisha

Jinsi ya kuandaa mahubiri ya kufundisha kanisani au kwenye semina.

Jinsi ya kuandaa mahubiri ya kufundisha kanisani au katika ibada. Zifuatazo ni dondoo chache zitakazoweza kukusaidia katika kuandaa Somo ambalo litakuwa na uvuvio wa Roho Mtakatifu.

1. Tafuta sehemu ya utulivu.

Hii ni hatua ya kwanza kabisa: Tafuta eneo lisilo na kelele, wala usumbufu, hakikisha husumbuliwi na mtu au simu. Hiyo inaweza kuwa katika chumba cha utulivu au mahali ambao hauwezi kusumbuliwa, Huo ni mlango wa kwanza unaouvuta uwepo wa Mungu karibu nawe, kwasababu maandiko yanasema Mungu wetu si Mungu wa machafuko (1Wakorintho 14:33) na pia ni Mungu anayezungumza katika mazingira tulivu.

1Wafalme 19:12 “na baada ya tetemeko la nchi kukawa na moto; lakini Bwana hakuwamo katika moto ule; na baada ya moto sauti ndogo, ya utulivu”.

Hivyo kabla ya kuanza kufikiri kuandaa somo au hubiri, jitenge na mazingira yote yatakayokuondolea utulivu, kwasababu ukikaa katika hayo mazingira hutamsikia Mungu, Hivyo zima simu kwa muda na pia kaa peke yako kwenye utulivu.

2. Kuwa na Kalamu na Karatasi.

Hii ni hatua ya pili: Andaa kalamu na karatasi kwasababu kabla ya kwenda kuwafundisha wengine, Roho Mtakatifu atakufundisha wewe kwanza.

Warumi 2:21  “basi wewe umfundishaye mwingine, je! Hujifundishi mwenyewe? Wewe uhubiriye kwamba mtu asiibe, waiba mwenyewe”

Kwahiyo wewe ni mwanafunzi wa kwanza wa Roho Mtakatifu kabla ya kwenda kuwafundisha wengine, na Mwanafunzi bora ni sharti awe na kalamu na karatasi kwa lengo la kuyarekodi yale anayojifunza. 

Usipokuwa na sehemu ya kurekodi yale utakayoenda kujifunza itakuwa ni ngumu hata kuyashika..

3. Fungua kwa Maombi.

Omba utakaso kwaajili ya nafsi yako, Omba uwepo wa Mungu ushuke mahali hapo, omba utakaso wa eneo ulilopo, omba roho ya ufunuo ishuke juu yako, kemea nguvu za giza na  zinazoshindana na azimio lako hilo (Tumia muda kidogo kuomba kwa kumaanisha).

4. Anza kusoma biblia na kutafakari

Baada ya maombi, anza kusoma biblia huku ukiruhusu akili yako itafakari. Wengi wakifika hii hatua wanafungua tu biblia na kutafuta mistari wanayoifahamu au watakayokutana nayo kwanza, pasipo kuruhusu tafakari katika fahamu zao.

Siri moja ya Roho Mtakatifu ni kwamba anazungumza na sisi pale tunapotafakari na si pale tunapoziba tafakari zetu. Unapokuwa katika kutafakari ndipo Roho Mtakatifu naye anaungana na tafakari zako pasipo kujua na ghafla unajikuta unafunguka akili na kujikuta unapokea vitu vipya, ambavyo ulikuwa huvijui, vitu hivyo vipya ambavyo ulikuwa huvijui vinavyokubaliana na Neno la Mungu ndio sauti ya Roho Mtakatifu, hivyo andiko hivyo ulivyovipokea kwasababu ndio vitakuwa sehemu ya somo lako ambalo Roho Mtakatifu anataka ujifunze wewe kwanza kisha ukawafundishe na wengine.

5. Omba tena

Hii ni hatua ya mwisho, baada ya kusoma na kutafakari kwa muda mrefu, na kupokea Funuo nyingi. Omba maombi ya mwisho ya kushukuru, kisha funga daftari lako.

Darasa lijalo tutajifunza jinsi ya kusimama na kufundisha kile ulichofundishwa na Roho Mtakatifu. Kwani ni muhimu pia kujua jinsi ya kufundisha ili usije ukajikuta unamzimisha Roho. (Kanuni ya kufundisha kwa matokeo yaliyokusudiwa ni rahisi sana, usikose darasa lijalo).

Maran atha

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

JE! UPO KATIKA MAJI YA UTULIVU?

NIFANYE NINI ILI MUNGU AYAJIBU MAOMBI YANGU?

Wanikolai ni watu gani? Katika biblia?

JINSI YA KUSOMA BIBLIA.

Guruguru na Goromoe ni wanyama gani? (Walawi 11:30)

Rudi nyumbani

Print this post

Mstari mfupi kwenye biblia

Mstari mfupi zaidi kwenye biblia ni upi? na umebeba ujumbe gani?

Mistari inatofautiana urefu kulingana na lugha na lugha.. Mstari unaoonekana mfupi katika lugha ya moja unapotafsiriwa katika lugha nyingine unaweza kuwa mrefu kuliko mistari mingine.

Kwamfano katika lugha ya kiingereza, mstari ulio mfupi kuliko yote unapatikana katika kitabu cha Yohana 11:35 unaosema kwa kiingereza “Jesus wept” Lakini tukiurudisha kwenye lugha Kiswahili unasomeka kama “Yesu akalia machozi”, Hivyo kuufanya mstari huo kutokuwa mfupi kuliko mingine katika lugha yetu.

Sasa mstari mfupi kuliko yote kwenye lugha ya Kiswahili ni upi? (Katika agano jipya).

Ni mstari unaopatikana katika kitabu cha 1Wathesalonike 5:20 unaosema “msitweze unabii”.

Huo ndio mstari mfupi kuliko yote, katika biblia ya Kiswahili, ( Agano jipya) Na ndio ujumbe mfupi kuliko yote aliouchagua Roho Mtakatifu kwa watu wanaozungumza lugha ya Kiswahili, kwamba “tusitweze unabii”, au kwa lugha rahisi “Tusidharau wala kupuuzia unabii”.

Na unabii unaozungumziwa hapo kwamba tusiudharau/ tusiutweze sio nabii zinazosikika sasahivi za wanaojiita manabii au wanaojulikana kama manabii, hapana! Bali Nabii zilizoandikwa kwenye biblia, mfano wa Nabii hizo ni zile Bwana Yesu alizozitaja katika Mathayo 24, zinazohusiana na kurudi kwake kwamba Nyakati kutatokea vita, njaa, manabii wa uongo, Tauni, matetemeko, upendo wa wengi kupoa n.k Hizo ndio nabii ambazo hatupaswi kuzipuuzia, kwa maana ni kweli zitatimia.

Kuzidi  kufahamu kwa kina Zaidi maana ya kutotweza unabii fungua hapa >>Msitweze unabii

Je umempokea Yesu?.. Je unajua kwamba kizazi tunachoishi ni kizazi ambacho kina uwezekano wa kushuhudia ujio wa pili wa Yesu dhahiri??

Maran atha!.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya ELOHIMU?

TABIA YA WAZI INAYOWATOFAUTISHA MANABII WA UONGO NA WALE WA UKWELI.

Je kunena kwa Lugha mpya kukoje?

NI YESU YUPI UMEMPOKEA?, NI ROHO IPI UMEIPOKEA? NA INJILI IPI UMEIPOKEA?

USIPOTEZWE NA MANENO YA MANABII WA UONGO.

FREEMASONS NI NINI? NA MTU ATATOKAJE HUKO?

Rudi nyumbani

Print this post

Miimo ni nini na kizingiti ni nini?

Katika biblia Miimo ni nini na kizingiti ni nini?

Jibu: Miimo ni nguzo mbili za mlango zinazosimama upande wa kuume na wa kushoto mwa mlango.

Mfano wa hiyo ni ile Samsoni aliyoing’oa ya geti la wafilisti

Waamuzi 16:3 “Basi Samsoni akalala hata usiku wa manane, akaondoka katikati ya usiku, akaishika milango ya lango la mji, NA MIIMO YAKE MIWILI, akaing’oa pamoja na komeo lake, akajitwika mabegani, akavichukua hata kilele cha mlima ule unaokabili Hebroni”.

Unaweza kusoma zaidi kuhusu Miimo katika mistari ifuatayo Kumbukumbu 6:9, 1Wafalme 6:33, na Isaya 57:8.

Na kizingiti ni nguzo moja ya mlango inayolala ambayo inakuwa upande wa juu wa mlango (wakati mwingine pia inawekwa upande wa chini wa mlango) Kwamfano utaona wakati wana wa Israeli wanatolewa Misri, waliambiwa wapake ile damu ya mwanakondoo kwenye vizingiti vya nyumba na  kwenye miimo yake, ili yule Malaika alitumwa kuharibu asiingie na kuua wazaliwa wa kwanza wa nyumba hizo.

Kutoka 12:7 “Nao watatwaa baadhi ya damu yake na kuitia katika miimo miwili na KATIKA KIZINGITI cha juu, katika zile nyumba watakazomla”.

Miimo na vizingiti vinaweza kuwa vya malighafi yoyote, aidha mbao, chuma, udongo au shaba.

Unaweza kusoma zaidi juu ya kizingiti/vizingiti katika mistari ifuatayo Ezekieli 10:4, 1Wafalme 6:31, na 1Wafalme 14:17.

Lakini Miimo na vizingiti vinafunua nini kiroho?

Maandiko yanasema Miili yetu ni Nyumba (Hekalu la Roho Mtakatifu) 1Wakorintho 6:19 na 1Wakorintho 3:16 na Kama ni Nyumba ya Roho Mtakatifu basi ni lazima ina Mlango, na kama ina mlango ni lazima ina miimo na vizingiti.

Sasa Mlango wa Hekalu la Roho Mtakatifu ni mioyo yetu..

Ufunuo 3:20 “Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami.”

Na kama mioyo yetu ni Malango basi ni lazima ina Miimo yake na Vizingiti vyake.. na hivyo si vingine zaidi ya Macho yetu na Masikio masikio yetu. Masikio ni vizingiti na macho ni miimo.

Mioyo yetu inapokea vile tunavyovisikia na na macho yetu vile tunavayoviona. Hivyo kama macho yetu yametakaswa kwa damu ya Yesu Kristo katika ulimwengu wa roho na masikio yetu yametakaswa kwa damu ya Yesu Kristo basi hapo ni sawa na ile nyumba iliyopakwa damu ya mwana kondoo katika miimo ya milango yake na vizingiti vyake nyakati za Israeli kutoka Misri, Na hivyo uharibifu utakapofika hautatukuta.

 Lakini kinyume chake kama Macho yetu ni ya uasi na masikio yetu ni ya ukaidi basi hata mioyo yetu itakuwa michafu na hivyo tutalinajisi Hekalu zima la Mungu ambalo ndio miili yetu na hivyo kujiweka katika hatari ya kuharibiwa sawasawa na maandiko yanavyosema.

1Wakorintho 3:17 “Kama mtu akiliharibu hekalu la Mungu, Mungu atamharibu mtu huyo. Kwa maana hekalu la Mungu ni takatifu, ambalo ndilo ninyi”

Je umeokoka?, je umetakaswa kwa damu ya Yesu?.. Kama bado unasubiri nini?, mpokee Yesu leo kwa kutubu na kubatizwa na kujazwa Roho Mtakatifu.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Tofauti ya kazi ya Damu ya Yesu na Jina la Yesu ni ipi?

MWANAMKE, USIFUNGUE MLANGO WA MAPEPO KUKUINGIA!.

Tofauti ya kazi ya Damu ya Yesu na Jina la Yesu ni ipi?

Je! Shetani anao uwezo wa kuumba, kama Mungu?

Bawa la mbuni hufurahi; Lakini mabawa yake na manyoya yake, je! Yana huruma? 

Rudi nyumbani

Print this post

Biblia inamaana gani inaposema tutoapo unabii tutoe kwa kadiri ya imani?

SWALI: Biblia inamaana gani inaposema tutoapo unabii tutoe kwa kadiri ya imani?(Warumi 12:6)


JIBU: Neno hilo utalipata katika vifungu hivi;

Warumi 12:5  Vivyo hivyo na sisi tulio wengi tu mwili mmoja katika Kristo, na viungo, kila mmoja kwa mwenzake.

6  Basi kwa kuwa tuna karama zilizo mbalimbali, kwa kadiri ya neema mliyopewa; ikiwa unabii, tutoe unabii kwa kadiri ya imani;

7  ikiwa huduma, tuwemo katika huduma yetu; mwenye kufundisha, katika kufundisha kwake;

8  mwenye kuonya, katika kuonya kwake; mwenye kukirimu, kwa moyo mweupe; mwenye kusimamia kwa bidii mwenye kurehemu, kwa furaha.

Andiko hili linatuonyesha kuwa kila mmoja wetu amepewa KIPIMO cha neema, na hicho kipimo, kwa lugha nyingine ndio kinaitwa ‘Imani’ kama ilivyotumika hapo. Maana yake ni kuwa ikiwa ni nabii, basi kuna tofauti ya viwango vya kinabii, kwamfano wapo wengine wanapewa taarifa za watu tu, wapo wengine wanapewa za nyakati zijazo, wapo wengine za mataifa, wapo wengine wanapewa taarifa dhahiri kabisa za moja kwa moja, na wapo wengine kwa njia za mafumbo n.k.. Vyote hivi vinajulikana kama ndio vipimo vya imani.

Lakini sasa ikiwa mtu hajajaliwa kuona jambo Fulani, kisha akalazimishia alione,ili tu aonekane yeye ni mwonaji wa mambo yote, maana yake mtu huyo ni kuwa amevuka kiwango cha imani alichopimiwa na Mungu.

Na hivyo ataishia kutoa taarifa za uongo ambazo Mungu hajazisema. Kwamfano mtu ataona maono, kisha asiyaelewe, hata baada ya kuomba hajayaelewa, lakini kwasababu hataki kushirikisha wenye karama za Hekima na Maarifa na upambanuzi, atataka yeye ndio atafsiri alichoonyeshwa, hivyo anatumia akili zake, na matokeo yake inakuwa ni upotoshaji badala ya ujengaji.

Vivyo hivyo na katika karama nyingine. Utakutana na mtu sio mwalimu, hajajaliwa karama hiyo, lakini kwasababu na yeye anataka kujionyesha ni mjuaji anafahamu yote, ataanza kufundisha, na hatimaye kuwapotosha watu kwa mafundisho yake dhaifu.

Mitume japokuwa walijaliwa wingi wa karama na vipawa vya Roho lakini hawakuwa hivyo. Paulo anasema..

2Wakorintho 10:12  “Kwa kuwa hatuthubutu kujihesabu pamoja na baadhi yao wanaojisifu wenyewe, wala kujilinganisha nao; bali wao wenyewe wakijipima nafsi zao na nafsi zao, na wakijilinganisha nafsi zao na nafsi zao, hawana akili.

13  Lakini sisi hatutajisifu zaidi ya kadiri yetu; bali kwa kadiri ya kipimo tulichopimiwa na Mungu, yaani, kadiri ya kufika hata kwenu.

14  Maana hatujitanui nafsi zetu kupita kadiri yetu, kana kwamba hatuwafikii ninyi; kwa sababu tulitangulia kufika mpaka kwenu katika injili ya Kristo;

Palepale ulipofikishwa na Bwana dumu hapo hapo, ikiwa Bwana atakuongezea neema basi itathibitika, lakini usijiongezee chochote, zaidi ya kile ulichopimiwa. Na hatari sana

Waefeso 4:7  Lakini kila mmoja wetu alipewa neema kwa kadiri ya kipimo cha kipawa chake Kristo

Bwana akubariki.

 Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Karama ya pili inayozungumziwa katika 2Wakorintho 1:15 ndio ipi?

UPO UMUHIMU MKUBWA WA KUMTOLEA BWANA!

USIJISIFIE KARAMA KWA UONGO.

Je! Umeona asali? Kula kadiri ya kukutosha;

KUWA WEWE.

Kwanini Daudi achukue mawe matano, na malaini na sio vinginevyo?

Rudi nyumbani

Print this post