Category Archive Uncategorized @sw-tz

NIMEYATUNZA MANENO YA KINYWA CHAKE ZAIDI YA RIZIKI YANGU.

Ayubu 23:12 “

[12]Sikurudi nyuma kuiacha amri ya midomo yake; Nimeyatunza maneno ya kinywa chake zaidi ya riziki yangu”,

Huyu ni Ayubu, …si ajabu kwanini Mungu alimwona ni mtu mkamilifu  aliyemcha Mungu, kuliko watu wote waliokuwa ulimwenguni wakati ule.

Kitendo cha kuyatunza maneno ya Mungu zaidi ya riziki..si jambo dogo, ni kumaanisha kwa hali ya juu sana.

Ni kawaida mtu akiamka asubuhi jambo la kwanza atakalowaza ni ale nini, anywe nini..haiwekezani mtu apitishe siku nzima bila kukumbuka kuna kitu kinapaswa kiwekwe tumboni, Au asifikirie miradi yake, au kazi zake zinakwendaje siku hiyo,. Labda awe na hitilafu katika neva za ubongo wake.

Lakini Ayubu, ilikuwa ni kinyume, chakula/rizki ilikuwa ni “B” …”A” alipoamka asubuhi alikuwa anatafakari atayatimiza vipi maagizo ya Mungu, alikuwa anawaza siku itapitaje pitaje bila kupiga hatua mpya ya ukamilifu.

Hicho ndicho kilichokuwa chakula chake, alionyesha tabia iliyokuwa kwa mkuu wake YESU KRISTO. Ambaye tunasoma wakati fulani alipofuatwa na wanafunzi wake  kuletewa chakula, aliwaambia maneno haya:

Yohana 4:30-34

[30]Basi wakatoka mjini, wakamwendea.

[31]Huko nyuma wanafunzi wakamsihi wakisema, Rabi, ule.

[32]Akawaambia, Mimi ninacho chakula msichokijua ninyi.

[33]Basi wanafunzi wake wakasemezana, Je! Mtu amemletea chakula?

[34]Yesu akawaambia, Chakula changu ndicho hiki, niyatende mapenzi yake aliyenipeleka, nikaimalize kazi yake.

Ayubu alipoamka asubuhi aliwaza toba,kwa ajili ya wengine.., (Soma Ayubu 1:5)

Alihakikisha Neno la Mungu halidondoki, alifanya agano na macho yake, asiwatazame wanawake akawatamani, (Ayubu 31:1). Aliwaza kuwafundisha wengine hekima na busara na kuwasaidia waliokuwa katika dhiki na uhitaji, (Ayubu 31:16-18), mtu wa namna hii Mungu hawezi acha kumwangalia na ndio maana tunasoma Habari zake mpaka leo.

Je na sisi tunaweza kufanana na watu kama hawa ambao walikuwa na tabia sawa na sisi. Kumbuka Ayubu hakuwa myahudi, wala nabii, wala kuhani..biblia inamwita MTU tu, fulani aliyetokea  katika nchi moja iliyoitwa USI.

Na sisi, hivi hivi tulivyo tuna wajibu wa kumaanisha kuyatunza maneno ya Mungu, katika wokovu wetu, tuhakikishe tunayafanya maneno yake ni sehemu ya maisha yetu ya kila siku, ili tusiwe wasahaulifu. 

Bwana Yesu alitupa amri tupendane..ni lazima tujifunze tabia hii, kila siku, alisema pia tusamehe, tusiposamehe Baba yetu naye hataweza kutusamehe makosa yetu.

Haijalishi umekosewa mara ngapi, umeibiwa mara ngapi, umedhulumiwa mali nyingi kiasi gani, kamwe usiyasahau maneno ya Bwana Yesu.. ‘samehe mara saba sabini…’

Bwana Yesu alisema, kesheni mwombe msije mkaingia majaribuni..ukilisahau hili neno ukawa ni mvivu wa kuomba walau saa moja kwa siku kama alivyosema, wewe sio mkamilifu.Ifikie hatua kama vile tukumbukavyo muda wa kula ndivyo tukumbuke muda wa maombi na ibada. Huko ndiko kuyatunza maneno yake zaidi ya riziki zetu.

Na kwa bidii hiyo Bwana atatuona na kujidhihirisha kwetu,kwasababu sikuzote anazunguka ulimwenguni kote kutafuta watu wenye kumaanisha huku kama Ayubu ajifunue kwao.

2 Mambo ya Nyakati 16:9

[9]Kwa maana macho ya BWANA hukimbia-kimbia duniani mwote, ili ajionyeshe mwenye nguvu kwa ajili ya hao, waliokamilika moyo kuelekea kwake…”

Bwana atutie nguvu.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 9 (Kitabu cha Ayubu).

HEKIMA NI NINI? NA UFAHAMU UNAPATIKANA WAPI?

JE UNA MATUMAINI YA KUPATA TENA KILE ULICHOPOTEZA?

Je Musa yupo anawashitaki watu..kulingana na Yohana 5:45?

Bwana alimaanisha nini kusema“maana mtenda kazi astahili posho lake”

MAOMBOLEZO YA HADADRIMONI.

Nini maana ya ugonjwa wa kufisha? (Yeremia 17:9)

Rudi nyumbani

Print this post

Biblia inapotumia neno “Bila kazi ya mikono”, ina maana gani?

JIBU: ‘Bila kazi ya mikono’ maana yake ni kuwa pasipo kisaidizi chochote cha kibinadamu, kwamfano neno hilo utalisoma katika vifungu hivi;

Danieli 2:34 “Nawe ukatazama hata jiwe likachongwa bila kazi ya mikono, nalo jiwe hilo likaipiga sanamu miguu yake, iliyokuwa ya chuma na udongo, likaivunja vipande vipande”.

Huu ni utabiri unaomwelezea Yesu Kristo, jinsi atakavyokuja kuangusha ngome zote za ufalme wa huu ulimwengu, yeye ndio hilo jiwe dogo linalozungumziwa hapo, Na biblia inasema, lilichongwa bila kazi ya mikono maana yake ni kuwa lilijichonga lenyewe kutoka mwambani, lilijimegua lenyewe, likaenda na kuipigia ile sanamu, kufunua kuwa Kristo, hakuletwa na mwanadamu hapa duniani, alizaliwa pasipo baba, halikadhalika atakapokuja kuangusha hizi falme sugu za ulimwengu, hatosaidiwa na mtu, wala hata tegemea msaada wa mtu yeyote yeye mwenyewe ataupiga kwa uweza wake, na wote utaanguka kisha atauweka utawala wake usio na mwisho, ambao utaifunika dunia nzima,

Kufahamu jinsi atakavyojua kuzipiga hizi falme za dunia Soma Ufunuo 19:11-16

“11 Kisha nikaziona mbingu zimefunuka, na tazama, farasi mweupe, na yeye aliyempanda, aitwaye Mwaminifu na Wa-kweli, naye kwa haki ahukumu na kufanya vita.

12 Na macho yake yalikuwa kama mwali wa moto, na juu ya kichwa chake vilemba vingi; naye ana jina lililoandikwa, asilolijua mtu ila yeye mwenyewe.

13 Naye amevikwa vazi lililochovywa katika damu, na jina lake aitwa, Neno la Mungu.

14 Na majeshi yaliyo mbinguni wakamfuata, wamepanda farasi weupe na kuvikwa kitani nzuri, nyeupe, safi.

15 NA UPANGA MKALI HUTOKA KINYWANI MWAKE ILI AWAPIGE MATAIFA KWA HUO. Naye atawachunga kwa fimbo ya chuma, naye anakanyaga shinikizo la mvinyo ya ghadhabu ya hasira ya Mungu Mwenyezi.

16 Naye ana jina limeandikwa katika vazi lake na paja lake, MFALME WA WAFALME, NA BWANA WA MABWANA”.

Lakini pia Neno hili, utalisoma katika vifungu vingine, ambavyo vinamwelezea mtawala katili aliyetokea zamani katika ufalme wa Uyunani, aliyeitwa Antiokia Epifane, mtawala huyu alikuwa ni kivuli cha mpinga-Kristo anayekuja, kwani, alikuwa na nguvu nyingi, na kwasababu hiyo akawaua wayahudi wengi, na kama hiyo haitoshi akalitia unajisi hekalu la Mungu, ambalo hata wafalme wengine walikuwa wanaogopa kufanya matendo kama hayo, yeye hakujali hiyo alikuwa anamtukana Mungu wa Israeli hadharani, na kuchukua nguruwe na kuwaingiza hekaluni, lakini biblia inasema alivunjika, bila kazi ya mikono.

Danieli 8:25 “Na kwa mashauri yake atafanikisha hila mkononi mwake; naye atajitukuza nafsi yake moyoni mwake; naye atawaangamiza wengi katika hali yao ya salama; naye atasimama kushindana naye aliye Mkuu wa wakuu; lakini atavunjika, bila kazi ya mikono”.

Maana yake ni kuwa, Mungu hatotumia jeshi, au wanadamu, au kitu chochote kijulikanacho kumuua, bali yeye mwenyewe atampiga na kufa ghafla, na ndivyo ilivyokuwa katika historia alipatwa na ugonjwa wa ajabu na ghafla, akafa. Kama alivyokuwa Herode wakati ule alivyoliwa na chango, baada ya kujitukuza kama Mungu. (Matendo 12:23).

Hii ni kufunua nini?

Kazi zote za huu ulimwengu ni mbovu, kama Yesu mwenyewe alivyosema katika Yohana 7:7, na ndio maana atakuja kuziondosha zote.  Falme zote zitaanguka, ustaarabu wote utaondolewa, Yesu atakuja kuweka ustaarabu wake mpya wa amani hapa duniani.

Sasa jiulize, mambo unayoyasumbukia leo hii, kana kwamba ndio uzima wako yatakufaidia nini huko mbeleni? Ishi ndani ya Kristo kama mpitaji na msafiri, ukijua kuwa huna makazi ya kudumu hapa, tumia nguvu zako, kuwekeza katika ufalme ujao udumuo, hata kwa hicho unachokisumbukia.

Kumbuka mambo haya yapo karibuni kutokea, huwenda hata ndani ya kizazi chetu, tukayashuhudia haya yote.

Maran Atha.

mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

DANIELI: Mlango wa 8

Je Elisha alimdanganya Ben-hadadi kuwa hatakufa kwa ugonjwa wake?

Wakati wakina Shadraka wanatupwa katika tanuru la moto, Danieli alikuwa wapi?

DANIELI: Mlango wa 2

Je mama mjamzito anaruhusiwa kufunga?

UTAKAPOKUWA MZEE, UTAINYOSHA MIKONO YAKO. NA MWINGINE ATAKUFUNGA

Majina mbalimbali ya Mungu na maana zake.

YOTE NAMTOLEA YESU_Tenzi za Rohoni.

Rudi nyumbani

Print this post

Hakuna mtu awezaye kuja kwangu isipokuwa amejaliwa na Baba yangu.

SWALI: Inakuwaje tunaambiwa mambo mengine tunajaliwa? Na si kwa jitihada zetu, kujaliwa ni nini kibiblia?


JIBU: Kujaliwa maana yake ni kuwezeshwa kufanya jambo ambalo wewe kwa nguvu zako kamwe huwezi kulitenda.

Haya ni mambo ambayo biblia inatuambia mtu anajaliwa kuyafanya.

1) Kupokea wokovu:

Bwana Yesu alisema..

Yohana 6:65 “Akasema, Kwa sababu hiyo nimewaambia ya kwamba hakuna mtu awezaye kuja kwangu isipokuwa amejaliwa na Baba yangu”.

Alisema maneno hayo, baada ya kuona wengi wa wanafunzi wake wanarudi nyuma kwa maneno yake magumu aliyokuwa anayesema, ya kuinywa damu yake na kuula mwili wake,. Hapo ndipo akasema maneno hayo. Ikiwa na maana kuwa hata sasa ukimwona mtu ameokoka kwelikweli kwa kumaanisha kumfuata Yesu na gharama zake, usidhani ni kwa nguvu zake, ameweza hivyo, hilo jambo halipo, hakuna mwanadamu mwenye asili ya dhambi anayeweza kujiamulia tu kwa akili zake kuamini mambo ya rohoni, asiyoyaona.

Alivutwa kwanza, na Mungu, kisha akapewa uwezo huo wa kukubaliana na vigezo vyake.

Yohana 6:44 “Hakuna mtu awezaye kuja kwangu, asipovutwa na Baba aliyenipeleka; nami nitamfufua siku ya mwisho”.

2) Kujua siri za ufalme wa mbinguni:

Si kila mtu atapewa kuzielewa siri za ufalme wa mbinguni. Yesu anasema hivyo katika..

Mathayo 13:10 “Wakaja wanafunzi, wakamwambia, Kwa nini wasema nao kwa mifano?

11 Akajibu, akawaambia, Ninyi mmejaliwa kuzijua siri za ufalme wa mbinguni, bali wao hawakujaliwa”.

Hiyo ni baada ya kuwapa mifano kadha wa kadha  ihusuyo ufalme wa mbinguni, bila kuwapa ufunuo wake, isipokuwa wanafunzi wake tu waliomfuata kumuuliza..ndipo akawaambia maneno hayo.

Ndugu kusoma biblia ni moja na kupokea ufunuo wa Mungu wa kweli ni jambo lingine, wapo watu wana elimu kubwa za theolojia, wanajua historia yote ya maandiko, wameirudia biblia mara 1000, kifungu baada ya kifungu, kama ilivyokuwa kwa mafarisayo na masadukayo, lakini wakashindwa kuelewa Neno dogo la ubatizo wa maji, kwamba ni lazima uwe wa kuzamishwa na kwa jina la Yesu. Au kufahamu kuwa sanamu hazipaswi kuhusianishwa ibada yoyote ya Mungu.

Hivyo ukiona wewe umepewa uelewa wa Neno la Mungu, mshukuru sana, wala usijisifu ukadhani ni kwa utashi wako, au uelewa wako mwepesi umeweza kujua hilo, Hapana bali umejaliwa  na Mungu..

3) Kuhudumu.

Kazi yoyote ya utumishi kwa Mungu, iwe ni ya madhabahuni au nje ya madhabahuni, ambayo unaifanya kwake, ujue kuwa, ni kwa nguvu ulizojaliwa na Mungu, wala si zako;

1Petro 4:11 “Mtu akisema, na aseme kama mausia ya Mungu; mtu akihudumu, na ahudumu kwa nguvu anazojaliwa na Mungu; ili Mungu atukuzwe katika mambo yote kwa Yesu Kristo. Utukufu na uweza una yeye hata milele na milele. Amina”.

Si wote, wamepewa nguvu hizo, hivyo tumika kwa uaminifu.

4) Kutooa/kutokuolewa kwa ajili ya Bwana.

Wapo watu ambao Bwana Yesu amewapa uwezo wa kuyatawala mapenzi yao. Hivyo wanaweza kukaa bila kuoa/kuolewa na wasione shida yoyote. Sasa watu wa namna hii, sio kwa nguvu zao bali Bwana Yesu anasema ni kujaliwa.

Mathayo 19:10 “Wanafunzi wake wakamwambia, Mambo ya mtu na mkewe yakiwa hivyo, haifai kuoa.

11 Lakini yeye akawaambia, Si wote wawezao kulipokea neno hili, ila wale waliojaliwa”.

Hivyo, kwa kuhitimisha ni kuwa uonapo tendo lolote, la ki- Mungu lililogumu kufanyika kwa binadamu wa kawaida, ujue kuwa limetokea kwa kujaliwa na Mungu, na sio kwa nguvu za  mtu yule.

Tukiyafahamu haya, basi tutajifunza kuitii sauti ya Mungu, na kumwomba sana, na kuwa wanyenyekevu ili asitupite, kama hatutajaliwa na Mungu, haijalishi tutahubiriwa injili mara ngapi, tutaona miujiza mingi kiasi gani, tutatokewa na Yesu mara ngapi, kamwe hatuwezi kubadilika, Farao aliona miujiza mkubwa sana kutoka kwa Musa, lakini Mungu hakumpa moyo wa kutubu.

Yuda alikuwa ni mtume ambaye hakutokewa na Yesu,(linaweza likawa ni jambo dogo) bali aliishi na Yesu kabisaa kwa miaka mitatu na nusu, lakini bado ndani yake kulikuwa hakuna badiliko la dhati, na ndio maana akaja kumsaliti baadaye.

Yohana 17:12 “Nilipokuwapo pamoja nao, mimi naliwalinda kwa jina lako ulilonipa, nikawatunza; wala hapana mmojawapo wao aliyepotea, ila yule mwana wa upotevu, ili andiko litimie”.

Hivyo uisikiapo sauti ya Mungu inaugua ndani yako, usiipuzie hata kidogo, chukua hatua haraka badilika. Kubali kutubu na kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo, Upokee kipawa cha Roho Mtakatifu. Kwasababu hiyo sauti haitadumu milele ndani yako. Upo wakati itanyamaza kimya. Hivyo maanisha kumtii Mungu.

Bwana atasaidie.

Shalom.

mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya ugonjwa wa kufisha? (Yeremia 17:9)

USIMPE NGUVU SHETANI.

Ni kweli hakuna mtu aliyewahi kuuona uso wa Mungu Zaidi ya Bwana Yesu?

Wala msimwite mtu baba duniani;..Hapo Bwana wetu Yesu anamaanisha nini kusema hivyo?

Kwanini Bwana Yesu alivikwa taji ya miiba?

Kiyama ni nini?

Je! Siku ya unyakuo watoto wachanga watanyakuliwa?

Rudi nyumbani

Print this post

KATAA KUWA EUTIKO, WA KUSINZIA IBADANI.

MAMBO YA KUZINGATIA KATIKA MAENEO YA IBADA: Sehemu ya 1


KATAA KUWA EUTIKO, WA KUSINZIA IBADANI.

Kuna mambo ambayo yanaonekana madogo, lakini yana madhara makubwa sana rohoni. Watu hawafahamu kuwa wanaweza kufa kabisa kiroho kwa tabia ya kuendekeza USINGIZI ibadani..

Embu tusome habari ya Eutiko, tuone ni jambo gani Bwana anataka tufahamu nyuma ya matukio yaliyokuwa yanaendelea pale..

Tusome.

Matendo ya Mitume 20:7-10

[7]Hata siku ya kwanza ya juma, tulipokuwa tumekutana ili kumega mkate, Paulo akawahutubu, akiazimu kusafiri siku ya pili yake, naye akafuliza maneno yake hata usiku wa manane.

[8]Palikuwa na taa nyingi katika orofa ile tulipokuwa tumekusanyika.

[9]Kijana mmoja, jina lake Eutiko, alikuwa ameketi dirishani, akalemewa na usingizi sana; hata Paulo alipoendelea sana kuhubiri, akazidiwa na usingizi wake akaanguka toka orofa ya tatu; akainuliwa amekwisha kufa.

[10]Paulo akashuka, akamwangukia, akamkumbatia, akasema, Msifanye ghasia, maana uzima wake ungalimo ndani yake.

Nataka tuyatathimini hayo mazingira..kwanza walipokuwa wanasilizia injili ni katika gorofa, na gorofa yenyewe si ya kwanza bali ni ya tatu.. 

Pili japokuwa mahali pale ilikuwa ni usiku lakini biblia inatuambia kulikuwa na taa nyingi sana..maana yake ni kuwa mazingira yote yalikuwa yanaonekana, yapo wazi hivyo mahali pa hatari palionekana, na mahali salama pia palionekana.

Lakini tunaona huyu Eutiko alichagua kwenda kukaa katika dirisha la gorofa, akijua kabisa mahali pale si salama kukaa endapo akiteleza kidogo na kuanguka..

Lakini hakujali hilo, baada ya muda kidogo akasinzia.. Na matokeo yake akaanguka kutoka katika ile gorofa ya tatu. Na alipofika chini alikuwa tayari ameshakufa..

Ni kwanini habari hii iandikwe hapa? Kumbuka kila hadhithi inayoandikwa katika biblia inafundisho kubwa sana nyuma yake.

Sasa kitendo cha kuwepo katika gorofa ya tatu.

Inamaanisha kuwa mahali popote Neno la Mungu, linahubiriwa, au ibada inaendelea, iwe ya jumapili, au fupi ya maombi au mikesha, Rohoni mnakuwa mmechukuliwa mpaka mbingu ya Tatu (ndio ile gorofa ya tatu), juu sana mahali ambapo Mungu yupo na kiti chake cha enzi kilipo.

Na huko kuna Nuru nyingi, kama tulivyoona jinsi taa nyingi zilivyokuwa pale gorofani. Ikiwa na màana kuwa wakati unajaribu kuchagua kusogea mbali na uwepo wa Mungu utatambua kabisa mahali ulipo si salama..

Tabia ya kusinzia inakutuma ukae dirishani mwa uwepo wa Bwana na sio ukumbini. Ni kuonyesha jinsi gani usivyo “siriazi” na Mungu.

Na hatimaye unaanguka kutoka uweponi mwa Bwana..na kufa moja kwa moja kiroho.

Leo imekuwa ni desturi na mtu/watu wengi kila wafikapo nyumbani kwa Mungu ni lazima wasinzie, na wenyewe wanaona ni kawaida, wanadhani pale ni sawa na ofisini kwao, au shuleni kwao, ambapo hakuna jambo lolote la rohoni linalokuwa linaendelea.

Wanasahau kuwa wamepewa neema ya kupandishwa hadi kwenye kiti cha enzi cha Mungu, lakini wanakaa madirishani.

Ndugu ikiwa wewe ni mmojawapo wacha hii tabia, ukiindekeza utaanguka na kufa kabisa kiroho. Nimeona watu wengi wenye tabii hii, wakirudi nyuma ulimwenguni, wengine wakichuliwa na mawimbi ya ibilisi.

Kuwa siriazi na Mungu wako, tambua kilichokupeleka pale, unapoona wengine hawasinzii, haimaanishi kuwa hawahisi usingizi kama wewe, wanahisi lakini watalalaje mbele ya kiongozi wao mkuu? Wanaogopa kumvunjia heshima yake. Vilevile wanataka wapokee kikamilifu kile kilichowapeleka pale,

Hivyo kataa usingizi na wenyewe utakukimbia, na hiyo inakuja kwa kuzingatia kwa makini kile  kinachoendelea pale, mawazo yako yote yakiwa pale, ukijua kabisa kila siku ni mpya nyumbani kwa Bwana, na Mungu anatembea.

Lakini kama utaenda kwa desturi na mazoea, au kukamilisha ratiba, utakuwa ni mtu wa kulala lala na siku moja utakufa kabisa kiroho kwasababu uwepo wa Mungu umekwisha kukuacha. Mheshimu Mungu.

Bwana atasaidie sana.

mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MIMI NI ALFA NA OMEGA.

DHAMBI YA MAUTI

YESU ANA KIU NA WEWE.

NI KIPI KINAMZUIA MUNGU KUZUNGUMZA NA SISI?

NDIPO HUENDA AKACHUKUA PEPO WENGINE SABA.

JINSI YA KUPOKEA UPONYAJI, TUNAPOMWOMBA BWANA ATUGUSE MARA YA PILI.

Sikio lisikialo, na jicho lionalo, BWANA ndiye aliyeyafanya yote mawili.

Rudi nyumbani

Print this post

Tufanyaje ili tuonekane tunampenda Mungu?

SWALI: Naomba kufahamu kumpenda Mungu kukoje, Je tufanyeje ili tuonekane tunampenda?


JIBU: Tofauti na sisi tunavyotafsiri upendo, kwamba ni kuonyesha hisia zilizo nzuri kwa mwingine, Kwamfano kuhurumia, kujali, kuthamini, kuhudumia, kusifia, kujitoa n.k.

Lakini kwa Mungu ili tuonekane tunampenda yeye, ni zaidi ya kuonyesha hisia.. Kwani waweza kuwa na hisia nzuri kwa Mungu, mpaka ukatoa machozi, unapotafakari matendo yake makuu, Unapotazama wema wake na fadhili zake, na uumbaji wake wote, vikakufanya ujihisi kumpenda sana Mungu.

Lakini hili mbele za Mungu linaweza lisihesabike, kwasababu si kile Mungu anachotaka kukiona kwetu..

Hivyo ni vizuri kufahamu mambo haya makuu matatu (3), ambayo  ukifanya bidii kuyatenda, bila hata kuonyesha hisia Fulani kubwa,  Mungu atakuona unampenda sana, na matokeo yake atajidhihirisha kwako. Mambo yenyewe ni haya;

1). Zishike amri zake:

Amri zake ni pamoja na kukaa mbali na dhambi, halikadhalika, kupendana sisi kwa sisi.

Biblia inasema..

1Yohana 5:3 “Kwa maana huku ndiko kumpenda Mungu, kwamba tuzishike amri zake; wala amri zake si nzito.

4 Kwa maana kila kitu kilichozaliwa na Mungu huushinda ulimwengu; na huku ndiko kushinda kuushindako ulimwengu, hiyo imani yetu”.

Umeona, Bado Bwana Yesu analirudia tena hilo hilo neno katika

Yohana 14:15 Mkinipenda, mtazishika amri zangu.

16 Nami nitamwomba Baba, naye atawapa Msaidizi mwingine, ili akae nanyi hata milele;

Na amri yake iliyo kuu aliyotupa, ni kupendana sisi kwa sisi, kama nafsi zetu (Yohana 13:34), na zaidi kuwapenda mpaka wale wanaotuchukia. Tukizingatia hayo mambo mawili, huku tukijilinda na dhambi, kwa maisha ya utakatifu, hiyo ni dalili ya kwanza inayofunua upendo wetu wa kweli kwa Mungu.

2) Uchukie ulimwengu:

Kuupenda ulimwengu kunakwenda kinyume na kumpenda Mungu, biblia inasema hivyo katika;

1Yohana 2:15 “Msiipende dunia, wala mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake.

16 Maana kila kilichomo duniani, yaani, tamaa ya mwili, na tamaa ya macho, na kiburi cha uzima, havitokani na Baba, bali vyatokana na dunia.

17 Na dunia inapita, pamoja na tamaa zake, bali yeye afanyaye mapenzi ya Mungu adumu hata milele.

Ukisema unampenda Mungu, halafu, bado unapenda fashion, unapenda anasa, unapenda party party, na tafrija tafrija, mipira, muvi muvi kila wakati, miziki ya kidunia, kampani za wenye dhambi, vijiwe vijiwe visivyo na maana.

Basi ufahamu upendo kwa Mungu hautakaa uwepo ndani yako, Biblia inasema hivyo. Jitenge na mambo ya kiulimwengu kwa jinsi uwezavyo, tafuta ndugu katika Bwana ndio wawe watu wako wa karibu, biblia ndio iwe novel yako, nyimbo za sifa ndio ziwe mziki wako, kanisani ndio pawe kijiweni pako. Ukizingatia hayo kwa bidii, basi kidogo kidogo, upendo kwa Mungu usio wa kinafki utaingia ndani yako. Na Mungu atauona.

3) Husisha kila kitu chako chote kwa ajili ya Mungu:

Biblia inasema..

Marko 12:29 “Yesu akamjibu, Ya kwanza ndiyo hii, Sikia, Israeli, Bwana Mungu wetu ni Bwana mmoja;

30 nawe mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote, na kwa nguvu zako zote”.

Hapo hajasema, “mpende tu Bwana Mungu wako”, halafu basi, bali anasema utampenda kwa mambo yote manne, yaani roho, moyo, mwili na akili.

Mungu hataki kupendwa kwenye roho tu, bali hata kwenye akili zako, na nguvu zako. Ikiwa unafikiria Mungu anataka umtafute tu siku za ibada, umwabudu halafu basi, bado hujakamilisha kumpenda, bali anataka nguvu zako unazokwenda kuzisumbukia huko katika kutanga tanga kwako ziishie kwake, Mali zako, kujitoa kwako katika kuujenga ufalme wa Mungu, na kusambaza habari zake.

Vilevile akili yako yote uitumie kwake, ubuni utafiti ni kwa jinsi gani, unaweza kuifanya kazi ya Mungu iwe bora zaidi, kama vile unavyofikiri kila siku ni jinsi gani unavyoweza kuyafanya maisha yako kuwa bora kwake, sio tu kumwachia mtumishi Fulani,au mchungaji Fulani afanye yeye kila kitu, angali vingine vipo ndani ya uwezo wako wewe.

Kwa kuzingatia mambo hayo matatu, basi utakuwa umempenda Mungu, na yeye atalijua hilo, na matokeo yake ni kujidhihirisha kwako, na kukuhudumia. Huko ndio kumpenda Mungu.

Zaburi 91:14 “Kwa kuwa amekaza kunipenda Nitamwokoa; na kumweka palipo juu, Kwa kuwa amenijua Jina langu.

15 Ataniita nami nitamwitikia; Nitakuwa pamoja naye taabuni, Nitamwokoa na kumtukuza;

16 Kwa siku nyingi nitamshibisha, Nami nitamwonyesha wokovu wangu”.

Bwana akubariki.

mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

TAFUTA UZIMA WA MILELE NA SI UZIMA TU!.

Kula uzao wa tumbo lako maana yake nini? (Kumbukumbu 28:53)

NI WAKATI GANI SHETANI ANAPENDA KUMSHAMBULIA MWAMINI?

UPENDO NI NINI NA JE! KUNA AINA NGAPI ZA UPENDO?

ZIFAHAMU KAZI TATU ZA ROHO MTAKATIFU KATIKA ULIMWENGU.

NI NINI TUNAJIFUNZA KWA YOANA NA MANAENI?

Rudi nyumbani

Print this post

Ila atapewa mara mia sasa,Ndugu wake(Marko 10:30)

SWALI: Mbona katika Marko 10:30 Bwana Yesu anasema tutapata mara mia ‘wake’? Hii si inatupa uthibitisho kuwa ndoa za mitara ni sawa?


JIBU: Tusome kwa ukaribu vifungu vyenyewe;

Marko 10:28 “ Petro akaanza kumwambia, Tazama, sisi tumeacha vyote tukakufuata wewe.
29 Yesu akasema, Amin, nawaambieni, Hakuna mtu aliyeacha nyumba, au ndugu waume, au
ndugu wake, au mama, au baba, au watoto, au mashamba, kwa ajili yangu, na kwa ajili ya Injili,
30 ila atapewa mara mia sasa wakati huu, nyumba, na ndugu waume, NA NDUGU WAKE, na mama,
na watoto, na mashamba, pamoja na udhia; na katika ulimwengu ujao uzima wa milele.
31 Lakini wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho; na wa mwisho watakuwa wa kwanza”.

Hapo hakuna mahali popote Bwana Yesu amesema tutapata mara mia ‘wake’, isipokuwa anasema tutapata mara mia  “ndugu wake”.  Akimaanisha ndugu wa KIKE, kama tu alivyosema ndugu WAUME, tutapata mara mia.

Maana yake ni kwamba mtu yeyote anayeingia gharama ya kumfuata Yesu kwa moyo wake wote, na kwa ajili ya injili yake, Bwana ameahidi kumrudishia kila kitu alichokipoteza mara100 zaidi.

Ikiwa aliwaacha dada  zake kumi(10), basi Bwana atamrudishia ndugu wadada mara mia zaidi.. yaani ndugu wadada elfu moja (1000), watakuja kuwa karibu naye.. wenye upendo kama tu ule wa wale wa kwanza   kwake.

Lakini tuseme, labda tuliacha wake zetu kwa ajili ya injili, Je! Mungu hataturudishia thawabu mara mia kwa kuwaacha wao?

Jibu ni kwamba ataturudishia pia mara mia, lakini haimaanishi kuwa tutapewa ‘wake’ tuwaoe, hapana, bali tutapewa ndugu, wenye Usaidizi kama tu wa wake.. Kumbuka, mwanamke aliumbwa kuwa msaidizi wa Adamu, hakuumbwa kuwa chombo cha starehe..

Hivyo hudumu aliyoitiwa mke duniani ni kuwa msaidizi.. Vivyo hivyo Mungu atakunyanyulia ndugu ambao watasimama kama wasaidizi kwako katika huduma, mara mia, kama wake.

Lakini haimaanishi utawaoa, hapana, kama itakavyokuwa kwa ndugu mara mia atakaokupa, hawataingia kwenye tumbo la mama yako na kuzaliwa ili wawe ndugu yako, bali watatoka nje, na kusimama kama ndugu.. Vivyo hivyo na kwa watoto na mambo mengine yote.

Lakini kwanini iwe hivyo? Ni ili kulitimiza lile neno la Bwana Yesu alilosema..

 “Kwa kuwa mtu atakaye kuiponya nafsi yake ataiangamiza, na mtu atakayeiangamiza nafsi yake
kwa ajili yangu ndiye atakayeisalimisha”.(Luka 9.24)

Bwana akubariki.

mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

TWEKA MPAKA VILINDINI.

KALAMU YENYE UONGO YA WAANDISHI IMEIFANYA KUWA UONGO.

Na hekima imejulikana kuwa ina haki kwa watoto wake wote.

Biblia inamaana gani iliposema “Dhambi ilipozidi, Neema ilizidi kuwa nyingi Zaidi”.

KWANINI KUWE NA UTAWALA WA MIAKA 1000

MADHARA YA KUTOIJUA KWELI YOTE!

KIASI NI NINI KATIKA UKRISTO?

Rudi nyumbani

Print this post

JINSI YA KUISHINDA DHAMBI INAYONITESA.

SWALI: Shalom. Naomba kufahamu nifanye nini ili niweze kuishinda ile dhambi inayonitesa.?


JIBU: Dhambi inayomtesa mtu kwa jina lingine inaitwa “dhambi izingayo kwa upesi”, ambayo tunaisoma katika;

Waebrania 12:1

[1]Basi na sisi pia, kwa kuwa tunazungukwa na wingu kubwa la mashahidi namna hii, na tuweke kando kila mzigo mzito, na dhambi ile ituzingayo kwa upesi; na tupige mbio kwa saburi katika yale mashindano yaliyowekwa mbele yetu,

Si kila dhambi, huwa inaondoka kirahisi ndani ya mtu pindi anapookoka..

Ni kweli asilimia kubwa ya dhambi mtu anajaliwa na Roho Mtakatifu kuziacha wakati ule anapotubu, na kudhamiria kumfuata Yesu kwa moyo wake wote, kwamfano mwingine alikuwa ni mwizi, mwongo, mshirikina, mzinzi n.k.

Lakini alipookoka hivi vyote akaviacha kiwepesi kabisa..Lakini ndani yake kukawa na shinikizo kubwa la kuendelea kufanya punyeto, au mawazo machafu kumtawala..hivyo hiyo hali ikawa inamtesa  kwa kipindi kirefu na kumfanya akose raha, wakati mwingine amejaribu kuomba sana lakini hali ipo vilevile.

Mwingine hayo yote ameweza  kuyashinda lakini dhambi ya usengenyaji imekuwa ni mzigo mzito sana kwake kuutua, mwingine ulevi, mwingine kutazama picha za ngono n.k.

Ndugu ikiwa umeokoka na unaona hiyo dhambi ni kikwazo kikubwa  kwako, nataka nikuambie huna budi kushindana nayo hadi uishinde..kwasababu usipoishinda itakupeleka jehanamu.

Kaini alikuwa na dhambi ya hasira na wivu, akaipuuzia, lakini  Mungu akamwambia, unapaswa uishinde

Mwanzo 4:6-7

[6]BWANA akamwambia Kaini, Kwa nini una ghadhabu? Na kwa nini uso wako umekunjamana?

[7]Kama ukitenda vyema, hutapata kibali? Usipotenda vyema dhambi iko, inakuotea mlangoni, nayo inakutamani wewe, walakini yapasa uishinde.

Dhambi kama hizi huwa zilishatia mizizi mrefu ndani ya mtu tofauti na nyingine, hivyo kuziondoa inahitaji nguvu ya zaida..

Na njia pekee ya kuzishinda hizi ni moja tu nayo ni “kwa Kuua vichocheo vyote vinavyokupelea kuitenda dhambi hiyo”..

Mithali 26:20 Inasema;

“Moto hufa kwa kukosa kuni;..”

Moto hauwezi kuendelea muda mrefu mahali ambapo hapana kichocheo chake kama kuni au mafuta..haijalishi utakuwa na nguvu kiasi gani, mwishowe utazima tu.

Hakuna dhambi yoyote iliyo ngumu kuishinda hapa duniani endapo vichocheo vyake vitauliwa kikamilifu.

Kwa mfano kufahamu ni jinsi gani utaweza kuishinda dhambi ya uzinzi fungua hapa..>>> MOTO HUFA KWA KUKOSA KUNI.HATA UASHERATI NAO

Kwa siku za mwanzo, utaona ni shida lakini kwa jinsi siku zinavyozidi kwenda Mungu anakutia nguvu na hatimaye inakuwa ni dhambi nyepesi sana kuishinda kuliko hata zote…

Ni kawaida hata gari lililo katika mwendo kasi likichuna breki kwa ghafla, haliwezi kusimama hapo hapo…litasogea mbele kidogo, ndipo litulie japokuwa tairi tayari zilishaacha kuzunguka, kitambo kidogo.

Vivyo hivyo na wewe katika hiyo dhambi inayokuzinga kwa upesi, inayokufanya usipige mbio kwa wepesi, katika safari yako ya ukristo, kwa siku za mwanzoni itaonyesha  kama kuleta ukinzani lakini kwa jinsi unavyokaa mbali na vichocheo vyake hatimaye itakufa tu ndani yako…ni kitendo cha muda.

Kwamfano kama wewe ni mvuta sigara, kiu ya kuvuta ikija, ondoka mazingira ya upatikanaji wake, vilevile wale marafiki uliokuwa unavuta nao jitenge nao waone kama kaburi, hicho kiu kitakutesa tu kwa muda mfupi, lakini uking’ang’ana utakuja kushangaa kimetoweka tu ghafla..hapo ndio tayari kimekufa..

Shindana, hadi ushinde…usikubali kusema mimi nimeshindwa kuacha hiki au kile, usikubali hiyo hali, usiwe mnyonge wa dhambi, kwasababu wanyonge wote hawataurithi uzima wa milele biblia inasema hivyo katika Ufunuo 21:27

Ikiwa ni fashion, wewe kama mwanamke ni lazima uishinde, ikiwa ni kamari, ikiwa ni miziki ya kidunia kanuni ni hiyo hiyo…Ua vichocheo vyote. Kaa mbali nayo, ulizoea kutazama picha za ngono mitandaoni, na ulipookoka mawazo yale yanajirudia rudia kwenye fahamu zako, endelea kukaa mbali na vichocheo hivyo, acha mazungumzo mabaya, left magroup yasiyokuwa na msingi kwako, epuka kutazama au kusikiliza kitu chochote chenye maudhui ya uzinzi, marafiki wazinzi waepuke, marafiki wasiokuwa na maana wa jinsi tofauti wapeuke, utafika wakati hayo mawazo machafu yatakukimbia..

Zingatia hayo, na matokeo utayaona.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

JINSI YA KUSOMA BIBLIA.

MLANGO MWINGINE WA ADUI KUTULETEA MAJARIBU.

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 5)

YAFUATAYO NI MAWAZO YA ADUI HIVYO USIYASIKILIZE.

CHUKIZO LA UHARIBIFU.

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita.

JE! NINAWEZA KUPOTEZA FURAHA YA WOKOVU?

Rudi nyumbani

Print this post

USIOGOPE KUMWADHIBU MWANAO.

Tunaishi katika ulimwengu ambao, maadili yameporomoka sana, na bado yanaendelea kuporomoka kwa vijana na watoto..Na hiyo inatufanya tuelekeze lawama kwa watoto; tukisema watoto wa siku hizi wamebadilika sana, lakini ukweli ni kwamba wazazi ndio wamebadilika, watoto ni walewale.

Malezo ya mzazi kwa mtoto ni muhimu sana, mtoto si kama nyau, ambaye kitu pekee anachohitaji ni chakula tu na sehemu ya kulala, hata ukimwacha mwaka mzima bila kumjali kwa vingine, hakuna hasara yoyote, bado ataendelea kuwa paka..

Lakini kwa mwanadamu sivyo..yeye hafugwi, bali analelewa..na malezi ni zaidi ya chakula na nguo na mahali pa kulala.. Hapo ndipo wazazi wengi wanashindwa kuelewa.

Kwasababu mtoto atahitaji kuwa na maarifa, nidhamu, uadilifu, hekima, busara, upendo, utiifu, upambanuzi n.k. Ili aweze kuishi vema katika huu ulimwengu.

Hivi vyote hazaliwi navyo, bali anajifunza anapokuwa duniani..hivyo akikosa msaada sahihi, basi ibilisi atatumia fursa hiyo kumfundisha elimu yake na nidhamu yake hapa ulimwenguni.

Hivyo wewe kama mzazi au mlezi una jukumu kubwa sana zaidi ya lile la kumlisha na kumvisha na kumsomesha..hizo ni hatua 3 katika ya 1000, anazopaswa azijue.

Ikiwa hukupata masomo yaliyotangulia ya malezi ya watoto, basi waweza kututumia ujumbe kwa namba hii, ili tuweze kukutumia chambuzi za nyuma. Au tembelea website yetu hii www.wingulamashahidi.org. au tutumie ujumbe kwa namba hizi +255693036618

Leo tutaona njia nyingine ya kumlea mtoto vema.

Na njia yenyewe si nyingine zaidi ya kutumia KIBOKO.

Lugha hii inaweza isiwe nzuri masikioni mwa wazazi lakini ni tiba nzuri kwa malezo yao. Hata ‘panadol’ haina ladha nzuri mdomoni, lakini pale inapotutibu tunaishukuru, ndio maana tunayo siku zote majumbani kwetu.

Lakini ni kwanini utumie kiboko kwa mtoto?

Sababu zipo mbili.

1) Ni kwasababu ujinga umefungwa moyoni mwake

2) Mungu naye huwa anatuadhibu sisi.

  1. Tukianzana na sababu ya kwanza biblia inatuambia..

Mithali 22:15

[15]Ujinga umefungwa ndani ya moyo wa mtoto; Lakini fimbo ya adhabu itaufukuzia mbali.

Ni vizuri ukafahamu kuwa mtoto kama mtoto huwa ana ujinga mwingi ndani yake..yule si kama wewe, unapoona anang’ang’ania kitu fulani kisichopendeza halafu wewe kama mzazi unaamua tu kumwachia kisa anakililia, usidhani kuwa anaelewa matokeo ya kile anachokitaka..

Kumbuka yule hatafakari, wewe unatafakari, hivyo basi ukimsikia anatukana, usisubiri apumzike bali hapo hapo shika kiboko chapa. Ukiona unamwagiza kitu hatii, chapa..ukiona hawaheshimu watu wazima hata baada ya kuonywa mara nyingi..chapa..usiogope labda atakufa…biblia inasema kiboko cha adili hakiui..

Mithali 23:13

[13]Usimnyime mtoto wako mapigo; [14] Maana ukimpiga kwa fimbo hatakufa.

Hiyo itamsaidia sana kuundoa ujinga mwingi wa kipepo ambao mwingine kwa maneno tu, peke yake au kwa kufundishwa hauwezi kutoka..

  • 2) Mungu naye anatuadhibu.

Na sababu ya pili kwanini tuwaadhibu watoto wetu kwa kiboko pale wanapokosea..ni kwasababu Mungu naye anatuadhibu sisi watoto wake.

Biblia inasema hivyo..

Waebrania 12:6-7

[6]Maana yeye ambaye Bwana ampenda, humrudi, Naye humpiga kila mwana amkubaliye.

[7]Ni kwa ajili ya kurudiwa mwastahimili; Mungu awatendea kama wana; maana ni mwana yupi asiyerudiwa na babaye?

Umeona..Sisi hatuna hekima ya kumzidi Mungu, tengeneza picha Bwana angekuwa anatuona tunatukana wengine halafu hachukui hatua yoyote anacheka tu..si tungaangamia..Mungu alipomuona Daudi anamchukua mke wa Huria halafu anaendelea kusema wewe ni mtumishi wangu unayeupendeza moyo wangu..Daudi leo angekuwa wapi kama sio kuzimu? Lakini Mungu alimuadhibu vikali…na baadaye akatubu akapona..

Nasi pia biblia inatuambia tutakuwa wakamilifu kama Baba yetu wa mbinguni alivyomkamilifu..(Mathayo 5:48)

Mzazi unayemtazama mwanao, anafanya ujinga, unaogopa kumchapa atalia..bado hujawa mkamilifu kama Mungu.

Hivyo anza sasa kutimiza huduma hii, ili kesho mtoto huyo afanyike baraka na neema kwa ulimwengu.

Lakini zingatia: Haimaanishi kuwa umpige pige mtoto ovyo kila saa anapokosea..hapana zipo sehemu zinastahili kiboko, zipo zinazostahili maonyo, zipo zinazostahili kuelimishwa..Zote zina umuhimu wake mkubwa bila kupuuzia hata moja.

Bwana akubariki

Shalom

mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MZAZI, JALI MAISHA YA KIROHO YA MTOTO WAKO.

KILEMBA CHA NEEMA, JE! UMEMVIKA MWANAO?

TUMEFANYIKA KUWA WANA WA MUNGU!

NINI MAANA YA SISI KUWA WATOTO WA MUNGU?

NI NINI KINATOKA KINYWANI MWA MTOTO WAKO?

MALEZI YA MTOTO MCHANGA.

Rudi nyumbani

Print this post

NAO WAKAMSHINDA KWA DAMU YA MWANA-KONDOO.

Mafundisho maalumu kwa waongofu wapya: Sehemu ya tatu.

Ikiwa wewe ni mwongofu mpya, yaani umeokoka hivi karibuni, basi mafundisho haya yanakufaa sana katika hichi kipindi ulichopo.

Ikiwa ulipitwa na mafundisho ya nyuma, basi waweza kututumia ujumbe kwa namba zetu hizi +255693036618 tukakutumia mafundisho hayo.

Ni muhimu kufahamu kuwa, unapookoka yupo adui atakayesimama kinyume chako kukupinga wakati wote, ili uiache imani. Na huyo si mwingine zaidi ya shetani. Hivyo katika hatua hizi za awali, huna budi kufahamu silaha madhubuti za kuweza kumwangusha, Kwasababu ukizikosa ujue kuwa utakufa tu kiroho. Na silaha yenyewe tunazisoma katika vifungu hivi;

Ufunuo 12:9 “Yule joka akatupwa, yule mkubwa, nyoka wa zamani, aitwaye Ibilisi na Shetani, audanganyaye ulimwengu wote; akatupwa hata nchi, na malaika zake wakatupwa pamoja naye.
10 Nikasikia sauti kuu mbinguni, ikisema, Sasa kumekuwa wokovu, na nguvu, na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake; kwa maana ametupwa chini mshitaki wa ndugu zetu, yeye awashitakiye mbele za Mungu wetu, mchana na usiku.
11 NAO WAKAMSHINDA KWA DAMU YA MWANA- KONDOO, na kwa neno la ushuhuda wao; ambao hawakupenda maisha yao hata kufa”.

Jiulize hapo kwanini haijasema wakamshinda kwa mafuta ya upako, au kwa kanisa zuri, au kwa maombi ya vita.. Bali kwa damu ya Mwana kondoo na kwa neno la ushuhuda wao.
Kuna nini katika damu ya Yesu? Na ushuhuda ulionao?
Ni lazima ufahamu umuhimu wa damu yake, katika maisha yako ya wokovu.
Damu ya Yesu ilifanya mambo makuu matatu

  1. Kuondoa dhambi
  2. Kunena juu yetu
  3. kukanyaga nguvu za ibilisi

1) Kuondoa dhambi.


Biblia inasema..

Waebrania 9:22 “Na katika Torati karibu vitu vyote husafishwa kwa damu, na pasipo kumwaga damu hakuna ondoleo”.

Katika agano la kale Utakaso wa kila namna, ulitegemea damu za wanyama, kwasababu ndio kanuni ya Mungu ya kiroho ya kuondoa dhambi, hivyo tangu zamani zile haikupatikana damu yoyote kamilifu isiyo na hila wala mawaa itakayoweza kuondoa dhambi za mtu moja kwa moja, bila kuacha kimelea chochote. Na ndio maana kumbukumbu la dhambi lilikuwepo wakati baada ya wakati , hivyo ilimpasa kuhani mkuu kila mwaka aingie kule hemani akiwa na damu ya wanyama ili kuwapatanisha wana wa Israeli,
Lakini sasa Yesu alipokuja, damu yake ilikuwa ni kamilifu zaidi ya wanyama, yeye tu ndiye aliyeweza, kusafisha na kuondoa kabisa dhambi ya mwanadamu isikumbukwe na Mungu milele, bila kuhitaji tena kuhani kila mwaka kwenda kuomba rehema kwa dhambi zilizotangulia.


Hii ikiwa na maana gani?
Ukiukosa ufunuo huu, kuhusiana na nguvu iliyopo katika damu ya Yesu iliyomwagika msalabani, basi ni ngumu sana, kuamini kama dhambi zako za kale Mungu alishazifuta na kuzisahau kabisa kabisa.
Ni kawaida kwa waongofu wapya kuletewa mawazo haya na ibilisi kwamba, bado Mungu anawaona ni wachafu, bado Mungu anakumbuka zile dhambi walizozitenda nyuma, zile mimba walizotoa, ule uzinzi walioufanya nje ya ndoa, rushwa walizokuwa wanakula, mauaji waliyoyafanya, waganga waliokuwa wanawafuata.


Hii ndio silaha kubwa ya ibilisi kwa waongofu wapya. Wanajiona kama vile bado hawajasamehewa vizuri, bado laana zinawafuatilia, Ndugu, ujue hayo ni mawazo ya shetani, kwasababu umekosa kujua gharama Yesu aliyoingia kwa ajili ya dhambi zako. Ile damu yake kumwagika, ilikuwa ni kukomesha dhambi zako zote na laana zako kabisa kabisa..


Ndio maana hapo biblia inasema, wakamshinda kwa damu ya mwana-kondoo, na ushuhuda wao, yaani ushuhuda wa kukombolewa na Yesu. Ndio silaha kubwa sana ya kumshinda ibilisi.
Hivyo mawazo kama hayo yakikujia yakatae, sema mimi nimeshasamehewa, ya kale yamepita, tazama yamekuwa mapya. Mimi sina deni la dhambi, Ukifanya hivyo, shetani atajua umeshafahamu nafasi yako, hivyo atakukimbia, na utaishi maisha ya amani na kutojihukumu.


2) Kunena juu yetu.


Damu pia inafanya kazi ya kunena.

Waebrania 12:24 “na Yesu mjumbe wa agano jipya, na damu ya kunyunyizwa, inenayo mema kuliko ile ya Habili”.

Kaini alipomuua ndugu yake Habili, Biblia inasema Mungu alimwambia Kaini sauti ya damu ya ndugu yake inamlilia kutoka ardhini (Mwanzo 4:10). Maana yake ni kuwa Mungu alikuwa anaisikia ili sauti ikinena, ikiomba, ikitaka haki itendeke, haikutulia tu.
Hata leo ukiona mtu anapitia majanga majanga fulani hivi, utasikia watu wakisema, ni kwasababu alimuua mama yake hivyo ile damu inamfuatilia..


Kuonyesha kwamba kuna uhalisia fulani katika damu ya mtu kupatiliza mema au mabaya.
Na ndivyo ilivyo kwa damu ya Yesu, inanena Mema, kuliko ile ya Habili, maana yake, hata sasa inazungumza, juu ya wale wote waliompokea yeye mbele ya kiti cha enzi cha Mungu. Inasema huyu anastahili kulindwa, huyu anastahili baraka, huyu anastahili furaha, huyu anastahili heshima, huyu anastahili kibali, afya n.k.


Hivyo wewe uliyeokoka ni wajibu wako kujua jambo hili, ili usiishi kama yatima hapa duniani. Ulipokuwa dhambini damu ya Yesu ilikuwa haineni juu yako, kwasababu haukuwa ndani ya agano lake. Lakini sasa upo, fahamu kuwa, Yesu anakuombea kila siku kwa Baba, hivyo kuwa na ujasiri ukijua kabisa nyuma yako ipo baraka, neema na habati wakati wote. Kwa jinsi siku zinavyozidi kwenda utayathibitisha hayo yote.

Warumi 8:33 “Ni nani atakayewashitaki wateule wa Mungu? Mungu ndiye mwenye kuwahesabia haki.
34 Ni nani atakayewahukumia adhabu? Kristo Yesu ndiye aliyekufa; naam, na zaidi ya hayo, amefufuka katika wafu, naye yuko mkono wa kuume wa Mungu; tena ndiye anayetuombea”.

Hivyo mishale yote ya hofu, wasiwasi, mashaka, ambayo shetani atajaribu kukutumia ili urudi nyuma, ikatae, mishale ya kesho nitaishije, nikipoteza kile kwasababu ya Yesu itakuwaje? ondoa hayo mawazo ya kuangamia, kwasababu ipo damu inayonena kwa ajili yako usiku na mchana, ili utembee katika njia salama ya uzima.

Zaburi 27:1 “Bwana ni nuru yangu na wokovu wangu, Nimwogope nani? Bwana ni ngome ya uzima wangu, Nimhofu nani?
2 Watenda mabaya waliponikaribia, Wanile nyama yangu, Watesi wangu na adui zangu, Walijikwaa wakaanguka.
3 Jeshi lijapojipanga kupigana nami, Moyo wangu hautaogopa. Vita vijaponitokea, Hata hapo nitatumaini.
4 Neno Moja nimelitaka kwa Bwana, Nalo ndilo nitakalolitafuta, Nikae nyumbani mwa Bwana Siku zote za maisha yangu, Niutazame uzuri wa Bwana, Na kutafakari hekaluni mwake”.
Lishike sana hili, ukilikosa, shetani atatumia upenyo huu kukurudisha nyuma, kama alivyofanikiwa kuwarudisha wengi.


3) Kukanyaga nguvu za ibilisi.

Utajiuliza ni kwanini Bwana Yesu, hakulisema hili neno “IMEKISHWA”, Mahali popote katika huduma yake, mpaka siku ile alipopelekwa pale msalabani? Ni kwamba alijua hakuna kuzimaliza nguvu na utawala wa ibilisi bila agano la damu timilifu.


Hivyo aliposema IMEKWISHWA, Ni kweli ilikwisha, na ndio maana aliwaambia mitume wake maneno haya;

Luka 10:18 “Akawaambia, Nilimwona Shetani, akianguka kutoka mbinguni kama umeme.
19 Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru.

Ni lazima ujue kwa damu ya Yesu, shetani, hana nguvu yoyote juu yako. Kwamfano mwanajeshi dhaifu akitambua kuwa bomu alilonalo la nyuklia linaweza kuteketeza mji mzima, hataweza kuwa na hofu, na wanajeshi 1000 wenye nguvu, wanaomjia na bunduki zao. Kwasababu anafahamu akilituma tu kombora lake moja, kikosi chote kinakuwa jivu.


Ndivyo ilivyo kwako wewe uliyeokoka, fahamu kuwa hatua uliyopo, shetani hana nguvu zozote za kukushinda, kwasababu tayari nguvu zako ni nyingi kuliko zake, haijalishi hali yako ya uchanga kiroho. Hivyo, usiogope wachawi, usiogope mapepo, usiogope hata maadui zako. Lolote linalokuja mbele zako, uwe ni udhaifu, magonjwa, mashambulizi ya shetani, kemea kwa jina la Yesu, vitaondoka, usiwe mnyonge kwa shetani, kwasababu yule ni kama kinyago tu kinasimama hapo kukutisha, lakini hakina nguvu yoyote.
Hivyo zingatia sana kuyatafakari hayo.


Na Bwana akubariki.

mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MAFUNDISHO MAALUMU KWA WAONGOFU WAPYA.

KAA MAJANGWANI.

USIMPE NGUVU SHETANI.

NIFANYE NINI ILI MUNGU AYAJIBU MAOMBI YANGU?

KUNA AINA NGAPI  ZA MAOMBI?

Nini maana ya “Nitaomba kwa roho, tena nitaomba kwa akili pia?

FUNGUO ZA UZIMA, MAUTI NA KUZIMU.

Rudi nyumbani

Print this post

KAA MAJANGWANI.

MAFUNDISHO MAALUMU KWA WAONGOFU WAPYA.

Sehemu ya pili: Kaa Majangwani:

Luka 1:80 “Yule mtoto akakua, akaongezeka nguvu rohoni, akakaa majangwani hata siku ya kutokea kwake kwa Israeli”.

Ni kawaida ya Mungu, kuwaandalia Watoto wake, mahali maalumu pa kukulia kiroho.. Ikiwa unatamani nguvu zako za rohoni ziongozeke kwa kasi wewe kama mwongofu mpya uliyezaliwa mara ya pili, huna budi kukaa majangwani.

Mungu alipowatoa wana wa Israeli Misri, hakuwavukisha moja kwa moja na kuwafikisha Kaanani ndani ya siku moja, bali aliwapitisha kwanza jangwani, kuwalisha huko na kuwakuza kiroho, kwa muda wa miaka 40, kwasababu walikuwa bado ni Watoto wachanga, na ndipo baadaye wakaingia Kaanani, wakiwa Hodari na nguvu nyingi rohoni.

Hosea 11:1 “Israeli alipokuwa mtoto, nalikuwa nikimpenda, nikamwita mwanangu atoke Misri”.

Biblia pia inatuambia Yohana mbatizaji alipozaliwa, alikimbilia majangwani huko kuishi, na matokeo yake akakua na kuongozeka nguvu nyingi sana rohoni kwa kasi, na ndio maana hatushangai kwanini Bwana Yesu anamshuhudia na kusema katika wazao wa wanawake hakuwahi kutokea mtu aliyekuwa mkuu kama Yohana Mbatizaji.(Mathayo 11:11).. Hiyo yote ni kwasababu gani? Ni kwasababu alitumia Muda mwingi majagwani.

Sasa Kiroho jangwani ni wapi?

Haimaanishi kuwa ni sisi tukimbilie majangwani tukaishi huko, ili tukue kiroho hapana… Kama tunavyojua jangwani ni mahali ambapo hapana uwepo wa wanadamu, ni mahali pa ukiwa, pasipokuwa na huduma zozote za kijamii.. Ndivyo inavyompasa mkristo aende rohoni.

Unapaswa katika hatua zako za awali za wokovu: Kwa bidii zote uwe tayari, kuukana huu ulimwengu. Kukaa mbali na mambo yote yanayousonga wokovu wako, bila kujali unapoteza nini, au unakosa nini..

Ukiokoka, kubali kuachana na wale marafiki zako wa kale uliokuwa unakwenda nao disco, uliokuwa unakunywa nao pombe, uliokuwa unatukana nao, kubali kuwa mpweke, kwa kipindi Fulani, kwani hivyo ndivyo unavyoiponya roho yako.

Ukiokoka, kubali wakati mwingine, kupoteza hiyo kazi isiyo halali kwa Mungu, kama unafanya biashara ya pombe acha, ..wala usidhani kuwa utaangamia, kwamba Mungu atakuacha ufe, hilo wazo ondoa, uwezo wa kukulisha Mungu anao, Kama alivyofanya kwa wana wa Israeli kule jangwani, atafanya na kwako pia..

Biblia inasema..

Ufunuo 12:13 “Na joka yule alipoona ya kuwa ametupwa katika nchi, alimwudhi mwanamke yule aliyemzaa mtoto mwanamume.

14 Mwanamke yule akapewa mabawa mawili ya tai yule mkubwa, ili aruke, AENDE ZAKE NYIKANI HATA MAHALI PAKE, hapo alishwapo kwa wakati na nyakati na nusu ya wakati, mbali na nyoka huyo”.

Umeona, Mungu ameshaandaa mahali pako huko nyikani, pa kukulisha kwa wakati wako na majira yako. Hivyo usiogope wewe uliyemzaa Kristo maishani mwako.

Kama wewe ni binti kubali kukaa mbali na Fashion, kubali kujisitiri na kuchoma hivyo vimini na masuruali, kubali kuonekana umerukwa na akili kwa ajili ya Kristo, hata ulimwengu mzima ukikuona mjinga, kubali hiyo hali, weka kando kila mzigo wa dhambi, kwasababu ndivyo unavyoiponya roho yako.

Je! Faida yake ni ipi?

Faida yake ni kwamba Yesu anapata nafasi ya kukupitisha katika madarasa yake, na kwasababu husongwi na mambo mengine, hivyo kasi yako ya kukua kiroho itakuwa ni kubwa sana..

Maandiko yanasisitiza hilo katika;

Isaya 40:3 “Sikiliza, ni sauti ya mtu aliaye, Itengenezeni nyikani njia ya Bwana; Nyosheni jangwani njia kuu kwa Mungu wetu”.

Kuonyesha kwamba mahali pekee ambapo utamtengenezea Mungu njia, katika maisha yako ni jangwani.

Leo hii utaona watu wengi wamedumu katika wokovu kwa miaka mingi, lakini huoni mabadiliko makubwa yoyote ndani yao, bado ni wachanga kila siku wanataka wanyweshwe tu maziwa, ni kwasababu gani?

Ni kwasababu hawakumpa Kristo, nafasi ya kuwafundisha majangwani..Walilikimbia jangwa, wakakaa ulimwenguni, na hivyo Bwana akawaacha.

Ndugu/Dada uliyeokoka hivi karibuni usiipuzie hiyo sauti inayokuambia, acha hiki, acha kile, mwache Rafiki yule, acha jambo lile..usiipuuzie kabisa, fanya hivyo, ni sharti upoteze, ili upate baadaye, majira haya ni kujikana nafsi yako, kuichukia nafsi yako, na kujitwika msalaba wako kumfuata Yesu, hilo haliwezi kuepukika ikiwa unataka ukue kiroho kwa kasi anayoihitaji Kristo ndani yako.

Mathayo 16:24 “Wakati huo Yesu aliwaambia wanafunzi wake, Mtu ye yote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake, anifuate.

25 Kwa kuwa mtu atakaye kuiokoa nafsi yake, ataipoteza; na mtu atakayepoteza nafsi yake kwa ajili yangu, ataiona.

26 Kwani atafaidiwa nini mtu akiupata ulimwengu wote, na kupata hasara ya nafsi yake? Au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake?

27 Kwa sababu Mwana wa Adamu atakuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika zake; ndipo atakapomlipa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake”.

Kabla ya kumzalia Mungu matunda ni lazima upitishwe jangwani, kutakaswa na Mungu, hivyo kuwa mwepesi kuacha udunia wako. Umfuate Yesu.

Bwana akubariki.

Shalom.

mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MAFUNDISHO MAALUMU KWA WAONGOFU WAPYA: Sehemu ya 1

EE MUNGU, MUNGU WANGU, NITAKUTAFUTA MAPEMA:

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

UNYAKUO.

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

BWANA AWEZA KUKUPA ZAIDI SANA KULIKO HIZO.

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 13 (Kitabu cha Hosea).

NAYE ALIKUWA HANA BUDI KUPITA KATIKATI YA SAMARIA.

Rudi nyumbani

Print this post