Je! mstari huu unahalalisha unywaji wa pombe?…(1Wakorintho 11:21 “kwa maana kila mmoja hutangulia kutwaa chakula chake katika kule kula; hata huyu ana njaa, na huyu AMELEWA.
22 Je! Hamna nyumba za kulia na KUNYWEA? Au mnalidharau kanisa la Mungu, na kuwatahayarisha hao wasio na kitu? Niwaambieni? Niwasifu? La! Siwasifu kwa ajili ya hayo.”)
JIBU: Watu wengi hususani wale wanaohalalisha ulevi katika makanisa yao ndio wanaoushikilia wakidhani kuwa Paulo alihalalisha ulevi kwamba waumini wakitaka kunywa mpaka walewe basi waende wakalewee majumbani kwao na sio kanisani.
Lakini Hebu tafakari huu mfano… “Watu wawili wamegombana katika nyumba ya Mungu (kanisani)…mpaka kufikia kupigana..Mhudumu wa kanisa akawakuta..na kwa hasira akawaambia “mmekosa sehemu za kupigania mpaka mnapigania kanisani”…Je! Kwa sentensi hiyo Mhudumu huyo atakuwa amehalalisha mapigano?…Jibu ni la! Hajayahalalisha hata kidogo…bali kwasababu anaiheshimu nyumba ya Mungu ikamlazimu yeye kusema vile. Kwamba nyumba ya Mungu sio ulingo wa mapambano..sio sehemu ya kufanyia dhambi wala mapambano…kama wameshindwa kuiheshimu nyumba ya Mungu na kutaka kuendelea kupigana basi wakapiganie sehemu nyingine huko lakini si nyumbani kwa Mungu.
Na hapa Mtume Paulo ndio anawaambia kwa ukali watu ambao wanaigeuza nyumba ya Mungu sehemu au vituo vya ulevi na ulafi. Watu ambao hawaiheshimu nyumba ya Mungu wala meza ya Bwana watu waovu, wana wa ibilisi. Hao ndio anaowaauliza je hawana nyumba za kunywea pombe zao?…maana yake wasiigeuze nyumba ya Mungu kuwa Bar… Kama tu Bwana alivyowafukuza wale watu hekaluni na kuwaambia wasiigeuze nyumba ya Baba yake kuwa pango la wanyang’anyi.
Picha kamili ya kinachoendelea katika kanisa la leo…watu wanakwenda kanisani ni walevi, wengine wanapafanya ni sehemu ya kunywea pombe kabisa rasmi bila aibu, wakitumia maandiko machache machache ya uongo waliyoyageuza kama walivyoligeuza hili…wengine wanapageuza kanisani ni mahali pa kwenda kutafuta wachumba wa kufanya nao uasherati, wengine wanapageuza mahali pa kwenda kupata burudani za nyimbo na mahubiri ya kuwachekesha n.k..
Hivyo tunaonywa vikali kwamba tumheshimu Mungu..kanisani sio sehemu ya kwenda kujiuza..wala si sehemu ya kwenda kutafuta makahaba…Unapovaa vimini na suruali na kuingia navyo kanisani ni unakwenda kupageuza pale danguro (ni sawa na unakwenda kujiuza pale)..na hivyo ni kujitafutia laana badala ya Baraka..
Kama umeamua kuwa hivyo ulivyo huna mpango na Mungu basi upo huru kuishi maisha unayoyataka wewe na unayoyachagua wewe..Toka kanisani nenda disko na nguo zako hizo, kule ni sehemu sahihi kwa mavazi hayo, nenda bar kule ni sehemu sahihi ya kulewa pombe lakini si katika nyumba ya Mungu. Nyumba ya Mungu ni nyumba takatifu ya sala, na ya kumwabudu Mungu, na ya Mungu muumba wa mbingu na nchi kwenda kukutana na sisi. Hivyo iheshimu.
Ubarikiwe. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
JE KUJIUA NI DHAMBI?
BUSTANI YA NEEMA.
DANIELI: Mlango wa 8
USIPOKUWA MWAMINIFU, NAFASI YAKO ITACHUKULIWA.
VICHEKESHO NA UTANI MADHABAHUNI
AMANI YA BWANA /AMANI YA MUNGU.
Rudi Nyumbani:
Print this post
Kuota mtu amekufa au ndugu amekufa.
Wakati mwingine unaweza ukaota umefiwa na mzazi, au kaka au dada, au mtu wako wa karibu sana. Na ndoto hizi huwa zinakuja kwa uzito sana, kiasi kwamba unaposhtuka huamini kama kweli ilikuwa ni ndoto, kwasababu unaona kama tukio hilo lilikuwa ni halisi kabisa..unabaki kuishia kumshukuru Mungu na kusema asante kwa kuwa ilikuwa ni ndoto tu..
Ndoto kama hizi huwa zinawapata watu wengi, na kama haijawahi kukutokea, basi itakuja kukupata siku moja katika maisha.. Lakini fahamu kuwa ni Mungu hapo anakukumbusha hatma ya maisha yako na ya ndugu zako itakavyokuwa..kwamba siku moja wataondoka duniani, sio lazima wafe kwa njia hiyo hiyo uliyoiona kwenye ndoto hapana bali inaweza ikaja kwa njia yoyote lakini lakini kitendo ni kile kile kifo..
Vilevile inaweza ikawa ni hivi karibuni, au isiwe hivi karibuni pengine baada ya miaka 5 au 10 au hata 50 lakini ujumbe ni ule ule, kifo kinakuja.
Hivyo ni wajibu wako kufanya mambo mawili makuu juu ya maisha ya ndugu zako angali wakiwa bado hai,
1Samweli 12:23 “Walakini mimi, hasha! Nisimtende Bwana dhambi kwa kuacha kuwaombea ninyi; lakini nitawaelimisha katika njia iliyo njema, na kunyoka.”
Unaona Nabii Samweli hakuacha kuiombea Israeli japokuwa ilikuwa inamchukiza Mungu kwa sanamu zao, lakini alikuwa akidumu katika kuwaombea..aliwaombea kwa bidii sana, na akahesabu kwamba ni dhambi kuacha kuwaombea ndugu zake,…na pia akawa anawaonya..hata Musa naye kule jangwani ni mara nyingi Mungu alitaka kuwaangamiza wana wa Israeli kwa matendo yao maovu lakini kwa maombi ya Musa Mungu alighahiri mabaya yao.
Hivyo na wewe ikiwa upo ndani ya Kristo ni rahisi Mungu kusikia maombi yako na Mungu akawaweka katika mstari sahihi ikiwa utaendelea kuomba kwa bidii juu yao bila kukata tamaa, na vile vile Mungu atawaepusha na mabaya na njama nyingi za ibilisi ziliyopangwa kinyume chao, ikiwemo vifo ambavyo sio vya wakati.
Lakini kama upo nje ya Kristo, hakuna dua yoyote itakuwa rahisi kwa ndugu zako. Hivyo nakushauri umpe Bwana Yesu maisha yako leo, tubu dhambi zako kwa kumaanisha kabisa kuziacha na kuwa tayari kumfuata yeye kwa moyo wako wote ili Bwana akuokoe kwanza wewe, ndipo iwe rahisi kusikia maombi yako kwa wengine.. Yesu sio wa watu wa dini Fulani tu, hata kama wewe ni muislamu, kimbilio lako ni YESU tu, wala hakuna mwingine..Yeye ndiye anayekuahidi uzima wa milele, yeye pekee ndio anayetoa faraja ya kweli ukiwa kwanza hapa duniani, na hata utakapofika kule..
Hivyo Ikiwa upo tayari kufanya hivyo leo basi hapo
Basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.
EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE. ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE. AMEN.
EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.
ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.
AMEN.
Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa kuukamlisha wokovu wako.
Ubarikiwe sana.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312 jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Au jiunge Whatsapp hapa
Tofauti kati ya ndoto na Maono ni ipi?
KUOTA UPO UCHI.
Kuota unafanya Mtihani.
KUOTA UNAPAA.
USIKIMBILIE TARSHISHI.
KAMA ZILIVYOKUWA SIKU ZA NUHU NA ZA LUTU.
CHUKIZO LA UHARIBIFU
Kwaresma ni nini?..Je! Kwaresma ipo katika Maandiko?..Na je ni lazima kufunga Kwaresma?, ni dhambi kuikatisha kwaresma? na je! ni dhambi kuishika kwaresma?
Neno Kwaresma limetokana na Neno la kilatini (Quadragesima) lenye maana “YA AROBAINI “… Kwahiyo siku ya 40 ndiyo inayoitwa Kwaresma..Kulingana na mapokeo ya, Madhehebu ya kikristo wanalitumia neno hilo kama kuwakilisha kipindi cha siku 40 cha mfungo kabla ya Pasaka.
Madhumini ya Mfungo huo ni kuwaandaa wakristo katika maombi, toba na kujinyenyekeza kwa ajili ya Pasaka ambayo itakuja baada ya siku hizo 40. Mfungo huo kulingana na mapokeo yao ni wa siku 40, lakini kiuhalisia ni zaidi ya siku 46..Kwasababu siku za jumapili huwa hazihesabiwi katika mfungo huo..Kwahiyo zinakuwepo jumapili 6 katika mfungo mzima..na kufanya Idadi ya siku za mfungo kuongezeka mpaka kufikia 46.
Mfungo huo pia unahusishwa na Bwana alivyofunga siku 40, akiwa jangwani, akijaribiwa na Ibilisi. Hivyo na wakristo wana jukumu la kufunga siku 40 kama Bwana alivyofunga.
JE KWARESMA IPO KIMAANDIKO?
Jibu ni La! Hapana sehemu yoyote katika maandiko kuna sharti la kuitimiza Kwaresma..Hayo ni mapokeo..Na mapokeo yapo yaliyo mazuri na yaliyo mabaya..Mazuri ni yale ambayo hayakinzani na Neno la Mungu na mabaya ni yale yanayokinzana na Neno la Mungu na kuwafanya watu wawe wa kidini zaidi, kuliko kuwa wa Kiroho.
JE NI DHAMBI KUISHIKA KWARESMA.
Katika Biblia ni wajibu wa kila Mkristo “kufunga na kusali”..Mambo hayo yanakwenda pamoja huwezi kusema unasali siku zote halafu hufungi hata mara moja, na pia huwezi kusema unafunga siku zote na husali hata siku moja. Kwahiyo Mfungo ni sharti kwa kila mwamini. Iwe ni mfungo wa wiki moja, wiki 2, siku 30, siku 40 au 50…Ni jambo la sharti. Na mfungo huo mtu auite kwa jina lolote iwe Kwaresma, jubilee, baragumu, au jina lolote lile ambalo mtu atapenda kuliita sio dhambi…
Kikubwa na cha msingi..Tendo lolote la kufunga halipaswi kuchukuliwa kidini..Kwamba mtu anafunga tu ili kutimiza sheria za dini yake, kama inavyofanyika leo. Haipaswi mtu kufunga halafu asiwe mwombaji…Wengi wanafunga lakini hata siku moja hawajawahi kutenga kusali hata lisaa limoja…huko ni kufunga kwa kidini ambako kuna matokeao madogo sana au kunaweza kusiwe na matokeo yoyote kabisa ikawa ni bure.
Hali kadhalika wakati wa Mfungo sio wakati wa kujichanganya na mambo ya kidunia, ni wakati wa kuwa katika utulivu wa roho na kujitesa nafsi, wakati wa kutubu kikweli kweli na wakati wa kuomba kwa bidii..Ni wakati wa kuongeza bidii sana katika mambo ya kiroho zaidi ya kimwili..Ndio maana unafunga kula..si wakati wa kuupendeza mwili ni wakati wa kuutiisha mwili.
Kwahiyo Mfungo huo unaoitwa Kwaresma kama hautafanyika kidini basi una matokeo makubwa sana kwa mhusika.
JE NI DHAMBI KUIKATISHA KWARESMA?
Mfungo mara nyingi ni kama Nadhiri, kabla ya kuanza kufunga mtu unaweka nadhiri kwamba unafunga siku 40, lakini ukisema unafunga halafu ndani ya mfungo huo unakuwa sio mwaminifu, utakuwa unajipotezea muda tu wewe mwenyewe..Kama umeamua kufunga sharti umalize siku zote na kama huwezi basi usifunge…Maana utakuwa hujafunga kwa Imani, na biblia imesema tendo lolote lisilotokana na Imani ni dhambi (Warumi 14:23)
JE NI LAZIMA KUFUNGA KWARESMA?
Jibu ni la!..sio lazima kufunga wakati huo unaoitwa Kwaresma…lakini ni wajibu wa kila Mkristo kufunga..Kama hutafunga msimu huo ambao ni rahisi kueleweka na watu wengi…basi hakikisha unatafuta kipindi kingine katikati ya mwaka ambacho utafunga. Na kama ni mkristo kikweli kweli na si wakidini, basi utafunga nawe siku hizo hizo 40 au zaidi. Kwasababu ukilijua lile neno linalosema..
Matendo 5:20 “Maana nawaambia ya kwamba, Haki yenu isipozidi hiyo haki ya waandishi na Mafarisayo, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni”
Kwasababu kama mtu unayemwita wewe wa kidini anakushinda idadi ya siku za kufunga…hapo ni nani wa kidini?…wewe au yeye?..Jibu ni wewe?..kwasababu huwezi kufanya hata anachokifanya yeye..na bado unamwita wa kidini. Sharti ufanye kama yeye tena vizuri zaidi umpite ili uwe na sababu ya kumrekebisha, lakini kama huwezi kumzidi, yeye ndio anayepaswa akurekebishe wewe.
Bwana akubariki
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
JUMATANO YA MAJIVU NI TENDO LA KIMAANDIKO?
NAMNA YA KUITAMBUA SAUTI YA MUNGU INAPOZUNGUMZA NA WEWE
ROHO YA MPINGA KRISTO IKITENDA KAZI SIKU HIZI ZA MWISHO
JE! NI DHAMBI KUIMBA WIMBO WA TAIFA?
YESU KWETU NI RAFIKI
MTINI, WENYE MAJANI.
WhatsApp
Jumatano ya majivu, ni mojawapo ya mapokeo ya kanisa katoliki..ambapo Ni kipindi cha mwanzo wa mfungo wa siku 40… Siku hii yanachukuliwa “matawi ya Mitende” na kuchomwa mpaka yawe jivu. Na kisha lile jivu linachukuliwa na kwenda kupakwa katika paji la uso la mwamini, ishara kama ya msalaba.
Na wakati mhudumu anampaka mwamini majivu yale anakuwa anayasema maneno haya “kumbuka u mavumbi wewe na mavumbini utarudi”.. Na baada ya hapo ndipo muumini ataanza mfungo wa siku 40
Je Tendo hilo la Jumatano ya Majivu ni la kimaandiko?
Jibu ni la! si la kimaandiko hata kidogo. Hakuna mahali popote katika biblia wakristo walikuwa wanadesturi za kufanya hayo mapokeo ya jumatano ya majivu. Ni mapokeo tu yaliyoanzishwa na wanadamu. Ingawa Tendo la Mfungo ni la kimaandiko, ambalo kila mwamini anapaswa alitekeleze pia, lakini jumatano ya majivu sio ya kimaandiko.
Kwahiyo hakuna ulazima wowote wa mkristo kushika hiyo siku ya “jumatano ya majivu” kana kwamba ni siku takatifu isiposhikwa au kuenziwa ni dhambi mbele za Mungu. Na kwamba yale majivu yana nguvu fulani ya kiMungu, kana kwamba ukipakwa au ukipaka kuna jambo fulani la kiroho linaongezeka kwa msharika. Hapana, vilevile Mtu anaweza kuanza kufunga siku alizozipanga yeye pasipo huo utaratibu.
Kwahiyo hayo sio mambo ya msingi hata kidogo na wala hayamwongezei chochote Muumini, zaidi ya kumfanya awe wa kidini kuliko kuwa wa kiroho kuamini kuwa kuna kitu cha kipekee kinaongezeka ndani yake anapopakwa yale majivu.
Mambo ya lazima na ya sharti kuyafanya tuliyoagizwa na Roho Mtakatifu sisi wakristo yapo manne nayo ni…. 1)KUUMEGA MKATE, 2)KUKUSANYIKA PAMOJA, 3)KUDUMU KATIKA FUNDISHO LA MITUME (yaani kudumu katika Neno la Mungu) na 4) KUSALI. (Matendo 2:42). Hayo ndio mambo manne na ya muhimu na ya lazima kufanya kwa kila Mwamini. Na sio kushika sikukuu ya majivu wala ijumaa kuu. Na hilo la Nne la kusali linajumuisha pia KUFUNGA..Kwasababu kufunga na kusali vinakwenda pamoja.
Bwana akubariki.
Maran atha!
KWARESMA IPO KIMAANDIKO?
TUWATAFAKARI NZIGE WA JANGWANI.
AMEFUFUKA KWELI KWELI.
Mbona Mungu anaruhusu watu wapate shida, ilhali ana uwezo wa kutuepusha?
KUOTA MAFURIKO,KUOTA MAJI MENGI,KUOTA MAWIMBI.
JE SALA YA ROZARI TAKATIFU NI YA KIMAANDIKO?
Siku zote Mungu akitaka kumuokoa mtu neema yake huwa anaizidisha sana kwa kiwango cha juu kiasi kwamba kwa nje ni rahisi kuona kama anatumia nguvu, au analazimisha ndivyo ilivyokuwa kwa Lutu na mke wake na watoto wake… Wale malaika wawili walipoona wanachelewa chelewa, wanakawia kawia waliwashika mikono yao na kuwavuta mpaka nje ya mji kwa nguvu kwa jinsi Mungu alivyowahurumia…
Mwanzo 19: 15 “Hata alfajiri ndipo malaika wakamhimiza Lutu, wakisema, Ondoka, mtwae mkeo na binti zako wawili waliopo hapa, usipotee katika maovu ya mji huu. 16 Akakawia-kawia; nao wale watu wakamshika mkono, na mkono wa mkewe, na mkono wa binti zake wawili, kwa jinsi Bwana alivyomhurumia, wakamtoa wakamweka nje ya mji.”
Mwanzo 19: 15 “Hata alfajiri ndipo malaika wakamhimiza Lutu, wakisema, Ondoka, mtwae mkeo na binti zako wawili waliopo hapa, usipotee katika maovu ya mji huu.
16 Akakawia-kawia; nao wale watu wakamshika mkono, na mkono wa mkewe, na mkono wa binti zake wawili, kwa jinsi Bwana alivyomhurumia, wakamtoa wakamweka nje ya mji.”
Lakini tendo hilo la kushikwa mikono halikuendelea milele walipofikishwa tu nje ya ule mji, wameshajua sasa yawapasayo kufanya jambo lililofuata waliambiwa..jiponyeni nafsi zetu msigeuke nyuma..Lakini Mke wa Lutu alijiharibia.
Mwanzo 19:17 “Ikawa walipomtoa nje, mmoja alisema, Jiponye nafsi yako usitazame nyuma, wala usisimame katika hilo bonde po pote; ujiponye mlimani, usije ukapotea”.
Ndugu, picha hii inatuonyesha kuwa wokovu ni tendo la neema kubwa sana, kiasi kwamba hakuna mtu anayeweza kujiokoa mwenyewe kwa nguvu zake…Na ndio maana Mungu aliona malaika hawatoshi kuja kutuokoa sisi na hukumu hiyo kubwa inayokuja huko mbele, badala yake akaamua kumtuma mwanawe kabisa , YESU KRISTO, ili aje kutuvuta sisi mbali na ile hukumu ya siku za mwisho na ziwa la moto…Yeye ndiye anayetushika mkono na kutuvusha kutoka katika ulee mji wa mauti na kutupeleka sehemu salama..
Lakini ikiwa ameshatuweka sehemu salama mbali na dunia, ni wajibu wa kila mmoja kuuthamini wokovu ule kwa kukimbia mbali zaidi na dhambi kama ilivyokuwa kwa Lutu na watoto wake..Ikiwa tulishaona mkono wa Mungu ulivyotuepua kutoka katika dhambi, hatupaswi kujilegeza tena, kusubiria tena neema itutoe kwenye dhambi tunazozitenda kwa uzembe wetu.. Tukishafikia hii hatua ni wakati wa kuziponya nafsi zetu…
Lakini embu tumtafakari mke wa Lutu ambaye ni mfano wa wale waliookolewa ambao mioyo yao bado ipo ulimwenguni, yeye alipogeuka nyuma alikuwa nguzo ya chumvi, unaweza kujiuliza ni kwanini awe nguzo ya chumvi na sio kitu kingine chochote labda tuseme nguzo ya mti, au ya chuma, au ya udongo?..Chumvi ni kiungo cha kipekee sana ambacho huwa kinadumu milele, yaani ukiihifadhi chumvi vizuri leo kwenye chupa mtu anatakaye kuja kuzaliwa miaka milioni moja mbele ataitumia na ikawa na ubora ule ule..
Na ndio maana Mungu sehemu nyingine alikuwa analifananisha Agano aliloingia na Daudi pamoja na wana wa Israeli kama agano la Chumvi, ikimaanisha kuwa ni agano la milele soma..
2Nyakati 13:5 “je! Haikuwapasa kujua ya kwamba Bwana, Mungu wa Israeli, alimpa Daudi ufalme juu ya Israeli milele, yeye na wanawe kwa agano la chumvi?”
Soma tena Hesabu 18:19..
Hivyo lile lilikuwa ni agano la kukataliwa milele kati yake na mke wa Lutu.. Hata sisi leo hii, ikiwa Bwana Yesu alishatuokoa, halafu tunauchezea wokovu wetu, leo tunaenda mbele, kesho tunarudi nyuma…hatuthamini ondoleo la dhambi tulilopewa siku ile tulipotubu bure, ..na wema wake wote Mungu aliotutenda, hatuoni kama kuokolewa kule ni jambo la bahati sana ambapo sio watu ulimwenguni wanaweza kupewa neema hiyo badala yake mguu mmoja kwa Kristo na mguu mwingine kwa shetani Tujue tu tupo hatarini kuwa MAWE YA CHUMVI katika roho..
Yaani Mungu kuingia na sisi agano la rohoni la milele kuwa hatukustahili kuokolewa na yeye, na matokeo yake ni kuwa safari yetu ya wokovu inakuwa imeishia pale pale, tunakuwa tumekufa,japo kwa nje tunaonekana tupo hai..Kumbuka hilo ni agano la milele, maana yake ni kuwa Mungu hatakaa akupokee wewe tena milele kwasababu ile nguvu ya kukuvuta kwake inakuwa haipo tena…utaendelea na ubaridi wako, mpaka siku unakufa ili uishie katika ziwa la moto..mifano hiyo ipo duniani leo hii, utakuta mtu alianza vizuri na Bwana, wengine hata walitokewa kabisa na malaika, wengine walisikia sauti ikizungumza nao, wengine wakaonyeshwa maono, wengine Mungu akawa anawapa chochote waombacho katika hatua za awali kabisa za wokovu wao, wengine wakaepushwa na hatari nyingi kimiujiza, wakajua kabisa sasa hapa safari imeanza..Lakini kwa tabia zao za kuyarudia rudia yale yale machafu ya nyuma kwa kipindi kirefu hiyo ikawafanya wageuke kuwa mawe ya chumvi..Ambao ndio hao leo hii huwezi kuamini hata kama walishawahi kumjua Kristo…
Wokovu sio jambo la kujaribu, na ndio maana biblia inatuambia..
Wafilipi 2:12 “………..utimizeni wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka. 2 Kwa maana ndiye Mungu atendaye kazi ndani yenu, kutaka kwenu na kutenda kwenu, kwa kulitimiza kusudi lake jema.
Wafilipi 2:12 “………..utimizeni wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka.
2 Kwa maana ndiye Mungu atendaye kazi ndani yenu, kutaka kwenu na kutenda kwenu, kwa kulitimiza kusudi lake jema.
Ikiwa ni wewe mmojawapo ndugu yangu unayesoma haya, na ndani yako bado kuna kanuru kadogo ambacho kanakaribia kuzima… basi usikubali izime kabisa…ni vizuri ukatubu kwa kumaanisha kabisa mbele za Mungu sasahivi, na kuacha kwa moyo wako wote mambo maovu yote unayoyafanya kwa vitendo, na kumfuata Kristo, neema hii bado ipo juu yako na ndio maana unasikia ndani yako kuhukumiwa unaposoma haya,….huyo ni Roho Mtakatifu anakuvuta kwake tena, anza kugeuka na kupiga hatua mbele, usipoitii hiyo sauti itafika kipindi hutaisikia tena ndani yako, utakuwa ukipita mahali na kukutana na maneno kama haya utaishia kudhihaki na kukejeli, lakini sasa kuna hofu ndani yako kiasi kwamba unaogopa hata kusema neno lolote la kejeli, hiyo hofu ni ya thamani na ya muhimu sana, na ndio inayokuvuta utubu,
Hivyo Tubu leo acha kwenda disko, acha ulevi, mrudie mke/mume wako, acha wizi, acha rushwa, acha kila aina ya dhambi unayoifanya maishani mwako na wala usigeuke nyuma kama mke wa lutu..…hizi ni siku za mwisho..Siku yoyote unyakuo unapita, na hii dunia inakwenda kuwa jivu, Maisha yatasimama…kilichosalia kwako sasa ni nini kama sio kuyasalimika maisha yako kwa Bwana Yesu ayaokoe, naye atakupokea kwasababu anakupenda na kukuhurumia…dini yako ya kiislamu haitakupeleka popote, dini ya kikristo haitakupeleka popote, dhehebu lako mashuhuri halitakupeleka popote bali YESU KRISTO pekee ndiye atakayekupeleka sehemu salama..
Hivyo Ikiwa upo tayari leo hii kuanza tena upya na Bwana..
Basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako.
Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.
Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.
Zingatia hayo na Bwana atakuwa pamoja na wewe daima. Ubarikiwe sana.
KAMA MUNGU ANABORESHA KAZI ZAKE, KWANINI WEWE USIBORESHE ZA KWAKO?.
NIFANYE NINI ILI NILITIMIZE KUSUDI LA MUNGU.
YEZEBELI ALIKUWA NANI
CHAGUA NI JIWE LIPI LITAKALO KUFAA KWA UJENZI.
MWAKA WA BWANA ULIOKUBALIWA.
Ni nani anayetawala dunia kati ya Mungu na shetani?
Yesu Kristo Bwana wetu…Amefufuka kweli kweli..
Kila tukio lililokuwa linatendeka wakati wa kusulubiwa kwa Bwana Yesu, wakati wa kuzikwa kwake na wakati wa kufufuka kwake lilikuwa na makusudi maalumu na lilikuwa lina ufunuo mkubwa sana..Hakuna tukio hata moja lililokuwa linatokea kwa bahati mbaya au nje ya mpango wa Mungu.
Mpaka tukio la Bwana Yesu kubeba msalaba wake kuelekea Goligotha huku akiwa na majeraha mwili mzima ni tukio ambalo lilikuwa tayari limeshatabiriwa… “lilifananishwa na kondoo anayepelekwa machinjoni”
Isaya 53:7 “Alionewa, lakini alinyenyekea, Wala hakufunua kinywa chake; Kama mwana-kondoo apelekwaye machinjoni, Na kama vile kondoo anyamazavyo Mbele yao wakatao manyoya yake; Naam, hakufunua kinywa chake”.
Tukio la Bwana kuchomwa mkuki ubavuni lilishatabiriwa (katika Zekaria 12:10), na lilikuwa linamaana kubwa katika roho na katika mwili..Katika Roho lilifunua utakaso wa damu na maji,. Kwa damu yake tunatakaswa dhambi zetu na kupata msamaha kabisa kabisa..na katika maji tunatakasika kwa Neno la Mungu (Waefeso 5:26)..
Na Kusudio lingine la kimwili, Bwana kuchomwa mkuki ubavuni wakati akiwa pale Kalvari..Ni kuhakiki kifo cha Bwana Yesu..Asingechomwa mkuki ubavuni watu wangesema alishushwa pale msalabani akiwa bado hajafa vizuri, na alipokwenda kupelekwa kaburini alikuwa hajafa vizuri hivyo uzushi mkubwa wa uongo ungezushwa wakati wa kufufuka kwake..
Kwahiyo Mungu wa mbingu na nchi alilijua hilo ndio maana akaruhusu wamchome mkuki Ubavuni ili wahakiki wenyewe kwamba amekufa…kwasababu katika hali ya kawaida hakuna mtu atakayeweza kuchomwa mkuki wa ubavu ukaingia mpaka ndani ya moyo halafu akabakia kuwa hai. Warumi walikuwa wanatumia njia hiyo kummalizia mtu ambaye hajafa vizuri.
Vivyo hivyo tukio la Pilato kuandika anwani kwa lugha tatu juu ya msalaba wa Bwana Yesu, tukio hilo halikuwa la bahati mbaya bali lilikuwa na maana kubwa sana katika roho..Kwani lilikuwa ni unabii kwamba siku zijazo Kristo atahubiriwa na kutangazwa kwa mataifa yote na kwa lugha zote.
Yohana 19:19 “Naye Pilato akaandika anwani, akaiweka juu ya msalaba, imeandikwa, YESU MNAZARETI, MFALME WA WAYAHUDI. 20 Basi anwani hiyo waliisoma wengi katika Wayahudi; maana mahali pale aliposulubiwa Yesu palikuwa karibu na mji; nayo iliandikwa kwa KIEBRANIA, NA KIRUMI, NA KIYUNANI. 21 Basi wakuu wa makuhani na Wayahudi wakamwambia Pilato, Usiandike, Mfalme wa Wayahudi; bali ya kwamba yule alisema, Mimi ni mfalme wa Wayahudi. 22 Pilato akajibu, Niliyoandika nimeyaandika”.
Yohana 19:19 “Naye Pilato akaandika anwani, akaiweka juu ya msalaba, imeandikwa, YESU MNAZARETI, MFALME WA WAYAHUDI.
20 Basi anwani hiyo waliisoma wengi katika Wayahudi; maana mahali pale aliposulubiwa Yesu palikuwa karibu na mji; nayo iliandikwa kwa KIEBRANIA, NA KIRUMI, NA KIYUNANI.
21 Basi wakuu wa makuhani na Wayahudi wakamwambia Pilato, Usiandike, Mfalme wa Wayahudi; bali ya kwamba yule alisema, Mimi ni mfalme wa Wayahudi.
22 Pilato akajibu, Niliyoandika nimeyaandika”.
Baada ya siku chache, siku ile ya Pentekoste…wale walioshukiwa na Roho Mtakatifu..walisikika wakinena kwa lugha mpya za mataifa yote yaliyokuwa yanajulikana duniani. Ikimaanisha kuwa wakati umefika habari za kufa kwa Yesu na kufufuka kwake kuhubiriwa ulimwenguni kote kwa kila lugha, na kila jamii ya watu. Tangu huo wakati injili ilianza kusambaa ulimwenguni kote. Wakati huo zilikuwa tu hizo lugha tatu maarufu duniani, kiebrania, kirumi na kiyunani…Lakini leo tuna lugha Zaidi ya elfu 6 duniani…Na katika hizo zote Kristo kashatangazwa.
Kadhalika kwanini Bwana alipowekwa kaburini liliwekwa jiwe kubwa kulifunga kaburi na juu ya jiwe hilo pakawekwa muhuri? ambapo kazi ya muhuri huo ilikuwa ni kuhakikisha kwamba kaburi limefungwa lote kisawasawa hakuna nafasi ya kupenya mtu au kitu chochote kile kuingia ndani. Na jiwe lile lilikuwa ni la uzani mkubwa sana..halikuwa kama yale yanayoonekana kwenye tamthilia..lilikuwa ni kubwa mno kiasi kwamba ilihitajika kukodi wanaume kadhaa kulisogeza..Ndio maana wale wanawake pamoja na idadi yao kuwa kubwa siku ile ya kwanza ya juma walipokuwa wanakwenda kaburini bado walihitaji mtu/watu wa kuwasaidia kulisogeza lile jiwe..
Marko 16: 2 “Hata alfajiri mapema, siku ya kwanza ya juma, wakaenda kaburini, jua lilipoanza kuchomoza; 3 wakasemezana wao kwa wao, Ni nani atakayetuvingirishia lile jiwe mlangoni pa kaburi? 4 Hata walipotazama, waliona ya kuwa lile jiwe limekwisha kuvingirishwa; nalo lilikuwa kubwa mno.”
Marko 16: 2 “Hata alfajiri mapema, siku ya kwanza ya juma, wakaenda kaburini, jua lilipoanza kuchomoza;
3 wakasemezana wao kwa wao, Ni nani atakayetuvingirishia lile jiwe mlangoni pa kaburi?
4 Hata walipotazama, waliona ya kuwa lile jiwe limekwisha kuvingirishwa; nalo lilikuwa kubwa mno.”
Na malaika yule hakuliviringisha jiwe karibu na mlango kama filamu zinavyoonesha…bali liliviringishwa mbali na kaburi.
Luka 24:1 “Hata siku ya kwanza ya juma, ilipoanza kupambazuka, walikwenda kaburini, wakiyaleta manukato waliyoweka tayari. 2 Wakalikuta lile jiwe limevingirishwa mbali na kaburi”
Luka 24:1 “Hata siku ya kwanza ya juma, ilipoanza kupambazuka, walikwenda kaburini, wakiyaleta manukato waliyoweka tayari.
2 Wakalikuta lile jiwe limevingirishwa mbali na kaburi”
Unaona ni mbali na kaburi..na si mbali na mlango …Ikiwa na maana kuwa lile jiwe lilihama kabisa kutoka katika yale mazingira ya makaburi.…jiwe walilikuta mbali kabisa, mahali ambapo hawakulitegemea…mahali ambapo si mazingira kabisa ya kusogezwa na mtu.
Kwahiyo Mungu aliruhusu liwe jiwe kubwa litumike, ili litakapoviringishwa mbali na kaburi..watu waamini kwamba hakika kuna kitu cha kimiujiza kimetendeka pale kaburini. Ni kweli Yesu kafufuka.
Na pia aliruhusu wale walinzi wawili wamwone yule malaika akishuka mbinguni kama umeme na waende kutoa habari za kufufuka kwake kwa wakuu wa makuhani (Mathayo 28:1-4)..maana pasingekuwepo mashuhuda upande wa makuhani pia, kungezuka uzushi mkubwa Zaidi ya ule uliozuka pale.
Sasa mambo hayo yote yalitokea ili sisi (mimi na wewe) tuamini kwamba ni kweli Yesu alisulubiwa, akafa na akafufuka kutoka katika wafu. Ukiamini hivyo leo hii basi utaokoka..Kama umeshawishika leo kuamini kwamba Kristo yupo hai leo, hayupo kaburini na kwamba anaweza kukuokoa maisha yako na wewe ukafufuka katika wafu… basi unachopaswa kufanya ni kutubu dhambi zako zote leo na kumwomba rehema..ulikuwa katika dhambi yeye anataka akusafishe na kukutakasa kwasababu anakupenda…
Upendo wake haupimiki wala haulinganishiki na kitu chochote..yupo tayari kukusamehe haijalishi umetenda dhambi ngapi kubwa..yeye atakusamehe zote na kusahau kabisa..na mbele zake utaonekana kama hujawahi kutenda dhambi kabisa….Sasa unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.
EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE,
NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.
Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithibitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, kama ulikuwa mwasherati usifanye tena uasherati, ulikuwa ni mtazamaji wa picha za ngono mitandaoni usifanye hivyo tena, ulikuwa mwizi, mtukanaji, mla rushwa, mtoaji mimba, muuaji, msagaji, mlawiti..usifanye hayo mambo tena…Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo namna hiyo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwabudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la BWANA YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.
Mungu akubariki, katika uamuzi wako wa busara unaoufanya..(huo ni uthibitisho wa kuamini kwamba Kristo amefufuka kweli kweli).
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789 001 312 jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
SAA YA KUHARIBIWA IIJIAYO ULIMWENGU WOTE.
Kwanini Mungu aliikubali sadaka ya Yeftha ya kumtoa binti yake kafara?
Kiungo chako kimoja kikikukosesha kikate.
FAHAMU ZA WATU HUWA ZINAONDOLEWA NA NINI?
Kwanini Bwana Yesu, aliruhusu yale mapepo yawaingie nguruwe?
IVUMBUE INJILI YA KRISTO KUTOKA KATIKA KILA JAMBO.
DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.
Kaini baada ya kumuua ndugu yake Habili, tunasoma pale Mungu alimlaani, na kumwambia.. “utakapoilima ardhi haitakupa mazao yake; utakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani”… Lakini tujiulize ni kwanini Mungu hakumrudishia Kaini mapigo ya uuwaji kama aliyoyafanya kwa ndugu yake badala yake akamwambia atakuwa mtu asiyekuwa na kikao duniani?.
Mwanzo 3:13 “Kaini akamwambia Bwana, Adhabu yangu imenikulia kubwa, haichukuliki. 14 Tazama, umenifukuza leo katika uso wa ardhi, nitasitirika mbali na uso wako, nami nitakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani; hata itakuwa kila anionaye ataniua”.
Mwanzo 3:13 “Kaini akamwambia Bwana, Adhabu yangu imenikulia kubwa, haichukuliki.
14 Tazama, umenifukuza leo katika uso wa ardhi, nitasitirika mbali na uso wako, nami nitakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani; hata itakuwa kila anionaye ataniua”.
Ndugu ni heri Mungu akuue, iishie hapo kuliko akuambie utakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani..
Sasa unaweza kutafsiri kwa nje kwamba laana hiyo ilimaanisha kuwa Maisha yake yote Kaini yatakuwa ya umaskini, atakuwa mtu atakayekosa mahali pa kulala, atakuwa omba omba, atakuwa mtu wa mitaani tu, lala hoi asiyekuwa na kitu au uelekeo wowote wa maisha…
Lakini sivyo hivyo Mungu alivyomaanisha kwa Kaini, angalia vizuri utagundua kuwa baada ya kutoka tu pale Kaini ndiye aliyekuwa na mafanikio makubwa sana kuliko hata ule uzao wa Sethi uliochukua mahali pa Habili. Mwanzoni tu pale tunaona alijenga mji mkubwa akauita Henoko jina la mwanawe(Mwanzo 4:17). Na tunaona pia uzao wake baada ya hapo, ulikuwa Hodari, ndio uliokuwa na ugunduzi wa hali ya juu wa teknolojia, vitu kama chuma na shaba zilianzia kwao.. Hivyo kwa ufupi Kaini alikuwa na mafanikio makubwa kuliko hata uzao wa Sethi tukizingumzia kwa namna ya kimwili…
Lakini bado laana ile ya Bwana kuwa atakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani ilikuwa juu yake..?
Sasa kama sio hivyo basi Mungu alimaanisha nini?. Sikuzote tunajua mtu mtoro asiye na kikao(makao) ni mtu ambaye hajapata pumziko lolote maishani mwake la kudumu..na ndio maana wanasema moja ya mahitaji makuu matatu ya mtu ni pamoja na kuwa na malazi, au makazi, ukikosa mahali pa kutulia, unakuwa kama mkimbizi ambaye Maisha yake sikuzote hayana pumziko, leo hii upo hapa kesho upo kule, kila mahali kwako sio kwako, ni mgeni daima..
Hivyo Mungu alivyomwambia Kaini kuwa atakuwa mtoro na mtu asiyekuwa na makao, alikuwa anazungumzia hali yake ya rohoni jinsi itakavyokuwa, Maisha yake yote atakuwa ni mtu wa kutafuta lakini hatopata makazi ya kustarehe ya nafsi yake….hatapata pumziko la moyo wake daima..hatopata, hata atufuteje hatoona atakuwa ni huko na kule, wimbi la bahari linalochukuliwa na upepo wa kila aina ya undanganyifu … jambo ambalo halikuonekana kwa Sethi na uzao wake, wao utaona tu muda mchache baada ya kumzaa mtoto wake Jina la Mungu lilianza kuitwa kwa nguvu.
Mwanzo 4:25 “Adamu akamjua mke wake tena; akazaa mwana mwanamume, akamwita jina lake Sethi; maana alisema, Mungu ameniwekea uzao mwingine mahali pa Habili; kwa sababu Kaini alimwua. 26 Sethi naye akazaa mwana; akamwita jina lake Enoshi. Hapo ndipo watu walipoanza kuliitia Jina la Bwana”.
Mwanzo 4:25 “Adamu akamjua mke wake tena; akazaa mwana mwanamume, akamwita jina lake Sethi; maana alisema, Mungu ameniwekea uzao mwingine mahali pa Habili; kwa sababu Kaini alimwua.
26 Sethi naye akazaa mwana; akamwita jina lake Enoshi. Hapo ndipo watu walipoanza kuliitia Jina la Bwana”.
Unaona? Muda mfupi tu uzao wa Sethi ulitambua ni wapi pumziko lipo, na haraka sana likayaendea makao ya kudumu ya roho zao.. Lakini uzao wa Kaini uliendelea kutangatanga na ulimwenguni na humo humo ndipo uchawi ukazaliwa, uovu ukazaliwa, uvuguvugu ukazaliwa, udunia ukazaliwa..n.k.
Hata leo hii, uzao wa Kaini na Sethi unajitambulisha kabisa kwa kazi zake..makundi yote mawili yapo duniani leo hii, lipo ambalo limeshatambua makao yao ya kudumu yapo wapi..Hawa ndio wale waliompokea Yesu Kristo na kupokea lile pumziko la kweli la nafsi zao.
Mathayo 11:28 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha. 29 Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu; 30 kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi”.
Mathayo 11:28 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.
29 Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;
30 kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi”.
Utawagundua kwa tabia zao, hata wakipitia dhiki, au shida, au misiba, au adha, hawapepesuki, kwasababu wanajua tayari yanayo makao yao ya kudumu milele mbinguni…hawana hofu ya Maisha kwasababu wanaye Kristo ndani yao….Amani ya Kristo inawatawala siku zote kwasababu walishampokea.
Lakini uzao ule mwingine wa Kaini kwasababu umeshalaaniwa ndio ule hautaki kumfuata Mungu japo unajijua kabisa unahitaji msaada wa nafsi zao..Huu upo buzy sikuzote kutafuta pumziko la nafsi zao katika kila wanachokiona, kama vile Kaini….Wana wa Kaini walioa wake wengi, na hawa wanatafuta pumziko kwa kuongeza idadi ya wake, (Mwanzo 4:19) na wakati mwingine kuacha wale walio nao na kuoa wengine. Roho zao zinazunguka zunguka kutafuta maana ya Maisha lakini haziwezi kuona kwasababu hazijui kuwa Maisha yapo katika Kristo tu peke yake..
Hawa tayari walishalaaniwa kama Kaini. Haijalishi wana mali au umaskini kiasi gani, bado wapo chini ya laana.
Swali ni je! Na wewe upo kundi lipi?. Ikiwa unasikia injili hutaki kuitii, ikiwa unahubiriwa habari za uhuru ulio katika YESU KRISTO halafu hutaki kuupokea basi fahamu kuwa Mungu hatakuua kama jinsi ambavyo hakumuua Kaini bali atakuacha uendelee na mambo yako ya kidunia ufanikiwe, uwe milionea, uwe mtu mashuhuri duniani, ujenge miji mikubwa kama ya Kaini uwe mgunduzi mpaka upokee tuzo za Nobeli lakini, rohoni uwe mtoro na mtu asiyekuwa na kikao duniani..
Utakuja kulithibitisha hilo siku ile umekufa, siku ile mwenzako wanatoka makubirini na unaowaona wanapewa miili mipya ya utukufu wanakwenda kuishi na Kristo milele katika majumba waliyoandaliwa kule mbinguni, wewe utakuwa huna kao lolote..bali mwisho wako utakuwa palepale kwenye lile ziwa la moto.
Hizi ni nyakati za mwisho mpendwa. Siku yoyote hapa paraparanda italia, mahubiri haya hatutayasikia tena, mavuno yataisha shambani, utakuwa ni wakati mwingine wa kuanza Maisha mapya ya umilele…Je utaimalizia umilele yako wapi? Jehanamu ya moto kwenye mauti ya milele au mbinguni?
Ni maombi yangu kuwa utatubu dhambi zako leo, ikiwa bado upo nje ya Kristo.. Umetanga tanga vya kutosha huu ni wakati wako sasa wa kutia nanga Kwa Kristo..kwasababu yeye ndio KAO LETU, na PUMZIKO LETU LA KWELI. Zingatia kurudi kwa Baba sawasawa na mfano ule wa mwana mpotevu Bwana alioutoa katika..(Luka 15:11-24)
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
WANA WA MUNGU, NA BINTI ZA WANADAMU.
MUNGU AKIKUPITA LEO, HAIMAANISHI KUWA HAJAKUCHAGUA.
TAZAMA, MWISRAELI KWELI KWELI, HAMNA HILA NDANI YAKE!
UMUHIMU WA YESU KWETU.
MADHABAHU NI NINI?
Je! vitabu vya biblia viliwezaje kukusanywa pamoja?
Je! Ni wakina nani hao katika (Mathayo 16:28) ambao Bwana alisema hawataonja mauti mpaka atakapokuja?
JIBU: Tusome..
Mathayo 16:27 “Kwa sababu Mwana wa Adamu atakuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika zake; ndipo atakapomlipa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake. 28 Amin, nawaambieni, Pana watu katika hawa wasimamao hapa, ambao hawataonja mauti kabisa, hata watakapomwona Mwana wa Adamu akija katika ufalme wake”
Mathayo 16:27 “Kwa sababu Mwana wa Adamu atakuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika zake; ndipo atakapomlipa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake.
28 Amin, nawaambieni, Pana watu katika hawa wasimamao hapa, ambao hawataonja mauti kabisa, hata watakapomwona Mwana wa Adamu akija katika ufalme wake”
Katika sentensi hiyo tunaona Bwana alikuwa anazungumza habari za kuja kwake jinsi kutakavyokuwa kwamba atakuja katika utukufu wa Baba yake na malaika zake na kufanya hukumu…Lakini wakati anazungumza maneno hayo akaongezea na sentensi moja ya kipekee sana kwamba “kuna watu ambao wamesimama naye pale wakati anaongea nao ambao hawataonja mauti hata watakapomwona Mwana wa Adamu akija katika ufalme wake”.
Sasa ukianzia juu tena kidogo utaona kuwa Bwana Yesu hakuwa anazungumza maneno hayo mbele ya makutano..utagundua alikuwa anazungumza na wanafunzi wake 12 tu!..Kumbuka si mambo yote Bwana alikuwa anazungumza mbele ya makutano..kuna mambo alikuwa anazungumza mbele ya watu wote na kuna ambayo alikuwa anazungumza na wanafunzi wake tu!..Sasa mojawapo ya aliyokuwa anazungumza na wanafunzi wake tu ndilo hili kwamba “wapo ambao hawataonja mauti mpaka watakapomwona anakuja”…Maana yake ni kwamba miongoni mwa wale wanafunzi 12, kuna ambao hawataonja mauti kabisa.
Sasa swali la kujiuliza ni kweli Bwana alikuwa anamaanisha hivyo kwamba wapo ambao hawatakufa kabisa au alikuwa anamaanisha vingine?
Biblia inataja baadhi ya mitume walikufa..na historia pia inathibitisha vifo vya mitume wengine wote waliosalia…Hivyo hakuna mtume hata Mtume mmoja ambaye hakufa…Kwahiyo maana yake Bwana pale hakumaanisha kuwa hawatakufa kabisa kabla ya kushuhudia kuja kwake kwa mara ya pili(Ingawa huo uwezo wa kumfanya mtu asife kabisa hata atakapokuja anao lakini kwa pale hakumaanisha vile)..Bali alikuwa anamaanisha kuwa wapo ambao hawatakufa mpaka “watakapoonyeshwa jinsi atakavyokuja katika utukufu wake siku za mwisho”..Na kuonyeshwa huko si kwingine bali kwa njia ya maono ya wazi kabisa…Yapo maono yanayokuja kwa mfumo wa ndoto, na yapo yanayokuja kwa njia ya dhahiri kabisa…Haya ya Dhahiri mara nyingine yanajumuisha watu Zaidi ya mmoja wanaona kitu kinachofanana kwa wakati mmoja…lakini pia hayo mengine mara nyingi yanamtokea mtu mmoja mmoja na yanakuwa kwa mfumo kama wa ndoto.
Sasa ni lini walionyeshwa maono hayo ya kuja kwa Bwana kwa nguvu na utukufu?
Ukishuka kidogo sura inayofuata mstari wa kwanza biblia inasema…
Mathayo 17:1 “Na baada ya siku sita Yesu akawatwaa Petro, na Yakobo, na Yohana nduguye, akawaleta juu ya mlima mrefu faraghani; 2 akageuka sura yake mbele yao; uso wake ukang’aa kama jua, mavazi yake yakawa meupe kama nuru. 3 Na tazama, wakatokewa na Musa na Eliya, wakizungumza naye. 4 Petro akajibu akamwambia Yesu, Bwana, ni vizuri sisi kuwapo hapa; ukitaka, nitafanya hapa vibanda vitatu, kimoja chako wewe, na kimoja cha Musa, na kimoja cha Eliya. 5 Alipokuwa katika kusema, tazama, wingu jeupe likawatia uvuli; na tazama, sauti ikatoka katika lile wingu, ikasema, Huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, ninayependezwa naye; msikieni yeye. 6 Na wale wanafunzi waliposikia, walianguka kifulifuli, wakaogopa sana. 7 Yesu akaja, akawagusa, akasema, Inukeni, wala msiogope. 8 Wakainua macho yao, wasione mtu ila Yesu peke yake. 9 Na walipokuwa wakishuka mlimani, Yesu aliwaagiza, akasema, Msimwambie mtu ye yote habari ya maono hayo, hata Mwana wa Adamu atakapofufuka katika wafu”
Mathayo 17:1 “Na baada ya siku sita Yesu akawatwaa Petro, na Yakobo, na Yohana nduguye, akawaleta juu ya mlima mrefu faraghani;
2 akageuka sura yake mbele yao; uso wake ukang’aa kama jua, mavazi yake yakawa meupe kama nuru.
3 Na tazama, wakatokewa na Musa na Eliya, wakizungumza naye.
4 Petro akajibu akamwambia Yesu, Bwana, ni vizuri sisi kuwapo hapa; ukitaka, nitafanya hapa vibanda vitatu, kimoja chako wewe, na kimoja cha Musa, na kimoja cha Eliya.
5 Alipokuwa katika kusema, tazama, wingu jeupe likawatia uvuli; na tazama, sauti ikatoka katika lile wingu, ikasema, Huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, ninayependezwa naye; msikieni yeye.
6 Na wale wanafunzi waliposikia, walianguka kifulifuli, wakaogopa sana.
7 Yesu akaja, akawagusa, akasema, Inukeni, wala msiogope.
8 Wakainua macho yao, wasione mtu ila Yesu peke yake.
9 Na walipokuwa wakishuka mlimani, Yesu aliwaagiza, akasema, Msimwambie mtu ye yote habari ya maono hayo, hata Mwana wa Adamu atakapofufuka katika wafu”
Umeona hapo mstari wa 2 unasema “AKAGEUKA SURA YAKE MBELE YAO; USO WAKE UKANG’AA KAMA JUA, MAVAZI YAKE YAKAWA MEUPE KAMA NURU.” Huo ndio utukufu ambao atakuja nao mwana wa Adamu siku za mwisho…ambapo kila jicho litamwona wakati huo uso wake utakuwa unang’aa kama jua, na mavazi yake yatakuwa meupi kama Nuru..Mataifa yote wataanguka chini na kuomboleza…naye atawahukumu waovu…
Kwahiyo hawa mitume watatu kati ya wale 12, ndio waliopata neema hiyo/bahati hiyo kuuona utukufu huo wa kuja kwa Yesu kabla hawajafa, na hivyo Neno la Yesu likatimia hapo kwamba wameuona utukufu wake kabla hawajafa. Na haikumaanisha kwamba wataendelea kuwa hai mpaka watakapomwona akija mara ya pili atakapotokea mawinguni hapana!….watakaomwona akitokea mawinguni kwa utukufu huo ni wale wote watakaokuwa wameachwa katika unyakuo, ambao wamebaki duniani na kuipokea chapa…lakini watakatifu wakati huo watakuwa wameshanyakuliwa na watakuja pamoja na Kristo siku hiyo ya utukufu wake…
Sasa tutazidi kujuaje kama hayo yote ni kweli?..Biblia inasema kwa vinywa vya mashahidi wawili, watatu kila neno lithibitike.
Tunaona tena Petro akilishuhudia jambo hilo…Jinsi alivyoona kuja kwake..
Tusome..
2Petro 1:16 “Maana hatukufuata hadithi zilizotungwa kwa werevu, tulipowajulisha ninyi nguvu zake Bwana wetu Yesu Kristo na KUJA KWAKE; bali tulikuwa tumeuona wenyewe ukuu wake. 17 Maana alipata kwa Mungu Baba heshima na utukufu, hapo alipoletewa sauti iliyotoka katika utukufu mkuu, Huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, ninayependezwa naye. 18 Na sauti hiyo sisi tuliisikia ikitoka mbinguni tulipokuwa pamoja naye katika mlima ule mtakatifu.”.
2Petro 1:16 “Maana hatukufuata hadithi zilizotungwa kwa werevu, tulipowajulisha ninyi nguvu zake Bwana wetu Yesu Kristo na KUJA KWAKE; bali tulikuwa tumeuona wenyewe ukuu wake.
17 Maana alipata kwa Mungu Baba heshima na utukufu, hapo alipoletewa sauti iliyotoka katika utukufu mkuu, Huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, ninayependezwa naye.
18 Na sauti hiyo sisi tuliisikia ikitoka mbinguni tulipokuwa pamoja naye katika mlima ule mtakatifu.”.
Uonaona hapo?..anasema hatukuhadithiwa na mtu kuhusu nguvu zake na KUJA KWAKE..(maana yake siku ile mlimani yeye pamoja na Yohana na Yakobo walionyeshwa KUJA KWAKE) na walishuhudia wenyewe.
Bwana akubariki sana.
SIKU ILE NA SAA ILE.
Shetani anatolea wapi fedha, angali tunajua Fedha na dhahabu ni mali ya Bwana?.
TAFUTA KUJUA MAMBO YAJAYO
Kuna tofauti gani kati ya SALA na DUA?
MAJINI WAZURI WAPO?
IPO NGUVU ITUVUTAYO KWA KRISTO, ITHAMINI!.
Historia fupi ya Rozari kama inavyosomwa na kanisa katoliki.(kulingana na wakatoliki inajulikana kama Rozari takatifu)
Rozari asili yake ni neno la kiingereza “rosary” lenye maana ya “bustani ya maua ya waridi”…Maua ya Rose kwa kiingereza ndio yanaitwa “waridi”..Kwahiyo bustani yake ndio inayoitwa rosary.
Katika sehemu za Ulaya kuna utaratibu wa kupelekeana maua hayo ya waridi ni kama ishara ya kuonyeshana upendo (Ingawa upendo halisi hauwakilishwi kwa maua)…
Hivyo yapo maua hayo ya waridi yaliyo ya rangi ya nyekundu na Nyeupe. Hivyo wakatoliki wanaamini kuwa Maria ni mama mtakatifu kwao, hivyo anastahili kupelekewa mfano wa ua hilo la waridi..na Hivyo sala ya rozari ndio kama ishara ya kumpelekea mama huyo ua hilo jeupe la Waridi kama ishara ya upendo wao kwake.
Sasa Historia ya hiyo sala ya rozari takatifu kwa wakatoliki ilianzia wapi?
Ilianzia karne ya 3 ambapo kulikuwa na watu wanaojulikana kama wahermiti kulingana na Wakatoliki. Watu hawa waliamua kuwa wanasoma kitabu cha Zaburi kila siku SURA ZOTE 150. Lakini baadaye wakazipunguza na kukusudia kusoma sura zote 150 kwa muda wa wiki moja.
Kwa kuwa walikuwa ni watu wasio na elimu, walitumia mbegu ndogo za mimea kuwakilisha kila zaburi moja wanayoisoma..Hivyo wakawa na mbegu 150, kwa idadi ya zaburi zote 150, hivyo kila walipokuwa wanamaliza kusoma zaburi moja waliweka mbegu moja katika kapu ili iweze kuwasaidia kujua wapo zaburi ya ngapi..n.k
Baadaye kulingana na kanisa katoliki, wanasema watu hao majirani zao walivutiwa na sala hiyo ya zaburi, na wao pia wakaanza sala kama hiyo lakini wakawa wanasali sala ya “Baba yetu uliye mbinguni” mara 150, badala hiyo ya Zaburi.
Baadaye tena wakabadilika na kuanza kutumia shanga 150 zilizopitishwa kwenye kamba badala ya vimbegu vidogo vya mimea walivyokuwa wanavitumia hapo kabla.
Ilipofika karne ya 11 kadinali wa kikatoliki Mt. Peter Damiani, aliibadilisha sala hiyo kutoka katika kusali “Baba yetu uliye mbinguni” mara 150…Na kuwa “salamu Maria” mara 150.
Baadaye tena akatokea kiongozi mwingine wa kikatoliki akazigawanya hizo sala katika makundi 15..na kila baada ya salamu Maria 10 aliiweka Baba yetu uliye mbinguni…ikiwa vile vile kamba yenye vishanga 150.
Baada ya kipindi fulani tena wakavipunguza vile vishanga na kubakia vishanga 50 tu. Hivyo ndio mpaka leo wanasali rozari yenye vishanga hivyo 50.
Lakini Je jambo hilo ni la kimaandiko?
Jibu ni la! Si la kimaandiko kwasababu hakuna sehemu yoyote katika maandiko tumeagizwa tusali sala ya “Salamu Maria”. Kwasababu Maria si mtu anayetuombea..yeye alishakufa, wafu wote hawana habari na mambo ya maisha yetu haya…..Anayetuombea ni mmoja tu biblia imemtaja ambaye ni ROHO MTAKATIFU.
Warumi 8:26 “Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu, kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo, lakini Roho mwenyewe hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa”.
Umeona? ni Roho Mtakatifu na si Bikira Maria. Na Roho Mtakatifu hatumuombi atuombee na kusema “Salamu Roho Mtakatifu tunaomba utuombee”..hapana Roho Mtakatifu anatuombea pale na sisi tunapoomba..aidha kwa kunena kwa lugha au kwa maneno dhahiri..Yeye ni kama Mkalimani wetu mbele za Mungu. Mkalimani hawezi kuzungumza kama wewe huzungumzi.n.k
Hivyo sala yoyote inayohusisha kumwomba Mtakatifu fulani aliyekufa atuombee ni sala ya upotofu..inayowafumba watu macho na kuwafanya wawe wavivu wa kuomba wenyewe na kutamani kila wakati kuombewa tu! Na mtu anayesali sala hiyo anamwabudu shetani bila yeye kujijua.
Hali kadhalika sala halisi inatoka ndani ya Moyo, na si desturi au utaratibu fulani au fomula fulani ya kufuata. Unapotumia mfumo fulani wa kuhesabu shanga na kutimiza idadi fulani ya maneno..hapo utakuwa husali chochote zaidi ya kutimiza wajibu tu..Na hatuendi kumwomba Mungu ili kutimiza wajibu..Mungu anataka ibada halisi inayotoka ndani ya moyo wa mtu hata kama itamchukua mtu maneno machache lakini maadamu imetoka katika moyo uliomiminika mbele zake..hiyo inathamani kubwa sana mbele za Mungu kuliko maneno elfu yasiyo na maana.
Ukitumia mfumo fulani bila kuomba kwa Roho ni sawa na umemwekea Mungu baba, nyimbo zilizorekodiwa katika kaseti azisikilize afurahi..Umeona? ukifanya hivyo ni kumdharau Mungu..anachotaka kutoka kwetu ni nyimbo zinazotoka ndani ya vinywa vyetu zinazotoka moyoni..na sio nyimbo zilizorekodiwa…Kadhalika na sala anataka zinazotoka mioyoni mwetu na si zinazojirudia rudia kama kaseti.
Hivyo kwa hitimisho..sala ya Rozari si sala ya kimaandiko..Imebuniwa na Shetani, na lengo lake ni kuwaharibu watu kiroho. Hivyo kama upo huko ndugu..toka haraka sana!..Anza kumwabudu Mungu leo katika Roho na Kweli..Tupa hiyo rozari usiisali tena…umeshaujua ukweli, na pia washirikishe wengine wasiojua ukweli huu..
Hizi ni nyakati za mwisho shetani anatumia kila namna kuwazuia watu wasiijue kweli. Na anawatumia watumishi wake ambao kwa nje wanaonekana ni watakatifu, wanaonekana ni watumishi wa Mungu kumbe ndani ni Mmbwa mwitu wakali.
Ikiwa bado hujaokoka na unatamani kuokoka basi hujachelewa..kumbuka kuokoka sio dini mpya..bali ni kitendo cha kumpokea Yesu maishani mwako na kufanyika kiumbe kipya..kumkiri kwamba yeye pekee ndiye njia ya kweli na mpatanishiwa wa Mungu na wanadamu. Ukimkiri namna hiyo na kudhamiria kuacha dhambi kwa vitendo na kujikana nafsi yako na kumfuata yeye…ataingia moyoni mwako na kukubadilisha na kukufanya kuwa kiumbe kipya. Hivyo tubu na baada ya kutubu nenda katafute ubatizo sahihi wa kimaandiko wa kuzamishwa katika maji tele (Yohana 3:23) na kwa Jina la Yesu Kristo.
Ubarikiwe.
ROHO HUTUOMBEA KWA KUUGUA KUSIKOWEZA KUTAMKWA!
UPAKO NI NINI?
SAKRAMENTI NI NINI, NA JE! IPO KATIKA MAANDIKO?
LITANIA YA BIKIRA MARIA JE! NI SALA YA KIMAANDIKO?
Je! Bikira Maria ni MALKIA WA MBINGUNI?
JE BIKIRA MARIAMU ALIZAA WATOTO WENGINE?
Ni sahihi kumuita Mariamu mama wa Mungu?
SWALI: Ndugu zangu Huyu Mariamu MAGDALENE ni nani?”..Je! Magdene ni jina la baba yake au ni Jina la ukoo wake?.
JIBU:
Mariamu Magdalene( wengine wanamwita Magdalena) ni yule mwanamke ambaye tunamwona kwenye biblia akitolewa pepo saba na Bwana Yesu..
Luka 8:2 “na wanawake kadha wa kadha ambao walikuwa na pepo wabaya na magonjwa wakaponywa; nao ni Mariamu aitwaye Magdalene aliyetokwa na pepo saba, 3 na Yoana mkewe Kuza, wakili wake Herode, na Susana, na wengine wengi, waliokuwa wakimhudumia kwa mali zao. “
Luka 8:2 “na wanawake kadha wa kadha ambao walikuwa na pepo wabaya na magonjwa wakaponywa; nao ni Mariamu aitwaye Magdalene aliyetokwa na pepo saba,
3 na Yoana mkewe Kuza, wakili wake Herode, na Susana, na wengine wengi, waliokuwa wakimhudumia kwa mali zao. “
Ni mwanamke aliyefuata na Bwana Yesu tangu huo wakati hadi mwisho wa huduma yake ambaye yeye pamoja na wenzake, ndio waliokuwa wanamuhudumia Bwana kwa mali zao.
Mariam Magdalene tunamwona tena siku za mwisho mwisho kabisa kabla za Bwana Yesu kupaa yeye ndiye aliyeagizwa kwenda kuwaeleza wanafunzi wake juu ya kufufuka kwake.
Yohana 20:11 “Lakini Mariamu alikuwa akisimama karibu na kaburi, nje yake, analia. Basi akilia hivi, aliinama na kuchungulia ndani ya kaburi. 2 12 Akaona malaika wawili, wenye mavazi meupe, wameketi, mmoja kichwani na mmoja miguuni, hapo ulipolazwa mwili wake Yesu. 13 Nao wakamwambia, Mama, unalilia nini? Akawaambia, Kwa sababu wamemwondoa Bwana wangu, wala mimi sijui walikomweka. 14 Naye akiisha kusema hayo, akageuka nyuma, akamwona Yesu amesimama, asijue ya kuwa ni Yesu. 15 Yesu akamwambia, Mama, unalilia nini? Unamtafuta nani? Naye, huku akidhania ya kuwa ni mtunza bustani, akamwambia, Bwana, ikiwa umemchukua wewe, uniambie ulipomweka, nami nitamwondoa. 16 Yesu akamwambia, Mariamu. Yeye akageuka, akamwambia kwa Kiebrania, Raboni! (Yaani, Mwalimu wangu). 17 Yesu akamwambia. Usinishike; kwa maana sijapaa kwenda kwa Baba. Lakini enenda kwa ndugu zangu ukawaambie, Ninapaa kwenda kwa Baba yangu naye ni Baba yenu, kwa Mungu wangu naye ni Mungu wenu. 18 Mariamu Magdalene akaenda, akawapasha wanafunzi habari ya kwamba, Nimemwona Bwana, na ya kwamba amemwambia hayo”.
Yohana 20:11 “Lakini Mariamu alikuwa akisimama karibu na kaburi, nje yake, analia. Basi akilia hivi, aliinama na kuchungulia ndani ya kaburi. 2
12 Akaona malaika wawili, wenye mavazi meupe, wameketi, mmoja kichwani na mmoja miguuni, hapo ulipolazwa mwili wake Yesu.
13 Nao wakamwambia, Mama, unalilia nini? Akawaambia, Kwa sababu wamemwondoa Bwana wangu, wala mimi sijui walikomweka.
14 Naye akiisha kusema hayo, akageuka nyuma, akamwona Yesu amesimama, asijue ya kuwa ni Yesu.
15 Yesu akamwambia, Mama, unalilia nini? Unamtafuta nani? Naye, huku akidhania ya kuwa ni mtunza bustani, akamwambia, Bwana, ikiwa umemchukua wewe, uniambie ulipomweka, nami nitamwondoa.
16 Yesu akamwambia, Mariamu. Yeye akageuka, akamwambia kwa Kiebrania, Raboni! (Yaani, Mwalimu wangu).
17 Yesu akamwambia. Usinishike; kwa maana sijapaa kwenda kwa Baba. Lakini enenda kwa ndugu zangu ukawaambie, Ninapaa kwenda kwa Baba yangu naye ni Baba yenu, kwa Mungu wangu naye ni Mungu wenu.
18 Mariamu Magdalene akaenda, akawapasha wanafunzi habari ya kwamba, Nimemwona Bwana, na ya kwamba amemwambia hayo”.
Na kuhusu Hilo jina la Magdalene sio jina la baba yake, au la ukoo wake, Hapana aliitwa Mariamu Magdalene kuonyesha asili yake tu, ili kumtofautisha na Mariamu wengine kwenye biblia…Kumbuka hili jina Mariamu limetumika mara nyingi kwenye biblia..Hivyo ili kuwatofautisha hawa Mariam wote, huyu aliitwa mariamu Magdalene kuonyesha na Mariam aliyetokea huko mji wa MAGDALENE uliokuwa kando kando magharibi mwa bahari ya Galilaya huko Israeli. Lakini hilo sio jina la Baba yake au ukoo wake..Hapana ni jina la mji aliotokea.
Ni kama tu yule mwanamke Msamaria, hilo jina Msamaria sio jina la baba yake, hapana bali ni jina la mji anaotokea unaoitwa SAMARIA uliopo katikati ya Israeli.
Pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312
RABONI!
Kwanini wanawake wengi huwa wanalipuka mapepo?
JINA LA MUNGU NI LIPI?
Je! ni vema kwa mkristo kwenda hospitali au kutumia miti shamba anapougua?
Tofauti ya kazi ya Damu ya Yesu na Jina la Yesu ni ipi?