SWALI: Mstari huu unamaana gani? Mithali 19:21 Mna hila nyingi moyoni mwa mtu; Lakini shauri la Bwana ndilo litakalosimama.
JIBU: Kila moyo wa mwanadamu, unamatamainio mengi, lakini uhalisia ni kwamba sio matamanio yote ni ya ukweli au yanania nzuri baadaye, kwamfano mtu atataka mali nyingi, lakini moyo wake unasema atakapopata nyumba kubwa na gari atawakomoa waliomdharau, atalipiza kisasi, atafanya anasa ,atatembea kwa majigambo, ataongeza Masuria.
Na ndio maana mengi ya malengo kama haya yawezi kusimama kwa watoto wa Mungu, kwasababu yana hila nyingi nyuma yake. Mtume Yakobo aliliweka wazi jambo hili, ni kwanini wakati mwingine hatupokei majibu ya maombi yetu alisema..
Yakobo 4:2 “Mwatamani, wala hamna kitu, mwaua na kuona wivu, wala hamwezi kupata. Mwafanya vita na kupigana, wala hamna kitu kwa kuwa hamwombi! 3 Hata mwaomba, wala hampati kwa sababu mwaomba vibaya, ili mvitumie kwa tamaa zenu”
Lakini kinyume chake anasema Shauri la Bwana ndilo litakalosimama. Maana yake ni kuwa Hekima ya Bwana inayopima haya yote imaamua cha kutoa na kutokutoa. Hivyo si matamainio yako yote unayoyaona ni mema, basi yatakuwa mema pia mbele za Mungu, mengine yana udaganyifu mwingi. Ndio maana Yeremia 17: 9 inasema “Moyo huwa mdanganyifu kuliko vitu vyote, una ugonjwa wa kufisha; nani awezaye kuujua”?
Hivyo tuombapo jambo ni busara kumalizia na kusema “Bwana mapenzi yako yatimizwe”.
Amen.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Utakapoketi kwa chakula pamoja na mtawala Mwangalie sana
JE UPANGA UMEINGIA MOYONI MWAKO?.
VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 11 (Mithali, Wimbo ulio bora, Mhubiri)
Mruba ni mdudu gani kwenye biblia?(Mithali 30:15)
JIFUNZE KUDUMU UWEPONI MWA MUNGU.
Je ni kweli Yuda hakuwa na dhambi kwa kumsaliti Bwana, kwasababu tayari ilikuwa imeshatabiriwa?
Swali: Maandiko yanatuonyesha Tera, baba yake Abramu aliishi jumla ya miaka 205 (Mwanzo 11:32) na tena yanaonyesha kuwa Tera alimzaa Abramu akiwa na miaka 70 (Mwanzo 11:26), na ukirudi kwenye Mwanzo 12:4 biblia inatuonyesha tena Abramu alitoka nchi ya Harani alipofikisha miaka 75.
Sasa ukipiga mahesabu vizuri utaona miaka aliyoishi Tera baba yake Abramu isingepaswa iwe 205, bali iwe miaka 145 yaani (70+75=145) kama Abramu aliondoka kwelii Harani baada ya kifo cha babaye! , Lakini tunaona biblia inatuambia umri wa Tera ulikuwa ni miaka 205. (Je biblia inajichanganya!)
Jibu: Jibu ni kwamba Biblia haijichanganyi na wala haijawahi kujichanganya, vinginevyo ingekuwa ni kitabu cha uongo!. Lakini tunaona maneno yaliyomo ndani ya biblia ni ya uzima tena yenye Nguvu.
Sasa tukirudi kwenye swali letu, je! Abramu alitoka Nchi ya Harani kabla au baada ya kufa baba yake? Jibu ni kwamba alitoka BAADA YA BABA YAKE KUFA!, Na si kabla!. Tunalithibitisho hilo Zaidi katika kitabu cha Matendo ya Mitume..
Matendo 7:2 “Naye akasema, Ndugu zangu na baba zangu, sikilizeni: Mungu wa utukufu alimtokea baba yetu Ibrahimu, alipokuwa katika Mesopotamia, kabla hajakaa Harani,
3 akamwambia, Toka katika nchi yako na katika jamaa zako, ukaende hata nchi nitakayokuonyesha.
4 Ndipo alipotoka katika nchi ya Wakaldayo, AKAKAA HARANI, AKATOKA HUKO BAADA YA KUFA BABAYE, Mungu akamhamisha mpaka nchi hii mnayokaa ninyi sasa.
Sasa kama ni hivyo kwanini hesabu ya miaka haikai sawa..badala ya miaka 145 anaonekana kufa akiwa na miaka 205?.
Jibu ni kwamba Tera hakumzaa Abramu akiwa na miaka 70, bali maandiko yanasema alipofikisha umri wa miaka 70 akamzaa Abramu, Nahori na Harani. (watoto watatu).
Mwanzo 11:26 “Tera akaishi miaka sabini, akamzaa Abramu, na Nahori, na Harani”.
Maana yake ni kwamba watoto hawa watatu walianza kuzaliwa baada ya Tera kufikisha miaka 70, na si kwamba wote watatu walizaliwa ndani ya mwaka mmoja, bali walizaliwa katika vipindi tofauti tofauti pengine walipishana miaka mitano mitano au hata kumi kumi au hata Zaidi ya hapo, lakini Tera alipofikisha miaka 70 ndipo alipoanza kuzaa!
Sasa swali la msingi hapa ni mtoto yupi aliyekuwa wa kwanza kuzaliwa na yupi aliyekuwa wa mwisho kati ya hao watatu..
Katika hiyo Mwanzo 11:26 tunaona Abramu akitajwa wa kwanza, sasa hiyo haimaanishi kuwa yeye ndiye aliyekuwa wa kwanza kuzaliwa!!.. Orodha hiyo imetajwa kufuatia heshima ya watu hao na si ukubwa!.. Abramu ndiye aliyetukuka mbele za Mungu Zaidi ya hao ndugu zake wawili ndio maana kawekwa hapo wa kwanza..kwasababu habari inayoendelea itamhusu yeye yeye na uzao wake.. hiyo ndio sababu ya yeye kutajwa wa kwanza na si nyingine.. Lakini kuhalisia aliyekuwa mkubwa kuliko wote pale ni Harani.
Tunajuaje Harani ndiye aliyekuwa mkubwa kuliko Abramu na Nahori?…
Kwanza Abramu alisafiri na Lutu, ambaye alikuwa ni mtoto wa Harani kaka yake.. Na wakati huo tayari Lutu alikuwa mtu mzima kipindi anasafiri na Abramu (Mwanzo 12:5)… Pili Abramu na Nahori aliyetajwa wa pili kwenye orodha alimwoa mtoto wa Harani kaka yake.
Mwanzo 11:29 “Abramu na Nahori wakajitwalia wake. Jina la mkewe Abramu aliitwa Sarai, na jina la mkewe Nahori ALIITWA MILKA, BINTI HARANI, ambaye alikuwa baba wa Milka na wa Iska”.
Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba Abramu hakuwa mtoto wa kwanza wa Tera bali huenda alikuwa wa pili au wa tatu, Harani ndiye aliyekuwa wa kwanza ingawa kwenye orodha ameonekana wa mwisho…na Tera hakumzaa Abramu akiwa na miaka 70 bali akiwa na miaka 130. Na Abramu aliondoka Harani alipofikisha miaka 75 baada ya kifo cha baba yake, ambaye alikufa akiwa na miaka 205.
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Je! biblia inajichanganya katika 1Petro 2:13 na Matendo 5:29.
Je Henoko aliyeenda na Mungu alikuwa ni mwana wa Kaini? (Mwanzo 4:16)
NINI KINAFUATA SIKU ILE ILE YA KUOKOKA!
Je Ni kweli haturuhusiwi kula nyama kulingana na Isaya 66:3?
Swali: Napenda kujua je!, idadi ya Wana wa Israeli waliouawa kwa pigo kule Shitimu ilikuwa ni Elfu 23 au elfu 24?..maana sehemu moja tunaona biblia inataja watu elfu 23 (1Wakorintho 10:8) na sehemu nyingine Elfu 24, (Hesabu 25:9) je biblia inajichanganya?.
Jibu: Biblia haijichanganyi sehemu yoyote kwasababu sio kitabu cha Uongo, bali ni kitabu kilichojaa maneno ya uzima wa Mungu, na ya kweli.
Sasa ili tuielewe vizuri tuisome habari yenyewe kuanzia ule mstari wa kwanza wa kitabu hicho cha Hesabu 25
Hesabu 25:1 “Basi Israeli akakaa Shitimu, kisha watu wakaanza kuzini pamoja na wanawake wa Moabu; 2 kwa kuwa waliwaalika hao watu waende sadakani, sadaka walizowachinjia miungu yao; watu wakala chakula, wakaisujudu hiyo miungu yao.
3 Ikawa Israeli kujiungamanisha na Baal-peori; hasira za Bwana zikawaka juu ya Israeli.
4 Kisha Bwana akamwambia Musa, Watwae wakuu wote wa hao watu, ukamtungikie Bwana watu hao mbele ya jua, ili kwamba hizo hasira kali za Bwana ziwaondokee Israeli.
5 Basi Musa akawaambia waamuzi wa Israeli, Waueni kila mtu watu wake waliojiungamanisha na Baal peori.
6 Na tazama, mtu mmoja miongoni mwa wana wa Israeli akaja na kuwaletea nduguze mwanamke Mmidiani mbele ya macho ya Musa, na mbele ya macho ya mkutano wote wa wana wa Israeli, hapo walipokuwa walia mbele ya mlango wa hema ya kukutania.
7 Naye Finehasi mwana wa Eleazari, mwana wa Haruni kuhani, alipoona jambo hilo, akaondoka hapo katikati ya mkutano, akashika fumo mkononi mwake;
8 akamwandama huyo mtu wa Israeli na kuingia ndani ya hema nyuma yake, naye akawachoma wote wawili kwa fumo lake, yule mume wa Israeli na huyo mwanamke kati ya tumbo lake. Basi pigo likazuiwa kwao wana wa Israeli.
9 Nao waliokufa kwa hilo pigo walikuwa WATU ELFU ISHIRINI NA NNE HESABU YAO”
Hapa tunaona ni watu elfu 24 waliokufa kwa pigo hilo… lakini tunaona idadi nyingine tofauti ikitajwa katika kitabu cha Waraka kwa wakorintho.
1Wakorintho 10:8 “Wala msifanye uasherati, kama wengine wao walivyofanya, WAKAANGUKA SIKU MOJA WATU ISHIRINI NA TATU ELFU”.
Sasa je! Biblia inajichanganya? Jibu ni La!
Ukweli ni kwamba idadi ya waliokufa kwa pigo ni watu elfu 24 na si elfu 23 lakini kwanini Paulo katika hiyo 1Wakorintho 10:8 aseme ni elfu 23?
Ni lazima uangalie ni nini Paulo alichokuwa anajaribu kukupitisha kwa watu wa wakorintho, Lengo na Nia ya Paulo ilikuwa ni kuwaonyesha madhara ya Uasherati, jinsi unavyoweza kuleta madhara makubwa ndani ya kipindi kifupi!.
Sasa hapa Paulo anasema walianguka watu elfu 23 “KATIKA SIKU MOJA”. Ikiwa na maana kuwa huwenda lile pigo lilienda Zaidi ya “siku moja” . Huwenda lilidumu siku mbili au Zaidi ya hapo! Ndipo likakoma!.. lakini katika ile siku moja tu ya kwanza walianguka watu elfu 23 (hiyo ni idadi kubwa sana)…na idadi ya wote waliokufa mpaka siku ya mwisho pigo lilipokoma ilikuwa ni watu elfu 24.
Sasa Paulo anajaribu kuwaonya Wakorintho jinsi uasherati unavyoweza kuleta madhara makubwa ndani ya kipindi kifupi kuliko wanavyodhania, kama ilivyokuwa kwa hawa wana wa Israeli walivyozini na wanawake wa Moabu..
Ndio maana tukirudi nyuma kidogo kwenye kitabu hicho hicho, mlango ule wa 6 utaona jinsi Paulo anavyoelezea ubaya wa dhambi ya uasherati..kwamba ni mbaya Zaidi ya dhambi zote mtu anazoweza kuzifanya katika mwili…
1Wakorintho 6:15 “Je! Hamjui ya kuwa MIILI YENU NI VIUNGO VYA KRISTO? Basi nivitwae viungo vya Kristo na kuvifanya viungo vya kahaba? Hasha!
16 Au hamjui ya kuwa yeye aliyeungwa na kahaba ni mwili mmoja naye? Maana asema, Wale wawili watakuwa mwili mmoja.
17 Lakini yeye aliyeungwa na Bwana ni roho moja naye.
18 Ikimbieni zinaa. Kila dhambi aitendayo mwanadamu ni nje ya mwili wake; ILA YEYE AFANYAYE ZINAA HUTENDA DHAMBI JUU YA MWILI WAKE MWENYEWE.
19 Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu? Wala ninyi si mali yenu wenyewe;
20 maana mlinunuliwa kwa thamani. Sasa basi, mtukuzeni Mungu katika miili yenu”.
Ni nini tunajifunza?
Kikubwa tunachoweza kujifunza ni madhara ya Uasherati, wengi wanasema nikishafanya uasherati nitatubu tu!..pasipo kujua kuwa uasherati wa mara moja unaweza kuleta madhara makubwa ndani ya muda mfupi!ll…Wana wa Israeli walipomaliza kufanya dhambi hiyo ndani ya siku moja walikufa watu elfu23, nafasi ya kutubu hawakuiona..
Vile vile dhambi ya uasherati inaweza kukuharibia mambo yako mengi ndani ya siku moja. Inaweza kukuharibia maisha yako moja kwa moja ndani ya siku moja, inaweza kukupeleka kuzimu ndani ya siku moja, na inaweza kukuletea majuto makubwa ndani ya siku moja, Zaidi sana biblia inasema mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa.
Mithali 6:32 “Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa; Afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake”.
Itaishindaje dhambi ya Uasherati?.. Je kwa kuomba tu? Jibu ni La!..bali kwa kuikimbia kama Yusufu alivyoikimbia..
1Wakorintho 6:18 “Ikimbieni zinaa..”
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Uasherati wa Kiroho maana yake nini?
Nini Tofauti kati ya uzinzi na uasherati ?
Nini maana ya siku moja kwa Bwana ni kama miaka elfu, na miaka elfu ni kama siku moja? (2Petro 3:8)
Mhubiri 10:16 “Ole wako, nchi, akiwa mfalme wako ni kijana, Na wakuu wako hula asubuhi!”
Mstari huu umegawanyika katika sehemu mbili;
Hapo mhubiri anajaribu kueleza uhusiano uliopo kati ya uongozi na ukomavu wa mtu. Akatumia mfano wa kijana, kwasababu mara nyingi ni ngumu sana kuipata busara kwa vijana, kutokana na kuwa hawana uzoefu mwingi wa maisha na pia hawajaandaliwa vya kutosha, kumudu nafasi za uongozi, kinyume chake kitakachowaongoza ni hisia tu za ujana na si vinginevyo. Na ndio maana mtu kama Sulemani alilitambua hilo alipotawadhwa tu mfalme akiwa bado kijana mdogo, alimwomba Mungu ampe hekima ya namna ya kuwaongoza watu wake. Na Bwana akamjalia.
1Wafalme 3:7 “Na sasa, Ee Bwana, Mungu wangu, umenitawaza niwe mfalme mimi mtumwa wako badala ya Daudi baba yangu; nami ni mtoto mdogo tu; sijui jinsi inipasavyo kutoka wala kuingia.
8 Na mtumwa wako yu katikati ya watu wako uliowachagua, watu wengi wasioweza kuhesabiwa, wala kufahamiwa idadi yao, kwa kuwa ni wengi.
9 Kwa hiyo nipe mimi mtumwa wako moyo wa adili niwahukumu watu wako, na kupambanua mema na mabaya; maana ni nani awezaye kuwahukumu hawa watu wako walio wengi? 10 Neno hili likawa jema machoni pa Bwana, ya kuwa Sulemani ameomba neno hili”
Walikuwepo pia wafalme wengine waliotawadhwa wakiwa wadogo kama Yoashi, lakini akasaidiwa na kuhani Yehoyada katika ufalme wake, na ukawa bora (2Wafalme 11-12)
Lakini tunakuja kuona kwa mwanawe Sulemani aliyeitwa Rehoboamu. Yeye naye alikuwa ni kijana lakini hakutaka mashauri kwa wazee waliomtangulia, kinyume chake, akasikiliza mashauri ya vijana wenzake Hivyo ikapelekea ufalme wake kugawanyika, na kupoteza makabila kumi kati ya kumi na mbili ya Israeli.(Soma 1Wafalme 12:1-16)
Maana yake kwamba kuwa na viongozi ambao wanatanguliza maslahi yao kabla ya kazi, nchi hiyo sikuzote huishia pabaya. Sikuzote watu wanakwenda kufanya kazi asubuhi, wakitarajia kile walichokihangaikia kutwa nzima ndio wakifaidi jioni, lakini hapa tunaona ni kinyume chake. Na jambo hili ni kweli, Tunaona katika baadhi ya mataifa yanayoendelea, wananchi wao wanapitia katika taabu, na umaskini wa hali ya juu, kutokana na kuwa viongozi wao, wanatazama maslahi yao binafsi wanapoingia madarakani na sio maslahi ya taifa.. Uchu wa madaraka na ukuu, ndio wanachokitazama lakini sio kujenga mataifa yao.
Hii inafunua nini rohoni?
Neno hili linawahusu, watumishi wote wa Mungu wanaosimama katika ngazi za uongozi. Ikiwa wewe bado ni kijana au mchanga katika huduma(hata kama una-mvi) na umepewa kundi ulichunge, Omba sana hekima kwa Mungu, pia kuwa tayari kujifunza kwa waliokutangulia, Sikuzote viongozi-wachanga, katika hatua za awali wanajiamini kuwa wanajua kila kitu, lakini kwa jinsi siku zinavyozidi kwenda ndivyo wanavyotambua kasoro zao nyingi. Hivyo ili kuepuka, kufanya makosa ya kiutumishi, tafuta sana msaada kwa Mungu katika hekima na mashauri.
Lakini pia, ikiwa wewe ni mchungaji, askofu, mtume, mwalimu, au unatumika katika huduma yoyote, epuka tamaa hususani ya mali. Si kila shilingi unayoipata uipeleke tumboni, au kujijengea majumba na biashara. Ni heri ukatazama kwanza hali ya kanisa la Kristo. Kama mchungaji mwema yakupasa kuipendezesha kwanza nyumba ya Bwana, kisha Baadaye Bwana mwenyewe ndio akupendezeshe wewe. Unatembelea gari ya Tsh milioni 40, halafu kanisa ni la makuti, Hapo ni nini unategemea kama sio ufukara wa kiroho hadi kimwili baadaye.
Kwahiyo hekima hizi zinatuonya, ili uongozi wetu usianguke mbeleni, hivyo tuzingatie sana maneno haya ya hekima. Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312 Au jiunge na makundi yetu ya mafundisho ya kila siku kwa kwa njia ya Whatsapp kwa kubofya hapa >>>> WHATSAPP GROUP
Mada Nyinginezo:
NJIA YA ‘UTAJIRI MKUU’ KWA KIJANA.
Je ile nyota ya asubuhi inamwakilisha shetani au Bwana Yesu?
Bwana Yesu alikufa akiwa na umri gani?
Vifungu vya biblia kuhusu Uongozi.
NITAJUAJE KAMA MAOMBI YANGU YAMEFIKA (YAMEJITOSHELEZA)?
Makerubi wenye sura nne, ni kweli wapo? na je! wanyama wataenda mbinguni?
Swali: Tukisoma Marko 6:8, tunaona Bwana Yesu anawaruhusu wanafunzi wake “wabebe fimbo”, lakini tukirejea katika Mathayo 10:10 tunasoma habari tofauti, Bwana Yesu anawakataza wasibebe chochote hata fimbo..sasa mwandishi yupi yupo sahihi na yupi hayupo sahihi? Je biblia inajichanganya yenyewe?.
Jibu: Biblia kamwe haijichanganya mahali popote, vinginevyo kitabu kizima kitakuwa ni cha uongo!. Lakini kama ni kitabu cha kweli kilichojaa maneno ya kweli ya uzima, na Roho Mtakatifu basi hakiwezi kuwa kitabu cha ushuhuda wa uongo!, au unaochanganya!..kinachochanganyikiwa ni fahamu zetu katika kukielewa kitabu hicho, lakini chenyewe kama chenyewe hakina kasoro yoyote.
Awali ya yote tuisome mistari hiyo…
Marko 6:7 “Akawaita wale Thenashara, akaanza kuwatuma wawili wawili, akawapa amri juu ya pepo wachafu;
8 akawakataza wasichukue kitu cha NJIANI ISIPOKUWA FIMBO TU; wala mkate, wala mkoba, wala pesa za bindoni;
9 lakini wajifungie viatu; akasema, Msivae kanzu mbili”.
Hapa ni kweli tunaona Bwana anawaambia wasibebe chochote ila Fimbo tu!… Tusome tena habari hiyo katika kitabu cha Mathayo..
Mathayo 10:7 “Na katika kuenenda kwenu, hubirini, mkisema, Ufalme wa mbinguni umekaribia.
8 Pozeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo; mmepata bure, toeni bure.
9 Msichukue dhahabu, wala fedha, wala mapesa mishipini mwenu;
10 wala mkoba wa safari, wala kanzu mbili, wala viatu, WALA FIMBO; maana mtenda kazi astahili posho lake”.
Hapa tunaona Bwana anawakataza hata Fimbo wasibebe, na ilihali kule kwenye kitabu cha Marko tunaona anawaambia wasibebe kitu kingine chochote isipokuwa Fimbo tu!.. Sasa mwandishi yupi ni wa kweli na yupi ni wa uongo?.
Jibu ni kwamba waandishi wote ni wa kweli hakuna aliye mwongo!,
Katika Marko Bwana anawaambia wasibebe vitu vya njiani isipikuwa FIMBO TU!.. Sasa fimbo hakikuwa chakula bali ni kifaa kinachomwezesha mtu kutembea katika milima na mabonde! Ni kama tu kiatu kilivyo msaada kwa miguu katika safari ndefu za miiba na mavumbi.. Fimbo na yenyewe ilikuwa ni hivyo hivyo..
Kwahiyo fimbo ilikuwa ni sehemu ya kitu cha msingi mtu anachoweza kuwa nacho kwa safari kama tu vile mtu alivyo na kanzu au kiatu au nguo.
Lakini sasa Bwana alichowakataza ni wao kubeba fimbo ya pili au ya tatu, kana Kamba moja ikivunjika basi kutakuwepo na akiba. Hicho ndicho kitu Bwana alichowakataza akawaambia wabebe fimbo moja tu!. Wasihofie endapo hiyo waliyonayo itapata itilafu, kwani huko wanakokwenda Mungu wa mbinguni atawafungulia mlango watapata nyingine.
Lakini pia sio Fimbo tu!, bali hata kanzu!.. wasibebe na kujifungasha mizigo ya kanzu nyingi, waende na hiyo moja tu iliyopo mwilini kwasababu huko waendako Baba yao wa mbinguni anajua kuwa wana haja na nazo, hivyo wasitie wasiwasi kwasababu mtenda kazi amestahili posho yake (watapata huko waendako). Ndio maana akawakataza wasibebe kanzu mbili…
Marko 6:8 “akawakataza wasichukue kitu cha NJIANI ISIPOKUWA FIMBO TU; wala mkate, wala mkoba, wala pesa za bindoni;
9 lakini wajifungie viatu; akasema, MSIVAE KANZU MBILI”.
Hapo mwisho anasema “msivae kanzu mbili” maana yake ile moja waliyonayo mwilini inatosha.. vile vile wasibebe fimbo nyingine ya pili, hiyo moja watakayokuwa nayo inatosha!..sawasawa na hiyo Mathayo 10:10..
Kwahiyo biblia haijichanganyi, bali shetani ndiye anayetuchanganya….
Sasa kufahamu ni somo gani tunaloweza kujifunza nyuma ya hii habari fungua hapa>>> Bwana alimaanisha nini kusema“maana mtenda kazi astahili posho lake”
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Je suruali ni vazi la kiume tu?
Ni kwa namna gani Yesu ni Simba wa Yuda?
Gongo na Fimbo ni nini? Na vinawezaje kumfariji mtu? (Zaburi 23:4).
Je! habari ya muda aliotawala Mfalme Yekonia inajichanganya? (2Wafalme 24:8 na 2Nyakati 36:9).
Jibu: Biblia haijichanganyi mahali popote na haijawahi kujichanganya isipokuwa viwango vyetu vya kutafakari ndivyo vinavyotufanya tuone kuna utata mwingi kwenye biblia (na kumbuka tunapozungumzia biblia tunamaanisha ile yenye vitabu 66) na si zaidi ya hivyo!.
Vitabu 66 vya biblia ndivyo vilivyohakikiwa na Roho Mtakatifu kwa vizazi vyote kama Neno la Mungu lililo hai.
Sasa kabla ya kwenda kuitafakari mistari hiyo hebu tuisome kwanza..
Mwanzo 15:13 “Bwana akamwambia Abramu, Ujue hakika ya kwamba uzao wako utakuwa mgeni katika nchi isiyo yake, watawatumikia watu wale, nao watateswa muda wa MIAKA MIA NNE.
14 Hata na taifa lile, watakaowatumikia, nitawahukumu; baadaye watatoka na mali mengi”
Tusome tena,..
Kutoka 12:40 “Basi wana wa Israeli kukaa kwao, maana, muda waliokaa ndani ya Misri, ulikuwa NI MIAKA MIA NNE NA THELATHINI.
41 Ilikuwa mwisho wa miaka hiyo MIA NNE NA THELATHINI, ilikuwa siku ile ile, ya kwamba majeshi yote ya Bwana yalitoka nchi ya Misri”.
Sasa swali ni hili, Mungu alimdanganya Abramu kuwa uzao wake utakaa miaka 400 na kumbe ni miaka 430?, je Mungu ni mwongo?
Jibu ni la! Hakudanganywa, kwasababu hiyo miaka 430 bado ipo katika namba mia nne, Mungu hakumwambia kuwa atakaa miaka mia nne kamili, bali alimwambia tu miaka mia nne, ikiwa na maana kuwa inaweza kuwa ni miaka mia nne kamili au miaka 410 au 430 au 470 au hata 490 lakini haitazidi hiyo miaka 400 na kuwa 500.
Ni sawa na mtu akuulize wewe una miaka mingapi na umwambie una miaka 30 au 40, unaweza kumpa namba ya ujumla lakini kiuhalisia huenda unayo miaka 30 na miezi 6 au na miezi 7,au una miaka 40 na miezi 8 au 9.. Kwahiyo wewe kumwambia kuwa una miaka 30 au 40 unakuwa hujamdanganya.. Ni kweli ndio miaka yako, isipokuwa hujapenda kumwambia na miezi iliyo mbele ya hiyo miaka..Ungekuwa umemdaganya endapo kama ungemwambia unayo miaka 30 kamili au 40 kamili, hapo utakuwa umemdanganya!..
Vile vile Bwana Mungu hakumwambia Abramu kuwa Uzao wake utakaa utumwani miaka 400 kamili, bali alimwambia tu utakaa miaka 400.. Na ndivyo ilivyokuwa.
Kwahiyo biblia haijichanganyi.. Tazama pia miezi aliyotawala Yekonia je inajichanganya? >>> YEKONIA ALITAWALA MUDA GANI?
Je umeokoka?..kumbuka kuwa hizi ni siku za mwisho, na unyakuo wa kanisa ni muda wowote kuanzia sasa.
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Mada Nyinginezo:
Je! kuna mambo ambayo Mungu hawezi kuyafanya kulingana na Waamuzi 1:19?
Makerubi wenye sura nne, ni kweli wapo? na je! wanyama wataenda mbinguni?
Je! habari ya muda aliyotawala Mfalme Yekonia inajichanganya? (2Wafalme 24:8 na 2Nyakati 36:9).
Je! biblia inajichanganya katika 1Petro 2:13 na Matendo 5:29.
Je kauli ya Bwana Yesu inajichanganya? Katika Yohana 8:14 na Yohana 5:31?
Jibu: Kabla ya ufafanuzi tuisome mistari hiyo..
2Wafalme 24:8 “Yekonia alikuwa na umri wa miaka kumi na minane alipoanza kutawala; akatawala MIEZI MITATU katika Yerusalemu; na jina la mama yake aliitwa Nehushta binti Elnathani wa Yerusalemu”.
Tusome tena,
2Nyakati 36:9 “Yekonia alikuwa na umri wa miaka kumi na minane alipoanza kutawala; akatawala katika Yerusalemu MIEZI MITATU NA SIKU KUMI; akafanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana”.
Hapa tunaona mwandishi wa kitabu cha Wafalme anataja miezi aliyotawala Yekonia ni mitatu (3) lakini mwandishi wa kitabu cha Mambo ya Nyakati ameongeza siku kadhaa mbele yake (miezi 3 na siku 10).
Swali, je! Ni yupi yupo sahihi na yupi hayupo sahihi?.. au je biblia inajichanganya?. Au ina makosa katika uandishi?
Jibu ni la! Biblia haijichanganyi mahali popote na haijawahi kujichanganya, na wala haina makosa mahali popote kwasababu endapo ikijichanganya au ikikosewa, basi yote itakuwa ni uongo na sio Neno la Mungu, lakini tunaona maneno yaliyoandikwa kule ni nguvu ya Mungu, na ni uweza wa Mungu, na tena ni Roho, na hayana makosa…
Sasa tukirudi katika hiyo habari ya muda aliotawala Yekonia, je! Mwandishi yupi yupo sahihi?.
Jibu ni kwamba wote wapo sahihi, hakuna aliyekosea.
Mtu akikwambia nitakuja kukutembelea mwezi wa 3 halafu akaja mwezi huo wa 3 tarehe 10 je atakuwa amekudanganya?..bila shaka atakuwa hajakudanganya kwasababu hiyo tarehe ipo ndani ya huo mwezi wa tatu (haijatoka ndani ya huo mwezi wa 3).. hata kama atakuja tarehe 20 au 21 au 25 atakuwa bado hajakudanganya kwasababu bado tarehe hizo zipo ndani ya mwezi wa huo wa tatu.
Hali kadhalika Mwandishi wa kitabu cha Samweli kasema tu “Yekonia katawala miezi 3” ingawa alikuwa anajua na siku alizotawala lakini kapenda tu kufupisha, hajapenda kutaja na siku wala masaa wala dakika wala sekunde lakini kafupisha tu! Miezi 3.
Lakini mwandishi wa kitabu cha Mambo ya Nyakati kapenda kutaja Miezi Mfalme Yekonia aliyotawala na Siku alizotawala, lakini hajapenda kutaja na masaa wala dakika wala sekunde… Huwenda angetokea na mwandishi mwingine angetaja Miezi aliyotawala, na siku na masaa na sekunde!.. na bado asingekuwa ametoa taarifa sahihi ambazo hazikinzani na za wale waliofupisha!.
Kwahiyo biblia haijajichanganya hapo!.wala haijichanganyi mahali popote. Tazama pia muda wana wa Israeli waliokaa Misri je ni miaka 400 au 430?..kujua hilo kwa urefu fungua hapa >>> Je! Miaka Israeli waliokaa Utumwani ilikuwa mingapi? (miaka 400 au 430) kulingana na Mwanzo 15:13 na Kutoka 12:40-42?, Je biblia inajichanganya?
Je unajua kuwa dhiki kuu itakuja baada ya unyakuo wa kanisa na unyakuo upo karibu?..tutumie ujumbe inbox kwa maelezo marefu juu ya hili.
Maran atha!
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
Mwandishi wa kitabu cha Zaburi ni nani?
UWEZA WA MUNGU UNAONEKANA WAPI?
TUSIIFUATISHE KAWAIDA YA ULIMWENGU HUU.
Swali: Katika 1Nyakati 21:5 tunasona waliohesabiwa kwa Israeli na Yuda jumla ni askari 1,570,000 lakini tukirudi katika 2Samweli 24:9 tunaona jumla ya idadi ya askari waliohesabiwa walikuwa ni 1,300,000 kwa Yuda na Israeli, je biblia inajichanganya?.
Jibu: Turejee,
1Nyakati 21:5 “Naye Yoabu akamtolea Daudi jumla ya hesabu ya watu. Na hao wote wa Israeli walikuwa watu elfu mara elfu, na mia elfu, wenye kufuta panga; na wa Yuda watu mia nne na sabini elfu, wenye kufuta panga”.
Tusome tena…
2Samweli 24:8 “Nao walipokwisha kuzunguka nchi yote, wakaja Yerusalemu mwisho wa miezi kenda na siku ishirini.
9 Naye Yoabu akamtolea mfalme jumla ya hesabu ya watu; nao walikuwa wa Israeli mashujaa wenye kufuta panga mia nane elfu; nao wa Yuda walikuwa watu mia tano elfu”.
Ni kweli katika mistari hii miwili, inaonyesha tofauti ya Askari waliohesabiwa, tunaona kitabu kimoja kinataja idadi ya juu sana, na kingine kinataja idadi ya chini, sasa swali ni je! biblia inajichanganya?
Jibu ni la! Biblia haijichanganyi kwasababu ni kitabu kilichovuviwa na Roho Mtakatifu. Fahamu zetu zinaweza kujichanganya katika kuielewa biblia lakini kamwe biblia haijawahi kujichanganya, hususani panapotokea habari moja kunukuliwa na waandishi wawili tofauti, kwasababu kama biblia itakuwa na makosa sehemu yoyote, basi kitabu kizima kitakuwa na mapungufu na hivyo hakiwezi kuwa kitabu kitakatifu.
Lakini mpaka Roho Mtakatifu aruhusu kidumu kwa nyakati zote na vizazi vyote ni wazi kuwa biblia yenye vitabu 66 ni maandishi matakatifu na ya kuaminiwa asilimia 100, kwaajili ya maarifa sahihi ya kiMungu, na haina makosa yoyote.
Sasa tukirudi katika hiyo habari tunayoisoma katika vitabu hivyo viwili (1Nyakati 21:5 na 2Samweli 24:9) kila mwandishi alijaribu kunukuu aina ya askari waliohesabiwa..
Mwandishi wa kwanza wa kitabu cha 2Samweli 24:9 alinukuu idadi ya Askari ambao walikuwa ni MASHUJAA TU! Ambao idadi yao ilikuwa ni hiyo 1,300,000 Na Mwandishi wa pili wa kitabu cha 1Nyakati 21:5 alinukuu idadi ya Askari wote kwa ujumla (Waliokuwa mashujaa na wasio mashujaa)..ndio maana utaona idadi imeongezeka mpaka kufikia hiyo 1,570,000. Kwahiyo biblia haijichanganyi.
Ilikuwepo tofauti ya Askari wa kawaida na waliokuwa Mashujaa, waliokuwa mashujaa na wale waliokuwa wakongwe na wazoefu katika vita wenye uwezo mkubwa wa kupambana, kwamfano utaona Mfalme Uzia biblia inaonyesha alikuwa na Askari wa kawaida na waliokuwa mashujaa, waliozoea vita, wepesi na hodari wa vita.
2Nyakati 26:11 “Zaidi ya hayo Uzia alikuwa na jeshi la watu wa kupigana, waliokwenda vitani vikosi vikosi, sawasawa na hesabu walivyohesabiwa na Yeieli mwandishi, na Maaseya msimamizi, chini ya mkono wa Hanania, mmojawapo wa maakida wa mfalme.
12 Hesabu yote ya wakuu wa nyumba za mababa, WATU MASHUJAA, ILIKUWA ELFU MBILI NA MIA SITA.
13 Na chini ya mkono wao kulikuwa na jeshi la askari, mia tatu na saba elfu, na mia tano, ambao walipigana vita kwa nguvu nyingi, kumsaidia mfalme juu ya adui”.
Je unajua Bwana Yesu alisema kuwa ”Kila mti usiozaa tunda zuri hukatwa ukatupwa motoni (Mathayo 7:19 )??”
Je ni matunda gani unayozaa?..Mazuri au mabaya..
Mathayo 7:17 “Vivyo hivyo kila mti mwema huzaa matunda mazuri; na mti mwovu huzaa matunda mabaya.
18 Mti mwema hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mwovu kuzaa matunda mazuri.
19 Kila mti usiozaa tunda zuri hukatwa ukatupwa motoni”
Maran atha.Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
LIPO LA KUJIFUNZA KWA WALE MASHUJAA 37 WA DAUDI.
Je Kauli ya Mungu katika Warumi 11:4 na 1Wafalme 19:18 inajichanganya?.
Nini maana ya Dirii, Chapeo na Utayari?
USIZITEGEMEE NGUVU ZAKO KUKUSAIDIA!
Jibu: Turejee,
Mwanzo 9:20 “Nuhu akaanza kuwa mkulima, akapanda mizabibu;
21 akanywa divai, akalewa; akawa uchi katika hema yake.
22 Hamu, BABA WA KANAANI, akauona uchi wa baba yake, akawaeleza ndugu zake wawili waliokuwa nje.
23 Shemu na Yafethi wakatwaa vazi, wakalitanda mabegani mwao wote wawili, wakaenda kinyumenyume, wakaufunika uchi wa baba yao; na nyuso zao zilielekea nyuma, wala hawakuuona uchi wa baba yao.
24 Nuhu akalevuka katika ulevi wake, akajua mwana wake mdogo alivyomtendea.
25 Akasema, NA ALAANIWE KAANANI; Atakuwa mtumwa kabisa kwa ndugu zake”.
Kumbuka hapo kwanza “Kaanani” halikuwa jina la Nchi, bali lilikuwa ni jina la ‘Mtu’. Na mtu huyo alikuwa ni mtoto wa nne (4) wa Hamu..
Mwanzo 10: 6 “Na wana wa Hamu ni Kushi, na Misri, na Putu, na Kanaani”.
Hatujui kwa undani mtoto huyu (Kanaani) alikuwa na tabia gani?..lakini ni wazi kuwa matendo yake yalikuwa kama ya baba yake Hamu, ndio maana akabeba laana ya moja kwa moja ya baba yake.
Sasa huyu Kanaani ndiye aliyelaaniwa na baadaye alikuja kuzaa watoto na uzao wake ukaitwa Uzao wa Kanaani, kufuatia jina la Baba yao, na walipotawanyika usoni pa nchi yote katika ule utawanyiko wa Babeli (Mwanzo 11:8-9) ndipo wakaenda kuishi mahali wana wa Israeli walipowakuta.
Kipindi wanaishi, ardhi ile ilijulikana kama nchi ya Wakanaani. Na kilichokuwa kimelaaniwa na Mungu si ile ardhi/nchi bali ni watu, (ambao ndio hao wakaanani)..ikiwa na maana kuwa hata kama wasingeishi katika ile ardhi na kwenda kuishi katika ardhi nyingine bado wangekuwa chini ya laana.
Kwahiyo wana wa Israeli wakati wanatoka Misri, Mungu aliwatoa Wakanaani kwenye ile ardhi na kuwaweka wana wa Israeli, kwasababu kilicholaaniwa katika Mwanzo 9:5 si ardhi bali ni watu, hivyo watu wanaweza kuondolewa na ardhi ikaendelea kutumika na wengine na ikawa nchi ya Baraka tu, ndio maana baada ya pale haikuitwa tena nchi ya wakanaani bali nchi ya Israeli.
Lakini swali ni je! Hawa Wana wa Hamu mpaka leo wamelaaniwa?.. Maana miongoni mwao kuna Kushi ambaye uzao wake ni watu weusi.
Jibu ni la! Kristo alikuja kuondoa laana zote pale Kalvari, na hivyo hakuna tofauti ya Myahudi na Mmisri, Mkushi na mwisraeli, mbele za Mungu… kama tumeokoka wote tunahesabiwa sawa mbele zake. Lakini kama hatutazaliwa mara ya pili kwa maji na kwa roho wote mbele zake ni kama tuliolaaniwa.
Wakolosai 3:10 “mkivaa utu mpya, unaofanywa upya upate ufahamu sawasawa na mfano wake yeye aliyeuumba.
11 Hapo hapana Myunani wala Myahudi, kutahiriwa wala kutokutahiriwa, mgeni wala mshenzi, mtumwa wala mwungwana, bali Kristo ni yote, na katika yote”.
Waefeso 2:16 “Akawapatanisha wote wawili na Mungu katika mwili mmoja, kwa njia ya msalaba, akiisha kuufisha ule uadui kwa huo msalaba”
Je umezaliwa mara ya pili?..
Yohana 3:3 “Yesu akajibu, akamwambia, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa mara ya pili, hawezi kuuona ufalme wa Mungu.
4 Nikodemo akamwambia, Awezaje mtu kuzaliwa, akiwa mzee? Aweza kuingia tumboni mwa mamaye mara ya pili akazaliwa?
5 Yesu akajibu, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuuingia ufalme wa Mungu”.
Bwana Yesu anarudi!Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Wakaanani walikuwa ni watu gani?
TUMEFANYA KAZI YA KUCHOSHA USIKU KUCHA.
NI KWANINI WATU WENGI WANASHINDWA KUMWELEWA MUNGU?
Je ni kweli Isaka alifarijika kwa kifo cha mamaye? (Mwanzo 24:67).
SWALI: Bwana yesu apewe sifa, Naomba kufahamu, Kwanini Wana wa Israeli walimuhifadhi mwana-kondoo siku nne kabla ya kuchinjwa katika sikukuu ya pasaka.Je Kuna ufunuo gani tunaweza kupata katika Tendo hilo (Kutoka 12:6)
JIBU: Tusome..
Kutoka 12:3-7
[3]Semeni na mkutano wote wa Israeli, mkawaambie, Siku ya kumi ya mwezi huu kila mtu atatwaa mwana-kondoo, kwa hesabu ya nyumba ya baba zao, mwana-kondoo kwa watu wa nyumba moja;
[4]na ikiwa watu wa nyumba ni wachache kwa mwana-kondoo, basi yeye na jirani yake aliye karibu na nyumba yake na watwae mwana-kondoo mmoja, kwa kadiri ya hesabu ya watu; kwa kadiri ya ulaji wa kila mtu, ndivyo mtakavyofanya hesabu yenu kwa yule mwana-kondoo.
[5]Mwana-kondoo wenu atakuwa hana ila, mume wa mwaka mmoja; mtamtwaa katika kondoo au katika mbuzi.
[6]Nanyi mtamweka hata siku ya kumi na nne ya mwezi ule ule; na kusanyiko lote la mkutano wa Israeli watamchinja jioni.
[7]Nao watatwaa baadhi ya damu yake na kuitia katika miimo miwili na katika kizingiti cha juu, katika zile nyumba watakazomla.
Bwana aliwapa agizo la kuwatenga wana-kondoo Kutoka katika kundi siku ya 10, Kisha siku ya 14 kuchinja.
Maana yake ni kuwa sadaka/dhabihu Yao, ilipaswa itambulike mapema Kisha ikatengwa. Kama wangekaidi agizo hilo na kuchagua mwanakondoo siku Ile Ile ya kuchinja au hata siku moja kabla ilikuwa ni kosa mbele za Mungu.
Na sisi pia Bwana anapendezwa na dhahibu zenye maandalizi, ambazo zimetengwa mapema…Kwamfano unapokwenda ibadani jijengee desturi ya kumwandalia Mungu sadaka zako mapema..hata ikiwezekena siku kadhaa kabla..Kwa jinsi unavyoandaa mapema ndivyo inavyokuwa na utukufu mwingi zaidi..
Lakini pia Unahakikisha unaitenga kabisa na hesabu zako nyingine..(yaani haiguswi), mpaka siku ya kumtolea.
Hiyo itaifanya sadaka Yako ipokelewe Kwa furaha na Mungu, kuliko kufikiria kumtolea Mungu muda huo huo wakati ulikuwa na nafasi ya kufanya maandalizi. Ndio ufunuo ulio nyuma ya agizo hilo la Pasaka.
Bwana akubariki.Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Makerubi wenye sura nne, ni kweli wapo? na je! wanyama wataenda mbinguni?
Kwanini Kristo aitwe Mwana-kondoo. (Yohana 1:29)
Tofauti kati ya zaka na sadaka ni ipi?
TUUTAFUTE USEMI MMOJA. TUUJENGE MNARA WA MUNGU
NI SAA KUMI NA MBILI (12) TU, ZA KRISTO KWAKO.
Bahari mbalimbali zilizoorodheshwa kwenye biblia.