Category Archive Home

NGUVU ZA MUNGU

Nguvu za Mungu ni nini?, Nguvu ya Imani ni nini? Na jinsi gani ya kupokea nguvu za Mungu..

Karibu tujifunze maswali haya machache..

NGUVU ZA MUNGU NI NINI?

Kabla ya kuelewa nguvu za Mungu ni nini, ni vizuri tukajua maana ya nguvu.. “Nguvu maana yake ni uwezo wa kufanya kitu au jambo”..Kwahiyo nguvu za Mungu ni uwezo wa Mungu kufanya mambo…Nguvu hizo zinapomwingia mtu, Mtu huyo anakuwa na uwezo wa kufanya jambo kama Mungu.

Sasa tukitazama ulimwengu tunaweza kuona vitu vilivyoumbwa..ikiwa na maana kuwa ilitumika nguvu fulani kuviumba vitu hivyo..Na hiyo ni dhahiri kuwa sio nguvu inayotokana na  chakula..kwasababu hakuna mtu mwenye misuli mikubwa anayetegemea misuli iliyotengenezwa na chakula anachokula mwenye  uwezo wa kulining’iniza jua kule juu kabisa, au kuujaza mlima kwa mawe na udongo kwa kiwango kile…Hiyo inamaanisha kuwa  ni lazima kuna nguvu nyingine imetumika kufanya hayo..isiyotokana na chakula. Sasa kuivumbua nguvu hiyo iliyoyafanya hayo yote ndio tunarudi kwenye kitabu kinachoitwa biblia kupata jibu lake.

Waebrania 11:3 “Kwa imani twafahamu ya kuwa ulimwengu uliumbwa kwa neno la Mungu, hata vitu vinavyoonekana havikufanywa kwa vitu vilivyo dhahiri”.

Kwa kupitia mstari huo tunaweza sasa kupata majibu yetu kwamba vitu vyote Mungu aliviumbwa kwa Imani. Hivyo Imani ndio Nguvu ya Mungu…Na imani ya KiMungu inaposhuka ndani yetu nasi pia tunakuwa na nguvu za kufanya makubwa kama aliyoyafanya Mungu wetu.

Na tafsiri ya Imani tunaipata katika biblia hiyo hiyo..

Waebrania 11:1 “Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana.”.

NGUVU YA IMANI

Imani ina uwezo wa kufanya mambo makubwa ambayo kwa namna ya kawaida yanaweza kuonekana kama hayawezekaniki…Biblia inasema kwa Imani mtu anaweza kuhamisha milima.(1Wakorintho 13:2)

Luka 17:6 “Bwana akasema, Kama mngekuwa na imani kiasi cha chembe ya haradali, mngeuambia mkuyu huu, Ng’oka, ukapandwe baharini, nao ungewatii”.

Mathayo 17:20 “amin, nawaambia, Mkiwa na imani kiasi cha punje ya haradali mtauambia mlima huu, Ondoka hapa uende kule; nao utaondoka; wala halitakuwako neno lisilowezekana kwenu.

NAMNA YA KUPOKEA NGUVU  ZA MUNGU.

Kama tulivyotangulia kusoma kwamba nguvu za Mungu ni IMANI, Hivyo kupokea nguvu hizo ni sawa na kusema kupokea Imani kama ile ya Mungu.

Sasa namna ya kuipata hiyo Imani ambayo ndiyo nguvu zenyewe za Mungu tunaisoma kwenye Biblia kama ifuatavyo.

Warumi 10:17 “Basi imani, chanzo chake ni kusikia; na kusikia huja kwa neno la Kristo”.

Unapolisikia  Neno la Kristo na kulitafakari na kulielewa..kiwango fulani cha Imani kinajengeka ndani yako..na ujasiri unaongezeka pia..na mtu anavyozidi kulielewa zaidi na zaidi ndivyo imani yake inavyozidi kukua zaidi na zaidi…mpaka anapofikia kiwango cha kufanya makubwa.

Hivyo Neno la Mungu ndio Biblia takatifu, na ndio Neno la Kristo…Popote panapozungumziwa Neno la Mungu ndio hilo hilo neno la Kristo, na ndio hiyo hiyo Biblia takatifu…maneno hayo matatu yasikuchanganye.

Ukiwa na nguvu hizi za Mungu za kutosha hakuna chochote kitakachoweza kukushinda kama vile kwa Mungu hakuna chochote kinachoweza kumshinda sasa…kwasababu ana nguvu nyingi.

Je unataka leo uanze kupokea Nguvu hizi za Mungu?..anza kwa kulisoma Neno hili la Kristo na kulitii…

Mathayo 11:28 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.

29 Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;

30 kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi”.

Ukilisoma Neno hili na kulielewa na kukata shauri la kutubu na kumfuata Yesu kwa moyo wako wote..utakuwa ndio mwanza wa kupokea Nguvu za Mungu.

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

NINI MAANA YA UCHAWI?

KWA KUWA NGUVU ZA MBINGUNI ZITATIKISIKA.

KUOTA UNAKULA CHAKULA.

NITAPOKEAJE NGUVU YA KUSHINDA DHAMBI?

HUDUMA YA (ELIFAZI, SOFARI, NA BILDADI).

NENO LA MUNGU NI TAA

TENZI ZA ROHONI

Rudi Nyumbani:

Print this post

KUOTA MAFURIKO,KUOTA MAJI MENGI,KUOTA MAWIMBI.

Wingu la Mashahidi
Wingu la Mashahidi
KUOTA MAFURIKO,KUOTA MAJI MENGI,KUOTA MAWIMBI.
/

Naomba kufahamu Je! Kuota mafuriko ni kiashiria cha nini?

Mafuriko kazi yake si nyingine Zaidi ya kugharikisha, tofauti na mvua ambayo kazi yake ni kustawisha na kuleta mazao.. Hivyo ikiwa unaota ndoto ya namna hii mara kwa mara, au imekujia mara moja lakini kwa uzito sana, ambao sio wa kawaida basi ujue bila shaka kuwa kuna mafuriko makubwa (rohoni) yapo mbele yako, wengine utakuta wanaota mto umefurika na unataka kuwachukua, na kwa chini maji yake yanakwenda kwa kasi sana, au wengine wanaota wapo baharini na mawimbi makubwa yanakipiga chombo chao kidogo, kisha kinaanza kuyumba yumba na kuanza kuzama, wangine wanaogelewa lakini maji yanawazidia wanashindwa kuendelea mbele..n.k. Hivyo Ukikutana na ndoto yoyote inayohusiana na maji mengi(mafuriko) ujumbe wake ni mmoja, kwamba HATARI IPO MBELE YAKO..Na mafuriko hayo hayaletwi na mwingine zaidi ya shetani.

Sasa ndoto hii inalenga makundi yote mawili.

Kundi la Kwanza:Ni la watu ambao hawajamjua bado Kristo. 

Watu ambao wapo mbali na wokovu, ambao Yesu Kristo hajawabadilisha Maisha yao. Ikiwa wewe ni mmojawapo na umeota ndoto ya namna hiyo, basi ujue kuwa ni Mungu anakuonyesha, ni jinsi gani, mwisho wako utakavyokuwa,..Nataka nikuambie Sikuzote ukiwa nje ya Yesu Kristo hakuna wimbi ambalo halitakuchukua, liwe kubwa au dogo..kwasababu nyumba yako hujaijengwa juu ya mwamba ulio imara..

Sikia Yesu anachokisema…

Mathayo 7:24  “Basi kila asikiaye hayo maneno yangu, na kuyafanya, atafananishwa na mtu mwenye akili, aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba;

25  mvua ikanyesha, MAFURIKO YAKAJA, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, isianguke; kwa maana misingi yake imewekwa juu ya mwamba.

26  Na kila asikiaye hayo maneno yangu asiyafanye, atafananishwa na mtu mpumbavu, aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga;

27  mvua ikanyesha, MAFURIKO YAKAJA, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, ikaanguka; nalo anguko lake likawa kubwa”.

Hivyo inategemea na maisha yako yalivyo, kama wewe ni mlevi basi ujue lipo furiko la mauti ibilisi amekuandalia kukuletea katika huo huo ulevi wako.., kama wewe ni mzinzi basi jiandae na furiko lihusianalo na uzinzi wako ambalo litakuchukua na kukupeleka moja kwa moja mpaka kuzimu..Kama wewe ni mlaji rushwa, ni mwizi, ni tapeli, ni muuaji, ni mshirikina, ni mwabudu sanamu, basi jiandae na furiko la mauti mbele yako..ambalo halitakuachia kichwa wala mkia..Utakwenda moja kwa moja, na ghafla utajikuta kuzimu..kwasababu hiyo ndio nia ya shetani sikuzote..Soma Ufunuo 12:14-17

Kundi la Pili: Watu ambao wameokoka.

Ikiwa wewe upo ndani ya Kristo(Umeokoka).. na unaota ndoto zihusianazo  na mafuriko, basi ujue ni aidha Mungu anakuonyesha hatari iliyopo mbele yako, hila ulizopangiwa na ibilisi hivyo Bwana anataka akuepushe nazo..

Hivyo hapo unapaswa uongeze viwango vyako vya maombi, usiwe mvivu omba kwa bidii, na kudumu katika utakatifu..Kiasi kwamba hata wimbi lolote(mafuriko) la ibilisi likikuta katika mazingira yoyote yale basi huwezi kupepesuka kwasababu umejengwa juu ya mwamba imara Yesu Kristo..

Au namna nyingine ni Mungu anakutahadharisha, utazame vizuri hali yako ya kiroho sasa…Pengine umerudi nyuma na hiyo itakuwa kwako rahisi kuchukuliwa na mawimbi ya mafuriko hivyo unapaswa uimarishe wokovu wako usimame imara..

ZABURI 124

“1 Kama si Bwana aliyekuwa pamoja nasi, Israeli na aseme sasa, 

2 Kama si Bwana aliyekuwa pamoja nasi, Wanadamu walipotushambulia. 

3 Papo hapo wangalitumeza hai, Hasira yao ilipowaka juu yetu 

4 Papo hapo maji yangalitugharikisha, Mto ungalipita juu ya roho zetu; 

5 Papo hapo yangalipita juu ya nafsi zetu Maji yafurikayo. 

6 Na ahimidiwe Bwana; Asiyetutoa kuwa mawindo kwa meno yao. 

7 Nafsi yetu imeokoka kama ndege Katika mtego wa wawindaji, Mtego umevunjika, nasi tumeokoka. 

8 Msaada wetu u katika jina la Bwana, Aliyezifanya mbingu na nchi”.

Amen.

Je! Ungependa kuokoka leo?

Ni vizuri ukafanya maamuzi hayo haraka..Usijiangalie labda wewe ni muislamu, au ni mkristo..ikiwa Kristo yupo mbali na wewe, haijalishi ulizaliwa katika dini au la, maisha yako sikuzote yatakuwa hatarini..Leo hii sikuambii umpe YESU Maisha yako, ili kusudi kwamba hatari hizo zisikukute mbeleni..Hapana pamoja na hayo ndani ya Kristo zipo faida nyingi utazipata..Kwanza kabisa atakupa uzima wa milele, Na Pili anakupenda na anakuhitaji wewe mwana wake uliyepotea.. aliyekuumba ukae katika uwepo wake..Umfurahie yeye na yeye akufurahie wewe.

Hivyo Ikiwa upo tayari leo hii Yesu aingie ndani yako..Na umemaanisha kweli kutaka kubadilika na akuokoe Maisha yako na dhambi zako zote basi..

Basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU  MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, . NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.

Ubarikiwe sana

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312

   Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo:

KUOTA UPO UCHI.

BONDE LA KUKATA MANENO.

NINI KINAFUATA SIKU ILE ILE YA KUOKOKA!

UVUMILIVU WA MUNGU ULIPOKUWA UKINGOJA.

TUUTAZAME PIA MWISHO WA UJENZI WETU.

UNYAKUO.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

KWANINI WENGINE WANYAKULIWE,NA WENGINE WAACHWE?

TOA SADAKA ISIYO NA KASORO KWA BWANA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

JINSI MUNGU ANAVYOIPIGA NA KUIPONYA AFRIKA.

Leo hii dunia nzima inaishangaa Afrika kwa mambo mawili makuu : La kwanza ni umaskini wake, na pili jinsi lilivyojikita katika mambo ya Imani . Bara pekee lenye idadi kubwa ya watu wanaoishi kwa kuamini  “mungu” kwasasa ni Afrika tu. Jambo ambalo huwezi kuliona katika bara lingine lolote duniani.

Leo hii tutaona sababu za kibiblia ni kwanini tupo hivi, ili na wewe ujue ni wapi unapopaswa usimame..katika nafasi yako Afrika.

Watu wasioamini Mungu, wala wasioisoma biblia wanatafsiri umaskini wa waafrika ni kutokana na uvivu wao, na ujinga wao, lakini ukweli ni kwamba zipo jamii zenye watu wavivu kuliko hata waafrika, lakini bado wanao maendeleo makubwa zaidi yetu,.

Vilevile licha ya biblia kutuonyesha kuwa maendeleo makubwa tangu zamani yalianzia katika bara la Afrika lakini historia pia inathibitisha hilo kwamfano yale mapiramidi yalio kule Misri, na Ethiopia hadi leo hii hakuna Uinjinia wowote umewahi kufikia ile teknolijia..Hiyo ni kuonyesha kuwa sio kwamba waafrika ni wajinga kama wanavyofikiriwa..

Lakini Biblia inatuambia kuwa ni yeye Mungu mwenyewe ndiye aliyeifanya Afrika kuwa duni kuliko mataifa yote ulimwenguni. Na hiyo yote ni kwasababu ya miungu yao na sanamu zao..Ukisoma Kitabu cha Isaya sura ya 19 chote na Ezekieli sura ya 29 vinaeleza unabii juu ya bara la Afrika. Hatuwezi kuandika aya zote hapa kwa nafasi yako unaweza ukazisoma..lakini tutaangalia baadhi ya aya..

  1. Awali ya yote biblia ilishatabiri kuwa waafrika watawaliwa.

Tusome

Isaya 19:4 “Nami nitawatoa hao Wamisri na kuwatia katika mikono ya bwana mgumu; na mfalme mkali atawatawala; asema Bwana, Bwana wa majeshi”.

Sasa kumbuka sehemu nyingine biblia inapoitaja Misri ujue inawakilisha bara zima la Afrika..

Ilishatabiri kuwa juu ya utawala wa wakoloni, wa kibepari..

  1. Vilevile ilishatabiri kuwa itachukuliwa utumwani, kama vile wana wa Israeli walivyochukuliwa utumwani:

Ezekieli 29:12 “Nami nitaifanya nchi ya Misri kuwa ukiwa, kati ya nchi zilizo ukiwa, na miji yake, kati ya miji iliyoharibika, itakuwa maganjo muda wa miaka arobaini; nami nitawatawanya Wamisri kati ya mataifa, nami nitawatapanya kati ya nchi mbalimbali.

13 Maana Bwana MUNGU asema hivi; Mwisho wa miaka arobaini nitawakusanya Wamisri, na kuwatoa katika hizo kabila za watu, ambazo walitawanyika kati yao;

14 nami nitawarejeza Wamisri walio katika hali ya kufungwa, nami nitawarudisha hata nchi ya Pathrosi, hata nchi ya kuzaliwa kwao; NA HUKO WATAKUWA UFALME DUNI.

15 UTAKUWA DUNI KULIKO FALME ZOTE; wala hautajiinua tena juu ya mataifa; nami nitawapunguza, ili wasitawale tena juu ya mataifa”.

Unabii, huo ulitimia, Afrika ilianza kuangia utumwani na kutawaliwa kuanzia karne ya 16 na mpaka kufikia karne ya 19, utumwa ulikoma, hiyo ni miaka 400 kama vile wana wa Israeli walivyokaa Misri. Na Mungu alishasema itakuwa duni kuliko mataifa yote.

Lakini Kwanini Mungu aliruhusu hivyo? Je analipiza kisasi au anawachukia waafrika?

Jibu ni hapana sura hizo mbili zinatuonyesha Mungu alimua kufanya hivyo kwa watu wa Afrika kwasababu ya miungu yao, na sanamu zao, na uchawi wao, na uganga wao, na upigaji ramli wao (Isaya 19:3), ambavyo vimefaraka naye.. aliwadhoofisha kwa makusudi ili wajue kuwa hivyo vitu haviwezi kuwasaidia na kwamba wakati umefika sasa Mungu anawahitaji waafrika wamtumike yeye.

Kama tu leo hii, Mungu ameliadhibu bara hili lakini bado unaona waganga na uchawi bado ni mwingi, angaliacha katika mafanikio yake liwe kama mabara mengine yaliyofanikiwa duniani unadhani lingekuwaje? ndio lingekuwa chanzo cha machukizo yote ya ulimwengu mzima kotekote..rohoni na mwilini…Uchawi uliokuwepo kuanzia Misri(ambayo ipo ndani ya Bara la Afrika) ulikuwa ni wa viwango vya juu sana..walikuwa na uwezo wa kubadilisha fimbo kuwa nyoka. Mungu asingeukomesha saa hii ungekuwa umefikia viwango gani?

Hivyo Mungu ametupiga ili tumgeukie yeye hiyo ndio sababu kuu..Na jambo hilo ni kweli limezaa matunda, kwasababu leo hii Neema ya Mungu kweli ipo Afrika, idadi kubwa ya watu waliomaanisha kumtafuta MUNGU ipo Afrika, Hapo ndipo Mungu alipotuponyea..

Kitendo cha sisi kuchukuliwa utumwani, na kutawaliwa na mabepari, kulitufanya sisi tumtafute Mungu wa kweli.

Soma hapa biblia inavyosema..

Isaya 19:20 “Nayo itakuwa ishara na ushuhuda kwa Bwana wa majeshi katika nchi ya Misri; kwa maana watamlilia Bwana kwa sababu ya watu wawaoneao, naye atawapelekea mwokozi mwenye kuwatetea, naye atawaokoa.

21 Na Bwana atajulikana na Misri, na Wamisri watamjua Bwana katika siku hiyo; naam watamtumikia kwa dhabihu na matoleo, nao watamwekea Bwana nadhiri, na kuzitekeleza.

22 NAYE BWANA ATAPIGA MISRI, AKIPIGA NA KUPONYA; NAO WAKIRUDI KWA BWANA, ATAKUBALI MAOMBI YAO NA KUWAPONYA.

23 Katika siku hiyo itakuwako njia kuu itokayo Misri na kufika hata Ashuru; Mwashuri atafika Misri, na Mmisri atafika Ashuru, na Wamisri wataabudu pamoja na Waashuri.

24 Katika siku hiyo Israeli atakuwa wa tatu pamoja na Misri na Ashuru, watakuwa baraka kati ya dunia;

25 kwa kuwa Bwana wa majeshi amewabariki, akisema, WABARIKIWE WATU WANGU MISRI; na wewe Ashuru, kazi ya mikono yangu; na wewe Israeli, urithi wangu”.

Unaona, Mstari wa 21 unatuambia waafrika watajulikana na Bwana, watamtumikia kwa dhabihu na matoleo.. Lakini vilevile anasema atapiga na kuponya… na mstari wa 25 Mungu anasema, WABARIKIWE WATU WANGU MISRI.

Hivyo suala la umaskini wa Afrika, limeruhusiwa kabisa kwasababu hii, ili tumrudie yeye kwasababu anatupenda..

Umaskini wetu umesababishia utajiri wa Imani kwa Mungu..na ndio maana biblia inasema..

Yakobo 2:5 “…..Je! Mungu hakuwachagua maskini wa dunia wawe matajiri wa imani na warithi wa ufalme aliowaahidia wampendao”?

Hivyo itakuwa ni jambo la kushangaza, Mungu amekuweka wewe na mimi katika nchi kama hizi, halafu bado huielewi sauti ya Mungu inataka nini kwako hutaki kuyasalimisha maisha yako kwa Bwana Yesu anayekupenda… Unaishi katika nchi ambazo utasikia injili kila kona ya barabara inahubiriwa,..lakini bado unapuuzia na kudhihaki, mataifa mengine wanaagiza wamishionari kutoka Afrika wawapelekee Neno la Mungu, lakini wewe unaichezea neema hii…Sasa hata hichi ukikikosa, ni nini basi utakuwa nacho ndugu?

Kumbuka hata hivyo neema hii nayo haitadumu huku milele, hivi karibuni Mungu atairejeza Israeli ilipoanzia, biblia inatabiri hivyo, na hapo ndipo mataifa yote ulimwenguni yataurudia upagani waliokuwa nayo mwanzoni na kwa pamoja sasa yatafanya kazi na mpinga-Kristo, ili baadaye yaje kuungana kuishambulia Israeli katika vita ile kuu ya mwisho ya Harmagedoni.. (Neema ni kama jua linachomoza upande huu na kuzama upande ule hivyo sio ya kudumu..ni kitu kinachohama..mataifa mengine Neema ya kuisikia injili haipo kabisa..yaani ile nguvu ya kuvutwa haipo…muda wao ni kama ulishapita..Na sisi muda wetu unakaribia kuisha, na neema hii itahamia Israeli..huku itakuwa kuamini injili ni ngumu kama ilivyo mataifa ya magharibi sasahivi)

Lakini sisi tulioipokea neema ya kumwamini YESU KRISTO na sio mtu mwingine yeyote, tutakuwa tumeshakwenda kwenye unyakuo kama haijahamia Israeli..Lakini wewe ambaye unaupenda ulimwengu huu, ambaye bado unaipenda miungu ya ukoo wenu, unakwenda kwa waganga, unapiga ramli, unadharau injili ya msalaba ambayo unapewa leo bure bila malipo yoyote..basi ujiandae tu na kupigwa na mkono wa Bwana kila siku, na baadaye kuishia katika ziwa la moto..

Hizi ni nyakati za hatari, na kila siku tunaona mabadiliko ya dunia..muda huu ni wa nyiongeza tu, Unyakuo ni wakati wowote, parapanda italia wafu watafufuka.. Je! Umejiweka tayari..Jibu lipo moyoni mwako.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Mitume wote waliopita walikuwa ni watu weupe hata manabii wote waliopita hadi Ma-papa ni ngozi nyeupe. ni kweli ngozi nyeusi ililaaniwa ?

WAKAMTUKANA MUNGU, WALA HAWAKUTUBU.

MJUMBE WA AGANO.

KIFO CHA MTAKATIFU POLIKAPI (Policarp).

UVUMILIVU WA MUNGU ULIPOKUWA UKINGOJA.

JINSI ROHO MTAKATIFU ANAVYOWAFUNULIA WATU MAANDIKO.

MAONO YA NABII AMOSI.

UNYAKUO.

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

MJUMBE WA AGANO.

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe..karibu tujifunze Biblia…

Malaki 3: 1 “Angalieni, namtuma mjumbe wangu, naye ataitengeneza njia mbele yangu; naye Bwana mnayemtafuta atalijilia hekalu lake ghafula; naam, yule mjumbe wa agano mnayemfurahia, angalieni, anakuja, asema Bwana wa majeshi”

Mpango wa Mungu katika kumwokoa mwanadamu umegawanyika katika sehemu mbili..Agano la kale(au kwa lugha nyingine agano la kwanza)..pamoja na Agano jipya (au agano la pili).

Ndio ni kawaida lazima viwepo vipande viwili ili kukikamilisha kiumbe hai..Na upande mmoja lazima uwe na nguvu kuliko mwingine…Kwamfano umbile la Mtu limegawanyika katika sehemu mbili zinazofanana…Upande wa kushoto na upande wa kulia…Ndio maana utaona mtu ana miguu miwili, macho mawili, mikono miwili, n.k Na kama ukizidi kuchunguza utaona pia..katika sehemu hizo mbili kuna upande mmoja upo na uwezo mkubwa kuliko upande mwingine..ndio utaona mtu anauwezo wa kuandika vizuri kwa kutumia mkono mmoja tu, na akijaribu kutumia upande mwingine inakuwa ni shida kidogo.. kadhalika anauwezo hata wa kupiga teke kitu kwa utashi Zaidi kupitia huo huo upande anaoutumia mkono wake kuandikia n.k Lakini pande zote hizo mbili zikishirikiana kwa pamoja uwezo unakuwa mkubwa Zaidi..mtu akinyanyua kitu kwa mikono miwili anafanikiwa Zaidi kuliko anayetumia mkono mmoja. N.k

Na biblia ni hivyo hivyo imegawanyika katika sehemu kuu mbili..Agano jipya na Agano la Kale. Agano jipya lina nguvu na uwezo na utashi Zaidi kuliko agano la kale…Ingawa maagano yote mawili ni lazima yaungane ili kulitimiza kusudi la Mungu. Kama vile tusivyoweza kusema hatuhitaji mkono wa kushoto kwasababu ni dhaifu kuliko wa kulia, au hatuhitaji mguu wa kushoto kwasababu ni dhaifu kuliko wa kulia..hapana..vyote viwili vina umuhimu wake..

Sasa Agano la kale mjumbe wake alikuwa Nabii Musa..ambaye ndiye aliyepewa zile amri na sheria awahubirie wana wa Israeli. Na sheria zile zilikuwa zinaandikwa kwenye mawe, na mbao..

Musa alihubiri….Mtu hatakiwi kuzini kwasababu sheria inasema usizini!…mtu hatakiwi kuiba kwasababu sheria inasema usiibe!…Ikiwa na maana kuwa kuna maandishi fulani ya kurejea ili kuzijua amri za Mungu..Kuna mahali fulani pameandikwa kwamba USIZINI! Ndio maana watu hawapaswi kuzini.

Hilo ndio Agano la kwanza…Sheria zilikuwa zimandikwa mahali fulani.

Lakini Agano la pili ambalo mjumbe wake ni Yesu Kristo..kama maandiko yanavyosema katika..

“Waebrania 12:24 “na Yesu mjumbe wa agano jipya, na damu ya kunyunyizwa, inenayo mema kuliko ile ya Habili”.

Yeye(Yesu) sheria za Mungu haziandiki kwenye mawe na mbao na kutupa sisi kama alivyofanya Musa…bali katika vilindi vya mioyo ya watu ndiko anapoziandikia…Maana yake ni kwamba mtu akitaka kupata uhakika kwamba ulawiti ni dhambi bila hata ya kwenda kurejea kwenye maandishi yoyote…inakuwa ile sheria tayari imeshaandikwa ndani yake..Kunakuwa kuna kitu fulani kinamshuhudia ndani yake na kumfundisha kwamba ulawiti ni machukizo kwa Mungu bila hata kwenda kusoma mahali popote…yaani zile sheria za Mungu zinakuwa zinaandikwa moyoni mwake. Kunakuwa kuna masomo fulani yanatiririka ndani yake kupitia hata vitu vya asili kiasi kwamba yule mtu anauwezo wa kutenda mapenzi ya Mungu bila hata kusukumwa sukumwa wala kuwekewa sheria na taratibu, na amri fulani za kufuata kama mtoto mdogo. Anakuwa kila kitu anachokifanya anajua sababu yake.

Ni kama mtu ambaye kakomaa kiakili ambapo anajua akilowa jasho tu anahitaji kwenda kuoga na kubadilisha nguo…anakuwa hana kitabu cha baolojia mbele yake ambacho anatembea nacho na kukirejea kila siku na kutafuta mahali panaposema mtu ni lazima aoge ndipo awe msafri Yeye mwenyewe tu ndani ya akili yake kuna masomo tayari ya umuhimu wa kujiweka msafi bila hata kufundishwa na mtu. Hahitaji kitabu cha baolojia kumfundisha umuhimu wa kuoga, hahitaji kuhubiriwa hubiriwa kila kona umuhimu wa kuoga..haihitaji kukalishwa semina na kukumbushwa kumbushwa…Kwani anajua wajibu wake..kwanza yeye mwenyewe tu atajikuta anapenda kuwa msafi…Na kila siku utakuwa anazidi kutafuta kujiweka kuwa msafi.

Na ndivyo hivyo hivyo Agano jipya linavyofanya kazi… linamfanya mtu atafute kuwa msafi (yaani Mtakatifu) bila kuwekewa sheria wala kusukumwa sukumwa..linamfanya mtu aone ndani yake kwamba kuna kila sababu ya yeye kujiweka mbali na uchafu wa ulimwengu huu, kujiweka mbali na anasa, uasherati, utukanaji, usagaji, wizi…Linazidi kumfanya aone sababu ya yeye kuiogesha roho yake kila siku kwa kujifunza Neno na maombi…Agano hili halihitaji kila siku kumkumbusha mtu wajibu wake.. Wote walioingia katika agano hili wanatimiza sheria ya Kristo ndani ya mioyo yao bila shuruti. Na hiyo yote inachochewa na Roho Mtakatifu atakayeingia ndani ya mtu.

Utauliza ni wapi katika maandiko, Agano hili la sheria kuandikwa ndani ya mioyo yetu lilitabiriwa..?

Waebrania 8:8 “Maana, awalaumupo, asema Angalia, siku zinakuja, asema Bwana, Nami nitawatimizia nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda agano jipya;

9 Halitakuwa kama agano lile nililoagana na baba zao, Katika siku ile nilipowashika mikono yao niwatoe katika nchi ya Misri. Kwa sababu hawakudumu katika agano langu, Mimi nami sikuwajali asema Bwana.

10 Maana hili ndilo agano nitakaloagana na nyumba ya Israeli Baada ya siku zile, asema Bwana; NITAWAPA SHERIA ZANGU KATIKA NIA ZAO, NA KATIKA MIOYO YAO NITAZIANDIKA; NAMI NITAKUWA MUNGU KWAO, NAO WATAKUWA WATU WANGU.

11 Nao hawatafundishana kila mtu na jirani yake, Na kila mtu na ndugu yake, akisema, Mjue Bwana; Kwa maana wote watanijua, Tangu mdogo wao hata mkubwa wao.

12 Kwa sababu nitawasamehe maovu yao, Na dhambi zao sitazikumbuka tena.

13 Kwa kule kusema, Agano jipya, amelifanya lile la kwanza kuwa kuukuu. Lakini kitu kianzacho kuwa kikuukuu na kuchakaa ki karibu na kutoweka”

Unaona hilo ndio agano jipya!… Ukitaka kutafuta ni wapi kwenye biblia Mungu kakataza sigara ni Dhahiri kuwa agano hili bado halijakuingia ndani yako..ukitaka kutafuta ni wapi kwenye biblia nguo za kubana na suruali, na vimini, na vipodozi vimekatazwa…fahamu kuwa bado agano hili halijaingia ndani yako, ukitafuta kwenye biblia ni wamendikwa usitoe mimba ni dhambi, au usitumie madawa ya kulevya.. Ni sawa na kutafuta ndani ya kitabu cha baolojia ni wapi pamekataza watu kupiga mswaki?

Je! Unataka kuingia ndani ya hili agano leo?..Yupo Mjumbe wake…ni lazima umkubali huyo kwanza…ukimkubali huyo na akiingia ndani yako atayaondoa yote ya kale na kuyafanya yote kuwa mapya..Atazibua ufahamu wako kwa Yule ROHO MTAKATIFU atakayekupa kiasi kwamba utaona kuzishika sheria za Mungu sio ngumu..utaona kuwa mtakatifu sio kugumu…

Unaona Watoto wadogo wanavyosumbua kuoga wenyewe mpaka uwalazimishe sana..lakini mtu mzima anakuwa anaoga hata mara 3 kwa siku kwa miaka 20..na wala hachoki?..Ndivyo na wewe Yesu Kristo atakachokifanya ndani yako…Ataigeuza akili yako kwa Roho wake Mtakatifu na kuwa kama ya mtu mzima…hutatamani hata kusikia harufu ya uasherati, wala matusi, wala uchungu, wala vinyongo, wala kujichua, wala kutazama picha chafu mitandaoni, wala pombe. Na juu ya hayo atakupa uzima wa milele.

Waebrania 9:15 “Na kwa sababu hii ni MJUMBE WA AGANO JIPYA, ILI, mauti ikiisha kufanyika kwa kukomboa makosa yaliyokuwa chini ya agano la kwanza, hao walioitwa waipokee ahadi ya urithi wa milele”.

Kama unataka leo Mjumbe huyo aingia ndani yako na kukutengeneza…

Basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, .

NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu katika Roho na Kweli, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.

Ubarikiwe sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

TOFAUTI KATI YA SHERIA YA ROHO WA UZIMA NA SHERIA YA DHAMBI NA MAUTI!

KWANINI WENGINE WANYAKULIWE,NA WENGINE WAACHWE?

WANA WA MUNGU, NA BINTI ZA WANADAMU.

Kwanini Bwana Yesu, aliruhusu yale mapepo yawaingie nguruwe?

Sanduku la Agano lilikuwa linawakilisha nini katika Agano jipya?

ANGALIA USIJE UKANG’OA NGANO KATIKATI YA MAGUGU.

MAJINI WAZURI WAPO?

JE KUPONYWA NI UTHIBITISHO WA MUNGU KUWA NA WEWE?

Rudi Nyumbani:

Print this post

NINI TOFAUTI KATI YA KARAMA, UTENDAJI KAZI NA HUDUMA.

Nini tofauti kati ya karama ya rohoni, utendaji kazi na huduma?. Vitu hivi vitatu ni ni ni hasa?

Shalom.Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe…Karibu tuongeze maarifa katika kujifunza Neno la Mungu..

Leo kwa Neema za Bwana tutajifunza  kidogo juu ya karama za Rohoni…Zinaitwa karama za rohoni kwasababu sio za mwilini..zipo karama za mwilini na za rohoni pia…Kila mwanadamu kaumbiwa na karama fulani ya mwilini…iwe anaijua au haijui..Na vile vile kila mtu anayo karama ya rohoni…

Karama ya rohoni lengo lake kuu ni kutumika kwaajili ya faida ya ufalme wa Mbinguni…Lakini mtu akiwa nje ya Kristo karama ile inakuwa inatumika na ajili ya ufalme wa giza aidha awe anajua au hajui. Sasa leo hatutaingia huko sana…bali tutajifunza maana ya KARAMA, HUDUMA na UTENDAJI KAZI.

Kama Umempa Yesu Kristo Maisha yako…na hujajua karama yako ni ipi..nakushauri ukatafute kujua maarifa hayo kwa bidii zote kwasababu ni muhimu sana kuyajua. Na kama hujui sehemu ya kuyapata tunalo somo juu ya hilo..kama ukilihitaji unaweza ukatutumia ujumbe ufupi inbox tukutumie.

Lakini leo hii tutaangazia tofauti kati ya KARAMA, HUDUMA na UTENDAJI KAZI.

Biblia inasema katika…

1Wakorintho 12:1 “Basi, ndugu zangu, kwa habari ya karama za roho, sitaki mkose kufahamu.

2  Mwajua ya kuwa mlipokuwa watu wa Mataifa, mlichukuliwa kufuata sanamu zisizonena, kama mlivyoongozwa.

3  Kwa hiyo nawaarifu, ya kwamba hakuna mtu anenaye katika Roho wa Mungu, kusema, Yesu amelaaniwa; wala hawezi mtu kusema, Yesu ni Bwana, isipokuwa katika Roho Mtakatifu.

4  Basi pana tofauti za KARAMA; bali Roho ni yeye yule.

5  Tena pana tofauti za HUDUMA, na Bwana ni yeye yule.

6  Kisha pana tofauti za KUTENDA KAZI, bali Mungu ni yeye yule azitendaye kazi zote katika wote.

7  Lakini kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho kwa kufaidiana”

Kama tunavyoona hapo pana vitu vitatu…Karama, huduma…na utendaji kazi…Wengi imewawia ngumu kutofautisha vitu hivi..lakini leo kwa Neema za Bwana tutajifunza tofauti zake tukijifunza kupitia mifano ya kimaisha.

Mungu anapompa mtu karama… anaweza kumpa karama moja, au wakati mwingine mbili au tatu kwa mpigo…Lakini wengi Bwana anawapa karama moja tu ya rohoni… Na karama moja inaweza kuwa na utendaji kazi tofauti…Karama moja inaweza kuwa na utendaji kazi hata mara 100 tofauti tofauti..

Tuchukue mfano…Hospitalini kunaweza kuwa na madaktari 100, lakini wote hawatendi kazi inayofanana…wengine utakuta wamebobea katika mifupa, wengine vinywa, wengine Ngozi, wengine macho n.k Lakini wote hawa karama yao ni moja “udaktari/utabibu”…Na huduma yao wote ni moja “UAGUZI” wanaagua watu.  Hivyo tunaweza kurahisisha na kusema katika hospitali hiyo kuna watu 100 wenye karama moja na huduma moja lakini utendaji kazi tofauti.

Vivyo hivyo tukirudi kwenye SHULE.. shule inaweza kuwa na waalimu 50, kati ya hao kuna waalimu wa fizikia, kiingereza, biolojia n.k lakini wote hao karama yao ni moja “kufundisha” na huduma yao ni moja nayo ni UALIMU. Na vitengo vingine vyote vya kimaaisha ni hivyo hivyo…kwa wahandisi ni hivyo hivyo, kwa wanajeshi ni hivyo hivyo, utendaji kazi unatofautia n.k.

Tukirudi katika kanisa la Kristo ambalo ndio kitengo kikuu na cha juu na Taasisi iliyo kuu kuliko zote mbele za Mungu..Nalo pia lina watu wenye karama tofauti tofauti, huduma tofauti tofauti na utendaji kazi tofauti.

Kwamfano..Katika karama ya uimbaji wanaweza kuwepo waimbaji 100, kila mmoja akawa na namna yake ya kuimba, wengine wamejaliwa kuimba vyema katika nyimbo za kuabudu, wengine katika nyimbo za sifa, wengine katika nyimbo za tenzi za rohoni n.k hawa wote wanatenda kazi tofauti tofauti lakini karama yao ni moja “kuimba”, na huduma yao ni moja UINJILISTI kwa njia ya NYIMBO.

Hali kadhalika kwenye huduma ya kiualimu,watakuwepo waalimu wa Watoto kanisani, watakuwepo waalimu wa vijana kanisani, watakuwepo waalimu wa kila namna kulingana na Neema kila mtu aliyopewa, wengine waalimu kwa njia ya vitabu, wengine waalimu kwa njia ya mitandao, nk. mwalimu mmoja hawezi kufanana na mwingine kwa kila kitu…sasa hawa wote karama yao ni moja “kufundisha” lakini huduma yao ni moja tu “WAALIMU”..Haijalishi watakuwa wamejigawanya gawanya katika vitengo vingapi..lakini huduma yao ni hiyo hiyo moja tu.

Warumi 12:6  “Basi kwa kuwa tuna karama zilizo mbalimbali, kwa kadiri ya neema mliyopewa; ikiwa unabii, tutoe unabii kwa kadiri ya imani;

7  ikiwa huduma, tuwemo katika huduma yetu; mwenye kufundisha, katika kufundisha kwake;

8  mwenye kuonya, katika kuonya kwake; mwenye kukirimu, kwa moyo mweupe; mwenye kusimamia kwa bidii mwenye kurehemu, kwa furaha”.

Hali kadhalika wapo katika kanisa ambao wamepewa karama ya ndoto kama Danieli, wengine maono, wengine unabii, n.k hawa huduma yao ni “UNABII”.

Na karama nyingine zote zilizosalia, kama miujiza, Imani, Neno la Hekima, unabii n.k.. zina utendaji kazi tofauti na huduma tofauti tofauti.

Hivyo kwa hitimisho ni kwamba…kila karama inayo huduma..Na karama moja inaweza kuwa na utendaji kazi tofauti tofauti kulingana na mtu. Hivyo usitafute kujilinganisha na mtu mwingine, wala usitafute kufanana na mwingine..wala usimdharau mwingine..

Kama wewe unaweza kuona maono ya nini kitatokea kesho..mwingine anaweza kupewa kuliona jambo hilo hilo kwa njia ya ndoto, mwingine si kwa ndoto wala maono bali kwa ufunuo…Hivyo usijisifu kwa kuona maono wala kwa ndoto, wala kwa ufunuo..wote karama yenu ni moja “unabii”  lakini zinatenda kazi tofauti tofauti..

Wewe una karama ya Matendo ya miujiza, ukimwekea mtu mkono anapokea uponyaji..usijisifu kwa mwingine, kwasababu mwingine anaweza kumtamkia tu mtu na akapokea uponyaji, ule ule ambao wewe ungeufanya kwa kumwekea mikono..Mna karama moja isipokuwa utendaji kazi tofauti.nk. nk NK

Hivyo ni muhimu kuwa wanyenyekevu na pia kukaa kila mtu katika nafasi yake pasipo kunia mkuu..

Warumi 12:3  “Kwa maana kwa neema niliyopewa namwambia kila mtu aliyeko kwenu asinie makuu kupita ilivyompasa kunia; bali awe na nia ya kiasi, kama Mungu alivyomgawia kila mtu kiasi cha imani.

4  Kwa kuwa kama vile katika mwili mmoja tuna viungo vingi, wala viungo vyote havitendi kazi moja;

5  Vivyo hivyo na sisi tulio wengi tu mwili mmoja katika Kristo, na viungo, kila mmoja kwa mwenzake”

SASA JAMBO KUU LA MWISHO LA KUKUMBUKA ni  kuwa  karama yoyote au huduma yoyote uliyopewa..lengo la kupewa karama hiyo ni kuujenga mwili wa Kristo, sio kujionyesha wewe ni mtaalamu..au mjuzi, au una uwezo Fulani wa kipekee Zaidi ya wengine.. Mtu mmoja aliniuliza mtumishi nifanye nini ili niwe  na upako, wa kufufua wafu, na kuwekea watu mikono wapone saa hiyo hiyo, nifanye miujiza mikubwa, nikamuuliza unataka hayo yote kwa lengo gani,..hana jibu..Ndugu karama za rohoni sio za kujitafutia umaarufu au kuwa nazo tu basi..

Hizo Mungu kaziweka ili kuokoa Roho za watu wake.. hivyo unapaswa uitumie katika kuwaleta watu katika ufalme, watubu wamgeukie Mungu na kuucha ulimwengu kama wewe ulivyouacha Hilo ndio lengo kuu…Usipoitumia inavyopaswa siku ile utatoa hesabu..Ikiitimia kujipatia pesa utatoa hesabu, ukiitumia kulaania watu utatoa hesabu, ukiitumia kupotosha watu utatoa hesabu, ukiitumia kujitengenezea umaarufu wako na watu badala ya kumwogopa Mungu na kumtumikia Mungu wanakuogopa wewe siku ile utatoa hesabu..ukiitumia karama uliyopewa kujichukulia utukufu wewe badala ya kumpa Mungu utukufu..siku ile utatoa hesabu ndugu yangu…Siku ile utapoangaliwa na kuonekana karama uliyopewa hajaleta watu wowote katika ufalme wa mbinguni, utawajibishwa katika hilo..

Leo tumejua tofauti kati ya karama, utendaji kazi na Huduma, Bwana azidi kutusaidia sana..tuwe waaminifu hata siku ile ya kuja kwake.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

NITAIFAHAMU VIPI KARAMA YANGU?.

ROHO YA MPINGA KRISTO IKITENDA KAZI SIKU HIZI ZA MWISHO

TOA SADAKA ISIYO NA KASORO KWA BWANA.

KWANINI MUNGU ALIMTUMIA MUSA KWA VIWANGO VILE?

FIMBO YA HARUNI!

KARAMA ILIYO KUU.

ITAMBUE KARAMA YA MUNGU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Je! Shetani alitolea wapi uovu?

SWALI: Ikiwa Mungu aliviumba viumbe vyake vikiwa vikamilifu Je! Shetani alitolea wapi uovu?. Na Je! ni nani aliyeiumba  dhambi?.

JIBU: Kitu chochote kizuri tunachokiona,  mpaka tumejuwa kuwa ni kizuri basi tujue kuwa ni lazima kilikuwepo  kingine kibaya  ambacho kimeuthibitisha uzuri wake..kwamfano unapolamba sukari mpaka umejuwa kuwa sukari ni tamu ni kwasababu ulishakutana na kitu kama chumvi huko nyuma chenye ladha tofauti n hiyo , au unapouona mwanga, mpaka umejua kuwa  hii ni nuru, ni kwasababu ulishawahi kuliona giza huko nyuma ndipo ukaweza kuielewa vizuri nuru ni nini, kamwe usingekaa ujue kuwa huu ni mchana kama usingekaa uuone usiku ulivyo, usingekaa ujijue kama wewe una afya kama usingewahi kuugua..Na vitu vingine vyote tunavyoviona ni vizuri vivyo hivyo..Utagundua kuwa kibaya kipo kwa lengo la kukithibitha kizuri,  mpaka kujua huyu mtu anayo hekima, ni kwasababu mpumbavu yupo, mpole-kwasababu mkali yupo, mpaka kujua kuwa kuna mrefu ni kwasababu mfupi yupo, mweupe-kwa-mweusi, mwanamke-kwa -mwanaume..n.k.

Sasa Mungu alipoanza kuviumba viumbe vyake, aliviumba vyote vikiwa vikamilifu, ndipo hapo akawauumbia WEMA ndani yao, lakini hakuishia hapo tu, alitaka pia wajitambue kuwa wao ni wema, na hivyo wazidi kuupenda wema ndipo hapo akauumba na UBAYA pia, ili uuweze kuuthibitisha wema..

Hivyo tangu mwanzo malaika zake walipewa Ujuzi huo wa kuweza kujua mema na mabaya..Ili kusudi kwamba wazidi kuupenda wema  waliokusudiwa kuwa nao, na kuuzidi kuuchukia ubaya usiowafaa.

Ndipo hapo sasa, Malaika wakawa wanajua sasa ili sisi tuwe watakatifu kama Mungu ni lazima tuchukie matendo  yasiyoendana na utakatifu, ili tuwe wema ni lazima tuukatae ubaya wa kumchukia malaika mwenzetu na Mungu wetu, ili tuwe wakweli ni lazima tusisemezane uongo sisi kwa sisi….

Isaya 45:7 “Mimi naiumba nuru, na kulihuluku giza; mimi nafanya suluhu, na kuhuluku ubaya; Mimi ni Bwana, niyatendaye hayo yote”.

Maombolezo 3:38 “Je! Katika kinywa chake Aliye juu Hayatoki maovu na mema”?

Lakini sasa mambo yakaja kubadilika baadaye..Baadhi ya malaika, wakiongozwa na baba yao shetani, wakaanza kukengeuka, wakawa wanataka kuijitawala wenyewe, hivyo wakaona ni bora wachague yale mabaya ili  kutimiza adhma yao, sasa badala ya kupenda wakaanza kuchukia, wakawachukia malaika wenzao waliomtii Mungu vilevile wakamchukia na muumba wao aliyewaumba wao,  wakaanza kusema uongo, wakaanza kuharibu n.k.

Hapo ndipo dhambi ilipopata nguvu ndani yao, wakapungukiwa na utukufu wa Mungu, wakaonekana ni waovu, wakafukuzwa watoke mbinguni katika makao ya Mungu matakatifu.

Hivyo ukiuliza  uovu ulitoka wapi, fahamu kuwa ouvu na wema viliumbwa vyote pamoja viliumbwa na Mungu kila kimoja kikae katika sehemu yake kutimiza kusudi lake..Lakini wale waliokengeuka walipoupenda ubaya zaidi ya wema ndipo wakaonekana wakosaji…Hivyo shetani alitolea wapi uovu?..jibu> aliumbiwa nao.

Hata sasa, iwe wewe ni mkristo au sio mkristo, ujuzi huo wa mema na mabaya upo ndani yako tangu Edeni. Ulikuwa ni Mpango wa Mungu kabisa ubaya uwepo ndani ya mtu kwa makusudi maalumu mema.. Sasa ni jambo la wewe kuchagua moja kati ya hilo, ukipenda wema basi utajitahidi ukae mbali na ubaya, vivyo hivyo ukiupenda ubaya basi utafanya juu chini uwe mbali na wema.

Yohana 3:19 “Na hii ndiyo hukumu; ya kuwa nuru imekuja ulimwenguni, na watu wakapenda giza kuliko nuru; kwa maana matendo yao yalikuwa maovu.

20 Maana kila mtu atendaye mabaya huichukia nuru, wala haji kwenye nuru, matendo yake yasije yakakemewa.

21 Bali yeye aitendaye kweli huja kwenye nuru, ili matendo yake yaonekane wazi ya kuwa yametendwa katika Mungu”.

Lakini sisi tuliokoka tumeipenda Nuru, a ndio maana hukumu ya Mungu haipo juu yetu…kama maandiko yanavyosema katika Warumi 8:1

 Ubarikiwe.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

NI KWASABABU YA YESU KRISTO.

JE WAJUA?

TOFAUTI KATI YA HEKALU, SINAGOGI NA KANISA NI IPI?

WANA WA MUNGU, NA BINTI ZA WANADAMU.

TUMAINI NI NINI?

MAMBO 5 AMBAYO KILA MKRISTO ANAPASWA KUFAHAMU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

KIFO CHA MTAKATIFU POLIKAPI (Policarp).

Tunaweza kujifunza nini juu ya Kifo cha Mtakatifu Polikapi?

Polikapi aliishi kati kipindi cha mwaka 69-159 WK. Alikuwa ni askofu wa kanisa la Smirna ambaye alikuwa pia ni mwanafunzi wa Mtume Yohana.

Wakati ule wa kanisa la kwanza kama wengi wetu tunavyojua, Utawala wa Roma ulikuwa na vita vikali sana dhidi ya wakristo wote ulimwenguni. Na sababu kuu ilikuwa ni wao kukataa kuabudu miungu yao ya kipagani na sanamu za kirumi, na pale wanapoona watu wengi wanavutwa kuiacha Imani yao na kumgeukia Kristo ndipo walipozidisha mapambano makubwa dhidi ya wakristo.. Ilikuwa ni unachagua moja aidha umkane Kristo uishi au umkiri Ufe..

Ndio maana kwa kanisa la Kwanza, lile Neno la Mtume Paulo, linalosema.

Warumi 10:9 ‘Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka’.

Lilikuwa linamaana kubwa sana, tofauti na linavyotafsiriwa sasa hivi..Kwasababu ilifikia hatua ukimkiri Yesu tu kuwa ni mwokozi wa huu ulimwenguni adhabu yake ilikuwa ni kifo cha kukatwa kichwa au kutupwa katika tundu la simba. Sio leo hii watu tunasema tumemkiri Yesu, lakini tukiambiwa tu tujitwike misalaba yetu tumfuate licha ya kuuawa, utasikia watu wanasema  hiyo ni dini ya itikadi kali..huo ni ulokole ule wa zamani..

Bwana atusaidie..

Sasa baada ya wakristo wengi kuuliwa katika kanisa la kwanza wengine kwa kutupwa katika viwanja vya simba na wengine kutundikwa kwenye miti, na wengine kukatwa vichwa ikafika wakati sasa wakawahitaji na wale viongozi wao wakuu wa juu kabisa wawaue, na mmojawapo alikuwa ni huyu Polikapi wa kanisa la Smirna lililokuwa Asia ndogo (ambayo ni Uturuki kwa sasa)..

Hapo ndipo harakati za kumtafuta Polikapi zilipoanza, wakatumiwa maaskari wa jeshi wengi sana kwenda kumtafuta, Lakini Polikapi aliposhauriwa na baadhi ya wafuasi wake ahame miji akimbilie mwingine, yeye alikataa, kinyume chake zile habari hata hazikumwogopesha bali alikwenda katika mojawapo ya nyumba ya marafiki zake, akawa akikaa huko usiku na mchana akiomba na kuliombea kanisa la Kristo ulimwenguni kote..Na siku tatu kabla ya kukamatwa kwake anasema aliona maono, katika maono hayo anasema aliona mto wa kulalia wa moto ulikuwa chini ya kichwa chake..Ndipo akaenda kuwaambia wafuasi wake kuwa atakwenda kuchomwa moto akiwa mzima…

Sasa wale askari walipofika  na kumkuta walishtuka kidogo, kumuona mbona ni mtu mzee ambaye hakukuwa hata na haja ya kumwendea na majeshi na askari na marungu, na mapanga?…Kama tu ile picha ya Bwana Yesu alipokuwa pale Gethsemane, wale askari walipomwendea na marungu na mapanga wakidhani atakuwa bonsa mwenye ma-boardguards na misuli mikubwa, lakini walimkuta jinsi wasivyotegemea…hata wakaanza kuhisi huyo siye Yesu waliotumwa kumtafuta labda kuna Yesu mwingine…ndio maana walikuwa wanakazana kumwambia Tunamtafuta Yesu, japo Bwana Yesu alikuwa anawaambia mnayemtafuta ndiye mimi..lakini bado walikuwa hawaamini wanachokiona.

Na vivyo Polikapi alipowaona wale askari, aliwakaribisha kwake kama vile wageni wake, akawapa chakula wakala, kisha akawaomba haja moja kabla hawajamchukua, nayo ni ‘kuomba Lisaa’ limoja kisha ndio wamchukue wampeleke kwenye uwanja wa mauaji..Ndipo wale askari wakamkubalia haja yake, Polikapi akaanza kuomba lakini maombi yake yalipitiliza mpaka masaa mawili, ndipo wale askari wakiwa pale wakaanza Kujijutia mioyoni ni kwanini walitumwa kuja kumshika mtu kama huyu mkarimu asiye na hatia…Lakini hakukuwa na namna ilibidi wafanye vile kama walivyoagizwa.

Na walipomleta sasa katika uwanja wa mauaji ambapo watu wengi walikuwa wanamngoja auawe, Lakini wale pia walipomwona kuwa ni mzee wakaona haileti maana sana  kumuua mzee kama yule. Hivyo utawala ukamtaka neno moja tu kwake kwamba “Amlaani Kristo, nao watamwachia”

Ndipo Polikapi akafungua kinywa chake na kuwaambia “Kwa miaka nane na mi-sita (akimaanisha miaka 86), nimekuwa nikimtumikia na hajawahi kunifanyia ubaya wowote. Nitawezaje kumkufuru Mwokozi wangu na mfalme wangu”?.

Lakini wale wakuu wa kirumi wakafanya kama,wanampa nafasi nyingine tena..wakamwambia.. “Wewe mzee Apa leo kwa mkuu wa Ngome hii na hiyo tu itatosha” tukuachie..(mkuu wa ngome ni mkuu wa miungu wanayoitumikia)..

Lakini Polikapi akawaambia.. “Kama mnamatumaini ninaweza kufanya kitendo kama hicho, nadhani mtakuwa mnajifanya kuwa hamjui mimi ni nani….Mnisikilize wote mimi ni mkristo!!

Wale wakuu wakaanza kumtishia kwa wale Wanyama wakali waliokuwa nao..Kisha wakamwambia tutakuchoma kwa moto..

Polikapi akawaambia “Mnanitishia kwa moto wa kitambo ambao baada ya muda mfupi tu utazima. Lakini mnajitoa ufahamu juu ya moto wa mateso ya milele ambao umeandaliwa kwa ajili ya watu waovu”.

Basi wakamchoma  Polikapi kama vile nyama choma iliyowekwa juu ya mkaa, lakini walipoona haungui wakammalizia kwa mkuki na alipokuwa anakiribia kufa alisema,

“Ninakubariki Baba kwa kunipangia hukumu hii ninayostahili, ili kwamba katika kundi la wafia Imani nami pia nikinywee kikombe cha Kristo”.

Hivyo ndivyo alivyokufa Mtakatifu Polikapi kama mshindania Imani mwaminifu..(kifo cha mtakatifu polikapi na watakatifu wengine vimebeba ujumbe wa muhimu sana kwetu)

Vivyo hivyo na sisi biblia inatuambia..

Waebrania 12:1  “Basi na sisi pia, kwa kuwa tunazungukwa na wingu kubwa la mashahidi namna hii, na tuweke kando kila mzigo mzito, na dhambi ile ituzingayo kwa upesi; na tupige mbio kwa saburi katika yale mashindano yaliyowekwa mbele yetu,

 2  tukimtazama Yesu, mwenye kuanzisha na mwenye kutimiza imani yetu; ambaye kwa ajili ya furaha iliyowekwa mbele yake aliustahimili msalaba na kuidharau aibu, naye ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Mungu”.

Ikiwa sisi hatujafikia hatua ya kumwaga damu, lakini tunaona ni shida kuishi Maisha ya kikristo tungekuwa wakati huo tungesemaje?. Lakini mimi na wewe tumepewa neema ya kumpokea Kristo katika kipindi cha amani kama hichi..Sasa tukishindwa kuipokea siku ile tutajiteteaje mbele za Mungu aliye hai?. Au tutajilinganishaje na mashahidi waaminifu kama hawa, wakina Antipa, Polikapi na wengine..?

Hivyo biblia inatuasa, tuitupilie mbali dhambi ile ituzingayo kwa upesi,..tupige mwendo..Tukubali sasa kujitwika misalaba yetu na kumfuata Kristo kwa gharama zozote, tukubali kuchekwa, kudharauliwa, tukubali kusemwa tunapotupa vimini na kuacha kuvaa suruali na wigi na kuacha usengenyaji …Tunapaswa tukubali hata dhihaka tunapoacha kuongozana na kampani za watenda mabaya, na walevi, na wezi….tunapoanza kuongeza viwango vyetu vya maombi, na kumtafuta Mungu kwa bidii..tukubali kupitia vita vya kiimani n.k.Hatupaswi kukisoma tu kifo cha Mtakatifu Polikapi na vifo vya watakatifu wengine kama hadithi bali kama mfano wa kuigwa katika vipindi tunavyopitia sasa.

Bwana atusaidie sana..

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

UNYAKUO.

USIMPE NGUVU SHETANI.

SAYUNI ni nini?

IVUMBUE INJILI YA KRISTO KUTOKA KATIKA KILA JAMBO.

HISTORIA YA ISRAELI.

KUFUKIZA UVUMBA NDIO KUFANYAJE?

Rudi Nyumbani:

Print this post

JE UNAMTHAMINI BWANA?

(Je unamthamini Bwana?) Jina la Bwana libarikiwe…Karibu tujifunze maandiko…

Neno la Mungu ni Mwanga wa njia yetu ielekeayo mbinguni na Taa iongozayo miguu yetu katika safari yetu ya mbinguni. (Zab 119:105).

Jambo la muhimu la kufahamu ni kuwa Mungu wetu aliyetuumba kamwe hawezi kumtumia mtu ambaye hayupo tayari..au moyo wake haupo tayari kumpokea yeye. Wakati mwingine mioyo yetu ya kutokuwa watoaji  inatuzuilia sisi kupokea Baraka kutoka kwa Mungu.

Hebu tujifunze mifano michache ya kwenye biblia jinsi Bwana alivyoweza kuwatumia watu katika kulitimiza kusudi lake..ambapo kwa kupitia mifano hiyo..tunaweza kutoka sehemu moja hadi nyingine kiimani..

Marko 14:12 “Hata siku ya kwanza ya mikate isiyochachwa, walipoichinja pasaka, wanafunzi wake wakamwambia, Ni wapi utakapo tuende tukuandalie uile pasaka?

13 Akatuma wawili katika wanafunzi wake, akawaambia, Nendeni zenu mjini; atakutana nanyi mwanamume amechukua mtungi wa maji; mfuateni;

14 na po pote atakapoingia, mwambieni mwenye nyumba, Mwalimu asema, Ki wapi chumba changu cha wageni, niile pasaka humo, pamoja na wanafunzi wangu?

15 Naye mwenyewe atawaonyesha orofa kubwa, imeandikwa tayari; humo tuandalieni.

16 Wanafunzi wakatoka, wakaenda mjini, wakaona kama alivyowaambia, wakaiandaa pasaka”.

Katika Tukio hilo..Tunamwona kuna mtu mmoja ambaye ni mcha Mungu biblia haijamtaja jina lake…Lakini Mtu huyu anaonekana alikuwa ni mtu mwenye uwezo kidogo kutokana na habari hiyo…kwasababu utaona anatajwa kuwa na Mtumwa, na pia anayo nyumba yenye ghorofa…Sasa kwa enzi hizo kumiliki nyuma ya ghorofa tena katikati ya Mji kama ule (Yerusalemu) si rahisi kama wewe sio mtu mwenye uwezo ni sawa na leo umilika nyumba ya ghorofa pale Posta Daresalaam…

Lakini pia kama ukichunguza mtu huyo ni lazima alikuwa anamjua Bwana Yesu sana..na pia alikuwa anafuatilia mafundisho yake na alikuwa anampenda sana…Ingawa pengine hakupata nafasi ya kukutana naye..Lakini pamoja na hayo ndoto yake kubwa ilikuwa ni siku moja akutane naye, amkaribishe kwake…

Sasa pengine alifunga na kuomba kwamba angalia msimu huu wa sikukuu amtembelee kwake…na hivyo akapanga pengine namna ya kumtafuta akakosa…moyoni mwake akiwa na mawazo hayo..wazo likamwingia aandae chumba kabisa kilicho kizuri tena ghorofani ili atakapompata Yesu wakati huo huo aingie kwenye chumba hicho isiwe baada ya kumpata ndipo aanze maandalizi.

Siku chache kabla ya sikukuu…moyo wake pengine ukiwa na shauku ya kumkaribisha Bwana…..Yesu akauona moyo huo maili kadhaa mbali na alipokuwa…kama vile alivyomwona Nathanieli siku ile alipokuwa chini ya mtini alipokwenda kuitwa na Filipo.

Yohana 1: 48 “Nathanaeli akamwambia, Umepataje kunitambua? Yesu akajibu, akamwambia, Kabla Filipo hajakuita, ulipokuwapo chini ya mtini nilikuona”.

Na ndivyo hivyo hivyo Bwana alivyouona moyo wa huyu mtu akiwa nyumbani kwake..tayari amemwandalia yeye chumba…Na kwasababu Roho ya kinabii ilikuwa juu ya Yesu akawaambia wanafunzi wake waende mjini watamkuta mtu kabeba mtungi wamfuate mpaka atakapoingia wamwulize mwenye nyumba

“Ki wapi chumba changu cha wageni, niile pasaka humo, pamoja na wanafunzi wangu”

Hebu tafakari hiyo sentensi… “Ki wapi chumba changu”..na si “ki wapi chumba chako”…Kitendo cha Yule mtu kukiweka tayari kile chumba kwaajili ya Bwana..tayari Bwana ameshakiheshimu na kukiita chumba chake na si cha Yule mtu tena…Hebu tafakari huyo mtu alifurahi kiasi gani kusikia vile??..Chumba kile alichomwandalia Bwana, Bwana amekijia…Ni furaha ya ajabu sana.

Ndugu yangu..Bwana hawezi kuja mahali ambapo hatujamwandalia…na Bwana akija mahali tulipomwandalia anakuja na Baraka. Sio kwamba Bwana alikuwa hana mahali pa kwenda…alikuwa na sehemu nyingi za kwenda lakini aliutazama mji mzima ni nani aliyekuwa na moyo wa kumpenda kwa dhati kuliko wote aende kwake…

Ndio maana sehemu nyingine Bwana Yesu alisema maneno haya…

Luka 4:25 “Lakini, kwa hakika nawaambia, Palikuwa na wajane wengi katika nchi ya Israeli zamani za Eliya, wakati mbingu zilipofungwa miaka mitatu na miezi sita, njaa kuu ikaingia nchi nzima;

26 wala Eliya hakutumwa kwa mmojawapo, ila kwa mjane mmoja wa Sarepta katika nchi ya Sidoni”.

Wajane walikuwepo wengi lakini Eliya hakutumwa isipokuwa kwa mwanamke wa Taifa la mbali..akakaa kwake na nyumba yake ikabarikiwa..mkate haukuwaishia.. Kadhalika kulikuwepo na matajiri wengi pale Yerusalemu lakini Bwana hakwenda hata kwa mmojawao isipokuwa kwa mtu huyu ambaye moyoni mwake alimpenda Bwana kiasi kwamba alikuwa tayari kumwandalia chumba kabla hata ya kumwona wala kumkaribisha.

Bwana anaitazama mioyo yetu ndugu?..Je tunamjali kiasi gani? Tafakari mfano mwingine tena huu wa mwisho..

Marko 11:1 “Hata walipokaribia Yerusalemu karibu na Bethfage na Bethania, kukabili mlima wa Mizeituni, aliwatuma wawili katika wanafunzi wake,

2 akawaambia, Nendeni mpaka kile kijiji kinachowakabili; na katika kuingia ndani yake, mara mtaona mwana-punda amefungwa, asiyepandwa na mtu bado; mfungueni, kamleteni.

3 Na mtu akiwaambia, Mbona mnafanya hivi? Semeni, Bwana anamhitaji na mara atamrudisha tena hapa.

4 Wakaenda zao, wakamwona mwana-punda amefungwa penye mlango, nje katika njia kuu, wakamfungua.

5 Baadhi ya watu waliosimama huko wakawaambia, Mnafanya nini kumfungua mwana-punda?

6 Wakawaambia kama Yesu alivyowaagiza, nao wakawaruhusu.

7 Wakamletea Yesu yule mwana-punda, wakatandika mavazi yao juu yake; akaketi juu yake”.

Katika habari hii, jambo ni lile lile…Hawa watu walikuwa na punda wao amefungwa pale..lakini pengine walishawahi kusikia habari za Yesu na kumwamini..na kutamani wangempatia angalau kitu Fulani…Na Bwana alipoiona mioyo yao…pale pale kwa kuwa yeye ni Nabii akawatuma wanafunzi wake kuwaomba punda yule amtumie kuingia naye Yerusalemu..Na wale wenye punda walipowauliza kwanini mnamfungua? Waliposikia kwamba ni Bwana anamhitaji…wala hawajauliza mara mbili mbili wala kuhoji..Ni wazi kuwa walifurahi mno na kujiona wenye bahati..

Ni wazi kuwa walikuwepo wengi wenye punda pale mjini lakini Bwana Yesu hakwenda kuchukua hata wa mmoja wao…Ni kwanini? Ni kwasababu hakuna chochote ndani yao cha kuuvuta Moyo wa Bwana Yesu uwaelekee wao…Pengine Bwana angeenda kwa mmoja wao na kuomba punda Yule wangeanza kusema…oo kwanza wewe unawapinga wazee wetu wa dini…oo kwanza wewe unajiita Mwana wa Mungu..oo wewe umetoka wapi, huna shughuli maalumu unazunguka tu…wengine wangeanza kumwita hata mwizi…wengine wangeanza kusema huna kazi ya kufanya unataka kuharibu mali za watu…

Vivyo hivyo walikuwepo wenye magari sio punda tu…kwasababu kipindi hicho yalikuwepo magari ya farasi watu wenye uwezo walikuwa wanayatembelea….Lakini hakukuwa na hata mmoja mwenye moyo wa dhati wa kutamani siku moja Bwana angelipanda gari lake…Lakini Bwana anauona moyo wa mtu mmoja anayetamani siku moja Bwana angepanda punda wake…Na Bwana anakwenda kwa Yule mwenye moyo uliomwelekea.

Ndugu yangu..habari hizi ni mifano inayotufundisha dhahiri..Jicho la Bwana linatazama kote kote ulimwenguni kila siku anatazama ni yupi, ni nani, na yuko wapi aliye tayari angalau kutoa chochote kwaajili yake?..Kumbuka yeye hana shida..lakini anaipenda mioyo ya utoaji…anaangalia ni mtaa gani kijiji gani kuna mtu ambaye anatamani angalau kitu chake kile, kingetumiwa na yeye…Anaangalia huku na huko..Anatamani sana kututembelea lakini hawezi kumtembelea mtu ambaye hataki kutembelewa na yeye..

Tafakari tena maneno haya ya kumalizia aliyoyasema juu ya siku ile ya mwisho itakavyokuwa..

Mathayo 25:31 “Hapo atakapokuja Mwana wa Adamu katika utukufu wake, na malaika watakatifu wote pamoja naye, ndipo atakapoketi katika kiti cha utukufu wake;

32 na mataifa yote watakusanyika mbele zake; naye atawabagua kama vile mchungaji abaguavyo kondoo na mbuzi;

33 atawaweka kondoo mkono wake wa kuume, na mbuzi mkono wake wa kushoto.

34 Kisha Mfalme atawaambia wale walioko mkono wake wa kuume, Njoni, mliobarikiwa na Baba yangu, urithini ufalme mliowekewa tayari tangu kuumbwa ulimwengu;

35 kwa maana nalikuwa na njaa, mkanipa chakula; nalikuwa na kiu, mkaninywesha; nalikuwa mgeni, mkanikaribisha;

36 nalikuwa uchi, mkanivika nalikuwa mgonjwa, mkaja kunitazama; nalikuwa kifungoni, mkanijia.

37 Ndipo wenye haki watakapomjibu, wakisema, Bwana, ni lini tulipokuona una njaa, tukakulisha, au una kiu tukakunywesha?

38 Tena ni lini tulipokuona u mgeni, tukakukaribisha, au u uchi, tukakuvika?

39 Ni lini tena tulipokuona u mgonjwa, au kifungoni, tukakujia?

40 Na Mfalme atajibu, akiwaambia, Amin, nawaambia, kadiri mlivyomtendea mmojawapo wa hao ndugu zangu walio wadogo, mlinitendea mimi.

41 Kisha atawaambia na wale walioko mkono wake wa kushoto, Ondokeni kwangu, mliolaaniwa, mwende katika moto wa milele, aliowekewa tayari Ibilisi na malaika zake;

42 kwa maana nalikuwa na njaa, msinipe chakula; nalikuwa na kiu, msininyweshe;

43 nalikuwa mgeni, msinikaribishe; nalikuwa uchi, msinivike; nalikuwa mgonjwa, na kifungoni, msije kunitazama.

44 Ndipo hao pia watajibu, wakisema, Bwana, ni lini tulipokuona wewe una njaa, au una kiu, au u mgeni, au u uchi, au u mgonjwa, au u kifungoni, tusikuhudumie?”

45 Naye atawajibu, akisema, Amin, nawaambia, Kadiri msivyomtendea mmojawapo wa hao walio wadogo, hamkunitendea mimi.

46 Na hao watakwenda zao kuingia katika adhabu ya milele; bali wenye haki watakwenda katika uzima wa milele.

Usipokubali kujitoa kwa Bwana kamwe usitegemee Baraka wala kupokea kutoka kwake…Naamini maarifa haya yatakusaidia kuchukua hatua ya kumthamini Bwana. (Je unamthamini Bwana?)

Ubarikiwe sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

SAKRAMENTI NI NINI, NA JE! IPO KATIKA MAANDIKO?

INGIENI KWA KUPITIA MLANGO ULIO MWEMBAMBA.

USIZITEGEMEE NGUVU ZAKO KUKUSAIDIA!

Ni sahihi kumuita Mariamu mama wa Mungu?

TOFAUTI KATI YA HEKALU, SINAGOGI NA KANISA NI IPI?

USIMPE NGUVU SHETANI.

Je! Ni kweli ubatizo wa maji hatuuhitaji tena?

UKITAKA KUMFUATA YESU NI SHARTI UACHE VYOTE!

Rudi Nyumbani:

Print this post

Ikiwa sisi tuliumbwa na Mungu,Je! Mungu aliumbwa na nani?

JIBU: Tukiweza kulijibu na swali hili “Ikiwa sisi tunakula ili tuishi, Je! Mungu naye anakula nini ili aishi?”…Basi tutaweza pia kulijibu hilo linaloulizwa kirahisi.

Awali ya yote ni vizuri kufahamu kuwa wazo lolote ambalo linakuja katika vichwa vyetu fahamu kuwa lilishawahi kuumbwa hapo kabla, Hivyo  wakati ulipofika na kuwekwa katika kichwa chako au changu, ndipo tukaliwaza, vinginevyo tusingekaa tuwe na wazo kama hilo vichwani mwetu kama hili la “Mungu aliumbwa na nani” kama halikuwahi kubuniwa na aliyetuumba.. hakuna wazo linalozuka lenyewe tu hewani, labda wewe ndio uwe wa kwanza kuligundua, ni kama kumputa tulizonazo kila kitu kilichomo ndani yake, kiliwekwa na mtu kwanza (installed)

Hivyo mpaka hapo ulipofikia kuwaza tu Mungu aliumbwa na nani, fahamu kuwa ni yeye mwenyewe alilibuni hilo wazo kisha akaliweka kwa makusudi katika ufahamu wako,..Hivyo usifikiri kuwa umegundua wazo la kumnasa Mungu, kama hilo la Mungu aliumbwa na nani,..nataka kwanza uondoe hilo akilini. Na aliamua kufanya hivyo ili wakati wake wa kufikirika ukifika ujiulize weee!!, uumize kichwa weee! kisha ukose majibu! … Wazo hilo alipenda tu ukose majibu yake, kama vile yale mengine alivyopenda upate majibu yake.

Jibu rahisi ni kuwa Mungu hatuwezi kumpima katika “wazo la kuumba au kuumbwa”..kwasababu hayo mawazo ya kuumba au kuumba aliyabuni yeye, hivyo hayawezi kuwa sehemu ya maisha yake..yeye, ni zaidi ya upeo wa fikra zetu.

Jaribu kuwazia mfano huu, unaohusiana na vitu tulivyoviumba sisi wanadamu ambavyo ni vya  elektroniki…Sasa kisa tu tumeviundia mfumo wa kutegemea umeme katika kujiendesha pale vinapoishiwa nguvu tunavichaji betri zako katika umeme.. Na kwamba visipochajiwa ni lazima tu vizime au vife kabisa, Simu zetu zinasema hivyo hivyo,  saa zetu hivyo hivyo , komputa zetu, na tochi zetu zinasema hivyo hivyo n.k..Halafu siku moja sasa eti  na vyenyewe vinaungana na kutuuliza  sisi tulioviumba maswali, vinasema Je! betri zenu ziko wapi, na mnachajiwa wapi? kwasababu hakuna maisha nje ya umeme?

Unaona lakini sisi je tunaishi kwa betri au umeme?…jibu ni la, maisha yetu yanaendeshwa na kitu kingine tofauti na wanachokifikiria, bali mambo hayo ya umeme  tumeviumbia vifaa vyetu vya elektroniki ili viishi kwayo..zaidi ya hapo haviwezi kujua jambo lingine linalotuhusu sisi..

Vivyo hivyo na sisi kwa kuwa tumezungukwa na mazingira ya  “kuumba na kuumbwa”,kila kitu tunaona ni lazima kiwe na chanzo chake ….Basi na sisi tunahitimisha na kusema Je Mungu naye kaumbwa na nani?..

Jibu  linalojitosheleza ndio hilo..Mungu hayupo katika viwango vya kibinadamu ni zaidi ya upeo wa fahamu zetu..hatuwezi kumpima katika mambo ya uumbaji.. ni sawa na leo uulize mwanga una ladha gani, au rangi ina harufu gani..na ndio maana tunapotoa jibu la mkato kuwa Mungu hajaumbwa basi ujue ni kwasababu hizo tunazozisema hapo juu….Mungu ni Zaidi ya upeo wa fikra na kwamba hatuwezi kumweka katika hilo kundi la uumbaji.

Ubarikiwe.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Kwanini Mungu hakumuua Nyoka, akamwacha Hawa ajaribiwe katika bustani ya Edeni?

Je! Mungu anasababisha ajali, kwamfano ajali ya kivuko cha MV Nyerere kuzama?

Kwanini Bwana Yesu, aliruhusu yale mapepo yawaingie nguruwe?

Nifanye nini ili niondokane na Hofu maishani mwangu?

Utii ni nini? na ni nani tunayepaswa kumtii au kutokumtii?

KIFO CHA REINHARD BONKEY KINAACHA UJUMBE GANI KWETU?

SI KILA KIPENDEZACHO KINATOKA KWA BWANA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

USIJARIBU KUMGEUZA MUNGU MGANGA WA KIENYEJI,UTAKUFA.

Ipo mifano mingi katika biblia ya watu ambao, walijaribu kumgeuza Mungu kama mganga wa kienyeji na mwisho wao ukawa mbaya sana. Siku zote watu wanaokwenda kwa waganga utagundua wengi wao hawafahamiani hata na hao waganga wanaowaendea, wala hawana uhusiano nao wowote.

Wakifika pale wanaeleza tu matatizo yao, kisha mganga anawatamizia haja zao, kisha wanakwenda zao..Sasa jambo kama hilo usijaribu kulifanya kwa Mungu ni hatari mno.

Wana wa Israeli kuna wakati Fulani walikuwa wanajaribu kufanya hivyo hivyo, unakuta mtu kamwacha Mungu zamani, ndani yake kuna vinyago, hashiki torati ya Mugu, lakini pale anapokumbwa tu na matatizo fulani labda anaumwa, au anataka kufanya jambo Fulani ndipo anataka kwenda kumuuliza Mungu kwa kupitia nabii wake..Sasa karibu wote waliokuwa wanafanya hivyo Mungu alikuwa anawaua bila huruma.

Utajiuliza anawauaje?

Kama huyo nabii ni nabii wa kweli wa Mungu aliyesimama. Mungu atamwambia moja kwa moja kuwa atakufa. Ndicho pia kilichomkuta Yeroboamu na mkewe walipokwenda kuuliza habari za uzima wa mtoto wao kwa nabii Ahiya, walitabiriwa mabaya na vifo soma (1Wafalme14).

Lakini kama nabii huyo ni nabii wa uongo au vuguvugu..Mungu anachofanya ni anamdanganya Yule nabii aliyemwendea, Na Mungu anajua kabisa kwasababu unamwamini nabii Yule kwamba chochote atakachokuambia utafanya, kumbe huo ndio unakuwa mtego wa kwenda kukuangamiza wewe, Mfano huo tunaouna kwa mfalme Ahabu, pale alipotaka kwenda kupigana vita na mfalme wa Shamu, na biblia inasema Mungu akawadanganya wale manabii 400 wote wakamtabiria ushindi kumbe ndio ulikuwa unakwenda kuwa mwisho wake.. Mungu atakuahikishia hata kwa nabii zaidi ya mmoja unachokifanya ni sahihi, kumbe ni uongo ujue kabisa amekusudia kukuua soma (1Wafalme 22:1-39)..Ndicho kilichomkuta Balaamu, ilikuwa ni nusu afe, punda ndiye aliyemuokoa japokuwa ni Mungu ndiye aliyemwambia aende (Hesabu 22:1-34)..Wote hawa ni mfano wa watu waliojaribu kumgeuza Mungu mganga wa kienyeji kwamba wao wapewe tu haja za mioyo yao, mengine zaidi ya hayo hawataki..

Angalia jambo aliloambiwa Ezekieli na Mungu..

Ezekieli 14:1 Ndipo baadhi ya wazee wa Israeli wakanijia, wakaketi mbele yangu.

2 Ndipo neno la Bwana likanijia, kusema,

3 Mwanadamu, watu hawa wametwaa vinyago vyao na kuvitia mioyoni mwao, nao wameweka kwazo la uovu wao mbele ya nyuso zao. Je! Ni laiki yangu niulizwe na wao katika neno lo lote?

4 Basi sema nao, uwaambie, Bwana MUNGU asema hivi; Kila mtu wa nyumba ya Israeli atwaaye vinyago vyake na kuvitia moyoni mwake, na kuliweka kwazo la uovu wake mbele ya uso wake, na kumwendea nabii; mimi, Bwana, nitamjibu neno lake sawasawa na wingi wa sanamu zake;

5 ili niwakamate nyumba ya Israeli kwa mioyo yao wenyewe, kwa sababu wamefarakana nami kwa vinyago vyao……

7 Kwa maana kila mtu wa nyumba ya Israeli, au wa wageni wakaao katika Israeli, ajitengaye nami, na kuvitwaa vinyago vyake na kuvitia moyoni mwake, na kuliweka kwazo la uovu wake mbele ya uso wake, kisha kumwendea nabii, na kuniuliza neno kwa ajili ya nafsi yake; mimi, Bwana, nitamjibu, mimi mwenyewe;

8 nami nitaukaza uso wangu juu ya mtu yule, na kumfanya kuwa ajabu, awe ishara na mithali, nami nitamkatilia mbali, asiwe kati ya watu wangu; nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana.

9 Na nabii akidanganyika, na kusema neno, mimi, Bwana, nimemdanganya nabii yule, nami nitaunyosha mkono wangu juu yake, na kumwangamiza, asiwe kati ya watu wangu Israeli.

10 Nao watauchukua uovu wao; uovu wa nabii utakuwa sawasawa na uovu wake yule amwendeaye aulize neno;

Unaona hapo mstari wa 9? Anasema mimi Bwana nimemdanganya nabii Yule.. Kama ulikuwa unahitaji kupona, pengine nabii Yule atakupa maagizo Fulani ambayo ni kweli ameyapokea kutoka kwa Mungu, labda tuseme atakuambia Mungu kaniambia, funga siku tatu, kisha kula chakula kisichokuwa na chumvi tu, baada ya hapo utakuwa mzima..Kumbe jambo hilo ndio linakwenda kukuangamiza kabisa.. Na Mungu anafanya hivyo kwasababu umemdharau yeye kwa kumgeuza kuwa kama mganga wa kienyeji, angali ulikuwa unajua kabisa ndani ya moyo wako kuna dhambi umekataa toba, na utakatifu halafu unamwendea yeye akupe haja ya moyo wako wa dhambi..

Hata leo hii, Mungu anawaangamiza watu wengi kwa namna hiyo pasipo wao kujijua.. Wakati Mungu anawapigia kelele kila siku watubu, waache dhambi, watoe vinyago ndani ya mioyo yao, hawataki kusikia wala kuzingatia maagizo hayo, wanadhani Mungu anafurahishwa nao, wanadhani Mungu ni wa neema siku zote badala yake wakiwa bado ni walevi, wala rushwa, wazinzi, waabudu sanamu, washirikina, watazamaji pornography, wasagaji wanamwendea Mungu, kwa kupitia mtu anayejiita nabii, au mtume, au mchungaji, amwombee au amtatulie matatizo yake pengine ya kiafya, au ya kiuchumi, au ya kifamilia…Wahudumiwe tu kisha waondoke wakaendelee na maisha yao ya kawaida ya kila siku..

Ndugu kama ni wewe mmojawapo usijaribu kufanya hivyo tena,..Kwasababu UTAKUFA.. nenda kawatafuta waganga wa kienyeji itakuwa ni salama kwako, lakini sio Mungu kama unamwendea Mungu halafu hutaki kuacha dhambi.. Nakuambia ukweli UTAKUFA NDUGU…

Utaishia kudanganywa tu,..tena na Mungu mwenyewe, unakimbilia mafuta ya upako, unausahau mafuta ya roho yako (Roho Mtakatifu) ambayo yanaokoa roho yako, unakimbilia maji, unasahau maji ya uzima ambayo yanaokoa roho yako.. Timiza kwanza agizo la msingi ambalo ni wokovu na utakatifu..Ndipo Mungu akupe neema ya kutatuliwa na hayo mengine.

Vinginevyo utakufa, hata kama sio kwa njia hiyo, itakuwa kwa nyingine.

Au wewe ni mlevi, mzinzi, mwendaji disko, mlaji rushwa, halafu unakwenda kanisa kila siku, kunakufaidia nini sasa? na kibaya zaidi unashiriki na meza ya Bwana kabisa..Huko ni kujitafutia kifo ndugu. Break! ya kwanza kwa Mungu ni utakatifu (Waebrania 14:12),Mungu hapambwi kwa sadaka, au kwenda kwako kanisani, anachohitaji kwako ni Utakatifu kama yeye alivyo mtakatifu. Nje ya hapo wewe ni adui wa Mungu.

Hiyo ni tahadhari kwako, wewe..Umekwisha sikia, Mungu hadhihakiwa, apandacho Mtu ndicho atakachokuna maandiko yanasema hivyo.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

UNAWAFAHAMU MANABII WA UONGO?

CHUKIZO LA UHARIBIFU

MPINGA-KRISTO

JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?

TAZAMA KRISTO YUPO HAPA,AU YUKO KULE MSISADIKI.

NGURUMO SABA

JUMA LA 70 LA DANIELI

DANIELI: Mlango wa 1

Rudi Nyumbani:

Print this post