Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe, Nakukaribisha katika kujifunza elimu ya ufalme wa mbinguni. Kumbuka kila habari katika biblia inayo ujumbe fulani nyuma yake. Hakuna habari isiyo na maana.
Leo kwa ufupi tutatazama habari ya mwamuzi mmoja aliyeitwa, Ehudi. Sasa wakati tunakwenda kutafakari habari zake naomba ufahamu kuwa Lengo la somo hili, ni kuamsha ile karama iliyo ndani yako ili itende kazi..
Kuna wakati wana wa Israeli walimkosea sana Mungu, hivyo Mungu akawaweka chini mkono wa adui yao aliyeitwa Elgoni mfalme wa Moabu kwa muda wa miaka 18. Lakini walipomlilia Mungu, Mungu akawasikia na kuwatumia huyu mwamuzi aliyeitwa Ehudi.
Biblia inatuambia Ehudi alikuwa ni mtu anayetumia SHOTO. Sasa biblia mpaka iandike habari kama hizo za mkono mtu anaotumia, inamaana kuwa lipo jambo la kujifunza. Ukisoma habari yenyewe pale utaona walimchukua huyu na kumpeleka kwa huyo mfalme wa Moabu ili awasilishe tunu zao ambazo walikuwa wanazipeleka kwa huyo mfalme mara kwa mara.
Sasa siku alipoenda, aliundaa upanga mrefu, kisha akauficha kwenye paja lake la kulia. Na alipofika mbele ya askari wake akazitoa zawadi hizo mbele yao..Lakini alipomalizia, hakuondoka bali aliomba aongee na mfalme faragha, kana kwamba kuna ujumbe amepewa na wakuu wa Israeli utokao kwa Mungu, amwambie, hivyo haipasi kila mtu asikie.
Ndipo mfalme akamchukua peke yake katika ukumbi wake, akawaondoa askari wake, akafunga milango. Sasa biblia inatuambia huyu Elgoni alikuwa ni mtu mkubwa sana, mwenye mraba minne, kiasi kwamba ili kumdondosha mtu kama huyo ilihitaji watu wengi, na sio mmoja tena wenye nguvu.
Lakini Mungu alilijua hilo, na ndio maana akawatumia mtu kama Ehudi anayetumia shoto na si kilia ili kumdondosha huyo.
Kama tunavyosoma habari, aliutoa ule upanga wake, na kwa nguvu aliuzamisha kwenye Tumbo lake, ambalo pengine lilikuwa limefunikwa kwa nguo nzito, lakini upanga ule ulipita kwa jinsi zile nguvu zilivyokuwa nyingi, kisha ukaenda kushikamana na mafuta ya tumboni na kutokea upande wa pili.. Lakini ni heri tu ungeingia upanga peke yake, biblia inasema, mpaka ule upini wa upanga ulizama ndani kabisa, usionekane. Jambo ambalo si rahisi hata kidogo kwa mtu kuuzamisha upini kwenye tumbo. Inahitaji presha kubwa sana ya kusukuma, ambayo kwa nguvu za kawaida za kibinadamu haiwezekani.
Waamuzi 3:21 “Ehudi akaunyosha mkono wake wa kushoto, akaushika huo upanga kuutoa hapo katika paja lake la kuume, akamtia tumboni mwake; 22 hicho kipini nacho kikaingia ndani pamoja na huo upanga wenyewe; nayo mafuta yakashikamana tena juu ya upanga, kwani hakuutoa tena upanga tumboni; nao ukatokea kwa nyuma”.
Waamuzi 3:21 “Ehudi akaunyosha mkono wake wa kushoto, akaushika huo upanga kuutoa hapo katika paja lake la kuume, akamtia tumboni mwake;
22 hicho kipini nacho kikaingia ndani pamoja na huo upanga wenyewe; nayo mafuta yakashikamana tena juu ya upanga, kwani hakuutoa tena upanga tumboni; nao ukatokea kwa nyuma”.
Unaona, ukisoma tena, utaona tena hata katika vita zamani, wana wa Israeli waliwachagua mashujaa wanaotumia shoto, kwasababu aliweka uwezo mkubwa sana wa shabaha ndani yao.
Waamuzi 20:15 “Hao wana wa Benyamini walihesabiwa siku ile kutoka hiyo miji, watu waume ishirini na sita elfu waliotumia upanga, zaidi ya hao waliokaa Gibea, ambao walihesabiwa watu wateule mia saba. 16 Katika watu hao wote walikuwako watu waume mia saba waliochaguliwa, wenye shoto; kila mmoja alikuwa anaweza kuutupia unywele mawe kwa teo, wala asikose”.
Waamuzi 20:15 “Hao wana wa Benyamini walihesabiwa siku ile kutoka hiyo miji, watu waume ishirini na sita elfu waliotumia upanga, zaidi ya hao waliokaa Gibea, ambao walihesabiwa watu wateule mia saba.
16 Katika watu hao wote walikuwako watu waume mia saba waliochaguliwa, wenye shoto; kila mmoja alikuwa anaweza kuutupia unywele mawe kwa teo, wala asikose”.
Tukiyafahamu haya turudi sasa katika kiini cha ujumbe wetu wa leo, kwasababu lengo sio kueleza umahiri wa watu wanaotumia shoto au kulia, hapana. Bali ni kutufundisha sisi mambo ya rohoni yahusuyo wokovu wetu.
Kumbuka mkono huu wa kushoto huwa haupewi heshima, wala hauwezi kutumiwa sehemu zote, hauwezi kutumia kulia chakula, au kumpia mtu mkono, n.k. Lakini uwezo na nguvu Mungu alioupa unazidi hata ule wa kulia.
Hiyo ni kuonyesha pia, Mwili wa Kristo unao viungo vingi, vingine Mungu amevikusidia kabisa vipewe heshima, lakini vingine Mungu amevikusudia pia visiwe na heshima yoyote, lakini vimepewa nguvu na ufasaha wa hali ya juu.
1Wakorintho 12:23 “Na vile viungo vya mwili vidhaniwavyo kuwa havina heshima, viungo vile twavipa heshima zaidi; na viungo vyetu visivyo na uzuri vina uzuri zaidi sana. 24 Kwa maana viungo vyetu vilivyo na uzuri havina uhitaji; bali Mungu ameuungamanisha mwili, na kukipa heshima zaidi kile kiungo kilichopungukiwa; 25 ili kusiwe na faraka katika mwili, bali viungo vitunzane kila kiungo na mwenziwe”
1Wakorintho 12:23 “Na vile viungo vya mwili vidhaniwavyo kuwa havina heshima, viungo vile twavipa heshima zaidi; na viungo vyetu visivyo na uzuri vina uzuri zaidi sana.
24 Kwa maana viungo vyetu vilivyo na uzuri havina uhitaji; bali Mungu ameuungamanisha mwili, na kukipa heshima zaidi kile kiungo kilichopungukiwa;
25 ili kusiwe na faraka katika mwili, bali viungo vitunzane kila kiungo na mwenziwe”
Umeona? Ni lazima tufahamu si kila mtu atakuwa mchungaji, si kila mtu atakuwa mtume, si kila mtu atakuwa nabii, si kila mtu atakuwa mwalimu, zipo karama nyingi nzito na zenye nguvu ambazo watu wanazo lakini wamezizimisha ndani yao kwasababu wanachofikiria tu ni kuwa pale watakapokuwa wakristo basi ni kwenda kuwa wachungaji, au mitume au watu fulani maarufu wanaojulikana.
Na ndio maana karama nyingi za kipekee kama za miujiza, uponyaji, karama za ufasiri wa lugha, karama za faraja, za kukirimu n.k. hazionekani au zimekufa kabisa katika kanisa, kwasababu hatuziangalii hizo sote tunataka tukawe mitume, wachungaji na manabii.
Ukiona lipo jambo linaamka ndani yako kwa ajili ya Mungu, ambalo pengine lipo tofauti na wengine na unaona kabisa linakupa furaha kulifanya, usilizimishe, lifanye hilo kwa bidii kwasababu huo ndio mwanzo wa kuijua karama yako. Na Mungu ameiweka hiyo ndani yako ili ilisaidie kanisa kwa sehemu kubwa sana. Fanya kile kitu kinachougua ndani yako sana.. Kama ni kumtolea Mungu, basi mtolee sana, kama ni kufundisha basi fundisha sana, kama ni kufanya uinjilisti ufanye huo kwa bidii, kama Mungu anakuonyesha mambo ya rohoni, yachochee hayo ili yakawe faida kwa mwili wote wa Kristo.
Kumbuka hakuna kiungo kisichokuwa na kazi kanisani, maadamu umeokoka na umejazwa Roho, umuhimu wake ni lazima utaonekana tu. Lakini kazi ya kiungo ni ngumu kuonekana kama kitakuwa chenyewe chenyewe, hivyo kaa na watakatifu wengine, ndipo hapo utajua kwa urahisi karama yako ni ipi. Karama nyingine haziwezi kufanya kazi kama zitakaa zenyewe nyumbani,
Jitahidi ujue nafasi yako ni ipi ili umtumikie Mungu katika hiyo. Kwasababu kila mmoja wetu anatarajiwa na Bwana amzalie matunda.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali. Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
NITAIFAHAMU VIPI KARAMA YANGU?.
NINI TOFAUTI KATI YA KARAMA, UTENDAJI KAZI NA HUDUMA.
Vyombo vya uzuri ni vipi vinavyotajwa katika biblia?
USINIE MAKUU.
Neno “Via” linamaanisha nini katika biblia?
Nini maana ya msiwe waalimu wengi (Yakobo 1:3)?
Mchokoo ni nini katika maandiko? (Matendo 26:14)
Rudi nyumbani
Print this post
Mungu anayo agenda, na usipojua agenda ya Mungu katika siku hizi za mwisho ni ngumu sana kuiona ile ng’ambo, Leo hii tunaishi maisha ya juu juu tu kwasababu hatujamjua YESU ni nani na tabia zake ni zipi kulingana na majira ya wakati.
Tunapenda kumjua tu katika ule upande wake mmoja, wa upole na unyenyekevu (Mathayo 11:29)..Lakini hatujui ule upande mwingine ambao anasema yeye ni MKEMEAJI, na MKANAJI, na MFUKUZAJI na MUUAJI WA WAOVU. Ikiwa leo hii hatutamwamini, halafu tukafa, au siku ile ya mwisho ikatukuta tupo katika njia zetu wenyewe, tujue kuwa tabia tutakazoziona kwake kipindi hicho zitatustaajabisha sana, tena sana.
Kanisa hili la mwisho tunaloishi linaloitwa Laodikia, ndio kanisa pekee kati ya yale saba, ambalo Bwana amelikemea vikali, kwa tabia zake, za kuwa vuguvugu.. Hii ikiwa na maana kuwa mimi na wewe kama tupo katika uvuguvugu huu uliopo sasa hivi duniani tujue kuwa tupo katika Hasira ya Kristo, ya kwenda kutapikwa.
Uvuguvugu wa kusema mimi nimeokoka, lakini maisha yako hayauhakisi wokovu ule wa kimaandiko, ndio tabia ya kanisa hili la mwisho ilivyo, mamilioni ya wakristo ndio hivyo walivyo leo hii. Jambo ambalo halikuwepo miaka ya zamani, ambayo watu hawakumchanganya Mungu na uovu, waliookoka walijulikana, waliokuwa waovu walijulikana. Hakukuwa na mtu aliyeshiriki meza ya Bwana na wakati huo huo ni mzinzi au mlevi, mtu anakwenda ibadani, halafu kesho pia anakwenda disco, hayakuwepo hayo. Waovu walijitenga, na watakatifu waliookolewa walijitenga, Lakini leo hii ni kawaida sana, kusikia hata mmiliki bar anasema ameokoka.
Ufunuo 3:15 “Nayajua matendo yako, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri kama ungekuwa baridi au moto. 3.16 Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu. 17 Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi. 18 Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, na mavazi meupe upate kuvaa, aibu ya uchi wako isionekane, na dawa ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona. 19 Wote niwapendao mimi NAWAKEMEA, na kuwarudi; basi uwe na bidii, ukatubu. 20 Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami”.
Ufunuo 3:15 “Nayajua matendo yako, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri kama ungekuwa baridi au moto.
3.16 Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu.
17 Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi.
18 Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, na mavazi meupe upate kuvaa, aibu ya uchi wako isionekane, na dawa ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona.
19 Wote niwapendao mimi NAWAKEMEA, na kuwarudi; basi uwe na bidii, ukatubu.
20 Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami”.
Lakini pia hakemei tu peke yake, kuna siku atasimama KUWAKANA na kuwaonea aibu watu wengi sana, mbele ya Baba yake, na mbele ya maelfu ya malaika zake huko mbinguni. Ikiwa leo hii unamwonea Kristo aibu unaogopa kuitwa mlokole, unaogopa kuvaa vizuri mavazi ya kujisitiri kisa utaitwa mshamba, unaona aibu kumtumikia Mungu wako, siku ile utakuonea aibu na wewe kweli kweli, hata hatapeleka jicho lake kukangalia.. wakati wengine akiwapongeza na kuwasifia.wewe utakuwa kama mtu baki tu.
Marko 8:38 “Maana kila mtu atakayenionea haya mimi, na maneno yangu, katika kizazi hiki cha uzinzi na dhambi, Mwana wa Adamu atamwonea haya mtu huyo, atakapokuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika watakatifu”.
Halikadhalika na kumkana vivyo hivyo, naye pia atakukana siku ile.
Kama hilo halitoshi Bwana Yesu pia anasema, atawafukuza watu wengi sana, siku ile, sio wachache, bali wengi sana. Na watakaofukuzwa sio watu wasiomjua Kristo bali, ni sisi sisi tuliopo kanisani, tunaolitumia jina lake kutenda miujiza lakini hatutaki kuishi maisha yampendezayo yeye. Tunapenda maisha ya uvuguvugu.
Mathayo 7:22 “Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi? 23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu”.
Mathayo 7:22 “Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?
23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu”.
Biblia bado inatuonyesha siku ile atakapotokea mawinguni atawaua wanadamu wengi sana watakaokuwa wameipokea ile chapa ya mnyama na kufanya vita naye..
Ufunuo 19:13 “Naye amevikwa vazi lililochovywa katika damu, na jina lake aitwa, Neno la Mungu. 14 Na majeshi yaliyo mbinguni wakamfuata, wamepanda farasi weupe na kuvikwa kitani nzuri, nyeupe, safi. 15 Na upanga mkali hutoka kinywani mwake ili awapige mataifa kwa huo. Naye atawachunga kwa fimbo ya chuma, naye anakanyaga shinikizo la mvinyo ya ghadhabu ya hasira ya Mungu Mwenyezi. 16 Naye ana jina limeandikwa katika vazi lake na paja lake, MFALME WA WAFALME, NA Bwana WA MABwana”.
Ufunuo 19:13 “Naye amevikwa vazi lililochovywa katika damu, na jina lake aitwa, Neno la Mungu.
14 Na majeshi yaliyo mbinguni wakamfuata, wamepanda farasi weupe na kuvikwa kitani nzuri, nyeupe, safi.
15 Na upanga mkali hutoka kinywani mwake ili awapige mataifa kwa huo. Naye atawachunga kwa fimbo ya chuma, naye anakanyaga shinikizo la mvinyo ya ghadhabu ya hasira ya Mungu Mwenyezi.
16 Naye ana jina limeandikwa katika vazi lake na paja lake, MFALME WA WAFALME, NA Bwana WA MABwana”.
Unaweza kuona jinsi mwonekano wa Bwana utakavyokuwa wa tofauti sana wakati ule?. Ndio hapo utakapojua ni kwanini biblia inasema mataifa watamwombolezea, kwasababu hatakuja tena na sura ya upole kama wengi wetu tunavyodhani, bali atakuja na jina jipya la kifalme, la kuteka na kutawala, la kutiisha lenye nguvu nyingi. Sio tena la kuokoa mtu.
Lakini kwa upande wa pili, kwa wale waliomtii, waliokubali kutembea katika njia zake, anasema atawakiri, na kuona fahari kwa ajili yao mbele za Mungu na za malaika wake, vilevile atawapa mamlaka ya kutawala pamoja naye kama wafalme, Na atawafuta machozi watakatifu wake wote.
Hivyo ndugu, leo hii Kristo bado kaketi kama mwana-kondoo, aliyechinjwa, mpole, mnyenyekevu, aokoaye, anakuvuta kwa upole mwingi kwake, ili usiopote katika aungamivu wa ulimwengu. Angalia wakati huu umebakia mchache sana, kabla ya yeye kwenda kubadilisha ofisi yake. Kwanini usitubu umrudie muumba wako?
Damu yake bado ipo kukuokoa, na kukusamehe kabisa, mkaribishe leo kwenye moyo wako, akupe uwezo mpya wa kuushindwa huu ulimwengu. Pengine ulishamwamini au kumpokea lakini umekuwa mkristo vuguvugu mkristo jin, jambo ambalo ndio halitaki kabisa, amelikemea, hivyo toka kwenye huo uvuguvugu wako, toka katika udhehebu, mfuate Yesu kweli kweli, ondoa vizuizi vyote vinavyokufanya usiwe safi mbele za Mungu. Na yeye mwenyewe atakutengeneza na kukufanya uwe tayari kwa ajili ya kwenda kwenye unyakuo ambao upo karibuni kutokea.
Natumai sote tutaanzana kuuonyesha mabadiliko mapya. Kabla ya mabadiliko yake hayajajidhihirisha kwetu.
Bwana akubariki sana.
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
KARAMU YA MWANA-KONDOO.
UFUNUO: Mlango wa 2 part 3
UFUNUO: Mlango wa 14
ESTA: Mlango wa 8, 9 & 10. (SIKU KUU YA PURIMU)
UFUNUO: Mlango wa 19
SWALI: Naomba kuuliza watumishi wa Mungu katika Mwanzo 17:20 anaposema kwa habari ya Ishmaeli atazaa maseyidi 12, hao ndio akina nani kwa Sasa?
2) Pia katika 1samweli 3:3 anasema kipindi Samweli anaitwa na Mungu taa ilikua haijazimika bado Nia taa gani hiyo? Asante Sana Ni hayo.
JIBU:
Mwanzo 17:18 “Ibrahimu akamwambia Mungu, Lau kwamba Ishmaeli angeishi mbele yako. 19 Mungu akasema, Sivyo, lakini Sara mkeo atakuzalia mwana wa kiume, nawe utamwita jina lake Isaka. Nami nitafanya agano langu imara kwake kuwa agano la milele kwa ajili ya uzao wake baada yake. 20 Na kwa habari za Ishmaeli nimekusikia, nimembariki, nitamzidisha, nami nitamwongeza sana sana. Atazaa maseyidi kumi na wawili, nami nitamfanya awe taifa kuu”.
Mwanzo 17:18 “Ibrahimu akamwambia Mungu, Lau kwamba Ishmaeli angeishi mbele yako.
19 Mungu akasema, Sivyo, lakini Sara mkeo atakuzalia mwana wa kiume, nawe utamwita jina lake Isaka. Nami nitafanya agano langu imara kwake kuwa agano la milele kwa ajili ya uzao wake baada yake.
20 Na kwa habari za Ishmaeli nimekusikia, nimembariki, nitamzidisha, nami nitamwongeza sana sana. Atazaa maseyidi kumi na wawili, nami nitamfanya awe taifa kuu”.
Neno Seyidi linamaanisha mtawala, hivyo hapo biblia ilimaanisha kuwa Ishmaeli atazaa watawala 12.. ambao utaona wakitajwa kwa majina katika Mwanzo 25:13
Mwanzo 25:13 “Na haya ndiyo majina ya wana wa Ishmaeli, kwa majina yao, na kwa vizazi vyao. Mzaliwa wa kwanza wa Ishmaeli, ni Nebayothi, na Kedari, na Abdeeli, na Mibsamu, 14 na Mishma, na Duma, na Masa, 15 na Hadadi, na Tema, na Yeturi, na Nafishi, na Kedema. 16 Hao ndio wana wa Ishmaeli, na hayo ni majina yao, katika miji yao, na katika vituo vyao, maseyidi kumi na wawili kwa kufuata jamaa zao.
Mwanzo 25:13 “Na haya ndiyo majina ya wana wa Ishmaeli, kwa majina yao, na kwa vizazi vyao. Mzaliwa wa kwanza wa Ishmaeli, ni Nebayothi, na Kedari, na Abdeeli, na Mibsamu,
14 na Mishma, na Duma, na Masa,
15 na Hadadi, na Tema, na Yeturi, na Nafishi, na Kedema.
16 Hao ndio wana wa Ishmaeli, na hayo ni majina yao, katika miji yao, na katika vituo vyao, maseyidi kumi na wawili kwa kufuata jamaa zao.
Katika historia wana hawa wa Ishmaeli walikuwa watu wakuu sana, na ndio chimbuko la mataifa ya kiharabu tunayoyaona sasahivi kule mashariki ya kati.
2) Je ni Taa ipi hiyo inayozungumizwa katika 1Samweli 3:1?,
Tusome.
1 Samweli 3:1 “Basi, mtoto Samweli akamtumikia Bwana mbele ya Eli. Na neno la Bwana lilikuwa adimu siku zile; hapakuwa na mafunuo dhahiri. 2 Ikawa wakati huo, Eli alipokuwa amelala mahali pake (tena macho yake yalikuwa yameanza kupofuka, hata asiweze kuona), 3 na taa ya Mungu ilikuwa haijazimika bado, na Samweli alikuwa amelala katika hekalu la Bwana, palipokuwa na sanduku la Mungu;
1 Samweli 3:1 “Basi, mtoto Samweli akamtumikia Bwana mbele ya Eli. Na neno la Bwana lilikuwa adimu siku zile; hapakuwa na mafunuo dhahiri.
2 Ikawa wakati huo, Eli alipokuwa amelala mahali pake (tena macho yake yalikuwa yameanza kupofuka, hata asiweze kuona),
3 na taa ya Mungu ilikuwa haijazimika bado, na Samweli alikuwa amelala katika hekalu la Bwana, palipokuwa na sanduku la Mungu;
Inadhaniwa kuwa hiyo ni ile taa ya hekaluni, lakini ukitafakari kwa ukaribu, utaona kuwa biblia haikumaanisha ile taa ya hekaluni au ile ya kwenye hema ya kukutania, bali ilimaanisha pumzi au uhai wa Eli, ukikumbuka kuwa habari iliyokuwa inazungumziwa hapo juu ni kuhusu uzee wa Eli, ambapo inasema umri wake ulikuwa umeshaenda sana mpaka macho yake yalikuwa yameshaanza kupofuka.
Biblia inasema..
Mithali 20:27 “Pumzi ya mwanadamu ni taa ya Bwana; Hupeleleza yote yaliyomo ndani yake”.
Unaona? Hivyo hapo ilimaanisha kuwa Pumzi ya uhai wa Eli ilikuwa bado haijamuacha.
Hiyo ni kutukumbusha pia, kuwa upo wakati na sisi Taa ya Mungu itazima ndani yetu. Na kama tunavyojua taa ikizimika huwa kunakuwa na giza na sikuzote gizani hakuna shughuli yoyote inayoendelea. Vivyo hivyo na siku ambayo kila mmoja wetu atakufa, huko atakapoenda hakuna jambo lolote la kimaendeleo atakalolifanya, Hatakuwa na nafasi ya pili ya kutubu ikiwa alikufa katika dhambi, hatakuwa na nafasi ya pili ya kufanya marekebisho ikiwa alizembea zembea katika masuala ya wokovu wake akiwa hapa duniani. Atakachokuwa anasubiria huko ni hukumu tu.
Mhubiri 9:5 “kwa sababu walio hai wanajua ya kwamba watakufa; lakini wafu hawajui neno lo lote, wala hawana ijara tena; maana kumbukumbu lao limesahauliwa”.
Hivyo tunapaswa tujithamini maisha yetu tunamalizaje mwendo tukiwa hapa duniani? . Kwasababu huko ng’ambo hakuna nafasi ya pili.
Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp
Kiango na Pishi ni nini (Mathayo 5:15)?
Kwanini Kuhani wa Mungu Eli alikufa kwa kuvunjika shingo?
JE NI LAZIMA KUBADILISHA JINA BAADA YA KUOKOKA?
Mafundisho
Isaya 10:22 “Maana watu wako, Ee Israeli, wajapokuwa wengi kama mchanga wa pwani, ni mabaki tu watakaorudi; kuangamiza kumekusudiwa, kunakofurika kwa haki”.
Wana wa Israeli walidhani, kuchukuliwa tena utumwani na kurudishwa (Babeli na Misri) kungekuwa ni kurahisi kama ilivyokuwa wakati ule walipotolewa Misri. Walidhani Mungu atakuja kuwatoa tena kama taifa kwa mkono hodari wa nabii kama Musa, na wote watarudi nchi yao.
Lakini mambo hayakuwa hivyo, Mungu aliwaonya mapema akiwaambia hilo jambo halitakuwepo, na ndio maana alitumia muda mrefu sana kuwasihi, watubu waache njia zao mbaya, lakini hawakusikia badala yake wakawa wanawapiga manabii wake na wengine kuwaua,
Lakini siku ya siku ilipofika, yale mataifa 10 yalichukuliwa utumwani Ashuru, na biblia inatuonyesha hakuna hata mmoja aliyerudi hadi wakati huu wa sasa.. watu wote waliendelea kubaki kule kule, hata na lile taifa moja la Yuda, ambalo lilikuja kuchukuliwa nalo baadaye Babeli na Nebukadreza, japokuwa nalo lilikuwa na watu wengi sana, lakini ni kikundi kidogo sana, yaani watu wachache sana ndio Mungu aliwarudisha, na hiyo ilikuwa tu ni kuwatunzia uzao vinginevyo wangefananishwa na Sodoma na Gomora, kwa jinsi ambavyo wangepotea wote.
Warumi 9:27 “Isaya naye atoa sauti yake juu ya Israeli, kusema, Hesabu ya wana wa Israeli,ijapokuwa ni kama mchanga wa bahari,ni mabaki yao tu watakaookolewa. 28 Kwa maana Bwana atalitekeleza neno lake juu ya nchi, akilimaliza na kulikata. 29 Tena kama Isaya alivyotangulia kunena, Kama Bwana wa majeshi asingalituachia uzao, Tungalikuwa kama Sodoma, tungalifananishwa na Gomora”.
Warumi 9:27 “Isaya naye atoa sauti yake juu ya Israeli, kusema, Hesabu ya wana wa Israeli,ijapokuwa ni kama mchanga wa bahari,ni mabaki yao tu watakaookolewa.
28 Kwa maana Bwana atalitekeleza neno lake juu ya nchi, akilimaliza na kulikata.
29 Tena kama Isaya alivyotangulia kunena, Kama Bwana wa majeshi asingalituachia uzao, Tungalikuwa kama Sodoma, tungalifananishwa na Gomora”.
Sasa biblia inasema mambo hayo yaliandikwa kwa mifano ili kututahadharisha na sisi tulio katika nyakati hizi za hatari (1Wakorintho 10:11). Kwasababu kanisa la Israeli la mwilini lilikuwa linawakilisha kanisa la Kristo la rohoni sasa hivi. Kumbuka mara baada ya Israeli kuingiliwa na ukengeufu, pale walipoanza kuabudu miungu mingine, hapo ndipo Mungu alipokusudia kuwaangamiza wote, mikononi mwa maadui zao.
Vivyo hivyo na katika Kanisa la Kristo leo hii, Bwana alishatabiri kuwa kuwa kuna majira litaingiliwa na ukengeufu..ndio yale magugu yaliyopandwa na ibilisi ndani ya kanisa (Mathayo 13:24-30).. Sasa ukengeufu huu, ndio unaowafanya wakristo wengi wawe vuguvugu kupita kiasi, Hatushangai kuona idadi ya watu wanaojiita wakristo duniani ikizidi kuongezeka, sasa hivi ni Zaidi ya bilioni tatu.. Ni kama mchanga wa bahari tu, hata zaidi ya walivyokuwa Israeli.
Lakini hiyo sio tija kwamba wote tutaokolewa siku ile. Ni mabaki tu ndio yatakayookoka, ambayo Yesu aliyafananisha na ‘kundi dogo’
Luka 12:32 “Msiogope, enyi kundi dogo; kwa kuwa Baba yenu ameona vema kuwapa ule ufalme”.
Na ndio maana Bwana Yesu alisema. Walioitwa ni wengi lakini wateule ni wachache. Hichi ni kipindi cha kurekebisha mienendo yetu kama wakristo, kwasababu kurudi Yerusalemu kwa sasa ni kugumu sio kama kule kwa kwanza. Nguvu ya kukuvuta umgeukie Mungu sasa sio kama ile ya kwanza ulipoanza kuamini.
Ni wachache tu ndio watakaorejea, na sisi tuwe miongoni mwa hao. Mungu anatuita kuache dhambi, tumgeukie yeye, tusiungalie ulimwengu, kwani unapoteza sana.. Kwasababu hizi ni nyakati za mwisho na Kristo yupo mlangoni, wakati huu ni ule wa kumalizia, siku yoyote, wakati wowote, tunaweza kushuhudia tendo hilo kuu la unyakuo. Ambapo kwa upande mmoja utakuwa ni furaha na shangwe, lakini kwa upande mwingine kilio na kusaga meno na majuto makubwa.
Bwana atusaidie.
Ni nani aliyesema “Nitume mimi”? katika (Isaya 6:8)
PINDO LA VAZI LAKE SASA LIMEREFUSHWA.
JE UPENDO WAKO UMEPOA?
Fuawe ni nini? Kama tunavyosoma katika Isaya 41:7
EPUKA KUUNDA MATARAJIO YAKO, KWENYE AHADI ZA MUNGU.
WhatsApp
Shalom, nakukaribisha katika kuyatafakari maneno ya uzima, biblia inatuambia..
Mithali 16:31 “KICHWA CHENYE MVI NI TAJI YA UTUKUFU, Kama kikionekana katika njia ya haki”.
Wengi wetu tunatafuta wokovu ili tu tuende mbinguni, tunadhani wokovu ni kumkiri tu Yesu na kubatizwa, basi imeishia hapo, tunachosubiria tu ni kufa na kwenda mbinguni.. Ndugu Mawazo kama hayo ndiyo yanatufanya kila siku tuwe watu wa kulegea legea watu wa kusubiri subiri, tukisema siku moja wataokoka, siku tunayokaribia kufa, siku ambayo tukishatimiza malengo yetu ndio tutakayomtumikia Mungu, hatujui kuwa kuchelewa kwetu kunatupotezea nafasi nyingi na kubwa sana mbinguni.
Ndugu yangu, maisha ya mwilini ni kivuli tosha cha maisha ya rohoni. Kama vile katika mwili kuna hatua, ya utoto, utu uzima na uzee, na kwamba ili mtu afikie ile ya mwisho ni lazima azipitie hizi za kwanza zote, vivyo hivyo na rohoni..
Kumbuka Uzee siku zote una kibali, una heshima, na una utukufu,
Walawi 19:32 “Mwondokeeni mtu mwenye mvi; heshimuni uso wa mtu mzee; nawe mche Mungu wako, Mimi ndimi Bwana”.
Unaona na utukufu wake unadhihirishwa kwa zile mvi zinazotokea juu ya kichwa chake. Hali kadhalika rohoni, kwa jinsi mtu anavyokua kiroho, anavyodumu katika wokovu, anavyomtumikia sana Bwana, ndivyo mvi zake zinavyoongezeka kidogo kidogo, na kwa jinsi atakavyoendelea kung’ang’ana na Bwana atafikia hatua kichwa chake chote kinajaa mvi, kinakuwa cheupe pe chote.
Ukishafikia hatua hiyo rohoni, ujue wewe ni mtu ambaye utakuwa karibu sana na Mungu utakapofika mbinguni.
Ukisoma kitabu cha Ufunuo, utawaona kuna wazee 24 mbinguni, Wale ni malaika wa Mungu, ambao wanafanana na wanadamu wazee, utajiuliza ni kwanini Mungu kawaweka pale kama wazee na si vijana au watoto ili wakizunguke kiti chake cha enzi, tena wakiwa katika idadi yao hiyo ndogo ya 24?. Hiyo ni kuonyesha kuwa watu wa namna hiyo, ndio watakaokuwa karibu sana na Mungu hata wakati ule ukifika.
Ufunuo 4:3 “na yeye aliyeketi alionekana mithili ya jiwe la yaspi na akiki, na upinde wa mvua ulikizunguka kile kiti cha enzi, ukionekana mithili ya zumaridi. 4 Na viti ishirini na vinne vilikizunguka kile kiti cha enzi, na juu ya vile viti naliona wazee ishirini na wanne, wameketi, wamevikwa mavazi meupe; na juu ya vichwa vyao walikuwa na taji za dhahabu”.
Ufunuo 4:3 “na yeye aliyeketi alionekana mithili ya jiwe la yaspi na akiki, na upinde wa mvua ulikizunguka kile kiti cha enzi, ukionekana mithili ya zumaridi.
4 Na viti ishirini na vinne vilikizunguka kile kiti cha enzi, na juu ya vile viti naliona wazee ishirini na wanne, wameketi, wamevikwa mavazi meupe; na juu ya vichwa vyao walikuwa na taji za dhahabu”.
Na kama tunavyojua ili kumtambua mzee utaona mvi nyeupe katika kichwa chake. Katika biblia tunamwona Bwana wetu Yesu Kristo akiwa kama mzee wetu wa kwanza rohoni mwenye nywele hizo nyeupe..
Ufunuo 1:14 “Kichwa chake na nywele zake zilikuwa nyeupe kama sufu nyeupe, kama theluji; na macho yake kama mwali wa moto”;
Sasa kama tulivyosema, mpaka mtu afikie hatua ya uzee, ni sharti kwanza apitie utoto na ujana,..Vivyo hivyo rohoni ili tufikie ukomavu Mungu anaoutarajia kwetu hatuna budi kuukulia wokovu vya kutosha angali tukiwa hapa hapa duniani.
Inashangaza kuona mtu anayachukulia maisha yake ya rohoni, kirahisi rahisi tu, leo inapita bado yupo katika dhambi, kesho nayo hivyo hivyo, mwezi unapita, miaka inapita, anasikia tu injili anapuuzia, bado hajali maisha yake ya milele yatakuja kuwaje huko atakapokwenda, yeye anajitaabisha tu na haya maisha ya kitambo ya miaka 80, lakini yale ya mabilioni ya miaka hayaangalii. Anadhani kule ni kufa na kuingia tu, hajui kuwa zipo nafasi na vyeo, ambavyo si watu wote watapewa na Mungu.
Mwingine atasema ameokoka, lakini miaka nenda rudi, bado ni mchanga kiroho, hakui yupo pale pale, maisha yake hayana ushuhuda, ukimuuliza ni nini umefanya kwa Mungu wako, hana, yeye ni kusikiliza tu, basi, akidhani ndicho Mungu alichotuitia hapa duniani.
Tunapaswa tukifika kule tutambuliwe kwa mvi zetu rohoni, tumemtumikia Mungu wetu kweli kweli, sio tunatambuliwa kama vitoto vichanga tena.
Unapoyasikia maneno haya, usiyapuuzie, kumbuka unapaswa uwe ndani ya Kristo ukimtumikia kwa muda wa kutosha ukiwa hapa duniani, ili ujijengee daraja zuri kule unapokwenda, usidhani wokovu ni kuamini tu basi..wokovu ni maisha, kila siku unajenga maisha yako ya baadaye, kama vile unavyojijengea maisha yako ya mwilini.
Hivyo mimi na wewe kuanzia sasa, tutamani kuwa karibu na Mungu, kwasababu tukifa kule tutatambuliwa kwa idadi ya mvi zetu rohoni.
Maran Atha.
Je! Kuna malaika wangapi mbinguni?
MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA KITABU CHA RUTHU:
JINSI YA KUEPUKA KUUMIZWA MOYO KUSIKOKUWA NA SABABU.
MZAZI, JALI MAISHA YA KIROHO YA MTOTO WAKO.
UTAKASO NI SEHEMU YA MAISHA YA MKRISTO YA KILA SIKU.
Shalom, nakusalimu katika jina kuu la Bwana wetu Yesu Kristo, karibu tuyatafakari maneno ya uzima pamoja.
Muda mfupi kabla ya Bwana Yesu kwenda kutukuzwa na maelfu ya watu kule Yerusalemu lipo agizo ambalo aliwapa wanafunzi wake wawili, na agizo lenyewe lilikuwa ni kwenda kumletea mwana punda aliyekuwa amefungwa mahali Fulani. Wengi wetu tunaweza kuona lile lilikuwa ni agizo jepesi, lakini kiuhalisia halikuwa jepesi kama tunavyodhani, kwani walipotumwa walioambiwa sio wakaombe wapewe, hapana bali wakachukue, kana kwamba hao punda walikuwa ni wa kwao.
Embu tusome kidogo;
Luka 19:29 “Ikawa alipokaribia Bethfage na Bethania, kwenye mlima uitwao wa Mizeituni, alituma wawili katika wale wanafunzi, 30 akisema, Nendeni mpaka kijiji kile kinachowakabili, na mtakapoingia ndani mtaona mwana-punda, amefungwa, ambaye hajapandwa na mtu ye yote bado, mfungueni mkamlete hapa. 31 Na kama mtu akiwauliza, Mbona mnamfungua? Semeni hivi, Bwana anamhitaji. 32 Na wale waliotumwa wakaenda wakaona kama alivyowaambia. 33 Na walipokuwa wakimfungua mwana-punda, wenyewe waliwaambia, Mbona mnamfungua mwana-punda? 34 Wakasema, Bwana ana haja naye”.
Luka 19:29 “Ikawa alipokaribia Bethfage na Bethania, kwenye mlima uitwao wa Mizeituni, alituma wawili katika wale wanafunzi,
30 akisema, Nendeni mpaka kijiji kile kinachowakabili, na mtakapoingia ndani mtaona mwana-punda, amefungwa, ambaye hajapandwa na mtu ye yote bado, mfungueni mkamlete hapa.
31 Na kama mtu akiwauliza, Mbona mnamfungua? Semeni hivi, Bwana anamhitaji.
32 Na wale waliotumwa wakaenda wakaona kama alivyowaambia.
33 Na walipokuwa wakimfungua mwana-punda, wenyewe waliwaambia, Mbona mnamfungua mwana-punda?
34 Wakasema, Bwana ana haja naye”.
Utajiuliza ni kwanini, Bwana atumie kauli hiyo, mfungue na sio waombeni mniletee? Unadhani hakujua kanuni za kuchukua mali za watu wengine? Alijua sana, lakini si kila wakati aliruhusu hilo, pengine wale wanafunzi walisema kwanini Bwana asituambie tukaanze na kuomba kwanza, si tutapewa tu, kuliko kwenda na kufungua wanyama ambao si wetu, si tutaitwa wezi?
Ni sawa na leo hii mtu akuambie, nenda pale mlimani city, utakuta gari limepakiwa, ingia kisha piga ufunguo, endesha uniletee, bila shaka utasema huyu mtu hanitakii mema bali mabaya.. anataka nikachomwe moto kama mwizi.
Lakini Kristo alikuwa na sababu kufanya vile, alijua mwisho wake utakuwaje..Vilevile alijua madhara ya kutanguliza kuomba omba vibali kwenye kazi yake, alijua milolongo ambayo wangekutana nayo, alijua vikwazo ambavyo shetani angevizusha mahali pale..pengine nyie ni wakina nani, mmesajiliwa wapi, shughuli yenu ni nini, hatuwatambui hapa mtaani, msimgolee yule punda, elimu yenu ni ipi, leta uthibitisho kwanza wa barua kutoka kwa huyo Bwana wenu, n.k. vinginevyo tutawashitaki..
Lakini wao hawakuongea chochote walipofika, badala yake walianza kufanya kama Yesu alivyowaagiza, kufungua punda na pengine katika hatua ya mwisho kabisa pale walipoanza kuondoka, ndipo wahusika walipowaona, na kuwauliza nyie mnafanya nini hapo? Mnawapeleka wapi hao punda?..Wakasema Bwana anawahitaji..
Sasa wale kuona tayari punda wao wameshafunguliwa na gharama imeshaingiwa, kuwarudisha itakuwa ni hatua ndefu sana wakaona ni bora wawache tu, pengine wawape masharti Fulani madogo ya kuwatumia, au walipie gharama Fulani kidogo tu. Hilo halijalishi maadamu punda wameshapatikana.
Vivyo hivyo na hata sasa, usitegemee kwanza ruhusu za watu kufanya jambo lolote la ki-Mungu, ni ngumu sana kusikilizwa au kusapotiwa, fanya kwanza kisha baadaye wakikuuliza kwanini ulifanya waambie ni kwababu Yesu aliniagiza..hata wakikasirika lakini tayari ulishafanya, lile agizo la Yesu litakulinda.
Vikwazo vya shetani ni vingi sana, unaweza ukajikuta haumfanyii Mungu lolote kisa, visheria Fulani vidogo vidogo, au viutaratibu Fulani vinakubana. Wewe fanya tu agizo lake litakulinda mbele ya safari. Unaweza hata usifanya huduma kisa hujakamilisha taratibu hii au ile, hayo tumeyaona sana sehemu nyingi, usingojee kukamilisha taratibu za wanadamu kwanza, endelea na taratibu za Mungu, kisha hizo za wanadamu zitafuata baadaye watakapokuuliza..kwasababu ukisema uanzie kwao, utavunjika moyo mapema mpendwa. Vikwanzo ni vingi kila kukicha.
Bwana Yesu alishatoa agizo, enendeni ulimwenguni kote, mkuhubiri injili kwa kila kiumbe. Hilo agizo halisemi, mkaombe kwanza kuhubiri, hapana, wewe kahubiri kwa jinsi Mungu alivyokujalia kisha wakikufuata, waeleze hilo ni agizo la Yesu. Kwa kufanya hivyo Yesu mwenyewe atafungua njia ya kukusaidia, atakuwekea wepesi, au kupewa kibali cha kuendelea na kazi ya Bwana.
LISHIKILIE SANA LILE AGIZO LA KWANZA.
Baghala ni nini katika maandiko?(2Wafalme 5:16).
Fitina maana yake nini kwenye biblia?
WAOMBEENI WANAOWAUDHI.
SWALI: Shalom naomba kufahamu maana ya huu mstari..
Luka 17:37 “Wakajibu, wakamwuliza, Wapi, Bwana? Akawaambia, Ulipo mzoga, ndipo watakapokutanika tai”.
JIBU: Kabla ya wanafunzi wa Yesu kumuuliza Bwana hilo swali “WAPI?”..Kuna maneno ambayo yalitangulia juu kidogo, ambayo tukiyasoma yatatusaidia kuelewa vizuri huo mstari ulimaanisha nini, embu tusome kidogo.
Luka 17:22 “Akawaambia wanafunzi, Siku zitakuja mtakapotamani kuona siku moja katika siku zake Mwana wa Adamu, msiione. 23 Tena watawaambia, Tazama, kule! Tazama, huku! Msiondoke mahali mlipo, wala msiwafuate”;
Luka 17:22 “Akawaambia wanafunzi, Siku zitakuja mtakapotamani kuona siku moja katika siku zake Mwana wa Adamu, msiione.
23 Tena watawaambia, Tazama, kule! Tazama, huku! Msiondoke mahali mlipo, wala msiwafuate”;
Ukisoma kwenye Mathayo imeeleza kwa undani zaidi, inasema..
Mathayo 24:23 “Wakati huo mtu akiwaambia, Tazama, Kristo yupo hapa, au yuko kule msisadiki. 24 Kwa maana watatokea makristo wa uongo, na manabii wa uongo, nao watatoa ishara kubwa na maajabu; wapate kuwapoteza, kama yamkini, hata walio wateule. 25 Tazama, nimekwisha kuwaonya mbele. 26 Basi wakiwaambia, Yuko jangwani, msitoke; yumo nyumbani, msisadiki”.
Mathayo 24:23 “Wakati huo mtu akiwaambia, Tazama, Kristo yupo hapa, au yuko kule msisadiki.
24 Kwa maana watatokea makristo wa uongo, na manabii wa uongo, nao watatoa ishara kubwa na maajabu; wapate kuwapoteza, kama yamkini, hata walio wateule.
25 Tazama, nimekwisha kuwaonya mbele.
26 Basi wakiwaambia, Yuko jangwani, msitoke; yumo nyumbani, msisadiki”.
Maneno hayo Yesu aliyatanguliza kama angalizo la nyakati za hatari zitakazotokea siku za mwisho, akiwaonya kwamba wengi watakuja wakiwavuta watu kwao wakiwaambia Kristo yupo huku au kule, kwa maneno yao ya ushawishi, wakijinadi, tuna hichi au kile, sisi tuna miujiza mikubwa, sisi tuna upako wa mafuta mabichi, sisi ni wataalumu wa tiba za kiroho, sisi tuna makanisa makubwa kuliko yote duniani n.k.
Hivyo Yesu kwa kulijua hilo kwamba litakuja kutokea akawapa tahadhari wanafunzi wake kwamba wasitoke kuwafuata, wasiwe wepesi kuwaendea, wabaki mahali walipo, wasiende popote, kwasababu watawapotosha..
Sasa katika mazingira hayo ya kutokwenda mahali popote ndipo wanafunzi wake mwishoni wakamuuliza swali, NI WAPI sasa patakuwa sahihi pa kwenda..au tutakwenda wapi?
Ndipo Yesu akawaambia palipo na mzoga ndipo watakaposanyika Tai.. Ikiwa na maana mahali palipo na chakula cha Tai ndipo watakapokuja hapo na kukusanyika..
Na kama tunavyojua ndege aina ya tai wanaouwezo wa kuona mbali sana, leo hii kama kuna mnyama kafa porini na angani hakuna ndege yoyote, ukikaa baada ya muda mfupi utawaona tai wengi wamekusanyika hapo.. utajiuliza wametokea wapi na wakati anga lilikuwa jeupe halina ndege hata mmoja? Ni kwasababu jicho la Tai huwa linaona chakula kutokea mbali sana. Tai anaona mahali ambapo wewe huwezi kumwona.
Ni kama tu vile, mahali Fulani pawe na kinyesi cha mnyama au mtu, dakika si nyingi utaona nzi wengi wamekusanyika, na utajiuliza wametoka wapi wadudu hao na mahali hapo ni porini..Jibu ni kwamba, Mungu kawaumbia uwezo mkubwa wa kunusa vitu vya asili yao, tokea mbali, na ndio maana utawaona hata kama eneo hilo limejificha namna gani, wataenda tu.
Vivyo hivyo na wana tai wa Mungu, Kristo kawawekea uwezo Fulani wa kujua chakula chao halisi kilipo haijalishi ni wapi walipo watakipata tu. Tai si kama kuku, ambaye anaona vya hapo chini tu, bali Tai anaona vya mbali sana. Vivyo hivyo na sisi kama ni wanatai, ni lazima tuwe wa kufuata kile chakula kilicho chetu tu..Si kila chakula cha kukikurupukia kisa kipo karibu na sisi, au kinavutia..
Bali tuwe na macho ya tai ya kujua chakula chetu kipo wapi..
Hizi siku za mwisho, usiwe wa kukurupukia kila aina ya mafundisho, au imani. Kristo ameshatuonya..
Tafuta chakula cha wakati wako unaoishi.
Nini maana ya “chakula hakituhudhurishi mbele za Mungu”?
Choyo ni nini kibiblia? (Luka 12:15, Zaburi 10:3)
NYAYO TUNAZOPASWA KUZIFUATA.
Ukoma wa nyumba ulifunua nini zamani?
Nini maana ya “yasiyokuwapo hayahesabiki”(Mh 1:15)
Bwana Yesu alisema..
Mathayo 5:43 “Mmesikia kwamba imenenwa, Umpende jirani yako, na, Umchukie adui yako; 44 lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi, 45 ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni; maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki….. 48 Basi ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu”.
Mathayo 5:43 “Mmesikia kwamba imenenwa, Umpende jirani yako, na, Umchukie adui yako;
44 lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi,
45 ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni; maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki…..
48 Basi ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu”.
Kumuombea anayekuudhi sio kitu kirahisi hata kidogo, huo ndio ukweli..afadhali ungeambiwa achana naye tu yapite, lakini unaagizwa umuombee, si jambo jepesi, Lakini hivyo ndivyo vipimo vya ukamilifu wa mtu kwa Mungu. Hakuna njia ya mkato.
Pale unapoona jirani yako anakuzungumzia vibaya, mpaka anakuharibia pengine siku yako, badala umchukie na kumwekea vinyongo, au umzungumze na wewe vibaya , unaambiwa na Yesu umuombee.. Ukishindwa kufanya hivyo, basi wewe bado hujawa na tabia kama za Mungu ndani yako, bado hujawa mkamilifu kulingana na maandiko.
Bwana Yesu alitoa, mfano hai akasema, hata Mungu mwenyewe, huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua yake waovu na wema..Kiasi kwamba mchawi anatoka kuwaloga watu usiku, na kuwasababishia matatizo, lakini asubuhi anaamka na mvua kwenye shamba lake, na linastawi vizuri sana , mpaka anavuna, na kuuza, na kupata chakula kwa ajili yake na watoto wake na cha akiba.
Jambazi, anatoka kuiba usiku na kuharibu, na akiamka asubuhi anakutana na jua kama wewe unavyoliona, sio kwamba Mungu anapendezwa na tabia zake, la, lakini anaonyesha rehema zake kwao pengine siku moja watatubu, na kuacha njia zao.
Na sisi pia kuna wakati tulishawahi kuwa waovu mbele za Mungu, kiasi kwamba ilikuwa ni haki ya Mungu atulipizie kisasi tuondoke chini ya jua, lakini mara nyingi tumeona hakufanya chochote, mpaka sasa tumetubu tumeokolewa, na tunamtumikia. Laiti kama asingekuwa mvumilivu kwetu, leo hii tungekuwa kwenye moto wa jehanumu.
Huo ndio ukamilifu wa Mungu, na yeye pia akatupa agizo hilo hilo kwamba tuwaombee wale wanaotuudhi, wale ambao tunawaona ni maadui zetu haswa haswa, tuwaombee, tusijifanye sisi ni washupavu sana, tunajua kupambana, tunajua kusimamia haki zetu, tukadhani kuwa mawazo ya Mungu ni kama ya kwetu, badala ya kuwaombea mema, tukaanza kuwaombea vifo, kuwaombea njaa, kuwaombea wasifanikiwe..n.k.
Mungu atahuzunishwa na sisi, na kutuona kama ni wachanga wa njia zake.
Kumbuka hatujaitwa kuwaiga wanadamu, bali tumeitwa kumuiga Mungu. Kama vile Yesu alivyosema,…
Yohana 5:19 “Mwana hawezi kutenda neno mwenyewe ila lile ambalo amwona Baba analitenda; kwa maana yote ayatendayo yeye, ndiyo ayatendayo Mwana vile vile”.
Haijalishi wanadamu wote watasema, wapige maadui zako. Lakini maneno ya Yesu ni tuwaombee. Hata kama yataonekana ni maombi magumu kwetu, lakini kwa Mungu ni manukato. Tujizoeshe kuwa watu na namna hiyo kila siku. Ndipo tutakapoona Mungu akituzidishia na sisi rehema zake kila siku.
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mafundisho mengine
VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 9 (Kitabu cha Ayubu).
Sikuzote roho haiji hivi hivi tu, bila kuwa na chanzo Fulani, na chanzo hicho kinaweza kuwa mtu, au kitu au sehemu, Sasa pale yule mtu anapoondoka, huwa anaacha tabia yake Fulani inayoendelea na tabia hiyo ikishakita mizizi vizuri ndio inaitwa roho,..
Kwamfano kwenye biblia utamwona mwanamke anaitwa Yezebeli, huyu mwanamke alikuwa ni mchawi, na mzinzi, na tabia zake tunazijua vizuri kwenye biblia, jinsi alivyoiharibu Israeli na kuigeuzwa kuwa nchi ya kichawi. Lakini tunasoma mara baada ya kufa kwake, roho yake iliendelea kutembea duniani, na ndio maana miaka mingi baadaye utaona Bwana Yesu anamzungumzia tena habari zake kana kwamba bado yupo duniani, katika kitabu cha Ufunuo,
Ufunuo 2:19 “Nayajua matendo yako na upendo na imani na huduma na subira yako; tena kwamba matendo yako ya mwisho yamezidi yale ya kwanza.20 Lakini nina neno juu yako, ya kwamba wamridhia yule mwanamke Yezebeli, yeye ajiitaye nabii na kuwafundisha watumishi wangu na kuwapoteza, ili wazini na kula vitu vilivyotolewa sadaka kwa sanamu”
Utamwona pia Eliya, pindi alipoondoka roho yake ilianza kutembea tena wakati baada ya wakati, Kumbuka hawi Eliya mwenyewe kama Eliya, Au Yezebeli kama Yezebeli, bali ile tabia ya rohoni iliyokuwa juu ya Eliya, ndiyo inayotembea juu ya watu kadha wa kadha, Roho hiyo ilikuja juu ya Elisha, baadaye Yohana Mbatizaji n.k. na itaendelea kutembea hadi wakati wa nyakati za mwisho kabisa.(Malaki 4:5)
Halikadhali Na Bwana wetu Yesu Kristo, yeye alitembea hapa duniani, kwa miaka 33 na nusu, lakini alipoondoka, hakuondoka hivi hii ilikuwa ni sharti aichalie Roho yake katikati yetu, na ndio Roho Mtakatifu tuliye naye sasa. Kiasi kwamba mtu akiyaamini maneno yote ya Bwana Yesu moja kwa moja anampokea Roho wake ambaye atamsaidia aishi maisha kama ya Yesu.
Sasa tukishaweka msingi kama huo, tuende moja kwa moja katika somo letu la leo ambalo linamzungumzia yule Elima mchawi aliyekutana na Paulo na Barnaba pindi walipokuwa wanahubiri injili huko Pafo, tusome.
Matendo 13:6 “Walipokwisha kupita katikati ya kisiwa chote mpaka Pafo, wakaona mtu mmoja, mchawi, nabii wa uongo, Myahudi jina lake Bar-Yesu;7 mtu huyu alikuwa pamoja na liwali Sergio Paulo, mtu mwenye akili. Yeye liwali akawaita Barnaba na Sauli waje kwake, akataka kulisikia neno la Mungu.8 Lakini Elima, yule mchawi (maana ndiyo tafsiri ya jina lake), akashindana nao, akitaka kumtia yule liwali moyo wa kuiacha ile imani.9 Lakini Sauli, ambaye ndiye Paulo, akijaa Roho Mtakatifu, akamkazia macho,10 akasema, Ewe mwenye kujaa hila na uovu wote, mwana wa Ibilisi, adui wa haki yote, huachi kuzipotoa njia za Bwana zilizonyoka?11 Basi, angalia, mkono wa Bwana u juu yako, nawe utakuwa kipofu, usilione jua kwa muda. Mara kiwi kikamwangukia na giza, akazunguka-zunguka na kumtafuta mtu wa kumshika mkono na kumwongoza.12 Ndipo yule liwali, alipoyaona yaliyotendeka, akaamini, akiyastaajabia mafundisho ya Bwana”`.
Huyu mtu alikuwa ni mchawi, na wakati huo huo ni nabii wa Uongo. Kazi yake na lengo lake, lilikuwa ni kuwafanya watu wasiiamini njia ya wokovu, pale tu wanapokutana na injili ya kweli ya msalaba. Ni mchawi aliyebobea kwenye kitendo cha kupinga tu, na kushawishi watu kuiacha imani, na ndio maana mtume Paulo alimwambia “Ewe mwenye kujaa hila na uovu wote, mwana wa Ibilisi, huachi kuzipotoa njia za Bwana zilizonyoka?”
Kwa kazi yake hii, mpaka akawa ameshawafikia kabisa na watu wakubwa na wenye akili kama huyu Sergio Paulo, ikiwa na maana kuwa huku chini tayari alishaburuza.
Kama tunavyoona hapo, Paulo alipoanza kumuhubiria huyu liwali, yeye bila kupoteza muda alianza kuwabishia wakina Paulo, na kutoa hoja zake za uongo, na pengine kumwambia yule liwali hawa watu ni waongo, wapiga dili, hakuna kitu kuokoka hapa duniani, huyo Yesu aliibiwa hajafufuka, hawa ni wapotoshaji n.k.
Lakini Paulo kulijua hilo, akamkemea saa ile ile akawa kipofu kwa muda.
Sasa huyu mtu alishakufa lakini aliiacha roho yake hapa duniani, na roho hiyo inatembea kwa kasi sana, sasa hivi duniani imewavaa watu wengi, na wenyewe hawajijui kuwa wanafanyika kuwa wachawi, pasipo wao kujijua.
Kuna watu kazi yao ni kupinga tu kila habari ya Kristo, wakiona kila mtumishi wa Mungu anahubiri, au kushuhudia, wanasema ni nabii wa uongo, wanasema ni wazinzi, wakisikia injili ya kweli inahubiriwa wanasema anapotosha,
Sasa kibiblia watu kama hao ni wachawi, hawajijui tu kama wameshafikia hiyo hatua
Katika nyakati hizi za kumalizia ni kujiangalia sana, si kila wazo la kila mtu la kulisikiliza, au kulipokea haijalishi atakuwa ni ndugu yako, au rafiki yako, au mfanyakazi mwenzako.
Bwana Yesu alisema, angalieni jinsi msikiavyo (Luka 8:18)
Kaa mbali nao, ikiwa unaona kila wakati tu wanakosoa habari za Mungu au watumishi wa Mungu, hakuna kipengele hata kimoja watakisifia, kaa mbali nao, wanakuwekea tu moyo mgumu wa kutokuamini.
Ukikutana na watu kama hao ujue unaongea na wachawi, jiupushe nao. Leo hii duniani utakutana nao wengi sana akina Elimu, Bar Yesu. Wewe jikite katika kumtafuta Muumba wako kwa bidii, mpende Mungu wako, sikiliza na soma Neno la Mungu, achana na hao wanaoipuuzia, au kukejeli kila kitu cha ki Mungu kinachokatiza mbele yao.
Jiepushe nao.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
JINSI PAULO ALIVYOPAMBANA NA UJINGA WA ROHONI.
JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?
Nini maana ya neno ‘Kuabiri’ kama linavyotumika katika biblia?
ILI NIWE KIELELEZO KWA WALE WATAKAOMWAMINI BAADAYE.
KUMTUMIKIA MUNGU, KUNAWEZA KUWE KINYUME NA MATARIJIO YAKO.
Jumapili ya tarehe 24 tutakuwa na ibada yetu ya pili. Tunawakaribisha Wakazi wa Daresalaam Na wengineo.
Pamoja na ushirika tutakuwa na muda wa kuuliza maswali ya biblia, Ushauri na maombezi
Hivyo mnakaribishwa wote.
Mahali ni Tegeta Nyuki.
Muda ni saa 3:00 asubuhi mpaka saa 6:30.
Karibuni sana.
Mwl. Denis.Wingu la Mashahidi.
Kwa mawasiliano: piga +255693036618 au +255789001312
Shalom.