Nini maana ya huu mstari? Mithali 11: 15 “Amdhaminiye mgeni hakosi ataumia; Achukiaye mambo ya dhamana yu salama”.
Biblia ni kitabu pekee ambacho kinamfundisha mtu kutembea katika kanuni zote (yaani za mwilini na rohoni), jinsi ya kuishi katika roho, vilevile na jinsi ya kuishi katika mwili, Na moja ya kitabu ambacho kinatufundisha kanuni za kutembea katika mwili na kufanikiwa ni hichi kitabu cha Mithali,
Ni kitabu ambacho kina mahusia kwa makundi yote ya watu kuanzia wanandoa, vijana, watoto, maskini, matajiri, vilevile kina maonyo kwa viongozi, hadi kwa watumwa, Hivyo, tukirudi katika swali, kwanini Sulemani kwa hekima ya Roho alisema.. “Amdhaminiye mgeni hakosi ataumia; Achukiaye mambo ya dhamana yu salama”.
Hapo Hakumaanisha kuwa, kumdhamini mtu yeyote, ni kosa, hapana, bali anatoa angalizo katika kutoa dhamana kwa mtu mgeni (usiyemfahamu), kunaweza kukuweka katika hatari kubwa sana ya kukumbana na shida. Kumchukulia mtu mkopo bank halafu, unaweka nyumba yako rehani, mtu ambaye umekutana naye kwa kipindi kifupi tu, bado hujui vizuri mwelekeo wake upoje, halafu unaweka mpaka na mali zako rehani, hapo ni rahisi sana kuishia pabaya,
Hatupaswi kukurupuka kumdhamini mtu, ili mradi tu mtu kisa tunafanya tendo jema. Hapana kinyume chake biblia inaturuhusu tuchukue muda wa kumtambua, kumfahamu, kumwelewa, ndipo tumdhamini kama kuna umuhimu wa kufanya hivyo, Lakini Zaidi sana tukibaki kama tulivyo, tukamwachia Mungu asimamie mambo hayo ya kudhamini, tutakuwa katika upande ulio salama Zaidi. Kwasababu bado wakati mwingine mtu anaweza akawa ni mwema kweli, au akawa na mwelekeo mzuri lakini kwa bahati mbaya mambo yakabadilikia ghafla njiani, labda kapata hasara, hapo atakayeumia ni wewe uliyemdhamini.
Na ndio maana bado Biblia bado inasisitiza suala hilo hilo katika vifungu vingine mbeleni kidogo inasema..
Mithali 22:26 “Usiwe mmoja wao wawekao rehani; Au walio wadhamini kwa deni za watu; 27 Kama huna kitu cha kulipa; Kwani ukaondolee kitanda chako chini yako?”
Lakini maneno haya yanatufundisha nini rohoni?
Yupo ambaye hakuogopa jambo hilo, aliingia katika hii hatari ya kutudhamini, huku akijua kabisa, anaowadhamini hawawezi kulipa madeni yao hata kidogo, lakini alijiingiza katika shida zao, na kwa nguvu zake, akafanikiwa kulipa makosa yetu yote.
Angeweza kuacha asitudhamini, kwasababu maandiko yametoa ruhusa hiyo kama tulivyosoma.. Lakini kwa upendo wake, usiopimika, alikubali kulipa madeni yetu yote. Na huyo si mwingine Zaidi ya Bwana wetu YESU KRISTO.
Hakika sifa heshima na utukufu vina yeye, milele na milele. Amina.
Ni kitendo cha kushangaza sana na cha aibu, kuona mpaka sasa kuna baadhi ya watu wapo nje ya neema yake.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
Nini maana ya kilichotarajiwa kikikawia kuja moyo huugua (Mithali 13:12)?.
Tofauti na inavyodhaniwa na wengi kuwa kutubu ni kuomba msamaha, lakini kiuhalisia kuomba msamaha kunakuja baada ya kutubu.
Kutubu maana yake ni “Kugeuka” yaani kuacha kile ulichokuwa unakifanya.
Maana yake unapojigundua kuwa wewe ni mkosaji, jambo la kwanza ni “Kuacha kile ulichokuwa unakifanya” kisichokuwa sawa. Kisha ndipo unakwenda kuomba msamaha.
Hakuna mtu anayekwenda kuomba msamahaka kabla hajaacha kile alichokuwa anakifanya.
Umemwibia mtu, au boss wako, je unaweza kwenda kumwomba msamaha huku bado unamwibia?
Jibu ni la!. Cha kwanza utakachokifanya ni kuacha kwanza wizi, kisha ndipo unakwenda kumwomba Msamaha. Maana yake matendo yako ndiyo yatakayoelezea kama kwenye kama umetubu kweli au la!, Na si maneno.
Na kwa Mungu ni hivyo hivyo, haangalii wingi wa maneno yetu, wala wingi wa machozi yetu, wala wingi wa majuto yetu, bali wingi wa Matendo yetu!.
Kwa Mungu “Matendo” ni Alama kubwa sana kuliko hata “Maombi”. Mtu anayetenda sana ni rahisi kufanikiwa zaidi na yule anayeomba sana bila kutenda.
Yakobo 2:17 “Vivyo hivyo na imani, isipokuwa ina matendo, imekufa nafsini mwake”.
Kadhalika na Toba ni matendo si maneno.
Ili tulielewe hili vizuri hebu tujikumbushe ile habari ya Yona.
Yona 3:3 “Basi Yona akaondoka, akaenda Ninawi, kama Bwana alivyonena. Basi Ninawi ulikuwa mji mkubwa mno, ukubwa wake mwendo wa siku tatu.
4 Yona akaanza kuuingia mji mwendo wa siku moja, akapaza sauti yake, akasema, Baada ya siku arobaini Ninawi utaangamizwa.
5 Basi watu wa Ninawi wakamsadiki Mungu; wakatangaza kufunga, wakajivika nguo za magunia, tangu yeye aliye mkubwa hata aliye mdogo.
6 Habari ikamfikia mfalme wa Ninawi, naye akaondoka katika kiti chake cha enzi, akavua vazi lake, akajivika nguo za magunia, na kuketi katika majivu.
7 Naye akapiga mbiu, akatangaza habari katika mji wa Ninawi, kwa amri ya mfalme na wakuu wake; kusema, Mwanadamu asionje kitu, wala mnyama wala makundi ya ng’ombe, wala makundi ya kondoo; wasile, wala wasinywe maji;
8 bali na wafunikwe nguo za magunia, mwanadamu na mnyama pia, nao wakamlilie Mungu kwa nguvu, naam, na wageuke, kila mtu akaache njia yake mbaya, na udhalimu ulio mikononi mwake.
9 Ni nani ajuaye kwamba Mungu hatageuka na kughairi, na kuiacha hasira yake kali, ili msiangamizwe?
10 Mungu akaona matendo yao, ya kuwa wameiacha njia yao mbaya. Basi Mungu akalighairi neno lile baya, ambalo alisema atawatenda; asilitende”
Nataka tuuone huo mstari wa 10 unaosema “Bwana akaona matendo yao, ya kuwa wameiacha njia yao mbaya”…hapo haisemi “Bwana akaona kufunga kwao na kujitesa kwao, wala kulia kwao”.
Sasa sio kwamba kufunga Mungu hakuoni, anakuona lakini kunapaswa kuje baada ya mtu kuacha njia zake mbaya.
Tunapokwenda kuumaliza mwaka tulikumbuke hili, inawezekana umeomba sana Msamaha kwa Mungu kwa mambo unayoyafanya, lakini nataka nikuambie kuwa ni muda tu ulikuwa unapoteza, hakuna msamaha wowote ulioupata endapo hukuamua mwenyewe kuacha njia zako mbaya, kama hawa watu wa Ninawi.
Kama hukuamua kuacha njia ya Ulevi,uzinzi, anasa, wizi, utukanaji, uuaji, utapeli, rushwa n.k bado toba yako haikukamilika, haijalishi uliongozwa sala ya Toba na nani?, Bado mbele za Mungu hujapokea msamaha wa dhambi.
Sasa swali ni wakati gani sahihi wa kutubu?
Biblia inasema saa ya Wokovu ni sasa, wakati uliokubalika ndio huu.
2 Wakorintho 6:2 “(Kwa maana asema,
Wakati uliokubalika nalikusikia,
Siku ya wokovu nalikusaidia;
tazama, wakati uliokubalika ndio sasa; tazama, siku ya wokovu ndiyo sasa.)”
Je Umetubu??..Yaani umegeuka na kuacha njia zako mbaya?. Kumbuka baada ya wewe kuamua kuacha njia zako mbaya ndipo Bwana kupitia Roho wake Mtakatifgu anakuongezea nguvu ya wewe kuweza kushinda dhambi, kwasababu Roho Mtakatifu ni msaidizi, maandiko yanasema hivyo, (kumbuka tena, Yeye ni msaidizi na si mtendaji). Watendaji ni sisi, yeye kazi yake ni kutusaidia, kutuongezea nguvu.
Sasa jiulize atamsaidiaje mtu ambaye hajaanza kufanya chochote??, Utamsaidiaje mtu aliyechoka kutembea na ilihali hata hiyo safari yenyewe hajaianza?.
Isaya 40:29 “[Huwapa nguvu wazimiao, humwongezea nguvu yeye asiyekuwa na uwezo”.
Leo kuna watu wengi wanaoshindwa na dhambi, ambao hawawezi kuacha ulevi, uzinzi, kujichua, kuiba, kusengenya n.k. Na hawajui tatizo ni nini?.
Tatizo ndio hilo, walitangulia kuomba msamaha kabla ya kuamua kuacha matendo yao.
Bwana alipofika nyumbani kwa Zakayo, alitubu wizi wake kwa matendo kwa kwenda kuwarudishia mara 4 (Luka 19:1-10) wale aliowadhulumu, na ndipo Bwana akamwambia leo wokovu umefika nyumbani kwake, hakutubu kwa maneno tu!.
Watu kama Zakayo ndio Bwana anawaongezea nguvu ya kushinda dhuluma, kwasababu wameshaanza safari ya kuacha dhuluma kwa vitendo.
Na wewe leo anza toba kamili kwa kumwacha huyo mke/mume ambaye si wako, kwa kumwacha huyo mtu mnayeishi kama girlfriend/boyfriend na ilihali hamjafunga ndoa, kwa kumrudishia mtu kitu ulichomdhulumu au kumwimbia.
Na baada ya kufanya hayo na kumwomba Bwana msamaha, utaona Amani fulani isiyoelezeka imeiingia ndani yako, hiyo itakuwa ni uthibitisho wa kwamba Toba yako imekubalika mbele za Bwana.
Na baada ya hapo Bwana atakuongezea nguvu ya wewe kushinda dhambi, ghafla utaona kiu ya kudhulumu imekufa, kiu ya kuzini imekufa, kiu ya kufanya mambo yote uliyokuwa unayafanya imekufa.
Bwana akubariki, na Bwana atubariki sote.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
Dhabihu kwa jina lingine ni “kafara”, zilikuwepo sadaka za kafara na vile vile zilikuwepo zisizo za kafara.
Katika agano la kale, kafara zilizokuwa zinatolewa kwa Mungu ni kafara za wanyama, kama kondoo, mbuzi na ng’ombe.
Ambapo, mtu binafsi au Taifa zima litamsogeza huyo mnyama mbele za Bwana katika hema yake, na kuhani atamchukua huyo mnyama kama ni ng’ombe, au mbuzi au kondoo na kumchinja na kutwaa damu yake na kufanya upatanisho kwa huyo mtu au kwa Taifa, na kutwaa baadhi ya viungo na kuvichoma juu ya madhabahu.
Sasa sadaka ya namna hiyo ndiyo inayoitwa dhabihu.
Zilikuwepo sadaka nyingine ambazo hazikuwa dhabihu.
Kwamfano sadaka za unga, sadaka za mazao, sadaka za fedha, sadaka za nguo, za malimbuko n.k hizo hazikuitwa dhabihu.. Dhabihu ni sadaka ya kafara inayohusisha mnyama kuchinjwa na damu kumwagika.
Leo hii tumezoea kusema “tunaenda kumtolea Bwana dhabihu tukimaanisha sadaka zetu za fedha”..lakini kiuhalisia hizo sio dhabihu tunazotoa bali ni sadaka tu!. Na zina baraka zake kubwa tu!, Lakini haziitwi dhabihu, ingawa hatutendi dhambi pia kuziita hivyo.
Sasa swali ni je! Mpaka leo hii tunapaswa tutoe sadaka za dhabihu? Yaani kafara za wanyama?
Jibu ni la! Katika agano jipya hatuna tena sadaka za dhabihu za wanyama, hatuhitaji tuchinje ng’ombe ili tupate kibali fulani au baraka fulani kutoka wa Mungu.
Kadhalika hatuhitaji damu ya kuku, au ya mbuzi, kupata ulinzi fulani wa kiMungu.
Jambo hilo liliwezekanika katika agano la kale, chini ya maagizo maalumu ya Bwana.
Lakini kwa sasa Agano jipya, hatuna hicho tena,
Sasa tunayo dhabihu moja ambayo imeshatolewa inayotufanya tusiwe na haja ya dhabihu za wanyama.
Na dhabihu hiyo Mwanakondoo Yesu Kristo, ambaye alitolewa sadaka kama kafara kwa ajili yetu, na damu yake ndio inayotupa upatanisho sisi na Mungu.
Sadaka nyingine za fedha, mazao, mavazi n.k tunaweza kuzitoa, lakini dhabihu ilishatolewa, na Mungu karidhika na hiyo, na hakuna nyingine yoyote tunaweza kumtolea ikamridhisha.
Waebrania 10:3 “Lakini katika dhabihu hizo liko kumbukumbu la dhambi kila mwaka.
4 Maana haiwezekani damu ya mafahali na mbuzi kuondoa dhambi.
5 Kwa hiyo ajapo ulimwenguni, asema,
Dhabihu na toleo hukutaka, Lakini mwili uliniwekea tayari;6 Sadaka za kuteketezwa na sadaka za dhambi hukupendezwa nazo;
7 Ndipo niliposema, Tazama, nimekuja (katika gombo la chuo nimeandikiwa) Niyafanye mapenzi yako, Mungu.
8 Hapo juu asemapo, Dhabihu na matoleo na sadaka za kuteketezwa na hizo za dhambi hukuzitaka, wala hukupendezwa nazo (zitolewazo kama ilivyoamuru torati),
9 ndipo aliposema, Tazama, nimekuja niyafanye mapenzi yako. Aondoa la kwanza, ili kusudi alisimamishe la pili.
10 Katika mapenzi hayo mmepata utakaso, kwa kutolewa mwili wa Yesu Kristo mara moja tu”.
Umeona hapo?. Kwa kutolewa mwili wa Yesu Kristo mara moja tu tumepata utakaso, hivyo Kristo ndio dhabihu iliyo hai leo.
Sasa swali ni kosa leo kuchinja kafara za wanyama?
Jibu ni ndio! kama wakristo hatupaswi leo kushiriki ibada zozote za kafara!. Wengi leo wanasema ni wakristo lakini vijijini kwao wanatoa kafara!..pasipo kujua kuwa wanamtolea dhabihu shetani na si Mungu.
Bwana atujalie neema yake, tuzidi kumjua yeye zaidi na mapenzi yake.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
Mahali pa juu palikuwa ni wapi kama tunavyosoma katika biblia?
Swali: Kurushwa upesi kunakozungumziwa katika Danieli 9:21 ndio kupi?
Vipindi vya ukristo huwa vinabadilika, mambo hayawezi kubaki vilevile tangu siku ulipookoka hadi siku unakufa. Yapo majira utamwona Kristo waziwazi katika Maisha yako, yapo majira Kristo hutamwona kwa uwazi kama unavyodhani, hapo ndipo itakapokugharimu kumtafuta, ili umpate.
Hiyo ni kanuni Mungu aliyoiweka, ambayo kila mtu aliyempokea yeye hana budi kuifahamu. Kuna watu wanashindwa kulielewa hili, na ndio maana wanapofikia hatua ya kutomwona Kristo kiurahisi, kama ilivyokuwa zamani wanaishia kurudi nyuma. Wakidhani kama hakuwa ni Mungu aliyewaita.
Embu tuitazame ile Habari ya mamajusi, wale watu walitokea nchi ya mbali sana huko Mashariki (Pengine nchi ya Babeli), lakini katika kutafuta tafuta kwao Habari za Mungu katika mambo yao ya anga, Mungu aliwapa neema ya kumwona Kristo katika njia hiyo.
Ndipo wakaiona nyota moja tofauti na nyingine iking’ara sana, na ghafla ile nyota ikaja kutua ulimwenguni, lakini haikutua sehemu nyingine yoyote Zaidi ya taifa la Israeli.. Ndipo wakaanza safari ya kuifuata.
Hivyo walipofika Israeli walitarajia kuwa wangeiona tena iwaelekeze mpaka eneo husika mtoto alipo, lakini hilo halikutokea, pengine wakatazama tena angani kwa umakini zaidi, lakini hawakuona chochote.. Hatujui ilipita muda gani wakiingojea itokee, lakini hakuna chochote kilichotokea, ndipo wakaanza kutafuta, kwa kuulizia Habari za Kristo kazaliwa awpi, wakafika mpaka wa Herode mfalme, kuulizia Habari hizo, ndipo wakapewa taarifa, kutoka kwa Herode kuwa mfalme anazaliwa Bethelehemu ya uyahudi..
Sasa wakati wanakwenda Bethlehemu ndipo ile nyota waliyokuwa wameipoteza wakaiona tena, katika nyumba aliyokuwa amelazwa mtoto, biblia inasema walipoiona walifurahi furaha kubwa mno,
Tusome..
Mathayo 2 :1 “Yesu alipozaliwa katika Bethlehemu ya Uyahudi zamani za mfalme Herode, tazama, mamajusi wa mashariki walifika Yerusalemu, wakisema,
2 Yuko wapi yeye aliyezaliwa mfalme wa Wayahudi? Kwa maana tuliiona nyota yake mashariki, nasi tumekuja kumsujudia.
3 Basi mfalme Herode aliposikia hayo, alifadhaika, na Yerusalemu pia pamoja naye.
4 Akakusanya wakuu wa makuhani wote na waandishi wa watu, akatafuta habari kwao, Kristo azaliwa wapi?
5 Nao wakamwambia, Katika Bethlehemu ya Uyahudi; kwa maana ndivyo ilivyoandikwa na nabii,
6 Nawe Bethlehemu, katika nchi ya Yuda, Hu mdogo kamwe katika majumbe wa Yuda; Kwa kuwa kwako atatoka mtawala Atakayewachunga watu wangu Israeli.
7 Kisha Herode akawaita wale mamajusi faraghani, akapata kwao hakika ya muda tangu ilipoonekana ile nyota.
8 Akawapeleka Bethlehemu, akasema, Shikeni njia, mkaulize sana mambo ya mtoto; na mkiisha kumwona, nileteeni habari, ili mimi nami niende nimsujudie.
9 Nao waliposikia maneno ya mfalme, walishika njia; na tazama, ile nyota waliyoiona mashariki ikawatangulia, hata ikaenda ikasimama juu ya mahali alipokuwapo mtoto.
10 Nao walipoiona ile nyota, walifurahi furaha kubwa mno.
11 Wakaingia nyumbani, wakamwona mtoto pamoja na Mariamu mamaye, wakaanguka wakamsujudia; nao walipokwisha kufungua hazina zao, wakamtolea tunu; dhahabu na uvumba na manemane.
12 Nao wakiisha kuonywa na Mungu katika ndoto wasimrudie Herode, wakaenda zao kwao kwa njia nyingine”.
Nachotaka uone ni kuwa, nyota ilionekana, ikapotea, ikaonekana tena..Lakini hawakukata tamaa na kusema turudi mashariki, tukaendelee na shughuli zetu, tuliona maruweruwe hapana, bali walimtafuta Kristo kwa bidii, na mwisho wa siku wakafika walipopakusudia.
Kipindi cha awali cha wokovu, ni rahisi kumwona Kristo katika kila hatua, lakini upo wakati atabadilisha mwonekano wake, atataka umtafute, atataka upate maarifa ya kutosha kuhusu yeye, hapo ndipo kunapokuja kujifunza kwa bidii, kuulizia Habari za wokovu, Habari za mbinguni, Habari za umilele, kuomba na kufunga, sio kukaa tu na kusema mimi nimeokoka Yesu ananipenda, halafu basi, hilo halipo katika safari ya wokovu.. Bwana ataruhusu hata wakati mwingine umtafute kutoka kwa maadui zake, kama vile mamajusi walivyotafuta taarifa kwa Herode adui wa Kristo.
Hivyo usiporudi nyuma, usipokata tamaa, ni uhakika kuwa mwisho wako utakuwa ni uzima wa milele. Hakuna mtu yeyote anayemtafuta Kristo kwa kumaanisha mwisho wake ukawa ni mbaya hakuna. Utamwona tu Kristo mwishoni. Utamfurahia kwa furaha kubwa, kuanzia hapa duniani hadi kule mbinguni.
Hivyo, ikiwa upo katika hatua kama hii, usipunguze mwendo wako, kinyume chake ndio uzidishe kumtafuta Bwana kwa bidi kwasababu ndivyo unavyokaribia kukutana naye tena.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
Naomba ufafanuzi wa mwanzo 3:14..kwamba hivi laana iliyotamkwa pale na Mungu kwamba nyoka atakula mavumbi…..hivi ni kweli nyoka anakula mavumbi leo?.
Jibu: Jibu ni la! Nyoka hali mavumbi leo na hakuwahi kula mavumbi kabla, na hakuna kiumbe hai cha Mungu chochote kinachokula mavumbi, kwasababu mavumbi si chakula.
Lakini kwanini biblia iseme Nyoka atakula mavumbi,
Labda tusome mistari hiyo, ili tuweze kuelewa kidogo..
Mwanzo 3:14 “BWANA Mungu akamwambia nyoka, Kwa sababu umeyafanya hayo, umelaaniwa wewe kuliko wanyama wote, na kuliko hayawani wote walioko mwituni; kwa tumbo utakwenda, na mavumbi utakula siku zote za maisha yako”
Hapo utaona matokeo ya Nyoka kuambiwa atatembea kwa tumbo ni kula Mavumbi.
Maana yake hapo kwanza alikuwa hatembei kwa tumbo, hivyo alikuwa hali mavumbi.
Maana yake sababu nyoka kula mavumbi ni kwasababu anatembea kwa tumbo.
Sasa anakulaje mavumbi? Hali kama chakula kwasababu vumbi haliwezi kuwa chakula, bali katika ile hali nyoka waliyopo ya kutembea kwa tumbo, maana yake nyuso zao, pua zao, na macho yao yapo katika usawa wa ardhi, hivyo kitendo cha kuchafuka kwa mavumbi wakati wanatembea kwa tumbo ni sawa na kula mavumbi, kwasababu kimo cha mdomo kipo karibu na usawa wa ardhi, tofauti na wakati hajalaaniwa.
Hebu wewe tengeneza picha sasahivi unaambiwa utambae kwa tumbo umbali wa kilometa moja, hebu jiulize safari yako mpaka iishe utakuwa umekula vumbi kiasi gani?. Ndivyo ilivyokuwa kwa Nyoka.
Hapo kwanza kabla Nyoka hajalaaniwa, alikuwa hatembei kwa tumbo hivyo alikuwa hali mavumbi, ni viumbe wengine tu wanaotambaa ndio waliokuwa wanakula mavumbi, kama mijusi, kenge n.k hivyo Nyoka naye akawa kama hao..
Utauliza ni wapi katika maandiko panaonyesha kuwa kuna viumbe wengine wanaokula mavumbi tofauti na nyoka.
Mika 7:17 “Watayaramba mavumbi kama nyoka, kama vitu vitambaavyo juu ya nchi watatoka katika mahali walimojificha, wakitetemeka; watakuja kwa BWANA, Mungu wetu, kwa hofu, nao wataogopa kwa sababu yako”.
Lakini ni somo gani tunalipata kwa Nyoka kutembea kwa matumbo na kula mavumbi?.
Umeona?..sio Nyoka peke yake anayelamba mavumbi.
Somo kuu tunaloweza kulipata ni kwamba tunapoasi na kujitenga na Mungu, basi tunajipeleka wenyewe mavumbini, kiroho na kimwili, Nyoka alikuwa hatembei kwa matumbo lakini akajikuta anatembea kwa matumbo na kuyalamba mavumbi ya nchi.
Lakini habari nzuri ni kwamba tunapotubu, Bwana anatutoa mavumbini, na kutupandisha juu.
1 Samweli 2:8 “Humwinua mnyonge kutoka mavumbini,
Humpandisha mhitaji kutoka jaani, Ili awaketishe pamoja na wakuu,
Wakakirithi kiti cha enzi cha utukufu, Kwa maana nguzo za dunia zina BWANA, Naye ameuweka ulimwengu juu yake”
Inawezekana leo upo mavumbini, na unakula mavumbi pasipo kujijua.
Tubu leo, mpokee Yesu naye atakupa uzima wa milele, na kukutoa mavumbini kiroho na kimwili.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
NJIA YA KUPATA WOKOVU.
Je! Shetani alitolea wapi uovu?
MTI WA UZIMA NA MTI WA MAARIFA.
DALILI NYINGINE INAYOUTAMBULISHA UZAO WA NYOKA
UWEZO WA KIPEKEE.
SWALI: Wanafunzi wa Yesu, walimaanisha nini kusema kama “Mambo ya mtu na mkewe yakiwa hivyo, haifai kuoa”?
JIBU: Walisema hivyo, baada ya kusikia majibu ya swali lililoulizwa na Mafarisayo kwa Bwana Yesu. Ambapo swali lenyewe lilikuwa linahusiana na talaka katika ndoa, Hivyo wakataka kujua je! Ni sawa mtu kumpa talaka mwanamke kwa sababu yoyote ile mtu anayoiona mbele yake?.
Waliuliza hivyo wakitazamia, majibu ya “Ndio” kutoka kwa Yesu, Lakini kinyume chake, Bwana aliwaambia, Mtu hapaswi kumwacha mke wake, kwa kila sababu anayoiona tu, labda ni mchafu, au mchoyo, au msengenyaji, au hawapendi ndugu zako, au anakudharau, n.k. Hapana, bali sababu tu ambayo aruhusiwa kumwacha mke wake ni ile ya usherati tu, lakini nyingine hakuna..
Mitume waliposikia hayo majibu, ndipo hapo wakamwambia sasa, kama Mambo ya mtu na mkewe yakiwa hivyo, haifai kuoa.. Ikiwa na maana kuwa kama sababu ni moja tu ya uzinzi? Mbona itahitaji uvumilivu mwingi sana kuiishi hiyo ndoa?.
Embu tusome…
Mathayo 19 :1 Ikawa Yesu alipomaliza maneno hayo, akatoka Galilaya akafika mipaka ya Uyahudi, ng’ambo ya Yordani.
2 Makutano mengi wakamfuata, akawaponya huko.
3 Basi Mafarisayo wakamwendea, wakamjaribu, wakimwambia, Je! Ni halali mtu kumwacha mkewe KWA KILA SABABU?
4 Akajibu, akawaambia, Hamkusoma ya kwamba yeye aliyewaumba mwanzo, aliwaumba mtu mume na mtu mke,
5 akasema, Kwa sababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja?
6 Hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi aliowaunganisha Mungu, mwanadamu asiwatenganishe.
7 Wakamwambia, Jinsi gani basi Musa aliamuru kumpa hati ya talaka, na kumwacha?
8 Akawaambia, Musa, kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu, aliwapa ruhusa kuwaacha wake zenu; lakini tangu mwanzo haikuwa hivi.
9 Nami nawaambia ninyi, Kila mtu atakayemwacha mkewe, isipokuwa ni kwa sababu ya uasherati, akaoa mwingine, azini; naye amwoaye yule aliyeachwa azini.
10 Wanafunzi wake wakamwambia, Mambo ya mtu na mkewe yakiwa hivyo, haifai kuoa.
11 Lakini yeye akawaambia, Si wote wawezao kulipokea neno hili, ila wale waliojaliwa.
Maana yake ni kwamba, Mwanamke anaweza akawa sio mzinzi, lakini hana heshima katika nyumba, na tayari kashakuwa mke wako, hapo hauruhusiwi kumwacha, utaendelea naye tu hivyo hivyo mpaka kifo kitakapowatenganisha, Ikiwa mke wako ni mshirikina, na haachi kufanya hivyo vitendo, hupaswi kumwacha na kwenda kuoa mwingine, utaendelea naye hivyo hivyo bila amani mpaka kufa kwako..
Ikiwa mke wako, ni mgumba, hawezi kuzaa, na mmeshaingia katika ndoa, hata kama hatazaa milele utaendelea naye hivyo hivyo bila watoto mpaka kufa kwako..hakuna kutoka nje ya ndoa.
Kanuni hii inatumika pande zote mbili pia hata kwa mwanamke, ikiwa mume wako ulipooana naye alikuwa hanywi pombe, lakini sasa hivi ni mlevi wa kupindukia na ameshindwa kurekebikika, hauruhusiwi kumwacha, utaendelea kuishi naye hivyo hivyo, mpaka kufa kwake,
Kama, alikuwa ni tajiri lakini sasa amefilisika, au kafukuzwa kazi, utaishi naye katika hiyo hali, Kama amepata ajali ni mlemavu, au anamadhaifu Fulani ya kindoa, utaishi naye hivyo hivyo..hakuna talaka
Ndio maana Mitume wakamwambia Bwana, ikiwa mambo ya mtu na mke wake yako hivi ni heri basi mtu aishi bila kuoa, kuepuka hayo yote.
Hivyo Habari hiyo inatufundisha kuwa, kabla ya kuingia katika ndoa tutambue kuwa zipo na changamoto zake nyingi sana,hivyo tuwe tayari kuzibeba, Lakini kama tutaona ni nzito kwetu basi ni heri tubakie kama tulivyo, tusioe wala tusiolewe. Kwani ni vizuri Zaidi, kwa Mungu.
Mithali 21:9 “Ni afadhali kukaa katika pembe ya darini, Kuliko katika nyumba pana pamoja na mwanamke mgomvi…
9 Ni afadhali kukaa katika nchi ya nyika; Kuliko na mwanamke mgomvi, mchokozi”.
Fikiri mara mbili,
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 1: Upande wa wanaume)
KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 2: Upande wa wanawake)
NJIA SAHIHI YA KUMPATA MWENZA WA MAISHA KIBIBLIA.
NINI KINATOKEA BAADA YA KIFO?
Jina la Bwana YESU KRISTO, aliye Mkuu wa mbingu na nchi libarikiwe.
Maandiko yanasema..
2 Wakorintho 5:6 “Basi siku zote tuna moyo mkuu; tena twajua ya kuwa, wakati tuwapo hapa katika mwili, tunakaa mbali na Bwana.
7 (Maana twaenenda kwa imani, si kwa kuona.)
Leo tujifunze nini maana ya “tunaenenda kwa Imani na si kwa kuona”.
Wengi wetu tunadhani kuona kwa macho ndio njia pekee ya kulithibitisha jambo, lakini kiuhalisia kuona sio njia pekee ya kuthibitisha jambo, hata hivyo ni moja ya njia hafifu sana.
Kwa mfano macho hayawezi kupambanua ubwabwa wenye chumvi na ule usio na chumvi, maana yake huwezi kutazama ubwabwa na kujua ule umewekwa chumvi au la!. Macho yatapambanua tu aina ya chakula kilichopo mbele yako, kwamba ule ni ubwabwa na si ugali lakini hayawezi kufanya kitu kingine zaidi ya hicho.
Lakini ulimi unaweza kupambanua vyote, ubwabwa ukiwekwa kinywani ulimi unaweza kupambanua kuwa ule ni ubwabwa na si ugali, vile vile unaweza kupambanua kuwa ubwabwa ule umewekwa chumvi au la!.
Kwahiyo kuona si njia kamilifu ya kuthibitisha jambo.
Na katika mambo ya rohoni ni hivyo hivyo, maandiko yanasema “hatwenendi kwa kuona bali kwa Imani”.
Macho yetu hayana uwezo kamilifu wa kupambanua mambo ya rohoni. Ndio maana leo hii Bwana hajaruhusu tuujue uso wake, au tuwe tunamwona, ndipo tumthibitishe kwamba yupo, au tuweze kumsikia na kumwelewa.
Ni kwasababu hata tukimwona bado hatutamjua, kama vile macho yalivyo na uwezo wa kuona jambo lakini si kuonja jambo. Vivyo hivyo hata leo hii katika maisha haya tukimwona Bwana kwa macho, haitatusaidia sana, zaidi ya kumwona kwa Imani.
Leo hii watu wengi sana wanatafuta kumwona Bwana katika mwili, wengi wanafunga na kuomba Bwana Yesu awatokee kwa namna ya kimwili, wamwone na kuzungumza naye.
(Hata mimi nilishawahi kufanya hivyo, nilifunga na kuomba Bwana anitokee na kusema nami, niliendelea hivyo kwa muda mrefu mpaka Bwana aliponipa ufahamu, na kujua kuwa maombi niombayo sio ya kishujaa bali ni ya kitoto.
Kwamba sio ushujaa kutokewa na Bwana na kuzungumza naye bali ni utoto na uchanga..na wlaa.hakitaniongezea chochote kiroho. Tomaso alitafuta kumwona Bwana kwa namna ya mwili baada ya kufufuka kwake, lakini baada ya kutokewa alidhani atasifiwa na Bwana, lakini hakusifiwa.
Yohana 20:29 “Yesu akamwambia, Wewe, kwa kuwa umeniona, umesadiki; wa heri wale wasioona,wakasadiki”
Nataka nikuambie na wewe usijaribu kufanya hivyo (Ndio unaweza kufanya hivyo, na Bwana akakusikia na kujidhihirisha kwako kwa namna ya kimwili,na ukamwona na mkazungumza), lakini nataka nikuambie Tukio kama hilo kukutokea ni nadra sana kwasababu sio njia kamilifu ya Bwana alitoichagua kwa nyakati hizi.
Ni sawa sawa na mtu aje akuombe wewe mzungumze kwa njia ya barua za posta na si SIMU, kwamba yupo Morogoro halafu akitaka kukujulia hali au kukupa ujumbe fulani basi atumie aandike barua aipeleke posta na kuituma, kisha wewe uipokee na kumjibu kwa njia hiyo hiyo ya posta!.
Umeona? Ni jambo ambalo ni gumu kwako wewe kulifanya kwasababu ni teknolojia ya zamani na inayogharimu fedha na muda.
Kadhalika na njia ya Mungu kuzungumza nasi kimwili kwake ni teknolojia ya Zamani.
Ndio maana ni ngumu leo hii kututokea na kuzungumza nasi.
Bwana Yesu kukaa katika hali hiyo ya kutotutokea tokea kimwili ni yeye ndio kaichagua hiyo njia kwa faida yetu sisi, na si kwasababu sisi ni wenye dhambi ndio maana hatutokei tokei, wala si kwasababu hatuna maombi ya kutosha ndio maana hatutokei..hapana ni kwasababu teknolojia hiyo ni ya zamani kwake na haitufai sana sisi.
Bwana alisema..
Yohana 16:7 “Lakini mimi nawaambia iliyo kweli; yawafaa ninyi mimi niondoke, kwa maana mimi nisipoondoka, huyo Msaidizi hatakuja kwenu; bali mimi nikienda zangu, nitampeleka kwenu”.
Umeona?.. hapo anasema mimi yanipasa niondoke ili msaidizi aje, na Si yeye aondoke kwasababu hatuombi au kwasababu sisi ni wenye dhambi.
Hakuna maombi yoyote ambayo yangeweza kumbakisha Bwana Yesu katika mwili hapa duniani.
Sasa swali “Tunaenendaje kwa Imani”?
Tunaenenda kwa Imani kwa kumpokea huyo Roho Mtakatifu, ambaye amemwagwa kwetu.
Tukimpata huyu hata Bwana Yesu asipotutokea kwa namna ya mwili katika maisha yetu yote, bado tutakuwa tumeyajua Yesu sana, tutakuwa tumemwelewa kwa undani wote kana kwamba yupo nasi katika mwili.
Yohana 16:13 “Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake.
14 Yeye atanitukuza mimi, kwa kuwa atatwaa katika yaliyo yangu na kuwapasha habari.
15 Na yote aliyo nayo Baba ni yangu; kwa hiyo nalisema ya kwamba atatwaa katika yaliyo yangu, na kuwapasheni habari”.
Leo hii wengi hawamtaki Roho Mtakatifu lakini wanamtaka Bwana Yesu katika mwili. Pasipo kujua kuwa Roho Mtakatifu ndio ukamilifu wote wa Bwana Yesu.
Na hawamtaki kwa matendo yao na si kwa midomo, ndio maana hawamwoni Yesu katika maisha yao, ndio maana hawamwelewi na ndio maana shetani anawasumbua sana.
Je na wewe umempata Roho Mtakatifu?
Kama bado na unamtamani uwe naye basi usihofu! Kwasababu haihitaji utoe fedha ili umpate, wala haihitaji ufunge kwa maombi, wala haihitaji uende kwenye shule au chuo cha biblia, wala huhitaji mhubiri au mchungaji ndipo akupatie..
Unachokihitaji sasa ni kanuni ya jinsi ya kumpata, na kanuni hiyo ni rahisi, na ipo katika biblia tu! Na hakuna sehemu nyingine unaweza kuipata.
Na kanuni hiyo ni KUTUBU DHAMBI ZAKO KWA KUMAANISHA KUTOZIFANYA TENA, NA KUBATIZWA!!…Basi!!!
Matendo 2:37 “Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?
38 Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.
39 Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie”.
Hapo mstari wa 39 hbiblia inasema… “Ahadi hiyo ni kwaajili YENU na watoto wenu”..
Maana yake ni kwaajili yako na wewe ndugu yangu!.
Sasa kama kanuni ni rahisi hivyo kwanini leo hii usitubu, na kwanini leo hii usibatizwe kwa jina la Yesu?
Bwana akupe kuchagua njia bora!
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
Shalom.
Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze biblia..
Maandiko yanasema.
Waefeso 6:10 “Hatimaye, mzidi kuwa hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu zake”.
Biblia inatufundisha kuwa mahodari katika Bwana na vile vile katika Uweza wa Nguvu zake.
Hapo kuna vitu viwili, 1). Kuwa Hodari katika Bwana. 2) Kuwa hodari katika uweza wa nguvu zake.
1) Kuwa hodari katika Bwana ni kupi?.
Kuwa Hodari katika Bwana ni katika kumtafuta yeye; yaani, kujituma katika kuutafuta uso wake.
Marko 12:30 “nawe mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote, na kwa nguvu zako zote.
2) Kuwa hodari katika uweza wa nguvu zake.
Kuwa hodari katika uweza wa nguvu zake ni kuwa na uwezo wa kuzitumia zile silaha za roho ambazo tunazisoma katika mistari inayofuata.
Tusome,
Waefeso 6:10 “Hatimaye, mzidi kuwa hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu zake.
11 Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani.
12 Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.
13 Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama.
14 Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani,
15 na kufungiwa miguu utayari tupatao kwa Injili ya amani;
16 zaidi ya yote mkiitwaa ngao ya imani, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu.
17 Tena ipokeeni chapeo ya wokovu, na upanga wa Roho ambao ni neno la Mungu”.
Biblia inatuasa tuwe hodari, tusiwe walegevu, kwasababu uweza wa Mungu unadhihirika katika uhodari wetu katika kuzitumia silaha hizo za roho.
Na silaha hizo ndio hizo zilizotajwa hapo ambazo ni Chepeo ya wokovu, Dirii ya Haki, Upanga wa Roho, Utayari miguuni, Kweli kiunoni na ngao ya Imani.
Askari ambaye si hodari ni yule ambaye anazo silaha lakini hana ujuzi au utaalamu wa kutosha wa kuzitumia.
Askari aliyeshika upanga halafu hana ujuzi wa kutosha namna ya kuutumia, adui akija atamdhuru pamoja na silaha yake.
Kadhalika na sisi tunapoushikilia upanga wa Roho, ambao ni Neno la Mungu, na tukawa hatujui namna ya kulitumia inavyopaswa, adui yetu shetani anaweza kutudhuru kirahisi au kutupokonya upanga huo na kutudhuru nao.
Ndio maana utaona Bwana alipokuwa kule jangwani, shetani alipomjia kumjaribu kupitia Neno la Mungu, Bwana alikuwa ni hodari katika kulitumia Neno, hivyo alimjibu shetani kwa kumwambia “tena imeandikwa”.
Au kama Apolo alivyokuwa hodari katika maandiko.
Matendo 18:24 “Basi Myahudi mmoja, jina lake Apolo, mzalia wa Iskanderia, mtu wa elimu, akafika Efeso; naye alikuwa hodari katika maandiko”.
Hivyo biblia inatuasa tuwe na ujuzi wa kulitumia kihalali Neno la Mungu.
2 Timotheo 2:15 “Jitahidi kujionyesha kuwa umekubaliwa na Mungu, mtenda kazi asiye na sababu ya kutahayari, ukitumia kwa halali neno la kweli”.
Je wewe ni hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu zake?.
Je umejivika silaha za wokovu, na kuweza kusimama, na kuzipinga hila za shetani.
1 Wakorintho 16:13 “Kesheni, simameni imara katika Imani, fanyeni kiume, mkawe hodari”.
Bwana atubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
Kama wakitenda mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu?
Ipo haki na ipo Haki yote.
Mathayo 3:13 “Wakati huo Yesu akaja kutoka Galilaya mpaka Yordani kwa Yohana ili abatizwe.
14 Lakini Yohana alitaka kumzuia, akisema, Mimi nahitaji kubatizwa na wewe, nawe waja kwangu?
15 Yesu akajibu akamwambia, Kubali hivi sasa; kwa kuwa ndivyo itupasavyo kuitimiza haki yote. Basi akamkubali”
Kuna maneno mawili hapo ambayo ningependa tuyatazame. 1) ITUPASAVYO 2) HAKI YOTE.
1) ITUPASAVYO.
Hapo Bwana hajasema, “Ndivyo inipasavyo kuitimiza haki yote” bali amesema “Ndivyo Itupasavyo”.. Maana yake hiyo haki haipaswi kutimizwa yeye peke yake tu, bali watu wote, na hao watu ni wale wote walio upande wake, ndio maana Bwana Yesu akasema Imet ujeupasa, maana yake yeye pamoja na wote watakaomfuata..ni lazima waitimize haki yote.
Sasa hiyo haki yote ni ipi?
2) HAKI YOTE.
Kama tulivyosema ipo haki na ipo haki Yote.
Unapomwamini Bwana Yesu, hapo umeitimiza haki, unaposhiriki meza ya Bwana hapo umeitimiza haki, unapohubiri hapo umetimiza haki, unapoishi maisha ya utakatifu hapo umetimiza haki, lakini bado si haki yote. Haki yote inakamilika na wewe kukamilisha UBATIZO WA MAJI.
Bwana Yesu alikuwa mkamilifu, alikuwa tayari mtakatifu kiasi kwamba asingekuwa na haja ya kubatizwa. Lakini aliona asipobatizwa atakuwa hajaitimiza haki yote.
Sasa kama Bwana Yesu alibatizwa ili kuitimiza haki yote, mimi na wewe leo ni nani tusibatizwe! Au tuone ubatizo hauna maana?.
Kumbuka tena Bwana anasema Imetupasa!!..maana yake sio yeye peke yake tu! Bali yeye na sisi, wote imetupasa kuitimiza Haki ya Mungu.
Katika siku hizi za mwisho shetani anawazuia watu kwa nguvu wasiitimize haki yote, anataka waitimize Nusu haki tu!..kwasababu anajua mtu akiitimiza haki yote atakuwa amempoteza, na yeye bado anataka watu wengi zaidi, wapotee naye kwenye ziwa la moto.
Na kumbuka sio kila ubatizo ni ubatizo sahihi, shetani kashafika mpaka hatua ya kuupindisha ubatizo.
Ubatizo sahihi ni ule wa maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo (Matendo 2:38), na si kwa kunyunyiziwa, Bwana Yesu hakwenda kwa Yohana mbatizaji na kunyunyiziwa, maandiko yanasema “alipanda kutoka majini” na si “kutoka kwenye kikombe chenye maji”.
Marko 1:9 “Ikawa siku zile, Yesu alikuja kutoka Nazareti ya Galilaya, akabatizwa na Yohana katika Yordani.
10 Mara alipopanda kutoka majini, akaona mbingu zinapasuka, na Roho, kama hua, akishuka juu yake”
Yohana alibatiza katika maji mengi sehemu zote (Yohana 3:23).
Sasa swali ni hili: Kama nisipobatizwa kabisa au nikibatizwa kwa ubatizo usio sahihi, baada ya kuujua ukweli sitaokolewa!
Jibu rahisi ni NDIO! Hutakolewa siku ya mwisho, kwasababu umeijua Njia ya Haki na hujaifuata, watakaopata neema ni wale ambao hawakuwahi kusikia kabisa, ambao pengine wangesikia ukweli unaoupata au tunaoupata, wangebadilika haraka sana.
Swali ni je! UMEITIMIZA HAKI YOTE?.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
Uchungu wa mauti ni nini, kibiblia?
Matendo 2:23 “mtu huyu alipotolewa kwa shauri la Mungu lililokusudiwa, na kwa kujua kwake tangu zamani, ninyi mkamsulibisha kwa mikono ya watu wabaya, mkamwua;
24 ambaye Mungu alimfufua, akiufungua uchungu wa mauti, kwa sababu haikuwezekana ashikwe nao.
JIBU: Uchungu wa mauti, ni kufa bila kuwa na matumaini ya kufufuka, yaani kuoza na kupotea kabisa, ndicho kilichowakuta wanadamu wote, waliokufa, kabla ya Kristo walioza wakapotea kabisa, roho zao zikawa zipo ardhini tu, (makao ya wafu), Lakini Bwana wetu Yesu Kristo, yeye alipokufa, hakupotelea mavumbini, wala hakuoza, bali alifufuka siku ya tatu. Akawa mtu wa kwanza, aliyekufa akafufuka, kisha akapaa mbinguni, akiishi milele.
Na ndio maana hapo biblia inasema..
“ambaye Mungu alimfufua, akiufungua uchungu wa mauti, kwa sababu haikuwezekana ashikwe nao”.
Walipodhani, Kristo hawezi kufufuka, mpaka wakamwekea na muhuri na walinzi kwenye kaburi lake, hilo bado halikuwezekana, alifufuka tu. Kwasababu haiwezekani, uchungu wa mauti umshike Bwana.
Hata sasa sisi, sote, tuliomwamini, tunapokufa, uchungu wa mauti hautukamati, na ndio maana siku ile Bwana alipofufuka alifufuka na watakatifu wake akawapeleka peponi, (Mathayo 27:51-53), sisi kama watakatifu tunapokufa hatulali makaburini tena, wala hatuendi jehanamu, bali tunahamishwa na kupelekwa peponi,(sehemu nzuri sana ya raha) tukingojea siku ile kuu ya ukombozi wa miili yetu, ndipo tutakapoichukua miili yetu ardhini, na moja kwa moja tutakwenda mbinguni, Bwana wetu Yesu Kristo alipo.
Lakini kama bado upo nje ya Kristo, uchungu wa mauti, ni lazima ukupate tu, kwasababu ukifa utakwenda jehanamu huko chini, kuteswa, huku ukisubiria siku ile ya ufufuo uhukumiwe, kisha utupwe katika lile ziwa la moto. Ndugu Usichukulie rahisi rahisi kifo kama wewe ni mwenye dhambi, uchungu wa mauti hauelezeki, soma ile Habari ya Tajiri na Lazaro,(Luka 16:19-31) ndipo utapata picha halisi ni nini kinawakuta watu wote, wanaokufa sasa nje ya Kristo.
Je bado unaishi katika dhambi? Bado unaishi Maisha ya uvuguvugu, kumbuka, hakuna anayejua siku yake ya kuondoka hapa duniani, Ikiwa leo ndio siku yako, Jiulize Huko utakapokwenda utakuwa mgeni wa nani?
Majibu tunayo sote mioyoni mwetu.
Shalom.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
Nini maana ya “Uchungu wa mauti ni dhambi, na nguvu za dhambi ni torati”