Category Archive Home

Nini maana ya ”Mizani ya hadaa ni chukizo kwa Bwana”?

Je! katika biblia mstari huu una maana gani? ”Mizani ya hadaa ni chukizo kwa Bwana Bali vipimo vilivyo sawasawa humpendeza’’? (Mithali 11:1)? ..Hiyo mizani ya hadaa ni ipi?


JIBU: Katika maisha ya kawaida Bwana anataka tuwe na haki, katika mambo yetu tunayoyafanya kila siku iwe ni katika biashara zetu au kazi zetu…Unapouza kitu uza kulingana na thamani ya kitu chenyewe unachouza, usizidishe thamani ya kitu kile ili upate faida kubwa vile vile usipunguze kipimo cha kitu kile ili upate faida kubwa…

USIPANDISHE THAMANI.

Kwa mfano kama wewe ni muuzaji wa mchele, na umenunua kilo moja kwa shilingi elfu mbili, na bei inayoziwa sokoni ni shilingi elfu na mia tano kwa wateja…Na unajua kabisa faida yako inapaswa iwe ni shilingi mia tano kwa kila kilo, au ikizidi sana mia 7.

Lakini wewe unakwenda kuuza kwa bei ya juu kuliko inavyotakiwa ili wewe upate faida kubwa bila kujali kuwa unamkandamiza yule unaye muuzia kisa tu anaouhitaji mkubwa wa kitu hicho..Labla tuseme unauuza mchele ule kwa shilingi elfu 4 kwa kilo moja..Hivyo kwa kufanya hivyo, Ni machukizo kwa Bwana. Hiyo ni mizani ya hadaa, hutendi haki.

USIPUNGUZE KIPIMO;

Vilevile Bwana hapendezwi na kupunguza kipimo cha bidhaa ile kwa hila, kwamfano unapunguza kwa makusudi kiwango cha upimaji, aidha katika mizani yako ili usiuze kingi upate faida kubwa..Hilo nalo ni chukizo kwa Bwana…Hiyo nayo ni mizani ya hadaa, hutendi haki.

Vilevile katika kazi nyingine zote tunazozifanya iwe ni kwa Mungu, au mashuleni, au  mahakamani, tunapaswa tuamue kwa haki bila kumpendelea mtu, kwa kutokujali fedha, au heshima, au cheo, au jinsia,..Bwana anapenda haki, na palipo na haki ndipo kiti chake cha enzi kilipo…..(Zaburi 97:2)

Zaburi 89: 14 Haki na hukumu ndio msingi wa kiti chako, Fadhili na kweli zahudhuria mbele za uso wako.

Na ndio maana biblia inasema .. Basi ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu. (Mathayo 5:48)

Bwana akubariki.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

TWEKA MPAKA VILINDINI.

WALIO NA HEKIMA NDIO WATAKAOELEWA.

UNYAKUO.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Rudi Nyumbani:

Print this post

NITAFUNGUAJE MILANGO ILIYOFUNGWA MBELE YANGU?

Nifanye nini ili niifungue milango iliyofungwa mbele yangu?

Jina la Bwana Yesu Kristo libarikiwe. Moja ya mada inayozungumzwa na wakristo wengi hususani wa kanisa hili la Mwisho ni juu ya namna ya kufungua milango iliyofungwa mbele yetu.

Na kwa haraka haraka wengi wetu tunatafuta njia za haraka haraka ilimradi tu, Milango iliyopo mbele yetu ifunguke. Ndio hapo utaona baadhi wanaenda kwa watumishi wawaombee, wengine watatafuta mahali panapouzwa Mafuta fulani, au maji fulani ya baraka au upako. Wengine watakwenda kutafuta kwa kuombewa nyota zao na kutabiriwa. Na mambo mengine mengi yanafanyika katikati ya wakristo. Na Bahati mbaya wengi baada ya kufanya hivyo hali inabakia kuwa vile vile. Ni kwanini?. Ni kwasababu hiyo sio njia au Namna Mungu aliyoiweka ya kufungua milango iliyofungwa mbele yetu.

Biblia inasema katika..

Ayubu 22:21 “Mjue sana Mungu, ili uwe na amani; Ndivyo mema yatakavyokujia.”

Kumjua Mungu maana yake ni kutafuta maarifa ya kujua ni nini Mungu anataka, Yakikosekana maarifa ya kumjua Mungu ni rahisi sana kuangamia.

Sasa leo kwa ufupi sana tutatumia biblia kujua namna yakufungua milango iliyopo mbele zetu. Na pia kumbuka kabla ya yote kuwa sio kila mlango uliofungwa mbele yako. Ni shetani kahusika! Hapana mingine ni Mungu mwenyewe kaifunga kwaajili ya makusudi yake. Na tunajua makusudi ya Mungu siku zote ni Mema. Hivyo tutazungumzia kwa ujumla namna ya kufungua milango yote (Iliyofungwa na Mungu au shetani)

Tusome.

Ufunuo 3:7 “Na kwa malaika wa kanisa lililoko Filadelfia andika; Haya ndiyo anenayo yeye aliye mtakatifu, aliye wa kweli, aliye na ufunguo wa Daudi, yeye mwenye kufungua wala hapana afungaye, naye afunga wala hapana afunguaye.

8 Nayajua matendo yako. Tazama, nimekupa mlango uliofunguliwa mbele yako, ambao hapana awezaye kuufunga, KWA KUWA UNAZO NGUVU KIDOGO, NAWE UMELITUNZA NENO LANGU, WALA HUKULIKANA JINA LANGU”.

Kwanza tunaona hapo kumbe Kristo anaweza kufunga kitu na hakuna awezaye kukifungua..Na pia anauwezo wa kufungua na hakuna awezaye kuufunga. (Hiyo ni point ya kwanza ya kuweka akilini). Ili tufahamu kuwa sio kila mlango uliofungwa mbele yetu ni shetani kahusika. Hapana bali mengine ni Kristo mwenyewe ndiye aliyehusika.

Lakini tukiendelea na mstari wa 8 ndio tutapata majibu ya swali letu. “Tutafunguaje milango iliyofungwa mbele yetu?”.

Bwana Yesu mwenye ufunguo wa mambo yote anaanza kwa kusema…Nayajua matendo yako!. Ikifunua kuwa mlango kufunguliwa au kufungwa unahusiana na “Matendo ya Mtu”..Anaendelea na kusema “nimekupa mlango uliofunguliwa mbele yako, ambao hapana awezaye kuufunga, KWA KUWA UNAZO NGUVU KIDOGO, NAWE UMELITUNZA NENO LANGU, WALA HUKULIKANA JINA LANGU”

Umeona sababu za huyu mtu kufunguliwa mlango?. Sababu zipo tatu.

Ya kwanza Kwa kuwa anazo nguvu kidogo. Ya pili Kwa kuwa amelitunza Neno lake. Na ya tatu Hakulikana jina lake.

Kristo hajabadilika sababu zile zile alizozitumia kale ndizo anazozitumia leo kufungua milango iliyofungwa mbele yetu.

Ni lazima kwanza tuwe na nguvu za rohoni. Biblia inasema.

1 Yohana 2: 14 “….Nimewaandikia ninyi, vijana, kwa sababu mna nguvu, na Neno la Mungu linakaa ndani yenu, nanyi mmemshinda yule mwovu”. Kuliweka Neno la Mungu ndani yetu ndio NGUVU ZA ROHONI. Mtu asiye na Neno la Mungu ndani yake, nguvu zake za rohoni zipo chini sana. Na kumbuka kuliweka Neno moyoni sio kujua vifungu vingi vya Biblia, kwa kuikariri. Hapana bali kuliweka Neno la Mungu moyoni ni kuliishi Neno moja lililoandikwa katika biblia. Ni kuona matokeo ya lile Neno katika maisha yako.

Kwamfano biblia inaposema “wapendeni Adui zenu, waombeeni wanaowaudhi..Mathayo 5:44”. Kama mtu kaushika huo mstari kwa kuukariri na hautendei kazi hicho kilichoandikwa hapo. Mtu huyo hajalishika Neno la Mungu moyoni mwake, lakini kama anakitendea kazi kwa kuwaombea wengine huyo kaliweka moyoni Neno la Mungu.

2) Sababu ya Pili ya Kufunguliwa mlango. Ni kwa kulitunza NENO LA MUNGU.

Kulitunza ni tofauti kidogo na kuliishi. Kulitunza maana yake unalitenda lile Neno kila siku katika maisha. Sio leo unalitenda kesho unaliacha.

3) Na sababu ya tatu na ya mwisho ni Kutolikana JINA lake.

Maana yake ni kutoikana Imani. Kulikana jina la Mungu na kuikana Imani ni kitu kimoja. Kuikana Imani kunajumuisha kurudi nyuma kiimani. Petro alimkana Bwana Yesu maana yake alirudi nyuma kiimani. Kadhalika mtu anayerudi nyuma kiimani ni sababu tosha ya kujifungia milango ya Baraka mbele yake.

Ndugu hatupaswi kukimbilia maji ya Upako kupata kibali mbele yetu. Au kupata fursa Fulani mbele yetu. Njia pekee ya kupata fursa ya kitu Fulani ni kurekebisha MATENDO YETU na KULITUNZA NENO LA MUNGU maishani mwetu. Na ndipo hayo yote yaliyosalia uliyokuwa unamwomba Mungu yanafunguka.

Kama ulikuwa hujampa Kristo maisha yako, unageuka sasa kwa kudhamiria kuacha dhambi kabisa. Na humfuati kwasababu tu unataka fursa Fulani. Hapana bali kwasababu umejigundua wewe ni mwenye dhambi na unahitaji kubadilishwa. Na Kristo mwenyewe anapenda watu wanaotubu dhambi zao na kukiri kuwa ni wakosaji. Yeye anawapa msamaha bure wote wanaokimbilia kwake haijalishi wameasi kiasi gani. Na baada ya kupata msamaha huo ambao utaambatana na AMANI Fulani moyoni isiyokuwa ya kawaida. Moja kwa moja usikawie nenda kakamilishe wokovu wako kwa kubatizwa katika maji tele(Yohana 3:23) na kwa jina la Yesu kulingana na (Matendo 2:38). Na Bwana mwenyewe atakupa kipawa cha Roho wake Mtakatifu ambaye atakuongoza katika kuijua kweli yote ya maandiko na kukusaidia kushinda dhambi ambazo ulikuwa huwezi kuzishinda kwa nguvu zako.

Hapo utakuwa umeokoka kwa kuzaliwa mara ya pili. Na utakuwa na tumaini la uzima wa milele. Na kwasababu umeupata kwanza ufalme wa Mungu na Haki yake. Na hizo fursa na milango iliyofungwa ambayo umekuwa ukiitabikia kwa muda mrefu itafunguka yenyewe pasipo stika wala chumvi.

Bwana akubariki,jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

DANIELI: Mlango wa 2

MIHURI SABA

USIPOLITENDEA KAZI NENO LA MUNGU.

Inaruhusiwa Kula nyama ya Nguruwe kwa Mkristo wa Kweli?

Rudi Nyumbani:

Print this post

NAMNA YA KUMTAMBUA BIBI ARUSI WA KWELI WA KRISTO.

Nitamtambuaje bibi arusi wa kweli?

Shalom.

Ni vizuri tukafahamu kuwa katika ukristo yapo makundi matatu ya waaminio. Tukilielewa hilo itatusaidia sisi kujipima tupo katika kundi lipi. Na hatua zipi tuchukue ili tusimame katika upande salama.

kundi la kwanza:

Ni kundi la watu wanaojiita wakristo, hawa wanaweza wakawa wamezaliwa katika familia za kikristo au walioupokea ukristo kama dini yao mpya tu,. Au kama kitambulisho chao tu, Na kuwatambua hawa ni rahisi, huwa hawana habari na Mungu hata kidogo, kinachowatofautisha tu wao na ulimwengu ni hicho kitambulisho cha kikisto walichozaliwa nacho au walichokipokea basi.

Lakini mambo mengine yote yaliyosalia hayana tofuati na watu wengine wote wasiomjua Mungu, ukimuuliza Je! unajua kama unyakuo upo karibu atakwambia sifahamu unazungumzia nini. Ukimuuliza Je umeokoka atakwambia hiyo dini siijui..hana habari na ibada wala, wala kitu chochote cha ki-Mungu yupo tu, kama wapagani, lakini anajivunia ukristo wake. Na hawa wapo wengi sana.

Kundi la Pili:

Ni kundi la wakisto ambao wanaamini kila kitu, wanafahamu kila habari katika maandiko. Wanahudhuria ibadan, lakini ni vuguvugu, nusu kwa Mungu, nusu kwa shetani, Biblia inawafananisha hawa na wale wanawali wapumbavu tunaowasoma katika Mathayo 25..Na kwa jina lingine wanajulikana kama Masuria, hawana muunganiko rasmi na Kristo.

Hawa ndio siku ile watakapojigundua wameachwa katika unyakuo ndio watakaolia n kuomboleza, kwasababu nao pia walikuwa wanamtazamia Kristo lakini kwasababu ya kuwa vuguvugu, wataachwa..Na hawa pia wapo wengi katika kanisa.

Kundi la Tatu:

Ni Wakristo ambao wamedhamiria kweli kuifuata njia ya Kristo. Ukristo sio dini yao, bali ni Imani yao. Hawa ndio wale wanawali werevu waliotwaa taa zao pamoja na mafuta ya ziada katika vyombo vyao vya pembeni..Na hawa ndio bibi arusi wa Kristo, ambao Kristo anawaandaa katika kila kipindi cha Kanisa..Na hawa ni wachache sana katika Kanisa.

Jambo la muhimu la kufahamu ni kuwa kati ya haya makundi matatu ya wanaojiita wakristo, ni kundi moja tu ndilo litakalonyakuliwa kwenda mbinguni..Nalo ndio hilo kundi la tatu. Bwana YESU leo hii hatafuti Masuria, wala watu walio baridi, bali anamwandaa bibi arusi wake haijalishi atakuwa ni mmoja au mia au elfu hilo halijalishi idadi yake ikishatimia haangalii ulimwengu mzima unafikiri vipi. Watanyakuliwa na kwenda mbinguni kwenye karamu ya mwana kondoo

Sasa kwa ufupi embu tuangalie ni kwa namna gani tunaweza kumtambua bibi arusi wa kweli wa Kristo.

Kama wengi wetu tunavyofahamu Ile habari ya Ibrahimu kwenda kumtafutia mwanawe Isaka mke katika nyumba ya baba yake. Ni habari inayofunua siri ya Kristo na bibi arusi wake jinsi atakavyompata katika siku za mwisho. Sasa tukisoma ile habari tunaona ulifika wakati Ibrahimu aliona mwanawe Isaka ameshakuwa mtu mzima. Na mama yake ameshafariki,hana mtu wa kumfariji, akaona ni vema akamtafutie mwanawe binti wa kuoa,..Ndipo akamtuma mtumwa wake alimwamini sana katika mali zake zote aliyeitwa Eliezeri afunge safari pamoja na Ngamia 10 watoke katika nchi ya Kaanani waende mpaka Mesopotamia nchi ya Baba yake,..asafiri umbali mrefu kusudi tu ampatie mwanawe mke aliye bora…

Na Ndivyo Mungu alivyofanya kwa mwanawe mpendwa YESU KRISTO, Hakumtafutia bibi Arusi wake safi kutoka katika kanisa la Israeli badala yake alikuja mbali kwa watu wa mataifa yaani mimi na wewe ili kututwaa tuwe pamoja naye katika kiti chake cha enzi..

Safari ya kwenda kumtafuta Bibi arusi.

Sasa Eliezeri akafunga safari mamia kwa mamia ya kilometa akiwa na ngamia zake 10 pengine alitumia wiki kadhaa au miezi kusafiri. Ndipo akafika karibu na nchi ile, nje kidogo na mji ambapo pana kisima cha maji ambapo mabinti wengi wa mji wanakitumia wakati wa jioni kuja kutweka maji. Kwa ajili ya shughuli za nyumbani.

Kama tunavyosoma habari ile, Eliezeri alimwomba Mungu ishara, akasema binti Yule nitakayemwomba maji ya kunywa katika mtungi wake, na kusema sitakupa tu wewe bali nitanyesha mpaka na ngamia zako basi huyo na awe mke wa mwana wa bwana wangu..Biblia inatuambia wakati wazo hilo bado lipo katika kichwa chake muda huo huo akatokea binti pale kisimani, kuchota maji tusome..

Mathayo 24:12-20.

Mwanzo 24: 12 “Naye akasema, Ee Bwana, Mungu wa bwana wangu Ibrahimu, nakuomba mambo yangu uyajalie yawe heri leo, ukamfadhili bwana wangu Ibrahimu.

13 Tazama! Nimesimama karibu na kisima cha maji, na binti za watu wa mjini wanatoka kuteka maji,

14 basi na iwe hivi; yule msichana nitakayemwambia, Tua mtungi wako, nakuomba, ninywe; naye akasema, Unywe, nami nitawanywesha na ngamia zako pia; basi huyu na awe ndiye uliyemchagulia mtumishi wako Isaka; na kwa hayo nitajua ya kuwa umemfadhili bwana wangu.

15 Ikawa, kabla hajaisha kunena, tazama, Rebeka anatokea, binti wa Bethueli mwana wa Milka, mkewe Nahori, ndugu wa Ibrahimu, naye ana mtungi begani pake.

16 Naye yule msichana alikuwa mzuri sana uso wake, bikira, wala mwanamume hajamjua bado; akashuka kisimani, akajaza mtungi wake, akapanda.

17 Ndipo yule mtumishi akapiga mbio kwenda kumlaki, akasema, Tafadhali unipe maji kidogo katika mtungi wako ninywe.

18 Naye akasema, Unywe, bwana wangu, akafanya haraka, akatua mtungi wake mkononi mwake, akamnywesha.

19 Hata alipokwisha kumnywesha akasema, Na ngamia zako nitawatekea, hata watakapokwisha kunywa.

20 Akafanya haraka, akamwaga maji ya mtungi wake katika birika, akapiga mbio kisimani ateke, akawatekea ngamia zake wote”.

Zoezi la kunywesha Ngamia 10.

Ukiendelea kusoma utaona Yule mtu ndipo alipopata uhakika kuwa huyu binti ndiye Mungu aliyemkusudia kuwa bibi arusi wa Isaka. Ni rahisi kuona kama alimwomba Mungu ampe ishara nyepesi, lakini ile haikuwa ishara ndogo kama ukichunguza vizuri, kwa mazingira yale yaliyokuwepo.

Embu jaribu kufikiria Yule alikuwa ni mtoto wa kike, pili alikuwa na mtungi mmoja tu mdogo labda tuseme wa lita 10 ambayo ni sawa na ndoo moja ya maji. Na unaambiwa ngamia ni mnyama anayekunywa maji haraka sana zaidi ya wanyama wengi, ndani ya dakika tatu tu tayari kashamaliza lita 200 za maji..Hivyo ilihitajika mitungi/ndoo 20 za maji kukata kiu ya ngamia mmoja..Ukizingatia ngamia walikuwa 10 pale, hivyo kama ni kuwanyeshwa ngamia basi inakugharimu si chini ya ndoo 200, kushuka kisima na kupanda kuwashibisha ngamia wote..Hilo sio zoezi ndogo..

Kwa wakati ule ilikuwa ni rahisi sana kusaidiwa kunyeshwa kondoo zako 100 za maji na mbuzi zako lakini si ngamia. Tena ilikuwa inafanywa na wanaume si wanawake..Hivyo Eliezeri kumwomba Mungu ishara kama ile, alitambua kabisa kwa namna ya kawaida ni kama haiwezekani…Lakini msichana Rebeka hakujali hilo, kwa jinsi roho ya kujali ilivyokuwa imejaa ndani yake.

Alikwenda hivyo hivyo alishuka kisimani, akapanda mpaka mitungi yote mia mbili akaimaliza. Na Eliezeri hakufanya chochote, wala hakumsaidia bali alikuwa anamwangalia tu, labda kama atakata tamaa katikati ya safari, aseme sio huyo, asubirie mwingine kuja kuchota maji lakini Rebeka alichota maji ndoo zote labda 200 mpaka akamaliza..

Je! jiulize wewe binti wa kike unaweza ukafanya ukarimu kama huo kwa mtu usiyemjua ikiwa tu kumpisha mzee kwenye daladala ni shida itakuwaje kwa kazi kama hiyo?. Hata kwa kulipwa tu unaweza usifanya..Na kumbuka Rebeka alikuwa ni mzuri wa uso sana, kuwazidi wengi. Lakini hakujali hilo.Hapo ndipo Eliezeri akapata uthibitisho sasa kuwa huyu Rebeka ndio bibi arusi mwenyewe..Ukiendelea kusoma habari utaona hadi alipochuliwa na kuletwa Kaanani kwa mume wake Isaka.

Lakini habari hiyo inafunua nini kwa kanisa la leo?.

Kumbuka Eliezeri anasimama kama kundi la watumishi wote wa Mungu ambao wametumwa ulimwenguni kote kuhubiri Injili. Kumtafutia Kristo bibi arusi safi wa kwenda naye mbinguni kwenye karamu ya mwana-kondoo.Kama Mtume Paulo anavyosema katika..

2Wakorintho 11: 2 “Maana nawaonea wivu, wivu wa Mungu; kwa kuwa naliwaposea mume mmoja, ili nimletee Kristo bikira safi”.

Na watumishi wa Mungu pia wamepewa ishara ya kuwatambua bibi Arusi hao, na Ishara yenyewe ni kama ile ya Rebeka..Ndugu Tukijiona tunahubiriwa injili lakini tunaishia tu kwenye kile tunachoambiwa, labda tuseme tutubu au tubatizwe , halafu baada ya hapo basi, hatuonyeshi bidii zetu binafsi za kuthibitisha wito wetu kwa Mungu..Basi tujue kuwa sisi bado sio bibi arusi wa Kristo.

Kama Sisi wenyewe binafsi hatutaki kumtafuta Mungu wetu atufundishe zaidi. Hatutaki kuomba wenyewe bila ya kushurutishwa, tunangojea tu tufundishwe biblia jumapili kwa jumapili sisi hatuna muda na mambo hayo tunaendelea na shughuli zetu. Basi tujue sisi tutakuwa ni Masuria tu, wale wanawali wapumbavu, Unyakuo utakapopita tutabaki hapo..

Bibi arusi kama Rebeka haridhiki na hali ile ile aliyopo kwa muda mrefu, anafanya zaidi ya yale anayoelekezwa na kuambiwa. Soma habari ile ya wanawali 10 utaona wale werevu walijiongeza, kutafuta mafuta ya ziada kwa ajili ya TAA zao. Kwasababu walijua yale pekee hayawatoshi. Usitegemee kuhubiriwa tu peke yake.

Ndugu hizi ni siku za hatari, watakaonyakuliwa ni wachache sana, tuombe Mungu na vilevile tuongezee bidii zetu binafsi ili tustahili kuwa miongoni mwa bibi arusi wa Kweli wa Kristo.

Bwana akubariki sana.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

UNYAKUO.

KARAMU YA MWANA-KONDOO.

Biblia inamaanisha nini kusema Yeye aliye na sikio, na asikie?

UNATAKA KUBARIKIWA? BASI USIKWEPE GHARAMA ZAKE.

Rudi Nyumbani:

Print this post

INGIENI KWA KUPITIA MLANGO ULIO MWEMBAMBA.

Tuingie kwa kupitia mlango ulio mwembamba. Shalom. Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe. Karibu tuyatafakari pamoja maandiko…Bwana Yesu alisema maneno yafuatayo katika kitabu cha Luka..

Luka 13:22 “Naye alikuwa akipita katika miji na vijiji, akifundisha, katika safari yake kwenda Yerusalemu.

23 Mtu mmoja akamwuliza, Je! Bwana, watu wanaookolewa ni wachache? Akawaambia,

24 Jitahidini kuingia katika mlango ulio mwembamba, kwa maana nawaambia ya kwamba wengi watataka kuingia, wasiweze.

25 Wakati mwenye nyumba atakaposimama na kuufunga mlango, nanyi mkaanza kusimama nje na kuubisha mlango, mkisema, Ee Bwana, tufungulie; yeye atajibu na kuwaambia, Siwajui mtokako;

26 ndipo mtakapoanza kusema, Tulikula na kunywa mbele yako, nawe ulifundisha katika njia zetu.

27 Naye atasema, Nawaambia, Siwajui mtokako; ondokeni kwangu ninyi nyote mlio wafanyaji wa udhalimu”

Moja ya sentensi zinazoogopesha ambazo Bwana Yesu alizizungumza ni hii..Nyingine ni ile ya Mathayo 12:31 anayosema…“ Kwa sababu hiyo nawaambia, Kila dhambi na kila neno la kufuru watasamehewa wanadamu, ila kwa kumkufuru Roho hawatasamehewa.”

Na nyingine ya Tatu ni hii…

Mathayo 7:22 “Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?

23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu.

Sentensi hizi tatu alizozizungumza Bwana Yesu kama ukizitafakari kwa makini zinaogopesha sana..Sio za kuzichukulia kiwepesi wepesi kabisa.. Ni sentensi nzito sana. Na kama tunavyojua Bwana Yesu anachokisema siku zote ni lazima kije kutimia. Alimwambia Petro kabla Jogoo kuwika utanikana mara tatu…Na tunaona masaa machache tu mbeleni unabii huo ulitimia kama ulivyo. Kadhalika aliposema siku ile wengi watakuja na kumwambia Bwana Bwana hatukutoa pepo, hatukufanya unabii. Hatukufanya miujiza mingi kwa jina lako Ni kweli siku hiyo itafika na watakapokuja maelfu ya watu mbele zake na kusema hayo maneno hivyo hivyo.

Watakuwepo wahubiri wengi siku hiyo watakaosema maneno hayo mbele zake na Bwana atawakataa. Hivyo ni kujitahidi kuwa makini sana na kumwomba Bwana atusaidie siku zote hao watu wasiwe sisi. Kwasababu hakuna wa kusalimika hapo kama Neema yake haitahusika.

Lakini leo tutaitafakari sentensi hiyo ya kwanza ambayo alisema “Tujitahidi kuingia katika mlango ulio mwembamba”.

Tusome tena mahali pengine alipozungumza maneno hayo ili tupate picha Zaidi..

Luka 7:13 “Ingieni kwa kupitia mlango ulio mwembamba; maana mlango ni mpana, na njia ni pana iendayo upotevuni, nao ni wengi waingiao kwa mlango huo.

14 Bali mlango ni mwembamba, na njia imesonga iendayo uzimani, nao waionao ni wachache.

Hapo kuna vitu viwili NJIA na MLANGO..Na anasema njia ni nyembamba, maana yake hiyo huwezi kupita kwa kifaa chochote kama gari au pikipiki. Wala hamwezi kupita ukiwa na mizigo, wala hawezi kupita mkiwa makundi. Ni mtu mmoja mmoja, kwasababu . Ulishawahi kupita kichochoroni na gari? Au na pikipiki?. Au ulishawahi kupita kichochoroni mkiwa mmeshikana mikono watu sita au 7 kwa pamoja?. Ni wazi kuwa hicho kitu hakiwezekani. Kwasababu njia ni nyembamba. Inahitajika apite mmoja mmoja. Na tena akiwa hana mizigo mizigo.

Kadhalika njia ya wokovu, ni habari ya mtu mmoja mmoja. Sio mtu na mke wake. Au mtu na baba yake. Inahitajika mtu kujikana nafsi peke yake na kuamua kumfuata Yesu. Na pia tunapomfuata Yesu yeye ni njia nyembamba hauendi na dini yako. Wala dhehebu lako litakalokusaidia kupita katika huo uchochoro. Unaweka dhehebu lako pembeni, dini yako pembeni. Unachukua msalaba wako unamfuata kama ulivyo.

Na pia anasema “MLANGO NI MWEMBAMBA”.

Maana yake mwisho wa hiyo NJIA nyembamba ya uchochoro ulio mwembamba utakutana na mlango. Na huo mlango pia ni mwembamba vile vile kama hiyo NJIA. Hapo ndipo Bwana anatuambia tujitahidi. Uchochoro utapita bila gari, bila baiskeli, bila pikipiki lakini mlangoni je?.

Hapo Itakubidi upunguze hata mwili. Kwasababu pengine mwili wako ukiwa mkubwa sana unaweza ukakwama mlangoni. Hivyo ili uingie itahitajika hata upunguze baadhi ya viungo..Ndio maana Bwana Yesu alisema.

Kiungo chako kimoja kikikukosesha kikate, Ni heri uingie katika ufalme wa mbinguni ukiwa kilema kuliko kuwa mzima na kuishia jehanamu.

Mathayo 5:30 “Na mkono wako wa kuume ukikukosesha, ukate uutupe mbali nawe; kwa maana yakufaa kiungo chako kimoja kipotee wala mwili wako mzima usitupwe katika jehanum”.

Hizo ndizo gharama! Na sio rahisi zina ugumu wake ndio maana Bwana hapo juu kasema TUJITAHIDI! Maana yake tufanye bidii kwa hali na mali tupite mlangoni. Tukitia Nia yeye katuahidi kutusaidia katika (Mathayo 19:26).

Je ni mali zako ndio zinazokukosesha na kukuzuia wewe kumtafuta Mungu? Ziweke pembeni kwa muda. Mtafute Kwanza Mungu na hizo zitakutafuata zenyewe baadaye. Je ni ndugu ndio wanaokuzuia kumgeukia Mungu na kufanya mapenzi yake?. Ikumbuke njia ile ni Nyembamba haiwezekani kupita makundi. Bwana Yesu alisema “apendaye Baba au mama kuliko mimi hanifai (Mathayo 10:37)”. Waambie ndugu zako kwa upendo, sasa umeokoka umeamua kumfuata Yesu kwa gharama zote.

Chochote kile kinachotuzuia kuingia katika ufalme wa Mbinguni sasa tunapaswa tujiepushe nacho, ili tukidhi vigezo vya kuingia katika huo mlango ulio mwembamba. Na hatupaswi kukawia kwasababu pale juu amesema. Utafika wakati mlango huo mwembamba utafungwa..Na watu watatamani kuingia watashindwa. Maisha ya ukristo ni Maisha ya mapambano, lakini Bwana akiwa upande wetu hakuna linaloshindikana. Tutashinda na Zaidi ya kushinda. Tukimfanya yeye kuwa tegemeo letu.

Bwana akubariki sana.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali share na wengine.


Mada Nyinginezo:

Naomba kujua watakaoenda mbinguni je! ni wengi au wachache?

NAFASI YA MWANAMKE KATIKA KANISA

Je! Kuna dhambi kubwa na ndogo, na kama hakuna je! Mtu aliyeua na aliyetukana je watapata adhabu sawa?

Biblia inamaana gani kusema;aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi?

Rudi Nyumbani:

Print this post

JE NI KWELI MTU ANAWEZA KUTOKA NJE YA MWILI WAKE?.

Inawezekana mtu kutoka nje ya mwili?

Ipo Imani ya kwamba mtu anaweza kutoka nje ya mwili wake au kwa lugha nyingine inajulikana kama Astral projection. Ni kwamba mtu kwa mapenzi yake mwenyewe sio kwa kuhimizwa na nguvu nyingine tofauti na yake labda tuseme ya Mungu au shetani hapana, bali yeye mwenyewe anao uwezo wa kujiamulia kutoka nje ya mwili wake, na kusafiri na kwenda mbali, mahali popote anapotaka na kurudi.

Ni ukweli usiopingika kuwa imani hii siku za hivi karibuni imezidi kushamiri sana, wanasema kitendo hicho salama mtu yeyote anaweza kufanya hata akiwa tu chumbani kwake, kinachohitajika tu ni utulivu wa akili wa hali ya juu sana, yaani kuulazimisha ubongo ukae katika hali ya kutowaza kitu chochote kwa muda fulani, na kuhakikisha pia hakuna hofu yoyote moyoni.

Pia mwili uwe katika utulivu na hiyo inaweza ikafanyika aidha mtu akiwa amelala kitandani mwake chali, huku anaangalia juu. Au ameketi katika chumba chake chenye utulivu mkubwa sana, na kuweka kitu chochote mbele yake aidha mshumaa unaowaka, au akaweka mlio Fulani wa chini wa dansi , huku anapumua taratibu sana, na kukitazama bila kuhamisha mawazo yake mahali pengine popote. Hiyo inafanywa sana sana na dini za huko ASIA kama vile wahindu, na Wabuddha, kama ulishawahi kusikia kitu kinachoitwa YOGA, nayo ni njia mojawapo mafunzo ya kutoka nje ya mwili (Astral projection).

Imani ya Yoga/Astral projection.

Wanasema mtu yeyote ambaye anaweza kufikia hatua hiyo basi atajiona kidogo kidogo roho yake inaachana na mwili wake. Na baadaye kabisa atatoka na kuuona mwili wake umeketi pale chini au umelala pale pale kitandani alipokuwa. Hivyo kuanzia hapo anaweza kutembea mahali popote anapoweza kwenda. Anaweza kuzunguka maeneo ya uwani, anaweza akapaa, anaweza kuenda sehemu ambazo hajawahi kufika kabisa..Na baadaye anaweza akarudi tena katika mwili wak,.

Wanasema kitendo hicho cha kutoka nje ya mwili(Astral projection) hakina madhara yoyote, kwanza ni kizuri kinamfanya mtu ajiamini, pili kinamfanya mtu aburudike. Na tatu kinamfanya mtu akue kiroho, na nne kinamfanya awe na afya njema..

Lakini Je! Imani hiyo ni sahihi au Inapotosha?

Kwanza jambo la kwanza ambalo tunapaswa kufahamu ni kuwa ni kweli kabisa mtu anaweza akatoka nje ya mwili wake..Lakini sio kwa matakwa yake mwenyewe au kwa mapenzi yake mwenyewe..Sisi wanadamu Mungu alivyotuumba hakutupa uwezo huo, alituumba katika mwili, hivyo uwezo wa kuingia katika Roho na kwenda nje haiwezekani kama mtu hatawezeshwa na nguvu Fulani inayotoka rohoni. Na nguvu hiyo ni aidha inatoka kwa Mungu au kwa Shetani, basi hakuna hapo katikati.

Tukianzana na Nguvu ya Mungu,.

Tunasoma katika maandiko Mtume Paulo anashuhudia na kusema alinyakuliwa na kupelewa hadi mbingu ya tatu(Sasa huko kunyakuliwa ndio kutoka nje ya mwili), akasema alipofika huko alionyeshwa mambo ambayo hayajuzu mwanadamu kuyanena..

2Wakorintho 12.:1 “Sina budi kujisifu, ijapokuwa haipendezi; lakini nitafikilia maono na mafunuo ya Bwana.

2 Namjua mtu mmoja katika Kristo, yapata sasa miaka kumi na minne, (kwamba alikuwa katika mwili sijui; kwamba alikuwa nje ya mwili sijui; Mungu ajua). Mtu huyo alinyakuliwa juu mpaka mbingu ya tatu.

3 Nami namjua mtu huyo, (kwamba alikuwa katika mwili sijui; kwamba alikuwa nje ya mwili sijui; Mungu ajua);

4 ya kuwa alinyakuliwa mpaka Peponi, akasikia maneno yasiyotamkika, ambayo haijuzu mwanadamu ayanene.”

Unaona Maneno haya yanathibitisha kweli kuwa mwanadamu anaweza kutoka nje ya mwili wake, jambo hilo hilo linaonekana pia kwa mtume Yohana alipokuwa katika kile kisiwa cha Patmo, naye alikuwa katika Roho.

Na hata leo hii Mungu anaweza kutoa watu na huwa anawatoa katika mwili na kuwapeleka sehemu nyingine kuwaonyesha mambo ya rohoni, hilo linawezekana lakini haliji kwa jinsi mtu anavyotaka yeye. Bali kwa jinsi Mungu anavyotaka yeye, hata kama mtu huyo ni nabii kiasi gani, au anayo mahusiano gani na Mungu, hajiamulii mwenyewe sasa nataka nione maono. Au nataka niingie katika roho, ni Mungu mwenyewe ndio anayepanga na inakuja kwa wakati asioutegemea.

Sasa Tukirudi katika upande wa pili wa nguvu za giza(Shetani).

Ni kwamba, pale mtu anapotaka kujaribu kutafuta au kujiingiza katika maarifa ya rohoni kwa matakwa yake mwenyewe. Hapo ndipo shetani anapopata mlango kirahisi wa kumwingia mtu huyo na kumdanganya..Kama ulikuwa hujui hivyo ndivyo watu wanavyozama katika uchawi na ushirikina,..

Zipo shuhuda nyingi sana siwezi kukuelezea zote hapa, na kama wewe ni msomaji mzuri wa vitabu nakuomba usome kitabu hichi ambacho kilipata umaarufu mkubwa duniani, na kimewasaidia watu wengi sana ambao walikuwa wamezama katika vifungo vya namna hiyo vya shetani na kutoka kinavyomweleza dada mmoja aliyeingia katika uchawi na kuwa malkia wa kuzimu na baadaye kukombolewa na Kristo.

Na kufunua njia zote na milango yote ambayo shetani anayoitumia kuwavuta watu wengi kwake..Kitabu hicho kipo katika lugha ya kiingereza kinaitwa, HE CAME TO SET THE CAPTIVES FREE. Ikiwa utakihitaji utaniambia nikutumie kwa njia ya email kwa mfumo wa pdf Ukisome, moja ya mambo anayoeleza huko ni pamoja na kuwaonya watu wasifanye hivyo kabisa (Astral Projection).

Na zipo shuhuda nyingi. Lakini hicho ni kizuri Zaidi.

Leo hii hata katika maeneo ya michezo na mazoezi (GYM). Wanafundishwa kufanya hivyo na kudai kuwa ni sehemu ya afya ya ubongo kufanya YOGA. Wanasema ukiweza kukaa katika hali hiyo bila kufikiria chochote au kuwaza chochote katika utulivu wa hali hiyo ya juu kwa muda mfupi tu hata wa nusu saa ni zaidi ya kupumzika kwa kulala usingizi. Nataka nikuambie usijaribu kufanya hivyo. Kwani shetani hapo ndipo anapopata upenyo kwa kupitia milango ya fahamu zako kukuteka na kukutoa katika mwili, na siku za mwanzoni utajiona kweli ni kama wewe unafanya lakini kumbe hujui tayari ni Pepo limekuchukua katika roho linakuzungusha. Unakuwa huna tofauti na mchawi anasafiri kwa ungo kutoka mji mmoja hadi mwingine kwa nusu saa.

Na kwa kuwa siku ya kwanza utapenda, kesho tena utataka ujaribu, na huko huko utakutana na mambo ya ajabu na nguvu za giza ambazo zitakupa maagizo zaidi ya kufanya ili uwe na uwezo huu au uwezo ule, na mwisho wa siku unajikuta umezama moja kwa moja katika uchawi wa hali ya juu.

Kumbuka mlango mmoja unafungua mwingine..

Kwamwe usikae umfungulie shetani mlango kama huo ukadhani unajaribu tu. Ukifanya hivyo ndio umepotea moja kwa moja…Na waganga wa kienyeji nao wanatoaga hayo masharti.

Shetani sikuzote anajua wanadamu wanapenda maarifa Fulani zaidi wa hayo waliyowekewa, hivyo anakuja na kitu kipya kwasababu anajua wakisikia hivyo watavutiwa nacho, ndicho alichofanya pale Edeni kumwambia Hawa Ati hivi ndivyo Mungu alivyosema, ukila matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya mtakufa?..Hakika hamtakufa kwasababu anajua siku mtakapokula MTAFUMBULIWA MACHO..

Vivyo hivyo leo hii anawaambia watu ukitoka nje ya mwili wako, basi utakuwa unajua kila kitu. Utakuwa unaweza kujiamrisha mwenyewe na kuongoza roho yako kwa jinsi unavyotaka..Lakini walioingia huko, wanahadhithia wanatamani kutoka lakini ni ngumu shetani kashawateka..

Hivyo epuka ujanja wa shetani. Mtu akikueleza habari hizo, tena mkemee. Dumu katika kulitafakari Neno la Mungu, na kuyatenda mapenzi yake, hiyo inatosha..Hizi ni nyakati za Hatari.

Mungu akubariki.

Tafadhali “Share” Ujumbe huu na kwa wengine.


Mada Nyinginezo:

JISHUSHE ILI MUNGU AKUHUDUMIE.

DUNIANI MNAYO DHIKI.

LULU YA THAMANI.

NIKUPE WEWE URITHI WA BABA ZANGU?

Rudi Nyumbani:

Print this post

MTUMAINIE YESU ASIYEISHA MATUKIO.

Mtumaini Yesu asiyeisha Matukio. Jina la Bwana Wetu Yesu Kristo libarikiwe. Neno la Mungu linasema katika..

Yohana 21:25 “Kuna na mambo mengi aliyoyafanya Yesu; ambayo yakiandikwa moja moja, nadhani hata ulimwengu usingetosha kwa vile vitabu vitakavyoandikwa”.

Kama ni Msomaji mzuri wa Biblia utagundua kuwa Injili zote nne za kwenye biblia yaani, Mathayo, Marko, Luka na Yohana, Zimeandika habari zinazofanana kuhusiana na Bwana Yesu Kristo. Lakini pia utagundua kuwa pamoja na kwamba zinalandana kwa sehemu kubwa lakini pia kuna habari ambazo utazikuta katika kitabu cha Mathayo ambazo hazipo katika Injili nyingine. Vivyo hivyo zipo ambazo utazipata tu katika kitabu cha Luka na hautaweza kuzipata katika kitabu kingine chochote cha Injili.

Kadhalika pia kuna habari ambazo utazipata katika kitabu cha Injili ya Yohana ambazo huwezi kuzipata katika Injili ya Mathayo au Luka wala Marko.

Kwamfano tunaweza kuona ile habari ya Mwanamke Msamaria. Ambaye alikutana na Bwana Yesu kisimani. Habari ile ipo tu katika kitabu cha Yohana Mtakatifu, na huwezi kuipata katika kitabu cha Mathayo au Luka au Marko. Hivyo endapo kitabu cha Injili ya Yohana kisingeandikwa pengine tungokosa tukio la Muhimu kama lile ambalo lilikuwa limebeba funzo kubwa sana kwetu.

Kadhalika kuna habari ya kufufuliwa kwa Lazaro. Tukio hilo pia ambalo Bwana Yesu alilifanya limeandikwa kwenye kitabu kimoja tu cha Yohana. Na halikurekodiwa katika vitabu vingine vya Injili.

Pia kuna Muujiza mwingine ambao Bwana Yesu aliufanya alipoingia mji mmoja unaoitwa Naini,

Pale alipomfufua mtoto wa pekee wa mwanamke mmoja mjane, ambaya alikuwa anachukuliwa kupelekwa makubirini kuzikwa.(Luka 7:11-17). Alimfufua akiwa ndani ya jeneza huku likiwa limebebwa na watu. Mji mzima ukaingiwa na hofu kwa tukio hilo.

Vivyo hivyo kuna tukio lingine tena ambalo tunalisoma katika kitabu cha Mathayo peke yake. Ambalo halipatikani katika vitabu vingine vya injili. Na tukio hilo ni lile la kunyanyuka kwa miili ya watakatifu waliokuwa wamelala makaburini, na kuuingia mji mtakatifu na kuwatokea wengi..(Mathayo 27:51). Tukio hilo endapo kitabu cha Mathayo kisingekuwepo tusingelifahamu.

Kadhalika na matukio mengine mengi ni hivyo hivyo. Utayakuta kwenye Injili hii lakini kwenye nyingine usiyakute. Kwahiyo tunaweza kusema endapo kila Mtume wa Bwana Yesu au kila mtu aliyemjua Bwana angepewa fursa ya kuandika mambo aliyoyaona kwa Bwana Yesu katika kipindi chote alichokuwepo nao duniani. Ni wazi kuwa tungesikia mambo ya ajabu sana ambayo yangetushangaza au hata pengine kutushtusha.

Ndio maana Biblia inasema..

Yohana 21:25 “Kuna na mambo mengi aliyoyafanya Yesu; ambayo yakiandikwa moja moja, nadhani hata ulimwengu usingetosha kwa vile vitabu vitakavyoandikwa”.

Leo hii kuna mamilioni ya vitabu yaliyoandikwa ulimwenguni kote. Kila sekunde yanachapishwa mapya, Lakini pamoja na mavitabu yote hayo bado hayajaujaza ulimwengu. Ili Neno “kuujaza ulimwengu” litimie inapaswa ukipita barabarani unakanyaga vitabu tu. Barabarani kote kumejaa vitabu tu, na kila kitabu kinaeleza habari tofauti na kingine, sio Nakala. Hebu tafakari ni mambo mangapi aliyafanya Yesu?.

Kwa ufupi kila sekunde kulikuwa na tukio la kimiujiza alikuwa analifanya. Kila sekunde kulikuwa na Neno la kinabii alilokuwa analitoa. Endapo Mariamu mama yake Yesu na yeye angepewa fursa ya kuelezea kwa maandishi mambo aliyoyaona kutoka kwa Bwana, tangu anazaliwa mpaka anaondoka duniani..pengine angeandika vitabu vyake 2000. Ni wazi kuwa kuna mambo mengi yakimiujiza ujiza yalikuwa yanatokea hata wakati anafanya kazi zake za useremala. Hayajaandikwa tu! Endapo Yusufu babayake angepewa fursa ya kuyandika tungesikia mengi.

Mke wa Pilato ambaye alimwona Bwana Yesu katika ndoto siku ile usiku kabla ya kusulibiwa, akamwambia mume wake,amwaache mtu huyu ni wa haki lakini mume wake hakusikia. Naamini angepewa fursa ya kuandika aliyoyaona kwenye ile ndoto kwa urefu kuhusu Yesu, angeandika vitabu viwili.

Wale walinzi ambao walishuhudia kufufuka kwake, walikuwa na mengi ya kuelezea.

Laiti wangepata fursa ya kuelezea kwa maandishi, Leo pengine tungesikia mambo ya ajabu sana Zaidi ya yale tunayoyajua yaliyotokea pale kaburini. N.k n.k

Hata sasa endapo mambo anayoyafanya katikati ya watu, kila mmoja akapewa tu fursa ya kuandika mambo machache aliyofanyiwa na Yesu. Jiulize ni vitabu vingapi vingechapishwa duniani? Mabilioni ya vitabu. Sasa kwanini mtu wa namna hii tusimtumainie aliyejaa matukio kiasi hichi?.

Hakuna mwanadamu yoyote ambaye alishawahi kutokea aliyefanya mambo mengi kama Yesu. Kama hayupo basi Huyu Yesu ndiye wa kumtumainia. Hadi sasa tunavyoongoa mtu ambaye ni maarufu wa kwanza duniani, tangu miaka 2000 iliyopita hadi sasa, mtu ambaye anazungumziwa zaidi sasa sekunde hii tu tunayozungumza kuliko watu wengine wote ni YESU KRISTO.

Hivyo nakutia moyo wewe unayemtumaini Yesu, kamwe usifikirie hata siku moja kwenda kutafuta msaada kwa mwingine, au kwa wanadamu ambao historia ya Maisha yao kama ikiandikwa ni kitabu kimoja au viwili. Haizidi hapo. Na tena hivyo viwili ni imerefushwa sana. Lakini Bwana Yesu kwa kipindi tu kile kifupi alichoishi duniani tayari matukio yake hata ulimwengu usingetosha. Bwana Yesu ndiye Mkuu wa Uzima, Ngome Imara. Na msingi wa kutegemewa milele. Mwamba wetu, kimbilio letu tegemeo letu, boma letu, fungu letu, na msaada wetu wa kwanza na wa mwisho.

Kama hujampokea upo hatarini sana.

Hivyo ni vyema ukafanya mageuzi haraka kabla muda wako wa kuishi duniani haujaisha. Tubu na yeye atakusamehe kabisa bure, Fikiria wokovu umegharamiwa hivyo, na unatolewa kirahisi hivi..Tubu tu na umfuate naye atakuondolea mzigo mzito wa dhambi ulionao na atakupa tumaini la Uzima wa Milele.

Bwana akubariki sana.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

Je! ni sahihi kwa Mkristo kusherekea siku yake ya kuzaliwa.[Birth day]?

Bwana Yesu alizaliwa mwaka gani?

“Ninyi ni chumvi ya dunia” Andiko hilo lina maana gani?

TUMAINI NI NINI?

Rudi Nyumbani:

Print this post

ZIKUMBUKE SIKU ZIJAZO ZA GIZA, KWA MAANA ZITAKUWA NYINGI.

Mhubiri anasema… “Naam, mtu akiishi miaka mingi, na aifurahie yote; lakini na azikumbuke siku zijazo za giza, kwa maana zitakuwa nyingi. Mambo yote yajayo ni ubatili”(Mhubiri 11:8 ).

Anaendelea na kusema…

9 Wewe kijana, uufurahie ujana wako, na moyo wako ukuchangamshe siku za ujana wako, ukaziendee njia za moyo wako, na katika maono ya macho yako, lakini ujue wewe ya kwamba kwa ajili ya hayo yote Mungu atakuleta hukumuni..”

Huyu ni Sulemani ambaye tunamjua alikuwa ni Mfalme mwenye hekima. Na bado ni Tajiri ambaye hakuonekana mfano wake katika historia, alipitia utoto kama vile wewe ulivyo mtoto leo, alipitia ujana kama vile wewe ulivyo kijana leo. Alipitia pia uzee kama vile wewe ulivyo mzee leo, na kila hatua aliliandikia hekima yake inayomfaa mtu husika. Lakini leo hii tutaangalia kipengele kimuhusucho kijana, anasema kama wewe ni kijana, uufurahie ujana wako, na moyo wako ukuchangamshe siku za ujana wako. ukaziendee njia za moyo wako, na katika maono ya macho yako, lakini ujue wewe ya kwamba kwa ajili ya hayo yote Mungu atakuleta hukumuni..

Mungu kakupa uzuri, Mungu kakupa urembo, Mungu kakupa afya njema, Mungu kakupa elimu nzuri, Mungu kakupa kipaji kizuri, Mungu kakupa hata utajiri, vyote hivyo ni vyema kuwa navyo, uvifurahie na kuviishi…Unafanya vyema kuwa na malengo mazuri, kuwa na biashara nzuri, kuwa na kampuni zuri, kuwa na mke mzuri,..lakini fahamu kuwa katika hayo hayo unayoyafikiria na kuyatenda sasa, huku huku ndiko Mungu atakapokuhukumia..

Mambo yote yataletwa hukumuni..

Ikiwa wewe katika ujana wako unaona ni vema uvae nusu uchi ukazunguke barabarani watu wote waoune uchi wako. Na umbile lako kisa tu wewe ni unajiona ni mrembo basi fahamu kwa ajili ya hayo Mungu atakuleta hukumuni..Ikiwa unafanya biashara na pesa yako inakujia kwa njia ya kuhonga basi ujue kuwa kwa ajili ya hayo yote Mungu atakuleta hukumuni. Ikiwa umemwona mke wa mtu, ukampenda ukamchukua ukaishi naye mkazaa naye mkawa na Maisha mazuri ya furaha yasiyo na masumbufu basi ufahamu kuwa ajili ya hayo unayoyafanya Mungu atakuleta hukumuni…Ikiwa leo hii unajionyesha kwamba wewe ni kijana wa kisasa, unakunywa pombe, unavuta sigara,. Unahudhuria disko, na unaona hakuna shida yoyote kufanya hivyo, ni mambo tu ya ujanani,

fahamu kuwa ajili ya hayo Mungu atakuleta hukumuni.

Jambo lolote lile leo hii unalolifanya au,unalojishughulisha nalo basi tarajia kuwa siku ile ikifika hicho hicho ndicho kitakachokupeleka hukumuni..Mungu hawezi kukuleta hukumuni kwa mambo usiyoyajua, au usiyoyafanya, au usiyoyafikiria, haiwezekana ukawa ni muuzaji wa madawa ya kulevya siku ile ukaenda kukuuliza habari za kwanini ulikuwa fisadi., hapana, palepale kwenye malengo yako, palepale kwenye shughuli yako hapo hapo ndipo patakapozungumza katika siku ile..

Na ndio maana mhubiri anatushauri na kusema.. Naam, mtu akiishi miaka mingi, na aifurahie yote; lakini na azikumbuke siku zijazo za giza, kwa maana zitakuwa nyingi…

Tunapopewa Maisha marefu, tunapoona tunafanikiwa katika jambo lolote lile, liwe ni baya au ni jema, basi tufahamu kuwa pia zipo siku za giza zinazokuja huko mbeleni. Ambazo nazo zitakuwa ni nyingi hata Zaidi ya hizi tunazoziishi, wakati ambayo kitabu cha kila mmoja kitafunguliwa, na kusomwa aya baada ya aya. kurasa baada ya kurasa, siku baada ya siku ya Maisha yako aliyokuwa anaishi hapa duniani…Hapo ndipo tutahukumiwa sawasawa na kile kitabu cha uzima.

Kama hujafahamu vizuri juu ya hichi kitabu cha uzima kitatuhukumu vipi, na ungehitaji kufahamu basi unifahamishe Inbox nikutumie somo lake…

Hivyo Mhubiri anatuonya tuyachunge Maisha yetu katika hizi spidi za Maisha tulizonazo, tuumie ujana wetu vizuri, kama wewe ni kijana, sio kila fashion inayokuja uikimbilie, sio kila fursa ya biashara inayokuja mbele yetu tunaichangamkia kisa tu inapesa, tuipime je itatukosesha na Mungu au la?.

Kwasababu kwa kupitia hiyo ndio tutahukumiwa. Sio kila mwanamke au mwanamume anayekuja mbele yetu ni wa kuoa au kuolewa kisa tu anayo fedha au ni mzuri, tuangalie je! Anakidhi vigezo vya Ukristo?. Je alishaoa au kuolewa kabla ya kukutana na wewe?. Tusije tukahukumiwa kwa dhambi za watu wengine. Kwa maana ukiolewa au ukioana na mtu ambaye amemwacha mke/mume wake ni unazini. Na wazinzi wote sehemu yao ni katika lile ziwa la moto, Biblia inasema hivyo.

Sio kila Rafiki ni wa kuongozana naye tuangalie je! Ni mtukanaji?. Ni mzinzi, ni mwizi n.k., tusije tukajifunza tabia zake takajikuta na sisi tunahukumiwa kwa ajili yao..Kwasababu yote tunayoyafanya, yanayotuzunguza ndio hayo tutakayo hukumiwa nayo. Ni heri tukakosa vingi lakini siku ile tuwe upande salama, kuliko kupata vyote na kujikuta katika ziwa la moto.

Mhubiri 4: 6 “Heri konzi moja pamoja na utulivu, Kuliko konzi mbili pamoja na taabu; na kujilisha upepo”.

Amen.

Ikiwa bado hujaokoka, Na unahitaji kumpa Bwana Maisha yako leo ayasafishe kwa damu yake. Na ayaongoze, awe mtetezi wako hata siku ile ya hukumu. Utakuwa umefanya jambo jema na la busara ambalo hutakaa ulijutie milele..Unachotakiwa kufanya hapo ulipo, ni ujitenge kwa muda kidogo peke yako.

Kisha piga magoti kuonyesha utiifu wako kwa Mungu na kwamba unahitaji msaada wake. Kisha hatua inayofuata ni kumweleza Mungu kwa kumaanisha kabisa kuwa umetubu dhambi zako zote leo. Na kwamba kuanzia sasa unataka umwishie yeye hadi siku ile utakapokwenda mbinguni…

Hakikisha unatubu kwa kumaanisha kabisa. Kwasababu toba halisi sio kuongozwa sala fulani kama inavyodhaniwa na watu wengi. Toba halisi ni kutoka moyoni, na Mungu akiona umemaanisha basi hapo hapo anakusamehe pasipo masharti…

Hivyo ukishatubu hatua inayofuata ni kwenda kubatizwa katika ubatizo sahihi wa kuzamwishwa katika maji mengi kwa Jina la YESU KRISTO sawasawa na Matendo 2:38, kama bado hujabatizwa. Na baada ya hapo Bwana mwenyewe atakupa kipawa cha Roho Mtakatifu kukusaidia na kukulinda mpaka siku ile ya ukombozi wa mwisho wa miili yetu.

Hivyo zingatia hatua hizo ili na wewe ufanyike kuwa mwana wa Mungu, mwenye kustahili kuuridhi uzima wa milele. Na hivyo siku ile ya hukumu mbawa za Kristo zitakufunika kwasababu umehesabiwa haki bure kwa neema yake kwa kumwamini tu yeye.

Ubarikiwe sana.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

FAIDA ZA MAOMBI YA USIKU

JE! UNAYO NAFASI MBINGUNI?

KUFUKIZA UVUMBA NDIO KUFANYAJE?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Uzao wa Mwanamke ni upi? Unaozungumziwa katika Mwanzo 3:15?

JIBU: Uzao wa Mwanamke ni Uzao wa Yesu Kristo. Wote waliozaliwa mara ya pili, kwa lugha nyingine ya rohoni wanajulikana kama “uzao wa mwanamke”. Sasa ni kwasababu gani wanaitwa hivyo?.

Tukirudi Pale Edeni tunafahamu kuwa mwanadamu wa Kwanza kuumbwa alikuwa ni Adamu. Watu wote tuliopo sasa wakike na wakiume asili yetu ni kutoka kwa huyu mtu mmoja Adamu!. Ambaye anajulikana kama Adamu wa Kwanza. Alikuwa hana Baba wala Mama. Aliumbwa kwa viganja vya Mungu mwenyewe.

Lakini Adamu wa pili hakuumbwa kutoka katika mavumbi ya ardhi kama Adamu wa kwanza. Bali alizaliwa kutoka katika tumbo la Mwanamke. Na huyo si mwingine zaidi ya Yesu Kristo mwokozi wetu. (1Wakorintho 15:45) ambaye alizaliwa kutoka katika Tumbo la mwanamke anayeitwa Mariamu. Hana Baba wa kimwili ndio maana hajaitwa ni uzao wa mwanamume bali wa mwanamke. Ndivyo ilivyompendeza Mungu iwe hivyo! Hakumhusisha mwanamume katika Kumleta Kristo bali alimhusisha mwanamke peke yake!. Kwasasa ile damu safi itakayowaokoa wanadamu isiyo na mawaa, ilipaswa itoke juu, kwa Mungu mwenyewe..

Sasa Bwana Yesu kuzaliwa na Mwanamke Mariamu hakumfanyi, Mariamu au mwanamke mwingine yeyote kuwa wa kipekee sana kuliko watu wengine, na hata kufikia kiwango cha kuhusishwa na mambo ya ibada kama Kanisa Katoliki linavyofanya. Hapana! Mariamu ametumika kama njia tu..Lakini hakuna la ziada hapo, baada ya kumzaa Yesu alihitaji wokovu tu kama wanawake wengine, alihitaji kumwamini, kutubu na ubatizwa na kuishi maisha matakatifu na ya uangalifu kama watu wengine tu.

Ni sawa na Daudi alivyotumika kama njia ya cheo cha ufalme wa Kristo. Lakini hakukumfanya Daudi kuwa mtu wa kipekee sana kuliko wengine. Kwasababu Yesu mahali pengine anajulikana kama MWANA WA DAUDI! Maandiko yanasema hivyo sehemu nyingi na yeye mwenyewe Yesu alisema yeye ni mzao wa Daudi katika Ufunuo .

Tunasoma katika..

Ufunuo 22:16 “Mimi Yesu nimemtuma malaika wangu kuwashuhudia ninyi mambo hayo katika makanisa. Mimi ndimi niliye Shina na Mzao wa Daudi, ile nyota yenye kung’aa ya asubuhi”.

Lakini sehemu nyingine pia anasema Daudi alimuita yeye Bwana, sasa iweje yeye awe tena Mwana wake tena.

Mathayo 22:41 Na Mafarisayo walipokusanyika, Yesu aliwauliza, akisema, Mwaonaje katika habari za Kristo?

42 Ni mwana wa nani? Wakamwambia, Ni wa Daudi.

43 Akawauliza, Imekuwaje basi Daudi katika Roho kumwita Bwana, akisema,

44 Bwana alimwambia Bwana wangu, Uketi mkono wangu wa kuume, Hata niwawekapo adui zako Kuwa chini ya miguu yako?

45 Basi, Daudi akimwita Bwana, amekuwaje ni mwanawe?

Au Sasa Tuanze kuweka sanamu za Daudi na kumwomba atuombee na kumwambia salamu Daudi Baba wa Yesu tuombee huko uliko??..Unaona haiingii akilini hata kwa mtoto mchanga wa kiroho anayejifunza biblia kwa mara ya kwanza leo? kama hatuwezi kufanya hivyo kwa Daudi hatupaswi pia kufanya hivyo kwa Mariamu wala mtu mwingine yeyote. Hao wote wametumika kama njia tu ya kupitishia kusudi la Mungu.

Bwana akubariki sana.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

YONA: Mlango wa 2

KWANINI YESU KRISTO NI MWANA WA DAUDI?

JE YESU ATARUDI TENA?

JE NI KWELI BWANA YESU SIKU YA KURUDI ATAFIKIA ISRAEL

Rudi Nyumbani:

Print this post

WATAMTAZAMA YEYE AMBAYE WALIMCHOMA; NAO WATAMWOMBOLEZEA.

Shalom.

Biblia inatuambia kipindi kifupi sana kabla ya kurudi kwa Kristo, na kile kipindi chenyewe cha kurudi kwake, kutakuwa na makundi mawili ya watu ambao watakuwa wakimwombolezea, Kundi la kwanza ni Waisraeli, biblia inatuambia hivyo katika Zekaria 12.

Tusome,

Zekaria 12:10 “Nami nitawamwagia watu wa nyumba ya Daudi, na wenyeji wa Yerusalemu, roho ya neema na kuomba; nao watamtazama yeye ambaye walimchoma; nao watamwombolezea, kama vile mtu amwombolezeavyo mwanawe wa pekee; nao wataona uchungu kwa ajili yake, kama vile mtu aonavyo uchungu kwa ajili ya mzaliwa wake wa kwanza.

11 Siku hiyo kutakuwa na maombolezo makuu huko Yerusalemu, kama maombolezo ya Hadadrimoni katika bonde la Megido.

12 Nayo nchi itaomboleza, kila jamaa peke yake; jamaa ya nyumba ya Daudi peke yao, na wake zao peke yao; jamaa ya nyumba ya Nathani peke yao, na wake zao peke yao;

13 jamaa ya nyumba ya Lawi peke yao, na wake zao peke yao; jamaa ya nyumba ya Shimei peke yao, na wake zao peke yao.

14 Jamaa zote zilizosalia, kila jamaa peke yake, na wake zao peke yao.”

Na kundi la Pili litakuwa ni watu wa mataifa yote duniani, tunasoma hilo katika,

Ufunuo 1:7 “Tazama, yuaja na mawingu; na kila jicho litamwona, na hao waliomchoma; na kabila zote za dunia wataomboleza kwa ajili yake. Naam. Amina”.

Lakini tunapaswa tujiulize, ni kwanini biblia inasisitiza sana juu ya hao walimchoma ndio watakaoomboleza, na sio labda hao waliomsulubisha au waliotemea mate, au waliopinga mijeledi au waliomvika taji la miiba, au waliomtukana au waliomuudhi…

Lakini badala yake ni wale waliomchoma?. Lipo jambo la kujifunza hapo, ili na sisi tuwe makini sana tusiwe miongoni mwa kundi hilo ambalo hukumu yake ilishatabiriwa miaka mingi hata kabla ya tukio lenyewe kutokea. Na kurudiwa kuzungumzwa tena miaka mingi baada ya tukio hilo kutokea.

Kama tukirudi kutazama matukio ya pale msalabani, utaona muda mfupi kabla ya Bwana Yesu kuchomwa mkuki ubavuni, mateso yote yalikuwa yameshamalizika. Na Kristo tayari alikuwa ameshakata roho, hivyo hata Roho yake haikuwepo tena pale. Lakini tunaona, wale askari wa kirumi, walipopewa maagizo ya kwenda kuivunja miguu yao wote waliosulibiwa msalabani. Walifanya hivyo kwa wale wafungwa wawili llakini walipofika kwa Bwana wetu YESU Kristo walimwona kama tayari ameshakufa. Hivyo hawakumvunja yeye miguu. Lakini waliamua kufanya jambo lingine ambalo pengine hawakuagizwa. Wakachukua mkuki mrefu, ili wamchome, mpaka kwenye moyo, wakithibitishe kifo chake.

Hivyo wakafanya kama walivyokusudia wakauzamisha ule mkuki kwa nguvu na kupasua mfuko wa maji unaozunguka moyo. Na kupenya mpaka kwenye moyo wa Kristo na kuupasua..Na uthibitisho kuwa ulifika mpaka kwenye moyo ni yale maji na damu vilivyotoka. Ndipo wakawa na uhakika sasa asilimia 100 huyu hata kama alikuwa katika Comma sasa atakuwa amekufa kweli kweli..

Lakini wao waliona ni kawaida, lakini kwa Mungu halikuwa ni jambo la kawaida hata kidogo. Majeraha yote ya nje Kristo aliyotiwa na wale watu Mungu hakuyaangalia, lakini lile jeraha lililoingia ndani tena isitoshe limepenyeza mpaka kwenye moyo wa Kristo. Moyo wa Mungu, hilo hakulisahau mpaka wakati wa mwisho..

Na kwa kupitia hilo hilo watu ndio watakaomwombolezea Kristo katika siku za mwisho.

Yohana 19:34 “lakini askari mmojawapo alimchoma ubavu kwa mkuki; na mara ikatoka damu na maji”.

Ndugu, maovu unayoyofanya sasahivi ni sawa na unamtia Kristo majeraha ya nje. Upo wakati hayo majeraha yatafika ndani ya moyo wake, na ukishafikia hiyo hatua Mungu hatakusemehe tena, kitakachokuwa kimebakia kwako mbeleni ni maombolezo..Leo hii ukishajiona tu umeachwa katika unyakuo basi ufahamu kuwa umemtia tayari Kristo jeraha hilo. Kinachofuata kwako ni maombolezo na kilio katika ile siku ya kisasi cha Bwana.

Kama ulikuwa hufahamu kalenda ya Mungu, ni kwamba kwasasa hivi tunachokingojea mbele yetu ni Unyakuo tu, dalili zote zimeshatimia, Na Unyakuo huo hautakuwa kwa watu wote, hapana bali utakuwa ni kwetu sisi watu wa mataifa tuliomwamini Kristo na wale wayahudi wachache sana ambao wamezaliwa katika Imani ya kikristo…(hao ndio bibi-arusi wa Kristo)

Lakini kundi la wayahudi wengi waliobakia, Unyakuo hautawahusu. Ukumbuke kuwa kwasasahivi Wayahudi wengi hawamwamini YESU KRISTO kama ni Masihi atayekuja, na hiyo yote Mungu amewapofusha macho kwa makusudi ili sisi watu wa mataifa tumwamini yeye,.Na hiyo itaendelea hadi wakati wetu utakapotia, ambapo utatimia na kitendo cha Unyakuo.

Sasa baada ya hapo hii neema ya injili tulionayo sasahivi, hii nguvu inayokushuhudia utubu dhambi sasa na unapuuzia, itahamia Israeli.

Mungu  atawafumbua macho yao, nao watagundua kuwa yule waliyemsulibisha miaka 2000 iliyopita kumbe ndio aliyekuwa masihi wao..Hapo ndipo na wao watakapooanza kuomboleza kama tunavyosoma hapo juu kwenye ule mstari wa Zekaria 12, Israeli nzima kutakuwa kuna maombolezo siku hiyo..Lakini wao Mungu atawapa rehema hivyo katika ile siku ya BWANA watafichwa, kwasababu walipigwa upofu na Mungu makusudi kwa ajili yetu..Hivyo Mungu atawasamehe, na baadaye watakaokolewa na kuingia katika ule utawala wa miaka 1000,…

Lakini sasa kwa haya mataifa mengine yaliyosalia, ambayo yalikosa unyakuo watakachokuwa wanakisubiria mara baada ya ile dhiki kuu ya mpinga-Kristo kuisha itakuwa ni kilio na kusaga meno, wataomboleza kwa vile walivyomchoma Kristo kwa Maisha yao ya kutokutubu walipokuwa wanaishi duniani, hapo ndipo kutakuwa na kilio na kusaga meno, na mara baada ya mapigo hayo tunayoyasoma katika Ufunuo 16, kitakachofuata ni ziwa la moto.

Sio pa kutamani kufika huko hata kidogo.

Je! Na wewe leo hii Unazidi kumtia Kristo majeraha?..Hizi ni nyakati za kumalizia ndugu Tubu kwa kumaanisha kabisa kumfuata Kristo, kwasababu siku ya karamu ya mwanakondoo aliyoiandaa kwa ajili yako na mimi mbinguni imekaribia kufika sana, na muda wowote parapanda italia, tutaalikwa kule.Roho anawashuhudia watu wengi, kuwa ile siku ya karamu imeshafika mlangoni. Hivyo Bwana atusaidie tufike ng’ambo yetu salama.

Ubarikiwe. Tafadhali “Share” Ujumbe huu na kwa wengine. Na Bwana atakubariki.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

UFUNUO: Mlango wa 7 & 11

KUVUNJA MAAGANO YA UKOO.

Shetani anatolea wapi fedha, angali tunajua Fedha na dhahabu ni mali ya Bwana?.

NIFANYE NINI ILI NIIKWEPE HUKUMU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

BUSTANI YA NEEMA.

Jina la Bwana Yesu litukuzwe. Karibu tujifunze Biblia tena.

Tunasoma katika kitabu cha Mwanzo. Baada ya Adamu na Hawa kula matunda ya mti wa ujuzi wa Mema na Mabaya ambayo waliagizwa wasiyale. Macho yao wote wawili yalifumbuliwa na kujijua kuwa wapo uchi.

Mwanzo 3:6 “Mwanamke alipoona ya kuwa ule mti wafaa kwa chakula, wapendeza macho, nao ni mti wa kutamanika kwa maarifa, basi alitwaa katika matunda yake akala, akampa na mumewe, naye akala.

7 Wakafumbuliwa macho wote wawili wakajijua kuwa wa uchi, wakashona majani ya mtini, wakajifanyia nguo”.

Matokeo ya kufumbuliwa macho ni kujisitiri. Na yaliyofumbuliwa ni macho yao ya rohoni, na si ya mwilini.

Baada ya kula tunda walichomwa mioyo na kujigundua kuwa wamefanya makosa makubwa sana. Ulishawahi kufanya kitu ambacho baada ya kumaliza kukifanya Moyo wako ukakuchoma sana! Kwa ulichokifanya?.

Au Ulishawahi kumkosea Mtu Fulani Labda ni boss wako au mkubwa wako mahali Fulani?ambaye sikuzote alikuwa ni mwaminifu kwako, na anakuamini na anakujali na kukupenda sana kwa dhati, wala hajawahi kukufanyia jambo lolote baya?. Halafu baadaye akajua ubaya uliomfanyia na hata baada ya kujua hajakuongelesha chochote.

Unajua huwa Kuna hali Fulani inakuja ambayo unaona aibu hata kukutana naye kumwangalia usoni! Unakuwa unamkwepa kwepa tu muda wote. Unaanza kujihukumu kabla hata ya yeye kukuhukumu.Hata ukikutana naye uso kwa uso unatamani uongee naye kwa dakika chache sana tena ikiwezekana huku umevaa miwani, au huku unaangalia chini. Maana utasikia aibu sio aibu. Usaliti sio usaliti, yaani hali Fulani isiyoelezeka.

Ndicho kilichowatokea wazazi wetu wa Kwanza Adamu na Hawa.

Kwa walichokifanya mbele ya macho ya Mungu iliwafanya wajione wao sio kitu tena, hawana maana tena. Wafiche wapi nyuso zao?. Wafiche wapi viungo vyao mbele za Mungu?. Watawezaje tena kumwangalia Mungu usoni, ambaye hapo kwanza alikuwa anatembea nao kama rafiki? Na anawaamini?..Ni uchungu uliochanganyikana na Aibu.

Suluhisho lililobaki ni kujificha tu mbele ya uso wa Mungu, na kutafuta njia ya kumkwepa kwepa. Ndio unaona sasa wakaamua kutengeneza nguo kwa majani ya mtini. Kumbuka hawakushona nguo kwasababu wanaoneana aibu wao kwa wao. Hapana wao walikuwa hawaoneani aibu. Waliyekuwa wanamwonea aibu ni Mungu.

Na pia nguo hizo za nyasi walizojitengenezea hazikufunika tu sehemu zao za siri, bali zilifunika mwili mzima mpaka kichwa. Kwasababu ni Aibu!. Utawezaje kuonyesha kifua chako tena mbele za Mungu? Uso tu shida, si zaidi mgongo au kifua au mapaja?. Ndio maana waliendelea mpaka kujificha katikati ya vichaka!. Kujishonea nguo za nyasi peke yake waliona haitoshi.

Ndugu sasahivi katika nyakati hizi tupo katika Bustani ya Mungu inayoitwa Neema. Bustani hii ni Bustani ya Yesu Kristo, ambayo anatembea na sisi kama Rafiki. Kama Mungu alivyotembea na Adamu pale Edeni.

Yohana 15:14 “Ninyi mmekuwa rafiki zangu, mkitenda niwaamuruyo.

15 Siwaiti tena watumwa; kwa maana mtumwa hajui atendalo bwana wake; lakini ninyi nimewaita rafiki; kwa kuwa yote niliyoyasikia kwa Baba yangu nimewaarifu”.

Neema ni kitu cha ajabu sana, Maana unaweza kupata chochote utakacho, kwa jina la Yesu, Msamaha wa dhambi unapatikana ndani ya Neema, uponyaji, Baraka n.k. Ni kama Edeni tu! Kila kitu kilikuwa kinapatikana pale bila nguvu nyingi.

Lakini Neema hii tulionayo sisi haitadumu milele maandiko yanasema hivyo. Wakati huu ambapo Yesu kwetu ni Rafiki. Kuna wakati utafika huyu huyu Yesu tunayempenda sasa na kumwona ni rafiki, Na kuufurahia wema wake atageuka na kuwa Mhukumu.

Wakati huo wewe unayeidharau injili sasa macho yako yatafumbuliwa na utasema!.. Nifiche wapi uso wangu huu na aibu hii kwa kuidharau Neema niliyokuwa nimepewa?..Hutatamani hata kusimama mbele za Bwana Yesu, ambaye leo hii anatembea kwako kama rafiki. Ambaye unaweza ukajiamulia chochote tu na asikueleze.

Adamu na Hawa hawakutamani hata kuuona uso wa Mungu kadhalika Yuda baada ya kumsaliti Bwana Yesu, yeye naye yalifumbuliwa macho yake na kujiona yupo uchi katika roho, aliona ni heri akajinyonge kuliko hata kwenda kumtazama pale msalabani. Akasema

Mathayo 27:3 “Kisha Yuda, yule mwenye kumsaliti, alipoona ya kuwa amekwisha kuhukumiwa, alijuta, akawarudishia wakuu wa makuhani na wazee vile vipande thelathini vya fedha, akasema, Nalikosa nilipoisaliti damu isiyo na hatia.

4 Wakasema, Basi, haya yatupasani sisi? Yaangalie haya wewe mwenyewe.

5 Akavitupa vile vipande vya fedha katika hekalu, akaondoka; akaenda, akajinyonga”.

Adamu na Hawa walijuta na hivyo kuishia Hukumu kubwa kama ile mpaka sisi vitukuu vya vitukuu tunashiriki laana yao.

Je! Itakuwaje siku ile macho yako yatakapofumbuliwa mbele ya kiti cha Hukumu? Ni majuto ya milele katika ziwa la moto, wala usifikiri siku ile utaona kama umeonewa! Utakiri kwamba ni kweli ulikosa na unastahili adhabu! Kama Yuda alivyokiri.

Wakati huu ambapo utukufu wa Neema ya Mungu upo. Wakati Kristo ni rafiki. Ushikilie wokovu, usisikilize uongo wa shetani, leo hii unaokuambia kunywa pombe sio shida, unaokuambia kuvaa vimini sio shida, kuvaa suruali kwa mwanamke sio shida! Kuishi na mtu ambaye hamjafunga naye ndoa sio shida!..Ukisikiliza huo uongo na kuutii ni kweli sasa hutaona kwamba ni shida sasa. Lakini siku ile utajuta sana macho yako yatakapofumbuliwa.

Waebrania 10:29 “Mwaonaje? Haikumpasa adhabu iliyo kubwa zaidi mtu yule aliyemkanyaga Mwana wa Mungu, na kuihesabu damu ya agano aliyotakaswa kwayo kuwa ni kitu ovyo, na kumfanyia jeuri Roho wa neema?

30 Maana twamjua yeye aliyesema, Kupatiliza kisasi ni juu yangu, mimi nitalipa. Na tena, Bwana atawahukumu watu wake.

31 Ni jambo la kutisha kuanguka katika mikono ya Mungu aliye hai”.

Ikiwa hujaokoka. Unapaswa uokoke sasa hivi. Na si kesho, kwasababu saa ya wokovu ni sasa. Hapo ulipo jitenge dakika chake peke yako, Omba toba ya dhati mbele ya Mungu Baba, mwambie akusamehe makosa yako yote uliyoyafanya huko nyuma na unayoyafanya sasa. Na kwamba hutaki kuyafanya tena. Na kisha baada ya toba hiyo, Amani Fulani ya kiMungu itakuja ndani yako. Ambayo utahisi kama kuna mzigo Fulani umeondoka. Amani hiyo ni uthibitisho kwamba umesamehewa.

Hivyo kuihifadhi hiyo amani shetani asiiibe, nenda katafute mahali wanapobatiza ubatizo sahihi wa maji tele na kwa jina la Yesu Kristo. Ubatizwe hapo kama hujabatizwa. Na kama ulishabatizwa hivyo kwa usahihi huna haja ya kubatizwa tena.

Utaanza kuona Roho Mtakatifu aliyeingia ndani yako akiyatengeneza maisha yako upya kwa namna ambayo hatuwezi tukaelezea hapa. Wewe mwenyewe utaona. Kikubwa hapo ni kumkubali tu Kristo tu katika Maisha yako na kufuta yote anayokulekeza, yaliyosalia yeye mwenyewe atayashughulikia.

Bwana akubariki.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo;

Nifanyaje ili nijue kuwa uamuzi ninaokwenda kuchagua kufanya ni mapenzi ya Mungu?

DHAMBI ILIYOMKOSESHA SHETANI:

KWANINI DAUDI ALIKUWA NI MTU ALIYEUPENDEZA MOYO WA MUNGU?

JISHUSHE ILI MUNGU AKUHUDUMIE.

Rudi Nyumbani;

Print this post