Category Archive Uncategorized @sw-tz

LAKINI SISI HATUKUIPOKEA ROHO YA DUNIA.

Biblia inasema..

1 Wakorintho 2:10-12

[10]Lakini Mungu ametufunulia sisi kwa Roho. Maana Roho huchunguza yote, hata mafumbo ya Mungu.

[11]Maana ni nani katika binadamu ayajuaye mambo ya binadamu ila roho ya binadamu iliyo ndani yake? Vivyo hivyo na mambo ya Mungu hakuna ayafahamuye ila Roho wa Mungu.

[12]LAKINI SISI HATUKUIPOKEA ROHO YA DUNIA, BALI ROHO ATOKAYE KWA MUNGU,makusudi tupate kuyajua tuliyokirimiwa na Mungu.

Zipo Roho mbili tu huku duniani.

Roho wa Mungu, na roho ya dunia. Kama mtu usipoipokea Roho ya Mungu, basi utaipokea roho ya dunia.

Hakuna mwanadamu anayejiongoza yeye mwenyewe  hapa duniani kwa roho yake tu. Hilo halipo.

Sasa kama jinsi hayo maandiko yanavyotuambia Roho wa Mungu huchunguza yote hata mafumbo ya Mungu.. Maana yake ni kuwa  yeye ndiye anayetufunulia siri za ufalme wa mbinguni, pamoja mambo ambayo Mungu anataka sisi tuyafanye tukiwa hapa duniani..ukisoma Yohana 16:13 inasema

[13]Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake.

Umeona hiyo ndio kazi ya Roho wa Mungu..ndio maana mtu aliyepokea kweli Roho Mtakatifu hawezi ishi kidunia kwasababu ni roho nyingine kutoka mbinguni kwa baba ipo yake ikimfundisha kuishi kulingana na misingi ya Mungu.

Lakini kinyume chake ni kweli. Watu wote ambao hawana Roho wa Mungu, wanayo roho ya dunia

Na yenyewe inachunguza mambo ya ulimwengu huu na kuwafundisha watu kuishi kiulimwengu. Ndio maana hushangai kuona tabia nyingi mbaya kila siku zikivumbiliwa lengo tu ni kuwafanya kuwa wakidunia.

Ukiona mwanamke unapenda fashion, vimini, kujichubua, unavaa suruali, unaweka mak-eups, kijana unavaa milegezo, unanyoa viduku, unakunywa pombe, unacheza kamari, unasikiliza nyimbo za kidunia,  unakwenda disco, unafanya ushirikina, unazini, unakula rushwa, unaiba, unapenda fedha, unadanganya ni uthibitisho kuwa roho ya dunia imekuvaa ndio maana inakuhimiza na kukufundisha kufanya hayo mambo kwa bidii.

Na mwenye roho hii ni shetani mwenyewe..Na kama ikitokea  Bwana Yesu amerudi leo..basi ujue utabaki hapa duniani. Kwasababu roho yako ni ya hapa hapa na ka  ikitokea umekufa basi utaenda moja kwa moja kuzimu kwasababu huko ndiko hatma ya roho hiyo itakapoishia..

Biblia ipo wazi kabisa inasema..

Warumi 8:9

[9]Lakini ikiwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu, ninyi hamwufuati mwili; bali mwaifuata roho. LAKINI MTU AWAYE YOTE ASIPOKUWA NA ROHO WA KRISTO, HUYO SI WAKE.

Ukikosa Roho wa Mungu, mbinguni huendi. Huu si wakati wa kumvumilia zaidi shetani, au kuwa rafiki wa dunia. Tunapojichanganya na mambo yake ndipo tunapovaliwa na roho hii chafu. Jiponye nafsi yako, ndugu, hizi ni siku za mwisho.

1 Yohana 2:15

[15]Msiipende dunia, wala mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake.

Hivyo ndugu, njia pekee ya kuipokea Roho ya Mungu ambayo itakusaidia na kukufundisha kuishi  maisha yanayompendeza Mungu. Ni kutubu kwa kumaanisha kabisa kugeuka na kuuacha ulimwengu..kisha ukishafanya hivyo unakuwa tayari kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo ikiwa kama haukubatizwa hapo mwanzo.

Baada ya huo wakati ni kuanza kuonyesha bidii ya kujifunza biblia, kuomba, kuzingatia fellowship zitakazokusaidia kukua kiroho. Na Roho wa Mungu akishaona umemaanisha hivyo, atashuka juu yako na kukutia Muhuri, na kukusaidia kuishi maisha ya wokovu.

Huku ukingojea siku yako ifike uende mbinguni, Roho hiyo ilipo.

Ikiwa utahitaji msaada ya kupokea wokovu, àu ubatizo sahihi.Basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi

+255693036618/ +255789001312

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizo

Mada Nyinginezo:

MFALME ANAKUJA

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 1)

BWANA AWEZA KUKUPA ZAIDI SANA KULIKO HIZO.

Kusubu ni nini? Miungu ya kusubu ni ipi?

Je tunaruhusiwa kushirikiana na wasanii wa kidunia katika kumwimbia Mungu?

TUKIO LA MUSA NA ELIYA KUMTOKEA BWANA, LIMEBEBA UJUMBE GANI?

Rudi nyumbani

Print this post

Kusubu ni nini? Miungu ya kusubu ni ipi?

Kusubu kibiblia ni kitendo cha kuyeyusha dhahabu au  fedha au ‘kito’ chochote kwa lengo la kuunda kitu kingine kipya.

Neno hilo utalisoma sehemu nyingi katika biblia kwa mfano hivi ni baadhi ya vifungu ambavyo utakutana nalo;

Mambo ya Walawi 19:4

[4]Msigeuke kuandama sanamu, wala msijifanyizie miungu ya kusubu mimi ndimi BWANA, Mungu wenu.

Maana yake msaifanye sanamu za kuyeyusha,

Kumbukumbu la Torati 27:15

[15]Na alaaniwe mtu afanyaye sanamu ya kuchonga, au ya kusubu, machukizo kwa BWANA, kazi ya mikono ya fundi, akaisimamisha kwa siri. Na watu wote wajibu, waseme, Amina.

Soma pia..

2Nyakati 24:4, 28:2, Waamuzi 17:3, Hesabu 33:52, 1Wafalme 7:23.

Maana yake ni ipi kiroho?

Hata sasa watu wengi, wanajiundia sanamu zao za kusubu rohoni bila wao kujijua…kwa kugeuza maumbile ya vitu vyema na kuvitumia isivyopasa..mpaka kuviabudu.

Kwa mfano fedha si mbaya lakini leo hii watu wameigeuza fedha kuwa mungu wao..kiasi kwamba kwao Mungu si kitu zaidi ya fedha, maisha yao yote ni kuhangaikia mali, kana kwamba hiyo ndio itakayowafikisha mbinguni, kaacha kumtumikia Mungu, hata muda na ibada hana, dai lake ni “Natafuta pesa’’ Sasa hizo ndio sanamu za kusubu..

Wengine biashara kwao zimeshageuka na kuwa sanamu za kusubu, wengine wanadamu., wengine muvi, wengine magemu, wengine mipira.

Tunapaswa tujilinde sana kwasababu sanamu za namna hii zinamtia Mungu WIVU, na wivu ni mbaya kuliko ghadhabu..

Ni heri Mungu akukasirikie kwa makosa mengine kuliko kwa kukuonea wivu.

kwasababu adhabu ya wivu ni mbaya sana kuliko ya hasira..

Mithali 27:4

[4]Ghadhabu ni kali, na hasira ni gharika;

Lakini ni nani awezaye kusimama mbele ya wivu.

Tujilinde mioyo yetu na ibada za sanamu. Mungu hakuwahurumia wana wa Israeli walipotengeneza ndama ya kusubu na kuiabudu kule jangwani. Japokuwa yeye ndiye aliyewaokoa kwa mkono hodari.

Vivyo hivyo na wewe ukisema umeokoka, epuka kugeuza kitu chochote kuwa Mungu wako. Usiruhusu kamwe chochote kuchukua sehemu ya Mungu yako.

Shalom.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Talanta ni nini katika biblia (Mathayo 25:14-30)

Shetri ni nini kama tunavyosoma katika Marko 3:38?

Kuvyaza ni nini katika biblia? (Ayubu 21:10).

Zeri ya Gileadi ni nini?

Nondo ni nini kama tunavyosoma katika biblia?

Rudi nyumbani

Print this post

BWANA AWEZA KUKUPA ZAIDI SANA KULIKO HIZO.

Kuna majira yakupasa uisikie sauti ya Mungu, kuliko hasara utakayoingia, ili kuiponya nafsi yako.

Kuna mfalme mmoja wa Yuda anaitwa Amazia, Huyu mfalme siku moja alijikuta anaingia katika vita na maadui zake (Waedomi), Hivyo alichokifanya ni kupanga vikosi vya wanajeshi yake, ili kwenda kushindana nao. Lakini bado aliona majeshi yake hayatoshi, hivyo akaenda kwa ndugu zake, waliokuwa upande wa Israeli, ili awaajiri wanajeshi wao kwa fedha nyingi sana..

Hivyo akawaajiri wanajeshi takribani Laki moja (100,000).

Lakini tunaona alipokuwa anakaribia kwenda vitani, nabii wa Mungu alimfuata, akamwambia, achana na hao askari uliowaajiri, kwasababu mimi sipo nao..Nenda mwenyewe na jeshi lako vitani.

Likawa ni jambo gumu kwake, kwasababu tayari anapunguza nguvu, na kama hiyo haitoshi, tayari alishalipa fedha nyingi sana kwa ajili ya majeshi hayo..Amewekeza fedha zake nyingi katika vita na haziwezi kurudishwa.

Lakini kwasababu Amazia alikuwa anamcha Mungu, alitii sauti ya Mungu, akawa tayari kuipokea hasara, hiyo. Akaenda vitani na jeshi lake dhaifu, na Bwana akamsaidia kushinda, tena kwa ushindi mnono.

2Nyakati 25:6 “Akaajiri pia watu mashujaa mia elfu wa Israeli kwa talanta mia za fedha.

7 Lakini mtu wa Mungu akamjia, akasema, Ee mfalme, usiwaache jeshi la Israeli waende nawe; kwa kuwa Bwana hayupo pamoja na Israeli, yaani, wana wote wa Efraimu.

8 Lakini ukitaka kwenda, haya, jitie nguvu upigane; Mungu atakuangusha mbele ya adui; maana MUNGU ANAZO NGUVU ZA KUSAIDIA, NA KUANGUSHA.

9 Amazia akamwambia mtu wa Mungu, Lakini tuzifanyieje zile talanta mia nilizowapa jeshi la Israeli? MTU WA MUNGU AKAJIBU, BWANA AWEZA KUKUPA ZAIDI SANA KULIKO HIZO”.

Ni mara ngapi, watu wengi wanashindwa kumfuata Yesu, kisa hasara watakazoingia kwa uamuzi huo?

Niliwahi kuzungumza na mtu mmoja, anasema anampenda Mungu kweli, lakini anamiliki bar tena sio moja bali kadha wa kadha, na anasema ndipo anapopatia rizki. Nikamwambia hana budi kuacha biashara hiyo, kwasababu Mungu anaouwezo wa kumpa kitu kingine bora kuliko hicho, ikiwa tu atamtii Kristo. Lakini jambo hilo likawa bado ni gumu kwake kulipokea, akaendelea na biashara yake.

Mwingine pia tulimshuhudia akawa yupo  tayari kuokoka, lakini madai yake ni kuwa hana kazi, anatumia njia ya kujiuza ili apate pesa za kulipa kodi, na bili za maji na umeme.. Anasema kabisa nikiokoa najua hii kazi nitaacha, na sitakuwa na chanzo chochote cha mapato, nitaishije mjini?

Ndugu ikiwa na wewe ni mmojawapo wa watu wanaoshindwa kuacha kazi za ibilisi, kisa tu, umewekeza pesa nyingi katika hizo, au unahofia utakuwa maskini, au ukifanya kazi nyingine utapata kipato kidogo.. Nataka ukumbuke hilo andiko hapo juu kuwa “Bwana anazo nguvu za kusaidia, na kuangusha”.. Na “tena, Anaweza kukupa Zaidi sana kuliko hizo”

Anaweza kukupa mara dufu ya hivyo. Na hata kama hatokupa basi anaweza kukufanya uishi kwa raha na amani kuliko hata hapo ulipokuwepo. Bwana Yesu anasema,..Itakufaidia nini uupate ulimwengu mzima, kisha upate hasara ya nafsi yako?. Amazia, alikubali kuingia hasara akijua kabisa Mungu kweli atampa Zaidi ya vyote alivyovipoteza.

Ni heri ukampa Yesu Maisha yako ayaokoe, kipindi hichi cha kumalizia, watu wengi wamenaswa kwenye vitanzi hivi…Wakiangalia mitaji yao yote imelalia kwenye michezo ya kamari, imelalia kwenye madawa ya kulevya, imelalia kwenye biashara za pombe na sigara, imelalia kwenye mavazi ya kikahaba na kidunia.

Achana nayo, mwamini Mungu anayekuita. Utakuwa salama, na atakusaidi kumudu Maisha yako..

Bwana akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

SINA PESA SASA, YESU ATANISAIDIA NINI?

Kwanini wakristo wengi ni maskini?

ORODHA YA WAFALME WA ISRAELI.

JAWABU LA MAISHA YA MTU.

APENDAYE FEDHA HASHIBI FEDHA.

NJONI, NUNUENI MLE NA MNYWE.

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 1)

Kuvyaza ni nini katika biblia? (Ayubu 21:10).

ENZI NA MAMLAKA AMEZIFANYA KUWA MKOGO

Uru wa Ukaldayo ni nini?

Rudi nyumbani

Print this post

Talanta ni nini katika biblia (Mathayo 25:14-30)

Talanta ni nini katika biblia.

Katika agano la kale Talanta kilikuwa ni kipimo cha uzito cha juu zaidi ya vyote (kilitumiwa hususani katika  kupima madini ya  dhahabu na fedha)..Talanta moja ina uzito wa Kg 34.2.

Neno hilo utalisoma katika vifungu hivi..

Kutoka 25:39, 38:25, Samweli 12:30, 1Wafalme 10:10.

Lakini katika agano jipya haikutumika tu kama kipimo cha uzito bali pia kama cha fedha.

Ambapo biblia inatuambia..Talanta 1 ilikuwa na thamani ya sh5,000 ya wakati ule.

Hivyo kulingana na mfano ule wa yule mtumwa ambaye alisamehewa deni lake lililokuwa kubwa sana la talanta 10,000, ambayo tukiibadili katika pesa ya sasa si chini ya Tsh. Bilioni 6…Tunaona yeye  akashindwa kumsaheme mdeni wake aliyekuwa na deni dogo..la Tsh. Laki 1.

Kama tunavyosoma habari Matokeo yake ikawa ni kukamatwa  na kwenda kutupwa gerezani kwa watesaji. (Mathayo 18: 21-35)

Mfano mwingine ni habari ya yule mtu aliyesafiri, kisha akawaita watumwa wake na kuwapa talanta wafanyie biashara.mmoja akampa tano, mwingine mbili, mwingine moja. (Mathayo 25:14-30)

Hivyo katika vipimo vyote viwe ni vya kifedha au vya kiuzito bado ni vipimo vikubwa na  vya  juu sana.

Lakini tunaona jambo lingine katika kitabu cha Ufunuo..juu ya ile ghadhabu ya Mungu atakayoishusha juu ya dunia nzima siku za mwisho.

Anasema mawe yatakayoporomoka kutoka mbinguni yatakuwa ni makubwa kama talanta..Tengeneza picha jiwe moja lenye uzito wa kg 34.2 linaanguka juu yako ..ni mawe yenye uwezo wa kuvunja fuvu la kichwa..

Ufunuo wa Yohana 16:20-21

[20]Kila kisiwa kikakimbia, wala milima haikuonekana tena.

[21]Na mvua ya mawe kubwa sana, ya MAWE MAZITO KAMA TALANTA, ikashuka kutoka mbinguni juu ya wanadamu. Wanadamu wakamtukana Mungu kwa sababu ya lile pigo la mvua ya mawe; kwa maana pigo lake ni kubwa mno.

Si ajabu watu wataomba wafe haraka..Ili tu kujisitiri na hiyo ghadhabu kali ya Mungu mwenyezi juu ya waovu wote.

Ufunuo wa Yohana 6:14-17

[14]Mbingu zikaondolewa kama ukurasa ulivyokunjwa, na kila mlima na kisiwa kikahamishwa kutoka mahali pake.

[15]Na wafalme wa dunia, na wakuu, na majemadari, na matajiri, na wenye nguvu, na kila mtumwa, na mwungwana, wakajificha katika pango na chini ya miamba ya milima,

[16]wakiiambia milima na miamba, Tuangukieni, tusitirini, mbele za uso wake yeye aketiye juu ya kiti cha enzi, na hasira ya Mwana-Kondoo.

[17]Kwa maana siku iliyo kuu, ya hasira yao, imekuja; naye ni nani awezaye kusimama?

Ni mambo ya kutisha sana yanayokuja huko mbeleni

Jiulize unyakuo ukikupita leo, tumaini lako litakuwa ni nini… Ni majuto na vilio vya kusaga meno, ukijua kabisa hata baada ya kufa huko kwa mateso, ni safari ya moja kwa moja hadi kuzimu.

Ni heri ukampa Kristo maisha yako leo maadamu neema ipo..Unyakuo ni wakati wowote, usipumabazwe na huu ulimwengu…achana nao kwasababu Bwana Yesu anasema siku hiyo wao itawajia kwa ghafla tuwala hawatatambua lolote kwasababu wapo gizani..Na sisi tusiwe kama wao gizani ..dalili zote zimeshatimia, tunachosubiria hapa ni unyakuo basi! Hakuna mtu asiyejua hilo. Injili tuliyonayo sio ya kubembelezewa tena wokovu, ni kujionea hali halisi na kuamka usingizini mwenyewe ..

Tengeneza taa yako. Maanisha kuishi maisha wokovu, kwasababu watakaoachwa pia ni wale wanawali wapumbavu, wakristo vuguvugu (Mathayo 25).

Maran atha.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

VIPIMO MBALIMBALI VYA KIBIBLIA.

Ratli/ Ratili ni nini katika biblia?

ANGALIA JINSI USIKIAVYO:

KWA KUWA WASEMA MIMI NI TAJIRI.

HERI WAPATANISHI, MAANA HAO WATAITWA WANA WA MUNGU

Marago ni nini? ( Waamuzi 10:18)

Wahiti ni watu gani?

HUTATAMBUA LOLOTE, SIKU YA UNYAKUO IKIFIKA.

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya ugonjwa wa kufisha? (Yeremia 17:9)

SWALI: Nini maana ya ugonjwa wa kufisha? Yeremia 17:9

Yeremia 17:9 “Moyo huwa mdanganyifu kuliko vitu vyote, una ugonjwa wa kufisha; nani awezaye kuujua”?


Kufisha; maana yake ni kusababisha kitu kife.

Hivyo hapo anaposema..moyo una ugonjwa wa kufisha.. Maana yake ni kuwa una ugonjwa wa kupelekea mauti, yaani ugonjwa usioponyeka.

Akiwa na maana kuwa, udanganyifu wa moyo ni mbaya sana, unaweza kukupeleka sio tu mauti ya mwili wako, bali mpaka roho yako pia. Kwamfano waweza kujiuliza shetani alidanganywa na nani kule mbinguni?. Jibu ni kuwa hakudanganywa na mtu yeyote, bali alidanganywa na moyo wake mwenyewe kwamba na yeye anaweza kuwa kama Mungu.

Na mwisho wa siku akapata hasara ambayo mpaka leo hii anaijutia ndani ya moyo wake. Hata sasa udanganyifu wa kwanza hautoki kwa shetani, bali unatoka ndani yetu wenyewe. Baadaye tukishadanganyika, ndipo shetani anapata nafasi ya kuuchochoa udanganyifu huo.

Biblia inasema,

Mithali 14:12 “Iko njia ionekanayo kuwa sawa machoni pa mtu, Lakini mwisho wake ni njia za mauti”.

Unaweza kuona kuvaa vimini na kujichubua ni sawa kwasababu moyo wako unakuambia hivyo, lakini kumbe ndio unakwenda kujiangamiza mwenyewe. Unaweza kudhani kumwabudu Mungu kwa kupitia chochote ni sawa tu kumbe, mwisho wake ni mauti.

Njia ni moja tu, nayo ni Yesu Kristo.

Hivyo andiko hilo, linatupa tahadhari kuwa, tumsikilize Mungu, kuliko mioyo yetu. Kwasababu wengi wamepotea, kwa kutii tamaa za mioyo yao, na sio Neno la Mungu.

Bwana atusaidie sana.

Neno “kufisha” utalisoma pia katika vifungu hivi;

Luka 16:17 “Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya;

18 watashika nyoka; hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapata afya”.

Zaburi 7:13 “Naye amemtengenezea silaha za kufisha, Akifanya mishale yake kuwa ya moto”.

Bwana akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Herode aliliwa na chango, Je, chango ni nini kibiblia?

Je Elisha alimdanganya Ben-hadadi kuwa hatakufa kwa ugonjwa wake?

Jehanamu ni nini?

Ni lini na wapi Ibrahimu aliioona siku ya Bwana akashangilia?

JIWE LILILO HAI.

VIPIMO MBALIMBALI VYA KIBIBLIA.

ZIFAHAMU NAMBA KATIKA BIBLIA NA MAANA ZAKE.

Rudi nyumbani

Print this post

KIASI NI NINI KATIKA UKRISTO?

Kiasi kama tafsiri yake  ilivyo ni  kuwa na uwezo wa kudhibiti jambo/tendo lisipitilize mipaka yake, yaani litendeke kwa sehemu tu.

Katika Ukristo, kiasi ni moja ya matunda tisa (9), ya Roho Mtakatifu.

Wagalatia 5:22 “Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, 23 upole, KIASI; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria”.

Ikiwa na maana ukipungukiwa nacho (kiasi), ni uthibitisho mojawapo kuwa Roho wa Mungu hayupo ndani yako.

Kwasababu huu  ulimwengu una mambo mengi, ambayo, pengine sio mabaya, lakini yakipitiliza matumizi yake, yanabadilika na kuwa mabaya na sumu kubwa sana, kuliko hata matendo yenyewe mabaya.

Sasa swali ni Je, tunapaswa tuwe na kiasi katika mambo gani?

Zifuatazo ni sehemu muhimu, ambazo, Roho Mtakatifu anataka sisi tuwe nazo na kiasi.

  1. Katika ndoa.

1Wakorintho 7:4 “Mke hana amri juu ya mwili wake, bali mumewe; vivyo hivyo mume hana amri juu ya mwili wake, bali mkewe.

5 Msinyimane isipokuwa mmepatana kwa muda, ili mpate faragha kwa kusali; mkajiane tena, Shetani asije akawajaribu kwa kutokuwa na kiasi kwenu”.

Kukosa kiasi katika tendo la ndoa, hupelekea watu wengi sana kumtenda Mungu dhambi, wengine wanatenda mambo hayo hata kinyume na maumbile, wengine kutafuta njia za visaidizi n.k. wengine muda wao wote wanachowaza ni tendo lile tu, akili zao zote zinafikiria humo, mpaka inawapelekea kukosa muda kusali. Hivyo kiroho chao kinapungua sana kwasababu ya kuendekeza tamaa za mwili.

Biblia inasema..

1Wakorintho 7:29 “Lakini, ndugu, nasema hivi, muda ubakio si mwingi; basi tokea sasa wale walio na wake na wawe kama hawana;

Ikiwa na maana, tuishi kama vile, hakuna jambo jipya tumeongeza, pale tulipooa au kuolewa, hiyo itatusaidia sana, kuishi Maisha ya utakatifu na kumcha Mungu, katika hichi kipindi kifupi tulichobakiwa nacho duniani.

2. Kiasi katika shughuli za ulimwengu;

Bwana ametuweka duniani tufanye kazi, pia tujitafutie rizki, lakini anatutahadharisha, tusipitilize, mpaka kufikia hatua ya mioyo yetu kuzama huko moja kwa moja tukamsahau yeye, hata muda wa ibada, au kuomba au kuwaeleza wengine Habari njema tukakosa..Hiyo ni hatari kubwa sana.

1Wakorintho 7:31 “Na wale wautumiao ulimwengu huu, kama hawautumii sana; kwa maana mambo ya ulimwengu huu yanapita”.

Yaani fanyakazi huku ukijua mahusiano yako, au ratiba yako na Mungu haivurugwi hata kidogo.. Kwasababu ukiupeleka moja kwa moja moyo wako huko, ni lazima tu ulale kiroho, na matokeo yake, utakufa na bado hujayatengeneza mambo yako vizuri na Mungu.

1Wathesalonike 5:6 “Basi tusilale usingizi kama wengine, bali tukeshe, NA KUWA NA KIASI.

7 Maana walalao usingizi hulala usiku, pia na walewao hulewa usiku.

8 Lakini sisi tulio wa mchana, tuwe na kiasi, hali tukijivika kifuani imani na upendo, na chapeo yetu iwe tumaini la wokovu”.

Usihangaishwe sana na shughuli za dunia hii.. Kuwa na kiasi katika hayo, ili mbegu yako imee vizuri. Zingatia sana hilo. Kama unatingwa na mihangaiko ya duniani, na moyoni mwako unaona ni sawa, basi ujue moyoni mwako Roho Mtakatifu hayupo.

3. Kiasi katika huduma

Mungu anataka watumishi wake pia wawe na kiasi.. Hamaanishi kiasi katika kumtumikia hapana, anataka sana tuzidi kumtimika kwa bidii,  bali anamaanisha kiasi katika karama.

Anasema..

Warumi 12:3 “Kwa maana kwa neema niliyopewa namwambia kila mtu aliyeko kwenu asinie makuu kupita ilivyompasa kunia; BALI AWE NA NIA YA KIASI, kama Mungu alivyomgawia kila mtu kiasi cha imani.

4 Kwa kuwa kama vile katika mwili mmoja tuna viungo vingi, wala viungo vyote havitendi kazi moja;

5 Vivyo hivyo na sisi tulio wengi tu mwili mmoja katika Kristo, na viungo, kila mmoja kwa mwenzake.

Hii ni kutuonyesha kuwa hakuna hata mmoja wetu mwenye karama zote, Ni YESU tu peke yake. Hivyo ridhika, na ulichokirimiwa, ukiwa ni mchungaji, usitake wewe wewe ndio uwe ni nabii, na mwalimu, na mwimbaji, na mwinjilisti, na mtume n.k. Huwezi kuwa Yesu.

Jifunze kuwapa wengine nafasi, na kunyanyua karama zao, pia fahamu kuwa wapo watakaokuwa na karama bora kukuzidi wewe. Ukilijua hilo utajifunza kuwa mnyenyekevu, na ndivyo Mungu atakavyokutumia Zaidi.

     4. Kiasi katika haki:

Mhubiri 7:16 “Usiwe na haki kupita kiasi; Wala usijiongezee hekima mno; Kwani kujiangamiza mwenyewe?

Hapa pia Mungu hamaanishi kwamba tusiwe na haki nyingi kupitiliza hapana, anapenda sana tuwe hivyo. Lakini anachomaanisha hapo ni kuwa tusiwe watu wa kujihesabia haki kupitiliza,(yaani kujisifia) kwani matokeo yake ni kujiangamiza wenyewe.

Bwana Yesu alitoa mfano wa yule Farisayo na mtoza ushuru waliokwenda kusali kule hekaluni, lakini yule Farisayo akaanza kumwambia Mungu mimi ni mkamilifu kuliko huyu mtoza ushuru, mimi ninafunga mara mbili kwa juma, mimi natoa zaka, mimi nahudhuria mikesha kila wiki, mimi nahubiri sana n.k. Lakini yule mtoza ushuru akasema Bwana nirehemu mimi ni mwenye dhambi..Matokeo yake yakawa yule mtoza ushuru akahesabiwa haki kuliko yule Farisayo..

Ndipo Yesu akasema..

Luka 18: 14 “…kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa”.

Uendapo mbele za Mungu, au mbele za wanadamu kuwa na kiasi.. Mwache Mungu akuhesabie haki mwenyewe. Usijifisie kwa lolote.

5. Kiasi katika kunena.

Biblia inasema..

Mithali 10:19 “Katika wingi wa maneno hapakosi kuwa na maovu; Bali yeye azuiaye midomo yake hufanya akili”.

Kwanini haisemi, katika Uchache wa maneno, hapakosi kuwa na maovu?..Ni kuonyesha kuwa, unapokuwa mzungumzaji kupitiliza, ni rahisi sana kujikwaa ulimi, lakini ukiwa si mwepesi wa kuzungumza zungumza,  yaani kila Habari au kila jambo unachangia, basi utajiepusha na maovu mengi.

Mhubiri 5:2 “Usiseme maneno ya ujinga kwa kinywa chako, wala moyo wako usiwe na haraka kunena mbele za Mungu; kwa maana, Mungu yuko mbinguni, na wewe upo chini, Kwa hiyo maneno yako na yawe machache”.

6. Kiasi katika vyakula, na vinywaji.

Vinywaji kama divai, vilikuwa ni vya kitamaduni Israeli, wakati ule, kwasababu pia ndani yake waliamini kuna tiba, (1Timotheo 5:23) hivyo vilikuwa vinanyweka kwa kiasi sana, kwasababu vilikuwa na kiwango cha  kileo ndani yake.

Paulo akamwagiza Timotheo kuhusiana na Mashemasi na wazee wa kike katika makanisa, akamwambia.

1Timotheo 3:8 “Vivyo hivyo mashemasi na wawe wastahivu; si wenye kauli mbili, si watu wa kutumia mvinyo sana,si watu wanaotamani fedha ya aibu.

Lakini sasa kwa watu kukosa kiasi, leo hii, wanakwenda kunywa pombe ambayo haiwasaidii chochote, wala haina umuhimu wowote katika mwili, Wakati wa sasa tunazo dawa, kwanini ukanywe divai.

Na biblia imeweka wazi kabisa, walevi wote sehemu yao itakuwa katika lile ziwa la moto (1Wakorintho 6:10).

Sio kila kitu ule, au unywe. Zuia koo lako, zuia tumbo lako. Wakati mwingine funga, Litunze hekalu la Mungu. Utaona faida yake

 7.Kiasi katika mwenendo.

Hapa anatoa angalizo, katika mienendo yetu na mionekano.  Hususani kwa vijana.

Tito 2:6 “Vivyo hivyo na vijana waume uwaonye kuwa na kiasi”;

Jiulize kwanini hasemi, wazee au Watoto? Anasema vijana kwasababu Anajua kabisa vijana wengi wakike na wakiume  waliokoka wanakosa, kiasi katika ujana wao.

Hakuna sababu ya kukesha katika muvi au magemu, au mipira kutwa kuchwa. Ukiwa umeokoka, ili hali unajua kabisa kusoma biblia, kuomba na kuhubiri kunakusubiria.

Hakuna sababu ya  binti wa Mungu avae/ aonekane kama mabinti wa ulimwengu huu. Unaweka mawigi, unavaa suruali, uweka kucha za bandia, n.k. Kuwa “natural”..

1Timotheo 2:9 “Vivyo hivyo wanawake na wajipambe kwa mavazi ya kujisitiri, pamoja na adabu nzuri, NA MOYO WA KIASI; si kwa kusuka nywele, wala kwa dhahabu na lulu, wala kwa nguo za thamani”;

Soma pia (1Timotheo 3:11)

Kijana, huna sababu ya kunyoa kiduku, uonekane kama msanii fulani, kwenye tv. Kumbuka Mwonekano wako unakupunguzia utukufu wako.

Kwahiyo, kwa kuhitimisha ni kuwa KIASI katika mambo yote ni muhimu sana. Hivyo tujitahidi kwa upande wetu kila mmoja aangalie ni wapi amekosa kiasi, basi arekebishe mapema, na Roho Mtakatifu atajaa tena ndani yetu kutusaidia kuushinda ulimwengu.

Kumbuka hizi ni nyakati za mwisho, Biblia inasema..

1Petro 5:8 “Mwe na kiasi na kukesha; kwa kuwa mshitaki wenu Ibilisi, kama simba angurumaye, huzunguka-zunguka, akitafuta mtu ammeze”.

Umeona! Ibilisi anawatufuta watu wanaokosa kiasi ili awemeze, Usiwe mmojawapo!

Bwana akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MATUNDA 9 YA ROHO MTAKATIFU

Unyenyekevu ni nini?

Je ushabiki wa mpira ni dhambi?

Wibari ni nani?(Mithali 30:26)

Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?

Nini maana ya mstari huu: (Mtu ambarikiye mwenzake kwa sauti kuu asubuhi na mapema; Itahesabiwa kuwa ni laana kwake.Mithali 27:14 )?

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 11 (Mithali, Wimbo ulio bora, Mhubiri)

Je! Mtu ambaye hajaoa anaruhusiwa kulichunga kundi?

“Vya Kaisari mpeni kaisari”  ni vipi hivyo tunavyopaswa tumpe?

Rudi nyumbani

Print this post

Nifanyeje niwe mwombaji mzuri, wa masafa marefu?

SWALI: Nifanyeje niwe mwombaji mzuri, wa masafa marefu na sio mtu wa kuomba omba tu, ilimradi?


JIBU: Katika vita lazima ujue adui wako mkuu ni nani.. Bwana Yesu alisema maneno haya;

Mathayo 26:40-41

[40]Akawajia wale wanafunzi, akawakuta wamelala, akamwambia Petro, Je! Hamkuweza kukesha pamoja nami hata saa moja?

[41]Kesheni, mwombe, msije mkaingia majaribuni; roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu.

Hapa  Bwana alitarajia, wakeshe, Yaani waombe naye masafa marefu, (kama vile wewe unavyotamani uwe na nguvu hata ya kukesha katika maombi mpaka asubuhi), lakini kinyume chake, hawakuweza kumaliza hata Saa moja..matumaini yao yaliishia katikati..

Lakini Bwana Yesu alipowakuta wamelala hakuwaambia kemea pepo hilo la uchovu, au wachawi hao waliotumwa kuwafanya mpige pige miayo ya usingizi, muda wote muombapo..

Bali aliwaambia maneno haya “ROHO I RADHI, LAKINI MWILI NI DHAIFU”..Akiwa na maana roho zao kweli zilikuwa zinatamani kukesha naye kule bustanini…na ndio maana walitii wito wa kwenda kuomba..kama roho zao zisingekuwa  radhi kufanya vile muda ule wangekuwa vitandani mwao wamelala..

Lakini Bwana anawaambia kikwazo ni nini.? Kikwazo ni MIILI yao.. Huyo ndio adui wao wa kwanza wanapaswa wamuangalie, sana

Tunashindwa kuomba, hata wakati mwingine kusoma Neno,..kwasababu ya mwili,..Lakini kama tukishindana na mwili ipasavyo basi tutaweza fungua milango mingi ya rohoni.

Sasa tutawezaje kuwa hivyo?

Ni kujitengenezea ”pumzi ya kiroho”..Kama vile wanariadha wafanyavyo katika mwili, kwa kawaida yule anayefanya mazoezi sana, huwa anajiongezea pumzi ya kukimbia umbali mrefu zaidi kuliko yule asiyefanya mazoezi yoyote, Atakimbia mzunguko mmoja tayari hoi.

Unapotaka uwe mwombaji mzuri, hata wa masafa marefu, ni lazima uanze kidogo kidogo, ukikumbuka kuwa adui wako wa kwanza sio shetani bali ni mwili wako..

Hivyo unaanza siku ya kwanza kuomba  dakika 15,  kesho huna budi kuongezea nyingine 5, kesho kutwa yake nyingine 5, hivyo hivyo, bila kurudi nyuma, Sasa kwa jinsi utakavyozidi kuongeza muda wako katika maombi ndivyo utakavyoona wepesi wa kuomba..

Kipindi cha mwanzoni utaona ni shida kumaliza saa moja katika maombi…lakini kama utakuwa ni mtu wa kuomba kila siku, utaona ni jepesi sana kama tu vile unavyoomba dakika 10..

Hautatumia nguvu kufikia huo muda, kwasababu tayari pumzi ya maombi ipo ndani yako.

Pengine jambo usilolijua ni kuwa wewe usiyeomba unaweza  kudhani yule anayeweza kukesha saa nyingi katika kuomba, anapata shida sana..lakini ukweli ni kwamba wewe ambaye unasali dakika chache, ndio unayechoka sana kuliko yule..kwasababu kuna kilele fulani mtu anayeomba  huwa anakifikia ile raha ya maombi inaingia ndani yake..wala haoni ugumu wa kuendelea mbele.

Hivyo jitahidi sana..Kushindana na mwili wako, ondoa mawazo yako sana kwa shetani, ni kweli upo wasaa ibilisi atataka kuvuruga ratiba zetu za maombi, lakini si jambo la kila siku…pindi unaposikia tu kuomba unalala, halafu unasema ni shetani…Ni huo mwili wako ndugu..

Anza leo kujizoeza kuomba. Shindana na usingizi, shindana na uchovu, shindana na uvivu.

Na hatimaye utakuwa mwombaji bora..Pia usingoje kuombewa, ombewa tu muda wote, vilevile usiseme Namwachia Mungu mwenyewe afanye, na ilihali hutaki kuomba..utapata hasara..Muda mwingine Kristo anasimama kutuombea..lakini wakati mwingine anataka kusimama na sisi kuomba, Kama alivyowaambia mitume wake hapo. Kesheni pamoja nami.

Mambo muhimu yatakayoweza kukupeleka rohoni haraka sana katika uombaji wako, Ni yapi?

  • Hakikisha kabla ya maombi..pata muda kidogo kukaa katika utulivu ukiwa umefunga macho..tafakari mambo yote mazuri, Mungu aliyokufanyia tangu utotoni mpaka hapo ulipofikia, kisha mpe shukrani, tafakari, uumbaji wa Mungu, tafakari, mbinguni siku ile utakapofika, tafakari mambo yote mazuri ya Mungu. N.k.
  • Pata muda tena wa kumsifu na kumwabudu kwa kinywa chako..imba nyimbo chache za shukrani na za kumtukuza Mungu.
  • Baada ya hapo mimina moyo wako mbele za Bwana, kwa kumwomba rehema na msamaha kwa makosa yako yote..

Kisha baada ya hapo ndio uingie moja kwa moja katika vipengele vyako vya maombi.

Zingatia hayo, na Mungu atakutia nguvu, katika hatua zako za maombi.

Bwana akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mada Nyinginezo:

TUTAWEZAJE KUMZALIA MUNGU MATUNDA?

YAFUATAYO NI MAWAZO YA ADUI HIVYO USIYASIKILIZE.

JINSI YA KUSOMA BIBLIA.

Kuna tofauti gani kati ya SALA na DUA?

Marago ni nini? ( Waamuzi 10:18)

MFANO WA MAMBO HAYO NI UBATIZO.

Ijumaa kuu ni nini? Na kwanini iitwe kuu?

FANYIKA SIPORA WA KRISTO, UNYAKUO UPO KARIBU.

Rudi nyumbani

Print this post

Marago ni nini? ( Waamuzi 10:18)

Marago ni mahali ambapo watu wanaweka makao ya muda kwa makusudi maalumu.

Kwamfano watu zamani walipokuwa wanakwenda vitani, waliweka makempu au makambi au mahema mahali mahali…hayo ndio yaliitwa marago..

Kwamfano ukisoma..

Waamuzi 10:17-18 inasema..

[17]Wakati huo wana wa Amoni walikutana pamoja, wakapanga marago huko Gileadi. Wana wa Israeli nao wakajikusanya wakapanga marago Mispa.

[18]Na hao watu, wakuu wa Gileadi, wakaambiana wao kwa wao, Je! Ni mtu yupi atakayeanza kupigana na wana wa Amoni? Yeye atakuwa ni kichwa juu ya wenyeji wote wa Gileadi.

Ikiwa na maana wote waliweka kambi zao za kijeshi huko Mispa.

Hali kadhalika Wana wa Israeli walipokuwa katika safari yao ya kuelekea nchi  ya ahadi waliweka makazi ya muda sehemu kadha wa kadha..

Kwamfano ukisoma..

Kutoka 29:13-14

[13]Kisha twaa mafuta yote yafunikayo matumbo, na kitambi kilicho katika ini, na figo mbili, na mafuta yaliyo juu yake, uyateketeze yote juu ya madhabahu.

[14]Lakini nyama yake huyo ng’ombe, na ngozi yake, na mavi yake, utayachoma kwa moto nje ya marago; ni sadaka kwa ajili ya dhambi.

Akiwa na maana hivyo viungo vya ndani watavichoma mbali na pale wana wa Israeli walipoweka makambi..

Neno hilo italisoma pia katika vifungu hivi;

Kutoka 36:6, Walawi 4:21, 10:5, Waamuzi 21:12.

Ni nini twajifunza kwa habari za marago.

Hata sisi hapa duniani ni kama tupo maragoni..Hatuna makazi ya kudumu..tumewekwa kwa makusudi maalumu..kusudi hilo likiisha..hakuna kukutanika tena..

Ibrahimu alilijua hilo..Kiasi kwamba japokuwa alikuwa na tajiri na mwenye mali nyingi..Moyo wake hakuuweka hapa duniani, hata kidogo..Bali kule kwenye mbingu mpya na nchi mpya(YERUSALEMU MPYA)..Na hiyo ndio ilikuwa sababu ya kuitwa Baba wa imani..Aliishi kama mpitaji hapa duniani..

Waebrania 11:9-10

[9]Kwa imani alikaa ugenini katika ile nchi ya ahadi, kama katika nchi isiyo yake, akikaa katika hema pamoja na Isaka na Yakobo, warithi pamoja naye wa ahadi ile ile.

[10]Maana alikuwa akiutazamia mji wenye misingi, ambao mwenye kuubuni na kuujenga ni Mungu….

[14]Maana hao wasemao maneno kama hayo waonyesha wazi kwamba wanatafuta nchi yao wenyewe.
[15]Na kama wangaliikumbuka nchi ile waliyotoka, wangalipata nafasi ya kurejea.
[16]Lakini sasa waitamani nchi iliyo bora, yaani, ya mbinguni. Kwa hiyo Mungu haoni haya kuitwa Mungu wao; maana amewatengenezea mji.

Je na sisi twaweza fanana na Ibrahimu?

Je tunaweza kuwa kama Ayubu ambaye japo alipoteza kila kila hakutetereka katika imani yake..kinyume chake ndio analibariki jina la Bwana.?

Hivyo nasi tuishi kama wapitaji. Kwasababu tukiwa ni watu wa namna hii, tunapata faida zote mbili kwanza ulimwengu hauwezi kutuzomba tukamsahau Mungu. Na pili Bwana atatubariki hata kwa hivyo tusivyovitazama..Kwasababu mioyo yetu haipo huko.

Bwana atusaidie.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Shetri ni nini kama tunavyosoma katika Marko 3:38?

Neno Buruji lina maana gani katika biblia?

Pomboo ni nini katika biblia?(Kutoka 25:5, Ezekieli 16:10)

Gumegume ni nini? (Isaya 50:7)

HERI WAPATANISHI, MAANA HAO WATAITWA WANA WA MUNGU

Easter ni nini?..Na je tunaruhusiwa kuisheherekea?

JIHUDHURISHE, ILI AANZISHE MAZUNGUMZO NA WEWE

Rudi nyumbani

Print this post

Kwa aibu yako mwenyewe, na kwa aibu ya uchi wa mama yako.

SWALI: Je? Daudi na Yonathani walikua wanashiriki mapenzi ya jinsia moja?

Kufuatana na vifungu hivi;

1 Samweli 20:30

[30]Basi hasira yake Sauli ikawaka juu ya Yonathani, akamwambia, Wewe, mwana wa mke mkaidi, asi, je! Mimi sijui ya kuwa umemchagua huyo mwana wa Yese, kwa aibu yako mwenyewe, na kwa aibu ya uchi wa mama yako.


JIBU: Andiko hilo halina uhusiano wowote wa Yonathani na Daudi kuwa na mahusiano ya jinsia moja..

Wazo kama hilo linakuja kichwani mwa watu kufuatana na lile andiko linalosema upendo wa Jonathan kwa Daudi ulikuwa zaidi ya upendo wa mwanamke (2Samweli 1:26).Ambalo nalo halihusiani na jambo hilo kabisa.

Katika andiko hilo tunaona Sauli alipoona kwamba mwanawe Jonathani anashikamana sana na Daudi na kwamba yupo tayari hata kumwachia ufalme wake ambao alistahili yeye kuumiliki..ilimfanya Sauli aghadhibike sana juu yake ndipo akamwambia maneno hayo..

1 Samweli 20:30 “… je! Mimi sijui ya kuwa umemchagua huyo mwana wa Yese, kwa aibu yako mwenyewe, na kwa aibu ya uchi wa mama yako”.

“Aibu ya uchi wa mama yake”..Akiwa na maana “aibu ya mama yake aliyemzaa” na si vinginevyo .

Yaani kwa tendo lile la kumruhusu Daudi aje kuwa mfalme wa Israeli badala yake italeta aibu kubwa na fedheha kwa mama yake, kwa kuzaa mtoto ambaye haendelezi ufalme katika familia

Na ikumbukwe kuwa wa-mama wa wafalme enzi zile walikuwa wanapewa heshima kubwa kiasi cha kuwekewa kiti cha enzi pembezoni mwa wafalme . Na ndio maana utaona sehemu nyingi mfalme mpya atajwapo huwa anaambatanishwa na jina la mama yake, na sio mke au mtoto kwasababu walipewa heshima yao, kipekee. ( soma 2Wafalme 21:19, 22:1).

Sasa hapa inapotokea Yonathani hapiganii kiti chake cha ufalme kinyume chake ndio yupo tayari kumpa Daudi ufalme wote..Ndio maana Sauli akamwambia tendo analolifanya ni aibu kubwa sana kwa mama yake.

Hii inatufundisha nini?

Upendo usio wa kinafki unakuwa tayari kujishusha pale panapostahili kufanya hivyo.

Hautafuti mambo yake wenyewe..sawasawa na 1Wakorintho 13:5

Unawatanguliza wengine mbele..

Si ajabu ni kwanini Daudi hakuufananisha upendo ule na wa mwanamke yeyote duniani.

Na sisi pia tupendane, kwa kuwa tayari kutangulizana. Kumuhesabu mwingine ni bora zaidi yetu sisi wenyewe, Hiyo itatupa kibali kikubwa sana kwa Mungu. Kama vile Yonathani ambaye hadi leo hii tunazisoma habari zake kwa mema.

Bwana akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MAMA, TAZAMA, MWANAO.

HERI WAPATANISHI, MAANA HAO WATAITWA WANA WA MUNGU

Upole ni nini?

Unyenyekevu ni nini?

MAOMBOLEZO YA HADADRIMONI.

Matulizo ya mapenzi ni nini? (Wafilipi 2:1).

Kiyama ni nini?

YESU NDIYE ATAKAYEKURUSHIA MAWE, USIPOTUBU.

Wakati wakina Shadraka wanatupwa katika tanuru la moto, Danieli alikuwa wapi?

Rudi nyumbani

Print this post

HERI WAPATANISHI, MAANA HAO WATAITWA WANA WA MUNGU

Unajua ni kwasababu gani Bwana Yesu aliitwa Mwana wa Mungu? ..Mungu kukuona wewe kama  mwana wake kweli kweli sio tu uwe umezaliwa na yeye kwa kumkiri na kubatizwa, hapana bali pia kuwa na huduma ya upatanisho ndani yako….

Biblia inasema..

Mathayo 5:9

[9]Heri wapatanishi;

Maana hao wataitwa wana wa Mungu.

Jiulize Kwanini isiseme wataitwa watakatifu, au wataitwa wafalme, au wataitwa makuhani wa Mungu..bali wana wa Mungu.

Hilo jambo ambalo Yesu Kristo alilijua ndio maana kusudi lake kubwa la yeye kuja duniani, lilikuwa ni kutupatanisha sisi na Mungu..Yaani sisi tuliokuwa tumefarakana na Mungu kwasababi ya dhambi, sasa tunawasiliana naye kwa kupitia Yesu Kristo mwana wake..

Tunalithibitisha hilo katika mistari hii..

2 Wakorintho 5:18-19

[18]Lakini vyote pia vyatokana na Mungu, aliyetupatanisha sisi na nafsi yake kwa Kristo, naye alitupa huduma ya upatanisho;

[19]yaani, Mungu alikuwa ndani ya Kristo, akiupatanisha ulimwengu na nafsi yake, asiwahesabie makosa yao; naye ametia ndani yetu neno la upatanisho.

Umeona? Tendo la Yesu kuacha enzi na mamlaka, na kuja duniani ili kutupatanisha tu sisi hilo ndio lililomfanya Mungu amwone kuwa ni mwana  bora kuliko wana wake wote aliokuwa nao.

Ndio maana akamshuhudia  mwenyewe..Huyu ni mwana wangu, mpendwa wangu, niliyependezwa naye. (Mathayo 3:17)

Akampa kibali cha kipekee kuliko wanadamu wote walioko ulimwenguni.

Hata sisi ili  Mungu atuone ni wana wake kwelikweli hatuna budi kuwa na huduma hii ya upatanisho ndani yetu.

Tuulete ulimwengu kwa Kristo. Lakini jambo ambalo hatujui ni kuwa kuwapatanisha watu waliogombana si jambo rahisi..la kwenda kuwashikanisha mikono tu halafu basi.. Hapana..lina gharama kubwa sana..kama ulishawahi kujaribu utalithibitisha hilo.

Ilimlazimu Yesu aache enzi na mamlaka, aje duniani, na kama hiyo haitoshi akataliwe kwanza na wale anaowapatanisha, (yaani sisi), na bado autoe uhai wake pia kwa ajili wao.

Kwa ufupi ni kwamba alikuwa anafosi upatanisho ambao ulikuwa hauwezekani kwa namna yoyote ile, ni uadui uliokuwa umekomaa..lakini hakukata tamaa, hadi mwisho wa siku ukatokea tu wenyewe.

Na sisi vivyo hivyo anasema ametupa huduma ya upatanisho. Yaani na sisi tukaupatanishe ulimwengu na Mungu kwa kupitia yeye.

Hivyo tufahamu kuwa tunapowahubiria watu, hadi kuokoka halitakuwa jambo rahisi kama sisi tunavyodhani..Watu wengi wamekatishwa tamaa  kuhubiri habari njema..kisa watu wanaowahubiria hawana geuko au badiliko, lolote..wengine ndio wanawatukana na kuwapiga

Hatuna budi kuendelea..kwasababu hakuna upatanisho ulio mwepesi. Ni unajitoa sadaka kwa vita ambayo si yako. Leo atakupuuzia, kesho atakutukana, lakini kesho kutwa ataokoka.

Ukifanikiwa kwa jambo hilo moja. Utajiongezea daraja la juu zaidi mbinguni..La kuwa mwana mpendwa wa Mungu. Na kwa jinsi unavyoendelea kufanya ndivyo kubali chako kinavyoongozeka kwa Mungu, hatimaye..kufikia kilele cha kufanana na Yesu Kristo..Ukimwomba Mungu lolote atakupa, na kazi zake zote utazifanya..Kama yeye alivyosema maneno haya..

Yohana 5:20-21

[20]Kwa kuwa Baba ampenda Mwana, naye humwonyesha yote ayatendayo mwenyewe; hata na kazi kubwa zaidi kuliko hizo atamwonyesha, ili ninyi mpate kustaajabu.

[21]Maana kama Baba awafufuavyo wafu na kuwahuisha, vivyo hivyo na Mwana awahuisha wale awatakao.

Umeona hiyo ndio faida za kuwa mwana wa Mungu kwelikweli.

Nasi pia tuanze kwa kuthamini wengine, kwa kuwahubiri habari njema, hapo tutakuwa tunaukiri UWANA wetu kwa Mungu..Ukimwona jirani yako amepotea basi pambana naye kwa hali na mali mpaka amgeukie Kristo kama wewe…wakati mwingine ugumu utakuwepo japo si kwa wote..

Ukifahamu kuwa hakuna upatanisho usiokuwa na gharama, basi utakuwa na uvumilivu na amani kwa yote utakayokutana nayo.

Bwana akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Uwe na utumishi mwema wa upatanisho.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MJUE SANA YESU KRISTO.

UVUVI BORA HAUCHAGUI, CHA KUVUA.

Heri maskini wa roho maana ufalme wa mbinguni ni wao.

Kwanini, tuimbe, je! kuna ulazima wowote wa kufanya hivyo?

Injili iliyopo kwa Samaki aina ya Eeli.

Kiyama ni nini?

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

MAUTI NA KUZIMU ZIKAWATOA WAFU WALIOKUWAMO NDANI YAKE.

Rudi nyumbani

Print this post