Title December 2020

Kwanini biblia inaitaja mara kwa mara dhahabu ya Ofiri?

SWALI:Kwanini biblia inaitaja mara kwa mara dhahabu ya Ofiri? Umuhimu wake ni upi?


Ofiri ni eneo, lililokuwa maarufu zamani enzi za biblia kwa biashara ya madini na vito, eneo hili lilikuwa maeneo ya huko Arabia. Kwamfano dhahabu zote Sulemani alizotumia kujengea hekalu alikwenda kuzichukulia huko Ofiri kwa merikebu zake (Wafalme 10:22)

Ni sawa na leo useme dhahabu ya Geita, Au Tanzanite ya mererani,. Ndivyo ilivyokuwa zamani dhahabu au mawe ya thamani yalikuwa yapatikana eneo hilo la Ofiri.

 Hivi ni baadhi ya vifungu ambavyo utaweza kukutana na Neno hilo;

1Wafalme 9:28 “Wakafika Ofiri, wakachukua toka huko dhahabu, talanta mia nne na ishirini, wakamletea mfalme Sulemani”.

1Wafalme 10: 11 “Tena merikebu za Hiramu, zilizochukua dhahabu kutoka Ofiri, zikaleta kutoka Ofiri miti ya msandali mingi sana, na vito vya thamani”.

1Wafalme 22: 48 “Yehoshafati akafanya merikebu za Tarshishi ziende Ofiri kuchukua dhahabu; walakini hazikuenda; kwa maana merikebu zilivunjika huko Esion-geberi”.

Ayubu 22: 24 “Nawe hazina zako ziweke mchangani, Na dhahabu ya Ofiri iweke kati ya mawe ya vijito”;

Soma pia, Ayubu 28:16,

Sasa tukilijua hilo, upo unabii ambao Isaya aliuzungumza kuhusu siku ile ya Bwana inayotisha, akasema jinsi Mungu atakavyoleta maangamizi, watu wataadimika sana, kama dhahabu, tena akaeleza kwa mifano kabisa akasema, wataadimika kama ile dhahabu ya Ofiri, watu wanaoifahamu sana,  ili watu wapate  picha yenyewe jinsi mambo yatakavyokuwa mabaya, ni sawa na leo tuseme, watu watakuwa adimu kama Tanzanite, ile Tanzanite ya mererani..

Tusome;

Isaya 13:9 “Tazama, siku ya Bwana inakuja, siku kali, ya hasira na ghadhabu kuu, ili iifanye nchi kuwa ukiwa, na kuwaharibu watu wake, wenye dhambi, wasikae ndani yake.

10 Maana nyota za mbinguni na matangamano havitatoa nuru yake; jua litatiwa giza wakati wa kucha kwake, na mwezi utaacha nuru yake isiangaze.

11 Nami nitaadhibu ulimwengu kwa sababu ya ubaya wake, na wenye dhambi kwa sababu ya hatia yao; nami nitaikomesha fahari yao wenye kiburi; nami nitayaangusha chini majivuno yao walio wakali;

12 nitafanya wanadamu kuadimika KULIKO DHAHABU SAFI, na WATU KULIKO DHAHABU YA OFIRI.

13 Kwa hiyo nitazitetemesha mbingu, na dunia itatikiswa itoke katika mahali pake, kwa sababu ya ghadhabu ya Bwana wa majeshi, na kwa sababu ya siku ya hasira yake kali”.

Siku hiyo  watu wengi sana watakufa,idadi isiyohesabika, watauliwa na Mungu mwenyewe, kiasi kwamba kumwona mwanadamu mwenzako ulimwenguni itakuwa ni kama vile kuona dhahabu..Kwa jinsi watakavyoadimika.

Leo hii duniani kuna watu si chini ya bilioni saba, hatushangai wakati huo wakabaki watu elfu moja tu, au hata chini ya hapo. Ni kama ilivyokuwa kipindi cha Nuhu kati ya mabilioni ya watu waliokuwepo duniani, walibaki watu nane tu, vivyo hivyo siku ile ya Bwana itakuwa kwa namna hiyo.

Siku hizo zipo karibu sana, kwasababu biblia inasema, uharibifu utakuja wa ghafla wakati ambao watu hawautarajii kabisa, wakati ambao  wanasema kuna amani. (1Wathesalonike 5:3)

Lakini habari njema ni kwamba mpaka hiyo siku ya Bwana ije duniani, unyakuo utakuwa tayari umeshapita, na watakatifu wameshanyakuliwa.

Vivyo hivyo na sisi wakati huu ni wa kujiweka tayari, kumtazama Bwana. Na kuhakikisha kuwa wokovu upo ndani yetu. Ili hata kama unyakuo utapita leo usiku basi, tuwe na uhakika hatubaki hapa duniani, kwenye ghadhabu na hasira ya Mungu.

Shalom

Ili kufahamu kwa undani siku hiyo itakavyokuwa tazama vichwa cha masomo mengine chini;

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

KIAMA KINATISHA.

UTAWALA WA MIAKA 1000.

ROHO YA MPINGA KRISTO IKITENDA KAZI SIKU HIZI ZA MWISHO

Rudi nyumbani

Print this post

Kwanini Mungu aliwaagiza wana wa Israeli wasikisaze chakula?

SWALI: Kwanini Mungu aliwaagiza wana wa Israeli siku ile ya kuondoka wasikisaze chakula hata asubuhi?


JIBU: Kusaza chakula maana yake ni kukibakisha ili ukimalizie kukila baadaye au kesho yake…Na hiyo inaweza kutokana na mtu kushiba sana wakati huo, hivyo badala ya kukimwaga anakuwa anakihifadhi hicho chakula ili akimalizie kukila tena wakati mwingine.

Kama tunavyojua siku ile wana wa Israeli walipokuwa wanatoka Misri, Mungu aliwapa maagizo kuwa usiku ule kabla ya kuondoka wamchinje mwanakondoo, na damu yake waipake kwenye miimo ya milango, na kisha wamle yule mwanakondoo waliomchinja, (na maagizo hayo yaliihusu kila familia), hivyo kila familia ilichinja mwanakondoo na damu yake kuipaka milangoni, na kumla yule mwanakondoo..Na yalikuwepo pia maagizo ya namna ya kumpika, utaona waliambiwa wasimtokose majini, yaani wasichemshe(wasile mchemsho), bali wamuoke motoni..vilevile  wamle pamoja na mboga chungu, na kwa haraka sana maana yake wasijivutevute wakajikuta kumepambazuka na bado hawajamaliza kula ikawa dhambi.

Sasa pamoja na maagizo yote hayo walipewa agizo lingine tena la msingi, kwamba Huyo mwanakondoo watakayemla, kila familia ihakikishe haisazi nyama yake mpaka asubuhi, maana yake ni kwamba aidha wamle wote amalizike, au wamle mpaka pale watakapoona wameshiba na kama  bado nyama ipo, basi waitwae ile nyama na waiteketeze kwa moto, kisisalie chochote kabla hakujapambazuka..Maana yake ni kwamba kama kuna familia haitafanya hivyo, itakuwa imetenda dhambi kwa Bwana Mungu. Unaweza kuyasoma maagizo hayo vizuri katika kitabu cha (Kutoka 12:1-13).

Sasa ni kwanini Mungu alitoa hayo maagizo?

Sababu ni  kwamba Bwana alikuwa ameanza kuwafundisha wana wa Israeli wamtegemee yeye kwa asilimia mia moja. Kwamba wasiwe na hofu ya kesho, watakula nini, watavaa nini.. bali akili zao zote zianze kumfikiria yeye. Kwasababu asingefanya hivyo, watu usiku ule ule wangekula kidogo na kusema tuache kingine kwaajili ya kesho asubuhi kunywea chai, hivyo wangeanza kufikiri matumbo zaidi ya kumfikiria Mungu.

Na pia utazidi kuona Mungu hata ile MANA ambayo walikuwa wanalishwa iliyotoka mbinguni, Bwana Mungu aliwakataza wasiweke akiba, wala wasiisaze, aliwaambia wakusanye chakula cha siku moja, wakile wakimalize chote wasikisaze wakile tena kesho, kwasababu hiyo kesho Mungu atawapa kingine..hivyo wasiwe na hofu ya kesho kwamba watakula nini?..Lakini baadhi yao hawakuitii sauti ya Mungu, wakawa wanakisaza matokeo yake vikatoa uvundo..

Kutoka 16:19 “Musa akawaambia, Mtu awaye yote asikisaze hata asubuhi.

20 Lakini hawakumsikiza Musa; wengine miongoni mwao wakakisaza hata asubuhi, nacho kikaingia mabuu na kutoa uvundo; Musa akawakasirikia sana.

21 Basi wakaokota asubuhi baada ya asubuhi, kila mtu kama ulaji wake ulivyokuwa; na hapo jua lilipokuwa ni kali, kikayeyuka”

Jambo hilo hilo ni somo kwetu, kwamba Tusiwe na hofu sana kuhusu maisha yetu, baada ya kuokoka.. Hatupaswi kuwa na hofu ya kupitiliza kuhusu kesho zetu, kwamba tutakula nini, au tutavaa nini, hata kama leo tunaona hakuna dalili ya kuiona hiyo kesho.Bado tunapaswa kufahamu kuwa ya kesho itajisumbukia, na Mungu atafungua mlango tu. Kama Bwana Yesu alivyosema mahali fulani..

Mathayo 6:31  “Msisumbuke, basi, mkisema, Tule nini? Au Tunywe nini? Au Tuvae nini?

32  Kwa maana hayo yote Mataifa huyatafuta; kwa sababu Baba yenu wa mbinguni anajua ya kuwa mnahitaji hayo yote.

33  Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa.

34  Basi msisumbukie ya kesho; kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe. Yatosha kwa siku maovu yake”.

Baba yetu anajua tuna haja na hayo yote, hawezi kutuokoa na kutuacha yatima kabisa..yupo pamoja na sisi kuhakikisha anatuhudumia kwa mahitaji yetu ya kila siku.

Sasa kama umeona ni wakati wa kuweka akiba sasa iweke, hufanyi dhambi, lakini jiangalie jinsi unavyojiwekea hiyo akiba, kwasababu kama utajiwekea akiba na huku moyoni mwako Mungu umemwacha, na huku tumaini lako lote lipo katika hiyo akiba yako uliyojiwekea, utapotea kama yule Tajiri wa kwenye Luka 16:19.

Lakini kama utajiwekea akiba kulingana na mapenzi ya Mungu, basi utafanikiwa…

Sasa swali utajiwekeaje akiba sawasawa na mapenzi ya Mungu ?

Turudi kwenye huo mfano wa Mana. Ukiendelea kusoma mbele kidogo utaona akiba iliyompendeza Mungu ilikuwa ni ipi..Tusome.

Kutoka 16: 21 “Basi wakaokota asubuhi baada ya asubuhi, kila mtu kama ulaji wake ulivyokuwa; na hapo jua lilipokuwa ni kali, kikayeyuka.

22 Basi ikawa siku ya sita wakaokota kile chakula sehemu maradufu, kila mtu pishi mbili; na wazee wote wa mkutano wakaenda na kumwambia Musa.

23 Akawaambia, Ndilo neno alilonena Bwana KESHO NI STAREHE TAKATIFU, SABATO TAKATIFU KWA BWANA; OKENI MTAKACHOOKA, NA KUTOKOSA MTAKACHOTOKOSA; NA HİCHO KITAKACHOWASALIA JİWEKEENI KILINDWE HATA ASUBUHI.

24 Basi wakakiweka hata asubuhi, kama Musa alivyowaagiza; NACHO HAKİKUTOA UVUNDO WALA KUINGIA MABUU.

25 Musa akasema, Haya, kuleni hiki leo; kwa kuwa leo ni Sabato ya Bwana; leo hamtakiona nje barani”.

Umeona hapo?.. Walipojiwekea akiba ili kwamba kesho yake (ambayo ni siku ya sabato), wasiwe bize kutafuta hicho chakula,ILA WAWE BIZE KUMTAFUTA MUNGU..Hapo ndipo akiba yako haikuoza, Na ndiyo akiba iliyompendeza Mungu, ndio maana hicho walichokiweka akiba hakikutoa uvundo kesho yake. Lakini pale walipojiwekea akiba kwa lengo la kujikusanyia hazina ya kesho, ili wastarehe tu ndani, kesho yake wasitoke kwenda kutafuta, wakafanye anasa, walale, wacheze, waruke, wafurahi, wacheze cheze kidogo, hapo ndipo akiba yao ilipoingia mabuu..

Hivyo na sisi akiba zinazompendeza Mungu, ni zile tutakazosema…Leo nitafanya kazi sana, au wiki hii yote nitatumia muda mwingi kufanya kazi sana, na kukusanya akiba ya wiki mbili…kwasababu wiki inayokuja yote nitakuwa bize kuomba, au nitakuwa bize kuhubiri, sitapata muda wa kushughulika…Ukiweka akiba kwa malengo hayo, hapo ndipo akiba hiyo inakuwa haiozi, na zaidi ya yote Mungu anafungua milango ya baraka mara mbili zaidi sasa.. Lakini akiba ya kujiwekea mali nyingi, na huku huna malengo yoyote na Mungu, akiba hiyo inaoza, unaweka akiba ili wiki ijayo upate muda wa kulala, upate nafasi ya kwenda disko, ili utakapokuwa mzee upumzike, utakapokuwa, uwe tajiri sana wa kuheshimika, hata mpaka jumapili huendi kanisani, … Kesho utaamka haipo, imepukutika yote, hiyo miaka itafika utaikuta hiyo akiba imeingia mabuu na inatoa uvundo.

Luka 12: 16  “Akawaambia mithali, akisema, Shamba la mtu mmoja tajiri lilikuwa limezaa sana;

17  akaanza kuwaza moyoni mwake, akisema, Nifanyeje? Maana sina pa kuyaweka akiba mavuno yangu.

18  Akasema, Nitafanya hivi; nitazivunja ghala zangu, nijenge nyingine kubwa zaidi, na humo nitaweka nafaka yangu yote na vitu vyangu.

19  Kisha, nitajiambia, Ee nafsi yangu, una vitu vyema vingi ulivyojiwekea akiba kwa miaka mingi; pumzika basi, ule, unywe, ufurahi.

20  Lakini Mungu akamwambia, Mpumbavu wewe, usiku huu wa leo wanataka roho yako! Na vitu ulivyojiwekea tayari vitakuwa vya nani?

21  NDIVYO ALIVYO MTU AJIWEKEAYE NAFSI YAKE AKIBA, ASIJITAJIRISHE KWA MUNGU”.

Bwana atusaidie na kutubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mada Nyinginezo:

Rudi nyumbani

Print this post

NI SAA KUMI NA MBILI (12) TU, ZA KRISTO KWAKO.

Shalom. Bwana Yesu alisema maneno haya;

Yohana 11:9 “…… Je! Saa za mchana si kumi na mbili? Mtu akienda mchana hajikwai; kwa sababu aiona nuru ya ulimwengu huu.

10 Bali akienda usiku hujikwaa; kwa sababu nuru haimo ndani yake”.

Utajiuliza ni kwanini Bwana Yesu alijifananisha  na Nuru ya ulimwengu?  Ambayo ni JUA linalofanya kazi saa kumi na mbili tu, Ukilitafakari hilo kwa ukaribu ndipo utakapofahamu kuwa hii neema tuliyopewa sio ya kuichezea hata kidogo.

Zamani watu walikuwa hawajua tabia ya jua, walikuwa wanadhani kule linapochomoza, limetoka kuamka, na kule linapokwenda kuzama ndio linakwenda kulala. Lakini sisi tunaoishi sasa ndio tunafahamu vizuri  mambo yote, kwamba jua halilali wala haliamki, isipokuwa linalala linalala na kuamka kwetu sisi tunaolitegemea. Lakini lenyewe kama lenyewe linaangaza daima.

Wakati ambapo jua hulioni, wapo wengine wanaliona upande wa pili wa dunia, na wakati ambapo wale wa upande wa pili  hawaliona lipo upande wako wewe linaangaza.. Na kama ilivyo kawaida wakati ambao unaliona ndio unatumia fursa hiyo  kufanya mambo yako, kwa kujali muda, tangu asubuhi mpaka jioni, kwasababu unajua kabisa, kuwa  giza likishaingia, hakuna shughuli yoyote unayoweza kuendelea kuifanya.

Kama wewe ni msusi, kazi yako ya ususi siku hiyo inakuwa imeisha, kama wewe ni mkulima, unaweka jembe lako mgongoni unarudi nyumbani, kama wewe ni fundi wa nyumba unafunga marago yako, unakwenda nyumbani kupumzika na familia yako.. Kwasababu hakuna kazi yoyote inayofanyika kwa ufanisi usiku..

Muda wa kazi kwako unakuwa umeshakishwa kwasababu nuru haipo, ni wakati wa watu wengine walio  upande wa pili wa dunia kuamka na kufanya kazi. Na ndivyo ilivyo hata kwa Kristo Yesu Bwana wetu. Alisema

Yohana 9:4 “Imetupasa kuzifanya kazi zake yeye aliyenipeleka maadamu ni mchana, usiku waja asipoweza mtu kufanya kazi.

5 MUDA NILIPO ULIMWENGUNI, MIMI NI NURU YA ULIMWENGU. Na tena alisema..

Yeye ni Nuru ambayo itaendelea kudumu kwa wakati wote humu duniani mpaka atakapurudi mara ya pili. Lakini wa bahati mbaya ni kuwa Nuru yake haidumu kwa watu wote ulimwenguni kwa wakati mmoja..

Ikiwa na maana  kuwa neema yake ya wokovu, haipo kwa watu wote duniani sasa hivi, kwa wakati mmoja. Hili jambo linaweza likawa ni gumu kwako kulielewa, lakini ndio ufahamu leo kuwa neema ya wokovu haipo kwa watu wote unaowaona leo hii duniani..

Biblia inatufundisha kuwa wayahudi walipata neema ya kuhubiriwa na Yesu lakini walimkataa, hawakujua kuwa hilo jambo sio la kudumu milele. Na ulipofika wakati wa masaa yao 12 kuisha neema hiyo ilihamia kwetu sisi watu wa mataifa, tukaanza kuhubiriwa na sisi  injili, wao wakabakia kama vile wapagani, na jambo hilo liliendelea kwa muda mrefu hadi sasa ni miaka takribani 2000 bado neema hiyo hajawarudia ya kuiamini injili. Hili jambo linatisha sana.

Sio kwamba mioyo yao ni mizito kupita sisi, hapana, ni kwasababu Nuru ya wokovu haipo tena kwao, ipo upande wa pili wa ulimwengu ambao ni ndio sisi watu wa mataifa..

Lakini hilo nalo sio la kujisifia, kwasababu na kwa upande wetu sisi, bado kila eneo na taifa, lina masaa yake 12, na ndio maana ukiangalia katika historia ya kanisa utaona, kanisa la kwanza lilianzia kule Bara la Asia, na wakati wao ulipopita, ikahamia, bara la Ulaya, na wao pia wakati wao ulipopita ilihamia bara la Amerika, na wakati wao pia ulipopita ndio ikarudi bara letu la Afrika.

Na ndio maana kwanini leo hii unaona kuna mwitikio mkubwa wa Mungu huku Afrika kuliko sehemu nyingine yoyote ulimwenguni, nikwasababu Nuru ya ulimwengu ipo kwetu sasa, Lakini na sisi tupo ukiongoni kabisa wa saa zetu 12,kwasababu sisi ndio tunaomalizia kabla ya neema hii kurudishwa Israeli tena. Kama ulikuwa hujui mpaka sasa wayahudi Mungu ameshawaandaa moyo ya kumwamini Kristo na neema hiyo ikishapita kwetu ndugu yangu, dunia nzima, yaani sisi tuliobakia mataifani, hakutakuwa na neema tena ya wokovu..tutabakia tu kuwa wapagani kuliko hata wapagani wenyewe walivyo.

Lakini hilo la neema kuwepo Afrika sio la kujivunia kwasababu bado neema hii, inazunguka kati ya mtu na mtu. Yaani mimi na wewe kila mmoja wetu, ametengewa muda wa kuiona Nuru hiyo ya ulimwengu (yaani Yesu Kristo), Na kama usipojua wakati wako wa kujiliwa ni upi na ni nini unapaswa ufanye kwa wakati huo, kama ilivyokuwa kwa Israeli wakati ule Yesu alipowalilia, hakapuuzia, na wewe ukadhani Roho Mtakatifu atakuwa na nafasi kila siku ya kukuvuta kwake umwamini Kristo, nataka nikuambie ndugu yangu umekwisha.

Ikiwa leo hii, unasikia msukumo fulani wa kumgeukia Kristo, ujue huyo ni Roho Mtakatifu ndani yako, ujue hiyo ni Nuru ya Kristo ndani yako inakumulikia, uone njia.  Ni jukumu lako kuifuata, na kuitii bila kupoteza poteza muda, na kutenda yanayokupasa kufanya..

Kumbuka tena alisema..

Yohana 11:9 “Yesu akajibu, Je! Saa za mchana si kumi na mbili? Mtu akienda mchana hajikwai; kwa sababu aiona nuru ya ulimwengu huu.

10 Bali akienda usiku hujikwaa; kwa sababu nuru haimo ndani yake”.

Akiwa na maana kuwa kuna wakati utafika,  hutampata  Kristo hajialishi kuwa utajifanya unamtafuta kiasi gani, utaishia tu kujikwaa, na unajua kujikwaa kunavyoumiza, Maana yake ni kuwa utakuwa unatilia shaka kila kitu kwenye maandiko, utafikia wakati utasema hata Mungu hayupo, utaishia kuamini, historia za wanasayansi, na sio Mungu tena, utaishia kudhihaki tu injili, au kusema hakuna Mungu, hiyo yote ni kwasababu Nuru hiyo haipo ndani yako tena. Hata uhubiriweje vipi, kamwe huwezi kushawishika tena tena kama unavyoshawishika leo.

 Lakini wakati huo huo utaona jirani yako, anaamini injili na anasimama, na Kristo anatembea naye, wewe utabakia kusema Yule ni mwandawazimu tu.

Umeona, hii neema sio ya kuchezea kabisa, ni kweli bado ipo duniani haijaondoka, lakini huwa haina tabia ya kuganda sehemu moja, inazunguka, , kama wakati wako umefika halafu unaipuuzia, ikiondoka hutaipata tena. Tujifunze kwa waisraeli ili tumwogope Mungu.

Lakini kama leo utaahirisha  maisha yako ya dhambi, na unataka kumpa Yesu maisha yako, akuokoe, basi tutafute inbox, au piga namba hizi tuombe kwa pamoja +255789001312

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mada Nyinginezo:

Rudi nyumbani:

Print this post

“Shinikizo” ni nini kibiblia, Na maana yake rohoni ni ipi?

Shinikizo ni shimo au kisima fulani kilichotengenezwa mahususi  kwa ajali ya kukamulia zabibu,. Zabibu zinavyokamuliwa leo ni tofauti jinsi zilivyokamuliwa zamani, leo hii ni mashine ndio zinazotumika kukamua juisi. Lakini zamani ilikuwa ni tofauti.

Walichokuwa wanakifanya mara baada ya kutengeneza au kuchimba a kisima hicho, walizitupa zababu ndani yake na kujaa, kisha wanaume walikuwa wanaingia ndani ya kisima hicho na kuanza kuzikanyaga kanyanga, wakisapotiwa na kamba kwa juu, ili wapate uwiano(balance),. Sasa kwa pembeni walikuwa wanatengeneza kimfereji ambacho, kilielekeza juisi yote ya zabibu katika kisima kingine kidogo, ambapo ndani ya hichi kijisima sasa waliweza kuichota juisi ile  ya zababu ikiwa safi kabisa kwa matumizi yao mbalimbali.. Tazama picha juu.

Hivi ni baadhi ya vifungu ambavyo unaweza kulisoma Neno hilo;

Mathayo 21:33 “Sikilizeni mfano mwingine. Kulikuwa na mtu mwenye nyumba, naye alipanda shamba la mizabibu, akalizungusha ugo, akachimba shimo la shinikizo ndani yake, akajenga mnara, akapangisha wakulima, akasafiri.

34 Wakati wa matunda ulipokuwa karibu, akawatuma watumwa wake kwa wale wakulima, wapokee matunda yake”.

Hagai 2:16 “katika wakati huo wote, mtu alipofikia chungu ya vipimo ishirini, palikuwa na vipimo kumi tu; na mtu alipofikia shinikizo apate kuteka divai ya vyombo hamsini, palikuwa na divai ya vyombo ishirini tu.

Soma pia kwa muda wako, Isaya 5:2, Hagai 2:16, Waamuzi 7:25, Nehemia 13:15, Ayubu 24:11, Isaya 63:3

SASA NENO HILI LINA MAANA GANI ROHONI?

Tukirudi katika kitabu cha Ufunuo tunaona, Yesu Kristo Bwana wetu, anajitambulisha kama yeye ndiye atakayekuwa mhusika mkuu wa  kukanyaga shinikizo la ghadhabu ya Mungu siku ile ya mwisho..

Ufunuo 19:15 “Na upanga mkali hutoka kinywani mwake ili awapige mataifa kwa huo. Naye atawachunga kwa fimbo ya chuma, naye anakanyaga shinikizo la mvinyo ya ghadhabu ya hasira ya Mungu Mwenyezi”.

Yaani kwa lugha iliyo rahisi ni kuwa Bwana Yesu atakaporudi, yeye ndiye atakayetekeleza ile hasira ya Mungu ambayo alikuwa amehifadha kwa ajili ya watu wote waovu waliopo ulimwenguni leo hii.  Wakati huo unyakuo utakuwa umeshapita, mataifa yote yatamwombolezea siku atakaporudi, kutakuwa na mambo ya kutisha sana, kiasi mpaka biblia inatuambia, watu watatamani hata milima iwaangukie, ili tu wajiepusha na ghadhabu hiyo kali ya Mungu itakayoachiliwa duniani wakati huo, lakini halitawezekana ni lazima washiriki mapigo hayo (Ufunuo 6:16). Na ni Yesu ndiye atakayeitekeleza ghadhabu hiyo. Watu watakufa kama kumbikumbi, damu nyingi sana zitamwagika duniani..

Ufunuo 14:19 “Malaika yule akautupa mundu wake hata nchi, akauchuma mzabibu wa nchi, akazitupa zabibu katika shinikizo hilo kubwa la ghadhabu ya Mungu.

20 Shinikizo lile likakanyagwa nje ya mji, damu ikatoka katika shinikizo mpaka kwenye hatamu za farasi, kama mwendo wa maili mia mbili”.

KUPEWA KIKOMBE CHA MVINYO YA GHADHABU YA HASIRA YAKE.

Kipindi hicho sio cha kukitamani ndugu yangu.. SIKU YA BWANA INATISHA SANA,…Kwa urefu wa habari hizo fungua link hizi upitie ndugu ili ufahamu kitakachokwenda kutokea kwa watu wote watakaoukosa unyakuo leo >>

  1. KIAMA KINATISHA.
  2. MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

Kimbuka kikombe hicho cha mvinyo wa ghadhabu ya Mungu, kila mwovu atakishiriki.

Ufunuo 16:19 “Na mji ule mkuu ukagawanyikana mafungu matatu, na miji ya mataifa ikaanguka; na Babeli ule mkuu ukakumbukwa mbele za Mungu, KUPEWA KIKOMBE CHA MVINYO YA GHADHABU YA HASIRA YAKE.

20 Kila kisiwa kikakimbia, wala milima haikuonekana tena.

21 Na mvua ya mawe kubwa sana, ya mawe mazito kama talanta, ikashuka kutoka mbinguni juu ya wanadamu. Wanadamu wakamtukana Mungu kwa sababu ya lile pigo la mvua ya mawe; kwa maana pigo lake ni kubwa mno”.

Hivyo mimi na wewe, tuhakikishe, leo hii kuwa tupo upande salama, kwa kumpa Yesu maisha yetu ayaokoe, ndani ya kipindi hichi kifupi cha neema tulichobakiwa nacho. Upo wakati hatutaiona hii neema tuliyonayo sasa. Hivyo tubu, mgeukie Kristo. Hizi ni siku za mwisho.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

UTAWALA WA MIAKA 1000.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

EPUKA MUHURI WA SHETANI

UFUNUO: Mlango wa 1

Rudi nyumbani

Print this post

Herode aliliwa na chango, Je, chango ni nini kibiblia?

Matendo 12:21 “Basi siku moja iliyoazimiwa, Herode akajivika mavazi ya kifalme, akaketi katika kiti cha enzi, akatoa hotuba mbele yao.

22 Watu wakapiga kelele, wakisema, Ni sauti ya Mungu, si sauti ya mwanadamu.

23 Mara malaika wa Bwana akampiga, kwa sababu hakumpa Mungu utukufu; akaliwa na chango, akatokwa na roho”.

Hili ni pigo, na sio ugonjwa wa kawaida, na ndio maana hakuna sehemu nyingine yoyote, unaweza kuona ugonjwa huu ukirekodiwa kwenye biblia. Ni sawa na wakati ule wa Mfalme Nebukadreza, alivyojitukuza mbele za Mungu, akajiona kuwa yeye ndiye mfalme wa dunia wala hakuna mwingine kama yeye duniani kote, japokuwa kuwa alionywa hapo kabla,  kwa hizo tabia zake lakini hakusikia, hakujua kuwa ni Mungu ndiye anayewamilikisha wafalme (Danieli 2:21) lakini yeye hakulisikia hilo.. Ndipo siku ya siku malaika wa Mungu akampiga kwa pigo ambalo mpaka sasa, halijulikani lilikuwa ni pigo la namna gani lile, lililomfanya mpaka awe kama mnyama  asiyeeleweka wa kufukuzwa, mbali na makazi ya watu.

Hivyo ndivyo  ilivyomkuta na huyu Herode. Siku moja alikaa katika kiti chake cha enzi akatoa hutuba yake pengine yenye ushawishi mkubwa, hotuba yenye hoja nzuri, iliyojaa sifa na utukufu wake mwenyewe.. Na watu walipoona vile, wakapiga kelele, wakimsifia sana, Lakini ni heri wangeishia hapo, wale watu wakafakia hatua ya kusema ile ni sauti ya Mungu sio ya mwanadamu..yaani kwa namna nyingine ni Mungu ndiye aliyesimama mbele yako na kuzungumza naye. Na yeye Herode akilijua hilo, kuwa yeye ni mwanadamu tu, akazipokea sifa zile. Zilichofuata baada ya pale ni malaika wa Mungu kumpiga kwa pigo hilo la ugonjwa wa ajabu akaliwa na chango.

Chango ni funza, unaweza kutengeneza picha, unatoka muda huo huo, unaanza kuugua na funza  wanatoka katika mwili wako bado ukiwa hai mpaka unakufa. Kama tunavyojua kwa namna ya kawaida  mpaka mtu afikie hatua hiyo ni kwamba alishakufa siku nyingi, mwili ushaoza ndipo funza wanatokeza nje. Lakini yeye yalimkuta bado akiwa fresh duniani.

 Ugonjwa huu kihistoria inasemekana ulimpata mfalme mmoja aliyeitwa Antiokia Epifane,  ambaye huyu alilinajisi hekalu la Mungu zamani, kabla ya Kristo kuzaliwa, enzi ya kipindi cha Wamakabayo, hadi kufikia hatua ya kuingiza nguruwe hekaluni mambo ambayo Mungu aliyakataza, lakini baadaye Mungu alimpiga kwa ugonjwa mfano kama huu, wa majipu mabaya sana ambayo yalimfanya funza watokezee nje ya mwili wake, na kufa.

Ni ugonjwa wa maumivu makali sana,.. Ni ugonjwa ambao si wa kawaida, kwasababu ni wapigo.

Vivyo hivyo na sisi pia tunapaswa, tuwe makini sana. Watu wengi wanadhani, utukufu wa Mungu unachukuliwa pale tu miujiza au uponyaji unapofanyika, katikati ya watumishi wa Mungu.. Jibu ni lala, wote hawa tuliowasoma hawakuwa wakristo. utukufu wa Mungu unachukuliwa hata na watu wa kidunia, na wao pia wanaweza kushiriki mapigo ya Mungu vilevile kama wale wanaoitenda kazi ya Mungu..

Isaya 42:8 “Mimi ni Bwana; ndilo jina langu; na utukufu wangu sitampa mwingine, wala sitawapa sanamu sifa zangu”.

Mungu ni Mungu mwenye wivu, unapokuwa kiongozi, halafu unataka watu wakusifie wewe, kana kwamba unafanya mambo hayo kwa nguvu zako, Humpi Mungu utukufu. uwe makini sana utaliwa na chango,

Unapojaliwa utajiri, au umaarufu kwa watu, halafu wewe kazi ya ni kujisifia tu, kujionyesha wewe ni Mungu-mtu duniani, huwi mnyenyekevu, jiangalie sana utakutwa na matatizo ambayo, hata jamii itashindwa kuelewa chanzo chake ni nini?

Jambo lolote unalolifanya liwe la ki-Mungu, au la Ki-binadamu, ambalo lina sifa yoyote ndani yake.. mrudishie Mungu utukufu, ili Mungu akuhurumie, hii dunia sio yetu, hii dunia ni ya Mola wetu, hivyo ni wajibu wa kila mmoja wetu, kuonyesha kuwa kila alichojaliwa nacho ni kwa uweza wa Mungu.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MLANGO MWINGINE WA ADUI KUTULETEA MAJARIBU.

Mlango uitwao “Mzuri” Unaozungumziwa katika Matendo 3:2 ndio upi?

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita..

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 10 (Kitabu cha Zaburi).

YEZEBELI ALIKUWA NANI

DANIELI: Mlango wa 12.

Rudi nyumbani

Print this post

MLANGO MWINGINE WA ADUI KUTULETEA MAJARIBU.

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze biblia.

Kama tunavyojua adui yetu wa kwanza na wa mwisho ni shetani, ambaye biblia inasema anazunguka huko na huko kama simba akitafuta mtu wa kummeza 1Petro 5:8, hivyo ni wajibu wetu kujua kuwa tupo katika shabaha ya adui.

Sasa ipo milango ambayo shetani anaitumia sana kuleta mashambulizi kwa mtu, na mashambulizi hayo yanaweza kuwa ni magonjwa ya kimwili, na ya kiroho (mfano kusumbuliwa na roho za mapepo, ikiwemo hofu, na mashaka, na madhaifu mbali mbali). Ukiona unazo dalili hizo basi kuna uwezekano mkubwa umeshambuliwa na adui.

Ifuatayo ni milango mikubwa ambayo inafungua fursa ya mashambulizi ya kiroho na kimwili, kutoka kwa adui.

UASHERATI NA ZINAA.

Huu ndio mlango wa kwanza na mkubwa, unaoharibu maisha ya watu wengi kiroho na kimwili. Mlango huu ndio wa kwanza hata zaidi ya ushirikina, mtu yeyote anayefanya uzinzi/ uasherati..katika roho ni kama ametangaza kuwa yeye ni nyumba ya kila roho chafu..Ni mlango tosha wa pepo la aina yeyote kumwingia huyo mtu.

Milango mingine ni pamoja na ushirikina, ibada za sanamu, kutokusamehe, chuki, uuaji n.k

Sasa unaweza kuwa hufanyi zinaa, wala sio mshirikina,huabudu sanamu, wala sio mlevi, wala muuaji..wala hufanyi mambo mengine yote yasiyompendeza Mungu, lakini bado unaona kuna mashambulizi unayapata..

Ukiona unapitia hali kama hiyo, basi fahamu kuwa shetani amekushambulia kwa mlango mwingine ambao huujui wewe wala hukuidhania.

NA HUO SI MWINGINE ZAIDI YA MLANGO WA MAOMBI.

Kumbuka maombi tunayoyazungumzia hapa sio maombi ya kuombewa, kwamfano kuwekewa mikono na mtumishi au mtu fulani, Hapana!, bali ni yale maombi ya mtu binafsi kumwomba Mungu juu ya mambo yake, na ya wengine. Na hayo sio ya dakika 5, wala 10…bali ni yale yasiyopungua saa moja. Na sio lisaa limoja kwa wiki au mwezi, bali angalau lisaa limoja kwa siku.

Shetani kawapotosha wengi na kufikiri ukishamwamini Yesu tu, basi hakuna sababu ya kuomba mara kwa mara, kwani tumeshafunikwa na damu, pale tulipompokea. Yanini kuomba kila siku?. Usidanganyike!..Bwana Yesu pamoja na ukamilifu wake wote, lakini alikuwa anaomba dua nyingi tena kwa machozi mengi kila siku. (Soma Waebrania 5:7).

Na Bwana Yesu huyo huyo alisema..

Luka 22:46 “Akawaambia, Mbona mmelala usingizi? Ondokeni, mkaombe, msije mkaingia majaribuni”

Mtu anayeomba kila siku ni kama vile mtu anayeoga kila siku, maana yake nafasi ya kupata magonjwa katika mwili wake anaipunguza kila siku, lakini mtu asiyekuwa mwombaji, lakini anaendelea kuwa msomaji wa Neno, ni sawa na mtu aliyeacha kuoga kabisa lakini anaendelea kula mlo kamili, na kupiga mswaki. Ni kweli mlo ule unaweza kumfanya afya yake ikawa thabiti, lakini hiyo itakuwa kwa kitambo tu, ule uchafu wa mwili unapozidi kujilundika juu ya mwili wake, utamletea magonjwa tu siku moja!..hata kama atakuwa anakula vizuri kiasi gani.

Ndivyo hivyo ivyo na mtu asiyeomba na huku anajitumainisha kwamba anasoma Neno tu, au hafanyi dhambi hii wala ile, (mashambulizi yake yatamjia kwa ghafla na wala hatajua yanakotokea)…Kwa kitambo kifupi sana roho yake itakuwa na afya na salama, lakini siku si nyingi tatizo litaingia kupitia kipengele hicho cha maombi alichokipuuzia au kizembea.

Lakini kama vyote vikienda pamoja, kusoma Neno,kujitenga na dhambi, pamoja na kusali kwa bidii…ni sawa na mtu anayekula mlo kamili, na pamoja na kula mlo kamili pia unausafisha mwili wake kila siku kwa kuoga, mtu wa namna hiyo ni ngumu kushambuliwa na magonjwa..Kwasababu milango yote yote kaifunga.

Mathayo 26:40 “Akawajia wale wanafunzi, akawakuta wamelala, akamwambia Petro, Je! Hamkuweza kukesha pamoja nami hata saa moja?

41 Kesheni, mwombe, msije mkaingia majaribuni; roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu.

Hivyo ndugu kama ni wewe bado unapata shida ya kusumbuliwa na mashambulizi ya kiroho, hebu tazama tena eneo lako la Maombi. Jiulize mara ya mwisho kuomba angalau lisaa limoja ni lini?, inawezekana hufanyi uasherati, wala mambo mengine ya kidunia ambayo ni milango ya mashambulizi ya kiroho, lakini katika kipengele hichi cha maombi umekizembea… Basi jua tatizo lipo hapo.

Yakobo 4: 4b “..Mwafanya vita na kupigana, wala hamna kitu kwa kuwa hamwombi!

Na hata kama husali na bado hujaona madhara yake, fahamu kuwa yanakuja…hivyo usisubiri mpaka shida zikupate ndipo ukumbuke kuomba, Hivyo anza kulirekebisha hilo leo. Na Mungu akubariki sana.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312 Au jiunge na makundi yetu ya mafundisho ya kila siku kwa kwa njia ya Whatsapp kwa kubofya hapa >>>> WHATSAPP GROUP

Mada Nyinginezo:

Rudi nyumbani

Print this post

Mruba ni mdudu gani kwenye biblia?(Mithali 30:15)

Mithali 30:15 Mruba anao binti wawili, Waliao, Nipe! Nipe! Kuna vitu vitatu visivyoshiba kamwe, Naam, vinne visivyosema, Basi!

16 Kuzimu; na tumbo lisilozaa; Nchi isiyoshiba maji; na moto usiosema, Basi!

Mrubu au ruba ni mdudu mfano wa  mnyoo, ambaye anapatikana sehemu za maji maji , na matope, kama vile kwenye madimbwi, mito, au mifereji. Wanaangukia katika kundi la wadudu wafyonza damu. Wana midomo ambayo inavutika kama mipira, kiasi kwamba wakinasa mahali, labda tuseme  kwenye ngozi au sehemu laini ya mwili ni ngumu kuwatoa, watakaa hapo wakifyonza tu damu mpaka basi,..Tazama picha juu.

Zamani walisifika kwa kuwanata sana sana farasi, kwenye pua zao na ndimi zao, pale walipokuwa wanakwenda kunywa maji kwenye mito.

Tabia pekee ya hawa wadudu ni kuwa, wanaponasa mahali hawatoki, kazi yao ni  kufyonza tu damu, bila kutosheka, watafanya hivyo hata kukaribia kupasuka. Hawana tabia ya kuridhika,.

Sasa picha aliyokuwa anaitoa huyu mfalme Aguri bin yake, ni kuwa kuna baadhi ya watu wanaweza kufananishwa na mdudu huyu na uzao wake;

Tujiulize je na sisi ni miruba?

Ikiwa  siku tu tunafanya maovu hatutosheki.. leo tunalewa, kesho tunalewa, kesho kutwa tunalewa..ukiona upo hivyo ujue wewe ni mruba usiye choka kusema nipe!, nipe.!

Tuna tamaa za mali, zilizopitiliza, mpaka tunafanya mambo yasiyompendeza Mungu, leo tunataka tuwe kama Yule, kesho kutwa kama Yule, hivyo tunaiba, tunatapeli , tunadhulumu n.k…Huo ni Uruba! Haswaa.

Paulo alisema ..

1Timotheo 6:6 “Walakini utauwa pamoja na kuridhika ni faida kubwa.

7 Kwa maana hatukuja na kitu duniani, tena hatuwezi kutoka na kitu;

8 ila tukiwa na chakula na nguo tutaridhika na vitu hivyo.

9 Lakini hao watakao kuwa na mali huanguka katika majaribu na tanzi, na tamaa nyingi zisizo na maana, zenye kudhuru, ziwatosazo wanadamu katika upotevu na uharibifu.

10 Maana shina moja la mabaya ya kila namna ni kupenda fedha; ambayo wengine hali wakiitamani hiyo wamefarakana na Imani, na kujichoma kwa maumivu mengi”.

Ridhika, na urefu wako, ridhika na rangi yako, ridhika na familia yako, ridhika na kipato chako. Ukiwa mtu wa kuridhika utaishi maisha ya amani, na ndivyo Mungu atakavyokuzidishia. Lakini ukiwa kama mruba, ambaye anafyonza tu damu,  haridhiki mpaka anakaribia kwenda kupasuka. Ujue upo katika hatari mbaya sana ya kuanguka katika imani ikiwa wewe ni mkristo.

Bwana atusaidie katika hilo;

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

KUNA MAJIRA MUNGU ATAIVURUGA MIPANGO YETU.

Ngome ni nini?  Kwanini Mungu anafananishwa na ngome?

Ni kwanini mifugo ya Yakobo iliongezeka kwa wingi kiasi kile?

Nyinyoro ni nini?

Je ni wanyang’anyi wawili waliomtukana Bwana Yesu au mmoja?

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya msiwe waalimu wengi (Yakobo 1:3)?

Jibu: Yakobo 3:1  “Ndugu zangu, msiwe waalimu wengi, mkijua ya kuwa mtapata hukumu kubwa zaidi”.

Sentensi hiyo ili ieleweke vizuri ni sawa na kusema “pasiwepo na waalimu wengi katikati yenu”.

Maneno hayo aliyazungumza Yakobo kwa uongozo wa Roho, kuifunua tabia inayoendelea katika kanisa leo . Pale ambapo kanisani kila mtu ni Mjuaji..(hakuna utaratibu). Jambo ambalo ni hatari sana…Kwasababu kanisa linaongozwa na karama za Roho.. Haiwezekani wote tukawa na karama moja, haiwezekani wote tukawa wainjilisti, au wote tukawa waalimu au wote wachungaji au wote manabii.

Lakini inapotokea ndani ya kanisa kila mtu ni mchungaji, au kila mtu ni mwalimu..Kitakachozalika hapo ni roho ya machafuko. Kwasababu mmoja labda karama yake ni matendo ya Miujiza, lakini atataka asimame na yeye afundishe na kuongoza na yeye kama mchungaji, mwisho wa siku kitakachozaliwa hapo ni machafuko, kwasababu vitafundishwa vitu ambavyo vingine hata havipo kwenye Neno, na kupata hatia ya kuliongeza au kulipunguza Neno la Mungu. Na hivyo kujitafutia hukumu.

Ufunuo 22:18  “Namshuhudia kila mtu ayasikiaye maneno ya unabii wa kitabu hiki, Mtu ye yote akiyaongeza, Mungu atamwongezea hayo mapigo yaliyoandikwa katika kitabu hiki.

19  Na mtu ye yote akiondoa lo lote katika maneno ya unabii wa kitabu hiki, Mungu atamwondolea sehemu yake katika ule mti wa uzima, na katika ule mji mtakatifu, ambao habari zake zimeandikwa katika kitabu hiki”.

Hivyo hilo ni neno la kutuonya na kutukumbusha na kututahadharisha tukae katika nafasi zetu, kila mmoja aliyoitiwa,  kama ni Mwalimu, mwalimu, kama ni mchungaji mchungaji, kama ni muinjilisti, muinjilisti n.k Sio umepewa karama ya uimbaji na wewe unatafuta kuwa mwalimu, Utajitafutia hukumu.

Bwana atubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

USINIE MAKUU.

JE NI LAZIMA KUBADILISHA JINA BAADA YA KUOKOKA?

JE UPENDO WAKO UMEPOA?

BABA YANGU ANATENDA KAZI HATA SASA!.

Je! ni halali kwa mtu wa Mungu kutumia njia za uzazi wa mpango,ikiwamo mipira?

Rudi nyumbani

Print this post

KUNA MAJIRA MUNGU ATAIVURUGA MIPANGO YETU.

Kuna mhubiri mmoja alisema Mungu havutiwi na ufanisi wetu kwake, bali anavutiwa na Imani yetu kwake, kwasababu biblia inasema.. …lakini mwenye haki ataishi kwa imani yake (Habakuki 2:4).

Ni kweli kabisa, kwa lugha rahisi, unaweza kudhani unapokuwa fanisi muda wote katika kazi ya Mungu, au mambo yako yanapokwenda sawasawa wakati wote kwenye kazi yake ndicho kinachomvutia sana Mungu.. Lakini ni vizuri tujue tabia za Mungu wakati mwingine zinafanyaje kazi ili yatakapotukutana na hali fulani au jambo fulani  katika ukristo au utumishi tuwe na amani katika hicho.

Haijalishi utakuwa unampendeza Mungu kiasi gani, kuna wakati Mungu ataruhusu mipango yako ivurugike, ataruhusu ratiba zako ziingiliwe, ataruhusu uchelewe au uvutwe nyuma, haijalishi unabidii kiasi gani.. Sasa unapofikia hatua kama hiyo hupaswi kusema kwanini Mungu karuhusu hichi, wakati sioni sababu ya hivi vitu kutokea.. Hatua kama hiyo hupaswi kukata tamaa, au kuhuzunika, bali ujue Mungu anataka uishi kwa kumwamini yeye katika hali zote.

Jiulize ni kwanini wakati mwingine Mungu aliruhusu mtume Paulo, aingiliwe ratiba yake ya kuhubiri injili? Na kupelekwa vifungoni? Unadhani ni kwasababu alikuwa na dhambi, au alikuwa hafanyi kazi ya Mungu kwa bidii? .Pengine alikuwa na mipango mingi sana ya kwenda kuwahubiria watu wengi waliokuwa na shida na vifungo, lakini ghafla mipango yake inaharibiwa.. Lakini hilo halikumfanya mtume Paulo azire, bali alimwamini Mungu, na wakati ulifika alitolewa na akasonga mbele.

Kuna wakati Yeremia anatoka kutoa unabii tu, anajiandaa arudi zake mjini  kwake kupumzika, apokee na mapato yake, ghafla walinzi wa mji wanamkamata na kumsingizia vitu vya uongo, kuwa yeye anakwenda kuwasaliti, matokeo yake wakamkamata na kumrudisha mjini na kumtupa gerezani shimoni kwa siku nyingi, sio kwamba Mungu alishindwa kuzuia yasimpate hayo mtumishi wake mwaminifu, lakini Mungu alikuwa anataka aishi kwa kumwamini yeye.. na sio kwa ufanisi wake.(Soma Yeremia 37). Ipo mifano mingi sana kwenye biblia,

Kuna wakati, Kristo alitaka awe  faragha na wanafunzi wake tu wapumzike na awafundishe, lakini makutano wanamsonga, kiasi kwamba itabidi ahairishe muda wake, awahudumie hao..aliingiliwa mara nyingi,. wakati mwingine wanataka wajitenge wapate nafasi kidogo ya kula lakini wanaingiliwa.(Soma Marko 6:30-42) .Tujiulize na sisi je tunaweza kuruhusu kuingiliwa katika mambo yetu? ..Je! mpendwa anaweza kukufuata wakati ambapo upo buzy kwenye mambo yako ya muhimu, ukayaacha hayo ukamuhudumia?

Tunapokuwa wakristo lazima tuwe tayari kuingiliwa, au kuvurugwa ratiba zetu na Mungu mwenyewe.. Wakati mwingine Bwana alipokuwa safarini kwenda kuhubiri ghafla anatokea mtu anamwambia Bwana twende ukamponye binti yangu, yupo hatarini kufa, anaacha kwenda katika shughuli zake, anakwenda kumponya..

Hivyo kama wewe ni mtumishi wa Mungu, kuna wakati kila kitu kinaweza kwenda kombo, ukaona kama kazi yote uliyoifanya nyuma ni bure, wema wote uliouonyesha ni sawa na bure, jitihada yako yote kwa Mungu inaishia katika hasara, hilo lisikuvunje moyo, hata kwa Yusufu ilikuwa ni hivyo, uaminifu wake wote, kwenye nyumba ya Potifa, alidhania wakati wote kwake utakuwa ni wa kufanikiwa tu, lakini siku mambo yalipomgeukia,pengine alijiuliza maswali mengi sana, ambayo hata wewe leo hii unajiuliza, ni kwanini Mungu aruhusu..

Watu wanaweza kusema kama huyo Mungu wako anakuthamini mbona ameruhusu ukutwe na hayo.. Lakini hawajui kuwa Mungu havutiwi na ufanisi wetu, havutiwi na umahiri wetu kwake, anavutiwa na Imani yetu kwake.. Kwasababu ni kweli kama ingekuwa ni hivyo kamwe asingekaa aruhusu watu wake, wapande na kushuka, wapitie hiki, au kile, wafungwe au wazuiliwe kufanya jambo fulani,  hata asingeruhusu wakati mwingine waugue..

Lakini anayaruhusu ili imani yetu iwepo kwake, siku zote, na yeye jinsi alivyomwanifu, anapotupitisha huko huwa anatuandalia yaliyo bora zaidi, kwahiyo katika hayo unayoyapitia, ni lazima umwamini Mungu kuwa, yeye bado yupo na wewe na kwamba unapaswa usonge mbele.

Hivyo usichukizwe,  usife moyo pale Mungu anapoivuruga mipango yako, kwa ajili ya jina lake. Mwamini yeye, na sikuzote atakuimarisha daima.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

JIFUNZE KUTOA KATIKA HAZINA YAKO VITU VIPYA NA VYA KALE.

BWANA AYAGANGE NA MACHO YETU PIA.

Ayala, Paa na Kulungu ni wanyama gani?

CHUKIZO LA UHARIBIFU

MWANZO WA INJILI YA YESU KRISTO.

Rudi nyumbani

Print this post

Je! Daudi hakuwa mtoto wa ndoa wa Yese? (Zab 51:5)

SWALI: Bwana asifiwe,ukisoma zaburi 51:5,Daudi ana sema mama yake alichukua mimba hatiani, Je kwa mistari hiyo ina maana hakuwa mtoto wa Ndoa wa Yese?


JIBU: Zaburi 51:5 inasema   “ Tazama, mimi naliumbwa katika hali ya uovu; Mama yangu alinichukua mimba hatiani”.

Hatuwezi kutumia kifungu hicho kuhitimisha kuwa Daudi alikuwa ni mtoto wa mke kahaba. Japokuwa kweli kulingana na mazingira yaliyokuwa yanaendelea wakati ule Nabii Samweli anamwendea Yese baba yake Daudi na kumwambia awalete watoto wake wote ili amchague mfalme , na matokeo yake  akawaleta wote na kumwacha Daudi maporini achunge kondoo, inatupa maswali mengi yasiyo na majibu. Kuwa pengine Daudi alikuwa ni mtoto wa nje.

Lakini pamoja na hayo mstari huu bado, haumaanishi kuwa Daudi alizaliwa na mama kahaba.. Kwasababu ukiusoma vizuri mstari huo, hauzungumzii tu siku ile alipotungishwa mimba, bali unakwenda nyuma zaidi hata kabla ya mimba kutungishwa mpaka siku aliyoubwa..anasema Naliumbwa katika hali ya uovu.

Unaona, Daudi alikuwa anajaribu kumweleza Mungu asili yake jinsi ilivyokuwa, kwamba yeye tangu kwenye mzizi huko kabla hata hajaja duniani alikuwa ni mtu ambaye yupo hatiani..

Na ndio maana mistari ya juu inasema..

1 Ee Mungu, unirehemu, Sawasawa na fadhili zako. Kiasi cha wingi wa rehema zako, Uyafute makosa yangu.

2 Unioshe kabisa na uovu wangu, Unitakase dhambi zangu.

3 Maana nimejua mimi makosa yangu Na dhambi yangu i mbele yangu daima.

4 Nimekutenda dhambi Wewe peke yako, Na kufanya maovu mbele za macho yako. Wewe ujulikane kuwa una haki unenapo, Na kuwa safi utoapo hukumu.

5 Tazama, mimi naliumbwa katika hali ya uovu; Mama yangu alinichukua mimba hatiani

Na ndio maana tena sehemu nyingine, anawasema watu waongo, kwamba watu hao hawajapotea siku ile wanaposema uongo, bali tangu walipokuwa tumboni mwa mama zao. Kuonyesha kuwa asili hiyo ilikuwepo ndani mwao, kabla hata hawajazaliwa.

Zaburi 58:3 “Wasio haki wamejitenga tangu kuzaliwa kwao; Tangu tumboni wamepotea, wakisema uongo”.

Unaona? Hata sisi sote, tumekuja katika hali ya hatia, tangu kuzaliwa kwetu, tangu kuumbwa kwetu, asili ya dhambi ipo ndani yetu..Ni mtu mmoja tu ambaye, hakuzaliwa na kosa, wala kutenda kosa lolote, wala chimbuko lake halikuwa na doa lolote na ndio maana alizaliwa na bikira..Na huyo si mwingine zaidi ya YESU KRISTO mwokozi wetu, yeye ndiye tangu kwenye mzizi, mpaka kwenye shina, mpaka kwenye tawi la matunda hakuwa na doa lolote, wala kosa lolote,wala hatia yoyote, alikuwa ni mkamilifu, hadi kufa kwake.

Hivyo hata kama Daudi alizaliwa na mwanamke kahabu, au mwanamke halali, hilo, sio la muhimu sana kwetu kujua. Tunachopaswa kujua ni kwamba mtu yeyote asipozaliwa mara ya pili haijalishi alizaliwa na kahaba, au mke halali, haijalishi alikuja kuwa yatima au mwenye wazazi, mjane au aliye na mume, tajiri au maskini, kama hujazaliwa mara ya pili na Yesu Kristo hawezi kuurithi ufalme wa mbinguni ..

Yohana 3:3 “Yesu akajibu, akamwambia, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa mara ya pili, hawezi kuuona ufalme wa Mungu”.

Kuzaliwa mara pili ndio kunaondoa ile hati ya mashtaka iliyo juu ya kila mmoja wetu, tangu asili.

Hivyo tubu dhambi zako, ukolewe. Ufanyike kiumbe kipya.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

TUNAMHITAJI SANA ROHO MTAKATIFU KATIKA KUYAELEWA MAANDIKO.

MAISHA ULIYOPITIA NYUMA NI USHUHUDA TOSHA WA WEWE KUMTUMIKIA MUNGU:

Ni kosa gani Daudi alilolifanya katika kuwahesabu watu, mpaka kupelekea vifo vya waisraeli wengi?

UTAWALA WA MIAKA 1000.

Fadhili ni nini? Nini maana ya “fadhili zake ni za milele” kibiblia?

MALIPO YA UPOTEVU.

Rudi nyumbani

Print this post