Duara ya Ahazi ni ipi? Na je! Kivuli cha Hezekia kilirudije nyuma?

Duara ya Ahazi ni ipi? Na je! Kivuli cha Hezekia kilirudije nyuma?

Zamani walikuwa hawana saa za mshale, au za kukonyeza kama tulizonazo sasa hivi ili kutambua majira ya siku, badala yake walitumia  njia nyingine mbalimbali zilizowasaidia kutambua saa za mchana, na njia kuu ilikuwa ni ya kukitazama kivule cha jua

Sehemu nyingine walituma kifaa kidogo maalumu ambacho kiliwekwa mahali pa wazi, ambapo jua litaweza kukipiga pande zote . Tazama picha..

duara ya muda

Sehemu nyingine zilitumika ngazi,ambazo zilijengwa pande zote, mashariki na magharibi, mwa eneo hilo la wazi, na pale jua lilipochomoza upande wa mashariki, kivuli kilichusha kwenye ngazi, na pale lilipozama upande wa magharibi kivuli kilinyanyuka, Hivyo kwa kutazama zile ngazi waliweza kutambua saa za asubuhi, mchana na jioni.. (Tazama picha juu kabisa mwanzoni mwa somo hili),.

Hivyo inawezekana duara la Ahazi lilikuwa ni la namna hii, japo biblia haijaeleza kwa marefu lakini tunaona, Hezekia, baada kuugua sana, na kuwa hatarini kufa, alimwomba Mungu kwa kumlilia amponye ugonjwa wake. Ndipo Mungu akamsikia na kumwambia kuwa atamponya, Lakini yeye akaomba Mungu ampe ishara kuwa jambo hilo litatendeka, ndipo akapewa nafasi ya kufanya uchaguzi wa upande wa kivuli hicho kitakapoangukia ndani ya   hilo duara la Ahazi baba yake Hezekia (ambaye alilijenga kwa ajili ya shughuli hiyo ya kutambua majira),..akaulizwa je! kiendelee mbele au kirudi nyuma.

Kwa kawaida jua linapokaribia kuzama, kivuli huwa kinakwenda mbele, hivyo Hezekia akaambiwa achugue je kivuli kizidi kwenda mbele zaidi, yaani akiwa na maana kama muda ule, kivuli kilikuwa kinaonyesha ni saa 8 mchana, basi kisogee mpaka kwenye saa 12 jioni.. Au achague kirudi nyuma, mpaka kwenye saa 1 asubuhi haijalishi kuwa muda huo utakuwa ni saa 8 mchana.

Ndipo Hezekia akachagua kirudishwe nyuma, kinyume cha asili, kwani kwenda mbele linaweza likawa ni jambo la kawaida..lakini kurudi nyuma inahitaji muujiza.

2Wafalme 20:8 “Hezekia akamwambia Isaya, Je! Kutakuwa na ishara gani ya kwamba Bwana ataniponya, nami siku ya tatu nitapanda nyumbani kwa Bwana.

9 Isaya akamwambia, Jambo hili litakuwa ishara kwako, itokayo kwa Bwana, ya kwamba Bwana atalifanya neno hilo alilolinena; je! Kivuli kiendelee madaraja kumi, au kirudi nyuma madaraja kumi?

10 Hezekia akajibu, Ni jambo jepesi kivuli kuendelea madaraja kumi; la, hicho kivuli na kirudi nyuma madaraja kumi.

11 Isaya nabii akamlilia Bwana; akakirudisha nyuma kile kivuli madaraja kumi, ambayo kilikuwa kimeshuka katika madaraja ya Ahazi”.

Isaya 38:7 “Jambo hili liwe ishara kwako, itokayo kwa Bwana, ya kuwa Bwana atalitimiza jambo hili alilolisema;

8 Tazama, nitakirudisha nyuma kivuli madaraja kumi, ambayo kilishuka juu ya duara ya Ahazi kwa sababu ya jua. Basi jua likarudi madaraja kumi katika hiyo duara, ambayo limekwisha kushuka”.

Tunajifunza nini?

Mungu huwa anaweza rudisha majira na nyakati, haijalishi kitakuwa kimechelewa kiasi gani, kwasababu hakuna jambo lolote linaloshindikana kwake. Aliweza kulisimamisha jua wakati wa Yoshua, jambo ambalo hata sasa linaweza kuonekana kama ni hadithi za kutunga lakini liliwezekana, aliweza kuurudisha ujana wa Ibrahimu na Sara, aliweza kuwapa uzao wakina Elizabeti na Zekaria. Hatashindwa kufanya muujiza na kwako, hata kama mambo yataonekana leo hii hayawezekani tena muda umekwenda,. Mungu anataka sisi tumwamini yeye, bila kuangalia hali zetu. Ndipo afanye.

Hivyo habari hiyo ni ya kututia moyo, tusichoke kumtumainia Mungu na kumwamini yeye, kwasababu hakuna linaloshindikana kwake.

Yeremia 32:27 “Tazama, mimi ni Bwana, Mungu wa wote wenye mwili; je! Kuna neno gumu lo lote nisiloliweza”?

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Makanwa ni nini katika biblia? (Danieli 6:22)

SIFONGO NA SIKI NI NINI?

Shekina ni nini? Na Je! Utukufu wa shekina unamaana gani?

Jaa ni nini katika biblia?

KIFO CHA MTAKATIFU PERPETUA NA FELISTA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments