Category Archive Home

Nini maana ya “mkilichukia hata vazi lililotiwa uchafu na mwili”?

SWALI: Biblia inamaanisha nini inaposema “mkilichukia hata vazi lililotiwa uchafu na mwili”?(Yuda 1:23)


JIBU: Maneno hayo utayasoma katika vifungu hivi;

 Yuda 1:22 “Wahurumieni wengine walio na shaka,

23 na wengine waokoeni kwa kuwanyakua katika moto; na wengine wahurumieni kwa hofu, MKILICHUKIA HATA VAZI LILILOTIWA UCHAFU NA MWILI.

24 Yeye awezaye kuwalinda ninyi msijikwae, na kuwasimamisha mbele ya utukufu wake bila mawaa katika furaha kuu”;

Kama tunavyosoma vifungu hivyo, vinaeleza wajibu wa kila aliyeokoka katika kuwavuta wengine katika Imani. Mtume Yuda anaeleza yapo makundi mbalimbali ya watu waonaopaswa kuokolewa, lipo kundi la watu  ambalo linapaswa lihurumiwe kwa hofu, yaani lichukuliwe katika uchanga, na utulivu, livutwe kwa upendo wa Mungu tokea mbali, kundi hili ni la watu wote ambao hawamjui Mungu, wanaoishi duniani leo hii. Walevi, wezi, wazinzi, waoabudu sanamu, n.k.

Lakini lipo kundi lingine linalopaswa kuokolewa kwa kunyakuliwa katika moto. Unajua mpaka mtu awe  ndani ya moto, huhitaji kumbembeleza bembeleza, ili kumtoa, unachopaswa kufanya ni kumnyakua  tu atoke kule kwa gharama zozote zile, kwasababu akiendelea kubaki kule muda si mrefu atakufa. wapo watu ambao unaona kabisa wanakwenda kuangamia kwa mienendo yao ya dhambi, wapo wengine unaona kabisa wapo katika dakika za mwisho wamalizie mwendo wao hapa duniani, na bado hawajaokoka, wapo watu ambao wameshakata tamaa kiasi cha kwamba kilichobakia kwao ni kujiua tu siku yoyote, wapo watu ambao wamefungwa katika minyororo na mateso ya ibilisi, wao wenyewe hawawezi tena kufanya chochote juu ya maisha yao , n.k. Sasa watu kama hawa wanapaswa waokolewe kwa nguvu ya ziada. Kwa kuwafungua na kuwaombea sana, na kuwafuatialia kwa ukaribu sana, na wengine kwa kuwahubiria injili ya Jehanamu ili wajue huko wanapoelekea ni wapi, waogope wageuke kabla kifo hakijawakuta..

Sasa katika kazi hiyo yote ya uokoaji, mwandishi anasema.. “mkilichukia hata vazi lililotiwa uchafu na mwili”. Yaani kujilinda nafsi zenu, na nyinyi msije mkachukuliwa katika dhambi zao. Na ndio maana hapo anatumia mfano wa vazi lililotiwa unajisi kwa uchafu. Katika agano la kale vazi lililotiwa unajisi ni vazi lililovaliwa na mtu mwenye ukoma. Ambalo lilikuwa ni rahisi kumuambikaza mtu mwingine ukoma huo endapo atalishika au kulivaa.  Yaani kwa ufupi Nguo zote zilizokuwa zinatiwa unajisi wa aina yoyote ile, uwe ni ule unaotoka mwilini au vyovyote vile uliweza kumtia unajisi hata mtu mwingine asiyestahili endapo tu atazigusa au kuzivaa. (Walawi 21:11, Hesabu 6:6).

Yapo matendo ambayo, ni rahisi kutiwa na watu wengine unajisi kwayo, unapokwenda kumubuhiria mzinzi, hakikisha na wewe huna uzinzi ndani yako, unapokwenda kumuhubiria mlevi hakikisha na wewe vimelea vya ulevi havipo ndani yako, vivyo hivyo na kila mtu unayekwenda kumshuhudia.  Unapaswa ujichunge wewe mwenyewe kwanza. Kwasababu shetani naye anatenda kazi.

Wagalatia 6:1” Ndugu zangu, mtu akighafilika katika kosa lo lote, ninyi mlio wa Roho mrejezeni upya mtu kama huyo kwa roho ya upole, UKIJIANGALIA NAFSI YAKO USIJE UKAJARIBIWA WEWE MWENYEWE”.

Hiyo ndio maana ya kulichukia hata vazi lililotiwa uchafu na mwili.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Swali: Kurushwa upesi kunakozungumziwa katika Danieli 9:21 ndio kupi?

MAMA UNALILIA NINI?

Je mtu anayeua anabeba dhambi zote za yule aliyemuua?

Herode aliliwa na chango, Je, chango ni nini kibiblia?

Rudi nyumbani

Print this post

Swali: Kurushwa upesi kunakozungumziwa katika Danieli 9:21 ndio kupi?

Jibu: Tusome.

Danieli 9:21 “naam, nilipokuwa nikinena katika kuomba, mtu yule, Gabrieli, niliyemwona katika njozi hapo kwanza, akirushwa upesi, alinigusa panapo wakati wa dhabihu ya jioni”.

Kurushwa upesi kunakozungumziwa hapo ni “kuruka kwa haraka” au kwa lugha rahisi zaidi ni “kuruka/kupaa kwa spidi”. Ndege wa angani huruka kwa upesi..Kwa mfano ni rahisi kumsogelea ndege kama njiwa, na akikuona tu, mara ghafla utamwona kapiga mbawa na kupotelea kwenye ukingo wa anga. Hiyo ndiyo maana ya kuruka kwa upesi.

Na Biblia inasema hapo Danieli alimwona Malaika Gabrieli akirushwa kwa upesi na Mungu..  Maana yake alikuwa anamwona katika maono, akija kwa kasi, na akiondoka kwa kasi.

Kumbuka wapo malaika wenye mbawa na wasio na mbawa (maana yake wasioruka)..Gabrieli ni miongoni mwa malaika wenye mbawa, na wa kupeleka ujumbe kwa watu.

Ni kawaida kile kitu kinachopeleka ujumbe kwa haraka sana ni bora kuliko kile kinachopeleka kwa taratibu. Hivyo Gabrieli ni malaika mwenye sifa ya kupeleka ujumbe kwa haraka sana

Malaika Gabrieli ameonekana katika agano la kale na vile vile katika agano jipya. Katika agano la kale, ndio hichi kipindi cha Nabii Danieli alipotumwa ampe ujumbe juu ya mambo yanayokuja.

Na katika Agano jipya alionekana kipindi cha Kuhani Zakaria, Baba yake Yohana Mbatizaji, alipotumwa na Mungu ampe ujumbe kuhusu kuzaliwa kwa Yohana Mbatizaji ambaye atatangulia kumtengenezea Bwana njia (Soma Luka 1:19). Na pia kipindi kifupi baadaya akaja kuonekana tena kwa Bikira Mariamu kumpa ujumbe wa kubeba mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu (Unaweza kusoma Luka 1:26).

Na hata leo Malaika Gabrieli anatumwa kwa watu wengi duniani walio waaminifu kwa Mungu kuwapa jumbe mbalimbali.

Kama utapenda kujua zaidi kuhusu Malaika unaweza kufungua hapa >> Malaika

Je umempokea Kristo?. Yesu anarudi.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

Je! Kuna malaika wangapi mbinguni?

MALAIKA WAPELELEZI WA HUKUMU WANAPITA SASA.

Je! mbinguni kuna malaika wa kike?. Na je! tukifika mbinguni tutafanana wote?

Kwanini Mungu anasema “Afanyaye malaika zake kuwa pepo”?

Rudi nyumbani

Print this post

MAMA UNALILIA NINI?

Leo tutajifunza jinsi gani matatizo yetu yanavyoweza kuweza kutupofusha hata tusiione miujiza yetu.

Kuna wakati Mungu, anakuwa ameshakwisha anza tayari kututendea miujiza, lakini kutokana na kuwa tunayapa sana matatizo yetu uzito mkubwa kuliko yanavyostahili, inatupelekea hata miujiza yenyewe tuiione kama si kitu pale inapoanza kuja.

Embu fikiria wakati Kristo alipokufa na kulazwa pale makaburini, tunaona kuna mambo mengi yalikuwa yanaendelea pale, lakini kikubwa ambacho tunaweza kujifunza leo ni lile tukio la Mariamu Magdalene. Yeye alipofika pale alianza kulia kwa uchungu, akifikiria miujiza yote aliyotendewa na Yesu tangu akiwa duniani, akifikiria jinsi alivyoishi maisha ya haki na upendo usiokuwa na unafiki, wala hakufanya kosa lolote, na leo hii, anaona wamemuua, tena afadhali ingekuwa wamemuua na kumsulubisha tu, na kumwacha, lakini safari  hii wameuiba  mpaka na mwili wake pia, hilo ndio lililomfanya alie sana kwa uchungu, kiasi cha kumfanya ashindwe kuondoka pale aendelee tu kulia,

 Lakini biblia inatuambia muda si muda, akiwa amesimama pale anachungulia ndani ya kaburi ghafla aliwaona malaika wawili, wamekaa, mmoja kichwani pa mahali walipomlazia Yesu na mwingine, miguuni..Lakini wale malaika wawili wakamuuliza swali, Mama unalilia nini?

Yohana  20:11 “Lakini Mariamu alikuwa akisimama karibu na kaburi, nje yake, analia. Basi akilia hivi, aliinama na kuchungulia ndani ya kaburi. 12 Akaona malaika wawili, wenye mavazi meupe, wameketi, mmoja kichwani na mmoja miguuni, hapo ulipolazwa mwili wake Yesu.

13 Nao wakamwambia, Mama, unalilia nini? Akawaambia, Kwa sababu wamemwondoa Bwana wangu, wala mimi sijui walikomweka”.

Fikiria, ule uchungu wa mawazo ulimfanya hata asahau kuwa wale ni malaika wa Mungu, Uchungu wa kuibiwa kwa Bwana kulimfanya hata asifikirie wale watu wawili wenye mavazi yaliyong’aa meupe wametokea wapi muda ule, na wanafanya nini pale..Yeye moja kwa moja anaanza kuzungumza nao kama vile, ni watu wa kawaida anaokutana nao barabarani siku zote.

Kama hilo halitoshi, wakati anaendelea kulia pal, nje, akamwona Tena mtu mwingine anatembea tembea karibu yake,(hakujua kama ndiye Yesu) ndipo Yesu akamuuliza swali lile lile aliloulizwa na wale malaika..Mama unalilia nini?..

Yohana 20:15 “Yesu akamwambia, Mama, unalilia nini? Unamtafuta nani? Naye, huku akidhania ya kuwa ni mtunza bustani, akamwambia, Bwana, ikiwa umemchukua wewe, uniambie ulipomweka, nami nitamwondoa.

16 Yesu akamwambia, Mariamu. Yeye akageuka, akamwambia kwa Kiebrania, Raboni! (Yaani, Mwalimu wangu)”.

Unaona, Yesu alipogeuka na kumshtua MARIAMU!!!..Ndipo akabutuka na kugundua kuwa Yule ni Yesu aliyesimama mbele yake.  Kama asingeshtuliwa, bado angeendelea kukaa katika majonzi yake tu, analia lia ovyo wakati Yesu anazungumza na yeye.

Wakati mwingine matamanio yetu yanakuwa makubwa kupitiliza,  mpaka yanatupofusha tunashindwa  hata kuona miujiza ya Mungu, kama sio kumwona Mungu mwenyewe.

Jambo kama hili utaliona kwa Balaamu pia, wakati ule anataka kwenda kuwalaani Israeli,  alipokuwa njiani, punda wake alifunguliwa kinywa na Mungu, na kuanza kuongea naye.. Sasa yeye kwasababu moyo wake wote tayari ulikuwa kule anapoelekea, kuwalaani Israeli, hata kuzungumza na Punda hakuona kama ni muujiza ule, badala yake akaanza kuzungumza naye kama anavyozungumza na mwanadamu mwenzake tu..Kama alivyofanya Mariamu.

Hesabu 22:28 “Bwana akakifunua kinywa cha yule punda, naye akamwambia Balaamu, Nimekutenda nini, hata ukanipiga mara tatu hizi?

29 Balaamu akamwambia punda; Kwa sababu umenidhihaki; laiti ningekuwa na upanga mkononi mwangu ningekuua sasa hivi.

30 Yule punda akamwambia Balaamu, Je! Mimi si punda wako, nawe umenipanda maisha yako yote hata leo? Nimezoea kukutenda hayo? Akasema, La!

31 Ndipo Bwana akafunua macho ya Balaamu akamwona malaika wa Bwana amesimama njiani, ana upanga mkononi mwake, umekwisha kufutwa naye akainama kichwa, akaanguka kifudifudi”.

Umeona? Pengine na wewe umekuwa ukizitazama sana shida zako, kuliko kuutazama uweza wa Mungu. Pengine ipo miujiza mikubwa Mungu ameshaanza kukufanyia lakini huwezi kuiona kwasababu wakati wote ukienda kwa Mungu unatazama tu ukubwa wa shida zako, na sio uweza wa Mungu.

Unasahau kuwa ni Malaika wa Bwana wamesimama pale pale unapopalilia, unasahau kuwa ni Yesu mwenyewe mkuu wa Uzima, amesimama pembeni yako kuzungumza na wewe na wewe juu ya hilo tatizo lako, lakini wewe unalia tu.. Leo nakuambia tuliza  moyo wako, usilie mahali ambapo tayari Mungu ameshakusikia, bali, mshukuru yeye, zungumza  na yeye, utaona miujiza mingi ambayo tayari ameshaanza kukufanyia katika maisha yako.

Mungu akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

NITAUPATAJE UPENDO WA KI-MUNGU NDANI YANGU?

Sadaka ya kuinuliwa ni sadaka ya namna gani?

YESU MPONYAJI.

NAWE UTAGEUZWA KUWA MTU MWINGINE.

NI SAA KUMI NA MBILI (12) TU, ZA KRISTO KWAKO.

TUMEPEWA AMRI YA KUKANYAGA NGE NA NYOKA.

Rudi nyumbani

Print this post

NITAUPATAJE UPENDO WA KI-MUNGU NDANI YANGU?

Shalom,

Kuna kipindi mitume walimpelekea Bwana hitaji hili;

Luka 17:5 “… Tuongezee imani”.

Kwao pengine hili lilikuwa ni hitaji jepesi sana , lakini kwa upande wa Bwana halikuwa ombi la kuwajibu kwa sentensi mbili, au kwa kuwawekea  mikono tu na kupokea, hapana, na ndio maana baada ya ulizo hilo, hakukuwa na jibu la moja kwa moja kutoka kwa Bwana.

Sehemu nyingine alipoona upungufu wa Imani yao Bwana Yesu aliwaambia , namna hii haiwezi kutoka isipokuwa kwa “kufunga na kuomba”(Mathayo 17:21)  Na sehemu nyingine biblia inasema, Imani huja kwa kukisikia Neno la Mungu(Warumi 10:17).. Ikiwa na maana kuwa kwa jinsi unavyosoma Neno la Mungu, na kuona uweza wa Mungu alioufanya, tangu enzi na enzi, sasa kwa jinsi unavyosoma sana na kusikia Neno lake, ndivyo imani yako inavyojengeka kwake, na hatimaye unakuwa na imani timilifu, hata ya kuweza kuamishi milima kwa jina lake.

Lakini katika yote hayo utagundua kuna kitu kimoja kinachoitwa BIDII ndani yake..Ikiwa na maana imani haiwezi kuja hivi hivi tu kwa kukaa, kama hutakuwa na bidii ya kuitafuta, haitakaa ije kwako kamwe, haiji kwa kuwekewa mikono, wala haiji kwa kuombewa,..

Sasa Imani ni nguzo mojawapo ya Ukristo, zipo nguzo nyingine mbili za Ukristo nazo ni Upendo na Tumaini. Lakini leo hatutazungumzia juu ya Tumaini, bali tutazungumzia juu ya Upendo, ambao ndio mkuu kuliko hata Imani au tumaini.

Upendo ni kilele cha Ukristo, Kwasababu biblia inasema Mungu mwenyewe ni Upendo.

Na Mkristo aliyekuwa sana kiroho, atatambulika kwa kiwango chake cha Upendo. Lakini wengi wetu tunadhani upendo ni kuonyesha tabasamu zuri kwa mtu, au kumsaidia mtu sana. Hivyo ni kweli ni vimelea vizuri vya Upendo, Lakini Upendo wa ki-Mungu unavuka hapo, na kwenda zaidi.

Embu tuvipitie baadhi ya vipengele vikuu,na mwishoni kabisa tutajifunza jinsi gani tutaupata huu Upendo mkamilifu.

1 Wakorintho 13

13:1 “Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika, kama sina upendo, nimekuwa shaba iliayo na upatu uvumao.

2 Tena nijapokuwa na unabii, na kujua siri zote na maarifa yote, nijapokuwa na imani timilifu kiasi cha kuweza kuhamisha milima, kama sina upendo, si kitu mimi.

3 Tena nikitoa mali zangu zote kuwalisha maskini, tena nikijitoa mwili wangu niungue moto, kama sina upendo, hainifaidii kitu.

4 Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni;

5 haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya;

6 haufurahii udhalimu, bali hufurahi pamoja na kweli;

7 huvumilia yote; huamini yote; hutumaini yote; hustahimili yote.

8 Upendo haupungui neno wakati wo wote; bali ukiwapo unabii utabatilika; zikiwapo lugha, zitakoma; yakiwapo maarifa, yatabatilika”.

Ukianzia kusoma ule mstari wa 4, utaona misingi inayoubeba upendo ikanza kuzungumziwa,  anasema huvumilia. Jiulize  je ndani yako ulishawahi kuvumilia mabaya mangapi pale ulipotendewa, je pale alipokuaibisha uliweza kutunza siri yake?, je, ulimsamehe pale alipokuaibisha, je ulivumilia yote hayo yote bila kuweka kinyongo, au kukomoa?

Anasema tena, Upendo hufadhili; Neno fadhili ni pana sana, ni zaidi ya kumfanyia mwenzako wema, ambao hauna malipo yoyote kwako. Anasema tena, hautakabari, haujivuni, huatafuti mambo yake mwenyewe, je maisha na namna hiyo yapo ndani yako? Wewe kama mkristo uliyeokoka?

Anasema Upendo haukosi kuwa na adabu, Je! Wewe wakati wote unayo adabu kwa watu wote?, hauoni uchungu, hauhesabu mabaya, yaani inafikia hatua hauoni mabaya bali mema tu mtu anayokufanyia, Je ulishawahi kuwa mtu wa namna hii?  Ulishawahi kuwa mtu wa kustahimili mambo yote, au kuvumilia mambo yote, au ni baadhi tu ya mambo umeyaweza? Kama ni baadhi tu basi Upendo wa ki Mungu bado haujakamilika ndani yako. Haijalishi utajiona ni mwema kiasi gani.

Hivyo utoshe tu kusema kwa namna ya kibinadamu  Pendo hili la Ki-Mungu, si rahisi kulipata kwa maneno tu, au kwa kuombewa au kwa kuwekewa mikono, , hauwezi kustahimili yote, yapo mengine ambayo yatakuudhi, upo wakati ambao utawahusudu wengine, upo wakati ambao, utahesabu mabaya tu n.k. Huo ndio ukweli.

Lakini sasa tufanyeje ili tuyashinde hayo yote?

Kanuni ni ile ile, kama ya IMANI, unapaswa uonyeshe bidii, katika kutekeleza hivyo vitu.

1Petro 4:8 “Zaidi ya yote IWENI NA JUHUDI NYINGI KATIKA KUPENDANA; kwa sababu upendano husitiri wingi wa dhambi”.

Inahitaji juhudi, mpaka ujijenge na kuwa tabia ndani yako, unapoona mwenzako amekutendea mabaya, unapaswa ujitahidi kwa nguvu zote, kuyaachilia yale mabaya anayokufanyia, na kujifunza kuyatafakari yale mazuri yake.. Ndio siku za mwanzoni mwanzoni, itakuwa ni ngumu lakini unavyojijengea utaratibu huo kwa nguvu, baadaye inageuka na kuwa ni tabia yako. Mpaka mwisho wa siku, hata jambo liwe ni gumu kiasi gani, utaona linatapita tu mbele yako kama upepo, bila kikusumbua hata kidogo .

Kumbuka tena vimelea hivyo vya upendo haviji hivi hivi tu, kwa kuombewa, au kusubiria, bali vinakuja kwa kuonyesha bidii, yaani kuvitendea kazi, mpaka ufikie hatua ya kutoona uchungu, au kutohusudu, kunahitaji kukataa usengenyaji kuanzia sasa, kukataa kusikiliza maneno ya watu mabarazani, pale wanapomzungumzia mtu mwingine kwa ubaya. Kunahitaji kujitoa kwa wengine, bila kujali unapata faida gani kwao..N.k.

Warumi 12:10 “Kwa pendo la udugu, mpendane ninyi kwa ninyi; kwa heshima mkiwatanguliza wenzenu;

11 kwa bidii, si walegevu; mkiwa na juhudi katika roho zenu; mkimtumikia Bwana;”

Upendo ni kitu cha kujazilishwa, yaani kila siku unakiongezea nyama mpya, kimoja huzaa kingine, na kingine huzaa kingine, mpaka tunafikia vile viwango vya Upendo wa ki-Mungu

2Petro 1:5 “Naam, na kwa sababu iyo hiyo mkijitahidi sana kwa upande wenu, katika imani yenu tieni na wema, na katika wema wenu maarifa,

6 na katika maarifa yenu kiasi, na katika kiasi chenu saburi, na katika saburi yenu utauwa,

7 na katika utauwa wenu upendano wa ndugu, na katika upendano wa ndugu, upendo.

8 Maana mambo hayo yakiwa kwenu na kujaa tele, yawafanya ninyi kuwa si wavivu wala si watu wasio na matunda, kwa kumjua Bwana wetu Yesu Kristo”.

Hivyo mimi na wewe kuanzia leo tuanze kuyatendea kazi haya, tujazilishe upendo wetu, siku baada ya siku tuongeze kimelea kipya cha upendo, Kwasababu tujue kuwa kitu cha kwanza ambacho kitatusogeza kwa Mungu kwa urahisi na haraka si Imani au tumaini bali ni Upendo, kwasababu yeye mwenyewe ni Upendo, na ndio maana Paulo anasema, hata nijapokuwa na Imani timilifu ya kuamisha milima kama sina Upendo mimi si kitu. Maana yake ni kuwa, huwezi kumwona au kumjua Mungu ukiukosa huo,

1Yohana 4:8 “Yeye asiyependa, hakumjua Mungu, kwa maana Mungu ni upendo”.

Hivyo jambo hili, na kuwa nalo siriazi, ni kulitendea kazi kwa bidii zote, kila wakati kila muda mpaka lijengeke na kuwa tabia yetu.

1Petro 1:22 “Mkiisha kujitakasa roho zenu kwa kuitii kweli, hata kuufikilia upendano wa ndugu usio na unafiki, basi jitahidini kupendana kwa moyo”.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

UPENDO WA MUNGU.

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU UPENDO.

Sadaka ya kuinuliwa ni sadaka ya namna gani?

Mtu mwenye “kitango” ni mtu wa namna gani kibiblia?

TUSIWE WATU WA KUPUNGUKIWA AKILI.

Rudi nyumbani

Print this post

Sadaka ya kuinuliwa ni sadaka ya namna gani?

Jibu: Sadaka ya kuinuliwa ni sadaka ambayo mtu anaiinua mbele za Mungu. Na ni sehemu ya sadaka iliyo ya heshima kuliko nyingine yoyote ile.

Kwamfano mtu anaweza kutoa sadaka ya kawaida ya kila siku, lakini isiwe iliyo kuu na ya heshima, lakini akatenga sadaka moja ambayo itakuwa ndio kaiheshimu kuliko zote.. ambayo atakwenda kuiinua mbele za Mungu, huku akiambatanisha na haja fulani, au shukrani fulani.

Hesabu 15:18 “Nena na wana wa Israeli, uwaambie, Mtakapoingia nchi niwapelekayo,

19 ndipo itakapokuwa ya kwamba hapo mtakapokula katika chakula cha nchi hiyo, mtamsongezea Bwana sadaka ya kuinuliwa”.

Mara nyingi sadaka hii ya kuinuliwa inakuwa ni ya “maandalizi”, sio tu ya kufikiri siku moja na kwenda kuitoa, na pia inakuwa ni ya kujitoa kweli kweli (maana yake ni ya kiwango kikubwa, au ya kugharimu), ikiwa sio ya kugharimu inakuwa haina tofauti na sadaka nyingine.

Kumbuka pia sadaka kama Zaka, na  Malimbuko hizo sio sadaka za kuinuliwa, hizo ni sadaka ambazo ni za wajibu, na hazipo katika kundi hili la sadaka za kuinuliwa.

Kumbuka tena sadaka hii ni tofauti na sadaka nyingine, ni lazima iwe na heshima kuliko nyingine, ndio maana imeitwa Sadaka ya KUINULIWA, maana yake ni ya hadhi ya juu zaidi kuliko nyingine, “Umeiinua kuliko nyingine”.  kwahiyo ni dhambi kumtolea Mungu sadaka kilema. Na kuiinua mbele za Mungu.

 Ni dhambi kumpa Mungu sadaka ya shukrani shilingi elfu moja, na kuisongeza mbele zake na kusema nimemwinulia Bwana sadaka hii, (tena na kujiona umemtolea kikubwa mbele zake) na unatoka ukijisifu kwamba umemtolea Mungu… na wakati kakufanyia muujiza wa mamilioni. Hapo ni sawa na umeiinua sadaka ambayo haistahili kuinuliwa, hivyo ni dhambi, ni heri usingetoa kabisa.

Ni sawa na umemwahidi mtu unampelekea zawadi nzuri na kubwa sana, baada ya jambo zuri alilokufanyia na tena ukainadi zawadi hiyo na kuitukuza sana mbele zake..na mwisho wa siku unampelekea zawadi ya hadhi ya chini sana, kuliko ya alivyotarajia, na tena ukaifunga kwenye box zuri. Unadhani ni nini kitafuata?..Ni wazi kuwa yule mtu atachukia atasema ni heri usingempa hiyo zawadi au ni kama ulikuwa unataka kumpa basi ungemwambia tu kwamba utampa kitu fulani kidogo, ili ajue na kujiandaa kabisa kwamba kitakachokuja kinaweza kuwa kidogo. Lakini kwa jinsi ulivyoisifia na kuiinua zawadi hiyo, halafu anakuta ni kidogo sana, ataishia kuchukia.

Ndio hivyo hivyo, pia sadaka ya kuinuliwa..inapaswa iwe kubwa na  iwe tofauti na sadaka nyingine..vinginevyo kama huwezi  basi toa tu sadaka yako ya kawaida ya kila siku ila usiinyanyue sana mbele za Mungu.

Lakini kama Bwana kakufanyia muujiza mkubwa sana, na wewe ukasema nitamsogezea sadaka ambayo nitaiinua mbele zake, na ukamtolea sehemu kubwa sana na iliyokugharimu angalau sawasawa au karibia na kile alichokufanyia. Hapo sadaka hiyo inakuwa na nguvu mara nyingi zaidi kuliko sadaka nyingine yoyote ya kawaida. Na inaachilia matokeo haraka sana, ikiwemo kuinuliwa kwa huyo mtu. Na Mungu anawaheshimu wale wote wanaomtolea kwa moyo na kwa bidii.

Bwana atubariki na kutusaidia.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

Je! ni vema kwa mkristo kwenda hospitali au kutumia miti shamba anapougua?

TOA SADAKA ISIYO NA KASORO KWA BWANA.

FUKUZA TAI WOTE JUU YA SADAKA YAKO.

Mlango uitwao “Mzuri” Unaozungumziwa katika Matendo 3:2 ndio upi?

Kuota upo nchi nyingine.

Rudi nyumbani

Print this post

Mtu mwenye “kitango” ni mtu wa namna gani kibiblia?

Neno hilo utalisoma katika vifungu hivi;

Mithali 20:13 “Mwenye kitango akisingizia hufunua siri; Bali mwenye roho ya uaminifu husitiri mambo.

Mithali 20:19 “Mwenye kitango akisingizia hufunua siri; Basi, usishirikiane naye afunuaye midomo yake sana”.

Mtu mwenye kitango kwa lugha ya sasa ambayo ni rahisi kueleweka na watu wengi ni mtu  “MMBEA”. Yaani mtu ambaye hawezi kusitiri jambo, yupo tayari kukizungumza kila kitu anachokisikia au kukiona kwa watu wengine.

Kwamfano utakuta mtu labda kakaribishwa nyumbani kwa jirani yake au ndugu yake wa mbali, ili akae au aishi tu pale kwa muda, sasa katika kuishi kwake akaona mapungufu fulani fulani ndani ya nyumba ile, ambayo hata wenye nyumba wenyewe hawakuona vema, kuyatangaza, lakini utakuta  yeye anatoka pale na kuanza kufichua siri za nyumba hiyo kwa watu wengine, bila hata kujali utu, wale wapo hivi, wapo vile, yule mwanaume kumbe yupo hivi au vile n.k… Sasa mtu kama huyo ni mtu mwenye kitango ambaye biblia imetuonya, tusishirikane naye.

Mwingine ataelezwa jambo la siri na rafiki yake pengine labda ugonjwa fulani usiotibika, na akaombwa sana asimwambie mtu yeyote iwe siri yake, lakini yeye anatoka pale, anaanza kutangaza mtaa mzima yule fulani ana hiki au kile, mpaka habari inamrudia yule mwenyewe muhusika. Sasa watu wa namna hiyo ni hatari sana, hatupaswi kushirikiana nao, kwasababu hata kwa namna ya kawaida ikiwa anaweza kufichua siri za watu wengine kwako, ni wazi  kuwa hata za kwako ameshawahi kuzifichua kwa watu wengine. Hivyo ukishakutana na watu kama hawa usijaribu kuwaeleza mambo yako ya siri, wala usikubali kusikiliza wanachokuambia.

Mara nyingi tunaziharibu siku zetu mapema kabisa kunapopambazuka, kwa midomo yetu wenyewe, biblia inasema;

1Petro 3:10 “Kwa maana, Atakaye kupenda maisha, NA KUONA SIKU NJEMA, Auzuie ulimi wake usinene mabaya, Na midomo yake isiseme hila”.

Ukitaka ufurahie maisha, jifunze,kuudhibiti ulimi wako, ukitaka siku yako ibarikiwe tangu asubuhi mpaka jioni, jifunze kuutawala mdomo wako, sio kila jambo unaloliona au unalolisikia ni la kutangaza kwa watu , jifunze kutunza siri za watu wengine, kwani kwa kufanya hivyo sio tu siku yako itakuwa ni nzuri, lakini pia utakuwa unampendeza Mungu, Kwasababu Mungu naye hachukui mambo yetu ya siri na kwenda kuyatangaza kwa watu ovyo ovyo, japokuwa anajua mambo yetu wote ya siri tunayoyafanya.

Mathayo 5:48 “Basi ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu”.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

KAMA UNAPENDA MAISHA, NA KUTAKA SIKU YAKO IWE NJEMA.

JIHADHARI NA DHAMBI YA WIVU/HUSUDA.

Vyombo vya uzuri ni vipi vinavyotajwa katika biblia?

Ngome ni nini?  Kwanini Mungu anafananishwa na ngome?

Tofauti kati ya lijamu na hatamu ni ipi kibiblia?

NI SAA KUMI NA MBILI (12) TU, ZA KRISTO KWAKO.

Rudi nyumbani

Print this post

Vyombo vya uzuri ni vipi vinavyotajwa katika biblia?

SWALI: Shalom mpendwa katika Bwana , swali langu lipo katika kutoka 33:5 BWANA alipomwambia Musa vueni “vyombo vyenu vya uzuri” ili nipate kujua nitakalowatenda . Nataka kujua aliposema hivyo alikuwa na maana gani?


JIBU: Tusome habari yenyewe tokea mstari wa kwanza, lipo jambo zaidi ya hilo la kujifunza;

Kutoka 33:1 “Bwana akanena na Musa, Haya, ondokeni, katokeni hapo, wewe na hao watu uliowaleta wakwee kutoka nchi ya Misri, waende nchi hiyo niliyomwapia Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo, niliposema, Nitakipa kizazi chako nchi hii;

2 nami nitamtuma malaika aende mbele yako; nami nitawafukuza Mkanaani, na Mwamori, na Mhiti, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi;

3 waifikilie nchi imiminikayo maziwa na asali; kwa maana mimi sitakwenda kati yenu; kwa sababu ninyi ni watu wenye shingo ngumu; nisiwaangamize ninyi katika njia.

4 Watu waliposikia habari hizo mbaya wakaomboleza WALA HAPANA MTU ALIYEVAA VYOMBO VYAKE VYA UZURI.

5 Bwana akamwambia Musa, Waambie wana wa Israeli, Ninyi ni watu wenye shingo ngumu; kama mimi nikiingia kati yenu dakika moja, nitawaangamiza; basi sasa VUENI VYOMBO VYENU VYA UZURI ili nipate kujua nitakalowatenda.

6 Basi wana wa Israeli wakavua vyombo vyao vyote vya uzuri, tangu mlima wa Horebu na mbele”.

Vyombo vya uzuri,ni  mapambo ya aina yote, ikiwemo mikufu, pete, hereni, vikuu, nguo za thamani n.k.. Wana wa Israeli baada ya kumkosea sana Mungu, kwa kutengeneza ndama  wa dhahabu, Mungu alikusudia kuanzia huo wakati kuwaacha  moja kwa moja asitembee nao tena, kinyume chake awape malaika wake wawe wanaenda badala yake, lakini sio yeye tena. Lakini wana wa Israeli waliposikia hivyo wakamlilia sana Mungu wasiachwe, ndipo watu wote wakavua vyombo vyao vya uzuri, yaani vitu vyao vya thamani, wakavaa nguo za maombolezo, wakamlilia sana Mungu na kutubu kwa uchungu mwingi ili tu wasiachwe.

Hiyo ilikuwa ni desturi ya Israeli tangu zamani, na hata mataifa mengine, inapofikia wakati wa kuomba toba, au kuomboleza, ni sharti uweke kando mavazi ya thamani, na mapambo yako, uvae nguo za magunia uomboleze.

Lakini ni nini, tunaweza kujifunza katika habari hiyo?

Wana wa Israeli walitamani waangukie mikononi mwa Mungu kuliko  mikononi mwa malaika zake, Kwasababu walimjua Mungu ndio uzima wao, licha ya kuwa ni mwenye ghadhabu nyingi, lakini pia bado ni mwenye rehema nyingi. Ni sawa na kilichomtokea Daudi kipindi kile, alipoambiwa na Mungu achague adhabu mojawapo kati ya zile tatu, yaani njaa miaka mitatu, au akimbizwe na adui zake miezi mitatu, au Tauni iletwe siku tatu juu ya nchi,. Daudi akachagua kuangukia mikononi mwa Mungu, kwa ile Tauni siku ya tatu, kwasababu alijua, mioyo ya wanadamu sio kama wa Mungu, kuliko kukimbizwa na maadui zake, ni heri aadhibiwe na Mungu..Na kweli japokuwa Mungu aliwaua maelfu ya watu, lakini baadaye aliuzuia mkono wake, akarehemu.

Je! Na wewe umechagua kuangukia mikononi mwa nani? Mungu, au mwanadamu?.

Daudi alisema..

Zaburi 118:18 “Bwana ameniadhibu sana, Lakini hakuniacha nife”.

Inasikitisha kuona kwamba watu wanakataa kuongozwa na Mungu, wanataka waongozwe na wanadamu, wanachukia kuadhibiwa na Mungu, wanataka wakaadhibiwe na wanadamu. Wana wa Israeli waliomboleza kusikia tu wanakwenda kuongozwa na malaika,ambao hata hawana shida yoyote, lakini waliona bado hakuna kiongozi mzuri na bora zaidi ya Bwana.

Ndugu yangu huna kimbilio lingine lililo salama kwako, zaidi ya Mungu.. Si hata malaika wake, si mwanadamu, au kiumbe kingine chochote, au kitu kingine chochote. Mkimbilie Bwana leo hii akuokoe, na ayasafishe maisha yako. Usizifiche dhambi zako mbele za Mungu, kwa hofu ya kwamba atayakemea matendo yako, ni kweli lazima ayakemee, na wakati mwingine akuadhibu, lakini adhabu zake ni dawa, na sio mauti. Hivyo chagua kuangukia mikononi mwake, uwe salama.

Ufunuo 3:19 “Wote niwapendao mimi nawakemea, na kuwarudi; basi uwe na bidii, ukatubu”.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

AINA TATU ZA WAKRISTO.

Swali: Je Ni sahihi kwa Mkristo kupeleka kesi mahakamani?

Je mtu anayeua anabeba dhambi zote za yule aliyemuua?

NI SAA KUMI NA MBILI (12) TU, ZA KRISTO KWAKO.

MLANGO MWINGINE WA ADUI KUTULETEA MAJARIBU.

Rudi nyumbani

Print this post

AINA TATU ZA WAKRISTO.

Nakusalimu katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo. Karibu tujifunze maneno matukufu ya uzima, maadamu tumeiona leo.

Wakristo wameganyika katika makundi makuu matatu, makundi hayo yanafananishwa na miti ya matunda.

Na Miti ya matunda ipo ya aina tatu;

  1. Miti inayozaa matunda halisi
  2. Miti isiyozaa matunda yoyote
  3. Miti inayozaa matunda mwitu.
  • Tukianzana na Miti inayozaa Matunda halisi.

Hii Ndio ile miti ambayo Bwana Yesu aliizungumzia katika mfano ule mfano wa mpanzi, akasema mbegu zake ndio zile zilizopandwa katika udongo mzuri ambazo nyingine zilizaa 30 nyingine 60 nyingine 100 (Mathayo 13:8). Akasema hao ni wakristo ambao, walistahimili vishindo vyote vya ibilisi, kwa kuvumilia ndipo wakaweza kumzalia Mungu matunda.

Luka 8:15 “Na zile penye udongo mzuri, ndio wale ambao kwa unyofu na wema wa mioyo yao hulisikia neno, na kulishika; kisha huzaa matunda KWA KUVUMILIA”.

Walivumilia nini?

 Walivumilia  dhiki na udhia shetani alizowaletea kutokana na ukristo wao, waliweza kulitunza Neno la Mungu mioyoni mwao, kwa kutoruhusu  masumbufu ya maisha haya kuwaingilia sana, mpaka kuwafanya wasilitendee kazi Neno., Na kundi hili lipo dogo sana. Na Kristo ameahidi kulipalilia, na kulisafisha ili liendelee kumzalia zaidi. (Yohana 15:2)

  • Miti isiyozaa matunda yoyote.

Mfano wa miti huu, ndio ile ambayo Bwana Yesu aliutolea mfano huu;

Luka 13:6 “Akanena mfano huu; Mtu mmoja alikuwa na mtini umepandwa katika shamba lake la mizabibu; akaenda akitafuta matunda juu yake, asipate.

7 Akamwambia mtunzaji wa shamba la mizabibu, Tazama, miaka mitatu hii naja nikitafuta matunda juu ya mtini huu, nisipate kitu; uukate, mbona hata nchi unaiharibu?

8 Akajibu akamwambia, Bwana, uuache mwaka huu nao, hata niupalilie, niutilie samadi;

9 nao ukizaa matunda baadaye, vema! La, usipozaa, ndipo uukate”.

Hawa ni wakristo, ambao mara baada ya kuokoka, wana-relax, wanadhani wokovu ni kukiri tu kwa kinywa na kuamini, basi, na baada ya hapo unaendelea na mambo yako mwenyewe. Hawataki kujishughulisha kutafuta mambo ya rohoni baada ya kuamini na kubatizwa, licha ya kwamba, Mungu anawatia samadi kila siku kwa kuwafundisha na kuwahubiria njia zake, lakini wao hawaonyesha badiliko lolote, Hawapo kwenye maovu, wala hawapo kwenye mema. Lakini wakati wote, wanasikiliza Neno la Mungu na kulipokea, kundi hilo lipo kubwa sana.

Kristo ameahidi kutochukuliana nalo muda mrefu sana, utafika wakati litakatwa, na ukishakatwa, ndio habari yako imeishia hapo, unakuwa umekufa kiroho, haijalishi utasema niliokoka zamani. Bwana Yesu anatazamia, tunapookoka, tuonyeshe matendo yanayotendana na wokovu wetu, kuanzia huo wakati, tuwe waombaji, wafungaji, tuwaambie na wengine habari njema za wokovu, tuchangie kwa mapato yetu kazi ya Mungu isonge mbele, n.k. Lakini tukiwa sisi ni wa kupokea tu vya Mungu, lakini hatumtolei na yeye, tujue kuwa safari yetu haitakuwa ndefu.

  • Miti inayozaa matunda mwitu;

Mfano wa miti hii, ndio kama huu Ambao Mungu aliizungumza katika Isaya sura ya 5.

Isaya 5:1 “Na nimwimbie mpenzi wangu wimbo wa mpenzi wangu katika habari za shamba lake la mizabibu. Mpenzi wangu alikuwa na shamba la mizabibu, Kilimani penye kuzaa sana;

2 Akafanya handaki kulizunguka pande zote, Akatoa mawe yake, Akapanda ndani yake mzabibu ulio mzuri, Akajenga mnara katikati yake, Akachimba shinikizo ndani yake; Akatumaini ya kuwa utazaa zabibu, Nao ukazaa zabibu-mwitu.

3 Na sasa, enyi wenyeji wa Yerusalemu, nanyi watu wa Yuda, amueni, nawasihi, kati ya mimi na shamba langu la mizabibu.

4 Je! Ni kazi gani iliyoweza kutendeka ndani ya shamba langu la mizabibu nisiyoitenda? Basi, nilipotumaini ya kuwa litazaa zabibu, mbona lilizaa zabibu-mwitu?

5 Haya basi, sasa nitawaambieni nitakalolitenda shamba langu la mizabibu; nitaondoa kitalu chake, nalo litaliwa; nitabomoa ukuta wake, nalo litakanyagwa;

6 nami nitaliharibu; wala halitapogolewa wala kulimwa, bali litamea mbigili na miiba; nami nitayaamuru mawingu yasinyeshe mvua juu yake.

7 Kwa maana shamba la mizabibu la Bwana wa majeshi ndilo nyumba ya Israeli, na watu wa Yuda ni mche wake wa kupendeza; akatumaini kuona hukumu ya haki, na kumbe! Aliona dhuluma; alitumaini kuona haki, na kumbe! Alisikia kilio”.

Kundi hili ndilo baya zaidi, kwasababu, ni kundi ambalo linazaa matunda ya upande mwingine,. Hawa ni wakristo ambao mara baada ya kuokoka, mara baada ya kukaa kanisani kwa muda mrefu, mambo wanayoyaonyesha kwa matendo yao ni kinyume kabisa na ukristo unavyopaswa uwe.. Utakuta mtu ni mzinzi wa muda mrefu, mwingine ni mtukanaji, mwingine ni mwizi, mwingine ni tapeli n.k. na bado  anasema nimeokoka, nimebatizwa, nimepokea Roho Mtakatifu, Yaani kwa ufupi yale mambo ambayo wanayafanya watu wa kidunia na yeye anayafanya, vivyo hivyo, hakuna tofauti yoyote.

Kundi hili nalo ni kubwa sana na Mungu  ameahidi kuliondolea kitalu chake (Kuliua)..

Tukiyajua hayo ni wajibu wako wewe kama mkristo kujichunguza ni kundi lipi unaloangukia, na matokeo yake mbeleni yatakuwaje, , Fahamu tu upo wakati mwenye shamba atakuja kukupeleleza,  Kwahiyo ni wajibu wako wewe kujua kuwa upo hapa duniani kwa malengo, na Mungu anatarajia kuona badiliko katika maisha yako katika kipindi alichokuweka hapa duniani. Kama upo miaka mingi katika wokovu na huoni kama kuna chochote unakifanya kinampendeza Mungu, au kinaisaidia injili yake isonge mbele, jiulize unaekea wapi? Je, ni wa Kukatwa au kupaliliwa. Jibu unalo, jibu ninalo.

Hivyo tubu ugeuke, umpokee Kristo kwa kumaanisha, na kuonyesha bidii katika kusoma Neno lake, kuomba, na kumfanyia ibada, ndipo utakapopata nguvu ya kumzalia yeye Matunda.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MATUNDA 9 YA ROHO MTAKATIFU

TUTAWEZAJE KUMZALIA MUNGU MATUNDA?

NAWE UTAGEUZWA KUWA MTU MWINGINE.

KUNA MAJIRA MUNGU ATAIVURUGA MIPANGO YETU.

JIFUNZE KUTOA KATIKA HAZINA YAKO VITU VIPYA NA VYA KALE.

Rudi nyumbani

Print this post

Swali: Je Ni sahihi kwa Mkristo kupeleka kesi mahakamani?

Jibu: Kwanza ni muhimu kufahamu kuwa makosa yote yanastahili msamaha. Hata kama tumetendewa makosa makubwa kiasi gani, mwisho wa siku ni lazima tusamehe, hiyo ndio sheria ya Imani. Hakuna ukristo bila msamaha, kwasababu kila mwanadamu katenda dhambi, na wote tunapata msamaha wa dhambi bure kupitia damu ya Yesu, tunapomwamini. Hivyo na sisi hatuna budi kusamehe kama Bwana alivyotusamehe sisi.

Lakini kuna jambo moja ambalo Bwana Yesu alilizungumza ambalo tukijifunza hilo vizuri tutapata kuelewa vizuri  muktakabadhi wa msahama

Tusome..

Luka 12:58  “Maana, unapofuatana na mshitaki wako kwenda kwa mwamuzi, hapo njiani fanya bidii kupatanishwa naye, asije akakuburuta mpaka mbele ya kadhi; yule kadhi akakutia mikononi mwake mwenye kulipiza, na yule mwenye kulipiza akakutupa gerezani.

59  Nakuambia, Hutoki humo kamwe hata uishe kulipa senti ya mwisho”

Hayo maneno yalizungumzwa na Bwana Yesu mwenyewe. Na kama ukiyatafakari kwa makini utagundua kuwa Bwana anaonyesha hatua za mtu ambaye ni Mdhulumuji, na hataki kukiri dhuluma zake, na kuzidi kujihesabia haki (au kwa lugha nyepesi yule mtu ambaye hataki kuacha njia zake mbaya), kama ni mwizi au tapeli, anatapeli leo na kesho anarudia inakuwa kama ni tabia yake, yeye kazi yake ni kusababisha wengine walie tu na kuhuzunika kila siku.

Sasa Bwana Yesu anasema mtu wa namna  hiyo akiri makosa yake mapema, aachane na hiyo kazi ya utapeli aiache(maana yake apatane na jamii yake, mapema) kabla hajashikwa na kupandishwa mahakamani na kuhukumiwa… Hapo Bwana Yesu anamalizia kwa kusema “NAKUAMBİA, HUTOKİ HUMO KAMWE HATA UİSHE KULİPA SENTİ YA MWİSHO” Ukisoma Mathayo 5:26 inasema … “ Amin, nakuambia, Hutoki humo kamwe hata uishe kulipa senti ya mwisho.”…. Neno Amin amini, maana yake ni Hakika!!… hakika!!

Sasa unaweza kujiuliza kwanini Bwana aseme maneno hayo?..Hakika hakika!! Hutoki huko.

Ni kwasababu anataka kuonyesha kuwa Mahakama na Vyombo vya dola vimepewa mamlaka makubwa ya kutawala kutoka mbinguni.. Ukitiwa mikononi mwa polisi kwa kosa lolote ambalo ni halali umelitenda ni sawa kabisa na umetiwa mikononi mwa Mungu mwenyewe kwaajili ya adhabu..

Hivyo kwa lugha rahisi kabisa tunaweza kusema polisi ni kiboko cha Mungu..

Warumi 13: 1  “Kila mtu na aitii mamlaka iliyo kuu; kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu; na ile iliyopo umeamriwa na Mungu.

2  Hivyo amwasiye mwenye mamlaka hushindana na agizo la Mungu; nao washindanao watajipatia hukumu.

3  Kwa maana watawalao hawatishi watu kwa sababu ya matendo mema, bali kwa sababu ya matendo mabaya. Basi, wataka usimwogope mwenye mamlaka? Fanya mema, nawe utapata sifa kwake;

4  kwa kuwa yeye ni mtumishi wa Mungu kwako kwa ajili ya mema. Lakini ufanyapo mabaya, ogopa; kwa maana hauchukui upanga bure; kwa kuwa ni mtumishi wa Mungu, amlipizaye kisasi mtenda mabaya kwa ajili ya ghadhabu.

5  Kwa hiyo ni lazima kutii, si kwa sababu ya ile ghadhabu tu, ila na kwa sababu ya dhamiri”

Kwahiyo basi kama umemwona mtu ni tapeli na anatapeli watu, na kuwafanya waumie..mwitie Polisi, hufanyi dhambi, atakwenda polisi na hatatoka huko!! Mpaka ameiva vizuri!!..Lakini kama akikiri njia yake mapema na kuiacha, hapo amepatana na wewe na jamii yote, hivyo umwache usifanye lolote, wala usimpeleke polisi. Na pia kama ni kibaka kakuibia, hapo hapo na ukamshika na akatubu mbele yako kwa kuomba radhi kabisa msamehe, usimripoti..

Lakini kama mtu ni muuaji, au jambazi.. mripoti polisi (hufanyi dhambi)...Lakini kama alikuwa ni muuaji miaka ya zamani na sasa kashabadilika ni mtu mwema na hata pengine kashaokoka, huna haja ya kuchimbua makosa yake ya zamani na kuyapeleka polisi.

Vivyo hivyo kama ni mbakaji, au ni mtu wa dhuluma, au ni mtu asiyefaa kitabia katika jamii, anayefanya mambo maovu kwa makusudi na huku anajua kabisa anayoyafanya sio sawa na anandelea kuyafanya, pamoja na kuonywa mara nyingi..Mtu huyo mripoti polisi utakuwa hujafanya dhambi na zaidi ya yote utakuwa umefanya jambo jema.

Vivyo hivyo kama umedhulumiwa mali zako na yule mdhulumuji unaona ni mtu aliyejizoeza kuyafanya hayo, na ameshawafanyia wengi, na anazidi kuwafanyia wengine..maana yake huyo kashaonywa mara nyingi lakini kashupaza shingo, mtu wa namna hiyo mpeleke mahakamani, utakuwa umesaidia asiendelee kufanya hivyo kwa watu wengine, na kusababisha huzuni na majonzi kwa watu wengine. Utakuwa hujafanya dhambi. Lakini kumbuka hatuzungumzii suala la kujichukulia sheria mkononi, kwamba ameiba sasa unampiga, au ameua sasa na wewe unatafuta kumuua.. Hapana! Ukifanya hivyo utakuwa unatenda dhambi…Kwasababu biblia hapo juu inasema Mamlaka ndio zimepewa ruhusa za kutoa hukumu, na Mungu mwenyewe, na si wewe wala mimi.

Na mambo mengine yoyote ambayo unaona kuna mtu au watu wanayafanya ambayo yanaleta au yataleta madhara makubwa sana katika jamii, na kuifanya jamii iharibike, au watu kupoteza maisha..Ripoti polisi, kwasababu vyombo hivyo pia vinatimiza kusudi la Mungu duniani.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

JE UPENDO WAKO UMEPOA?

NAWE UTAGEUZWA KUWA MTU MWINGINE.

MATUNDA YAPATANAYO NA TOBA!

Shokoa ni nini katika biblia?

LILE TUMAINI LILILO NDANI YETU LINAPOULIZIWA.

Yeshuruni ni nani katika biblia?

Rudi nyumbani

Print this post

Je mtu anayeua anabeba dhambi zote za yule aliyemuua?

Jibu: Si kweli kwamba mtu anayeua anakuwa anazibeba dhambi zote za yule aliyemuua, na kwamba yule aliyeuawa yupo huru, (anakuwa hana dhambi tena huko anakokwenda).

Kama mtu atamkataa Mungu na ghafla akafa katika dhambi zake, kwa kifo cha aina yeyote ile, iwe kwa kuuawa, au labda kwa kugongwa na gari, au kupewa sumu, au kupigwa mpaka kufa.. Mtu huyo dhambi zake anazibeba mwenyewe, na anakwenda nazo huko anakokwenda, hakuna yeyote atakayezuchukua. Yule aliyemuua atabeba dhambi ya mauaji, kwa alilolifanya lakini si dhambi za yule aliyemuua.

Wagalatia 6: 5  “Maana kila mtu atalichukua furushi lake mwenyewe”.

Ni kitu kimoja tu ambacho Mungu atamdai mtu yule ambaye hatamwonya mwingine aiache njia yake mbaya. Na hicho si kingine zaidi ya Damu ya huyo mtu.

Ezekieli 3:18 “Nimwambiapo mtu mbaya, Hakika utakufa; wewe usimpe maonyo, wala husemi na huyo mtu mbaya ili kumwonya, kusudi aache njia yake mbaya na kujiokoa roho yake; mtu yule mbaya atakufa katika uovu wake; lakini damu yake nitaitaka mkononi mwako”.

Sasa nini maana ya kuwa hatia na damu ya mtu?.

Kuwa na hatia ya damu ya mtu, si kuzichukua dhambi zake na kuzibeba.. La!..Bali maana yake ni kuwa na kila sababu za kuwajibishwa kwa kumsababishia mwingine madhara. Maana yake ni kwamba kama hujamwonya mtu aache njia mbaya, na ilihali ulikuwa na nafasi ya kufanya hivyo, na yule mtu akafa bila kusikia maonyo yoyote, basi wewe ambaye ulipaswa umwonye, kuna adhabu itakayokuja juu yako. Na adhabu hiyo inaweza kuwa laana au wakati mwingine hata kifo.

Ili tuelewe vizuri tafakari tu, mtu aliyemuua mwenzako…katika sheria za nchi, yule aliyeua hachukui madeni ya yule aliyemuua.. Maana yake ni kwamba, kama yule aliyeuawa alikuwa na madeni ya benki, au madeni mengine yoyote, madeni hayo hatayarithi yule aliyemuua. Yule aliyemuua atahukumiwa kwa kosa la mauaji (ambayo adhabu yake ndio hiyo ambayo inaweza kuwa hata kifo), lakini hatatwikwa madeni yote ya yule aliyemuua kwamba benki imfuate imwambie alipe deni la marehemu . Ndio hivyo hivyo pia kwa mtu aliyemuua mwingine, hatabeba dhambi za aliyekufa.

Hivyo tunachojifunza ni kwamba tuwe makini, hususani kama umeshaokolewa, ni wajibu wako kuwapelekea wengine injili, ili damu yao isiwe juu yako, kama Mtume Paulo alivyosema mahali fulani..

Matendo 20:25  “Na sasa, tazameni, mimi najua ya kuwa ninyi nyote niliowahubiria ufalme wa Mungu, nikienda huko na huko, hamtaniona uso tena.

26  Kwa hiyo nawashuhudia wote siku hii ya leo, ya kuwa mimi sina hatia kwa damu ya mtu awaye yote.

27  Kwa maana sikujiepusha na kuwahubiria habari ya kusudi lote la Mungu”

Na kuipeleka injili sio tu kwenda kuhubiri, bali kuchangia hata kuichangia kazi ya Mungu, pia ni kuipeleka injili.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

Aina za dhambi

Je! Kuna dhambi kubwa na ndogo, na kama hakuna je! Mtu aliyeua na aliyetukana je watapata adhabu sawa?

DHAMBI YA MAUTI

Je! Ni dhambi kumpiga au kumuua mnyama bila sababu yoyote?

6# SWALI : Dhambi ya kumkufuru Roho Mtakatifu ni ipi?

Rudi nyumbani

Print this post