Title December 2020

AOGOPACHO MTU ASIYE HAKI NDICHO KITAKACHOMJILIA.

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe.

Silaha moja kubwa ya adui ni Hofu.  Na biblia inatuambia Hofu ina adhabu (1Yohana 4:18).. Leo hii tutaona adhabu kuu ya hofu ni nini..

Tukisoma Mithali Mithali 10:24  Inatuambia..

“Aogopacho mtu asiye haki ndicho kitakachomjilia;..”

Leo hii kiini cha ukristo hakipo tena katika mafundisho ya wokovu na ufalme wa mbinguni, bali kipo katika elimu za uchawi na uganga. Kiasi kwamba mtu hajui ubatizo wa Roho Mtakatifu ni nini, lakini ukimuuliza kuhusu habari za wachawi anajua A-Z. Hilo jambo ni hatari sana, mimi sipingi uchawi, lakini tuangalie  katika biblia, je! uchawi umepewa uzito gani katika maisha yetu ya wokovu ya kila siku?

Kwanini mitume au Bwana Yesu hakutufundisha au kutusisitiza  sana juu ya siri za wachawi? .Unadhani hawakuwepo? Walikuwepo wengi, lakini waliijua nguvu nyingine iliyo kubwa zaidi ya wao, na ndio hiyo walijikita kuwahubiria watu waiamini, kwasababu walijua hiyo wakishaipata, ni ulinzi tosha, dhidi ya nguvu zote za Yule adui.

Hofu ya uchawi imewashika watu wengi, na kibaya zaidi imewakamata na wakristo waliookoka pia, wao ambao ndio wangepaswa kuwa wakwanza kuzidharau.

Sasa hizi ni baadhi ya hofu za hofu zinazowakamata wengi leo hii;

Kwamfano kama utaona mjusi ndani kwako, na kusema ile ni roho , ujue kuwa hofu hiyo imeshakuvaa.

Kama utaona panya ndani,  au mende, au sisimizi, au konokono, au nzi vitu ambavyo vingehitaji  usafi tu kuviondoa, na ukasema hizo ni roho, ujue kuwa hofu hiyo ipo ndani yako.

Kama utaona paka, na ukahisi ni wachawi wamekutembelea, basi ujue hofu hiyo ipo ndani yako.

Kama utaona, mtu fulani na ukahisi ni mchawi na atakudhuru kwa nguvu za giza, basi ujue hofu hiyo ipo ndani yako. N.k.

Sasa kama biblia inavyotuambia, hofu ina adhabu.. basi ujue adhabu yenyewe ndio hii “Aogopacho mtu asiye haki ndicho kitakachomjilia;..” hiyo ndio adhabu!!

Ukiona roho ndani ya konokono, ujue kuwa shetani anaumbika nyuma ya konokono huyo, na inakuwa roho hai kweli, na madhara yatakukuta kupitia konokono huyo, kwasababu pepo la hofu ya uchawi umeliruhusul ifanye kazi ndani ya konokono, na hivyo madhara yote yatokanayo na pepo hilo utayapata tu.

Ukiamini, kuwa miti fulani ni ya kichawi, ukweli ni kwamba hilo jambo litaaumbika kwako na madhara hayo utayapata ya kutosha, kama ni kifo utakipata, lakini wakati huo huo  utaona jirani yako anao mti kama huo, na wala hakuna lolote baya linalompata.

Kwasababu hofu yoyote ina adhabu..

Ukiamini panya ndani kwako ndio wanaokusababishia umaskini na usisonge mbele, basi umaskini wako utakujia kwa njia ya hao hao panya, utafunga usiku kucha kuomba, na kukemea, bado hali itakuwa ngumu kwako, panya mwingine atakapokatiza ndani kwako,.. kwasababu umeshafungua mlango wa hofu kwa kupita viumbe hao, lakini jirani yako ataona panya, atakachofanya ni kukumbuka kuwa mazingira yake hayapo safi, hivyo atayaweka sawa kwa kufanya usafi na kutafuta namna ya kuwaua , akaendelea kuishi maisha yake ya furaha.

Hiyo ndio adhabu ya hofu ndugu.. Ukikutana na bundi ukaamini katumwa kukuletea msiba, basi msiba huo utakujia tu kwa mlango wowote,

Kwasababu Biblia inasema Imani ni kuwa na uhakika, wa mambo yatarajiwayo..Ukiwa na uhakika kwamba utapata msiba kutokana na bundi uliyemwona, basi ni kweli utakuja kwa njia hiyo hiyo uliyoamini.

kumbe bundi alikuwa anapita tu katika safari yake usiku na kwa bahati nzuri au mbaya akakutana na wewe, lakini kwasababu wewe umelipa nafasi pepo la hofu ya mauti na uchawi, nalo likapata nafasi kupitia ndege Yule huyo mrembo. Na siku si nyingi unasikia msiba,, na wewe unadhani unabii umetimia, kumbe ni hofu imekuzalia matunda yake, uliyokuwa unayatarajia.

Ndugu ukiwa ndani ya Kristo huhitaji kuishi maisha ya kuogopa ogopa kila kitu, hata kama kweli ni nguvu za giza, zipo ndani yao, lakini Bwana Yesu alituambia..

Luka 16.18 “watashika nyoka; hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa;..”

Utatumiwa uchawi, lakini hautakudhuru ikiwa upo ndani ya Kristo, utatengewa chakula cha kichawi, kilichotoka kuzimu kabisa, lakini hakitakuwa na madhara yoyote ndani yako, kwasababu nguvu iliyo ndani yako NI KUBWA kuliko yao. Lakini ukianza kuhangaika huko na huko, unafuta kila njia ya kujilinda mwenyewe dhidi ya kila kitu unachokiona, utapata shida nyingi sana hapa duniani, na wala hutaufurahia wokovu wako, hata kidogo.

Kwasababu maisha yako yatakuwa ni ya vita kila siku, visivyokuwa na sababu.

Hivyo  Ikiwa wewe ni mmojawapo wa walioathirika na mafundisho hayo manyonge, ambayo yanahubiriwa kila mahali, nataka nikuambie leo hii anza upya na Kristo, toka kwenye hicho kifungo, kisha jibidiishe katika kusoma biblia, kuliko kusikiliza hadithi hizo za kimila, na za wachawi, na kidogo kidogo utaanza kupata amani moyoni mwako, kama vile biblia inavyosema;

Yohana 8:32 “tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru”.

Shalom!.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312/+255 693036618


Mada Nyinginezo:

JE! PAKA KULIA USIKU NI ISHARA YA UCHAWI?

Ni kosa gani Daudi alilolifanya katika kuwahesabu watu, mpaka kupelekea vifo vya waisraeli wengi?

USIWE NA HOFU, USHUKAPO CHINI.

USIKATE TAMAA UNAPOPITIA MAGONJWA.

Mungu anaposema “nitaliweka jina langu” ana maana gani?

Rudi Nyumbani:

Print this post

DO NOT BE CONCEITED.

Blessed be the name of our Lord Jesus Christ.Let’s learn and share in the Word of life.

 In Romans 12:3,the Bible says; “For I say,through the grace given unto me,to every man that is among you,not to think of himself more highly than he ought to think;but to think soberly,according as God hath dealt to every man the measure of faith.”

What does it mean to think of oneself more highly than you ought to think?To get a clear answer,let’s read the next verses:

Romans 12:4-8

For as we have many members in one body, and all members have not the same office:

So we, being many, are one body in Christ, and every one members one of another.

Having then gifts differing according to the grace that is given to us, whether prophecy, let us prophesy according to the proportion of faith;

Or ministry, let us wait on our ministering: or he that teacheth, on teaching;

Or he that exhorteth, on exhortation: he that giveth, let him do it with simplicity; he that ruleth, with diligence; he that sheweth mercy, with cheerfulness.

To think of oneself more highly means being proud to the extent they you feel you can have more of or all the spiritual gifts. For instance, one would to be an evangelist,an apostle, a great prophet, a teacher among others. In other words,it’s like all the gifts belong to them.They feel it’s not possible to have just one gift.He or she should either be a pastor and a teacher or a prophet and an evangelist as well,and so on.However, the Bible warns us against such things. We are to think soberly,according to the measure of faith Christ has dealt each person.

When comes pride,God’s presence in a person ceases.For the Lord resists the proud,but delights in those who are lowly.Humility does not flourish in the garden of pride. 1 Peter 5:5;”…..

for God resisteth the proud,and giveth grace to the humble. “

The gifts that are given unto us are not meant for a show-off or comparing ourselves to see those that are better than others.Any gift being used for vain or selfish reasons is a sign that it has been invaded by the devil so that it is working under Satan’s influence. Remember, we are differently but equally gifted for a reason.These gifts have been given to us to equip us for the works of service, so that the body of Christ may be built up.We have no right to boast or exalt ourselves above others

Ephesians 4:11-12

11 And he gave some, apostles; and some, prophets; and some, evangelists; and some, pastors and teachers;

12 For the perfecting of the saints, for the work of the ministry, for the edifying of the body of Christ:

 Have you invited Christ into your life as your Saviour and Lord?Remember, the days are gone,and we have a very short period of time,and the end will come.The trumpet could at any time and Jesus will come to take with him his church into the eternal glory.The day of the Lord’s coming will be such a doomsday.He will come in vengeance to those living on the face of the earth.Let’s dread it so that we won’t fall in God’s judgment onthat day.Turn from your evil ways and give your life to Jesus today

Heaven is real and hell is also real.it’s upon us to choose between LIFE and DEATH during our stay on earth .When we die,there’s no more chance to make choices.Eternal life or eternal doom(death) will be the consequences of the choices we made while we living in the world.The choices we make will determine where we will spend eternity;whether away from God or with God.Life is short.Make things right with God before your days come to an end.Be wise.Choose life and enter into safety.There’s no place any safer than in Christ.

God bless you!

Maran Atha.

Related topics:

PRAY WITHOUT CEASING.

JONAH’S VINE.

JESUS WILL PASS SOMEDAY AND PEOPLE SHALL NOT KNOW IT.

THY KINGDOM COME.

THE WILL OF THE LORD JESUS ​​TO HIS DISCIPLES.

Home:

.

Print this post

PATANA NA MSHITAKI WAKO KWANZA.

Shalom, Biblia inasema;

Luka 12:58 “Maana, unapofuatana na mshitaki wako kwenda kwa mwamuzi, hapo njiani fanya bidii kupatanishwa naye, asije akakuburuta mpaka mbele ya kadhi; yule kadhi akakutia mikononi mwake mwenye kulipiza, na yule mwenye kulipiza akakutupa gerezani.

59 Nakuambia, Hutoki humo kamwe hata uishe kulipa senti ya mwisho”.

Hapo mwanzoni nilidhani mshitaki wetu ni shetani tu peke yake kama tunavyosoma katika 1Petro 5:8, na Ufunuo 12:10, lakini biblia inatuonyesha kuwa wapo washitaki wengine ambao watatushitaki sisi huko tunapokwenda, ambao sisi hatuwajui..

Ukiuchunguza huo mstari kwa makini, unaposema patanishwa  na mshitaki wako, kabla ya kufika kwa mwamuzi, utajiuliza shetani atapatanishwaje na sisi? sisi hatuwezi kupatanishwa  na yeye kwa lolote kwasababu yeye sikuzote ni mpingamizi na ni adui.. Hivyo wapo washitaki wengine wanaozungumziwa, ambao Bwana Yesu aliwamaanisha hapo,.. Na hao si washitaki, wa kidunia labda wa mahakamani,hapana ni kweli ukisoma hapo alitumia mfano wa washitaki wa kidunia, lakini alikuwa anamaanisha washitaki wengine wa rohoni.

Je washitaki hao ni wakina nani?

Tukirudi nyuma katika mazingira ya Kristo aliyokuwepo, waisraeli wengi walikataa kumsikiliza kwa kisingizio kuwa wanaye Musa, (Wakiwa na maana wanaifuata torati yake, na sio maneno ya tu mwingine yeyote). Lakini kiuhalisia torati yenyewe walikuwa hawaishiki, na kwa mantiki hiyo Bwana Yesu kuna mahali akawaambia maneno haya;

Yohana 5:45 “Msidhani kwamba mimi nitawashitaki kwa Baba; yuko anayewashitaki, ndiye Musa, mnayemtumaini ninyi.

46 Kwa maana kama mngalimwamini Musa, mngeniamini mimi; kwa sababu yeye aliandika habari zangu”.

Wana wa Israeli hawakujua kuwa Musa wanayemwamini ndiye atakayekuwa mshitaki wao siku ile ya mwisho kwanini hawakuyashika alichowaagiza.. Na ndio maana Bwana Yesu akatumia mfano huo, na kuwaambia patana kwanza na mshitaki wako, Patana kwanza na Musa, patana kwanza na torati, kabla hamjafika kwa kadhi, Kadhi hapo anamaanishi Mungu, katika siku ile ya Hukumu.

Kwasababu ukishajikuta mbele ya kadhi (yaani Mungu) siku ile , kitakachofuata si kingine zaidi ya Hukumu, na ukishahukumiwa utawekwa mikononi mwa mwenye kulipiza,(Askari), ambao ni malaika watakatifu, kisha hao watakukamata, na kwenda kukutupa kwenye ziwa la moto.

Anamalizia kwa kusema..

Ukishafikia hatua hiyo, hutoki huko mpaka utakapolipa senti ya mwisho, maana yake ni kwamba Ukishashushwa kuzimu, habari yako ndio imeisha hapo rafiki, hakuna cha msamaha, hakuna cha dhamana, hakuna cha kulipa kidogo kidogo ukiwa nje..Utaishia huko milele na milele.

JE! NA SISI PIA TUNAO WASHITAKI?

Waisraeli walijifanya kuwa ni watoto wa Musa, hivyo Musa akawa mshitaki wao, vivyo hivyo na sisi, washitaki wetu ni mitume na manabii.. Tunasema sisi ni wakristo, tunayoiamini biblia, tunasema tumejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii  lakini walichokisema mitume baba zetu hatukifanyi katika maisha yetu.. Hao ndio watakaokuwa washitaki wetu. Hizo Injili zao ndizo zitakazotushitaki siku ile..

Na ndio maana biblia inatusisitiza sana, tuhakikishe tunapatanishwa  nao, angali tukiwa hapa katikati njiani, Maana yake ni angali tukiwa angali hapa duniani,hatujafa  bado,  tunayo nafasi ndogo, kabla hatujamaliza mwendo, tuhakikishe, wokovu tunaupata, tuhakikishe tunalizingatia lile andiko linalosema, tafuteni kwa bidii, kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu ambao hakuna mtu atakayemwona Mungu asipokuwa nao (Waebrania 12:14). Tuhakikishe hayo tunayo, tuhakikishe tumebatizwa kweli kwa Roho Mtakatifu. Tumetiwa muhuri.

Kwasababu hawa ndio watakaosimama siku ile kutushitaki, kuwa walituambia lakini sisi tulikataa.

Paulo alisema..

Warumi 2:16 “katika siku ile Mungu atakapozihukumu siri za wanadamu, sawasawa na injili yangu, kwa Kristo Yesu”.

Bwana atusaidie tuitii injili.

Je umeokoka? Je, unaouhakika wa maisha yako ya milele kwamba hata ukifa leo utakwenda mbinguni? Kama sivyo, basi leo tubu, mkabidhi Yesu maisha yako ayasafishe, kwasababu hizi ni siku za mwisho, wote tunalijua hilo, tunaishi katika dakika za nyiongeza tu, dakika za majeruhi, Unyakuo ni wakati wowote, Hivyo sote kwa pamoja tuamke, tumgeukie Muumba wetu.  Ni wakati wa kujitwika msalaba wako wewe kama wewe, na kumfuata  Kristo, ni wakati wa kuchagua lililo la msingi kwanza, na hayo mengine ndio yafuate baadaye kama yanayoulazima. Hii mizigo ya duniani tuipe pumziko kidogo tufanya lililo la kwanza, ili tuwe mahali salama.

Tupatanishwe na washitaki wetu.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

SI MAPEPO YOTE NI YA KULIPUKA.

NI NINI TUNAJIFUNZA JUU YA MT. DENIS WA UFARANSA?

NYAYO TUNAZOPASWA KUZIFUATA.

WAPE WATU WANGU RUHUSA ILI WAPATE KUNITUMIKIA.

USITAFUTE KUKANWA NA BWANA SIKU ILE.

Rudi Nyumbani:

Print this post

SI MAPEPO YOTE NI YA KULIPUKA.

Nyuma kidogo nilikuwa nadhani mtu mwenye mapepo, ni lazima yalipuke, na ikiwa hayalipuka, basi hana mapepo ndani yake. Kumbe mtazamo huu sio sahihi. Tunapaswa tujue kuwa mtu yeyote ambaye hayupo ndani ya Kristo kwa namna moja au nyingine lipo pepo ambalo linaishi ndani yake, aidha kwa kujua au kwa kutokujua, haijalishi kuwa litamlipuka au halimtalipuka.

Biblia inatufundisha hivyo, Si wakati wote Mapepo yote yaliyokutana na Yesu yalilipuka, au yalitolewa kwa kukumewa kama tunavyodhani.. Embu tusome habari hii pengine ulishawahi kuisoma mara nyingine lakini jambo hili hukulijua..tusome.

Luka 13:10 “Siku ya sabato alikuwa akifundisha katika sinagogi mojawapo.

11 Na tazama, palikuwa na mwanamke aliyekuwa NA PEPO WA UDHAIFU muda wa miaka kumi na minane, naye amepindana, hawezi kujinyosha kabisa.

12 Yesu alipomwona alimwita, akamwambia, Mama, umefunguliwa katika udhaifu wako.

13 Akaweka mikono yake juu yake, naye akanyoka mara hiyo, akamtukuza Mungu”.  

Kwa mistari hiyo michache tunaweza kusema, Yesu alijua kabisa huyu mama kilichokaa nyuma yake si kingine zaidi ya Pepo, na hilo pepo nalo lilijua kabisa aliyesimama mbele yake ni Yesu mkuu wa uzima. Lakini pepo hili limekaa nyuma ya kivuli cha udhaifu, nyuma ugonjwa wa kibiongo, wala halipigi kilele, wala halijidhihirishi kama ilivyo desturi yao. Ndipo Yesu akamwita, akamwekea mikono yake, na hilo pepo likaondoka saa ile ile, na mama yule akawa mzima.

Lilipotoka Mama huyu hakujua chochote, kwasababu hakugarara chini, au hakupiga kelele, kilichomfanya ajue kuwa pepo limeondoka na mabadiliko ya ghafla aliyoanza kuyaona katika mwili wake baada ya pale.

Nachotaka kusema ni kuwa, nguvu za giza hazichagui wa kumwingia, maadamu upo nje ya “himaya ya Kristo Yesu” hayatakosa mahali popote tu pa kukaa, panaweza pasiwe katika ugonjwa, panaweza pasiwe katika mwili, utaenda kanisani kama kawaida, mtafanya maombi ya nguvu pengine, na wala lisilipuke pepo lolote. Lakini linaweza likakukaa katika ulevi, likakukaa katika uzinzi, likakukaa katika wizi, likakaa katika usengenyaji  n.k. Au katika tabia fulani ambayo wewe mwenyewe inakushinda. Na hayo yote hutajua kama yalikuwa ndani yako mpaka utakapookolewa na Yesu.

Lakini kama upo ndani ya wokovu Pepo haliwezi kuwa na nafasi ndani yako.

Hivyo wewe unayeusoma ujumbe huu, na hujaokoka pengine ulikuwa hujui kuwa kuna maroho ya giza yamekuzunguka kwenye maisha yako. Na leo umejua, basi fahamu kuwa njia pekee ya kuzishinda roho hizo, ni kwa kujikabidhi kwa Bwana Yesu.  Yeye pekee kwa damu yake iliyomwagika pale msalabani ndiyo yenye nguvu ya kuweza kuondoa na anayeweza Kufuta laana yote ya dhambi iliyokuwa juu yako, pamoja na kufukuza miungu yote migeni inayoishi humo nafsini mwako. Ikiwa tu utakubali leo hii kutubu, na kuyasalimisha maisha yako kwake kikamilifu, kwa kumaanisha kabisa kutoka katika moyo wako, kwamba hutorudi nyuma tena. Basi leo hii anaweza kukusamehe kabisa.

Hivyo Kama upo tayari kwa hilo hii, basi fuatisha sala hii fupi kwa imani, ukijua kuwa Mungu anakusikia, na kwa kufanya hivyo Bwana ataanza kuunda jambo jipya katika maisha yako, kuanzia leo. Fungua tu moyo wako.

Mahali ulipo jitenge kasha piga magoti sehemu ya utulivu kisha Sema maneno haya;

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU  MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE IONDOE UOVU WANGU WOTE SASA NDANI YANGU, NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa sala hiyo imetoka moyoni mwako, ujue kuwa hiyo ni hatua ya kwanza, kuelekea kufanywa huru kweli kweli na Bwana Yesu. hatua inayofuata kwako ni kupokea Ubatizo sahihi, ambao ni ule wa kuzamishwa katika maji tele (Yohana 3:23) na uwe katika jina la BWANA YESU KRISTO sawasawa na Matendo 2:38,8:16,10:48,19:5.  Na ukilikamilisha hilo kuanzia hapo Bwana mwenyewe atakupa kipawa cha Roho wake Mtakatifu.

Hivyo kama utakuwa tayari kwa ajili ya Tendo hili la ubatizo ambalo ni maagizo la msingi tuliyopewa na Bwana wetu Yesu Kristo kwamba kila aaminiye na kubatizwa ataokoka.(Luka 16:16), itakuwa ni vema sana. Hivyo wewe tayari umeshaamini, hatua iliyobaki kwako ni kubatizwa. Usipuuzie agizo hilo. Tafuta ubatizo sahihi kwa ajili ya kuukamilisha wokovu wako.

Kama utakuwa tayari kwa tendo hilo, basi wasiliana na sisi, inbox au kwa namba hizi hapa chini, tujue pa kukusaidia kwa mahali ulipo. +255693036618 / +255789001312,

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hapo juu.

Mada Nyinginezo:

YESU MPONYAJI.

FAHAMU JINSI KRISTO ANAVYOPONYA WATU ROHO.

NYAYO TUNAZOPASWA KUZIFUATA.

RABI, UNAKAA WAPI?

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 6

TUMEPEWA AMRI YA KUKANYAGA NGE NA NYOKA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Mlima wa Mizeituni  unaumuhimu gani kwetu?

Mlima wa Mizeituni ni moja ya milima saba ambayo inauzunguka mji wa Yerusalemu kule Israeli . Mlima huu upo upande  wa Mshariki mwa mji huo,  umbali usiozidi kilometa moja, mpaka kuuingia mjini Yerusalemu. Hivyo haupo mbali sana.

Umeitwa mlima wa Mizeituni, kutokana na kuwa na sifa ya kuzungukwa na miti mingi ya mizeituni pembezoni mwa mlima huo.

Mlima huu umetajwa mara mbili katika agano la kale, mara ya kwanza ni siku ile Daudi alipokuwa anafukuzwa na mwanawe Absalomu, biblia inatuambia aliupanda mlima huu akiwa analia peku, akiambatana na wale watu aliokuwa nao kwenye ufalme.(2Samweli 15:30).

Sehemu nyingine ni katika kitabu cha Zekaria ambacho kinaeleza unabii wa masihi siku atakaposhuka mara ya pili hapa duniani, kwamba atashukia kwanza juu ya mlima huu;

Zekaria 14:3 “Hapo ndipo atakapotokea Bwana, naye atapigana na mataifa hayo, kama vile alipopigana zamani siku ya vita.

4 Na siku hiyo miguu yake itasimama juu ya mlima wa Mizeituni, unaoelekea Yerusalemu upande wa mashariki, nao mlima wa Mizeituni utapasuka katikati yake, upande wa mashariki na upande wa magharibi; litakuwako huko bonde kubwa sana; na nusu ya mlima ule utaondoka kwenda upande wa kaskazini, na nusu yake itaondoka kwenda upande wa kusini”.

Lakini katika agano jipya mlima huu umetajwa mara nyingi kidogo;

Lakini cha kufahamu zaidi ni kuwa habari zote ambazo  Yesu Kristo alizitaja kuhusiana na siku za mwisho na kurudi kwake mara ya pili duniani, alizizungumzia juu ya mlima huu wa mizeituni. Utasoma hayo katika (Mathayo 24, Marko 13, Luka 21)

Hata  siku ile Yesu alipoulilia mji wa Yerusalemu, juu ya maangamizi yake yaliyo mbeleni, alikuwa amesimama juu ya mlima huu.(Luka 19:37-44)

Na juu ya mlima huu, ndio aliopaa kutoka ulimwenguni, mara ya mwisho  alipokutana na wanafunzi wake baada ya siku zile 40 na kuwapa maagizo ya kuhubiri injili, na kuingojea ahadi ya Roho Mtakatifu..

Matendo 1:9 “Akiisha kusema hayo, walipokuwa wakitazama, akainuliwa, wingu likampokea kutoka machoni pao.

10 Walipokuwa wakikaza macho mbinguni, yeye alipokuwa akienda zake, tazama, watu wawili wakasimama karibu nao, wenye nguo nyeupe,

11 wakasema, Enyi watu wa Galilaya, mbona mmesimama mkitazama mbinguni? Huyu Yesu aliyechukuliwa kutoka kwenu kwenda juu mbinguni, atakuja jinsi iyo hiyo mlivyomwona akienda zake mbinguni”.

JE! MLIMA HUU UNAO UMUHIMU WOWOTE KWETU? NA JE! NI SAHIHI KWENDA KUOMBA JUU YA MLIMA HUU?.

mizeituni, mlima,

Ni wajibu wetu kujua kuwa huu ndio mlima ambao Kristo atashukia siku ile atakaporudi mara ya pili kuuhukumu ulimwengu na kutawala kama mfalme. Na kama tulivyosoma katika unabii wa Zekaria ni kwamba siku hiyo atakapokuja, mlima huu utagawanyika katikati, upande wa Mashariki, na Upande wa Magharibi, na hapo katikati kutakuwa na bonde kubwa sana. Siku hiyo  atauwa waovu wote watakaokuwepo duniani kwa wakati huo.. Kipindi hichi ndio kile biblia inasema  kila jicho litamwona, na mataifa yote watamwombolezea, watu watatamani milima iwaungukie kwasababu watauliwa na Kristo mwenyewe. (Mambo hayo watakutana nao wale watakaoukosa unyakuo)

Kwa urefu wa somo hilo fungua hapa >>WATAMTAZAMA YEYE AMBAYE WALIMCHOMA;

Na baadaye akishawamaliza waovu wote ataingia  mji wa Yerusalemu, na kisha atatawala kama Mfalme wa Wafalme na Bwana wa Mabwana, juu ya dunia nzima kwa muda wa miaka 1000,

Ataitengeneza upya hii dunia, kutakuwa na amani ya milele isiyoelezeka. Dunia itakuwa kama paradiso. Na wakati huo upo karibuni sana. Hivyo ni wajibu wetu sisi sote kujua mambo yatakayoendelea Israeli katika siku za mwisho, ikiwemo juu ya mlima huu wa mizeituni, ili tujue  leo hii tunasimama wapi. Tusiishi tu kama watu wengine wa ulimwengu, wasioona mambo ya mbeleni.

Lakini sasa tukirudi kwenye sehemu ya pili ya swali letu  je! Ni Sahihi kwenda kuomba juu ya mlima huu?

Watu wengi wamekuwa wakienda Yerusalemu, kupeleka maombi yao, wakidhania kuwa mahali pale ndipo Mungu atawasikia vizuri zaidi kuliko huku walipo, wengine wamekuwa wakikesha kwenye ule ukuta wa maombolezo, wengine juu ya mlima huu wa Mizetuni, wengine kwenye mto Yordani n.k..

Lakini ukweli ni kwamba kufanya hivyo ni kukosa maarifa ya kutosha juu ya agano tulilo nalo leo hii. Bwana Yesu alimwambia Yule mwanamke;..

Yohana 4:21 “Yesu akamwambia, Mama, unisadiki, saa inakuja ambayo hamtamwabudu Baba katika mlima huu, wala kule Yerusalemu….

4.23 Lakini saa inakuja, nayo sasa ipo, ambayo waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli. Kwa maana Baba awatafuta watu kama hao wamwabudu.

Agano la Damu ya Yesu, ni agano la kimbinguni, kiasi kwamba mtu yeyote mahali popote atasikiwa na Mungu ikiwa tu ataingizwa katika agano hilo lililo bora. Na Mtu ataingia ndani ya agano hilo, kwanza kwa kumwamini Yesu Kristo, kisha kutubu dhambi zake, na baada ya hapo kuwa tayari kubatizwa na kupokea Roho Mtakatifu. Akikamilisha hatua hizo anakuwa ameshaokoka.

Na mtu kama huyo maombi yake yanasikiwa, ziadi hata mtu aliyekwenda kuomba juu ya mlima huu.

Je! Wewe umeingizwa kwenye agano hili?. Je! Una habari kuwa Yesu Kristo yupo mlangoni kurudi? Na unabii huo upo mlangoni kutimia? Unasubiri nini usimkaribishe Kristo moyoni mwako. Bado unatangatanga na ulimwengu ili siku ile ikujie ghafla?.  Mambo yatakayoendelea huku duniani kwa watakaoukosa unyakuo hayaelezeki ndugu yangu, Ni heri leo ukayakabidhi maisha yako kwa Yesu. Kama moyo wako leo hii upo tayari kufanya hivyo. Basi uamuzi huo ni wa busara sana. Hivyo fungua hapa kwa ajili ya kupata maelekezo ya sala ya Toba.  >>> SALA YA TOBA

Na Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

UFUNUO: Mlango wa 20

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita..

UTAWALA WA MIAKA 1000.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Uchaji ni nini kama tunavyosoma katika 1Timotheo 2:10?

Tusome..

1Timotheo 2:10 “bali kwa matendo mema, kama iwapasavyo wanawake wanaoukiri uchaji wa Mungu”

Uchaji ni kitendo cha “kumcha Mungu”. Ni sawa na neno “Ulaji wa chakula” ni neno linalotokana na kitendo cha “kula chakla” Na vivyo hivyo uchaji, ni kitecho cha kumcha Mungu.

Lakini tukirudi kwenye mstari huo, tukianzia juu kidogo kina jambo lingine la kujifunza..Tusome,

1Timotheo 2.9 “Vivyo hivyo wanawake na wajipambe kwa mavazi ya kujisitiri, pamoja na adabu nzuri, na moyo wa kiasi; si kwa kusuka nywele, wala kwa dhahabu na lulu, wala kwa nguo za thamani;

10  bali kwa matendo mema, kama iwapasavyo wanawake wanaoukiri uchaji wa Mungu”

Mstari huo unawahusu wanawake, yaani vigezo vya wanawake wanaoukiri Uchaji wa Mungu, kwamba wanapaswa wawe watu wa kujisitiri, maana yake ni kuwa mwanamke ambaye hajisitiri, haijalishi anafanya kazi gani ya kanisa, au anamwimbia Mungu..Bado Hamchi Mungu..Huyo ni wa kidunia, ni mfano wa Yezebeli.

Kumbuka hili binti wa Mungu, Mwanamke hapaswi kuvaa hereni, mikufu, hapaswi kuvaa suruali (iwe pana au nyembamba), hapaswi kuchonga nyusi, hapaswi kusuka rasta, hapaswi kupaka rangi kucha, wala kupaka rangi mdomoni na mambo mengine yanayofanana na hayo. Na sababu pekee ni kwamba Miili yetu ni hekalu la Roho Mtakatifu, na sisi sio mali yetu wenyewe, ni mali ya mwingine hivyo hatuna uhuru asilimia zote wa kufanya yale tunayotaka.

Kadhalika mwanamke asiye na adabu na moyo wa kiasi, huyo pia Hamchi Mungu haijalishi anahudhuria kanisani mara ngapi, au anaimba kwaya. Huyo ni wa shetani.

Hivyo mwanamke/mama/dada kama huukiri Uchaji wa Mungu kwa kufanya hayo yaliyoorodheshwa hapo juu. Huu ni wakati wako wa kukata shauri la kuokoka. Kwasababu bado ulikuwa hujaokoka kama ulikuwa unavaa vimini. Basi tubu leo na kumpokea Yesu, na ukabatizwe ufanyike kiumbe kipya, na Roho Mtakatifu atakuja juu yako kukutengeneza kama anavyotaka Mungu.

Marana atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Mlango uitwao “Mzuri” Unaozungumziwa katika Matendo 3:2 ndio upi?

UFUNUO: Mlango wa 1

NITAONGEZAJE NGUVU ZANGU ZA ROHONI?

OLE WAO WANAOJITAHIDI KUMFICHA BWANA MASHAURI YAO.

USHIRIKINA NA MADHARA YAKE.

Je tunapaswa tushiriki Meza ya Bwana mara ngapi?

MAMBO 5 AMBAYO KILA MKRISTO ANAPASWA KUFAHAMU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

MWANZO WA INJILI YA YESU KRISTO.

Nakusalimu katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo. Karibu katika kujifunza maneno yale yale ya uzima ambayo yalikuwepo tangu zamani, ukweli pekee uliodumu na utakaodumu duniani kwa wakati wote.

Leo tutajifunza jambo moja katika kitabu cha Marko.. Tukisoma pale mwanzoni Inasema..

Marko 1:1 “Mwanzo wa Injili ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.

2 Kama ilivyoandikwa katika nabii Isaya, Tazama, namtuma mjumbe wangu Mbele ya uso wako, Atakayeitengeneza njia yako”.

Kama tunavyoona hapo kitabu hichi cha Marko, kimeanza na utambulisho wake, ambao ni “mwanzo wa injili ya Yesu Kristo”, tofauti na kitabu kama cha Yohana, ambacho chenyewe kinaanza kwa utambulisho wa “Hapo mwanzo kulikuwa na Neno, naye Neno alikuwa kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu.”.. Sasa ni vizuri tukazingatia sana tambulisho hizi za mwanzoni mwa Vitabu, kwani hiyo itatusaidia kujua maudhui ya injili nzima inaegemea wapi.

Na ndio maana ukisoma kitabu cha Yohana chote, utaona, hakijajikita katika kueleza mizunguko ya Yesu na kazi alizozifanya sana..Bali kilikuwa kimejikita kwa sehemu kubwa kumshuhudia Yesu kama Nuru ya ulimwengu. Ni kitabu kinachomzungumzia Bwana Yesu kama Neno la kweli, la Mungu kwa namna ya kipekee sana, kiasi kwamba ukikisoma katika utulivu chini ya uongozo wa Roho Mtakatifu, utajikuta unampenda Bwana zaidi na imani yako kuimarika sana.

Sasa tukirudi kwenye kitabu cha Marko nacho kinaanza kwa namna yake, kinasema “Mwanzo wa Injili ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.”..Hii ikiwa na maana kuwa  kitabu hiki kimeegemea sana katika kuizungumzia injili yake. Sasa ni lazima tujue injili hiyo ilikuwa ni ya namna gani, na alihubiri nini..Ili na sisi tujifunze misingi ya injili ya kweli inavyopaswa iwe.

Hivyo ukiendelea mbele kidogo kwenye mstari wa 14 tutaona ni nini Yesu alianza kukihubiri katika huduma yake, Tusome;

Marko 1:14 “Hata baada ya Yohana kutiwa gerezani, Yesu akaenda Galilaya, akiihubiri Habari Njema ya Mungu,

15 akisema, WAKATI UMETIMIA, na UFALME WA MUNGU UMEKARIBIA; TUBUNI, na KUIAMINI INJILI”.

Umeona, injili yake iliegemea katika  vipengele hivyo vinne.

  1. WAKATI UMETIMIA; Hii ikiwa na maana wakati wa mataifa kuokolewa umetima. Wakati uliokuwa unasubiriwa ndio umefika. Wakati wa wokovu kupatikana bure kwa kila kiumbe duniani haijalishi atakuwa ni muafrika, mzungu, mpagani, muabudu miungu. Na sisi pia tunapaswa kuhubiri kwetu tuhubiri kutimia kwa wakati huu. Ni wakati ambao mlango umefunguliwa kwa watu wote. Hivyo kila mmoja ni wajibu wake kuhakikisha neema hiyo haimpiti.
  2. UFALME WA MUNGU UMEKARIBIA: Kwamba mwisho wa kila kitu umekaribia; Dunia haitakuwa na wakati mrefu kabla ya mambo yote kuisha, Na utawala mpya wa Mungu kuanza..dalili zote zinaonyesha. Hivyo watu waelekeze macho yako sana mbinguni, kuliko kwenye mambo ya ulimwengu huu.
  3. TUBUNI: Sasa kwa kuwa wakati umetia, na ufalme wa mbinguni umekaribia sana, kilichobakia kwa mtu ni kutubu dhambi zake. Kukubali kuoshwa dhambi zake, kukubali kumgeukia muumba wake, katika wakati mchache aliobakiwa nao.
  4. NA KUIAMINI INJILI: Maana yake ni kuamini maneno yote ya uzima na kuyaishi. Kuyasikiliza mafundisho yote ya Yesu Kristo. Katika hali ya utakatifu.

Hivyo ni vipengele mama, vya injili. ili injili ikamilike ni lazima vipengele hivyo viwepo. Huko ndiko kulikuwa kuhubiri kwa Bwana wetu Yesu, na kwa namna hiyo Mungu alimthibitisha kuwa ndiye mwana wake wa pekee.

Hivyo na sisi tuende katika nyayo hizo hizo. Vilevile tujue kuwa hizi ni nyakati za mwisho Jiulize! Wewe kama wewe Je! upo ndani ya wokovu kisawasawa?. Embu chunguza maisha yako, uangalie umesimama wapi. Saa ya wokovu ni sasa na sio kesho…

Ukiwa unaichezea hii neema, ujue haitadumu siku zote juu ya maisha yako. Kuna wakati itaondoka, na ndio maana ikaitwa neema, maana yake ni kama offer tu, ambayo hukustahili wala hatukustahili, na siku zote offer huwa haidumu wakati wote, kuna kipindi itaondolewa, vivyo hivyo na neema itaondoka tu wakati Fulani ukitimia juu yako, kama hutaiamini injili, unyakuo utapita na wale wote ambao hawajampokea Yesu watabaki hapa duniani. Kama Mungu aliiondoa kwa Israeli wateule wake Israeli na kutupa sisi. Hatashindiwa kutuondolea na sisi na kuwapa wengine.

Warumi 11:17 “Lakini iwapo matawi mengine yamekatwa, na wewe mzeituni mwitu ulipandikizwa kati yao, ukawa mshirika wa shina la mzeituni na unono wake,

18 usijisifu juu ya matawi yale; au ikiwa wajisifu, si wewe ulichukuaye shina, bali ni shina likuchukualo wewe.

19 Basi utasema, Matawi yale yalikatwa kusudi ili nipandikizwe mimi.

20 Vema. Yalikatwa kwa kutokuamini kwao, na wewe wasimama kwa imani yako. Usijivune, bali uogope.

21 Kwa maana ikiwa Mungu hakuyaachia matawi ya asili, wala hatakuachia wewe”.

Hivyo tubu, ukabatizwe kama bado hujabatizwa katika ubatizo sahihi. Na Mungu atakupa Roho wake Mtakatifu.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

JE UDHAIFU WANGU UNAWEZA KUZUIA INJILI?

IVUMBUE INJILI YA KRISTO KUTOKA KATIKA KILA JAMBO.

HATARI YA KUHUBIRI INJILI TOFAUTI NA ILIYOANDIKWA KWENYE BIBLIA.

KUTOKUIHUBIRI INJILI,KUNA MADHARA GANI?

Naomba kujua nini maana ya kuteguka uvungu wa paja?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Duara ya Ahazi ni ipi? Na je! Kivuli cha Hezekia kilirudije nyuma?

Zamani walikuwa hawana saa za mshale, au za kukonyeza kama tulizonazo sasa hivi ili kutambua majira ya siku, badala yake walitumia  njia nyingine mbalimbali zilizowasaidia kutambua saa za mchana, na njia kuu ilikuwa ni ya kukitazama kivule cha jua

Sehemu nyingine walituma kifaa kidogo maalumu ambacho kiliwekwa mahali pa wazi, ambapo jua litaweza kukipiga pande zote . Tazama picha..

duara ya muda

Sehemu nyingine zilitumika ngazi,ambazo zilijengwa pande zote, mashariki na magharibi, mwa eneo hilo la wazi, na pale jua lilipochomoza upande wa mashariki, kivuli kilichusha kwenye ngazi, na pale lilipozama upande wa magharibi kivuli kilinyanyuka, Hivyo kwa kutazama zile ngazi waliweza kutambua saa za asubuhi, mchana na jioni.. (Tazama picha juu kabisa mwanzoni mwa somo hili),.

Hivyo inawezekana duara la Ahazi lilikuwa ni la namna hii, japo biblia haijaeleza kwa marefu lakini tunaona, Hezekia, baada kuugua sana, na kuwa hatarini kufa, alimwomba Mungu kwa kumlilia amponye ugonjwa wake. Ndipo Mungu akamsikia na kumwambia kuwa atamponya, Lakini yeye akaomba Mungu ampe ishara kuwa jambo hilo litatendeka, ndipo akapewa nafasi ya kufanya uchaguzi wa upande wa kivuli hicho kitakapoangukia ndani ya   hilo duara la Ahazi baba yake Hezekia (ambaye alilijenga kwa ajili ya shughuli hiyo ya kutambua majira),..akaulizwa je! kiendelee mbele au kirudi nyuma.

Kwa kawaida jua linapokaribia kuzama, kivuli huwa kinakwenda mbele, hivyo Hezekia akaambiwa achugue je kivuli kizidi kwenda mbele zaidi, yaani akiwa na maana kama muda ule, kivuli kilikuwa kinaonyesha ni saa 8 mchana, basi kisogee mpaka kwenye saa 12 jioni.. Au achague kirudi nyuma, mpaka kwenye saa 1 asubuhi haijalishi kuwa muda huo utakuwa ni saa 8 mchana.

Ndipo Hezekia akachagua kirudishwe nyuma, kinyume cha asili, kwani kwenda mbele linaweza likawa ni jambo la kawaida..lakini kurudi nyuma inahitaji muujiza.

2Wafalme 20:8 “Hezekia akamwambia Isaya, Je! Kutakuwa na ishara gani ya kwamba Bwana ataniponya, nami siku ya tatu nitapanda nyumbani kwa Bwana.

9 Isaya akamwambia, Jambo hili litakuwa ishara kwako, itokayo kwa Bwana, ya kwamba Bwana atalifanya neno hilo alilolinena; je! Kivuli kiendelee madaraja kumi, au kirudi nyuma madaraja kumi?

10 Hezekia akajibu, Ni jambo jepesi kivuli kuendelea madaraja kumi; la, hicho kivuli na kirudi nyuma madaraja kumi.

11 Isaya nabii akamlilia Bwana; akakirudisha nyuma kile kivuli madaraja kumi, ambayo kilikuwa kimeshuka katika madaraja ya Ahazi”.

Isaya 38:7 “Jambo hili liwe ishara kwako, itokayo kwa Bwana, ya kuwa Bwana atalitimiza jambo hili alilolisema;

8 Tazama, nitakirudisha nyuma kivuli madaraja kumi, ambayo kilishuka juu ya duara ya Ahazi kwa sababu ya jua. Basi jua likarudi madaraja kumi katika hiyo duara, ambayo limekwisha kushuka”.

Tunajifunza nini?

Mungu huwa anaweza rudisha majira na nyakati, haijalishi kitakuwa kimechelewa kiasi gani, kwasababu hakuna jambo lolote linaloshindikana kwake. Aliweza kulisimamisha jua wakati wa Yoshua, jambo ambalo hata sasa linaweza kuonekana kama ni hadithi za kutunga lakini liliwezekana, aliweza kuurudisha ujana wa Ibrahimu na Sara, aliweza kuwapa uzao wakina Elizabeti na Zekaria. Hatashindwa kufanya muujiza na kwako, hata kama mambo yataonekana leo hii hayawezekani tena muda umekwenda,. Mungu anataka sisi tumwamini yeye, bila kuangalia hali zetu. Ndipo afanye.

Hivyo habari hiyo ni ya kututia moyo, tusichoke kumtumainia Mungu na kumwamini yeye, kwasababu hakuna linaloshindikana kwake.

Yeremia 32:27 “Tazama, mimi ni Bwana, Mungu wa wote wenye mwili; je! Kuna neno gumu lo lote nisiloliweza”?

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Makanwa ni nini katika biblia? (Danieli 6:22)

SIFONGO NA SIKI NI NINI?

Shekina ni nini? Na Je! Utukufu wa shekina unamaana gani?

Jaa ni nini katika biblia?

KIFO CHA MTAKATIFU PERPETUA NA FELISTA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Makanwa ni nini katika biblia? (Danieli 6:22)

Neno hilo tunaweza kulisoma katika kifungu hichi;

Danieli 6:22 “Mungu wangu amemtuma malaika wake, naye ameyafumba makanwa ya simba, nao hawakunidhuru; kwa kuwa mbele zake mimi nalionekana kuwa sina hatia; tena, mbele yako, Ee mfalme, sikukosa neno”.

Makanwa kwa jina lingine ni midomo.

Katika habari hiyo tunaona, baada ya Danieli kushitakiwa kwa makosa ambayo hakustahili kutokana na uaminifu wake kwa Mfalme Dario, walimkamata na kumtupa katika tundu la Simba. Simba wale walikuwa ni simba wenye njaa sana, ambao waliweza wakakaa wiki kadhaa, au hata mwezi bila kuona chakula chochote, na hata chakula kikiletwa  kilikuwa ni kidogo sana cha kuweza kuwatosheleza simba wote waliokuwa katika shimo lile, kwani chakula chao kilikuwa ni  wanadamu na si wanyama, hivyo ilikuwa mpaka aonekane mwanadamu muovu, ndipo simba hao wapate chakula.

Walifanya hivyo ili kuhakikisha kuwa mtu yeyote atakayetupwa huko ataliwa bila kubakishwa kitu chochote, mpaka mifupa yao kusagwa sagwa. Na ndicho walichomfanyia Danieli wakitazamia kuwa atakapotupwa, mara moja wale simba watamrukia, na kumpasua pasua angali akiwa bado juu, lakini tunaona Mungu alimtuma malaika wake na kuwafumba MAKANWA yao, (yaani midomo yao) wale simba.,..

Badala yake wao walipotupwa, biblia inatuambia simba wale walipokea angali wakiwa bado juu,(Danieli 6:24)

Je! Tunapata somo gani katika jambo hilo?

Mungu akifumba kinywa cha mlaji, hata kama ana njaa nyingi kwako, hawezi kula kilicho cha kwako..

Walaji sio simba tu, Mungu analo jeshi lingine la walaji, ambalo amelifananisha  ni tununu, nzige , parare na madumadu.. (Soma Yoeli 1:4) . Hawa wanaweza kuwa ni taifa, au jamii ya watu, au viongozi n.k. ambao Mungu anaweza kuwatumia kufunua makanwa yao kwako, wakakuharibu  kote kote bila kukuachia kitu, kama wewe si mtu wa haki, au ni mtenda dhambi. Utaona Mungu aliyaruhusu mataifa mbalimbali yaipige Israeli, na mengine kuwachukua utumwani kwa makosa yao tu ya kumwasi Mungu, ikapelekea makanwa ya wanadamu na mataifa kufunuliwa juu yao.

Na pia biblia inatuonyesha yapo mapepo ambayo yataachiliwa katika siku za mwisho yaliyofananishwa na nzige. Na hiyo itakuwa baada ya unyakuo kupita, na kazi yao itakuwa ni kuwauma wanadamu wote  ambao watakuwa hawana muhuri wa Mungu, juu ya vipaji vya nyuso zao.(Ufunuo 7:3). Kwa maelezo marefu juu ya habari hiyo fungua hapa>>> JINA LAKE KWA KIEBRANIA NI ABADONI,

Hata sasa, ibilisi anafunua makanwa yake na kuwameza , na kuwatafuna watu wengi pasipo wao kujua, biblia inasema….

1Petro 5:8 “Mwe na kiasi na kukesha; kwa kuwa mshitaki wenu Ibilisi, kama simba angurumaye, huzunguka-zunguka, akitafuta mtu ammeze”.

Lakini walio na muhuri wa Mungu (yaani Roho Mtakatifu) kama vile Danieli, Mungu anawaepusha nao. Swali ni je wewe nawe umetiwa muhuri huu wa Mungu?(Waefeso 4:30). Kumbuka  Roho Mtakatifu hawezi kuja juu ya mtu ikiwa mtu huyo, hajatubu dhambi zake kwa kumaanisha kabisa kuziacha, na kubatizwa.

Hivyo ikiwa leo hii utapenda kumkaribisha Yesu ndani ya maisha yako au kubatizwa, basi fungua hapa kwa ajili ya kupata maelekezo ya sala ya Toba.>>>  SALA YA TOBA

Ubarikiwe.Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

DANIELI: Mlango wa 1

OLE WAKO KORAZINI NA BETHSAIDA.

UTAWALA WA MIAKA 1000.

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 10 (Kitabu cha Zaburi).

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita..

Rudi Nyumbani:

Print this post