Konzi ni nini?(Mhubiri 4:6)

Konzi ni nini?(Mhubiri 4:6)

Konzi ni kiasi cha kujaa mkono.

Kama vile ilivyo kiasi cha kujaa ndoo kinavyoitwa debe, vivyo hivyo na kiasi cha kujaa mkono kinaitwa konzi. Tazama picha juu.

Hivi ni baadhi ya vifungu ambavyo utakutana na Neno hilo;

Mithali 30:4 “Ni nani aliyepanda mbinguni na kushuka chini? Ni nani aliyekamata upepo kwa makonzi yake? Ni nani aliyeyafunga maji ndani ya nguo yake? Ni nani aliyefanya imara ncha zote za nchi? Jina lake ni nani? Na ni nani jina la mwanawe, kama wajua”?

Mhubiri 4:6 “Heri konzi moja pamoja na utulivu, Kuliko konzi mbili pamoja na taabu; na kujilisha upepo”.

Isaya 40:12 “Ni nani aliyeyapima maji kwa konzi ya mkono wake, na kuzikadiri mbingu kwa shubiri, na kuyashika mavumbi ya dunia katika pishi, na kuipima milima kwa uzani, na vilima kama kwa mizani”?

Kutoka 9:8 “Bwana akawaambia Musa na Haruni, Jitwalieni konzi za majivu ya tanuuni, kisha Musa na ayarushe juu kuelekea mbinguni mbele ya Farao”.

Soma pia, Ezekieli 13:19, Walawi 2:2

Lakini biblia inatuambia pia..

Mhubiri 4:6 “Heri konzi moja pamoja na utulivu, Kuliko konzi mbili pamoja na taabu; na kujilisha upepo”.

Tunapokuwa na kidogo lakini kinatupa amani, ni bora kuliko kuwa na vingi lakini vya malalamiko,manung’uniko, vinyongo, hasira, au  wivu.n.k. Bwana atusaidie.

Shalom.

Tazama tafsiri ya maneno mengine ya biblia chini.

Ikiwa utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Baghala ni nini katika maandiko?(2Wafalme 5:16).

Mavyaa ni nani kibiblia?(Mika 7:6)

SIFONGO NA SIKI NI NINI?

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments