Category Archive Home

Ashuru ni nchi gani kwa sasa?

Ashuru ni wapi?

Ashuru ilikuwa ni nchi iliyokuwepo maeneo ya Iraq, Uturuki, na Syria..Mataifa haya matatu yamechangia sehemu ya nchi hiyo ya Ashuru, kama vile mataifa matatu (Kenya, Uganda na Tanzania), yalivyo na sehemu katika ziwa Victoria, kadhalika na Iraq, Uturuki na Syria ni sehemu ya Taifa hilo liliokuwa linaitwa Ashuru.

Lakini kwasasa duniani hakuna Taifa linaloitwa Ashuru. Kwani baada ya mataifa hayo matatu kuzaliwa hilo la Ashuru likafa.

Na Uliokuwa mji mkuu wa Taifa la Ashuru, uliitwa NINAWI. Ninawi ndio mji Nabii Yona alioambiwa akahubiri Injili, lakini kinyume chake akakimbilia Tarshishi..Kujua Ninawi ni wapi kwa sasa fungua hapa>NINAWI.

Vile vile kujua Tarshihi ni wapi kwasasa fungua hapa > TARSHISHI.

Asili ya Taifa la Ashuru kibiblia ni kutoka kwa Nimrodi..

Mwanzo 10:8 “Kushi akamzaa Nimrodi, akaanza kuwa mtu hodari katika nchi.

9 Alikuwa hodari kuwinda wanyama mbele za Bwana. Kwa hiyo watu hunena, Kama Nimrodi, hodari wa kuwinda wanyama mbele za Bwana.

10 Mwanzo wa ufalme wake ulikuwa Babeli na Ereku, na Akadi, na Kalne, katika nchi ya Shinari.

11 Akatoka katika nchi ile akaenda mpaka Ashuru, akajenga Ninawi, na Rehoboth-iri, na Kala;

12 na Reseni, kati ya Ninawi na Kala, nao ni mji mkubwa”.

Lakini Taifa la Ashuru ndilo lililowachukua Israeli na kuwapeleka utumwani katika Taifa hilo. Lakini baadaye walirudi katika Taifa lao chini ya amri ya Koreshi Mwajemi.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

Rudi nyumbani

Print this post

Je wale waliomsulubisha Bwana, wataenda mbinguni, kwakuwa walisamehewa?

Bwana Yesu alisema “Baba uwasamehe kwakuwa hawajui walitendalo (Luka 23:34)”. Je kwa kusema hivyo ina maana wote walisamehewa dhambi zao, kiasi cha kwamba hata wangekufa pale wangeenda mbinguni?.


Jibu: Dhambi waliyosamehewa ni hiyo ya kumsulibisha Bwana, na Bwana Yesu aliwasamehe kutoka moyoni, na hivyo Baba aliwasamehe pia.
Lakini kusamehewa kosa hilo, haimaanisha wamesamehewa na mengine yote..haimaanishi wamesamehewa uuaji waliofanya jana, au matusi waliyotukana juzi, au mauaji waliyoyatekeleza wiki iliyopita, au wizi walioufanya mwezi uliopita.

Hapana!..walichosamehewa ni hicho kimoja tu!..yaani kosa hilo la kumsulubisha Bwana Yesu!.

Ni sawa na wewe leo umsamehe mtu aliyekutapeli jana, na hivyo ukaghairi kumpeleka polisi, hiyo haimaanishi kasamehewa dhambi zake zote za utapeli alizowafanyia na wengine. Wewe umemsamehe kweli na Mungu pia kamsamehe.

Lakini hatia za makosa mengine aliyowafanyia wengine bado hajasamehewa mpaka atakapotubu.

Vile vile na waliomsulubisha Bwana walisamehewa tu dhambi hiyo moja ya kumsulubisha Bwana, nyingine zilizosalia walipaswa watubu.(Waungame dhambi zao zote, ndipo wawe salama).

Zaidi sana kama walikufa bila kumwamini Yesu, vile vile watahukumiwa kwa dhambi hiyo, hatakama walisamehewa ile kumsulubisha Bwana.

Yohana 3:18 “Amwaminiye yeye hahukumiwi; asiyeamini amekwisha kuhukumiwa; kwa sababu hakuliamini jina la Mwana pekee wa Mungu.

19 Na hii ndiyo hukumu; ya kuwa nuru imekuja ulimwenguni, na watu wakapenda giza kuliko nuru; kwa maana matendo yao yalikuwa maovu”.

Hivyo kama Bwana Mungu alipanga kuwapiga kwa kosa la kumsulibisha Bwana, alighairi na kuyaondoa hayo madhara, lakini ghadhabu ya makosa mengine waliyoyafanya ilikuwa pale pale, na zaidi sana ghadhabu ya wao kutomwamini Bwana bado haikuondolewa. Hiyo inaondolewa kwa mtu kuyasalimisha maisha yek kwa Yesu.

Hiyo ikitufundisha kuwa tunapaswa tuungame dhambi zetu zote kwa Bwana.

1 Yohana 1:9 “Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote”.
Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

TUMEFANYIKA KUWA WANA WA MUNGU!

FUATILIA NDOTO HII, UTAJIFUZA KITU.

HUYU MELKIZEDEKI NI NANI?

YANAYOENDELEA SASA KATIKA MADHABAHU YA MUNGU ROHONI.

Hema ya kukutania ni nini, na ilikuwaje?

Rudi nyumbani

Print this post

HUJAPEWA MBAWA ZA KUKIMBIA MATATIZO

Ni kawaida mwanadamu anapopitia matatizo mengi au shida nyingi, huwa anatamani hata  afanane na mnyama asiyejua shida, anatamani angekuwa kama ndege apae zake aende mbali na makao ya watu akaishi humo.

Ndivyo Daudi alivyosema..kipindi ambacho anafukuzwa na Sauli huko majangwani, alisema..

Zaburi 55:5-8
[5]Hofu na tetemeko limenijia,
Na hofu kubwa imenifunikiza.
[6]Nikasema, Ningekuwa na mbawa kama njiwa,
Ningerukia mbali na kustarehe.
[7]Ningekwenda zangu mbali, 
Ningetua jangwani.
[8]Ningefanya haraka kuzikimbia
Dhoruba na tufani.

Lakini jinsi Mungu alivyotuumba, kamwe hatuwezi kuzitoroka dhoruba na tufani za maisha…fahamu kuwa watu wanaokuudhi ndio hao hao utaendelea kuishi nao, na kama hutaishi nao nyumba moja, basi kuna kipindi mtakutana tu katika nukta fulani ya maisha..

Maadui zako, watesi wako, pamoja na wachawi hakuna siku Mungu atakutenga nao akupeleke katika dunia yako mwenyewe uishi huko kwa starehe, hicho kipindi hutakaa ukifikie haijalishi wewe ni mtakatifu kiasi gani.

Mungu anachokifanya kwetu ni kutulinda na kutuepusha tu na madhara yao, yasitufikie. Lakini kuishi katikati yao ni jambo endelevu mpaka mwisho.
Bwana Yesu alisema;

Yohana 17:15
[15]Mimi siombi kwamba uwatoe katika ulimwengu; bali uwalinde na yule mwovu.

Wakati mwingine, Mungu anapotaka kukupa rizki, anatumia hata njia ya hao hao, unakula katikati yao wakikuona..

Zaburi 23:5
[5]Waandaa meza mbele yangu,
Machoni pa watesi wangu.
Umenipaka mafuta kichwani pangu,
Na kikombe changu kinafurika.

Hivyo ndugu uliyeokoka, acha kutaabika kwa ajili ya wanadamu, wala usipeleke akili zako mbali sana, ukidhania kuwa hao watu walio na wewe kama mwiba kuna siku watatoweshwa milele, uishi peke yako kwa starehe..Kanuni hiyo Mungu hajaichagua japo tunaitamani.

Zaidi sana jifunze kuyatimiza mapenzi ya Mungu katikati yao. Utakuwa na furaha katika maisha.
Kumbuka Mbawa kama za njiwa hatujapewa wanadamu.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

Kwanini wakristo wengi ni maskini?.

ALAMA KATIKA VIPAJI VYA NYUSO.

KWANINI MTINI KATIKATI YA MIZABIBU?

Swali: Kurushwa upesi kunakozungumziwa katika Danieli 9:21 ndio kupi?

Rudi nyumbani

Print this post

Je shetani anaweza kushusha moto kutoka mbinguni?

Swali: Ayubu alijaribiwa na shetani, iweje biblia iseme “Moto wa Mungu ulishuka kutoka mbinguni kuteketeza kondoo zake”?.


Jibu: Tusome,

Ayubu 1:14 “Huyo alipokuwa akali akinena, akatokea na mwingine, na kusema, Moto wa Mungu umeanguka kutoka mbinguni na kuwateketeza kondoo, na wale watumishi, na kuwaangamiza; mimi peke yangu nimepona, mimi tu, kukuletea habari”.

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo, libarikiwe..

Ikumbukwe kuwa Ayubu pamoja na watumwa wake wote hapo mwanzo hawakujua kuwa ni shetani ndiye anayewajaribu.. Ayubu alijua ni Mungu ndiye kamletea majaribu yote yale, ingawa hakujua sababu.. Halikadhalika watumwa wake wote na marafiki zake wote walijua ni Mungu ndiye katuma moto kuwateketeza wale kondoo na kumpiga Ayubu kwa mapigo yote yale. Ndio maana tunaona hata hapo huyo mtumwa akitaja huo moto, kana kwamba ni kutoka kwa Mungu.

Ni baadaye sana, Mungu alipomtokea Ayubu katika upepo wa kisulisuli na kumfunulia jambo lililokuwa linaendelea rohoni, jinsi shetani alivyopeleka mashitaka mbele zake dhidi yake Ayubu. Ndipo Ayubu alipoelewa sababu ya matatizo yote ni shetani, na aliyewaua wanawe ni shetani, na aliyeleta moto ni shetani na si Mungu…Lakini hapo mwanzo wakati anajaribiwa hakujua hilo.. yeye alijua ni Mungu tu!, ndio maana utaona Ayubu naye alisema..

Ayubu 1:21 “akasema, Mimi nilitoka tumboni mwa mama yangu nili uchi, nami nitarudi tena huko uchi vilevile; BWANA ALITOA, NA BWANA AMETWAA; jina la Bwana na libarikiwe”.

Umeona hapo anasema BWANA AMETOA NA BWANA AMETWAA!!.. Maana yake alikuwa anajua kabisa kuwa aliyewaua wanawe wote 10 ni Mungu, na si shetani!. Ambapo kiuhalisia ni shetani ndiye aliyewaua isipokuwa kwa kibali maalumu kutoka kwa Mungu.

Hiyo inatufundisha nini?.

Tunaweza kupitia majaribu fulani tukadhani ni Mungu kayaleta kumbe ni shetani?..isipokuwa kwa kibali maalumu kutoka kwa Mungu. Na majaribu hayo yamegawanyika katika sehemu kuu (2)

 1. Majaribu ya shetani kwa Mtakatifu.

Kama umesimama katika imani kama Ayubu na unajikuta unapitia majaribu mazito!, kama magonjwa, misiba, dhiki, n.k basi fahamu kuwa ni Mungu kamruhusu shetani akujaribu.. Hivyo simama usiogope kwasababu mwisho wako utakuwa ni mzuri kuliko mwanzo, Kama ulivyokuwa wa Ayubu.

 2. Majaribu ya shetani kwa Mtu ambaye hajaokoka!

Kama hujampokea Yesu, na ni mtu wa kiulimwengu, na unajikuta katika majaribu mazito mazito kama misiba, magonjwa, dhiki, mateso. Jua ni Mungu kamruhusu shetani akujaribu kwa kukuletea hayo matatizo ili utubu umgeukie yeye. Lakini usipoitii sauti ya Mungu na kutubu basi shetani atakumaliza kabisa kabisa. Maana lengo lake yeye(shetani) ni wewe ufe katika dhambi na mateso.

Hivyo suluhisho la haraka hapo ni wewe kumpokea Bwana Yesu, akusafishe dhambi zako na kukuosha na kisha atakupa kipawa cha Roho wake Mtakatifu. Na hivyo ule ulinzi wa kiMungu utaongezeka juu yako.

Hivyo kwa hitimisho ni kwamba shetani ndiye aliyeuleta ule moto!, na si Mungu.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

JE! JICHO LAKO LINAONA NINI KATIKATI YA MAJARIBU?

MAJARIBU MATATU YA YESU KRISTO

USITUPE LULU ZAKO MBELE YA NGURUWE.

KUMBE MUNGU ANAWEZA KUKULIPA KWA USICHOSTAHILI!

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya huu mstari? “Yeye mwenyewe ataokolewa lakini ni kama kwa moto”

Tusome,

1 Wakorintho 3:11 “Maana msingi mwingine hakuna mtu awezaye kuuweka, isipokuwa ni ule uliokwisha kuwekwa, yaani, Yesu Kristo.

12 Lakini kama mtu akijenga juu ya msingi huo, dhahabu au fedha au mawe ya thamani, au miti au majani au manyasi, kazi ya kila mtu itakuwa dhahiri.

13 Maana siku ile itaidhihirisha, kwa kuwa yafunuliwa katika moto; na ule moto wenyewe utaijaribu kazi ya kila mtu, ni ya namna gani.

14 Kazi ya mtu aliyoijenga juu yake ikikaa, atapata thawabu

15 Kazi ya mtu ikiteketea, atapata hasara; ILA YEYE MWENYEWE ATAOKOLEWA; LAKINI NI KAMA KWA MOTO.”.

Awali ya yote ni muhimu kufahamu aina za Hukumu za Mungu.

Kuna aina kuu mbili (2) za Hukumu; 1)Hukumu ya Waovu na 2)Hukumu ya watakatifu.

Hukumu ya waovu ni ile inayotajwa katika Ufunuo 21, ambayo inajulikana kama hukumu ya kiti cheupe cha Mungu. Katika hukumu hii, wafu wote waliokufa katika dhambi watafufuliwa na kuhukumiwa kulingana na matendo yao mabaya waliyokuwa wanaifanya…

Kadhalika ipo hukumu ya Watakatifu, ambayo hii itakuwa mbinguni.

Hii haitakuwa hukumu ya kulaumiwa bali ya thawabu.. Wale walioshinda watasimamishwa mbele za Bwana na kila mtu atapewa thawabu kulingana na utumishi wake hapa duniani. Waliofanya vizuri watapewa thawabu kubwa na wale ambao hawakufanya vizuri sana watapewa thawabu kidogo na wengine hawatapewa kabisa.. Ingawa wataingia mbinguni kwasababu walikuwa watakatifu!.

Hivyo hukumu hiyo inayozungumzwa hapo katika (1 Wakorintho 3:13) ya kazi ya kila mtu kupimwa kwa Moto!, sio hukumu inayowahusu waovu!,  la! bali inayowahusu wale walioshinda, (watakatifu) ambao wataingia mbinguni..

Kwahiyo hawa walioshinda kama huku duniani walikuwa watakatifu lakini katika eneo la utumishi, hawakufanya vizuri..(maana yake waliyapunguza maneno ya Mungu, hawakuwafundisha watu kweli yote)…aidha kutokanana na hofu fulani, au kuhofia shinikizo Fulani..basi siku ile watapata hasara kubwa sana mbinguni.

Kwamfano utaona kuna watu wanajua kabisa, kuwa pasipo utakatifu hakuna mtu atakayemwona Mungu, lakini baada ya kujua hayo, wanaogopa kuwasisitiza watu wawe watakatifu mwilini na rohoni kama wao walivyo, wakihofia kuwakwaza wale watu..utaona wanawaambia tu! Juu juu lakini kamwe hawazami ndani kuwaeleza madhara ya kutokuwa watakatifu. Mwisho wanajikuta wanatengeneza watu wengi ambao hawataenda mbinguni siku ya mwisho, kwasababu ni vuguvugu..bali watatupwa katika ziwa la moto.

Biblia inasema maneno ya Mungu ni kama Moto. Kwahiyo siku ile matunda yao yote yatajaribiwa kwa moto.. (watu wote waliowahubiria wao)..

Sasa moto ni nini?

Biblia inasema maneno ya MUNGU NDIO MOTO!

Yeremia 23:29 “Je! NENO LANGU SI KAMA MOTO? Asema Bwana; na kama nyundo ivunjayo mawe vipande vipande?”

Na mfano wa maneno ya Mungu ambayo ni moto ni haya…

Wagalatia 5:19 “Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi,

20 ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi,

21 husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, KATIKA HAYO NAWAAMBIA MAPEMA, KAMA NILIVYOKWISHA KUWAAMBIA, YA KWAMBA WATU WATENDAO MAMBO YA JINSI HIYO HAWATAURITHI UFALME WA MUNGU.”

Mtu yeyote tuliyemhubiria atajaribiwa kwa Maneno hayo katika siku ile ya Mwisho.. Na kama atafaulu kipimo hicho, maaana yake ataingia mbinguni, kule tulipo sisi, na hivyo sisi tuliyemhubiria tutapata faida!..hapo ndio litatimia hilo neno (… Maana siku ile itaidhihirisha, kwa kuwa yafunuliwa katika moto; na ule moto wenyewe utaijaribu kazi ya kila mtu, ni ya namna gani. Kazi ya mtu aliyoijenga juu yake ikikaa, atapata thawabu).

Lakini matunda tuliyoyahubiria yakifeli hicho kipimo cha maneno hayo, basi yatatupwa katika ziwa la moto na sisi tuliyoyahubiria tutapata hasara!, (hakuna thawabu yoyote tutakayopewa)..na ndio litatimia hilo neno… “Kazi ya mtu ikiteketea, atapata hasara; ila yeye mwenyewe ataokolewa; lakini ni kama kwa moto.”

Sasa kwanini hapo iseme..“Ataokolewa lakini kama kwa moto” ??

Kikawaida mtu anapopata hasara, na huku alitegemea kupata faida! Moyoni hatafurahia sana..tofauti na yule ambaye alitegemea kupata faida na kule akakuta kapata faida kubwa Zaidi.

Hivyo yule aliyepata hasara lakini kaokolewa, ataingia mbinguni huku akiwa amekosa vile alivyovitarajia,(maana alitarajia thawabu kubwa lakini hakuzipata) hivyo hiyo hali ya kukosa vile alivyovitarajia na huku anaona wengine wakivishwa mataji ya ushindi ndio inaitwa “kuokolewa kama kwa moto”.

Baadhi ya dini zinatumia andiko hili kuhalalisha Imani ya “toharani” kwamba mtu akifa katika dhambi, anaweza kupitishwa kwenye mateso ya moto kwa kitambo kichache kisha akatolewa kule.. kwasababu hapo imesema ..“Ataokolewa lakini kama kwa moto”.

Imani hiyo ni Imani potofu, kutoka kwa yule adui shetani, hakuna nafasi ya pili, kwa mtu atakayekufa katika dhambi (Waebrania 9:27). shetani kalipandikiza hilo fundisho katika baadhi ya dini, ili watu wastarehe katika dhambi huku wakiamini kwamba hata wakifa katika dhambi zao, basi ipo nafasi ya pili.. watapitishwa kwenye moto kidogo kisha watatolewa siku moja.

Usidanganyike, wala tusidanganyike!..mtu akifa leo katika dhambi, Habari yake imeisha..atakachotazamia ni hukumu na kisha kutupwa katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti.

Je! Na wewe leo unahubiri injili gani?..unajenga jengo la namna gani?, la nyasi, fito au Mawe ya thamani.

Mawe ya thamani ni wale watu wanaosikia injili ya kweli isiyoghoshiwa, ambayo haujachanganywa na chochote.

Nyasi na fito ni wale watu ambao wanahubiriwa kuwa Mungu haangalii mwili anaangalia tu roho!, ni wale wanaohubiriwa mambo ya ulimwengu tu, hawahubiriwi juu ya hatima ya roho zao.

Je na wewe unatengeneza watu wa namna gani?, unajenga jengo gani?

Maran atha

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

Walakini ataokolewa kwa uzazi wake.

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 2)

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 2)

Nini maana ya ‘Hukumu haina huruma kwake yeye asiyeona huruma’?

Kwanini Paulo, alihukumu wakati hukumu hairuhusiwi?

Rudi nyumbani

Print this post

EE MUNGU, MUNGU WANGU, NITAKUTAFUTA MAPEMA:

Daudi alikuwa ni kijana mdogo, lakini aliona jinsi muda unavyokimbia kweli kweli, aliona jinsi, siku zinavyotoweka kwa kasi, na huku bado hajatengeneza mambo yake sawa na Mungu.

Japokuwa katika hatua aliyofikia tayari alikuwa ni kipenzi cha Mungu, lakini hakuridhika na hali yake ya kiroho, akataka ayatengeneze mapema mambo yake na Mungu, asiwe na doa lolote kwake, Ndipo akaandika Zaburi hii akasema;

ZABURI 63:1 “Ee MUNGU, Mungu wangu, NITAKUTAFUTA MAPEMA, Nafsi yangu inakuonea kiu, Mwili wangu wakuonea shauku, Katika nchi kame na uchovu, isiyo na maji”.

Alijua thamani ya ujana wake, kwamba akiuacha tu ukiyeyuka, mpaka kufikia uzee bila kumtafuta muumba wake, atakuwa ameshindwa vita vikubwa vya Maisha.. Ndio maana akatia bidii sana, kumtafuta Muumba wake mapema, angali bado ni kijana mdogo. Akawa siriazi na Mungu wake,

Alilitambua vizuri lile andiko linalosema..

Mhubiri 12:1 “Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, Kabla hazijaja siku zilizo mbaya, Wala haijakaribia miaka utakaposema, Mimi sina furaha katika hiyo”.

Kwamba ipo miaka ambayo akiifikia mtu hatapata raha yoyote Maishani mwake, kama ujana wake uliishia katika mambo yasiyokuwa na maana.. Hivyo akasema, nitamtafuta Mungu wangu mapema, haijalishi ni mateso gani au vikwazo gani nitavipitia sasa, na akalithibitisha kweli lile alilolisema kwa vitendo.

Hakungojea uzee, au afikishe umri Fulani wa makamo ndio aache njia za uovu, hakufikia uzee ndio amfanye Bwana kuwa ngao yake.. Bali umri wake ule ule wa ujana alimtafuta Mungu wake kwa bidii.

Swali la kujiuliza na wewe kama kijana, au wewe kama mtu mzima, bado unaona una muda wa kusubiri kwa Mungu wako?

Mtafute Mungu wako mapema, kesho si yako. Hizo nguvu za kiroho Mungu alizoziweka ndani yako, hazitakuwepo kesho. Neema ya wokovu, huwa haidumu milele.
Inatabia ya kuzunguka na kuhamia kwa wengine, jambo ambalo watu wengi hawalijui. Ilikuwepo kwa wayahudi, lakini sasa ipo kwetu. Na Mungu ameahidi siku hizi za mwisho itaondoka kwetu itarudi kwa wayahudi tena. Je unalifahamu hilo?

Bwana Yesu alisema..

Yohana 11:9 “… Je! Saa za mchana si kumi na mbili? Mtu akienda mchana hajikwai; kwa sababu aiona nuru ya ulimwengu huu.
10 Bali akienda usiku hujikwaa; kwa sababu nuru haimo ndani yake”.

Akimaanisha kuwa, nuru ya ulimwengu (yaani JUA) huwa linafanya kazi saa 12 tu. Baada ya hapo ni giza. Na ndivyo Yesu anavyoifananisha neema yake na JUA. Kwamba inadumu kwa kipindi Fulani tu, baada ya hapo haitaonekana tena.

Leo hii unaipuuzia injili, hutaki kutubu dhambi zako, kuna wakati nguvu ya kuvutwa kwa Yesu itaondoka kwako na kuamia kwa wengine. Kipindi hicho kikifika, milele hutakaa umgeukie Kristo utabakia kuwa mtu wa kudhihaki na kejeli kwenye mambo ya ki-Mungu. Kwasababu neema iliyokuwa inakuvuta imeshaondoka.

Kuwa makini sana na nyakati hizi za majeruhi. Mtafute Mungu wako mapema. Muda tuliobakiwa nao ni mchache mpaka Kristo atakapokuja, kizazi tunachoishi mimi na wewe, kimekidhi vigezo vyote vya kinabii kushuhudia tukio la unyakuo, na lile la kurudi kwa pili kwa Yesu duniani.. Unadhani tutakuwa na kizazi kingine? Soma biblia vizuri uone.

Unangoja nini?, Unamsubiria nani? Mgeukie Yesu mapema hii. Kanisa tulilopo ndio la saba na la mwisho lijulikanalo kama Laodikia, (Ufunuo 3:14-21), Na hakutakuwa na kanisa lingine Zaidi ya hili.

Tubu dhambi zako kwa kumaanisha, kweli kweli, mimina moyo wako kwa Bwana, salimisha ujana wako kwake, jitwike msalaba wako angali una kipindi kifupi bado, saa ya wokovu ni sasa, sio kesho, kama maandiko yasemavyo.

Ndugu, ikiwa unataka leo, kurudi kwa Bwana wako, na umedhamiria kwa dhati kufanya hivyo, basi fahamu Bwana Yesu anaweza kukupokea na kukusamehe dhambi zako.

Ni wewe tu kumaanisha kufungua moyo wako, kwani leo leo anaweza kukusamehe na kukupokea kama kiumbe kipya kwake. Akakusamehe kabisa dhambi zako. Basi Ikiwa upo tayari kufanya hivyo unaweza tafuta mahali pa utulivu, kisha piga goti, hata kwa machozi fuatisha sala hii ya toba kwa Imani, na Bwana atakusamehe;

Sema…

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.
ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.
AMEN.

Unaweza kurudia tena hiyo sala, hata mara mbili au tatu, mpaka utakaposikia amani moyoni mwako.

Basi ikiwa umekamilisha hilo..Hatua iliyobakia kwako ni ubatizo, kama hukubatizwa ipasavyo kwa maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo.

Ikiwa utahitaji msaada huo na mafundisho ya kuukulia wokovu basi unaweza wasiliana nasi kwa namba zetu hizi;

+255693036618/ +255789001312

Tafadhali shea na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

MAISHA ULIYOPITIA NYUMA NI USHUHUDA TOSHA WA WEWE KUMTUMIKIA MUNGU

KWANINI DAUDI ALIKUWA NI MTU ALIYEUPENDEZA MOYO WA MUNGU?

Je Lutu alikwenda kuwahukumu watu wa Sodoma na Gomora? Kulingana na Mwanzo 19:9?

WAPE WATU WANGU RUHUSA ILI WAPATE KUNITUMIKIA.

HUTATAMBUA LOLOTE, SIKU YA UNYAKUO IKIFIKA.

Rudi nyumbani

Print this post

TUYATENDE MAMBO YOTE KWA UZURI NA UTARATIBU.

Ipo kanuni moja ya kuuvuta uwepo wa Mungu na miujiza ya kiMungu karibu nasi. Na kanuni yenyewe ni KUKAA KATIKA UTARATIBU. Mungu siku zote ni Mungu wa utaratibu!, mahali pasipo na utaratibu basi pia Mungu hayupo hapo!.. Hiyo ndio kanuni yake, na hawezi kubadilika!, yeye siku zote atabaki kuwa wa utaratibu…

1Wakorintho 14:40 “Lakini mambo yote na yatendeke kwa UZURI NA KWA UTARATIBU”.

Upo utaratibu katika Nyumba ya Mungu. Ambao huo tukiufuata basi tutaona baraka za Mungu zikijizidisha kwa kasi sana… Na utaratibu wenyewe ni kukaa katika mipaka.

Kanisa likikosa mipaka ya Jinsia, Umri, na Marika.. Ni ngumu Mungu kutembea hapo, kadhalika likikosa utaratibu wa utendaji wa karama, pia kuna shida!. Katika kanisa Wanawake hawana budi kujitofautisha na wanaume, kimwonekano na kiutendaji.. Kadhalika kanisa ni lazima kuwe na utaratibu bora na mpangilio bora..

Hebu tujifunze mfano mmoja kwenye biblia, ambao utatusaidia kuelewa Zaidi..

Marko 6:38 “Akawaambia, Mnayo mikate mingapi? Nendeni mkatazame. Walipokwisha kujua wakasema, Mitano, na samaki wawili.

39 AKAWAAGIZA WAWAKETISHE WOTE, VIKAO VIKAO, PENYE MAJANI MABICHI.

40 WAKAKETI SAFU SAFU, HAPA MIA HAPA HAMSINI.

41 Akaitwaa ile mikate mitano na wale samaki wawili, akatazama mbinguni, akashukuru, akaimega ile mikate, akawapa wanafunzi wake wawaandikie; na wale samaki wawili akawagawia wote.

42 Wakala wote wakashiba.

43 Wakaokota vipande vilivyomegwa vya kuweza kujaza vikapu kumi na viwili; na vipande vya samaki pia.

44 Na walioila ile mikate WAPATA ELFU TANO WANAUME”.

Umeona hapo?..Bwana asingeweza kuigawa ile mikate mahali ambapo hapakuwa na utaratibu!, watu wamekaa shaghala bhagala, watu wamechanganyikana wanaume na wanawake Pamoja.. Lakini walipokaa katika safu, na katika vikao vikao, ndipo ilipojulikana idadi ya Wanaume na wanawake na Watoto.. Na ndipo Bwana akaongeza baraka zake.

Na sisi pia hatuna budi kukaa katika safu, tuwapo katika nyumba ya Mungu, hatuna budi kujipanga na kujitofautisha kwasababu Mungu anafanya kazi zake katika utaratibu.. Hali kadhalika karama hazina budi kufanya kazi katika utaratibu.. Mmoja akiongea sharti wengine wote watulie wasikilize..

1Wakorintho 14:29 “Na manabii wanene wawili, au watatu, na wengine wapambanue.

30 Lakini mwingine aliyeketi akifunuliwa neno, yule wa kwanza na anyamaze.

31 Kwa maana ninyi nyote mwaweza kuhutubu mmoja mmoja, ili wote wapate kujifunza, na wote wafarijiwe.

32 Na roho za manabii huwatii manabii.  Kwa maana Mungu si Mungu wa machafuko, bali wa amani; vile vile kama ilivyo katika makanisa yote ya watakatifu”.

Vile vile wanawake katika kanisa wanapaswa wawe watulivu..Maandiko yanasema wanawake wajifunze katika utulivu.. Huo ni utaratibu Mungu aliouweka!.. tukiuvunja huo Basi hata Bwana hatatuvunjia mikate ya baraka..Tutabaki na vurugu zetu, na hatutaambulia chochote!.

Je upo katika Safu?..upo katika utaratibu wa Bwana?..Upo katika utulivu?

Je unaingia nyumbani kwa Bwana kama unavyoingia disko?..fahamu kuwa unajipunguzia baraka zako mwenyewe..Nyumbani kwa Bwana sio kijiwe cha kupiga stori wala jukwaa la matamasha, kwamba unaweza kukaa tu utakavyo na kufanya utakalo.

Bwana atusaidie tukae katika utaratibu wake.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

TUJIFUNZE JAMBO KWA WANAWAKE HAWA WAWILI:

NAMNA YA KUMTAMBUA BIBI ARUSI WA KWELI WA KRISTO.

MAMA UNALILIA NINI?

MAMA UNALILIA NINI?

MWANAMKE, BINTI, MAMA. (Sehemu ya 3)

Rudi nyumbani

Print this post

MUNGU ALIVICHAGUA VITU AMBAVYO HAVIKO.

Nakusalimu katika jina kuu la Bwana wetu Yesu Kristo, ukuu na uweza vina yeye milele na milele. Amina.

Mtume Paulo aliandika, ANGALIENI MWITO WENU, Akiwa na maana, kwamba tunapaswa tuwe na ufahamu tosha juu ya wito wa Mungu katika Maisha yetu jinsi unavyokuja. Tofauti na tunavyodhani kuwa Mungu akikuuita, ni mpaka uwe shupavu au hodari Fulani. Mpaka uwe na miguu miwili, mpaka uwe na digrii Fulani ya dini, mpaka uwe na kipato Fulani au familia nzuri, mpaka uwe na kipaji Fulani cha kitofauti, Hapana..

Bali yeye huwa anakwenda kinyume chake..Tunalithibitisha hilo katika vifungu hivi;

1Wakorintho 1:26 “Maana, ndugu zangu, angalieni mwito wenu, ya kwamba si wengi wenye hekima ya mwilini, si wengi wenye nguvu, si wengi wenye cheo walioitwa;

27 bali Mungu aliyachagua mambo mapumbavu ya dunia awaaibishe wenye hekima; tena Mungu alivichagua vitu dhaifu vya dunia ili aviaibishe vyenye nguvu;

28 tena Mungu alivichagua vitu vinyonge vya dunia na vilivyodharauliwa, naam, VITU AMBAVYO HAVIKO, ili avibatilishe vile vilivyoko;

29 mwenye mwili awaye yote asije akajisifu mbele za Mungu”.

Bwana anasema, anavichagua vitu ambavyo haviko, akiwa na maana sio kwamba haviko kabisa ulimwenguni, hapana, bali uwepo wake, ni kama tu vile haviko. Kwamfano nikija na kukutajia nchi kama “Marekani” au “Ufaransa” ni wazi kuwa ulishawahi kuzisikia mahali Fulani nchi hizi, kwasababu kila siku zinatajwa aidha katika vyombo vya Habari au midomoni mwa watu, Lakini nikikutajia nchi kama “Tuvalu” au “Kiribati” pengine leo ndio inaweza ikawa mara yako ya kwanza kuzisikia hizi nchi, Ni kama vile hazipo duniani sio ndio!. Lakini ni nchi ambazo zipo, na zinamfumo huru unaojiendesha kama tu vile nchi yako.

Vivyo hivyo, wito wa Mungu, unachagua, watu ambao “hawapo” yaani wasiojulikana, wasiosikika hata katika masikio ya watu, waliosahaulika zamani, kama vile Daudi, alivyoitwa hao akiwa huko maporini, ndio jicho la Mungu linawatazama sana, ili awatumie.

Pengine umekata tamaa, au unajidharau, au unajiona wewe si kitu, huna elimu yoyote, huna uzuri, huna ujuzi, upo upo tu, huna marafiki wengi, huwezi kujichanganya sana, pengine ni mlemavu, au ni mzito wa kutenda,.

Nataka nikuambie, wito wa Mungu upo karibu sana na wewe kuliko unavyodhani, kuliko kwa watu wenye nguvu, ikiwa tu, utakubali kujisogeza karibu na yeye. Wengi wa Mitume wa Kristo walikuwa hawana elimu yoyote biblia inasema hivyo katika ( Matendo 4:13), walikuwa ni wavuvi tu, lakini walipoitwa na Mungu, walitii na kumfuata kwa ukamilifu wote, bila kuwa na mawazo mawili mawili. Na ndio hao Mungu aliwatumia kwa viwango vya juu mpaka, tunawaita mababa wa Imani.

Na sisi pia, tusione madhaifu yetu, au unyonge wetu, kama ndio sababu ya kutomtumikia Mungu, kinyume chake, ndio tumtafute kwa bidii kwasababu katika hali hizo wito wake ndio mkubwa kushinda pale tunapokuwa na nguvu.

Udhaifu wowote, tuunaona ndani yetu, ndio uweza wa Mungu unapotimilikia hapo.

2Wakorintho 12:9 “Naye akaniambia, Neema yangu yakutosha; maana uweza wangu hutimilika katika udhaifu. Basi nitajisifia udhaifu wangu kwa furaha nyingi, ili uweza wa Kristo ukae juu yangu.

10 Kwa hiyo napendezwa na udhaifu, na ufidhuli, na misiba, na adha, na shida, kwa ajili ya Kristo. Maana niwapo dhaifu ndipo nilipo na nguvu”.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

Amri zilizo ndogo alizozizungumzia Yesu ni zipi?

Chuo cha vita vya Bwana ni kipi?(Hesabu 21:14)

JE WEWE NI LAZARO YUPI, WA KWANZA AU WA PILI?

Rudi nyumbani

Print this post

Sinagogi kufumakana maana yake nini? (Matendo 13:43).

Jibu: Tusome,

Matendo 13:42 “Na walipokuwa wakitoka, wakawasihi waambiwe maneno haya sabato ya pili.

43 SINAGOGI ILIPOFUMUKANA, Wayahudi na waongofu watauwa wengi wakashikamana na Paulo na Barnaba; ambao, wakisema nao, wakawatia moyo kudumu katika neema ya Mungu.

44 Hata sabato ya pili, watu wengi, karibu mji wote, wakakusanyika walisikie neno la Mungu.

45 Bali Wayahudi, walipowaona makutano, wakajaa wivu, wakayakanusha maneno yaliyonenwa na Paulo, wakibisha na kutukana”.

Maana ya Sinagogi KUFUMUKANA ni sinagogi Kutawanyika!.. Yaani Tendo la watu kutawanyika baada ya ibada, ndio KUFUMUKANA!. Hivyo mstari huo ili ueleweke vizuri tunaweza kuuweka hivi..

Matendo 13:42 “Na walipokuwa wakitoka, wakawasihi waambiwe maneno haya sabato ya pili.

43 WATU WALIPOTAWANYIKA Wayahudi na waongofu watauwa wengi wakashikamana na Paulo na Barnaba; ambao, wakisema nao, wakawatia moyo kudumu katika neema ya Mungu”.

Tunachoweza kujifunza katika Habari hiyo ni Utayari wa Mitume wa kanisa la kwanza katika kuhubiri injili. Waliweza kuingia kila mahali na kuwafanya watu wamgeukie Kristo kwa nguvu nyingi za Roho, hata kila mahali baada ya mahubiri yao, watu wengi waliungana nao.

Na sisi hatuna budi kuwa na bidii katika kuifanya kazi ya Mungu kama waliyokuwa nayo Mitume, ili Bwana atuongezee Neema yake.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

MAWE YALIYOKWISHA KUCHONGWA MACHIMBONI.

TOFAUTI KATI YA HEKALU, SINAGOGI NA KANISA NI IPI?

Nini maana ya msiwe waalimu wengi (Yakobo 1:3)?

JISHUSHE ILI MUNGU AKUHUDUMIE.

WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.

Rudi nyumbani

Print this post

Na ulimi laini huvunja mfupa.(Mithali 25:15)

SWALI: Biblia ina maana gani kusema “Na ulimi laini huvunja mfupa”? (Mithali 25:15)

Mithali 25:15 “Kwa uvumilivu mwingi mkuu husadikishwa; Na ulimi laini huvunja mfupa”.


JIBU: Ulimi ni kiungo kilaini kuliko vyote katika mwili. Lakini biblia inatupa ufunuo wake, kuwa kinauwezo  wa kuvunja mifupa?

Je kinavunjaje mifupa?

Hiyo ni lugha ya ki-mithali tu, kuonyesha kwamba ulimi unaweza kuleta matokeo au madhara makubwa ya nje, kuliko hata kinavyoweza kudhaniwa.

  1. Ulimi ukitumika vyema unaweza kuleta suluhu ya matatizo makubwa yaliyoshindikana…

    2.  Vilevile ukitumika isivyopasa unaweza kuleta, matatizo makubwa kupita kiasi.

Tutazame kwenye biblia mfano wa pale ulimi ulipotumika vibaya:

Mtoto wa Sulemani, alilisababishia taifa la Israeli kugawanyika mara mbili, kwasababu  tu ya ulimi wake, usiokuwa na busara, kwa wana wa Israeli. Na hilo alilisema kutokana na malalamika ya baadhi ya wayahudi ambao waliomba wapunguziwe utumwa ambao baba yake Sulemani aliwatwisha.. Lakini yeye badala ya kusikiliza mashauri ya wazee, akasikiliza mashauri ya vijana wanzake, Na kibaya Zaidi badala awapooze kwa maneno mazuri akawaambia, utumwa wangu utakuwa ni Zaidi hata ya ule utumwa wa baba yangu.

Hivyo maneno hayo yakawakasirisha sana wayahudi wengi, mpaka, wakakataa kutawaliwa na uzao Daudi wakajitenga, ndio hapo pakawa mwanzo wa mataifa mawili kuundwa ndani ya nchi moja (yaani Israeli na Yuda), kwa miaka mingi sana.

1Wafalme 12:13 “Mfalme akawajibu watu wale kwa ukali, akaliacha shauri lile wazee walilompa;

14 akawajibu kama vile walivyomshauri vijana, akasema, Baba yangu alilifanya zito kongwa lenu, bali mimi nitaongeza kongwa lenu; baba yangu aliwapiga kwa mijeledi, bali mimi nitawapigeni kwa nge.

15 Basi mfalme hakuwasikia wale watu; maana jambo hili lilitoka kwa Bwana, ili alitimize neno lake, Bwana alilomwambia Yeroboamu mwana wa Nebati kwa kinywa cha Ahiya Mshiloni.

16 Basi Israeli wote walipoona ya kuwa mfalme hakuwasikia, hao watu walimjibu mfalme, wakasema, Tuna sehemu gani katika Daudi? Wala hatuna urithi katika mwana wa Yese. Haya! Nendeni zenu hemani kwenu, enyi Israeli; sasa itunze nyumba yako mwenyewe, Ee Daudi. Hivyo Israeli wakaenda zao hemani kwao”.

Huo ni mfano wa mahali ambapo ulimi ulitimika vibaya;

Mahali pengine ambapo ulimi ulitumika vizuri, na ukabatilisha mashauri mabaya;

Ni pale Daudi alipoonyesha fadhila zake nyingi kwa mtu mmoja aliyeitwa Nabali, lakini pale naye alipotaka chakula, Nabali alimjibu kwa maneno ya kukasirisha na kashfa, hivyo Daudi akaapa kuwa atakwenda kuwaangamiza watu wote wa nyumbani mwake, japokuwa aliwasaidia hapo kabla. Lakini alipokuwa njiani, mke wa Nabali alipata taarifa hizo kuwa Daudi na jeshi lake wanakuja kuwaangamiza, hivyo akamwendea Daudi, kwa kujinyenyekeza na kumpa maneno malaini ya kutuliza hasira. Ndipo Daudi akaghahiri uuaje wake aliokusudia, kwa ukoo mzima wa Nabali.

1Samweli 25:21 “Basi Daudi alikuwa amesema, Hakika ni bure nilivyokuwa nikilinda nyikani yote aliyo nayo mtu huyu, asipotewe na kitu cho chote cha mali yake yote; naye amenilipa mabaya badala ya mema.

22 Mungu naye awafanyie hivyo adui za Daudi, na kuzidi, nikimwachia katika wote walio wake hata mtoto mume mmoja, kutakapopambazuka asubuhi.

23 Ndipo hapo Abigaili alipomwona Daudi, alifanya haraka kushuka juu ya punda wake, akamwangukia Daudi kifulifuli, akainama mpaka nchi.

24 Akamwangukia miguuni pake, akasema, Juu yangu, bwana wangu, juu yangu mimi na uwe uovu; tafadhali mjakazi wako na anene masikioni mwako, nawe uyasikilize maneno ya mjakazi wako.

25 Nakusihi, bwana wangu, wewe usimwangalie huyu mtu asiyefaa, yaani, Nabali; kwa maana kama lilivyo jina lake ndivyo alivyo yeye; jina lake ndilo Nabali, na upumbavu anao; lakini mimi, mjakazi wako, sikuwaona hao vijana wa bwana wangu aliowatuma.

26 Basi sasa, bwana wangu, aishivyo Bwana, na iishivyo nafsi yako, kwa kuwa Bwana amekuzuia usimwage damu, tena usijilipize kisasi mkono wako mwenyewe, basi sasa adui zako, na hao wamtakiao bwana wangu mabaya, wawe kama Nabali.

27 Na sasa zawadi hii, mjakazi wako aliyomletea bwana wangu, na wapewe vijana wamfuatao bwana wangu.

28 Nakuomba ulisamehe kosa lake mjakazi wako, kwa kuwa hakika Bwana atamfanyia bwana wangu nyumba iliyo imara, kwa sababu bwana wangu anavipiga vita vya Bwana; tena uovu hautaonekana ndani yako siku zako zote.

29 Na hata ijapokuwa binadamu angeinuka akuwinde, na kuitafuta nafsi yako, hiyo nafsi ya bwana wangu itafungwa katika furushi ya uhai pamoja na Bwana, Mungu wako; na nafsi za adui zako ndizo atakazozitupa nje, kama kutoka kati ya teo.

30 Tena itakuwa, hapo Bwana atakapokuwa amemtendea bwana wangu sawasawa na mema yote aliyoyanena juu yako, na kukutawaza juu ya Israeli;

31 hili halitakuwa kwazo, wala chukizo la moyoni kwa bwana wangu, ama ya kuwa umemwaga damu bure, ama ya kuwa bwana wangu amejilipiza kisasi mwenyewe; tena hapo Bwana atakapokuwa amemtendea bwana wangu mema, ndipo umkumbuke mjakazi wako.

32 Naye Daudi akamwambia Abigaili, Na ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, ambaye amekuleta hivi leo kunilaki;

33 na ibarikiwe busara yako, na ubarikiwe wewe, uliyenizuia hivi leo nisimwage damu, wala kujilipiza kisasi kwa mkono wangu mwenyewe.

34 Kwa kuwa ni kweli, aishivyo Bwana, Mungu wa Israeli, aliyenizuia nisikudhuru, kwamba hungefanya haraka kuja kunilaki, hakika huyu Nabali asingaliachiwa hata mtoto mume mmoja, kutakapopambazuka asubuhi.

35 Basi Daudi akapokea mkononi mwake vitu vile alivyomletea; akamwambia, Haya! Kwea kwa amani kwenda nyumbani kwako; tazama, nimeisikiliza sauti yako, nami nimeukubali uso wako”.

Ndio maana Biblia inamalizia kwa kusema..

Yakobo 3:5 “Vivyo hivyo ulimi nao ni kiungo kidogo, nao hujivuna majivuno makuu. Angalieni jinsi moto mdogo uwashavyo msitu mkubwa sana.

6 Nao ulimi ni moto; ule ulimwengu wa uovu, ule ulimi, umewekwa katika viungo vyetu, nao ndio uutiao mwili wote unajisi, huuwasha moto mfulizo wa maumbile, nao huwashwa moto na jehanum.

7 Maana kila aina ya wanyama, na ya ndege, na ya vitambaavyo, na ya vitu vilivyomo baharini, vinafugika, navyo vimekwisha kufugwa na wanadamu.

8 Bali ulimi hakuna awezaye kuufuga; ni uovu usiotulia, umejaa sumu iletayo mauti.

9 Kwa huo twamhimidi Mungu Baba yetu, na kwa huo twawalaani wanadamu waliofanywa kwa mfano wa Mungu”.

Hivyo tujifunze kutumia ndimi zetu vizuri. Kwasababu kwa hizi tutajibariki wenyewe na kwa hizi tutajiangamiza wenyewe.

Kumbuka; ulimi laini huvunja mfupa.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya kilichotarajiwa kikikawia kuja moyo huugua (Mithali 13:12)?.

DORKASI AITWAYE PAA.

CHANGIA SASA.

UTAONA MAMBO MAKUBWA KULIKO HAYA.

MKAMCHUKUE SALAMA.

Rudi nyumbani

Print this post