Huu mstari una maana gani?
Zaburi 91:1 “Aketiye mahali pa siri pake Aliye juu Atakaa katika uvuli wake Mwenyezi”.
Maandiko hayo yanatuonyesha kumbe Mungu anao uvuli wake. Na uvuli huo hawakai watu wote ilimradi tu, bali wale tu wanaokaa katika mahali pake pa siri.
Sasa swali utajiuliza huko mahali pake pa siri ni wapi?
Kuna madaraja ya kumfikia Mungu, yapo yanayofikiwa na wakristo wa kawaida tu, wale wanaomtafuta Mungu jumapili kwa jumapili, au mwezi kwa mwezi, lakini pia yapo yanayofikiwa na wakristo waliojikana, na kudhamiria kumfuata Kristo katika Maisha yao.
Hao wanaojikana ndio wanaofikia mahali pa siri pa Mungu.
Wanafananisha na makuhani, ambao, katika ile hema ya kukutania, au hekalu la Mungu, ni wao tu walikuwa na uwezo wa kupaingia patakatifu, na kule patakatifu pa patakatifu, palipo na kile kiti cha rehema cha Mungu.Kumbuka si kila mwisraeli, alifika pale, si kila mtu anayejiona anamcha Mungu aliweza kufika pale, kwa mtu wa kawaida ukijitahidi sana, uliishia katika ule ua wa hema ya kukutanikia, lakini ndani, sehemu za siri za Mungu walioweza kuingia makuhani tu.
Vivyo hivyo katika agano jipya, Mungu anao sehemu yake ya siri, na ni watu baadhi tu wanaoweza kufika huko, Mfano hai katika biblia ni mwanamke kama ANA, yeye, aliweza kupafikia hapo..na ndio maana alikuwa miongoni mwa watu wachache sana waliofunuliwa mpango wa Mungu wa wokovu,yaani kuja kwake Yesu duniani..
Lakini hiyo yote ni kwasababu alikuwa ni mwanamke aliyeupoteza ubinti wake, autumie kwa Mungu hadi uzee wake, haundoki hekaluni, mchana na usiku akisali na kufunga.
Luka 2:36 “Palikuwa na nabii mke, jina lake Ana, binti Fanueli, wa kabila ya Asheri, na umri wake ulikuwa miaka mingi, alikuwa amekaa na mume miaka saba baada ya uanawali wake.
37 Naye ni mjane wa miaka themanini na minne; haondoki katika hekalu, ila huabudu usiku na mchana kwa kufunga na kuomba.
38 Huyu alitokea saa ile ile akamshukuru Mungu, na wote waliokuwa wakiutarajia ukombozi katika Yerusalemu akawatolea habari zake”.
Mwingine, ni Simeoni, naye pia biblia inasema alikuwa ni mtu wa haki, na anaye mcha Mungu, tena Zaidi alikuwa anautazamia wokovu wa taifa lake Israeli, yaani wakati wayahudi wapo bize na mali na fedha, yeye alikuwa kama Danieli, akiomba na kutafuta Habari za kuja kwa masihi duniani.
Luka 2:25 “Na tazama, pale Yerusalemu palikuwa na mtu, jina lake Simeoni, naye ni mtu mwenye haki, mcha Mungu, akiitarajia faraja ya Israeli; na Roho Mtakatifu alikuwa juu yake.
26 Naye alikuwa ameonywa na Roho Mtakatifu ya kwamba hataona mauti kabla ya kumwona Kristo wa Bwana.
27 Basi akaja hekaluni ameongozwa na Roho; na wale wazazi walipomleta mtoto Yesu ndani, ili wamfanyie kama ilivyokuwa desturi ya sheria,
28 yeye mwenyewe alimpokea mikononi mwake, akamshukuru Mungu, akisema,
29 Sasa, Bwana, wamruhusu mtumishi wako, Kwa amani, kama ulivyosema;
30 Kwa kuwa macho yangu yameuona wokovu wako”,
Makundi ya watu kama hawa, huwa wanaonjeshwa kitu kingine tofauti na watu wa kawaida, huo ndio uvuli wake Mungu. Wanapewa mafunuo ya ndani sana, wanapewa ulinzi wa majeshi ya Malaika wengi,mfano Elisha, wanajaliwa haja za mioyo yao na Mungu. Kwasababu tayari wapo chini ya uvuli wake.
Je! Na sisi tunaweza kufikia mahali hapo?
Kama jibu ni ndio,
Basi hatuna budi, kufanana na makuhani wa Mungu kweli, wana wa Lawi, ambao wametengwa na dhambi na unajisi, Si tu kumkiri Kristo na kuendelea kuishi Maisha ya juu juu, bali tujikane na nafsi zetu pia kwake, yaani tuwe tayari kujitwika na misalaba yetu tumfate Kristo. Tukubali ulimwengu utupite na mambo yake yote.
Na kwa kufanya hivyo kwa neema zake, atatufikisha mahali pake pa siri.
Bwana atusaidie sote.
Amen.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Mada Nyinginezo:
Mahali pa juu palikuwa ni wapi kama tunavyosoma katika biblia?
Ni SIRI gani Paulo aliyokuwa anaimaanisha katika Waefeso 5:32?
Barazani pa Mungu ni wapi? Kama tunavyosoma katika Yeremia 23:18?
Neno Bushuti limeonekana mara moja tu katika biblia, na maana ya Neno hilo ni “Blanketi”.
Waamuzi 4:18 “Yaeli akatoka kwenda kumlaki Sisera, akamwambia, Karibu Bwana wangu, karibu kwangu; usiogope. Akakaribia kwake hemani, naye akamfunika kwa bushuti”.
Kipindi Sisera, Adui wa wayahudi anamkimbia Baraka, alifika kwenye nyumba ya mwanamke mmoja aliyeitwa Yaeli, na mwanamke huyu alimlaghai kwa hila na kumwua.
Kabla ya kumwua maandiko yanasema alimlaza na kumfunika kwa hilo Bushuti (yaani blanketi), na alipopata usingizi alimwua.
Habari hiyo kamili inapatikana katika mlango wa 4 wa kitabu hicho cha Waamuzi.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Mada Nyinginezo:
Mithali 15:10a “Adhabu kali ina yeye aiachaye njia;..”.
Mapigo ya Mungu yanatofautiana na mtu na mtu.. Tofauti na tunavyodhani kuwa muuaji ndiye atakayeadhibiwa sana siku ile kuliko mtu aliyeuacha wokovu.
Jibu la la! Maandiko yanatuambia, “Adhabu kali ina yeye aiachaye njia”, hasemi tu ‘adhabu’ ina yeye aichaye njia, hapana, bali adhabu KALI..
Bwana Yesu alirudia , maneno hayo hayo tena katika
Luka 12:47 “Na mtumwa yule aliyejua mapenzi ya bwana wake, asijiweke tayari, wala kuyatenda mapenzi yake, atapigwa sana.
48 Na yule asiyejua, naye amefanya yastahiliyo mapigo, atapigwa kidogo. Na kila aliyepewa vingi, kwake huyo vitatakwa vingi; naye waliyemwekea amana vitu vingi, kwake huyo watataka na Zaidi”.
Leo hii inasikitisha kuona kuwa watu wengi wanakiri kwa vinywa vyao kuwa wameokoka, lakini kimatendo wapo mbali na Kristo, hawa wote ni kundi la wakristo walioicha njia, au waliojua mapenzi ya Bwana wao lakini wasiyafanye, wanaojua kuwa kutazama pornography hakumpendezi Mungu, lakini wanatazama, kuishi na mume/mke ambaye si wako ni dhambi mbele za Mungu lakini wao bado wanaendelea kuishi nao, tena wanazaa nao,
Wanaojua, kabisa kuvaa nguo za nusu uchi, na kujichubua ni dhambi, lakini bado wanaendelea kufanya mambo kama hayo,. Wachungaji na watumishi wanaojua kabisa, uasherati ni kosa kubwa sana kwa watu kama hao, lakini sasa imeshakuwa desturi yao. Hao ndio Kristo anaowazungumzia kuwa watakuwa na adhabu kali sana kule kuzimu.
Ndugu yangu, mateso yaliyopo kule, usidiriki kuyapima kwa akili zako, ni mahali ambapo hata hao wanaoteswa huko hawatamani, kukuona mtu kama wewe umefika huko, ni mateso makali sana, yasiyoelezeka, soma (Luka 16:27-29).
Na ndio maana Bwana Yesu alisema maneno haya;
Marko 9:45 “Na mguu wako ukikukosesha, ukate; ni afadhali kuingia katika uzima, u kiwete, kuliko kuwa na miguu miwili, na kutupwa katika jehanum; [
46 ambamo humo funza wao hafi, wala moto hauzimiki.]
47 Na jicho lako likikukosesha, ling’oe, ulitupe; ni afadhali kuingia katika ufalme wa Mungu, una chongo, kuliko kuwa na macho mawili, na kutupwa katika jehanum;
48 ambamo humo funza wao hafi, wala moto hauzimiki”.
Ndugu,unaposikia injili halafu huitendei kazi, ujue kuwa inageuka na kuwa adhabu kwako, na kwa jinsi unavyoendelea kuisikia ndivyo unavyojiongezea mapigo. Yathamini Maisha yako ya rohoni, siku hizi ni za mwisho, Unyakuo ni wakati wowote, Bado hujui siku zako za kuishi hapa duniani zimebakia ngapi, sikuzote kifo huwa kinakuja ghafla tu, hakina hodi je! Mimi na wewe tumejiandaaje? Kwa injili zote hizi tulizozisikia?
Ni heri tuyasalimishe Maisha yetu kwa Bwana leo, atuokoe, na kutufungua, tumaanishe kabisa kumfuata yeye bila lawama yoyote, tuweke kando mambo ya ulimwengu yanayopita, tuutafute utakatifu kwa bidii, kwasababu pasipo huo kamwe mbingu hatutaiona (Waebrania 12:14),
Lakini Ikiwa utatamani kutubu leo, na kuanza Maisha yako upya na Bwana, katika kipindi hichi kifupi tulichobakiwa nacho, basi yeye yupo tayari kukusamehe.. Ukiiomba sala hii fupi ya TOBA, ukiisema kwa Imani, basi utapokea msamaha hapo hapo ulipo.. Hivyo kama upo tayari kuyasalimisha leo Maisha yako kwa Bwana.
Hapo ulipo unaweza kutafuta mahali pa utulivu peke yako, kisha piga magoti, nyosha mkono wako mmoja juu, kama ishara ya kuyasalimisha Maisha yako kwa Bwana. Kisha, ukishakuwa katika utulivu, sema maneno haya, kwa sauti:
BABA YANGU, NAJA MBELE ZAKO, NINAKIRI KUWA NIMEKUWA MWANA MWASI MBELE ZAKO KWA MUDA MREFU, KWA WINGI WA DHAMBI ZANGU, NIMESTAHILI ADHABU NA MAPIGO MAKALI KUTOKA KWAKO, NI KWELI BWANA NILIYAJUA MAPENZI YAKO LAKINI SIKUYATENDA. LAKINI LEO MIMI MWANAO (TAJA JINA LAKO) NIMEDHAMIRIA KUYAANZA MAISHA YANGU UPYA NA WEWE. NAOMBA UNISAMEHE BABA YANGU.
KUANZIA LEO NINAACHA NJIA ZANGU MBAYA ZOTE, NINAMKATAA SHETANI NA KAZI ZAKE ZOTE, NINAUKATAA ULIMWENGU. NAOMBA DAMU YA MWANAO YESU KRISTO, UNISAFISHE NA KUNITAKASA KABISA.
ASANTE BWANA YESU KWA KUNISAMEHE. KAMA ULIVYOSEMA KATIKA NENO LAKO, YEYOTE AJAYE KWANGU SITAMTUPA NJE KWAKE. NAMI NAAMINI UMENIPOKEA, NA KUNIFANYA KIUMBE KIPYA LEO. NAOMBA UNIPE UWEZO WA KUUSHINDA ULIMWENGU NA KUUISHIA WOKOVU SIKU ZOTE ZA MAISHA YANGU.
ASANTE BWANA YESU KWA NEEMA YAKO, NA MSAMAHA WAKO.
AMEN.
Basi ikiwa umeisema sala hiyo ya Imani, fahamu kuwa Mungu anatazama moyo wako, na sio sala tu. Yupo mwanamke ambaye alikuwa na dhambi nyingi, lakini kwa jinsi alivyomaanisha tu mbele za Yesu, kabla hata hajaomba msamaha au kujieleza chochote, muda huo huo Bwana alimwambia “umesamehewa dhambi zako”. Hiyo ni kuonyesha kuwa Toba hasaa haipo katika maneno matupu tu, bali katika moyo.(Luka 7:36-50)
Na wewe pia ikiwa toba yako, imeambatana na kuachana na huyo mume/mke wa mtu, imeambatana na kuacha kutazama picha za ngono mitandaoni milele, imeambatana na kuacha kuishi na huyo girlfriend/boyfriend ambaye hamjaona naye.. Ujue kuwa msamaha kutoka kwa Bwana umeshaupokea.
Hivyo, kuanzia leo, anza kuishi Maisha ya kuukulia wokovu, na kama hukubatizwa unapaswa ubatizwe, Ikiwa utahitaji msaada huo, basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi 0693036618/0789001312 tutakusaidia kwa neema za Bwana.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Bwana akubariki sana.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
Kwanini Mungu awachome watu kwenye ziwa la moto na hali yeye ndiye aliyewaumba?
TABIA YA WAZI INAYOWATOFAUTISHA MANABII WA UONGO NA WALE WA UKWELI.
Wale Nyoka waliowadhuru wana wa Israeli jangwani walikuwa wana maumbile ya moto au?. Maana maandiko yanasema walikuwa ni Nyoka wa moto, Na kama walikuwa wenye maumvile ya moto, waliwaumaje watu na walitokea wapi? Walishushwa au?
Jibu: Tusome,
Hesabu 21:6 “BWANA akatuma nyoka za moto kati ya watu, wakawauma, watu wengi wakafa”
Neno “moto” hapo halijatumika kuelezea maumbile (yaani miili) ya hao nyoka, kwamba wana miili iliyoundwa kwa malighafi ya moto, hapana!. Bali limetumika kuelezea “Rangi” ya hao Nyoka, kwamba wana rangi ya moto.
Rangi ya moto, inafananishwa na rangi ya “Shaba”. Mtu anaposema “sahani ile ni ya shaba” na anayesema “sahani ile ni ya moto” Ni kitu kimoja, wote wanamaanisha kitu kimoja.
Ndio maana baada ya pale utaona Musa anaagizwa atengeneze nyoka wa shaba, kuwakilisha rangi ya hao nyoka.
Hesabu 21:8 “Bwana akamwambia Musa, Jifanyie nyoka ya shaba, ukaiweke juu ya mti, na itakuwa kila mtu aliyeumwa, aitazamapo ataishi.
9 Musa akafanya nyoka ya shaba, akaiweka juu ya mti, hata ikiwa nyoka amemwuma mtu, alipoitazama ile nyoka ya shaba, akaishi”.
Nyoka hao wenye rangi ya moto, ni jamii ya Nyoka maarufu sana wenye sumu kali wanaopatikana jangwani, hadi leo wapo (Ni nyoka wa asili kabisa), maisha yao ni jangwani tu hawawezi kuishi mahali pengine, na huwa wanajificha chini ya mchanga, na kubakisha sehemu ndogo tu ya kichwa juu, hivyo si rahisi kuonekana.
Na endapo mtu akipita na bahati mbaya akakanyaga mchanga mahali ambapo nyoka huyo kajificha, basi aling’atwa na hakukuwa na matibabu.
Hivyo kwa hitimisho, walikuwa ni nyoka wa asili, isipokuwa rangi yao ni ya Moto (au shaba).
Lakini pamoja na hayo kulikuwa na ufunuo mkubwa juu ya tukio hilo lililowatokea wana wa Israeli, na huyo nyoka wa shaba, mpaka akaitwa Nehushtani.
Kwa maelezo marefu juu ya Nehushtani, unaweza kufungua hapa>> NEHUSHTANI.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Mada Nyinginezo:
SWALI: Huu mstari una maana gani ?
Mithali 20:12
[12]Sikio lisikialo, na jicho lionalo,
BWANA ndiye aliyeyafanya yote mawili.
JIBU: Utajiuliza ni kwanini haijasema “Sikio na jicho” Bwana ndiye aliyeyafanya yote mawili..badala yake inasema ..
Sikio lisikialo, na jicho lionalo,
BWANA ndiye aliyeyafanya yote mawili.
Hii ni kuweka msisitizo katika kazi zao jinsi zinavyojitegemea…sikio haliwezi kuona, wala jicho kusikia, kwasababu kila moja limeundiwa mfumo wake tofauti wa kipekee..Lakini kutokufanana kwao haviwafanyi viwe na miungu miwili tofauti..bali ni Mungu yule yule mmoja aliyeviumba vyote.
Hata sasa tunapaswa tutambue kuwa Mungu ni Mungu anayeumba vitu katika mionekano tofauti tofauti..mmoja atamfanya mchina mwingine mwafrika, sio kwamba kuna itilafu au mapungufu katika jamii fulani ndio maana ikawa hivyo hapana.. ndivyo Mungu alivyotaka watu wake wasiwe na mionekano na maumbile yanayofanana, amependa tu iwe hivyo
Vilevile katika Kanisa Mungu ameweka vipawa mbalimbali..mwingine mwinjilisti, mwingine mwalimu, mwingine mchungaji..hata katikati ya hao wainjilisti au manabii bado kawatofautisha wote wasifanane..
Kutokuhubiri kwa kufoka au kwa utulivu kama yule hakukufanyi wewe usiwe na karama ile..
1 Wakorintho 12:4-6
[4]Basi pana tofauti za karama; bali Roho ni yeye yule.
[5]Tena pana tofauti za huduma, na Bwana ni yeye yule.
[6]Kisha pana tofauti za kutenda kazi, bali Mungu ni yeye yule azitendaye kazi zote katika wote.
Hivyo tuonapo tofauti hizi, ndani ya kanisa lake, au ulimwenguni tusinyoosheane vidole na kusema yule sio Mungu, maadamu tupo katika mstari ule ule wa imani, hatupaswi kushangaa sana au kulazimisha mambo yote yafanane..bali tukumbuke tu huu usemi..
Sikio lisikialo, na jicho lionalo,
BWANA ndiye aliyeyafanya yote mawili.
Itambue nafasi yako, Mungu aliyokuchagulia, kisha isimamie hiyo kwa bidii kwasababu vyote ni kwa utukufu wake mwenyewe.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Mada Nyinginezo:
https://wingulamashahidi.org/wp-admin/post.php?post=18939&action=edit#
Ni kweli hakuna mtu aliyewahi kuuona uso wa Mungu Zaidi ya Bwana Yesu?
Biblia ina maana gani inaposema akonyezaye kwa jicho huleta masikitiko?
Kama Mungu ndiye kaumba kila kitu, je ni yeye huyo huyo ndiye aliyeumba dhambi pia?
SWALI: Naomba kuuliza kwamfano mimi ni mkristo mwenye uwezo wa kifedha, nikiombwa kuchangia ujenzi wa msikiti, Je! Ni halali kufanya hivyo?
JIBU: Tumeruhusiwa, kutoa misaada yoyote ile (Isiyokinzana na Neno la Mungu) kama tupendavyo kwa jinsi Bwana alivyotujalia bila kujali dini, Imani, jinsia au rangi, kabila n.k.. Kwamfano ukiombwa kujenga shule, au kutoa chakula, au kufadhili wazee wa Imani nyingine waruhusiwa kufanya hivyo, tena ni vema Zaidi, kwasababu unaonyesha upendo ule wa ki-Mungu kwao, ambao hautoki kwa sababu Fulani.
Lakini ikiwa ni mambo yanayokinzana na Neno la Mungu kama vile kusapoti ujenzi wa kiwanda cha pombe, au kusapoti madhabahu nyingine tofauti na ile ya YEHOVA, tunayemwabudu katika Kristo Yesu, hapo hatujaruhusiwa.
Kwasababu upo uhusiano mkubwa sana kati ya sadaka na madhabahu. Kumbuka kiroho Sadaka ni Ibada kamili.
Mathayo 6:21 “kwa kuwa hazina yako ilipo, ndipo utakapokuwapo na moyo wako”.
Moyo wako hauwezi kuwepo katika kanisa la Kristo, na wakati huo huo uwepo katika msikiti, au katika hekalu la Buddha, au la Baniani ambao mungu wao ni ng’ombe,. Hapo utakachokuwa unakifanya ni uzinzi wa kiroho, unazini na miungu migeni, bila wewe mwenyewe kujijua.
Na biblia inasema Mungu wetu ni Mungu mwenye wivu. Anatufananisha sisi na wake zake. Mungu hatazami tu pale tunapoisujudia au kuitumikia miungu migeni ndio achukizwe hapana, bali anatazama pia na sadaka zetu tuzitoazo.. Je tunazielekeza wapi? Kwake yeye, au kwa miungu migeni. Hapo tunapaswa tuwe makini sana.
Hivyo, kwa kuhitimisha ni kuwa, sisi kama wakristo, hatupaswi kuchangia ujenzi wa madhabahu za wasioamini. Ukiulizwa ni kwanini? Jibu lako ni kuwa IMANI YAKO HAIRUHUSU. Hivyo tu,
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Mada Nyinginezo:
Je! Ni sahihi kwa mkristo kuoa/kuolewa na mtu wa imani nyingine?
Tofauti na tunavyomchukulia Mungu kuwa ni Mkuu sana, hana haja ya kuambiwa chochote wala kujuzwa jambo, lakini kiuhalisia Mungu mwenyewe hajachagua kujiweka katika hiyo nafasi, tabia ya Mungu ni unyenyekevu.
Ijapokuwa anajua kila kitu, lakini wakati mwingine anajishusha kana kwamba hajui,
Vile vile ijapokuwa anauweledi na hakuna anayeweza kumshauri lakini wakati mwingine anajishusha na kukubali mashauri ya viumbe wake.
Kwamfano utaona Mungu anakubali ushauri wa Musa mara kadhaa.
Kutoka 32:9 “Tena BWANA akamwambia Musa, Mimi nimewaona watu hawa, na tazama, ni watu wenye shingo ngumu
10 basi sasa niache, ili hasira zangu ziwake juu yao, niwaangamize, nami nitakufanya wewe uwe taifa kuu.
11 Musa akamsihi sana BWANA, Mungu wake, na kusema, BWANA, kwa nini hasira zako kuwaka juu ya watu wako uliowaleta kutoka nchi ya Misri kwa uweza mkuu, na kwa mkono wenye nguvu?
12 Kwa nini Wamisri kunena, wakisema, Amewatoa kwa kuwatenda uovu, ili apate kuwaua milimani, na kuwaondoa watoke juu ya uso wa nchi? Geuka katika hasira yako kali, ughairi uovu huu ulio nao juu ya watu wako.
13 Mkumbuke Ibrahimu, na Isaka, na Israeli, watumishi wako, ambao uliwaapia kwa nafsi yako, na kuwaambia, Nitazidisha kizazi chenu mfano wa nyota za mbinguni; tena nchi hii yote niliyoinena nitakipa kizazi chenu nao watairithi milele.
14 Na BWANA akaughairi ule uovu aliosema ya kwamba atawatenda watu wake”.
Kadhalika ijapokuwa Bwana anafahamu kila kitu, lakini utaona kuna wakati anajishusha na kuanza kufanya uchunguzi wa jambo mpaka analivumbua, utalithibitisha hilo katika kile kitabu cha Ayubu 28, wakati anafanya uchunguzi wa kuitafuta hekima.
Vile vile ijapokuwa anatujua wanadamu wote na matendo yetu lakini utaona kuna wakati anajishusha na kuanza utafiti kama mwanadamu kupima kiwango cha maovu duniani, utalithibitisha hilo kipindi anataka kuiangamiza Sodoma na Ghomora, kabla ya maangamizi alishuka katika mwili na kwenda kuhakiki mwenyewe kama kweli yaliyomfikia juu ndio hayo yanayoendelea chini..
Mwanzo 18:20 “BWANA akasema, Kwa kuwa kilio cha Sodoma na Gomora kimezidi, na dhambi zao zimeongezeka sana,
21 basi, nitashuka sasa nione kama wanayotenda ni kiasi cha kilio kilichonijia; na kama sivyo, nitajua”.
Na sehemu nyingine nyingi ni hivyo hivyo. Utaona Mungu anajishusha na kuonesha tabia kama za mwanadamu, anajifanya dhaifu.. Ukitafakari sana unaweza kuona ni kama jambo lisilokuwa na maana, ni kama upumbavu hivi, lakini biblia inasema…
1 Wakorintho 1:25 “…. upumbavu wa Mungu una hekima zaidi ya wanadamu, na udhaifu wa Mungu una nguvu zaidi ya wanadamu”
Mungu amejifanya kama mdhaifu kwetu, kwa faida yetu sisi na si yake.
Hebu tafakari leo hii Mungu asingejishusha na kuuvaa mwili unaiotwa Yesu, leo hii tungekuwaje?, tungemwabuduje?, tungemwelewaje, Tungepata wapi nguvu ya kumtumikia?.
Tungesema Mungu hajui maumivu yetu, hajui shida zetu, hajui mzigo aliotutwika, hajui tabu tunazozipitia, yeye ni diktekta.
Lakini yeye Mungu mwenyewe naye alijishusha na kuwa mwanadamu, na yeye akapitia umaskini, na yeye anakipitia kujifunza, na yeye akapitia kutukanwa, na yeye akapitia kudhihakiwa na kukataliwa na kuumizwa na hata kifo ili atupe tumaini sisi.
Ili pale anaposema kwamba anayajua maumivu yetu, tufahamu kuwa ni kweli anayajua, anaposema anaujua umaskini wetu tujue ni kweli anamaanisha kuujua kwasababu na yeye aliupitia, anaposema anazijua tabu zetu, iwe kweli kwasababu naye pia alizipitia alipokuwa duniani.
Anaposema atatufufua tujue ni kweli kwasababu naye pia alikufa na kuona kifo hakimstahili mtu yeyote wa Mungu.
Hivyo udhaifu wake ni faida kubwa sana kwetu, una nguvu kuliko hekima zetu, Hekima zetu zingesema Mungu hawezi kujishusha kama mwanadamu.
Wafilipi 2:4 “Kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, bali kila mtu aangalie mambo ya wengine.
5 Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu;
6 ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho;
7 bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu;
8 tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba”.
Ni nini tunachoweza kujifunza kwa Bwana?
Kama Mungu alivyo mnyenyekevu kwa faida yetu sisi, kadhalika na sisi hatuna budi kuwa wanyenyekevu kwa faida ya wengine.
Hapo mstari wa 5 maandiko yanasema “Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu”.
Umeona?..Nia ya Kristo ni kujishusha kwa faida yetu, na sisi hatuna budi kuwa hivyo hivyo..
1 Petro 5:5 “…Naam, ninyi nyote jifungeni unyenyekevu, mpate kuhudumiana; kwa sababu Mungu huwapinga wenye kiburi, lakini huwapa wanyenyekevu neema”.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Mada Nyinginezo:
Atamaniye faida huifadhaisha nyumba yake mwenyewe; Bali achukiaye zawadi ataishi.
JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 1)
SWALI: Naomba kufahamu Bibliainaposema “Wewe uchukiaye sanamu, wateka mahekalu?” inamaana gani? Kuteka mahekalu ndio kukoje?
Warumi 2:21 “basi wewe umfundishaye mwingine, je! Hujifundishi mwenyewe? Wewe uhubiriye kwamba mtu asiibe, waiba mwenyewe?
22 Wewe usemaye kwamba mtu asizini, wazini mwenyewe? Wewe uchukiaye sanamu, wateka mahekalu?
JIBU: Maneno hayo aliyasema mtume Paulo kwa uweza wa Roho Mtakatifu, lakini hakutoa maelezo marefu, ni kwa namna gani wayahudi walikuwa wanateka mahekalu.
Lakini kulingana na maneno yake, ni kuwa kulikuwa ni desturi mbaya kwa baadhi ya wayahudi waliokuwa wanaishi kwenye mataifa ya wapagani, ya kuvamia mahekalu yao, kisha kuiba miungu yao, ambayo haswaa ilikuwa inatengenezwa kwa vito vya thamani kubwa kama vile fedha, au dhahabu.
Hivyo wenyewe walikuwa wanaviiba na kwenda kuviuza kama vilivyo , au wanaviyeyusha na kuviuza kama VITO kinyume chake,. Jambo ambalo si tu Mungu alilipinga, bali pia lilikuwa ni kinyume na sheria za watu wa mataifa..
Jambo kama hilo utaliona likitajwa tena katika ile Habari ya Paulo, alipokuwa kule Efeso, wale watu walipoleta vurugu kwasababu ya Paulo kuhubiri habari ambazo zinakinzana na ibada za miungu yao. Utaona pale walipopeleka mashitaka, wale waamuzi hawakuona kosa lolote juu ya akina Paulo,..Na moja ya makosa ambayo walitazamia kuyaona kwa mitume, ni hilo la kuiba vitu vya mahekalu yao.
Matendo 19:36 “Basi kwa kuwa mambo haya hayawezi kukanushwa, imewapasa kutulia; msifanye neno la haraka haraka.
37 Kwa maana mmewaleta watu hawa, wasioiba vitu vya hekalu wala kumtukana mungu mke wetu”.
Sasa tukirudi katika swali, kwanini Mtume Paulo aliposema “Wewe uchukiaye sanamu, wateka mahekalu?”, Alimaanisha kuwa Ikiwa umeamua kutojihusisha na ibada za sanamu, iweje basi uibe vitu vyao na kuvifanyia biashara?.. Je! Kuna tofauti yoyote na wale wanaovifanyia ibada?
Mungu alishakataza tabia kama hiyo katika kitabu cha Kumbukumbu la Torati, soma;
Kumbukumbu 7:25 “Sanamu za kuchonga za miungu yao mtaziteketeza kwa moto; usitamani fedha wala dhahabu iliyo juu yao, wala usiitwae iwe yako usije ukanaswa nayo; kwa maana ni machukizo kwa Bwana, Mungu wako”;
Hii inatufundisha nini?
Tukikataa dhambi Fulani basi tusiwe wanafki, kuitenda katika maumbile mengine..Kwamfano, tukisema hatunywi pombe, hatupaswi kwenda kuiba/kuchukua chupa za bia na kwenda kuziuza..Ikiwa hatuvuti sigara, hatupaswi pia kwenda kununua HISA za sigara, katika masoko ya fedha, kisa tu zina faida kubwa. Ikiwa hatuzini, hatupaswi pia kufanya biashara za guesthouse kwa wazinzi.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Mada Nyinginezo:
Bwana aliposema kuwa yeye ni “Mungu wa miungu” alikuwa na maana gani?..je! yeye ni Mungu wa sanamu?
Nini maana ya huu mstari.“Haiwezekani kuwafanya upya tena hata wakatubu” (Waebrania 6:6)
Tusome,
Waebrania 6:4 “Kwa maana hao waliokwisha kupewa nuru, na kukionja kipawa cha mbinguni, na kufanywa washirika wa Roho Mtakatifu,
5 na kulionja neno zuri la Mungu, na nguvu za zamani zijazo,
6 wakaanguka baada ya hayo, haiwezekani kuwafanya upya tena hata wakatubu; kwa kuwa wamsulibisha Mwana wa Mungu mara ya pili kwa nafsi zao, na kumfedhehi kwa dhahiri”.
Kipengele cha muhimu cha kuzingatia hapo ni hicho.. “Hata wakatubu”.
Maana ya andiko hilo kwa lugha rahisi ni kwamba “watu waliopewa Nuru (Maana yake walioipokea Neema ya Wokovu) na kufanywa washirika wa Roho Mtakatifu, kama ikitokea wakaiacha Imani, kwa makusudi, na kurudia tena mambo machafu ya ulimwengu haitawezekana kuwafanya tena WATUBU”.
Sio kwamba wataomba msamaha na Mungu hatawasamehe, hapana!…bali haitawezekana tena kuwa na huo moyo wa kutubu!..Kwasababu nguvu ya kutubu inaletwa na Roho Mtakatifu, hakuna mtu yeyote amewahi kutubu na kumgeuka kwa nguvu zake.
Yohana 6:44 “Hakuna mtu awezaye kuja kwangu, asipovutwa na Baba aliyenipeleka; nami nitamfufua siku ya mwisho”.
Na pia maandiko yanazidi kusema..
Yohana 15:16 “Si ninyi mlionichagua mimi, bali ni mimi niliyewachagua ninyi; nami nikawaweka mwende mkazae matunda…”
Maana yake ni kwamba, tunatubu kwasababu ni Mungu katuwekea moyo wa toba, lakini kama tumemfedhehesha Roho Mtakatifu anayetupa moyo wa toba, na akaondoka kwetu?..Je! Tutafanyaje ili tutubu?..tutabaki tu kuendelea na maisha ya dhambi.
Hiyo ni tahadhari kwetu tuliomwamini Bwana Yesu na kusimama katika Imani, na kuvionja vipawa vya Roho, na kuona kwamba Bwana ni mwema ni lazima tuchukue tahadhari, tuangalie tusiurudie ulimwengu na kuishi tena maisha ya dhambi kama zamani.
1 Wakorintho 10:12 “Kwa hiyo anayejidhania kuwa amesimama na aangalie asianguke”.
Mtume Petro ameliweka tena hilo vizuri kwa kusema.
2 Petro 2:20 “Kwa maana wale waliokwisha kuyakimbia machafu ya dunia kwa kumjua Bwana na Mwokozi Yesu Kristo, kama wakinaswa tena na kushindwa, hali yao ya mwisho imekuwa mbaya kuliko ile ya kwanza.
21 Maana ingekuwa heri kwao kama wasingaliijua njia ya haki, kuliko kuijua, kisha kuiacha ile amri takatifu waliyopewa
22 Lakini imetukia kwao sawasawa na ile mithali ya kweli, Mbwa ameyarudia matapiko yake mwenyewe, na nguruwe aliyeoshwa amerudi kugaa-gaa matopeni.”.
Pengine wewe unayesoma ujumbe huu ulikuwa umeshaanza kurudi nyuma, ingawa ulishavionja vipawa vya Mungu, Na sasa umesikia huu ujumbe na umekuogopesha na kukushtua.
Hiyo hofu iliyoingia ndani yako ni kuonesha kuwa bado Neema haijaondoka juu yako, lakini ipo mbioni kuondoka kwako kama hautageuza njia zako (Hiyo ni kulingana na maandiko).
Siku itakapoondoka hutashtushwa tena na habari kama hizi, wala hutamwona tena Yesu ni wa maana katika maisha yako, utaishia kuwa mtu wa kudhihaki na kutokujali, Toba itakuwa mbali sana nawe.
Lakini sasa bado neema ipo nawe, ndio maana sasa hivi una hofu usikiapo habari za kiMungu.
Sasa Nini cha kufanya?
Ule ulevi ambao tayari ulikuwa umeuacha usiurudie tena, ule uzinzi, uasherati, uuaji, wizi n.k ambao ulikuwa umeshauacha, usiufanye tena, kwasababu kuna hatari kubwa kuyarudia mambo tuliyokuwa tumeyaacha.
Bwana atubariki.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Mada Nyinginezo:
Ni kwa namna gani Bwana amekuja kuwafanya wanaoona wawe vipofu?
Maandiko yanasema kila jambo lina majira yake..
Mhubiri 3:1 “Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu”.
Maana yake ni kwamba kuna mambo ambayo unaweza kuyatamani yatokee lakini kama si majira yake hayawezi kutokea.
Kama muembe haujafika majira yake ya kuzaa maembe, haijalishi utaumwagia maji kiasi gani, au utauwekea mbolea kiasi gani, kamwe hautazaa..
Kwanini?
Kwasaababu sio msimu wa maembe, sio majira yake ya kuzaa..Lakini utakapofika wakati wake hata usipomwagiwa maji wala kuwekewa mbolea bado utazaa tu!!.
Kadhalika pia katika mambo ya rohoni, kuna vitu vinavyopatikana kwa msimu tu!. Sio kila wakati vipo, Na moja wapo ya hivyo ni NEEMA YA WOKOVU.
Tofauti na inavyofikiriwa na wengi kuwa Neema ya wokovu ni ya milele na ya wakati wote!.. Lakini kiuhalisia! Sio ya Milele, ni ya kupindi fulani tu!.
Kabla ya Bwana Yesu kuja duniani, neema hii ilikuwa haipatikani, hakukuwa na kitu kinaitwa msamaha wa dhambi, (Dhambi zote zilikuwa zinafunikwa tu).
Daudi, Musa, Eliya, na manabii wengine wote hawajawahi kuondolewa dhambi zao, badala yake zilikuwa zinafunikwa tu!, Na kila mwaka kunakuwa na kumbukumbu la dhambi.
Na hiyo si kwasababu walikuwa hawaombi sana, au hawakuwa na bidii..la! Walikuwa na bidii kuliko hata sisi (Maandiko yanasema Eliya alikuwa ni mtu wa kuomba sana kwa bidii, Yakobo 5:17).
Sasa kama ni hivyo kwanini, Hawakupewa hii Neema?.
Jibu ni kwasababu haukuwa Wakati wa Neema kuachiliwa duniani, haukuwa msimu wa Neema ya Mungu kudhihirika duniani, haijalishi wangeomba kiasi gani, bado hii Neema tuliyonayo sisi wasingeipata, kwasababu haukuwa wakati uliokubalika.
Lakini baada ya Bwana kuja duniani, ndipo majira mapya yakaanza.. Ukawa ni wakati uliokubalika wa Neema ya Mungu kumwagwa duniani.
Luka 4:18 “Roho wa Bwana yu juu yangu, Kwa maana amenitia mafuta kuwahubiri maskini habari njema.
Amenituma kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao, Na vipofu kupata kuona tena, Kuwaacha huru waliosetwa,
19 Na kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa”.
Hapo mstari wa 19, anasema “Kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa”.
Hajaishia kusema tu “Mwaka wa Bwana”..bali pia “uliokubaliwa”.
Maana upo wakati uliokubalika na wakati ambao sio wa kukubalika.
Sasa tukishayajua hayo tunapaswa tufanye nini?
Biblia imetupa ushauri..
2 Wakorintho 6:1 “Nasi tukitenda kazi pamoja naye twawasihi msiipokee neema ya Mungu bure.
2 (Kwa maana asema,Wakati uliokubalika nalikusikia,Siku ya wokovu nalikusaidia; tazama, wakati uliokubalika ndio sasa; tazama, siku ya wokovu ndiyo sasa.)
Hapo anasema “wakati uliokubalika nalikusikia”..na “siku ya Wokovu nalikusaidia”
Kwa lugha rahisi ni kwamba “msimu wa neema nitakusikia” “Na msimu wa kuokolewa nitakusaidia”. Maana yake msimu tofauti na huo hakuna wokovu. Kama vile misimu ya matunda ilivyo.
Ndugu hii Neema ipo ukingoni sana kuisha, na itaisha siku ile Unyakuo utakapotokea duniani, baada ya hapo hata ulieje, hakuna wokovu kwasababu sio saa ya wokovu, siku hiyo hata ufungeje kwa maombi na dua na sala hutasikiwa kwasababu sio wakati uliokubalika.
Je umeichukuliaje hii Neema leo?
Manabii wa zamani walitamani kukiona hichi kipindi tulichopo lakini hawakukiona.
Huu ndio wakati wa kusikiwa maombi yetu na sala zetu na Mungu, wakati unakuja mbingu zitafungwa.
Je umeingia ndani ya Neema leo?
Unaingiaje ndani ya neema?Unaingia kwa kumkiri Yesu na kutubu dhambi zako zote na kubatizwa kwa Jina la Yesu.
Kanuni rahisi tu hiyo, inakusogeza karibu sana na Mungu kwa viwango vingine.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Mada Nyinginezo: