Title 2023

Jinsi ya kuandaa Somo la kufundisha

Jinsi ya kuandaa mahubiri ya kufundisha kanisani au kwenye semina.

Jinsi ya kuandaa mahubiri ya kufundisha kanisani au katika ibada. Zifuatazo ni dondoo chache zitakazoweza kukusaidia katika kuandaa Somo ambalo litakuwa na uvuvio wa Roho Mtakatifu.

1. Tafuta sehemu ya utulivu.

Hii ni hatua ya kwanza kabisa: Tafuta eneo lisilo na kelele, wala usumbufu, hakikisha husumbuliwi na mtu au simu. Hiyo inaweza kuwa katika chumba cha utulivu au mahali ambao hauwezi kusumbuliwa, Huo ni mlango wa kwanza unaouvuta uwepo wa Mungu karibu nawe, kwasababu maandiko yanasema Mungu wetu si Mungu wa machafuko (1Wakorintho 14:33) na pia ni Mungu anayezungumza katika mazingira tulivu.

1Wafalme 19:12 “na baada ya tetemeko la nchi kukawa na moto; lakini Bwana hakuwamo katika moto ule; na baada ya moto sauti ndogo, ya utulivu”.

Hivyo kabla ya kuanza kufikiri kuandaa somo au hubiri, jitenge na mazingira yote yatakayokuondolea utulivu, kwasababu ukikaa katika hayo mazingira hutamsikia Mungu, Hivyo zima simu kwa muda na pia kaa peke yako kwenye utulivu.

2. Kuwa na Kalamu na Karatasi.

Hii ni hatua ya pili: Andaa kalamu na karatasi kwasababu kabla ya kwenda kuwafundisha wengine, Roho Mtakatifu atakufundisha wewe kwanza.

Warumi 2:21  “basi wewe umfundishaye mwingine, je! Hujifundishi mwenyewe? Wewe uhubiriye kwamba mtu asiibe, waiba mwenyewe”

Kwahiyo wewe ni mwanafunzi wa kwanza wa Roho Mtakatifu kabla ya kwenda kuwafundisha wengine, na Mwanafunzi bora ni sharti awe na kalamu na karatasi kwa lengo la kuyarekodi yale anayojifunza. 

Usipokuwa na sehemu ya kurekodi yale utakayoenda kujifunza itakuwa ni ngumu hata kuyashika..

3. Fungua kwa Maombi.

Omba utakaso kwaajili ya nafsi yako, Omba uwepo wa Mungu ushuke mahali hapo, omba utakaso wa eneo ulilopo, omba roho ya ufunuo ishuke juu yako, kemea nguvu za giza na  zinazoshindana na azimio lako hilo (Tumia muda kidogo kuomba kwa kumaanisha).

4. Anza kusoma biblia na kutafakari

Baada ya maombi, anza kusoma biblia huku ukiruhusu akili yako itafakari. Wengi wakifika hii hatua wanafungua tu biblia na kutafuta mistari wanayoifahamu au watakayokutana nayo kwanza, pasipo kuruhusu tafakari katika fahamu zao.

Siri moja ya Roho Mtakatifu ni kwamba anazungumza na sisi pale tunapotafakari na si pale tunapoziba tafakari zetu. Unapokuwa katika kutafakari ndipo Roho Mtakatifu naye anaungana na tafakari zako pasipo kujua na ghafla unajikuta unafunguka akili na kujikuta unapokea vitu vipya, ambavyo ulikuwa huvijui, vitu hivyo vipya ambavyo ulikuwa huvijui vinavyokubaliana na Neno la Mungu ndio sauti ya Roho Mtakatifu, hivyo andiko hivyo ulivyovipokea kwasababu ndio vitakuwa sehemu ya somo lako ambalo Roho Mtakatifu anataka ujifunze wewe kwanza kisha ukawafundishe na wengine.

5. Omba tena

Hii ni hatua ya mwisho, baada ya kusoma na kutafakari kwa muda mrefu, na kupokea Funuo nyingi. Omba maombi ya mwisho ya kushukuru, kisha funga daftari lako.

Darasa lijalo tutajifunza jinsi ya kusimama na kufundisha kile ulichofundishwa na Roho Mtakatifu. Kwani ni muhimu pia kujua jinsi ya kufundisha ili usije ukajikuta unamzimisha Roho. (Kanuni ya kufundisha kwa matokeo yaliyokusudiwa ni rahisi sana, usikose darasa lijalo).

Maran atha

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

JE! UPO KATIKA MAJI YA UTULIVU?

NIFANYE NINI ILI MUNGU AYAJIBU MAOMBI YANGU?

Wanikolai ni watu gani? Katika biblia?

JINSI YA KUSOMA BIBLIA.

Guruguru na Goromoe ni wanyama gani? (Walawi 11:30)

Rudi nyumbani

Print this post

Mstari mfupi kwenye biblia

Mstari mfupi zaidi kwenye biblia ni upi? na umebeba ujumbe gani?

Mistari inatofautiana urefu kulingana na lugha na lugha.. Mstari unaoonekana mfupi katika lugha ya moja unapotafsiriwa katika lugha nyingine unaweza kuwa mrefu kuliko mistari mingine.

Kwamfano katika lugha ya kiingereza, mstari ulio mfupi kuliko yote unapatikana katika kitabu cha Yohana 11:35 unaosema kwa kiingereza “Jesus wept” Lakini tukiurudisha kwenye lugha Kiswahili unasomeka kama “Yesu akalia machozi”, Hivyo kuufanya mstari huo kutokuwa mfupi kuliko mingine katika lugha yetu.

Sasa mstari mfupi kuliko yote kwenye lugha ya Kiswahili ni upi? (Katika agano jipya).

Ni mstari unaopatikana katika kitabu cha 1Wathesalonike 5:20 unaosema “msitweze unabii”.

Huo ndio mstari mfupi kuliko yote, katika biblia ya Kiswahili, ( Agano jipya) Na ndio ujumbe mfupi kuliko yote aliouchagua Roho Mtakatifu kwa watu wanaozungumza lugha ya Kiswahili, kwamba “tusitweze unabii”, au kwa lugha rahisi “Tusidharau wala kupuuzia unabii”.

Na unabii unaozungumziwa hapo kwamba tusiudharau/ tusiutweze sio nabii zinazosikika sasahivi za wanaojiita manabii au wanaojulikana kama manabii, hapana! Bali Nabii zilizoandikwa kwenye biblia, mfano wa Nabii hizo ni zile Bwana Yesu alizozitaja katika Mathayo 24, zinazohusiana na kurudi kwake kwamba Nyakati kutatokea vita, njaa, manabii wa uongo, Tauni, matetemeko, upendo wa wengi kupoa n.k Hizo ndio nabii ambazo hatupaswi kuzipuuzia, kwa maana ni kweli zitatimia.

Kuzidi  kufahamu kwa kina Zaidi maana ya kutotweza unabii fungua hapa >>Msitweze unabii

Je umempokea Yesu?.. Je unajua kwamba kizazi tunachoishi ni kizazi ambacho kina uwezekano wa kushuhudia ujio wa pili wa Yesu dhahiri??

Maran atha!.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya ELOHIMU?

TABIA YA WAZI INAYOWATOFAUTISHA MANABII WA UONGO NA WALE WA UKWELI.

Je kunena kwa Lugha mpya kukoje?

NI YESU YUPI UMEMPOKEA?, NI ROHO IPI UMEIPOKEA? NA INJILI IPI UMEIPOKEA?

USIPOTEZWE NA MANENO YA MANABII WA UONGO.

FREEMASONS NI NINI? NA MTU ATATOKAJE HUKO?

Rudi nyumbani

Print this post

Miimo ni nini na kizingiti ni nini?

Katika biblia Miimo ni nini na kizingiti ni nini?

Jibu: Miimo ni nguzo mbili za mlango zinazosimama upande wa kuume na wa kushoto mwa mlango.

Mfano wa hiyo ni ile Samsoni aliyoing’oa ya geti la wafilisti

Waamuzi 16:3 “Basi Samsoni akalala hata usiku wa manane, akaondoka katikati ya usiku, akaishika milango ya lango la mji, NA MIIMO YAKE MIWILI, akaing’oa pamoja na komeo lake, akajitwika mabegani, akavichukua hata kilele cha mlima ule unaokabili Hebroni”.

Unaweza kusoma zaidi kuhusu Miimo katika mistari ifuatayo Kumbukumbu 6:9, 1Wafalme 6:33, na Isaya 57:8.

Na kizingiti ni nguzo moja ya mlango inayolala ambayo inakuwa upande wa juu wa mlango (wakati mwingine pia inawekwa upande wa chini wa mlango) Kwamfano utaona wakati wana wa Israeli wanatolewa Misri, waliambiwa wapake ile damu ya mwanakondoo kwenye vizingiti vya nyumba na  kwenye miimo yake, ili yule Malaika alitumwa kuharibu asiingie na kuua wazaliwa wa kwanza wa nyumba hizo.

Kutoka 12:7 “Nao watatwaa baadhi ya damu yake na kuitia katika miimo miwili na KATIKA KIZINGITI cha juu, katika zile nyumba watakazomla”.

Miimo na vizingiti vinaweza kuwa vya malighafi yoyote, aidha mbao, chuma, udongo au shaba.

Unaweza kusoma zaidi juu ya kizingiti/vizingiti katika mistari ifuatayo Ezekieli 10:4, 1Wafalme 6:31, na 1Wafalme 14:17.

Lakini Miimo na vizingiti vinafunua nini kiroho?

Maandiko yanasema Miili yetu ni Nyumba (Hekalu la Roho Mtakatifu) 1Wakorintho 6:19 na 1Wakorintho 3:16 na Kama ni Nyumba ya Roho Mtakatifu basi ni lazima ina Mlango, na kama ina mlango ni lazima ina miimo na vizingiti.

Sasa Mlango wa Hekalu la Roho Mtakatifu ni mioyo yetu..

Ufunuo 3:20 “Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami.”

Na kama mioyo yetu ni Malango basi ni lazima ina Miimo yake na Vizingiti vyake.. na hivyo si vingine zaidi ya Macho yetu na Masikio masikio yetu. Masikio ni vizingiti na macho ni miimo.

Mioyo yetu inapokea vile tunavyovisikia na na macho yetu vile tunavayoviona. Hivyo kama macho yetu yametakaswa kwa damu ya Yesu Kristo katika ulimwengu wa roho na masikio yetu yametakaswa kwa damu ya Yesu Kristo basi hapo ni sawa na ile nyumba iliyopakwa damu ya mwana kondoo katika miimo ya milango yake na vizingiti vyake nyakati za Israeli kutoka Misri, Na hivyo uharibifu utakapofika hautatukuta.

 Lakini kinyume chake kama Macho yetu ni ya uasi na masikio yetu ni ya ukaidi basi hata mioyo yetu itakuwa michafu na hivyo tutalinajisi Hekalu zima la Mungu ambalo ndio miili yetu na hivyo kujiweka katika hatari ya kuharibiwa sawasawa na maandiko yanavyosema.

1Wakorintho 3:17 “Kama mtu akiliharibu hekalu la Mungu, Mungu atamharibu mtu huyo. Kwa maana hekalu la Mungu ni takatifu, ambalo ndilo ninyi”

Je umeokoka?, je umetakaswa kwa damu ya Yesu?.. Kama bado unasubiri nini?, mpokee Yesu leo kwa kutubu na kubatizwa na kujazwa Roho Mtakatifu.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Tofauti ya kazi ya Damu ya Yesu na Jina la Yesu ni ipi?

MWANAMKE, USIFUNGUE MLANGO WA MAPEPO KUKUINGIA!.

Tofauti ya kazi ya Damu ya Yesu na Jina la Yesu ni ipi?

Je! Shetani anao uwezo wa kuumba, kama Mungu?

Bawa la mbuni hufurahi; Lakini mabawa yake na manyoya yake, je! Yana huruma? 

Rudi nyumbani

Print this post

Biblia inamaana gani inaposema tutoapo unabii tutoe kwa kadiri ya imani?

SWALI: Biblia inamaana gani inaposema tutoapo unabii tutoe kwa kadiri ya imani?(Warumi 12:6)


JIBU: Neno hilo utalipata katika vifungu hivi;

Warumi 12:5  Vivyo hivyo na sisi tulio wengi tu mwili mmoja katika Kristo, na viungo, kila mmoja kwa mwenzake.

6  Basi kwa kuwa tuna karama zilizo mbalimbali, kwa kadiri ya neema mliyopewa; ikiwa unabii, tutoe unabii kwa kadiri ya imani;

7  ikiwa huduma, tuwemo katika huduma yetu; mwenye kufundisha, katika kufundisha kwake;

8  mwenye kuonya, katika kuonya kwake; mwenye kukirimu, kwa moyo mweupe; mwenye kusimamia kwa bidii mwenye kurehemu, kwa furaha.

Andiko hili linatuonyesha kuwa kila mmoja wetu amepewa KIPIMO cha neema, na hicho kipimo, kwa lugha nyingine ndio kinaitwa ‘Imani’ kama ilivyotumika hapo. Maana yake ni kuwa ikiwa ni nabii, basi kuna tofauti ya viwango vya kinabii, kwamfano wapo wengine wanapewa taarifa za watu tu, wapo wengine wanapewa za nyakati zijazo, wapo wengine za mataifa, wapo wengine wanapewa taarifa dhahiri kabisa za moja kwa moja, na wapo wengine kwa njia za mafumbo n.k.. Vyote hivi vinajulikana kama ndio vipimo vya imani.

Lakini sasa ikiwa mtu hajajaliwa kuona jambo Fulani, kisha akalazimishia alione,ili tu aonekane yeye ni mwonaji wa mambo yote, maana yake mtu huyo ni kuwa amevuka kiwango cha imani alichopimiwa na Mungu.

Na hivyo ataishia kutoa taarifa za uongo ambazo Mungu hajazisema. Kwamfano mtu ataona maono, kisha asiyaelewe, hata baada ya kuomba hajayaelewa, lakini kwasababu hataki kushirikisha wenye karama za Hekima na Maarifa na upambanuzi, atataka yeye ndio atafsiri alichoonyeshwa, hivyo anatumia akili zake, na matokeo yake inakuwa ni upotoshaji badala ya ujengaji.

Vivyo hivyo na katika karama nyingine. Utakutana na mtu sio mwalimu, hajajaliwa karama hiyo, lakini kwasababu na yeye anataka kujionyesha ni mjuaji anafahamu yote, ataanza kufundisha, na hatimaye kuwapotosha watu kwa mafundisho yake dhaifu.

Mitume japokuwa walijaliwa wingi wa karama na vipawa vya Roho lakini hawakuwa hivyo. Paulo anasema..

2Wakorintho 10:12  “Kwa kuwa hatuthubutu kujihesabu pamoja na baadhi yao wanaojisifu wenyewe, wala kujilinganisha nao; bali wao wenyewe wakijipima nafsi zao na nafsi zao, na wakijilinganisha nafsi zao na nafsi zao, hawana akili.

13  Lakini sisi hatutajisifu zaidi ya kadiri yetu; bali kwa kadiri ya kipimo tulichopimiwa na Mungu, yaani, kadiri ya kufika hata kwenu.

14  Maana hatujitanui nafsi zetu kupita kadiri yetu, kana kwamba hatuwafikii ninyi; kwa sababu tulitangulia kufika mpaka kwenu katika injili ya Kristo;

Palepale ulipofikishwa na Bwana dumu hapo hapo, ikiwa Bwana atakuongezea neema basi itathibitika, lakini usijiongezee chochote, zaidi ya kile ulichopimiwa. Na hatari sana

Waefeso 4:7  Lakini kila mmoja wetu alipewa neema kwa kadiri ya kipimo cha kipawa chake Kristo

Bwana akubariki.

 Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Karama ya pili inayozungumziwa katika 2Wakorintho 1:15 ndio ipi?

UPO UMUHIMU MKUBWA WA KUMTOLEA BWANA!

USIJISIFIE KARAMA KWA UONGO.

Je! Umeona asali? Kula kadiri ya kukutosha;

KUWA WEWE.

Kwanini Daudi achukue mawe matano, na malaini na sio vinginevyo?

Rudi nyumbani

Print this post

Maana yake nini, Mwe na hofu wala msitende dhambi? (Zaburi 4:4)

Swali: Ni hofu gani inazungumziwa katika Zaburi 4:4?

Jibu: Turejee,

Zaburi 4:4 “Mwe na hofu wala msitende dhambi, Tafakarini vitandani mwenu na kutulia,

5 Toeni dhabihu za haki, Na kumtumaini Bwana”.

Hapa maandiko yanasema “Mwe na hofu WALA msitende dhambi” haisemi “Mwe na hofu ILA msitende dhambi” Kana kwamba hiyo hofu ikizidi sana italeta madhara, hapana bali kinyume chake, inapaswa iwepo nyingi.

Sasa swali ni hofu gani hiyo inayozungumziwa hapo?

Hofu inayozungumziwa hapo si hofu ya kumwogopa mwanadamu, au kumhofu shetani, La! Bali ni hofu ya kumwogopa Mungu (Hofu ya Mungu), ambayo Daudi aliitaja pia katika Zaburi 36:1

Zaburi 36:1 “Kuasi kwake yule mwovu hunena moyoni mwake, HAKUNA HOFU YA MUNGU mbele ya macho yake”

Hofu ya Mungu ni ile hali ya mtu kuogopa kuyaasi maneno ya Mungu, hivyo mtu huyo anakuwa anajiweka katika hali ya kujitenga na dhambi siku zote za maisha yake yote. Lakini mtu asiye na hofu ya Mungu anaweza kufanya anayojisikia pasipo kujali kuwa anayoyafanya yanamchukiza Mungu.

Mfano wa watu ambao biblia imewataja hawakuwa na hofu ya Mungu, ni watu wa nchi ya Gerari, ile Ibrahimu aliyoikimbilia.

Mwanzo 20:9 “Kisha Abimeleki akamwita Ibrahimu, akamwambia, Umetutenda nini? Nimekukosa nini, hata ukaleta juu yangu na juu ya ufalme wangu dhambi kuu? Umenitenda matendo yasiyotendeka.

 10 Abimeleki akamwambia Ibrahimu, Umeona nini hata ukatenda jambo hili?

 11 Ibrahimu akasema, Kwa sababu naliona, Yakini HAPANA HOFU YA MUNGU MAHALI HAPA, nao wataniua kwa ajili ya mke wangu”

Na dunia tunayoishi sasa (mimi na wewe) ni Zaidi ya miji ya Gerari, ni Zaidi ya Sodoma na Gomora, Hofu ya Mungu haipo tena. Na biblia inaonya “tuwe na hofu”, na wala tusitende dhambi.

Je! hofu ya Mungu ipo ndani yako?.. kama hofu ya Mungu ipo ndani yako utaogopa kutenda mabaya, hivyo huwezi kuendelea na ulevi unaoufanya, huwezi kuendelea na rushwa unazokula, huwezi kuendelea na uasherani na uzinzi, huwezi kuendelea la mauaji na kutokusamehe.. ni lazima utajitenga na hayo yote, kwasababu hofu ya Mungu ipo ndani yako.

Bwana atusaidie.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

SIKU YA HOFU YANGU NITAKUTUMAINI WEWE.

BASI NIKAOGOPA, NIKAENDA NIKAIFICHA TALANTA YAKO.

Waoga ambao hawataurithi uzima wa milele ni watu wa namna gani?(Ufunuo 21:8).

YESU KATIKA USINGIZI WAKE.

MWIMBIE BWANA ZABURI KATIKA NYAKATI ZA FURAHA.

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya Mathayo 23:15 inaposema namfanya kuwa mwana wa jehanum mara mbili zaidi kuliko ninyi wenyewe.

SWALI: mnamfanya kuwa mwana wa jehanum mara mbili zaidi kuliko ninyi wenyewe.(Mathayo 23:15)

Mathayo 23:15

Ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnazunguka katika bahari na nchi kavu ili kumfanya mtu mmoja kuwa mwongofu; na akiisha kufanyika, mnamfanya kuwa mwana wa jehanum mara mbili zaidi kuliko ninyi wenyewe.


JIBU: Bwana Yesu anaanza Kwa kueleza bidii ya mafarisayo, kwamba ni hodari wa kuieneza dini zao kiasi cha kufanya umisheni wa kuzunguka hata sehemu za mbali nje ya taifa lao ili kuwafundisha watu mapokeo Yao. Lakini Bwana hawakemei Kwa bidii Yao hiyo ya kuzunguka huku na huko, Bali anawakemea Kwa Imani yanayoisambaza Kwa watu, ambayo ni potofu.

Imani ya kinafki, inayoacha kufundisha mambo ya adili kama (Imani katika Mungu, Upendo, kuja Kwa mwokozi duniani), Bali katika zaka na michango kama ndio tiketi ya kukubaliwa na Mungu (Mathayo 23:23)..

Na matokeo yake ni kwamba wale wanaogeuzwa Huwa wanakuwa na kiu ya dhati ya kusimama. Hivyo Kwa kuwa wanafundishwa uongo, basi wanafanyika kuwa Wana wa udanganyifu mara mbili zaidi ya Hao wenyewe.

Ndio hapo utamwona mtu kama Paulo, alipogeuzwa akawa chini ya elimu ya mafarisayo, lakini matokeo yake yalizidi hata wakufunzi wake wakina Gamalieli, alianza kuwauwa na kuwaburuta wakristo, na ndio ulivyokuwa Kwa watoto wao wote..walikuwa wabaya zaidi Yao, Wana wa jehanamu mara mbili zaidi ya wao.

Hata Leo angalia matokeo ya dini, madhehebu na Imani za uongo. Utagundua kuwa wale wafuasi wao ndio wanaokuwa wabaya zaidi ya wale viongozi, 

Na ndio maana akawaambia hukumu Yao itakuwa kubwa zaidi ya wengine (Mathayo 23:14)

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya “wanawake saba watamshika mtu mume mmoja”

NINI KINATOKEA BAADA YA KIFO?

Kuzimu kuna nini?

NI NANI ATAKAYEWAPA ILIYO YENU WENYEWE?

Jehanamu ni nini?

MJUE SANA YESU KRISTO.

FAHAMU MAISHA YA YESU KABLA YA HUDUMA.

Rudi nyumbani

Print this post

KAMA MKRISTO NI LAZIMA UWE NA DESTURI HII.

Je biblia inatufundisha wakristo kuwa na desturi?.

Jibu ni Ndio!, Biblia inatufundisha kuwa na desturi, ikiwa na maana kuwa desturi ina nyongeza kubwa sana katika Imani ya mkristo.

Sasa desturi ni nini?

Desturi ni kitu chochote mtu anachokifanya kwa kurudia rudia.(Ni Kanuni ya daima ya mtu)

Sasa si kila desturi ni nzuri lakini zipo chache zilizo nzuri, na leo tutaenda kutazama moja ambayo kila mkristo lazima awe nayo.

  1. KUKUSANYIKA

Hii ni desturi ya kwanza na ya msingi  tunayopaswa kuwa nayo, ambayo biblia imeihakiki!

Kukusanyika katika ibada, semina, na mikutano ni jambo ambalo linapaswa liwe desturi ya kila mkristo (maana yake mtu akilala akiamka anapaswa ajue kuwa kukusanyika ni sehemu ya maisha yake) na si jambo la kuamua leo kukusanyika na kesho kutokukusanyika. Biblia inatufundisha kuwa ni lazima liwe desturi kwetu,…sasa utauliza hilo tunalisoma wapi katika biblia..

Waebrania 10:25 “WALA TUSIACHE KUKUSANYIKA PAMOJA, kama ilivyo DESTURI YA WENGINE; bali tuonyane; na kuzidi kufanya hivyo, kwa kadiri mwonavyo siku ile kuwa inakaribia”.

Umeona?

Kumbe kukusanyika ilikuwa ni desturi ya kundi Fulani la watu wa Mungu, na hapa biblia inatufundisha hayo hayo, kwamba na sisi tusiache kukusanyika KAMA ILIVYO DESTURI YA WENGINE. Maana yake inapaswa iwe desturi yetu na sisi, liwe jambo endelevu.

Kukusanyika ibadani hakupaswi kuwa tendo la leo kuamua na kesho kutoamua, bali linapaswa liwe desturi, iwe unajisikia au hujisikii, kukusanyika ni lazima iwe desturi yako, shetani amewafumba watu macho wasione kama kukusanyika ni desturi badala yake waone kama ni tendo kujisikia au kutojisikia, na hivyo kuwanyonyea Baraka zao!

Hivyo atakachokifanya ni kuwatengenezea udhuru  na vijisababu kwenye vichwa vyao ili awawafanye wasikusanyike na wengine.

Zifuatazo ni sababu kuu nne (4) za kuzikataa na kuzikimbia ambazo zitaharibu desturi yako njema ya kukusanyika na wengine.. kwasababu zinatoka kwa shetani.

1.Nimechoka:

Hii ni sababu ya kwanza ya kuikataa kwasababu hata siku nyingine za wiki unakuwa umechoka lakini huachi kwenda kwenye majukumu yako. Kwahiyo kama ilivyo desturi yako kwenda kazini, basi na kwenda kanisani kufanye kuwa desturi yako.

2.Naumwa:

Hii ni sababu ya pili yenye nguvu inayotoka kwa shetani, hata kama unasikia kuumwa kiasi gani usiache kukusanyika ibadani, kwasababu huko huendi kuongeza ugonjwa bali kuuondoa, kwasababu ugonjwa uliopata umetoka kwa shetani na kanisani shetani hayupo!.

Kama utakuwa na uwezo wa kuamka na kwenda hospitali pamoja na kwamba ni mgonjwa, kwanini usiamke na kwenda kanisani mahali penye uponyaji wa kiungu?

3.Mvua:

Hii ni sababu ya tatu ya shetani, ambayo inaharibu desturi ya wengi ya kwenda ibadani. Mvua isikuzuie kwenda ibadani.. bali nunua mwavuli na makoti ya mvua, na dhamiria kuwa iwe jua au mvua ni lazima ufike ibadani, kama mvua haiwezi kukuzuia kwenda kutafuta riziki za kimwili kwanini ikuzuie kwenda kutafuta riziki za kiroho?

4.Dharura

Dharura ni kitu chochote kinachonyanyuka wakati wa wewe kwenda ibadani, na hizo zinaweza kuwa ni za kikazi, familia, na nyinginezo..  Utakuta mtu anapigiwa simu na kuombwa ahudhurie mahali Fulani, na pasipo aibu ya uso anakubali na ilihali anajua kabisa siku hiyo ni maalumu kwa Mungu wake kukusanyika na wengine, lakini mtu huyo huyo akipokea simu siku za kazi yupo radhi kukataa kuvunjiwa ratiba zake za kazini na kuiheshimu kazi yake, lakini Nyumbani kwa Mungu kwake si kitu, Ukatae huo udhuru utaharibu desturi yako iliyo njema.

Na zipo sababu nyingine nyingi, hizi ni chacche tu, lakini katika hizo zote kataa visababu lakini jenga Desturi.. Huenda Desturi yako leo imeharibiwa na shetani, lakini Bwana Yupo kukusaidia ndio maana unayasikia haya leo.

Unachopaswa kufanya kuanzia leo ni kuomba rehema na kisha kutendea kazi hiki unachokisikia kuanzia leo, weka ratiba ambayo haibadiliki. Kwasababu desturi ya kwenda kanisani imehakikiwa na Roho Mtakatifu kuwa ni desturi njema. Hatuhitaji kuongozwa na Roho Mtakatifu au kupokea maono ya kwenda kanisani au la! Biblia tayari imeshatuelekeza kuwa inapaswa iwe desturi yetu.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Je ni kweli ilikuwa desturi ya Bwana kuishika sabato?(Luka 4:16)

TUSIIFUATISHE KAWAIDA YA ULIMWENGU HUU.

EPUKA KUCHELEWA IBADA.

KATAA KUWA EUTIKO, WA KUSINZIA IBADANI.

Uishi kwa furaha pamoja na mke umpendaye, siku zote

Rudi nyumbani

Print this post

Kwanini Daudi achukue mawe matano, na malaini na sio vinginevyo?

SWALI: Naomba kufahamu maana ya mawe matano ya kombeo na jiwe la kwanza maana yake nini na la pili hata la tano, na kwa nini mawe laini asingeokota jiwe ni jiwe tu?


JIBU: Daudi alipokutana na Goloathi maandiko yanatuambia akashuka katika kijito Cha maji akayaokota mawe matano malaini, kama silaha yake ya kumwangusha Goliathi.

1 Samweli 17:40

[40]Akaichukua fimbo yake mkononi, akajichagulia mawe laini matano katika kijito cha maji, akayatia katika mfuko wa kichungaji aliokuwa nao, maana ni mkoba wake, na kombeo lake alikuwa nalo mkononi mwake, akamkaribia yule Mfilisti.

Lakini Swali linakuja, Kwanini yawe matano, na je yanafunua Nini rohoni? Na pia Kwanini yawe malaini?

Baadhi ya watu wanaamini pengine Daudi hakuwa na Imani ya kutosha Kwa Mungu ya kuamini kuwa jiwe Moja tu lingetosha kumwangusha Goloathi, ndio maana akachukua matano. Lakini uhalisia ni kwamba Daudi alikuwa na Imani, hata kitendo tu Cha kukataa kubeba silaha za vita alizopewa na mfalme ilikuwa ni Imani kubwa.

Wengine wanaamini mawe Yale matano, yanafunua mambo matano ambayo Daudi alikuwa nayo yaani  1) Imani, 2) utiifu, 3)utumishi, 4)maombi na 5) Roho Mtakatifu.

Wengine wanaamini kuwa yanasimama kuwawakilisha wale watoto 5 wa Yule jitu aliyeitwa Refai, ambapo, Goliathi akiwa mmojawapo.(2Samweli 21:15-22). Hivyo Daudi alionyesha kuwa wote atawaangamiza.

Wengine wanaamini kuwa mawe yale matano yanafunua zile huduma tano (5), Waefeso 4:11. Ambazo hizo zinasimama kama msingi wa kumuangusha shetani  katika kanisa.

Lakini tukirudi  katika muktadha wa habari yenyewe, kiuhalisia ni kuwa Daudi alichukua mawe matano, akiamini kuwa la kwanza likimkosa bado la pili lipo atarusha tena, na kama la pili likimkosa basi bado lipo la tatu atarusha tena..Kufunua jinsi gani alivyokuwa na akiba ya imani. Bwana Yesu alisema, Imetupasa kuomba sikuzote bila kukata tamaa,  (Soma Luka 18:1-8), Upo wakati utaomba jambo kwa Bwana, halafu usijibiwe muda huo huo, je! Utakata tamaa kesho tena usiombe? Yesu anatuambia tuombe bila kukoma. Daudi aliamini hata ikitokea jiwe la kwanza limegonga dirii ya chuma, sio wakati wa kuvunjika moyo, ni kuvuta lingine, na kuendelea na mapambano. Vivyo hivyo na sisi yatupasa tuwe watu wenye akiba nyingi ya imani ndani yetu. Tunaomba tena na tena na tena, kwasababu hatujui ni jiwe lipi litaleta majibu, kama ni la kwanza au la katikati au la mwisho.

Lakini pia utaona hekima nyingine Daudi aliyoitumia ni kwenda kuyachukua mawe yake kwenye kijito cha maji. Jiulize ni kwanini iwe kwenye maji na sio penginepo? Kwasababu kimsingi mawe yapo kila mahali. angeweza kuokota tu ardhini.

Ni kufunua nini? Daudi alitambua VIJITO VYA MAJI YA UZIMA, ndipo wokovu ulipo. Ambavyo ni Yesu Kristo (Yohana 7:28). Usalama wa imani yake uliegemea kwa Mungu.  Hata sasa Bwana anataka imani yetu iegemee kwa Yesu Kristo, huko ndiko asili ya nguvu zetu ilipo, Kama mkristo usipolitambua hili ukawekeza imani yako kwenye elimu, au mali, au vitu vya ulimwengu huu, tambua kuwa huwezi mpiga adui yako ibilisi, kwa lolote.

Na mwisho kabisa Daudi aliyatwaa mawe laini kwanini yawe malaini.  Hata katika maji, yapo mawe ya maumbile mbalimbali, yapo makubwa yapo madogo, yapo yenye ncha, yapo malaini. Lakini alitambua kuwa jiwe litakalokaa katika kombeo lake, na litakalopaa vizuri na kumwangusha adui yake, sio kubwa, wala lenye ncha, wala zito sana. Bali laini, la mviringo. Kufunua nini.. Hauhitaji imani kubwa ya kuhamisha milima ili kumwangusha ibilisi. Bali kipimo cha imani yako, ukikitumia vema kinatosha kabisa kumdondosha Shetani.

Warumi 12:3  Kwa maana kwa neema niliyopewa namwambia kila mtu aliyeko kwenu asinie makuu kupita ilivyompasa kunia; bali awe na nia ya kiasi, kama Mungu alivyomgawia kila mtu kiasi cha imani. 4  Kwa kuwa kama vile katika mwili mmoja tuna viungo vingi, wala viungo vyote havitendi kazi moja; 5  Vivyo hivyo na sisi tulio wengi tu mwili mmoja katika Kristo, na viungo, kila mmoja kwa mwenzake.

Ukitumia vema nafasi yako uliyopewa na Mungu. Katika udogo wako, unyonge wako, umaskini wako, utamwangusha adui. Kila mmoja wetu amepewa nguvu hizo na Mungu. Hivyo usisubiri uwe Fulani ndio udhani utauangusha ufalme wa shetani. Hapo hapo ulipo ikiwa umeokoka, jiwe lako Kristo amekutolea. Litumie vizuri, lirushe vema, Goliathi atalala chini.

Bwana akubariki

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Je! aliyemwua Goliathi ni Daudi au Elhanani.

WALA HAKUACHA MTU ACHUKUE CHOMBO KATI YA HEKALU.

LIONDOE JIWE.

YESU NDIYE ATAKAYEKURUSHIA MAWE, USIPOTUBU.

YESU NDIYE ATAKAYEKURUSHIA MAWE, USIPOTUBU.

JIWE LILILO HAI.

TEMBEA NDANI YA SUKOTHI YAKO.-Maafundisho maalumu kwa watumishi

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya Mithali 27:21  inaposema “mtu hujaribiwa kwa sifa zake?”

SWALI: Nini maana ya Mithali 27:21  inaposema “Kalibu ni kwa fedha, na tanuru kwa dhahabu; Na mtu hujaribiwa kwa sifa zake”


JIBU: Kalibu na tanuru hizi ni sehemu za moto, ambapo, madini kama ya shaba, fedha, au dhahabu yanapitishwa na kuyeyushwa  ili kutenganisha uchafu uliogandamana na madini hayo. Hivyo hakuna namna nyingine ambayo unaweza kuifanya dhahabu au fedha ing’ae isipokuwa kuvipitisha kwenye matanuru hayo makali ya moto yaliyotengenezwa, na baadaye yatokee katika uzuri wake.

Vivyo hivyo na hapo anasema, ili kuupima moyo wa Mtu, kama ni kweli ndivyo alivyo au sivyo si katika kitu kingine chochote bali katika SIFA zake?

Sasa sifa zake ni zipi?

Ni vitu ambavyo vinavyoweza kumfanya asifiwe katika hivyo, Kwamfano, labda kipaji chake, cha kuimba. Ukimwona mtu hakengeushwi na kipawa hicho, yaani kiburi hakinyanyuki, staha inadumu, nidhamu na unyenyekevu unakaa naye, ijapokuwa ni maarufu, lakini viwango chake vya kiroho ni vilevile. Basi huyu ni mtu aliyekamilika kweli.

Au mwingine, Bwana kamjalia kupata pesa nyingi hivyo amekuwa tajiri sana na kuwazidi wengi. Lakini utajiri wake, haumfanyi adharau wengine, haumfanyi asimwabudu Mungu, haumfanyi achague watu wa kuishi nao, haumfanyi asiwasaidie wengine. Huyu ujue ni dhahabu safi kwelikweli, tabia yake ya mwanzo ilikuwa ni kweli.

Utakuta Mwingine labda kapata Elimu kubwa kuwazidi wengine, akabadilika tabia, akawa tena hajichanganyi na walio chini yake, kama ilivyokuwa zamani, hana muda wa kupokea simu za watu ambao anawaona hawamsaidii, hana nafasi ya kuhudhuria kwenye makanisa ambayo hayana wasomi, tofauti na alipokuwa hana elimu kubwa aliishi na kila mtu. moto wake umemtambulisha kwa sifa zake.

Vivyo hivyo kila jambo ambalo utasifiwa kwalo, iwe ni uzuri wako, hapo ndipo patakapoeleza tabia zako. Unajiwekaje wekaje, je! Hiyo ndio sababu ya wewe kutembea na vimini barabarani na suruali, au ndio sababu ya wewe kujisitiri.

Hivyo hekima inatupa kipimo sahihi cha kumtambua mtu alivyo rohoni. Sio katika mazungumzo yake, au kutenda kwake sasa, bali katika vitu vitakavyompa Sifa. Hapo paangalie sana. Utakuta  ni mtumishi wa Mungu kweli kweli na huduma yake ilipokuwa changa, alikuwa ni mnyenyekevu, mwombaji, anahubiri kweli ya Neno la Mungu, anawasaidia watu wote. Lakini pindi ilipokuwa na imejulikana sana, au huduma ipo katika daraja lingine, amebadilika, na kuwa kama mtu spesheli kama kiongozi wa nchi, mpaka umwone, lazima uwe na kadi yako ya mwaliko tena wa kiwango Fulani cha fedha, mafundisho anayoyahubiri ni ya kujinadi, au kujisifia yeye. Hapo ndipo panapoeleza tabia halisi ya huyo mhubiri, na sio kule chini alipokuwepo. Kule alikuwa anaigiza tu.

Hivyo, kila mmoja ajichunguze, je! Nitakaposifiwa, au nitakapopandishwa viwango vingine, nitabakia kuwa yeye Yule kama Bwana wetu Yesu alivyokuwa. Nikipata kazi, nitapoa kimaombi? Nikiolewa nitawadharau ambao hawajaolewa?.

 Bwana atusaidie.

Je! Upo ndani ya Kristo?  Kama ni la! Unangojea nini? Tambua kuwa tupo katika dakika za majeruhi, usiishi kama mnyama ambaye anaamka asubuhi anachowaza ni kula tu, ikifika jioni ni kurudi bandani. Wewe umewekewa kusudi la kufanya hapa duniani, na lenyewe ni kuyatenda mapenzi ya Mungu, na sio kula na kunywa na kujenga nyumba. Embu geuka sasa mkabidhi YESU maisha yako, ili parapanda ya mwisho itakapolia uwe na uhakika wa kwenda naye katika unyakuo. Ikiwa upo tayari kutubu dhambi zako leo, basi fungua hapa kwa mwongozo huo>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Kalibu maana yake nini? (Mathayo 6:30).

Wakati wakina Shadraka wanatupwa katika tanuru la moto, Danieli alikuwa wapi?

HEKIMA NI NINI? NA UFAHAMU UNAPATIKANA WAPI?

Nini maana ya Mithali 5:15-18 anaposema Unywe maji ya birika lako mwenyewe?

Fahamu maana ya Mithali 29:4 “Mfalme huithibitisha nchi kwa hukumu; Bali yeye apokeaye rushwa huipindua.

Shetani anaishi wapi, Je! Amefungwa au yupo kuzimu?

Rudi nyumbani

Print this post

Je biblia inatuhubiria kucheza Mieleka au kuitazama? (Mwanzo 32:24)

Swali: Tunaona Yakobo alishindana mweleka na Malaika wa Mungu (Mwanzo 32:24), je kuna ubaya wowote na sisi kutazama mieleka kwenye Tv?.

Jibu NI La! Biblia haijawahi kutufundisha wakati wowote kuipenda dunia, Zaidi sana imesema tusiipende dunia, wala mambo yaliyomo duniani na kama tukiipenda dunia na mambo yake basi upendo wa Mungu haupo ndani yetu. (1Yohana 2:15).

Na Mieleka ni moja ya mambo ya kidunia, pamoja na mipira!.

Sasa utajiuliza mbona Yakobo alipigana Mieleka katika Mwanzo 32:24?

Yakobo hakuketi na kupanga mechi na yule Malaika, kana kwamba walikuwa wanaburudishana au kupimana nguvu.. La! Haikuwa hivyo.. Kilichotokea ni kwamba Malaika wa Mungu alimtembelea Yakobo katika mwili wa kibinadamu, na baada ya kumaliza kilichompeleka pale, wakati anataka kuondoka, Yakobo alimzuia asiondoke, lengo ni kutaka kupokea Baraka kutoka kwa Malaika yule.

Sasa wakati Malaika anataka kuondoka, Yakobo anamvuta na kumrudisha nyuma mwisho ukageuka kuwa mweleka, lakini si wa lengo la kujiburudisha wala kudhuriana, wala kupimana nguvu bali la kuzuiana!!!

Mwanzo 32:24 “Yakobo akakaa peke yake; na mtu mmoja akashindana naye mweleka hata alfajiri. 

25 Naye alipoona ya kuwa hamshindi, alimgusa panapo uvungu wa paja lake; ukateguka uvungu wa paja la Yakobo alipokuwa akishindana naye. 

26 Akasema, Niache, niende, maana kunapambazuka. Akasema, Sikuachi, usiponibariki. 

27 Akamwuliza, Jina lako n’nani? Akasema, Yakobo. 

28 Akamwambia, Jina lako hutaitwa tena Yakobo, ila Israeli, maana umeshindana na Mungu, na watu, nawe umeshinda. 

29 Yakobo akamwuliza, akasema, Niambie, tafadhali, jina lako? Akasema, Kwa nini waniuliza jina langu? Akambariki huko.

30 Yakobo akapaita mahali pale, Penueli, maana alisema, Nimeonana na Mungu uso kwa uso, na nafsi yangu imeokoka”.

Lakini Mieleka inayoonekana kwenye Luninga zama hizi za mwisho ni Mapando ya shetani asilimia mia, Ndio maana utaona wanaocheza michezo hiyo wanakuwa wapo nusu uchi!. na wanatangaza vitu vya kiulimwengu.

Hivyo na sisi hatupaswi kupigana Mieleka ya kidunia isiyo na maana, badala yake tupigane Mieleka ya kiroho ambayo matokeo yake ni sisi kubarikiwa. Tung’ang’anie baraka zetu zilizoandikwa katika NENO LA MUNGU, (biblia). Na pia tushidane kwa kumponda yule adui yetu shetani chini ya miguu yetu.

Waefeso 6:12 “Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.

13 Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama”

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Kucheza karata ni sahihi kwa Mtu aliye MKRITO?

Je ushabiki wa mpira ni dhambi?

MWINUE YESU KRISTO KATIKA MAISHA YAKO.

Je Mungu anaweza kumdanganya mtu?

Kwanini Yakobo alimshinda Mungu, Je! Mungu huwa anashindwa na wanadamu?

Rudi nyumbani

Print this post