Warumi 8:26 “Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu, kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo, lakini Roho mwenyewe hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa. 27 Na yeye aichunguzaye mioyo aijua nia ya Roho ilivyo, kwa kuwa huwaombea watakatifu kama apendavyo Mungu. 28 Nasi twajua ya kuwa katika mambo yote Mungu hufanya kazi pamoja na wale wampendao katika kuwapatia mema, yaani, wale walioitwa kwa kusudi lake”
Warumi 8:26 “Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu, kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo, lakini Roho mwenyewe hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa.
27 Na yeye aichunguzaye mioyo aijua nia ya Roho ilivyo, kwa kuwa huwaombea watakatifu kama apendavyo Mungu.
28 Nasi twajua ya kuwa katika mambo yote Mungu hufanya kazi pamoja na wale wampendao katika kuwapatia mema, yaani, wale walioitwa kwa kusudi lake”
Haijalishi tuna ujuzi wa kuongea kiasi gani?, haijalishi tuna vipaji vya kuongea na vya kupangilia maneno kiasi gani, haijalishi tunayajua maandiko kiasi gani…Mbele za Mungu watu wote ulimwenguni hatujui kuomba jinsi ipasavyo! Hata kama tunaweza kujiona tumeomba vizuri kiasi gani au tumebobea kiasi gani…bado hatujui kuomba jinsi ipasavyo…
Utauliza hata mchungaji, au Nabii, au Mwalimu, au Askofu aliyekaa kwenye wokovu miaka mingi, bado atakuwa hajui kuomba jinsi ipasavyo?..Jibu ni ndio! Hata kama atakuwa amekaa miaka mia katika wokovu, na kila siku anasali, na anajua maandiko yote na kuyanukuu kisahihi wakati wa kuomba…Bado pasipo Roho Mtakatifu atakuwa hajui kuomba jinsi ipasavyo, na hivyo maombi yake huwa hewa mbele za Mungu.
Leo tutajifunza Umuhimu wa Kuwa na Roho Mtakatifu katika kuomba! Kwa maana yeye ndiye atusaidiaye kuomba!…Sasa Utauliza Roho Mtakatifu anatuombeaje? Je yupo huko mbinguni amekaa akituombea kwa Baba muda wote akipeleka mahitaji yetu hata kama wakati tukiwa tumelala au vipi?..Na swali lingine ni kwamba je! Kama anatuombea sisi tuna haja gani tena ya kuomba..maana yeye ndiye anayetuombea vizuri Zaidi.
Ili kupata majibu ya maswali hayo, tujifunze kwanza kidogo jinsi Roho Mtakatifu anavyotenda kazi katika kuwavuta watu kwake..
Mtu aliyejaa Roho Mtakatifu, anapokwenda kuhubiri kwa watu walio nje ya Kristo, yule Roho aliyeko ndani yake, anaingia ndani ya wale watu ambao wapo nje ya Kristo, na kumsaidia kuhubiri ndani ya mioyo yao…Kwahiyo huyu mhubiri mwenye kigugumizi na asiyejua kuongea vizuri, labda pengine atazungumza maneno machache tu lakini kwasababu anaye Roho Mtakatifu anayemsaidia kuhubiri katika mioyo ya wale wenye dhambi upande wa pili…unakuta wale wenye dhambi kuna nguvu ndani yao inayowashawishi mara mbili zaidi watubu waache dhambi, watajikuta hata hawategemei tena maneno ya yule mhubiri, lakini ile nguvu ndani yao inaanza kuwahubiria dhambi na kuhukumu maisha yao ya dhambi……
Sasa hicho kitendo cha wenye dhambi kusikia kama wanahubiriwa kwa nguvu mara mbili Zaidi katika mioyo yao zaidi ya wanavyosikia katika masikio ya nje…Huo ndio unaoitwa Msaada wa Roho Mtakatifu kwa yule Mhubiri..Hivyo kitendo hicho tunaweza kukiweka katika sentensi hii..
“Roho Mtakatifu amemsaidia yule Mhubiri, kuwahubiria wale wenye dhambi mioyoni mwao kwa kuugua kusikoweza kutamkika” Matokeo yake wale wenye dhambi wakawahi kukubali kumpa Yesu Maisha yao kuliko yule Mhubiri angekosa huo msaada.
Yohana 16:7 Lakini mimi nawaambia iliyo kweli; yawafaa ninyi mimi niondoke, kwa maana mimi nisipoondoka, huyo Msaidizi hatakuja kwenu; bali mimi nikienda zangu, nitampeleka kwenu. 8 Naye akiisha kuja, huyo atauhakikisha ulimwengu kwa habari ya dhambi, na haki, na hukumu.
Yohana 16:7 Lakini mimi nawaambia iliyo kweli; yawafaa ninyi mimi niondoke, kwa maana mimi nisipoondoka, huyo Msaidizi hatakuja kwenu; bali mimi nikienda zangu, nitampeleka kwenu.
8 Naye akiisha kuja, huyo atauhakikisha ulimwengu kwa habari ya dhambi, na haki, na hukumu.
Sasa endapo huyo Mhubiri angekuwa hana Roho Mtakatifu ndani yake, wale watu mioyoni mwao wasingesikia chochote kinachowahubiria hivyo wangemsikiliza yule mhubiri na kigugumizi chake, na mwisho wa siku wangeishia kumcheka na kumwona anapoteza muda..na wangemwona hajui kuongea wala kujieleza na wasingetubu!..Au hata kama ungekuwa unajua kuongea vizuri na kupangilia maneno na kunukuuu, wangekusifia tu kwamba unajua kuongea vizuri na kwamba ni mhubiri mzuri lakini ndani ya mioyo yao wasingesikia chochote kinachowasukuma wao kutubu dhambi, na hivyo kuishia kupata hasara badala ya faida.
Sasa kwa formula hiyo hiyo, ndiyo Roho Mtakatifu anayotusaidia kuomba mbele za Mungu…Unapoingia magotini kumwomba Mungu, hoja zako wewe zina madhaifu mengi, na wala hazieleweki mbele za Mungu, hata kama umejiona umezipangilia kiasi gani, hata kama umejiona umenukuu maandiko kiasi gani…Lakini kwasababu tu hunaye Roho Mtakatifu, Unakuwa una msaada wa anayekusaidia kuomba upande wa pili, katika moyo wa Mungu.
Sasa Roho Mtakatifu anakusaidia kuzipeleka zile hoja zako mbele za Moyo wa Mungu, kiasi kwamba unanena maneno machache, lakini huku nyuma Roho anayahubiri yale maneno uliyoyanena moyoni mwa Baba mbinguni kwa ufasaha Zaidi, na hivyo kuuchoma na kuugusa moyo wa Mungu kwa namna isiyoweza kutamkika mpaka kufikia kuleta majibu yanayotakiwa. Haleluya!
Huo ndio umuhimu wa Roho Mtakatifu kwa mwaminio yeyote! Tunamhitaji sana Roho Mtakatifu katika mambo yote maana pasipo yeye sisi hatuwezi, ndio maana biblia imemwita “MSAIDIZI” Msaidizi maana yake anatusaidia pale tunapokwama..
Tunaposali tunamhitaji huyu msaidizi, hakuna chuo chochote cha kwenda kusomea jinsi ya kuomba! Roho Mtakatifu pekee yake ndiye anayeweza kutuombea jinsi ipasavyo…Na anatuombea pale tunapoomba! Sio wakati tumelala…hapana! Hata mhubiri anamsaidia kuhubiri pale anapohubiri, sio wakati ambao hahubiri.
Hivyo kama mtu hana Roho Mtakatifu basi umekosa kitu kikubwa sana na cha maana sana, ni heri angekosa utajiri wote wa ulimwengu huu au kukosa kila kitu kuliko kumkosa Roho Mtakatifu..kwasababu Biblia imesema katika Warumi 8:9 kuwa “Mtu yeyote asiye na Roho huyo sio wa Mungu”
Je! Umepokea Roho Mtakatifu?…Au bado unaomba tu bila msaada wake?..Lakini Utauliza nitampokeaje? Jibu lipo ndani ya Biblia Takatifu katika Mstari ufuatao…
Matendo 2:37 “Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu? 38 Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu. 39 Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie”
Matendo 2:37 “Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?
38 Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.
39 Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie”
Fomula ya kumpokea ndiyo hiyo, kutubu kwanza kwa kumaanisha kuacha Maisha ya dhambi kama ulevi, anasa, uasherati, uvutaji sigara, chuki, visasi, utazamaji picha chafu, utukanaji, ulawiti, usagaji, ushoga, ushirikina, uchawi, n.k Kisha ukishatubu kutoka moyoni kabisa na Bwana akiiona Toba yako na Imani yako kuwa ni ya dhati kabisa…ATAKUSAMEHE KABISA! Na baada ya msamaha huo wa Bure utakaoupata hatua inayofuata ni kwenda kutafuta ubatizo sahihi, ambao huo ni wa kuzamishwa mwili wote kwenye maji na kwa JINA LA YESU KRISTO, Kisha baada ya huo Roho Ataingia ndani yako, Msaidizi wetu ambaye ni Zawadi kutoka kwa Baba, ambayo tumepewa sisi na Watoto wetu na wote tutakaowahubiria kumjua yeye.
Hakuna mfariji wa kweli kama ROHO MTAKATIFU.
Bwana akubariki.
Pia kwa Maombezi, Ushauri, Maswali au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba
+225693036618/ +225789001312
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?
MATUNDA 9 YA ROHO MTAKATIFU.
HATUA ZA ROHO MTAKATIFU KATIKA KUTUONGOZA.
JE! KARAMA NI UTHIBITISHO WA KUWA NA MUNGU?
NGURUMO SABA
UNYAKUO.
Rudi Nyumbani:
Print this post
Jinsi Mungu anavyotuhudumia sisi ni tofauti na sisi tunavyoweza kufikiri, Sisi tunatazamia Mungu atatuhudumia kutoka mbinguni, lakini yeye yupo tofauti, msaada wake ameuweka sehemu ya chini sana, ambayo imedharauliwa na wengi, Leo hii ukimwomba Mungu jambo basi toa yale mawazo kwamba atakupa majibu kutoka katika mambo makubwa….Ni kweli matokeo ya majibu yatakuwa makubwa, lakini chanzo cha majibu yako kinaweza kisiwe huko unapokitazamia. Naamani alikuwa mkuu wa majeshi wa Taifa la Shamu, ambalo lilikuwa ni moja ya mataifa makubwa sana enzi zile za wafalme, lakini alisumbuliwa na ukoma kwa muda mrefu sana mpaka siku moja aliposikia kuna nabii wa Mungu Israeli, ambaye ni Elisha, tunaona lakini alipomfuata ili aponywe majibu yake yalikuwa ni tofauti na alivyotazamia. Tusome:
2Wafalme 5:9 “Basi Naamani akaja na farasi wake na magari yake, akasimama mlangoni pa nyumba ya Elisha. 10 Naye Elisha akampelekea mjumbe, akisema, Enenda ukaoge katika Yordani mara saba, na nyama ya mwili wako itakurudia, nawe utakuwa safi. 11 Lakini Naamani akakasirika, akaondoka, akasema, Tazama, nalidhania, Bila shaka atatoka kwangu, na kusimama, na kuomba kwa jina la Bwana, Mungu wake, na kupitisha mkono wake mahali penye ugonjwa, na kuniponya mimi mwenye ukoma. 12 Je! Abana na Farpari, mito ya Dameski, si bora kuliko maji yote ya Israeli? Je! Siwezi kujiosha ndani yake, na kuwa safi? Akageuka, akaondoka kwa hasira. 13 Watumishi wake wakamkaribia, wakamwambia, wakasema, Baba yangu, kama yule nabii angalikuambia kutenda jambo kubwa, usingalilitenda? Je! Si zaidi basi, akikuambia, Jioshe, uwe safi? 14 Ndipo akashuka, akajichovya mara saba katika Yordani, sawasawa na neno lake yule mtu wa Mungu; nayo nyama ya mwili wake ikarudi ikawa kama nyama ya mwili wa mtoto mchanga, akawa safi.”
2Wafalme 5:9 “Basi Naamani akaja na farasi wake na magari yake, akasimama mlangoni pa nyumba ya Elisha.
10 Naye Elisha akampelekea mjumbe, akisema, Enenda ukaoge katika Yordani mara saba, na nyama ya mwili wako itakurudia, nawe utakuwa safi.
11 Lakini Naamani akakasirika, akaondoka, akasema, Tazama, nalidhania, Bila shaka atatoka kwangu, na kusimama, na kuomba kwa jina la Bwana, Mungu wake, na kupitisha mkono wake mahali penye ugonjwa, na kuniponya mimi mwenye ukoma.
12 Je! Abana na Farpari, mito ya Dameski, si bora kuliko maji yote ya Israeli? Je! Siwezi kujiosha ndani yake, na kuwa safi? Akageuka, akaondoka kwa hasira.
13 Watumishi wake wakamkaribia, wakamwambia, wakasema, Baba yangu, kama yule nabii angalikuambia kutenda jambo kubwa, usingalilitenda? Je! Si zaidi basi, akikuambia, Jioshe, uwe safi?
14 Ndipo akashuka, akajichovya mara saba katika Yordani, sawasawa na neno lake yule mtu wa Mungu; nayo nyama ya mwili wake ikarudi ikawa kama nyama ya mwili wa mtoto mchanga, akawa safi.”
Unaona, hata leo watu wengi wamemwomba Mungu awafanyie mambo Fulani Fulani katika maisha yao, wengine wanayo magonjwa yanawasumbua wengine ni matatizo, lakini walipofika kwa Mungu waliposikia kuna maagizo Fulani ya kuzingatia, kwamba wanapaswa waokoke kwanza wao wanapuuzia, kwamfano biblia inaagiza kila mmoja anapaswa abatizwe kwa kuzamishwa katika maji mengi ili apate ondoleo la dhambi zake…
Lakini mtu akisikia hivyo utaona anaanza kutoa udhuru, wakitoa tafsiri zao, aah! Ubatizo haumpeleki mtu mbinguni!, Ubatizo hauondoi dhambi kinachoondoa dhambi ni damu ya YESU, wengine watasema, dini yetu haituagizi hivyo, wengine watasema batizo zote ni sawa za kunyunyiziwa na za kuzamwishwa ni sawa, wengine watasema nenda mto Yordani na wewe ukabatizwe kama Bwana Yesu ndio tujue kuwa kweli umebatizwa ipasavyo n.k Mtu huyo huyo pia atakuwa tayari kwenda kila mwisho wa wiki kuogelea baharini au kwenye mabwawa ya starehe kwa masaa mengi bila hata kukinai wala kuchoka, lakini kuingia katika yale maji kubatizwa mara moja tu katika jina la Bwana Yesu, ni vita! Ujue ni roho ya namna gani ipo ndani ya mtu wa namna hiyo!
Na mtu huyu huyu bado anasema ameokoka, na amekaa katika wokovu kwa miaka mingi..Nataka nikuambie kitendo cha kubatizwa kinaweza kisiwe na maana sana kwako, lakini kina maana kubwa sana kwa YESU aliyetoa maagizo hayo..
Unatazamia uwekewe mikono lakini Bwana anakwambia kashuke kwenye yale maji nawe utapona!….Unatazamia Bwana akwambie funga masaa mengi na uombe watu wakuombee au utoe sadaka nyingi….lakini Bwana anakupa maagizo marahisi tu, jishushe kafanye ibada ya kuwaosha miguu watakatifu nawe utaona matokeo makubwa tu!….wapo wengine wanasema kushiriki meza ya Bwana au kutawadhana miguu watakatifu havina maana yoyote, lakini Bwana Yesu alisema Heri ninyi mkiyafanya hayo.
Yohana 13:14 Basi ikiwa mimi, niliye Bwana na Mwalimu, nimewatawadha miguu, imewapasa vivyo kutawadhana miguu ninyi kwa ninyi. 15 Kwa kuwa nimewapa kielelezo; ili kama mimi nilivyowatendea, nanyi mtende vivyo. 16 Amin, amin, nawaambia ninyi, Mtumwa si mkuu kuliko bwana wake; wala mtume si mkuu kuliko yeye aliyempeleka. 17 Mkiyajua hayo, heri ninyi mkiyatenda”.
Yohana 13:14 Basi ikiwa mimi, niliye Bwana na Mwalimu, nimewatawadha miguu, imewapasa vivyo kutawadhana miguu ninyi kwa ninyi.
15 Kwa kuwa nimewapa kielelezo; ili kama mimi nilivyowatendea, nanyi mtende vivyo.
16 Amin, amin, nawaambia ninyi, Mtumwa si mkuu kuliko bwana wake; wala mtume si mkuu kuliko yeye aliyempeleka.
17 Mkiyajua hayo, heri ninyi mkiyatenda”.
Wewe utajiona na hadhi yako, huwezi kushika miguu ya mwingine na kuiosha, Bwana Yesu aliyekuwa ni Mungu katika mwili lakini alifanya hivyo, mimi na wewe ni nani tusifanye?..yeye aliiosha miguu ya wavuvi, sisi ni nani tusioshane miguu?..
Sasa Maagizo ya msingi kama hayo mtu hataki kuzingatia anategemea vipi Mungu atampatia haja yake kwa haraka, kama anavyotaka yeye?..anatazamia aambiwe njoo nunua maji ya upako, au awekewe mikono na watumishi, au afunge na kuomba,..akidhani hayo ndio maagizo sahihi ya Mungu kama Naamani alivyofikiri kumbe sio. Wayahudi walimtazamia MASIHI wao atakuja kama mfalme mkuu sana, ambaye ataketi katika kiti cha enzi cha Daudi pale Israeli na kuwapigania dhidi ya maadui zao Warumi, lakini alipokuja katika familia ya kimaskini walipoteza shabaha, alipokuja hashiki silaha bali anahubiri upendo walimkosa, walipomuona amesulibiwa msalabani ndipo wakasema kabisa huyu amelaaniwa, lakini hawakujua kuwa Yule ndio Mungu mwenyewe aliyeuvaa mwili anaishi na sisi.
Vivyo hivyo na sisi tukitaka Mungu atuhudimie tunapaswa tujishushe, na kujishusha kwenyewe ni kuyatii maagizo yake mepesi aliyotupa, tusijione sisi ni wa rohoni sana, au tunajua zaidi yake mpaka tukadharau anachotuelekeza kufanya..Soma biblia ili ufahamu ukweli, na ukisha ujua ukweli basi uwe tayari kubadilika bila kujali dini yako au dhehebu lako linaamini vipi, na hiyo ndio dalili kubwa itakayokutambulisha kuwa ROHO WA MUNGU hajazimika bado ndani yako, ikiwa upo tayari kuyatii maagizo yake yote sawasawa na maandiko yanavyotulekeza.
Biblia inasema: “Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa”. (Ufunuo 2:7)
Maran Atha.
ALIYE MKUU KATIKA UFALME WA MBINGUNI.
JINSI YA KUITUMIA VYEMA NEEMA YA MUNGU ILIYO JUU YANGU.
NGUVU ZA ZAMANI ZIJAZO:
MWISHO WA HAO WAMSAHAUO MUNGU.
SIRI YA MUNGU.
BABA YANGU ANATENDA KAZI HATA SASA!
Katika biblia nzima hakuna mahali utaona pametabiriwa kwa wazi kuwa Kristo atakaa kaburini siku tatu, na baada ya siku ya tatu atafufuka. Hakuna mahali popote kwenye Biblia palipoandikwa ufunuo huo…Tunaona unabii wa Kristo kuzaliwa na Bikira uliandikwa wazi katika Isaya 7:14 kwamba atazaliwa na Bikira, kadhalika unabii wa Kristo kuzaliwa Bethlehemu ya Uyahudi ulitabiriwa wazi katika kitabu cha Mika.
Mika 5: 2 “Bali wewe, Bethlehemu Efrata, uliye mdogo kuwa miongoni mwa elfu za Yuda; kutoka kwako wewe atanitokea mmoja atakayekuwa mtawala katika Israeli; ambaye matokeo yake yamekuwa tangu zamani za kale, tangu milele”…
Kadhalika unabii wa Bwana Yesu kuteswa kwa ajili ya dhambi zetu uliandikwa wazi katika Isaya
Isaya 53:4 “Hakika ameyachukua masikitiko yetu, Amejitwika huzuni zetu; Lakini tulimdhania ya kuwa amepigwa, Amepigwa na Mungu, na kuteswa. 5 Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona”.
Isaya 53:4 “Hakika ameyachukua masikitiko yetu, Amejitwika huzuni zetu; Lakini tulimdhania ya kuwa amepigwa, Amepigwa na Mungu, na kuteswa.
5 Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona”.
Na Nabii nyingine Nyingi zimuhusuzo Yesu ziliandikwa wazi hata za kuja kwake mara ya pili…Lakini katika unabii wa kukaa kaburini siku tatu, huo haukuandikwa wazi..Uliihitaji Ufunuo wa kipekee wa Roho ili kuujua…Kwasababu Yesu mwenyewe alisema ilipaswa yote yatimie yaliyoandikwa na Manabii, Torati na Zaburi. Na pia ulipaswa utimie unabii alioandikiwa yeye kuhusu kukaa kaburini siku tatu.
Luka 24:44 “ Kisha akawaambia, Hayo ndiyo maneno yangu niliyowaambia nilipokuwa nikali pamoja nanyi, ya kwamba ni lazima yatimizwe yote niliyoandikiwa katika TORATI YA MUSA, NA KATIKA MANABII NA ZABURI. 45 Ndipo akawafunulia akili zao wapate kuelewa na maandiko. 46 Akawaambia, NDIVYO ILIVYOANDIKWA, KWAMBA KRISTO ATATESWA NA KUFUFUKA SIKU YA TATU;”
Luka 24:44 “ Kisha akawaambia, Hayo ndiyo maneno yangu niliyowaambia nilipokuwa nikali pamoja nanyi, ya kwamba ni lazima yatimizwe yote niliyoandikiwa katika TORATI YA MUSA, NA KATIKA MANABII NA ZABURI.
45 Ndipo akawafunulia akili zao wapate kuelewa na maandiko.
46 Akawaambia, NDIVYO ILIVYOANDIKWA, KWAMBA KRISTO ATATESWA NA KUFUFUKA SIKU YA TATU;”
Sasa ni wapi palipotabiriwa kuwa Kristo atakaa kaburini siku tatu?
Pasipo ufunuo wa Roho hakuna mtu angejua kuwa Yesu Kristo alitabiriwa hayo, hata Wanafunzi wa Yesu walikuwa hawajui, si Zaidi Mafarisayo..Lakini tunaona Roho Mtakatifu mwenyewe alifichua fumbo hilo na kutuonesha sisi katika maandiko kuwa ni wapi Kristo alitabiriwa kukaa siku tatu kaburini…tunasoma katika..
Mathayo 12:39 “Akajibu, akawaambia, Kizazi kibaya na cha zinaa chatafuta ishara, wala hakitapewa ishara, ila ishara ya nabii Yona. 40 Kwani kama vile Yona alivyokuwa siku tatu mchana na usiku katika tumbo la nyangumi, hivyo ndivyo Mwana wa Adamu atakavyokuwa siku tatu mchana na usiku katika moyo wa nchi”
Mathayo 12:39 “Akajibu, akawaambia, Kizazi kibaya na cha zinaa chatafuta ishara, wala hakitapewa ishara, ila ishara ya nabii Yona.
40 Kwani kama vile Yona alivyokuwa siku tatu mchana na usiku katika tumbo la nyangumi, hivyo ndivyo Mwana wa Adamu atakavyokuwa siku tatu mchana na usiku katika moyo wa nchi”
Unaona? Kumbe Maisha ya Yona yalikuwa ni UFUNUO WA YESU KRISTO kukaa kaburini siku tatu?? Nani alikuwa analijua hilo?? Hata Yona mwenyewe alikuwa halijui.
Sasa kama Maisha ya Yona yalikuwa yamebeba siri nzito namna ile, inayomhusu Yesu….ya Yusufu yatakuaje? Ya Musa yatakuaje?, ya Ayubu na Danieli yatakuwaje?..Tunamhitaji Roho Mtakatifu atufunulie maandiko tuweze kumwelewa. Hakika pasipo yeye hatutaelewa chochote katika maandiko.
Yohana 14:26 “Lakini huyo Msaidizi, huyo Roho Mtakatifu, ambaye Baba atampeleka kwa jina langu, atawafundisha yote, na kuwakumbusha yote niliyowaambia”.
Ukisoma tena katika maandiko utaona Bwana YESU alikuwa yupo tayari kutueleza pia mambo ya mbinguni, lakini kwa kutokuamini kwetu, hakutueleza(Yohana 3:12),.. Lakini Kristo mwenyewe aliahidi kuwa huyo Roho Mtakatifu atakapokuja atayatwaa yaliyo yake na kutupasha sisi habari,(Yohana 16:14).
Umeona umuhimu wa kuwa na Roho Mtakatifu sasa?, Swali ni Je! Umempata?..Na hata kama unaye je! amejaa kwa wingi ndani yako? Bwana atusaidie!
Kama hujampa Yesu Kristo Maisha yako, mlango wa Neema bado upo wazi, lakini hautakuwa hivyo siku zote.Tubu kwa kumaanisha kuacha dhambi kama hujatubu, na zingatia kutafuta ubatizo sahihi, wa kuzama mwili wote majini na kwa jina la Yesu Kristo kulingana na Matendo 2:38. Na yeye mwenyewe atakupa kipawa cha Roho Mtakatifu bure kama alivyoahidi katika Neno lake kwa wale wote waaminio.
Maran atha!
UMUHIMU WA ROHO MTAKATIFU KATIKA KUZAA MATUNDA.
JE! HIZI ROHO SABA ZA MUNGU NI ZIPI? NA JE ZINATOFAUTIANA NA ROHO MTAKATIFU?
DHAMBI YA KUMKUFURU ROHO MTAKATIFU NI IPI?
UKIAMINI NA UKIMKIRI YESU KWA KINYWA CHAKO, UTAOKOKA.
JE! BIKIRA MARIA NI MALKIA WA MBINGUNI?
1Wafalme 21:1 “Ikawa baada ya hayo, Nabothi Myezreeli alikuwa na shamba la mizabibu katika Yezreeli, karibu na nyumba ya kifalme ya Ahabu mfalme wa Samaria. 2 Ahabu akasema na Nabothi, akamwambia, Nipe shamba lako la mizabibu nilifanye shamba la mboga, maana ni karibu na nyumba yangu; nami nitakupa badala yake shamba la mizabibu lililo zuri zaidi; au ukipenda, nitakupa fedha sawasawa na thamani yake. 3 Nabothi akamwambia Ahabu, BWANA APISHE MBALI NIKUPE WEWE URITHI WA BABA ZANGU. 4 Basi Ahabu akaenda nyumbani kwake, ana moyo mzito, tena amekasirika, kwa sababu ya neno lile aliloambiwa na Nabothi Myezreeli, akisema, Sitakupa urithi wa baba zangu. Akajilaza kitandani pake, akageuza uso wake, akakataa kula”.
1Wafalme 21:1 “Ikawa baada ya hayo, Nabothi Myezreeli alikuwa na shamba la mizabibu katika Yezreeli, karibu na nyumba ya kifalme ya Ahabu mfalme wa Samaria.
2 Ahabu akasema na Nabothi, akamwambia, Nipe shamba lako la mizabibu nilifanye shamba la mboga, maana ni karibu na nyumba yangu; nami nitakupa badala yake shamba la mizabibu lililo zuri zaidi; au ukipenda, nitakupa fedha sawasawa na thamani yake.
3 Nabothi akamwambia Ahabu, BWANA APISHE MBALI NIKUPE WEWE URITHI WA BABA ZANGU.
4 Basi Ahabu akaenda nyumbani kwake, ana moyo mzito, tena amekasirika, kwa sababu ya neno lile aliloambiwa na Nabothi Myezreeli, akisema, Sitakupa urithi wa baba zangu. Akajilaza kitandani pake, akageuza uso wake, akakataa kula”.
Katika agano la kale ilikuwa ni sheria hakuna mtu yeyote kuuza shamba la familia au ukoo, vitu vingine vyote viliweza kuuzwa lakini linapokuja suala la shamba la urithi ni utaratibu uliokuwepo hakuna mtu yeyote kuuza shamba hilo haijalishi kafilisika au halitumii, hata sasa kwenye jamii zetu nyingi mambo kama hayo tunayaona, mtu ukiuza shamba la ukoo, anaweza akatengwa kama sio kufukuzwa kabisa na ndivyo ilivyokuwa hata katika desturi za wayahudi..
Hapa tunaona mtu mmoja wa kawaida tu aliyeitwa Nabothi alikuwa na shamba lake lililokuwa karibu sana na hekalu la Raisi wake, Ahabu..Hiyo inatupa picha kamili kuwa shamba hilo lilikuwa ni lenye thamani nyingi sana, kama angekuwa ni mtu mwenye tamaa basi angeliuza kwa gharama kubwa sana, kiasi kwamba angepata pesa ya kununua mashamba mengine kama yale hata zaidi ya 10 mahali pengine na bado angebakiwa na pesa na kujenga na kula katika maisha yake yote na familia yake…
Shamba hilo ni wazi kuwa lilikuwa zuri sana, kiasi cha kwamba lilimfanya hata mfalme Ahabu akose usingizi kwa kunyimwa kuuziwa shamba lile na mmiliki mwenyewe Nabothi, Sio kwamba Nabothi alipenda kumdharau mfalme, au hakuwa na shida na mali hapana, lakini alijua kuwa shamba la urithi haliuuzwi, haijalishi ni nani amesimama mbele yake, ni mkuu,au sio mkuu, ni tajiri au sio tajiri, kanuni ni ile ile shamba la urithi haliuzwi… Nabothi alikuwa tayari kufa lakini sio kuachia shamba lile liende nje ya ukoo wake. Ukiendelea kusoma pale utaona mpaka Yezebeli anamuundia visa auawe ili alichukue shamba lile.
Biblia inatuambia mambo hayo yaliandikwa kwa mifano ili kutufundisha sisi, ambao sisi tutakuja kuishi katika agano lililo bora zaidi (1Wakorintho 10:11).. Na sisi pia tunao urithi tulioachiwa na mababa zetu wa Imani (Mitume), na urithi huo si mwingine zaidi ya YESU KRISTO,
1Petro 1:3 “Ahimidiwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, ambaye kwa rehema zake nyingi alituzaa mara ya pili ili tupate tumaini lenye uzima kwa kufufuka kwake Yesu Kristo katika wafu; 4 TUPATE NA URITHI USIOHARIBIKA, usio na uchafu, usionyauka, uliotunzwa mbinguni kwa ajili yenu. 5 Nanyi mnalindwa na nguvu za Mungu kwa njia ya imani hata mpate wokovu ulio tayari kufunuliwa wakati wa mwisho”.
1Petro 1:3 “Ahimidiwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, ambaye kwa rehema zake nyingi alituzaa mara ya pili ili tupate tumaini lenye uzima kwa kufufuka kwake Yesu Kristo katika wafu;
4 TUPATE NA URITHI USIOHARIBIKA, usio na uchafu, usionyauka, uliotunzwa mbinguni kwa ajili yenu.
5 Nanyi mnalindwa na nguvu za Mungu kwa njia ya imani hata mpate wokovu ulio tayari kufunuliwa wakati wa mwisho”.
Unaona mtu yeyote aliyempokea Kristo moja kwa moja tayari, ameupokea Urithi usioharibika ambao ulianza tangu enzi na enzi za mitume Baba zetu ambao hao walikuwa watangulizi wetu waliokuwa tayari hata kufa lakini wasiuuze urithi waliopewa na Mungu mbinguni yaani Kristo maishani mwao, na walipoondoka wakaturithisha na sisi urithi huo huo ambao ni YESU KRISTO Bwana wetu, ili na sisi pia wakati ukifika tuwarithishe Watoto wetu, sasa cha kushangaza leo hii utaona watu wengi wanasema wao ni wakristo, wameokoka, lakini wapo tayari kuuza urithi huu kirahisi rahisi tu, mtu yupo tayari kumwacha Kristo kwa ajili ya mali, yupo tayari kumwacha Kristo kwa ajili ya wazazi, au ndugu, yupo tayari kumwacha Kristo kwa ajili ya mwanamke au mwanaume…Yupo tayari kurudi nyuma ki-wokovu kwa ajili ya rafiki zake, kwa ajili ya wafanyakazi wenzake, kwa ajili ya boss wake, kwaajili ya ujana wake, kwaajili ya umaarufu wake…Kirahisi rahisi tu, jambo lolote likijitokeza ambalo anaona kabisa ni kinyume na imani yake yupo tayari kuacha mara moja, akidhani kuwa Imani hiyo akishaichia ipo siku ataipata tena,,Ndugu yangu usidanganyike biblia inatumbia IMANI hii tuliyonayo tunakabidhiwa mara moja tu, hakuna cha mara mbili wala mara tatu..soma…
Yuda 1:3 “Wapenzi, nilipokuwa nikifanya bidii sana kuwaandikia habari ya wokovu ambao ni wetu sisi sote, naliona imenilazimu kuwaandikia, ili niwaonye kwamba mwishindanie imani waliyokabidhiwa watakatifu mara moja tu”.
Na hiyo ndio inatufanya tuwe makini sana kuilinda kwasababu tukishaipoteza kuipata tena ni ngumu..
Ni sawa na mtu anayeliuza shamba, akishaliuza mara moja, basi hatakaa alipate tena milele, linakuwa ni milki halali ya mtu mwingine..Vivyo hivyo na leo hii wewe unayeuuza wokovu wako kirahisi rahisi tu, unarudi nyuma kirahisi rahisi tu, siku Roho Mtakatifu akiondoka kwako basi ndio moja kwa moja hivyo , hakuna toba hapo.. Umesikia injili mara ngapi lakini bado wiki hii unaompango wa kwenda kuzini, unamfanyia jeuri Roho wa Mungu, unadhani kuna siku itafika utubu…tambua hakuna jambo kama hilo saa ya wokovu ni sasa, jitwike msalaba wako mfuate YESU.
Marko 8:35 “Kwa kuwa mtu atakaye kuiponya nafsi yake, ataiangamiza, na mtu atakayeiangamiza nafsi yake kwa ajili yangu na kwa ajili ya Injili, huyu ataisalimisha. 36 Kwa kuwa itamfaidia mtu nini kuupata ulimwengu wote, akipata hasara ya nafsi yake? 37 Ama mtu atoe nini badala ya nafsi yake? 38 Maana kila mtu atakayenionea haya mimi, na maneno yangu, katika kizazi hiki cha uzinzi na dhambi, Mwana wa Adamu atamwonea haya mtu huyo, atakapokuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika watakatifu”.
Marko 8:35 “Kwa kuwa mtu atakaye kuiponya nafsi yake, ataiangamiza, na mtu atakayeiangamiza nafsi yake kwa ajili yangu na kwa ajili ya Injili, huyu ataisalimisha.
36 Kwa kuwa itamfaidia mtu nini kuupata ulimwengu wote, akipata hasara ya nafsi yake?
37 Ama mtu atoe nini badala ya nafsi yake?
38 Maana kila mtu atakayenionea haya mimi, na maneno yangu, katika kizazi hiki cha uzinzi na dhambi, Mwana wa Adamu atamwonea haya mtu huyo, atakapokuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika watakatifu”.
Ifikie wakati uwe na ujasiri wa kumwambia ibilisi ki-vitendo “Nikupe wewe urithi wa Baba zangu?”..weka mbali mambo ya ulimwengu huu uanze kuulinda urithi wako.
Bwana akubariki sana.
USIONDOE ALAMA YA MPAKA ILIYOWEKWA NA MABABA.
KAMA MWIZI USIKU WA MANANE:
CHUKIZO LA UHARIBIFU.
EDENI YA SHETANI:
CHUKIZO LA UHARIBIFU
YEZEBELI ALIKUWA NANI?
Yohana 16:33 “Hayo nimewaambieni mpate kuwa na amani ndani yangu. Ulimwenguni mnayo dhiki; lakini jipeni moyo; mimi nimeushinda ulimwengu”.
Maneno hayo yalitoka kinywani mwa Bwana wetu YESU KRISTO mwenyewe ambaye yeye hakuwa na dhambi hata moja. Ni mtu aliyependwa na Baba kuliko mtu mwingine yeyote ambaye alishawahi kutokea hapa duniani kwa jinsi tu ule mwenendo wake ulivyokuwa mkamilifu..Mtu ambaye alikuwa akimwomba Mungu jambo lolote anafanyiwa haraka sana, angetaka utajiri wote duniani angepewa, angetaka kuabudiwa angeabudiwa, alikuwa hana shida ya jambo lolote, lakini bado hapa tunaona anawaambia wanafunzi wake “Ulimwenguni mnayo dhiki; lakini jipeni moyo; mimi nimeushinda ulimwengu”…
Hivyo dhiki haijalishi wewe ni mtakatifu kiasi gani, maadamu upo tu duniani utakumbana nazo kwa namna moja au nyingine, dhiki zinazokuja kutokana na Imani yako, kuchukiwa kutengwa, kudharauliwa, kupigwa, kufungwa, kuwindwa, kupungukiwa, kufiwa na ndugu wa karibu, magonjwa n.k.
Lakini pamoja na hayo alituahidi kuwa atakuwa nasi sikuzote hadi ukamilifu wa dahari (Mathayo 28:20)na kwamba hatutajikwaa hata tukitembea katika majaribu mazito namna gani atatembea na sisi kuhakikisha hatuanguki, kama tu bado tutakuwa katika wokovu.
Zaburi 34:7 “Malaika wa Bwana hufanya kituo, Akiwazungukia wamchao na kuwaokoa”.
Zaburi 91:11 “Kwa kuwa atakuagizia malaika zake Wakulinde katika njia zako zote. 12 Mikononi mwao watakuchukua, Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe”.
Zaburi 91:11 “Kwa kuwa atakuagizia malaika zake Wakulinde katika njia zako zote.
12 Mikononi mwao watakuchukua, Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe”.
Na ndio maana akatuambia hapo TUJIPE MOYO. Kama yeye ameyashinda, basi tuwe na uhakika kuwa na sisi tutayashinda kwasababu yeye yupo pamoja na sisi kutusaidia..Kwahiyo ndugu yangu mkristo, uliyeokoka ambaye upo katika tumaini la kumngojea Bwana, nataka nikuambie usifadhaishwe na dhiki ya aina yoyote mbele yako wewe JIPE MOYO, aliye ndani yako hawezi kukuacha. Hakumwacha Danieli katika tundu la Simba, hawezi kukuacha na wewe, kukutana na simba haikumaanisha ndio mwisho wa kila kitu, wewe kukutana na dhiki haimaanishi ndio mwisho wako umefika, jipe moyo tu, hakuwaacha akina Shedraka, Meshaki na Abadnego katika tanuru la moto mkali namna ile hatoweza kukuacha na wewe..Hakumwacha Yusufu katika dhiki zile kule gerezani milele ulifika wakati akamfariji hatakuacha na wewe. Ikiwa bado unaishikilia imani yako, na kudhamiria kweli kweli kumfuata Kristo bila kigugumizi.
Wakati wako utafika mawimbi yote yatakwisha, lakini maadamu upo sasahivi katika hali hiyo liweke hili Neno moyoni, JIPE MOYO, JIPE MOYO, JIPE MOYO…Bwana yu pamoja nawe..USHINDI NI LAZIMA. Kama yeye alivyoshinda hivyo SONGA MBELE..
Maran Atha!
JIPE MOYO.
BADO KITAMBO KIDOGO HAMNIONI
VIUNO VYENU VIWE VIMEFUNGWA NA TAA ZENU ZIWE ZINAWAKA.
WACHUNGAJI WA BWANA MAKONDENI.
VITA BADO VINAENDELEA.
TUKAZE MWENDO ILI TUUFIKILIE UTIMILIFU.
Luka 13:32 “Akawaambia, Nendeni, mkamwambie yule mbweha, Tazama, leo na kesho natoa pepo na kuponya wagonjwa, siku ya tatu nakamilika.
33 Pamoja na hayo imenipasa kushika njia yangu leo na kesho na kesho kutwa; kwa kuwa haimkini nabii aangamie nje ya Yerusalemu”.
ULE MSALABA UNAOWEKWA KWENYE KABURI, NA ILE IBADA INAYOFANYWA VINA UMUHIMU WOWOTE KWA MKRISTO?
KIFAA BORA CHA MATUMIZI.
JE! MBINGUNI KUNA MALAIKA WA KIKE?. NA JE! TUKIFIKA MBINGUNI TUTAFANANA WOTE?
TOBA IGUSAYO MOYO WA BWANA.
NG’OMBE MWEKUNDU ALIYEZALIWA ISRAELI, ANAFUNUA NINI?
Kuna tofauti kati ya kuwaza na kutafakari, kuwaza ni kitendo cha kurudia rudia kwenye akili yako ile kumbukumbu ambayo tayari unayo, kwa mfano labda mtu kutwa nzima alikuwa yupo sokoni anatafata mboga nzuri ya kununua….Sasa wakati yupo katika utulivu ametulia anajikuta akili yake inaanza kufikiria yale mambo ambayo alikuwa anayaona, aina za mboga, nafaka, matunda n.k…yaani mtu huyo akili yake inakuwa inazunguka kwenye kile tu alichokiona..
Lakini kutafakari ni tofauti na kuwaza, Kutafakari sio tu kurudia rudia kwenye akili kile ulichokiona au kukifanya, hapana bali kwenda mbali zaidi ni kitendo cha kutathimini kwa undani vile ulivyoviona..kwamfano tuchukue ule ule mfano wa sokoni, mtu anayetafakari anajiuliza maswali mengine kichwani kwake, Je! Zile mbona zinatolewa wapi? Mbona sizioni zikilimwa mkoani kwetu, atajiuliza lile soko kwanini limewekwa pale, na kwanini aina ile ya nafaka inauzwa na watu wengi zaidi, je! Wanunuzi wa hapa ni watu wa aina gani, Je kazi wanaoifanya hapa inawalipa vizuri? n.k..,Sasa mtu anayewaza kwa namna hiyo, huyo ndiye anayetafakari , na utaona mtu wa namna hiyo mwishowe huwa anakuja na suluhisho lilio bora zaidi, pengine na yeye utamwona siku moja pale sokoni amekuwa muuzaji.
Vivyo hivyo na katika biblia, tunapaswa tulitafakari Neno la Mungu, na sio kuliwaza tu, tunaposoma biblia tunapaswa tujiulize je! Hii hadithi inafunua nini rohoni?, Je! Tafsiri yake katika maisha yetu ni nini, Mungu hapa alikuwa na maana gani kusema hivi, ni kwanini afanye vile, na asifanya hivi,,Sasa mtu unapokuwa katika hali ya maswali na namna hiyo katika kusoma kwako biblia, mawazo yako yanapata kibali mbele za Mungu na ndipo Roho Mtakatifu anachuka nafasi ndani yake kukufundisha na kukumfunulia..
Zaburi 19: 14 “Maneno ya kinywa changu, NA MAWAZO YA MOYO WANGU, Yapate kibali mbele zako, Ee Bwana, Mwamba wangu, na mwokozi wangu”.
Tofauti na Yule ambaye anasoma tu hadithi labda tuseme ile ya YONA jinsi alivyomezwa na samaki, anatoka pale anaifurahia ile hadithi anaiwaza tu juu juu jinsi alivyomezwa na samaki Yule na jinsi alivyotapikwa halafu basi ile hadithi inabakia tu kichwani kwake kama kumbukumbuku, hakuna kingine chochote za ziada anaweza kujiuliza juu ya hilo. Mtu kama huyo Neno la Mungu litabakiwa kuwa fumbo kubwa ndani yake, japo anaweza kujiona anaifahamu biblia nzima. .. Lakini kama mtu akiitafakari kwa undani ndipo hapo Roho Mtakatifu anampa ufunuo mkubwa kama ule wa YESU kukaa kaburini siku tatu kwa kupitia tu kuitafakari habari ya Yona.
Halikadhalika Bwana Yesu aliposema yatafakarini maua, watafakarini kunguru..(Luka 12:24) Ni zaidi ya kuwaangalia tu wanavyoruka, bali jinsi wanavyoishi, wanavyokula bila kupanda, bila kuvuna, wasivyojiwekea hazina ghalani, wasivyomeza vidonge n.k. Hivyo tukiweza kutafakari Neno la Mungu kwa namna hiyo Roho Mtakatifu hatapata shida kutufunulia siri zake kiwepesi.
Ni wajibu wetu kulitafakari Neno lake kila siku.
Ubarikiwe sana.
TABIA YA KIPEKEE USIYOIJUA KUHUSU NENO LA MUNGU.
NENO LA MUNGU KATIKA UTIMILIFU WOTE.
JE! KUBET NI DHAMBI?
NYOTA ZIPOTEAZO.
HATARI YA KUTOKUITAFAKARI BIBLIA VIZURI?
TABIA ZA ROHONI.
Ufunuo 17:3 “Akanichukua katika Roho hata jangwani, nikaona mwanamke, ameketi juu ya mnyama mwekundu sana, mwenye kujaa majina ya makufuru, mwenye vichwa saba na pembe kumi. 4 Na mwanamke yule alikuwa amevikwa nguo ya rangi ya zambarau, na nyekundu, amepambwa kwa dhahabu, na kito cha thamani, na lulu, naye alikuwa na kikombe cha dhahabu mkononi mwake, kilichojawa na machukizo, na machafu ya uasherati wake. 5 Na katika kipaji cha uso wake alikuwa na jina limeandikwa, la siri, BABELI MKUU, MAMA WA MAKAHABA NA MACHUKIZO YA NCHI. 6 Nikamwona yule mwanamke amelewa kwa damu ya watakatifu, na kwa damu ya mashahidi wa Yesu. Nami nilipomwona nikastaajabu ajabu kuu”
Ufunuo 17:3 “Akanichukua katika Roho hata jangwani, nikaona mwanamke, ameketi juu ya mnyama mwekundu sana, mwenye kujaa majina ya makufuru, mwenye vichwa saba na pembe kumi.
4 Na mwanamke yule alikuwa amevikwa nguo ya rangi ya zambarau, na nyekundu, amepambwa kwa dhahabu, na kito cha thamani, na lulu, naye alikuwa na kikombe cha dhahabu mkononi mwake, kilichojawa na machukizo, na machafu ya uasherati wake.
5 Na katika kipaji cha uso wake alikuwa na jina limeandikwa, la siri, BABELI MKUU, MAMA WA MAKAHABA NA MACHUKIZO YA NCHI.
6 Nikamwona yule mwanamke amelewa kwa damu ya watakatifu, na kwa damu ya mashahidi wa Yesu. Nami nilipomwona nikastaajabu ajabu kuu”
Kuna Maswali machache hapo ya kujiuliza;
1.Kwanini Yohana alichukuliwa katika Roho mpaka jangwani na si mpaka msituni…Ni wazi kuwa roho iliyopo jangwani si roho ya Mungu bali ya yule Adui..Kwasababu Bwana Yesu alisema katika Mathayo 12:43 “Pepo mchafu, amtokapo mtu, hupitia mahali pasipo maji, akitafuta mahali pa kupumzika, asipate”. Mahali pasipo maji ni jangwani…Hivyo Yohana alichopelekwa kukiona jangwani ni roho ya yule Adui.
2. Swali la pili; Kwanini jambo la kwanza Yohana kuliona ni mwanamke?..Maana alimwona mwanamke na alipomtazama vizuri akamwona ameketi juu ya mnyama mwekundu…Hiyo ikifunua lengo kubwa la yeye kupelekwa huko ni kumwona huyo mwanamke. Na huyo Mwanamke ni nani? na anaonekana amelewa!..Huyo Si mwingine zaidi ya kanisa fulani ambalo tutakuja kuliona mbeleni kidogo. Kwasababu katika maandiko mwanamke anawakilisha kanisa (Waefeso 5:31-32, 2Wakoritho 11:2, Ufunuo 21:9,)
3. Jambo lingine ni kwanini Mnyama aliyempanda huyo mwanamke alikuwa mwekundu sana?..Rangi nyekundu siku zote inaashiria damu!..yaani umwagikaji wa damu! Maana yake huyo mnyama ni mwuuaji…Tengeneza picha Mtu aliyelewa amepanda simba na huku anachupa yake mkononi ya pombe, halafu anazunguka naye mtaani na huyo simba anaonekana ana ghadhabu nyingi, ana meno makali..Utapata picha gani? Ni wazi kuwa utaona huyo mtu kakusudia kudhuru watu kupitia huyo mnyama wake anayemwendesha. Ndivyo huyu mwanamke anavyoonekana hapa.
Hivyo kwa tafsiri yake ni kwamba kanisa hilo linatumia mfumo fulani kuua watu, lilitumia mfumo huo kuua watu katika enzi za zamani, na litatumia huo mfumo kuua watu wakati wa dhiki kuu, huo mfumo ndio mnyama..
4. Jambo la Nne Mwanamke yule katika kipaji cha uso wake ana jina limendikwa kwa siri..kumbuka sio kwa wazi! kwa siri! ikimaanisha hataki ajulikane yeye ni nani? na jina hilo linasomeka BABELI MKUU MAMA WA MAKAHABA NA MACHUKIZO YA NCHI.
Kwanini ni Babeli Mkuu?..Ikimaanisha kuwa kulikuwa na Babeli nyingine zilipita lakini sio KUU, Babeli ile iliyotengeneza mnara ilikuwa ni Babeli lakini sio kuu!..Babeli ya Nebkadneza ilikuwa ni Babeli lakini si kuu!…Hivyo hiyo Yohana aliooneshwa ndio kuu!!
Na kwanini tena ni MAMA WA MAKAHABA?, Ikimaanisha anao watoto ambao nao ni makahaba, na yeye mwenyewe anafanya ukahaba..Na kama yeye ni kanisa ni wazi kuwa waototo wake nao watakuwa ni makanisa na wote wanafanya ukahaba…..Kanisa linalofanya ukahaba kibiblia ni kanisa linaloabudu sanamu, na kuacha sheria za Mungu…Na mwisho inamalizia NA MACHUKIZO YA NCHI…Na sio machukizo ya Mbingu…maaana yake anafanya machukizo akiwa hapa hapa duniani! machukizo ni jambo lolote linalomchukiza Mungu.
Ndugu huyo mwanamke si mwingine zaidi ya KANISA KATOLIKI, Hilo ndio lililohusika kuua zaidi ya wakristo milioni 60 wakati wa kipindi cha giza. Ni kanisa la uongo, lenye kivuli cha ukweli..Na mpinga-Kristo atatokea katika kanisa hilo, na cheo chake kimeshafunuliwa, na hicho si kingine zaidi ya cheo cha PAPA!
Kwa kutumia mfumo wake huo wa kikatili (yaani huyo mnyama) atawaua watu wengi sana katika kipindi cha dhiki kuu, wakati ambao unyakuo utakuwa umeshapita! Wale watakaoachwa watalazimishwa kupokea chapa ya huyo mnyama, na kupewa kila sababu ya kuingia katika lile ziwa la Moto.
Je! Una uhakika wa kwenda kwenye unyakuo ili uepukane na mambo hayo yote? Kuna mambo mengi sana yatatokea mpinga kristo atakayoyafanya katika siku hizi za mwisho tunazoishi, huu ni ufupisho tu.
Maran atha, Bwana wetu anakuja
CHAPA YA MNYAMA NI NINI?
ROHO YA MPINGA KRISTO IKITENDA KAZI SIKU HIZI ZA MWISHO
MPINGA-KRISTO NI NANI?
NITAJUAJE KAMA NDOTO NI YA MUNGU AU YA SHETANI?
WhatsApp
Uthibitisho wa kwanza wa mtu kuwa na Roho Mtakatifu ni Utakatifu atakaouonesha, na Utakatifu kwa ujumla ndio tunda la Roho. Na uthibitisho wa Pili ndio karama aliyo nayo…. Na Mtu Mtakatifu ni lazima aoneshe vitu 9 vifuatavyo..pamoja na vingine vingi, lakini hivi 9 ndio msingi wa UTAKATIFU WA MTU.
Tabia hizi 9 zinapatikana kutoka katika kitabu cha Wagalatia..
Wagalatia 5:22 Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, 23 upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria.
Wagalatia 5:22 Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu,
23 upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria.
Mtu Mwenye Roho Mtakatifu lazima awe navyo hivi vyote kwa pamoja! hapaswi kukosa hata kimoja..kwasababu vyote kwa pamoja ndio vinaitwa TUNDA LA ROHO, na si MATUNDA YA ROHO…Ikiwa na Maana ni lazima viende kwa pamoja.
Ubarikiwe.
FAIDA ZA MAOMBI.
EPUKA KUTOA UDHURU.
JE! NI SAHIHI KUJIPA CHEO MFANO MIGHTY PROPHET, CHIEF APOSTLE N.K?
BIBLIA INAKATAZA KUAPA KABISA, LAKINI KWANINI WATU WANAAPA MAHAKAMA?
Mpagani ni mtu yeyote asiye Mkristo…Mtu yeyote anayeabudu miungu mingine tofauti na Mungu wa Israeli, ambaye anaabudiwa kwa kupitia mwanawe wa pekee Yesu Kristo, mtu huyo ni “Mpagani”…
Mchawi ni mpagani, watu wasio na dini ni wapagani, waabudu miti, mawe, sanamu wote ni wapagani, kadhalika na wakristo-jina wote ni wapagani, na waislamu ni wapagani. Upagani hauna tofauti sana na “ukafiri”
Mtu aliyemwamini Yesu Kristo, na kubatizwa katika ubatizo sahihi na kupokea Roho Mtakatifu, na kuuishia wokovu kulingana na Biblia, yaani kuishi maisha ya utakatifu na ya kumcha Mungu, mtu huyo pekee ndiye ambaye si MPAGANI.
Shalom.
KAFIRI NI NANI?
“HERI WALIO MASKINI WA ROHO MAANA UFALME WA MBINGUNI NI WAO” JE HATUNA RUHUSA YA KUWA MATAJIRI KATIKA ROHO?
BWANA ALIMAANISHA NINI KUSEMA “WAACHE WAFU WAZIKE WAFU WAO“
MATUMIZI YA DIVAI.
ROHO I RADHI, LAKINI MWILI NI DHAIFU.