Jibu: Tusome,
Luka 12:24 “Watafakarini kunguru, ya kwamba hawapandi wala hawavuni; hawana GHALA wala UCHAGA, na Mungu huwalisha. Bora ninyi mara nyingi kuliko ndege!”
“Ghala” ni chumba/nyumba ndogo ya kuhifadhia nafaka, lakini “Uchaga” ni jengo kubwa lililotengenezwa kwaajili ya kuhifadhia nafaka pamoja na aina nyingine ya vyakula vya mifugo na binadamu.
Hivyo Bwana Yesu aliposema, tuwatafakari kunguru, kwamba hawana “Ghala” wala “Uchaga”, alimaanisha kunguru hawana mahali pa kuhifadhia chakula kwaajili ya vipindi vigumu vinavyokuja mbeleni, Lakini muujiza ni kwamba ijapokuwa hawana sehemu za kuweka akiba ya chakula, unapokuja msimu wa kiangazi bado hawafi kwa njaa, wanaishi!!
Utakumbuka kisa cha Nabii Eliya, kipindi ambacho mbingu zimefungwa miaka mitatu na Nusu, kipindi ambacho watu na Wanyama wanakufa kwa kukosa chakula, utaona kunguru bado walikuwa wanaishi na wanakula vizuri, na hata Mungu kuwatumia hao kumpelekea chakula mtumishi wake.
1Wafalme 17:2 “Neno la Bwana likamjia, kusema,
3 Ondoka hapa, geuka, uende upande wa mashariki, ujifiche karibu na kijito cha Kerithi kinachokabili Yordani.
4 Itakuwa utakunywa maji ya kile kijito; NAMI NIMEWAAMURU KUNGURU WAKULISHE HUKO.
5 Basi akaenda akafanya kama alivyosema Bwana; kwa kuwa akaenda akakaa karibu na kijito cha Kerithi, kinachokabili Yordani.
6 KUNGURU WAKAMLETEA MKATE NA NYAMA ASUBUHI, na mkate na nyama jioni, akanywa maji ya kile kijito”.
Umeona?.. wakati watu wanakufa kwa njaa, Kunguru na Watoto wao wanakula mpaka wanasaza, mpaka wanakuwa na akiba ya kumpelekea Eliya, mtumishi wa Mungu.
Lakini sasa Bwana Yesu anakuja kusema katika Luka 12:24, kwamba TUWATAFAKARI HAO!!.. Kama Baba wa mbinguni anawapa chakula hao, na ijapokuwa hawana maghala wa uchaga, si Zaidi sisi endapo tukimwamini na kumtegemea yeye?.. Kwasababu sisi ni bora kuliko kunguru mara nyingi.
Baba yetu anatuhurumia sisi mara nyingi Zaidi, kuliko anavyowahurumia kunguru!. Tunapomtegemea yeye, hata kama tutapitia hali ngumu na za ukame kiasi gani, basi Bwana Yesu hatatuacha tupungukiwe kabisa…atakuwa na sisi na kutuhudumia kuliko anavyowahudumia kunguru.
Waebrania 13:5 “Msiwe na tabia ya kupenda fedha; mwe radhi na vitu mlivyo navyo; kwa kuwa yeye mwenyewe amesema, Sitakupungukia kabisa, wala sitakuacha kabisa.
6 Hata twathubutu kusema, Bwana ndiye anisaidiaye, sitaogopa; Mwanadamu atanitenda nini?”
Je umempokea Yesu leo?, je umefanyika mtoto wake?, kama bado kumbuka dunia si salama, wala haina mshahara wowote Zaidi ya mauti, dunia itakususha thamani Zaidi ya kunguru siku ya mateso, kipindi cha Eliya wote waliokuwa wanaitumainia dunia, walikufa kwa njaa, lakini kunguru wakawa wanaishi…wote waliokuwa wanaabudu mabaali waliangamia, lakini kunguru waliishi!..Lakini waliomtegemea Mungu waliishi na kudumu,
Mpokee Yesu leo kama bado hujampokea, pia ukabatizwe katika ubatizo sahihi kwaajili ya ondoleo la dhambi na upokee kipawa cha Roho Mtakatifu.
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
KAMA MKRISTO FAHAMU ZIPO HATUA UTAPIGISHWA NA MUNGU.
JIHADHARI NA ROHO ZIDANGANYAZO.
TUSIWE WATU WA KUPUNGUKIWA AKILI.
Biblia inamaana gani iliposema “Dhambi ilipozidi, Neema ilizidi kuwa nyingi Zaidi”.
KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 1: Upande wa wanaume)
Ukienda kuomba kazi yoyote halali, kikawaida huwezi kupewa majibu ya papo kwa papo na kuambiwa anza kazi leo, bila ya kutaka kwanza taarifa Fulani kutoka kwako, hata kama ni ile ndogo ya kufagia, vipo vigezo vitaambatanishwa tu na kazi hiyo, aidha utaulizwa umri wako, au hali yako ya kiafya, au fani uliyonayo, au jinsia yako, au elimu yako n.k. Lakini ikiwa hujasoma vigezo vyao, halafu ukapeleka maombi yako kienyeji, Ni wazi kuwa barua yako itatupwa kapuni.
Vivyo hivyo na kwa Mungu, tunapopeleka maombi yetu, ni sharti tujue vigezo vya kujibiwa, vinginevyo, tutabakia kumlaumu Mungu, mbona tulifunga, na kukesha lakini hujasikia maombi yetu.
Hivi ndio vigezo kivuu vya maombi yetu kujibiwa na Mungu
Hili ndio jambo la kwanza na la msingi; Dhambi ndiyo inayomdhoofisha Mungu, na kumdumaza kwenye eneo la kujibiwa maombi yetu.
Isaya 59:1 “”Tazama, mkono wa Bwana haukupunguka, hata usiweze kuokoa wala sikio lake si zito, hata lisiweze kusikia;
2 lakini maovu yenu yamewafarikisha ninyi na Mungu wenu, na dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, hata hataki kusikia”.
Hakikisha unakaa mbali na mambo yote yanayomchukiza Mungu, yaliyo ndani yako, mfano uzinzi, ulevi, uongo, rushwa, wivu, matusi n.k.
Kuomba vizuri, sio kupangalia maneno katika uombaji, hapana, bali kuomba jambo linalotimiza mapenzi ya Mungu.
Yakobo 4:2 “Mwatamani, wala hamna kitu, mwaua na kuona wivu, wala hamwezi kupata. Mwafanya vita na kupigana, wala hamna kitu kwa kuwa hamwombi!
3 Hata mwaomba, wala hampati kwa sababu mwaomba vibaya, ili mvitumie kwa tamaa zenu”.
Jiulize unachokiomba je kina lengo gani, ni ili umkomoe yule adui yako?, au ili ukaongezee mtaji wa ile biashara yako ya bar?, au ili uonekane mwanamke wa kisasa mfano wa Yezebeli? Kama sivyo ni Ili nini?..Fahamu kuwa Mungu anachunguza mioyo. Hakikisha unachokiomba ni kwa utukufu wa Mungu. Vinginevyo hutapokea chochote.
Bwana Yesu alisema..
Mathayo 6:5 “Tena msalipo, msiwe kama wanafiki; kwa maana wao wapenda kusali hali wamesimama katika masinagogi na katika pembe za njia, ili waonekane na watu. Amin, nawaambia, Wamekwisha kupata thawabu yao.
6 Bali wewe usalipo, ingia katika chumba chako cha ndani, na ukiisha kufunga mlango wako, usali mbele za Baba yako aliye sirini; na Baba yako aonaye sirini atakujazi”.
Mawazo yako yanapaswa yamwelekee Mungu, na sio Mungu Pamoja na wanadamu. Ukilijua hilo, basi hutaona sababu ya kujionyesha kwa watu ili wakupe utukufu.
Ukweli ni kwamba yapo maombi utahitaji kuonyesha bidii kwa Mungu ili uyapate, na sio kuomba dakika 5 halafu basi, hapo unaweza usipokee chochote, bali yakupasa kung’ang’ana mbele za Mungu ndipo yaje kutokea.
Yakobo 5:16 “… Kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana, akiomba kwa bidii.
17 Eliya alikuwa mwanadamu mwenye tabia moja na sisi, akaomba kwa bidii mvua isinyeshe, na mvua haikunyesha juu ya nchi muda wa miaka mitatu na miezi sita.
18 Akaomba tena, mbingu zikatoa mvua, nayo nchi ikazaa matunda yake.
Hivyo ongeza misuli yako ya maombi. Hata ya masafa mrefu na mikesha.
Yakupasa ujifunze uvumilivu. Uvumilivu ni muhimu sana ikiwa hujajibiwa leo, haimaanishi kuwa Mungu hajakusikia, bali omba tena kesho, na kesho kutwa, kwasababu ipo sababu kwanini hujakipata kwa muda huo.
Luka 18 : 1-8
18:1 “Akawaambia mfano, ya kwamba imewapasa kumwomba Mungu sikuzote, wala wasikate tamaa.
2 Akasema, Palikuwa na kadhi katika mji fulani, hamchi Mungu, wala hajali watu.
3 Na katika mji huo palikuwa na mwanamke mjane, aliyekuwa akimwendea-endea, akisema, Nipatie haki na adui wangu.
4 Naye kwa muda alikataa; halafu akasema moyoni mwake, Ijapokuwa simchi Mungu wala sijali watu,
5 lakini, kwa kuwa mjane huyu ananiudhi, nitampatia haki yake, asije akanichosha kwa kunijia daima.
6 Bwana akasema, Sikilizeni asemavyo yule kadhi dhalimu.
7 Na Mungu, je! Hatawapatia haki wateule wake wanaomlilia mchana na usiku, naye ni mvumilivu kwao?
8 Nawaambia, atawapatia haki upesi; walakini, atakapokuja Mwana wa Adamu, je! Ataiona imani duniani”?
Ni jambo dogo, lakini linamatokeo makubwa sana rohoni. Sio kwamba Mungu anahaja na fedha zetu hapana, lakini umtoleapo unaonyesha upendo wako kwake. Ukipelekea maombi yako kwake, jijengee utaratibu pia wa kuambatanisha na sadaka, kwa kile ulichojaliwa, ikiwa ni senti mbili, au milioni 10, mpelekee Bwana. Wengi waliotenda hivi walifanikiwa.
Malaki 3:10 “”Leteni zaka kamili ghalani, ili kiwemo chakula katika nyumba yangu, mkanijaribu kwa njia hiyo, asema Bwana wa majeshi; mjue kama sitawafungulia madirisha ya mbinguni, na kuwamwagieni baraka, hata isiwepo nafasi ya kutosha, au la”.
Hivyo kwa kuzingatia, mambo hayo sita, basi ni hakika Mungu atakujibu maombi yako. Na utamfurahia yeye.
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Nifanyeje niwe mwombaji mzuri, wa masafa marefu?
MLANGO MWINGINE WA ADUI KUTULETEA MAJARIBU.
JINSI YA KUPOKEA UPONYAJI, TUNAPOMWOMBA BWANA ATUGUSE MARA YA PILI.
Tofuati kati ya kifo na mauti ni ipi?
Kujazi maana yake ni kulipa.
Kwamfano tusome Neno hilo jinsi lilivyotumika na kumaanisha katika maandiko;
Mathayo 6:2 “Basi wewe utoapo sadaka, usipige panda mbele yako, kama wanafiki wafanyavyo katika masinagogi na njiani, ili watukuzwe na watu.
3 Amin, nawaambieni, Wamekwisha kupata thawabu yao. Bali wewe utoapo sadaka, hata mkono wako wa kushoto usijue ufanyalo mkono wako wa kuume;
4 sadaka yako iwe kwa siri; na Baba yako aonaye sirini atakujazi”.
Maana yake ni kwamba, unapokuwa mtu wa kutoa sadaka bila kuwa na nia ya kuonekana mbele za watu, basi Mungu atakulipa kwa utoacho.
Mathayo 6:6 “Bali wewe usalipo, ingia katika chumba chako cha ndani, na ukiisha kufunga mlango wako, usali mbele za Baba yako aliye sirini; na Baba yako aonaye sirini atakujazi”.
Mathayo 6:17 “Bali wewe ufungapo, jipake mafuta kichwani, unawe uso;
18 ili usionekane na watu kuwa unafunga, ila na Baba yako aliye sirini; na Baba yako aonaye sirini atakujazi”.
Vilevile unapokuwa mtu wa kuomba na kufunga, lengo lako likuwa ni kujisogoza mbele za Mungu na sio kufanya mashindano, au kuonekana na watu kuwa ni wa kiroho sana, basi Mungu atakulipa kwa hicho ukifanyacho.
Ruthu 2:11 “Naye Boazi akajibu, akamwambia, Nimeelezwa sana yote uliyomfanyia mkweo, tangu alipokufa mumeo; na jinsi ulivyowaacha baba yako na mama yako, na nchi yako uliyozaliwa, ukawafikilia watu usiowajua tangu hapo.
12 Bwana akujazi kwa kazi yako, nawe upewe thawabu kamili na Bwana, Mungu wa Israeli, ambaye umekuja kukimbilia chini ya mabawa yake”.
Tunaona pia hapa Boazi akimbariki Ruthu, kwa wema wake aliomfanyia mkwewe, na kumwambia Bwana akulipe kwa kazi yako njema.
Lakini ni ujumbe gani Bwana anapitisha katika haya?
Ni kuonesha kuwa hakuna tendo jema tutakalomfanyia Mungu asirudishe malipo, endapo tutafanya ipasavyo. Kama kweli utaomba mbele zake, utafunga kwa ajili yake, utamtolea sadaka zako, kama kweli utatenda wema wowote, fahamu kuwa hilo Bwana atakulipa tu kwa wakati wake, thawabu yako haitakupita.
Hivyo atukuzwe Mungu awezaye kutuona na kuturehemu na kutubariki. Sifa, heshima na utukufu vina yeye milele na milele. Amina.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Sadaka ya kutikiswa ilikuwaje?
Nini maana ya ampokeaye Nabii atapata thawabu ya Nabii? (Mathayo 10:41).
JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 1)
HERI WAPATANISHI, MAANA HAO WATAITWA WANA WA MUNGU
Mapooza ni nini? Na je! Twawezaje kuepukana nayo?
Nini maana ya huu mstari? “Yeye mwenyewe ataokolewa lakini ni kama kwa moto”
Jina kuu la Bwana na Mwokozi wa Ulimwengu, Simba wa kabila la Yuda, na Mkuu wa wafalme wa dunia, Yesu Kristo libarikiwe. Karibu tujifunze biblia, neno la Mungu wetu, lililo mwanga wa njia yetu, na taa iongozayo miguu yetu.
Upo wakati wakati ambao tutahitaji Bwana atuguse mara ya pili, lakini ni vizuri kujua kanuni ya kupokea Uponyaji pindi tunapomsihi Bwana atuguse tena…
Hebu tusome kisa kimoja katika biblia na kisha tutafakari na tujifunze, kanuni ya kupokea uponyaji mkamilifu.
Tusome Marko 8:22-26, (Zingatia maneno yaliyoanishwa kwa herufi kubwa).
Marko 8:22 “Wakafika Bethsaida, wakamletea kipofu, wakamsihi amguse.
23 Akamshika mkono yule kipofu, akamchukua nje ya kijiji, AKAMTEMEA MATE YA MACHO, akamwekea mikono yake, akamwuliza, Waona kitu?
24 AKATAZAMA JUU, AKASEMA, NAONA WATU KAMA MITI, INAKWENDA.
25 Ndipo akaweka tena mikono yake juu ya macho yake, NAYE AKATAZAMA SANA; akawa mzima, akaona vyote waziwazi.
26 Akampeleka nyumbani kwake, akisema, Hata kijijini usiingie”.
Katika kisa hichi hebu tujiulize swali lifuatalo, kisha tuendelee mbele..
Je inawezekana mtu atazame juu halafu aone watu?, tena watu wenyewe wanatembea? Na tena wanatembea kwa kasi kama miti?… Nilitegemea hata angesema anaona “ndege wanaruka, wanakimbia kama miti”!! Lakini yeye anasema anaona watu!!……Bila shaka ulishawahi kusafiri na basi linalokwenda kasi, na njiani ukaona namna miti inavyoonekana kama inarudi nyuma kwa kasi sana…Ndivyo alivyoona huyu mtu alipotazama juu..aliona watu!..
Kwa kawaida, huu sio uponyaji!!.. Huyu mtu hakuwa amepata uponyaji wowote, bali alikuwa katika hatua za mwanzo za kupokea uponyaji..ni kama tu TV iliyowashwa ambayo bado haijakamata mawimbi!!..inakuwa inaonyesha tu chenga chenga…
Lakini tunaona tabia ya kipekee ya huyu kipofu baada ya kuguswa na Bwana mara ya pili.
Utaona huyu kipofu mara ya kwanza alipoguswa, alitazama juu hakutumia muda mrefu kutazama, badala yake, kwa haraka haraka akakimbilia kumjibu Bwana kwa kusema “anaona watu kama miti”….. lakini baada ya kuguswa na Bwana mara ya pili, ni kama alijifunza kitu kuwa hana budi kutokuwa na haraka ya mambo…utaona alitulia na KUTAZAMA SANA!! (pengine alitumia dakika kadhaa kutazama juu), akawa bado anaona ile ile miti, lakini hakuacha kutazama…..
Na alipozidi KUTAZAMA SANA, pengine akaanza kuona ile miti inafutika kidogo kidogo, akaanza kuona anga linakuwa jeupe na kidogo kidogo akaanza kuona mawingu, na pengine akaanza kuona ndege wanaruka, na alipotazama mbele akamwona Bwana Yesu, ndipo akasema sasa ninaona!!! Haleluya.
Na sisi hatuna budi KUTAZAMA SANA!!..Tusiishie kutazama kidogo tu! tusiishie kuzungumza, wala kunung’unika, wala kukosoa, wala kutoa hitimisho, pale tunapoona uponyaji haujakamilika….bali turuhusu uponyaji wa Bwana ufanye kazi!… Tuwe na Subira huku tukiliamini Neno lake.
Kutazama sana, ni kudumu katika kumwamini Mungu, hata kama unaona lile tatizo bado halijatatuka… wewe endelea kumwamini Bwana na kusubiri, bila kutoa uso wako juu mpaka muujiza wako utakapokamilika..
Pengine ulimwomba Bwana kuhusu hali unayopitia ya kiroho au kimwili, lakini uliishia kuona chenga chenga katika huo ugonjwa, au hilo tatizo..lakini sasa umeijua kanuni..Msii Bwana akuguse tena kwa mara nyingine, lakini safari hii USIRUHUSU IMANI YAKO IPUNGUE, WALA USIUKIRI UGONJWA.…Utaona muujiza wa ajabu, ukitendeka!!.
Bwana akubariki.
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
AMEFANYIKA BORA KUPITA MALAIKA!
KWANINI YESU NI ADAMU WA PILI?
JINSI YA KUMSIKIA MUNGU, NA KUPOKEA MAFUNUO AU JUMBE KUTOKA KWAKE.
Jina kuu la Bwana na Mwokozi wetu, Yesu Kristo libarikiwe!. Karibu tuyatafakari maandiko,
Neno la Bwana wetu, lililo chakula cha roho zetu linasema hivi..
Warumi 10:10 “Kwa maana KWA MOYO mtu huamini HATA KUPATA HAKI, na KWA KINYWA hukiri HATA KUPATA WOKOVU”.
Ipo sababu kwanini Biblia imetenganisha hayo mambo mawili, HAKI na WOKOVU. Watu wengi leo wameishia kupata HAKI tu, lakini si WOKOVU.. Wapo wengi leo waliomwamini Bwana Yesu mioyoni mwao na kuishia kupata haki sawasawa na Warumi 5:1 na Wagalatia 2:16, lakini hawana WOKOVU, maishani mwao, Na Wokovu unakuja kwa kumkiri Yesu na maneno yake kwa kinywa!.
Wakati Bwana Yesu akiwa duniani, walikuwepo Mafarisayo na wakubwa wengi waliomwamini mioyoni mwao, lakini katika Vinywa vyao, hawakumkiri..na hivyo Imani yao ikahesabika si kitu!.
Yohana 12:42 “Walakini hata katika wakuu WALIKUWAMO WENGI WALIOMWAMINI; lakini kwa sababu ya Mafarisayo HAWAKUMKIRI, wasije wakatengwa na sinagogi”.
Umeona?. walivifunga vinywa vyao, kuhofia kutengwa na dini zao, au madhehebu yao, au wakubwa wenzao, au kuonekana washamba na waliorukwa na akili!!..
Ndugu unapomwamini Bwana Yesu na maneno yake, ndani ya moyo wako, hiyo bado haitoshi kukupa wewe wokovu.. Huna budi kumkiri kwa kinywa chako kila siku katika Maisha yako.. Wokovu wa siri siri, na wakujificha ficha huo sio wokovu kibiblia!!.. Bwana Yesu alisema mtu yeyote akimwonea yeye na maneno yake, yeye naye atamwonea haya mtu huyo mbele za baba yake na malaika zake.
Luka 9:26 “Kwa sababu kila ATAKAYENIONEA HAYA MIMI NA MANENO YANGU, Mwana wa Adamu ATAMWONEA HAYA MTU HUYO, atakapokuja katika utukufu wake na wa Baba na wa malaika watakatifu”.
Soma tena..
Mathayo 10:32 “Basi, kila mtu atakayenikiri mbele ya watu, NAMI NITAMKIRI MBELE ZA BABA YANGU ALIYE MBINGUNI”.
Umeona?..kumbe unaweza kuwa umemwamini Bwana Yesu moyoni mwako, lakini kwasababu tu! Humkiri maishani mwako, siku ile naye akakukana!!..kumbe wokovu wetu unakamilika pia kwa kumkiri Bwana Yesu.
Wakati Fulani, Bwana Yesu alimponya kipofu mmoja, ambaye alizaliwa katika hali hiyo ya upofu.. Na baada ya kumponya..Wazazi wake yule kipofu, walimwamini Bwana Yesu kuwa ni Kristo, lakini kwa hofu ya kutengwa hawakumkiri kwa vinywa vyao, lakini mwanao ambaye alikuwa kipofu, alimwamini Bwana Yesu na kumkiri..
Yohana 9:18 “Basi Wayahudi hawakusadiki habari zake, ya kuwa alikuwa kipofu, kisha akapata kuona; hata walipowaita wazazi wake yule aliyepata kuona.
19 Wakawauliza wakisema, Huyu ndiye mwana wenu, ambaye mnasema kwamba alizaliwa kipofu? Amepataje, basi, kuona sasa?
20 Wazazi wake wakawajibu, wakasema, Tunajua ya kuwa huyu ndiye mwana wetu, tena ya kuwa alizaliwa kipofu;
21 lakini jinsi aonavyo sasa hatujui; wala hatujui ni nani aliyemfumbua macho. Mwulizeni yeye mwenyewe; yeye ni mtu mzima; atajisemea mwenyewe.
22 Wazazi wake waliyasema hayo kwa sababu WALIWAOGOPA WAYAHUDI; kwa maana Wayahudi walikuwa wamekwisha kuafikiana kwamba MTU AKIMKIRI KUWA NI KRISTO, ATATENGWA NA SINAGOGI.
23 Ndiyo sababu wale wazazi wake walisema, Ni mtu mzima, mwulizeni yeye”.
Umeona hawa wazazi, walikuwa na Imani mioyoni mwao, lakini Imani yao haikuwasaidia..Bwana Yesu hakuwafuata…lakini mbele kidogo, utaona Bwana anamfuata yule kipofu, na kujidhihirisha kwake kwasababu alimkiri..
Yohana 9:33 “Kama huyo asingalitoka kwa Mungu, asingeweza kutenda neno lo lote.
34 Wakajibu, wakamwambia, Ama! Wewe ulizaliwa katika dhambi tupu, nawe unatufundisha sisi? Wakamtoa nje.
35 YESU AKASIKIA KWAMBA WAMEMTOA NJE; NAYE ALIPOMWONA ALISEMA, WEWE WAMWAMINI MWANA WA MUNGU?
36 NAYE AKAJIBU AKASEMA, NI NANI, BWANA, NIPATE KUMWAMINI?
37 YESU AKAMWAMBIA, UMEMWONA, NAYE ANAYESEMA NAWE NDIYE.
38 AKASEMA, NAAMINI, BWANA. AKAMSUJUDIA”.
Leo Bwana Yesu ajidhihirishi kwa wengi, kwasababu hiyo moja tu!.. ya KUTOMKIRI YEYE!!.. Tunampenda na kumwamini kweli Yesu, lakini hatuwezi kumkiri mbele ya mabosi zetu, hatuwezi kumkiri mbele ya wanafunzi wenzetu, hatuwezi kumkiri mbele ya wafanyakazi wenzetu, hatuwezi kumkiri mbele ya ndugu zetu…huku tukidhani kuwa ndio tunao wokovu..kumbe bado hatuna wokovu!!!.
Vile vile ukiyaonea haya maneno yake yote ya kwenye biblia..bado hauna wokovu!!.. Haijalishi unalijua Neno kiasi gani, au unaijua biblia kiasi gani…
Siku zote kumbuka hilo, Wokovu wetu unakamilika na KUMKIRI BWANA YESU NA MANENO YAKE!!!!..(Usilisahau hilo kamwe).
Warumi 10:8 “Lakini yanenaje? Lile neno li karibu nawe, KATIKA KINYWA CHAKO, na katika MOYO WAKO; yaani, ni lile neno la imani tulihubirilo.
9 Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka
10 Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu”
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
USIMLAANI KIZIWI, WALA USITIE KWAZO MBELE YA KIPOFU.
Kama tunaokolewa kwa neema kwanini wokovu tuupate kwa nguvu?
Nakusalimu katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo. Karibu tena tuyatafakari maneno matukufu ya mola wetu. Leo napenda tuutafakari huu mstari kwa ukaribu sana, kwasababu una maana kubwa nyuma yake huwenda tofauti na vile tunavyoufahamu.
Biblia inasema..
Mithali 23:29 “Ni nani apigaye, Yowe? Ni nani aliaye, Ole? Ni nani mwenye ugomvi? Ni nani mwenye mguno? Ni nani aliye na jeraha zisizo na sababu? Ni nani aliye na macho mekundu?
30 NI WALE WAKAAO SANA KWENYE MVINYO; Waendao kutafuta divai iliyochanganyika”.
Mwandishi anaeleza matokeo, ya mtu kufikiwa na hayo mambo yote sita(6) mabaya kwa mpigo ni nini.. Yaani Yowe, ole, ugomvi, mguno, jeraha zisizo na sababu, na macho mekundu.. ni nini..
> Anaposema Yowe, sote tunafahamu, mpaka mtu apige yowe, ni matokeo ya kakumbwa na jambo baya sana, ambalo linamfanya ahitaji msaada wa haraka sana, pengine labda anafukuzwa auawe, au anapigwa vikali , au amekumbwa na taarifa za kushtusha sana..Hivyo kwa kawaida hakuna yowe inayotokana na mema.
> Vilevile anaposema ni nani aliaye ole..Tunafahamu ole ni baada ya kutahadharishwa kwa mabaya. Lakini mpaka mtu analia ole, “kusema ole wangu mimi,” ni mtu ambaye tayari ameshakumbwa na mabaya hayo,aidha vifungo, magonjwa, taabu, mateso n.k.
> Halikadhalika anaposema, ni nani mwenye mguno; Anamaanisha mtu mwenye malalamiko, mwenye maneno yasiyofaa, au kueleweka, mtukanaji, mtu wa kashfa. Jambo hili nalo haliji kutoka katika mema.
> Vilevile aliye na jeraha zisizo na sababu, ni mtu aliyejiingiza katika matatizo ambayo hakustahili au hakupaswa kukumbwa nayo. Pengine amrukwa na akili, au uzembe uliopitiliza usio wa kibinadamu.
> Anaposema tena ni “nani mwenye ugomvi”..Yaani mtu anayezua ugomvi, malumbano, yasiyo na maana au sababu, kufoka, na ukorofi.
> Na pia mwenye macho mekundu, .Yaani macho yaliyolegezwa na pombe.
Sasa ukisoma kwa makini, vyote hivyo sita (6), haviji hivi hivi kwa wanywaji pombe kidogo, wanaweza wakafikia kiwango Fulani..Lakini mpaka tabia hizo zitokee kwa mlevi ni lazima awe ni mtu wa “KUKAA SANA KWENYE MVINYO” kama maandiko yanavyosema..Walevi waliopitiliza, ndio huwa wanaanguka mitaroni na kujiumiza miza wenyewe ovyo bila sababu, ndio wenye macho yaliyolegea mpaka kuwa mekundu, ndio wanaopiga piga makelele njiani na majumbani, ndio wanaopata hasara ya mali zao, na kupiga mayowe, anayetapika ovyo n.k… Hii hali mpaka afikie mtu, ni lazima atukuwa mule mlevi wa kishinda kilabuni usiku kucha.
Ni kutuonyesha jinsi kitu chenye ulevi kinapotumiwa kwa muda mrefu na sanaa, kinavyoweza kuleta matokeo yakubwa Zaidi..
Lakini biblia inatuambia kuwa ipo DIVAI MPYA. Ambayo sisi wakristo, tunakunywa na katika hiyo, tunalewa. Lakini kanuni ni ileile hatutaweza kulewa vema na kutoa matokeo yake, kama hatutakaa sana katika kuinywa..
Na divai yenyewe si mwingine Zaidi ya ROHO MTAKATIFU.
Siku ile ya Pentekoste mitume walipojazwa Roho Mtakatifu, walionekana kama walevi, waliolewa kwa mvinyo mpya..Kumbe hawakujua kuwa alikuwa ni Roho Mtakatifu kawafanya vile. Kuonyesha kuwa Roho naye huwa anawalewesha watu wake pia katika roho.
Matendo 2:12 “Wakashangaa wote wakaingiwa na shaka, wakiambiana, Maana yake nini mambo haya?
13 Wengine walidhihaki, wakisema, wamelewa kwa mvinyo mpya.
14 Lakini Petro akasimama pamoja na wale kumi na mmoja, akapaza sauti yake, akawaambia, Enyi watu wa Uyahudi, na ninyi nyote mkaao Yerusalemu, lijueni jambo hili, mkasikilize maneno yangu.
15 Sivyo mnavyodhani; watu hawa hawakulewa, kwa maana ni saa tatu ya mchana;
16 lakini jambo hili ni lile lililonenwa kwa kinywa cha nabii Yoeli,
17 Itakuwa siku za mwisho, asema Mungu, nitawamwagia watu wote Roho yangu, na wana wenu na binti zenu watatabiri; na vijana wenu wataona maono; na wazee wenu wataota ndoto”.
Na matokeo ya kuleweshwa kisawasawa na Roho Mtakatifu, ni kutoa matunda yake.. ambayo tunayasoma katika, Wagalatia 5:22 na pia kufanya kazi kama za mitume, walizofanya baada ya kupokea Roho..
Wagalatia 5:22 “Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu,
23 upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria”.
Hivyo hatuwezi kuwa na Upendo, kama hatutakaa sana uweponi mwa Mungu tulewe mema yake kisawasawa, hatutakaa tufikie furaha timilifu, kama tutakuwa tunamtafuta Mungu jumapili kwa jumapili, na sio muda wote.. Hatutakaa tuwe na kiasi, na upole na amani, kama hatujibidiishi, kuutafuta uso wa Mungu, kwa wakati mrefu. Hatuwezi kuzidhihirisha karama za Roho kama hatutampa muda wa kutosha mioyoni mwetu.
Tukae sana kwenye mvinyo wetu (Roho Mtakatifu), ili tumzalie Bwana matunda ya haki.
Hivyo, tukiwa na bidii katika Mungu, kusali, kufunga, kutafakari sana, maneno ya Mungu Pamoja na wapendwa wenzetu, Kidogo kidogo tunakuwa walevi, na kwa jinsi tunavyozidisha ndivyo tutakavyoyatoa hayo matunda ya Roho kirahisi sana ndani yetu.
Hivyo sote kwa Pamoja tuanze kuzidisha bidi zetu kwa Bwana. Ili Bwana naye apate nafasi ya kutuponya
Bwana akubariki.
Ikiwa hujaokoka, kumbuka kuwa hizi ni siku za mwisho, siku yoyote Yesu anarudi kulinyakua kanisa lake. Kumbuka injili iliyobakia sasa sio ya kubembelezewa wokovu, ni wewe mwenyewe kuona hali halisi na kujiokoa nafsi yako. Ikiwa upo tayari kutubu leo na kumpa Yesu Maisha yako, basi utakuwa umefanya uamuzi wa busara, katika dakika hizi za majeruhi tulizopo.
Hivyo kama utapenda kupata msaada huo. Basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi, ili tuweze kuomba na wewe na pia kukuongoza sala ya Toba (Bure). >>> +255693036618/ +255789001312 .
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Nini maana ya “Siku moja nyuani mwa Bwana ni bora kuliko siku elfu”?
JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?
Mapooza ni nini? Na je! Twawezaje kuepukana nayo?
Kwanini Bwana Yesu alisema “Msimwamkie mtu njiani”?
Bwana alimaanisha nini kusema “kila mtu atatiwa chumvi kwa moto”
Je! Bwana Yesu alikunywa kileo mpaka watu wakasema ni mlafi na mlevi? Kulingana na Mathayo 11:19?
1. MTUMWA
Mtumwa ni mfanyakazi wa jinsia ya kiume. Kawaida ya mtumwa, anakuwa anatawaliwa uhuru wake na maamuzi yake kwa asilimia kubwa na yule anayemtumikisha au aliyemwajiri. Hivyo mwanaume yeyote anayetumika chini ya bwana wake kwa namna hiyo anaitwa MTUMWA.
Sisi tuliokoka tunakuwa ni watumwa wa Bwana Yesu (2Timetheo 2:24)..na wote ambao hawajamwamini Bwana Yesu, wanakuwa ni watumwa wa dhambi.
Yohana 8:33 “Wakamjibu, Sisi tu uzao wake Ibrahimu, wala hatujawa watumwa wa mtu wakati wo wote; nawe wasemaje, Mtawekwa huru?
34 Yesu akawajibu, Amin, amin, nawaambia, KILA ATENDAYE DHAMBI NI MTUMWA WA DHAMBI.
35 Wala mtumwa hakai nyumbani sikuzote; mwana hukaa sikuzote.
36 Basi Mwana akiwaweka huru, mtakuwa huru kweli kweli”.
2. MJAKAZI.
Mjakazi ni mtumwa wa kike, sifa zile zile alizonazo mtumwa wa kiumbe, ndizo hizo hizo alizonazo mjakakazi.
Mfano wa aliyekuwa Mjakazi katika biblia ni Hajiri.
Mwanzo 16:1 “Basi Sarai mkewe Abramu hakumzalia mwana, naye alikuwa na mjakazi, Mmisri, JINA LAKE HAJIRI”.
3. KIJAKAZI.
Kijakazi ni Mjakazi wa hadhi ya chini Zaidi. Ni sawa na kutumia neno “kitoto” badala ya “mtoto”..ndivyo ilivyo kwa “Kijakazi” na “Mjakazi”..Mfano wa vijakazi katika biblia ni BILHA NA ZILPA.
Mwanzo 35:25 “Wana wa Bilha, KIJAKAZI WA RAHELI, ni Dani na Naftali.
26 Wana wa Zilpa, KIJAKAZI WA LEA, ni Gadi na Asheri”.
Biblia inatushauri tusiwe “watumwa wa wanadamu”, bali wa Bwana.
1Wakorintho 7:23 “Mlinunuliwa kwa thamani; msiwe watumwa wa wanadamu”.
Vile vile tusiwe watumwa wa dhambi ambao ndio Mbaya Zaidi.. Dhambi inapomtumikisha mtu, mshahara wake ni MAUTI!!. Heri mwadamu akiisha kutumikisha atakulipa fedha, au mali..lakini dhambi inakulipa Mauti.
Warumi 6:23 “Kwa maana MSHAHARA WA DHAMBI NI MAUTI; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu”.
Sasa ili kuondokana na utumwa wa dhambi, tunafanyaje?
Bwana Yesu alisema maneno yafuatayo..
Mathayo 11:28 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.
29 Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;
30 kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi”.
Jitie Nira ya Bwana Yesu, ufanyike mtumwa wake, kwasababu Mshahara wake ni UZIMA WA MILELE!!!.
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 1)
MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA KITABU CHA FILEMONI.
LEO WOKOVU UMEFIKA NYUMBANI HUMU
Milima ya Ararati, mahali ambapo Safina ya Nuhu ilitua, ipo wapi kwasasa?
JIbu: Tusome,
Mwanzo 8:4 “Mwezi wa saba, siku ya kumi na saba ya mwezi, safina ikatua juu ya MILIMA YA ARARATI.”.
Milima ya Ararati, ipo katika Nchi ya UTURUKI ya sasa, (Mashariki mwa Uturuki).Tazama picha juu.. Milima hiyo mpaka leo ipo, na watu wanaitembelea.
Eneo la Mashariki ya nchi ya Uturuki, zamani lilikuwa linajulikana kama Ararati. Utaona kwenye biblia limetajwa mara kadhaa…
2Wafalme 19:37 “Ikawa, alipokuwa akiabudu nyumbani mwa Nisroki, mungu wake, Adrameleki na Shareza wakampiga kwa upanga; wakaikimbilia NCHI YA ARARATI. Na Esar-hadoni mwanawe akatawala mahali pake.”
Pia katika Kitabu cha Isaya na Yeremia, Ufalme wa Ararati umetajwa.
Isaya 37:38 “Ikawa alipokuwa akiabudu katika nyumba ya Nisroki, mungu wake, Adrameleki na Shareza, wanawe, wakampiga kwa upanga; wakakimbilia NCHI YA ARARATI; naye Esar-hadoni, mwanawe, akamiliki badala yake”.
Na
Yeremia 51:27 “Itwekeni bendera katika nchi, pigeni tarumbeta kati ya mataifa, yawekeni mataifa tayari juu yake; ziiteni juu yake FALME ZA ARARATI, na Mini, na Ashkenazi; agizeni jemadari juu yake; wapandisheni farasi, kama tunutu”.
Lakini swali ni je!.. Kuna kitu chochote cha kiungu katika hiyo milima sasa? Kiasi kwamba tukienda kutembea katika milima hiyo, tutaongeza chochote cha kiungu ndani yetu?
Jibu ni la!.
Milima hiyo haina chochote cha kiungu leo, kiasi kwamba labda tukienda kule kuna chochote tutafaidika nacho.
Lakini pako mahali ambapo tukienda leo basi tutamwona Mungu..na mahali penyewe Bwana Yesu alipataja katika mistari ifuatayo..
Yohana 4:20 “BABA ZETU WALIABUDU KATIKA MLIMA HUU, nanyi husema ya kwamba huko Yerusalemu ni mahali patupasapo kuabudia.
21 Yesu akamwambia, Mama, unisadiki, saa inakuja ambayo hamtamwabudu Baba katika mlima huu, wala kule Yerusalemu.
22 Ninyi mnaabudu msichokijua; sisi tunaabudu tukijuacho; kwa kuwa wokovu watoka kwa Wayahudi.
23 LAKINI SAA INAKUJA, NAYO SASA IPO, AMBAYO WAABUDUO HALISI WATAMWABUDU BABA KATIKA ROHO NA KWELI. KWA MAANA BABA AWATAFUTA WATU KAMA HAO WAMWABUDU
24 MUNGU NI ROHO, NAO WAMWABUDUO YEYE IMEWAPASA KUMWABUDU KATIKA ROHO NA KWELI”.
Umeona?
Ni lazima tumwabudu baba katika ROHO NA KWELI, na maana ya kumwabudu Bwana katika roho na kweli, sasa nini maana ya kumwabudu Baba katika roho na kweli? Fungua hapa >>Nini maana ya kumwabudu Mungu katika Roho na kweli?
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
JIHADHARI NA ROHO ZIDANGANYAZO.
Mlima Gerizimu na Ebali ni ipi, na umuhimu wao rohoni ni upi?
Mwandamo wa mwezi/Mwezi mpya Ni nini kibiblia?
Kisiwa cha Patmo kipo nchi gani?.
Jibu: Tusome,
Mathayo 16:16 “Simoni Petro akajibu akasema, WEWE NDIWE KRISTO, MWANA WA MUNGU ALIYE HAI.
17 Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni.
18 Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, NA JUU YA MWAMBA HUU NITALIJENGA KANISA LANGU; WALA MILANGO YA KUZIMU HAITALISHINDA ”
Kufuatia andiko hilo mwamba unaozungumziwa hapo ambao kanisa litajengwa juu yake sio Petro!!.. kanisa la Mungu halijawahi kujengwa juu ya mtu wala kujengwa na mtu.
Bali Mwamba uliokuwa unazungumziwa hapo ni huo ufunuo Petro alioupokea wa YESU kuwa NI KRISTO, MWANA WA MUNGU ALIYE HAI.
Juu ya ufunuo huo ndio kanisa lake litajengwa..Yesu Kristo ndio Msingi wa kanisa, YEYE NDIO MWAMBA IMARA ambao kanisa litajengwa juu yake..na si juu ya mtu mwingine. Ndio maana waumini wa kanisa la Mungu wanajulikana kama Wakristo, sio waPetro…Kwasababu msingi sio Petro bali ni Kristo.
Ili tulithibitishe hilo vizuri, tusome mistari ifuatayo.
1 Wakorintho 3:10 “Kwa kadiri ya neema ya Mungu niliyopewa, mimi, kama mkuu wa wajenzi mwenye hekima, naliuweka msingi, na mtu mwingine anajenga juu yake. Lakini kila mtu na aangalie jinsi anavyojenga juu yake.
11 Maana msingi mwingine hakuna mtu awezaye kuuweka, isipokuwa ni ule uliokwisha kuwekwa, YAANI YESU KRISTO”.
Umeona msingi huo ni nani??
Si mwingine zaidi ya BWANA YESU KRISTO (MKUU WA UZIMA!!). Na ndio maana utaona mitume wote walimhubiri Yesu, ikiwemo Petro mwenyewe..(Na wala Petro hajawahi kusema popote kwamba yeye ndiye Mwamba).
Zaidi sana katika waraka wake kwa kinywa chake mwenyewe aliandika na kusema na kushuhudia kwamba Yesu ndiye, Mwamba na tena ndiye Jiwe kuu la pembeni.
Tusome,
1 Petro 2:3-8 “ikiwa mmeonja ya kwamba Bwana ni mwenye fadhili.
4 Mmwendee yeye, JIWE LILILO HAI, lililokataliwa na wanadamu, bali kwa Mungu ni teule, lenye heshima.
5 Ninyi nanyi, kama mawe yaliyo hai, mmejengwa mwe nyumba ya Roho, ukuhani mtakatifu, mtoe dhabihu za roho, zinazokubaliwa na Mungu, kwa njia ya Yesu Kristo.
6 Kwa kuwa imeandikwa katika maandiko Tazama, naweka katika Sayuni jiwe kuu la pembeni, teule, lenye heshima, Na kila amwaminiye hatatahayarika.
7 Basi, heshima hii ni kwenu ninyi mnaoamini. Bali kwao wasioamini,
Jiwe walilolikataa waashi, Limekuwa jiwe kuu la pembeni.
8 Tena, Jiwe la kujikwaza mguu, na MWAMBA WA KUANGUSHA maana hujikwaza kwa neno lile, wasiliamini, nao waliwekwa kusudi wapate hayo”.
Huyo ni Petro, anayesema maneno hayo!..Sasa ingekuwa ndio ule mwamba bao kanisa litajengwa juu yake, si angejitaja wazi kabisa hapo kuwa yeye ndio huo mwamba!!!..lakini tunaona anaushuhudia mwamba mwingine ambao ni YESU!.
Zaidi sana tafsiri ya jina Petro sio Mwamba bali ni “jiwe”..tena “jiwe dogo, la kurusha”..
Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba Yesu ndio Mwamba, na si Petro, au kuhani yeyote au mwalimu yeyote, au mchungaji yeyote, au padri yeyote, au papa yeyote au kasisi yeyote au mtu mwingine yeyote.
Mtu anayechukua nafasi hiyo ya Kristo na kusema yeye ni mwamba basi huyo ni mpinga kristo.
Lakini swali ni je!..umemwamini Yesu, na kutubu na kubatizwa na kupokea Roho Mtakatifu?.
Kama bado ni vizuri ukafanya hivyo sasa, kabla nyakati za hatari hazijafika.
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Ngome ni nini? Kwanini Mungu anafananishwa na ngome?
Gumegume ni nini? (Isaya 50:7)
Ni kweli hakuna mtu aliyewahi kuuona uso wa Mungu Zaidi ya Bwana Yesu?
Mapooza ni kitu/vitu/mambo yote yasiyoweza kuzalisha chochote, au kufikia kilele chake cha kutoa matunda kamili.
Neno mapooza limetokana na neno kupooza. Kwamfano tunaposema mtu amepooza mkono, maana yake ni kwamba anao mkono lakini hana uwezo wa kufanya kazi ya mkono, yaana unakuwa kama vile umekufa tu lakini upo.
Nazi zote zinazotoka katika mti wa mnazi, si zote zinafaa kama kiungo, bali nyingine ni koroma, Sasa hizo koroma ndio mapooza yenyewe, japo kwa nje zinaonekana ni nazi.
Neno hilo utalisoma katika vifungu hivi kwenye biblia;
Ufunuo 6:12 “Nami nikaona, alipoifungua muhuri ya sita, palikuwa na tetemeko kuu la nchi; jua likawa jeusi kama gunia la singa, mwezi wote ukawa kama damu,
13 na nyota zikaanguka juu ya nchi kama vile mtini upukutishavyo mapooza yake, utikiswapo na upepo mwingi.
6 Mbingu zikaondolewa kama ukurasa ulivyokunjwa, na kila mlima na kisiwa kikahamishwa kutoka mahali pake”.
Katika habari hii ni Mungu anaifananisha ile siku ya Bwana, na kama mtini upukutishavyo mapooza yake. Yaani kama vile tunavyofahamu miti ya matunda, huwa si matunda yote yanakomaa wakati wa mavuno, bali kuna mengine huwa yanaendelea kubaki katika miti, hadi wakati wa msimu wa upepo mkali wa upukutishaji unapovuma ndipo yanapoondoka hayo yaliyosalia (ambayo ndio mapooza)..Hivyo siku ya Bwana ndivyo itakavyokuwa wakati ambapo Mungu anaiondoa mbingu, hakuna nyota hata moja itakayobakia juu.
Utalisoma pia, katika ile Habari ya Elisha..
2Wafalme 2:19 “Watu wa mjini wakamwambia Elisha, Angalia, twakusihi, mahali pa mji huu ni pazuri, kama bwana wangu aonavyo; lakini maji yake hayafai, na nchi huzaa mapooza.
20 Akasema, Nileteeni chombo kipya, mtie chumvi ndani yake. Wakamletea.
21 Akatoka akaenda mpaka chemchemi ya maji, akatupa ile chumvi humo ndani, akasema, Bwana asema hivi, Nimeyaponya maji haya; hakutatoka huko tena kufa wala kuzaa mapooza.
22 Hivyo yale maji yakapona hata leo, sawasawa na neno la Elisha alilolinena.
Maana yake ni kwamba yale maji waliyokuwa wanayanywa au wanayatumia kwa mimea yalikuwa si mazuri yanazaa mapooza, yaani vitu vyake havistawi au kuleta matunda, mimba za wanawake zilikuwa zinatoka, mboga mboga zilizokuwa zinanyeshewa zilikuwa hazikuwi, ipasavyo, wala miti haikuivisha matunda yake,
Hivyo Elisha alipoagizwa na Mungu kutia chumvi katika yale maji, wakati ule ule yakaponywa. Hivyo kukawa hakuzaliwi mapooza tena katika ile nchi.
Utalisoma pia Neno hilo katika Ayubu 15:32.
Jibu ni ndio, kwamfano, wewe ni mwanamke halafu, kila unaposhika mimba, kabla hujajifungua inatoka, huwenda kuna mapooza nyuma yake.
Au unafanya shughuli Fulani, ambayo kwa muda mrefu sana, haijakuletea mafanikio yoyote, hayo pia ni mapooza,
Au unalihangaikia jambo lolote lile jema, lakini kwa muda mrefu, unaona kama kuna dalili njema zinaonekana lakini mwishoni linakufa. Ujue pia mapooza yapo hapo.
Una karama ya muda mrefu lakini haina matunda yoyote katika ufalme wa Mungu,
Je suluhisho ni nini?
Yapo mambo mawili makuu ya kuyafanya.. Hususani hili la kwanza, ukilipuuzia hili ukakimbilia hilo la pili, ufahamu kuwa hali yako haitaweza kuwa na mabadiliko.
Kama vile Elisha, alivyoagizwa akatie chumvi ndani ya yale maji yaliyozaa mapooza, vivyo hivyo na wewe, huna budi kukubali kuwatiwa chumvi ili mapooza yaondoke ndani yako..
Hapa hatuzungumzii chumvi za upako, tunazungumzia Neno la Mungu. Mungu kumuagiza Elisha atie chumvi sio kwamba alikuwa anatuonyesha kuwa kuna upako ndani ya chumvi hapana, bali alikuwa anatoa taswira ya kufahamu chumvi ni nini katika ulimwengu wa roho, na sisi tunatiwaje chumvi..
Bwana Yesu alisema..
Marko 9:47 “Na jicho lako likikukosesha, ling’oe, ulitupe; ni afadhali kuingia katika ufalme wa Mungu, una chongo, kuliko kuwa na macho mawili, na kutupwa katika jehanum;
48 ambamo humo funza wao hafi, wala moto hauzimiki.
49 Kwa sababu kila mtu atatiwa chumvi kwa moto”.
Tafakari vema, jiulize, kwanini baada ya kutoa maagizo makali kama hayo, mwishoni akamalizia kwa kusema.. kila mtu atatiwa chumvi kwa moto..
Maana yake ni kuwa ili utiwe chumvi, huwezi epuka moto.. ili Maisha yako yaponywe, huwezi epuka kukata baadhi ya viungo vyako vinavyokukosea..
Viungo hivi ndio kama vipi..
Hivyo hiyo ndio njia ya kwanza yenye matokeo.. Kataa kwa nguvu zote, kuacha watu/vitu/mambo ambayo yanakufanya usiwe safi mbele za Mungu.
Kwa lugha nyepesi ni kwamba unapaswa uokoke kwa kumaanisha kabisa kumfuata Yesu Kristo. Hakikisha umejitwika msalaba wako. Hii ndio njia kuu ya kuondoa mapooza yoyote ndani yako.
Hivyo nitaomba Pamoja na wewe.. Kisha kwa Imani Bwana atakufungua, wewe ambaye, tayari umeshampokea Yesu na kumfuata, au wewe ambaye unaahidi tangu sasa utafanya hivyo..
Hapo ulipo elekeza mawazo yako palipo na mapooza..kisha sema sala hii kwa sauti na kwa Imani, na kuanzia leo utaona mabadiliko yanakuja katika eneo hilo hilo unaloliombea..
PIGA MAGOTI, kisha sema maneno haya kwa sauti.
Mungu wangu, hakika nifahamu kuwa pasipo wewe mimi siwezi kuzalisha chochote, nami kama mwanao nakuja mbele zako, nikiomba msamaha unisamehe dhambi zangu zote, nilizokukosea, katika Maisha yako tangu nazaliwa. Nikakiri Yesu kuwa wewe ni Bwana na mwokozi na kiongozi wa Maisha yangu, wala Zaidi yako hakuna mwingine awezaye kuokoa. Tangu sasa naomba unifanye kiumbe kipya, na jina langu uliandike katika kitabu cha uzima, unipe uwezo wa kufanyika mwana wako kweli kweli, nami nimekubali tangu sasa kutiwa chumvi kwa maneno yako Bwana Yesu. Nakubali kuacha mambo/watu/vitu vyote viovu visivyokupendeza wewe bila kujali vitanigharimu kiasi gani.Najua wewe ni mwaminifu na utanisaidia, sawasawa na Neno lako ..Naomba Bwana unione tena katika hii shida yangu na uniponye (Taja eneo lako la mapooza). Asante Bwana Yesu kwa kuniponya.Naombi nikimaini. Amen.
Basi kama umeifuatisha hiyo sala ya Imani.. Fahamu kuwa Bwana ameshaanza kufanya muujiza katika hilo eneo lako la maishaa..Hivyo zingatia sasa kudhihirisha Imani yako kwa matendo kwa kujiepusha na mambo yote maovu yasiyompendeza Mungu, tangu leo, ishi maisha ya kujikana nafsi, mfuate Bwana Yesu. Hizi ni siku za mwisho, zidisha ukaribu wako kwa Bwana.
Bwana akubariki.
Amen.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
UKIOKOKA,HIZI FIKRA ZIKIJA NDANI YAKO, ZIKATAE.
Mti wa MLOZI alioonyeshwa nabii Yeremia 1:12 tafsiri yake ni nini?
Sadaka ya kinywaji ilikuwaje? Na inawakilisha nini?
USIWE MSIKIAJI TU! BALI MTENDAJI.
Hazina za gizani ni zipi? (Isaya 45:3).
AKAJIFUNGA VAZI LAKE, AKAJITUPA BAHARINI.
Nini maana ya “wazimu” katika biblia?