Category Archive Uncategorized @sw-tz

Wakati wakina Shadraka wanatupwa katika tanuru la moto, Danieli alikuwa wapi?

SWALI: Je Wakati Mfalme Nebukadreza anawatupa Shadraka, Meshaki na Abednego kwenye tanuru la Moto, Danieli alikuwa wapi?


JIBU: Kwasababu biblia haiandiki kila habari, bali inachagua yale matukio muhimu tu, yatakayotusaidia, ndivyo ilivyo katika habari hii, haielezi habari za Danieli kwa wakati huo, alikuwepo wapi, lakini katika sintofahamu hiyo, tuna la kujifunza.
Hivyo hapo mambo matatu yanawezekana,

La kwanza ni aidha Danieli hakuwepo, wakati huo, ambapo Nebudreza, anatoa amri, kwasababu utakumbuka kuwa yeye aliyewekwa juu ya waganga wote, na wenye hekima (Danieli 5:11). Hivyo kuna uwezekano, alipewa jukumu lingine la kwenda kulifanya nje ya Babeli kwa wakati huo , na mbio ilipopigwa yeye hakuwepo.

La pili, ni aidha, watu waliokuwa pamoja na mfalme agizo hilo halikuwahusu, kwasababu ukichunguza utaona, Nebukadreza, aliwaita wakuu wake wote waliokuwa katika majimbo yake yote ulimwenguni. Na lengo la kuwaita, lilikuwa ni kuwapima utiifu wao kwa serikali yake moja ya ulimwengu. Ndio maana akawalazimisha wakuu wote ambao wapo mbali naye waje kuisujudia sanamu yake. Hivyo kwasababu Danieli alikuwa katika jumba la mfalme agizo hilo halikumuhusu.

Danieli 2:49 “Tena, Danielii akamwomba mfalme, naye akawaweka Shadraka, na Meshaki, na Abednego, wawe juu ya mambo yote ya uliwali wa Babeli; lakini huyo Danielii alikuwa akiketi katika lango la mfalme”.

Na mwisho, ni kwamba Danieli, tangu mwanzo alisimama katika misingi ya Imani yake, utakumbuka, walipoitwa na kutaka kulishwa Divai, pamoja na vyakula najisi, moja kwa moja walivikataa yeye pamoja na hao wenzake watatu. (Danieli 1:8-16) Hivyo uwezekano pia wa Danieli kumweleza mfalme misimamo wake, ulikuwepo, na mfalme akamwelewa, akamwacha peke yake asiisujudie miungu yake.

Lakini kusema kwamba alitii amri ya mfalme, hilo jambo halipo, wala lisingewezekana kwa Danieli, kwasababu utakumbuka, hata baadaye sana, jaribio kama hilo lilitaka kufanyika, la kumzuia asimwabudu Mungu wake, lakini alikaidi amri yao bila kujali nani kasema, au adhabu gani imetolewa.

Lakini habari hii ya kutokuwepo kwa Danieli inatufundisha nini?
Ni kwamba, upo wakati Mungu atakuepusha na majaribu ambayo nafasi ya kuyakwepa ni ndogo sana, lakini pia upo wakati Mungu atakupitisha katika majaribu ya adui. Mwanzoni kikombe kile hakikumuhusu Danieli, lakini mwishoni, alishiriki kikombe cha kutupwa katika tundu la Simba.

Nasi pia, kuna nyakati ngumu zitapita mbele yetu katika eneo la imani yetu, na Mungu atatuvusha salama bila hata ugumu wowote, lakini pia zipo nyakati ataziacha zipite juu yetu. Lakini yote katika yote, tunapaswa tuwe katika msimamo wetu kama vile Danieli.

Nyakati zote za mvua, na joto, misingi ya imani yetu isitikiswe.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

DANIELI: Mlango wa 1

UMEDI NA UAJEMI ZILITAWALAJE?

Santuri ni nini? (Danieli 3:5,10)

Nini maana ya kuutia moyo ufahamu? (Danieli 10:12)

Rudi nyumbani

Print this post

FANYA BIDII ZOTE ULE MATUNDA YA UZIMA.

Mwanzo 2:9

[9]BWANA Mungu akachipusha katika ardhi kila mti unaotamanika kwa macho na kufaa kwa kuliwa; na mti wa uzima katikati ya bustani, na mti wa ujuzi wa mema na mabaya.

Unaweza kujiuliza kulikuwa na sababu gani Mungu kuuweka mti wa ujuzi wa mema na mabaya pale bustanini wakati alikuwa anajua kabisa una kifo ndani yake?

Kwanini asingeuacha tu ule wa uzima na ile mingine ..ili mwanadamu aishi milele kwa furaha pale Edeni.

Je Ni kwamba Mungu hana mipango ya kueleweka kwa watu wake au?(tukizungumza kibinadamu)

Jibu la La! Nataka nikuambie mipango ya Mungu ni mikamilifu sikuzote na ni mizuri..tofauti na tunavyodhani kuwa ule mti  wa ujuzi wa mema na mabaya ulikuwa ni mbaya, haukustahili kuwepo pale.

Ukweli ni kwamba ule mti ulikuwa ni mzuri na unafaa sana, tena twamshukuru Mungu kwa kuuweka pale bustanini….Unajua ni kwasababu gani?

Ni kwasababu sisi kamwe tusingeweza kuwa kama Mungu, na malaika zake kama tusingepata ujuzi ndani yetu.

Kumbuka ujuzi ni jambo ambalo mwanadamu hakuumbiwa tangu mwanzo,  si asili yetu..sisi tuliumbwa kutokujua mambo kama aibu, ustaarabu, mipango, maamuzi, ibada n.k hayo yote yalikuja baada ya kula matunda yale,

Sasa, Mungu aliliona hilo tangu mwanzo, hivyo akaona  njia pekee ya kumkamilisha mwanadamu ili afanane na yeye ni kumpa ujuzi huo ndani yake..lakini aliona pia hatari yake..kwamba siku zote ujuzi una nguvu kubwa ya kupoteza,(1Wakorintho 8:1) hivyo akamtaadharisha mapema.

Ujuzi wa kujua mtu anahitaji kuishi katika nyumba na sio porini, kwamba anahitaji kujenga nyumba, kufanya biashara, kugundua vitu, kuvaa nguo na sio kukaa uchi, kujijengea mfumo n.k Mungu aliona mwisho wake utampoteza mtu, japo ujuzi wenyewe sio mbaya.

Ndipo akabuni njia ya kuweza kudhibiti tatizo hilo. Akaweka mti mwingine bustanini unaoitwa mti wa Uzima. Ambao mwanadamu akiyala matunda yake ataurejesha ule uzima ambao angeupoteza kwa kupokea ujuzi.

Na hapo mwanadamu atakuwa amepata faida mara mbili, kwanza ni kufanana na Mungu, pili ni kurejesha uzima wa milele.

Nachotaka ujue ni kuwa kila mwanadamu anayeishi  duniani..ujuzi huu upo ndani yake..Na ndio maana unaweza kujiamulia mambo yako mwenyewe, unaweza kusema hapana au ndio..unaweza kusema nataka au sitaki..huwi kama mnyama, Au kama roboti bali una ujuzi wote wa kufanya unachotaka mwenyewe bila hata kumtegemea Mungu, mwanadamu au shetani..

Lakini nakuambia hii ni hatari kubwa kwasababu uhuru huu wa kifikra umetufanya wanadamu ndio tuende mbali sana na Mungu wetu, tupotee kabisa, tuone Mungu ni nani, mbona tunaweza kufanya wenyewe bila yeye, rangi zetu pekee hazitoshi, tujichubue kidogo, tujichore tatoo kidogo tupendeze, tuvute sigara, tunywe pombe tuwe fresh, tuzini na Wanyama, kwani kuna shida gani? . Kwa kifupi ni kuwa tumepotea kama tutaishi katika hii hali pasipo kuifahamu kinga.

Tunauhitaji mti wa uzima. Na mti wenyewe ni YESU KRISTO. Hakuna namna utaweza kuishi kwa ujuzi wako, au akili zako bila Yesu Kristo kukusaidia. Mwisho wa siku utakufa tu na kupotelea motoni.

Yohana 14:6

[6]Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.

Watu wengi leo wanadhani elimu zao, ndio zitawapa maisha, wanadhani tafiti zao ndio zitawafikisha ng’ambo, wanadhani mawazo yao na imani zao na teknolojia zao na ustaarabu wao ndio zitakazowavusha..

Hawajui kuwa mioyo yetu sisi wanadamu huwa ni midanganyifu kuliko kitu chochote huku duniani.

Yeremia 17:9

[9]Moyo huwa mdanganyifu kuliko vitu vyote, una ugonjwa wa kufisha; nani awezaye kuujua?

Na ndio maana Bwana Yesu alisema “Mtakufa katika dhambi zenu, kama msiposadiki kuwa mimi ndiye.”(Yohana 8:24)..tusipookolewa..hakuna tumaini ndugu. Bwana Yesu ndiye mti wenyewe wa uzima. Shusha kiburi chako, yasalimishe maisha yako kwake..akusaidie.

Siku hizi ni za mwisho, wakati wowote parapanda inalia hakuna mtu asiyelijua hilo, ipo wazi kulingana na dalili tunazoziona sasa. Hii dunia inafikia mwisho, mtafute Yesu Kristo, akuokoke na udanganyifu wa ujuzi.

Kama hujaokoka basi mkaribishe leo Yesu katika maisha yako, kisha ukabatizwe katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo, kisha utapokea ondoleo la dhambi.

Mungu akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

HUTATAMBUA LOLOTE, SIKU YA UNYAKUO IKIFIKA.

USITUPE LULU ZAKO MBELE YA NGURUWE.

Nini maana ya kilichotarajiwa kikikawia kuja moyo huugua (Mithali 13:12)?.

Nini maana ya “yasiyokuwapo hayahesabiki”(Mh 1:15)

UFUNUO: Mlango wa 22

Rudi nyumbani

Print this post

MIAMBA YENYE HATARI.

SWALI: Biblia inamaana gani inaposema “Watu hawa ni miamba yenye hatari”. Hii miamba yenye hatari ni ipi?

JIBU: Tusome..

Yuda 1:12 “Watu hawa ni miamba yenye hatari katika karamu zenu za upendo walapo karamu pamoja nanyi, wakijilisha pasipo hofu; ni mawingu yasiyo na maji, yachukuliwayo na upepo; ni miti iliyopukutika, isiyo na matunda, iliyokufa mara mbili, na kung’olewa kabisa;

13 ni mawimbi ya bahari yasiyozuilika, yakitoa aibu yao wenyewe kama povu; ni nyota zipoteazo, ambao weusi wa giza ndio akiba yao waliowekewa milele”.

Hapa ni mtu Yuda alikuwa anawalinganisha wachungaji na mitume wa uongo kama miamba yenye hatari.

Sasa miamba inayomaanishwa hapo, si hii miamba tuionayo nchi kavu, hapana, bali ni ile miamba ya habarini ambayo baadhi yao inatabia ya kuchomoza juu hadi karibu na usawa wa bahari. Miamba hii ni hatari sana kwa mabaharia, kwasababu huwa haionekani, lakini meli inapopita karibu nayo, inaichana, kama sio kuiharibu kabisa na matokeo yake, ni aidha meli kugotea palepale, au kuzama kabisa.

Kama mabaharia wasipokuwa waangalifu, kwa kupita njia zilezile walizozithibitisha ni rahisi sana kukutana na hii miamba na kuzipoteza meli zao moja kwa moja.

Sasa hapo anaposema “Watu hawa ni miamba yenye hatari katika karamu zenu za upendo walapo karamu pamoja nanyi, wakijilisha pasipo hofu”;

Anamaanisha, wachungaji hawa, au watumishi hawa wa uongo ni ngumu kuwatambua, kama tu vile miamba hii hatari ilivyo ngumu kuiona habarini, pale ambapo Habari inaonekana shwari na tulivu yafaa kwa kusafiria kumbe ndipo ilipojifichia, halikadhalika, watumishi hawa wa uongo, mahali ambapo mpo katika karamu zenu za Upendo, yaani wakati ambapo mnamfurahia Mungu wenu, mnatangaza Habari njema, mkidhani kuwa wapo na nyie, kumbe ni mbwa mwitu katika mavazi ya kondoo.

Mfano wa watu hawa alikuwa ni Yuda,alitembea na Bwana Pamoja na mitume wengine, lakini haikuwa rahisi kumgundua, hadi dakika ya mwisho, utaona alipokuwa katika mlo wa jioni, kama mpelelezi, hakuna aliyemtambua isipokuwa Bwana tu peke yake.

Mtume Paulo aliliona hilo hata wakati wa kuondoka kwake akasema..

Matendo 20:29 “Najua mimi ya kuwa baada ya kuondoka kwangu mbwa-mwitu wakali wataingia kwenu, wasilihurumie kundi;

30 tena katika ninyi wenyewe watainuka watu wakisema mapotovu, wawavute hao wanafunzi wawaandamie wao”.

Hadi sasa, inasikitisha kuona watumishi wa namna hii wapo wengi katika kanisa la Mungu, ,hawaoni shida kuwadanganya watu, wengine ni wachawi, wengine ni matapeli, wengine wapo kwa lengo la kuzivuruga tu kazi za Mungu, ili watu watusiishi Maisha matakatifu, hawawahurumii watu wanaotaka kumjua Mungu, lakini cha ajabu ukiwaangalia kwa nje, wanalitaja jina la Yesu, wanaongoza makanisa, wanashiriki katika kampeni zote za kidini.

Huu ni wakati wa kuwa makini sana, Ni wakati ambao wewe kama mkristo, kuondoa uvivu wa kusoma biblia, tunadanganywa kwasababu hatuna maarifa ya kutosha kuhusu Mungu wetu na utendaji kazi wake. Hatuwezi kumshinda shetani kwa maneno tu, au kwa kumkemea, tutamshinda shetani kwa lile Neno lililokaa ndani yetu kwa wingi, ndiyo silaha ambayo Bwana Yesu aliitumia kumshinda shetani pale alipokuwa anajaribiwa nay eye kule jangwani.

Vinginevyo tukiyaendesha Maisha yetu hivi hivi tu kwa jinsi tunavyotaka, tujiandae kukutana na hii miamba yenye hatari, isiyoonekana. Tukiwa wavivu kujifunza biblia, hakuna namna tutamkwepa shetani, hakuna namna.

Bwana atusaidie.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 1

UNAWAFAHAMU MANABII WA UONGO?

FANYIKA SIPORA WA KRISTO, UNYAKUO UPO KARIBU.

USIPOTEZWE NA MANENO YA MANABII WA UONGO.

JINSI YA KUSOMA BIBLIA.

Rudi nyumbani

Print this post

Mwandamo wa mwezi/Mwezi mpya Ni nini kibiblia?

Katika biblia ukiona neno “mwandamo wa mwezi”, au “mwezi mpya”, ujue ni neno lile lile moja linalomaanisha “siku ya kwanza ya mwezi”.

Katika agano la kale siku hii iliheshimiwa na kufanywa kama mojawapo ya siku takatifu, kama  tu vile ilivyokuwa  siku ya sabato, ambayo ni siku ya saba. Vivyo hivyo kila siku ya kwanza ya mwezi mpya, tarehe moja (kwa kalenda ya kiyahudi), ilikuwa ni takatifu kwao, na ni lazima watu wakamtolee Mungu sadaka za kuteketezwa, Sadaka za unga na vinywaji,  Pamoja na kupiga tarumbeta juu ya sadaka hizo, (Hesabu 28:11-15), .Vilevile hukuruhusiwa kufanya shughuli yoyote au biashara yoyote(Nehemia 10:31-33)

Hesabu 28:11 “Tena katika mianzo ya miezi yenu mtamsongezea Bwana sadaka ya kuteketezwa; nayo ni ng’ombe waume wadogo wawili, na kondoo mume mmoja, na wana-kondoo waume wa mwaka wa kwanza, wakamilifu, saba;

12 pamoja na sehemu ya kumi tatu za efa za unga mwembamba kuwa sadaka ya unga, uliochanganywa na mafuta, kwa kila ng’ombe; na sehemu ya kumi mbili za unga mwembamba kuwa sadaka ya unga, uliochanganywa na mafuta, kwa huyo kondoo mume mmoja;”

Hesabu 10:10 “Tena katika siku ya furaha yenu, na katika sikukuu zenu zilizoamriwa, na katika kuandama miezi kwenu, mtapiga hizo tarumbeta juu ya sadaka zenu za kuteketezwa, na juu ya dhabihu za sadaka zenu za amani; nazo zitakuwa kwenu ni ukumbusho mbele za Mungu wenu; mimi ndimi Bwana, Mungu wenu”.

Lakini kuna wakati wayahudi, walizifanya sikukuu hizo kama mazoea tu, wakawa hawazitoi katika utakatifu, bali kama agizo tu la kidini  na huku nyuma mioyo yao ipo mbali na Mungu, hivyo hiyo ikamfanya  Mungu akasirishwe nao na hatimaye kuzitaa sikukuu zao hizo za mwandamo wa mwezi.

Isaya 1:13 “Msilete tena matoleo ya ubatili; uvumba ni chukizo kwangu; mwezi mpya na sabato, kuita makutano; siyawezi maovu hayo na makutano ya ibada.

14 Sikukuu zenu za mwezi mpya na karamu zenu zilizoamriwa, nafsi yangu yazichukia; mambo hayo yanilemea; nimechoka kuyachukua”.

Neno hili utalisoma pia katika vifungu hivi;

Zaburi 81:3 “Pigeni panda mwandamo wa mwezi, Wakati wa mbalamwezi, sikukuu yetu”.

1Samweli 20:5 “Naye Daudi akamwambia Yonathani, Tazama, kesho ni mwandamo wa mwezi, nami hainipasi kukosa kuketi chakulani pamoja na mfalme; lakini niache nijifiche bondeni hata siku ya tatu jioni.

Soma pia, 2Nyakati 2:4, 8:13, Ezra 3:5, Hosea 2:11.

Lakini je! Sheria hii bado inaendelea hadi sasa?

Jibu ni la! Kama tu vile hatujapewa takwa la kuitunza sabato kama sheria , vivyo hivyo, na katika mwandamo wa mwezi mpya.

Wakolosai 2:16 “Basi, mtu asiwahukumu ninyi katika vyakula au vinywaji, au kwa sababu ya sikukuu au mwandamo wa mwezi, au sabato;

17 mambo hayo ni kivuli cha mambo yajayo; bali mwili ni wa Kristo”.

Lakini Bwana anatufundisha nini katika agizo hili alilowapa?

Ni kwamba tuthaminishe nyakati zetu mpya kwake. Wiki yako inapoisha na kuanza nyingine bila kumfanyia Mungu wako ibada, ni hatari kubwa sana, kama kwako  ni jumapili, au jumamosi, ndio unamfanyia Mungu ibada, hakikisha unakutanika na wengine, kumwabudu Mungu wako, usiruhusu wiki yako ipite hivi hivi tu.

Halikadhalika, mwezi wako mpya unapoanza, usianze hivi hivi tu, bali chukua muda kwenda kumshukuru Mungu nyumbani kwake, ni muhimu sana. Ukiona wiki yako inapita hivi hivi tu, mwezi wako unapita hivi hivi tu, mwaka wako unapita hivi hivi tu, huna Habari na Mungu. Angalia  Maisha yako ni lazima yatakuwa na kasoro Fulani tu.

Hivyo tujitahidi sana, tusiwe na mapengo pengo kwa Mungu wetu.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

SIKUKUU 7 ZA KIYAHUDI ZINAFUNUA NINI KWETU?

SABATO ILIFANYIKA KWAAJILI YA MWANADAMU NA SI MWANADAMU KWAAJILI YA SABATO!

Sadaka ya kutikiswa ilikuwaje?

MWEZI WA ABIBU/NISANI NI MWEZI GANI?

Rudi nyumbani

Print this post

AKETIYE MAHALI PA SIRI PAKE ALIYE JUU.

Huu mstari una maana gani?

Zaburi 91:1 “Aketiye mahali pa siri pake Aliye juu Atakaa katika uvuli wake Mwenyezi”.


Maandiko hayo yanatuonyesha kumbe Mungu anao uvuli wake.  Na uvuli huo hawakai watu wote  ilimradi tu,  bali wale tu wanaokaa katika mahali pake pa siri.

Sasa swali utajiuliza huko mahali pake pa siri  ni wapi?

Kuna madaraja ya kumfikia Mungu, yapo yanayofikiwa na wakristo wa kawaida tu, wale wanaomtafuta Mungu jumapili kwa jumapili, au mwezi kwa mwezi,  lakini pia yapo yanayofikiwa na wakristo waliojikana, na kudhamiria kumfuata Kristo katika Maisha yao.

Hao wanaojikana ndio wanaofikia mahali pa siri pa Mungu.

Wanafananisha na makuhani, ambao, katika ile hema ya kukutania, au hekalu la Mungu, ni wao tu walikuwa na uwezo wa kupaingia patakatifu, na kule patakatifu pa patakatifu, palipo na kile kiti cha rehema cha Mungu.Kumbuka si kila mwisraeli, alifika pale, si kila mtu anayejiona anamcha Mungu aliweza kufika pale, kwa mtu wa kawaida ukijitahidi sana, uliishia katika ule ua wa hema ya kukutanikia, lakini ndani, sehemu za siri za Mungu walioweza kuingia makuhani tu.

Vivyo hivyo katika agano jipya, Mungu anao sehemu yake ya siri, na ni watu baadhi tu wanaoweza kufika huko, Mfano hai katika biblia ni mwanamke kama ANA, yeye, aliweza kupafikia hapo..na ndio maana alikuwa miongoni mwa watu wachache sana waliofunuliwa mpango wa Mungu wa wokovu,yaani kuja kwake Yesu duniani..

Lakini hiyo yote ni kwasababu alikuwa ni mwanamke aliyeupoteza ubinti wake, autumie kwa Mungu hadi uzee wake, haundoki hekaluni, mchana na usiku akisali na kufunga.

Luka 2:36 “Palikuwa na nabii mke, jina lake Ana, binti Fanueli, wa kabila ya Asheri, na umri wake ulikuwa miaka mingi, alikuwa amekaa na mume miaka saba baada ya uanawali wake.

37 Naye ni mjane wa miaka themanini na minne; haondoki katika hekalu, ila huabudu usiku na mchana kwa kufunga na kuomba.

38 Huyu alitokea saa ile ile akamshukuru Mungu, na wote waliokuwa wakiutarajia ukombozi katika Yerusalemu akawatolea habari zake”.

Mwingine, ni Simeoni, naye pia biblia inasema alikuwa ni mtu wa haki, na anaye mcha Mungu, tena Zaidi alikuwa anautazamia wokovu wa taifa lake Israeli, yaani wakati wayahudi wapo bize na mali na fedha, yeye alikuwa kama Danieli, akiomba na kutafuta Habari za kuja kwa masihi duniani.

Luka 2:25 “Na tazama, pale Yerusalemu palikuwa na mtu, jina lake Simeoni, naye ni mtu mwenye haki, mcha Mungu, akiitarajia faraja ya Israeli; na Roho Mtakatifu alikuwa juu yake.

26 Naye alikuwa ameonywa na Roho Mtakatifu ya kwamba hataona mauti kabla ya kumwona Kristo wa Bwana.

27 Basi akaja hekaluni ameongozwa na Roho; na wale wazazi walipomleta mtoto Yesu ndani, ili wamfanyie kama ilivyokuwa desturi ya sheria,

28 yeye mwenyewe alimpokea mikononi mwake, akamshukuru Mungu, akisema,

29 Sasa, Bwana, wamruhusu mtumishi wako, Kwa amani, kama ulivyosema;

30 Kwa kuwa macho yangu yameuona wokovu wako”,

Makundi ya watu kama hawa, huwa wanaonjeshwa kitu kingine tofauti na watu wa kawaida, huo ndio uvuli wake Mungu. Wanapewa mafunuo ya ndani sana, wanapewa ulinzi wa majeshi ya Malaika wengi,mfano Elisha, wanajaliwa haja za mioyo yao na Mungu. Kwasababu tayari wapo chini ya uvuli wake.

Je! Na sisi tunaweza kufikia mahali hapo?

Kama jibu ni ndio,

Basi hatuna budi, kufanana na makuhani wa Mungu kweli, wana wa Lawi, ambao wametengwa na dhambi na unajisi, Si tu kumkiri Kristo na kuendelea kuishi Maisha ya juu juu, bali tujikane na nafsi zetu pia kwake, yaani tuwe tayari kujitwika na misalaba yetu tumfate Kristo. Tukubali ulimwengu utupite na mambo yake yote.

Na kwa kufanya hivyo kwa neema zake, atatufikisha mahali pake pa siri.

Bwana atusaidie sote.

Amen.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

Mahali pa juu palikuwa ni wapi kama tunavyosoma katika biblia?

Ni SIRI gani Paulo aliyokuwa anaimaanisha katika Waefeso 5:32?

Barazani pa Mungu ni wapi? Kama tunavyosoma katika Yeremia 23:18?

Bwana alimaanisha nini aliposema mtu akija kwangu naye HAMCHUKII baba yake hawezi kuwa mwanafunzi wangu?

Rudi nyumbani

Print this post

ADHABU KALI KUTOKA KWA MUNGU, ITAMPATA MTU WA NAMNA GANI?

Mithali 15:10a “Adhabu kali ina yeye aiachaye njia;..”.

Mapigo ya Mungu yanatofautiana na mtu na mtu.. Tofauti na tunavyodhani kuwa muuaji ndiye atakayeadhibiwa sana siku ile kuliko mtu aliyeuacha wokovu.

Jibu la la! Maandiko yanatuambia, “Adhabu kali ina yeye aiachaye njia”, hasemi tu ‘adhabu’ ina yeye aichaye njia, hapana, bali adhabu KALI..

Bwana Yesu alirudia , maneno hayo hayo tena katika

Luka 12:47 “Na mtumwa yule aliyejua mapenzi ya bwana wake, asijiweke tayari, wala kuyatenda mapenzi yake, atapigwa sana.

48 Na yule asiyejua, naye amefanya yastahiliyo mapigo, atapigwa kidogo. Na kila aliyepewa vingi, kwake huyo vitatakwa vingi; naye waliyemwekea amana vitu vingi, kwake huyo watataka na Zaidi”.

Leo hii inasikitisha kuona kuwa watu wengi wanakiri kwa vinywa vyao kuwa wameokoka, lakini kimatendo wapo mbali na Kristo, hawa wote ni kundi la wakristo walioicha njia, au waliojua mapenzi ya Bwana wao lakini wasiyafanye, wanaojua kuwa kutazama pornography hakumpendezi Mungu, lakini wanatazama, kuishi na mume/mke ambaye si wako ni dhambi mbele za Mungu lakini wao bado wanaendelea kuishi nao, tena wanazaa nao,

Wanaojua, kabisa kuvaa nguo za nusu uchi, na kujichubua ni dhambi, lakini bado wanaendelea kufanya mambo kama hayo,. Wachungaji na watumishi wanaojua kabisa, uasherati ni kosa kubwa sana kwa watu kama hao, lakini sasa imeshakuwa desturi yao. Hao ndio Kristo anaowazungumzia kuwa watakuwa na adhabu kali sana kule kuzimu.

Ndugu yangu, mateso yaliyopo kule, usidiriki kuyapima kwa akili zako, ni mahali ambapo hata hao wanaoteswa huko hawatamani, kukuona mtu kama wewe umefika huko, ni mateso makali sana, yasiyoelezeka, soma (Luka 16:27-29).

Na ndio maana Bwana Yesu alisema maneno haya;

Marko 9:45 “Na mguu wako ukikukosesha, ukate; ni afadhali kuingia katika uzima, u kiwete, kuliko kuwa na miguu miwili, na kutupwa katika jehanum; [

46 ambamo humo funza wao hafi, wala moto hauzimiki.]

47 Na jicho lako likikukosesha, ling’oe, ulitupe; ni afadhali kuingia katika ufalme wa Mungu, una chongo, kuliko kuwa na macho mawili, na kutupwa katika jehanum;

48 ambamo humo funza wao hafi, wala moto hauzimiki”.

Ndugu,unaposikia injili halafu huitendei kazi, ujue kuwa inageuka na kuwa adhabu kwako, na kwa jinsi unavyoendelea kuisikia ndivyo unavyojiongezea mapigo. Yathamini Maisha yako ya rohoni, siku hizi ni za mwisho, Unyakuo ni wakati wowote, Bado hujui siku zako za kuishi hapa duniani zimebakia ngapi, sikuzote kifo huwa kinakuja ghafla tu, hakina hodi je! Mimi na wewe tumejiandaaje? Kwa injili zote hizi tulizozisikia?

Ni heri tuyasalimishe Maisha yetu kwa Bwana leo, atuokoe, na kutufungua, tumaanishe kabisa kumfuata yeye bila lawama yoyote, tuweke kando mambo ya ulimwengu yanayopita, tuutafute utakatifu kwa bidii, kwasababu pasipo huo kamwe mbingu hatutaiona (Waebrania 12:14),

Lakini Ikiwa utatamani kutubu leo, na kuanza Maisha yako upya na Bwana, katika kipindi hichi kifupi tulichobakiwa nacho, basi yeye yupo tayari kukusamehe.. Ukiiomba sala hii fupi ya TOBA, ukiisema kwa Imani, basi utapokea msamaha hapo hapo ulipo.. Hivyo kama upo tayari kuyasalimisha leo Maisha yako kwa Bwana.

Hapo ulipo unaweza kutafuta mahali pa utulivu peke yako, kisha piga magoti, nyosha mkono wako mmoja juu, kama ishara ya kuyasalimisha Maisha yako kwa Bwana. Kisha, ukishakuwa katika utulivu, sema maneno haya, kwa sauti:

BABA YANGU, NAJA MBELE ZAKO, NINAKIRI KUWA NIMEKUWA MWANA MWASI MBELE ZAKO KWA MUDA MREFU, KWA WINGI WA DHAMBI ZANGU, NIMESTAHILI ADHABU NA MAPIGO MAKALI KUTOKA KWAKO, NI KWELI BWANA NILIYAJUA MAPENZI YAKO LAKINI SIKUYATENDA. LAKINI LEO MIMI MWANAO (TAJA JINA LAKO) NIMEDHAMIRIA KUYAANZA MAISHA YANGU UPYA NA WEWE.  NAOMBA UNISAMEHE BABA YANGU.

KUANZIA LEO NINAACHA NJIA ZANGU MBAYA ZOTE, NINAMKATAA SHETANI NA KAZI ZAKE ZOTE, NINAUKATAA ULIMWENGU. NAOMBA DAMU YA MWANAO YESU KRISTO, UNISAFISHE NA KUNITAKASA KABISA.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNISAMEHE. KAMA ULIVYOSEMA KATIKA NENO LAKO, YEYOTE AJAYE KWANGU SITAMTUPA NJE KWAKE. NAMI NAAMINI UMENIPOKEA, NA KUNIFANYA KIUMBE KIPYA LEO. NAOMBA UNIPE UWEZO WA KUUSHINDA ULIMWENGU NA KUUISHIA WOKOVU SIKU ZOTE ZA MAISHA YANGU.

ASANTE BWANA YESU KWA NEEMA YAKO, NA MSAMAHA WAKO.

AMEN.

Basi ikiwa umeisema sala hiyo ya Imani, fahamu kuwa Mungu anatazama moyo wako, na sio sala tu.  Yupo mwanamke ambaye alikuwa na dhambi nyingi, lakini kwa jinsi alivyomaanisha tu mbele za Yesu, kabla hata hajaomba msamaha au kujieleza chochote, muda huo huo Bwana alimwambia “umesamehewa dhambi zako”. Hiyo ni kuonyesha kuwa Toba hasaa haipo katika maneno matupu tu, bali katika moyo.(Luka 7:36-50)

Na wewe pia ikiwa toba yako, imeambatana na kuachana na huyo mume/mke wa mtu, imeambatana na kuacha kutazama picha za ngono mitandaoni milele, imeambatana na kuacha kuishi na huyo girlfriend/boyfriend ambaye hamjaona naye.. Ujue kuwa msamaha kutoka kwa Bwana umeshaupokea.

Hivyo, kuanzia leo, anza kuishi Maisha ya kuukulia wokovu, na kama hukubatizwa unapaswa ubatizwe, Ikiwa utahitaji msaada huo, basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi 0693036618/0789001312 tutakusaidia kwa neema za Bwana.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

TOBA IGUSAYO MOYO WA BWANA.

Je! Kuna dhambi kubwa na ndogo, na kama hakuna je! Mtu aliyeua na aliyetukana je watapata adhabu sawa?

Kwanini Mungu awachome watu kwenye ziwa la moto na hali yeye ndiye aliyewaumba?

TABIA YA WAZI INAYOWATOFAUTISHA MANABII WA UONGO NA WALE WA UKWELI.

Mungu anaposema “nitaliweka jina langu” ana maana gani?

Rudi nyumbani

Print this post

Sikio lisikialo, na jicho lionalo, BWANA ndiye aliyeyafanya yote mawili.

SWALI: Huu mstari una maana gani ?

Mithali 20:12
[12]Sikio lisikialo, na jicho lionalo,
BWANA ndiye aliyeyafanya yote mawili.


JIBU: Utajiuliza ni kwanini haijasema “Sikio na jicho” Bwana ndiye aliyeyafanya yote mawili..badala yake inasema ..

Sikio lisikialo, na jicho lionalo,
BWANA ndiye aliyeyafanya yote mawili.

Hii ni kuweka msisitizo katika kazi zao jinsi zinavyojitegemea…sikio haliwezi kuona, wala jicho kusikia, kwasababu kila moja limeundiwa mfumo wake tofauti wa kipekee..Lakini kutokufanana kwao haviwafanyi viwe na miungu miwili tofauti..bali ni Mungu yule yule mmoja aliyeviumba vyote.

Hata sasa tunapaswa tutambue kuwa Mungu ni Mungu anayeumba vitu katika mionekano tofauti tofauti..mmoja atamfanya mchina mwingine mwafrika, sio kwamba kuna itilafu au mapungufu katika jamii fulani ndio maana ikawa hivyo hapana.. ndivyo Mungu alivyotaka watu wake wasiwe na mionekano na maumbile yanayofanana, amependa tu iwe hivyo

Vilevile katika Kanisa Mungu ameweka vipawa mbalimbali..mwingine mwinjilisti, mwingine mwalimu, mwingine mchungaji..hata katikati ya hao wainjilisti au manabii bado kawatofautisha wote wasifanane..

Kutokuhubiri kwa kufoka au kwa utulivu kama yule hakukufanyi wewe usiwe na karama ile..

1 Wakorintho 12:4-6
[4]Basi pana tofauti za karama; bali Roho ni yeye yule.
[5]Tena pana tofauti za huduma, na Bwana ni yeye yule.
[6]Kisha pana tofauti za kutenda kazi, bali Mungu ni yeye yule azitendaye kazi zote katika wote.

Hivyo tuonapo tofauti hizi, ndani ya kanisa lake, au ulimwenguni tusinyoosheane vidole na kusema yule sio Mungu, maadamu tupo katika mstari ule ule wa imani, hatupaswi kushangaa sana au kulazimisha mambo yote yafanane..bali tukumbuke tu huu usemi..

Sikio lisikialo, na jicho lionalo,
BWANA ndiye aliyeyafanya yote mawili.

Itambue nafasi yako, Mungu aliyokuchagulia, kisha isimamie hiyo kwa bidii kwasababu vyote ni kwa utukufu wake mwenyewe.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

https://wingulamashahidi.org/wp-admin/post.php?post=18939&action=edit#

KWANINI TUNAPASWA TUJIZUIE?

Biblia ina maana gani inaposema akonyezaye kwa jicho huleta masikitiko?

JE! NI DHAMBI KUIMBA WIMBO WA TAIFA?

Rudi nyumbani

Print this post

Biblia inamaana gani inaposema “Wewe uchukiaye sanamu, wateka mahekalu?”

SWALI: Naomba kufahamu Bibliainaposema “Wewe uchukiaye sanamu, wateka mahekalu?” inamaana gani? Kuteka mahekalu ndio kukoje?

Warumi 2:21 “basi wewe umfundishaye mwingine, je! Hujifundishi mwenyewe? Wewe uhubiriye kwamba mtu asiibe, waiba mwenyewe?

22 Wewe usemaye kwamba mtu asizini, wazini mwenyewe? Wewe uchukiaye sanamu, wateka mahekalu?


JIBU: Maneno hayo aliyasema mtume Paulo kwa uweza wa Roho Mtakatifu, lakini hakutoa maelezo marefu, ni kwa namna gani wayahudi walikuwa wanateka mahekalu.

Lakini kulingana na maneno yake, ni kuwa kulikuwa ni desturi mbaya kwa baadhi ya wayahudi waliokuwa wanaishi kwenye mataifa ya wapagani, ya kuvamia mahekalu yao, kisha kuiba miungu yao, ambayo haswaa ilikuwa inatengenezwa kwa vito vya thamani kubwa kama vile fedha, au dhahabu.

Hivyo wenyewe walikuwa wanaviiba  na kwenda kuviuza kama vilivyo , au wanaviyeyusha na kuviuza kama VITO kinyume chake,. Jambo ambalo si tu Mungu alilipinga, bali pia lilikuwa ni kinyume na sheria za watu wa mataifa..

Jambo kama hilo utaliona  likitajwa tena katika ile Habari ya Paulo, alipokuwa kule Efeso, wale watu walipoleta vurugu kwasababu ya Paulo kuhubiri habari ambazo zinakinzana na ibada za miungu yao. Utaona pale walipopeleka mashitaka, wale waamuzi hawakuona kosa lolote juu ya akina Paulo,..Na moja ya makosa ambayo walitazamia kuyaona kwa mitume, ni hilo la kuiba vitu vya mahekalu yao.

Matendo 19:36 “Basi kwa kuwa mambo haya hayawezi kukanushwa, imewapasa kutulia; msifanye neno la haraka haraka.

37 Kwa maana mmewaleta watu hawa, wasioiba vitu vya hekalu wala kumtukana mungu mke wetu”.

Sasa tukirudi katika swali, kwanini Mtume Paulo aliposema “Wewe uchukiaye sanamu, wateka mahekalu?”, Alimaanisha kuwa Ikiwa umeamua kutojihusisha na ibada za sanamu, iweje basi uibe vitu vyao na kuvifanyia biashara?.. Je! Kuna tofauti yoyote na wale wanaovifanyia ibada?

Mungu alishakataza tabia kama hiyo katika kitabu cha Kumbukumbu la Torati, soma;

Kumbukumbu 7:25 “Sanamu za kuchonga za miungu yao mtaziteketeza kwa moto; usitamani fedha wala dhahabu iliyo juu yao, wala usiitwae iwe yako usije ukanaswa nayo; kwa maana ni machukizo kwa Bwana, Mungu wako”;

Hii inatufundisha nini?

Tukikataa dhambi Fulani basi tusiwe wanafki, kuitenda katika maumbile mengine..Kwamfano,  tukisema hatunywi pombe, hatupaswi kwenda kuiba/kuchukua chupa za bia na kwenda kuziuza..Ikiwa hatuvuti sigara, hatupaswi pia kwenda kununua HISA za sigara, katika masoko ya fedha,  kisa tu zina faida kubwa. Ikiwa hatuzini, hatupaswi pia kufanya biashara za guesthouse kwa wazinzi.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

Maashera na Maashtorethi ni nini?

Bwana aliposema kuwa yeye ni “Mungu wa miungu” alikuwa na maana gani?..je! yeye ni Mungu wa sanamu?

Je! ni sahihi kwa mkristo kujifukiza?

Maswali na Majibu

Rudi nyumbani

Print this post

“Amdhaminiye mgeni hakosi ataumia;Achukiaye mambo ya dhamana yu salama

Nini maana ya huu mstari? Mithali 11: 15 “Amdhaminiye mgeni hakosi ataumia; Achukiaye mambo ya dhamana yu salama”.


Biblia ni kitabu pekee ambacho kinamfundisha mtu kutembea katika kanuni zote (yaani za mwilini na rohoni), jinsi ya kuishi katika roho, vilevile na jinsi ya kuishi katika mwili,  Na moja ya kitabu ambacho kinatufundisha kanuni za kutembea katika mwili na kufanikiwa ni hichi kitabu cha Mithali,

Ni kitabu ambacho kina mahusia kwa makundi yote ya watu kuanzia wanandoa, vijana, watoto, maskini,  matajiri, vilevile kina maonyo kwa viongozi, hadi kwa watumwa, Hivyo, tukirudi katika swali, kwanini Sulemani kwa hekima ya Roho alisema.. “Amdhaminiye mgeni hakosi ataumia; Achukiaye mambo ya dhamana yu salama”.

Hapo Hakumaanisha kuwa, kumdhamini mtu yeyote, ni kosa, hapana, bali anatoa angalizo katika kutoa dhamana kwa mtu mgeni (usiyemfahamu), kunaweza kukuweka katika hatari kubwa sana ya kukumbana na shida. Kumchukulia mtu mkopo bank halafu, unaweka nyumba yako rehani, mtu ambaye umekutana naye kwa  kipindi kifupi tu, bado hujui vizuri mwelekeo wake upoje, halafu unaweka mpaka na mali zako rehani, hapo ni rahisi sana kuishia pabaya,

Hatupaswi kukurupuka kumdhamini mtu, ili mradi tu mtu kisa tunafanya tendo jema. Hapana kinyume chake biblia inaturuhusu tuchukue muda wa kumtambua, kumfahamu, kumwelewa, ndipo tumdhamini kama kuna umuhimu wa kufanya hivyo, Lakini Zaidi sana tukibaki kama tulivyo, tukamwachia Mungu asimamie mambo hayo ya kudhamini, tutakuwa katika upande ulio salama Zaidi. Kwasababu bado wakati mwingine mtu anaweza akawa ni mwema kweli, au akawa na mwelekeo mzuri lakini kwa bahati mbaya mambo yakabadilikia ghafla njiani, labda kapata hasara, hapo atakayeumia ni wewe uliyemdhamini.

Na ndio maana bado Biblia bado inasisitiza suala hilo hilo katika vifungu vingine mbeleni kidogo inasema..

Mithali 22:26 “Usiwe mmoja wao wawekao rehani; Au walio wadhamini kwa deni za watu; 27 Kama huna kitu cha kulipa; Kwani ukaondolee kitanda chako chini yako?”

Lakini maneno haya yanatufundisha nini rohoni?

Yupo ambaye hakuogopa jambo hilo, aliingia katika hii hatari ya kutudhamini, huku akijua kabisa, anaowadhamini hawawezi kulipa madeni yao hata kidogo, lakini alijiingiza katika shida zao, na kwa nguvu zake, akafanikiwa kulipa  makosa yetu yote.

Angeweza kuacha asitudhamini, kwasababu maandiko yametoa ruhusa hiyo kama tulivyosoma.. Lakini kwa upendo wake, usiopimika, alikubali kulipa madeni yetu yote. Na huyo si mwingine Zaidi ya Bwana wetu YESU KRISTO.

Hakika sifa heshima na utukufu vina yeye, milele na milele. Amina.

Ni kitendo cha kushangaza sana na cha aibu, kuona mpaka sasa kuna baadhi ya watu wapo nje ya neema yake.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya kilichotarajiwa kikikawia kuja moyo huugua (Mithali 13:12)?.

Je! kuna madhara kuchukiwa na kila mtu kwasababu huna mali?. Kama biblia inavyosema katika Mithali 14:20?.

Kuwaogopa wanadamu huleta mtego,(Mithali 29:25)

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

UNYAKUO.

Rudi nyumbani

Print this post

YUKO WAPI MFALME WA WAYAHUDI?

Vipindi vya ukristo huwa vinabadilika, mambo hayawezi kubaki vilevile tangu siku ulipookoka hadi siku unakufa. Yapo majira utamwona Kristo waziwazi katika Maisha yako, yapo majira Kristo hutamwona kwa uwazi kama unavyodhani, hapo ndipo itakapokugharimu kumtafuta, ili umpate.

Hiyo ni kanuni Mungu aliyoiweka, ambayo kila mtu aliyempokea yeye hana budi kuifahamu. Kuna watu wanashindwa kulielewa hili, na ndio maana wanapofikia hatua ya kutomwona Kristo kiurahisi, kama ilivyokuwa zamani  wanaishia kurudi nyuma. Wakidhani kama hakuwa ni Mungu aliyewaita.

Embu tuitazame ile Habari ya mamajusi, wale watu walitokea nchi ya mbali sana huko Mashariki (Pengine nchi ya Babeli), lakini katika kutafuta tafuta kwao Habari za Mungu katika mambo yao ya anga, Mungu aliwapa neema ya kumwona Kristo katika njia hiyo.

Ndipo wakaiona nyota moja tofauti na nyingine iking’ara sana, na ghafla ile nyota ikaja kutua ulimwenguni, lakini haikutua sehemu nyingine yoyote Zaidi ya taifa la Israeli.. Ndipo wakaanza safari ya kuifuata.

Hivyo walipofika Israeli walitarajia kuwa wangeiona tena iwaelekeze mpaka eneo husika mtoto alipo, lakini hilo halikutokea, pengine wakatazama tena angani kwa umakini zaidi, lakini hawakuona chochote.. Hatujui ilipita muda gani wakiingojea itokee, lakini hakuna chochote kilichotokea, ndipo wakaanza kutafuta, kwa kuulizia Habari za Kristo kazaliwa awpi, wakafika mpaka wa Herode mfalme, kuulizia Habari hizo, ndipo wakapewa taarifa, kutoka kwa Herode  kuwa mfalme anazaliwa Bethelehemu ya uyahudi..

Sasa wakati wanakwenda Bethlehemu  ndipo ile nyota waliyokuwa wameipoteza wakaiona tena, katika nyumba aliyokuwa amelazwa mtoto, biblia inasema walipoiona walifurahi furaha kubwa mno,

Tusome..

Mathayo 2 :1 “Yesu alipozaliwa katika Bethlehemu ya Uyahudi zamani za mfalme Herode, tazama, mamajusi wa mashariki walifika Yerusalemu, wakisema,

2 Yuko wapi yeye aliyezaliwa mfalme wa Wayahudi? Kwa maana tuliiona nyota yake mashariki, nasi tumekuja kumsujudia.

3 Basi mfalme Herode aliposikia hayo, alifadhaika, na Yerusalemu pia pamoja naye.

4 Akakusanya wakuu wa makuhani wote na waandishi wa watu, akatafuta habari kwao, Kristo azaliwa wapi?

5 Nao wakamwambia, Katika Bethlehemu ya Uyahudi; kwa maana ndivyo ilivyoandikwa na nabii,

6 Nawe Bethlehemu, katika nchi ya Yuda, Hu mdogo kamwe katika majumbe wa Yuda; Kwa kuwa kwako atatoka mtawala Atakayewachunga watu wangu Israeli.

7 Kisha Herode akawaita wale mamajusi faraghani, akapata kwao hakika ya muda tangu ilipoonekana ile nyota.

8 Akawapeleka Bethlehemu, akasema, Shikeni njia, mkaulize sana mambo ya mtoto; na mkiisha kumwona, nileteeni habari, ili mimi nami niende nimsujudie.

9 Nao waliposikia maneno ya mfalme, walishika njia; na tazama, ile nyota waliyoiona mashariki ikawatangulia, hata ikaenda ikasimama juu ya mahali alipokuwapo mtoto.

10 Nao walipoiona ile nyota, walifurahi furaha kubwa mno.

11 Wakaingia nyumbani, wakamwona mtoto pamoja na Mariamu mamaye, wakaanguka wakamsujudia; nao walipokwisha kufungua hazina zao, wakamtolea tunu; dhahabu na uvumba na manemane.

12 Nao wakiisha kuonywa na Mungu katika ndoto wasimrudie Herode, wakaenda zao kwao kwa njia nyingine”.

Nachotaka uone ni kuwa, nyota ilionekana, ikapotea, ikaonekana tena..Lakini hawakukata tamaa na kusema turudi mashariki, tukaendelee na shughuli zetu, tuliona maruweruwe hapana, bali walimtafuta Kristo kwa bidii, na mwisho wa siku wakafika walipopakusudia.

Kipindi cha awali cha wokovu, ni rahisi kumwona Kristo katika kila hatua, lakini upo wakati atabadilisha mwonekano wake, atataka umtafute, atataka upate maarifa ya kutosha kuhusu yeye, hapo ndipo kunapokuja kujifunza kwa bidii, kuulizia Habari za wokovu, Habari za mbinguni, Habari za umilele, kuomba na kufunga, sio kukaa tu na kusema mimi nimeokoka Yesu ananipenda, halafu basi, hilo halipo katika safari ya wokovu.. Bwana ataruhusu hata wakati mwingine umtafute kutoka kwa maadui zake, kama vile mamajusi walivyotafuta taarifa kwa Herode adui wa Kristo.

Hivyo usiporudi nyuma, usipokata tamaa, ni uhakika kuwa mwisho wako utakuwa ni uzima wa milele. Hakuna mtu yeyote anayemtafuta Kristo kwa kumaanisha mwisho wake ukawa ni mbaya hakuna. Utamwona tu Kristo mwishoni. Utamfurahia kwa furaha kubwa, kuanzia hapa duniani hadi kule mbinguni.

Hivyo,  ikiwa upo katika hatua kama hii, usipunguze mwendo wako, kinyume chake ndio uzidishe kumtafuta Bwana kwa bidi kwasababu ndivyo unavyokaribia kukutana naye tena.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Zile tunu (Dhahabu, uvumba na manemane) Mamajusi walizozitoa kwa Bwana (Mathayo 2) . ziliwakilisha nini?

BASI, IWENI NA HURUMA, KAMA BABA YENU ALIVYO NA HURUMA(Luka 6:36)

ALAMA ZA BENDERA YA ISRAELI ZINAWAKILISHA NINI?

TUJIFUNZE JAMBO KWA WANAWAKE HAWA WAWILI.

KUSUDI LA MIMI KUWEPO DUNIANI NI LIPI?

Rudi nyumbani

Print this post