Title March 2022

Tofauti ya deni na dhambi ni nini?

Katika Marko 6:12 maandiko yanasema…“Utusamehe deni zetu, kama sisi nasi tuwasamehevyo wadeni wetu”… Hizi deni ndio zipi??

Jibu: Mtu aliyekutukana ana deni kwako la kuja kukuomba radhi!..Hilo ni deni lake kwako, awe anajua au hajui…Na kulilipa ni yeye kuja kukuomba wewe radhi!.. Asipokuja kukuomba radhi basi hilo litabaki kuwa deni kwake. (wewe utakuwa unamdai). Labda wewe uamue kumsamehe tu!

Hali kadhalika na sisi tunapomfanyia Mungu dhambi, tunakuwa na deni kwake la KUUNGAMA! (Maana yake kukiri makosa yetu na kuomba radhi kwake)!. Hayo ni madeni kwetu kwa Mungu..

Kwa maana dhambi ni kosa lolote mtu analolifanya dhidi ya Mungu.

Lakini Bwana wetu Yesu alitufundisha kuwa ni lazima tuwasamehe watu madeni yao ili na sisi tusamehewe yetu!.. Maana yake, yale mambo ambayo wangepaswa waje waungame mbele yetu (yaani kukiri na kuomba radhi), wanapoungama basi tunawasamehe, na hata wasipokuja kuomba radhi vile vile tunapaswa tuwasamehe.

Na wakati mwingine watu wanatukosa pasipo hata wao kujua kama wametukosa, hivyo hawawezi kuja kutuomba radhi kwasababu hata hawajui kama wametukosea, (Hivyo wanabakia kuwa na madeni kwetu ambayo hawajui hata kama wanayo)..

Kadhalika na sisi tunamkosea Mungu kwa mambo mengi, ambayo wakati mwingine hatujui kama tunamkosea (Jambo linalotufanya tuwe na madeni mengi mbele za Mungu), hata pasipo sisi wenyewe kujua.

Kwahiyo tunapoomba hiyo sala ya Baba yetu!, na kusema “utusamehe deni zetu”.. Maana yake tunamsihi Mungu atusamehe yale makosa ambayo hatukuyatubia au yale tuliyoyafanya pasipo kujua kuwa ni makosa…Na Mungu ni mwaminifu, anatusamehe…lakini kama tu na sisi tutakuwa tayari kuwasamehe wengine madeni yao.

Swali ni Je!, na wewe umemsamehe yule aliyekutukana au kukusengenya au kukutapeli? au unasubiri aje kukuomba radhi?…nakuambia usingoje!..wewe msamehe hata bila yeye kukuomba radhi, ndivyo na Mungu atakavyokusamehe na wewe makosa ambayo hata wewe hukumwomba radhi!..

Bwana wetu Yesu Kristo, aliwasamehe wale wote, ambao walimsulubisha, (Aliwasamehe pasipo wao kumwomba msamaha).. kwakufanya vile alitupa na sisi kielelezo, kwamba na sisi tuwasamehe wenzetu kama yeye alivyotusamehe. Kwasababu tusipowasamehe watu makosa yao na Mungu wetu hatatusamehe sisi.

Mathayo 18:21“Kisha Petro akamwendea akamwambia, Bwana, ndugu yangu anikose mara ngapi nami nimsamehe? Hata mara saba?

22 YESU AKAMWAMBIA, SIKUAMBII HATA MARA SABA, BALI HATA SABA MARA SABINI.

23 Kwa sababu hii ufalme wa mbinguni umefanana na mfalme mmoja aliyetaka kufanya hesabu na watumwa wake.

24 Alipoanza kuifanya, aliletewa mtu mmoja awiwaye talanta elfu kumi.

25 Naye alipokosa cha kulipa, bwana wake akaamuru auzwe, yeye na mkewe na watoto wake, na vitu vyote alivyo navyo, ikalipwe ile deni.

26 Basi yule mtumwa akaanguka, akamsujudia akisema, Bwana, nivumilie, nami nitakulipa yote pia.

27 Bwana wa mtumwa yule akamhurumia, akamfungua, akamsamehe ile deni.

28 Mtumwa yule akatoka, akamwona mmoja wa wajoli wake, aliyemwia dinari mia akamkamata,akamshika koo,akisema Nilipe uwiwacho.

29 Basi mjoli wake akaanguka miguuni pake, akamsihi, akisema, Nivumilie, nami nitakulipa yote pia.

30 Lakini hakutaka, akaenda, akamtupa kifungoni, hata atakapoilipa ile deni.

31 Basi wajoli wake walipoyaona yaliyotendeka, walisikitika sana, wakaenda wakamweleza bwana wao yote yaliyotendeka

32 Ndipo bwana wake akamwita, akamwambia, Ewe mtumwa mwovu, nalikusamehe wewe deni ile yote, uliponisihi;

33 nawe, je! Haikukupasa kumrehemu mjoli wako, kama mimi nilivyokurehemu wewe?

34 Bwana wake akaghadhibika, akampeleka kwa watesaji, hata atakapoilipa deni ile yote.

35 Ndivyo na Baba yangu wa mbinguni atakavyowatenda ninyi, msiposamehe kwa mioyo yenu kila mtu ndugu yake.”

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

REKEBISHA YAFUATAYO ILI UCHUMI WAKO UKAE SAWA.

JE KUNA UISLAMU KATIKA BIBLIA?

Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?

NI KIPI KINAMZUIA MUNGU KUZUNGUMZA NA SISI?

Kwa namna gani mauti hufanya kazi ndani yetu na uzima kwa wengine? (2Wakorintho 4:12).

Rudi nyumbani

Print this post

Rushwa inapofushaje macho?

Biblia inasema rushwa inawapofusha macho hao waonao? (Kutoka 23:8) Ni kwa namna gani rushwa inaweza kumpofusha mtu macho?

Jibu: Tusome,

Kutoka 23:8 “Nawe usipokee rushwa; kwani hiyo rushwa huwapofusha macho hao waonao, na kuyapotoa maneno ya wenye haki”.

Ili tuelewe vizuri, hebu tutafakari mfano ufuatao..

Hakimu mahakamani anaona kabisa mhalifu fulani amefanya kosa linalostahili kifungo (yaani macho yake yanaona kabisa lile ni kosa alilolifanya, na anapaswa ahukumiwe kulingana na sheria)..Lakini anapopewa rushwa, palepale anajiziba macho, na kumwachia yule mhalifu, na kulifunika kosa lake.. (Sasa kitendo hicho cha hakimu kujiziba macho na kulifunika kosa, ndicho kinachoitwa kupofuka macho).. na hiyo yote ni kwasababu ya rushwa!..Laiti asingepokea rushwa angelitazama kosa na kulihukumu jinsi inavyostahili..

Ndio maana biblia inasema…“Rushwa huwapofusha macho hao waonao”..Wanaona na kujua kabisa jambo Fulani sio sawa, lakini rushwa inawafanya wasilione kama ni kosa tena..(macho yao yamepofuka!).

Na sio tu!, kuwapofusha macho hao wanaoipokea, bali pia “inayapotoa maneno ya wenye haki”.. maana yake.. wale watu wastahilio kupata haki, hawapati hiyo haki, wanaonena maneno ya haki, maneno yao yanapotoshwa kwasababu ya rushwa iliyotolewa na mwingine.

Ni mara ngapi, watu wasio na hatia wanafungwa, kwasababu tu upande mmoja umetoa rushwa?..

Biblia utaona inazidi kuliweka hilo wazi katika kitabu cha Kumbukumbu la Torati..

Kumbukumbu 16:19 “Usipotoe maamuzi; wala usipendelee uso wa mtu; WALA USITWAE RUSHWA; KWA KUWA RUSHWA HUPOFUSHA MACHO YA WENYE AKILI, NA KUGEUZA DAAWA YA WENYE HAKI”.

Na sisi kama wakristo hatupaswi kupokea wala kutoa rushwa!..kwasababu rushwa ina laana nyuma yake.

Mithali 17:23 “ASIYE HAKI HUTOA RUSHWA KIFUANI, Ili kuzipotosha njia za hukumu”.

Katika biblia utaona mojawapo ya sababu iliyomfanya Nabii Samweli akubalike mbele za Mungu na watu, na kuzidi kupata kibali cha kuiamua Israeli mpaka uzee wake, ni mwenendo wake wa kutokubali Rushwa..

1Samweli 12:1 “Kisha Samweli akawaambia Israeli wote, Angalieni, nimeisikiliza sauti yenu katika hayo yote mliyoniambia, nami nimemtawaza mfalme juu yenu.

2 Basi sasa, angalieni, mfalme anakwenda mbele yenu; na mimi ni mzee, mwenye mvi; tena, tazameni, wana wangu wapo pamoja nanyi; nami nimekwenda mbele yenu toka ujana wangu hata leo.

3 NAMI NIPO HAPA; BASI, MNISHUHUDIE MBELE ZA BWANA, NA MBELE YA MASIHI WAKE,NALITWAA NG`OMBE WA NANI? AU NALITWAA PUNDA WA NANI? AU NI NANI NILIYE MDHULUMU? NI NANI NILIYEMWONEA? AU KWA MKONO WA NANI NIMEPOKEA RUSHWA INIPOFUSHE MACHO? NAMI NITAWARUDISHIA NINYI.

4 NAO WAKASEMA, HUKUTUDHULUMU, WALA HUKUTUONEA, WALA HUKUPOKEA KITU KWA MKONO WA MTU AWAYE YOTE.

5 Akawaambia, Bwana ni shahidi juu yenu, na masihi”

Umeona?..Samweli hakuwahi kupokea rushwa Maisha yake yote, na ndio ikawa sababu ya yeye kudumu katika Uamuzi wa Israeli, Lakini sasa kinyume chake, wanawe wawili aliowazaa hawakuwa kama yeye, wao walikuwa wanapokea rushwa..

Jambo ambalo liliwafanya wana hao wa Samweli kutolewa katika kiti cha Uamuzi wa Israeli, na hiyo ni kwasababu tu ya RUSHWA walizokuwa wanazipokea kutoka kwa watu..na matokeo yake ikasababisha Israeli nzima kuingia katika dhambi ya kutaka mfalme, kutokana na kwamba waliona Watoto hao wa Samweli hawafai..

1Samweli 8:1 “Hata Samweli alipokuwa mzee, aliwafanya wanawe wawe waamuzi juu ya Israeli.

2 Na jina la mwanawe mzaliwa wa kwanza aliitwa Yoeli; na jina la wa pili Abiya; walikuwa waamuzi katika Beer-sheba.

3 ILA WANAWE HAWAKUENDA KATIKA NJIA ZAKE, BALI WALIZIACHA, ILI WAPATE FAIDA; WAKAPOKEA RUSHWA, NA KUPOTOSHA HUKUMU.

4 Ndipo wazee wote wa Israeli wakakutana pamoja, wakamwendea Samweli huko Rama”

5 wakamwambia, Angalia, wewe umekuwa mzee, na wanao hawaendi katika njia zako; basi, tufanyie mfalme atuamue, mfano wa mataifa yote.

Hiyo ikitufundisha kuwa Rushwa, siku zote inatokosesha kibali mbele za Bwana na mbele za watu!…

Ukitaka udumu katika Nafasi yoyote uliyopo, ambayo ni Mungu kakuweka, basi kaa mbali na rushwa!.. ukitaka udumu katika utumishi (wa Mungu) kaa mbali na rushwa, ukitaka udumu katika kazi ya mikono unayoifanya basi kaa mbali na rushwa.. Wanadamu wengi wanaweza wasikuone unayoyafanya kwa siri, lakini Mungu anakuona, na yeye ndiye atakayekuvua hiyo nafasi..na Zaidi ya yote utakapokufa bila kuacha rushwa, basi utahukumiwa.

Ayubu 15:34 “Kwa kuwa jamii ya hao wasiomcha Mungu watakuwa tasa, NA MOTO UTATEKETEZA MAHEMA YENYE RUSHWA”.

Bwana atusaidie..

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

JE! JICHO LAKO LINAONA NINI KATIKATI YA MAJARIBU?

IELEWE SAUTI YA MUNGU.

Bwana aliposema “sikuja kutangua torati bali kuitimiliza” alikuwa anamaanisha nini?

NINI TOFAUTI KATI YA MATENDO YA SHERIA NA MATENDO YA IMANI?

Ni kwanini Yesu alisema Na wakisikia wasikie, wasielewe Wasije wakaongoka?

Rudi nyumbani

Print this post

Unyenyekevu ni nini?

Unyenyekevu ni nini, kibiblia, ili mtu awe ni mnyenyekevu anapaswa aweje?


Tafsiri ya Unyenyekevu ni Kujishusha. Pale unapokuwa na uwezo wa kutumia nguvu, au sauti, au mamlaka, kuhimiza jambo, lakini unajishusha chini, kana kwamba wewe si kitu, huo ndio unaitwa unyenyekevu.

Unyenyekevu sio kushushwa, bali kujishusha. Na kinyume cha Unyenyekevu ni kiburi, yaani kujipandisha juu, kujiona wewe unaweza yote, wewe ni bora kuliko vyote, wewe una nguvu kuliko wote, wewe una sauti zaidi ya wote.

Unyenyekevu ni mgumu sana kuufikia, kwasababu asili ya mwanadamu ni kutaka kujipandisha juu. Lakini ukiupata unyenyekevu basi umepata mpenyo mkubwa sana wa kumfikia Mungu.

Kiwango cha unyenyekevu kinatofautiana, kwa jinsi mtu anavyoteremka ngazi moja chini, ndivyo kiwango chake cha unyenyekevu kinavyokuja juu, na pale anapoongeza ngazi nyingine na nyingine ndivyo unyenyekevu wake unavyofikia kilele cha juu sana.

Ni kwanini tuwe wanyenyekevu?

  1. Ni kwasababu Kristo naye alikuwa mnyenyekevu;

Wafilipi 2:6 “ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho;

7 bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu;

8 tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba”.

2) Kwasababu Mungu anawapinga wenye kiburi

Yakobo 4:6 “Lakini hutujalia sisi neema iliyozidi; kwa hiyo husema, Mungu huwapinga wajikuzao, bali huwapa neema wanyenyekevu”.

Mungu ni adui mkubwa kwa kiburi, hivyo tukilijua hilo ni kujitahidi sana tuwe mbali na kitu hicho.

Faida za kuwa wanyenyekevu ni zipi?

  1. Mungu anakuwa karibu nasi:

Mungu alikuwa karibu na Bwana Yesu, kuliko mtu mwingine yeyote, na hiyo yote ni kwasababu ya unyenyekevu wake:

Mathayo 11:28 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.

29 Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;

     2) Mungu anatukweza juu;

Utaona baada ya Bwana Yesu kujishusha, Mungu alimkweza juu Zaidi ya vitu vyote ulimwenguni.

Wafilipi 2:8 “tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba.

9 Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina;

10 ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi;

11 na kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI Bwana, kwa utukufu wa Mungu Baba”.

Tunakuwaje wanyenyekevu?

  1. Kumuhesabu mwenzako ni bora kuliko nafsi yako mwenyewe.

Wafilipi 2:3 “Msitende neno lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake”.

     2) Kuuzuia ulimi:

Kuwa wa mwisho kunena, na kuzuia hasira zako, usitoe maneno ya majigambo;

Yakobo 3:5 “Vivyo hivyo ulimi nao ni kiungo kidogo, nao hujivuna majivuno makuu. Angalieni jinsi moto mdogo uwashavyo msitu mkubwa sana.

6 Nao ulimi ni moto; ule ulimwengu wa uovu, ule ulimi, umewekwa katika viungo vyetu, nao ndio uutiao mwili wote unajisi, huuwasha moto mfulizo wa maumbile, nao huwashwa moto na jehanum”.

  3) Kutojihesabia haki, mbele za Mungu:

Luka 18:9 “Akawaambia mfano huu watu waliojikinai ya kuwa wao ni wenye haki, wakiwadharau wengine wote.

10 Watu wawili walipanda kwenda hekaluni kusali, mmoja Farisayo, wa pili mtoza ushuru.

11 Yule Farisayo akasimama akiomba hivi moyoni mwake; Ee Mungu, nakushukuru kwa kuwa mimi si kama watu wengine, wanyang’anyi, wadhalimu, wazinzi, wala kama huyu mtoza ushuru.

12 Mimi nafunga mara mbili kwa juma; hutoa zaka katika mapato yangu yote.

13 Lakini yule mtoza ushuru alisimama mbali, wala hakuthubutu hata kuinua macho yake mbinguni, bali alijipiga-piga kifua akisema, Ee Mungu, uniwie radhi mimi mwenye dhambi”.

14 Nawaambia, huyu alishuka kwenda nyumbani kwake amehesabiwa haki kuliko yule; kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa.

     4) Kukubali kujishughulisha na mambo manyonge

Warumi 12:16 “Mpatane nia zenu ninyi kwa ninyi. Msinie yaliyo makuu, lakini mkubali kushughulishwa na mambo manyonge. Msiwe watu wa kujivunia akili”.

Si lazima, kila jambo la juu tung’ang’anie kulifanya. Bwana Yesu alikuwa ni Mungu, lakini akaona kule kuwa sawa naye sio kitu cha kushikamana nacho. Akawa kama mtumwa..Vivyo hivyo na sisi tupende utumwa kuliko ukubwa.

Mwisho kabisa tukumbuke kuwa Unyenyekevu kibiblia, upo kwa namna mbili; Unyenyekevu wa sisi kwa sisi, na unyenyekevu kwa Mungu. Vyote viwili vinakamilisha Unyenyekevu wa ki-Mungu. Kama vile ulivyo upendo. Ili tukamilike katika huo ni sharti, tupendane sisi kwa sisi, na vilevile tumpende Mungu.

Ndio maana Bwana Yesu aliwatawaza miguu watakatifu wake, akatupa na sisi kielelezo kuwa tunyenyekeane sisi kwa sisi, kama yeye alivyofanya.

Hivyo tuizingatie sana nguzo hii muhimu katika ukristo wetu. Ili tumfurahie Mungu wetu.

Bwana akubariki.

Group la whatsapp Kwa mgawanyo bora wa masomo download App hapa>> App wingu la mashahidi

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

Upole ni nini?

Furaha ni nini?

UPENDO NI NINI NA JE! KUNA AINA NGAPI ZA UPENDO?

TUMAINI NI NINI?

Jehanamu ni nini?

Rudi nyumbani

Print this post

Dusumali ni nini katika biblia?

Dusumali ni nini?, Mafurungu ni nini?, na Matalasimu ni nini?.. kama tunavyosoma katika Isaya 3:20?


Jibu: Tusome,

Isaya 3:20 “na dusumali, na mafurungu, na vitambi, na vibweta vya marashi, na matalasimu”

 1. Dusumali ni nini?

Dusumali ni aina ya mavazi ambayo yalikuwa yanavaliwa kichwani..ambayo yalikuwa yanatengenezwa na malighafi tofauti tofauti kulingana na tamaduni za jamii husika. Na waliokuwa wanazivaa sana ni watu mashuhuri au viongozi wa jamii hiyo…Kwajamii za maeneo ya Afrika, dusumali zilikuwa zinatengenezwa na manyoya ya ndege(Tazama picha juu).. Maeneo ya Misri, zilikuwa zinatengenezwa kwa vitambaa maalum.

 2. Mafurungu ni nini?

Mafurungu ni urembo unaofungiwa katika miguu ya wanawake..(Tazama picha chini).

mafurungu

 3. Matalasimu ni nini?

Matalasimu ni vitu ambavyo watu wanavivaa shingoni, au wanajifungia katika sehemu za miili yao, kama kinga yao. (kwa lugha ya sasa zinaweza kuitwa hirizi).

Lakini mavazi haya yote ni ya kidunia.. na watu wa Mungu waliookoka (wakiume na wakike) hawapaswi kuyavaa, kwani ni machukizo, ndio maana utaona hapo katika hiyo isaya mlango wa 3, Bwana anasema atawapiga wavaao hayo, kwasababu matendo yao yanaendana na mavazi yao..

Isaya 3:16 “Bwana akasema tena, Kwa sababu binti za Sayuni wana kiburi, na kuenenda na shingo zilizonyoshwa, na macho ya kutamani, wakienenda kwa hatua za madaha, na kuliza njuga kwa miguu yao;

17 Basi, kwa hiyo, Bwana atawapiga binti za Sayuni kwa pele za utosini, na Bwana ataifunua aibu yao”.

18 Siku hiyo Bwana atawaondolea uzuri wa njuga zao, na kaya zao;

19 na pete za masikio, na vikuku, na taji zao;

20 na dusumali, na mafurungu, na vitambi, na vibweta vya marashi, na matalasimu;

21 na pete, na azama”

Biblia inasema miili yetu ni HEKALU LA ROHO MTAKATIFU. Na si Nyumba tu!..bali hekalu (1Wakorintho 6:19)..Kama ni hekalu maana yake halipaswi kuvikwa hirizi, halipaswi kuvikwa vitu vya kikahaba.. kwani Mafurungu pamoja na vikuku na hazama, walikuwa wanavaa makahaba..

Kama binti wa kiMungu unapenda kujipamba basi biblia imetoa mwongozo mzuri wa namna ya kujipamba na kupendeza..

1Timetheo 2:9 “Vivyo hivyo wanawake NA WAJIPAMBE KWA MAVAZI YA KUJISITIRI, PAMOJA NA ADABU NZURI, NA MOYO WA KIASI; SI KWA KUSUKA NYWELE, WALA KWA DHAHABU NA LULU, WALA KWA NGUO ZA THAMANI;

10 BALI KWA MATENDO MEMA, KAMA IWAPASAVYO WANAWAKE WANAOUKIRI UCHAJI WA MUNGU”.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

Kikuku/vikuku ni nini katika biblia?

Hazama ni nini katika biblia?(Ezekieli 16:12, Kutoka 24:47)

PINDO LA VAZI LAKE SASA LIMEREFUSHWA.

Ni nani aliyesema Nitume mimi? katika (Isaya 6:8)

Shubaka ni nini kibiblia? (Mithali 7:6)

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya “Kandake” (Matendo 8:27)

SWALI: Tunasoma yule mkushi alikuwa ni mwenye mamlaka chini ya Kandake Malkia wa Kushi.. Naomba kufahamu Neno Kandake lina maana gani?


JIBU: Filipo, Mhubiri wa injili, aliagizwa na Malaika wa Bwana, aende njia ya jangwani (Gaza), Lakini alipokuwa njia kushuka huko alikutana na huyu mkushi ambaye alikuwa ni towashi, ndipo akamuhubiria injili, na siku hiyo hiyo akabatizwa, baada ya hapo Filipo akatoweshwa na Roho Mtakatifu na kupelekwa  sehemu nyingine.

Matendo 8:26 “Malaika wa Bwana akasema na Filipo, akamwambia, Ondoka ukaende upande wa kusini hata njia ile itelemkayo kutoka Yerusalemu kwenda Gaza; nayo ni jangwa.

27  Naye akaondoka, akaenda; mara akamwona mtu wa Kushi, towashi, mwenye mamlaka chini ya Kandake malkia wa Kushi, aliyewekwa juu ya hazina yake yote; naye alikuwa amekwenda Yerusalemu kuabudu”

Lakini biblia inasema huyu mkushi alikuwa ni mwenye mamlaka chini ya Kandake malkia wa Kushi.  Kandake ni jina la Mamalkia wote wa nchi ya Kushi (Kushi ndio nchi ya Ethiopia). Kumbuka sio jina la mtu binafsi bali ni jina la cheo. Kama vile ilivyokuwa kwa Farao, au Kaisari. Kwamba wafalme wote waliitwa Farao, au Kaisari. Ndivyo ilivyokuwa kwa mamalkia wote wa Kushi waliitwa Kandake.

Ndio huyu towashi aliwekwa chini ya umalkia huo ili kuilinda na kuitunza hazina yote ya taifa hilo la Kushi. Na unaweza kujiuliza ni kwanini awe ni towashi?. Ilikuwa ni desturi, kwa falme nyingi za zamani, pindi wanapotaka kuwaweka chini ya mamalkia wao, na chini ya sekta nyeti kama hizo za fedha. Waliwaasi, watumwa hao, ili kusudi kwamba wasivutwe na tamaa za mwili, na pia wasifikirie kuacha utumwa wao, na kujali familia zao( yaani Watoto wao na wake), Zaidi ya maslahi ya nchi. Hivyo hiyo ilikuwa inawafanya wawe wanyenyekevu na wawe makini sana katika kazi walizowekewa chini yao.

Inatufundisha nini?

Hata kuwekwa chini ya kazi maalumu za Mungu ni hivyo hivyo, Kunategemea sana uaminifu wetu. Rohoni tunapaswa tuwe kama matowashi. Tufe kwa Habari za tamaa za ulimwengu. Kiasi kwamba hata ukijaribiwa kwa mali, hali yako ni ile ile, ukijaribiwa kwa uzinzi, hutikisiki, ukijaribiwa kwa umaarufu, unabakia kuwa yule yule, kama Bwana Yesu, hugeuki kuwa nabii wa uongo.

Hapo ndipo Bwana anapopahitaji sote tupafikie, ili atuamini na kutuweka katika kazi zake maalumu. Hivyo Bwana anataka tufanane na matowashi rohoni mwetu. Kama alivyokuwa Ayubu mtumishi wake (Ayubu 31:1, 25)

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

“Vya Kaisari mpeni kaisari”  ni vipi hivyo tunavyopaswa tumpe?

Deraya ni nini? Kama tunavyosoma katika Isaya 59:17

Ninawi ni nchi gani kwasasa?

Nini kinatokea baada ya kifo

GOGU NA MAGOGU, Katika biblia ni nani?

Rudi nyumbani

Print this post

MADHARA YA KUTOIJUA KWELI YOTE!

Kuna madhara makubwa sana ya KUTOIJUA KWELI YOTE!.. Unaweza kuijua kweli tu!, lakini usiijue kweli yote…Watu wengi leo hii wanaijua kweli… “lakini hawaijui kweli yote”.. Jambo ambalo linafungua mlango mkubwa sana wa shetani kuleta Uharibifu.

Hebu tuangalie mfano wa watu wawili ambao waliijua kweli, lakini si YOTE!.

 1. MFALME ABIMELEKI

Ibrahimu, alimwambia Mfalme Abimeleki kuwa Sara ni “Dada yake” ..lakini hakumwambia kuwa Sara pia ni “mke wake”.. alimwambia vile kwa hofu ya kuuawa..kwasababu Sara alikuwa ni mzuri wa uso.

Sasa sio kwamba Ibrahimu alimdanganya Mfalme Abimeleki!.. hapana! Hakumdanganya kwasababu ni kweli Sara alikuwa ni dada Ibrahimu.. Wameshea baba mmoja, ila mama mbali mbali. Kwahiyo alikuwa ni kweli dada yake. Hivyo hakumwambia uongo Mfalme Abimeleki.. Lakini tatizo ni kwamba hakumwambia KWELI yote!.. alimwambia kweli iliyo NUSU tu!.. na matokeo yake ni kumletea Abimeleki hatari ya kuawa na Mungu..

Tusome,

Mwanzo 20:1 “Ibrahimu akaondoka huko kwenda nchi ya kusini, akakaa kati ya Kadeshi na Shuri, naye akatembea katika Gerari.

2 Ibrahimu akamnena Sara mkewe, Huyu ni ndugu yangu. Basi Abimeleki mfalme wa Gerari akapeleka watu akamtwaa Sara.

3 Lakini Mungu akamjia Abimeleki katika ndoto ya usiku, akamwambia, Umekuwa mfu wewe kwa sababu ya mwanamke huyu uliyemtwaa, maana ni mkewe mtu.

4 Basi Abimeleki alikuwa hakumkaribia, akasema, Ee Bwana, Je! Utaua hata taifa lenye haki?

5 Je! Hakuniambia mwenyewe, Huyu ni ndugu yangu? Na mwanamke mwenyewe naye alisema, Huyu ni ndugu yangu. Kwa ukamilifu wa moyo wangu, na kwa kuwa safi mikono yangu, nimefanya hivi.

6 Mungu akamwambia katika ndoto, Nami nimejua ya kwamba kwa ukamilifu wa moyo wako umefanya hivi, ndipo nami nikakuzuia usinitendee dhambi, kwa hiyo sikukuacha umguse.

7 Basi sasa umrudishe mwanamke kwa mtu huyo, maana yeye ni nabii, naye atakuombea, upate kuishi. Bali usipomrudisha, fahamu ya kwamba kwa hakika utakufa wewe na watu wote ulio nao.

8 Abimeleki akaamka asubuhi na mapema, akawaita watumwa wake wote, akawaambia maneno hayo yote masikioni mwao, nao watu hao wakaogopa sana.

9 Kisha Abimeleki akamwita Ibrahimu, akamwambia, Umetutenda nini? Nimekukosa nini, hata ukaleta juu yangu na juu ya ufalme wangu dhambi kuu? Umenitenda matendo yasiyotendeka.

10 Abimeleki akamwambia Ibrahimu, Umeona nini hata ukatenda jambo hili?

11 Ibrahimu akasema, Kwa sababu naliona, Yakini hapana hofu ya Mungu mahali hapa, nao wataniua kwa ajili ya mke wangu.

12 NAYE KWELI NI NDUGU YANGU, BINTI WA BABA YANGU ILA SIYE MWANA WA MAMA YANGU, NDIPO AKAWA MKE WANGU”.

Umeona hapo mstari wa 12?.. “Ibrahimu hakusema uongo, alisema Kweli lakini si yote”

 2. HAWA

Hawa aliambiwa ukweli na shetani, lakini hakuambiwa ukweli wote!.. Aliambiwa kwa kula tunda, “Atakuwa kama Mungu, akijua mema na mabaya”..huo ni ukweli kabisa! Kwani alipokula tu lile tunda, alikuwa kama Mungu kwa kujua mema na mabaya…

Mwanzo 3:22 “Bwana Mungu akasema, Basi, huyu mtu amekuwa kama mmoja wetu, kwa kujua mema na mabaya; na sasa asije akanyosha mkono wake akatwaa matunda ya mti wa uzima, akala, akaishi milele”

Lakini shetani hakumwambia ukweli wote kwamba, licha ya kuwa utakuwa kama Mungu akijua mema na mabaya lakini Zaidi ya hayo, atakuwa pia amejitenga mbali na uwepo wa MUNGU, na umemuasi Mungu moja kwa moja. (Hayo hakumwambia)..kwasababu laiti angemwambia Hiyo kweli yote!, Hawa asingelisogelea lile tunda!.

Umeona Madhara ya kutoijua kweli yote?..

Yalimletea Mfalme Abimeleki hatari ya kifo, kwa kumtwaa Sara.. vile vile, yalimletea Hawa anguko kubwa ambalo mpaka leo tunaona madhara yake.

Vile vile shetani leo hii, anawaambia watu ukweli, lakini hawaambii kweli yote!..na watu wanajitumainisha katika ile kweli, lakini hawataki kuitafuta kweli yote..

Kwamfano Neno linasema, kila amwaminiye Bwana Yesu amevuka kutoka mautini kuingia uzimani..

Yohana 5:24 “Amin, amin, nawaambia, Yeye alisikiaye neno langu na kumwamini yeye aliyenipeleka yuna uzima wa milele; wala haingii hukumuni, bali amepita kutoka mautini kuingia uzimani”.

Hiyo ni KWELI KABISA!..Lakini kweli yote inasema hatuna budi kubatizwa na kupokea Roho Mtakatifu na kuishi Maisha matakatifu baada ya hapo..

Mathayo 16:16 “Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa”.

Maana yake hatuishii kumwamini Bwana Yesu tu!, halafu basi..bali tunapaswa pia tubatizwe!..Na pia haiishii kubatizwa tu..bali pia tunapaswa tujazwe Roho Mtakatifu na tuishi Maisha matakatifu baada ya hapo ndipo tutakapomwona Mungu..

Waebrania 12:14 “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, NA HUO UTAKATIFU, AMBAO HAPANA MTU ATAKAYEMWONA BWANA ASIPOKUWA NAO”.

Na sio tu katika eneo la wokovu tunahitaji kuijua kweli yote, bali katika mambo mengine yote!.. leo hii watu wanaamini kuwa Mungu anaangalia moyo!..Hiyo ni kweli, lakini SI KWELI YOTE!.. Kweli yote inasema..

Warumi 12:1 “Basi, ndugu zangu, nawasihi, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, ya kumpendeza Mungu, ndiyo ibada yenu yenye maana”.

Na tena inasema..

1Wakorintho 6:19 “Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu? Wala ninyi si mali yenu wenyewe”

Kwahiyo hatupaswi miili yetu, kuivika vibaya, hatupaswi kuichora, kuitoboa toboa, kuilevya, au kuiharibu kwa namna yoyote ile.(www wingulamashahidi org)

Sasa swali la kujiuliza?..Utawezaje kuijua KWELI yote!.

Ashukuriwe Mungu, kwa zawadi ya Roho aliyotumwagia.. huyo ndio suluhisho la mambo yote..

Yohana 16:13 “Lakini yeye atakapokuja, HUYO ROHO WA KWELI, ATAWAONGOZA AWATIE KWENYE KWELI YOTE; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe…”

Je! Leo unataka kuyajua mapenzi ya Mungu, katika ukamilifu wote?..unataka kuijua kweli yote ya Maisha yako ya kiroho na kimwili?..Basi tafuta Roho Mtakatifu…sasa utauliza, utampataje Roho Mtakatifu ndani yako?..Biblia imetupa kanuni..kuwa ni kwa kutubu, na kubatizwa..

Matendo 2:37 “Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?

38 PETRO AKAWAAMBIA, TUBUNI MKABATIZWE KILA MMOJA KWA JINA LAKE YESU KRISTO, MPATE ONDOLEO LA DHAMBI ZENU, NANYI MTAPOKEA KIPAWA CHA ROHO MTAKATIFU.

39 Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie”.

Bwana akubariki

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

Ni madhara gani yatampata mtu yule anayetafsiri Neno isivyopaswa!

NINI KINATOKEA BAADA YA KIFO?

NINI KINATOKEA BAADA YA KIFO?

Kama wakitenda mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu?

MUUNGANO WA DINI NA MADHEHEBU YOTE, UMEKARIBIA.

Rudi nyumbani

Print this post

“Vya Kaisari mpeni kaisari”  ni vipi hivyo tunavyopaswa tumpe?.

Na pombe na sigara si ni vya Kaisari (yaani serikali imevihalalisha), hivyo si ni sawa kuvitumia..?

Jibu: Kumekuwa na tafsiri nyingi juu ya huo mstari “Vya Kaisari mpeni Kaisari na vya Mungu mpeni Mungu”… Wengine wanatafsiri vya Kaisari kama vitu vyote viovu vya ulimwengu.. Hivyo tumepewa ruhusa ya kuvifanya hivyo, lakini pia tusiache kuvifanya vya Mungu.. “Kwamba tunapoenda disko hapo tumempa Kaisari vya kwake, vile vile tunapoenda kanisa, hapo tumempa Mungu vya kwake”..

Lakini je! Hiyo ndio tafsiri yake au ndio maana ya huo mstari?

Tusome..

Luka 20:21 “Wakamwuliza, wakisema, Mwalimu, twajua ya kwamba wasema na kufundisha yaliyo ya haki, wala hujali cheo cha mtu, bali unafundisha njia ya Mungu kwa kweli

22 JE! NI HALALI TUMPE KAISARI KODI, AU SIVYO?

23 Lakini yeye alitambua hila yao, akawaambia,

24 Nionyesheni dinari. Ina sura na anwani ya nani? Wakamjibu, Ya Kaisari.

25 Akawaambia, Basi, vya Kaisari mpeni Kaisari, na vya Mungu mpeni Mungu”.

Hapo utaona Vya Kaisari Bwana alivyovimaanisha ni “KODI” na mambo yote yanayofanana na hayo..(Kwa ufupi mambo yote mema)..kama Ushuru, uwajibikaji, utulivu, amani n.k

Ndio maana Bwana akawauliza swali, sarafu hiyo ina sura ya nani?..wakajibu ya Kaisari..na ndipo akajibu vya Kaisari mpeni Kaisari..Maana yake vile vyote Kaisari anavyovihimiza na kuvihitaji vya lazima  “basi apewe” kwasababu havihitaji kwa lengo baya!!.. bali zuri kwa watu wake!.

Kama maandiko yanavyosema katika…

1Wakorintho 13:3 “KWA MAANA WATAWALAO HAWATISHI WATU KWA SABABU YA MATENDO MEMA, bali kwa sababu ya matendo mabaya. Basi, wataka usimwogope mwenye mamlaka? FANYA MEMA, NAWE UTAPATA SIFA KWAKE;

4 kwa kuwa yeye ni MTUMISHI WA MUNGU KWAKO KWA AJILI YA MEMA…”

Umeona hapo?.. maandiko yanasema watawalao ni watumishi wa Mungu kwako KWA AJILI YA MEMA!!…Kwahiyo yote ya lazima ambayo Kaisari aliyahitaji kutoka kwa watu, ni mambo MEMA na si Mabaya!!

Sasa mambo hayo ni yapi?..ambayo Kaisari aliyahitaji na ambayo ni lazima “apewe”?

 1. KODI

Kaisari alihitaji “kodi” na lengo la kodi, sote tunajua kuwa sio Baya!….kwasababu kodi hazitumiki kwenda kumnufaisha yeye, bali kuwanufaisha wananchi wote, kwa kutengeneza miundo mbinu ya msingi, na matumizi mengine muhimu.. Hivyo Taifa lisilokusanya kodi haliwezi kuendelea.. Kwahiyo Kodi ni jambo ambalo halikinzani na Neno la Mungu..Ndio maana Bwana Yesu akaamuru tuwape kodi wenye mamlaka.

1Wakorintho 13:6 “KWA SABABU HIYO TENA MWALIPA KODI; KWA KUWA WAO NI WAHUDUMU WA MUNGU, WAKIDUMU KATIKA KAZI IYO HIYO.

7 Wapeni wote haki zao; mtu wa kodi, kodi; mtu wa ushuru, ushuru; astahiliye hofu, hofu; astahiliye heshima, heshima”.

 2. AMANI na UTULIVU.

Kaisari, alihubiri “Amani na utulivu”…kwasababu watu wakiwa watulivu, Ufalme wake utajengeka… hivyo hakuhitaji wauaji, hakuhitaji waasi, hakuhitaji watu wenye vurugu, hakuhitaji wezi, hakuhitaji wahuni n.k.

Hivyo mtu akiwa muuaji, (alikuwa hajampa Kaisari yaliyo yake)…kwasababu yeye alikuwa anahitaji watu walio wazuri (na ilikuwa ni amri sio ombi)…Ilikuwa si ruhusa kuua mtu, wala kujichukulia sheria mkononi n.k”.

Na mambo mengine yote ya lazima, (kumbuka yapo mambo ya lazima ambayo wenye mamlaka waliyaagiza na yapo yasiyo ya lazima).. Hakuna Mfalme anayewalazimisha watu wake wanywe pombe!..lakini atawalazimisha wawe na Amani na Utulivu na vile vile walipe kodi. Sasa mambo hayo ambayo ni ya Lazima, MENGI NI MAZURI!!.. Ndio maana Bwana aliamuru tuyafanye hayo.

Vile vile hata sasa… tunapaswa tunayo amri ya kumpa Kaisari yaliyo yake!.. (Tunapaswa tulipe kodi, au ushuru pale inapotubidi)..hali kadhalika sheria za nchi zinatulazimisha kuwa watulivu, watu wa amani na watiifu, na watu wa Staha..hatuna budi kuwa hivyo..(Na kwa kufanya hivyo tutakuwa tumempa Kaisari yaliyo yake)..Kwasababu mambo hayo hayakinzani na Neno la Mungu.

Lakini swali ni je!.. Kama vya Kaisari ni Kodi, ushuru, na mambo mengine yanayofanana na hayo, je ya Mungu nayo ni yapi?..Ambayo Bwana Yesu alisema tumpe!. (..Akawaambia, Basi, vya Kaisari mpeni Kaisari, NA VYA MUNGU MPENI MUNGU..”.

Tusome,

Mathayo 9:13 “Lakini nendeni, mkajifunze maana yake maneno haya, NATAKA REHEMA, WALA SI SADAKA; kwa maana sikuja kuwaita wenye haki, bali wenye dhambi”.

Bwana anahitaji tumwombe yeye Rehema, (anahitaji tutubu)!.. Hicho ndio kitu cha kwanza anachokihitaji kutoka kwetu..na wala si sadaka zetu!!.. Sasa sio kwamba sadaka zetu hazina maana kwake la!.. zina maana kubwa sana, lakini kinachotangulia ni Rehema..

Tusome,

Mathayo 23:23 “Ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnalipa zaka za mnanaa na bizari na jira, lakini mmeacha mambo makuu ya sheria, yaani, adili, NA REHEMA, na imani; hayo imewapasa kuyafanya, WALA YALE MENGINE MSIYAACHE”.

Umeona hapo?..sadaka tunapaswa kumpa Bwana, lakini REHEMA ni muhimu Zaidi.. Toba ni muhimu sana…

Na toba halisi ni ile inayoendana na matendo.. Maana yake tunatubu, kwa kumaanisha kuziacha dhambi!.. Hicho ndicho Mungu anachokihitaji kwetu.. Hali kadhalika hata baada ya kutubu, na kukaa katika Imani, hatuna budi kuendelea kujitakasa kila siku, kwa Neno la Mungu..(Hayo ndio mambo ambayo Mungu anayataka kutoka kwetu).

Je umeokoka?.. Umetubu dhambi zako kwa kumaanisha kuziacha, na kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Bwana Yesu Kristo?, na kupokea Roho Mtakatifu?…Na hata kama umeshaokoka.. je unajitakasa kila siku kwa Neno la Mungu??

Kama bado basi bado hujaanza kuyafanya mapenzi ya Mungu, haijalishi unatoa sadaka kiasi gani?.. Sicho kitu cha kwanza Mungu anachokihitaji kutoka kwako, bali anahitaji wewe upate Rehema kutoka kwake kwa kutubu.

Hivyo kama leo hii ungependa kutubu na kumkaribia Mungu Zaidi.. basi unaweza kuwasiliana nasi kwa namba (katika mwisho wa somo), ili tuweze kukuongoza sala fupi ya Toba..ambayo itamkaribisha Bwana Yesu katika Maisha yako.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

Vyombo vya uzuri ni vipi vinavyotajwa katika biblia?

YANAYOENDELEA SASA KATIKA MADHABAHU YA MUNGU ROHONI.

Bahari mbalimbali zilizoorodheshwa kwenye biblia.

Mizimu ni nini?

UFUNUO: Mlango wa 3 part 3

Rudi nyumbani

Print this post

JE MGOGORO WA URUSI NA UKRAINE,UMETABIRIWA KIBIBLIA?

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze biblia.

Leo tutajifunza juu ya mgogoro wa Urusi na Ukraine, Je Mgogoro huu umetabiriwa katika biblia?

Awali ya yote, kabla hatujaendelea mbele, tusome kwanza mstari ufuatao..

Mathayo 24:6 “NANYI MTASIKIA HABARI ZA VITA NA MATETESI YA VITA; angalieni, msitishwe; maana hayo hayana budi kutukia; lakini ule mwisho bado.

7 Kwa maana taifa litaondoka kupigana na taifa, na ufalme kupigana na ufalme; kutakuwa na njaa, na matetemeko ya nchi mahali mahali.

8 Hayo yote ndiyo mwanzo wa utungu”.

Hapo anasema, kutatokea na tetesi za vita lakini “ule mwisho bado”.

Kwahiyo “Tetesi hizi za vita”…ndio Mwanzo wa Utungu tu!..(Maana yake ndio tumeukaribia ule mwisho)..Lakini mwisho wenyewe bado haujafika..(Unyakuo bado haujapita, lakini ndio upo karibuni kutokea).

Sasa tukirudi kwenye swali, je Mgogoro wa Urusi na Ukraine, ni wapi umetabiriwa katika biblia?

Mgogoro wa Urusi na Ukraine, haujatabiriwa popote katika biblia, kama vile vita vya Maji-Maji na Mau-Mau, jinsi ambavyo havikutabiriwa katika biblia, ndivyo hivyo hivyo Urusi na Ukraine, biblia isingeweza kuandika kila kitu!.

Lakini mgogoro huu, UNAFUNGUA NJIA kwaajili ya vita kuu iliyo karibuni kutokea kipindi si kirefu kati ya URUSI na TAIFA LA ISRAELI.. Vita kati ya Urusi na Israeli ndiyo iliyotabiriwa katika biblia (Ambayo vita hiyo tunaisoma katika kitabu cha Ezekieli 38 na 39).

Vita hii ipo karibu sana kupiganwa.. Ambapo Taifa la Urusi, (Gogu na Magogu) Kwa kiburi chake litaingia katika mgogoro na Taifa la Israeli, na mataifa ya kiarabu, yaliyo na uadui na Taifa la Israeli yataungana na Urusi kupanga kuiondoa katika ramani ya dunia.. Lakini siku hiyo maandiko yanasema..Mungu atatokea na kuwapigania Israeli, kama alivyowapigania zamani..

Mataifa yanayotajwa kushirikiana na Urusi katika vita hiyo ni Irani, Libya, Uturuki, Palestina, Jordani na mataifa ya kando kando ya Israeli. Biblia haijatoa sababu ya Urusi kutaka kuivamia Israeli ni ipi, lakini litazuka jambo tu ambalo litayapeleka mataifa hayo mawili katika vita hivyo.

Na lengo la Mungu kuruhusu vita hivyo ni kulifuta Taifa la Urusi, lililonyanyuka moyo wake, hali kadhalika kuyaondoa baadhi ya Mataifa ya kiarabu yanayoiilaani Israeli. Na Ijapokuwa Urusi ni Taifa kubwa, na lenye nguvu kiuchumi na kijeshi, lakini siku hiyo Bwana ataligeuza kuwa vumbi, kutakuwa hakuna tena Taifa la Urusi duniani!.

Ezekieli 38:14 “Basi, mwanadamu, tabiri, umwambie Gogu, Bwana MUNGU asema hivi; Katika siku ile watu wangu, Israeli, watakapokaa salama, hutapata habari?

15 NAWE UTAKUJA KUTOKA MAHALI PAKO, KUTOKA PANDE ZA MWISHO ZA KASKAZINI, WEWE, NA WATU WA KABILA NYINGI PAMOJA NAWE, WOTE WAMEPANDA FARASI, KUSANYIKO KUBWA, NA JESHI KUU;

16 nawe utapanda juu uwajilie watu wangu, Israeli, kama wingu kuifunika nchi; itakuwa katika siku za mwisho, nitakuleta upigane na nchi yangu, ili mataifa wanijue, nitakapotakaswa kwako, Ewe Gogu, mbele ya macho yao.

17 Bwana MUNGU asema hivi; Je! Wewe ndiwe niliyemnena zamani za kale, kwa vinywa vya watumishi wangu, manabii wa Israeli, waliotabiri siku zile kwa muda wa miaka mingi, ya kwamba nitakuleta upigane nao?

18 ITAKUWA KATIKA SIKU HIYO, GOGU ATAKAPOKUJA KUPIGANA NA NCHI YA ISRAELI, ASEMA BWANA MUNGU, GHADHABU YANGU ITAPANDA KATIKA MIANZI YA PUA YANGU.

19 Kwa maana katika wivu wangu, na katika moto wa ghadhabu yangu, nimenena, Hakika katika siku ile kutakuwako tetemeko kubwa katika nchi ya Israeli;

20 hata samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama wa kondeni, na vitu vyote vitambaavyo juu ya nchi, na wanadamu wote walio juu ya uso wa nchi, watatetemeka mbele ya uso wangu; nayo milima itatupwa chini, na magenge yataanguka, na kila ukuta utaanguka chini.

21 Nami nitaita upanga, uje juu yake katika milima yangu yote, asema Bwana MUNGU; nao upanga wa kila mtu utakuwa juu ya ndugu yake.

22 Nami nitamhukumu kwa tauni, na kwa damu; nami nitanyesha mvua ifurikayo, na mvua ya mawe makubwa sana, na moto na kiberiti juu yake, na vikosi vyake, na watu wa kabila nyingi walio pamoja naye.

23 Nami nitajitukuza, na kujitakasa, na kujidhihirisha, mbele ya macho ya mataifa mengi; nao watajua ya kuwa mimi ndimi Bwana”.

Katika vita hiyo maandiko yanasema Mizoga ya watu watakaouawa, itakusanywa kwa kipindi cha miezi 7, (Mizoga itazagaa kila mahali). Warusi wengi watakufa ndani ya ardhi ya Israeli, na dunia nzima itamwogopa Mungu wa Israeli..

Ezekieli 39:11 “Tena, itakuwa katika siku hiyo, nitampa Gogu pa kuzikia katika Israeli, bonde la wapitao, upande wa mashariki wa bahari; nalo litawazuia wapitao; na huko watamzika Gogu na watu wake jamii yote; nao wataliita, Bonde la Hamon-Gogu.

12 NA KWA MUDA WA MIEZI SABA nyumba ya Israeli watakuwa wakiwazika, wapate kuisafisha nchi.

13 Naam, watu wote wa nchi hiyo watawazika; itakuwa ni sifa kwao katika siku ile nitakapotukuzwa, asema Bwana MUNGU.

14 Nao watawachagua watu wa kufanya kazi ya daima, watakaopita kati ya nchi, ili kuwazika waliosalia juu ya uso wa nchi, ili kuisafisha; miezi saba itakapokwisha kupita watatafuta.

15 Na hao wapitao kati ya nchi watatafuta; na mtu ye yote aonapo mfupa wa mtu, ndipo atakapoweka alama karibu nao, hata wazishi watakapouzika katika bonde la Hamon- Gogu.

16 Tena, Hamona litakuwa jina la mji. Hivyo ndivyo watakavyosafisha nchi”.

JE VITA HII YA URUSI NA UKRAINE NI NINI INAONGEZA KWA URUSI?

Vita hii, inaiongezea Urusi Ujasiri, na kuiaminisha kuwa inaweza kufanya jambo Fulani la kuisumbua dunia. Ujasiri huo unaongeza kiburi chake dhidi ya Mungu, na unaandaa mazingira ya kuishukia Israeli, kama vile Mfalme wa Ashuru, (Senakeribu) alivyojiongezea Ujasiri hata kupanga kuishukia Yuda, huku akimtukana Mungu wa Israeli..kwasababu tu aliyashinda mataifa mengine yote yaliyomzunguka, hivyo akalidharau Taifa dogo la Yuda, na hata kufikia hatua ya kumtukana Mungu wa Israeli

Lakini Mungu alikishusha kiburi chake kwa kuliangamiza jeshi lake lote pasipo kupigana vita, vile vile na kwa kumuua yeye mwenyewe. (2Wafalme 19:1-37). Ndicho kitakachotokea kwa Taifa la Urusi, litalidharau Taifa la Israeli na kumbe ndio litakuwa limejipeleka kwenye mwisho wake.

Vita hiyo ya Urusi na Israeli, ipo karibuni sana kutokea, ghafla tu, litanyanyuka kama lilivyoanza kwa Ukraine, na kupanga kuivamia Israeli, na wakati huo huo mataifa ya kiarabu yataungana..Baada ya hapo dunia itakuwa imebakisha vita moja ya Harmagedon, (ya Mungu mwenyezi na mataifa yote ya dunia yaliyosalia).

Na unyakuo wa kanisa unaweza kutokea kipindi kifupi kabla ya vita hii, au kipindi kifupi baada ya vita hiyo (ya Urusi na Israeli), kutokea..

Lakini yote katika yote ni kwamba tunaishi katika siku za Mwisho, na Yesu yupo mlangoni kurudi, kuwachukua watakatifu wake. Je umejiandaaje?

Umempokea Bwana Yesu?, umebatizwa?, umepokea Roho Mtakatifu?.. kama bado unangoja nini leo hii usiokoke.. Au unasubiri siku ile ya hukumu ya Mungu ikujie kwa ghafla?

1Wathesalonike 5:3 “Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa”.

Kama leo hii umeamua kuanza Maisha ya wokovu, kwa kumpokea Bwana Yesu Maishani mwako, basi unaweza kuwasiliana nasi kwa namba hizi hapa chini, ili tukuongoze sala ya Toba, itakayomkaribisha Yesu ndani yako.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

JE NI KWELI SAMAKI NGUVA YUPO?

NAYE AKASIMAMA JUU YA MCHANGA WA BAHARI.

Chuo cha vita vya Bwana ni kipi?(Hesabu 21:14)

MAUAJI YA HALAIKI NDANI YA KANISA.

MAISHA ULIYOPITIA NYUMA NI USHUHUDA TOSHA WA WEWE KUMTUMIKIA MUNGU

Rudi nyumbani

Print this post

Watu wenye ulemavu wa akili, wataenda mbinguni?

Jibu: Hapana!, watu wenye ulemavu wa akili kikweli kweli, Bwana akirudi hawataenda!, watabaki kukumbana na ghadhabu ya Mungu.!.

LAKINI SISI TUNAVYOMTAFSIRI MTU MWENYE ULEMAVU WA AKILI, NI TOFAUTI NA MUNGU ANAVYOMTAFSIRI.

Sisi tunamtafsiri mtu mwenye ulemavu wa akili ni yule tunayemwona haeleweki anapozungumza, anatokwa na mate mdomoni, na hawezi kujimudu mwenyewe!..na mtu aliye na akili timamu ni yule, tunayemwona anaoga vizuri na kuwa nadhifu na mwenye utashi wa kidunia! Anayekubalika kila mahali.. lakini kwa Mungu sivyo.

1Wakorintho 3:18 “Mtu asijidanganye mwenyewe; kama mtu akijiona kuwa mwenye hekima miongoni mwenu katika dunia hii, na awe mpumbavu, ili apate kuwa mwenye hekima.

19 MAANA HEKIMA YA DUNIA HII NI UPUZI MBELE ZA MUNGU. KWA MAANA IMEANDIKWA, YEYE NDIYE AWANASAYE WENYE HEKIMA KATIKA HILA YAO”.

Sasa mtu mwenye MATATIZO YA AKILI, kibiblia ni yupi?

Tusome, mistari ifuatayo ili tuweze kujua “Mlemavu wa akili ni yupi mbele za Mungu”.

 1. MTU MZINIFU.

Mithali 6:32 “Mtu aziniye na mwanamke HANA AKILI KABISA; Afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake”.

Wakati unaona mtu anayedondosha mate, kama hana akili, kumbe Mungu anakuona wewe unayezini kuwa HUNA AKILI KABISA!.. Tena hasemi “huna akili” tu!..bali anamalizia na neno “kabisa”. Kwahiyo kumbe mtu anayezini ni Tahira!, mbele za Mungu… ni heri uwe unashindwa kuyamudu mate yako kuliko kuwa mzinifu.

 2. MTU ANAYEDHARAU WENGINE.

Mithali 11:12 “ASIYE NA AKILI HUMDHARAU MWENZIWE; Bali mtu aliye na ufahamu hunyamaza”.

Kama unamdharau huyo  unayemwona hawezi kuongea kama wewe, au hawezi kupambanua kama wewe, au hana heshima kama yako, au uwezo kama wako.. basi tambua kuwa mbele za MUNGU, Wewe ndio HUNA AKILI (Una matatizo ya akili) kuliko huyo unayemdharau.

1Wakorintho 3:18 “Mtu asijidanganye mwenyewe; kama mtu akijiona kuwa mwenye hekima miongoni mwenu katika dunia hii, na awe mpumbavu, ili apate kuwa mwenye hekima.”

 3. MTU ANAYEWAONEA WENGINE!

Mithali 28:16 “Mkuu ALIYEPUNGUKIWA NA AKILI HUWAONEA WATU SANA; Bali achukiaye kutamani ataongeza siku”

Ikiwa una cheo Fulani, au wewe ni mkubwa kicheo au kiumri, katikati ya watu, na hutendi haki bali unawaonea wengine, basi fahamu kuwa mbele za Mungu, unayo matatizo ya akili, haijalishi dunia nzima inakuona una akili, mbele za Mungu unao ulemavu wa akili.

Kwaufupi kuishi Maisha ya dhambi na ya kutomtafuta Mungu, na huku unajua kabisa kuwa unapaswa umtafute Mungu, HUKO NI KUKOSA AKILI.

Zaburi 14:2 “Toka mbinguni Bwana aliwachungulia wanadamu, Aone kama yuko mtu mwenye akili, Amtafutaye Mungu”.

Kwahiyo, kwa hitimisho ni kwamba “wale tunaowaona sisi ni walemavu wa akili, waliopo mahospitalini”..Mungu hawaoni hivyo!.. Na Bwana anateta nao!, kwa namna yao, na watahukumiwa kwa namna yao!..Wewe huwezi kuongea nao, lakini Bwana anaweza kuongea nao, kwasababu yeye ndio aliyewaumba…

Wewe huwezi kuwaelewa lakini Bwana anawaelewa, kwasababu ni yeye ndiye kawaumba..hawezi kukiumba kitu ambacho kitamshinda yeye kukielewa.

Wewe huwezi kuona kama wanamwabudu Mungu, au wanamtukuza Mungu, au wana dhambi lakini Mungu ndiye anayewajua mienendo yao…

Hivyo kwasababu Bwana ndiye anayewajua na ndiye atakayewahukumu, wapo watakaoingia mbinguni, na wapo ambao hawataingia.. (Wanadamu wote siku za mwisho watasimama mbele ya kiti cha hukumu).

Lakini sisi tunaojiona tuna akili timamu, huku tunazini, au tunafanya dhambi, huku tunatembea nusu-tupu barabarani, huku tunapaka rangi nyuso zetu, huku tunajichora Ngozi zetu, huku tunaabudu sanamu!..tujue mbele zake Mungu ni “walemavu wa akili” , haijalishi dunia nzima itatuthaminisha kiasi gani, basi mbele zake ni “walemavu wa akili”. Hivyo ili tuwe na akili hatuna budi kumtafuta Mungu, kwa kumwamini Bwana Yesu na kuyashika maneno yake.

Mathayo 7:24 “Basi kila asikiaye hayo maneno yangu, na kuyafanya, atafananishwa na mtu mwenye akili, aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba;

25 mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, isianguke; kwa maana misingi yake imewekwa juu ya mwamba”.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

Nini maana ya “Nitaomba kwa roho, tena nitaomba kwa akili pia?

CHAPA YA MNYAMA

Wibari ni nani?(Mithali 30:26)

INJILI YA MANENO LAINI ITAKUGHARIMU.

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 3

Rudi nyumbani

Print this post

AKAJIFUNGA VAZI LAKE, AKAJITUPA BAHARINI.

Bwana Yesu asifiwe.

Ulishawahi kulitafakari kwa ukaribu lile tukio, ambalo Bwana Yesu aliwatokea wanafunzi wake kwa sura nyingine, walipokuwa baharini wanavua?. Utaona muda wote aliokuwa anazungumza nao wasimtambue Petro alikuwa uchi, Lakini Yohana alipomtambua, kuwa ni Bwana Yesu yupo katikati yao, moja kwa moja alimwambia Petro ufunuo huo.

Na tukio lililofuata pale, utaona Petro hakwenda kumkumbatia, au kumsalimia, au kumsujudia..Bali, tukio la kwanza alilolifanya ni kuificha aibu yake mbele za Bwana. Ndio maana muda ule ule akavaa nguo zake, na akaona hilo halitoshi akajitupa kabisa baharini, kujisitiri,

Yohana 21:5 “Basi Yesu akawaambia, Wanangu, mna kitoweo? Wakamjibu, La.

6 Akawaambia, Litupeni jarife upande wa kuume wa chombo, nanyi mtapata. Basi wakatupa; wala sasa hawakuweza kulivuta tena kwa sababu ya wingi wa samaki.

7 Basi yule mwanafunzi ambaye Yesu alimpenda akamwambia Petro, Ndiye Bwana. Naye Simoni Petro, aliposikia ya kwamba ni Bwana, akajifunga vazi lake, (maana alikuwa uchi), akajitupa baharini.

Hiyo ni kutufundisha nini? Kuwa Bwana anapenda heshima, hapendezwi na watu wasiojiheshimu miili yao, pale wanaposimama mbele yake. Petro ni mwanaume, anasimama mbele ya mwanaume mwenzake, lakini anaona aibu kukaa uchi..

Jiulize wewe mwanamke, ambaye, unajisikia amani, kuvaa vimini, Una Roho Mtakatifu kweli? Na kibaya Zaidi unamfuata Yesu kanisani, unajifanya kumlilia, na kumwimbia na mavazi ambayo huwezi kwenda nayo hata kwa wazazi wako!!. Huoni kama unamvunjia Kristo heshima?

Unajisikiaje, unapovaa suruali kama mwanaume halafu unakwenda kumwabudu Kristo?. Unavaa nguo za migongo wazi, unatembea barabarani, halafu unasema umeokoka, kivipi? Wewe sio mtumwa wa Kristo,  kwasababu watumwa wa Kristo, kama Petro huwa wanaona aibu kukaa uchi, mpaka wanajitupa baharini.

Embu kachome hizo nguo, kuonyesha kweli unamuheshimu Kristo, vaa mavazi ya kujisitiri ya kike, kwani unapunguka nini Ukivaa sketi ndefu au gauni, dada utaumwa? Sasa kwanini ufunue mapaja yako barabarani, kila mtu ayatazame?

Petro alipokwisha kujisitiri, ndipo utaona Bwana Yesu anazungumza naye, lugha ya kiutumishi.. Anamwambia Petro wanipenda? Anasema ndio, Bwana anaendelea kumwambia Chunga, kondoo wangu!, Lisha kondoo zangu!. Lakini hapo kabla hakuzungumza naye lugha kama hizo kwasababu, alikuwa uchi mbele zake.

Jitose baharini dada, Ona aibu, kuwa tayari kuacha mavazi ya kikahaba, achana na fasheni, Onekana mshamba mbele za watu, lakini kwa Kristo mwerevu. Hakuna namna vimini na suruali vitakusogeza kwa Kristo, hakuna namna dada!, ni lazima uukimbie ulimwengu tu.

1Yohana 2:15 “Msiipende dunia, wala mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake”.

Injili za manabii wa uongo zinazokuambia Mungu anaangalia roho, haangalii mwili, jiangalie sana, kama ni hivyo  basi hata hiyo afya na rizki unazomuomba kila siku hana haja ya kukupa kwasababu haangalii mwili anangalia Roho yako tu, akupe uzima wa milele.

Ndugu,Vyote Bwana anavijali, isitoshe, hata siku ile ya mwisho, miili yetu pia itaokolewa, haitapotezwa na kutupwa motoni kama watu wanavyodhani, bali itaokolewa kwa kuvikwa miili ya kimbinguni(1Wakorintho 15:53-54). Yaani kwa ufupi hutakwenda mbinguni, kama mwili wako haujakombolewa.

Maandiko kama haya, hayajaandikwa kama stori kutuonyesha jinsi gani Petro anajua kujirusha baharini, na kuvaa nguo, bali ni kutufundisha sisi, tuwejeke sawa, pale tunapotaka kusimama mbele ya Bwana wetu, na mwokozi wetu.

Bwana atujalie kuliona hili.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

UVUVI BORA HAUCHAGUI, CHA KUVUA.

Kwanini wakristo walipomuona Petro akigonga walisema “Ni malaika wake”?

Je suruali ni vazi la kiume tu?

ISHARA ITAKAYONENEWA

Rudi nyumbani

Print this post