Category Archive Home

NAO WATAKAOUAWA NA BWANA WATAKUWA WENGI.

Isaya 66:15 “Maana Bwana atakuja na moto, na magari yake ya vita kama upepo wa kisulisuli; ili atoe malipo ya ghadhabu yake kwa moto uwakao, na maonyo yake kwa miali ya moto.

16 Kwa maana Bwana atateta na wote wenye mwili, kwa moto na kwa upanga wake; nao watakaouawa na Bwana watakuwa wengi’.

Bwana Yesu atakaporudi mara ya pili, yaani siku ile mbingu zitakapofunguka na kila jicho kumwona hatarudi tena kwa upole kama alivyokuja hapo mwanzo, biblia inatuambia atakuja na jina jipya..Siku hiyo hataitwa tena YESU, Jina linalomaanisha mwokozi, hapana kwasababu hatakuja tena kuokoa, bali atakuja na jina jipya ambalo kwasasa bado halijafunuliwa..

Jina hilo litakuwa ni la kifalme, la kimamlaka, lenye uweza na ukuu mwingi sana..Watu watakamwona siku hiyo duniani hatawaamini kuwa huyu ndiye Yule tuliyekuwa tunamsikia habari zake, akihubiriwa na watu dhaifu…Kwasababu hatakuwa vile tena..

Siku hiyo wale watakaomwona, hakuna atakayesaliwa na nguvu hata kidogo, kwasababu wataingiwa na hofu kubwa, wataomboleza kusivyokuwa kwa kawaida, na ndio maana tunapaswa tusiichezee hii neema kabisa, kwasababu haitakuwa hivi siku zote.

Mtu mmoja nilikuwa ninamweleza habari za hukumu ya mwisho, na jinsi watu waovu watakavyoangamizwa, akaniambia ninamhukumu…Nikamuuliza nimekuhukumu wapi?..Akanipa lile andiko la Yule mwanamke aliyefumaniwa katika uzinzi, ambaye Yesu aliwaambia wale watu waliomleta kwake, kuwa asiyekuwa na dhambi awe wa kwanza kumtupia Yule mawe…Nikamwambia ni kweli mimi sitakutupia mawe lakini Kristo siku ile atakutupia mawe wewe..na utakufa, kama usipotubu sasa.

Najua unaweza kuuliza ni wapi Kristo anaua..

Soma hapa..

Ufunuo 2:22 “Tazama, nitamtupa juu ya kitanda, na hao wazinio pamoja naye, wapate dhiki kubwa wasipotubia matendo yake;

23 NAMI NITAWAUA WATOTO WAKE KWA MAUTI. Na makanisa yote watajua ya kuwa mimi ndiye achunguzaye viuno na mioyo. Nami nitampa kila mmoja wenu kwa kadiri ya matendo yake”.

Hayo ni maneno yaliyotoka katika kinywa cha Kristo mwenyewe!. ATAWAUA WAOVU..Na kama vile yale maandiko pale juu yanavyotuambia..watakaouliwa hawatakuwa wachache bali ni wengi sana..

Ndugu, kikombe cha ghadhabu ya Mungu kinakaribia kujaa, (kama hujui vizuri kasome kitabu cha Ufunuo 16) Unyakuo ukishapita yatakayofuata si mambo mazuri!, ni mambo mabaya ambayo laiti ungeonyeshwa leo, usingetamana hata adui yako awepo hicho kipindi, Kwasababu siku atakaposhuka, jua litazimwa lote, na nyota na mwezi vitaondoshwa, duniani kutakuwa giza tororo, kutakuwa na tetemeko kubwa ambalo halijawahi kutokea tangu dunia iumbwe, na baada ya yeye kushuka wale ambao watakuwa bado hai atawaua mara moja..Hakuna huruma!.

Ufunuo 19:11 “Kisha nikaziona mbingu zimefunuka, na tazama, farasi mweupe, na yeye aliyempanda, aitwaye Mwaminifu na Wa-kweli, naye kwa haki ahukumu na kufanya vita.

12 Na macho yake yalikuwa kama mwali wa moto, na juu ya kichwa chake vilemba vingi; naye ana jina lililoandikwa, asilolijua mtu ila yeye mwenyewe.

13 Naye amevikwa vazi lililochovywa katika damu, na jina lake aitwa, Neno la Mungu.

14 Na majeshi yaliyo mbinguni wakamfuata, wamepanda farasi weupe na kuvikwa kitani nzuri, nyeupe, safi.

15 NA UPANGA MKALI HUTOKA KINYWANI MWAKE ILI AWAPIGE MATAIFA KWA HUO. Naye atawachunga kwa fimbo ya chuma, naye anakanyaga shinikizo la mvinyo ya ghadhabu ya hasira ya Mungu Mwenyezi.

16 Naye ana jina limeandikwa katika vazi lake na paja lake, MFALME WA WAFALME, NA Bwana WA Mabwana………..

20 Yule mnyama akakamatwa, na yule nabii wa uongo pamoja naye, yeye aliyezifanya hizo ishara mbele yake, ambazo kwa hizo aliwadanganya watu wale walioipokea ile chapa ya huyo mnyama, nao walioisujudia sanamu yake; hao wawili wakatupwa wangali hai katika lile ziwa la moto liwakalo kwa kiberiti;

21 na wale waliosalia waliuawa kwa upanga wake yeye aliyeketi juu ya yule farasi, upanga utokao katika kinywa chake. Na ndege wote wakashiba kwa nyama zao.”.

Bado tu unayapenda maisha ya dhambi? Bado tu unazidi kutazama pornografia, unafanya uasherati, unakula rushwa, unakwenda Disko, unaiba, unatembea na waume/wake za watu?…

Usilisahau hili Neno.. “WATAKAUAWA NA BWANA WATAKUWA NI WENGI”

Ni heri tumkimbilie yeye maadamu bado anaokoa sasa, Kabla Bwana hajaondoka Mtume Yohana alikuwa anaegemea kifuani kwake alikuwa anadeka kama mtoto karibu na Bwana, lakini Yohana huyo huyo anamwona Bwana Yesu Yule Yule kwenye maono Patmo kama miale ya moto, anatisha sana mpaka anaanguka chini ya miguu yake kwa hofu…Hivyo wakati wa neema ukiisha, Kristo hatakuwa Yule tunayemjua sasa…hivyo Bwana atusaidie neema hii tuithamini sana.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312.

Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

KUOTA UNATEMBEA JUU YA MAJI.

SHETANI ANAITHAMINI HATA MAITI YAKO.

MALEZI YA MTOTO MCHANGA.

Biblia inamaanisha nini inaposema “Tusitweze unabii”?

NI WAKATI WA KUJIPIMA, WEWE KAMA MTUMISHI WA MUNGU!

Rudi Nyumbani:

Print this post

 Je! Ni sahihi kutumia maji ya upako,katika kufanya maombezi?

SWALI: Je! Ni sahihi kutumia maji ya upako, mafuta ya upako au chumvi katika kufanya maombezi?


JIBU: Kwanza ni muhimu kufahamu kuwa kinachomponya mtu ni damu ya Yesu Pekee. Na ndani ya damu ya Yesu ndio kuna Jina la Yesu…Hivyo jina la Yesu linapotajwa ni tangazo maalumu la damu ya Yesu katika utendaji kazi wake, hivyo kila ugonjwa au tatizo kwa jina la Yesu linaondoka na kupotea kabisa!.

Kwahiyo haipaswi kwa vyovyote vile kufikiri au kuamini kwamba kitu kingine zaidi ya damu ya Yesu kinaweza kumponya mtu au kinaweza kuondoa matatizo ya mtu au kumbariki. Kuamini hivyo hakuna tofauti na kuabudu sanamu.

Sasa pamoja na hayo, Mungu ameruhusu uponyaji wa damu ya Yesu wakati mwingine ufuatane na maagizo Fulani…Kwamfano daktari anaweza kutoa dawa kwa mgonjwa wa ngozi na kutolea maagizo kwamba akameze vidonge hivi na maji ya kutosha..au akampa vidonge vingine na kumwambia akavitie kwenye maji kisha aogee, afanye hivyo mara tatu kwa siku tatu na huo ugonjwa huo wa ngozi utamwisha..Au anaweza asimpe kidonge chochote na badala yake akamchoma sindano tu na bado ukapona vile vile…Ni kwajinsi tu yeye atakavyopenda kuchagua njia iliyobora.

Na Roho Mtakatifu ni hivyo hivyo…katika suala la kumponya mtu, mara nyingine anaweza kuambatanisha na maagizo Fulani…aidha mtu atumie mafuta, au udongo kwa jinsi Roho Mtakatifu atakavyopenda…kama alivyofanya Bwana katika Yohana 9:6 (alimwongoza atumie tope la mate yake), au anaweza akampa mtu maelekezo atumie unga kama Elisha alivyofanya katika 2Wafalme 4:41, au chumvi kama alivyofanya Elisha katika 2Wafalme 2:21 au kutumia leso kama alivyofanya Paulo katika Matendo 19:11-12..au chochote kile…Lakini ni kulingana na uongozo wa Roho Mtakatifu…Na sio kama mtindo!..kama inavyofanyika leo na wengi wanaofahamika kama watumishi wa Mungu.

Leo hii kila tatizo linatatuliwa na chumvi wanazoziita chumvi za upako, au mafuta …hata mtu akiugua tu, suluhisho ni mafuta ya upako! Au maji ya upako!..kila kitu ni mafuta ya Upako na ni kitendo endelevu na kinachojirudia kila siku…Sasa hilo sio agizo la Roho Mtakatifu…kwasababu Roho Mtakatifu hana mtindo Fulani/staili Fulani ya kumponya mtu.

Kwasababu hata Bwana Yesu sio kila mahali watu walipomjia mwenye matatizo Fulani alikuwa anatema mate chini na kutengeneza tope na kuwapaka na kufunguliwa shida zao!…utaona alifanya hivyo mara moja tu! Na tena kuna jambo alikuwa anafundisha, Na hakuna sehemu nyingine yoyote alirudia kufanya hivyo, kuonyesha kuwa nyakati zote alikuwa anasubiria maagizo ya Roho Mtakatifu, na hakufanya agizo Fulani la Roho Mtakatifu kuwa kama mtindo.

Na sio yeye tu! Hata Elisha hakuwa na staili/mtindo wake maalumu, wala hata Mtume Paulo ambaye nguo zake na Leso yake kuna wakati ilitumika hata kuondoa mapepo(Matendo 19:12)…utaona kuwa haikuwa hivyo kila mara, na wala Paulo hakugeuza kuwa kama mtindo..kwamba kila aliyekutana naye alimtupia leso ili afunguliwe!..hutaona akizituma nguo zake korintho au Galatia watu wakafunguliwe wala hakuwahi kuhubiri hayo mambo… sehemu kubwa sana alikuwa anatumia jina la Yesu…na alikuwa anamuhubiri Kristo na si mavazi yake wala leso zake. Na mitume wengine wote wa Bwana Yesu ni hivyo hivyo…tunamsoma Mtume Petro kuna wakati hadi kivuli chake kilikuwa kikimpitia mtu mwenye ugonjwa, Yule mgonjwa anafunguliwa! (kasome Matendo 5:15). Lakini hutaona mahali popote Petro akiitumia hiyo kama ndio staili yake/mtindo wa kuwafanya watu wafunguliwe…bali utaona mara karibia zote alikuwa anatumia Jina la Yesu tu!..

Matendo 3:3 “Mtu huyu akiwaona Petro na Yohana wakiingia hekaluni aliomba apewe sadaka.

4 Na Petro, akimkazia macho, pamoja na Yohana, akasema, Tutazame sisi.

5 Akawaangalia, akitaraji kupata kitu kwao.

6 Lakini Petro akasema, Mimi sina fedha, wala dhahabu, lakini nilicho nacho ndicho nikupacho. KWA JINA LA YESU KRISTO WA NAZARETI, SIMAMA UENDE.

7 Akamshika mkono wa kuume, akamwinua, mara nyayo zake na vifundo vya miguu yake vikatiwa nguvu.

8 Akaondoka upesi akasimama, akaanza kwenda; akaingia ndani ya hekalu pamoja nao, akienda, akiruka-ruka, na kumsifu Mungu”.

Hapo Petro hakutumia “kivuli” chake!…Bali jina kuu la YESU KRISTO!.

Sasa utauliza mbona kuna watu wanayatumia maji ya upako, au mafuta ya upako kama mtindo wao na wanafunguliwa?

Wengi wanaofunguliwa ni wale ambao ni wachanga kiimani, ambao ndio kwanza wamemjua Kristo, au wameingia kwenye imani ya kikristo, Hivyo Bwana anaruhusu wapokee miujiza yao kwa njia yoyote ile..ili wazidi kumsogelea Mungu katika hivyo vipindi vya awali, lakini baada ya kipindi Fulani kupita wakaujua ukweli, au kusikia injili kwa muda mrefu na kushupaza shingo, zinabadilika kwao kuwa ibada za sanamu, na havitawapii chochote zaidi ya kuzidi kuwaweka mbali na Mungu, na hata wakati mwingine kuingiliwa na mapepo, na kupoteza hata vile walivyo navyo kwasababu ni ibada za sanamu…wanatanga huko na huko kutafuta na kununua maji ya upako, chumvi ya upako…Na kwasababu wengi wao hawapendi kuzidi kumjua Mungu wanadanganyika!

Na manabii wengi wa uongo wamezuka sasa, katika siku hizi za mwisho kama ilivyotabiriwa…Mungu ameachilia nguvu ya upotevu kwa wale wote wanaoukataa ukweli…Na nguvu hiyo ya upotevu kaiweka ndani ya manabii wa uongo…Na lengo la nguvu hiyo ni ili watu wote wanaoukataa ukweli wazidi kudanganyika!…ili tofauti ya magugu na ngano ionekane kwaajili ya mavuno.(Mavuno hayawezi kuja bila magugu na ngano kujitenga kisawasawa!..)

2Wathesalonike 2:10 “na katika madanganyo yote ya udhalimu kwa hao wanaopotea; kwa sababu hawakukubali kuipenda ile kweli, wapate kuokolewa.

11 Kwa hiyo Mungu AWALETEA NGUVU YA UPOTEVU, wauamini uongo;

12 ili wahukumiwe wote ambao hawakuiamini kweli, bali walikuwa wakijifurahisha katika udhalimu”.

Hivyo ni wakati wa kuwa makini sana na kuwa macho, na kujihadhari na roho zidanganyazo!…Kama hujapewa maagizo yoyote na Roho Mtakatifu basi usikurupuke kutumia maji,chumvi, udongo, au chochote kile ni hatari sana kwa roho yako!…Tumia Jina la Yesu tu pekee linatosha…

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 693036618/ 0789001312.

Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

WAKATI ULIOKUBALIKA NDIO SASA.

MAMBO MENGINE HAYATOKI ISIPOKUWA KWA KUFUNGA.

JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?

BIRIKA LA SILOAMU.

Nini tofauti kati ya Amri, sheria na Hukumu?

Mtu astahiliye hofu ni yupi?

Rudi Nyumbani:

Print this post

DAKIKA MOJA TU, INAKUFANYA UMWAMINI SHETANI?

Luka 4:5 “ Akampandisha juu, akamwonyesha milki zote za ulimwengu KWA DAKIKA MOJA.

6 Ibilisi akamwambia, Nitakupa wewe enzi hii yote, na fahari yake, kwa kuwa imo mikononi mwangu, nami humpa ye yote kama nipendavyo”.

Hilo ni moja ya jaribu shetani alilomletea Bwana kule jangwani..

Lakini jiulize ni kwa nini iwe kwa dakika moja?, kwanini amwonyeshe ndani ya muda mfupi kiasi hicho, kwani alikuwa na haraka gani? Chukulia mfano mtu aje na kukwambia nataka kukuonyesha plani ya mji wetu na shughuli zote zinazofanyika ndani yake kwenye CD..Ni wazi kuwa hawezi kumaliza kukuonyesha kila kitu kwa dakika moja, itachukua dakika nyingi sana kama sio masaa, lakini tunaona hapa kwa ibilisi iliwezekana..

Alifanikiwa kumuonyesha Bwana milki zote za ulimwenguni kwa kitendo cha dakika moja..Ni kwanini afanye hivyo? Sio kwamba alikuwa hawezi kumwonyesha milki zote kidogo kidogo, huo uwezo alikuwa nao lakini sikuzote ni desturi yake, kutompa nafasi mtu ya kutafakari vizuri kazi zake..

Hakutaka Bwana atafakari nyuma ya milki zile kuna nini? Bali alikuwa anamwonyesha haraka haraka, ule upande mzuri tu wa fahari hizo, ili kusudi kwamba Bwana achukue maamuzi ya haraka haraka ya kumsujudia bila hata kutafakari vema, ili awe amemshinda. Hakumwonyesha Bwana wagonjwa waliolala hoi mahospitalini waliokuwa wanahitaji msaada, hakumwonyesha watu waliofungwa kwa kuonewa, au wanaotumikishwa na nguvu za giza, hakumwonyesha maskini wa roho, wala mayatima ambao wazazi wao waliuawa na huyo huyo shetani, hakumwonyesha uchawi uliokithiri katika hiyo miji n.k ..yeye alimwonyesha tu mali, na fahari..Lakini hakumweza Bwana kwasababu pale alikutana na Mkuu wa Uzima mwenyewe ambaye anajua vyema kuzipambanua roho!.

Hii ni mbinu ambayo shetani anaitumia hata sasa kuwaangusha wengi katika dhambi..kwamfano akitaka leo kummaliza mtu na dhambi ya uasherati, mara moja atamletea katika mawazo yake uzuri wa kufanya lile jambo..Lakini hatamruhusu kutafakari ni nini kipo nyuma yake, na yeye bila kutafakari vyema, moja kwa moja ataingia humo, kuitenda, hajui kuwa nyuma yake kuna hata hatari hata ya kifo hata kupata ukimwi, nyuma yake kuna mimba zisizotarajiwa, nyuma yake kuna kupata aibu, na kibaya Zaidi kuliko vyote ni kuwa nyuma yake kuna laana itokayo kwa Mungu..

Au mwingine shetani anamletea mawazo ya kuwa Tajiri kwa dakika moja, atamwambia njoo utapata utajiri wa haraka, bila kufikiri vema kuwa akienda kule, atakutana na waganga wa kienyeji waliolaaniwa, hajui kuwa nyuma yake kuna kutoa kafara, kuna uchawi, kuna kutumikishwa, na mwisho wake ni kifo, na baada ya hapo ni ziwa la moto..au anakutana na kazi ya wizi au utapeli, pasipo kutafakari nyuma yake kuna kifo, au kifungo, mtu anaingia huko…..Sasa yeye kwasababu kaonyeshwa pesa tu za haraka haraka ambazo hazihitaji kuzihangaikia sana, anaingia humo na kupotelea humo..

Mwingine, anakutana tu na kazi Fulani ya ghafla, halafu baada ya hapo anashurutishwa akaifanye, lakini yeye badala achukue muda kumwomba Mungu na kuichunguza kazi ile, moja kwa moja atakwenda kuingia nayo mkataba na kuifanya kisa tu imemuahidia mshahara mzuri, hajui kuwa kazi ile ililetwa na shetani, ili kuharibu utaratibu wake aliokuwa nao wa kusali, wa kumtumikia Mungu, na kibaya Zaidi anakuja kugundua kazi yenyewe inafanya shughuli za kipepo kama uuzaji pombe, au bidhaa haramu na mambo mengine ya ajabu.

Mwingine atakuwa anatembea madukani, ghafla anakutana na simu ya mtu imejiegesha mahali ambapo haionekani, na saa hiyo hiyo shetani anaanza kumletea mawazo ya dakika moja ya wizi, kumwonyesha faida za simu ile akienda kuuza atapata laki kadhaa, ndani ya dakika chache baadaye..kisha atanunua hiki na kile.. Na yeye bila kuruhusu fikra zake kuwaza mbali anakwenda kuiiba, bila kujua nyuma yake, kuna kupigwa na watu, kuna kuchomwa moto, kuna kufungwa, na kibaya Zaidi kuna laana ya Mungu, kwamba hata kama hatakufa pale siku ya mwisho atakwenda motoni..

Mithali 13:11 “Mali iliyopatikana kwa haraka itapunguka; Bali yeye achumaye kidogo kidogo atazidishiwa”.

Mwingine kamwona mwanamke na hapo hapo kamtamani, bila kupata muda mrefu wa kumchunguza tabia zake, yeye wazo la dakika moja tu, anaingia humo, na ndio hapo baadaye anakuja kugundua alikuwa ni mke wa mtu aliyemwacha mume wake, au kahaba tu, na ghafla matatizo ndani ya nyumba yanaanza. Vivyo hivyo na mwanamke naye, shetani atampitishia dakika moja mwanaume mwenye fedha, na yeye bila kujitafakarisha anaingia moja kwa moja, kumbe ndio kaenda kuharibu Maisha yake moja kwa moja.

Na sehemu nyingine nyingi za Maisha ni vivyo hivyo..Shetani huwa anawaletea watu mawazo ya chap-chap ..Ya dakika moja tu yanayovutia lakini nyuma yake yana miaka mingi ya majuto.

Ndugu, tusiwe wateja wa shetani..biblia inasema..

1Yohana 2:15 “Msiipende dunia, wala mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake.

16 Maana kila kilichomo duniani, yaani, TAMAA YA MWILI, NA TAMAA YA MACHO, na kiburi cha uzima, havitokani na Baba, bali vyatokana na dunia.

17 Na dunia inapita, pamoja na tamaa zake, bali yeye afanyaye mapenzi ya Mungu adumu hata milele”.

Zingatia hilo, ni moja kati ya majaribu makuu 3 ya ibilisi aliyoyaona yanawazomba watu wengi kwake, na ndio maana akamchagulia na Bwana, hivyo hatashindwa kutuletea na sisi (mimi na wewe), hivyo tuwe makini sana na mambo ya humu ulimwenguni

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312 / 0693036618

Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

MAJARIBU MATATU YA YESU KRISTO

MTAIFAHAMU KWELI NAYO HIYO KWELI ITAWAWEKA HURU.

Kati ya Unyakuo,dhiki kuu, utawala wa miaka 1000 kipi kinaanza

MOTO HUFA KWA KUKOSA KUNI.HATA UASHERATI NAO

NJIA SAHIHI YA KUMPATA MWENZA WA MAISHA KIBIBLIA.

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita..

Rudi Nyumbani:

Print this post

Kuungama ni nini?

SWALI: Kuungama maana yake ni nini?

JIBU: Maana ya kuungama ni “kukiri jambo kwa wazi” kukubali….Kwamfano mtu anayetubu kwa kuzikiri dhambi zake kwa wazi kwamba yeye ni mwenye dhambi mbele za Mungu, mtu huyo ni “ameungama dhambi zake”

1Yohana 1:9 “Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote”.

Mathayo 3:5 Ndipo walipomwendea Yerusalemu, na Uyahudi wote, na nchi zote za kandokando ya Yordani;

6 naye akawabatiza katika mto wa Yordani, huku wakiziungama dhambi zao”.

Kadhalika kuikiri imani mbele za watu ni “kuiungama imani”..na kuukiri uongo ni kuungama uongo!

Bwana wetu Yesu Kristo alipopelekwa mbele ya Pontio Pilato, na Pilato alipomwuliza je wewe ndiwe Kristo?..Alikiri (aliungama) wazi kuwa yeye ndiye!

Luka 23:3 “Pilato akamwuliza, akisema, Wewe ndiwe mfalme wa Wayahudi? Akajibu akamwambia, Wewe wasema”…..

Neno “wewe wasema” maana yake ni “kama ulivyosema”..Kwahiyo Kristo alikiri kwa wazi pasipo hofu mbele ya Pilato kwamba yeye ndiye Kristo!..Hivyo aliungawama Imani yake kwa wazi.

1Timotheo 6:13 “Nakuagiza mbele za Mungu anayevihifadhi hai vitu vyote, na mbele za Kristo Yesu, ALIYEYAUNGAMA MAUNGAMO MAZURI yale mbele ya Pontio Pilato,

14 kwamba uilinde amri hii pasipo mawaa, pasipo lawama, hata kufunuliwa kwake Bwana wetu Yesu Kristo”

Kadhalika na sisi kama hatujatubu mbele za Mungu…tunapaswa tuziungame dhambi zetu kwanza, (maana yake tuzikiri kwa dhati kwamba sisi ni wenye dhambi, tusipokiri na kukubali kwamba sisi ni wakosaji mbele zake kamwe hatuwezi kupata msamaha kutoka kwake!)..kisha tumwombe Mungu rehema naye atatusamehe…Na tukiishaziungaa dhambi zetu na kuipokea Imani kwa kumwamini mwanawe mpendwa Yesu Kristo tunapaswa kila siku TUUNGAME MAUNGAMO YA IMANI YETU!…maana yake tuikiri Imani ya kikristo kila mahali tuendapo, na popote pale tusimamishwapo pasipo hofu wala kujali ni nani yupo mbele yetu!..kama Bwana wetu Yesu alivyoungama..

1Timotheo 6:12 “Piga vita vile vizuri vya imani; shika uzima ule wa milele ulioitiwa, UKAUNGAMA MAUNGAMO MAZURI MBELE YA MASHAHIDI WENGI”.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312 / 0693036618.

Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

NI NANI ATAKAYETUTENGA NA UPENDO WA KRISTO?

YONA: Mlango wa 4

Je ni sahihi kumtenga mtu anapofanya dhambi kanisani?

TOFAUTI KATI YA HEKALU, SINAGOGI NA KANISA NI IPI?

Rudi Nyumbani:

Print this post

USISUBIRI MPAKA MUNGU AKUAMBIE, NDIO UFANYE!

Unajua ni kwanini Daudi alipewa jina kuu na kubwa kuliko wafalme wote na watu wote waliomtangulia katika Israeli? Ni kwasababu kuna kipindi aliwaza, Mungu amenipa vyote, amenipa ufalme, amenipa uongozi bora juu ya Israeli yote, amenipa nyumba nzuri ya kukaa, lakini mbona ni mimi tu ananifanyia wema, na mimi simfanyii chochote?. Akatazama huku na kule, akaangalia ni wapi pamepunguka, akagundua kuwa Mungu hana maskani yoyote ya kukaa, akatazama akaona lile sanduku la agano la Mungu linakaa kwenye mapazia, katika giza nene (1Wafalme 8:12) kwenye vihema vilivyochoka na kuchakaa..

Akajiwazia tu moyoni akasema hii haiwezekani, nitamjengea Mungu nyumba ya kukaa..

Lakini biblia inatuambia usiku huo huo Neno la Mungu lilimfikia Nadhani nabii wa Mungu, kwa Daudi kumwambia kwamba Mungu anasema: Je nilishawahi kusema Neno lolote kwa mwamuzi yoyote wa Israeli juu ya kujengewa mimi nyumba? Nilishawahi kumdokeza Yoshua juu ya jambo hilo? Nilishawahi kumdokeza Gideoni kuhusu kunijengea nyumba, Au Samsoni, au Ehudi au Yeftha, au Samweli juu ya jambo hilo?

Kwa namna nyingine Bwana alikuwa anamaanisha kumwambia Daudi hivi..

Sikuwahi kuwauliza chochote, ili nisionekane kama nawalazimisha, bali niliwaacha wao wenyewe waligundue hilo, lakini hakuna hata mmoja aliyelijali jambo hilo isipokuwa wewe Daudi, Sasa Basi kwa kuwa umefikiria hivyo, kunipa heshima, kunitoa katika giza nene, kwenye vihema vibovu, mimi nami nitakupa jina kuu sana, na sehemu nzuri Zaidi.

2 SAMWELI: MLANGO 7

1 Ikawa, mfalme alipokuwa akikaa katika nyumba yake, hapo Bwana alipomstarehesha, asiudhiwe na adui zake waliomzunguka pande zote,

2 mfalme akamwambia Nathani, nabii, Angalia sasa, mimi ninakaa katika nyumba ya mierezi, bali sanduku la Mungu linakaa ndani ya mapazia.

3 Nathani akamwambia mfalme, Haya, fanya yote yaliyomo moyoni mwako; maana Bwana yu pamoja nawe. 4 Ikawa usiku uo huo, neno la Bwana likamfikia Nathani kusema,

5 Enenda, ukamwambie mtumishi wangu, Daudi, Bwana asema hivi, Je! Wewe utanijengea nyumba, nikae ndani yake?

6 Kwa maana mimi sikukaa ndani ya nyumba, tangu siku ile niliyowatoa wana wa Israeli katika Misri, hata leo, lakini nimekaa katika hema na maskani.

7 Mahali mwote nilimokwenda na wana wa Israeli wote, je! Nimesema neno lo lote na mtu ye yote wa waamuzi wa Israeli, niliyemwagiza kuwalisha watu wangu Israeli, nikisema, Mbona hamkunijengea nyumba ya mierezi?

8 Basi, sasa, mwambie mtumishi wangu, Daudi, maneno haya, Bwana wa majeshi asema hivi, Nalikutwaa katika zizi la kondoo, katika kuwaandama kondoo, ili uwe mkuu juu ya watu wangu, juu ya Israeli;

9 nami nimekuwa pamoja nawe kila ulikokwenda, na kuwakatilia mbali adui zako wote mbele yako; NAMI NITAKUFANYIA JINA KUU, KAMA JINA LA WAKUU WALIOKO DUNIANI”.

Na tunaona Daudi alianza maandalizi yote ya ujenzi wa hekalu la Bwana, na mwanawe Sulemani akaja kulimalizia..

Sasa leo hii sisi ndio tunaojua vizuri ni jinsi gani Mungu amempa Daudi jina kuu kuliko wengine wote waliomtangulia.. (hata Bwana wetu Yesu katokea katika huo huo uzao wa Daudi katika mwili) Lakini hiyo yote ni kutokana na kwamba hakusubiri aambiwe ndipo afanye..

Hata leo hii, zipo kazi za Mungu nyingi sana zimepwaya, Na Mungu amekaa kimya anaangaalia, wala hasemi chochote, Ni kweli ataendelea kuwa na sisi kama Watoto wake, kama watumishi wake, atatutumia sisi kama manabii wake, mfano wa Samweli, Lakini kama hatutachunguza na kuchukua hatua ni wapi palipopunguka, tusitazamie kamwe kama Mungu siku moja atakuja kutuambia naomba unifanyie hiki au kile.

Vivyo hivyo ikiwa wewe umeokoka, na unajua kabisa ni jukumu lako kumtolea Mungu, kamwe usidhani ipo siku Mungu atakuuliza mbona hujanitolea, au mbona hujanifanyia hichi au kile….hilo jambo hawezi kufanya kabisa, wewe ndio unapaswa ulitambue hilo si yeye.

Unajua kabisa unapaswa ukaisambaze injili kwa wengine kwa karama Mungu aliyoiweka ndani yako, halafu unasubiria siku moja Mungu akutokee akwambie nenda kahubiri, hilo wazo lifute kabisa, ni rahisi kumwambia yule ambaye ndio kwanza anaingia kwenye wokovu lakini wewe ambaye umeshakaa miezi, na miaka, na huna ushuhuda wowote, unasubiri siku moja Mungu akuambie uipeleke Habari njema katika maono, hawezi kufanya, kwasababu anajua kabisa unajua jukumu lako, kwanini tena akuambie, si itakuwa kama anakulazimisha?..

Pale tunapochukua hatua ndipo hapo Mungu anatuongezea na hatua nyingine..(Usisubiri mpaka Mungu akuambie)

Hivyo siku ya leo ya tarehe hii na mwezi huu, biblia inatufundisha kuwa na jicho kama la Daudi, ili na sisi pia Bwana atupe jina lililo kuu huku na kule ng’ambo tutakapofika.

Bwana atubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312 / 0693036618.

Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

VITA VYA IMANI NI VITA ENDELEVU.

Kwanini Mungu anasema “Afanyaye malaika zake kuwa pepo”?

NA MTU MMOJA AKAVUTA UPINDE KWA KUBAHATISHA, AKAMPIGA MFALME

KUOTA MTU AMEKUFA/NDUGU AMEKUFA.

Ni kura ya aina gani waliipiga wale watu waliosafiri na Yona?

JE MUSA ALIFIA WAPI?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Mahali pa hukumu upo uovu,Na mahali pa haki upo udhalimu.

SWALI: Huu mstari una maana gani? Mhubiri 3:16-17 “Zaidi ya hayo,nikaona tena chini ya jua ya kwamba,Mahali pa hukumu upo uovu,Na mahali pa haki upo udhalimu.17 Nikasema moyoni mwangu,Mungu atawahukumu wenye haki na wasio haki, kwa kuwa kuna wakati huko kwa kila kusudi na kwa kila kazi”.


JIBU: Hizi ni hekima zilizoandikwa na mfalme Sulemani ambae alimwomba Mungu ampe hekima badala ya Mali (Jambo la kwanza na la muhimu sana ambalo na sisi pia tunapaswa tuanze kumwomba Mungu)..

Hapo katika mstari huo anasema kwa hekima ya Roho “nikaona tena chini ya jua ya kwamba,Mahali pa hukumu upo uovu,Na mahali pa haki upo udhalimu”….Zingatia hapo anaanza na neno “NIKAONA CHINI YA JUA!”..Maana yake sio mbinguni, bali ni duniani. Ikiwa na maana kuwa mbinguni mahali pa haki hapana udhalimu, vilevile Hukumu za mbinguni Mungu alipo hazina uovu,

Ayubu 34:12 “Naam, hakika, Mungu hatatenda mabaya, Wala Mwenyezi hatapotosha hukumu”.

Lakini kinyume chake hukumu za duniani (chini ya jua) ndizo zenye uovu, na haki za duniani ndio zina udhalimu…Kama Mhubiri anavyosema hapo juu.

Na hiyo ni kweli kabisa..je! huoni leo, hata mahakamani (mahali ambapo pangepaswa kutolewa hukumu ya haki)..wapo mahakimu wanaopotosha hukumu?..wanaopokea rushwa na kumnyima haki yule anayestahili haki, na kumpatia yule asiyestahili?..na wapo wengi wanaopewa kesi ambazo sio zao kwasababu tu ya rushwa..n.k

Kwahiyo ni kweli kabisa chini ya jua na si mbinguni…hukumu nyingi zinapotoshwa!..Mahali ambapo ni pa hukumu kuna uovu na mahali pa haki kuna udhalimu…mahali ambapo mtu anapaswa apate haki, ananyimwa haki yake.

Na ndio maana katika mstari wa mwisho kabisa amesema.. “Mungu atawahukumu wenye haki na wasio haki”. Maana yake ni kwamba Wale wanaosimamia haki duniani kama mahakimu watasimama katika kiti cha hukumu pia kutoa hesabu ya uhakimu wao, kadhalika na wasio haki(maana yake waovu wote) pia watasimama mbele ya kiti cha hukumu) siku ile ya mwisho, na kila mtu atahukumiwa kulingana na matendo yake.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312 / 0693036618.

Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

Maana ya ‘Usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake’

Nini maana ya mstari huu: (Mtu ambarikiye mwenzake kwa sauti kuu asubuhi na mapema; Itahesabiwa kuwa ni laana kwake.Mithali 27:14 )?

https://wingulamashahidi.org/2019/09/01/maana-ya-huu-mstari-ni-ipi-mithali-144-zizi-ni-safi-ambapo-hapana-ngombebali-nguvu-za-ngombe-zaleta-faida-nyingi/

JE KUPONYWA NI UTHIBITISHO WA MUNGU KUWA NA WEWE?

https://wingulamashahidi.org/2018/06/27/maswali-na-majibu/

BWANA AKAMWAMBIA SHETANI, BWANA NA AKUKEMEE EWE SHETANI;

Rudi Nyumbani:

Print this post

NA UPEPO WA KUSI ULIPOANZA KUVUMA KIDOGO,

Na upepo wa kusi ulipoanza kuvuma kidogo, wakidhani ya kuwa wamepata waliyoazimu.


Shalom jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe.

Si kila dalili nzuri inayoonekana mbele yetu, itatuletea mwisho mwema, Kama hatutakaa chini kutaka kutafuta mashauri ya Mungu, tuwe na uhakika kuwa kuna uwezekano mkubwa sana wa kupotea..Kama vile biblia inavyotuambia katika…

Mithali 14:12 “Iko njia ionekanayo kuwa sawa machoni pa mtu, Lakini mwisho wake ni njia za mauti”.

Tukiiangalia mfano ile safari ya Mtume Paulo kutoka Yerusalemu kwenda Rumi kama mfungwa, haikuwa safari ya kawaida, kama sio neema ya Mungu tu kuwa pamoja na Paulo basi asingenusurukia mtu yeyote kwenye ile safari waliyosafiri yeye pamoja na wafungwa wengine, pamoja na maasakari wote na manahodha wote..Lakini hiyo yote ilisababishwa na wengi wao kuyadharau mashauri ya Mungu na kuyafuata mawazo yao wenyewe na akili zao wenyewe zinavyowatuma.

Kwani walipofika kwenye kisiwa kimoja kinachoitwa bandari nzuri, walitulia pale kwa muda wakingoja hali iwe shwari kidogo kisha waanze safari tena, Lakini ghafla kukaanza kuvuma upepo mzuri sana unaovutia ujulikanao kama upepo wa Kusi , Upepo huu ukivuma basi manahodha huwa wanafurahi kwasababu ni upepo rafiki kwa kusafiria baharini, na zaidi ya yote unawafanya safari yao kuwa nyepesi Zaidi na isiyogharimu.. Lakini Mtume Paulo kwa kuonywa na Roho aliwaambia wasisafiri, kwani mbeleni alionyeshwa watakumbana na madhara makubwa ambayo sio tu ya kupoteza shehena na merikebu bali yatahatarisha pia na maisha yao… Jambo hilo Yule Akida wa askari wala hakulizingatia, kwani aliyasikiliza zaidi mashauri ya mabaharia ambao wao kila siku wapo vilindini wenye uzoefu wa mambo hayo, pengine akajisemea moyoni huyu mfungwa maskini anatueleza nini..

Lakini biblia inatuambia walipoondoka tu kwenye kisiwa kile, hawakufikia hata mbali ule upepo wa kusi uligeuka na kuwa upepo wa Tufani wa aina nyingine ujulikanao kama Eurakilo.

Matendo 27:13 “Na upepo wa kusi ulipoanza kuvuma kidogo, wakidhani ya kuwa wamepata waliyoazimu kupata, wakang’oa nanga, wakasafiri karibu na Krete pwani kwa pwani.

14 Baada ya muda mchache ukavuma upepo wa nguvu wa namna ya tufani, uitwao Eurakilo,

15 merikebu iliposhikwa, na kutoweza kushindana na upepo, tukaiacha tukachukuliwa”.

Tufani ya namna hii ikikukumba ukiwa katikati ya bahari basi kupona hapo ni jambo ambalo haliwezekani, tufani za namna hii huwa zinakwenda kuathiri mpaka makazi ya watu nchi kavu, sasa jiulize kwa wale waliokuwa baharini ilikuwaje?..Na ndio maana ukisoma pale utaona jinsi safari ile ilivyowagharimu sana maisha,baada ya merikebu kuvunjwa, Kama sio mwenye haki mmoja kuwepo kwenye ile meli asingepona mtu kabisa..

Hayo ni mambo ambayo tunapaswa tujifunze katika maisha, tunaweza tukawa tunauzoefu mwingi wa kimaisha, tunaweza tukawa na ujuzi Fulani wa mambo, lakini tusipokaa chini na kuyatafuta mapenzi ya Mungu katika maisha yetu, badala yake tukawa tunagemea akili zetu tu, ziamue kila jambo..tufahamu kuwa Eurakilo ipo mbele yetu..siku moja itatuangamiza tu.. Haijalishi hapo mwanzo zilishatusaidia mara ngapi, ipo siku tutanasika tu.

Tunaweza tukasema mbona jambo hili au shughuli hii, inauelekeo wa kunifikisha ninapotaka kufika? Ndugu je kabla hujaliendea ulishawahi kumshirikisha kwanza Mungu? Kama ni mapenzi yake au la?

Madhara ya kutomshirikisha Mungu njia zetu ni Mengi sana.. Na mojawapo ni ghafla tu tutajikuta tumepotea, tukiangalia kumbe ni mambo Fulani yalituponza mpaka tukafikia pale.

Hivyo maandiko haya matatu yakiwapo akilini mwetu, basi kuna uwezekano mkubwa wa kuufikia mwisho mwema..

  1. Mithali 14:12 “Iko njia ionekanayo kuwa sawa machoni pa mtu, Lakini mwisho wake ni njia za mauti”.

Na hili..

  1. Zaburi 119:9 “Jinsi gani kijana aisafishe njia yake? Kwa kutii, akilifuata neno lako”.

Na la mwisho ni hili…

  1. Mithali 16:3 “Mkabidhi Bwana kazi zako, Na mawazo yako yatathibitika”.

Bwana atubariki na kutuongoza katika njia zetu katika Jina la Yesu Kristo.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312 / 0693036618.

Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

IKO NJIA IONEKANAYO KUWA SAWA MACHONI PA MTU.

SIRI YA KUFANIKIWA KWA MTUME PAULO.

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!

NJONI, NUNUENI MLE NA MNYWE.

ZIKIMBIE TAMAA ZA UJANANI! NA MTU YEYOTE ASIUDHARAU UJANA WAKO.

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

VITA VYA IMANI NI VITA ENDELEVU.

Maadamu tunaishi hapa duniani, kila siku tupo mapambanoni….Unapomwamini Yesu Kristo tu na kuamua kumfuata kwa moyo wote, kwa kitendo hicho tu tayari umeshatangaza vita na ufalme wa giza..Na vita hivyo huna budi kuvikabili mpaka siku unaondoka hapa duniani. Hakuna siku hivi vita vya imani vitaisha..utapitia hiki, utatulia kidogo ghafla kitanyanyuka kingine, lakini Bwana atakuwa upande wako kukupa ushindi. Lakini shetani huwa hakati tamaa kama sisi wanadamu…Kuanzia mwanzo wa safari yako mpaka mwisho utakuwa vitani tu!…kwahiyo jiandae kwa hilo…Kama alikupa shamba wakati ukiwa wake, leo umemsaliti atalidai shamba lake, kama alikupa heshima hiyo heshima atakunyang’anya na atawatumia watumishi wake.

Tunaweza kujifunza kwa ufupi kwa Bwana wetu Yesu, jinsi shetani alivyoanzana naye kwenye huduma yake na alivyomaliza naye. Inadhaniwa na wengi kuwa siku ile shetani alipomjaribu Bwana kule jangwani ndio ilikuwa mwisho wa majaribu.. Lakini nataka nikuambie sivyo!…Ndio ilikuwa ni mwanzo tu wa majaribu…ingekuwa ndio ilikuwa mwisho sidhani kama Bwana angesulubiwa…Hebu tusome.

Luka 4:12 “Yesu akajibu akamwambia, Imenenwa, Usimjaribu Bwana Mungu wako.

13 Basi alipomaliza kila jaribu, Ibilisi akamwacha AKAENDA ZAKE KWA MUDA”.

Nataka uone hicho kipengele cha mwisho kinachosema “akaenda zake kwa muda!”…Maana yake ni kwamba atarudi tena baadaye!. Anakwenda kuandaa vita vingine vipya..hivyo kakubali kashindwa lakini hiyo haimpi sababu ya kukata tamaa…Na utaona aliporudi tena alirudi kwa nguvu nyingi akishindana na Bwana kupitia watu na wakuu…Aliwavaa mpaka viongozi wa dini wakubwa, na wakuu wa nchi kupambana na Yesu…Mpaka ilifikia wakati mfalme Herode anatafuta kumuua Bwana Yesu. Hebu jiweke kwenye nafasi kama hiyo,!..viongozi wa dini wanakupinga! Na bado mkuu wa nchi anatafuta kukuua?..Bila shaka hivyo ni vita vikali sana..

Na haikutosha hapo, kuonyesha jinsi gani shetani hakati tamaa…japokuwa alimshindwa, lakini bado hata wakati yupo pale msalabani anamjia tena na kumwambia maneno yale yale kama aliyomwambia kule jangwani… “ikiwa kweli wewe ni mwana wa Mungu jishushe msalabani!”…bado anaamini anaouwezo wa kumwangusha Bwana hata akiwa bado amebakisha dakika moja ya pumzi ya uhai wake…Mpaka sekunde ya mwisho Bwana yupo vitani.. Na ndio maana Bwana aliwaambia hivi wanafunzi..

Yohana 16:33 “Hayo nimewaambieni mpate kuwa na amani ndani yangu. Ulimwenguni mnayo dhiki; lakini jipeni moyo; mimi nimeushinda ulimwengu”.

Sasa dhiki inayozungumziwa hapo ndio hayo majaribu…Na mfano wa dhiki hizo sio kuvunjiwa bar yako iliyokuwa inakupatia kipato, au kuibiwa fedha zako na mfanyakazi wako wa Bar!…au kupigwa baada ya kufumaniwa, au kuingizwa jela baada ya kushikwa unaiba!… Hapana hizo sio dhiki(sio vita vya imani) bali ni majibu ya dhambi zako!…Dhiki hasa ni zile unazozipitia baada ya wewe kuukataa ubaya!..mfano unafukuzwa kazi kwasababu umekataa kufanya uasherati, unasingiziwa kitu Fulani kwasababu umekataa kwenda katika njia zao, unachukiwa na kutengwa kwasababu umebadilisha njia zako na umeacha kuwa wa kidunia au kuabudu sanamu, au mizimu au kufanya matambiko…Mfano wa dhiki hizo ndio majaribu..

Kwasababu majaribu haya yataendelea mpaka mwisho wa maisha yetu!..biblia inatuonya TUVUMILIE! Na TUSTAHIMILI na pia tusiogope!…kwasababu Bwana atakuwa upande wetu kutusaidia tukijua kuwa lipo taji la uzima linatungojea huko mbeleni.

Yakobo 1:12 “Heri mtu astahimiliye majaribu; kwa sababu akiisha kukubaliwa ataipokea TAJI YA UZIMA, Bwana aliyowaahidia wampendao”.

Ufunuo 2:9 “Naijua dhiki yako na umaskini wako, (lakini u tajiri) najua na matukano ya hao wasemao ya kuwa ni Wayahudi, nao sio, bali ni sinagogi la Shetani.

10 USIOGOPE MAMBO YATAKAYOKUPATA; tazama, huyo Ibilisi atawatupa baadhi yenu gerezani ili mjaribiwe, nanyi mtakuwa na dhiki siku kumi. Uwe mwaminifu hata kufa, nami nitakupa TAJI YA UZIMA”.

Bwana akubariki.

Kama hujaokoka, mlango wa neema upo wazi..lakini hautakuwa hivi siku zote…nyakati hizi muda unaenda kwa kasi sana…kufumba na kufumba dunia itaisha..na utaanza utawala mpya wa Bwana wetu Yesu Kristo..ambapo Huko atawalipa watakatifu wake kwa kadri ya Uvumilivu wao…Waliostahimili zaidi watapewa thawabu kubwa zaidi..Bwana atusaidie tufike huko.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312 / 0693036618.

Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

JE UNAMTHAMINI BWANA?

Mitume wote waliopita walikuwa ni watu weupe hata manabii wote waliopita hadi Ma-papa ni ngozi nyeupe. ni kweli ngozi nyeusi ililaaniwa ?

JE! KUBET NI DHAMBI?

Je ni kweli huwezi kuijua karama yako mpaka uwekewe mikono na wazee?

WAKATI ULIOKUBALIKA NDIO SASA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

BWANA AKAMWAMBIA SHETANI, BWANA NA AKUKEMEE EWE SHETANI;

Shalom jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe. Karibu tujifunze biblia.

Tunaweza kujiuliza maswali mengine ni kwanini mara nyingi malaika walipokuwa wakishindana na shetani, hawakutumia uweza wao wote kupambana naye,bali walimwachia Mungu aamue, japokuwa walikuwa na mamlaka na uwezo wa kufanya lolote juu yake..

Tunaweza kuona baadhi ya maeneo katika biblia, kwamfano kama lile tukio la Yoshua kuhani mkuu alipokuwa anahudumiwa na Yule malaika, na shetani naye akiwa pembezoni mwao kulipinga kusudi la Mungu..Utaona pale yule malaika hakutoa maneno ya kulaani , japokuwa ibilisi ni mlaaniwa sikuzote..bali alisema..

Zekaria 3:1 “Kisha akanionyesha Yoshua, kuhani mkuu, amesimama mbele ya malaika wa Bwana, na Shetani amesimama mkono wake wa kuume ili kushindana naye.

2 Bwana akamwambia Shetani, Bwana na akukemee Ewe Shetani; naam, Bwana, aliyechagua Yerusalemu, na akukemee; je! Hiki si kinga kilichotolewa motoni”?

Unaona? Sehemu nyingine tena ni pale Mikaeli alipopewa jukumu la kuuhifadhi mwili wa Musa, lakini shetani akatokea ghafla ili kushindana naye lakini utaona hakudiriki, kumtamkia hukumu palepale, japokuwa tayari ibilisi ni mlaaniwa, badala yake alimkabidhi Mungu hukumu yote..

Yuda 1:9 “Lakini Mikaeli, malaika mkuu, aliposhindana na Ibilisi, na kuhojiana naye kwa ajili ya mwili wa Musa, hakuthubutu kumshitaki kwa kumlaumu, bali alisema, Bwana na akukemee’.

Kama hilo halitoshi, malaika watakatifu bado, wanapotuona tunafanya mambo yasiyompendeza Mungu, wanaporudisha ripoti mbinguni juu ya mienendo yetu duniani, wanapofika mbele ya kiti cha enzi cha Mungu, hawatupelekei yale mashitaka mabaya kwa Mungu, wanajaribu kuyasitiri kwa kadiri wawezavyo, Uone jinsi wanavyoogopa hata kutoa neno la laana kwa kiumbe chochote cha Mungu kiwe ni kizuri au kibaya..

2Petro 2:11 “Wenye ushupavu, wenye kujikinai, hawatetemeki wakiyatukana matukufu; IJAPOKUWA MALAIKA AMBAO NI WAKUU ZAIDI KWA UWEZO NA NGUVU, HAWALETI MASHITAKA MABAYA JUU YAO MBELE ZA BWANA.

12 Lakini hao kama wanyama wasio na akili, ambao walizaliwa kama wanyama tu wa kukamatwa na kupotezwa, wakikufuru katika mambo wasiyoyajua, wataangamizwa katika maangamizo yao”

Hiyo ni kutufundisha na sisi pia tunavyopaswa tuchukuliane na maadui zetu mbele za MUNGU, Pale wanaposhindana na sisi, Je na sisi tushindane nao kwa kuwalaani au kuwalaumu?..Pale unaposikia umesengenywa kidogo je na wewe uende kuwaombea mabaya mbele za Mungu, wapigwe? Je! wewe ni mtu wa kupeleka mashitaka tu kila siku zote mbele za Mungu..Huna lingine..?

Wapigwe, waangushwe, warudishwe nyuma, wafedheheshwe, ni hayo tu ndio tunayoweza kumwambia Mungu kwenye maombi yetu ya kila siku?, Hatuna Muda wa kumuomba Mungu ufalme wake uje juu ya roho zetu kama Bwana alivyotufundisha, sisi ni kushindana na maadui zetu ?

Yuda 1:9 “Lakini Mikaeli, malaika mkuu, aliposhindana na Ibilisi, na kuhojiana naye kwa ajili ya mwili wa Musa, hakuthubutu kumshitaki kwa kumlaumu, bali alisema, Bwana na akukemee.

10 Lakini watu hawa huyatukana mambo wasiyoyajua, na mambo wayatambuayo kwa asili wajiharibu kwayo kama wanyama wasio na akili.

11 Ole wao! Kwa sababu walikwenda katika njia ya Kaini, na kulifuata kosa la Balaamu pasipo kujizuia, kwa ajili ya ujira, nao wameangamia katika maasi ya Kora”.

Kaka/Dada watu watakaokwenda kinyume na wewe watakuwepo tu daima kutupinga, lakini sisi tumwachie hayo Mungu ayashughulikie kama wafanyavyo malaika, tuendelee na kusudi lililotuleta hapa duniani la kumtafuta Mungu na hiyo ndio ishara nzuri ya unyenyekevu tunayopaswa tuige kwa malaika watakatifu dhidi ya maadui zetu (wanadamu).

Mithali 24:17 “Usifurahi, adui yako aangukapo; Wala moyo wako usishangilie ajikwaapo;

18 Bwana asije akaliona hilo, likamkasirisha; Akageuzia mbali naye hasira yake”.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312 / 0693036618.

Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

MAPAMBANO DHIDI YA SHETANI.

Ni uthibitisho upi unaoonyesha kuwa kuna MBINGUNI na KUZIMU?

FAHAMU TAFSIRI ZA NDOTO MBALIMBALI.

WANA WA MUNGU, NA BINTI ZA WANADAMU.

HISTORIA YA WILLIAM BRANHAM

Rudi Nyumbani:

Print this post

Usimwache mwanamke mchawi kuishi! Biblia ilimaanisha nini?

SWALI: Nina swali juu ya uchawi, Biblia iliposema kuwa usimwache mwanamke mchawi kuishi ilimaanisha nini?


JIBU: Katika agano la kale Mungu aliwapa wana wa Israeli hukumu…akawaambia wazishike hizo..na hukumu hizo ni kwa wale wote watakaokwenda kinyume na Torati…Kwamfano Torati ilikataza KUZINI..Mojawapo wa zile amri kumi ilikuwa ni USIZINI.

Hivyo mwanamke/mwanamume yeyote atakayeivunja hiyo sheria..adhabu yake ilikuwa ni KIFO!..Na walioitekeleza hiyo hukumu walikuwa ni hao hao wana wa Israeli kufuatia maagizo waliyopewa na Mungu mwenyewe…Kwamfano mwanamke aliyefumaniwa katika uzinzi, adhabu yake ilikuwa ni kupigwa mawe mpaka kufa!..aliyekamatwa vilevile analala na mnyama adhabu yake ilikuwa ni kifo,

Hebu tusome baadhi ya hukumu hizo

Walawi 20:10 “Na mtu aziniye na mke wa mtu mwingine, naam, yeye aziniye na mke wa jirani yake, mtu mume aziniye, na mwanamke aziniye, hakika watauawa.

11 Na mtu mume atakayelala pamoja na mke wa baba yake amefunua utupu wa baba yake; wote wawili hakika watauawa; damu yao itakuwa juu yao.

12 Na mtu mume akilala na mkwewe mwanamke wote wawili hakika watauawa; wamefanya yaliyo uchafuko; damu yao itakuwa juu yao.”

Kutoka 22: 19 “Mtu awaye yote alalaye na mnyama sharti atauawa”.

Na sio hizo tu!…kulikuwa na sheria zilizokuwepo za kumuua ndugu yako wa damu endapo atakwenda kuabudu miungu mingine tofauti na Mungu wa Israeli. Na zaidi ya hayo Mungu alikataza shughuli zozote za kishirikina na kichawi katika Taifa takatifu la Israeli..

Kumbukumbu 18: 9 “Utakapokwisha kuingia katika nchi akupayo Bwana, Mungu wako usijifunze kutenda kwa mfano wa machukizo ya mataifa yale.

10 Asionekane kwako mtu ampitishaye mwanawe au binti yake kati ya moto, wala asionekane mtu atazamaye bao, wala mtu atazamaye nyakati mbaya, wala mwenye kubashiri, wala msihiri,

11 wala mtu alogaye kwa kupiga mafundo, wala mtu apandishaye pepo, WALA MCHAWI, wala mtu awaombaye wafu.

12 Kwa maana mtu atendaye hayo ni chukizo kwa Bwana; kisha ni kwa sababu ya hayo Bwana, Mungu wako, anawafukuza mbele yako.

13 Uwe mkamilifu kwa Bwana, Mungu wako”.

Sasa yeyote Yule aliyekiuka amri hiyo Mungu aliyoitoa ya kutojihusisha na ushirikina na uchawi..hukumu yake ilikuwa ni kifo tu!..Ndio hapo Musa akaiandika hiyo hukumu katika..

Kutoka 22:18 “Usimwache mwanamke mchawi kuishi. 19 Mtu awaye yote alalaye na mnyama sharti atauawa”.

Maana yake mwanamke/mwanamume akikamatwa katika ushirikina ni kuuawa kwa aidha kupigwa kwa mawe au kwa vyovyote vile…(ilimradi afe tu)

Kwahiyo sheria ya kuwaua wachawi ilikuwepo kama tu sheria ya kumuua mwanamke aliyekamatwa katika uzinzi..

Lakini sasa katika agano jipya la Bwana na mwokozi wetu Yesu Kristo..wanadamu hatujapewa tena mamlaka ya kuhukumu kutoka kwa Mungu, kama wana wa Israeli walivyopewa amri ya kuhukumu na Mungu mwenyewe. Hatuna tena hukumu ya jino kwa jino, jicho kwa jicho, mguu kwa mguu, Wakati huu wa sasa wa agano jipya, Hukumu yote amekabidhiwa Yesu Kristo.

Yohana 5:22 “Tena Baba hamhukumu mtu ye yote, BALI AMEMPA MWANA HUKUMU YOTE”

Umeona hapo? Mwana (yaani Yesu Kristo) Ndio kakabidhiwa hukumu yote sasa…na ndiye atakayewahukumu walio hai na walio kufa (Kasome 2Timotheo 4:1)…hakuna tena mtu yeyote mwenye mamlaka ya kumuua mwanamke aliyeshikwa katika uzinzi, wala kumuua mtu aliyekamatwa analala na mnyama wala kumuua mwanamke/mwanamume aliyekamatwa katika uchawi. Hukumu hizo Yesu Kristo ndio kakabidhiwa na Baba, na sasa ametupa neema….Ambapo tunamkosea Mungu lakini tuna nafasi ya kutubu kabla ya kuhukumiwa…

Maasi tunayoyafanya sasa tunastahili kuhukumiwa na Bwana Yesu papo kwa hapo!!…lakini tumependelewa na kupewa nafasi ya kukimbilia msalabani na kupata msamaha kabla ya hukumu ya mwisho!…Utafika wakati hii neema itaisha na huyu Yesu Kristo tunayemwona sasa anayeturehemu bure watu tusiostahili kurehemiwa, atafunga mlango wa Neema na atasimama kwenye kiti chake cha hukumu na atawahukumu wazinzi wote, wachawi wote na watenda dhambi wote kwa kuwatupa katika ziwa la moto..Lenye adhabu kali kuliko ya kupigwa kwa mawe.

Hivyo haturuhusiwi kwa namna yoyote kuwaua wezi kwa kuwapiga kwa mawe,wala kuwaua tuliowafumania katika uzinzi wala tuliowakamata katika uchawi, wala kulaani mtu yeyote yule..kwa kuutumia huo mstari wa “usimwache mwanamke mchawi kuishi”..Wasiolielewa Neno ndio wanaoutumia huo mstari kwa kukosa maarifa…lakini mimi na wewe tusikose hayo maarifa…Kwasababu hakuna astahiliye kuhukumu sasa isipokuwa Mwana wa Mungu pekee.

Jukumu letu ni sisi kuomba kwa bidii dhidi ya nguvu zote za giza, kwamba zisiwe na nguvu juu yetu, wala juu ya watu wetu na familia yetu, na vitu vyetu…na kumwomba Mungu awaokoe ndugu zetu waliozama katika nguvu za giza, ambao wanatumika na mamlaka ya giza aidha kwa kujua au kwa kutokujua, kwasababu nao pia ni watu kama sisi wanaohitaji wokovu, na sio kutafuta njama za kuwaua,au kuwaombea vifo ni kinyume na maandiko…

Bwana atubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312 / 0693036618.

Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

Nini tofauti kati ya Amri, sheria na Hukumu?

UTUKUFU NA HESHIMA.

Kwanini Bwana aliongea na Abramu baada ya kutengeana na Lutu?

UNATAKA KUBARIKIWA? BASI USIKWEPE GHARAMA ZAKE.

Uasherati wa Kiroho maana yake nini?

Rudi Nyumbani:

Print this post