Title 2020

Ni vitu vipi hivyo viwili visivyoweza kubadilika? (Ebr 6:18)

SWALI: Naomba kuuliza, huu mstari una maana gani? “..VITU VIWILI visivyoweza kubadilika ambavyo kwa hivyo Mungu hawezi kusema uongo”?! (Waebrania 6:18).


JIBU: Shalom..

Tusome…

Waebrania 6:17  “Katika neno hilo Mungu, akitaka kuwaonyesha zaidi sana warithio ile ahadi, jinsi mashauri yake yasivyoweza kubadilika, alitia kiapo katikati;

18  ili kwa vitu viwili visivyoweza kubadilika, ambavyo katika hivyo Mungu hawezi kusema uongo”

Kama ukianza kusoma kuanzia  mstari wa 13 kwa umakini, mpaka mstari wa 18, utajua kuwa Vitu hivyo viwili visivyoweza kubadilika ni AHADI YAKE na KIAPO CHAKE.

Hivyo ndio vitu viwili pekee vya Mungu visivyoweza kubadilisha Neno la Mtu.

Kwa mfano katika Maisha ya kawaida, Mtu akitaka kuthibitisha neno lake Huwa anatoa Ahadi..Kwamfano unaweza kumwambia mtu nitakuja kesho kukutembelea…Na yule mtu ili kupata uhakika zaidi na kwamba hutamdanganya ataweza kukuambia “embu niahidi”..na wewe utamwahidi…Na ili kupata uthitisho ulio mkubwa zaidi anaweza pia kukuambia “hebu Niapie kwamba utakuja”..

Maana yake kwa ahadi uliyomuahidi, na kiapo ulichomwapia…Ni ngumu wewe kuwa umemdanganya! Ni lazima utamtembelea tu kwa vyovyote vile hiyo siku ya kesho, Na hata kama kikitokea kitu ambacho kitazuia safari hiyo, utakapokumbuka kwamba ulishatoa ahadi, na tena ulishaapa, basi unajikuta unatimiza ahadi yako kwa gharama zozote zile.. (Sasa huo ni mfano tu, sisi wakristo haturuhusiwi kuapa).

Vivyo hivyo Mungu, ili kutuhakikishia kuwa Neno lake ni kweli…Neno hilo kaligeuza na kuwa Ahadi, na hajaishia tu kulifanya kuwa ahadi, bali kaenda mbele Zaidi kaliapia…ili kwa vitu hivyo viwili, (Ahadi na kiapo) atuhakikishie sisi Watoto wake kwamba yeye si MWONGO, Maana yake ni lazima atalitimiza tu neno lake alilolitamka kutoka katika kinywa chake.

Ndio maana Mtume Paulo hapo, anachukua mfano wa Ibrahimu, jinsi Mungu alivyolithibitisha Neno lake kwa kumwapia zile ahadi alizompa.

Waebrania 6:13  “Kwa maana Mungu, alipompa Ibrahimu ahadi, kwa sababu alikuwa hana mkubwa kuliko yeye mwenyewe wa kumwapa, aliapa kwa nafsi yake,

14  akisema, Hakika yangu kubariki nitakubariki, na kuongeza nitakuongeza”.

Hivyo Neno la Mungu limehakikiwa kwa “ahadi na kiapo”…kwamfano aliposema kwenye Neno lake

Yohana 16:23b “… Amin, amin, nawaambia, Mkimwomba Baba neno lo lote atawapa kwa jina langu”.

Hapo mzizi wa hilo neno ni kwamba “tumwombe Baba” basi, lakini Bwana Yesu akituambia tumwombe tu Baba bila kutupa ahadi yoyote, tusingeamini kwamba tutapata majibu..Hivyo ili kulithibitisha hilo neno, akaongezea mbele yake ya kwamba “tukimwomba atatupa”…hilo neno “atatupa” tayari ni Ahadi…. Lakini hajaishia hapo ili kulithibitisha kuwa hajatudanganya akaongezea na kiapo juu yake na kuanza kwa kusema “Amin…Amin nawaambia”..tukimwomba Baba kwa jina lake atatupatia.

Hivyo tunapomwomba Baba popote pale, tufahamu kuwa ni haki yetu kupokea majibu yetu kama tumeomba sawasawa na mapenzi yake…hajatudanganya!, kwasababu katupa ahadi na kiapo..

Unaweza pia kusoma maneno mengine mfano ya hayo, kwa kuongeza maarifa, kasome Yohana 14:12, Luka 18:29-30.

Zaburi 138:2b “….Kwa maana umeikuza ahadi yako, Kuliko jina lako lote”

Bwana atubariki.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618

Mada Nyinginezo:

Kwanini madhabahu zilitengenezwa kwa mawe yasiyochongwa?

SIFONGO NA SIKI NI NINI?

ROHO MBAYA KUTOKA KWA BWANA.

Mount Gerizim and Mount Ebal: Their Meaning and Spiritual Significance

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Kwanini madhabahu zilitengenezwa kwa mawe yasiyochongwa?

SWALI: Kwanini Musa aliagizwa awaambie wana wa Israeli watengeneze madhabahu kwa mawe yasiyochongwa? Kwanini yawe mawe yasiyochongwa?


JIBU: Tusome vifungu vyenyewe;

Kutoka 20:24 “….. kila mahali nitakapotia ukumbusho wa jina langu, hapo ndipo nitakapokujilia na kukubarikia.

25 Nawe ukinifanyia madhabahu ya mawe, hutaijenga ya mawe yaliyochongwa; kwa kuwa ukiwa wewe umetumia chombo chako katika kuichonga umeitia unajisi”.

Kumbukumbu 27:5 “Na huko umjengee madhabahu Bwana, Mungu wako, madhabahu ya mawe, usitumie chombo cha chuma juu yake.

6 Jenga hiyo madhabahu ya Bwana, Mungu wako, kwa mawe yasiyochongwa; ukamtolee Bwana, Mungu wako, sadaka za kuteketezwa juu yake;

7 ufanye na sadaka za amani, ukale huko; nawe furahi mbele za Bwana, Mungu wako”.

Yoshua 8:30 “Ndipo Yoshua alijenga madhabahu kwa Bwana, Mungu wa Israeli katika mlima Ebali.

31 Kama Musa, mtumishi wa Bwana, alivyowaamuru wana wa Israeli, kama ilivyoandikwa katika kitabu cha torati ya Musa, madhabahu ya mawe yasiyochongwa, ambayo mtu hakutumia juu yake chombo cha chuma; nao wakatoa juu yake sadaka za kuteketezwa kwa Bwana, na kuchinja sadaka za amani”.

Shalom,

Madhabahu sikuzote inasimama kama kiunganishi cha kufikisha maombi yetu, dua zetu, sadaka zetu na shukrani zetu kwa Mungu, na pia inasimama kama nyenzo ya sisi kuwasiliana na Mungu. Ni kama tu mnara wa simu, mahali ambapo hapana mnara unaorusha mawimbi ya sauti mbali, kamwe hatuwezi kuwasiliana haijalishi simu zetu zitakuwa za kisasa kiasi gani.

Sasa kwenye agano la kale madhabahu zilikuwa zinatengenezwa kwa kupanga mawe kuanzia chini, mpaka kimo fulani, na kisha juu ya mawe hayo zinapangwa kuni kavu, na juu ya kuni hizo panawekwa sadaka ya kuteketezwa ambayo ilikuwa ni aidha Wanyama au ndege, na sadaka hiyo inachomwa na moshi kupanga juu..

Hivyo katika agano la kale Wana wa Israeli walipewa maagizo kwamba mahali popote atakapopachagua Mungu ili wamjengee  madhabahu ya mawe ni sharti kwamba wasitumie ujuzi wao katika kuitengeneza, hii ikiwa na maana kuwa wakikutana na jiwe ambalo limezidi kimo kidogo katika ujenzi wao, walitumie hilo hilo, wasilichonge kulipunguza, wakikutana na lilililopungua vilevile walitumie hilo hilo, wasilichonge wala kulipiga nyundo, vinginevyo madhabahu hiyo itakuwa batili.

Sasa hicho kilikuwa ni kivuli cha jinsi madhabahu halisi ya Mungu itakavyokuja kujengwa katika agano jipya. Mungu aliwapa maagizo hayo kufunua madhabahu halisi ya agano lililo bora itakavyokuja kuwa.

Na YESU KRISTO ndiye madhabahu yetu kwasasa. Yeye ndio kiunganishi chetu sisi na Mungu.

Na tunamuunda kama madhabahu yetu kwa namna mbili;

Namna ya kwanza ni pale tunapokuwa kanisani, tunapokusanyika pamoja sisi tuliookoka, sasa kule kuja pamoja ni sawa na tunavileta viungo vyote sehemu moja na hapo mwili wa Kristo unaumbika, na Kristo mwenyewe anakuwepo, na madhabahu inatokea, Hivyo tunapokutanika ni wajibu wetu kujua kuwa karama zinatolewa na Mungu mwenyewe na si wanadamu..Pale tunapozizuia karama za Roho kujidhihirisha katikati ya viungo vya Kristo (mawe), badala yake tukaweka uongozi ambao tunaouna unafaa mbele ya macho yetu wenyewe na si mbele za Mungu, tunaweka vyeo vya kibinadamu vituongoze, vyeo vya kisiasa n.k…ni sawa na tumechonga mawe hayo wenyewe, na hivyo madhabahu hiyo inakuwa najisi mbele za Mungu. Uweza wa Mungu haushuki mahali hapo.

Na namna ya pili  ni tunaijenga sisi wenyewe (binafsi),

Pale tunapokuwa peke yatu aidha nyumbani, au mahali pa utulivu kuwasiliana na Mungu, ni lazima madhabahu iwepo na hiyo si nyingine zaidi ya Yesu Kristo moyoni mwetu, yeye ndiye jiwe ambalo halijatiwa unajisi kwa dhambi yoyote, halijachongwa na mwanadamu yoyote halijachongwa kwa siasa au kitu kingine chochote,

Hivyo ikiwa umempokea Yesu moyoni mwako na umebatizwa na umepokea Roho Mtakatifu, tayari Yesu kashaingia moyoni mwako na kuweka makao, na hivyo madhabahu imeshatokea, basi maombi yako, dua zako, sadaka zako zina uhakika kumfikia Mungu..Lakini ukiyachonga mawe yako mwenyewe, yaani unaenda mbele za Mungu kwa kumuonyesha matendo yako, uungwana wako, uzuri wako, sadaka zako unazozitoa na huku Kristo umemtupa nje, hana nafasi kabisa katika moyo wako, hapo unafanya kazi bure ndugu yangu. Mungu hapokei uso wa mwanadamu yeyote, anapokea uso wa Yesu Kristo tu.

Hivyo ni wajibu wetu kujua kuwa madhabahu sahihi inajengwaje mioyoni mwetu, na katika kanisa.. Tusipende karama za kuchonga, tusijitumaishe na matendo yetu na huku Yesu yupo mbali na sisi.

Kama bado upo katika dhambi ni heri umgeukie yeye leo kwasababu yeye ndiyo jumla ya mambo yote hapa duniani. Bila yeye leo hii dunia ingekuwa imebakia kuwa historia tu, hivyo na wewe usisibiri uwe historia siku za usoni, Mpe Yesu maisha yako leo ayaokoe, upokee uzima wa milele. Usidhani utaweza kushinda haya maisha bila Yesu. Hilo halipo, wala halijawahi kuwepo.

Wokovu unakuja kwa kumwamini Yesu, na  kutubu dhambi zako, kisha kubatizwa katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa Jina la YESU KRISTO,(Matendo 2:38, Matendo 8:16), Kama hujabatizwa na unahitaji kufanya hivyo, utawasiliana nasi inbox, au tutafute katika namba hii +255789001312 / 0693036618

Bwana akubariki.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

TAFUTA KUWA NA AMANI NA WATU WOTE.

TUMEFANYIKA KUWA WANA WA MUNGU!

YESU ANA KIU NA WEWE.

Nasaba ni nini kibiblia?(1Nyakati 9:1, Tito 3:9)

Kuna Mbingu ngapi?

Ni uthibitisho upi unaoonyesha kuwa kuna MBINGUNI na KUZIMU?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Kuchelea ni nini?(2Wakorintho 11:3)

Nini maana ya neno kuchelea kama tunavyolisoma katika biblia?


Kuchelea ni hofu au wasiwasi, husanani ule unaotokana na kuzuka kwa madhara Fulani.

Kwa mfano tusome mstari huu;

2Wakorintho 11:2 Maana nawaonea wivu, wivu wa Mungu; kwa kuwa naliwaposea mume mmoja, ili nimletee Kristo bikira safi.

3 Lakini nachelea; kama yule nyoka alivyomdanganya Hawa kwa hila yake, asije akawaharibu fikira zenu, mkauacha unyofu na usafi kwa Kristo.

Hapo ni Paulo anaonyesha wasiwasi wake, kwa kanisa la Kristo kudanganywa na ibilisi haraka, na kuuacha unyofu wa moyo. Na ndio maana ukiendelea kusoma mistari inayofuata utaona Paulo, akiwatahadharisha, wasipokee injili nyingine, au Yesu mwingine au roho mwingine ambao wao hawakumuhubiri kwao..Ili wawe salama na uongo wa ibilisi.

2Wakorintho 12:20 “Maana nachelea, nisije nikawakuta si kama vile nitakavyo kuwakuta, nikaonekana kwenu si kama vile mtakavyo; nisije nikakuta labda fitina na wivu, na ghadhabu, na ugomvi, na masingizio, na manong’onezo, na majivuno, na ghasia”;

Vifungu vingine vinavyozungumzia Neno hili, ni kama vifuatavyo;

Matendo 23:9 “Pakawa na makelele mengi. Waandishi wengine wa upande wa Mafarisayo wakasimama, wakateta, wakisema, Hatuoni uovu wo wote katika mtu huyu; bali ikiwa roho au malaika amesema naye, ni nini?

10 Ugomvi mkubwa ulipotokea, yule jemadari akachelea Paulo asije akararuliwa nao, akaamuru askari washuke na kumwondoa kwa nguvu mikononi mwao, na kumleta ndani ya ngome”.

(Hapo ni jemedari alikuwa anaonyesha hofu yake ya kuuliwa kwa Paulo katikati ya baraza lile)

Soma tena;

Matendo 27:29 “Wakachelea tusije tukapwelewa mahali penye miamba, wakatupa nanga nne za tezi, wakaomba kuche”.

Soma pia Wagalatia 4:11.

Bwana akubariki.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tazama pia maana ya maneno mengine chini.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618

Mada Nyinginezo:

Kutahayari ni nini katika biblia?(2Timotheo 2:15)

Mlima Gerizimu na Ebali ni ipi, na umuhimu wao rohoni ni upi?

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!

Daawa ni nini kama tunavyosoma katika biblia?

Mavyaa ni nani kibiblia?(Mika 7:6)

Rudi Nyumbani:

Print this post

Kutahayari ni nini katika biblia?(2Timotheo 2:15)

Kutahayari maana yake ni kuweka katika aibu, kuaibisha, kuaibishwa, kuaibika.

Hivi ni baadhi ya vifungu vinavyolieeleza Neno hilo;

2Timotheo 2:15 “Jitahidi kujionyesha kuwa umekubaliwa na Mungu, mtenda kazi asiye na sababu ya kutahayari, ukitumia kwa halali neno la kweli”.

Hapo ni Paulo akimwambia Timotheo, ajitahidi kuishi maisha yanayopendeza Mungu, ili asiwe na sababu ya kuona aibu katika kuitenda kazi ya Mungu. Kwamfano kama Timotheo angekuwa ni mlevi, na huku anahubiri injili, asingekuwa na ujasiri wa kuwahubiria walevi, angeona aibu, lakini akijionyesha kwa matendo yake kuwa hanywi pombe, hataona aibu kuwahubiria walevi, hata tahayari.

Vifungu vingine ni kama hivi;

2Wakorintho 7:14 “Kwa maana, ikiwa nimejisifu mbele yake katika neno lo lote kwa ajili yenu, sikutahayarishwa; bali, kama tulivyowaambia mambo yote kwa kweli, vivyo hivyo na kujisifu kwetu kwa Tito kulikuwa kweli”.

(Maana yake sikuaibishwa)

2Wathesalonike 3:14 “Na ikiwa mtu awaye yote halishiki neno letu la waraka huu, jihadharini na mtu huyo, wala msizungumze naye, apate kutahayari”;

(Maana yake apate kuona aibu)

Ayubu 11:3 “Je! Majivuno yako yawanyamazishe watu wawe kimya? Nawe hapo ufanyapo dhihaka, je! Hapana mtu atakayekutahayarisha”?

(Maana yake atakayekuaibisha)

Soma pia;

Isaya 50:7 “Maana Bwana MUNGU atanisaidia; kwa sababu hiyo sikutahayari, kwa sababu hiyo nimekaza uso wangu kama gumegume, nami najua ya kuwa sitaona haya”.

2Wakorintho 7:14, Isaya 44:11.

Bwana akubariki.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali angalia chini maana ya maneno mengine ya ki-biblia.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618

Mada Nyinginezo:

Neno Korbani linamaanisha nini? (Marko 7:11)

USIPIGE MATEKE MCHOKOO!

UTAJI ULIOKUWA JUU YA USO WA MUSA.

WINGU KUBWA LA MASHAHIDI.

Mshulami ni msichana gani?

Rudi Nyumbani:

Print this post

SIFONGO NA SIKI NI NINI?

SWALI: Sifongo na siki ni nini, alizopewa Bwana Yesu pale Msalabani?

JIBU: Tusome..

Yohana 19: 28  “Baada ya hayo Yesu, hali akijua ya kuwa yote yamekwisha kumalizika ili andiko litimizwe, akasema, Naona kiu.

29  Kulikuwako huko chombo kimejaa siki; basi wakatia sifongo iliyojaa siki juu ya ufito wa hisopo, wakampelekea kinywani.

30  Basi Yesu alipokwisha kuipokea ile siki, alisema, Imekwisha. Akainama kichwa, akaisalimu roho yake”

Sifongo ni kiswahili cha neno la kiingereza “sponge” ambalo sisi tumezoea kujitaja neno hilo kama SPONCHI au SPONJI...Sasa yapo masponchi ya aina nyingi…yaliyozoeleka sana ni yale yaliyotengenezwa na malighafi ya godoro, Mara  nyingi yanatumika kwa kuoshea vyombo na matumizi mengine, kwasababu yanakuwa yanauwezo wa kufyoza maji na kutengeneza povu. Enzi za zamani (za Bwana Yesu) yalikuwepo pia masponji, ambayo yalikuwa yanakaribiana sana kufanana na haya ya kwetu ya sasa. (Tazama picha chini, mfano wa sifongo za kale)

sifongo

Hivyo Sifongo ni sponji. Sasa tukirudi kwenye maandiko tunasoma yule askari, alitwaa hiyo Sifongo na kulitia kwenye SIKI, na lengo la kufanya hivyo ni ili hiyo SIKI ijifyonze kwenye hiyo sifongo.

SASA SIKI NI NINI?

Siki ni kiungo ambacho kinakuwa katika kimiminika, kinachotengenezwa kwa kuchachushwa kama vile zinavyotengenezwa pombe…Na kimiminika hicho kazi yake ni kuongeza ladha kwenye chakula au kukihifadhi chakula kisiharibike…Zipo siki za aina nyingi kulingana na jamii za watu na tamaduni. Huku kwetu Afrika hususani Afrika mashariki, Siki haziwi katika mfumo wa kimiminika kizito sana…lakini nchi nyingine zinatengenezwa viwandani na kuwa kama Maji (mfano wa hizo ni zile vanilla zinazotumika kwenye ice-cream na keki ambazo zinakuwa zinahifadhiwa kwenye kachupa kadogo), na pia maeneo ya Mashariki ya kati, ikiwemo Taifa la Israeli, siki zao zilitengenezwa na Zabibu, hivyo zilikuwa hazina tofauti sana na Divai.

Kwahiyo siki iliyotumika pale msalabani ilikuwa ni kama Divai, lakini si divai kabisa…Na zilitumika katika matumizi ya vyakula.  Hivyo wale askari walichovya sifongo kwenye siki na kuiweka kwenye mti, ili ifike juu pale msalabani alipokuwepo Bwana Yesu.(Tazama mfano wa siki ya divai katika picha ya juu kabisa ya somo hilo)

Na kwasababu siki kwaasili ni INA UKALI, inaukakasi na ni chungu na ina tindikali nyingi, kwa ufupi haifai kuwekwa katika kinywa cha mwanadamu kwa ukali wake, walifanya vile ili Mwili wa Bwana Yesu ukaukiwe maji…kwasababu walimsikia akisema Naona kiu.

Sasa ipo siri kubwa sana katika tukio hilo lililotendeka hapo juu msalabani, Kama utapenda kufahamu zaidi siri hiyo basi unaweza kufungua hapa >> YESU ANA KIU NA WEWE

Bwana akubariki.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618


Mada Nyinginezo:

Hanithi ni nini katika biblia? (kumbukumbu 23:17)

Mount Gerizim and Mount Ebal: Their Meaning and Spiritual Significance

Pomboo ni nini katika biblia?(Kutoka 25:5, Ezekieli 16:10)

Mkomamanga ni nini? Na katika biblia unawakilisha nini?

Rudi Nyumbani:

Print this post

YESU ANA KIU NA WEWE.

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe. Karibu tuyatafakari maandiko pamoja.

Kama tunavyojua hakuna wokovu kwa mwingine yoyote, isipokuwa kwa Bwana wetu Yesu, haijalishi dunia itasema nini, haijalishi imani nyingine zote zitasema nini lakini ukweli upo pale pale, Kristo alikufa, akafufuka, akapaa mbinguni na sasa YU HAI.. Na yupo pamoja na wale aliowaita akitembea nao mpaka ukamilifu wa Dahari. Na wote wamtumainiao, ni kama mlima wa Sayuni, hawatatikisika kamwe, wanadumu milele..(Zab.125:1).

Kuna tukio lililotokea pale msalabani..ambalo liliwashangaza wengi…Lakini kabla hatujalizungumzia hilo jambo hebu tuyazungumzie kwanza mateso ya Bwana wetu Yesu pale msalabani.

Siku ile ya mateso ya Bwana, bila shaka mimi na wewe tungekuwepo pale..tungemwaga machozi yasiyokuwa ya kawaida ya uchungu kwa jinsi alivyojeruhiwa…Biblia inasema “uso wake uliharibiwa sana kuliko watu wote”( Isaya 52:14), wengi wetu ng’ombe wakati anachinjwa tu hata hatudhubutu kutazama, ajali ikitokea mahali, hata hatudhubutu kuzitazama zile maiti, mwizi akipigwa tu na kuingizwa kwenye tairi achomwe, hisia tunazozipata hazielezeki……Sasa siku ile Bwana anasulubiwa laiti tungekuwepo wengine tungezimia.

Kwanza jana yake hakulala usiku kucha, alikuwa akizungumza na wanafunzi wake na kuwapa wosia mrefu, na kuomba… mpaka ilipofika alfajiri jogoo wa kwanza anawika, alikuwa tayari kashashikwa na wale maaskari, kulipopambazuka tayari alikuwa ameshateswa vikali, wakaanza kumtembeza na kumwangaisha, kwa miguu kutoka kwa mfalme huyu kwenda kwa huyu…kutoka kwa Pilato kwenda kwa Herode, halafu anarudishwa tena kwa Pilato, huku kichwani anataji ya miiba..na huku anapigwa na kutemewa mate…Baadaye anapewa msalaba aubebe…na apande nao Golgotha…Pale Golgotha ni eneo la kilima kirefu…Mwili wote ulikuwa umeshaishiwa nguvu hata kutembea alishindwa ikabidi asaidiwe ule msalaba.

Na baadaye akitundikwa msalabani…Damu ilimwagika nyingi na mwili uliishiwa nguvu na maji.

Sasa Yule Yesu aliyesema maneno haya….

“Mimi ni Alfa na Omega, Mwanzo na Mwisho. Mimi nitampa yeye mwenye kiu, ya chemchemi ya maji ya uzima, bure! (Ufunuo 21:6)”

Na tena aliyesema maneno haya…..

Yohana 7:37 “Hata siku ya mwisho, siku ile kubwa ya sikukuu, Yesu akasimama, akapaza sauti yake akisema, MTU AKİONA KİU, NA AJE KWANGU ANYWE.

38 Aniaminiye mimi, kama vile maandiko yalivyonena, mito ya maji yaliyo hai itatoka ndani yake”.

Na leo hii anakuja kusema maneno haya…

Yohana 19:28“Baada ya hayo Yesu, hali akijua ya kuwa yote yamekwisha kumalizika ili andiko litimizwe, akasema, NAONA KİU”

Ni jambo la kushangaza kidogo! Ambalo hata sisi tunaweza kulihoji..Siku chache nyuma alisema “wote wenye kiu waje kwangu kunywa maji, na leo anasema ANAONA KIU, yaani anataka sisi ndio tumpe maji??”..Bila shaka huyu anaweza kuwa amerukwa na akili… Na kweli! Anavyoonekana ameshochoka na kakauka mwili, ni lazima atataka maji ya kunywa tu!..bila shaka wengi walicheka na kubeza…Na ili kumkomoa kabisa wakampa SIKI, ili ikaushe maji yote mwilini, ili ASIKIE KIU KISAWASAWA.

Lakini baadaye kidogo kuna jambo lilitokea lililowashangaza na kuwabadilisha mitazamo yao…na wengine waliokoka pale pale..

Ule mwili waliounyesha siki!, Ule mwili uliokuwa umeonekana umekauka maji yote, na damu yote…Ule mwili ulioonekana umekufa kwa KIU kikali na kwa KUMWAGIKA DAMU nyingi, na kwa maumivu makali…dakika chache baadaye, ULIMWAGA LITA KADHAA ZA MAJI MBELE YA MACHO YAO. Ndipo walipojua kuwa huyu Mtu alikuwa hasikii KIU cha MAJI, bali alikuwa anasikiu kingine.

Hebu tusome kidogo..

Yohana 19:32 “Basi askari wakaenda, wakamvunja miguu wa kwanza, na wa pili, aliyesulibiwa pamoja naye.

33 Lakini walipomjia Yesu na kuona ya kuwa amekwisha kufa, hawakumvunja miguu;

34 lakini askari mmojawapo alimchoma ubavu kwa mkuki; NA MARA İKATOKA DAMU NA MAJİ.

35 Naye aliyeona ameshuhudia, na ushuhuda wake ni kweli; naye anajua ya kuwa anasema kweli ili ninyi nanyi mpate kusadiki”.

Achana na zile picha unazoziona kwenye tamthilia, kimchirizi kidogo tu cha maji kinatoka ubavuni mwa Bwana.. Haikuwa hivyo ndugu!…ingekuwa hivyo huyu askari, asingeokoka hapo!..Pale maji yaliyotoka ni mengi mno, na yalitoka kwa presha nyingi..ndio maana askari huyu aliamini pale pale, kwasababu alishachoma maiti nyingi lakini kwa hiyo ya Bwana kwake lilikuwa ni tukio jipya.

Ndipo wale askari walipojua kuwa Yesu Kristo ni chemchemi ya Maji yaliyo hai..Na pale hakuwa anasikia kiu cha maji yao, bali kiu cha kuwapa wao maji ya uzima!…Na pale pale msalabani akaanza kuwapa, wakanywa yale maji, nao pia wakatoka kwenda kushuhudia habari za mwokozi.

“Naye aliyeona ameshuhudia, na ushuhuda wake ni kweli; naye anajua ya kuwa anasema kweli ili ninyi nanyi mpate kusadiki”

Na leo hii Kristo yu hai, na tangazo lake ni lile lile…

Ufunuo 21:6 “Mimi ni Alfa na Omega, Mwanzo na Mwisho. Mimi nitampa yeye mwenye kiu, ya chemchemi ya maji ya uzima, bure!”

BWANA ANA KIU NA WEWE NDUGU…ANA KIU YA KUKUPA WEWE MAJI YA UZIMA. Maji haya aliyatoa baada ya kupigwa kwake, Ndio shauku yake kuona unayapata hayo maji, anakuona una kiu, hivyo anataka kuikata hiyo kiu…Una kiu ya kupata furaha, yeye anayo furaha, una kiu ya kupata amani, yeye anayo amani, una kiu ya kupata raha, yeye anatoa raha (Mathayo 11:28), Una kiu ya kuthaminika, yeye anaweza kukuthaminisha…Anatamani kukupa hayo yote kuliko wewe unavyotamani.

Hivyo unachopaswa kufanya ni kumkaribisha tu katika maisha yako kama bado hujafanya hivyo, na unafanya hivyo kwa kutubu na kuziacha dhambi zako, kwa moyo wako wote, ili umsafishie sehemu ya kuwekea maji atakayokupa…Na ukishatubu, tafuta ubatizo sahihi wa kimaandiko ambao ni wa maji tele na wa kuzamishwa kwa jina la Yesu, na baada ya hapo Roho Mtakatifu ataingia ndani yako, kukusaidia kuishi maisha yanayompendeza yeye pamoja na kukupa zawadi zote hizo hapo juu…Atakata kiu yako kwa namna ambayo utashangaa wala haihitaji mtu kukuhadithia.. Wewe onja tu!maji ya Bwana halafu utakuja kutoa ushuhuda mwenyewe…

Zaburi 34:8 “Onjeni mwone ya kuwa Bwana yu mwema; Heri mtu yule anayemtumaini”.

Bwana akubariki.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.


Mada Nyinginezo:

WINGU KUBWA LA MASHAHIDI.

MASHAHIDI 40 WALIOUAWA MJINI SEBASTE, NI UJUMBE KWETU.

JIEPUSHE NA MANENO YA MANABII WA UONGO.

USO WAKE ULIKUWA UMEHARIBIWA SANA ZAIDI YA MTU YE YOTE.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Mount Gerizim and Mount Ebal: Their Meaning and Spiritual Significance

Introduction

In the heart of ancient Israel’s journey into the Promised Land lie two significant mountains: Mount Gerizim and Mount Ebal. Located in Samaria and facing each other directly, these two mountains were not just geographical landmarks but served as vivid illustrations of the covenant between God and His people. Through them, God presented the Israelites with a life-altering choice—blessing for obedience and curse for disobedience.

This symbolic moment reveals a deep theological truth: God’s covenant demands a response, and the results of that response echo through our lives, both physically and spiritually.


The Biblical Account

While still in the wilderness, Moses gave Israel a prophetic instruction from God. After crossing the Jordan River into Canaan, the Israelites were to hold a covenant-renewal ceremony at Mount Gerizim and Mount Ebal.

“And when the Lord your God brings you into the land that you are entering to take possession of it, you shall set the blessing on Mount Gerizim and the curse on Mount Ebal.”
Deuteronomy 11:29, 

They were to build an altar (on Ebal), write the entire Law on large stones, and divide the tribes into two groups. Half of the tribes would stand on Mount Gerizim to pronounce blessings, while the other half would stand on Mount Ebal to declare curses. In the valley between stood the Levitical priests with the Ark of the Covenant, representing God’s presence and authority.

“And half of them shall stand on Mount Gerizim to bless the people, and half of them on Mount Ebal for the curse…”
Deuteronomy 27:12–13

Later, Joshua fulfilled this exact command after leading the Israelites across the Jordan:

“And all Israel, sojourner as well as native born, with their elders and officers and their judges, stood on opposite sides of the ark before the Levitical priests… Half of them in front of Mount Gerizim and half of them in front of Mount Ebal…”
Joshua 8:33

This dramatic gathering was a powerful reminder: God’s covenant involves both promise and responsibility.


Theological Significance

  1. Covenant Relationship and Free Will
    Mount Gerizim and Ebal represent the dual outcomes of the covenant—blessing and curse—which depend on human response to God’s Word. This reflects the theological principle of human responsibility in divine covenant. God initiates relationship, but we are called to respond in obedience.

    “I call heaven and earth to witness against you today, that I have set before you life and death, blessing and curse. Therefore choose life…”
    Deuteronomy 30:19

  2. Symbol of Judgment and Grace
    Mount Ebal (where the altar was built) is where the Law and the sacrifices met—highlighting that even under judgment, God provided a way of forgiveness through sacrifice. This points forward to Jesus Christ, the ultimate sacrifice for our sins.

    “For the law was given through Moses; grace and truth came through Jesus Christ.”
    John 1:17

  3. Foreshadowing the Gospel
    Though these mountains aren’t often mentioned in the New Testament, Jesus indirectly referenced Mount Gerizim during His encounter with the Samaritan woman:

    “Our fathers worshiped on this mountain, but you say that in Jerusalem is the place where people ought to worship.”
    John 4:20

    The Samaritans still honored Mount Gerizim as sacred. But Jesus responded with a revelation of New Covenant worship:

    “The hour is coming when neither on this mountain nor in Jerusalem will you worship the Father… true worshipers will worship the Father in spirit and truth.”
    John 4:21, 23

    In Christ, physical locations give way to spiritual realities. True blessing is not tied to geography but to relationship with God through Jesus.


Spiritual Application for Believers Today

Even today, Mount Gerizim and Mount Ebal stand as spiritual metaphors. Every believer faces a similar choice: to walk in obedience and receive God’s blessings (Gerizim), or to reject His Word and suffer the spiritual consequences (Ebal).

God’s Word is clear—those who walk in His ways will experience the fruit of obedience:

“Blessed is the man who walks not in the counsel of the wicked… but his delight is in the law of the Lord.”
Psalm 1:1–2

But those who reject His truth will find themselves cut off from His blessing:

“But they refused to pay attention… therefore great wrath came from the Lord of hosts.”
Zechariah 7:11–12


Conclusion

Mount Gerizim and Mount Ebal are more than historical sites—they are enduring symbols of the choices we make daily in our walk with God. The Law, blessings, curses, sacrifice, and grace all intersect on those slopes. Through Christ, the curse is broken, and the blessing is fulfilled in those who believe and obey.

We now live not under the shadow of the Law, but in the reality of grace. Yet the principle remains: our lives are shaped by our response to God’s Word.

Will you choose the path of Gerizim or Ebal? The mountain of blessing or the mountain of judgment?

Shalom.

 

Print this post

Nini maana ya “katika wingi wa hekima mna wingi wa huzuni”.


SWALI: Biblia ina maana gani kusema “Katika wingi wa hekima mna wingi wa huzuni” Je! si sahihi kutafuta hekima?

Mhubiri1:17 “Nikatia moyo wangu ili kuijua hekima, na kujua wazimu na upumbavu; nikatambua ya kwamba hayo yote nayo ni kujilisha upepo.

18 Yaani, Katika wingi wa hekima mna wingi wa huzuni, Naye aongezaye maarifa huongeza masikitiko”.

JIBU: Ukisoma Sura hiyo ya kwanza yote, na zinazofuata utaona Sulemani alikuwa anaeleza jinsi alivyojibidiisha katika kutafuta mambo ya ulimwenguni, na hekima yake na kazi zote “zinazofanywa chini ya mbingu (Mhubiri 1:13)”.

Lakini hasemi alikuwa anayatafuta  mambo ya ki-mbinguni, hapana, na ndio maana utaona kila mahali anaishia kusema ni ubatili mtupu, sehemu zote, yaani maudhui ya kitabu cha mhubiri kinaeleza hatma ya kazi zote na shughuli zote zinazofanywa na wanadamu chini ya jua, na ndio maana mwishoni kabisa  mwa kitabu hicho utaona sasa Sulemani anatoa jibu la jambo la muhimu ambalo mwanadamu anapaswa alitafute siku zote za maisha yake..Anasema na hilo si lingine zaidi ya kumcha Mungu basi. (Soma Mhubiri 12:13).

Sasa tukirudi kwenye mstari huo anaposema “Katika wingi wa hekima mna wingi wa huzuni,Naye aongezaye maarifa huongeza masikitiko” Hamaanishi Hekima ya kimbinguni au maarifa ya kimbinguni,..Hapana!, kinyume chake hekima ya kimbinguni na maarifa ya kimbinguni ndio yanayomfanya mtu awe na amani na furaha na utulivu wa nafsi..Kumjua Yesu ambaye ndio hekima ya Mungu (sawasawa na 1Wakorintho 1:24), ni mwisho wa masumbuko yote, unakuwa umefunguliwa milele, hakuna huzuni yoyote wala masikitiko.. Unapolisoma gombo( ambalo ni Neno la Mungu), ndipo unapopata maarifa sahihi ya kuishi hapa duniani, na unafungua milango yote iliyofungwa.

Hivyo maarifa yanayozungumziwa hapo ni haya maarifa ya kiduniani tuliyonayo, kwasababu, pale mtu anapokuwa na elimu kubwa sana, inadhaniwa kuwa ndio itampa furaha ya kweli katika moyo wake, lakini matokeo yanaonyesha kuwa hilo sio kweli, Sulemani alilipata hilo akadhani ndio lingempa furaha aliyokuwa anaitazamia, lakini akagundua kuwa ni ubatili.

Ni jambo la kawaida, wanasayansi wanaokesha maabara usiku kucha, kutafiti na kugundua, asilimia kubwa huwa maisha yao sio ya furaha, kwasababu wanakuwa na hofu ya vitu vingi, hilo likitokea, au lile likizuka itakuwaje, maadui zetu wakitengeneza bomu la atomiki kama hili tunalotengeneza sisi itakuwaje? Dawa au kemikali hii madhara yake yatakuwaje miaka 10 mbele? N.k.n.k.. Maarifa yao na hekima zao zinapozidi kuongezeka huzuni nazo zinazidi kuongezeka…

Hivyo mwisho wa siku inakuwa ni huzuni juu ya huzuni tu na masikitiko juu ya masikitiko na ndio maana biblia inatuasa, tupende kuongeza maarifa kwa Mungu wetu zaidi kuliko sehemu nyingine yoyote kwasababu huko ndiko tutapata furaha ya kweli idumuyo na utulivu na amani isiyoisha.

Bwana Yesu (ambaye ndio hekima ya Mungu) anasema;

Mathayo 11:28 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.

29 Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;

30 kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi”.

Kwa Bwana Yesu ndipo penye pumziko la kweli.

Shalom.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.


Mada Nyinginezo:

Hanithi ni nini katika biblia? (kumbukumbu 23:17)

WOSIA WA BWANA YESU KWA WANAFUNZI WAKE.

Bwana Yesu alimaanisha nini aliposema; Mafarisayo Hupanua HIRIZI zao, na kuongeza MATAMVUA yao?

SIKUKUU YA VIBANDA.

BWANA alimaanisha nini kwenye mstari huu Marko 2:21″ Hakuna mtu ashonaye kiraka cha nguo mpya katika vazi kukuu;?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Hanithi ni nini katika biblia? (kumbukumbu 23:17)

Hanithi ni nini?


Hanithi kibiblia ni mwanaume anayeingiliwa kinyume na maumbile, (Kwa lugha ya sasa wanajulikana kama mashoga), watu wote waliokuwa wanafanya hivi vitendo, waliitwa mahanithi,  na adhabu yake ilikuwa ni mpaka kifo.

Kumbukumbu 23:17 “Pasiwe na kahaba katika binti za Israeli, wala pasiwe na hanithi katika wana wa Israeli wanaume”.

Zamani katika Israeli watu wote waliokuwa wanahudumu kwenye madhabahu za miungu kama vile maashera n.k., walikuwa na desturi ya kufanya hivi vitendo kwa heshima ya miungu yao.

1Wafalme 14:23 “Maana hao pia wakajijengea mahali pa juu, na nguzo, na maashera, juu ya kila kilima kirefu, na chini ya kila mti wenye majani mabichi.

24 Na mahanithi walikuwako katika nchi, wakafanya sawasawa na machukizo yote ya mataifa Bwana aliowafukuza mbele ya wana wa Israeli”.

1Wafalme 15:11 “Basi, Asa akafanya yaliyo mema machoni pa Mungu, kama alivyofanya babaye Daudi.

12 Akawafukuza mahanithi katika nchi, akaziondoa sanamu zote walizozifanya baba zake”.

2Wafalme 23:7 “Akaziangusha nyumba za mahanithi, waliokuwamo nyumbani mwa Bwana, wanawake walipofuma mapazia ya Ashera”.

Hii ni roho ambayo mpaka sasa inatenda kazi, na katika hizi siku za mwisho, ilitabiriwa itajirudia kwa nguvu kama ilivyokuwa katika siku za Sodoma na Gomora, Unaweza kuona leo hii wimbi hili la watu linavyozidi kuongezeka kwa kasi duniani kiasi kwamba hata sheria za nchi zinaruhusu, na baadhi ya dini za uongo, na mpaka wanayo bendera yao duniani, kama unavyoweza kuiona katika picha juu, bendera hiyo yenye rangi ya upinde wa mvua, ndio kauli mbiu yao kuwa Mungu hataiangamiza dunia tena kama alivyoahidi, hivyo ndivyo wanavyojidanganya.. Lakini hawajui kuwa Mungu alisema  kweli hataigharikisha dunia kwa maji, lakini alisema ataiangamiza kwa moto.

2Petro 3:6 “kwa hayo dunia ile ya wakati ule iligharikishwa na maji, ikaangamia.

7 Lakini mbingu za sasa na nchi zimewekwa akiba kwa moto, kwa neno lilo hilo, zikilindwa hata siku ya hukumu, na ya kuangamia kwao wanadamu wasiomcha Mungu”.

Unaona? Hiyo ni dalili ya wazi kuwa hii dunia inakwenda kuangamizwa wakati sio mwingi.

Lakini sisi tuyoanapo hayo, ni wajibu wetu kujiimarisha na kusimama imara katika hichi kipindi kifupi tulichobakiwa nacho, kwasababu Unyakuo upo karibu.

Swali ni Je! Tumejiwekaje tayari kwa Kurudi kwa Bwana mara ya pili?

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.

Mada Nyinginezo:

JINSI SODOMA NA GOMORA ILIVYOKUWA INAVUTIA SANA..

MAONO YA NABII AMOSI.

HIZI NI NYAKATI ZA KUJIINGIZA KWA NGUVU.

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Uzima wa milele ni nini?

Uzima wa milele ni nini kama unavyotajwa sehemu mbalimbali?


Jibu fupi, uzima wa milele ni maisha yasiyokuwa na mwisho. Yaani unaishi tu, na utaendelea kuishi, hivyo hivyo kwa siku zisizokuwa na ukomo, miaka milioni moja itapita, bado utaendelea kuishi, miaka trilioni moja itapita bado utaendelea kuishi, na hapo hata bado hujaanza kuishi, utaendelea na kuendelea, kamwe hakuna siku itakayofika na ukasema leo ni ukomo wa mimi kuwa hai, kamwe hutakaa ufe, utakuwa hai hivyo hivyo daima..huo ndio uzima wa milele.

Jambo kama hilo ukilifikiria sana, kuna mahali hata akili yako itafika na kugota, jaribu uone,, kwasababu ni jambo ambalo tangu umezaliwa halijawahi  kuwa sehemu ya maisha yako, tangu ulipokuwa mdogo mpaka unakua umekuwa ukijua kuwa siku moja maisha yako yatakwisha kwa kifo, lakini pale unaposikia kuwa hutakaa ufe tena, akili yako inaweza kushindwa  kulipokea jambo hilo kwa wakati huo.Lakini ukweli ni kwamba hilo litawezekana, lakini sio kwa kila mtu anayeishi leo hii duniani, bali kwa kundi Fulani tu la watu, si watu wote wataishi milele.

Na ndio maana biblia inasema, Karama ya Mungu ni uzima wa milele.

Warumi 6:23 “Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu”.

Karama ni zawadi, hivyo zawadi kubwa kuliko zote ambayo Mungu anaweza kumpa mwanadamu, si nyingine zaidi ya uzima wa milele. Yaani maisha yasiyokuwa na ukomo..Huoni kama hiyo ni zawadi iliyopitiliza?

Lakini kama hiyo mistari inavyojieleza, Mungu haitoi karama hiyo hivi hivi tu, bali  inasema anaitoa “katika Yesu Kristo Bwana wetu”. Yaani kwa kupitia Yesu Kristo, maana yake ni kuwa usipookolewa na Yesu huwezi kupokea uzima wa milele kwa namna yoyote ile, haijalishi una matendo mema kiasi gani.

Huwezi kuupata uzima huo kwa mwanadamu mwingine yoyote duniani au mbinguni, anayejiita, mtume, au nabii, au kuhani n.k. hakuna mwanadamu yoyote zaidi ya Yesu Kristo peke yake ndiye anayeweza kuachilia karama hiyo ya uzima wa milele ndani ya Mtu.

Na ndio maana yeye mwenyewe alisema.

Yohana 3:36 “Amwaminiye Mwana yuna uzima wa milele; asiyemwamini Mwana hataona uzima, bali ghadhabu ya Mungu inamkalia”.

Hivyo kila mtu anayemwamini na kumpokea, anakuwa tayari na uhakika huo kuwa ndani yake uzima wa milele upo. Hata akifa leo, siku ile ya ufufuo atafufuliwa na kuungana na watakatifu wengine, na kwa pamoja wataishi milele na Mungu mbinguni milele.

Yohana 3:16 “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele”.

Sasa, mtu anampokeaje Yesu?. Anampokea Yesu kwanza kwa kutubu dhambi zake kwa kumaanisha kuziacha, na baada ya hapo anakua tayari kubatizwa katika ubatizo sahihi, Na kupokea Roho Mtakatifu. Hivyo kama wewe ni mmojawapo wa ambao hawana uzima wa milele ndani yao, na upo tayari leo kumruhusu Yesu ayabadilishe maisha yako.

Basi fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba na maagizo mengine >>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Na ikiwa umefuatisha maagizo hayo kwa dhati na kwa moyo wako wote, basi uwe na uhakika kuwa umeshapokea karama hiyo ya uzima wa milele ndani yako

Kwahiyo endelea kujifunza Neno la Mungu, na tafuta kanisa la kiroho litakalokusaidia kukua kiroho na Bwana atakuwa na wewe sikuzote. Mpaka siku ile ya paraparanda ya mwisho.

Shalom.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.

Mada Nyinginezo:

USIUZE URITHI WAKO.

Nini maana ya maneno haya ya Bwana? “Nami nikiinuliwa juu ya nchi,NITAWAVUTA WOTE KWANGU”(Yohana12:32).

NAO WALIOKUWA WAMEKUSUDIWA UZIMA WA MILELE WAKAAMINI.

JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?

MADHARA YA KUPUUZIA MAAGIZO YA MSINGI MUNGU ANAYOKUPA.

Rudi Nyumbani:

Print this post