Category Archive Uncategorized @sw-tz

Je! Mwandishi wa kitabu cha Warumi alikuwa ni Paulo au Tertio?

SWALI: Je! Mwandishi wa kitabu cha Warumi alikuwa ni Paulo au Tertio? kulingana na mstari huu;

Warumi 16:22 “Mimi Tertio, niliyeandika waraka huu, nawasalimu katika Bwana”.


JIBU: Paulo katika maneno yake ya utangulizi alishatupa  mwangaza kuwa yeye ndiye aliyekiandikia kitabu hicho, kiwaelekee watakatifu wote waliokuwa Rumi. Tusome;

Warumi 1:1 “PAULO, MTUMWA WA KRISTO YESU, ALIYEITWA KUWA MTUME, NA KUTENGWA AIHUBIRI INJILI YA MUNGU;

2 ambayo Mungu amekwisha kuiahidi kwa kinywa cha manabii wake katika maandiko matakatifu;

3 yaani, habari za Mwanawe, aliyezaliwa katika ukoo wa Daudi kwa jinsi ya mwili,

4 na kudhihirishwa kwa uweza kuwa Mwana wa Mungu, kwa jinsi ya roho ya utakatifu, kwa ufufuo wa wafu, Yesu Kristo Bwana wetu;

5 ambaye katika yeye tulipokea neema na utume ili mataifa yote wapate kujitiisha kwa imani, kwa ajili ya jina lake;

6 ambao katika hao ninyi mmekuwa wateule wa Yesu Kristo;

7 KWA WOTE WALIOKO RUMI, WAPENDWAO NA MUNGU, WALIOITWA KUWA WATAKATIFU. Neema na iwe kwenu na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu, na kwa Bwana Yesu Kristo”.

Lakini baadaye karibia na mwishoni mwa waraka huu tunakuja kumwona mtu mwingine aliyeitwa Tertio akijitokeza na kusema ameuandika waraka ule. Sio kwamba mtume Paulo hakuhusika hapana, Jibu ni kwamba Tertio alikuwa ni mwandishi wa mtume Paulo, aliyekuwa anamwandikia nyaraka zake. Aidha kwa kuandika kile alichokuwa anaambiwa au kwa kunakili kile alichoandikiwa na Paulo, japo hakuna sehemu nyingine katika biblia Tertio anaonekana akitajwa.

Na kulikuwa na sababu ya mtume Paulo kutokutumia mkono wake mwenyewe kuandikia waraka huu, pengine Tertio alikuwa ni mwandishi  mwaminifu anayejulikana sana  na watakatifu waliokuwa Rumi kwa umahiri na ufanisi wa kazi zake zilizothibitishwa. Hivyo mtu akiona waraka ulionakiliwa na yeye, basi ilikuwa ni rahisi kuamini uhalisia wa yule mwandishi husika. Kwasababu wakati huo walikuwepo pia watu waliojifanya ni mitume, na kutoa kopi zao wakidai kuwa ni za mitume, ili tu kuwachanganganya watu.

Na ndio maana mtume Paulo ili kuthibitisha nyaraka zake, sehemu nyingine alikuwa anatia sahihi yake mwishoni, soma(2Wathesalonike 3:17), na pia na hapa aliona  ni vema amtumie huyu Tertio kuuandika kwa warumi, iwe kama sahihi yake.

Hivyo waraka huu uliandikwa na Paulo, lakini aliyeunakili ni Tertio.

Hii ni kutufundisha kuwa, si kila kazi ya Mungu, hata kama tutaiona  ni nyepesi kiasi gani, tuifanye sisi mwenyewe, wakati mwingine tutahitaji tushirikiane na viungo vingine vya Kristo, ili kuleta ufanisi Zaidi wa kazi hiyo kwa watu wake.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho

Mada Nyinginezo:

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 6

Je Musa yupo anawashitaki watu..kulingana na Yohana 5:45?

Tofauti kati ya mtume na mwanafunzi ni ipi kibiblia?

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA KITABU CHA FILEMONI.

Kwa herufi gani kubwa nimewaandikia kwa mkono wangu mimi mwenyewe.

Rudi nyumbani

Print this post

Je! tunapaswa kukiamini Kitabu cha Henoko?

SWALI: Kitabu cha Henoko ndio kitabu kipi hicho, Je! Sisi kama wakristo tunapaswa kukiamini?


JIBU: Kitabu cha Henoko ni moja ya vitabu vya Apokrifa ambavyo viliandika kati ya miaka 200 kabla ya Kristo(KK), na  miaka 400 baada ya Kristo(WK). Vitabu hivi  vinaaminiwa na baadhi ya wakristo kuwa  vilihifadhiwa kwa siri, kutokana na kuwa vilikuwa na siri za ndani sana kuhusu Mungu na historia ya ulimwengu kwa ujumla, kiasi kwamba havikuweza kujumuishwa moja kwa moja kwenye biblia yenye vitabu 66 ambayo tunayo hivi sasa.

Lakini si kweli, vitabu hivi havikujumuishwa katika biblia takatifu kwasababu vilikuwa na siri za Mungu hapana badala yake vilionekana kujaa habari nyingi za kutungwa, ambazo zinakinzana na misingi ya imani ya Kikristo.

Sasa tukirudi katika hichi kitabu cha Henoko, kiligunduliwa kwenye miaka ya 1700 huko Ethiopia, baadaye kikasafirishwa mpaka Uingereza kwa ajili ya kutafsiriwa katika lugha nyingine, Kitabu hichi kilijulikana kama Henoko wa  Kwanza (1Henoko), kwasababu kulikuja kuwa pia na matoleo mengine yaliyofuata baadaye.

Vipande vya nyaraka vya kitabu hichi pia viligunduliwa huko Israeli mnao mwaka 1947, kwenye mapango yalikuwa katika fukwe za bahari ya chumvi (dead sea), Na kwenye mapango hayo kulionekana pia machapishi ya vitabu vyote vya agano la kale isipokuwa tu kitabu cha Esta, inasadikika ni vitabu ambavyo vilikuwa vimehifadhiwa huko na watu wa kale ambao waliishi kabla hata ya Kristo kuja duniani.

Sasa kitabu hiki kinamueleza Henoko ambaye alikuwa ni mtu wa saba kutoka Adamu kama tunavyosoma katika biblia Mwanzo 5:18-24…Henoko hakuonja mauti kama ilivyokuwa kwa wanadamu wengine, bali alinyakuliwa kama Eliya. Hiyo imekuwa ikawafanya watu wengi waamini kuwa mtu huyu alipewa siri nyingi za rohoni na kuziandika kwa ajili ya watu wa baadaye.

Hivyo kitabu hichi kilipogunduliwa, kilidhaniwa  kuwa mwandishi wake  ni Henoko, japo hilo jambo halikuthibitika kuwa ni kweli. Kitabu hichi kimejaa historia zinaeleza visa vya dunia ya kwanza kugharikishwa na maji, kinasema baadhi malaika wa Mungu  ambao walikuwa ni waangalizi wa huku ulimwenguni, ambao idadi yao ilikuwa ni 200 waliwaona binti za wanadamu, kisha wakawatamani, , hivyo wakashauriana washuke duniani wajitwalie wake, waishi nao, na kweli wakafanya hivyo  wakashuka duniani wakawapa mimba wanawake, ndio wakazaa wale majitu ambayo tunayasoma katika Mwanzo 6

Zaidi ya yote, malaika hawa kwa kuwa walikuwa na ujuzi, wakawafundisha wanadamu, kubuni silaha za chuma, kufanya uharibifu, wengine wakawafundisha wanadamu kufanya uchawi, na wengine kusoma nyota za mbinguni. Pamoja na hayo watoto wao waliowazaa wakawa wakatili kupita kiasi, ndio wale wanefili, wakawa wanaharibu kila kitu ikiwemo mimea, wanyama, mpaka wanadamu. Urefu wa majitu hayo ulikuwa ni futi 4500, sawa na Jengo la ghorofa 415. Jambo ambalo ni ngumu kusadikika,  Hakuna kiumbe cha namna hiyo kinaweza kuzaliwa na mwanamke. Japo wanefili kweli walikuwa ni wakubwa lakini sio kwa kiwango hicho.

Baadaye baadhi ya malaika wa mbinguni wakampelekea Mungu habari zao,  lakini Mungu akakataa kuwasamehe, akawafunga katika vifungo vya giza, ndio hapo Mungu akamwambia Henoko kuwa atakwenda kuiangamiza dunia kwa gharika.  Hii ndio habari ambayo inafahamika sana

Zipo habari nyingine katika kitabu hicho ambazo kiuhalisia hazina uhalisia wowote  na maandiko.

Tunapaswa tujue vitabu hivi vimejaa hadithi nyingi za kutungwa, ambazo ni sumu kwa Mkristo, na ndio maana huwezi kuziona vikijumuishwa katika biblia yenye vitabu 66 vilivyovuviwa na Roho Mtakatifu, kwasababu vinakinzana na misingi ya kweli ya maandiko.

Bwana Yesu alisema..

Mathayo 22:29 “Yesu akajibu, akawaambia, Mwapotea, kwa kuwa hamyajui maandiko wala uweza wa Mungu.

30 Kwa maana katika kiyama hawaoi wala hawaolewi, bali huwa kama malaika mbinguni”.

Unaona? Hakuna andiko lolote linaloonyesha kuwa malaika wanaoa, au wanazaliana, malaika hawakuumbiwa viungo vya uzazi kama tulivyonavyo sisi, hawahitaji kuzaliana, wao tayari walishaumbwa, ndivyo walivyo na idadi yao tayari ipo kamili, Lakini kusema walishuka duniani, ni fundisho la uongo ambalo wakristo wengi wanaliamini mpaka leo, na chanzo chake walikitoa katika hichi kitabu cha Henoko.

Waliowaona binti za wanadamu wakawatamani, walikuwa ni watakatifu wa Mungu, ambao hao hawakujichanganya na mambo ya ulimwengu tangu mwanzo, bali walitumia sehemu kubwa ya maisha yao, kuliita jina la Bwana na kumwabudu Mungu soma Mwanzo 4:26 utalithibitisha hilo ndio ule  uzao wote wa Sethi (Wakina Henoko, Methusela, Na Nuhu).. Lakini binti za wanadamu walikuwa ni watu wa kidunia tu, ambao walitokea katika ule uzao wa Kaini..hao ndio tangu mwanzo walikuwa na ujuzi mkubwa, na hodari na pia wakatili ukisoma pale Mwanzo 4:16-23 utaona ni jinsi gani, uzao wa Kaini ulivyokuwa hodari, wenye ujuzi mwingine, lakini pia mwovu kwa uuaji, kama Baba yao alivyokuwa.

Baadaye sasa walipojichanganya mbegu ndipo Mungu akakasirika, akaghahiri na kuuangamiza ulimwengu wote, ni sawa na leo hii, Mungu aone, watakatifu wake wote, wanaiga na kufanya mambo ya ulimwengu, wanawake wanavaa vimini, wanatembea nusu uchi barabarani, wanaume watakatifu wanakuwa mashoga n.k. kiasi kwamba huwezi kuona tofauti yoyote kati yao na ulimwenguni, hapo kinachofuata ni Mungu kuuteketeza ulimwengu, ndivyo ilivyokuwa kwa watu wa kipindi kile. Watakatifu walijitofautisha kabisa na wana wa ulimwengu..

Hivyo hakuna sababu ya mkristo kuamini, moja kwa moja vyanzo ambavyo havipo katika biblia, kwasababu vingi kati ya hivyo vinakasoro nyingi na vimejaa hadithi nyingi zilizotungwa na wanadamu lakini sio kwa uvuvio wa Roho Mtakatifu.

Kwamfano kwasasa Kanisa Katoliki, limeamua kuchukua baadhi ya hivi vitabu vya Apokrifa na kuviongezea kwenye biblia takatifu yenye vitabu 66, kufikia 73. Vitabu vyenyewe ikiwemo Yudithi, Baruku, Yoshua bin Sira, Wamakabayo 1&2,  Hekima.

Vitabu hivi vinakinzana na misingi ya imani, kwamfano, vinafundisha kwenda toharani, yaani mtu mwenye dhambi anaweza kwenda mbinguni tena, lakini baada ya kupitishwa mahali panapoitwa toharani ili kutakaswa,.,Fundisho lingine ni kuwa Mungu, anasikia maombi ya wafu, mambo ambayo ni uongo, biblia inasema, mtu ameandikiwa kuishi mara moja na baada ya kifo ni hukumu (Waebrania 9:27).

Kwahiyo, vitabu vya Aprokifa, sio vya kuviamini, kama uaminivyo biblia, iwe ni kitabu cha Henoko, au kingine chochote kile nje ya vitabu 66 vya biblia sio vya kuiamini vinamakosa mengi na wakati mwingine vimejaa uongo mwingi, ambao unapotosha kabisa.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Kitabu cha YASHARI kinachozungumziwa katika 2Samweli 1:17-18, ni kitabu gani?

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

Chuo cha vita vya Bwana ni kipi?(Hesabu 21:14)

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 7 (Yeremia na Maombolezo)

UNYAKUO.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Rudi nyumbani

Print this post

KOIKOI ANGANI AJUA NYAKATI ZAKE ZILIZOAMRIWA.

Yeremia 8:7 “Naam, koikoi angani ajua nyakati zake zilizoamriwa; na hua na mbayuwayu na korongo huangalia wakati wa kuja kwao; bali watu wangu hawazijui amri za Bwana”.

Koikoi, mbayuwayu na korongo ni ndege wa ajabu sana, ni ndege wenye uwezo wa kusoma majira ya dunia, Na hiyo imewasaidia sana, kuishi maisha ya salama salmini huku duniani, pasipo kukumbana na changamoto zozote  zisizo na maana.

Hawa ni ndege ambao kikikaribia kipindi cha baridi wanahama wote maeneo yao wanayoishi kwa muda, na kusafiri umbali mrefu sana, kwenye pembe ya pili ya dunia kutafuta msimu tulivu aidha wa vuli au  wa joto ulipo wakatulie, kisha baadaye hali ya baridi ikishakwisha wanarudi katika makazi yao ya awali kuendelea na maisha yao ya kawaida.

Kumbuka baridi tunayoizungumzia ni ile baridi haswaa, ya kutengeneza barafu iliyopo huko nchi za ulaya, ambayo hata mtu wa kawaida akikaa nje masaa machache tu anageuka kuwa jiwe la barafu, haijalishi atavaa masweta makubwa kiasi gani.. Baridi ya namna hiyo watu wanaoishi huko wanatumia muda wao mwingi kuwepo ndani, na hata kazi zao wanazifanyia ndani katika nyumba zilizojengwa kitaalamu kuhifadhi joto ndani, kwani nyumba za kawaida kama hizi zetu, kule hazijengwi kwasababu zinapitisha baridi, kiasi kwamba ukibaki ndani yake, ukakaa huko mpaka asubuhi ukiamka umeganda. Huku kwetu Afrika hatuna baridi ya namna hiyo.

Sasa, ndege hawa, wanaelewa kabisa kwa namna ya kawaida hawawezi kuishi katika mazingira hayo ya baridi kali, kwasababu hata viota vyao vitaganda.. Sasa ili kulitatua hilo tatizo inawagharimu wahame kwa muda, ndio hapo wanasafiri maelfu ya kilometa wanakuja mpaka huku kwetu Afrika, au nchi nyingine zenye joto, wanakaa  huko mpaka msimu wa baridi  utakapokwisha kule Ulaya ndio wanarudi sasa, kuendeleza maisha yao ya sikuzote.

Sasa Mungu ametumia mfano wa ndege hawa wasio na akili, kutushangaa sisi wanadamu wenye akili timamu kwanini hatujui hukumu zake alizoziweka hapa duniani..anasema..

“Naam, koikoi angani ajua nyakati zake zilizoamriwa; na hua na mbayuwayu na korongo huangalia wakati wa kuja kwao; bali watu wangu hawazijui amri za Bwana”

Hii ikiwa na maana tunashindwa kujua wakati wa neema ni upi, na wakati wa hukumu za Mungu ni upi.. Sisi tupo tu hatujui majira yetu, tunadhani wakati wote, hii neema ya wokovu itaendelea kuwepo, tunadhani wakati wote, hali itakuwa kama ilivyo sasa hivi, utahubiriwa injili kama unavyohubiriwa sasa hivi..

Ndugu yangu, fahamu kuwa neema hii inakwenda kuisha siku sio nyingi, Dhiki kubwa ambayo haijawahi kutokea tangu dunia iumbwe na wala haitakaa iwepo itakwenda kutokea ulimwenguni kote..Dalili zote zinaonyesha, pengine katika wakati wetu huu tunaoishi tutayashuhudia hayo..Haya majira ya neema ndio yanaishia hivyo, muda huu tulionao ni wa nyongeza tu, dunia ingepaswa iwe imeshakwisha tangu zamani, lakini kwasababu tu ile nuru ndogo ya jioni ipo ndio maana unaona mambo bado yapo hivi..

Tumeshafikia wakati ambao Yesu hatuhubirii  tena injili ya kutuvuta kwenye wokovu, kama ilivyokuwa zamani bali anatuhubiria injili ya kuthibitisha ulichokiamini. Sikiliza anavyosema..

Ufunuo 22:10 “Akaniambia, Usiyatie muhuri maneno ya unabii wa kitabu hiki, kwa maana wakati huo umekaribia.

11 Mwenye kudhulumu na azidi kudhulumu; na mwenye uchafu na azidi kuwa mchafu; na mwenye haki na azidi kufanya haki; na mtakatifu na azidi kutakaswa.

12 Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo”.

Unaona, hiyo yote ni kwasababu ya unafki tulionao sasa, kwasababu kama tunaweza kuyatambua majira ya nchi, kwamba huu ni msimu wa masika na hivyo tunaanza kuyaandaa mashamba yetu kabla ya mvua kunyesha, au tunahama mabondeni mapema mafuriko yasitukute, inakuwaje basi, tunashindwa kuzitambua siku hizi kuwa ni siku za mwisho? Korona inakufundisha nini? Vimbunga vinakufundisha nini, Hili wimbi la manabii wa uongo unaloliona leo hii limezuka duniani kwa ghafla linakufundisha nini? . Bado tu huoni, hizo ni dalili za wazi kabisa ambazo zinatutambulisha kuwa tukio la unyakuo lipo karibu?

Yesu alisema..

Luka 12:54 “Akawaambia makutano pia, Kila mwonapo wingu likizuka pande za magharibi mara husema, Mvua inakuja; ikawa hivyo.

55 Na kila ivumapo kaskazi, husema, Kutakuwa na joto; na ndivyo ilivyo.

56 Enyi wanafiki, mwajua kuutambua uso wa nchi na mbingu; imekuwaje, basi, kuwa hamjui kutambua majira haya”?

Itakuwa ni ajabu sana tukishindwa akili na akina koikoi. Tujitathimini sana, tuamke katika usingizi huu mzito, hukumu ya Mungu juu ya ulimwengu wote ipo karibu. Kama upo nje ya safina, anza safari upesi, mkimbilie Kristo kwa kumaanisha kabisa kwa moyo wako wote akuokoe, kwasababu hatuna muda mrefu hapa duniani,

mbingu na nchi zitapita lakini maneno ya Bwana Yesu hayatapita milele.

Mbingu ipo, lakini pia kuzimu ipo, uchaguzi ni wa wako,

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

UNYAKUO.

Nini maana ya ombeni kukimbia kwenu kusiwe wakati wa baridi wala siku ya sabato?.

WAENDEE WANA WA ISAKARI, UWE SALAMA.

KWASABABU MUDA TULIOBAKIWA NAO SI MWINGI.

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 9 (Kitabu cha Ayubu).

Rudi nyumbani

Print this post

Tofauti kati ya mtume na mwanafunzi ni ipi kibiblia?

SWALI: Tofauti kati ya mtume na mwanafunzi ni ipi?

Kwanini kuna mahali Bwana Yesu anawaita wale aliowaita mitume, na sehemu nyingine anawaita wanafunzi, tofauti yao ni ipi? Au ni kitu kimoja?


JIBU: Si kila mwanafunzi ni mtume, lakini kila mtume ni lazima awe mwanafunzi wa Yesu.

Mwanafunzi ni mtu ambaye anaketi chini kufundishwa, kupewa ujuzi au utashi au maarifa ya kumsaidia kuishi au kufanya jambo Fulani, Na Bwana Yesu naye alikuwa na watu wa namna hiyo hiyo,

Lakini kumbuka si wote waliomfuata waliitwa wanafunzi wake, isipokuwa wale tu waliokidhi vigezo vyake alivyoviweka, na vigezo vyenyewe ndio hivi;

Luka 14:25 “Makutano mengi walipokuwa wakifuatana naye, aligeuka, akawaambia,

26 Kama mtu akija kwangu naye hamchukii baba yake, na mama yake, na mke wake, na wanawe, na ndugu zake waume na wake; naam, na hata nafsi yake mwenyewe, hawezi kuwa mwanafunzi wangu.

27 Mtu ye yote asiyeuchukua msalaba wake na kuja nyuma yangu, hawezi kuwa mwanafunzi wangu.

28 Maana ni nani katika ninyi, kama akitaka kujenga mnara, asiyeketi kwanza na kuhesabu gharama, kwamba anavyo vya kuumalizia?

29 Asije akashindwa kuumaliza baada ya kuupiga msingi, watu wote waonao wakaanza kumdhihaki,

30 wakisema, Mtu huyu alianza kujenga, akawa hana nguvu za kumaliza.”.

Lakini Mtume maana yake ni “aliyetumwa”,   Wale walioitwa na Bwana Yesu na kuandaliwa kwa jukumu Fulani maalumu waliitwa mitume, ambao walikuwa kumi na mbili tu kwa wakati ule. Na kusudi lenyewe waliloitiwa lilikuwa hili;

Mathayo 28:19 “Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu;

20 na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa Dahari”.

Mitume pia waliendelea kuitwa na Kristo hata baada ya yeye kuondoka duniani.. Mfano utawaona  mitume  kama  Paulo,  Barnaba, na Epafrodito (Wafilipi 2:25)

Hata kwa wakati huu wa sasa, watumishi wote wa Mungu wanaofanya kazi kama waliyoifanya mitume, Yesu anawatambua kama mitume wake, hawa ni Zaidi ya wanafunzi, kwasababu hawawi wakristo tu peke yake, bali Zaidi wanajitaabisha kwa ajili ya ufalme wa mbinguni.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

KUNA WAKATI YESU ATAPITA NA WATU HAWATAJUA.

JINSI MTUME PAULO ALIVYOUTHAMINI WITO WAKE, JUU YA WENYE VYEO.

Nini maana ya “Tumejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii”?

USITAFUTE KUKANWA NA BWANA SIKU ILE.

Rudi nyumbani

Print this post

Fumo ni nini kama tunavyosoma katika biblia? (Hesabu 25:7)

Fumo ni mkuki, lakini katika biblia Neno mkuki linatumika kwa namna mbili, upo mkuki wa kuchomea, na pia upo mkuki wa kurusha.

Ule mkuki wa kuchomea ndio unaoitwa Fumo, ambao askari wanaubeba, na kuchoma maadui zao pale wanapowakaribia,  na kwa kawaida unakuwa ni mizito kidogo na mrefu na wenye ncha kali. Lakini ule mwingine wa kurusha wenyewe kibiblia unajulikana kama mkuki tu hivyo hivyo, isipokuwa wenyewe ni mwepesi kidogo na umetengenezwa hivyo ili utakaporushwa uweze kufika mbali zaidi adui alipo. Zote hizi ni silaha za kivita.

Hivyo unaweza kukutana na haya maneno mawili kwenye biblia yakakuchanganya.. kwa mfano baadhi ya vifungu vinayatajwa maneno yote mawili ni kama vifuatavyo.

1Samweli 17:45 “Ndipo Daudi akamwambia yule Mfilisti, Wewe unanijia mimi na upanga, na fumo, na mkuki, bali mimi ninakujia wewe kwa jina la Bwana wa majeshi, Mungu wa majeshi ya Israeli uliowatukana”.

Ayubu 41:26 “Mtu akimpiga kwa upanga, haumwingii; Wala fumo, wala mshale, wala mkuki wenye ncha”.

Vifungu vingine ambavyo utakutana na hili neno “Fumo” Ni kama vifuatavyo;

Hesabu 25:7 “Naye Finehasi mwana wa Eleazari, mwana wa Haruni kuhani, alipoona jambo hilo, akaondoka hapo katikati ya mkutano, akashika fumo mkononi mwake;

8 akamwandama huyo mtu wa Israeli na kuingia ndani ya hema nyuma yake, naye akawachoma wote wawili kwa fumo lake, yule mume wa Israeli na huyo mwanamke kati ya tumbo lake. Basi pigo likazuiwa kwao wana wa Israeli”.

1Samweli 17:7 “Na mti wa fumo lake ulikuwa kama mti wa mfumaji; na kichwa cha mkuki wake kilikuwa shekeli mia sita za chuma uzito wake; na mtu aliyemchukulia ngao yake akamtangulia”.

1Samweli 26:12 “Basi Daudi akalitwaa lile fumo, na lile gudulia la maji, kichwani pa Sauli; nao wakaenda zao, wala hapana mtu aliyeliona jambo hili wala kulijua, wala kuamka; maana wote walikuwa wamelala; kwa kuwa usingizi mzito kutoka kwa Bwana umewaangukia”.

Soma pia 2Samweli 1:6, Ayubu 39:23,

Halikadhalika na sisi  kama wakristo rohoni ni lazima tuwe na FUMO zetu na MIKUKI yetu mikononi mwetu, ili tuitwe askari kamili wa  Kristo, hizo ndio zile silaha za mkono wa kuume zinazozungumziwa katika 2Wakorintho 6:7… Kwa hizo, ndivyo tutakavyoweza kumpiga shetani, tukizikosa, tujue kuwa shetani hatoweza kutuogopa, na silaha yenyewe ni ufahamu wa kuyatambua mamlaka tuliyopewa katika jina la YESU na DAMU yake. Na kuyatumia..

Yeye mwenyewe alisema..

Luka 10:19 “Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru”.

Kila mmoja wetu ambaye anasema ameokoka anapaswa ajue kuwa mamlaka hayo amepewa, Hivyo simama kama shujaa, hubiri, haribu kazi za shetani, wafungue watu, mwaribu shetani na kazi zake zote katika maombi. Kwasababu Fumo zetu na mikuki yetu ipo  mikononi mwetu.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Mkatale ni nini katika biblia? (Matendo 16:24)

Birika ni nini?, na yale Matao matano katika birika la Bethzatha ni nini?.

Chuo cha vita vya Bwana ni kipi?(Hesabu 21:14)

NYAYO TUNAZOPASWA KUZIFUATA.

Nini maana ya ombeni kukimbia kwenu kusiwe wakati wa baridi wala siku ya sabato?.

Rudi nyumbani

Print this post

Alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru

SWALI: Naomba kufahamu nini maana ya huu mstari?

Wakorintho 3:17 “Basi ‘Bwana’ ndiye Roho; walakini alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru”.


JIBU: Kauli hiyo kinyume chake ni kuwa, kama  Roho wa Bwana hayupo basi mahali hapo hapana uhuru wowote, kwa mujibu wa biblia.

Lakini ni uhuru wa aina gani Roho Mtakatifu analeta.

kibiblia Roho Mtakatifu alikuja kuleta Uhuru wa aina mbili.

  • Uhuru wa kutuondoa katika utumwa wa dhambi na mateso.

  • Uhuru wa kututoa katika utumwa wa sheria.

1). Tukianzana na uhuru wa kutuondoa katika utumwa wa dhambi;

Siku ile Bwana Yesu alipoanza huduma yake ya kuhubiri alisema maneno haya..

Luka 4:18 “Roho wa Bwana yu juu yangu, Kwa maana amenitia mafuta kuwahubiri maskini habari njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao, Na vipofu kupata kuona tena, Kuwaacha huru waliosetwa,

19 Na kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa”.

Umeona hiyo ni kuonyesha kuwa Roho Mtakatifu aliposhuka juu ya watu wake na katika kanisa alikuwa na kazi ya kuwatoa watu katika vifungo vya dhambi na mateso ya  ibilisi, yaani waliokuwa wanasumbuliwa na mapepo, waliokuwa wanateswa na magonjwa, na hofu, na mauti, na shida  vyote hivyo vilikuja kuondolewa na Roho Mtakatifu mwenyewe,

na pia ukizidi kusoma tena katika Isaya 61:3-4 utaona unabii huo wa Roho Mtakatifu unaendelea kusema..

“…kuwafariji wote waliao; 3 kuwaagizia hao waliao katika Sayuni, wapewe taji ya maua badala ya majivu, mafuta ya furaha badala ya maombolezo, vazi la sifa badala ya roho nzito; wapate kuitwa miti ya haki, iliyopandwa na Bwana, ili atukuzwe”.

Unaona anafanya pia kazi ya kuwatoa watu katika huzuni zao, kuwafariji,kuwapa mataji ya utukufu na sifa. huo ni Zaidi ya Uhuru, ambao hakuna mtu yeyote hapa duniani angeweza kuutoa.

2). Uhuru wa sheria;

Pia alikuja kutukomboa sisi tuliokuwa chini ya sharia, tutoke katika laana ya sheria..

Wagalatia 4:3 “Kadhalika na sisi, tulipokuwa watoto, tulikuwa tukitumikishwa na kawaida za kwanza za dunia.

4 Hata ulipowadia utimilifu wa wakati, Mungu alimtuma Mwanawe ambaye amezaliwa na mwanamke, amezaliwa chini ya sheria,

5 kusudi awakomboe hao waliokuwa chini ya sheria, ili sisi tupate kupokea hali ya kuwa wana.

6 Na kwa kuwa ninyi mmekuwa wana, Mungu alimtuma Roho wa Mwanawe mioyoni mwetu, aliaye, Aba, yaani, Baba.

7 Kama ni hivyo, wewe si mtumwa tena bali u mwana; na kama u mwana, basi, u mrithi kwa Mungu”.

Roho Mtakatifu alikuja kututoa katika utumwa wa sheria, ili tupate kuhesabiwa haki kwa njia ya kumwamini Yesu Kristo na sio kwa matendo yetu tena. Kwasababu hapo mwanzo tulijitahidi sana kumpendeza Mungu kwa kushika sheria, lakini sheria ilituzidi nguvu, kwasababu ya udhaifu wa miili yetu. Hivyo tangu enzi za agano la kale, hakuwahi kuonekana hata mmoja aliyeweza kumpendeza Mungu kwa matendo yake mwenyewe, haijalishi walijitahidi kiasi gani.

Hivyo ili Mungu kutuokoa,  alimtuma mwanawe Yesu Kristo duniani, ili yeye peke yake atende mema, pasipo kufanya dhambi yoyote, kisha Mungu amuhesabie haki yeye peke yake kwa matendo yake, na ndipo sasa sisi  tutakaomwamini Yesu baadaye tuhesabiwa haki kama vile yeye, kwa njia ya matendo yake na sio yetu..

Kwahiyo, ikiwa wewe umemwamini Yesu, na ukampokea Roho wake, basi ujue Mungu haangalii matendo yako, kama ndio kipimo cha yeye kukubali, bali anamwangalia mwana wake YESU KRISTO uliyemwamini, na hivyo unahesabiwa haki, kama vile hujawahi kumkosea Mungu, kwasababu VAZI la Yesu linakufunika mbele yako.

Huoni kama huo ni uhuru mkubwa sana? Unahesabiwa haki kwa kumwamini tu!  Lakini ikumbukwe kuwa hiyo haimaanishi kuwa tuendelee kutenda dhambi kisa tu hatuhesabiwi haki kwa matendo yetu, hapana, hata kwa namna ya kawaida, huwezi kwenda kupeleka mkono kwenye tundu la nyoka akung’ate kila saa, kisa tu dawa ya kutibu sumu ipo, hapana, vinginevyo utakuwa mwendawazimu, bali utachukua tahadhari kubwa sana, kwa kuzidi kukaa mbali na nyoka, kwasababu unajua sumu yake sikuzote ni kifo..

Na sisi vivyo hivyo maadamu tunahesabiwa haki kwa kumwamini Yesu Kristo ni jukumu letu sote, tukae mbali na dhambi, kwa kadiri tuwezavyo, katika utakatifu wote ili tupate kumzalia Mungu matunda. Na hiyo ndio ishara ya kuamini kwetu.

Hivyo kwa kuhitimisha ni kuwa Roho Mtakatifu ametuletea uhuru mkubwa sana hapa duniani.  kiasi kwamba mtu yeyote atakayempokea, atakuwa HURU KWELI KWELI. Jambo ambalo watu wengi hawalifahamu, wakidhani kwa Mungu ni utumwa.

Swali ni je wewe umeshampokea ndani yako? Kama jibu ni la, unasubiri nini? Kumbuka Pasipo Roho Mtakatifu huwezi kwenda katika unyakuo, na haji ndani yako isipokuwa  kwanza umemwamini  Yesu Kristo, kwa kutubu dhambi zako kwa kumaanisha kabisa na kuwa tayari kuyaacha mambo yako maovu uliyokuwa unayafanya huko nyuma. Na pili kwa kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji tele, na kwa jina la YESU KRISTO sawasawa na Matendo 2:38, Na hapo ndipo Mungu atakapokupa kipawa cha Roho Mtakatifu ndani yako bure.

Hivyo ikiwa utapenda kumkaribisha Yesu maishani mwako, basi tafuta mchungaji yoyote, au mtumishi yoyote aliyesimama katika Imani, akusaidie, au wasiliana nasi kwa namba hizi: +255693036618 / +255789001312

Mungu akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Ufunuo 12 inaelezea vita vya wakati upi?

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

UTENDAJI KAZI MWINGINE WA ROHO MTAKATIFU USIOUFAHAMU.

 Nini maana ya “Uchungu wa mauti ni dhambi, na nguvu za dhambi ni torati”

NGAZI 7 AMBAZO MKRISTO NI LAZIMA AZIPANDE KUUFIKIA UKAMILIFU.

Rudi nyumbani

Print this post

LAKINI NINYI, NDUGU, MSIKATE TAMAA KATIKA KUTENDA MEMA.

2Wathesalonike 3:13 inasema..

“Lakini ninyi, ndugu, msikate tamaa katika kutenda mema”.

Unajua mpaka biblia inakuambia usikate tamaa, inamaanisha kuwa si kitu chepesi kukishikilia wakati wote. Si kitu ambacho unaweza ukaona faida yake moja kwa moja pale unapokifanya.. Lakini katika yote hayo bado inakuambia usikate tamaa.

Ili jambo lolote liwe wema, ni lazima malipo yake yasilingane na huduma iliyotolewa. Kwamfano mtu anapokwenda kuwasaidia yatima au maskini, huo ni wema, kwasababu hawana cha kumlipa hata baada ya kuwapa mahitaji yao, au pale anapowasomesha ndugu, huo nao ni wema, kwasababu pesa hizo ungeweza kuzitumia katika mambo yake mengine lakini ameona vema, ujinyime yeye uwape wengine maarifa.. Au unapowapa wengine chakula au mavazi bila kuwachaji pesa au kuwadai kitu chochote huo ni wema.. Au unapowapa wengine maarifa ya ufalme wa mbinguni bila malipo yoyote huo nao ni wema mkuu sana n.k.

Lakini katika hayo, kuna wakati akili inaweza kukujia, ukajisikia kuchoka na kusema nimeshasaidia watu sana mbona sioni faida yoyote ya kufanya hivyo? Au mbona sioni nikirudishiwa fadhila yoyote kutoka kwao? Wacha nipunguze wema wangu, nianze kujijali mimi mwenyewe. Au nitafute mambo yangu mwenyewe.

Katika mazingira kama hayo, biblia inasema.. usichoke kutenda wema..Kwasababu ni mbegu nzuri sana ambayo unaipanda leo, lakini siku moja utavuna matunda yake ukiwa mvumilivu.

Wagalatia 6:9 “Tena tusichoke katika kutenda mema; maana tutavuna kwa wakati wake, tusipozimia roho”.

Hata kama utaona wale uliowatendea mema wamekutangulia,wewe umekuwa daraja kwao la kufika juu, au wengine wamekudharau kwa ukarimu wako, bado usichoke katika kutenda kwako, kwasababu hicho unachokipanda thamani yake ni kubwa kuliko fedha au dhahabu. Utakuja kujua vizuri utakapovuka kule ng’ambo.

Katika biblia, tunamwona, mtu mmoja aliyeitwa Mordekai, yeye alikuwa ni mlinda mlango wa mfalme, lakini siku moja baadhi ya watumishi walipanga njama ili wamuue mfalme. Mordekai alipopata habari, kwasababu alikuwa ni mtu mwema, hakukaa kimya bali alikwenda kutoa taarifa ya njama hizo, na hatimaye mfalme akanusurika kifo, lakini biblia inatuonyesha akasahaulika, muda mrefu ukapita, wala hakuna aliyekumbuka wala kujali wema wake.

Siku moja akiwa katika hatihati ya kuuliwa na adui yake aliyeitwa Hamani, biblia inatuambia usiku huo huo mfalme alikosa uzingizi kabisa, ndipo akaanza kupitia vitabu vya kumbukumbu za taarifa za kifalme, ndipo akakutana na tukio la wema alilofanyiwa na Mordekai, mfalme akauliza je mtu huyu alitendewa fadhila gani?, wakasema, hakutendewa lolote. Ndipo akatoa maagizo kwamba avikwe mavazi yake ya kifalme anayoyavaa yeye, kisha apandishwe kwenye farasi ambaye yeye mwenyewe ndiye anayempanda, kisha wamzungushwe mji mzima, huku akipigiwa mbiu, ili atukuzwe mbele ya watu wote, kwasababu mfalme AMEMUHESHIMU biblia inasema hivyo;. Soma Esta 6

Sasa mambo hayo yanafunua na ya rohoni pia. Ukiwa ni mtenda wema, ipo Heshima ya kipekee sana, itokayo kwa Mungu mwenyewe, italetwa juu yako, siku ile ikifika. Atakugawia ule utukufu wake mwenyewe,.. Biblia inasema..

Warumi 2:6 “atakayemlipa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake; 7 wale ambao KWA SABURI KATIKA KUTENDA MEMA WANATAFUTA UTUKUFU NA HESHIMA NA KUTOKUHARIBIKA, watapewa uzima wa milele; 8 na wale wenye fitina, wasioitii kweli, bali wakubalio dhuluma, watapata hasira na ghadhabu; 9 dhiki na shida juu ya kila nafsi ya mwanadamu atendaye uovu, Myahudi kwanza na Myunani pia; 10 BALI UTUKUFU NA HESHIMA NA AMANI KWA KILA MTU ATENDAYE MEMA, Myahudi kwanza na Myunani pia”;

Unaona? hivyo, usichoke kutenda mema, kumbuka wema mkuu ni pamoja na kuwakumbuka walio katika dhambi na kuwavuta kwa Bwana. Pia kuwafariji na kuwaombea wale waliowadhaifu katika Imani. Swali ni je! Katika maisha yako, ni mema mangapi, ulishawahi kufanya kwa ajili ya Mungu?

Bwana atusaidie, tuyatimilize yote.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

NGAZI 7 AMBAZO MKRISTO NI LAZIMA AZIPANDE KUUFIKIA UKAMILIFU.

TUSIWE WATU WA KUPUNGUKIWA AKILI.

INJILI YA MANENO LAINI ITAKUGHARIMU.

FAHAMU UWIANO MUNGU ANAOHITAJI KUUONA KWETU.

Nini maana ya mhubiri 9:11? si wenye mbio washindao katika michezo?

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya mhubiri 9:11? si wenye mbio washindao katika michezo?

SWALI: Shalom wana wa Mungu Naomba msaada kuelewa andiko hili;

Mhubiri 9:11 “Nikarudi, na kuona chini ya jua, ya kwamba si wenye mbio washindao katika michezo, wala si walio hodari washindao vitani, wala si wenye hekima wapatao chakula, wala si watu wa ufahamu wapatao mali, wala wenye ustadi wapatao upendeleo; lakini wakati na bahati huwapata wote”.


JIBU: Ukisoma utaona Sulemani anasema, nikarudi na kuona chini ya jua, ikiwa na maana kuwa ni jambo ambalo amekuwa akiliona likitokea mara kwa mara duniani, hivyo akaona aandike, pengine na sisi tukilichunguza tunaweza kuliona, au pengine tulishawahi kuliona sehemu fulani.

Kwamba si wote wenye mbio, au ujuzi, au maarifa, au nguvu, ustadi au hekima mara zote zinawasaidia kupata mafanikio makubwa kuliko wale wengine wasiokuwa navyo. Na ndio maana hapo mwishoni mhubiri anamalizia kusema “lakini wakati na bahati huwapata wote”..Ikiwa na maana  majira hubadilika, leo elimu yako inaweza ikawa na faida ikakuletea mfanikio mengin lakini kesho, isiwe na maana sana, lakini yule mwingine ambaye hakuwa na elimu mambo yakambadilikia pengine kwa ujuzi wake tu wa kuzaliwa aliokuwa nao ukamfanya apate fursa nyingi kuliko wewe, na matokeo yake akawa juu yako.

Na ndio maana tunapaswa tujue majira hayo yanayobadilika yapo mikononi mwa Mungu, Bahati hizo anazitoa Mungu mwenyewe na sio mwanadamu.. Paulo alisema..

Warumi 9:16 “Basi, kama ni hivyo, si katika uwezo wa yule atakaye, wala wa yule apigaye mbio; bali wa yule arehemuye, yaani, Mungu”.

Vivyo hivyo na sisi, kwa kuwa hatujui ni majira gani yapo mbele yetu, basi tujifunze kuwa  wanyenyekevu chini ya Mungu atoaye mema yote, bila kuwadharau wengine, haijalishi tutakuwa na maarifa mengi kiasi gani kuwazidi wao, au elimu kubwa kiasi gani, au nguvu hatupaswi kujiona tumefika, vinginevyo, neno hili linaweza kutimia mbele ya macho yetu kwa wale tunaowadharau.

1Petro 5:6 “Basi nyenyekeeni chini ya mkono wa Mungu ulio hodari, ili awakweze kwa wakati wake”;

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo:

Rudi nyumbani

Print this post

NA VIUNGO VYETU VISIVYO NA UZURI VINA UZURI ZAIDI SANA.

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe,  Nakukaribisha katika kujifunza elimu ya ufalme wa mbinguni. Kumbuka kila habari katika biblia inayo ujumbe fulani nyuma yake. Hakuna habari isiyo na maana.

Leo kwa ufupi tutatazama habari ya mwamuzi mmoja aliyeitwa, Ehudi. Sasa wakati tunakwenda kutafakari habari zake naomba ufahamu kuwa Lengo la somo hili, ni kuamsha ile karama iliyo ndani yako ili  itende kazi..

Kuna wakati wana wa Israeli walimkosea sana Mungu, hivyo Mungu akawaweka chini mkono wa adui yao aliyeitwa Elgoni mfalme wa Moabu kwa muda wa miaka 18. Lakini walipomlilia Mungu, Mungu akawasikia  na kuwatumia huyu mwamuzi aliyeitwa Ehudi.

Biblia inatuambia Ehudi alikuwa ni mtu anayetumia SHOTO. Sasa biblia mpaka iandike habari kama hizo za mkono mtu anaotumia, inamaana kuwa lipo jambo la kujifunza. Ukisoma habari yenyewe pale utaona walimchukua huyu na kumpeleka kwa huyo mfalme wa Moabu ili awasilishe tunu zao ambazo walikuwa wanazipeleka kwa huyo mfalme mara kwa mara.

Sasa siku alipoenda, aliundaa upanga mrefu, kisha akauficha kwenye paja lake la kulia. Na alipofika mbele ya askari wake akazitoa zawadi hizo mbele yao..Lakini alipomalizia, hakuondoka bali aliomba aongee na mfalme faragha, kana kwamba kuna ujumbe amepewa na wakuu wa Israeli utokao kwa Mungu, amwambie, hivyo haipasi kila mtu asikie.

Ndipo mfalme akamchukua peke yake katika ukumbi wake, akawaondoa askari wake, akafunga milango. Sasa biblia inatuambia huyu Elgoni alikuwa ni mtu mkubwa sana, mwenye mraba minne, kiasi kwamba ili kumdondosha mtu kama huyo ilihitaji watu wengi, na sio mmoja tena wenye nguvu.

Lakini Mungu alilijua hilo,  na ndio maana akawatumia mtu kama Ehudi anayetumia shoto na si kilia ili kumdondosha huyo.

Kama tunavyosoma habari, aliutoa ule upanga wake, na kwa nguvu aliuzamisha kwenye Tumbo lake, ambalo pengine lilikuwa limefunikwa kwa nguo nzito, lakini upanga  ule ulipita kwa jinsi zile nguvu zilivyokuwa nyingi, kisha ukaenda kushikamana na mafuta ya tumboni na kutokea upande wa pili.. Lakini ni heri tu ungeingia upanga peke yake, biblia inasema, mpaka ule upini wa upanga ulizama ndani kabisa, usionekane. Jambo ambalo si rahisi hata kidogo kwa mtu kuuzamisha upini kwenye tumbo. Inahitaji presha kubwa sana ya kusukuma, ambayo kwa nguvu za kawaida za kibinadamu haiwezekani.

Waamuzi 3:21 “Ehudi akaunyosha mkono wake wa kushoto, akaushika huo upanga kuutoa hapo katika paja lake la kuume, akamtia tumboni mwake;

22 hicho kipini nacho kikaingia ndani pamoja na huo upanga wenyewe; nayo mafuta yakashikamana tena juu ya upanga, kwani hakuutoa tena upanga tumboni; nao ukatokea kwa nyuma”.

Unaona, ukisoma tena, utaona tena hata katika vita zamani, wana wa Israeli waliwachagua mashujaa wanaotumia shoto, kwasababu aliweka uwezo mkubwa sana wa shabaha ndani yao.

Waamuzi 20:15 “Hao wana wa Benyamini walihesabiwa siku ile kutoka hiyo miji, watu waume ishirini na sita elfu waliotumia upanga, zaidi ya hao waliokaa Gibea, ambao walihesabiwa watu wateule mia saba.

16 Katika watu hao wote walikuwako watu waume mia saba waliochaguliwa, wenye shoto; kila mmoja alikuwa anaweza kuutupia unywele mawe kwa teo, wala asikose”.

Tukiyafahamu haya turudi sasa katika kiini cha ujumbe wetu wa leo, kwasababu lengo sio kueleza umahiri wa watu wanaotumia shoto au kulia, hapana. Bali ni kutufundisha sisi mambo ya rohoni yahusuyo wokovu wetu.

Kumbuka mkono huu wa kushoto huwa haupewi heshima, wala hauwezi kutumiwa sehemu zote, hauwezi kutumia kulia chakula, au kumpia mtu mkono, n.k. Lakini uwezo na nguvu Mungu alioupa unazidi hata ule wa kulia.

Hiyo ni kuonyesha pia, Mwili wa Kristo unao viungo vingi, vingine Mungu amevikusidia kabisa vipewe  heshima, lakini vingine Mungu amevikusudia pia visiwe na heshima yoyote, lakini vimepewa nguvu na ufasaha wa hali ya juu.

1Wakorintho 12:23 “Na vile viungo vya mwili vidhaniwavyo kuwa havina heshima, viungo vile twavipa heshima zaidi; na viungo vyetu visivyo na uzuri vina uzuri zaidi sana.

24 Kwa maana viungo vyetu vilivyo na uzuri havina uhitaji; bali Mungu ameuungamanisha mwili, na kukipa heshima zaidi kile kiungo kilichopungukiwa;

25 ili kusiwe na faraka katika mwili, bali viungo vitunzane kila kiungo na mwenziwe”

Umeona? Ni lazima tufahamu si kila mtu atakuwa mchungaji, si kila mtu atakuwa mtume, si kila mtu atakuwa nabii, si kila mtu atakuwa mwalimu, zipo karama nyingi nzito na zenye nguvu  ambazo watu wanazo lakini wamezizimisha ndani yao kwasababu  wanachofikiria tu ni kuwa pale watakapokuwa wakristo basi ni kwenda kuwa wachungaji, au mitume au watu fulani maarufu wanaojulikana.

Na ndio maana karama nyingi za kipekee kama za miujiza, uponyaji, karama za ufasiri wa lugha, karama za faraja, za kukirimu n.k. hazionekani au zimekufa kabisa katika kanisa, kwasababu hatuziangalii hizo sote tunataka tukawe mitume, wachungaji na manabii.

Ukiona lipo jambo linaamka ndani yako kwa ajili ya Mungu, ambalo pengine lipo tofauti na wengine na unaona kabisa  linakupa furaha kulifanya, usilizimishe, lifanye hilo kwa bidii kwasababu huo ndio mwanzo wa kuijua karama yako. Na Mungu ameiweka hiyo ndani yako ili ilisaidie kanisa kwa sehemu kubwa sana. Fanya kile kitu kinachougua ndani yako sana.. Kama ni kumtolea Mungu, basi mtolee sana, kama ni kufundisha basi fundisha sana, kama ni kufanya uinjilisti ufanye huo kwa bidii, kama Mungu anakuonyesha mambo ya rohoni, yachochee hayo ili yakawe faida kwa mwili wote wa Kristo.

Kumbuka hakuna kiungo kisichokuwa na kazi  kanisani, maadamu umeokoka na umejazwa Roho, umuhimu wake ni lazima utaonekana tu. Lakini kazi ya kiungo ni ngumu kuonekana kama kitakuwa chenyewe chenyewe, hivyo kaa na watakatifu wengine, ndipo hapo utajua kwa urahisi karama yako ni ipi. Karama nyingine haziwezi kufanya kazi kama zitakaa zenyewe nyumbani,

Jitahidi ujue nafasi yako ni ipi ili umtumikie Mungu katika hiyo. Kwasababu kila mmoja wetu anatarajiwa na Bwana amzalie matunda.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

NITAIFAHAMU VIPI KARAMA YANGU?.

NINI TOFAUTI KATI YA KARAMA, UTENDAJI KAZI NA HUDUMA.

Vyombo vya uzuri ni vipi vinavyotajwa katika biblia?

USINIE MAKUU.

Neno “Via” linamaanisha nini katika biblia?

Nini maana ya msiwe waalimu wengi (Yakobo 1:3)?

Mchokoo ni nini katika maandiko? (Matendo 26:14)

Rudi nyumbani

Print this post

YESU ANAKWENDA KUIBADILISHA OFISI YAKE.

Mungu anayo agenda, na usipojua agenda ya Mungu katika siku hizi za mwisho ni ngumu sana kuiona ile ng’ambo, Leo hii tunaishi maisha ya juu juu tu kwasababu hatujamjua YESU ni nani na tabia zake ni zipi kulingana na majira ya wakati.

Tunapenda kumjua tu katika ule upande wake mmoja, wa upole na unyenyekevu (Mathayo 11:29)..Lakini hatujui ule upande mwingine ambao anasema yeye ni MKEMEAJI, na MKANAJI, na MFUKUZAJI na MUUAJI WA WAOVU. Ikiwa leo hii hatutamwamini, halafu tukafa, au siku ile ya mwisho ikatukuta tupo katika njia zetu wenyewe, tujue kuwa tabia tutakazoziona kwake kipindi hicho zitatustaajabisha sana, tena sana.

Kanisa hili la mwisho tunaloishi linaloitwa Laodikia, ndio kanisa pekee kati ya yale saba, ambalo Bwana amelikemea vikali, kwa tabia zake, za kuwa vuguvugu.. Hii ikiwa na maana kuwa mimi na wewe kama tupo katika uvuguvugu huu uliopo sasa hivi duniani tujue kuwa tupo katika Hasira ya Kristo, ya kwenda kutapikwa.

Uvuguvugu wa kusema mimi nimeokoka, lakini maisha yako hayauhakisi wokovu ule wa kimaandiko, ndio tabia ya kanisa hili la mwisho ilivyo, mamilioni ya wakristo ndio hivyo walivyo leo hii. Jambo ambalo halikuwepo miaka ya zamani, ambayo watu hawakumchanganya Mungu na uovu, waliookoka walijulikana, waliokuwa waovu walijulikana. Hakukuwa na mtu aliyeshiriki meza ya Bwana na wakati huo huo ni mzinzi au mlevi, mtu anakwenda ibadani, halafu kesho pia anakwenda disco, hayakuwepo hayo. Waovu walijitenga, na watakatifu waliookolewa walijitenga, Lakini leo hii ni kawaida sana, kusikia hata mmiliki bar anasema ameokoka.

Ufunuo 3:15 “Nayajua matendo yako, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri kama ungekuwa baridi au moto.

3.16 Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu.

17 Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi.

18 Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, na mavazi meupe upate kuvaa, aibu ya uchi wako isionekane, na dawa ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona.

19 Wote niwapendao mimi NAWAKEMEA, na kuwarudi; basi uwe na bidii, ukatubu.

20 Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami”.

Lakini pia hakemei tu peke yake, kuna siku atasimama KUWAKANA na kuwaonea aibu watu wengi sana, mbele ya Baba yake, na mbele ya  maelfu ya malaika zake huko mbinguni. Ikiwa leo hii unamwonea Kristo aibu unaogopa kuitwa mlokole, unaogopa kuvaa vizuri mavazi ya kujisitiri kisa utaitwa mshamba, unaona aibu kumtumikia Mungu wako, siku ile utakuonea aibu na wewe kweli kweli, hata hatapeleka jicho lake kukangalia.. wakati wengine akiwapongeza na kuwasifia.wewe utakuwa kama mtu baki tu.

Marko 8:38 “Maana kila mtu atakayenionea haya mimi, na maneno yangu, katika kizazi hiki cha uzinzi na dhambi, Mwana wa Adamu atamwonea haya mtu huyo, atakapokuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika watakatifu”.

Halikadhalika na kumkana vivyo hivyo, naye pia atakukana siku ile.

Kama hilo halitoshi Bwana Yesu pia anasema, atawafukuza watu wengi sana, siku ile, sio wachache, bali wengi sana. Na watakaofukuzwa sio watu wasiomjua Kristo bali, ni sisi sisi tuliopo kanisani, tunaolitumia jina lake kutenda miujiza lakini hatutaki kuishi maisha yampendezayo yeye. Tunapenda maisha ya uvuguvugu.

Mathayo 7:22 “Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?

23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu”.

Biblia bado inatuonyesha siku ile atakapotokea mawinguni atawaua wanadamu wengi sana watakaokuwa wameipokea ile chapa ya mnyama na kufanya vita naye..

Ufunuo 19:13 “Naye amevikwa vazi lililochovywa katika damu, na jina lake aitwa, Neno la Mungu.

14 Na majeshi yaliyo mbinguni wakamfuata, wamepanda farasi weupe na kuvikwa kitani nzuri, nyeupe, safi.

15 Na upanga mkali hutoka kinywani mwake ili awapige mataifa kwa huo. Naye atawachunga kwa fimbo ya chuma, naye anakanyaga shinikizo la mvinyo ya ghadhabu ya hasira ya Mungu Mwenyezi.

16 Naye ana jina limeandikwa katika vazi lake na paja lake, MFALME WA WAFALME, NA Bwana WA MABwana”.

Unaweza kuona jinsi mwonekano wa Bwana utakavyokuwa wa tofauti sana wakati ule?. Ndio hapo utakapojua ni kwanini biblia inasema mataifa watamwombolezea, kwasababu hatakuja tena na sura ya upole kama wengi wetu tunavyodhani, bali atakuja na jina jipya la kifalme, la kuteka na kutawala, la kutiisha lenye nguvu nyingi. Sio tena la kuokoa mtu.

Lakini kwa upande wa pili, kwa wale waliomtii, waliokubali kutembea katika njia zake, anasema atawakiri, na kuona fahari kwa ajili yao mbele za Mungu na za malaika wake, vilevile atawapa mamlaka ya kutawala pamoja naye kama wafalme, Na atawafuta machozi watakatifu wake wote.

Hivyo ndugu, leo hii Kristo bado kaketi kama mwana-kondoo, aliyechinjwa, mpole, mnyenyekevu, aokoaye, anakuvuta kwa upole mwingi kwake, ili usiopote katika aungamivu wa ulimwengu. Angalia wakati huu umebakia mchache sana, kabla ya yeye kwenda kubadilisha ofisi yake. Kwanini usitubu umrudie muumba wako?

 Damu yake bado ipo kukuokoa, na kukusamehe kabisa, mkaribishe leo kwenye moyo wako, akupe uwezo mpya wa kuushindwa huu ulimwengu. Pengine ulishamwamini au kumpokea lakini umekuwa mkristo vuguvugu mkristo jin, jambo ambalo ndio halitaki kabisa, amelikemea, hivyo toka kwenye huo uvuguvugu wako, toka katika udhehebu, mfuate Yesu kweli kweli, ondoa vizuizi vyote vinavyokufanya usiwe safi mbele za Mungu.  Na yeye mwenyewe atakutengeneza na kukufanya uwe tayari kwa ajili ya kwenda kwenye unyakuo ambao upo karibuni kutokea.

Natumai sote tutaanzana kuuonyesha mabadiliko mapya. Kabla ya mabadiliko yake hayajajidhihirisha kwetu.

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

KARAMU YA MWANA-KONDOO.

UFUNUO: Mlango wa 2 part 3

UFUNUO: Mlango wa 14

ESTA: Mlango wa 8, 9 & 10. (SIKU KUU YA PURIMU)

UFUNUO: Mlango wa 19

Rudi nyumbani

Print this post