NI KIZAZI KIPI WEWE UPO?

Kibiblia  Kizazi ni kundi la watu linalozuka ghafla lenye tabia zinazofanana, linaweza kuzuka aidha kutokana na mabadiliko ya nyakati, au mabadiliko ya mazingira. Kwamfano, Wana wa Israeli walipokuwa Misri, chini ya Yusufu, waliishi kwa raha sana, Lakini Yusufu alipokufa pamoja na Yule Farao, kilinyanyuka kizazi kingine kisichokumbuka wema wa Yusufu, na hapo ndipo utumwa mgumu ulipoanza.

Vilevile, Wana wa Israeli walipofika katika nchi yao ya  Ahadi, mwanzoni waliishi maisha ya kumcha Mungu sana, lakini wakati ulipopita mrefu kilinyanyuka kizazi kingine kisichomjali Yehova, hapo ndipo Israeli ilipoanza kuingia katika matatizo mengi sana.(Waamuzi 2:10)

Na katika hichi kipindi cha Siku za mwisho, tunapaswa tuwe makini sana, Zipo tabia ambazo utaziona kwa watu wengi sana, lakini kiuhalisia hazikuwepo huko nyuma. Hivyo ni vizuri ukafahamu aina ya vizazi vilivyopo duniani sasa hivi  kulingana na biblia ili ujue wewe upo wapi na jinsi gani unapaswa ujiupeshe navyo.

  1. Kizazi cha uzinzi na zinaa:

 Bwana Yesu alisema..

Mathayo 12:39 “Akajibu, akawaambia, Kizazi kibaya na cha zinaa chatafuta ishara, wala hakitapewa ishara, ila ishara ya nabii Yona”.

Ni kizazi cha watu kinachozuka kinapenda tu usherati na uzinzi kuliko kitu kingine chochote ulimwenguni. Leo hii tazama  mawazo ya vijana wengi yalivyo, sikiliza mazungumzo yao,  mambo wanayoyafanya kwa siri,vitu wanavyotazama mitandaoni, video za ngono, ni jambo la kawaida kwao, na kibaya zaidi sio tu vijana, hadi wazee na watoto wamo katika kundi hili. Jambo ambalo hapo zamani halikuwepo. Hiyo ni kuthibitisha kuwa ni hiki ni kizazi kingine kimezuka, ambacho ni hatari sana.

Bwana Yesu alisema..

Marko 8:38 “Maana kila mtu atakayenionea haya mimi, na maneno yangu, katika KIZAZI HIKI CHA UZINZI na dhambi, Mwana wa Adamu atamwonea haya mtu huyo, atakapokuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika watakatifu”.

Ndugu, jiupeshe, na mkondo huu, si lazima uishe kama ulimwengu unavyotaka, kizazi hiki kimeshahukumiwa na Mungu.

     2) Kizazi cha nyoka:

Kipo kizazi cha Nyoka.

Mathayo 3:7 “Hata alipoona wengi miongoni mwa Mafarisayo na Masadukayo wakiujia ubatizo wake, aliwaambia, Enyi wazao wa nyoka, ni nani aliyewaonya ninyi kuikimbia hasira itakayokuja?

8 Basi zaeni matunda yapasayo toba;

9 wala msiwaze mioyoni mwenu kwamba, Tunaye baba, ndiye Ibrahimu; kwa maana nawaambia ya kwamba Mungu aweza katika mawe haya kumwinulia Ibrahimu watoto”.

10 Na shoka limekwisha kuwekwa penye mashina ya miti; basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni.

Soma pia..Mathayo 12:34

Nyoka, alikuwa mwerevu sana kuliko wanyama wote mwituni, lakini alikubali kuwa chombo teule cha shetani. Uzao wake, ndio uliendelea mpaka kwa Kaini, na ndio maana watu wale walikuwa hodari sana , wagunduzi na wavumbuzi wakubwa, lakini waovu waliopindukia (Mwanzo 6:4). Ni watu ambao walikuwa hawana muda na Mungu, lakini kwa upande wa pili uzao wa Mungu, ulikuwa ni mnyenyekevu unaomtafuta Mungu usiku na mchana, vilevile na usio na masumbufu mengi ambao ulipitia kwa Sethi. (Mwanzo 4:26).

Inafunua hadi sasa, kwamba kizazi hiki kipo, Angalia dunia ya sasa, imestaarabika kuliko ile ya zamani, watu wanaelimu kubwa sana, wanagundua mambo makubwa  sana, wamekwenda mpaka mwezini, lakini ukiwagusia habari za Mungu, wanakuambia  hayo ni mawazo yako tu, hakuna Mungu,dini imetengenezwa na watu, wamejikita katika mambo ya mwilini, tu, elimu, utajiri, uvumbuzi basi, Mungu hayupo.

Ndugu, ikiwa na wewe upo katika jopo hili la watu, jiangue haraka sana, hichi ni kizazi, ambacho kipo ulimwenguni sasa.

   3) Kizazi cha watu wasiowatii wazazi wao.

Mithali 30:11 “Kuna kizazi cha watu wamlaanio baba yao; Wala hawambariki mama yao”.

Kuporomoka kwa maadili na nidhamu unakokuona leo, hakukuwepo huko nyuma. Leo utasikia mtoto anajibizana na mzazi wake, mwingine anampiga, mwingine anamzungumzia vibaya, wengine wametengeneza mpaka uadui na wazazi wao.. Kesi hizi ni nyingi sana sikuhizi..Wewe kama mtoto, wewe kama kijana, kuwa makini sana, kizazi hiki kimezuka ulimwenguni sasa. Unapoona, wenzako hawawaheshimu wazazi wao, na wewe usiwe mmojawapo.

Katika agano la kale mtu aliyejaribu kuonyesha utomvu wa nidhani kwa mzazi wake, sheria yake ilikuwa ni kifo. Jitathmini unawatii wazazi wako, Unawapenda?, unawabariki? Unawanenea mema? Unawaombea?.. Hata kama mzazi anakuudhi, huna ruhusu ya kurudisha baya kwa baya kwake. Vinginevyo upo chini ya laana ya kizazi hiki.

4) Kizazi cha watu wanaojiona siku zote wapo sawa:

Mithali 30:12 “Kuna kizazi cha watu walio safi machoni pao wenyewe; Ambao hawakuoshwa uchafu wao”.

Hili kundi ni kubwa sana, Mtamuhubiria mtu na kumwambia pasipo kumwamini Kristo, huwezi kuokolewa, yeye atakuambia, mimi naamini matendo yangu ni safi, ninaamini Mungu hiyo inatosha, siwezi kuhukumiwa. Atakuwa radhi, kujihesabia haki, hata kama ni mzinzi, au mlevi..Haoni hatia yoyote kwa anayoyafanya. Yeye anachoamini ni kuwa Mungu hawezi kumchoma motoni milele,.Nimeshakutana na watu wa namna hii wengi sana. Wanaodhani kuwa kwa kile wanachokiamini, ndio tiketi ya Mungu kuwaokoa siku ile.

Ndugu kama upo katika hili kundi jiepushe nalo, Ikiwa bado hujaokoka, mkimbilie Yesu, yeye pekee ndiye mwenye uwezo wa kukusafisha dhambi zako, na sio kile unachokiamini.

 5) Kizazi cha watu wenye kiburi:

Mithali 30:13 “Kuna kizazi cha watu ambao macho yao yameinuka kama nini! Na kope zao zimeinuka sana”.

Wapo watu ambao, kujishusha hakupo ndani yao. Wanajiona kuwa hakuna chochote kinachoweza kuwa msaada kwao, Mungu si kitu kwao, kwanini wakaombe, kwanini waende ibadani. Wapo radhi hata kuutukana wokovu, au kazi ya Mungu. Wanatumaini, mali zao, au ujuzi wao.

Kama tabia hizo zimeanza kuonekana ndani yako, geuka upesi.

  6) Kizazi wa watu wasio na huruma.

Mithali 30:14 “Kuna kizazi cha watu ambao meno yao ni panga; Na vigego vyao ni kama visu. Ili kuwala maskini waondolewe katika nchi, Na wahitaji katika wanadamu”.

Utu umeondoka duniani, Yupo radhi kufanya biashara haramu, bila kujali kinaleta madhara mangapi kwa jamii, anauza madawa ya kulevya, anauza bidhaa zilizoisha ubora, wanadhulumu haki za wajane na mayatima kwa faida zao wenyewe. Anaua, ili apate mali, n.k.

Tunayoyaona, hayakuwepo zamani, tusiwe watu wenye tamaa ya mali.

  7) Kizazi cha wenye adili:

Lakini pamoja na kuwepo kwa vizazi hivi vyote, vya watu waovu.. Biblia inasema pia, kitakuwepo kizazi cha watu wenye adili, wanaomcha Mungu, wanaotenda mapenzi yake.

Zaburi 112:1 “Haleluya. Heri mtu yule amchaye Bwana, Apendezwaye sana na maagizo yake.

2 Wazao wake watakuwa hodari duniani; Kizazi cha wenye adili kitabarikiwa”.

Na ndio maana unaona pia wapo watakatifu wa Mungu leo duniani. Hawa ndio Bwana anaowatazama, na siku moja itafika Kristo atawahamisha kutoka katika huu ulimwengu kwa tukio la UNYAKUO na kuwapeleka mbinguni. Swali ni je wewe upo katika kizazi kipi?

Matendo 2:40 “Akawashuhudia kwa maneno mengine mengi sana na kuwaonya, akisema, Jiokoeni na kizazi hiki chenye ukaidi”.

Jibu unalo moyoni mwako.

Kumbuka Unyakuo upo karibu sana, dalili zote zimeshatimia, huna haja ya kuendelea kutangatanga na huu ulimwengu tena. Mgeukie Kristo akuokoe, ili uwe mmojawapo wa kizazi cha watu waadilifu.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp yanayotumwa kila siku basi bofya hapa >>>  WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita..

BADO UPO YERUSALEMU TU..GALILAYA HUTAKI KWENDA?

Nini maana ya msiwe waalimu wengi (Yakobo 1:3)?

FANYIKA SIPORA WA KRISTO, UNYAKUO UPO KARIBU.

Marago ni nini? ( Waamuzi 10:18)

Rushwa inapofushaje macho?

Rudi nyumbani

WITO WA MUNGU HAUVUKI NENO LAKE.

Bwana Yesu atukuzwe ndugu yangu. Karibu tuyatafakari maneno ya uzima pamoja..

Tunaposoma biblia..tujue kuwa tunausoma ufahamu wa Mungu. Mtu asiyeitafakari biblia halafu anakimbilia kwenda kumtumikia Mungu.. Ajue kuwa anajiweka katika hatari kubwa sana ya kuangamizwa na Mungu.

Ni sawa na mtu anayekimbilia kufanya biashara ambayo hajaifanyia utafiti kujua changamoto zake.faida zake na hasara zake..

Leo tutatazama ni kwa namna gani.

Ndugu usipumbazwe hata kidogo kuona Mungu anasema nawe..anakuonyesha maono makubwa..anakusifia..anakutokea..anakutuma ukawahubirie watu injili.. Usipumbazwe kabisa na jambo hilo. Kama maagizo yaliyopo katika Neno lake huyatii..Kufa unaweza tu kufa.

Jambo kama hilo tutaliona kwa Musa. Kila mtu anafahamu kuwa alitokewa na Mungu mwenyewe katika mwali wa moto. Mungu akampa ishara kubwa..akamtuma aende Misri kwenda kuwaokoa mamilioni ya watu..Lakini cha ajabu tunashangaa Mungu alitaka kumuua njiani..

Yaani kama sio mke wake Sipora,kumsaidia habari ya Musa ingekuwa imeishia pale na maono yake na wito wake.

Kutoka 4:21-25

[21]BWANA akamwambia Musa, Hapo utakaporudi Misri, angalia ukazifanye mbele ya Farao zile ajabu zote nilizozitia mkononi mwako; lakini nitaufanya mgumu moyo wake, naye hatawapa ruhusa hao watu waende zao.

[22]Nawe umwambie Farao, BWANA asema hivi, Israeli ni mwanangu mimi, mzaliwa wa kwanza wangu;

[23]nami nimekuambia, Mpe mwanangu ruhusa aende, ili apate kunitumikia, nawe umekataa kumpa ruhusa aende; angalia basi, mimi nitamwua mwanao, mzaliwa wa kwanza wako.

[24]Ilikuwa walipokuwa njiani mahali pa kulala, BWANA akakutana naye akataka kumwua.

[25]Ndipo Sipora akashika jiwe gumu na kuikata govi ya zunga la mwanawe, na kuibwaga miguuni pake akasema. Hakika wewe u bwana arusi wa damu kwangu mimi.

Sasa ni kwanini Mungu alitaka kumuua ni kwasababu alipuuzia maagizo ya msingi ya kuwatahiri watoto wake..Mambo ambayo Mungu alikuwa ameshawaagiza  wana wa Israeli wote wafanye hivyo kulithibitisha agano lake..Lakini yeye hakuona umuhimu huo..kisa tu Mungu amemtokea..amemtuma kama nabii mkuu Misri..hivyo hakuna sababu ya kuhangaika na yale mengine..

Ni wangapi leo hii wamepatwa na kiburi cha kukataa maagizo ya Mungu kama vile ubatizo sahihi wa maji..kwa kisingizio kuwa Mungu anazungumza na wao..Mungu kawatokea..Mungu kawaagiza waende kutumika..ubatizo hauna maana yoyote ukishamkiri tu Kristo inatosha..Wewe si zaidi sana ya nabii  Musa..Mungu hashindwi kukuua.

Unaweza kusema ni Musa tu peke yake yalimkuta haya..Yupo nabii mwingine huko mbeleni anaitwa Balaamu.. Yeye naye alitokewa na Mungu katika safari yake ya kwenda kuwalaani Israeli.

Mara ya kwanza Mungu akamuonya lakini hakusikia.. Akataka zaidi kufanya hivyo..baadaye Mungu akamruhusu na akamuhakikishia kuwa atakuwa pamoja naye..Lakini njiani Mungu alikuwa ameshamweka malaika wake tayari amuue. Kama si yule Punda kumsaidia habari yake ingekuwa naye imeisha pale…

Ni kwanini sasa iwe vile ni kwasababu alipuuzia maagizo ya awali ya Mungu “..amlaaniye Israeli na yeye atalaaniwa”(Mwanzo 12:3)..hivyo yeye akataka kulipindua hilo Neno kwa maono yake..au mitazamo yake mwenyewe. Akawa katika hatihati ya kufa..

Hesabu 22:12-13

[12]Mungu akamwambia Balaamu, Usiende pamoja nao; wala usiwalaani watu hawa, maana wamebarikiwa.

[13]Balaamu akaondoka asubuhi akawaambia wakuu wa Balaki, Enendeni zenu hata nchi yenu; kwa maana BWANA amekataa kunipa ruhusa niende pamoja nanyi….

Lakini baada ya kushurutishwa sana na wale wakuu wa Balaki..utaona alijifanya tena kwenda kumuuliza Mungu..hichi ndio kitu alichoambiwa mara ya pili

Hesabu 22:20-22

[20]Mungu akamjia Balaamu usiku, akamwambia, Kwa kuwa watu hawa wamekuja kukuita, enenda pamoja nao; lakini neno lile nitakalokuambia ndilo utakalolitenda, basi.

[21]Balaamu akaondoka asubuhi, akatandika punda wake, akaenda pamoja na wakuu wa Moabu.

[22]Hasira ya Mungu ikawaka kwa sababu alikwenda; malaika wa BWANA akajiweka njiani, ili kumpinga. Basi alikuwa amepanda punda wake, na watumishi wake wawili walikuwa pamoja naye.

Ndugu..tuzifahamu tabia za Mungu..wapo watu wengi wameonyeshwa mambo makubwa sana katika wito wao. Lakini unashangaa hakuna hata moja limetimia..hadi siku anakufa..Ni kwanini?

Nikwasababu alikwenda pasipo kujua kanuni za Mungu. Tuishi kwa Neno la Mungu na sio kwa ndoto au sauti au maono. Haijalishi wito huo utakuwa mkubwa kiasi gani..hauwezi kuzidi Neno lake.. Neno linasema mwanamke hana nafasi ya kufundisha kanisani (palipo na mchanganyiko wa wanaume na wanawake) 1Timotheo 2:12..Lakini mwingine atasema Mungu kaniita kuwa Mchungaji..kanitokea kabisa na kunitia mafuta..

Mama kuwa makini..kasome biblia yako kwanza umwelewe Mungu ndipo ukatumike..

Hivyo ili tuwe salama.. kabla ya kuitii sauti yoyote ya nje..Tuitii kwanza Sauti ya Mungu iliyo katika Neno lake.  Ndio hayo mengine yafuate.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp ya kila siku basi jiunge kwa kubofya hapa >>> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

USIPOTEZWE NA MANENO YA MANABII WA UONGO.

JE UNAIFANYA KAZI YA MUNGU?

MAJARIBU MATATU YA YESU KRISTO

TAFUTA MSAMAHA HALISI, NA SI MSAMAHA TU!

UTAWALA WA MIAKA 1000.

Nini maana ya “wazimu” katika biblia?

JINSI PAULO ALIVYOPAMBANA NA UJINGA WA ROHONI.

PINDO LA VAZI LAKE SASA LIMEREFUSHWA.

Rudi nyumbani

Je Bwana Yesu alikuwa na mchoro (tattoo) katika paja lake?

Tusome..

Ufunuo 19:16 “Naye ana jina limeandikwa katika vazi lake na paja lake, MFALME WA WAFALME, NA BWANA WA MABWANA”

Mstari huu unatumika na wengi wanaohalalisha uchoraji wa tattoo katika miili yao, kuwa hata Bwana Yesu mwenyewe alijichora tattoo katika paja lake.

Je ni kweli hiyo ndio maana ya huo mstari?
Jibu ni la! Katika Maono hayo Yohana aliyoyaona, hakuona nyama ya paja la Bwana Yesu ikiwa limeandikwa hayo maneno, bali alichokiona ni vazi lililofunika paja limeandikwa maneno hayo, BWANA WA MABWANA na MFALME WA WAFALME.

Kwamfano kuna andiko linasema jifunge upanga pajani mwako..

Zaburi 45:3 “Jifungie upanga wako pajani, wewe uliye hodari, Utukufu ni wako na fahari ni yako”.

Je kwa mstari kwa huo biblia imemaanisha, kuchua upanga na kuubandika kwenye nyama ya paja?..

Bila shaka haikumaanisha hivyo bali ilimaanisha funga upanga katika ghala iliyopo viununo mwetu.

Au labda mtu akupe maagizo ya kubeba kiroba cha mzigo Begani, je atakuwa anamaanisha uvue nguo ubaki bega wazi ndio ubebe mzigo huo?.

Au mtu akwambie vaa mkanda kiunoni, atakuwa amemaanisha uvue nguo zote halafu ujifunge mkanda kwenye nyama ya kiuno chako? Jibu ni la!..bali amemaanisha katika vazi lililopo kiunoni kama ni suruali au nguo nyingine yoyote, ifungwe kwa mkanda.

Vile vile katika mwonekano mwingine wa Bwana kuna mahali, maandiko yanasema alionekana kafungwa mshipi wa dhahabu “matitini”.

Ufunuo wa Yohana 1:13 “na katikati ya vile vinara nikaona mtu mfano wa Mwanadamu, amevaa vazi lililofika miguuni, na kufungwa mshipi wa dhahabu matitini”.

Bila shaka mstari huo haukumaanisha ndani ya kifua cha Bwana kuna mshipi umedungwa wa dhahabu, bali biblia imemaanisha kwenye vazi lake la nje, sehemu ya kifua palikuwa na mshipi (yaani mkanda).

Kadhalika katika mstari huo,wa Ufunuo 19:16, biblia haijamaanisha kuwa kuna maneno yaliyoandikwa kwenye nyama ya paja, bali imemaanisha maneno yaliyoandikwa katika vazi lililofunika paja.

Hakuna mahali popote maandiko yanaagiza wala kutufundisha kujichora tattoo.

Kujichora kwa aina yoyote ile, ikiwemo kupaka hina ni dhambi kibiblia, Na wote wanaojichora hawataurithi uzima wa milele (Kwa maelezo marefu kuhusu kujichora na kujichanja kibiblia unaweza kufungua hapa Kujichota ni dhambi

Je umempokea Yesu?..je umebatizwa katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jinala Yesu?, Mambo haya mawili ndio msingi wa wokovu, na kila mtu lazima ayafanye ili awe mkristo.

Bwana atubariki.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp ya kila siku basi jiunge kwa kubofya hapa >>> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

JE! WEWE NI MFUNGWA WA BWANA?

NAMI NINAZO FUNGUO ZA MAUTI, NA ZA KUZIMU.

WAKAMCHA BWANA, NA KUITUMIKIA MIUNGU YAO WENYEWE.

HAPANA MFUPA WAKE UTAKAOVUNJWA.

Ni lini na wapi Ibrahimu aliioona siku ya Bwana akashangilia?

USO WAKE ULIKUWA UMEHARIBIWA SANA ZAIDI YA MTU YE YOTE.

Rudi nyumbani

NA ABARIKIWE KILA AKUBARIKIYE, NA ALAANIWE KILA AKULAANIYE.

SWALI: Nini maana “nitawabariki wakubarikio, naye akulaaniye nitamlaani;”..Je! Ni kwa namna gani tunapaswa tulibariki taifa la Israeli.  Je! Ili tubarikiwe tunapaswa, tufunge na kuliombea Taifa la Israeli usiku na mchana, au tuwe na bendera za taifa lile makanisani kwetu au majumbani mwetu?.

Ni kwa namna gani tutapokea Baraka kwa kulibariki tu taifa hilo?


JIBU: Maneno hayo, kwa mara ya kwanza tunaona Mungu akiyatamka kwa Ibrahimu katika;

Mwanzo 12:1 “Bwana akamwambia Abramu, Toka wewe katika nchi yako, na jamaa zako, na nyumba ya baba yako, uende mpaka nchi nitakayokuonyesha;

2 nami nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, na kukubariki, na kulikuza jina lako; nawe uwe baraka;

3 nami nitawabariki wakubarikio, naye akulaaniye nitamlaani; na katika wewe jamaa zote za dunia watabarikiwa”.

Maandiko hayo hayatupi tafsiri ya kwamba tukeshe kuliombea taifa la Israeli usiku na mchana ili tubarikiwe, hapana utaona maneno hayo, Mungu alisema akilenga wakati ambapo watu wanapanga kuliangusha, au kuliporomosha au kuliletea vitisho taifa hilo, aidha kwa kulivamia, au kuliloga, n.k. kwa namna yoyote ile, hapo ndipo anayejaribu kufanya hivyo anakumbushwa,kuwa aibarikiye Israeli, atabarikiwa, na ailaaniye Israeli atalaaniwa.

Jambo kama hilo tunalithibitisha kwa Yule Balaamu mchawi, ambaye aliajiriwa na Balaki, ili aende kuwalaani Israeli, (yaani kuwaloga) kwa ushirikina ili wasifanikiwe kuvuka katika nchi ya Balaki. Lakini Ilikuwa nusura Mungu amuue Yule Balaamu, kwa kitendo tu hicho cha kujaribu kuliloga taifa teule. Kinyume chake ikabidi alibariki ili tu awe salama..Mpaka yeye mwenyewe akakiri,na kusema hapana uchawi katika Israeli wala uganga..

Hesabu 23:21 “Hakutazama uovu katika Yakobo, Wala hakuona ukaidi katika Israeli. Bwana, Mungu wake, yu pamoja naye, Na sauti kuu ya mfalme i katikati yao.

22 Mungu amewaleta kutoka Misri, Naye ana nguvu kama nguvu za nyati”.

Hiyo ni kuonyesha kuwa, hata sasa yapo mataifa mengi ambayo yameshatangaza uadui na Israeli, mojawapo ni Somalia, na Libya, embu yaangalie mataifa hayo leo hii yapoje., na hiyo yote ni kwasababu yamejaribu kuleta vita na vitisho kwa taifa teule la Mungu, na matokeo yake ni kuwa yamepigwa, kila kukicha ni vita. Na mengine yanalitamkia maneno ya laana kama vile Palestina,, na mengine kuliwekea vikwazo.  Embu Yatazame ustawi wao hayo mataifa au hao watu leo hii walivyo.

Halikadhalika, taifa ambalo halitaki shari na Israeli, bali linalitakia mema amani na mafanikio daima, basi taifa hilo au Mtu huyo Mungu  atambariki. Hivyo  umeona hapo, inalenga katika habari ya amani na shari, yaani pale ambapo unalazimishwa utamke mabaya, uwalaani, uwatukane,  au upigane vita kinyume chao, hapo unapaswa uende kinyume chake, uwabariki, na kuwatakia amani. Ndipo utakapobarikiwa.

Lakini sio kuacha kufuata kanuni za Mungu za kimaandiko na kukesha kuliombea taifa la Israeli ili tubarikiwe. Mpaka tunasafiri kwenda kule Yerusalemu, kupokea Baraka hizo, Mungu havutiwi sana na sisi tunapofanya hivyo, anavutiwa na sisi pale tunapoishi kulingana na Neno lake, hivyo tu. Kwahiyo, usipeleke fikra zako sana Israeli, bali zipeleke kwenye maisha yako, vilevile maombi yako, yaelekeze kwa watu wenye dhambi leo hii ulimwenguni. Kesha kuwaombea hao, na kuiombea Injili.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp  yanayotumwa kila siku basi fungua bofya hapa ujiunge >>> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

ALAMA ZA BENDERA YA ISRAELI ZINAWAKILISHA NINI?

Israeli ipo bara gani?

Mataifa ni nini katika Biblia?

Bwana Yesu alimaanisha nini kusema “yamfaa afungiwe shingoni jiwe kubwa la kusagia, na kutoswa katika kilindi cha bahari?”

REKEBISHA YAFUATAYO ILI UCHUMI WAKO UKAE SAWA.

Je Mkristo kutembea na walinzi (Bodyguards),ni sawa?

Rudi nyumbani

ALAMA ZA BENDERA YA ISRAELI ZINAWAKILISHA NINI?

Wakati Mungu anawatoa Israeli kutoka Misri, Mungu hakuwapa bendera kuwa kama Ishara ya Taifa hilo, Hivyo bendera kwa Israeli ni kitu kilichokuja kuzalika miaka mingi baada ya Kristo kuja duniani katika harakati za kutafuta uhuru.

Sasa swali, ni je zile rangi katika bendera hiyo zinawakilisha nini?, Na ile nyota iliyopo katikati ya bendera inawakilisha nini?.

Bendera ya Israeli ina rangi mbili tu! Nyeupe na Blue (kwa kiswahili Samawi).
Rangi nyeupe inawakilisha utakatifu wa Mungu. Na Blue inawakilisha utukufu wa Mungu.

Tukitazama juu mbinguni, anga linaonekana la rangi ya Blue(Samawi).

Kufunua utukufu wa Mungu.Hata vitu vingine vya asili kama milima, bahari utaona vina mwonekano wambwa wa rangi hii ya blue kufunua utukufu wa Mungu.

Lakini kitu cha mwisho katika bendera ya Israeli, ni ile alama kama ya Nyota, yenye pembe sita, iliyopo katikati ya bendera hiyo.
Alama hiyo inajulikana kama Nyota ya Daudi au Ngao ya Daudi.

Imejulikana hivyo, kwasababu inaaminika Ngao ya Daudi ilikuwa na umbile hilo mfano wa hiyo nyota, na inaaminika ngao hiyo ilikuwa ina nguvu fulani ya kiungu.
Vile vile zile pembe sita katika hiyo ngao zinawakilisha zile tabia sita za Roho wa Mungu katika Isaya 11.

Isaya 11:2 “Na roho ya BWANA atakaa juu yake, roho ya hekima na ufahamu, roho ya shauri na uweza, roho ya maarifa na ya kumcha BWANA”.

Na vile vile kama ilivyokuwa na pembe tatu mbili, moja inaangalia juu na nyingine chini, inawakilisha uhusiano wetu sisi na Mungu.

Ingawa hakuna mahali popote katika torati wala biblia nzima, nyota hiyo ilitajwa kwa sifa hizo, lakini wayahudi wa karne ya 17, walishawishika kuamini hivyo na kuitumia hiyo kama ishara ya Nembo ya Taifa lao, na hata kuitumia katika bendera yao.

Lakini katika jicho lingine, nyota hiyo inaaminika kama ishara ya Masihi, yaani Yesu Kristo, yeye ndiye Uzao wa Daudi, na ndiye ile nyota ing’aayo, ambaye Mataifa yote watamtumainia.

Ufunuo 22:16 “Mimi Yesu nimemtuma malaika wangu kuwashuhudia ninyi mambo hayo katika makanisa. Mimi ndimi niliye Shina na Mzao wa Daudi, ile nyota yenye kung’aa ya asubuhi”.

Lakini swali ni je! Bendera hiyo kwetu sisi wakristo, ina manufaa yoyote kiroho?, Kwamba tunapokuwa na bendera ya Israeli katika makanisa yetu, au katika vyombo vyetu vya usafiri, au katika nyumba zetu, tunakuwa tunajiongezea baraka??.

Jibu ni la!. Bendera ya Taifa la Israeli haituongezei chochote, zaidi sana mtu anapoiweka ndani kwake, na kuifanya kama mungu wake atakuwa anajizombea laana badala ya baraka. Kwasababu kwake yeye ni kama mungu.

Baraka pekee tunayoweza kuipata sisi ni kuishi kulingana na Neno lake na kanuni zake, utakatifu sawasawa na Waebrania 12:14, ndiyo bendera yetu, na alama ya kukubaliwa na Mungu..na sio bendera ya Israeli ndani kwetu.

Hivyo hakuna ulazima wowote wa Mkristo au mhubiri kutembea na bendera kana kwamba ndio kitovu chake cha baraka, labda atembee nayo kwa lengo lingine lakini sio hilo la kutafuta baraka kupitia hiyo.

Maandiko yaliposema “ambarikiye Israeli amebarikiwa” hiyo sio maana yake..Maana yake ni nyingine kabisa.

Bwana akubariki.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kama utapenda uwe unafikiwa na masomo ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP basi bofya hapa ujiunge moja kwa moja  >>>> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

MAISHA ULIYOPITIA NYUMA NI USHUHUDA TOSHA WA WEWE KUMTUMIKIA MUNGU

WEKA KUMBUKUMBU YA MAMBO BWANA ANAYOKUFANYIA KWASABABU YATAKUFAA MBELENI.

Neno Kupatiliza maana yake nini katika biblia?

Babewatoto ni nani katika biblia?(Isaya 34:14).

Ni kosa gani Daudi alilolifanya katika kuwahesabu watu, mpaka kupelekea vifo vya waisraeli wengi?

Maana Ya Maneno Katika Biblia.

Rudi nyumbani

Atamaniye faida huifadhaisha nyumba yake mwenyewe;

SWALI: Nini maana ya huu mstari..

Mithali 15:27

[27]Atamaniye faida huifadhaisha nyumba yake mwenyewe;

Bali achukiaye zawadi ataishi.


JIBU: Mstari huo ni mgumu kueleweka kidogo kwasababu kiswahili kilichotumika hapo ni kile cha zamani..

Ukiangalia tafsiri nyingine..mstari huo unamaana hii.. Atamaniye kupata vingi kwa njia isiyohalali huifadhaisha nyumba yake mwenyewe bali achukiaye rushwa ataishi.

Jambo ambalo ni kweli..kwamfano Mtu anayejiingiza katika biashara ya madawa ya kulevya kwa tamaa tu ya kupata fedha nyingi..hajui kuwa mwisho wake ni kujibomoa yeye mwenyewe na pamoja nyumba yake yote.

Habakuki 2:9

[9]Ole wake yeye aipatiaye nyumba yake mapato mabaya, ili apate kukiweka kioto chake juu, apate kujiepusha na mkono wa uovu!

Mwingine utakuta anatoa rushwa ili bidhaa zake zisilipishwe kodi..lakini hajui mwisho wake utakuwa mbaya siku moja.

Lakini kinyume chake biblia inasema atakayeyakwepa hayo yote ataishi..

Sikuzote tamaa ya  za haraka haraka mwisho wake huwa ni mitegoni..

Mhubiri 4:6

[6]Heri konzi moja pamoja na utulivu,

Kuliko konzi mbili pamoja na taabu;

na kujilisha upepo.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kama utapenda uwe unafikiwa na masomo ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP basi bofya hapa ujiunge moja kwa moja  >>>> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

SABATO ILIFANYIKA KWAAJILI YA MWANADAMU NA SI MWANADAMU KWAAJILI YA SABATO!

Maana ya huu mstari ni ipi? Mithali 14:4 ‘Zizi ni safi ambapo hapana ngombe;bali nguvu za ngombe zaleta faida nyingi’.

UMEDI NA UAJEMI ZILITAWALAJE?

KUNA AINA NGAPI  ZA MAOMBI?

HUANGUA MAYAI YA FIRA, NA KUSUKA WAVU WA BUIBUI;

Karama ya pili inayozungumziwa katika 2Wakorintho 1:15 ndio ipi?

Tusome,

2Wakorintho 1:15 “Nami nikiwa na tumaini hilo nalitaka kufika kwenu hapo kwanza, ili mpate karama ya pili

Sio wakati wote neno “karama” linapotumika kwenye biblia linamaanisha “karama ya roho kama vile unabii, uchungaji, ualimu n.k”. Bali karama pia ni neno linalomaanisha “Zawadi au Baraka”.

Kwamfano kuna andiko linasema “karama ya Mungu ni uzima wa milele”.

Warumi 6:23 “Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu”.

 Sasa hapo haimaanishi kwamba Mungu karama yake ni “Uzima wa milele” kama sisi karama zetu zilivyo kutoa unabii, au Kunena kwa lugha, au kutabiri nk.

Mungu yeye hana kipawa fulani maalumu, kwasababu vyote vinatoka kwake.

Bali hapo biblia imemaanisha kuwa “Zawadi ya Mungu ni uzima wa milele”..au “Baraka ya Mungu kwetu ni uzima wa milele”

Kadhalika Mtume Paulo aliposema  kuwa “nalitaka kufika kwenu hapo kwanza, ili mpate karama ya pili” hakumaanisha kuwa kuna karama nyingine ya pili tofauti na hiyo ya kitume aliyokuwa nayo,  au nyingine mpya  hivyo anataka kwenda kuwapa, au kuwanufaisha katika hiyo, hapana!, bali alimaanisha “Baraka ya Pili”.

Ni sawa mhubiri aliyeko Dar es Salaam, aende kuhubiri Morogoro, kwa wiki moja na kisha arudi Dar, na ghafla apate tena safari ya kwenda Dodoma kuhubiri baada ya wiki moja wakati kasharudi Dar, bila shaka hawezi kufika Dodoma bila kupita Morogoro, hivyo Mhubiri huyu akawasiliana na wale aliokwenda kuwahubiria hapo kwanza  (Watu wa Morogoro) kwamba atapita tena kuhubiri kwa siku moja na siku inayofuata atakwenda Dodoma.. Hivyo watu wa Morogoro wakawa wamepata Baraka mara mbili. Ndicho Mtume Paulo alichomaanisha hapo!.

Kwamba alishapita kwao (watu wa Korintho) na kuwabariki kwa Mafundisho akaondoka, lakini alitaka tena kupita kwao kwa mara nyingine ya pili wakati anaelekea Makedonia ili wapate Baraka mara mbili.

Maisha ya Paulo yanatufundisha kuwa na bidii na jitihada katika kuifanya kazi ya Mungu, ijapokuwa Paulo alikuwa anapitia vita vikali katika kuhubiri, lakini mara zote alitafuta kurudia kuhubiri mahali ambapo ameshapita kuhubiri.

Matendo 15:36 “Baada ya siku kadha wa kadha Paulo akamwambia Barnaba, Haya! Mrejee sasa tukawaangalie hao ndugu katika kila mji tulipolihubiri neno la Bwana, wa hali gani”.

Bwana atusaidie na sisi tuwe kama watakatifu hawa wa kanisa la kwanza.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kama utapenda uwe unafikiwa na masomo ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP basi bofya hapa ujiunge moja kwa moja  >>>> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

KWANINI YESU NI ADAMU WA PILI?

Kuhubiri injili kwa husuda na fitina ndio kupi?

NA VIUNGO VYETU VISIVYO NA UZURI VINA UZURI ZAIDI SANA.

USIRUDI NYUMA KWA KUITUMAINIA HAKI YAKO.

Talanta ni nini katika biblia (Mathayo 25:14-30)

Rudi nyumbani

Kwanini kabla ya Kristo, miaka ilikuwa inahesabiwa kwa kurudi nyuma?

Nyakati zote kabla na hata baada ya Kristo miaka inahesabiwa kwa kwenda mbele, hakuna wakati wowote au kipindi chochote miaka ilihesabiwa kwa kurudi nyuma.

Litakuwa ni jambo lisilo la kiakili kama miaka itahesabiwa kwa kurudi nyuma..yaani kwa mfano leo ni mwaka 2021 halafu mwakani iwe mwaka 2020 badala ya 2022.

Sasa kama ni hivyo tunaweza kujiuliza ni kwanini, miaka ya nyuma inaonekana kama inahesabika kwa kurudi nyuma?.

Ili tuelewe vizuri hilo hebu tujifunze katika huu mfano mdogo.

Tuseme mwaka 2019 kulitokea janga kubwa la dunia la Korona lililobadilisha mfumo mzima wa maisha ya walimwengu.

Na kisha mtu mmoja akataka kurejea  tukio fulani lililotokea mwaka2015 ambapo kulitokea janga la kimbunga,na akasema.. “miaka 4 kabla ya Korona kuzuka duniani, kulitokea kimbunga kikubwa kikaharibu miundo mbinu”.

Na mwingine labda akataka kurejea tukio lililotokea mwaka 1978, wakati Tanganyika inapigana na Idd Amini wa Uganda, badala ya kusema mwaka 1978 kulitokea vita, akasema miaka 41, kabla ya janga la korona (41Kk) kulitokea vita kati ya Tanganyika na Uganda, vilivyogharimu uhai wa watu wengi.

Vile vile mtu mwingine labda akataka kurejea vita vya pili vya dunia vilivyotokea mwaka 1945, hivyo badala ya kutaja huo mwaka 1945 akasema, miaka 74 kabla ya Korona,(74kk) ilitokea vita kubwa sana ya dunia iliyogharimu maisha ya watu wengi..

Tuseme na mwingine akataka kurejeatukio la ajali lililotokea mwaka 2021, hivyo badala ya kusema mwaka 2021 kulitokea ajali mbaya sana, akasema miaka miwili baada ya Korona kuzuka duniani(2Bk), kulitokea ajali mbaya sana. N.k hiyo ni mifano tu.

Sasa kwa kusema hivyo haimaanishi, kwamba kuanzia mwaka huo wa 2019 janga la Korona lilipotokea kushuka chini, miaka ilikuwa inahesabiwa kwa kurudi nyuma.

La! Miaka ilikuwa inahesabiwa kwa kupanda, lakini kwasababu kulitokea tukio kubwa na maarufu mwaka 2019 ikabidi kalenda ibadilike, matukio yote ya nyuma yatajwe kwa kurejea tukio fulani kubwa lililowahi kutokea.

Kadhalika Kuzaliwa kwa MKUU WA UZIMA, NA MWANZILISHI WA MAMBO YOTE, YESU KRISTO. Ni lazima dunia itetemeke, tarehe haziwezi kubaki vile vile, majira hayawezi kubaki vile vile, kadhalika na kuzimu haiwezi kubaki vile vile. Ni lazima mabadiliko makubwa yaambatane na kuzaliwa kwake, kwasababu kitu alichokileta ulimwenguni ni kikubwa, Damu yake iliyomwagika pale Kalvari, imeleta mageuzi makubwa katika ulimwengu wa mwili na roho.

Maandiko yanasema..Kristo alikuja kuutangaza MWAKA WA BWANA uliokubaliwa (Isaya 61:1-2). Hivyo haiwezekani “aje autangaze mwaka wa Bwana” halafu tarehe zibaki vile vile. Ni lazima tu matukio yote ya kabla au baada yarejee kuzaliwa kwake.

Isaya 61:1 “Roho ya Bwana MUNGU i juu yangu; kwa sababu BWANA amenitia mafuta niwahubiri wanyenyekevu habari njema….

2 Kutangaza mwaka wa BWANA uliokubaliwa, na siku ya kisasi cha Mungu wetu; kuwafariji wote waliao”.

Bwana Yesu amekuwa Jiwe kuu la pembeni, Jiwe la kurejea..Korona imetikisa dunia lakini bado haijaweza kubadilisha majira, wapo wanadamu waliokuwa maarufu lakini hawajabadili majira, wamekuja na kupita, ni mkuu wa Uzima (Yesu), pekee yake ndiye ambaye mpaka leo, alama yake ipo katika kila mwanzo wa barua, mwanzo wa siku, na miezi na Miaka. Kuonesha kwamba yupo hai mpaka sasa hivi, na hakuna aliyemzidi,  leo hii hakuna mahali utakwenda usilisikie jina la Yesu likitajwa.

Na kama jinsi yeye alivyokuwa nguzo ya kurejewa, atabaki kuwa hivyo hivyo milele.

Je! Umemwamini leo?.. Umetubu dhambi zako kwa kumaanisha kuziacha?, umebatizwa katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Yesu upate ondoleo la dhambi zako?. Kama bado ni vyema ukafanya hivyo leo, maadamu mlango wa neema upo wazi, siku utakapofungwa kutakuwa hakuna nafasi tena ya kutubu.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

TABIA YA WAZI INAYOWATOFAUTISHA MANABII WA UONGO NA WALE WA UKWELI.

BIBLIA INAITAJA NJIA KUU YA MFALME, NJIA HII NI IPI?

Jiepushe na tamaa ya Mali/kupenda fedha.

USITAZAME NYUMA!

SI MAPEPO YOTE NI YA KULIPUKA.

Rudi nyumbani

Amwimbiaye nyimbo mtu mwenye moyo mzito.

Mithali 25: 20 “Amwimbiaye nyimbo mtu mwenye moyo mzito, Ni kama yeye avuaye nguo wakati wa baridi; Ni kama siki juu ya magadi”.

Anaposema amwimbiaye nyimbo..anamaanisha nyimbo za furaha, au za shangwe kumwimbia mtu mwenye moyo mzito, kwa kudhania kuwa ndio zitatuliza uchungu wake, kumbe kinyume chake, ndio zinamwongezea masikitiko moyoni mwake.

Sulemani kwa hekima ya ki-Mungu aliliona hilo, kwamba, ni vema kuendana na hisia za mtu, kwamfano, kuna watu wapo katika uchungu mzito sana mioyoni mwao, pengine labda wa kufiwa  na mume/mke wake, au mzazi wake, au ndugu yake wa karibu sana, na wewe kwa mawazo yako ukaona ili kuwatuliza ni kwenda kuwachekesha, chekesha, au kuwaburudisha kwa nyimbo za furaha,..Ujue kuwa hapo hautatui tatizo. Ni lazima ujue hali ya mtu wakati huo, yupo katika uchungu wa namna gani.

Biblia inasema..

Warumi 12:15 “Furahini pamoja nao wafurahio; lieni pamoja nao waliao”.

Lakini kama unaonyesha kufurahi pamoja na hao walioa, ukidhani ndio kiashiria cha kuwachangamsha..Ni rahisi kuwasha moto mwingine,

Kwasababu mtu Yule anaweza kudhani hujathamini hata kile anachokipitia, na matokeo yake atachukia badala ya kupona,..Ni ndio hapo anasema sawa na kumvua mtu nguo zake wakati wa baridi kali, ni nini kinatokea? Ni mateso zaidi kama sio kifo.

Kwahiyo tuwe na hekima ya kujua ni dawa ipi tunaitumia kumponya mtu aliyevunjika moyo. Ikiwa kweli anahitaji, furaja za nyimbo tutumie hizo, lakini kama yupo katika uchungu mwingi sana wa moyo, tuendane na hisia zake, hiyo ndio dawa pekee ya kuwaponya watu kama hao.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

SIFONGO NA SIKI NI NINI?

Nini maana ya Mungu amemfanya mwanadamu mnyofu?

Kuwaogopa wanadamu huleta mtego,(Mithali 29:25)

 Nini maana ya “Uchungu wa mauti ni dhambi, na nguvu za dhambi ni torati”

Zaburi maana yake nini, katika Biblia?

NGUVU ZA ZAMANI ZIJAZO:

Rudi nyumbani

SABATO ILIFANYIKA KWAAJILI YA MWANADAMU NA SI MWANADAMU KWAAJILI YA SABATO!

Lengo la Mungu kuwapa watu amri ya kuitunza sabato lilikuwa ni tofauti na lilivyochukuliwa au kutafsiriwa.Tuchukue mfano wa kawaida wa kimaisha…

Kikawaida, kila mtu ni lazima katika siku moja anao muda wa kulala (kupumzika), ili mwili wake uwe katika ustawi bora, hakuna mtu asiyelala kabisa.Hivyo ni sawa na kusema usingizi umeumbwa kwa ajili yetu sisi, ili tupate kuwa na afya bora na sio sisi tumeumbwa tuutumikie usingizi.
Kwa mantiki hiyo basi, ingawa tuna sheria ya kulala kila siku, lakini hatuna sheria ya muda wa kulala au wakati wa kulala.

Wengine watalala kuanzia saa 3 usiku na kuamka saa 11 alfajiri ili kuwahi shughuli zao..hivyo wakawa wamelala masaa 8.

Wengine wataanza kulala kuanzia saa 6 usiku na kuamka saa 2 asubuhi na wakawa wamelala masaa yaleyale 8..wengine hawatalala kabisa usiku bali watalala mchana..

Hao wote wametimiza sheria ya kulala,ilitowekwa na Mungu, hakuna hata mmoja aliyeivunja..isipokuwa kila mtu kaitimiza kwa wakati wake aliouona unafaa.

Hivyo muda wa kulala haujalishi kinachojalisha ni masaa na matokeo baada ya kulala..kwamba wote mtalala na miili itakuwa imepumzika..Na usipolala mwili wenyewe utakutumia taarifa ya deni la usingizi, hivyo hilo deni utalilipa tu, na taarifa hiyo sio Mungu anayekutumia bali ni mwili ndio unaokutumia.

Lakini sasa inapotokea kwamba ni amri kwamba kila saa 3 usiku mpaka saa 11 asubuhi watu wote wawe vitandani wamelala, hapo tutakuwa tunauabudu usingizi, tutakuwa ni watumwa wa usingizi, na tutakuwa wajinga na maana ya kulala itakuwa imepotea kabisa.

Kwasababu kuna wakati itakubidi uwahi kulala ili uwahi kuamka, kuna kipindi utachelewa kulala kutokana na dharura za kimaisha na hivyo utajikuta unachelewa kuamka pia, kuna wakati utaugua utakuwa kitandani muda wote, au usiwe unapata usingizi kabisa..Hivyo usingizi upo lakini ni sisi ndio tunaouendesha na sio wenyewe unatuendesha sisi..Hatuwi watumwa wa usingizi!

Na Sabato ni hivyo hivyo..

Maandiko yanasema Sabato ilifanyika kwaajili yetu na sio sisi kwaajili ya sabato.

Marko 2:27 “Akawaambia, Sabato ilifanyika kwa ajili ya mwanadamu, si mwanadamu kwa ajili ya sabato”

Mungu aliiweka sabato ili tupumzike tupate muda wa kumtafakari yeye, na kutengeneza mambo yetu ya kiroho katika wiki inatofuata mbele yetu, kama vile usingizi ulivyowekwa kwamba tupumzike ili miili yetu istawi, ipate nafasi ya kujitengeneza upya kwaajili ya kuiendea siku inayofuata.
Hivyo ni kweli tumepewa amri ya kuishika sabato, lakini hiyo hatuishiki kwa kanuni fulani maalumu, kwamba ni lazima iwe ni kila jumamosi, kiasi kwamba mtu ukiabudu siku tofauti na hiyo ni kosa!…au kwamba ni lazima iwe kila jumapili kiasi kwamba mtu akiabudi jumamosi ni kosa, hapo tutakuwa hatujaelewa maana ya Sabato!.

Hivyo siku ya Bwana ni chaguzi wetu, kwamba siku ipi ni bora kwetu, kama ni jumamosi, au jumapili, au jumatatu, au jumanne au siku nyingine yeyote maadamu, katika hiyo tutaifanya siku nzima iwe takatifu kwa Bwana.

Kulingana na mfumo wa kalenda ya nchi yetu, siku ambazo hazina masumbufu ni jumamosi na jumapili, hizo ni siku ambazo ni nzuri kuzifanya kuwa za Bwana, lakini pia sio amri, hata jumanne ni siku iliyokubalika, hata jumatano, lakini shida ya siku hizo ni kwamba zina masimbufu mengi ya kimaisha, hivyo ni ngumu kuzitakasa.

Mataifa ya kiarabu, siku ya ijumaa ndio siku isiyo na masumbufu kwao, kama vile ilivyo jumapili na jumamosi kwetu, kwao ni ijumaa…hivyo siku kama hiyo kulingana na kalenda za mataifa hayo ni vizuri kuifanya siku ya Bwana iwe Ijumaa kuliko jumapili au jumamosi kwasababu, siku ya jumapili ni sheria watu wao kwenda makazini kama kawaida tofauti na huku kwetu.

Ni jambo la aibu mkristo kushindania siku ya kuabudu.
Utakuta mtu hafahamu kitu kingine chochote zaidi ya kushabikia jumamosi au jumapili. Mtu kama huyo anakuwa hana tofauti na mtu anayeshabikia muda wa kulala.

Bwana atupe macho ya kuyaona haya, na tutokane na upofu huo, ambao unaufanya ukristo usieleweke kwa watu waliopo nje.

1 Wakorintho 14:40 “Lakini mambo yote na yatendeke kwa uzuri na kwa utaratibu”

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Neno Saumu lina maana gani katika biblia?

IMESALIA RAHA YA SABATO KWA WATU WA MUNGU.

TUSIRUHUSU MAMBO YA KUSUBIRISHA, YAVURUGE MUDA WETU NA MUNGU.

Neno Saumu lina maana gani katika biblia?

Sabato halisi ni lini, Je! ni Jumapili au Jumamosi?, Ni siku gani itupasayo kuabudu?

Rudi nyumbani