Je Bwana Yesu alioa mke au kuwa na mahusiano na mwanamke yeyote?
Jibu: Bwana Yesu hakuoa wala kujihusisha na mahusano yoyote na mtu yeyote yule.
Alizaliwa na kuishi bila kuoa ili ayatende mapenzi ya Baba yake. Na zaidi ya yote hakuwahi kutenda dhambi hata moja, ikiwamo ya kutamani.
Yohana 8:46 “Ni nani miongoni mwenu anishuhudiaye ya kuwa nina dhambi? Nami nikisema kweli, mbona ninyi hamnisadiki?”
Ipo mitazamo inayosema kuwa Bwana Yesu alikuwa katika mahusiano na Mariamu, Magdalena.
Mitazamo hiyo imetengenezwa na adui, ili kuwapotosha watu, na kuwafanya watu wamwone Bwana Yesu kama alikuwa mtu wa kawaida tu kama watu wengine. Hiyo imekuwa ni kawaida ya shetani siku zote, kujaribu kushusha vitu vya kiMungu hadhi, ili visivutie.
Lakini haisadii kwasababu kuna Roho Mtakatifu, ndiye anayeishawiahi mioyo, na si ushawishi wa maneno..Hivyo iwe kwa husuda au kwa haki, Kristo atahubiriwa na ataaminiwa tu, hakuna kitakachoweza kuzuia hilo..
Wafilipi 1:18 “Yadhuru nini? Lakini kwa njia zote, ikiwa ni kwa hila, au ikiwa ni kwa kweli, Kristo anahubiriwa; na kwa hiyo nafurahi, naam, nami nitafurahi”.
Watu waliokusudiwa kumwamini mwokozi, watamwamini tu, na wote watakaomwamini, shetani hawezi kuwanyakua kutoka mikononi mwake.
Utukufu una yeye, Mkuu wa Uzima, Yesu Kristo, milele na milele.
washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 2: Upande wa wanawake)
Ni kweli hakuna mtu aliyewahi kuuona uso wa Mungu Zaidi ya Bwana Yesu?
Kwanini wakristo walipomuona Petro akigonga walisema “Ni malaika wake”?
Mbwa ni mnyama anayeweza kuwakilisha vitu vitatu:
1) Mlinzi
2) Adui
3)Kitu najisi/Mchafu.
Inategemea hiyo ndoto imekuja katika mazingira gani..na pia kama imekuja katika mazingira ya kujirudia rudia au katika hali ya uzito wa kitofauti basi haipaswi kupuuzwa, inayo maana rohoni.
Kama tunavyojua mbwa ni mlinzi. Na katika biblia watumishi wa Mungu pia wanafananishwa na mbwa walinzi.
Vilevile watumishi ambao hawasimami katika nafasi zao kikamilifu za kuwalinda kondoo wa Mungu wanafanishwa na mbwa walinzi wasioweza kubweka wala kung’ata.
Isaya 56:9-11
[9]Enyi hayawani wote wa nyikani, njoni, Mle, enyi hayawani wote wa mwituni.
[10]Walinzi wake ni vipofu, wote pia hawana maarifa; wote ni mbwa walio bubu, hawawezi kulia; huota ndoto, hulala, hupenda usingizi.[11]Naam, mbwa hao wana choyo sana, hawashibi kamwe; na hao ni wachungaji wasioweza kufahamu neno; wote pia wamegeuka upande, wazifuate njia zao wenyewe, kila mmoja kwa faida yake, toka pande zote.
Kwahiyo unapoota..mbwa mara kwa mara..pengine amesimama getini tu..au anafukuza kitu au anafanya kitu fulani kwa ujasiri lakini hana shida na wewe.. hana mpango wa kukudhuru wewe..basi ni Mungu anakukumbusha kuwa uzidi kusisima vema katika nafasi yako kama mlinzi.
Lakini kama unaona mbwa huyo ni mwoga..anakimbizwa kimbizwa tu..anajificha ficha ujue huna nguvu rohoni..hivyo tengeneza mambo yako na Mungu ikiwa wewe ni mtumishi wa Mungu. Kwasababu Mungu anakuona kama mlinzi lakini bado hujakamilika katika kazi yako.
2) Maana ya pili ni kama Adui.
Kibiblia mbwa pia anawakilisha Adui.
Zaburi 22:16
“[16]Kwa maana mbwa wamenizunguka; Kusanyiko la waovu wamenisonga; Wamenizua mikono na miguu”.
Zaburi 22:20 “Uniponye nafsi yangu na upanga, Mpenzi wangu na nguvu za mbwa”.
Ukiota unakimbizwa na mbwa..au unashambuliwa nao. Au wanakutisha.au wanakuvizia kuchukua kitu chako..Ujue kuwa upo katika vita rohoni.
Ibilisi anataka kuiba kilicho chako.au kukuangamiza kabisa.. Hapo kama umeokoka huna budi kuwa mwombaji sana..mwambie Bwana akulinde na kukuhifadhli mbali na mashbulizi yote ya adui..pia zidisha kiwango chako cha kumtumikia Bwana ni ulinzi mkubwa sana.
Wafilipi 3:2 Jihadharini na mbwa, jihadharini na watendao mabaya, jihadharini na wajikatao.
Lakini kama hujaokoka..fanya hima mapema sana umrudie Mungu wako. Vinginevyo upo hatarini kuangamia kabisa.
3) Maana ya tatu ni kitu najisi.
Kibiblia mbwa pia anawakilisha kitu najisi” au kichafu .Mbwa huwa hajali ni nini anakula anaweza rudia hata matapishi yake biblia inasema hivyo katika.. Mithali 26:11..
Ni wanyama wasiostahili heshima yoyote..
Mathayo 15:26 Akajibu, akasema, Si vema kukitwaa chakula cha watoto na kuwatupia mbwa.
Mbwa hajali ni yupi anakutana naye katika kupata watoto..anaweza kutanana hata na mama yake.
Hivyo kwa ujumla ni kwamba mbwa anawakilisha pia watu waovu..waliodhambini ambao hawajali maisha yao ya kiroho hata kidogo.
Kwahiyo kama unaota mara kwa mara mbwa ambao huelewi wapo kwa lengo gani..leo unamwona hivi kesho vile…ujue kuwa ndivyo Mungu akuonavyo.
Tubu dhambi zako mgeukie Mungu wako kama wewe ni mwenye dhambi..kumbuka katika hali kama hiyo uliyopo sasa ukifa ujue ni moja kwa moja kuzimu..biblia inasema hivyo kwa watu walio hivyo rohoni..
Ufunuo 22:15 Huko nje wako mbwa, na wachawi, na wazinzi, na wauaji, na hao waabuduo sanamu, na kila mtu apendaye uongo na kuufanya.
Ikiwa upo tayari leo kumkaribisha Kristo ndani ya maisha yako akubadilishe basi fungua hapa kwa ajili ya kupokea mwongozo wa sala ya Toba..>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Bwana akubariki.
Kwa mgawanyo bora wa masomo download App hapa>> App wingu la mashahidi
Mada Nyinginezo:
Je! Mtu wa kwanza kufa alikuwa nani?.
Jibu: Kulingana na maandiko mtu wa kwanza kufa alikuwa ni HABILI, mwana wa ADAMU.
Mwanzo 4:8 “Kaini akamwambia Habili nduguye, [Twende uwandani].
Ikawa walipokuwapo uwandani, Kaini akamwinukia Habili nduguye, akamwua”.
Sababu ya Kaini kumuua Habili ndugu yake ilikuwa ni wivu. Kwani sadaka yake haikukubaliwa na Mungu lakini ya ndugu yake Mungu aliikubali kwasababu aliitoa katika vitu vilivyonona..na kutoka kwa wazaliwa wa kwanza.
Mwanzo 4:3 “Ikawa hatimaye Kaini akaleta mazao ya ardhi, sadaka kwa BWANA.
4 Habili naye akaleta wazao wa kwanza wa wanyama wake na sehemu zilizonona za wanyama. BWANA akamtakabali Habili na sadaka yake;
5 bali Kaini hakumtakabali, wala sadaka yake. Kaini akaghadhibika sana, uso wake ukakunjamana.
6 BWANA akamwambia Kaini, Kwa nini una ghadhabu? Na kwa nini uso wako umekunjamana?
7 Kama ukitenda vyema, hutapata kibali? Usipotenda vyema dhambi iko, inakuotea mlangoni, nayo inakutamani wewe, walakini yapasa uishinde”.
Roho ya Habili, ipo peponi sasa, yaani paradiso sehemu ya watakatifu..akingoja ufufuo wa watakatifu, utakaotokea katika siku za mwisho, wakati parapanda ya mwisho itakapolia.
Na pia tunajifunza tusiwe watu wasiomjali Bwana, kimatoleo kama Kaini, yeye alitoa tu ilimradi…lakini mwenzake alitoa katika vitu vilivyonona na katika wazao wa kwanza, pia tusiwe watu, wenye wivu kama Kaini.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
Je! Ni kosa tu la kugeuza shingo na kutazama nyuma ndilo lililomgharimu mke wa Lutu maisha?.. Bila shaka Mungu asingeweza kumhukumu kwa kosa hilo, ni wazi kuwa kuna jambo lingine la ziada alilifanya..
Leo tutajifunza nini maana ya kugeuka nyuma, na mke wa Lutu aligeukaje nyuma hata ikamgharimu maisha yake..
Awali ya yote hebu tusome mstari ufuatao…
Luka 9:61 “Mtu mwingine pia akamwambia, Bwana, nitakufuata; lakini, nipe ruhusa kwanza nikawaage watu wa nyumbani mwangu.
62 Yesu akamwambia, Mtu aliyetia mkono wake kulima, KISHA AKAANGALIA NYUMA, hafai kwa ufalme wa Mungu”.
Kwa mfano huo Bwana alitafsiri kuwa “kitendo cha kuamua kurudi nyuma baada ya kukusudia kumfuata yeye” ni sawa na “kutazama nyuma baada ya kudhamiria kwenda shambani”. Hivyo kutazama nyuma hapo, ni kumwacha Bwana Yesu kwa kitambo, kwenda kurekebisha mambo fulani kisha kumrudia.
Sasa mpaka kufikia hapo tutakuwa tumeshaanza kupata kuelewa nini maana ya mke wa Lutu kutazama nyuma.. Kwamba alimwacha Lutu na kurudi nyuma..
Lakini ili tulithibitishe hilo vizuri, hebu tusome tena maneno ya Bwana Yesu mahali pengine, ambapo aliieleza habari hiyo ya Mke wa Lutu vizuri zaidi..
Luka 17:28 “Na kadhalika, kama ilivyokuwa katika siku za Lutu, walikuwa wakila na kunywa, walikuwa wakinunua na kuuza, wakipanda na kujenga;
29 lakini siku ile Lutu aliyotoka Sodoma kulinyesha moto na kibiriti kutoka mbinguni vikawaangamiza wote.
30 Hivyo ndivyo itakavyokuwa siku ile atakayofunuliwa Mwana wa Adamu.
31 Katika siku ile, aliye juu ya dari, na vyombo vyake vimo ndani ya nyumba, asishuke ili kuvitwaa; NA KADHALIKA, ALIYE SHAMBANI ASIREJEE NYUMA.
32 MKUMBUKENI MKEWE LUTU”.
Hapo Bwana anaifananisha siku za kufunuliwa kwake na siku za Lutu, na anaelezea au anatoa ushauri jinsi ya kuokoka na ghadhabu ya Mungu kipindi itakapokaribia kumwagwa duniani kote, kama ilivyomwagwa katika miji ya Sodoma na Gomora.
Anasema siku hiyo “mtu aliye shambani asirejee nyuma”.. “maana akirudi huku atakutana na hatari itakayomgharimu maisha, hivyo abaki huko huko, au akimbie mbali zaidi”…na baada ya Bwana kusema maneno hayo anahitimisha kwa kusema “MKUMBUKENI MKEWE LUTU”.
Sasa jiulize kwanini aseme “Mkumbukeni mkewe Lutu”.. Maana yake kuna somo la kujifunza kutoka kwake, ili na sisi kipindi ghadhabu hiyo inakaribia kumwagwa duniani, tusiangamie kama yeye… Maana yake ni kwamba “mke wa Lutu alirejea nyuma”..aliangukia kwenye hilo kundi ambalo Bwana alisema, “aliye shambani asirejee nyuma”.. yeye alirejea nyuma na kukumbana na ghadhabu ya Mungu, ule moto na kiberiti na ile ardhi ya chumvi, ya Sodoma ambayo biblia inasema haiwezi kupandwa wala kumea, (Kumbukumbu 29:22-23), vikagandamana na mwili wake na kutengeneza umbile kama la mtu aliyesimama, kama nguzo, ambapo hata baada ya moto ule kuisha katika hiyo miji, na kila kitu kiteketea umbile lake lilibaki kama sanamu za kumbukumbu zinazotengenezwa na kuwekwa kwenye maingilio ya miji.
Hiyo yote ni kwasababu alirejea nyuma.. alianza kuitamani mikoba yake ya fedha aliyoiacha kule nyumbani.. Hakuwa na lengo la kurudi kuishi Sodoma, bali alivitamani vyombo vyake, mali zake, akazichukue na kisha aondoke nazo…ili huko aendako ziweze kumsaidia kuendesha maisha, lakini mambo yakabadilika, kabla ya kumaliza safari moto ulikuwa umeshamzunguka kila mahali.
Hiyo inatufundisha na sisi, tulioianza safari ya wokovu. Hii dunia tayari imeshatamkiwa hukumu, hakuna maombi yoyote yanayoweza kuifuta hukumu ya huu ulimwengu. Yaliyotamkwa na kuandikwa yatatimia kama yalivyo..
Hivyo kilichobaki kwetu ni sisi kuondoka na kujiokoa nafsi zetu, na katika safari yetu, hatupaswi kurejea nyuma..tunapaswa tukazane kuzidi kusonga mbele, kwasababu nyuma yetu, moto unazidi kusogea huku tuendako, hivyo tunakaza mwendo.
Kurejea nyuma ni kitendo cha kupiga hatua kabisa kuurudia ulimwengu.. ulikuwa umeshaushinda uzinzi lakini sasa umeurudia, ulikuwa umeshaishinda pombe na ulevi, na utukanaji, ulikuwa umeshaanza kumtumikia Mungu, lakini sasa umeacha, ulikuwa umeshaanza mambo yote ya ulimwengu, ikiwemo uvaaji mbaya, na kujipodoa..lakini sasa umerejea nyuma, umeanza kuyafanya hayo tena na ziaid ya hayo.. Bwana anakuambia.. “mkumbuke mkewe Lutu”..mkumbuke..mkumbuke..
Hakuna mtu mwingine yeyote Bwana aliyetuambia tumkumbuke katika biblia nzima… Ni huyu tu! Mke wa Lutu, ndiye aliyetuasa tumkumbuke…tusimsahau, maana yake tujifunze kwake.
Kama bado hujampokea Yesu maishani mwako mpokee leo, na kama tayari ulikuwa umeanza kurejea nyuma, basi ahirisha hiyo safari kabla hujafika mbali, kwasababu kuna wakati utatamani kumrudia Bwana lakini utashindwa, unyakuo wa kanisa upo karibu sana.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
Kati ya yale makanisa 7 tunayoyasoma katika kitabu cha Ufunuo, Kanisa la Thiatira, lilikuwa ni la tofauti sana, kwani lenyewe lilisifiwa sana na Bwana kwa jinsi lilivyokuwa linapanda viwango, siku baada ya siku, kiimani, kihuduma, pamoja na kiupendo, tofauti na makanisa mengine sita, hadi Bwana Yesu alilipongeza kwa kuliambia, matendo yake ya mwisho yamezidi yale ya kwanza..(Ufunuo 2:18-29)
Lakini pamoja na kuwa lilienda katika uaminifu huo, Shetani naye hakukaa nyuma. Bali alibuni njia ya kitofauti sana ya kuliangamiza, na njia yenyewe ndio hiyo ya kutumia MAFUMBO. Alibadili mbinu zake za kawaida, akawa anakuja tofauti na walivyotarajia. Na kwa njia hiyo alifanikiwa kulishusha kwa spidi kubwa kanisa lile, kwasababu baadhi yao walidhani kwamba wanaendelea vizuri na Mungu, kumbe wanamwabudu shetani moja kwa moja.
Leo kwa neema za Bwana tutajifunza baadhi ya FUMBO za shetani, wengi wetu hatuzijui ambazo anazitumia hata leo, na hizo zimewafanya watu wengi warudi nyuma, kama sio kuanguka kabisa kiroho.
Hizi ndio fumbo zake;
Wakati ule mtume Paulo anafika kwa mara ya kwanza, Mji huo wa THIATIRA, alikutana na kijakazi mmoja aliyekuwa na pepo la utambuzi, na lilipomwona Paulo, lilimshuhudia Paulo ukweli, kwamba yeye ni mtumishi wa Mungu aliyejuu, na liliendelea kufanya hivyo kwa muda mrefu tu, lengo lake likiwa ni kumpumbaza Paulo adhani ile ni roho ya Mungu ikimshuhudia, ili tu lisisumbuliwe kutenda kazi zake, Lakini mtume Paulo kwa kufunuliwa na Roho akatambua kuwa Yule sio Roho wa Mungu bali ni shetani, ndipo akalikemea likamtoka.
Mtendo 16:16 “Ikawa tulipokuwa tukienda mahali pale pa kusali, kijakazi mmoja aliyekuwa na pepo wa uaguzi akatukuta, aliyewapatia bwana zake faida nyingi kwa kuagua.
17 Akamfuata Paulo na sisi akipiga kelele, akisema, Watu hawa ni watumishi wa Mungu aliye juu, wenye kuwahubiria njia ya wokovu.
18 Akafanya hayo siku nyingi. Lakini Paulo akasikitika, akageuka akamwambia yule pepo, Nakuamuru kwa jina la Yesu Kristo, mtoke huyu. Akamtoka saa ile ile.
19 Basi bwana zake walipoona ya kuwa tumaini la faida yao limewapotea, wakawakamata Paulo na Sila, wakawakokota mpaka sokoni mbele ya wakuu wa mji;
Hata leo, Shetani anawajia watu kwa namna hii, na wao bila kujua kumbe tayari wameshanaswa katika mitego yake. Ndugu si kila habari ya kweli inatoka kwa Mungu, Nabii kukueleza habari sahihi za maisha yako, hata ibilisi anaweza kufanya hivyo. Mpime kwa Neno la Mungu, na matunda anayoyatoa ndani yake. Hicho ndio kigezo. Usiridhishwe na maneno tu, ridhishwa na maisha nyuma ya hayo maneno.
2) Anataka tudhani kuwa hawezi kuwepo kanisani:
Hili hili kanisa la Thiatira, lilidhani hivyo, Mpaka Bwana Yesu alipolifumbua macho na kuliambia kuna mwanamke Yezebeli katikati yao, (Ambaye anawakilisha watumishi wa uongo waletao mafundisho mageni ndani ya kanisa), Anawafundisha njia potofu.
Ufunuo 2:18 “Na kwa malaika wa kanisa lililoko Thiatira andika; Haya ndiyo anenayo Mwana wa Mungu, yeye aliye na macho yake kama mwali wa moto, na miguu yake mfano wa shaba iliyosuguliwa sana.
19 Nayajua matendo yako na upendo na imani na huduma na subira yako; tena kwamba matendo yako ya mwisho yamezidi yale ya kwanza.
20 Lakini nina neno juu yako, ya kwamba wamridhia yule mwanamke Yezebeli, yeye ajiitaye nabii na kuwafundisha watumishi wangu na kuwapoteza, ili wazini na kula vitu vilivyotolewa sadaka kwa sanamu.
21 Nami nimempa muda ili atubu, wala hataki kuutubia uzinzi wake.
22 Tazama, nitamtupa juu ya kitanda, na hao wazinio pamoja naye, wapate dhiki kubwa wasipotubia matendo yake;
23 nami nitawaua watoto wake kwa mauti. Na makanisa yote watajua ya kuwa mimi ndiye achunguzaye viuno na mioyo. Nami nitampa kila mmoja wenu kwa kadiri ya matendo yake.
24 Lakini nawaambia ninyi wengine mlioko Thiatira, wowote wasio na mafundisho hayo, WASIOZIJUA FUMBO ZA SHETANI, kama vile wasemavyo, Sitaweka juu yenu mzigo mwingine”.
Hata leo, wapo watu wa Mungu wazuri, wanabidii kweli katika kumtafuta Mungu, lakini hawajui kuwa viongozi wao wanawakosesha kwa Mungu pasipo wao kujua, kwamfano, wambiwapo bikira Maria anaweza kuwa mpatanishi wako na Mungu, hayo ni machukizo, ufundishwapo mafundisho ya kutumia mafuta ya upako, chumvi, sabuni n.k. kana kwamba hivyo vitu vinatosha kumponya mtu, hizo ni ibada za sanamu. Lakini kwasababu unamwamini kiongozi wako kwamba hawezi kukosea, unamtii, ukidhani Mungu atakuridhia na wewe. Kuwa makini na kila fundisho geni unaloletewa na kiongozi wako.
3) Tudhani kuwa sikuzote anatisha na mwenye mapembe:
Wengi ukiwaambia shetani yupoje moja kwa moja, wanachowaza katika akili yao ni kitu cha kutisha chenye mapembe, na kichwa cha nyoka. Ni kweli hivyo vitu vinamwakilisha yeye. Lakini yeye hayupo hivyo, kumbuka, alikuwa ni malaika kama malaika wengine, na alipofukuzwa hakuondolewa chochote alichokuwa nacho, hata nguvu zake, bali alifukuzwa tu kwenye makao yake mbinguni.
Kwahiyo sasa alipo bado anatumia njia yake ya uzuri kuwadanganya watu wengi. Hii imewafanya watu wadhani shetani yupo katika vitu vichafu chafu, au vibaya baya, na shida na umaskini, vichaa, na wagonjwa.. Lakini Siku ile alimpofuata Bwana Yesu ili kumjaribu alikuja kama tajiri, mwenye milki zote za ulimwengu. Biblia inasema anaweza kujibadilisha kuwa malaika wa Nuru,
Kwahiyo usitazamie kuwa wakati wote atakufuata tu katika ndoto mbaya usiku au katika uchawi, au katika magonjwa. Wakati mwingine atakuja na amani feki, na utulivu, na utajiri. Ukadhani ni Mungu huyo kumbe ni shetani, anakutega ili kukuangamiza. Usikurupukie kila mafanikio mazuri, au fursa iliyopo mbele yako.
4) Tudhani kuwa hawezi kuzitetea njia za Mungu.
Tunaweza kudhani shetani hawezi, kujifanya anaisapoti kazi ya Mungu, au kuitetea, unafki huo anao. Wakati ule Bwana Yesu alipowaambia wanafunzi wake kuhusiana na mateso yake, utaona wakati huo huo shetani akamwingia Petro kujifanya, yeye ni mtetezi wa Bwana..
Mathayo 16:22 “Petro akamchukua, akaanza kumkemea, akisema, Hasha, Bwana, hayo hayatakupata.
23 Akageuka, akamwambia Petro, Nenda nyuma yangu, Shetani; u kikwazo kwangu; maana huyawazi yaliyo ya Mungu, bali ya wanadamu”.
Ni kawaida yake, hata wakati akina Zerubabeli wanajenga hekalu la Bwana, maadui zao walijitokeza kwa kivuli cha kuwa wanataka kuwasaidia ujenzi, lakini walipofukuzwa ndio hapo wakaonyesha makucha yao, wao ni akina nani.(Ezra 4)
Shetani akishaona una kitu ndani yako cha ki-Mungu atakuja kwa njia ya msaada au utetezi, kuwa makini sana, na misaada unayoipokea katika utumishi wako au unachokifanya. Hakikisha unaifahamu na unaelewa kwa undani nyuma yake kuna roho gani. Vinginevyo utaingia katika matatizo makubwa sana.
5) Tudhani kuwa hawezi kukubali kushindwa.
Si kila wakati ibilisi atakuja kama mpingamizi, au mharibifu, hapana, lengo lake litakuwa ni hilo ndio, lakini atakuja kwa ujanja wa kujionyesha ameshindwa wewe una nguvu nyingi, atajiweka chini yako, ajifanye kuwa yeye siku zote ni mnyonge tu.. lakini kumbe ameshakuweza. Ndicho kilichomtokea Yoshua alipovuka Jordani, sababu mojawapo ya yeye kushindwa kuwaondoa wenyeji wote wa Kaanani ilikuwa ni hiyo, ya kumsikiliza shetani unyonge wake . Pale walipojifanya, wametokea nchi ya mbali, wanaomba sharti ya amani wasidhuriwe, kwasababu wamesikia ushujaa wao, kumbe ni watu wa karibu tu (Yoshua 9)
Leo hii mapepo yanaweza kukusifia sana, kujishusha, kusema wewe ni mkuu, unatisha,una upako, una nguvu, yakajifanya yanatetemeka mbele zako, ili tu uchukulie mambo rahisi rahisi, lakini kumbe tayari yanatenda kazi kwa nguvu ndani yenu bila kujua.. Usikisikilize kilio cha shetani. Ni mwongo.
6) Tudhani kuwa hajui mambo mengi.
Shetani anayotabia ya kujifanya mjinga, hajui kila kitu. Pale Edeni alimfuata mwanamke na kuanza kumwambia Ati, hivi ndivyo Mungu alivyosema, msile “matunda ya miti yote”?. Anajifanya kama hajui, ni matunda gani yaliyokatazwa, na ndio maana anasema “miti yote”. Anakusubiria utiririke, ndipo akunasie mahali fulani.
Hila hii anayo hata sasa, huyo kijana anakuja anajifanya hajui uzinzi ni nini..anataka taarifa kwako, umwambie kwa muhtasari, ndipo hapo akupeleke mpaka kwenye vilindi vya dhambi. Kila jambo baya, kabla ya kukuingiza, atataka wewe ndio umfundishe kwanza.
Kwahiyo hiki ni kipindi cha kuishi kwa umakini, tuzijue FUMBO ZA IBILISI. Ili asifanikiwe kutunasa popote pale. Tuzitambue fikra zake, tumpinge.
Swali ni je! Umeokoka? Je! Unaouhakika kuwa Kristo akirudi leo hii, utakwenda naye mbinguni? Kumbuka hizi ni siku za mwisho kweli kweli, siku yoyote unyakuo utapita, na ibilisi analijua hilo, na ndio maana anafanya kazi kwa nguvu nyingi sana kutafuta watu wa kuwameza.
Hivyo tubu dhambi zako kwa kumaanisha kabisa kumfuata Yesu. Ili akuweke huru.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
Jina la Bwana Yesu Kristo libarikiwe.
Je unajua ni kwanini Bwana Yesu aliwaagiza Mitume wake pamoja na sisi wote kwamba tuende ulimwenguni kote tukawafanye watu wote kuwa WANAFUNZI na si WAKRISTO? (Mathayo 28:19).
Je! Unajua neno Ukristo mara ya kwanza lilizaliwa wapi?
Tusome Matendo 11:26..
Matendo 11:26 “hata alipokwisha kumwona akamleta Antiokia. Ikawa kwa muda wa mwaka mzima wakakusanyika pamoja na kanisa na kuwafundisha watu wengi. Na WANAFUNZI waliitwa WAKRISTO kwanza hapo Antiokia”.
Umeona hapo?..Maana yake kabla akina Petro, akina Yohana, na wengine wote waliomwamini Yesu kujulikana kama wakristo, walikuwa wanajulikana kama wanafunzi, hapo kabla.
Maana yake kuwa mkristo ni kuwa MWANAFUNZI WA YESU. Hili ni jambo la muhimu kujua sana.
Sasa swali tunakuwaje wanafunzi wa Bwana Yesu?..au watu wa kanisa la kwanza walikuwa wanafanyikaje kuwa wanafunzi?.
Bwana Yesu alitoa vigezo..Katika kitabu cha Luka..
Luka 14:27 “Mtu ye yote asiyeuchukua msalaba wake na kuja nyuma yangu, hawezi kuwa mwanafunzi wangu”
Sasa tukirudi katika Matendo biblia inasema “Wanafunzi waliitwa wakisto kwa mara ya kwanza hapo Antiokia”..Maana yake mkristo yeyote ni mwanafunzi.
Kwa mantiki hiyo basi sentensi ya Bwana aliyoisema katika Luka 14:27 ni sahihi kabisa kuiweka hivi…
“Mtu ye yote asiyeuchukua msalaba wake na kuja nyuma yangu, hawezi kuwa MKRISTO”.
Umeona hapo?..Hebu tosegee tena mbele kidogo..
Luka 14:26 “Makutano mengi walipokuwa wakifuatana naye, aligeuka, akawaambia,
26 Kama mtu akija kwangu naye hamchukii baba yake, na mama yake, na mke wake, na wanawe, na ndugu zake waume na wake; naam, na hata nafsi yake mwenyewe, hawezi kuwa mwanafunzi wangu”.
Maana ya hiyo sentensi ni kwamba..
26 “Kama mtu akija kwangu naye hamchukii baba yake, na mama yake, na mke wake, na wanawe, na ndugu zake waume na wake; naam, na hata nafsi yake mwenyewe, HAWEZI KUWA MKRISTO”.
Kuchukia wazazi kunakozungumziwa hapo kuwachukia kwa chuki, bali kuchukia mawazo yao au mipango yao inayokinzana na mapenzi ya Mungu, kwamfano mzazi au ndugu anakuambia inakupasa urithi mikoba ya uchawi, au urithi chuki zake kwa mtu fulani, hapo Bwana anasema hatuna budi kuyachukia hayo mawazo na kuyakataa na kutoshirikiana nao hata kama watakutenga..hapo ni sawa na umewachukia ndugu zako, Kristo anakokuzungumzia..na ndio vigezo vya kuwa mwanafunzi yaani MKRISTO.
Tusogee tena mbele kidogo..
Bwana anasema..
Luka 14:33 “Basi, kadhalika kila mmoja wenu asiyeacha vyote alivyo navyo, hawezi kuwa mwanafunzi wangu”.
Kufuatia Matendo 11:26 inayosema kuwa Wanafunzi ndio wakristo..basi ni sahihi kabisa kuyaweka haya maneno ya Bwana katika hii Luka 14:33 hivi…
“Basi, kadhalika kila mmoja wenu asiyeacha vyote alivyo navyo, HAWEZI KUWA MKRISTO”.
Hiyo ikifunua kuwa kumbe miongoni mwa lile kundi lote lililokuwa linamfuata Bwana, wakristo walikuwa ni wachache sana..yaani ni wale wanafunzi wake tu, wa kike na wakiume, ambao walijikana nafsi na kujitwika misalaba yao na kumfuata Bwana Wengine wote hawakuwa wakristo.
Na maandiko yanasema Yesu ni yeye yule, jana na leo na hata milele. (Waebrania 13:8).
Ikiwa na maana kuwa kama vigezo vyake vya mtu kuwa mwanafunzi (yaani mkristo) vilikuwa ni kujikana nafsi na kubeba msalaba…basi vitakuwa ndio hivuo hivyo hata leo, kwasababu yeye ni yule yule habadiliki..
Waebrania 13:8 “Yesu Kristo ni yeye yule, jana na leo na hata milele”.
Je! Wewe ni MKRISTO?…Umejikana nafsi? Umeuchukia ulimwengu na kuuacha?..kama bado basi fahamu kuwa wewe si mkristo, haijalishi unasali katika dhehebu kubwa au umebatizwa, bado sio mkristo.
Kama bado unalewa, au unazini, au unavaa nguo za kubana na kuonyesha maungo yako, bado sio mkristo..
Amua leo kujikana nafsi na kuubeba msalaba wako, wacha dunia ikuone umechanganyikiwa lakini wewe unajua unayafanya mapenzi ya Baba yako aliye mbinguni..
Bwana Yesu alisema..“Kwa kuwa itamfaidia mtu nini kuupata ulimwengu wote, akipata hasara ya nafsi yake? ( Marko 8:36 ).
Itakufaidia nini uonekane wa kisasa halafu huendi mbinguni??
Bwana atupe macho ya kuona.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp
Mada Nyinginezo:
Kibiriti tofauti na kinavyojulikana leo kwamba, ni kipande kidogo cha boksi kilichojaa chiti zinazotumika katika kuwashia moto. Lakini tafsiri halisi ya “kibiriti” au “kiberiti” sio hiyo. Kibiriti ni aina ya mawe, yanayopatikana duniani, yajulikanayo kwa jina hilo la kibiriti au Salfa..Kwa lugha ya kiingereza ni “Sulfur”.
Mawe haya kwa mwonekano yana rangi ya “manjano iliyofifia”..Tabia ya mawe haya ni kwamba yanawaka “kiwepesi” kama vile mafuta ya taa yanavyowaka kiwepesi yanapokutana na moto.. kadhalika na mawe haya ni myepesi kuwaka yanapokutana na moto.
Katika hali yake ya asili yanapokutana na moto kidogo tu! Yanaanza kuyeyuka taratibu taratibu na mwisho kuwa Uji mzito mweusi, kama tope!..ambao ni wa moto sana, usiozimika kirahisi, mfano wa Magma ya volkano. Lakini pia jiwe hilo hilo, likipelekwa kiwandani linaweza kuchanganywa na malighafi nyingine kutengeneza bidhaa nyingine zinazowaka kirahisi kama “Njiti za kiberiti” au “Unga wa risasi”. Lakini katika hali yake ya asili jiwe hilo la Salfa(kiberiti) likichomwa bila kuchanganywa na kitu kingine chochote, linayeyuka na kuwa tope zito la moto.
Lakini tukirudi kwenye biblia tunana sehemu kadhaa jiwe hili la Salfa(kiberiti) likitajwa.
Sehemu ya kwanza lilitajwa kipindi cha Sodoma na Gomora, wakati Bwana alipoiangamiza miji ile kwa moto. Biblia inasema moto na kibiriti vilishuka kutoka mbinguni.
Luka 17:28 “Na kadhalika, kama ilivyokuwa katika siku za Lutu, walikuwa wakila na kunywa, walikuwa wakinunua na kuuza, wakipanda na kujenga;
29 lakini siku ile Lutu aliyotoka Sodoma KULINYESHA MOTO NA KIBIRITI kutoka mbinguni vikawaangamiza wote”.
Kiberiti kinachozungumziwa hapo ni hayo mawe ya Salfa yaliyochanganyikana na moto, ambayo yalishuka kutoka juu..Na yaliposhuka moja kwa moja yakaanza kuyeyuka na kuwa TOPE ZITO JEUSI kama la volcano na kuchoma kila kitu.
Mpaka hapo utakuwa umeshaanza kuelewa kwanini Jehanamu ya moto, sehemu nyingine inafahamika kama ZIWA LA MOTO. Kwasababu huwezi kutaja neno ziwa bila kumaanisha “kimiminika” hivyo ziwa la moto maana yake ni “ni moto mwingi ulio katika mfumo wa kimiminika” mfano wa huo moto wa KIBIRITI (Salfa).
Ufunuo 21:7 “Yeye ashindaye atayarithi haya, nami nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwanangu.
8 Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ZIWA LIWAKALO MOTO NA KIBERITI. Hii ndiyo mauti ya pili”.
Utasoma tena neno hilo katika..
Ufunuo 14:9 “Na mwingine, malaika wa tatu, akawafuata, akisema kwa sauti kuu, Mtu awaye yote akimsujudu huyo mnyama na sanamu yake, na kuipokea chapa katika kipaji cha uso wake, au katika mkono wake,
10 yeye naye atakunywa katika mvinyo ya ghadhabu ya Mungu iliyotengenezwa, pasipo kuchanganywa na maji, katika kikombe cha hasira yake; NAYE ATATESWA KWA MOTO NA KIBERITI mbele ya malaika watakatifu, na mbele za Mwana-Kondoo.
Na pia Ufunuo 19:30 inazungumzia jambo hilo hilo…
Ufunuo 19:20 “Yule mnyama akakamatwa, na yule nabii wa uongo pamoja naye, yeye aliyezifanya hizo ishara mbele yake, ambazo kwa hizo aliwadanganya watu wale walioipokea ile chapa ya huyo mnyama, nao walioisujudia sanamu yake; hao wawili wakatupwa wangali hai katika lile ZIWA LA MOTO LIWAKALO KWA KIBERITI;
Na mwisho neno hilo limetajwa katika…
Ufunuo 20:10 “Na yule Ibilisi, mwenye kuwadanganya, AKATUPWA KATIKA ZIWA LA MOTO NA KIBERITI, alimo yule mnyama na yule nabii wa uongo. Nao watateswa mchana na usiku hata milele na milele”.
Sasa kwanini biblia imesema shetani na malaika zake WATATESWA katika Moto na Kiberiti, na SI WATACHOMWA TU!!.
Ni kwasababu Moto wa kiberiti ni tofauti na moto wa kawaida, moto wa kawaida wenyewe unaunguza tu! Na kuteketeza, lakini moto ulio katika mfumo wa kimiminika, tena kama uji uji huo ni unatesa.. Ndio maana kuungua kwa moto wa kawaida ni heri kuliko kuungua kwa vimiminika kama maji au uji..
Wanaofanya kazi za kuyeyusha Salfa(kibiriti) wanakuwa katika uangalifu mkubwa sana kwasababu wanasema moto ule ni mbaya kuliko moto mwingine wowote kwasababu “ule uji wake unapogusa mwili unakuwa unagandamana na ngozi” kwahiyo ili kuuondoa ni lazima ngozi ichubuke, na unakuwa na maumivu makali sana yanayotesa. Ndicho kilichowatokea watu wa Sodoma na Gomora, (walikufa kwa mateso na si kwa kuchomeka tu basi!.)
Na ndicho kitakachowakuta watu wote watakaotupwa katika lile ziwa la Moto.. watateswa katika ziwa la moto.
Swali ni je!, umempokea Yesu?.. Maandiko yanasema.. “Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ZIWA LIWAKALO MOTO NA KIBERITI.”
Je na wewe ni miongoni mwa wachukizao?, ni miongoni mwa wachawi, ni miongoni mwa wazinzi na waabudu sanamu?. Kama ndio!, basi tubu leo kwasababu Neema ya Kristo bado ipo, Ziwa la moto kaandaliwa shetani na malaika zake lakini si sisi!, lakini endapo tukiasi kama shetani alivyoasi basi na sisi tutaadhibiwa vile vile kama wao katika ziwa la moto.
Huko ni sehemu ya Mateso, moto ule ni kwa lengo la kutesa, na sio kuchoma tu!.
Bwana atusaidie tusifike huko, bali tuishi maisha ya kumpendeza yeye na kuyaishi maagizo yake.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
(Moto na kiberiti, www.wingulamashahidi.org)
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
Kwanini Mungu awachome watu kwenye ziwa la moto na hali yeye ndiye aliyewaumba?
Hili ni swali ambalo linaulizwa na wengi, hususani watu ambao walimwekea Mungu nadhiri huko nyuma lakini mwisho wa siku wamejikuta hawawezi kuzitoa.
Sasa kabla ya kwenda kuona kama msamaha upo au haupo, Jambo la kwanza unalopaswa kufahamu kuhusu nadhiri ni kwamba lile ni tendo la hiyari ambalo mtu anamwekea Mungu mwenyewe, na hapo ndipo Mungu anataka umakini sana kwasababu hakumlazimisha kufanya hivyo.
Biblia inasema ni heri, usiweke kabisa nadhiri kuliko kuiweka, halafu ukashindwa kuitoa,
Mhubiri 5: 4 “Wewe ukimwekea Mungu nadhiri, usikawie kuiondoa; kwa kuwa yeye hawi radhi na wapumbavu; basi, uiondoe hiyo uliyoiweka nadhiri.
5 Ni afadhali usiweke nadhiri, Kuliko kuiweka usiiondoe”.
Unaona hapo? Mungu anasema yeye hawi radhi na wapumbavu. Ikiwa na maana kuwa nadhiri ambayo haitolewi kwa wakati, Ni haki ya Mungu kumwadhibu huyo mtu kwa jinsi atakavyo yeye.
Kwahiyo kabla hujatamka nadhiri yoyote kwa kinywa chako mbele za Mungu, hakikisha kwanza unaelewa unachokitamka, na una uwezo wa kukisimamia.Biblia inasema..
Mithali 20: 25 “Ni mtego, mtu aseme kwa haraka, Kitu hiki ni wakfu; Na baada ya kuweka nadhiri kuuliza-uliza habari”.
Sasa tukirudi kwenye kiini cha somo, Je! Kutotimiza nadhiri zako, Mungu hawezi kukusamehe?
Tukumbuke katika biblia ni dhambi moja tu isiyosameheka kwa Mungu, na dhambi yenyewe ni “Kumkufuru Roho Mtakatifu” Lakini hiyo haimaanishi kuwa adhabu za dhambi nyingine hazipo hapana.. Kuna dhambi ambazo Mungu atakusamehe bila adhabu, lakini pia zipo dhambi ambapo Mungu atakusamehe pamoja na adhabu. Kwa urefu wa somo hilo fungua hii link>>>>>> https://wingulamashahidi.org/2018/07/17/dhambi-ya-mauti/
Sasa ikiwa mtu hajamtimizia Mungu nadhiri zake, anaweza akatubu na pengine Mungu akamsamehe kabisa na mbinguni akaenda, lakini adhabu ya kosa lake, bado akaitumikia hapa hapa duniani, adhabu inaweza ikawa pengine hata kifo,n.k.
Lakini bado tukirudi katika biblia tunaona wapo watu ambao walihalifu nadhiri zao, lakini hawakuadhibiwa na Mungu, mmojawapo ni Daudi wakati ule anataka kwenda kumuua Nabali, aliapa kwa Mungu kwamba kama hatamuua Nabali na nyumba yake yote, basi Mungu amfanyie yeye hivyo . Lakini tunaona hakumuua Nabali alipofika katika nyumba ile, na Mungu vilevile hakumuua Daudi na nyumba yake kwa kutotimiza nadhiri zake. Hizo ndizo zinazojulikana kama nadhiri wa wapumbavu.
1Samweli 25: 22 “Mungu naye awafanyie hivyo adui za Daudi, na kuzidi, nikimwachia katika wote walio wake hata mtoto mume mmoja, kutakapopambazuka asubuhi”.
Sehemu nyingine, utaona ni wakati Sauli anapigana na wafilisti naye pia aliweka nadhiri kuwa mtu yeyote asionje chochote mpaka atakapomaliza kupigana na wafilisti na kuwashinda, atakayeonja atauawa lakini mwanae Yonathani, hakusikia agizo hilo, yeye akala, na Sauli alipopata taarifa akataka kumwangamiza, lakini Israeli wakamzuia, kwasababu yeye ndiye aliyeleta wokovu katika taifa. Na baada ya hapo hatuoni kama Mungu alimwangamiza Sauli kwa kuhalifu agizo lile.(Soma 1Samweli 14)
Lakini tunaona pia kulikuwa na mwamuzi mwingine aliyeitwa Yeftha, yeye alimwekea Mungu nadhiri kuwa atakaporudi kutoka vitani na ushindi, basi chochote kitakachotokea cha kwanza mbele yake, atamtolea Mungu kama sadaka ya kuteketezwa. Hakufikiria kwamba anaweza kutokea mtu mbele yake..
Lakini kweli Mungu alipomfanikisha katika vita, kitu cha kwanza kutokea mbele yake, hakikuwa ng’ombe, au mbuzi, bali binti yake wa pekee. Hivyo ikambidi aende kumchinja mwanawe na kumtoa kafara kwa Mungu, japo ambalo ni kinyume kabisa na maagizo ya Mungu, na ni machukizo. Yeftha Alikuwa na uwezo wa kuizuia nadhiri yake ya kipumbavu, kama alivyofanya Daudi au Sauli, lakini alitimiza nadhiri isiyokuwa na maana yoyote mbele za Mungu.
Hivyo, Mungu anaweza akaadhibu au asiadhibu, yote yapo katika uwezo wake mwenyewe..
Lakini katika yote, Mungu tangu zamani kwa hekima yake alishaona kuwa wapo watu wake, ambao watakuja kutamka nadhiri zao bila hata ya kufikiria, na ili kuwaepusha na adhabu, akampa maagizo Musa, juu ya nadhiri za wapumbavu kama hizo akasema..
Walawi 5:4 “au, kama mtu akijiapisha, kwa kutamka haraka kwa midomo yake, kutenda uovu, au kutenda mema, neno lo lote mtu atakalolitamka kwa kiapo pasipo kufikiri, na neno hilo likamfichamania; hapo atakapolijua, ndipo atakapokuwa na hatia katika mambo hayo mojawapo;
5 kisha itakuwa, hapo atakapokuwa na hatia katika mambo hayo mojawapo, ndipo atakapoliungama jambo hilo alilolikosa;
6 naye atamletea Bwana sadaka yake ya hatia kwa ajili ya hiyo dhambi yake aliyoifanya, mwana-kondoo wa kike, au mbuzi mke, kutoka katika kundi lake, kuwa ni sadaka ya dhambi; kisha kuhani atamfanyia upatanisho kwa ajili ya hiyo dhambi yake”.
Umeona?, Mtu kama huyo ambaye alitamka tu maneno bila kufikiri hatma yake itakuwaje mbeleni, pengine mwingine alisema mimi sitaoa au kuolewa maisha yangu yote, bila kupiga gharama zake. Mungu alimwambia Musa, mtu huyo atubu, kisha sio kutubu tu, bali aambatanishe na sadaka yake ya makosa kama vile atakavyoelekezwa na kuhani.
Hii ikiwa na maana, hata sasa wapo watu waliotamka nadhiri zako mbele za Mungu, lakini sasa wameshindwa kuzitoa, jambo la kwanza wanalopaswa kulifanya hapo ni kutubu kwa kumaanisha kabisa, sio kutubu kwa dakika mbili au tatu, hapana ni kulia kwa kumaanisha mbele za Mungu kwa kipindi fulani (ukikumbuka kuwa Mungu hawi radhi na wapumbavu, anaweza kukuondoa duniani kwa kosa hilo tu)..Kisha baadaye ukishamaliza maombi yako ya toba ya muda mrefu, andaa sehemu nono ya ulichonacho nacho (yaani sadaka), kisha kipeleke madhabahuni pa Mungu kwa ishara ya unyenyekevu kwa hofu nyingi.
Na baada ya hapo Mungu atakusamehe.
Shalom.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp
Mada Nyinginezo:
Jina la Bwana Yesu libarikiwe, karibu tujifunze biblia, Neno la Mungu wetu.
Leo tutajifunza, mambo Matatu ambayo, kama Mkristo ukiyarekebisha hayo basi uchumi wako utaimarika zaidi.
1. KUWA MWAMINIFU KWA MUNGU WAKO.
Dawa ya kwanza ya mafanikio yoyote yale, yawe ya kimwili au kiroho, ni kuwa MWAMINIFU KWA BWANA.
Mithali 3:7
“ Usiwe mwenye hekima machoni pako;
Mche BWANA, ukajiepushe na uovu.8 Itakuwa afya mwilini pako,
Na mafuta mifupani mwako.
Kumcha Bwana ni kuishi maisha matakatifu na yanayompendeza yeye, ambayo Nuru yako inakuwa inaangaza kila mahali.
Jambo moja kubwa wakristo wengi wasilolijua ni kwamba, tumewekwa ulimwenguni ili tuhubiri injili, licha ya kwamba Mungu anataka sisi tupate faida katika mambo yetu kutoka kwake, lakini pia Mbingu inategemea kupata faida kutoka kwetu.. Na faida yenyewe ni sisi kuwavuta wengine waingie katika ufalme.
Kwahiyo maana yake ni kwamba kama wewe unafanya biashara, au kazi yoyote ya kuajiriwa au kujiajiri.. Mungu anategemea maisha yako yawe sababu ya kuwavuta wengine.
Hivyo Bwana akikuamini, atakuvutia watu wengi kwako, kama ni wateja au watu wa fursa wakujie, lengo si tu waje kununua bidhaa zako, au kukupa wewe fursa, bali Mungu anawasogeza kwako ili wapate kuiona nuru yako na wamgeukie Mungu na kutubu..Hivyo wewe unafanyika daraja la wao kumfikia Mungu zaidi.
Lakini kama wewe maisha yako hayana ushuhuda wowote,maana yake ni maisha ya uzinzi, ya wizi, ya ulevi, utukanaji, umbea, usengenyaji n.k.
maana yake Mungu akikuletea watu, ni sawa na kampelekea shetani kondoo..Hivyo ili awalinde watu wake wasizidi kupotea, anazuia wateja wasije kwako, kwasababu utawaharibu kwa tabia zako..na Mungu hapendi watu wake wapotee.
Atawazuia wasije kwako, na atawapeleka kwa watu wengine wenye staha zaidi..Huku nyuma wewe utabaki kufikiri umelogwa, kumbe ni wewe mwenyewe umejiharibu kwa kutokuwa mwaminifu kwa Mungu wako.
Mathayo 5:14
“Ninyi ni nuru ya ulimwengu. Mji hauwezi kusitirika ukiwa juu ya mlima.15 Wala watu hawawashi taa na kuiweka chini ya pishi, bali juu ya kiango; nayo yawaangaza wote waliomo nyumbani.
16 Vivyo hivyo nuru yenu na iangaze mbele ya watu, wapate kuyaona matendo yenu mema, wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni”.
Angaza Nuru yako ili milango ifunguke.
2. KUWA MWAMINIFU KATIKA KAZI UNAYOIFANYA.
Hili ni jambo la pili ambalo, ni muhimu kulijua.
Wengi wetu hatujui kuwa Mungu si Mungu wa kuwadhuru watu, bali wa kuwapatia watu mema.. Mteja yeyote Mungu anayemleta kwako, ni kwasababu Mungu anataka apate huduma bora ya viwango, ili aweze kumshukuru Mungu baada ya hapo, na Mungu apokee shukrani zake..
lakini hawezi kumleta kwako wewe unayeuza kitu kilichoisha muda wake wa matumizi (kime-expire). Hapo Mungu atakuwa muuaji na mkatili na si Mungu mwenye fadhili..
Alisema..
Mathayo 7:9
“9 Au kuna mtu yupi kwenu, ambaye, mwanawe akimwomba mkate, atampa jiwe?10 Au akiomba samaki, atampa nyoka?
11 Basi ikiwa ninyi, mlio waovu, mnajua kuwapa watoto wenu vipawa vyema, je! Si zaidi sana Baba yenu aliye mbinguni atawapa mema wao wamwombao?”
Hiyo ndio maana watu wateja hawawezi kuja kwako, kwasababu Mungu hawezi kuwaongoza watoto wake kwenda kula sumu, au vitu vilivyo chini ya ubora..vinginevyo atakuwa mwongo hapo aliposema.. “Basi ikiwa ninyi, mlio waovu, mnajua kuwapa watoto wenu vipawa vyema, je! Si zaidi sana Baba yenu aliye mbinguni atawapa mema wao wamwombao?”.
Hebu tengeneza picha wewe umeamka asubuhi, na kumwomba Baba akulinde na yule mwovu na pia akupe riziki njema..halafu unatoka hapo Mungu anakuongoza kwenda kununua Soda iliyo-expire! Kwenye duka la mtu fulani…huyoo Mungu si atakuwa mkatili sana?..
Hivyo ili Mungu kumpa mtoto wake kipawa chema sawasawa na Neno lake hilo, atamwepusha kuja kwenye duka lako, au kukupa wewe ajira..badala yake anampeleka kwenye duka lingine au kumpa mtu mwingine ajira ambaye atatoa huduma iliyo bora na kuleta faida katika ufalme wa mbinguni.
Hiyo ndio sababu wakristo wengi Mungu anaifunga milango ya riziki katika biashara zao, au katika mambo yao mengine na kuishia kudhani wamelogwa, na kuzunguka huku na huko kutafuta maombezi kumbe ni kwasababu wao wenyewe sio waaminifu katika kazi zao na hawatoi huduma iliyo bora!.
Na vile vile kuwa mwaminifu katika kumtolea Mungu, maandiko yanasema wote wasiomtolea Mungu zaka ni wezi, wanamwibia Mungu..hivyo Mungu hawezi kuwabariki wezi.
Malaki 3:8 “Je! Mwanadamu atamwibia Mungu? Lakini ninyi mnaniibia mimi. Lakini ninyi mwasema, Tumekuibia kwa namna gani? Mmeniibia zaka na dhabihu.
9 Ninyi mmelaaniwa kwa laana; maana mnaniibia mimi, naam, taifa hili lote”
Mithali 3:9 “Mheshimu BWANA kwa mali yako,Na kwa malimbuko ya mazao yako yote.
10 Ndipo ghala zako zitakapojazwa kwa wingi, Na mashinikizo yako yatafurika divai mpya”.
3. IMARISHA KAZI YAKO, AU UJUZI WAKO.
Hili ni jambo lingine pia la muhimu kujua.
Wengi wetu hatupendi kuziimarisha kazi zetu, au ni walegevu katika kuziimarisha, wakati mwingine tukidhani si mpango wa Mungu.
Lakini leo nataka nikuambie kuwa kuiimarisha kazi yako, ni jambo la muhimu sana na la kimaandiko.
Kila siku buni na tafuta mbinu mpya na ongeza ujuzi katika shughuli unayojishughulisha nayo au unayoifanya..hayo ni mapenzi ya Mungu pia!
Bwana Mungu baada ya kuimaliza kazi yake ya uumbaji pale Edeni, alipumzika, lakini baada ya kipindi fulani alinyanyuka tena na kusema..”Si vyema mtu huyu awe peke yake nitamfanyizia msaidizi wa kufanana naye”.Ndipo akamletea Hawa kama msaidizi.
Kadhalika na sisi hatuna budi kusema siku zote “si vyema kazi hii ikabaki yenyewe, basi niongeze nyingine kama hii, na nyingine na nyingine”.
Si vyema kazi hii iwe kama ilivyokuwepo mwaka jana, basi nitaiimarisha hivi na hivi..si vyema ujuzi huu nilionao nikaendelea nao, basi nitauongeza tena na tena..
Kwa kufanya hivyo, Bwana atakubariki kwasababu na yeye pia anafanya matengenez kila siku katika maisha yetu.
Haya ndiyo mambo makuu matatu yanayozuia uchumi wetu kusonga mbele.
Na yaliyo ya muhimu zadi ni hayo mawili ya kwanza.
Tofauti na wengi wanaofikiri kwamba matatizo mengi yanasababishwa na uchawi.
Uchawi wa kwanza shetani anaologa nao mtu sio kuifanya biashara yake isifanikiwe..anachokifanya cha kwanza, na tena anakifanya kwa bidii ni kumfanya MTU AWE MTENDA DHAMBI!.
Kwasababu anajua Dhambi ndio mzizi na chanzo chaatatizo yote na shida na dhiki.
Mtu aliyejitenga na dhambi kamwe shetani hamwezi, na wala hakuna uchawi mwingine wowote utakaoweza kufanya kazi juu yake.
Lakini kama mtu hajajitenga na dhambi, basi uchawi mwingine wowote utafanya kazi juu yake na kumletea madhara.
Swali ni je?
WEWE NI MWAMINIFU KWA MUNGU?…NA JE! NI MWAMINIFU KATIKA KAZI YAKO?..NA JE UMEJITENGA NA DHAMBI?
Kumbuka hakuna mtu yeyote kwa nguvu zake anaweza kuishinda dhambi, Bali tunaishinda dhambi kwa Kumwamini kwanza Bwana Yesu, kwamba yeye ni Bwana na Mwokozi na anaweza kutusamehe dhambi zetu na kutuosha..
Kwa kumwamini huko, na kubatizwa basi yeye mwenyewe anaingia ndani yetu, na kutupa huo UWEZO WA KIPEKEE WA KUSHINDA DHAMBI, ambao unatufanya kuwa Wana wa Mungu.
Yohana 1:12 “ Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake”.
Uwezo huo unatufanya tuwe watu wengine tofauti na tulivyokuwa hapo kwanza..Ndio hapo zile pombe tulizokuwa hatuwezi kuziacha ghafla tunajikuta tunaweza kuziacha, ule uasherati tuliokuwa tunaona ni mgumu kuuacha tunajikuta tunaushinda, yale matusi ambayo tulikuwa tunaona ni mepesi kuyatamka ulimini mwetu tunajikuta hatuyatoi tena vinywani mwetu n.k.
Bwana atubariki.
Maran atha!
Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp
Tafadhali washirikishe na wengine habari
hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp
Mada Nyinginezo:
Lumbwi ni jina lingine la mnyama anayeitwa KINYONGA.
[29]Tena katika vitu vile vitambaavyo, vitambaavyo juu ya nchi, hivi ni najisi kwenu; kicheche, na panya, na mjombakaka, kwa aina zake,[30]na guruguru na kenge, na mjusi na goromoe, na lumbwi.[31]Wanyama hao ndio walio najisi kwenu katika hao watambaao; awaye yote atakayewagusa, wakiisha kufa, atakuwa ni najisi hata jioni.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
Biblia inamaanisha nini inaposema “Mwenye haki huufikiri uhai wa mnyama wake”?