Category Archive maswali na majibu

Masihi ni nani?

Je! neno Masihi linamaanisha nini?

“Masihi” ni Neno la Kiebrania, linalomaanisha “Mpakwa mafuta” (Yaani mtu aliyeteulewa na Mungu kwa kusudi Fulani). Katika biblia watu walioteuliwa na Mungu rasmi kuwa Wafalme, hao waliitwa masihi wa Bwana, vile vile waliochaguliwa na Mungu kuwa manabii, nao pia waliitwa masihi wa Bwana.

Tafsiri nyingine ya neno Masihi ni “Kristo”. Kwahiyo katika biblia mamasihi (yaani makristo au watiwa mafuta) walikuwa wengi lakini aliyekuwa MASIHI KIKWEKWELI alikuwa ni Mmoja tu! Ambaye ni YESU KRISTO.

Mamasihi wengine ni kweli walipakwa mafuta na Mungu lakini hawakuwa wakamilifu asilimia zote..Daudi alikuwa ni masihi wa Bwana (Soma 1Samweli 16:6-13) lakini hakuwa mkamilifu asilimia zote, kwani aliua na pia alimtwaa mke wa Uria na kumfanya wake.

Vile vile Mfalme Sauli maandiko yanasema alikuwa ni masihi wa Bwana lakini tunasoma alikuja kukengeuka na kumdharau Mungu na maagizo yake..

1Samweli 24:9 “Daudi akamwambia Sauli, Kwa nini unasikiliza maneno ya watu wasemao, Tazama, Daudi anataka kukudhuru?

10 Tazama, leo hivi macho yako yameona jinsi Bwana alivyokutia mikononi mwangu pangoni, na watu wengine wakaniambia nikuue; lakini nikakuacha; nikasema, Sitaki kuunyosha mkono wangu juu ya bwana wangu; kwa maana yeye ni masihi wa BWANA”.

Soma pia 1Nyakati 16:22

Hawa wote walikuwa ni watiwa mafuta lakni walikuwa na kasoro nyingi,  Lakini Yesu Kristo alikuwa ni mkamilifu kuliko hao wote..Kwahiyo yeye ndiye aliyetiwa Mafuta Makuu kuliko wote, ndio maana tunasema aliye Masihi peke yake ni YESU.

Waebrania 1:8 “Lakini kwa habari za Mwana asema, Kiti chako cha enzi, Mungu, ni cha milele na milele; Na fimbo ya ufalme wako ni fimbo ya adili.

9 Umependa haki, umechukia maasi; Kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekutia mafuta, Mafuta ya shangwe kupita wenzio”.

Kwahiyo Wayahudi wote, na wasamaria wote, walikuwa wanautazamia ujio wa huyu Masihi mmoja ambaye atakuwa mkamilifu, asiyekuwa na dhambi hata moja, ambaye atawafundisha sheria za Mungu na kuwaokoa na dhambi zao.

Yohana 4:25 “Yule mwanamke akamwambia, Najua ya kuwa yuaja Masihi, (aitwaye Kristo); naye atakapokuja, yeye atatufunulia mambo yote.

26 Yesu akamwambia, Mimi ninayesema nawe, ndiye”

Yohana 1:40 “Andrea, nduguye Simoni Petro, alikuwa mmoja wa wale wawili waliomsikia Yohana na kumfuata Yesu.

41 Huyo akamwona kwanza Simoni, ndugu yake mwenyewe, akamwambia, Tumemwona Masihi (maana yake, Kristo). .

Huyu Masihi Yesu Kristo, alishakuja miaka zaidi ya elfu 2 iliyopita, akapaa mbinguni, na sasa yupo hai, na pia amekaribia sana kurudi. Atakapokuja hatakuja tena kwa kusudi la wokovu, bali kwa HUKUMU.

Yohana 5:22 “Tena Baba hamhukumu mtu ye yote, bali amempa Mwana hukumu yote”

Je umemwamini Masihi Yesu?.. Umetii agizo lake la ubatizo?, na je umempokea Roho wake Mtakatifu.. Fahamu kuwa kama umekosa vitu hivyo vitatu, bado hujaokolewa kulingana na Neno lake. Hivyo ni vyema ukafanya uamuzi wa kumwamini na kutubu leo na kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo, na mambo mengine yaliyosalia Roho Mtakatifu utakayempokea atakuongoza katika kweli yote.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

ISHARA ITAKAYONENEWA

JUMA LA SABINI (70) LA DANIELI

Je tunaruhusiwa kujipaka mafuta au kujipulizia marashi?

 Je! Ni sahihi kutumia maji ya upako,katika kufanya maombezi?

IFAHAMU HUZUNI NA FURAHA YA MALAIKA.

Rudi nyumbani

Print this post

Miji ya Tiro na Sidoni ni miji gani kwasasa?

Jibu: Tiro na Sidoni ni miji iliyokuwa katika nchi inayoitwa LEBANONI. Tofauti na nchi nyingine ambazo zilibadilika majina baada ya miaka mingi kupita, lakini nchi ya Lebanoni, imeitwa kwa jina hilo hilo tangu nyakati za biblia hata leo.

Tiro na Sidoni ni miji ambayo ipo karibu karibu, (Kusini Mashariki mwa Nchi ya Lebanoni), na miji hii enzi za biblia ilikuwa ni miji ya kibiashara, lakini iliyojaa machukizo mengi.

Kwasasa nchi ya Lebanoni ina miji mikubwa minne, Ambayo ni Beiruti, Tripoli, Sidoni na Tiro.  Mji wa Sidoni ni mkubwa kuliko Tiro na katika Lebanoni ndiko ulipokuwepo pia Mji wa Tarshishi, ule ambao Yona aliukimbilia ili apate kujiepusha na uso wa Bwana.

Kwasasa nchi hii ya Lebanoni inakaliwa na Waarabu, na ni nchi ambayo ipo katika upande wa Kaskazini mwa Israeli,  Eneo kubwa la Nchi ya Lebanoni, ni misitu na ndio huko Mfalme Sulemani alipotolea Miti aina ya Mierezi kwaajili ya ujenzi wa Hekalu la Mungu.

Nchi ya Lebanoni kwasasa ina uadui mkubwa sana na Nchi ya Israeli. Na unabii unaonyesha katika Ezekieli 38 na 39 kuwa siku za mwisho Lebanoni pamoja na nchi za kando kando zitashirikiana na Nchi ya Urusi kwa lengo la kuifuta Israeli katika uso wa dunia, lakini zitapigwa zote, kwasababu Mungu wakati huo atasimama upande wa watu wake  Israeli.

Kwaufupi miji ya Tiro na Sidoni imebeba ufunuo mkubwa katika matukio ndani ya biblia. Kasome Mathayo 11:21-22, Yoeli 3:4, Zekaria 9:1-4, na Matendo 12:20

Lakini lililo kubwa zaidi ni ufunuo mji huo uliobeba, kumhusu shetani.. Biblia inamtaja mkuu wa Mji wa Tiro katika ulimwengu wa roho, kwamba ni shetani mwenyewe.

Ezekieli 28:1 “Neno la Bwana likanijia tena, kusema, 

2 Mwanadamu, mwambie mkuu wa Tiro, Bwana MUNGU asema hivi; Kwa kuwa moyo wako umeinuka, nawe umesema, Mimi ni Mungu, nami nimeketi katika kiti cha Mungu, kati ya bahari; lakini u mwanadamu wala si Mungu, ujapokuwa umeweka moyo wako kama moyo wa Mungu……

13 Ulikuwa ndani ya Adeni, bustani ya Mungu; kila jiwe la thamani lilikuwa kifuniko chako, akiki, na yakuti manjano, na almasi, na zabarajadi, na shohamu, na yaspi, na yakuti samawi, na zumaridi, na baharamani, na dhahabu; kazi ya matari yako na filimbi zako ilikuwa ndani yako; katika siku ya kuumbwa kwako zilitengenezwa tayari. 

14 Wewe ulikuwa kerubi mwenye kutiwa mafuta afunikaye; nami nalikuweka hata ukawa juu ya mlima mtakatifu wa Mungu, umetembea huko na huko kati ya mawe ya moto. 

15 Ulikuwa mkamilifu katika njia zako tangu siku ile ulipoumbwa, hata uovu ulipoonekana ndani yako”.

Na shetani si mkuu tu wa Tiro, bali biblia imezidi kutupa mwangaza kuwa ni mungu wa ulimwengu mzima (2Wakorintho 4:4).. Yaani mifumo yote ya kishetani iliyopo duniani ni yeye muasisi.

Je umempokea Yesu?

Kumbuka hizi ni siku za mwisho na Kristo yupo Mlangoni.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312. Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mada Nyinginezo:

Kwanini Herode aliwakasirikia watu wa Tiro na Sidoni? (Matendo 12:20)

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 5)

Mwerezi ni nini?

Ninawi ni nchi gani kwasasa?

Yerusalemu ni nini?

Rudi nyumbani

Print this post

Je jina Eva na Hawa ni sawa?

Swali: Katika Mwanzo 3:20 na Mwanzo 4:1 mkewe Adamu ni Hawa. Nmekuwa nikisikia mkewe Adamu pia ni Eva. Je! jina Eva na Hawa ni sawa?

Jibu: Hawa na Eva ni jina moja isipokuwa katika lugha mbili tofauti ni sawa na jina YESU na JESUS; ni jina moja isipokuwa katika lugha mbili tofauti, yaani ya kiingereza na ya  kiswahili.

Kadhalika na Eva (au Eve) ni kiingereza na HAWA ni kiswahili chake.

Sasa swali ni kwanini, tafsiri zake zionekane kama mbalimbali, yaani Kutoka Eve mpaka Hawa ni kama hazikaribiani?. Kwanini Eve isingetafsiriwa tu Eva kwa lugha ya kiswahili badala yake ikawa Hawa?

Jibu ni kwamba lugha ya kiswahili sehemu nyingi imeitafsiri herufi “V” kwa “W” katika majina ya watu au vitu. Kwamfano utaona jina “LAWI”, kwa lugha ya kiingereza ni “LEVI”.

Vilevile mji wa “Ninawi” kwa lugha ya kiingereza ni “NINEVEH”n.k

Kwahiyo hata Eva kiswahili chake ni lazima kirudi kwenye herufi “w” na kuwa “Hawa

Ni kama vile majina yote yanayoanza na herufi “J” yanavyobadilika na kuanza na herufi  “Y” yanapokuja katika lugha ya kiswahili…Kwamfano Jina Jesus-Yesu, Jonah-Yona, Joshua-Yoshua, Jezebel- Yezebeli n.k Ndivyo ilivyo kwa majina yote yenye herufi “V”, yalibadilika na kuwa “W” yanapoletwa katika lugha ya kiswahili.

Kwahiyo kwa hitimisho mtu anayetumia Jina Hawa na anayetumia Eva wote wapo sahihi, na wanamlenga mtu mmoja.

Je umempokea Yesu?..je umebatizwa?..je umepokea Roho Mtakatifu?..Kama bado unasubiri nini?. Kumbuka hizi ni nyakati za mwisho na Kristo yupo mlangoni kurudi.

Maran atha!.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya ELOHIMU?

KUMBE MUNGU ANAWEZA KUKULIPA KWA USICHOSTAHILI!

Je! dhambi zote ni sawa Kuna dhambi kubwa na ndogo?

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

Njia zote za mtu ni safi machoni pake mwenyewe;(Mithali 16:2)

Rudi nyumbani

Print this post

“Humfukuza punda wake asiye baba”, nini maana ya mstari huu? (Ayubu 24:3)

Jibu: Tusome kuanzia ule wa 2 ili tuweze kuelewa vizuri.

Ayubu 24:2 “Wako waziondoao alama za mipaka; Huyachukua makundi kwa jeuri na kuyalisha.

3 Humfukuza punda wake asiye baba, Humtwaa rehani ng’ombe wake mwanamke mjane.”.

Hapa Ayubu anazungumzia juu ya kundi la watu wabaya ambao wanawaonea Mayatima na kuwadhulumu wajane.

Ndio hapo anasema wapo (watu duniani) ambao.

1. Wanaondoa alama za Mipaka, na kuyachukua makundi kwa jeuri na kuyalisha.

Maana yake wanawadhulumu watu mashamba/ardhi kwa kuondoa mipaka iliyokuwepo na kuweka mipaka ya uongo!,..na baada ya kumiliki ardhi kwa dhuluma namna hiyo bado wanalisha mifugo yao juu ya hizo ardhi za dhuluma.

2. Humfukuza punda wake asiye baba,

Maana yake humfukuza Punda wa Yatima, (mtoto asiye na Baba). Punda wake anapoingia mahali kula vichache vilivyosalia katika  mashamba yao, wao humfukuza punda Yule, pasipo kuzingatia kuwa Yule ni yatima asiye na uwezo wa kujimudu mwenyewe, asiye na uwezo wa kununulia chakula punda wake, lakini wao hawajali hayo yote, bali wanazifukuza punda zake.

3. Humtwaa rehani ng’ombe wake mwanamke mjane.

Hawa watu pia wanachukua Ng’ombe za wanawake wajane, ambao wamefiwa na waume zao, na hata nguvu za kufanya kazi tena hawana!.. wanachukua Ng’ombe zao na kuwaweka Rehani, kutokana na mikopo wanawake hao waliyoichukua.. Jambo ambalo ambalo si jema machoni pa Mungu..Wangepaswa wawahurumie na kuwapa mikopo bila kuwawekea rehani chochote kwasababu wao hawana tumaini msaada wowote wapo wao kama wao, na umri wao umeshakwenda..

 Kumbukumbu 24:17 “Usipotoshe hukumu ya mgeni, wala ya yatima; wala usitwae mavazi ya mjane, yawe rehani; 

18 bali kumbuka ya kuwa ulikuwa mtumwa katika Misri, Bwana, Mungu wako, akakukomboa huko; kwa hiyo nakuamuru kutenda neno hili”

Hivyo watu wa namna hii ambao wanawatesa Wajane na Mayatima, Bwana Mungu alitaja hukumu yao katika kitabu cha Kutoka 22:22

Kutoka 22: 22 “Usimtese mjane ye yote aliyefiwa na mumewe, wala mtoto yatima.

 23 Ukiwatesa watu hao katika neno lo lote, nao wakanililia mimi, hakika yangu nitasikia kilio chao, 

24 na hasira yangu itawaka moto, nami nitawaua ninyi kwa upanga; na wake wenu watakuwa wajane, na watoto wenu mayatima”.

Hivyo na sisi hatuna budi kuwatendea Mema watu hawa, na kuwapenda ili na Bwana atubariki

Shalom

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Mtu asiye na akili ni nani kibiblia?

Kwanini wajane vijana hawakupaswa kuandikwa?

NI WAPI MAHALI SAHIHI PA KULIPA ZAKA?

TENDA AGIZO LA YESU, HILO NDIO LITAKALOKULINDA.

Nini maana ya “wazimu” katika biblia?

Rudi nyumbani

Print this post

Mikono iliyotakata ni mikono ya namna gani? (1Timotheo 2:8).

Swali: Katika 1Timotheo 2:8 tunaona Mtume Paulo akiwataja wanaume kuwa wanaposalisha wanyanyue mikono iliyotakata, sasa hii mikono iliyotakata ndio mikono ya namna gani?

Jibu: Tusome,

1Timotheo 2:8  “Basi, nataka wanaume wasalishe kila mahali, huku wakiinua mikono iliyotakata pasipo hasira wala majadiliano”

Mikono iliyotakata ni mikono isiyo na “Dosari”..Sasa ili tuelewe mikono isiyo na Dosari ni mikono ya namna gani, hebu tuangalie mikono yenye Dosari ni ipi. Tusome Isaya 1:15-17.

Isaya 1:15 “Nanyi mkunjuapo mikono yenu, nitaficha macho yangu nisiwaone; naam, mwombapo maombi mengi, sitasikia; mikono yenu imejaa damu. 

16 Jiosheni, jitakaseni; ondoeni uovu wa matendo yenu usiwe mbele za macho yangu; acheni kutenda mabaya;

 17 jifunzeni kutenda mema; takeni hukumu na haki; wasaidieni walioonewa; mpatieni yatima haki yake; mteteeni mjane”.

Umeona Mikono yenye dosari ni ipi?.. Ni ile inayomwaga damu, inayoonea wanyonge, inayokula rushwa, mikono inayoabudu sanamu…kwaufupi mwenye dhambi yoyote Yule mikono yake ni michafu, na ina dosari mbele za Mungu.

Kwahiyo tukirudi kwenye biblia hapo maandiko yanaposema kuwa “..wanaume wasalishe kila mahali, huku wakiinua mikono iliyotakata..” imemaanisha kuwa wawapo katika ibada, au kanisani wakiabudu au kuomba, au kumtolea Mungu wahakikishe mikono yao haina hila..sio watu wa kumwaga damu, sio watu wa kula rushwa, sio watu wa kuonea watu n.k Soma pia Zaburi 58:1. Isaya 37:1 na Isaya 59:3, utaona jambo hilo hilo.

Hivyo huo ni ujumbe kwetu wote, kwamba tuitakase mikono yetu.. sio tunakwenda kumfanyia Mungu ibada au kumtolea matoleo na huku mikono yetu ni michafu..Bwana hatazitakabari sadaka zetu kama alivyozikataa zile za Kaini, vile vile tunaponyosha mikono yetu ambayo ina visasi, au ina vinyongo, au ina rushwa, na kumwabudu Mungu kwayo, kibiblia ni machukizo mbele zake.

Yakobo 4:8 “Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi. ITAKASENI MIKONO YENU, enyi wenye dhambi, na kuisafisha mioyo yenu, enyi wenye nia mbili”.

Je umempokea Yesu katika maisha yako?.. Fahamu kuwa Yesu ndiye Njia, Kweli na Uzima.. wala hakuna mtu atakamwona Mungu, pasipo kupitia kwake yeye. Hivyo tubu leo kwa kumaanisha kuziacha dhambi zako na tafuta ubatizo sahihi ambao ni wa maji mengi (Yohana 2:23) na kwa jina la Bwana Yesu Kristo (Matendo 2:38), na Roho Mtakatifu atakuongoza na kukutia katika kweli yote sawasawa na ahadi yake (Yohana 16:13).

Marana atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Biblia inapotumia neno “Bila kazi ya mikono”, ina maana gani?

MIKONO YENU IMEJAA DAMU.

UTAKAPOKUWA MZEE, UTAINYOSHA MIKONO YAKO. NA MWINGINE ATAKUFUNGA

USIZISHIRIKI DHAMBI ZA WATU WENGINE.

FAHAMU JINSI MUNGU NA SHETANI WANAVYOZUNGUMZA NA WATU.

Rudi nyumbani

Print this post

Aibusu midomo atoaye jawabu la haki (Mithali 24:26)

SWALI: Nini maana ya huu mstari?

Mithali 24:26 “Aibusu midomo atoaye jawabu la haki”


JIBU: Kwa namna nyingine inasomeka hivi “ Atoaye jawabu la haki, ni sawa na mtu abusuye mdomo wa rafiki yake”

Kwa tamaduni za kale za kiyahudi, ishara ya kuonyesha upendo wa dhati kwa mtu ilikuwa ni kubusiana midomo, sio kama sasa inavyotumika kama ishara ya mahusiano ya kimwili.

Na ndio maana katika maandiko utaona mitume wanaagiza watakatifu wasalimiane kwa busu takatifu (Warumi 16:16), halikadhalika utaona Yuda alipomsaliti Bwana alimbusu.

Lakini kwa tamaduni zetu, sasa ishara ya upendo ni kupeana mikono, na mahali pengine kukumbatiana, lakini sio kubusiana.

Tukirudi katika mstari, anaposema, ‘atoaye jawabu la haki’ Yaani mtu ‘anapoamua kwa haki’  au ‘anapozungumza ukweli kwa mwenzake, au kwa jirani yake, bila unafiki au upendeleo, , rohoni anatafsirika kama ni mtu ambusuye rafiki yake, mtu ampendaye rafiki yake sana, kwa kumkumbatia au kumpa mkono.

Tofauti na inavyoeleweka. Na wengi, kwamba ukimweleza mwenzako ukweli, ni kuunda uadui. Lakini Bwana wetu hakulijali hilo, ndio maana japokuwa alichukiwa na viongozi wengi wakidini kwa kuwa kwake muwazi (Yohana 8:40-45), lakini leo hii tunauona upendo wa dhati aliokuwa nao kwetu kwa kufanya hivyo.

Nasi pia Bwana atusaidie tuwe na ‘jawabu la haki’ vinywani mwetu. Tudhihirishe upendo wa kweli.

Shalom

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Rafiki hupenda sikuzote; Na ndugu amezaliwa kwa siku ya taabu.

SAUTI NYUMA YA ISHARA.

MAPEPO YANATAFUTA HIFADHI NDANI YAKO KWA BIDII SANA.

NINI TOFAUTI KATI YA MATENDO YA SHERIA NA MATENDO YA IMANI?

Ni nani aliyesema “Nitume mimi”? katika

MIMI SIOMBI KWAMBA UWATOE KATIKA ULIMWENGU.

UNYAKUO WA KANISA UMEPITA LEO!!

Rudi nyumbani

Print this post

Je! Ni Kristo au Kristu? Lipi ni neno sahihi?

JIBU: Neno Kristo limetoka katika lugha ya kigiriki (Khristos) ambalo likitafsiriwa katika Kiswahili linatamkika kama KRISTO.

Lakini Neno hili hili, kwa lugha ya kilatini  (Christus), likitafsiriwa katika Kiswahili linatamkika kama  KRISTU.

Swali ni Je! Ipi ni tafsiri sahihi?

Tufahamu kuwa biblia yetu  (husasani sehemu kubwa ya agano jipya) haikuandikwa katika lugha ya kilatini, au kiingereza, au kichina, au kifaransa.. Hapana bali iliandikwa katika lugha ya Kigiriki ya kale. Hivyo tafsiri ya biblia yetu ya Kiswahili tunaitolea moja kwa moja kutoka katika lugha hiyo ya kigiriki, na sio kiingereza au kilatino.

 Hivyo ni vizuri tukitumia lahaja ya lugha ya asili, iliyotumika kwenye biblia(Kigiriki) kuliko nyingine.

Japo wapo wanaotumia lahaja ya kilatino (Kristu), pia hawafanyi makosa, maadamu ni Kristo Yule Yule analengwa na sio mwingine. Ni sawa na anayesema ‘Sulemani’ au ‘Solomoni’. Ni Yule Yule mlengwa isipokuwa katika lahaja mbili tofauti.

Maana ya Kristo ni “Mtiwa-Mafuta” Ambapo kwa lugha ya kiyahudi anaitwa “MASIHI”. Hivyo tunaposema Yesu Kristo, tunamaanisha Yesu mtiwa mafuta.  Yaani Yesu aliyeteuliwa na Mungu mahususi kwa kazi ya kuwakomboa wanadamu. Ni yeye tu ndiye mwokozi wa ulimwengu wala hapana mwingine.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

JINA LA MUNGU NI LIPI?

Akida ni nani kibiblia, na kazi yake ni ipi? (Mathayo 8:5)

Nini maana ya ELOHIMU?

SEMA KWA LUGHA NYINGINE.

Babewatoto ni nani katika biblia?(Isaya 34:14).

Ni nani aliye kipofu, ila mtumishi wangu?

Mharabu ni nani katika biblia?

Rudi nyumbani

Print this post

Awanyimaye watu nafaka, watu watamlaani

SWALI: Nini maana ya huu mstari?

Mithali  11: 26 “Awanyimaye watu nafaka, watu watamlaani; Auzaye nafaka, baraka itakuwa kichwani pake”.


JIBU: Kuna wakati sukari ilikuwa adimu sana katika taifa letu, baadhi ya wafanyabiashara wakubwa walipoona janga hilo limetokea, wakanunua sukari nyingi, tani kwa matani, wakazificha, hivyo ikaifanya sukari (hata hiyo kidogo iliyokuwepo) kuwa adimu zaidi.. Lengo lao ni sukari izidi kupanda bei ili waiuze kwa bei ya juu sana wapate faida kubwa.

Lakini jambo hili liliwaathiri watu wengi, hususani wafanyabishara wadogo wanaotegemea sukari  kuzalisha bidhaa zao, pamoja na watu wa hali ya chini wasioweza kununua sukari kwa bei ya juu. Matokeo yake ikawa ni watu kulaumu na kuwakasirikia sana wanaofanya vitendo hivyo.

Au wakati ambapo maji ni adimu, baadhi ya watu hupadisha bei, kwa lengo la kujipatia faida kubwa zaidi, watakaa na maji yao kwenye visima mpaka atakapotekea mwenye bei kubwa. Watu wa namna hii ukichunguza utaona wanaishia kulaaniwa sana na watu wanaowazunguka.

Ndio maana ya huo mstari “Awanyimaye watu nafaka, watu watamlaani; Auzaye nafaka, baraka itakuwa kichwani pake”..

watu watampenda na kumbariki Yule ambaye atawauzia huduma yake kama ilivyo desturi ya sikuzote.

1Yohana 3:17  “Lakini mtu akiwa na riziki ya dunia, kisha akamwona ndugu yake ni mhitaji, akamzuilia huruma zake, je! Upendo wa Mungu wakaaje ndani yake huyo?”

Na rohoni pia ni vivyo hivyo,..Wakati tuliopo sasa maandiko yalitabiri ni wakati wa njaa kubwa sana ya kiroho, watu wakizunguka huko na kule kutafuta Neno la kweli la Mungu (Amosi 8:11-12). Lakini inasikitisha kuona baadhi ya watu wakificha maarifa, au huduma, kisa tu, hawalipwi vizuri..kumuona mtume/nabii ni sh. Laki moja. Kununua kitabu cha mhubiri Fulani ni sh.elfu themanini. Badala tuuze kwa bei nafuu, tunauza kibiashara, kisa tunafahamu ni lazima tu vitanunuliwa kwasababu sisi ni maarufu.

Bwana atusaidie. Tutoe nafaka tusiizuie

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Maana ya huu mstari ni ipi? Mithali 14:4 ‘Zizi ni safi ambapo hapana ngombe;bali nguvu za ngombe zaleta faida nyingi’.

Kusemethi ni nini katika biblia?

Uga ni nini? Na kazi yake ni ipi kibiblia?

KWA KUWA WASEMA MIMI NI TAJIRI.

Njia zote za mtu ni safi machoni pake mwenyewe;(Mithali 16:2)

Gengeni ni wapi, wale nguruwe walipoteremkia? (Marko 5:13)

KWA WINGI WA WASHAURI HUJA WOKOVU.

Rudi nyumbani

Print this post

Je! Siku ilihesabiwaje kabla ya jua na mwezi kuumbwa?

Swali: Katika kitabu cha Mwanzo tunasoma jua na mwezi viliumbwa katika siku ya 4 , sasa napenda kujua kabla ya hapo siku zilihesabiwaje, maana jua ndilo linalotenga mchana na usiku…na maandiko yanatuonyesha kuwa lilikuja kuumbwa siku ya 4?

Jibu: Ni kweli jua na mwezi viliumbwa siku ya 4, tena baada ya miti na miche ya kondeni kuumbwa (Mwanzo 1:14).

Lakini ukisoma kuanzia mstari wa pili katika kitabu hiko cha Mwanzo, utaona Mungu tayari alikuwa ameshaumba mchana na usiku na ameshatenga giza na nuru.

Mwanzo 1:1 “Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi.

2 Nayo nchi ilikuwa ukiwa, tena utupu, na giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji; Roho ya Mungu ikatulia juu ya uso wa maji.

3 Mungu akasema, Iwe nuru; ikawa nuru.

4 Mungu akaiona nuru, ya kuwa ni njema; MUNGU AKATENGA NURU NA GIZA.

5 MUNGU AKAIITA NURU MCHANA, NA GIZA AKALIITA USIKU. IKAWA JIONI IKAWA ASUBUHI, SIKU MOJA”.

Umeona?..kumbe tayari Mungu alikuwa ameshaumba mchana na usiku kabla hata ya kuumba jua. Maana yake hata kama asingeumba jua bado majira na mchana na usiku yangekuwepo kwasababu yeye mwenyewe ndio Nuru ya ulimwengu (mwilini na rohoni).

Yohana 8:12 “Basi Yesu akawaambia tena akasema, Mimi ndimi nuru ya ulimwengu, yeye anifuataye hatakwenda gizani kamwe, bali atakuwa na nuru ya uzima”.

Ndio maana katika ile mbingu mpya na nchi mpya hakutakuwepo  na jua na bado Nuru itakuwepo.

Ufunuo 21:23 “Na mji ule hauhitaji jua wala mwezi kuuangaza, kwa maana utukufu wa Mungu huutia nuru, na taa yake ni Mwana-Kondoo”.

Kwahiyo kwa hitimisho ni kuwa Mungu aliumba mchana na usiku, kabla ya kuliumba jua..na hiyo ni kuonyesha utukufu wake yeye, na pia kuonyesha kuwa yeye ndiye Nuru halisi Na ndio chanzo cha Nuru yote.

Je umempokea Bwana Yesu aliye Nuru ya kweli? Kama bado fahamu kuwa bado upo gizani ijapokuwa jua linakumulika…kwahiyo ni vyema ukafanya maamuzi thabiti leo ya kumpokea na kuokoka.

Yohana 12:46 “Mimi nimekuja ili niwe nuru ya ulimwengu, ili kila mtu aniaminiye mimi asikae gizani”

Soma pia Yohana 9:5 na Yohana 11:9.

Bwana Yesu akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Je! mwanadamu wa kwanza kuumbwa ni yupi?

HAMA KUTOKA GIZANI

NI SAA KUMI NA MBILI (12) TU, ZA KRISTO KWAKO.

Biblia inamaanisha nini iliposema “wakidhania kuwa ulevi wakati wa mchana ni anasa;?

Je mke wa Musa alikuwa ni Mweusi?

Rudi nyumbani

Print this post

Paulo alikuwa na maana gani aliposema “nimeaminiwa uwakili”

SWALI: Mtume Paulo alikuwa na maana gani aliposema “nimeaminiwa uwakili”?

1Wakorintho 9:16  “Maana, ijapokuwa naihubiri Injili, sina la kujisifia; maana nimewekewa sharti; tena ole wangu nisipoihubiri Injili! 17  Maana nikiitenda kazi hii kwa hiari yangu nina thawabu; ila ikiwa si kwa hiari yangu, nimeaminiwa uwakili”.


JIBU: Mtume Paulo aliifanya kazi ya Mungu, kana kwamba ni muajiwa/kibarua aliyepewa dhamana ya kusimamia kazi zote alizowekewa chini yake kwa uangalifu, kana kwamba akipoteza chochote au akileta hasara ya jambo lolote atawajibishwa, na boss wake utakapofika muda wa mahesabu.

Tofauti na mtu aliyejitolea tu kazi, kama kusaidia, mtu wa namna hiyo hata akiacha wakati wowote, hawezi kuwajibishwa zaidi sana atapewa shukrani, kwa kutoa mchango wake katika shughuli hiyo, na kupewa viposho.

Ndio maana ya hiyo kauli, “nimeaminiwa uwakili”..kwa lugha nyepesi “nimeamiwa kazi ya mtu mwingine niisimamie kama kijakazi” Na hiyo ndiyo iliyompelekea Mtume Paulo, kusema mimi ni ‘mtumwa na mfungwa’ wa Yesu Kristo (Warumi 1:1,Waefeso 3:1).. Kwasababu hiyo akaitenda kazi ya Mungu kwa uaminifu wote, na kwa umakini wote, hata zaidi ya mitume wengine.

Ni funzo gani tunalipata.

Nasi pia tukiichukulia kazi ya Mungu kama sio jambo la hiari, au la kujitolea tu, bali kama ndio sehemu ya kazi yetu tuliyoajiriwa na Mungu hapa duniani, na kwamba tusipoifanya kwa uaminifu tukaleta hasara, tutatolea hesabu yake siku ya mwisho,..

Yaani tukimtumikia Mungu kama vile tuzitumikiavyo kazi zetu maofisi, bila kuwa na udhuru wowote.

basi tutajifunza kuitenda bila ulegevu Na mwisho wake utakuwa ni kupewa thawabu kubwa na kutukuzwa sana na Bwana Yesu  tutakapofika kule mbinguni.

Lakini kama tutajitoa kwa Mungu pale tunapojisikia tu, au tunapokuwa na nafasi, au tunapokumbushwa, au tunapofanikiwa sisi si watumwa au wafungwa wa Yesu Kristo, bali ni watumishi wake tu. Hatujafikia hatua hiyo ya kuitwa watumwa wake.

Bwana atujalie utumishi bora, kama huo, wa kuaminiwa uwakili

Shalom

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

JIFANYIE RAFIKI KWA MALI YA UDHALIMU.

Mungu alikuwa anaongea na nani aliposema na “Tumfanye mtu kwa mfano wetu”

Bwana aliposema “sikuja kutangua torati bali kuitimiliza” alikuwa anamaanisha nini?

Pesa za bindoni ni nini?(Marko 6:8)

Kutazama Nyakati mbaya ni kufanyaje?.

UTAMBUE UJUMBE WA SAA UNAYOISHI.

Rudi nyumbani

Print this post