Title 2020

Nyuni ni nini?(Mathayo 13:32, Sefania 2:14)

Nyuni ni neno linalomaanisha ndege.

Hivi ni baadhi ya vifungu katika biblia vinavyolitaja neno hilo;

Mathayo 13:31 “Akawatolea mfano mwingine, akisema, Ufalme wa mbinguni umefanana na punje ya haradali, aliyoitwaa mtu akaipanda katika shamba lake;

32 nayo ni ndogo kuliko mbegu zote; lakini ikiisha kumea, huwa kubwa kuliko mboga zote, ikawa mti, hata nyuni wa angani huja na kukaa katika matawi yake”.

Zaburi 102:5 “Kwa ajili ya sauti ya kuugua kwangu Mifupa yangu imegandamana na nyama yangu.

6 Nimekuwa kama mwari nyuni wa jangwani, Na kufanana na bundi wa mahameni”.

Sefania 2:14 “Na makundi ya wanyama watalala kati yake, wanyama wote wa mataifa; mwari-nyuni na nungu watakaa juu ya vichwa vya nguzo zake; sauti yao itasikiwa madirishani; vizingitini mwake mtakuwa ukiwa; kwa maana ameifunua kazi ya mierezi”.

Soma pia Kumb 14:11,Ayubu 12:7

Kibiblia watu wa mataifa(wasiomjua Mungu) wanafananishwa na nyuni wa angani, na ndio maana utaona Bwana Yesu anaufananisha ufalme wa mbinguni na chembe ya haradali na kusema japo ni ndoto kuliko mbegu zote..Lakini inapokuwa ndani ya mtu inageuka na kuwa kubwa sana, kiasi cha kutoa matawi makubwa na watu kukaa chini yake kupumzika(yaani kujifunza Neno la Mungu, na kupokea baraka zote)

Hivyo na sisi pia tunapewa hamasa, tupende kuutafuta ufalme wake, kwani leo hii unaweza kuonekana ni kitu kisichokuwa na maana, lakini kama tukiendelea kumtafuta Mungu na kutaka kujua mapenzi yake ni nini maishani mwetu, Basi kesho tutakuwa ni msaada mkubwa kwa maelfu ya watu(Nyuni) kumjua yeye.

Bwana akubariki.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tazama tafsiri ya maneno mengine ya biblia chini.

Ikiwa utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618

Mada Nyinginezo:

Arabuni maana yake ni nini?

Kutabana ni nini? (Mika 5:12)

Fumbi ni nini?(Ayubu 6:15)

ONDOKA YESU, TUACHIE MAPEPO.

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!

Rudi Nyumbani:

Print this post

Kutabana ni nini? (Mika 5:12)

Kutabana ni kitendo kinachofanywa na wachawi cha kutabiri mambo yajayo kwa kutazama vitu fulani. Kwamfano wasomaji nyota, wasomaji viganja, watazamaji wa nyakati mbaya n.k. wote wanatabana

Utalisoma neno hilo kwenye kifungu hiki;

Mika 5:12 “nami nitakatilia mbali uchawi, usiwe mkononi mwako; wala hutakuwa tena na watu wenye kutabana;

13 nami nitakatilia mbali sanamu zako na nguzo zako, zitoke kati yako; wala hutaiabudu tena kazi ya mikono yako”.

Ukweli ni kwamba hakuna kiumbe chochote duniani, mbinguni au kuzimu chenye uwezo wa kutabiri au kujua mambo yajayo isipokuwa Mungu tu peke yake. Alishaliweka hilo wazi kuwa hakuna kitu chochote kinachoweza kujua hatma ya mtu isipokuwa yeye peke yake. Anasema;

Isaya 41:21 “Haya, leteni maneno yenu, asema Bwana; toeni hoja zenu zenye nguvu, asema mfalme wa Yakobo.

22 Wayatangaze na kutujulisha yatakayokuwa; watuonyeshe mambo ya zamani, ni mambo gani, tukapate kuyatia moyoni, tukajue mwisho wake; au wamdhihirishie yatakayotokea baadaye.

23 Tujulisheni yatakayokuwa baadaye, nasi tutakiri ya kuwa ninyi ni miungu; naam, tendeni mema au tendeni mabaya, ili tujipime, tukaone pamoja.

24 Tazameni, ninyi si kitu, tena kazi yenu si kitu; awachaguaye ninyi ni chukizo”.

Hivyo hatupaswi kufiriki kutabana kunaleta matokeo yoyote, zaidi ni kudanganywa  kama sio kurushiwa mapepo. Shetani sikuzote ni mwongo.

Isaya 46:9 “kumbukeni mambo ya zamani za kale; maana mimi ni Mungu, wala hapana mwingine; mimi ni Mungu, wala hapana aliye kama mimi;

10 nitangazaye mwisho tangu mwanzo, na tangu zamani za kale mambo yasiyotendeka bado; nikisema, Shauri langu litasimama, nami nitatenda mapenzi yangu yote”.

Kama ukiwa ndani ya Kristo, yeye mwenyewe atakufunulia hatma njema ya maisha yako ya sasa na ya baadaye. Lakini ikiwa utatafuta ujuzi au maarifa yoyote ya mambo yajayo kutoka kwa wasoma nyota ujue unapotezwa.

Hivyo kama hujaokoka,  na upo tayari kutubu na kumkabidhi Kristo maisha yako, akufanye kiumbe kipya ni uhakika kuwa mbele yako ipo salama. Je! Upo tayari kufanya hivyo leo? Kama jibu ni ndio basi fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba na kupata maelekezo mengine ya kiroho  >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tazama maana za maneno mengine ya biblia chini;

Na kama  utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618

Mada Nyinginezo:

Fumbi ni nini?(Ayubu 6:15)

Chamchela ni nini kwenye biblia?(Zaburi 58:9, Amosi 1:14)

Zaburi maana yake nini, katika Biblia?

Hori ni nini kibiblia (Waamuzi 5:17, Luka 2:7)?

JINSI WATU WANAVYOZAMA KATIKA USHIRIKINA NA UCHAWI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Nini maana ya “chakula hakituhudhurishi mbele za Mungu”?

SWALI: Biblia ina maana gani inaposema “chakula hakituhudhurishi mbele za Mungu”?

Jibu: Tusome..

1Wakorintho 8:8 “Lakini chakula hakituhudhurishi mbele za Mungu; maana, tusipokula hatupunguziwi kitu, wala tukila, hatuongezewi kitu.

9  Lakini angalieni huu uwezo wenu usije ukawakwaza wale walio dhaifu”.

“Kuhudhurisha” maana yake ni “kutusogeza karibu na kitu”.. Hivyo biblia inaposema chakula hakituhudhurishi mbele za Mungu, maana yake ni kwamba “chakula hakitusogezi sisi kuwa karibu na Mungu”.

Huwezi kula mboga nyingi au nyama, au aina fulani ya chakula kikamfanya Mungu awe karibu na wewe zaidi, au huwezi kula chakula fulani kikakufanya Mungu asikukaribia..Kitu pekee ambacho kitatufanya sisi tumkaribie Mungu au Mungu ajitenge na sisi ni dhambi!..basi hicho tu!, wala hakuna kingine..

Isaya 59:1 “Tazama, mkono wa Bwana haukupunguka, hata usiweze kuokoa wala sikio lake si zito, hata lisiweze kusikia;

2 lakini maovu yenu yamewafarikisha ninyi na Mungu wenu, na dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, hata hataki kusiki”

Kwahiyo tukila chakula chochote iwe nyama ya nguruwe, ya ng’ombe au chochote kile, hata tukila mboga, au aina yoyote ya chakula, hiyo haitusogezi wala kutuweka mbali na Mungu. Ndio maana ukiendelea kusoma mbele..Mtume Paulo anaendelea kusema maneno haya..“maana, tusipokula hatupunguziwi kitu, wala tukila, hatuongezewi kitu.”

Sasa unaweza kuuliza, Vipi kuhusu pombe?, na majani ya bangi je? Ni sahihi kuyatumia kama mboga?. vipi kuhusu sumu? Tunywe sumu na kusema haituhudhurishi mbele za Mungu?.

Pombe yoyote ile ina kilevi, ambacho kwa jinsi mtu anavyozidi kuinywa,inambadilisha mtu huyo akili (inamtoa katika hali ya asili, na kumpeleka katika hali nyingine isiyo ya asili ya kiakili, ambapo matokeo ya hiyo hali ni kuzaliwa kwa mambo maovu..mfano wa mambo hayo  ni ugomvi, uasherati, mizaha, matusi, hasira, mafarakano, kutokujali na mambo mengine mengi ambayo ndiyo yanayomchukiza Mungu).

Kwahiyo pombe sio sawa kuinywa, vile vile na bangi sio sawa kuivuta wala kutumia majani yake kama mboga, kwasababu zina vilevi ambavyo vinamuharibu akili na kumfanya atoe mambo maovu moyoni, na kumfanya awe najisi kama Bwana Yesu alivyosema katika… Mathayo 15:19 “ Kwa maana moyoni hutoka mawazo mabaya, uuaji, uzinzi, uasherati; wivi, ushuhuda wa uongo, na matukano; 20  hayo ndiyo yamtiayo mtu unajisi”

Kimiminika chenye kilevi kama Spirit, kinaweza kutumika kwa matumizi mengine ya nje kama ya kusafishia vidonda, au kuoshea vifaa lakini si kwa kuinywa, kwasababu hizo tulizojifunza hapo juu…lakini nyama ya nguruwe au ya ng’ombe haina kilevi chochote, ambacho mtu akitoka hapo, ataharibika akili na kuwa mtukanaji, au kuropoka, au kuwa na mizaha, au hasira, au itamfanya atafute kufanya uasherati wala uzinzi.

Waefeso 5:17  “Kwa sababu hiyo msiwe wajinga, bali mfahamu ni nini yaliyo mapenzi ya Bwana.

18  Tena msilewe kwa mvinyo, ambamo mna ufisadi; bali mjazwe Roho”

Ufisadi unaozungumziwa hapo sio ule wa “kuiba pesa” bali ni “tabia ya uasherati uliopindukia, ambyo imechanganyikana na mizaha, na kutokujali”

Kwahiyo chakula chochote kile ambacho hakitufanyi tutoe mambo machafu mioyoni mwetu,  hicho sio dhambi kukila, kwasababu hakituongezei chochote mbele za Mungu wala hakitupunguzii chochote kama biblia ilivyosema hapo.

Sasa swali la mwisho ambalo utauliza ni je! Kama chakula hakitusogezi mbele za Mungu, vipi kuhusu Meza ya Bwana?..je kile si chakula?, na mbona maandiko yanasema tunapoinywa damu yake tunatangaza mauti yake hata ajapo?.

Agizo la kushiriki meza ya Bwana ni agizo la kiibada, kadhalika na agizo la ubatizo..Hatuwezi kusema mkate ule ni chakula kitakatifu kwamba kila tunapokula hata tukiwa nyumbani au tukiwa kwenye sherehe ni kitu kitakatifu, hapana!… wapo wanaoitengeneza mikate ile kwa mfumo ule ule na kuitumia nyumbani mwao kama chakula cha siku zote, na isihesabike kama wameshiriki, kwasababu zile ni kama chapati tu! İsipokuwa zenyewe ni ngumu kidogo..Kwahiyo hata mtu asiyeamini anaweza kutengeneza nyumbani kwake akala kama chakula kingine tu, na isihesabike chochote kwake.

Umeona?..lakini Mkate ule unapotumika kwenye ibada ya meza ya Bwana (Pale waumini wanapokutana na kusema huu ni ishara ya mwili wa Kristo), tayari unabadilika maana, kulingana na tukio hilo, kadhalika maji yanapotumika katika ibada ya ubatizo, tayari yanabadilika maana kulingana na tukio hilo. Lakini baada ya tukio la ibada, yale maji ni kama maji mengine yoyote yanaweza kutumika kuogea au kunyeshea au yakamwagwa… Kadhalika mikate ile inayotumika katika meza ya Bwana au ngano ile baada ya ibada, inakuwa ni ngano kama ngano nyingine tu…haitusogezi mbele za Mungu.

Je umempokea Yesu?..au bado unatanga tanga na mambo ya duniani tu!..Biblia inasema katika Mhubiri 12:1 “Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, Kabla hazijaja siku zilizo mbaya, Wala haijakaribia miaka utakaposema, Mimi sina furaha katika hiyo”.

Umeona?..usipotaka kumgeukia muumba wako leo..Ipo miaka inakuja huko mbeleni, ambayo nafasi unayoichezea leo, hutaipata tena..Miaka hiyo utakosa furaha na kutakuwa hakuna msaada..Hivyo kama hujampokea Yesu, nafasi ni sasa..Unachopaswa kufanya ni kutubu kwa kumaanisha kuziacha dhambi zako zote. Kisha kwenda kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji tele na kwa Jina la Yesu, na kisha kupokea Roho Mtakatifu na kudumu katika Imani. Ukikubali kufanya hivyo Bwana atakupokea na kukutengeneza

Marana atha.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Je! Wana wenu huwatoa kwa nani? maana yake ni nini?

USIKATE TAMAA UNAPOPITIA MAGONJWA.

Sabato halisi ni lini, Je! ni Jumapili au Jumamosi?, Ni siku gani itupasayo kuabudu?

JE! SISI KAMA WAKRISTO NI DHAMBI KUSHEHEREKEA KRISMASI?.

SIKUKUU 7 ZA KIYAHUDI ZINAFUNUA NINI KWETU?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Fumbi ni nini?(Ayubu 6:15)

Fumbi ni ni neno linalomaanisha kijito,

Utalisoma katika mstari huu;

Ayubu 6:15 “Ndugu zangu wametenda udanganyifu kama kijito cha maji. Mfano wa fumbi la vijito vipitavyo.

16 Vilivyokuwa vyeusi kwa sababu ya barafu, Ambamo theluji hujificha”.

Angalia tafsiri maneno mengine ya biblia chini.

Ikiwa utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

Chamchela ni nini kwenye biblia?(Zaburi 58:9, Amosi 1:14)

Zaburi maana yake nini, katika Biblia?

Shokoa ni nini katika biblia?

Hori ni nini kibiblia (Waamuzi 5:17, Luka 2:7)?

SIFONGO NA SIKI NI NINI?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Chamchela ni nini kwenye biblia?(Zaburi 58:9, Amosi 1:14)

Chamchela ni neno linalomaanisha  ‘kisulisuli’,

Utalisoma neno hilo kwenye vifungu hivi katika biblia;

Zaburi 58:9 “Kabla ya masufuria yenu kupata moto wa miiba, Ataipeperusha kama chamchela, Iliyo mibichi na iliyo moto. ”

Isaya 29:5 “Lakini wingi wa adui zako utakuwa kama mavumbi membamba, na wingi wao watishao utakuwa kama makapi yapitayo; naam, itakuwa mara na kwa ghafula.

6 Naye atajiliwa na Bwana wa majeshi kwa ngurumo, na tetemeko la nchi, na sauti kuu, na chamchela, na tufani, na mwali wa moto uteketezao”.

Amosi 1:14 “lakini nitawasha moto katika ukuta wa Raba, nao utayateketeza majumba yake; pamoja na kupiga kelele siku ya vita, pamoja na tufani katika siku ya chamchela”;

Hivyo,Chamchela au kisulisuli ni moja ya njia ambayo Mungu aliitumia kuonyesha mambo mawili makuu. Jambo la kwanza ni ili kudhihirisha ukuu wake kwa wanadamu, na jambo la pili ni kuonyesha ghadhabu yake kwa waovu.

Kwamfano utaona alijifunua kwa Ayubu kwa njia hii pale alipotaka kumuonyesha ukuu wake na uweza wake.

Ayubu 38:1 “Ndipo Bwana akamjibu Ayubu katika upepo wa kisulisuli, na kusema,

2 Ni nani huyu atiaye mashauri giza Kwa maneno yasiyo na maarifa”?

Soma pia Ayubu 40:6

Vilevile utaona pia anajidhihirisha kwa njia hii, kuonyesha ukali wa hasira yake jinsi anavyoweza kuwapeperusha waovu wasionekane kabisa kwa mfano wa kisulisuli.

Isaya 41:16 “Utawapepeta, na upepo utawapeperusha; upepo wa kisulisuli utawatawanya; nawe utamfurahia Bwana, utajitukuza katika Mtakatifu wa Israeli”.

Yeremia  23:19 “Tazama, tufani ya Bwana, yaani, ghadhabu yake, imetokea; ni dhoruba ya kisulisuli; itapasuka, na kuwaangukia waovu vichwani. 20 Hasira ya Bwana haitarudi, hata atakapokwisha kuyatimiza makusudi ya moyo wake; katika siku za mwisho mtalifahamu neno hili kabisa”.

Nasi pia tunapaswa tuishi maisha yampendezayo Mungu angali tukiwa hapa duniani, ili Bwana atakapojifunua kwetu, ajifunue kwa sauti ya upole na utulivu, kama alivyofanya kwa Eliya na sio kwa Chamchela.

Shalom.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tazama maana ya maneno mengine ya kwenye biblia chini.

Ikiwa utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.

Mada Nyinginezo:

Zaburi maana yake nini, katika Biblia?

Kongwa ni nini kwenye biblia?(Wagalatia 5:1)

Hori ni nini kibiblia (Waamuzi 5:17, Luka 2:7)?

Neno Bildi linamaanisha nini kwenye biblia(Matendo 27:28) ?

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Rudi Nyumbani:

Print this post

Je! Wana wenu huwatoa kwa nani? maana yake ni nini?

SWALI: Bwana Yesu alimaanisha nini kusema “je! Wana wenu huwatoa pepo kwa uweza wa nani?” pale Mafarisayo walipomwambia kuwa yeye anatoa pepo kwa Beelzebuli mkuu wa pepo?


JIBU: Tusome kuanzia juu kidogo habari yenyewe,

Mathayo 12:24 “Lakini Mafarisayo waliposikia, walisema, Huyu hatoi pepo, ila kwa Beelzebuli mkuu wa pepo.

25 Basi Yesu akijua mawazo yao, akawaambia, Kila ufalme ukifitinika juu ya nafsi yake, hufanyika ukiwa; tena mji au nyumba yo yote ikifitinika juu ya nafsi yake, haitasimama.

26 Na Shetani akimtoa Shetani, amefitinika juu ya nafsi yake; basi ufalme wake utasimamaje?

27 Na mimi nikitoa pepo kwa Beelzebuli, JE! WANA WENU HUWATOA KWA NANI? KWA SABABU HIYO HAO NDIO WATAKAOWAHUKUMU.

28 Lakini mimi nikitoa pepo kwa Roho wa Mungu, basi ufalme wa Mungu umekwisha kuwajilia”.

Tukumbuke kuwa neema ya Mungu ya uponyaji ilikuwepo tangu zamani za agano la lake, isipokuwa tu haikuwa imefunuliwa katika utimilifu wote kama ilivyokuwa kwetu sisi wa agano jipya kwa kupitia Yesu Kristo mwokozi wetu. Utaona kuna wakati Mungu alikuwa anawaponya wayahudi pale walipokuwa wanamwomba, japo halikuwa jambo la papo kwa papo kama alivyokuja kufanywa na Bwana Yesu mwenyewe, mti wa uzima.

Kwa mfano ukisoma Yohana 5, utaona kulikuwa na birika moja mashuhuri lililoitwa Bethzatha huko Yerusalemu, ambapo kuna wakati Mungu analikuwa anamtuma malaika wake, kuyatibua maji kisha yule mtu wa kwanza kutumbukia alikuwa anaponywa ugonjwa wake saa ile ile .Haijalishi alikuwa anasumbuliwa na vifungo vya magonjwa au mapepo ya udhaifu mengi kiasi gani,  ilikuwa akiingia tu mule ni lazima atoke mzima, na ndio maana utaona yule mtu ambaye alikuwa anasumbuliwa na ule ugonjwa wa udhaifu kwa muda wa miaka 38, (na bila shaka lilikuwa ni pepo la udhaifu)? Bwana Yesu alimfungua badala yake, Utauliza tumejuaje alikuwa na pepo la udhaifu? Ni kwasababu mwishoni kabisa Bwana Yesu alimwambia asifanye dhambi tena yasiye yakamkuta yaliyo mabaya zaidi ya yale aliyokuwa nayo..Kumbuka hilo ndio lile Yesu alilolisema katika Luka 11:24 kwa habari ya mapepo, ambayo hayo yana tabia ya kufanya hali ya mtu kuwa mbaya zaidi pale yanaporudi na kukuta nyumba yao imefagaliwa.

Kwahiyo ni wazi kuwa mtu Yule alikuwa na mapepo ya udhaifu, na kwamba kama angeingia tu kwenye yale maji, basi mapepo hayo yangemwondoka. Hivyo huo ni mfano tu mmojawapo wa Mungu alioutumia kuwafungua wayahudi, zipo njia nyingine pia walizomwombea Mungu, na Mungu akawasikia na kuponywa hata na mapepo. Hivyo jambo la kutoa pepo lilikuwa linafanywa na wayahudi hata kabla ya kuja kwa Bwana Yesu, utalithibitisha hilo kwa wale wayahudi wapunga pepo, (Matendo 19:13), ambao walikurupuka tu na wao wakajaribu kulitaja jina la Yesu, bila kujua linahitaji mamlaka ili kulitaja. Lakini wao wakajaribu kufanya kwa njia zao, na huku matendo yao maovu, yakawakuta yaliyowakuta.

Lakini sasa tukirudi kwenye ile habari, tunaona walipokuja kwa Yesu na kuona mambo mapya yanafanyika, yaani kitendo cha Neno moja tu, mapepo yanatoka, magonjwa yanatoweka, wafu wanafufuliwa, tofauti na wao walivyokuwa wanaomba, au wanafanya, wakahitimisha kuwa huyu atakuwa anatumia nguvu za giza. Na ndio hapo Yesu akawauliza swali tu la kufikirikika, ikiwa mnasema mimi ninatoa pepo kwa beelzebuli, Je! Hao wana wenu (wanafunzi wenu), huwatoa kwa nani?, wanapoingia katika lile birika la Bethzatha na kufunguliwa ni kwa uweza wa pepo gani? Wanapomwomba Mungu wakati mwingine juu ya mapepo na mapepo yanawatoka, je! Ni kwa uwezo wa pepo wa namna gani?  Lakini Kama mnaamini ni kwa msaada wa Mungu wa Ibrahimu wanafanya hivyo na sio mapepo, kwanini mnahitimisha kuwa na mimi ninatoa pepo kwa uwezo wa mashetani?. Kumbukeni hao ndio watakaowahukumu.

Unaona? Nasi tunapaswa tuwe makini, palipo na nguvu za Mungu za kweli zinawaponya watu, hatupaswi kuhitimishi na kusema ule ni uchawi, hiyo ni dhambi ya kumkufuru Roho Mtakatifu, ambayo haiwezekaniki kusameheka, sio kila mtumishi unayemwona ni mchawi, hivyo tuchunge vinywa vyetu. Tuzungumze tu pale ambapo tumethibitisha kuwa hizi ni nguvu za giza, lakini sio kuhitimisha kila mahali unapoona nguvu za Mungu zinadhihirika kuwa ni nguvu za giza. Hapo tutakuwa tumejiweka vitanzini wenyewe.

Bwana atusaidie.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.

Mada Nyinginezo:

KUNA UMUHIMU WA KUWA MTU WA KURIDHIKA.

Zaburi maana yake nini, katika Biblia?

ONDOKA YESU, TUACHIE MAPEPO.

UTENDAJI KAZI WA MPINGA-KRISTO.

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita..

Rudi Nyumbani:

Print this post

KUNA UMUHIMU WA KUWA MTU WA KURIDHIKA.

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe.

Karibu tujifunze biblia,

Neno la Mungu linasema..

1Timotheo 6:7 “Kwa maana hatukuja na kitu duniani, tena hatuwezi kutoka na kitu;

8  ila tukiwa na chakula na nguo tutaridhika na vitu hivyo”..

Hili ni moja la andiko linalochukiwa na wengi..Hususani watu wenye uchu wa kupata mali. Lakini wanalisahau pia hili neno..

Mhubiri 5:10 “Apendaye fedha hatashiba fedha, Wala apendaye wingi hatashiba maongeo. Hayo pia ni ubatili”.

Maana yake ni kwamba kama wewe ni mtu wa kuzipenda fedha mno, usifikiri utafika wakati utasema sasa sizihitaji tena.. Hata upate nyingi kiasi gani, bado utazidi kuzitafuta tu!.. Hekima ndio inasema hivyo..Siku zote mwenye fedha nyingi ndio yupo busy kuzitafuta kuliko yule asiyekuwa nazo. Matajiri wote wakubwa ulimwenguni ndio wapo bize kuliko watu wasio na fedha nyingi.

Ndivyo hekima inavyosema.. Mhubiri 5:12 “Usingizi wake kibarua ni mtamu, kwamba amekula kidogo, au kwamba amekula kingi; lakini kushiba kwake tajiri hakumwachi kulala usingizi”.

Rafiki yangu mmoja mwenye kazi nzuri na mshahara mzuri sana, (ambaye ni kama boss tu huko kazini kwake) siku moja alinifuata huku akiwa amenyong’onyea, isivyo kawaida..Wakati naanza kuzungumza naye tu, akaniambia leo nimejifunza kitu kikubwa sana nikiwa kazini,

Akaniambia kazini, mahali anapofanya kazi kuna watu ambao kazi yao ni kufanya usafi, ambao mishahara yao ni laki moja, aliyezidi sana analipwa laki moja na nusu. Akasema kilichomshangaza zaidi ni kwamba siku hiyo kawakuta wamejikusanya wanasheherekea na kufurahi na kucheka pamoja mwisho wa mwezi, hivyo wamenunua soda na kukata keki, wakifurahi. Nikazidi kumuuliza kwani wao kufanya hivyo kumekuathiri nini wewe?. Akasema alipowaona wanafurahi huku wanamishahara midogo, ambayo kwa kiwango hicho, cha laki moja yeye anaweza kukitumia kwa siku moja tu na kinaweza kisimtoshe…..Akashangaa inakuwaje wao wenye mishahara midogo wana furaha na raha, na yeye hana raha na ana mshahara mkubwa!….. akasema “Hilo jambo kwa kweli limenigusa sana na nahisi kuna kitu natakiwa nijifunze”.

Sasa huyu alikuwa hajui kama hicho anachokisema tayari biblia ilishakisema miaka mingi sana huko nyuma …. Mhubiri 5:12 “Usingizi wake kibarua ni mtamu, kwamba amekula kidogo, au kwamba amekula kingi; lakini kushiba kwake tajiri hakumwachi kulala usingizi”.

Ndugu hatuna budi kila siku kujifunza kuridhika… Kwa kusema hivi sio kwamba nasema tuwe masikini au nauunga mkono umasikini hapana!..Ni mapenzi ya Mungu tutajirike, lakini hata katika utajiri pia tunaweza kujifunza kuridhika.

Kuridhika katika hali ya utajiri ni huku… “Aidha siku imepata kingi au vichache, kumshukuru kwako Mungu kupo palepale, kumfurahia kuko pale pale, kutenda kwako mema kupo pale pale”..Kwaufupi moyo wako haupo kwenye mali kabisa.. Na hata ukikosa au ukipata, vyote kwako ni sawasawa tu wewe utabaki kuwa yule yule, kama Ayubu.

Ayubu 31:25 “Kama nilifurahi kwa kuwa mali yangu yalikuwa mengi, Na kwa sababu mkono wangu umepata vitu vingi”

ZIFUATAZO NI FAIDA CHACHE ZA KURIDHIKA.

  1. Unapata nafasi ya kumtafakari Mungu:

Hii ni faida ya kwanza ya kuridhika, unaporidhika unakuwa unafungua mlango  mkubwa katika ufahamu wako wa kufanya jambo lingine ambalo linaweza kuwa la muhimu. Na jambo la muhimu kuliko yote ni muda wa kumtafuta Mungu. Lakini unapoingia katika tamaa ya mali zinazotokana na kutokuridhika, kamwe muda wako siku zote unakuwa umebana, hutapata hata nafasi ya kushika biblia, wala kulisoma Neno lake.

  1. Unapata Furaha:

Unaporidhika, na huku Mungu akiwa moyoni mwako, utapata furaha ya kudumu, kwasababu hutaingia kwenye mashindano na Mtu na wala hutaendeshwa na mali, hivyo hutakuwa mtumwa wa vitu hivyo, na hivyo utakuwa ni mtu wa furaha siku zote.

  1. Utajiepusha na Mitego na Vitanzi vya shetani:

Biblia inasema katika hiyo 1Timotheo 6: 9  “Lakini hao watakao kuwa na mali huanguka katika MAJARİBU NA TANZİ, na tamaa nyingi zisizo na maana, zenye kudhuru, ziwatosazo wanadamu katika upotevu na uharibifu.

Wote wanaojiingiza katika mauaji, ni kwasababu ya tamaa ya mali, inayotokana na kutokuridhika na hali walizonazo, wanaojiingiza katika ukahaba na wizi ni kwasababu ya tamaa ambayo inatokana na kutokuridhika..

  1. Hutafarakana na Imani:

1Timotheo 6: 10  “Maana shina moja la mabaya ya kila namna ni kupenda fedha; ambayo wengine hali wakiitamani hiyo WAMEFARAKANA NA IMANİ, na kujichoma kwa maumivu mengi”.

Ukiridhika na mshahara, hutamdhulumu mtu wala kusaka njia za kando kando kutafuta mali..Na hivyo Imani yako haiwezi kuathirika.

Kumbuka biblia inatuambia kwamba “Hatukuja na kitu wala hatutaondoka na kitu” na pia Bwana Yesu alisema… “itatufaidia nini (au kwa lugha rahisi, tutapata faida gani), tukiupata ulimwengu mzima halafu tukapata hasara ya nafsi zetu”?. Hilo ni swali tumepewa mimi na wewe na Bwana, la kutafakari!..

Bwana akubariki.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Kama hujampokea Yesu lakini upo bize na shughuli za ulimwengu huu, nakushauri, simamisha kwanza shughuli zako, tafuta uhakika wa usalama wa roho yako, ukishaupata rudi endelea na shughuli zako kama zinampendeza Mungu.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618


Mada Nyinginezo:

TAFUTA KUWA NA AMANI NA WATU WOTE.

SALA YA ASUBUHI

Jiepushe na tamaa ya Mali/kupenda fedha.

JE! MTUMISHI KUTOKUWA NA FEDHA NI ISHARA KUWA KUNA TATIZO KATIKA IMANI YAKE?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Zaburi maana yake nini, katika Biblia?

Zaburi maana yake ni “nyimbo takatifu”. Hivyo kitabu cha Zaburi katika biblia, ni kitabu cha Nyimbo takatifu. Zimeitwa nyimbo takatifu kwasababu zimetungwa kwa lengo la kumrudisha mtu kwa muumba wake, kwa njia hiyo ya kusifu na kumwimbia. Pia Pamoja na kwamba zilikuwa ni nyimbo, lakini ndani yake pia zilikuwa zimejaa unabii wa mambo yanayokuja.

Katika agano la kale nyimbo hizo ziliimbwa na wayahudi (yaani waisraeli) wakati wa kuabudu katika masinagogi yao, na hata leo wakristo tunatumia baadhi ya mashairi hayo kutengeneza nyimbo nzuri za kumwimbia Mungu wetu na kumshukuru na kumsifu.

Kitabu  cha Zaburi katika biblia kimeandikwa sehemu kubwa na Mfalme Daudi, wapo wengine wachache walioshiriki kuandika kitabu hicho kizima, lakini sehemu kubwa imeandika na Daudi. Na Daudi alianza kumwimbia Mungu tangu udogoni, biblia inasema hivyo.

Pia wapo wengine walioandika Zaburi (Nyimbo) katika biblia, ambazo mashairi yao hayawekwa katika kitabu cha Zaburi. Mfano wa watu hao ni Musa na Sulemani.  Kwamfano Zaburi za Musa unaweza kuzisoma katika kitabu cha Kumbukumbu la Torati 32.

Jambo dogo tunaloweza kujifunza ni kwamba..Zaburi hizi zilizoandikwa na Daudi, zimewezwa kutukuzwa na Mungu mwenyewe mpaka leo, kwasababu zimejaa maneno ya sifa kwa Mungu, na ya kumtukuza sana. Kwamfano hebu tafakari maneno ya mistari hii..

Zaburi 145:1 “Ee Mungu wangu, Mfalme, nitakutukuza, Nitalihimidi jina lako milele na milele.

2 Kila siku nitakuhimidi, Nitalisifu jina lako milele na milele.

3 Bwana ndiye mkuu mwenye kusifiwa sana, Wala ukuu wake hautambulikani.

4 Kizazi kwa kizazi kitayasifu matendo yako, Kitayatangaza matendo yako makuu.

5 Nitaifikiri fahari ya utukufu wa adhama yako, Na matendo yako yote ya ajabu.

6 Watu watayataja matendo yako ya kutisha, Nami nitausimulia ukuu wako.

7 Watalihubiri kumbukumbu la wema wako mkuu. Wataiimba haki yako.

8 Bwana ana fadhili, ni mwingi wa huruma, Si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa rehema,

9 Bwana ni mwema kwa watu wote, Na rehema zake zi juu ya kazi zake zote”.

Hivyo na sisi pia inapendeza kama tukimwimbia Mungu wetu, wimbo wa sifa za kweli za kumtukuza yeye na kumpa yeye utukufu, kwasababu Mungu anaketi katika sifa, na ni vizuri kabisa tukamwimbia kwa vinanda vya zote,

Zaburi 147:1 “Haleluya. Msifuni Bwana; Maana ni vema kumwimbia Mungu wetu, Maana kwapendeza, kusifu ni kuzuri”

 Zaburi 149:1 “Haleluya. Mwimbieni Bwana wimbo mpya, Sifa zake katika kusanyiko la watauwa”

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

TENZI ZA ROHONI

SIKU YA HUKUMU ITAKUWAJE?

JE KUHUDUMU KWA NYIMBO ZA INJILI KUKOJE?

YOTE NAMTOLEA YESU_Tenzi za Rohoni.

MWAMBA WENYE IMARA

Rudi Nyumbani:

Print this post

USIKATE TAMAA UNAPOPITIA MAGONJWA.

Unaweza kuwa umempokea Yesu, na unapitia ugonjwa ambao ni mbaya sana, na pengine usio na tiba, Na unajiuliza inawezekanikaje mimi mtu wa Mungu niwe na ugonjwa kama huu?, au mwanangu? Na mimi namcha Mungu sana na kujitahidi kwenda katika njia zake?.

Ukishafikia hali kama hiyo usianze kunung’unika, badala yake huo ndio uwe wakati wa kutafuta kulijua Neno la Mungu zaidi, kwasababu Neno la Mungu ndio dawa ya kutibu hali unayoipitia.

Sasa kama wewe unadhani ni mtumishi wa Mungu na unapitia hilo tatizo, hebu mtafakari Ayubu, labda yeye alimpendeza Mungu kuliko wewe, lakini aliponywa shida yake wakati wa Bwana ulipofika.

Tukimwacha huyo, yupo mtumishi mwingine wa Mungu, mkubwa sana katika biblia…ambaye Mungu alikuwa anazungumza naye uso kwa uso. Na biblia inasema baada yake hakukuwahi kutokea nabii kama huyo..

Kumbukumbu 34:10 “Wala hajainuka tena katika Israeli NABII KAMA MUSA, ambaye Bwana alimjua uso kwa uso;

11 katika ishara zote na maajabu yote, ambayo Bwana alimtuma kuyatenda katika nchi ya Misri, kwa Farao, na kwa watumishi wake wote, na kwa nchi yake yote”

Huyo ni Musa ambaye wengi wetu tunamjua. Lakini Pamoja na Nabii huyu kupata kibali  hicho cha kipekee mbele za Mungu, lakini siku moja alishawahi kupata ugonjwa wa laana usio na tiba. Siku moja alishawahi kupata UKOMA tena ule mweupe unaowaka kama theluji.

Kutoka 4: 6 “Bwana akamwambia tena, Sasa tia mkono wako kifuani mwako. Akautia mkono wake kifuani mwake; naye alipoutoa, kumbe! MKONO WAKE ULIKUWA UNA UKOMA, umekuwa mweupe kama theluji”

Huyo ni mtumishi wa Mungu kapata ukoma, ugonjwa ambao ulikuwa ni mbaya kuliko wote nyakati za hizo, na ulikuwa ni ugonjwa wa laana na pigo na usiokuwa na tiba. Hivyo Musa aliupata huu ugonjwa mbele za Mungu. Unaweza kujiuliza kwanini Mungu hakufanya ishara nyingine, mfano wa hizo za nyoka, badala yake akampa hiyo ya Ugonjwa?.

Kwanini asingemwambia tu, tia mkono wako kifuani na ghafla kutokee katika mkono wake dhahabu au almasi, lakini kinyume chake mkono wake uligeuka kuwa mauti,

Na kwanini aitumie hiyo ishara kwenye mwili wa Musa mtumishi wake, na wala si kwa mtu mwingine asiye wake au mnyama?.

Hiyo ni kuonyesha kwamba hata watu wanaompendeza Mungu wakati mwingine watapitia pia magonjwa, tena yale hatari kabisa yasiyo na uwezekano wa kupona, lakini Bwana atayaondoa kama alivyoondoa kwa Ayubu na Musa..

Zaburi 34: 18 “Bwana yu karibu nao waliovunjika moyo, Na waliopondeka roho huwaokoa.

19 Mateso ya mwenye haki ni mengi, Lakini Bwana humponya nayo yote”.

Na ndio maana Bwana akamwonyesha Musa ile ishara ya kuugua na kuponywa, kuonyesha kwamba yeye ni Mungu atuponyaye..

“Akasema, Tia mkono wako kifuani mwako tena. Akautia mkono wake kifuani mwake tena, na alipoutoa kifuani mwake, kumbe! Umerudia hali ya mwili wake”.

Hivyo magonjwa, na dhiki za kitambo zisituogopeshe, na kutufanya tunung’unike, au moto wako wa kumtafuta Mungu uzime!.. ni za muda tu! Na zitaisha, Usiache kumwamini Mungu wala usipunguze kumtumikia, kwasababu Mungu atakuponya tu kwa wakati wake..na kila kitu kitarudi kama kilivyokuwa. Wala usiruhusu mawazo yako kila dakika yafikirie ugonjwa wako, mawazo kama hayo yakija yakatae na yapeleke kutafakari vitu vingine, kwasababu vita vikubwa vya shetani vipo katika akili zetu na mawazo yetu.

Mwisho, Neno la Mungu ndio silaha kama tulivyotangulia kusema..usipotaka kusoma Neno binafsi, na mara kwa mara, huwezi kamwe kumshinda shetani, hata uwe mwombaji kiasi gani.. Kwasababu shetani kinachomwogopesha sana, ni jinsi tunavyoyaelewa maandiko. Akijua unayaelewa maandiko vizuri, anakuwa anakuhofu sana..lakini akijua Neno hulielewi vizuri, wewe ndio unakuwa rafiki yake, atakutesa kwa kila aina ya mateso anayoyajua yeye. Na kama hujampokea Kristo neema inakuita leo, mpokee Yesu ufanyike kiumbe kipya.

Bwana akubariki sana.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618


Mada Nyinginezo:

USIWE NA HOFU, USHUKAPO CHINI.

NI JAMBO GANI LINALOMTAMANISHA SANA BWANA TUMWOMBE BILA KUKATA TAMAA?

RUDIA, TENA NA TENA KUMWOMBA MUNGU USIKATE TAMAA.

UTAFIKA WAKATI WA WEWE KUACHWA NYIKANI.

RUDI KUMPA MUNGU UTUKUFU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Kongwa ni nini kwenye biblia?(Wagalatia 5:1)

Kongwa ni kifungo cha shingoni. Kwa jina lingine ni nira. Tazama picha.

Hivi ni baadhi ya vifungu vinavyolitaja neno hilo;

Kumb 28:48 “kwa hiyo utawatumikia adui zako atakaowaleta Bwana juu yako, kwa njaa, na kwa kiu, na kwa uchi, na kwa uhitaji wa vitu vyote; naye atakuvika kongwa la chuma shingoni mwako, hata atakapokwisha kukuangamiza”.

Matendo 15:10 “Basi sasa mbona mnamjaribu Mungu na kuweka kongwa juu ya shingo za wanafunzi, ambalo baba zetu wala sisi hatukuweza kulichukua”.

Wagalatia 5:1 “Katika ungwana huo Kristo alituandika huru; kwa hiyo simameni, wala msinaswe tena chini ya kongwa la utumwa”.

1 Timotheo 6:1 “Wo wote walio chini ya kongwa, hali ya utumwa, na wawahesabie bwana zao kuwa wamestahili heshima yote, jina la Mungu lisitukanwe wala mafundisho yetu.

Walawi 26:13 “Mimi ndimi Bwana, Mungu wenu, niliyewaleta mtoke katika nchi ya Misri, ili msiwe watumwa wao; nami nimeivunja miti ya kongwa lenu, nikawaendesha mwende sawasawa”.

1Wafalme12:4 “Baba yako alilifanya zito kongwa letu; basi sasa utupunguzie utumwa mzito tuliotumikishwa na baba yako, na lile kongwa zito alilotutwika, nasi tutakutumikia”.

Swali ni je! sisi tupo chini ya kongwa la nani? La Mungu au la shetani?. Mtu yeyote ambaye hajaokoka, haijalishi atakuwa na mafanikio makubwa kiasi gani, tayari yupo chini ya kongwa la shetani, na anaongozwa kuelekea kuzimu. Lakini aliyemwamini Yesu na kuoshwa dhambi zake, yupo chini ya kongwa/Nira ya Kristo, akiongozwa kuelekea uzimani (Mathayo 28:11).

Hivyo tujitathimini sisi tupo upande gani, na kama hatujaokoka, basi tumpe Bwana leo maisha yetu ayaokoe, kwasababu hizi ni nyakati za mwisho.

Shalom.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618

Mada Nyinginezo:

Hori ni nini kibiblia (Waamuzi 5:17, Luka 2:7)?

Nyungu ni nini kibiblia?(Ayubu 41:20,31, Waamuzi 6:19)

Areopago ni nini? Kwanini mtume Paulo walimpeleka huko?

Arabuni maana yake ni nini?

Nyama zilizosongolewa ni zipi?Je kunywa damu ni dhambi?

Rudi Nyumbani:

Print this post