Title November 2020

Sodoma ipo nchi gani?

Sodoma ipo nchi gani?


Sodoma na Gomora ni miji iliyokuwa katika nchi ya Kaanani (Ambayo ndio Israeli ya Sasa). Miji hii miwili ni moja kati ya miji mitano iliyokuwa katika bonde la Yordani..mingineyo  ikiwemo, ni Adma, Seboimu, na Lasha.

Kama tunavyoijua habari, miji hii miwili (yaani Sodoma na Gomora) ndiyo iliyokuwa kiini cha maovu yote katika bonde hilo.

Mwanzo 19:24 “Ndipo Bwana akanyesha juu ya Sodoma na juu ya Gomora kiberiti na moto toka mbinguni kwa Bwana.

25 Akaangusha miji hiyo na Bonde lote, na wote waliokaa katika miji hiyo, na yote yaliyomea katika nchi ile”.

Hata hiyo mingine nayo haikupona, nayo pia iliangamizwa;

Kumbukumbu 29:23 “ya kuwa nchi yake nzima ni kibiriti, na chumvi, na kuteketea, haipandwi, wala haizai, wala nyasi hazimei humo, kama mapinduko ya Sodoma na Gomora, Adma na Seboimu, aliyoipindua Bwana kwa ghadhabu yake na hasira zake”;

Lakini ni tahadhari gani tunapaswa tuchukue tunaposoma habari ya miji hii miovu?

Licha ya kuwa ilikuwa ni miovu lakini biblia inatuambia ilikuwa ni miji yenye kuvutia sana, mfano wa Edeni, Bustani ya Bwana soma (Mwanzo 13:10). Mfano tu wa dunia ya sasa. Ulimwengu wa sasa umejengeka na unavutia kuliko ule wa zamani,hilo lipo wazi, starehe za wakati ule haziweki kulinganishwa hata kidogo na starehe za wakati huu, lakini maovu yake ni  zaidi ya yale ya Sodoma na Gomora.

Ushoga sio jambo la kushangaza tena, kiasi kwamba nchi zimefanikiwa kuhalalisha jambo hilo, na sehemu nyingine mpaka kwa yanayoyaita makanisa (ambayo kiuhalisia si makanisa), yamevuka mpaka huo na kuhalalisha ushoga bila hata kuogopa kumuhusianisha Mungu na matendo kama hayo maovu. Hiyo ni kuonyesha kuwa mwisho wa huu ulimwengu upo karibuni sana. Wapo watu wanajidanganya kuwa hii dunia haitaangamizwa, kwasababu Mungu alishasema hivyo wakati ule wa Gharika kuwa hatagharikisha.. Lakini hawajui kuwa ni kweli Mungu hatauangamiza huu ulimwengu kwa maji, lakini amesema ataugharikisha moto. Ambapo kila mtu mwovu, na kila kitu kitafumuliwa, biblia inasema hivyo soma.

2Petro 3:7 “Lakini mbingu za sasa na nchi zimewekwa akiba kwa moto, kwa neno lilo hilo, zikilindwa hata siku ya hukumu, na ya kuangamia kwao wanadamu wasiomcha Mungu……..

10 Lakini siku ya Bwana itakuja kama mwivi; katika siku hiyo mbingu zitatoweka kwa mshindo mkuu, na viumbe vya asili vitaunguzwa, na kufumuliwa, na nchi na kazi zilizomo ndani yake zitateketea.

11 Basi, kwa kuwa vitu hivi vyote vitafumuliwa hivyo, imewapasa ninyi kuwa watu wa tabia gani katika mwenendo mtakatifu na utauwa,

12 mkitazamia hata ije siku ile ya Mungu, na kuihimiza; ambayo katika hiyo mbingu zitafumuliwa zikiungua, na viumbe vya asili vitateketea na kuyeyuka”?

Unaona?  Swali la kujiuliza ni je! Sisi tumejiwekaje? Katika kipindi hichi cha mwisho? Je na sisi tutapumbazwa na Ulimwengu huu kama Lutu na mke wake? Tukaacha kubaki mahali Mungu alipotuweka tukaenda kushikamana na mambo ya ulimwengu huu yanayodanganya?. Huu ni wakati wa kujiokoa nafsi yako, na si wakati wa kumwangalia ndugu, au rafiki, au mjomba anasemaje, kwasababu mwisho upo karibu.

Je umeokoka?

Kama bado na upo tayari kufanya hivyo leo, huo ni uamuzi wa busara sana kwako, kama upo tayari kumpa Yesu maisha yako leo, basi fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba, na maelekezo mengine >>>>  SALA YA TOBA

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

JINSI SODOMA NA GOMORA ILIVYOKUWA INAVUTIA SANA..

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

Israeli ipo bara gani?

CHUKIZO LA UHARIBIFU

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

Rudi Nyumbani:

Print this post

HEKIMA YA KIMUNGU, INAINGIAJE MIOYONI MWETU?

Shalom!. Karibu tuyatafakari pamoja maandiko.

Elimu yoyote ile ya kidunia ni hekima..hekima sio tu kujua Nahau, na misemo na methali. Mtu anayekwenda kusoma elimu fulani labda ya uchumi au udaktari, anaingiza hekima ndani yake ya namna ya kumtibu mtu au namna ya kufanya biashara. Kadhalika na Elimu nyingine zote mtu anazokwenda kuzisomea, anakuwa anajiongezea hekima katika nyanja hiyo anayokwenda kuisomea.

Sasa fomula ya kujiongezea maarifa katika mambo ya kidunia, haina tofauti sana na ile ya kujiongezea hekima katika mambo ya kiMungu. Tunapomwomba Mungu atupe hekima na maarifa katika kumjua yeye, haitakuja tu kwa kumwomba na kisha kukaa kusubiri, hapana!..Bali inakuja kwa kumwomba kwanza, na kisha kwenda kuitafuta.. Unapokwenda kuitafuta kwasababu ulishamwomba Mungu, anachokifanya yeye ni kuifanikisha njia yako katika kwenda kuitafuta…anakupa uwezo wa kuelewa kiwepesi zaidi kuliko kama ungekuwa hujamwomba.

Ni fomula ile ile tu ya mwanafunzi anayemwomba Mungu amfanikishe katika masomo yake, hawezi kuomba Mungu ampe uwezo wa kuelewa na kufanya vizuri katika mitihani na huku ameacha kusoma kabisa, hapo hatapata chochote, lakini kama amemwomba Mungu kwa Imani, na kwenda kusoma ndipo akili yake inaongezewa uwezo mara dufu zaidi ya kuelewa tofauti na yule mwanafunzi ambaye hajamwomba Mungu kabisa.

Na pia katika kuitafuta Hekima ya kiMungu ni hivyo hivyo, Tunapomwomba Mungu atupe hekima ya kiMungu sawasawa na Yakobo 1:5, hatupaswi kusubiri tu!..Ni wakati wa kuiweka imani katika matendo baada ya hapo..kwa kwenda kuanza kulisoma Neno lake kwa bidii na kumtafuta yeye kwa bidii zote, na kwa nguvu zote.

Mathayo 22:37  “Akamwambia, Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote. Hii ndiyo amri iliyo kuu, tena ni ya kwanza”

Ukianza kuweka bidii katika kumjua Mungu, kwa moyo wako wote kiasi kwamba moyo wako wote upo kwake, na unatumia akili zako zote ulizopewa na Mungu katika kumtafuta yeye, na kuifanya kazi yake, na pia unatumia nguvu zako zote Mungu alizokujali za kimwili na kiroho..Hekima ya kiMungu itazidi kuingia ndani yako, na utakuwa unazidi kumjua Mungu na kuwa na uwezo mkubwa wa kuchambua mambo kwa kadri siku zinavyozidi kwenda.. Bwana ataisafisha njia yako na utakuwa na hekima nyingi.

Utauliza vipi na Sulemani, na yeye aliipata hekima kwa njia hiyo hiyo?

Jibu ni ndio!..Sulemani baada ya kumwomba Mungu hekima, hakukaa tu na ghafla akaanza kujikuta anaelewa mambo…La! hakufanya hivyo, kinyume chake baada ya kumwomba Mungu hekima, alianza kutafuta huko na huko kwa kusoma mambo mengi ya kiMungu na kimaisha, ndipo hekima ikaingia ndani yake, Mungu akamsaidia kupata alichokiomba…Maandiko yanasema hivyo katika mstari ufuatao..

Mhubiri 12: 9 “Walakini, kwa sababu huyo Mhubiri alikuwa na hekima, aliendelea kuwafundisha watu maarifa, naam, akatafakari, akatafuta-tafuta, akatunga mithali nyingi.

10 Huyo Mhubiri akatafuta-tafuta ili apate kuona maneno yapendezayo, na yale yaliyoandikwa kwa unyofu, yaani, maneno ya kweli”.

Huyo ni Sulemani, ambaye baada ya kuomba hekima, akajikita katika kwenda kuitafuta huko na huko, akajikita katika kutafakari sana..na alipopata uelewa wa mambo ndipo akazitunga mithali..Na alikuwa akitafuta kuelewa mambo KWA KUSOMA VİTABU VİNGİ, na kufanya utafiti mwingi, na alikuwa mpaka anachoka mwili kwaajili ya kusoma tu. Mpaka akasema “Kusoma sana kwa uchosha mwili”..

Mhubiri 12: 12 “….. hakuna mwisho wo wote wa kutunga vitabu vingi; NA KUSOMA SANA HUUCHOSHA MWİLİ”

Je! Wewe ulishawahi kuzitafuta habari za Mungu kwa bidii namna hiyo mpaka Mwili ukachoka?..na uchovu anaouzungumzia hapo na Sulemani sio uchovu wa usingizi (maana kuna mtu atasoma Neno dakika 10 na kusikia usingizi, na mwisho akasema amechoka..Hapo! hujachoka! Bali umekuwa mvivu). Uchovu unaozungumziwa hapo na Sulemani ni kama ule mwanafunzi anaochoka wakati karibia na anapohitimu, baada ya kusoma miaka mingi. Pale ambapo kichwa chake kimejaa maarifa ya kutosha ya kuweza kukabiliana na mtihani wowote unaokuja mbele yake, lakini mwili wake umekuwa dhaifu kwa kuihangaikia hiyo elimu, alipokuwa akijitesa na kujizuia kwa mambo mengi ilimradi tu aipate hiyo elimu.

Bwana atusaidie nasi tuwe kama Sulemani, na tumpende Bwana Mungu wetu kwa mioyo yetu yote, kwa akili zetu zote, na kwa nguvu zetu zote, ili tuweze kuipata hekima ya kiMungu ndani yetu…

Mithali 2:10 “Maana hekima itaingia moyoni mwako, Na maarifa yatakupendeza nafsi yako”.

Kama hujaokoka, Kristo yupo mlangoni, hizi ni siku za mwisho, na wokovu ndio mwanzo wa hekima..Hivyo mpokee Kristo leo kwa kumwamini na kutubu dhambi zako zote, na kubatizwa. Naye atakukubali, kama alivyosema katika Neno lake.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Moyo wake mwenye hekima upo upande wa kuume, maana yake nini?

WALIO NA HEKIMA NDIO WATAKAOELEWA.

MAASI KUONGEZEKA NI ISHARA YA NINI?.

Nini maana ya “katika wingi wa hekima mna wingi wa huzuni”.

MAMBO 5 AMBAYO KILA MKRISTO ANAPASWA KUFAHAMU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Nini maana ya “kila tendo lisilotoka katika imani ni dhambi?”

Jibu: Tusome mstari huo kuanzia juu kidogo.

Warumi 14:21  “Ni vyema kutokula nyama wala kunywa divai wala kutenda neno lo lote ambalo kwa hilo ndugu yako hukwazwa.

22  Ile imani uliyo nayo uwe nayo nafsini mwako mbele za Mungu. Heri mtu yule asiyejihukumu nafsi yake katika neno lile analolikubali.

23  Lakini aliye na shaka, kama akila, amehukumiwa kuwa ana hatia, kwa maana hakula kwa imani. NA KILA TENDO LISILOTOKA KATIKA IMANI NI DHAMBI”

Tukirudi juu Zaidi katika Mstari wa 14, Neno la Mungu linasema..

Warumi 14:14  “Najua, tena nimehakikishwa sana katika Bwana Yesu, ya kuwa hakuna kitu kilicho najisi kwa asili yake, lakini kwake yeye akionaye kitu kuwa najisi, kwake huyo kitu kile ni najisi”

Katika mistari hii, biblia ilikuwa inazungumzia juu ya vyakula..Na katika agano jipya, biblia imesema hakuna chakula chochote kilicho najisi.. Kwasababu kinachomwingia mtu mdomoni hakimtii unajisi, bali kile kimtokacho moyoni mwake ndicho kinachomtia mtu unajisi..Ni Bwana wetu Yesu ndiye aliyetupa ufunuo huo, ambao ni kweli kabisa..kasome Mathayo 15:16-20.

Kwahiyo katika agano jipya, nguruwe sio najisi, Kambale sio najisi, hata wanaokula nyoka hawapati unajisi wowote.

Lakini kwasababu ufunuo huo umekuwa mgumu kueleweka kwa wengi, kwamba vyakula vyote vimetakaswa.. Hivyo bado wanabaki kuamini kuwa vipo baadhi vilivyo najisi, kama nguruwe, Kambale, na vingine baadhi…. Sasa hawa ndio biblia inawataja kuwa “DHAIFU WA IMANI” (Warumi 14:1), haijalishi wao watajiona wana Imani kiasi gani, lakini biblia imewataja kuwa ni dhaifu wa Imani. Na miongoni mwao wapo Wakristo na wasio wa Kristo.

Sasa kwasababu biblia ni kitabu cha Hekima, imetufundisha jinsi ya kuenenda na hawa watu,

Kwanza: hatupaswi kuyahukumu mawazo yao (Maana yake kuwalazimisha waamini tunachoamini sisi, ikiwemo pia kushindana nao hatupaswi kushindana nao).

Pili: hatupaswi kuutumia ujuzi huo tulionao sisi kuwafanya wamkosee Mungu, au wamwache Kristo au kumchukia.

Maana yake ni kwamba labda umemhubiria Muislamu, akamwamini na kumpokea Kristo, lakini bado akawa anaamini kuwa nguruwe ni najisi. Na wewe kwasababu una UJUZI wa kujua kuwa hakuna kilicho najisi, hupaswi kwenda kula nguruwe mbele yake..au kumlazimisha ale nguruwe, ukifanya hivyo mwisho wa siku utamhuzunisha na kumfanya arudi nyuma au auchukie ukristo moja kwa moja..Na tukimkosesha mtu mmoja kwaajili ya chakula biblia inasema tunamtenda Kristo dhambi (Ndio hapo biblia inasema ni heri nisilie nyama kabisa kama itamkosesha ndugu yangu)..

1Wakoritho 8:11 “Na yule aliye dhaifu aangamizwa kwa ujuzi wako, naye ni ndugu ambaye Kristo alikufa kwa ajili yake.

12  Hivyo, mkiwatenda dhambi ndugu zenu na kuitia jeraha dhamiri iliyo dhaifu, mnamtenda dhambi Kristo.

13  Kwa hiyo, chakula kikimkwaza ndugu yangu, hakika sitakula nyama hata milele, nisije nikamkwaza ndugu yangu”

kwasababu hata asipokula hivyo vyakula tunavyokula sisi haviwafanyi wao wasiende mbinguni. Wasipokula nguruwe Maisha yao yote au Kambale, na wakawa wamempokea Kristo, watafika mbinguni tu.. Hivyo hatupaswi kutumia UJUZI wetu kuiharibu kazi ya Mungu ya wokovu.

Ndivyo biblia inavyosema katika..

Warumi 14: 1  “Yeye aliye DHAIFU WA IMANI, mkaribisheni, walakini msimhukumu mawazo yake.

2  Mtu mmoja anayo imani, anakula vyote; lakini yeye aliye dhaifu hula mboga.

3  Yeye alaye asimdharau huyo asiyekula, wala yeye asiyekula asimhukumu huyo alaye; kwa maana Mungu amemkubali.

4  Wewe u nani unayemhukumu mtumishi wa mwingine? Kwa bwana wake mwenyewe yeye husimama au huanguka. Naam, atasimamishwa, kwa kuwa Bwana aweza kumsimamisha”

Sasa kwa huyu mtu ambaye ni DHAIFU WA IMANI, ambaye moyoni mwake “anaamini kabisa kwamba kula nguruwe ni dhambi, au kula chakula Fulani ni dhambi”.. mtu huyu akaacha kufanya hicho kitu anachokiamini na kwenda kula nguruwe au chakula kingine chochote ambacho anajua sio sawa kulingana na anachokiamini moyoni mwake. Huyo mtu ni wazi kuwa baada ya kula, moyoni mwake ATASIKIA HALI YA KUHUKUMIWA. Sasa hiyo hali ya kuhukumiwa anayoisikia maana yake ni kwamba, amefanya kitu kinyume na anachokiamini, Hapo tayari kafanya tendo ambalo halijatokana na kile anachokiamini, na hivyo ANATENDA DHAMBI!!…Hiyo ndio maana ya “KILA TENDO LISILOTOKA KATIKA IMANI NI DHAMBI”,

Lakini kama macho yake yalifumbuka na kupata ufunuo kuwa “ni kweli hakuna kilicho najisi” na kwa ufunuo huo akaenda kula chakula ambacho hapo kwanza alikuwa anakiona ni najisi..Ni wazi kuwa mtu huyo baada ya kula hatasikia kuhukumiwa moyoni mwake, kwasababu amefanya kitu akiwa na uhakika kwamba hamtendi Mungu dhambi, na hivyo atakuwa kafanya jambo lile kwa Imani, na kwake hiyo haitahesabika kuwa ni dhambi.

Hivyo ndugu unayesoma ujumbe huu, ambaye ni mkristo, kama unaamini kuwa bado kuna vyakula najisi, na hivyo dhamiri yako inakushuhudia kwamba hupaswi kula, basi usivile lakini hakikisha unaushikilia utakatifu wote na kukaa katika maagizo ya Mungu.

Na kama wewe haupo katika Imani ya kikristo (maana yake ni Muislamu au mtu wa Imani nyingine), fahamu kuwa Yesu anakupenda na alikufa kwaajili yako..Njoo kwa Yesu na heshima yako hiyo hiyo uliyonayo, yeye atakuongezea nyingine juu ya hiyo itakayodumu milele, …njoo kwa Yesu na ustaarabu wako huo huo, hatakupokonya, badala yake atakuongezea na mwingine mwingi udumuo milele…njoo kwa Yesu na maadili yako hayo hayo, na kujisitiri kwako huko huko, atakuongezea na mwingine mwingi…Njoo kwa Yesu ukiwa huli nguruwe hivyo hivyo, wala hatakuambia uanze kuzila nguruwe..anachokihitaji ni roho yako na si tumbo lako, akuokoe akupe uzima wa milele bure!..Kwasababu yeye ndiye aliyetumwa kuukomboa ulimwengu, wala hakuna mwingine.

Hivyo kama umeamua leo kumpokea hatua inayofuata ni rahisi sana, hapo ulipo piga magoti, kisha fuatilisha sala hii  kwa kufungua hapa >>> SALA YA TOBA

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

SIKUKUU 7 ZA KIYAHUDI ZINAFUNUA NINI KWETU?

KUOTA UNAKULA CHAKULA.

CHAKULA CHA ROHONI.

Katika Mathayo 15:21-28, Yesu alikuwa na maana gani alipomwambia huyu Mama kwamba chakula cha watoto hawapewi mbwa?

Mstari huu una maana gani? “Tupa chakula chako usoni pa maji; Maana utakiona baada ya siku nyingi”. (Mhubiri 11:1)

Rudi Nyumbani:

Print this post

USIOMBE MAOMBI YASIYOKUWA NA MAJIBU NA WALA USIMTUKANE MUNGU.

Luka 23:42  “Kisha akasema, Ee Yesu, nikumbuke utakapoingia katika ufalme wako.Yesu akamwambia, Amin, nakuambia, leo hivi utakuwa pamoja nami peponi”.

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe. Karibu tujifunze biblia.

Kama tunavyojua wengi wetu, kwamba Kristo hakusulubiwa peke yake pale Kalvari, bali alisulubiwa pamoja na wanyang’anyi wengine wawili. Na wote walikuwa wametundikwa msalabani kama Bwana, kufunua kuwa na wao pia wapo katika mateso na uchungu. Lakini kilichowashangaza  zaidi ni kuona anayejiita ni mkombozi naye pia yupo katika mateso kama wao. Katika hali ya kawaida ni jambo linalochanganya kidogo. Hivyo kila mmoja akawa na neno la kumwambia Bwana Yesu.

Wa kwanza akatangulia kumwambia Bwana,……

“Na mmoja wa wale wahalifu waliotungikwa alimtukana, akisema, Je! Wewe si Kristo? Jiokoe nafsi yako na sisi. Lakini YESU HAKUMJIBU NENO. (Luka 23.39 )”

Kitendo tu cha kuanza kwa  kumwambia Bwana…wewe si Kristo?..hicho tayari ni kitendo cha kukosa heshima!..na hakujua kama tayari kamtukana Mungu, kwa kusema tu hivyo..

Mfano kamili wa watu wengi wa siku hizi za Mwisho, Wapo katika dimbwi kubwa la matatizo, na shida lakini watasimama mbele za Mungu, na kusema “kama wewe Mungu upo na una nguvu, mbona huniokoi na shida hizi” na pia “mbona baadhi ya watu wako wana shida nyingi, waokoe watu wako kwanza na shida zao na ndio utusaidie sisi”.

Hawajui kwamba tayari wanamtukana Mungu kwa hayo maneno. Sasa watu wa namna hii, kamwe wasitazamie kupokea majibu yoyote kutoka kwa Mungu, kwasababu wamekosa unyenyekevu…

Ndio maana unaona huyo mnyang’anyi alitazamia atajibiwa na Bwana kwa kejeli zake, lakini Kristo hakutoa neno lolote hata la kumwambia atubu!

Lakini tukiendelea na Mtu wa pili, ambaye naye pia alikuwa anaswali kama hilo hilo kichwani?, isipokuwa huyu alituliza akili yake na kufikiri mara mbili, na kujua kuwa yaliyompata amestahili kupokea malipo yake, na kwamba Kristo yaliyompata hakustahili, maana yake ni kwamba amejitoa kusulubiwa kwaajili ya makosa ya watu wengine, na si kwa makosa yake….kwa kutafakari sana..roho ya unyenyekevu ikamwingia, na ya kuomba msaada..

Luka 23:40  “Lakini yule wa pili akamjibu akamkemea, akisema, Wewe humwogopi hata Mungu, nawe u katika hukumu iyo hiyo?

41  Nayo ni haki kwetu sisi, kwa kuwa tunapokea malipo tuliyostahili kwa matendo yetu; bali huyu hakutenda lo lote lisilofaa.

42  Kisha akasema, EE YESU, NİKUMBUKE UTAKAPOİNGİA KATİKA UFALME WAKO.

43  Yesu akamwambia, Amin, nakuambia, leo hivi utakuwa pamoja nami peponi”

Hebu mtafakari huyu mtu wa pili, Hata hakuomba kushushwa msalabani aendelee na maisha yake, hakumwomba Yesu amshushe arudi akaione familia yake, hakuomba Yesu amwokoe pale msalabani arudi kwenye biashara yake, hakuomba Yesu amwokoe pale msalabani ili asiendelee kuteseka na maumuvi ya misumari…lakini alimwomba Yesu UZIMA BAADA YA KIFO. Alikikubali kifo, lakini aliomba tu uzima baada ya hicho kifo. Alisema nitastahimili shida ninayoipata sasa, nikipata msamaha wa kushushwa hapa msalabani sawa, nisipopata pia ni sawa, nitavumilia mateso, lakini tu, niupate huo UZIMA WA MILELE, baada ya kufa kwangu. Huyo pekee yake ndiye Kristo aliyemjibu!.

Lakini yule wa Kwanza hakujibiwa Neno hata moja. Na matokeo yake alikufa katika mateso yake na akakosa vyote, akakosa maisha ya dunia aliyokuwa bado anayatamani, na vile vile akakosa uzima baada ya kifo.

Ndugu yangu, huu sio wakati wa kumfuata Kristo ili upate MALI, na huku huna uzima wa milele moyoni mwako..Kristo hatakujibu chochote!..Unapitia shida sasa za kidunia, sio wakati wa kulia uondolewe kwenye hizo shida huku shida ya roho yako bado ipo, huku hutaki kusikia hata habari za Neno lake, Ukisikia habari za Yesu kwako ni habari za kupoteza muda tu, comedy zinazolikebehi Neno lake ndizo zinazokuchekesha… hapo usitazamie kujibiwa chochote.

Tafuta uhakika  kwanza wa uzima wa maisha baada ya haya kuisha, Ndio kitu cha muhimu kwa sasa. Ukikimbilia kuomba msaada wa mambo ya kidunia, kuna uwezekano mkubwa usikipate hicho unachokitafuta na ukafa katika shida zako, na ukakosa vyote (ukakosa Uzima wa Milele pamoja na Mali unazozitafuta).

Mathayo 6: 33  “Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa”.

Leo umesikia ujumbe huu, pengine ulikuwa unamtukana na kumdhihaki Mungu pasipo kujua..Upo kwenye shida kweli lakini umekuwa mtu wa kulalamika mpaka kufikia kumdhihaki Mungu… ndio maana leo umekutana na ujumbe kama huu ni kwasababu Kristo bado anakupenda, ndio maana bado hujafa..Upo hapo msalabani umening’inia na shida zako, zinakutesa kweli, unatamani kutoka hapo…Usikimbilie kutafuta msaada wa kutoka hapo kwanza, kwasababu kwa dhambi zako umestahili kuwepo hapo ulipo…Unachopaswa kufanya sasa, ni kuanguka chini, kwa unyenyekevu na kutubu na kumwomba Bwana Yesu msamaha kwa dhambi zako, na kumwambia kuanzia leo nakufuata naomba unipe uzima wa milele…Hata kama usiponitoa katika haya mateso ninayopitia sasa, naomba unipe UZİMA WA MİLELE,  hata kama nikifa leo pasipo kupata chochote katika haya maisha naomba Uzima wa milele baada ya kifo..hicho ndio cha kwanza tunachokihitaji sisi.

Ukiomba maombi ya namna hiyo Roho Mtakatifu atashuka ndani yako kukupa jibu la maombi yako, amani ya ajabu itashuka ndani yako, na utaona akili yako imebadilika na kuwa kama ya Bwana Yesu, kiasi kwamba hizo shida zitakuwa sio kitu kwako, kwajinsi hiyo furaha itakavyokuwa kubwa ndani yako.

Lakini kwanza mpokee Kristo katika maisha yako, na tubu…Na pia kama umetubu hakikisha unatafuta ubatizo sahihi, ambao ni wa maji tele (Yohana 3:23) na kwa jina la Yesu Kristo (Matendo 2:38) kukamilisha wokovu wako.

Na pia kama utapenda kushare ujumbe huu na wengine, tunaomba usiondoe chochote, ikiwemo anwani ya www wingulamashahidi org pamoja na namba zetu hizi 0789001312.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

FAIDA ZA MAOMBI.

NAWAAMBIA MAPEMA!

UFUNUO: Mlango wa 1

UNAZO KILA SABABU ZA KUMSHUKURU MUNGU

KUNA UMUHIMU WA KUWA MTU WA KURIDHIKA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Biblia ina vitabu vingapi?

Je! Biblia ina vitabu vingapi?


Biblia takatifu ina jumla ya vitabu 66, kati ya hivyo 39 ni vya agano la kale, na 27 ni vya agano jipya.

Hii ni orodha ya vitabu vya agano la kale:

  1. Mwanzo
  2. Kutoka
  3. Mambo ya walawi
  4. Hesabu
  5. Kumbukumbu la Torati
  6. Yoshua
  7. Waamuzi
  8. Ruthu
  9. 1 Samweli
  10. 2 Samweli
  11. 1 Wafalme
  12. 2 Wafalme
  13. 1 Mambo ya Nyakati
  14. 2 Mambo ya Nyakati
  15. Ezra
  16. Nehemia
  17. Esta
  18. Ayubu
  19. Zaburi
  20. Mithali
  21. Mhubiri
  22. Wimbo ulio bora
  23. Isaya
  24. Yeremia
  25. Maombolezo
  26. Ezekieli
  27. Danieli
  28. Hosea
  29. Yoeli
  30. Amosi
  31. Obadia
  32. Yona
  33. Mika
  34. Nahumu
  35. Habakuki
  36. Sefania
  37. Hagai
  38. Zekaria
  39. Malaki

Ifuatayo ni orodha ya vitabu vya agano jipya:

  1. Mathayo
  2. Marko
  3. Luka
  4. Yohana
  5. Matendo
  6. Warumi
  7. 1 Wakorintho
  8. 2 Wakorintho
  9. Wagalatia
  10. Waefeso
  11. Wafilipi
  12. Wakolosai
  13. 1 Wathesalonike
  14. 2 Wathesalonike
  15. 1 Timotheo
  16. 2 Timotheo
  17. Tito
  18. Filemoni
  19. Waebrania
  20. Yakobo
  21. 1 Petro
  22. 2 Petro
  23. 1 Yohana
  24. 2 Yohana
  25. 3 Yohana
  26. Yuda
  27. Ufunuo

Zipo zinazosemekanakuwa ni biblia, ambazo zina vitabu 72 na nyingine zaidi. Na zinatumiwa na baadhi ya madhehebu ya kikristo kama vile Katoliki na Othrodoksi.  Vitabu hivyo vilivyoongezwa havijathibitishwa kuwa vimevuviwa na Roho Mtakatifu hivyo hatupaswi kuviamini.

Biblia tunayopaswa kuiamini ni ile yenye vitabu hivyo 66 vilivyoorodheshwa hapo juu.

Shalom.

Je! utapenda uwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp? kama ndivyo basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Biblia ni nini?

Watoto wa Ibrahimu/Wana wa Ibrahimu walikuwa ni wangapi?

JIFUNZE KULIGAWANYA VYEMA NENO LA MUNGU.

JINSI YA KUSOMA BIBLIA.

WINGU KUBWA LA MASHAHIDI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Wakaldayo ni watu gani?

Wakaldayo ni wenyeji wakongwe wa Mji wa Babeli. Mji wa Babeli ulikuwepo maeneo ya nchi ya Iraq kwasasa.

Hawa wakaldayo ndio waliowachukua mateka wana wa Israeli na kuwapeleka utumwani Babeli..

Yeremia 21:8 “Nawe waambie watu hawa, Bwana asema hivi, Tazama naweka mbele yenu njia ya uzima, na njia ya mauti.

9 Yeye atakayekaa katika mji huu atakufa kwa upanga, na kwa njaa, na kwa tauni; bali yeye atakayetoka, na kujitia pamoja na Wakaldayo wanaowahusuru, yeye ataishi, na maisha yake yatakuwa nyara kwake.

10 Maana nimeweka uso wangu juu ya mji huu niuletee mabaya, wala nisiuletee mema, asema Bwana; utatiwa katika mkono wa mfalme wa Babeli, naye atauteketeza”.

Ezra 5:12 “Lakini hapo baba zetu walipomkasirisha Mungu wa mbingu na nchi, hata akaghadhibika, akawatia katika mkono wa Nebukadreza, mfalme wa Babeli, Mkaldayo, naye ndiye aliyeiharibu nyumba hii, akawachukua watu mateka mpaka Babeli”

Pia Ibrahimu kabla ya kuhamia nchi ya Kaanani, alikuwa anaishi huko Uru ya Wakaldayo. Kwasababu Babeli tayari ilikuwepo miaka mingi kabla hata ya Taifa la Israeli kuwepo, ndipo ule Mnara wa Babeli ulipotengenezewa.

Mwanzo 11:31 “Tera akamtwaa Abramu mwanawe, na Lutu mwana wa Harani, mwana wa mwanawe, na Sarai mkwewe, mke wa Abramu mwanawe, wakatoka wote katika Uru wa Wakaldayo, waende nchi ya Kanaani, wakafika mpaka Harani wakakaa huko”.

Hivyo popote biblia inapowataya Wakaldayo ina maanisha Wenyeji wa Babeli.

Je una habari kuwa Babeli iliyowachukua wana wa Israeli mateko kwa namna ya kimwili, ipo leo kwa namna ya kiroho?..Kama ulikuwa hujui basi kasome kitabu cha ufunuo mlango wa 17 na kuendelea.

Na Babeli hiyo ya rohoni inawachukua utumwa watu wengi leo pasipo wao kujua, na mwisho wa siku inawaua kiroho na kuwapeleka kuzimu. Na Babeli hii sasa inafanya kazi kwa nguvu katika dini na madhehebu, na Bwana ataihukumu katika siku za mwisho.

Ufunuo 14:8 “Kisha mwingine, malaika wa pili, akafuata, akisema, Umeanguka, umeanguka Babeli, mji ule ulio mkubwa, maana ndio uliowanywesha mataifa yote mvinyo ya ghadhabu ya uasherati wake”.

Kwa urefu kuhusu Babeli hii ya rohoni fungua hapa >> BABELI YA ROHONI

Je umeokoka?.  Kumbuka Kristo anarudi saa na wakati usiodhani?..Wakati unafikiri bado sana ndio wakati anaokuja..

Waebrania 10:37 “Kwa kuwa bado kitambo kidogo sana, Yeye ajaye atakuja, wala hatakawia”.

Kama hujampokea ni vizuri ikampokea sasa hivi, wala usisubiri hata dakika 5 mbele, kwasababu hujua yatakayojitokeza dakika mbili mbele. Hivyo hapo ulipo piga magoti, kisha tubu dhambi zako zote kwa kumaanisha kuziacha, na Bwana wa huruma na Neema atakusamehe bure, na kukutakasa. Na baada ya hapo tafuta ubatizo sahihi, wa maji mengi na kwa jina la Yesu, na  tafuta kanisa la Kristo la kiroho, lililo karibu nawe,  jiunge hapo na wakristo wenzako ili ujengeke kiroho, na Roho Mtakatifu atakuongoza kufanya yaliyosalia.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

MNARA WA BABELI

Mto Frati upo nchi gani, Umuhimu wake katika biblia ni upi?

Kongwa ni nini kwenye biblia?(Wagalatia 5:1)

NENO LA MUNGU NI DAWA ILIYO TOFAUTI NA DAWA NYINGINE.

JUKUMU LA MUHIMU LINALOKWEPWA NA WENGI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Wibari ni nani?(Mithali 30:26)

SWALI: Wibari ni nani? Na kwanini wanatajwa kama moja wa viumbe wanne wenye akili nyingi?(Mithali 30:26)


JIBU: Wibari ni wanyama wadogo wanaokaribia kufanana na sungura, kwa jina lingine wanajulikana kama pimbi, au kwanga, au perere, tazama kwenye picha.

Wanyama hawa utawaona wakitajwa kwenye vifungu hivi katika biblia;

Walawi 11:4 “Pamoja na hayo, wanyama hawa hamtawala katika wale wenye kucheua, na katika wale walio na kwato; ngamia, kwa sababu yuacheua lakini hana kwato, yeye ni najisi kwenu. 5 Na wibari, kwa sababu yeye hucheua lakini hana kwato, yeye ni najisi kwenu”.

Zaburi 104:18 “Milima mirefu ndiko waliko mbuzi wa mwitu, Na magenge ni kimbilio la wibari”.

Mithali 30:24 “Kuna viumbe vinne duniani vilivyo vidogo; Lakini vina akili nyingi sana.

25 Chungu ni watu wasio na nguvu; Lakini hujiwekea chakula wakati wa hari.

26 Wibari ni watu dhaifu; Lakini hujifanyia nyumba katika miamba”.

Lakini ni kwanini wametajwa kama moja ya viumbe vinne vyenye akili nyingi duniani?

Ni kwasababu ya tabia yao, wanyama hawa ni waoga, hawali nyama, wala hawapo machachari sana ukilinganisha na wanyama wengine, hawawezi kukimbia sana, kwa ufupi ni viumbe dhaifu ambavyo ni rahisi kukamatwa na maadui zao, lakini katika udhaifu wao, wanajua ni wapi pa kujihifadhi nafsi zao, na si hapo pengine zaidi ya kwenye miamba.

Wibari wanatengeneza nyumba zao kwenye mapango ya miamba, mirefu, na migumu, kiasi kwamba adui zao ni ngumu kuwaona au kuwakamata, tofauti na wanyama wengine kama ngiri au sungura n.k ambao wao wanachimba mashimo ambayo hata adui zao wanaweza kuwafuatilia na kuyafukua na kuwakamata, au mvua ikija ikajaza mashimbo yao wakafa, au upepo mkubwa ukivuma unaweza kufukia mashimo yao kwa udongo utakaoporomoka au kuingia, hivyo hiyo inawafanya maisha yao kuwa hatarini sana japokuwa ni machachari au wana uwezo mkubwa wa kukimbia.

Lakini wibari kweli sio kama wanyama wengine, ni wadhaifu sana lakini wanafahamu ni wapi wanaweza kuwa salama.

Je na sisi, tutashindwa akili na wibari?

Usalama wetu upo wapi? Je tumeyajenga maisha yetu wetu wapi? Je, ni mashimoni au kwenye vichuguu, au kwenye miti au kwenye mwamba?. Tujue tu kuwa mwamba ni mmoja tu, naye ni YESU KRISTO peke yake. Ukiwa nje ya Kristo, fahamu kuwa maisha yako yapo katika hatari zote, haijalishi utajiona wewe ni mjanja kiasi gani, haijalishi utajiona ni hodari kiasi gani, haijalishi ni tajiri  kiasi gani, shetani atakumaliza tu..Huna safari ndefu..

Sikiliza maneno ya Yesu..

Mathayo 7:24 “Basi kila asikiaye hayo maneno yangu, na kuyafanya, atafananishwa na mtu mwenye akili, aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba;

25 mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, isianguke; kwa maana misingi yake imewekwa juu ya mwamba.

26 Na kila asikiaye hayo maneno yangu asiyafanye, atafananishwa na mtu mpumbavu, aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga;

27 mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, ikaanguka; nalo anguko lake likawa kubwa”.

Kweli itakuwa ni ajabu sana tukishindwa akili na mnyama pimbi.

Shalom.

[embedyt] https://www.youtube.com/watch?v=mJ0AkfAcM4I[/embedyt]

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Mavu ni nini katika biblia?(Kutoka 23:28, Kumb 7:20)

IKO NJIA IONEKANAYO KUWA SAWA MACHONI PA MTU.

Nini maana ya “katika wingi wa hekima mna wingi wa huzuni”.

NJIA YA ‘UTAJIRI MKUU’ KWA KIJANA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Bustani ya Edeni ipo nchi gani?

Bustani ya Edeni ipo nchi gani kwa sasa duniani?


Mungu alipoiumba dunia, alichagua eneo moja, na kulifanya kuwa la kipekee na la kitofauti na maeneo mengine yote aliyoyaumba duniani. Eneo hilo akaliita Edeni. Edeni maana  yake ni eneo la furaha kuu, utulivu,paradiso ya Mungu.

Lakini hakuishia hapo tu bali ndani ya hiyo Edeni upande wa mashariki alitengeneza bustani nzuri sana,  ambayo inajulikana na wengi kama bustani ya Edeni. Bustani hii ndiyo  Mungu aliyomweka mwanadamu wa kwanza hapo aishi (yaani Adamu na uzao wake.)

Lakini kama tunavyosoma biblia, wazazi wetu wa kwanza walipoasi, walifukuzwa kutoka katika bustani ile, na kuanzia hapo, hakuna aliyejua makao halisi ya bustani ya Edeni yalikuwa wapi, vifunguu pekee vinavyotupa taswira ya eneo la bustani ya Edeni ni hivi;

Mwanzo 2:8 “Bwana Mungu akapanda bustani upande wa mashariki wa Edeni, akamweka ndani yake huyo mtu aliyemfanya.

9 Bwana Mungu akachipusha katika ardhi kila mti unaotamanika kwa macho na kufaa kwa kuliwa; na mti wa uzima katikati ya bustani, na mti wa ujuzi wa mema na mabaya.

10 Ukatoka mto katika Edeni wa kuitilia bustani maji, na kutokea hapo ukagawanyika kuwa vichwa vinne.

11 Jina la wa kwanza ni Pishoni; ndio unaozunguka nchi yote ya Havila, ambako kuna dhahabu;

12 na dhahabu ya nchi ile ni njema; huko kuna bedola, na vito shoham.

13 Na jina la mto wa pili ni Gihoni; ndio unaozunguka nchi yote ya Kushi.

14 Na jina la mto wa tatu ni Hidekeli; ndio unaopita mbele ya Ashuru. Na mto wa nne ni Frati”.

Kama tunavyoona hapo, kulikuwa na mto uliokuwa unatoa maji kutoka bustanini na baadaye ukagawanyika katika vichwa vinne, na viwili kati ya hivyo (yaani Hidekeli na Frati) vinajulikana  mpaka sasa na vipo maeneo ya nchi ya Iraq, ili kusoma na kufahamu zaidi historia yao fungua hapa >>>> Mto frati na Hidekeli Na hiyo imewafanya masomi wengi wa biblia kudhania kuwa Edeni ilikuwa maeneo ya nchi ya Iraq au kando kando yake.

Lakini vile vingine viwili (yaani Pishoni na Gihoni) havijajulikana bado. Na iyo imewafanya wengine kudhani bustani ya Edeni ilikuwa nchi ya Uturuki ya sasa n.k.

Hivyo, hakuna uthibitisho wa moja kwa moja wa kudhania kuwa Edeni ilikuwa Iraq, au Uturuki au sehemu nyingine yoyote. Na hiyo ni kwasababu ya mabadiliko makubwa ya nchi yaliyokuwa yanatokea wakati wa gharika na  ule wakati wa kugawanyika kwa nchi (Mwanzo 10:25). Historia inaonyesha kuwa dunia ilibadilika mwonekano wake kwa sehemu kubwa sana.

Lakini ni wazi kuwa Edeni haikuwa pengine zaidi ya mashariki ya kati, na sio Afrika kama wanasayansi wanavyoamini, nami naamini ilikuwa katika nchi Kaanani (Yaani Israeli ya sasa).

Lakini ikiwa biblia haikutupa maelezo ya kutosha kuhusu jeografia ya bustani ya Edeni baada ya wazazi wetu wa kwanza kuasi, ni wazi kuwa hakuna umuhimu sana wa kujua bustani hiyo iko wapi kwasasa, kwasababu hayo yalishapita. Bali sasa Mungu ametutilia mkazo hasaa kutufahamisha juu ya Edeni yetu ya mbinguni inayokuja.

Yaani ile Yerusalemu mpya, mji mtakatifu ushukayo kutoka mbinguni kwa Mungu. Na Yerusalemu hiyo itashuka juu ya mbingu mpya na nchi mpya zitakazoumbwa kwa wakati huo baada ya utawala wa miaka elfu moja kuisha. Kama vile tu ilivyokuwa  Edeni ilivyoumbwa juu ya dunia ya wakati ule. Kufahamu zaidi juu ya utawala wa miaka 1000 fungua hapa >>>  UTAWALA WA MIAKA 1000.

Lakini kisichojulikana na wengi ni kuwa, si kila mtu atakayeruhusiwa kuingia ndani ya mji huo. Bali wale watakatifu tu watakaoshinda ulimwengu huu.

Tujiulize, Je! Mimi wewe tutakuwa miongoni mwa hao watakaouingia huo  mji mpya wa dhahabu yaani Yerusalemu ya Mbinguni, Edeni halisi ya Mungu? Je! Mambo ya ulimwengu huu bado yanatusonga, mpaka siku ile itukute ghafla tukaachwa?. Je! Unajua kuwa unyakuo upo karibu sana, na dalili zote za kurudi Kristo duniani zimeshatimia?

Ikiwa wewe bado hujaokoka na leo hii utapenda kumkabidhi Kristo maisha yako ayaokoe na akupe uweza wa kufanyika mtoto wake, basi uamuzi huo utakuwa ni wa busara sana kwako ambao hautaujutia milele. Hivyo kama upo tayari, basi fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba>>>  SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

   Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

MTO YORDANI UKO NCHI GANI KWA SASA?

Israeli ipo bara gani?

ORODHA YA WAFALME WA ISRAELI.

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

UFUNUO: Mlango wa 1

Rudi Nyumbani:

Print this post