Title November 2021

Kuwaogopa wanadamu huleta mtego,(Mithali 29:25)

SWALI: Naomba kufahamu maana ya mstari  huu”

Mithali 29:25 “Kuwaogopa wanadamu huleta mtego, ..”
Ni mitego gani hiyo hukupata iwapo utamwogopa mwanadamu?..


JIBU: Ukiendelea kusoma inasema..
Mithali 29:25
[25]Kuwaogopa wanadamu huleta mtego;
Bali amtumainiye BWANA atakuwa salama.
Hofu ya kwamba mwanadamu atakuonaje, ukitenda jambo fulani la haki..hofu ya mwanadamu atakuchukuliaje siku ukivaa mavazi ya kujisitiri ,hofu ya wazazi,  watakupokeaje pale unapoamua kuokoka..n.k kwa kawaida hofu kama hizi za kuwapendeza wanadamu mwisho wa siku huwa zinakupeleka katika mtego wa kupotea..
Kwamfano..
Sauli aliupoteza ufalme wake kwa kuwaogopa watu na kumwacha Agagi hai. 1Samweli 15:25
Haruni alikuwa katika hatihati ya kuuliwa na Mungu kwa kosa la kuwapendeza wana wa Israeli pale walipomwomba awatengenezee ndama wa dhahabu wamwabudu.
Kutoka 32:22-24
Herode alimwua Yohana mbatizaji kwa kumpendeza mke wake na binti wake Marko 6:21-27..
Herode mwingine naye alimuua Yakobo mtume wa Bwana..pamoja na kumfunga Petro kwa lengo tu la kuwapendeza wayahudi.Matendo 12:1-4
Umeona wote hawa waliishia katika mitego mibaya kwa hofu za wanadamu…
Lakini kinyume chake ni kuwa wanaomtumaini Mungu watakuwa salama.
Shedraka, Meshaki na Abednego walikaidi amri ya mfalme na kumtii Mungu japokuwa walitupwa katika tanuru la moto lakini walitoka salama..
Danieli kwa hofu ya Mungu alikuwa tayari kutupwa katika tundu simba lakini Mungu alitomtoa salama huko nako..
Bwana Yesu alisema  …
Yohana 5:44
[44]Mwawezaje kuamini ninyi mnaopokeana utukufu ninyi kwa ninyi, na utukufu ule utokao kwa Mungu aliye wa pekee hamwutafuti?
Na sisi ili tuwe salama tuutafute utukufu unaotoka kwa Mungu..tukubali njia Kristo aliyoichagua  hata kama dunia nzima itatutenga..na njia yenyewe ni ile ya wokovu na kujikana nafsi.
HivyoTubu dhambi zako ikiwa wewe ni mwenye dhambi. Yesu yupo mlangoni kurudi. Unyakuo ni wakati wowote, kwasababu tunaishi katika kizazi kilichoshuhudia kutimia kwa dalili zote za kurudi kwake mara ya pili.
Shalom.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

MTEGO HUTEGWA BURE, MBELE YA MACHO YA NDEGE YE YOTE.

Nini maana ya “yasiyokuwapo hayahesabiki”(Mh 1:15)

SIKU YA HOFU YANGU NITAKUTUMAINI WEWE.

AOGOPACHO MTU ASIYE HAKI NDICHO KITAKACHOMJILIA.

Waoga ambao hawataurithi uzima wa milele ni watu wa namna gani?(Ufunuo 21:8).

Rudi nyumbani

Print this post

Gombo ni nini?

Gombo ni aina ya vitabu vilivyo katika mfumo wa kuviringishwa, kwa lugha ya kiingereza “Scrolls” (tazama picha juu).

Aina ya vitabu hivi vilitumika sana katika enzi za zamani na vilikuwa mara nyingi ni vya ngozi.

Lakini katika zama zetu hizi za sasa, hatuvitumii tena kutokana na kuongezeka kwa maarifa.

Vitabu tunavyotumia sasa, vinatengenezwa kwa karatasi, na vinakuwa na kurasa..Lakini Gombo hazikuwa na kurasa, bali ni ngozi uliyokuwa na maandishi na kuviringishwa.

Mfano wa Gombo ni lile tunalolisoma katika kitabu cha Ezekieli na Ufunuo.

Katika kitabu cha Ufunuo, tunasoma Bwana Yesu akikipokea kile kitabu chenye mihuri saba. Sasa kitabu hicho hakikuwa kama vitabu vyetu hivi vyenye kurasa la!..bali kilikuwa ni gombo, yaani kitabu kilichoviringishwa, na vitabu hivi vya kuviringishwa ndivyo vilivyokuwa vinafungwa kwa mihuri.. vilikuwa vinafungwa kama vile shati linavyofungwa kwa vifungo vyake, (tazama picha chini).

Mfumo wa kuviringishwa

Kwahivyo popote katika biblia panapotajwa neno kitabu, palimaanisha aina hiyo ya vitabu (yaani Gombo)..na haikumaanisha aina ya vitabu tulivyo navyo sisi.

Unaweza kulipata neno hilo Gombo katika biblia, kupitia mistari ifuatayo. Zaburi 40:7, Yeremia 36:2-6, Ezekieli 2:9, Ezekieli 3:3, Zekaria 5:1-2, na Waebrania 10:7.

Kwa msingi huo wa kuelewa nini maana ya Gombo, utatusaidia kuelewa vizuri juu ya juu ya MIHURI SABA ya kitabu cha ufunuo.
Kama utapenda kujua juu ya ufunuo wa Mihuri saba unaweza kufungua hapa >> Mihuri saba

Je umempokea Yesu?, je Umebatizwa ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Yesu?, Je umepokea Roho Mtakatifu a unaishi maisha matakatifu ya kumpendeza Mungu?.

Kumbuka Bwana yupo mlangoni, na unyakuo wa kanisa ni siku yoyote.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Biblia ina vitabu vingapi?

Tofauti kati ya kuhukumu na kulaumu ni ipi?

Nini maana ya “Roho za manabii huwatii manabii?

USIPUNGUZE MAOMBI.

HEKIMA YA KIMUNGU, INAINGIAJE MIOYONI MWETU?

Rudi nyumbani

Print this post

Je ushabiki wa mpira ni dhambi?

Je! Kucheza mpira au kushabikia mpira ni dhambi kulingana na maandiko?.


Bwana kutuumba miili yetu hii ili kuishughulisha, hajatuumbia ikae tu bila kujishughulisha..Na njia mojawapo ya kuishughulisha ni kwa kufanya mazoezi.

Na mazoezi hayo yanaweza kufanyika kwa njia ya kawaida au ya kucheza..Kwamfano watu wawili marafiki wanaweza kusimama na kushindana mbio, na mwisho wa mbio wakafurahi na kucheka, hatimaye wakawa wamecheza na hapo hapo kufanya mazoezi.
Sasa kucheza kwa namna hiyo sio dhambi lakini tatizo linakuja mfumo unaochanganyikana na mchezo huo.

Kwamfano mchezo unapohusisha kuvaa kuilimwengu, au matusi, au miziki ya kiulimwengu, au mambo yoyote yasiyo na adabu mchezo huo ni dhambi, na sisi wakristo hatupaswi kuushiriko.

Kwamfano riadha za siku hizi ili wanawake au wanaume washiriki, hawana budi kubaki na nguo za ndani tu!..na sehemu nyingine yote ya mwili kubaki wazi.

Utakuta wanawake wanakimbia riadha wakiwa na chupi tu, na wanaume hivyo hivyo. Sasa michezo ya namna hiyo ni dhambi kushiriki kwa mkristo.

Na kama ni dhambi, basi na hata kuishabikia vile vile ni dhambi.

Kadhalika watu wawili wanaweza kitengeneza mpira wao na kisha kuipiga piga kwa miguu yao kujifurahisha..jambo hilo sio dhambi.

Lakini inapotokea mchezo huo unachanganyikana na mfumo fulani wa kishetani, tayari mchezo huo unakuwa ni najisi kwakristo, kwamfano utakuta mchezo fulani unadhaminiwa na shirika la pombe au la sigara, au la kubeti kiasi kwamba hata sare za mchezo huo ni nembo la mashirika hayo najisi.

Au utakuta michezo mingine ni lazima ihusishe miziki ya kidunia ambayo ni najisi kwa mkristo.

Hapo hatupaswi sisi kama wakristo kushiriki michezo hiyo, wala kuwa wafuasi wa hiyo michezo.

Hivyo kwaasili michezo sio mibaya,
Hata Yakobo alicheza Mieleka na yule Malaika..

Lakini mieleka ya leo ni lazima ubakiwe na nguo za ndani tu!..Na tena siku hizi ni jinsia mbili tofauti zinapigana mieleka, kiasi kwamba huwezi kutazama mara mbili michezo hiyo imejaa matusi na ushetani.

Imefungamana na ushetani kiasi kwamba kitendo cha kuangalia tu tayari umenajisika..

Na siku zinavyozidi kwenda hiyo mifumo inazidi kuongezwa juu ya hiyo michezo na kuharibu kabisa maana ya michezo.

Huko mbeleni, riadha zitakuwa zinafanyika uchi wa mnyama kabisa, tofauti na leo ambapo ni nguo za ndani tu ndio zina sitiri.
Kama tunataka kucheza (sisi kama wakristo), tunaweza kucheza sisi kwasisi bila kutumia mifumo hiyo ya kishetani.

Lakini pia biblia imetuonya kuwa na kiasi, maana yake sio kucheza mpaka unakuwa unafanana na watu wa kidunia.

Vile vile mambo yote tunapaswa kuyafanya kwa utukufu wa Mungu. Ukicheza na mtoto wako inaweza ikatosha, ukicheza na kaka yako inatosha, ukicheza na rafiki zako wawili au watatu inatosha, sio lazima tujichangange na harambee za watu wengi wa kiulimwengu, kushiriki nao michezo iliyojaa unajisi na mizaha.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

TUMEKUWA TAMASHA KWA DUNIA; KWA MALAIKA NA WANADAMU.

Kucheza karata ni sahihi kwa Mtu aliye MKRITO?

YANAYOENDELEA SASA KATIKA MADHABAHU YA MUNGU ROHONI.

JE! KUBET NI DHAMBI?

KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 1: Upande wa wanaume)

Rudi nyumbani

Print this post

MAOMBI YA KUFUNGULIWA KIUCHUMI.

Kabla ya kwenda katika maombi Awali ya yote ni vizuri ukafahamu kuwa mafanikio ya kiuchumi yanaweza kuletwa na vitu vikuu vitatu

  1. Mwanadamu mwenyewe.
  2. Shetani.
  3. Mungu.

Na kila mmoja anayo kanuni yake ya kuyafikia hayo mafanikio.

Kwamfano kwa mwanadamu, ili aweze kujikomboa kiuchumi, kanuni ni moja nayo ni “kuwa na bidii katika kufanya kazi”..haijalishi kazi hiyo itakuwa ni ya kuuza pipi, maadamu unatia bidii ndani yake, utafanikiwa kwasababu  katika bidii hiyo, huko huko ndio unazalika ubunifu  na mikakati, ya kupiga hatua, na kuwekeza,n.k. na mwisho wa siku utafanikiwa, Hata kama hatofikia utajiri ule, lakini mwisho wa siku utajikomboa kiuchumi, haijalishi atafanya hivyo kwa muda gani. Na hapo atakuwa tayari kashajikomboa kiuchumi.

Lakini kanuni za ibilisi ni tofauti na zile za kibinadamu. Pengine kwake si lazima ujishughulishe sana, lakini akakupa mafanikio tu, Kwasababu ndicho alichojaribu kufanya kwa Bwana Yesu, kwa kumwambia  tu amsujudie ndipo atakapompa mali zote.

Mathayo 4:9 “akamwambia, Haya yote nitakupa, ukianguka kunisujudia.”

Unapokwenda kwa waganga watakupa mafanikio, lakini wakiwa na masharti yao kwamba ni lazima ufanye kitu fulani kwa shetani n.k..

Lakini tunaporudi kwa Mungu, napo pia kuna kanuni zake, za kufanikiwa. Ukienda nje ya hizo, na huku unahitaji mafanikio, au kukombolewa kiuchumi usijidanganye, unapoteza muda. Nenda tu kajibidiishe huko kama wanadamu wengine, utafanikiwa pia kwa njia hizo.

Lakini Kanuni za Mungu za kumkomboa mtu kiuchumi  ni zipi?;

Kabla ya kuombewa ni lazima uwe mwana wake. Na mtu anakuwa mwana wake kwa kutubu dhambi zake zote, na kubatizwa, kisha kupokea Roho Mtakatifu. Na baada ya hapo kuanzia huo wakati na kuendelea kuishi maisha yampendezayo Mungu.

Biblia inasema..

Mathayo 6:31 “Msisumbuke, basi, mkisema, Tule nini? Au Tunywe nini? Au Tuvae nini?

32 Kwa maana hayo yote Mataifa huyatafuta; kwa sababu Baba yenu wa mbinguni anajua ya kuwa mnahitaji hayo yote.

33 Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa”.

Unaona? Ukishautafuta kwanza ufalme wake na haki yake, kuanzia huo wakati unakuwa tayari sasa, kushiriki Baraka zote kutoka kwa Mungu, kiwepesi  pale unapomwomba.

Neno la Mungu linasema hivi..

2Wakorintho 8:9 “Maana mmejua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, jinsi alivyokuwa maskini kwa ajili yenu, ingawa alikuwa tajiri, ili kwamba ninyi mpate kuwa matajiri kwa umaskini wake”.

Na pia Yesu mwenyewe alisema..

Mathayo 19:28 “Yesu akawaambia, Amin, nawaambia ya kwamba ninyi mlionifuata mimi, katika ulimwengu mpya, atakapoketi Mwana wa Adamu katika kiti cha utukufu wake, ninyi nanyi mtaketi katika viti kumi na viwili, mkiwahukumu kabila kumi na mbili za Israeli.

29 Na kila mtu aliyeacha nyumba, au ndugu wa kiume au wa kike, au baba, au mama, au watoto, au mashamba, kwa ajili ya jina langu, atapokea mara mia, na kuurithi uzima wa milele.

30 Lakini wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho, na walio wa mwisho watakuwa wa kwanza”.

Hivyo kabla ya kwenda kukuombea Baraka zako kutoka kwa Mungu.. ni sharti kwanza uwe  tayari leo kumkabidhi Bwana Yesu maisha yako, kwa kumaanisha kabisa. Kama upo tayari basi hapo ulipo tafuta sehemu yenye utulivu, kisha piga magoti, kisha sema sala hii kwa imani, kwa kumaanisha kabisa, na Mungu atakuokoa siku ya leo.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU  MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa kwa sala hiyo fupi, amini kuwa Bwana Yesu ameshakusamehe, Na kuanzia sasa unakuwa tayari kushiriki, Baraka zote kutoka kwa Mungu.

Yeye mwenyewe alisema maneno haya;

Kumbukumbu: MLANGO 28

1 Itakuwa utakaposikia sauti ya Bwana, Mungu wako, kwa bidii, kutunza kuyafanya maagizo yake yote nikuagizayo leo, ndipo Bwana, Mungu wako, atakapokutukuza juu ya mataifa yote ya duniani;

2 na baraka hizi zote zitakujilia na kukupata usikiapo sauti ya Bwana, Mungu wako.

3 Utabarikiwa mjini, utabarikiwa na mashambani.

4 Utabarikiwa uzao wa tumbo lako, na uzao wa nchi yako, na uzao wa wanyama wako wa mifugo, maongeo ya ng’ombe wako, na wadogo wa kondoo zako.

5 Litabarikiwa kapu lako, na chombo chako cha kukandia unga.

6 Utabarikiwa uingiapo, utabarikiwa na utokapo.

7 Bwana atawafanya adui zako wainukao juu yako kupigwa mbele yako; watakutokea kwa njia moja, lakini watakimbia mbele yako kwa njia saba.

8 Bwana ataiamuru baraka ije juu yako katika ghala zako, na mambo yote utakayotia mkono wako; naye atakubarikia katika nchi akupayo Bwana, Mungu wako.

9 Bwana atakuweka uwe taifa takatifu kwake, kama alivyokuapia; utakaposhika maagizo ya Bwana, Mungu wako, na kutembea katika njia zake.

10 Na mataifa yote ya duniani watakuona umeitwa kwa jina la Bwana, nao watakuwa na hofu kwako.

11 Bwana atakufanya uwe na wingi wa uheri, katika uzao wa tumbo lako, na uzao wa wanyama wako wa mifugo, na uzao wa nchi yako, katika nchi Bwana aliyowaapia baba zako kwamba atakupa.

12 Atakufunulia Bwana hazina yake nzuri, nayo ni mbingu, kwa kutoa mvua ya nchi yako kwa wakati wake, na kwa kubarikia kazi yote ya mkono wako; nawe utakopesha mataifa mengi, wala hutakopa wewe.

13 Bwana atakufanya kuwa kichwa, wala si mkia; nawe utakuwa juu tu, wala huwi chini; utakapoyasikiza maagizo ya Bwana, Mungu wako, nikuagizayo hivi leo, kuyaangalia na kufanya;

14 msipokengeuka katika maneno niwaamuruyo leo kwa lo lote, kwenda mkono wa kuume wala wa kushoto, kwa kuifuata miungu mingine na kuitumikia.

Baraka hizo zote, zitakufuata endapo utadumu tu katika WOKOVU.

Basi sasa, nitakuombea, ili milango hii ifunguke, katika maisha yako. Hapo ulipo Piga tena magoti, niombe kwa ajili yako. Fuatisha kwa sauti sala hii;

Baba Mwenyezi, Mungu wa milele, ahsante kwa kutupa zawadi ya kutuletea mkombozi duniani, Bwana wetu Yesu Kristo. Asante kwa kuwa alikuja kutukomboa kutoka katika dhambi zetu na laana zetu. Lakini hakuishia hapo tu, bali alitukomboa, mpaka na UCHUMI wetu.

Nami leo hii nimempokea na kumkiri kwa kumaanisha kabisa kumfuata tangu sasa hadi milele. Naomba Mungu wako zile Baraka zote ulizoziahidi katika Kumbukumbu la Torati 28:1-14, zinijilie juu yangu. Nami nikawe Baraka kwa jamii na kwa kanisa lako. Kuanzia sasa ikiwa kuna kazi zozote za ibilisi zilizotangulia nyuma yangu kunizuilia Baraka zangu, ninazikataa kwa jina la Yesu Kristo. Naiita Damu ya Yesu ikasafishe kapu langu, na mfuko wangu.

Asante Mungu wangu kwa kunikomboa.

Amen.

Basi, ikiwa umeyafuatilisha maombi hayo, ujue kuanzia sasa, Mungu atatembea na wewe katika uchumi wako, kwa kile unachokifanya, tenda mapenzi ya Mungu, utaona akikupigania. Lakini kumbuka Kama tulivyotangulia kusema, inahitaji Kutembea na Mungu ili akukamilishie ahadi hizo, sio tu kukiri kwa mdogo, unakwenda kuendelea na mambo yako..nikuambie ukweli tu, inahitaji maisha.

Mungu akubariki sana.

Ikiwa utahitaji msaada zaidi wa kumjua Mungu, au ubatizo, au unaswali lolote kuhusu biblia,  basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi Simu/Whatsapp: +255693036618 /  +255789001312

Mada Nyinginezo:

REKEBISHA YAFUATAYO ILI UCHUMI WAKO UKAE SAWA.

TWEKA MPAKA VILINDINI.

NI YESU YUPI UMEMPOKEA?, NI ROHO IPI UMEIPOKEA? NA INJILI IPI UMEIPOKEA?

HUTATAMBUA LOLOTE, SIKU YA UNYAKUO IKIFIKA.

Rudi nyumbani

Print this post

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU WATOTO.

  1. MISTARI YA WAZAZI/WALEZI KUHUSU WATOTO.

Haya Mafungu ya biblia ambayo wazazi/walezi wanapaswa wayajue kuhusu watoto wao.

Zaburi 8:2a “Vinywani mwa watoto wachanga na wanyonyao Umeiweka misingi ya nguvu;..”

Mungu anaonyesha kuwa kupitia watoto wachanga, ambao unaweza kuwadharau hawajui kitu, hapo ndipo Mungu ameweka nguvu zake. Hivyo anza kumlea mtoto katika misingi ya kumcha Mungu tangu akiwa mdogo, kwasababu hapo ndipo Mungu anapoketi.

 Na ndio maana biblia inasema..

Mithali 22:6 Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee.

Tabia ya kudharau watoto, au kuona kama umri wao wa kumjua Mungu bado, Yesu aliukemea sana, tunalithibitisha hilo katika..

Marko 10:13 “Basi wakamletea watoto wadogo ili awaguse; wanafunzi wake wakawakemea.

14 Ila Yesu alipoona alichukizwa sana, akawaambia, Waacheni watoto wadogo waje kwangu, msiwazuie; kwa maana watoto kama hawa ufalme wa Mungu ni wao.

15 Amin, nawaambieni, Ye yote asiyeukubali ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo hatauingia kabisa.

16 Akawakumbatia, akaweka mikono yake juu yao, akawabarikia”.

Biblia inasema pia..

Zaburi 127:3 “Tazama, wana ndio urithi wa Bwana, Uzao wa tumbo ni thawabu”.

Biblia bado inasisitiza wazazi, wasiwaudhi watoto wao, kwasababu zisizo na msingi, kisa tu wao ni watoto,

Waefeso 6:4 “Nanyi, akina baba, msiwachokoze watoto wenu; bali waleeni katika adabu na maonyo ya Bwana.

Kwasababu malaika wao mbinguni wanawatazama uwatendeapo mabaya..

Mathayo 18:10 “Angalieni msidharau mmojawapo wadogo hawa; kwa maana nawaambia ya kwamba malaika wao mbinguni siku zote huutazama uso wa Baba yangu aliye mbinguni”.

Zaidi pia Bwana Yesu anataka wazazi/walezi wajifunze kupitia watoto walionao, hivyo kwa kupitia wao tutapata kujua siri kubwa za ufalme wa mbinguni.

Mathayo 18 : 1-5

“1 Saa ile wanafunzi wakamwendea Yesu wakisema,

2 Ni nani basi aliye mkuu katika ufalme wa mbinguni? Akaita mtoto mmoja, akamweka katikati yao,

3 akasema, Amin, nawaambia, Msipoongoka na kuwa kama vitoto, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni.

4 Basi, ye yote ajinyenyekeshaye mwenyewe kama mtoto huyu, huyo ndiye aliye mkuu katika ufalme wa mbinguni.

5 Na ye yote atakayempokea mtoto mmoja mfano wa huyu kwa jina langu, anipokea mimi;”

Lakini bado Mungu anasisitiza juu ya kuwarekebisha watoto, kwamba ni jukumu la kila mzazi/mlezi kumwadhibu mtoto wake, pale anapokosea . Hilo ni agizo la Mungu. Usipomwajibisha mtoto wako, Mungu atakuwajibisha wewe siku ile, kwa kutomtengeneza mwanao.

Mithali 22:15 “Ujinga umefungwa ndani ya moyo wa mtoto; Lakini fimbo ya adhabu itaufukuzia mbali”.

Mithali 23: 13 “Usimnyime mtoto wako mapigo; Maana ukimpiga kwa fimbo hatakufa.

14 Utampiga kwa fimbo, Na kumwokoa nafsi yake na Kuzimu”.

2) WAJIBU WA MTOTO.

Vilevile mzazi, unapaswa umfundishe mwanao wajibu wake kama mtoto, Sawasawa na Neno la Mungu linavyosema,

Na mojawapo ni kuwafundisha kukutii wewe.

Waefeso 6:1 “Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika Bwana, maana hii ndiyo haki.

2 Waheshimu baba yako na mama yako; amri hii ndiyo amri ya kwanza yenye ahadi,

3 Upate heri, ukae siku nyingi katika dunia”.

Mithali 1:8 “Mwanangu, yasikilize mafundisho ya baba yako, Wala usiiache sheria ya mama yako,

9 Kwa maana hayo yatakuwa kilemba cha neema kichwani pako, Na mikufu shingoni mwako”.

Pia umfundishe kujua wajibu wake wa kumtafuta Mungu tangu akiwa mdogo..kwasababu kwa Mungu hakuna utoto.

Yeremia 1:6 “Ndipo niliposema, Aa, Bwana MUNGU! Tazama, siwezi kusema; maana mimi ni mtoto.

7 Lakini Bwana akaniambia, Usiseme, Mimi ni mtoto; maana utakwenda kwa kila mtu nitakayekutuma kwake, nawe utasema kila neno nitakalokuamuru”.

Na mwisho Mkumbushe pia hata watoto watahukumiwa, na  kuzimu wapo watoto ambao hawakuwajibika katika kuwatii wazazi wao, na kumcha Mungu.

Ufunuo 20:12 “Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa na matendo yao”.

Bwana akubariki.

Maran atha.

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Rudi nyumbani

Print this post

Unyenyekevu ni nini?

Biblia inasema nini kuhusu unyenyekevu?

Unyenyekevu ni ile hali ya “kujishusha” na kuwa tayari “kutumika kwa utumishi ule usiostahili kutumika” bila kiburi wala majivuno.

Biblia inasema Mungu huwapinga wote wenye kiburi na wajikuzao lakini “wanyenyekevu” anawapa Neema.

Yakobo 4:6 “Lakini hutujalia sisi neema iliyozidi; kwa hiyo husema, MUNGU HUWAPINGA WAJIKUZAO, bali huwapa neema wanyenyekevu”.

1Petro 5:5 “Vivyo hivyo ninyi vijana, watiini wazee. Naam, ninyi nyote jifungeni unyenyekevu, mpate kuhudumiana; kwa sababu MUNGU HUWAPINGA WENYE KIBURI, LAKINI HUWAPA WANYENYEKEVU NEEMA”.

Na tena kitabu cha Mithali kinasema…

Mithali 3:33 “Laana ya Bwana i katika nyumba ya waovu, Bali huibariki maskani ya mwenye haki.

34 Hakika yake huwadharau wenye dharau, Bali huwapa wanyenyekevu neema.”

Na zaidi ya yote, Injili ya Bwana Yesu ni kwa wote walio wanyenyekevu..

Isaya 61:1 “Roho ya Bwana MUNGU i juu yangu; kwa sababu Bwana amenitia mafuta NIWAHUBIRI WANYENYEKEVU HABARI NJEMA; amenituma ili kuwaganga waliovunjika moyo, kuwatangazia mateka uhuru wao, na hao waliofungwa habari za kufunguliwa kwao”.

Maana yake ni kwamba “watu wajikwezao” na “wenye kiburi”.. Hawawezi kuipokea Habari njema ya Yesu, Neema ya Wokovu inakuwa haipo juu yao.

Na pia Bwana Yesu alitufundisha ni kwa namna gani tutakuwa wa kwanza, katika ufalme wa Mbinguni.. alisema tukitaka kuwa wa kwanza, basi hatuna budi kujinyenyekeza na kuwa wadogo kuliko wote, maana yake tuwe watumwa na watumishi kwa wengine.. tofauti na hekima ya dunia inavyosema au kufundisha kuwa mtu mkubwa ni Yule anayetumikiwa na mwenye kiburi.

Marko 10.42 “Yesu akawaita, akawaambia, Mwajua ya kuwa wale wanaohesabiwa kuwa wakuu wa Mataifa huwatawala kwa nguvu, na wakubwa wao huwatumikisha.

43 Lakini haitakuwa hivyo kwenu; bali mtu anayetaka kuwa mkubwa kwenu, atakuwa mtumishi wenu,

44 na mtu anayetaka kuwa wa kwanza wenu, atakuwa mtumwa wa wote.

45 Kwa maana Mwana wa Adamu naye hakuja kutumikiwa, bali kutumika, na kutoa nafsi yake iwe fidia ya wengi”.

Hivyo biblia inatufundisha kuwa wanyenyekevu siku zote, yaani kuwa “wadogo”, sehemu nyingine Bwana Yesu anasema tunapaswa tujinyenyekeze na kuwa kama vitoto.

Mathayo 18:3 “akasema, Amin, nawaambia, Msipoongoka na kuwa kama vitoto, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni.

4 Basi, YE YOTE AJINYENYEKESHAYE mwenyewe kama mtoto huyu, huyo ndiye aliye mkuu katika ufalme wa mbinguni”.

Unaweza kusoma pia, Mathayo 11:11, Waefeso 5:21, Zaburi 138:6, Mithali 11:2, na Mithali 18:12.

Hivyo na sisi hatuna budi kuwa wanyenyekevu siku zote, ili tukwezwe na tupate NEEMA zaidi, na sio tu kuwa wanyenyekevu kwa Mungu, bali pia kwa watu wengine wote, ikiwemo wazazi, wafanyakazi wenzetu na maboss zetu na kwa wenye mamlaka pia (Tito3:1).

Lakini tukiwa ni watu wa kiburi, au tukijiinua basi tutashushwa chini kama maandiko yanavyosema..

Luka 14:11 “Kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa”.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.

Neema ni nini?

SALA YA ASUBUHI

ILI NIWE KIELELEZO KWA WALE WATAKAOMWAMINI BAADAYE.

NI SAA KUMI NA MBILI (12) TU, ZA KRISTO KWAKO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Ni kwa namna gani Yesu ni Simba wa Yuda?

Bwana Yesu amejulikana kwa majina mengi tofauti tofauti katika biblia, kuna sehemu katajwa kama Mwanakondoo (Yohana 1:29), sehemu nyingine kama nyota ya asubuhi, sehemu nyingine kama Mzao wa Daudi (ufunuo 22:16), sehemu nyingine kama Imanueli, sehemu nyingine kama Simba wa Yuda n.k.

Leo tutaangalia ni kwanini amejulikana kama Simba wa Yuda.

Bwana Yesu kama Simba wa Yuda ametajwa mara moja tu Katika biblia yote!. Na ametajwa hivyo ndani ya kitabu cha ufunuo.

Ufunuo wa Yohana 5:5 “Na mmojawapo wa wale wazee akaniambia, Usilie; tazama, Simba aliye wa kabila ya Yuda, Shina la Daudi, yeye ameshinda apate kukifungua kile kitabu, na zile muhuri zake saba”.

Sasa ili tuelewe kwanini ni Simba?.

Hebu turudi tujikumbushe baraka za ambazo Yakobo aliwabarikia watoto wake wale 12.

Utaona kila mtoto alipewa maneno ya kinabii kwake yeye binafsi, na uzao wake wote utakaofuata baada yake..tunaweza kusoma baraka hizo katika kitabu cha Mwanzo 49.

Mwanzo 49:1 “Yakobo akawaita wanawe, akasema, Kusanyikeni, ili niwaambie yatakayowapata siku za mwisho.

2 Kusanyikeni, msikie, enyi wana wa Yakobo,
Msikilizeni Israeli, baba yenu.

Sasa turuke mpaka mstari wa 8, tuone unabii wa Yuda mwana wa nne wa Yakobo..

8 Yuda, ndugu zako watakusifu,
Mkono wako utakuwa shingoni mwa adui zako. Wana wa baba yako watakuinamia.

9 Yuda ni mwana-simba, Kutoka katika mawindo, mwanangu, umepanda; Aliinama akajilaza kama simba, Na kama simba mke; ni nani atakaye mwamsha?

10 Fimbo ya enzi haitaondoka katika Yuda, Wala mfanya sheria kati ya miguu yake, Hata atakapokuja Yeye, mwenye milki, Ambaye mataifa watamtii.

Umeona hapo mstari wa 9 unasema “Yuda ni mwana Simba”..na tena anasema katika mstari wa 10… “Fimbo ya enzi haitaondoka katika Yuda”.

Ikiwa na maana kuwa kuna mmoja atakayezaliwa katikati ya kabila la Yuda, ambaye atatawala kama Simba, na tena atakwa ni Mfalme. Na huyo si mwingine zaidi ya Bwana Yesu. Yakobo alimwona Bwana Yesu miaka mingi kabla ya kuja kwake ndani ya uzao wa mwanae Yuda, kama vile Balaamu alivyomwona Yesu ndani ya kusanyiko la Israeli..

Hesabu 24:17 “Namwona, lakini si sasa; Namtazama, lakini si karibu; Nyota itatokea katika Yakobo Na fimbo ya enzi itainuka katika Israeli; Nayo itazipiga-piga pembe za Moabu, Na kuwavunja-vunja wana wote wa ghasia.

18 Na Edomu itakuwa milki Seiri pia itakuwa milki, waliokuwa adui zake; Israeli watakapotenda kwa ushujaa.

19 Mwenye kutawala atakuja toka Yakobo, Atawaangamiza watakaobaki mjini”.

Ndio maana kwenye Ufunuo hapo anakuja kutajwa kama Simba wa kabila la Yuda.

Sasa kwanini awe simba na Dubu au Chui?

Ni kwasababu Simba ni jasiri, haogopi, tena ana nguvu na tena anajulikana kama Mfalme wa pori.

Na Bwana Yesu, maandiko yanasema atakuja kuitawala dunia kwa fimbo ya chuma,  hivyo kama vile simba alivyo mfalme wa pori, kadhalika na Bwana Yesu atakuja kutawala kama Simba baada ya unyakuo wa kanisa kupita.

Je umemwamini Yesu leo?.. Leo kaja kwetu kama Mwana-kondoo, mpole aendae machinjoni, tukikosa kwake tunaomba rehema na anatusamehewa kwasababu neema bado ipo.

Utafika wakati baada ya unyakuo wa kanisa kupita, kutakuwa hakuna tena rehema, huyu Yesu anayetuita sasa kwa sauti ya upole atageuka na kuwa Simba angurumaye..atawararua waovu wote katika ghadhabu ya Mungu mwenyezi, na katika vita vya Harmagedon na kuwatupa waovu wote katika ziwa la moto, mahali ambapo hakuna msamaha. Maandiko yanasema atakanyaga shinikizo la mvinyo ya ghadhabu ya Mungu mwenyezi..

Ufunuo 19:11 “Kisha nikaziona mbingu zimefunuka, na tazama, farasi mweupe, na yeye aliyempanda, aitwaye Mwaminifu na Wa-kweli, naye kwa haki ahukumu na kufanya vita.

12 Na macho yake yalikuwa kama mwali wa moto, na juu ya kichwa chake vilemba vingi; naye ana jina lililoandikwa, asilolijua mtu ila yeye mwenyewe.

13 Naye amevikwa vazi lililochovywa katika damu, na jina lake aitwa, Neno la Mungu.

14 Na majeshi yaliyo mbinguni wakamfuata, wamepanda farasi weupe na kuvikwa kitani nzuri, nyeupe, safi.

15 Na upanga mkali hutoka kinywani mwake ili awapige mataifa kwa huo. Naye atawachunga kwa fimbo ya chuma, naye anakanyaga shinikizo la mvinyo ya ghadhabu ya hasira ya Mungu Mwenyezi.

16 Naye ana jina limeandikwa katika vazi lake na paja lake, MFALME WA WAFALME, NA Bwana WA MABwana”.

Na unyakuo wa kanisa ni siku yoyote kuanzia sasa hivi. Mlango wa rehema utakuwa umefungwa.

Swali ni je!, umempokea Yesu? na kuishi maisha ya utakatifu?.

Kama bado hujampokea, basi ni vyema ukafanya hivyo sasahivi, kabla nyakati hizo za hatari hazijafika.. tubu sasa na ukabatizwe katika ubatizo sahihi wa maji tele na kwa jina lake Yesu, upate ondoleo la dhambi (Matendo 2:38). Na Bwana atakurehemu na kukupa uzima wa milele.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Makanwa ni nini katika biblia? (Danieli 6:22)

Kwanini Bwana Yesu alitokea katika ukoo wa Yuda?

Bwana Yesu alikuwa kabila gani?

TOFAUTISHA KATI YA MAFUNDISHO YA YESU, NA YA WAANDISHI.

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 1

Rudi nyumbani

Print this post

Vifungu vya biblia kuhusu Uongozi.

Aina za Uongozi

Uongozi umegawanyika katika aina kuu tatu. 1) Uongozi wa Madhabahuni, 2) Uongozi wa kiserikali na 3) Uongozi wa kijamii.

          1. Uongozi wa Madhabahuni

Uongozi wa madhabahuni, ndio uongozi wa ngazi ya juu kuliko mwingine wowote ule. Uongozi huu ndio unahusisha Wachungaji, Wainjilisti, Waalimu, mitume na Manabii. Watu hawa ndio Mungu kawachagua katika kulingoza kanisa lake (Waefeso 4:11), na katika uongozi wa kanisa, ni wanaume tu ndio waliopewa hiyo dhamana.. Maana yake, biblia haijaruhusu wanawake, kuwa wachungaji wala waalimu.

1Timotheo 2:11 “Mwanamke na ajifunze katika utulivu, akitii kwa kila namna.

12 Simpi mwanamke ruhusa ya kufundisha, wala kumtawala mwanamume, bali awe katika utulivu.

13 Kwa maana Adamu ndiye aliyeumbwa kwanza, na Hawa baadaye”.

               2. Uongozi wa Kiserikali.

Uongozi wa kiserikali ndio unahusisha, viongozi wote wa kimamlaka.. mfano, Raisi, Mawazili, wabunge, madiwani, wakuu wa mikoa, mameya, wenyekiti wa mitaa, na hata wajumbe.

Hawa maandiko yanasema pia ni watumishi wa Mungu, lakini katika utumishi wa mambo ya kimwili.

Warumi 13:1 “Kila mtu na aitii mamlaka iliyo kuu; kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu; na ile iliyopo umeamriwa na Mungu.

2 Hivyo amwasiye mwenye mamlaka hushindana na agizo la Mungu; nao washindanao watajipatia hukumu”.

Na Mkristo yeyote Yule anaweza kushika mojawapo ya hizi nafasi, lakini Haiwezekani kutumika katika nafasi ya Uongozi wa madhabahuni na uongozi wa kiserikalini kwa wakati mmoja.. Haiwezekani kuwa Mchungaji na hapo hapo kuwa Raisi au mbunge.

Majukumu ya kiongozi wa Serikali kibiblia ni yapi?

  1. Kuwa Mwaminifu kwa Mungu aliyeruhusu uishike hiyo nafasi.

 mfano wa akina Shedraki, Meshaki na Abednego.. Ambao walikuwa ni mawaziri wa Mfalme Nebukadneza, siku walipoambiwa waisujudie sanamu ya Nebukadneza, walimheshimu Mungu zaidi ya mwanadamu, na hivyo Mungu akawaokoa na lile tanuru la Moto.

  1. Kuwa Mwaminifu kwa aliyekupa dhamana ya uongozi.

Kama umepewa dhamana hiyo na wananchi, basi kuwa mwaminifu kwao kwa kutekeleza yote uliyowaahidi kwa wakati, na kama umepewa dhamana hiyo kwa kuteuliwa na kiongozi aliye juu yako, basi kuwa mwaminifu katika hiyo nafasi kwa kutenda yale yote uliyoteuliwa kuyafanya, kwa uaminifu wote na utakatifu.. Mfano wa Danieli.

Danieli aliwekwa kuwa kama Waziri mkuu katika ufalme wa Uajemi, lakini siku zote alikuwa mwaminifu kwa mfalme, na wala hakuwahi kula rushwa kama maliwali wengine.

Danieli 6:1 Ilimpendeza Dario kuweka juu ya ufalme maliwali mia na ishirini, wawe juu ya ufalme wote;

2 na juu yao akaweka wakubwa watatu, na Danielii alikuwa mmoja wao; ili maliwali hawa watoe hesabu kwao, mfalme asipate hasara.

3 Basi Danielii huyo alipata sifa kuliko wakubwa na maliwali, kwa kuwa roho bora ilikuwa ndani yake; naye mfalme akaazimu kumweka juu ya ufalme wote.

4 Basi mawaziri na maamiri wakatafuta sana kupata sababu za kumshitaki Danielii kwa habari za mambo ya ufalme; lakini hawakuweza kuona sababu wala kosa; kwa maana alikuwa mwaminifu, wala halikuonekana kosa wala hatia ndani yake.

         3. Uongozi wa kijamii

Mfano wa uongozi wa kijamii ni ule wa kifamilia, au kikabila.. Baba anaweza kuwa kiongozi wa familia, kadhalika mtu fulani anaweza kuwa kiongozi wa kabila fulani, mwanafunzi anaweza kuwa kiongozi wa wanafunzi wenzake (yaani kiranja) n.k

Majukumu ya kiongozi wa aina hii yanafanana na hayo ya uongozi wa kiserikali. Maana yake unahitaji UAMINIFU, kwa aliyekupa hiyo dhamana.

Hayo ndio mambo muhimu katika uongozi ya kuzingatia. Kumbuka tena jambo hili, siku zote “Uongozi ni dhamana”. Hivyo ukitaka ufanikiwe katika uongozi wa aina yeyote ile basi huna budi kuwa mwaminifu kwa aliyekupa hiyo dhamana, iwe ni Utumishi wa madhabahuni au wa kiserikali au kijamii, UAMINIFU NDIO SILAHA.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

WAOMBEENI WANAOWAUDHI.

Kama wakitenda mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu?

INJILI YA MANENO LAINI ITAKUGHARIMU.

YANAYOENDELEA SASA KATIKA MADHABAHU YA MUNGU ROHONI.

Konzi ni nini?(Mhubiri 4:6)

Rudi nyumbani

Print this post

Binadamu wa kwanza aliishi miaka mingapi?

Binadamu wa kwanza alikuwa ni “Adamu” na maandiko yanasema aliishi miaka 930.

Mwanzo 5:5 “ Siku zote za Adamu alizoishi ni miaka mia kenda na thelathini, naye akafa”.

Adamu, hakuwa mtu aliyeishi miaka mingi kuliko wote. Maandiko yanarekodi kuwa Methusela ndiye aliyeishi miaka mingi zaidi, miaka 969 (Mwanzo 5:27).

Na mtu wa kwanza kuishi duniani, hakuwa “Nyani” kama Sayansi inavyosema, bali mtu wa kwanza alikuwa ni Adamu, ambaye aliumbwa na Mungu, na baadaye Hawa, na baada ya hapo, ndipo vizazi vya wanadamu vikatokea kupitia Adamu na Hawa.

Kwahiyo binadamu wa kwanza aliishi miaka mingapi?..Jibu: Aliishi miaka 930, na tangu Adamu mpaka sasa hivi karne hii ya 21, ni tofauti ya miaka takribani elfu sita (6,000), ambayo imegawanyika katika vipindi vitatu.

Kipindi cha kwanza ambacho kwa madirio ni miaka elfu mbili, ni tangu Adamu aumbwe mpaka Gharika ya Nuhu, na baada ya Gharika ya Nuhu mpaka kipindi cha kuzaliwa kwa Bwana Yesu ni tofauti ya miaka mingine elfu mbili, na baada ya Bwana Yesu mapaka sasa ni miaka zaidi ya Elfu mbili mingine, hivyo Jumla ya miaka tangu Adamu mpaka sasa katika karne hii ya 21, ni miaka takribani elfu 6 na miaka kadhaa.

Lakini yote katika yote, Adamu mtu wa kwanza alikufa, ila yupo mwingine ambaye anajulikana kama Adamu wa pili, ambaye anadumu milele, alikufa akafufuka na sasa anaishi, na hafi tena, na huyo si mwingine zaidi ya Yesu Kristo.

Huyo ndiye wa kumtegemea katika wakati huu wa sasa, kwasababu mamlaka yote ya mbinguni na duniani kakabidhiwa yeye, baada ya Adamu kuyapoteza pale Edeni.

Hivyo kila mtu amwaminiye Yesu, anapata ondoleo la dhambi, na ahadi ya uzima wa milele, na asiyemwamini atahukumiwa.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.

JISHUSHE ILI MUNGU AKUHUDUMIE.

KUJIPAMBA NI DHAMBI?

Bwana Yesu alikufa akiwa na umri gani?

Rudi nyumbani

Print this post

JE NI LAANA KULELEWA NA BABA AU MAMA WA KAMBO?

Shalom, Jina la Bwana wetu, Yesu Kristo libarikiwe. Karibu tujifunze biblia, Neno la Mungu wetu.

Katika ulimwengu wa sasa, ukitaja mama wa kambo, au baba wa kambo, tayari picha ya kwanza inayotengenezeka kwenye vichwa vya wengi ni MATESO.

Lakini leo napenda tujifunze kitu kingine tofauti na hicho, ili tusije tukajikuta tunazuia baraka zetu pasipo sisi kujua.

Jambo la kwanza la kufahamu kabla hatujaingia kwenye kiini cha somo ni kwamba, popote pale unapojikuta upo, au umezaliwa, na kulelewa..jua Mungu kakuweka hapo kwa kusudi maalumu, ambalo ni la baraka.

Sasa turudi kwenye swali letu!. Je! Ni laana au mkosi, kuzaliwa au kulelewa na mama wa kambo au baba wa kambo?.

Tutalijibu swali hili, kwa kujifunza juu ya maisha mmoja katika biblia, na huyo si mwingine zaidi ya Bwana Yesu, Mkuu wa uzima..

Maandiko yanasema “tujifunze kwake”..Maana yake tumtazame yeye, tuyaangalie maisha yake, na tupate masomo (Mathayo 11:29).

Na leo tutapata somo lingine kutoka katika maisha yake.

Sasa wengi wetu hatujui kuwa Bwana wetu Yesu, alilelewa na Baba wa kambo katika mwili (Ni lugha ngumu kidogo hii, lakini ndivyo ilivyo).

Yusufu hakuwa Baba kamili wa Bwana Yesu. Mimba aliyoipata Mariamu haikumhusisha baba, ilikuwa ni kwa uweza wa Roho Mtakatifu (soma Mathayo 1:18).

Baba wa Bwana Yesu, alikuwa ni Roho Mtakatifu.

Hivyo ni sahihi kabisa kusema, Yusufu alikuwa ni baba wa kambo wa Bwana Yesu.

Lakini ulishawahi kujiuliza ni kwanini Mungu aruhusu aishi na baba wa kambo?, kwani alishindwa kumfungulia Mariamu mlango, aishi mwenyewe tu na mtoto Yesu?.. Mungu angeweza kufanya hivyo, kwani yeye ni mweza wa kila kitu.

Angeweza kufungua mlango wa mali nyingi, kipindi Bwana Yesu anazaliwa na kumfanya Mariamu aishi maisha ya kifahari peke yake na mtoto Yesu, na pia angeweza kuzuia Yusufu asipose Mariamu kabisa..

Lakini hakufanya hivyo bali kinyume chake, baada tu ya Mariamu kuposwa ndipo mimba inaonekana..Na baada ya Yesu kuzaliwa, akaanza kubebwa na baba huyo huyo wa kambo, na hata wakati wa kazi ya ufundi, alifanya kazi ya baba huyo huyo wa kambo!.

Bwana aliruhusu maisha yake yawe hayo, ili kutufundisha na sisi kuwa si laana kuishi hayo maisha.

Sasa kulikuwa kuna nini kwa Yusufu, mpaka mkuu wa Uzima, Yesu Kristo apitie pale?

Yusufu alikuwa ni maskini kweli, hakuwa tajiri, lakini alikuwa amebeba ahadi ya kifalme, kumbuka Mungu alimwahidi Daudi, kwamba kupitia uzao wake atatokea Mfalme. Na Yusufu alikuwa ni wa Uzao wa Daudi.

Hivyo ili Bwana Yesu awe mfalme kupitia ahadi hiyo ya Daudi, ilikuwa hana budi azaliwe katika Hema ya Yusufu..angezaliwa pengine popote, ahadi hiyo ya Mungu isingetimia.

Mpaka hapo utakuwa umeanza kuona hata wewe ni kwasababu gani… umelelewa na huyo baba wa kambo Au mama wa kambo.

Haijalishi anakutesa kiasi gani, au ni maskini kiasi gani, lipo kusudi kwanini upo hapo, au umelelewa hapo, kuna baraka ambazo huwezi kuziona kwa macho!..

Kuzaliwa kwa Bwana kwenye lile zizi, chini ya Bwana Yusufu asiyekuwa na kitu, kulikuwa na maana kubwa.

Na wewe vile vile..tengeneza mambo yako vizuri sasahivi kwasaababu kuna baraka tele, mbele yako.

Ishi na Baba yako huyo vizuri, mheshimu, mbariki kwasababu ni Mungu ndiye aliyekuweka hapo, hujajiweka mwenyewe..na Mungu ndiye anayeijua mbele yetu..

Usianze kuharibu mambo kwa kunung’unika, unapopitia vikasoro vidogo vidogo, wewe tazama mbele, ongeza utii na heshima.

Kadhalika na kama wewe ni baba au ni mama na una watoto wa kambo, ishi nao vizuri, kwasababu nao pia wamebeba ahadi, ahadi hiyo isingeweza kukamilika pasipo wewe. Na mwisho utaona faida kubwa mbeleni.

Utasema vipi na mama wa kambo?

Musa alilelewa na Mama wa kambo, Binti Farao, hakujua atakuja kuwa nani..lakini maandiko yanasema, baadaye Mungu alikuja kumfanya Musa kuwa kama “mungu kwa Farao”.

Kutoka 7:1 “BWANA akamwambia Musa, Angalia, nimekufanya wewe kuwa kama Mungu kwa Farao; na huyo ndugu yako Haruni atakuwa nabii wako”.

Alienda kwa binti Farao, ili kupata jina hilo MUSA, Jina hilo alipewa na “mama wa Kambo”…hakupewa na mama yake mzazi, wala halikuwa jina la kiyahudi..

Na cha ajabu ni kwamba, Mungu hakumbadilisha jina Musa…aliendelea nalo hilo hilo, Sauli alibadilishwa na kuwa Paulo, Yakobo alibadilishwa na kuwa Israeli, lakini Musa amebakia kuwa Musa mpaka leo…kumbe wito wake ulikamilishwa pia na mama wa kambo.

Hivyo tunachoweza kujifunza ni kuwa macho ya kiroho kuona mbele na si hapa tu..katika nafasi uliyopo kama unaishi na baba au mama wa kambo, mheshimu kama Baba yako na kama mama yako, unapoona shetani ananyayuka na kujaribu kuharibu uhusiano wenu.. basi ni wakati wa wewe nyanyuka na kuongeza maombi…usiende kusikiliza simulizi za kishetani zinazosimuliwa huko na huko katika mitandao na katika vijiwe kuhusu ubaya wamama au wababa wa kambo, utajizolea elimu zitakazoharibu maisha yako..Biblia ndio kitabu chetu na mwongozo wetu.

Kama Bwana Yesu aliishi na Baba wa kambo, na kufanya naye kazi moja na bado akawa mfalme, ni kitu gani kitakachokuzuia wewe kufikia baraka zako, kupitia huyo mzazi au mlezi ambaye si wako?.

Kadhalika na kama wewe ni mzazi, au mlezi wa mtoto ambaye si wako, usimkatae mtoto wa kambo, kwasababu hujui ana ahadi gani kupitia wewe.. Na Mungu amekuchagua wewe, kwasababu na wewe pia unabaraka juu yake.

Hivyo kwa hitimisho ni kwamba hakuna laana yoyote kuishi au kulelewa na Baba au mama wa kambo. Vile vile hakuna laana yoyote au mkosi, kulea mtoto wa kambo.

Bwana akubariki.

Ikiwa bado hujamwamini Bwana Yesu, ni vyema ukakata shauri sasa kwasababu siku tunazoishi hizi ni siku za mwisho.

Na Bwana Yesu alisema.. “Itatufaidia nini tupate ulimwengu mzima halafu tupate hasara ya nafsi zetu”

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

MWANAMKE, BINTI, MAMA. (Sehemu ya 3)

TUMEFANYIKA KUWA WANA WA MUNGU!

TUMEFANYIKA KUWA WANA WA MUNGU!

YANAYOENDELEA SASA KATIKA MADHABAHU YA MUNGU ROHONI.

Rudi nyumbani

Print this post