Category Archive Uncategorized @sw-tz

MWANAMKE, BINTI, MAMA. (Sehemu ya 3)

Hii ni sehemu ya tatu ya mfululizo wa masomo kwa wanawake, katika sehemu ya kwanza  na ya pili tumeona, ni kwanini Bwana aliwatambua baadhi ya wanawake, kwa jinsia zao, na sio kwa majina yao, kwa kuwaita “wanawake”, na sehemu nyingine kuwatambua kwa mionekano yao kwa kuwaita “Binti” na sio labda kwa majina yao..ipo sababu, ikiwa hujapata bado, chambuzi zake, basi tutumie msg inbox tukutumie..

Lakini leo tutasonga mbele tena, kuona ni kwanini baadhi ya wanawake, aliwatambua kwa majina ya “MAMA”.

Mama ni cheo cha ukomavu, kwasababu mpaka uitwe mama ni wazi kuwa lazima utakuwa na watoto uliowazaa au unaowalea chini yako. Sasa tukirudi kwa Bwana Yesu, kuna wanawake aliwaona ni “Wamama rohoni”, sio mwilini, kwasababu kulikuwa na wanawake wengi, lakini si wote aliwaita “Mama” kama tu vile si wote aliwaita “Binti yangu”, bali baadhi tu.

Sasa embu twende tukasome baadhi ya Habari katika biblia kisha tuone, ni nini Bwana anatufundisha katika Habari husika. Mwanamke wa kwanza tutakayemtazama ni yule mkananayo. Tusome;

Mathayo 15:21 “Yesu akaondoka huko, akaenda kando pande za Tiro na Sidoni.

22 Na tazama, mwanamke Mkananayo wa mipaka ile akatokea, akampazia sauti akisema, Unirehemu, Bwana, Mwana wa Daudi; binti yangu amepagawa sana na pepo.

23 Wala yeye hakumjibu neno. Nao wanafunzi wake wakamwendea, wakamwomba, wakisema, Mwache aende zake; kwa maana anapiga kelele nyuma yetu.

24 Akajibu, akasema, Sikutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli.

25 Naye akaja akamsujudia, akisema Bwana, unisaidie.

26 Akajibu, akasema, Si vema kukitwaa chakula cha watoto na kuwatupia mbwa.

27 Akasema, Ndiyo, Bwana, lakini hata mbwa hula makombo yaangukayo mezani pa bwana zao.

28 Ndipo Yesu akajibu, akamwambia, MAMA, IMANI YAKO NI KUBWA; na iwe kwako kama utakavyo. Akapona binti yake tangu saa ile”.

Angalia asili ya huyu mwanamke, hakumtafuta Bwana kwa shida zake mwenyewe, au kwa matatizo yake mwenyewe, bali alimtafuta Bwana Yesu kwa shida za mwanawe.. Japokuwa mwanzoni hakujibiwa chochote, hata baada ya pale alipewa na maneno ya kukatishwa tamaa ya kuitwa mbwa, lakini bado hakuacha kuomba kwa shida ya mtu mwingine, kwasababu uzito wa mwanae ulikuwa kama wakwake.

Hiyo ni kuonyesha ni jinsi gani asivyojali vya kwake tu, bali hata vya wengine…

Mwanamke mwingine ni Mama yake Yesu mwenyewe, ambaye tunamsoma katika Yohana 2:1-4 siku ile alipoalikwa katika Harusi..

Yohana 2:1 “Na siku ya tatu palikuwa na arusi huko Kana, mji wa Galilaya; naye mama yake Yesu alikuwapo.

2 Yesu naye alikuwa amealikwa arusini pamoja na wanafunzi wake.

3 Hata divai ilipowatindikia, mamaye Yesu akamwambia, Hawana divai. 4 Yesu akamwambia, MAMA, TUNA NINI MIMI NAWE? Saa yangu haijawadia”.

Angalia tabia yake alijali shida za wengine, aibu za wengine, akazifanya kama ni za kwake. Na kumpelekea Kristo, na muda huo huo akamwita “mama”

Mwingine ni Mariamu Magdalena, asubuhi ile ya kufufuka kwa Bwana, alikuwa akilia pale makaburini ndipo Yesu akamtokea na kumwambia “Mama unalilia nini?” Saa hiyo hiyo Yesu akamtuma kwa ndugu zake kwenda kuwatangazia injili. Akawa mtu wa kwanza kupewa neema ya kuwahubiria watu wengine Habari za kufufuka kwa Bwana Yesu. (Yohana 20:11-18)..

Neema hiyo si kila mwanamke atapewa, bali ni wale “wamama rohoni tu” Wanawake waliokomaa kiroho,ambao wanajua wajibu wao kwa Bwana, wanajua kuwaongoza wengine katika njia za Mungu, haijalishi umri wao Rohoni watu kama hawa, wanawekwa kundi moja na akina Sara, na Rebeka, na Mariamu, na Elizabeti na wengineo. Kwasababu wamevuka viwango cha utoto, hadi kufikia hatua ya utu uzima ya kuzaa na kulea.

Swali ni je! Wewe, dada upo katika kundi gani? Bwana anapokuona anakutambuaje? msichana? Au Mtu? Mtoto? Au Mama?. Kabla hujafikiria kuyatazama Maisha ya mitume wa Yesu mfano wakina Petro waliishije, embu tafakari kwanza, Maisha ya wanawake wacha Mungu katika biblia waliishije. Hiyo itakusaidia sana mwanamke.

Tamani sana, Kristo akutambue kama “Mama” Ni heshima ya juu sana, Kristo anaweza kumpa mwanamke, iliyosawa na ya “Kitume”. Kua kiroho timiza wajibu wako wa kuitangaza injili na pia kuwasaidia wengine kumjua Mungu rohoni.

Bwana akubariki.

Maran atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Rudi nyumbani

Print this post

Je! Siku ya unyakuo watoto wachanga watanyakuliwa?

SWALI: Je! Siku ya unyakuo watoto wachanga watanyakuliwa? Na vipi kuhusu walio bado tumboni, na wenyewe watanyakuliwa au wataachwa?


JIBU: Hili ni moja ya swali gumu  kwasababu biblia haijaeleza moja kwa moja ni nini kitawatokea watoto siku ile ya Unyakuo, Hivyo tutajaribu kueleza kwa kadiri ya tunavyoona katika baadhi ya vifungu kwenye maandiko.

Ukitazama katika biblia, utaona, wapo watoto walipata neema kutokana na haki za wazazi wao, mfano wa hawa ni watoto wa Nuhu, na Lutu,  vilevile wapo watoto walioadhibiwa kutokana na makosa ya wazazi wao. Utaliona hilo pia katika vile vizazi vyote vya Sodoma na Gomora, pamoja na gharika  vyote viliteketezwa, hadi watoto walipata adhabu kwa dhambi za wengine. Lakini hiyo haimaanishi kuwa wataadhibiwa tena baada ya kifo.

Pia tukumbuke kuwa hata katikati ya kipindi cha dhiki kuu, bado watu wataendelea kutungishwa mimba na kuzaliwa, hivyo litakuwepo kundi la vichanga ambavyo vitazaliwa katikati ya dhiki kuu na vitakufa katika maangamizi yao..Hilo tunalithibitisha katika andiko hili;

Mathayo 24:19 “Ole wao wenye mimba na wanyonyeshao siku hizo!

20 Ombeni, ili kukimbia kwenu kusiwe wakati wa baridi, wala siku ya sabato.

21 Kwa kuwa wakati huo kutakuwapo dhiki kubwa, ambayo haijatokea namna yake tangu mwanzo wa ulimwengu hata sasa, wala haitakuwapo kamwe.

22 Na kama siku hizo zisingalifupizwa, asingeokoka mtu ye yote; lakini kwa ajili ya wateule zitafupizwa siku hizo”.

Unaona? Kwahiyo siku ile ikifika, kuna uwezekano wa watoto wengine kunyakuliwa (hata wale walio tumboni), na vilevile wengine kubaki, japo hatuwezi kusema hivyo ndivyo ilivyo, Yote tunamwachia Mungu. Ikiwa ni wote watanyakuliwa, au ni baadhi, Tunachopaswa kufahamu ni kuwa Mungu ni wa haki, atayaleta yote katika mizani, na yote yatakuwa sawa tu mwisho wa siku, na tutaona kabisa hukumu zake ni za haki. Kama vile Malaika mbinguni wanavyokiri hivyo..

Ufunuo 16:7 “Nikaisikia hiyo madhabahu ikisema, Naam, Bwana Mungu Mwenyezi, ni za kweli, na za haki, hukumu zako”.

Cha muhimu tunachopaswa kujua ni kuwa sisi ambao tayari tumeshafikia kimo cha kuyajua mema na mabaya, Kama hatutayatengeneza mambo yetu sasa, kwa kumpokea Bwana Yesu Kristo kwa kumaanisha kabisa, na kujitwika misalaba yetu na kumfuata, tujue kuwa unyakuo ukipita tutaachwa. Na matokeo yake, yatakuwa ni kuingia katika mateso makali ya dhiki kuu pamoja na Jehanamu ya moto.

Je! Umeokoka? Je! Umebatizwa katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako? Kumbuka Unyakuo ni wakati wowote, tubu umruidie muumba wako. Parapanda ni siku yoyote inalia, hakuna dalili iliyosalia..

Bwana Yesu akubariki.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Rudi nyumbani

Print this post

Je! Karamu za ‘Idi’ ndio zipo hizo tunazozisoma katika Hosea (12:9)

Hosea 12:9 Lakini mimi ni Bwana, Mungu wako tangu ulipotoka katika nchi ya Misri; nitakukalisha tena katika hema, kama siku za KARAMU YA IDI.


JIBU: Tofauti na inavyodhaniwa hapo, na watu wa dini tofauti, kwamba Biblia inazitambua sherehe za kiislamu!. Jambo ambalo si kweli.

Ni vizuri kufahamu kuwa lugha yetu ya Kiswahili imetohoa maneno mengi sana kutoka katika lugha ya kiharabu, hata wakati ambapo biblia inatafsiriwa katika Kiswahili ilifuata mkondo huo huo. Kwamfano Sehemu nyingine utaona neno “shehe” likitajwa (1Samweli 5:8), na hapa unaona pia Neno “Idi” .

Kulingana na lugha ya  kiharabu neno IDI, linamaanisha “Sherehe”. Haijalishi ni sherehe ya aina gani, inaweza ikawa ni ya kidini au ya kitaifa, au ya kitamaduni, au ya kimuungano..

Hivyo imezoeleka na watu wengi wasioilewa lugha ya kiharabu kudhani kuwa Idi ni neno la sikukuu ya kiislamu, kumbe sio.

Katika biblia ya kiharabu, mahali popote, kulipotajwa sherehe ya kiyahudi, Neno Idi liliandikwa pale. Mfano, palipoandikwa sikukuu ya pasaka, iliandikwa “idi ya pasaka” n.k..

Hivyo, hatushangai na Neno hilo kuonekana katika baadhi ya vifungu kwenye biblia. Hiyo yote ni kwasababu lugha yetu ya Kiswahili, imeundwa kutoka katika lugha nyingi mbalimbali. Kwahiyo inayozungumziwa hapo sio sikukuu ya kiislamu, bali ni sikukuu ya vibanda, ambayo wana wa Israeli walikuwa wakiisheherekea kwa katika vibanda pindi walipokuwa jangwani.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

SIKUKUU 7 ZA KIYAHUDI ZINAFUNUA NINI KWETU?

UFUNUO: Mlango wa 19

ESTA: Mlango wa 5, 6 & 7

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

Je kunena kwa Lugha mpya kukoje?.Na hizi lugha ni zipi, na je! ni lazima kila mkristo aliyepokea Roho Mtakatifu anene kwa lugha mpya?

Rudi nyumbani

Print this post

MWANAMKE, BINTI, MAMA. (Sehemu ya 2)

Hii ni sehemu ya pili ya mfululizo wa masomo kwa wanawake, katika sehemu ya kwanza tumeona, ni kwanini Bwana alipokutana na yule mwanamke mwenye dhambi, alimtambua kwa jinsia yake (Yaani “mwanamke”) na sio kwa mwonekano wake wa kike pengine wa kiumri au  wa kimaumbile. Hiyo ni kufunua kuwa ujumbe alioubeba yule mwanamke ulikuwa ni wa kijinsia.. yaani maalumu kwa wanawake. Hivyo kama hukupata maelezo yake, unaweza kunitumia ujumbe inbox nikakutumia.

Leo tutaenda katika sehemu ya pili: ya BINTI.

Mahali pengine, Bwana Yesu, aliwatambua wanawake wengine kama, binti zake.. Na cha ajabu ni kuwa, wengine walikuwa pengine wana umri mkubwa kuliko yeye, lakini bado aliwaita BINTI zake, akifunua kuwa kutazama kwake hakukuwa katika jicho la kimwili bali la rohoni. Embu tusome, kisa hiki kimoja..kisha tuone ni ujumbe gani Bwana alitaka kuupitisha kwa ulimwengu kupitia mwanamke huyu.

Mathayo 9:20 “Na tazama, mwanamke aliyekuwa na ugonjwa wa kutoka damu muda wa miaka kumi na miwili, alikuja kwa nyuma, akaugusa upindo wa vazi lake.

21 Kwa maana alisema moyoni mwake, Nikigusa tu upindo wa vazi lake nitapona.

22 Yesu akageuka, akamwona, akamwambia, Jipe moyo mkuu, BINTI YANGU; imani yako imekuponya. Yule mwanamke akapona tangu saa ile.”.

Swali la kujiuliza ni kwanini alimtambua mwanamke huyu kama binti na sio pengine kama Mama, au bibi?

Ni kwasababu ya Imani yake ya kipekee aliyokuwa nayo kwake..Ambayo hakuiona kwa watu wengine wote waliomfuata, ijapokuwa alihangaika kwa miaka 12 kutafuta suluhu la matatizo yake asipate, lakini alipofika kwa Yesu kwa mara ya kwanza tu hakumuhesabia kama mmojawapo wa wale matapeli aliokutana nao, huko nyuma, waliomchukulia fedha zake.

Bali alimwamini moja kwa moja kwa asilimia 100, akasema, nitakapoligusa tu pindo la vazi lake, muda huo huo nitakuwa mzima, kumbuka hakusema sio “naamini nitapona, au pengine nitapona” hapana, bali alisema “NITAPONA” kuonyesha kuwa alikuwa na uhakika wa yule aliyekutana naye sio mbabaishaji au tapeli…. Na ndio maana akaona hata hakuna sababu ya kwenda kumsumbua kuzungumza naye, au kumwomba aje kumtembelea, Bali aliona pindo la vazi lake, tu linatosha yeye kuwa mzima..

Na Yesu alipoiona Imani yake saa ile ile akamgeukia na kumwita “Binti yangu”.. Akampa nafasi ya kipekee sana Kama Mtoto wa kike aliyemzaa yeye mwenyewe, ambaye ana haki zote za kupokea mema yote ya Baba yake.

Tujiulize ni wanawake wangapi leo Bwana anaweza kuwaita binti zangu? Usidhani Kristo kukuita binti yake, kwasababu ya umri wako mdogo, au mrembo wako, au utanashati wako, hilo halipo, yeye hana jicho la mwilini, kama sisi tulilonalo, haangalii umri wala umbile.

Kama wewe ni mwanamke lakini unafika kwa Kristo ili kujaribu jaribu tu, uone kama Bwana atakujibu au la!,atakusaidia au la! unamlinganisha na wale waganga wa kienyeji uliowahi kuwatembelea huko nyuma.. uone kama atajibu au la!. Ujue kuwa wewe sio binti wa Yesu.

Mabinti wa Yesu, tangu walipokutana na Yesu utawakuta wametulia kwa Bwana hadi sasa, wanaouhakika na waliyemwendea, hawahitaji kusaidiwa na mtu, kuelewa kuwa Yesu ni muweza, wanafanya mambo yao wakiwa wame-relax, huwezi kuwakuta leo kanisani Kesho, disco,  leo wamevaa magauni, Kesho wanakatiza barabarani na visuruali na vikaptura, leo kwa nabii huyu Kesho kwa yule..huwezi kuwakuta wapo namna hiyo.

Hao ndio binti za Mungu. Na faida yao ni kuwa kwasababu wameshaitwa binti za Mungu, tayari wanaourithi kutoka mbinguni. Jambo ambalo wengi hawajui wakidhani kila mtu atakuwa mrithi wa kila baraka ya Mungu mbinguni.

Dada/mama/bibi tambua ni nini Kristo anatamani kuona kwako, acha kutangatanga na huu ulimwengu, Acha kujaribu jaribu, maanisha kumfuata Kristo.. Yeye mwenyewe anasema.

2Wakorintho 6:17 “Kwa hiyo, Tokeni kati yao, Mkatengwe nao, asema Bwana, Msiguse kitu kilicho kichafu, Nami nitawakaribisha.

18 Nitakuwa Baba kwenu, Nanyi mtakuwa kwangu WANANGU WA KIUME NA WA KIKE”,

Kumbuka hizi ni siku za mwisho, Kristo anarudi siku yoyote. Bado tu hujatulia kwa Bwana? Injili tuliyobakiwa nayo sasa hivi sio ya kubembelezewa tena wokovu, ni wewe mwenyewe aumke usingizini, umtafute Mungu wako. Kwasababu muda umeshaisha.

Maran atha..

Usikose sehemu ya tatu na ya mwisho ya Makala hii, ambayo, tutaona pia ni kwanini Bwana Yesu aliwatambua wanawake wengine kama MAMA.

Bwana akubariki..

Maran atha

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya ‘Hukumu haina huruma kwake yeye asiyeona huruma’?

SWALI: Nini maana ya  “hukumu haina huruma kwake yeye asiyeona huruma”?(Yakobo 2:13)


 Yakobo 2:13 Maana hukumu haina huruma kwake yeye asiyeona huruma. Huruma hujitukuza juu ya hukumu.

JIBU: Ukianzia kusoma tokea ule  mistari wa kwanza utaona Yakobo, anajaribu kulionya kanisa juu ya Upendo, yaani kufanya mambo bila upendeleo, akatolea mfano wa waaminio wawili, mmoja Tajiri mwingine maskini, halafu, ikatokea kanisa limstahi yule Tajiri kwa kumpa heshima kubwa ya viti vya mbele, na yule maskini likamweka sehemu mbaya, Yakobo anahoji anasema; Kanisa halioni kama litakuwa linahukumu vibaya?

Ndipo hapo sasa akaja kusema mbeleni, kuwa hukumu huwa haina huruma kwake yeye asiye na huruma.. Ikiwa na maana kuwa, mfano wewe ukampiga mwenzako mpaka akafa bila kumuhurumia, usitegemee kuwa sheria itakusamehe kwa kosa hilo?  Haiwezi kukuhurumia, hata kama utaomba msamaha vipi, kinyume chake ni lazima itakuwajibisha kulingana na kosa ulilolifanya..

Vivyo hivyo, mbele za Mungu, ikiwa hatutawahurumia wengine naye Mungu hatatuhurumia sisi, ikiwa tutawependelea wengine naye Mungu atawapendelea wengine badala yetu sisi siku ile itakapofika..

Bwana Yesu alisema katika

Luka 6:36 “Basi, iweni na huruma, kama Baba yenu alivyo na huruma.

37 Msihukumu, nanyi hamtahukumiwa; msilaumu, nanyi hamtalaumiwa; achilieni, nanyi mtaachiliwa.

38 Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa; kipimo cha kujaa na kushindiliwa, na kusukwa-sukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa vifuani mwenu. Kwa kuwa kipimo kile kile mpimacho ndicho mtakachopimiwa”.

Unaona,  tukiwa na huruma, maana yake ni kuwa hukumu haiwezi kuwa na nguvu juu yetu. Ndipo linapotimia hili neno “Huruma hujitukuza juu ya hukumu”.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

BASI, IWENI NA HURUMA, KAMA BABA YENU ALIVYO NA HURUMA

Biblia inamaanisha nini inaposema “Mwenye haki huufikiri uhai wa mnyama wake”?

Kwanini Paulo, alihukumu wakati hukumu hairuhusiwi?

NINI KINATOKEA BAADA YA KIFO?

Rudi nyumbani

Print this post

IIGE RATIBA YA MUNGU YA WIKI IKUSAIDIE

Nakusalimu katika jina kuu sana la Bwana wetu Yesu Kristo, karibu tujifunze maneno ya uzima.

Tunaposoma kile kitabu cha Mwanzo sura ya kwanza , wengi wetu tunachokiona pale ni tendo la uumbaji tu lakini hatuoni mikakati na ratiba alizojipangia Mungu ili kuukamilisha huo mpango wake mzima wa uumbaji.

Walimwengu wanasema, mtu mwenye akili huwa anajifunza kwa waliofanikiwa.. Sasa sisi wanadamu hatuna aliyefanikiwa Zaidi ya Mungu wetu si ndio?. Tunapoziangalia mbingu na nchi tunachokiona ni kazi stadi iliyobuniwa kwa  umakini  sana isiyokuwa na mapungufu au madhaifu yoyote, hivyo na sisi pia kama tunataka tuwe na mafanikio makubwa hatuna budi kujifunza ratiba ya Mungu jinsi alivyoweza kupangilia mambo yake. Mpaka tukakiona hichi tunachokiona sasa hivi.

Sasa katika zile siku 7 za uumbaji, Mungu alizigawanya shughuli zake katika vipengele vikuu vitatu.

Kipengele cha kwanza: Alijikita katika kufanya kazi ya utenganisho

Kipengele cha pili :Kilikuwa ni uumbaji

Na kipengele cha  tatu: Kupumzika.

Tukianza na kipengele cha Kwanza: Kufanya utenganisho.

Ukisoma Mwanzo 1:2 Utaona utenganisho wa kwanza alioufanya Mungu katika siku ya kwanza ulikuwa ni kati ya Nuru na giza.

Mwanzo 1:3 Mungu akasema, Iwe nuru; ikawa nuru.

4 Mungu akaiona nuru, ya kuwa ni njema; Mungu akatenga nuru na giza.

Siku ya pili tena akaendelea na kazi hiyo hiyo.. akayatenga maji ya juu ya chini, na ya chini ya nchi kwa kuweka kitu kinachoitwa anga katikati..

Mwanzo 1:7 Mungu akalifanya anga, akayatenga yale maji yaliyo juu ya anga na yale maji yaliyo chini ya anga; ikawa hivyo.

8 Mungu akaliita lile anga Mbingu. Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku ya pili.

Unaona Kama hiyo haitoshi, bado aliendelea hadi siku ya tatu kufanya matenganisho, kati ya maji na ardhi, ili nchi kavi ionekane

Mwanzo1:9 Mungu akasema, Maji yaliyo chini ya mbingu na yakusanyike mahali pamoja, ili pakavu paonekane; ikawa hivyo.

10 Mungu akapaita pale pakavu Nchi; na makusanyiko ya maji akayaita Bahari; Mungu akaona ya kuwa ni vyema.

Na Siku ya Nne pia, akatenganisha, siku na siku, na mwezi na mwezi, na mwaka na mwaka,..kwa kuumba jua na mwezi na nyota..

Soma Mwanzo 1:16-19 utalithibitisha hilo

Sasa mpaka anafikia siku ya nne, alikuwa bado hajaumba mnyama yoyote, ni kazi tu ya utenganisho tukiachilia mbali mimea ambayo iliumbwa siku ya tatu..

Mungu kuanzana na utenganisho ni kutufundisha nini?

Hii ni kutufundisha kuwa, hatupaswi kukimbilia kufanya jambo lolote,kwanza  kama kuna mambo ambayo bado hayajatenganishwa na sisi rohoni. Tutumie nguvu kubwa kutenganisha nuru na giza kwenye wiki yetu, ..Usianze tu wiki yako hivi hivi, bila kuiambia kwanza iwe nuru kwako,kwa kwenda ibadani nyumbani kwa Bwana usianze wiki bila kuomba, hakikisha unayatenga mambo maovu mbali na wewe kwa kadiri uwezavyo. Ndicho Mungu alichokuwa anakifanya katika siku za mwanzo.

Kama kuna mtu umemdhulumu mlipe..kama una madeni ya watu yasawazishe..kama kuna dhambi ulitenda ziungame mbele za Bwana.

Kipengele cha  Pili: Ni uumbaji,

baada ya pale ndipo utaona Mungu anaanza kuumba, samaki , na wanyama wa kila namna wa mwituni na wa kufungwa pamoja na ndege wote angani..na mwisho kabisa akamwuumba na mwanadamu, katika siku ile ya sita.

Hii ni kutufundisha kuwa, mara baada ya kutenganisha mambo yasiyofaa mbali nasi ndipo hapo sasa tuwe na uhakika kuwa kila tunachotia mkono kukifanya, kitakuwa ni chema sana.. Kisichokuwa na mapungufu au kasoro..Kama Mungu alivyoona jinsi uumbaji wake ulivyokuwa vema sana usio na mapungufu yoyote.

Mwanzo 1:31 Mungu akaona kila kitu alichokifanya, na tazama, ni chema sana. Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku ya sita.

Kipengele cha Tatu: Kupumzika.

Sasa alipomaliza kazi yake yote, kwa siku 6, akaona ni vema atenge siku moja apumzike. Akatenga muda wa saa 24 wa kutofanya kazi yoyote.

Hii ni kutufundisha pia, kuwa sisi tusijifanye tupo buzy sana kuliko Mungu, ikiwa yeye alipumzika, wewe ni nani usipumzike? Kama unatenda kazi kama mashine wiki nzima, usiku na mchana huna muda wa kupumzika, wiki nenda wiki rudi, miaka nenda miaka rudi.. Tambua kuwa hata hicho unachokifanya hakiwezi kuwa na ubora wowote. Hivyo na wewe ukienenda kwa ratiba kama hii ya Mungu katika wiki yako, jiandae kukutana na matokeo chanya katika mambo yako yote unayoyasumbukia. Uwe ni mtumishi wa Mungu katika huduma yako, au mwanafunzi, au mfanyakazi, au kiongozi, ijaribu ratiba hii ya Mungu uone.Lakini kama wewe  ibada si kitu cha muhimu kwako, unachowaza siku zote ni kazi tu, hujitenganishi, na kazi haramu, au marafiki wabaya, au mazungumzo mabaya, hujitengi na dhambi, huna muda na kuomba, au kujifunza Neno la Mungu, au kujirekebisha, unachowaza ni pesa tu ujue kuwa wiki yako, na masumbuko yako ni hasara tu. Kwasababu unapanda katika giza..unaumba katika maji..mahangaiko yako uwe na uhakika yatakuwa ni bure tu..

Kumbuka tunapoizungumzika ratiba hii ya Mungu, haimaanisha na wewe uifuate hivyo hivyo kwamba siku ya 1-4 ufanye hivi au vile, hapana, bali, walau katika wiki yako nzima, uhakikishe kila kipengele umekigusua, kwa muda unaolingana na huo Mungu alioutumia. Kama ni kupumzika, unaweza usiwe na saa 24 mfululizo, lakini hakikisha walau kwa wiki hukosi hizo saa 24 za kupumzika, vivyo hivyo na hayo mengine yote.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

MWANZO WA INJILI YA YESU KRISTO.

NAMNA YA KUITAMBUA SAUTI YA MUNGU INAPOZUNGUMZA NA WEWE

AHADI YA ROHO ILIYOSALIA SASA KWA KIPINDI CHETU.

JE UNAIFANYA KAZI YA MUNGU?

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

Rudi nyumbani

Print this post

JIPE MOYO MKUU.

Ukimtafakari yule mwanamke ambaye alitokwa na damu kwa muda wa miaka 12, na kwenda kushika pindo la vazi lake, unaweza kudhani aligundua jambo la maana sana machoni pake, au machoni pa watu waliomfuata Yesu, Jibu ni la!,

Kwa namna ya kawaida kuacha kutafuta Uso wa Yesu, unakimbilia nguo, tena sehemu ya mwisho kabisa ya nguo (pindo), ni uendawazimu na ndio maana ikambidi afanye  hilo jambo kwa siri sana, kutomshirikisha mtu yeyote, hadi Yesu mwenyewe alipouliza ni nani kanigusa bado aliogopa kusema… kwasababu hata yeye mwenyewe machoni pake lilikuwa ni kama jambo la kijinga..akijua kinachofuata kama sio kugombezwa, au kuzomewa, basi ni kufukuzwa.

Lakini tunaona, Bwana Yesu alipogeuka..majibu yake yalikuwa ni tofauti, badala ya kumgombeza na kumfukiza alimwambia, “Jipe moyo mkuu”, binti yangu..kuonyesha kuwa Kristo anayathamini sana mawazo manyonge, maadamu yamekusudiwa tu kwake kwa moyo wote.

Mathayo 9:20 “Na tazama, mwanamke aliyekuwa na ugonjwa wa kutoka damu muda wa miaka kumi na miwili, alikuja kwa nyuma, akaugusa upindo wa vazi lake.

21 Kwa maana ALISEMA MOYONI MWAKE, Nikigusa tu upindo wa vazi lake nitapona.

22 Yesu akageuka, akamwona, akamwambia, Jipe moyo mkuu, binti yangu; imani yako imekuponya. Yule mwanamke akapona tangu saa ile”.

Leo hii watu wengi wamekuwa na mawazo mengi ya kufanyia Mungu, Lakini wamevunjwa moyo pengine na dhamiri zao wenyewe, au na wanadamu, mpaka mawazo yale mazuri yamekufa ndani yao, wakidhani kuwa kumtumikia Mungu ni mpaka uwe askofu au shemasi. Kumbe katika mawazo hayo yanayoonekana ni ya kijinga sana, mbele za Mungu yanathamani kubwa mno, maadamu tu yameelekezwa kwake.

Hujawa mchungaji, hujawa mtume, hujawa shemasi, hujawa mwinjilisti, hujawa mwalimu, hilo lisikufanye kuona kuwa kitu kingine chochote unachoweza kumfanyia Mungu, kitakuwa hakuna umuhimu kwake..

Bwana anachokuambia leo ni kuwa JIPE MOYO MKUU. Hilo wazo ulilonalo kwake si, dogo.. pengine unaujuzi wa kuchora picha zenye jumbe tofauti tofauti za ki-Mungu, na kuzisambaza sehemu mbalimbali wazo hilo ni rahisi kudharaulika miongoni mwa watakatifu, lakini kwa Yesu, sivyo anakuambia Jipe moyo mkuu..mtumikie yeye katika hilo.

Pengine Umekuwa na wazo la kuchapisha jumbe fupi fupi, na kuzisakafia kwa karatasi gumu la plastiki, na kwenda kuzigongelea kwenye nguzo za mabarabarani..Usivunjike moyo fanya hivyo… Kama waganga wa kienyeji hawaoni shida, kwanini wewe uone haya? Jipe moyo mkuu.

Umekuwa na wazo la utengenezaji bustani kwenye nyumba za Mungu bure..fanya tu, hata kama litadharauliwa na watu. Unataka kutengeneza studio ya kurekodi kipindi vya shuhuda, bila shida fanya hivyo.. Au Unajisikia, kutoa, kitu Fulani, au mali au eneo, au uanzishe mradi Fulani ambao lengo lake kuu ni kwa ajili ya kuifikisha injili ya Bwana mbele na si kitu kingine, zidi kuitenda. N.k.

Kwasababu, huko pia kuna umuhimu mkubwa sana ambao Bwana Yesu anapafikiria pia japokuwa watu wengi hawapaoni, ni mahali ambapo panaweza kumfanya Kristo ageuke aache kuwahudumia makutano akutazame wewe na kukubariki.

Hivyo usipuuzie mawazo manyonge yaliyowahi kuingia kichwani pako kwa ajili ya Kristo. Bali yatekeleze na Bwana atakufurahia. Uwe na nia njema tu!

Kumbuka, “mwishoni mwa vazi la YESU kuna huduma na pia upo uponyaji”. Hivyo Usikae bila kufikiria ni nini utamfanyia Mungu wako angali ukiwa hapa duniani. Yeye mwenyewe alisema,

Ufunuo 22:12 “Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo”.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

MAISHA ULIYOPITIA NYUMA NI USHUHUDA TOSHA WA WEWE KUMTUMIKIA MUNGU:

NUNUA MAJI YA UZIMA.

UKIOKOKA,HIZI FIKRA ZIKIJA NDANI YAKO, ZIKATAE.

Je! Bwana Yesu alibatiza akiwa hapa duniani?

Rudi nyumbani

Print this post

NI NANI ALIYEKUPA MAMLAKA HII UYATENDE HAYA?

Ulishawahi kujiuliza hoja ya msingi shetani aliyotumia kumshitakia Yesu mpaka kufanikiwa kumpeleka msalabani ilikuwa ni ipi?

Tukilifahamu hilo tutaelewa ni wapi ibilisi anapandaa ili kuwaletea dhiki wakristo katika siku za mwisho.

Ukisoma biblia utaona Wakati ule wayahudi wanatafuta sababu nyingi sana za kumshitaki Bwana Yesu lakini hawakuziona, mpaka dakika za mwisho mwisho wakatokea na hoja nyingine moja, ambayo ilikuwa na mashiko sana kwao..

Na hoja yenyewe ilikuwa ni katika lile HEKALU.

Mathayo 26:59 “Basi wakuu wa makuhani na baraza yote wakatafuta ushuhuda wa uongo juu ya Yesu, wapate kumwua;

60 wasiuone wangawa walitokea mashahidi wa uongo wengi.

61 Hata baadaye wawili wakatokea, wakasema, Huyu alisema, Naweza kulivunja hekalu la Mungu, na kulijenga kwa siku tatu.

Nataka ujifunze jambo moja, kulikuwa na kauli nyingi sana zenye makwazo ambazo wayahudi wangeweza kuzisimamia kumuulia Yesu, kwamfano alipowaita wao ni wa baba yao Ibilisi na sio Ibrahimu(Yohana 8:44). Kwa kauli kama hiyo kwamfano ingetosha tu kumfanya wamuue. Lakini sio hiyo ya  kusema “Bomoeni hili Hekalu nami nitalijenga ndani ya siku tatu…”

Ulishawahi kujiuliza, kwanini kauli hiyo ilipata nguvu?

Hilo ni jambo ambalo shetani alijaribu kulijenga tangu zamani za akina Zerubabeli katika ujenzi wa Hekalu, kama wewe ni msomaji wa biblia, utakumbuka kuwa kipindi wanalijenga Hekalu la pili, maadui zao (ambao hawakuwa wayahudi) waliomba waungane nao ili kulijenga hekalu la Mungu, lakini Zerubabeli na wenzake kwa ufunuo wa Roho, wakawakatalia, kwasababu walijua madhara yake yatakayokuja huko baadaye (Ezra 4:3)..

Lakini muda mrefu ulipopita mamia ya miaka, hekalu hilo lilichakaa, likawa kama limepitwa na wakati, kwa ujenzi wake. Hapo ndipo akatokea mtawala mmoja wa ki-Rumi aliyeitwa HERODE, Akaomba alikarabati hekalu lile,. Sasa wayahudi bila ya Kutaka kumuuliza Mungu, wakakurupuka wakamruhusu, hivyo Herode akaanza kulikarabati tena, akalijenga kwa fedha nyingi sana na kwa muundo wa kisasa.

Muda alioutumia kukarabati ulizidi hata muda uliotumika kujenga Hekalu lile, kwani Herode alitumia miaka 46 kulikarabati, (Soma Yohana 2:20 utaona), wakati wakina Zerubabeli walitumia miaka  isiyozidi 7. Na alifanikiwa kulipamba kweli kweli, mpaka wakati Fulani mitume wakaenda kumuonyesh Bwana uzuri wa jengo hilo jinsi lilivyopambwa vizuri.

Sasa kitendo kile kilikuwa na agenda ya ibilisi nyuma yake. Kwasababu alijua upo wakati Masihi atakuja, na ataingia katika hekalu lile na kuwafundisha watu sheria za Mungu, Hivyo akatumia nguvu zake nyingi sana kutafuta namna ya  kupalimiliki. Ndipo hapo akamwingia Herode, ambaye roho ya mpinga-Kristo ilikuwa nyuma yake, mtu ambaye alikuwa hana hata upendo na Mungu, na ndio maana wakati tu Kristo anazaliwa badala afurahie mwokozi kaja ulimwenguni, kinyume chake akatuma watu kwenda kumuangamiza, lakini cha ajabu ndio mtu huyo huyo aliyelikarabati Hekalu la Mungu.

Sasa kwasababu yeye ndiye aliyelitengeneza upya. Mamlaka yote ikahamia mikononi mwake kutoka kwa wayahudi, wayahudi wakawa hawana la kusema, hapo ndipo akaanzisha biashara kubwa kubwa sana , ndani ya hekalu, akalifanya pia kuwa kama eneo la kitalii, la watu kuja kushangaa uzuri wake.

Vilevile kukawekwa sheria kali, mtu yeyote akitaka kufanya jambo, au kuleta mfumo mpya ni lazima kwanza apokee kibali kutoka kwa HERODE, vinginevyo utaonekana kama ni muhalifu, na msaliti, ambaye anastahili adhabu ya kifo.

Kwahiyo, hakukuwa na mtu aliyeweza kufumbua kinywa chake, kukemea jambo lolote baya lililofanyika katika hekalu la Mungu takatifu, kwa hofu ya Herode na wayahudi. Hivyo hiyo ikaifanya  hali ikaendelea kuwa mbaya kupindukia hadi wakati Kristo anatokea dunia,

Ibilisi alijua kabisa, mwisho wa Siku Bwana Yesu, ni lazima aje aingie katika hekalu lake takatifu. Na kweli wakati ulifika akaingia, ndipo akasambaratisha  biashara zote, na shughuli zote zilizokuwa zinaendelea ndani ya Hekalu.

Wayahudi kuona vile, wakadhani maagizo hayo kapewa na Herode ndipo walipomuuliza…..

Luka 20:2 “wakamwambia, wakisema, Tuambie, unatenda mambo hayo kwa mamlaka gani? Tena, ni nani aliyekupa mamlaka hii?”

Na baada ya kugundua kuwa hakuyapokea Kwa Herode, hapo ndipo wakajua mtu huyu ni msaliti, na gaidi, anataka kutuletea harufu mbaya duniani, ili sisi tuonekane kama waasi, ni lazima tumuue.

Ndipo wakamshitakia kwa kitendo chake kile, na kauli ile.

Nachotaka tuone ni kwamba. Shetani anafahamu kuwa Kristo yupo mlangoni kurudi tena mara pili kulinyakua kanisa lake takatifu. Hivyo alichokifanya tangu kile kipindi cha mitume hadi sasa ni kujiingiza kwa siri , ili kujifanya kama analisaidia kanisa la Mungu..

Lakini lengo lake sio Kristo, na ndio maana utaona sasa, madhehebu mengi ya uongo, yamefanikiwa sana, lakini ukijaribu kuchunguza mifumo yao utaona ipo mbali sana na biblia.

Ukiuliza ibada za sanamu za kumwomba bikira Maria zipo wapi kwenye biblia, au kwenda toharani tunakupata wapi, utaishia kuonekana ni msaliti, na gaidi, msambaza, chuki. Shetani sikuzote hataki mfumo wake mbovu kuhojiwa.. Hataki kwasababu anajua pale sio mahali pake.

Leo hii, bado hajapokea nguvu kamili,za kuleta uharibifu kwa watu, wakati unafika atapokea nguvu ya kuleta mauaji kwa wale wakristo ambao UNYAKUO utakuwa umewapita. Atataka kuwaondosha wote asibakie mtu.

Je! Umeokoka ndugu yangu? Au bado unajisifia dini na madhehebu? Hautanyakuliwa kwa dhehebu lako zuri, utanyakuliwa kwa kukamilishwa katika wokovu, yaani kutubu na kubatizwa na kupokea Roho Mtakatifu, na kuishi katika utakatifu. Tubu leo kama hujatubu, Kumbuka wakati wowote Kristo anarudi.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Kikoto ni nini?(Yohana 2:15)

UFUNUO: Mlango wa 11

TUJIFUNZE JAMBO KWA WANAWAKE HAWA WAWILI:

UNYAKUO.

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

Rudi nyumbani

Print this post

Kuhubiri injili kwa husuda na fitina ndio kupi?

SWALI: Mtume Paulo alikuwa anamaanisha nini aliposema..”Wengine wanahubiri habari za Kristo kwa sababu ya husuda na fitina; na wengine kwa nia njema.”(Wafilipi 1:15)? Huko kuhubiri injili kwa husuda ndio kukoje?


JIBU: Ili kuelewa Paulo alimaanisha nini ni vema tukaisoma habari yote tokea juu..

Wafilipi 1:12-18

[12]Lakini, ndugu zangu, nataka mjue ya kuwa mambo yote  yametokea zaidi kwa kuieneza Injili;

[13]hata vifungo vyangu vimekuwa dhahiri katika Kristo, miongoni mwa askari, na kwa wengine wote pia.

[14]Na wengi wa hao ndugu walio katika Bwana, hali wakapata kuthibitika kwa ajili ya kufungwa kwangu, wamezidi sana kuthubutu kunena neno la Mungu pasipo hofu.

[15]Wengine wanahubiri habari za Kristo kwa sababu ya husuda na fitina; na wengine kwa nia njema.

[16]Hawa wanamhubiri kwa pendo, wakijua ya kuwa nimewekwa ili niitetee Injili;

[17]bali wengine wanamhubiri Kristo kwa fitina, wala si kwa moyo mweupe, wakidhani kuongeza dhiki za kufungwa kwangu.

[18]Yadhuru nini? Lakini kwa njia zote, ikiwa ni kwa hila, au ikiwa ni kwa kweli, Kristo anahubiriwa; na kwa hiyo nafurahi, naam, nami nitafurahi.

Waraka huu Paulo aliuandika akiwa gerezani..Sasa akiwa huko kifungoni kulizuka makundi mawili ya watu ambao walianza kuihubiri injili kama ile ile aliyoihubiri..

Kundi la kwanza lilikuwa na Nia njema kwa Bwana kama ile aliyokuwa nayo Paulo. Kuzihurumia roho za watu na kuifanya kazi ya injili kwa kujitoa kwa upendo bila kujali kama wanapata faida yoyote au la..

Lakini kundi la pili lilikuwa la tofauti..lilianza kuhubiri kwalengo la kumkomoa Paulo na kutaka kujionyesha kuwa na wao wana mamlaka kama yake..N hiyo yote ni kwasababu ya kukua na kujulikana sana kwa huduma ya Paulo ulimwenguni..Hivyo wivu ulipowajaa  wakatumia fursa ya kufungwa kwake kuhubiri injili kwa lengo la kumuonyesha Paulo hana chochote cha ziada kushinda wao. 

Na wengine wakawa wanahubiri huku wakimnenea habari mbaya ili tu kumzidishia vifungo vyake kwa maaskari.

Lakini cha ajabu ni kuwa taarifa hizo zilipokewa tofauti na Paulo..badala ya kuchukia ndio kwanza akafurahia..kwasababu hata kwa njia hiyo injili inahubiriwa na watu wanaokoka..

Ni jambo gani tunaweza kujifunza kwa Paulo na hao wahubiri injili kwa fitina..

Hiyo ni kuonyesha kuwa injili inaweza kuhubiriwa na mtu yeyote na ikaleta matokeo yale yale ya wokovu..hata sasa wapo wahubiri wengi wa uongo wanawavuta watu wa Kristo..lakini hilo haliwafanyi wao kupokelewa na Kristo siku ile ya hukumu..

Bwana Yesu aliliweka wazi hilo katika; 

Mathayo 7:21-23

[21]Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.

[22]Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?

[23]Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu.

Hivyo tuwe makini na kuhubiri kwetu..Je Nia yetu ni kwa Bwana? au kwa lengo la kushindana na mtumishi fulani au mtume fulani au mchungaji fulani au nabii fulani…

Vivyo hivyo…Sisi kama wahubiri hatuna haja ya kurudisha mashambulizi pale tunapoona watumishi wa uongo wanashindana nasi..ikiwa injili wanayoihubiri ni ya kweli basi sisi tufurahie matunda kama alivyofanya Paulo..hayo mengine tumuchie Mungu atayahukumu mwenyewe siku ile..

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Fitina maana yake nini kwenye biblia?

Ni kwa namna gani malaika wa mbinguni wanaweza kutuhubiria sisi injili?

Je! Watu ambao hawajawahi kusikia injili kabisa siku ya mwisho watahukumiwa?

UTAYAFIKIAJE MANENO SAFI YA MUNGU?

Rudi nyumbani

Print this post

FAHAMU JINSI MUNGU NA SHETANI WANAVYOZUNGUMZA NA WATU.

Ulishawahi kuyatafakari kwa makini haya maneno ya Bwana Yesu?

Yohana 8:38 “Niliyoyaona kwa Baba ndiyo niyanenayo; nanyi vivyo hivyo mliyoyasikia kwa baba yenu ndiyo myatendayo”.

Maneno hayo aliwaambia wayahudi (Mafarisayo na waandishi) kipindi kile walipotaka kumuua?. Lakini unaweza kujiuliza ni lini walishakaa chini na kumsikiliza shetani, akizungumza nao kisha akawapa maagizo ya kumwangamiza Bwana Yesu? Ni lini?

Hatuwezi kudhani kuwa shetani alishawahi kukaa chini, na kuanza kunong’ona kwenye masikio yao, na kuwaambia “sasa wanangu wakati wa kumuua Yesu umefika haya nendeni”, Hilo halipo, lakini Bwana Yesu hawezi kusema uongo, ni lazima aliwaona wakimsikiliza shetani, kisha wakaitii sauti yake, na wakafanikiwa kuyafanya yale yote waliyoagizwa na shetani kutenda.. Na ndio maana ukiendelea kusoma pale, utaona anasema..

Yohana 8:44 “Ninyi ni wa baba yenu, Ibilisi, na TAMAA ZA BABA YENU NDIZO MPENDAZO KUZITENDA. Yeye alikuwa mwuaji tangu mwanzo; wala hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake. Asemapo uongo, husema yaliyo yake mwenyewe; kwa sababu yeye ni mwongo, na baba wa huo”.

Ndugu, sauti ya shetani, kamwe usitazamie utaisikia katika maono au ndoto, au kwa mapepo, hali kadhalika sauti ya Mungu vivyo hivyo, Utaisikia sauti ya Mungu kwa kutazama tu yale Mungu anatenda.. Vilevile utaisikia na kuielewa sauti ya shetani pale unapotazama ni nini anatenda..

Kwamfano, tukianzana na hawa wayahudi, ilifikia wakati walimwonea Yesu wivu kisa Mungu anamtumia kwa ukamilifu wote kuwavuta watu wote kwenye nuru, hapo ndipo wakaingiwa na wazo la kutaka kumuua, wazo ambalo walishawahi kuona watu fulani huko nyuma wakilifanya likawaletea matunda, na wao pia wakalichukua. Kumbe hawajui hilo wazo ndio sauti ya shetani yenyewe ikiwapa maelekezo.

Hata leo, wazo la wewe kutaka kurudi nyuma kuzini, tayari hiyo ni sauti ya shetani, na ndio hapo unaitii kwa kuanza kutazama picha za ngono mitandaoni,  unafanya punyeto, unakwenda disco, unatazama muvi zenye maudhui ya mapenzi mapenzi wakati wote, hujui kuwa ni tamaa za ibilisi unazozifanya.. yaani katika ulimwengu wa roho, Yesu anakuona umeketi na shetani kwenye meza moja, ukimsikiliza sauti yake kwa makini sana.

Lakini vivyo hivyo kwa watoto wa Mungu pia kanuni ni ile ile, nao wanamsikiliza Mungu kwa kumtazama vile atendavyo, Kama vile Bwana Yesu alivyosema “Niliyoyaona kwa Baba ndiyo niyanenayo”. Sio maono, hapana, Bwana aliona kazi nyingi za Mungu ulimwenguni hivyo akaziiga akazitenda..

Kwamfano moja ya kazi ambazo Yesu aliziona Baba yake anazifanya akaiga ni pamoja na kuwa na HURUMA,  KUSAMEHE, KUWAPENDA MAADUI na KUFADHILI hata kwa wasio na shukrani.

Luka 6:35 “Bali wapendeni adui zenu, tendeni mema, na kukopesha msitumaini kupata malipo, na thawabu yenu itakuwa nyingi; nanyi mtakuwa wana wa Aliye juu, kwa kuwa yeye ni mwema kwa wasiomshukuru, na waovu.

36 Basi, iweni na huruma, kama Baba yenu alivyo na huruma.

Unaona, hivyo na wewe ukionyesha tabia hizo, kuonyesha fadhili kwa watu wasio na malipo kwako, basi rohoni unaonekana umeketi na Mungu kwenye meza moja ukimsikiliza kwa makini akikupa maagizo ya kufanya, hiyo ni zaidi ya sauti, au ndoto, au maono elfu kumi, unayoweza kuyasikia.

Mathayo 5:46 “Maana mkiwapenda wanaowapenda ninyi mwapata thawabu gani? Hata watoza ushuru, je! Nao hawafanyi yayo hayo?

47 Tena mkiwaamkia ndugu zenu tu, mnatenda tendo gani la ziada? Hata watu wa mataifa, je! Nao hawafanyi kama hayo?

48 Basi ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu”.

Kwahiyo, tujifunze kuitambua sauti ya Mungu wetu kwa kuzitazama kazi zake, vilevile tujifunze kuielewa sauti ya adui yetu ibilisi, ili tuweze kumkwepa na yeye, kwasababu kamwe tusitazamie, sikumoja atakuja kutunong’oneza kwenye masikio yetu “nenda ukazini”, hilo halipo.

Je! Umeokoka? Je! Unafahamu kuwa tupo katika muda wa nyongeza tu, siku yoyote Kristo anarudi. Unasubiri nini huko nje? Utajisikiaje usikie unyakuo umepita halafu wewe umebaki, utamweleza nini Bwana Yesu. Tubu dhambi zako leo kwa kumaanisha kabisa kumrudia Mungu wako, injili tuliyobakiwa nayo sio ya kubembelezewa wokovu tena, ni wewe mwenyewe kuona na kuchukua hatua. Muda umeisha.

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Je ni kweli imani ya mtu ndiyo itakayomuokoa, na si kitu kingine?

UNYAKUO.

TUMEFANYIKA KUWA WANA WA MUNGU!

Makerubi wenye sura nne, ni kweli wapo? na je! wanyama wataenda mbinguni?

Rudi nyumbani

Print this post