Mintarafu ni nini?

Mintarafu ni nini?

Maana ya neno “Mintarafu” ni “kuhusiana na”. Kwamfano ukitaka kutamka sentesi hii >> “sifahamu chochote kuhusiana na ujio wa pili wa Kristo” …. unaweza kusema… “Sifahamu chochote mintarafu ujio wa pili wa Kristo”..Hivyo neno mintarafu linasimama kuwakilisha neno “kuhusiana na”.

Katika biblia takatifu yenye vitabu 66, neno hilo limeonekana mara mbili tu. Na mara zote hizo mbili ni ndani ya kitabu kimoja cha Zaburi.

Zaburi 17:4 “Mintarafu matendo ya wanadamu; Kwa neno la midomo yako Nimejiepusha na njia za wenye jeuri.

5 Nyayo zangu zimeshikamana na njia zako, Hatua zangu hazikuondoshwa”.

Na pia tunasoma katika..

Zaburi 87: 5 “Naam, mintarafu Sayuni itasemwa, Huyu na huyu alizaliwa humo. Na Yeye Aliye juu Ataufanya imara.  6 Bwana atahesabu, awaandikapo mataifa, Huyu alizaliwa humo”.

Hivyo ndugu, kama hufahamu chochote kuhusiana na ujio wa pili wa Kristo, basi fahamu kuwa upo hatarini sana, ni vyema ukatafuta kwa bidii kujua saa, nyakati na majira tunayoishi.

Hizi ni siku za mwisho na Kristo yupo mlangoni. Je umejiandaa?

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

NAMNA YA KUITAMBUA SAUTI YA MUNGU INAPOZUNGUMZA NA WEWE

UFUNUO: Mlango wa 19

CHUKIZO LA UHARIBIFU

NA VIUNGO VYETU VISIVYO NA UZURI VINA UZURI ZAIDI SANA.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments