Title November 2020

Mpumbavu ni nani katika biblia? (Zaburi 14:1, Mithali 10:14)

Katika kitabu cha Zaburi na Mithali Neno mpumbavu linatajwa sana, naomba kufahamu mpumbavu ni mtu wa namna gani kibiblia?


Biblia haielezi moja kwa moja maana ya mpumbavu, bali inaeleza tabia zinazoambatana  na mtu mpumbavu, embu tupitie baadhi ya vifungu vinavyolizungumzia neno hilo na mwisho kabisa hivyo ndivyo vitakavyotusaidia kujua mpumbavu ni mtu wa nanma gani;

Zaburi 14:1 “Mpumbavu amesema moyoni, Hakuna Mungu; Wameharibu matendo yao na kuyafanya chukizo, Hakuna atendaye mema”.

Mithali 10:8 “Aliye na akili moyoni mwake atapokea agizo; Bali mpumbavu mwenye maneno mengi ataanguka”.

Mithali 9:13 “Mwanamke mpumbavu hupiga kelele, Ni mjinga, hajui kitu”.

Mithali 10:14 “Watu wenye akili huweka akiba ya maarifa; Bali kinywa cha mpumbavu ni uangamivu ulio karibu”.

Mithali 10:23 “Kwa mpumbavu kutenda maovu ni kama mchezo; Bali mtu mwenye ufahamu ana hekima”.

Mithali 12:15 “Njia ya mpumbavu imenyoka machoni pake mwenyewe; Bali yeye aliye na hekima husikiliza shauri”.

Mithali 12:16 “Ghadhabu ya mpumbavu hujulika mara; Bali mtu mwerevu husitiri aibu”.

Mithali 14:1 “Kila mwanamke aliye na hekima hujenga nyumba yake; Bali aliye mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe”.

Mithali 15:5 “Mpumbavu hudharau kurudiwa na babaye; Bali yeye aangaliaye maonyo hupata busara”.

Mithali 14:16 “Mwenye hekima huogopa, akajitenga na uovu; Bali mpumbavu ana ufidhuli, na kujitumai”.

Mithali 20:3 “Mtu kujitenga na ugomvi ni heshima kwake; Bali kila mpumbavu ataka kugombana”.

Mithali 14:3 “Katika kinywa cha mpumbavu mna fimbo ya kiburi, Bali midomo ya wenye hekima huwahifadhi”.

Mithali 15:20 “Mwana mwenye hekima humfurahisha babaye; Bali mpumbavu humdharau mamaye”.

Hivi ni baadhi ya vifungu tu, lakini unaweza  kuona mpumbavu ni  mtu anayetajwa kuwa ana dharau, asiye na heshima, anayeropoka ropoka, asimcha Mungu, asiamini hata kama kuna Mungu, asiyetaka kurekebishwa, anayependa ugomvi,  anayesambaza habari za uzushi n.k.

Na tabia zote hizi huwa zinafanya na mtu mwenye dhambi, kwasasa ni mtu ambaye hajakombolewa na Yesu.

Hivyo tafsiri hasaa ya Neno mpumbavu, ni mtu ambaye hajazaliwa mara pili.

Kwahiyo  ikiwa wewe upo nje ya Kristo, haijalishi utakuwa msomi kiasi gani, au utakuwa tajiri kiasi gani, a utakuwa na ushawishi mwingi kiasi gani, wewe ni mpumbavu kibiblia, kwasababu hutakosa tabia mojawapo ya wapumbavu zinayozungumziwa katika biblia.

Ni Yesu pekee ndio mwenye uwezo wa kumgeuza mtu moyo wake na kumfanya kuwa mtu mwingine kabisa. Yeye mwenyewe alisema.. Wote wanaompokea anawapa UWEZO wa kufanyika watoto wa Mungu. (Yohana 1:12). Hii ikiwa na maana ukimkaribisha Yesu katika maisha yako, ni uhakika kuwa UWEZO huo utakuja ndani yako, wa kuweza kuzishinda tabia zote za wapumbavu,  yaani kushinda ulevi, kushinda uzinzi, kushinda anasa, kushinda usengenyaji n.k..

Hivyo kwanini usimpe leo YESU maisha yako ayaokoe, na utoke kuwa mojawapo ya wapumbavu mpaka kuwa mwana wa Mungu mteule, mbarikiwa aliyeandaliwa kwa ajili ya kuurithi uzima wa milele? Ikiwa upo tayari leo kuokoka, basi fungua hapa kwa ajli ya kuongozwa sala ya Toba na kupata maelekezo mengine  ya kiroho >>>>>  SALA YA TOBA

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

HEKIMA NI NINI? NA UFAHAMU UNAPATIKANA WAPI?

Nini maana ya Usiwe mwovu kupita kiasi? (Mhubiri 7:17)

USIONDOE ALAMA YA MPAKA ILIYOWEKWA NA MABABA.

Wibari ni nani?(Mithali 30:26)

Maana ya huu mstari ni ipi? Mithali 14:4 ‘Zizi ni safi ambapo hapana ngombe;bali nguvu za ngombe zaleta faida nyingi’.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Nini maana ya K.K, na B.K?  (B.C na A.D).

Hivi ni vifupisho vya nyakati.

K.K – Maana yake ni  Kabla ya kuzaliwa Kristo Yesu. Kwa kiingereza (B.C – Before Christ)

Na

B.K  ­- Maana yake ni Baada ya kuzaliwa kwake Kristo Yesu. Kwa kiingereza (A.D– Anno Domino- Katika mwaka wa Bwana )

Lakini mahali pengine wanatumia kifupi cha K.W.K kumaanisha K.K. na  WK kumaanisha B.K. Husasani kwa watu ambao sio wakristo, au hawaamini habari za Yesu Kristo, Lakini maana ni ile ile moja.

K.W.K maana yake ni Kabla ya wakati wa kawaida. Kwa kiingereza (B.C.E – Before the common Era)

Na,

W.K Maana yake ni Wakati wa kawaida. Kwa kiingereza (C.E– Common Era)

Kwamfano unaweza kukutana na habari fulani ya historia kwa mfano inasema kitabu cha Danieli kiliandikwa mwaka 600 KK, au 600 KWK, Hiyo inamaanisha kuwa kiliandikwa miaka 600 kabla ya kuzaliwa kwa Kristo.

Au utakutana na habari inasema Hekalu la Yerusalemu lilibomolewa mwaka 70 BK, Au 70 WW. Maana yake ni hekalu lilibomolewa mwaka wa 70 baada ya Kristo kuzaliwa duniani.

Hivyo tunaposema huu ni mwaka fulani wa 2000 + haimaanishi tangu dunia iumbwe ni miaka elfu mbili imepita hapana, bali ni miaka 2000 baada ya kuzaliwa kwa Bwana wetu Yesu Kristo. Kabla ya hapo kulikuwa na miaka mingine mingi iliyopita, zaidi ya 4000, ambayo ndiyo inahesabika kama miaka kabla ya Kristo.

Bwana akubariki.

Je! Umeokoka? Je! Unahabari kuwa hatuna muda mrefu sana, mpaka unyakuo upite? Yote yaliyotabiriwa yameshatimia, na kwamba pengine kizazi chetu kitashuhudia tukio zima la mwisho wa dunia? Swali la kujiuliza je na sisi tumejiwekaje.

Ikiwa upo nje ya Kristo na unataka leo ayageuze maisha yako. Basi uamuzi huo utakuwa ni wa busara sana kwako. Fungua hapa kwa ajili ya Sala ya Toba na maelekezo mengine >>> SALA YA TOBA

 Na Bwana akubariki sana.

Pia Tazama maana ya maneno mengine ya kibiblia chini.

Kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Nini Maana ya Hosana?

Mataifa ni nini katika Biblia?

Wakaldayo ni watu gani?

Bustani ya Edeni ipo nchi gani?

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

NAMI NINAZO FUNGUO ZA MAUTI, NA ZA KUZIMU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Nini Maana ya Hosana?

Hosana ni neno la kiyahudi lenye maana ya “OKOA”. Neno hili limeonekana mara ya kwanza kwenye biblia kipindi wakati Bwana Yesu anaingia Yerusalemu, ambapo wenyeji walimpokea kwa furaha, wakimwimbia na kumtukuza Mungu kwa shangwe nyingi..

Yohana 12: 12 “Nayo siku ya pili yake watu wengi walioijia sikukuu walisikia ya kwamba Yesu anakuja Yerusalemu;

13  wakatwaa matawi ya mitende, wakatoka nje kwenda kumlaki, wakapiga makelele, HOSANA! Ndiye mbarikiwa ajaye kwa jina la Bwana, Mfalme wa Israeli!”

Habari hiyo hiyo unaweza kuisoma tena katika Mathayo 21:9, Mathayo 21:15, na Marko 11:9-10.

Sasa swali la kujiuliza ni kwanini, Hao watu watumie hilo Neno “Hosana” na si Neno lingine lolote…labda “karibu Ee Masihi..karibu ee Masihi”..badala yake wanamkaribisha kwa kumwambia “Hosana” yaani “okoa..okoa”.

Ikumbukwe kuwa Wayahudi (yaani Waisraeli), wakati Bwana Yesu yupo duniani walikuwa wapo chini ya utawala wa kirumi.. Wakati huo dola ya kirumi ndiyo iliyokuwa inatawala dunia nzima chini ya Mfalme Kaisari aliyeko Rumi.

Kwahivyo wakati Kristo yupo duniani, Israeli ilikuwa ni koloni la hawa warumi, Ndio maana utaona pia waliomsulubisha Bwana ni askari wa kirumi. Hivyo waisraeli wote walikuwa wanalazimishwa kumpa Kodi Kaisari, na walikuwa wanamtumikia. Na kwasababu walikuwa wanayajua maandiko kwamba ipo siku Masihi (yaani Kristo), atakuja na kuwaokoa na utumwa wote na maadui zote..kama maandiko yanavyosema…katika Zekaria

Zekaria 14: 3 “Hapo ndipo atakapotokea Bwana, naye atapigana na mataifa hayo, kama vile alipopigana zamani siku ya vita”.

Hivyo Wayahudi wote walikuwa wanaitazamia hiyo siku ambayo Masihi atakuja kuwaokoa kwa mkono mkuu. Na baadhi waliokuwa wamemwamini Yesu kama ndiye Masihi huyo kafika, hivyo wakabeba matawi ya mitende na kumshangilia na kumfurahia alipoingia Yerusalemu, huku wakimwimbia..Hosana… hosana..au okokoa…okoa!

Na wanafunzi wake pia walitazamia wakati huo ndio ulikuwa umefika au umekaribia wa wakovu, wakati wa Masihi kuwapigania na kuwarudishia ufalme..wasiwe tena koloni la Taifa lingine. Ndio maana utaona kipindi kifupi tu baada ya kufufuka kwake, walimwuliza hilo swali..

Matendo 1:6  “Basi walipokutanika, wakamwuliza, wakisema, Je! Bwana, wakati huu ndipo unapowarudishia Israeli ufalme?

7  Akawaambia, Si kazi yenu kujua nyakati wala majira, Baba aliyoyaweka katika mamlaka yake mwenyewe.

8  Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi.

9  Akiisha kusema hayo, walipokuwa wakitazama, akainuliwa, wingu likampokea kutoka machoni pao”.

Hivyo ule haukuwa wakati wa Masihi kuwaokoa Israeli, dhidi ya utawala unaowatumikisha. Iliwapasa kwanza wakahubiri injili kwa watu wa mataifa yote kwanza, na injili itakapokwisha kuhubiriwa na watu kuokolewa, Ndipo huo wokovu mkuu kwa Israeli uje.

Hivyo utafika wakati ambapo Kristo atashuka kutoka mbinguni kwa nguvu nyingi, naye atawapigania Israeli na kuwaokoa, wakati huo injili itakuwa imeshamalizika kuhubiriwa kwa mataifa yote na unyakuo utakuwa umeshapita, na ndio utakuwa mwanzo wa utawala wa Miaka 1000 ya Yesu Kristo hapa duniani, ambapo utakuwa utawala wa Amani, na atatawala akiwa pale Yerusalemu, Israeli Pamoja na watakatifu wake aliowanyakua.

Je! Wakati huo utakuwepo Pamoja na Kristo katika utawala huo, au utakuwa jehanamu?. Maisha yako ndio jibu lako.

Kama hujaokoka Mlango wa Neema upo wazi sasa, ila hautakuwa hivyo siku zote..Ukimpokea leo Kristo, utafanyika kiumbe kipya na utakuwa na uhakika wa kuzirithi ahadi za Mungu walizoandaliwa wote wampendao.

Kama umeamua leo kumpa Kristo Maisha yako basi fuatilisha sala hii ya toba hapa >> SALA YA TOBA.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

WAISRAELI WENGI SANA WANARUDI KWAO SASA.

Je! Bwana Yesu alitumwa kwa Waisraeli tu peke yao?

SABATO TATU NI NINI?

TAZAMA, MWISRAELI KWELI KWELI, HAMNA HILA NDANI YAKE!

JIHADHARI NA UONGO WA SHETANI UNAOKARIBIANA NA UKWELI.

MAWE YALIYOKWISHA KUCHONGWA MACHIMBONI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Mataifa ni nini katika Biblia?

Watu wa mataifa mengine yote ya ulimwengu tofauti na Taifa la Israeli, ndio wanaojulikana kama “watu wa Mataifa”.

Mungu alipoanza mpango wake wa kurejesha uhusiano wake na mwanadamu ambao ulipotea tangu pale Edeni, alianza na Taifa moja tu lijulikanalo kama “Israeli”, Na Taifa hili lilianza na mtu mmoja ajulikanaye kama Ibrahimu, ambaye huyu Ibrahimu akamzaa Isaka,.Isaka akamzaa Yakobo, Yakobo akazaa Watoto 12, na kwa kupitia majina ya Watoto hao ndipo yakazaliwa majina ya makabila 12 ya Israeli. Na hao Watoto wakazaa wana, na hatimaye likawa jeshi kubwa la watu wengi wa jamii ya Israeli, na kuwa Taifa.

Sasa watu wengine wote tofauti na uzao huo wa Ibrahimu, ndio watu wa mataifa. Kwasababu duniani kulikuwa na watu wengine wengi wa jamii nyingi, walikuwepo waMisri (ambao ndio sasa nchi ya Misri), walikuwepo waashuri (Ambao kwasasa ni maeneo ya Syria), walikuwepo wakushi (ambao sasa ni maeneo ya huku Afrika)..walikuwepo Wakaldayo (ambao sasa ni maeneo ya Iraq), walikuwepo watu wa bara la Hindi (ambao sasa ndio India), walikuwepo watu wa Uajemi na Umedi ambao ndio kwasasa maeneo ya (Kuwait,Qatar, UEA{Dubai} na sehemu za magharibi ya Saudi Arabia), walikuwepo Warumi (ambao sasa ndio Italy), walikuwepo Wayunani (kwasasa ni Ugiriki) na mataifa mengine mengi (Yote hayo yalijulikana kama Mataifa).

Sasa Mungu amekuwa akitembea na Taifa la Israeli pekee Kwa miaka Zaidi ya 1,500, wakati huo wote Mungu hakushughulika na hayo mataifa mengi yote (haijalishi yalikuwa yameendelea kiasi gani au yalikuwa yana watu wazuri kiasi gani). Taifa lake teule na pekee lilikuwa ni moja tu ambalo ni Israeli, ndio maana utaona Amri 10, walipewa Israeli na si watu wa Mataifa mengine, na agano lote la kale inahusu Habari za wana wa Israeli mwenendo wao na Mungu wao.

Sasa sio kwamba Mungu alikuwa hana mpango kabisa na watu wa Mataifa!. La! Alikuwa ana mpango nao mkubwa sana. Lakini siku zote hakiwezi kuzaliwa cha pili, kabla ya kuzaliwa cha kwanza, hawezi kunyonya mtoto wa pili kabla hajanyonya wa kwanza, hawezi kukumbatiwa mtoto wa pili kabla ya wa kwanza. Hata mama anayejifungua Watoto, ni lazima azaliwe mtoto wa kwanza, ndipo afuate wa pili… Na yule wa kwanza atapendwa na kutunza kabla ya yule wa pili.

Kwahiyo Taifa la Israeli ni mzaliwa wa kwanza kwa Mungu, na watu wa mataifa ni mzaliwa wa pili..

Kutoka 4: 22 “Nawe umwambie Farao, Bwana asema hivi, Israeli ni mwanangu mimi, mzaliwa wa kwanza wangu;

23 nami nimekuambia, Mpe mwanangu ruhusa aende, ili apate kunitumikia, nawe umekataa kumpa ruhusa aende; angalia basi, mimi nitamwua mwanao, mzaliwa wa kwanza wako”.

Hivyo ulipofika muda wa “mzaliwa wa pili  kuzaliwa, (yaani wakati wa watu wa mataifa nao kukumbukwa na Mungu). Mungu alianza mpango wake huo kwa kumleta Mwanawe mpendwa Yesu Kristo, awe sababu ya wokovu kwa watu wote wa mataifa.

Kama kuku aliyeacha vifaranga vyake vya kwanza, kwa kuvidonoa na kuanza malezi mapya ya uzao wa pili, Ndicho alichokifanya Mungu kwa Israeli, Neema iliondoka kwao na kuhamia kwa watu wa mataifa (yaani mimi na wewe).

Warumi 11:25 “ Kwa maana, ndugu zangu, sipendi msiijue siri hii, ili msijione kuwa wenye akili; ya kwamba kwa sehemu ugumu umewapata Israeli, mpaka utimilifu wa Mataifa uwasili”.

Tangu wakati wa Bwana Yesu mpaka sasa, watu wa mataifa yote..tunaweza kumkaribia Mungu, na kuzirithi baraka zile zile za rohoni, kama walizokirimiwa Israeli.

Hiyo ndiyo SIRI YA MUNGU, ambayo ilifichwa kwa miaka mingi, ambayo hata wana wa Israeli wenyewe hawakujua kwamba ingefika siku moja, watu wa Mataifa nao watapata upendeleo kwa Mungu kama wao.

Paulo ambaye ni Muisraeli aliiandika siri hiyo kwa ufunuo wa Roho na kusema..

Waefeso 3:4  “Kwa hayo, myasomapo, mtaweza kuutambua ufahamu wangu katika siri yake Kristo.

5  Siri hiyo hawakujulishwa wanadamu katika vizazi vingine; kama walivyofunuliwa mitume wake watakatifu na manabii zamani hizi katika Roho;

YA KWAMBA MATAIFA NI WARITHI PAMOJA NASI WA URITHI MMOJA, NA WA MWILI MMOJA, NA WASHIRIKI PAMOJA NASI WA AHADI YAKE ILIYO KATIKA KRISTO YESU KWA NJIA YA INJILI”.

Hivyo tangu Bwana Yesu aondoke duniani, imepita Zaidi ya miaka 2,000 kipindi kirefu Zaidi ya kile Mungu alichotembea na wana wa Israeli peke yao.. Maana yake ni kuwa kipindi cha Neema kwetu sisi watu wa mataifa nacho kinaenda kufikia ukomo. Na kitafikia ukomo kwa unyakuo.

Unyakuo ukishapita mlango wa Neema unakuwa umefungwa kwa watu wa Mataifa. Mungu atawarudia tena watu wake Israeli kwa kipindi kifupi sana cha juma moja ambalo ni sawa na Miaka 7, baada ya hapo, hukumu ya mataifa itaanza na Utawala wa amani wa Yesu Kristo wa miaka elfu.

Je umempokea Kristo?..Upo ndani ya neema?. Kama bado upo nje, basi jua umechelewa sana..hivyo usiendelee kupoteza muda, ingia ndani ya neema uisalimishe roho yako. Yesu anakupenda na alikufa kwa ajili yako.

kumbuka pia, watu wote ambao hawajaokoka, katika agano letu jipya huitwa watu wa mataifa,

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

MPAKA UTIMILIFU WA MATAIFA UTAKAPOWASILI.

Masheki ni nini?(Zaburi 105:22, Ayubu 29:10)

ORODHA YA WAFALME WA ISRAELI.

WEWE U MWALIMU WA ISRAELI,NA MAMBO HAYA HUYAFAHAMU?

Nabii Elisha alikuwa ana maana gani kulia na kusema”Gari la Israeli na wapanda farasi wake”?

Nifanye nini ili niishi maisha ya ushindi siku zote?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Kuota upo nchi nyingine.

Kuota upo nchi nyingine.


Kama tunavyojua ukisafiri mahali ambapo ni tofuati na makazi yako ya asili, utakutana na mabadiliko mengi sana, hususani pale unapovuka mipaka na kuingia katika nchi nyingine, si ajabu kukutana na hali ya hewa ya aina nyingine, kukutana na watu wa jamii nyingine, kukutana na lugha gheni, n.k..

Na hiyo itakufanya usijione upo huru sana kama ulivyokuwa katika nchi yako mwenyewe.Na wakati mwingine inaweza kukufanya ujione haupo sehemu salama sana, kwasababu sio nchi yako, na haujaizoea.

Wana wa Israeli walipokuwa wanachukuliwa utumwani kupelekwa Babeli, wakiwa njiani walilia sana, hata wale wakaldayo,walipowashurutisha wawaimbie nyimbo za nchini mwao walikataa, wakasema tutaimbaje wimbo wa Bwana nchi ya ugenini?

Zaburi 137:1 “Kando ya mito ya Babeli ndiko tulikoketi, Tukalia tulipoikumbuka Sayuni.

2 Katika miti iliyo katikati yake Tulivitundika vinubi vyetu.

3 Maana huko waliotuchukua mateka Walitaka tuwaimbie; Na waliotuonea walitaka furaha; Tuimbieni baadhi ya nyimbo za Sayuni.

4 Tuuimbeje wimbo wa Bwana Katika nchi ya ugeni”?

Kwasababu walijua kabisa wanakwenda katika nchi ambayo sio ya kwao, katika mazingira ambayo hawajayazoea. Kwenye tamaduni mpya,

Hivyo unapojiona kwenye ndoto upo katika nchi ya ugenini, unaishi huko, au unatembea, Yapo mambo mawili hapo ambayo Mungu anakuonyesha.

Jambo la kwanza; Ikiwa wewe umeokoka, (yaani umeokolewa na Bwana Yesu), Hapo ni Mungu anakuonyesha wazi jinsi itakavyokuwa pale utakapotoka katika hifadhi yake. Utakuwa kama mtumwa, hivyo, jiangalie na jithibitishe, zidi kukaa katika mapenzi ya Mungu na kama ulikuwa umeshaanza kupoa, basi mgueukie Mungu wako kwa moyo wako wote. Ili ubakie katika nchi yako ya wokovu aliyokukusudia.

Lakini ikiwa hujaokoka, ni Mungu anakuonyesha hali yako ilivyo leo hii, upo katika nchi ya ugenini, japo hustahili kuwepo huko. Maisha yako yapo ugenini, hivyo huwezi kuwa huru, huwezi kuwa na amani, haijalishi pataonekana  ni pazuri namna gani, Wana wa Israeli walilia, walipokuwa wanaenda ugenini. Hivyo na wewe pia uliye dhambini, upo ugenini, pengine kampani unazotembea nazo sio ambazo Mungu amekukusudia utembee nazo, Mungu anakuhitaji wewe ukae na watakatifu wenzako uyatafakari maisha ya mbinguni. Pengine ulevi, anasa, wizi n.k., sivyo ambavyo vinakupasa mtu kama  wewe, na hilo unalijua kabisa, lakini bado unashikama nalo.

Embu yatafakari maisha yako, Je! Tangu ulipokuwa katika maisha ya dhambi ni raha gani umeipata au faida gani umepata?. Kwanini usizingatie kurudi nyumbani, kama yule mwana mpotevu aliyekwenda kuponda mali katika nchi ya mbali, lakini baadaye akazingatia kurudi kwa baba yake..Kwanini na wewe usizingatie kurudi kwa Baba yako wa mbinguni leo umwombe msamaha baada ya kupotea kwa muda mrefu.?

Ukisoma biblia utamwona Kaini yule aliyemuua ndugu yake ndiye aliyekuwa mtu asiye na kikao duniani, kama vile mapepo. Je na wewe unataka uwe mtu asiye na makao yake maalumu?

Leo hii ukikubali kutubu dhambi zako, Yesu atakupokea na kukusamehe, haijalishi wewe ni wa dini gani au dhehebu gani. Atakupokea, na kukukaribisha kwake, na atakupa raha nafsini mwako. Hivyo Kama upo tayari kufanya hivyo leo, basi fungua hapa kwa ajili ya maelekezo ya sala ya Toba, na Bwana akubariki. >>> SALA YA TOBA

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312/

Pia kwa ushauri/ratiba za ibada/ maombezi.

Jiunge kwenye magroup yetu ya Whatsapp kwa masomo ya kila siku ya Neno la Mungu.

Group la whatsapp  Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo:

KUOTA UMEACHWA NA GARI.

KUOTA UPO UCHI.

Wakaldayo ni watu gani?

HEKIMA YA KIMUNGU, INAINGIAJE MIOYONI MWETU?

PALE AHADI ZA MUNGU ZINAPOKUJARIBU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Sodoma ipo nchi gani?

Sodoma ipo nchi gani?


Sodoma na Gomora ni miji iliyokuwa katika nchi ya Kaanani (Ambayo ndio Israeli ya Sasa). Miji hii miwili ni moja kati ya miji mitano iliyokuwa katika bonde la Yordani..mingineyo  ikiwemo, ni Adma, Seboimu, na Lasha.

Kama tunavyoijua habari, miji hii miwili (yaani Sodoma na Gomora) ndiyo iliyokuwa kiini cha maovu yote katika bonde hilo.

Mwanzo 19:24 “Ndipo Bwana akanyesha juu ya Sodoma na juu ya Gomora kiberiti na moto toka mbinguni kwa Bwana.

25 Akaangusha miji hiyo na Bonde lote, na wote waliokaa katika miji hiyo, na yote yaliyomea katika nchi ile”.

Hata hiyo mingine nayo haikupona, nayo pia iliangamizwa;

Kumbukumbu 29:23 “ya kuwa nchi yake nzima ni kibiriti, na chumvi, na kuteketea, haipandwi, wala haizai, wala nyasi hazimei humo, kama mapinduko ya Sodoma na Gomora, Adma na Seboimu, aliyoipindua Bwana kwa ghadhabu yake na hasira zake”;

Lakini ni tahadhari gani tunapaswa tuchukue tunaposoma habari ya miji hii miovu?

Licha ya kuwa ilikuwa ni miovu lakini biblia inatuambia ilikuwa ni miji yenye kuvutia sana, mfano wa Edeni, Bustani ya Bwana soma (Mwanzo 13:10). Mfano tu wa dunia ya sasa. Ulimwengu wa sasa umejengeka na unavutia kuliko ule wa zamani,hilo lipo wazi, starehe za wakati ule haziweki kulinganishwa hata kidogo na starehe za wakati huu, lakini maovu yake ni  zaidi ya yale ya Sodoma na Gomora.

Ushoga sio jambo la kushangaza tena, kiasi kwamba nchi zimefanikiwa kuhalalisha jambo hilo, na sehemu nyingine mpaka kwa yanayoyaita makanisa (ambayo kiuhalisia si makanisa), yamevuka mpaka huo na kuhalalisha ushoga bila hata kuogopa kumuhusianisha Mungu na matendo kama hayo maovu. Hiyo ni kuonyesha kuwa mwisho wa huu ulimwengu upo karibuni sana. Wapo watu wanajidanganya kuwa hii dunia haitaangamizwa, kwasababu Mungu alishasema hivyo wakati ule wa Gharika kuwa hatagharikisha.. Lakini hawajui kuwa ni kweli Mungu hatauangamiza huu ulimwengu kwa maji, lakini amesema ataugharikisha moto. Ambapo kila mtu mwovu, na kila kitu kitafumuliwa, biblia inasema hivyo soma.

2Petro 3:7 “Lakini mbingu za sasa na nchi zimewekwa akiba kwa moto, kwa neno lilo hilo, zikilindwa hata siku ya hukumu, na ya kuangamia kwao wanadamu wasiomcha Mungu……..

10 Lakini siku ya Bwana itakuja kama mwivi; katika siku hiyo mbingu zitatoweka kwa mshindo mkuu, na viumbe vya asili vitaunguzwa, na kufumuliwa, na nchi na kazi zilizomo ndani yake zitateketea.

11 Basi, kwa kuwa vitu hivi vyote vitafumuliwa hivyo, imewapasa ninyi kuwa watu wa tabia gani katika mwenendo mtakatifu na utauwa,

12 mkitazamia hata ije siku ile ya Mungu, na kuihimiza; ambayo katika hiyo mbingu zitafumuliwa zikiungua, na viumbe vya asili vitateketea na kuyeyuka”?

Unaona?  Swali la kujiuliza ni je! Sisi tumejiwekaje? Katika kipindi hichi cha mwisho? Je na sisi tutapumbazwa na Ulimwengu huu kama Lutu na mke wake? Tukaacha kubaki mahali Mungu alipotuweka tukaenda kushikamana na mambo ya ulimwengu huu yanayodanganya?. Huu ni wakati wa kujiokoa nafsi yako, na si wakati wa kumwangalia ndugu, au rafiki, au mjomba anasemaje, kwasababu mwisho upo karibu.

Je umeokoka?

Kama bado na upo tayari kufanya hivyo leo, huo ni uamuzi wa busara sana kwako, kama upo tayari kumpa Yesu maisha yako leo, basi fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba, na maelekezo mengine >>>>  SALA YA TOBA

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

JINSI SODOMA NA GOMORA ILIVYOKUWA INAVUTIA SANA..

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

Israeli ipo bara gani?

CHUKIZO LA UHARIBIFU

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

Rudi Nyumbani:

Print this post

HEKIMA YA KIMUNGU, INAINGIAJE MIOYONI MWETU?

Shalom!. Karibu tuyatafakari pamoja maandiko.

Elimu yoyote ile ya kidunia ni hekima..hekima sio tu kujua Nahau, na misemo na methali. Mtu anayekwenda kusoma elimu fulani labda ya uchumi au udaktari, anaingiza hekima ndani yake ya namna ya kumtibu mtu au namna ya kufanya biashara. Kadhalika na Elimu nyingine zote mtu anazokwenda kuzisomea, anakuwa anajiongezea hekima katika nyanja hiyo anayokwenda kuisomea.

Sasa fomula ya kujiongezea maarifa katika mambo ya kidunia, haina tofauti sana na ile ya kujiongezea hekima katika mambo ya kiMungu. Tunapomwomba Mungu atupe hekima na maarifa katika kumjua yeye, haitakuja tu kwa kumwomba na kisha kukaa kusubiri, hapana!..Bali inakuja kwa kumwomba kwanza, na kisha kwenda kuitafuta.. Unapokwenda kuitafuta kwasababu ulishamwomba Mungu, anachokifanya yeye ni kuifanikisha njia yako katika kwenda kuitafuta…anakupa uwezo wa kuelewa kiwepesi zaidi kuliko kama ungekuwa hujamwomba.

Ni fomula ile ile tu ya mwanafunzi anayemwomba Mungu amfanikishe katika masomo yake, hawezi kuomba Mungu ampe uwezo wa kuelewa na kufanya vizuri katika mitihani na huku ameacha kusoma kabisa, hapo hatapata chochote, lakini kama amemwomba Mungu kwa Imani, na kwenda kusoma ndipo akili yake inaongezewa uwezo mara dufu zaidi ya kuelewa tofauti na yule mwanafunzi ambaye hajamwomba Mungu kabisa.

Na pia katika kuitafuta Hekima ya kiMungu ni hivyo hivyo, Tunapomwomba Mungu atupe hekima ya kiMungu sawasawa na Yakobo 1:5, hatupaswi kusubiri tu!..Ni wakati wa kuiweka imani katika matendo baada ya hapo..kwa kwenda kuanza kulisoma Neno lake kwa bidii na kumtafuta yeye kwa bidii zote, na kwa nguvu zote.

Mathayo 22:37  “Akamwambia, Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote. Hii ndiyo amri iliyo kuu, tena ni ya kwanza”

Ukianza kuweka bidii katika kumjua Mungu, kwa moyo wako wote kiasi kwamba moyo wako wote upo kwake, na unatumia akili zako zote ulizopewa na Mungu katika kumtafuta yeye, na kuifanya kazi yake, na pia unatumia nguvu zako zote Mungu alizokujali za kimwili na kiroho..Hekima ya kiMungu itazidi kuingia ndani yako, na utakuwa unazidi kumjua Mungu na kuwa na uwezo mkubwa wa kuchambua mambo kwa kadri siku zinavyozidi kwenda.. Bwana ataisafisha njia yako na utakuwa na hekima nyingi.

Utauliza vipi na Sulemani, na yeye aliipata hekima kwa njia hiyo hiyo?

Jibu ni ndio!..Sulemani baada ya kumwomba Mungu hekima, hakukaa tu na ghafla akaanza kujikuta anaelewa mambo…La! hakufanya hivyo, kinyume chake baada ya kumwomba Mungu hekima, alianza kutafuta huko na huko kwa kusoma mambo mengi ya kiMungu na kimaisha, ndipo hekima ikaingia ndani yake, Mungu akamsaidia kupata alichokiomba…Maandiko yanasema hivyo katika mstari ufuatao..

Mhubiri 12: 9 “Walakini, kwa sababu huyo Mhubiri alikuwa na hekima, aliendelea kuwafundisha watu maarifa, naam, akatafakari, akatafuta-tafuta, akatunga mithali nyingi.

10 Huyo Mhubiri akatafuta-tafuta ili apate kuona maneno yapendezayo, na yale yaliyoandikwa kwa unyofu, yaani, maneno ya kweli”.

Huyo ni Sulemani, ambaye baada ya kuomba hekima, akajikita katika kwenda kuitafuta huko na huko, akajikita katika kutafakari sana..na alipopata uelewa wa mambo ndipo akazitunga mithali..Na alikuwa akitafuta kuelewa mambo KWA KUSOMA VİTABU VİNGİ, na kufanya utafiti mwingi, na alikuwa mpaka anachoka mwili kwaajili ya kusoma tu. Mpaka akasema “Kusoma sana kwa uchosha mwili”..

Mhubiri 12: 12 “….. hakuna mwisho wo wote wa kutunga vitabu vingi; NA KUSOMA SANA HUUCHOSHA MWİLİ”

Je! Wewe ulishawahi kuzitafuta habari za Mungu kwa bidii namna hiyo mpaka Mwili ukachoka?..na uchovu anaouzungumzia hapo na Sulemani sio uchovu wa usingizi (maana kuna mtu atasoma Neno dakika 10 na kusikia usingizi, na mwisho akasema amechoka..Hapo! hujachoka! Bali umekuwa mvivu). Uchovu unaozungumziwa hapo na Sulemani ni kama ule mwanafunzi anaochoka wakati karibia na anapohitimu, baada ya kusoma miaka mingi. Pale ambapo kichwa chake kimejaa maarifa ya kutosha ya kuweza kukabiliana na mtihani wowote unaokuja mbele yake, lakini mwili wake umekuwa dhaifu kwa kuihangaikia hiyo elimu, alipokuwa akijitesa na kujizuia kwa mambo mengi ilimradi tu aipate hiyo elimu.

Bwana atusaidie nasi tuwe kama Sulemani, na tumpende Bwana Mungu wetu kwa mioyo yetu yote, kwa akili zetu zote, na kwa nguvu zetu zote, ili tuweze kuipata hekima ya kiMungu ndani yetu…

Mithali 2:10 “Maana hekima itaingia moyoni mwako, Na maarifa yatakupendeza nafsi yako”.

Kama hujaokoka, Kristo yupo mlangoni, hizi ni siku za mwisho, na wokovu ndio mwanzo wa hekima..Hivyo mpokee Kristo leo kwa kumwamini na kutubu dhambi zako zote, na kubatizwa. Naye atakukubali, kama alivyosema katika Neno lake.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Moyo wake mwenye hekima upo upande wa kuume, maana yake nini?

WALIO NA HEKIMA NDIO WATAKAOELEWA.

MAASI KUONGEZEKA NI ISHARA YA NINI?.

Nini maana ya “katika wingi wa hekima mna wingi wa huzuni”.

MAMBO 5 AMBAYO KILA MKRISTO ANAPASWA KUFAHAMU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Nini maana ya “kila tendo lisilotoka katika imani ni dhambi?”

Jibu: Tusome mstari huo kuanzia juu kidogo.

Warumi 14:21  “Ni vyema kutokula nyama wala kunywa divai wala kutenda neno lo lote ambalo kwa hilo ndugu yako hukwazwa.

22  Ile imani uliyo nayo uwe nayo nafsini mwako mbele za Mungu. Heri mtu yule asiyejihukumu nafsi yake katika neno lile analolikubali.

23  Lakini aliye na shaka, kama akila, amehukumiwa kuwa ana hatia, kwa maana hakula kwa imani. NA KILA TENDO LISILOTOKA KATIKA IMANI NI DHAMBI”

Tukirudi juu Zaidi katika Mstari wa 14, Neno la Mungu linasema..

Warumi 14:14  “Najua, tena nimehakikishwa sana katika Bwana Yesu, ya kuwa hakuna kitu kilicho najisi kwa asili yake, lakini kwake yeye akionaye kitu kuwa najisi, kwake huyo kitu kile ni najisi”

Katika mistari hii, biblia ilikuwa inazungumzia juu ya vyakula..Na katika agano jipya, biblia imesema hakuna chakula chochote kilicho najisi.. Kwasababu kinachomwingia mtu mdomoni hakimtii unajisi, bali kile kimtokacho moyoni mwake ndicho kinachomtia mtu unajisi..Ni Bwana wetu Yesu ndiye aliyetupa ufunuo huo, ambao ni kweli kabisa..kasome Mathayo 15:16-20.

Kwahiyo katika agano jipya, nguruwe sio najisi, Kambale sio najisi, hata wanaokula nyoka hawapati unajisi wowote.

Lakini kwasababu ufunuo huo umekuwa mgumu kueleweka kwa wengi, kwamba vyakula vyote vimetakaswa.. Hivyo bado wanabaki kuamini kuwa vipo baadhi vilivyo najisi, kama nguruwe, Kambale, na vingine baadhi…. Sasa hawa ndio biblia inawataja kuwa “DHAIFU WA IMANI” (Warumi 14:1), haijalishi wao watajiona wana Imani kiasi gani, lakini biblia imewataja kuwa ni dhaifu wa Imani. Na miongoni mwao wapo Wakristo na wasio wa Kristo.

Sasa kwasababu biblia ni kitabu cha Hekima, imetufundisha jinsi ya kuenenda na hawa watu,

Kwanza: hatupaswi kuyahukumu mawazo yao (Maana yake kuwalazimisha waamini tunachoamini sisi, ikiwemo pia kushindana nao hatupaswi kushindana nao).

Pili: hatupaswi kuutumia ujuzi huo tulionao sisi kuwafanya wamkosee Mungu, au wamwache Kristo au kumchukia.

Maana yake ni kwamba labda umemhubiria Muislamu, akamwamini na kumpokea Kristo, lakini bado akawa anaamini kuwa nguruwe ni najisi. Na wewe kwasababu una UJUZI wa kujua kuwa hakuna kilicho najisi, hupaswi kwenda kula nguruwe mbele yake..au kumlazimisha ale nguruwe, ukifanya hivyo mwisho wa siku utamhuzunisha na kumfanya arudi nyuma au auchukie ukristo moja kwa moja..Na tukimkosesha mtu mmoja kwaajili ya chakula biblia inasema tunamtenda Kristo dhambi (Ndio hapo biblia inasema ni heri nisilie nyama kabisa kama itamkosesha ndugu yangu)..

1Wakoritho 8:11 “Na yule aliye dhaifu aangamizwa kwa ujuzi wako, naye ni ndugu ambaye Kristo alikufa kwa ajili yake.

12  Hivyo, mkiwatenda dhambi ndugu zenu na kuitia jeraha dhamiri iliyo dhaifu, mnamtenda dhambi Kristo.

13  Kwa hiyo, chakula kikimkwaza ndugu yangu, hakika sitakula nyama hata milele, nisije nikamkwaza ndugu yangu”

kwasababu hata asipokula hivyo vyakula tunavyokula sisi haviwafanyi wao wasiende mbinguni. Wasipokula nguruwe Maisha yao yote au Kambale, na wakawa wamempokea Kristo, watafika mbinguni tu.. Hivyo hatupaswi kutumia UJUZI wetu kuiharibu kazi ya Mungu ya wokovu.

Ndivyo biblia inavyosema katika..

Warumi 14: 1  “Yeye aliye DHAIFU WA IMANI, mkaribisheni, walakini msimhukumu mawazo yake.

2  Mtu mmoja anayo imani, anakula vyote; lakini yeye aliye dhaifu hula mboga.

3  Yeye alaye asimdharau huyo asiyekula, wala yeye asiyekula asimhukumu huyo alaye; kwa maana Mungu amemkubali.

4  Wewe u nani unayemhukumu mtumishi wa mwingine? Kwa bwana wake mwenyewe yeye husimama au huanguka. Naam, atasimamishwa, kwa kuwa Bwana aweza kumsimamisha”

Sasa kwa huyu mtu ambaye ni DHAIFU WA IMANI, ambaye moyoni mwake “anaamini kabisa kwamba kula nguruwe ni dhambi, au kula chakula Fulani ni dhambi”.. mtu huyu akaacha kufanya hicho kitu anachokiamini na kwenda kula nguruwe au chakula kingine chochote ambacho anajua sio sawa kulingana na anachokiamini moyoni mwake. Huyo mtu ni wazi kuwa baada ya kula, moyoni mwake ATASIKIA HALI YA KUHUKUMIWA. Sasa hiyo hali ya kuhukumiwa anayoisikia maana yake ni kwamba, amefanya kitu kinyume na anachokiamini, Hapo tayari kafanya tendo ambalo halijatokana na kile anachokiamini, na hivyo ANATENDA DHAMBI!!…Hiyo ndio maana ya “KILA TENDO LISILOTOKA KATIKA IMANI NI DHAMBI”,

Lakini kama macho yake yalifumbuka na kupata ufunuo kuwa “ni kweli hakuna kilicho najisi” na kwa ufunuo huo akaenda kula chakula ambacho hapo kwanza alikuwa anakiona ni najisi..Ni wazi kuwa mtu huyo baada ya kula hatasikia kuhukumiwa moyoni mwake, kwasababu amefanya kitu akiwa na uhakika kwamba hamtendi Mungu dhambi, na hivyo atakuwa kafanya jambo lile kwa Imani, na kwake hiyo haitahesabika kuwa ni dhambi.

Hivyo ndugu unayesoma ujumbe huu, ambaye ni mkristo, kama unaamini kuwa bado kuna vyakula najisi, na hivyo dhamiri yako inakushuhudia kwamba hupaswi kula, basi usivile lakini hakikisha unaushikilia utakatifu wote na kukaa katika maagizo ya Mungu.

Na kama wewe haupo katika Imani ya kikristo (maana yake ni Muislamu au mtu wa Imani nyingine), fahamu kuwa Yesu anakupenda na alikufa kwaajili yako..Njoo kwa Yesu na heshima yako hiyo hiyo uliyonayo, yeye atakuongezea nyingine juu ya hiyo itakayodumu milele, …njoo kwa Yesu na ustaarabu wako huo huo, hatakupokonya, badala yake atakuongezea na mwingine mwingi udumuo milele…njoo kwa Yesu na maadili yako hayo hayo, na kujisitiri kwako huko huko, atakuongezea na mwingine mwingi…Njoo kwa Yesu ukiwa huli nguruwe hivyo hivyo, wala hatakuambia uanze kuzila nguruwe..anachokihitaji ni roho yako na si tumbo lako, akuokoe akupe uzima wa milele bure!..Kwasababu yeye ndiye aliyetumwa kuukomboa ulimwengu, wala hakuna mwingine.

Hivyo kama umeamua leo kumpokea hatua inayofuata ni rahisi sana, hapo ulipo piga magoti, kisha fuatilisha sala hii  kwa kufungua hapa >>> SALA YA TOBA

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

SIKUKUU 7 ZA KIYAHUDI ZINAFUNUA NINI KWETU?

KUOTA UNAKULA CHAKULA.

CHAKULA CHA ROHONI.

Katika Mathayo 15:21-28, Yesu alikuwa na maana gani alipomwambia huyu Mama kwamba chakula cha watoto hawapewi mbwa?

Mstari huu una maana gani? “Tupa chakula chako usoni pa maji; Maana utakiona baada ya siku nyingi”. (Mhubiri 11:1)

Rudi Nyumbani:

Print this post

USIOMBE MAOMBI YASIYOKUWA NA MAJIBU NA WALA USIMTUKANE MUNGU.

Luka 23:42  “Kisha akasema, Ee Yesu, nikumbuke utakapoingia katika ufalme wako.Yesu akamwambia, Amin, nakuambia, leo hivi utakuwa pamoja nami peponi”.

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe. Karibu tujifunze biblia.

Kama tunavyojua wengi wetu, kwamba Kristo hakusulubiwa peke yake pale Kalvari, bali alisulubiwa pamoja na wanyang’anyi wengine wawili. Na wote walikuwa wametundikwa msalabani kama Bwana, kufunua kuwa na wao pia wapo katika mateso na uchungu. Lakini kilichowashangaza  zaidi ni kuona anayejiita ni mkombozi naye pia yupo katika mateso kama wao. Katika hali ya kawaida ni jambo linalochanganya kidogo. Hivyo kila mmoja akawa na neno la kumwambia Bwana Yesu.

Wa kwanza akatangulia kumwambia Bwana,……

“Na mmoja wa wale wahalifu waliotungikwa alimtukana, akisema, Je! Wewe si Kristo? Jiokoe nafsi yako na sisi. Lakini YESU HAKUMJIBU NENO. (Luka 23.39 )”

Kitendo tu cha kuanza kwa  kumwambia Bwana…wewe si Kristo?..hicho tayari ni kitendo cha kukosa heshima!..na hakujua kama tayari kamtukana Mungu, kwa kusema tu hivyo..

Mfano kamili wa watu wengi wa siku hizi za Mwisho, Wapo katika dimbwi kubwa la matatizo, na shida lakini watasimama mbele za Mungu, na kusema “kama wewe Mungu upo na una nguvu, mbona huniokoi na shida hizi” na pia “mbona baadhi ya watu wako wana shida nyingi, waokoe watu wako kwanza na shida zao na ndio utusaidie sisi”.

Hawajui kwamba tayari wanamtukana Mungu kwa hayo maneno. Sasa watu wa namna hii, kamwe wasitazamie kupokea majibu yoyote kutoka kwa Mungu, kwasababu wamekosa unyenyekevu…

Ndio maana unaona huyo mnyang’anyi alitazamia atajibiwa na Bwana kwa kejeli zake, lakini Kristo hakutoa neno lolote hata la kumwambia atubu!

Lakini tukiendelea na Mtu wa pili, ambaye naye pia alikuwa anaswali kama hilo hilo kichwani?, isipokuwa huyu alituliza akili yake na kufikiri mara mbili, na kujua kuwa yaliyompata amestahili kupokea malipo yake, na kwamba Kristo yaliyompata hakustahili, maana yake ni kwamba amejitoa kusulubiwa kwaajili ya makosa ya watu wengine, na si kwa makosa yake….kwa kutafakari sana..roho ya unyenyekevu ikamwingia, na ya kuomba msaada..

Luka 23:40  “Lakini yule wa pili akamjibu akamkemea, akisema, Wewe humwogopi hata Mungu, nawe u katika hukumu iyo hiyo?

41  Nayo ni haki kwetu sisi, kwa kuwa tunapokea malipo tuliyostahili kwa matendo yetu; bali huyu hakutenda lo lote lisilofaa.

42  Kisha akasema, EE YESU, NİKUMBUKE UTAKAPOİNGİA KATİKA UFALME WAKO.

43  Yesu akamwambia, Amin, nakuambia, leo hivi utakuwa pamoja nami peponi”

Hebu mtafakari huyu mtu wa pili, Hata hakuomba kushushwa msalabani aendelee na maisha yake, hakumwomba Yesu amshushe arudi akaione familia yake, hakuomba Yesu amwokoe pale msalabani arudi kwenye biashara yake, hakuomba Yesu amwokoe pale msalabani ili asiendelee kuteseka na maumuvi ya misumari…lakini alimwomba Yesu UZIMA BAADA YA KIFO. Alikikubali kifo, lakini aliomba tu uzima baada ya hicho kifo. Alisema nitastahimili shida ninayoipata sasa, nikipata msamaha wa kushushwa hapa msalabani sawa, nisipopata pia ni sawa, nitavumilia mateso, lakini tu, niupate huo UZIMA WA MILELE, baada ya kufa kwangu. Huyo pekee yake ndiye Kristo aliyemjibu!.

Lakini yule wa Kwanza hakujibiwa Neno hata moja. Na matokeo yake alikufa katika mateso yake na akakosa vyote, akakosa maisha ya dunia aliyokuwa bado anayatamani, na vile vile akakosa uzima baada ya kifo.

Ndugu yangu, huu sio wakati wa kumfuata Kristo ili upate MALI, na huku huna uzima wa milele moyoni mwako..Kristo hatakujibu chochote!..Unapitia shida sasa za kidunia, sio wakati wa kulia uondolewe kwenye hizo shida huku shida ya roho yako bado ipo, huku hutaki kusikia hata habari za Neno lake, Ukisikia habari za Yesu kwako ni habari za kupoteza muda tu, comedy zinazolikebehi Neno lake ndizo zinazokuchekesha… hapo usitazamie kujibiwa chochote.

Tafuta uhakika  kwanza wa uzima wa maisha baada ya haya kuisha, Ndio kitu cha muhimu kwa sasa. Ukikimbilia kuomba msaada wa mambo ya kidunia, kuna uwezekano mkubwa usikipate hicho unachokitafuta na ukafa katika shida zako, na ukakosa vyote (ukakosa Uzima wa Milele pamoja na Mali unazozitafuta).

Mathayo 6: 33  “Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa”.

Leo umesikia ujumbe huu, pengine ulikuwa unamtukana na kumdhihaki Mungu pasipo kujua..Upo kwenye shida kweli lakini umekuwa mtu wa kulalamika mpaka kufikia kumdhihaki Mungu… ndio maana leo umekutana na ujumbe kama huu ni kwasababu Kristo bado anakupenda, ndio maana bado hujafa..Upo hapo msalabani umening’inia na shida zako, zinakutesa kweli, unatamani kutoka hapo…Usikimbilie kutafuta msaada wa kutoka hapo kwanza, kwasababu kwa dhambi zako umestahili kuwepo hapo ulipo…Unachopaswa kufanya sasa, ni kuanguka chini, kwa unyenyekevu na kutubu na kumwomba Bwana Yesu msamaha kwa dhambi zako, na kumwambia kuanzia leo nakufuata naomba unipe uzima wa milele…Hata kama usiponitoa katika haya mateso ninayopitia sasa, naomba unipe UZİMA WA MİLELE,  hata kama nikifa leo pasipo kupata chochote katika haya maisha naomba Uzima wa milele baada ya kifo..hicho ndio cha kwanza tunachokihitaji sisi.

Ukiomba maombi ya namna hiyo Roho Mtakatifu atashuka ndani yako kukupa jibu la maombi yako, amani ya ajabu itashuka ndani yako, na utaona akili yako imebadilika na kuwa kama ya Bwana Yesu, kiasi kwamba hizo shida zitakuwa sio kitu kwako, kwajinsi hiyo furaha itakavyokuwa kubwa ndani yako.

Lakini kwanza mpokee Kristo katika maisha yako, na tubu…Na pia kama umetubu hakikisha unatafuta ubatizo sahihi, ambao ni wa maji tele (Yohana 3:23) na kwa jina la Yesu Kristo (Matendo 2:38) kukamilisha wokovu wako.

Na pia kama utapenda kushare ujumbe huu na wengine, tunaomba usiondoe chochote, ikiwemo anwani ya www wingulamashahidi org pamoja na namba zetu hizi 0789001312.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

FAIDA ZA MAOMBI.

NAWAAMBIA MAPEMA!

UFUNUO: Mlango wa 1

UNAZO KILA SABABU ZA KUMSHUKURU MUNGU

KUNA UMUHIMU WA KUWA MTU WA KURIDHIKA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Biblia ina vitabu vingapi?

Je! Biblia ina vitabu vingapi?


Biblia takatifu ina jumla ya vitabu 66, kati ya hivyo 39 ni vya agano la kale, na 27 ni vya agano jipya.

Hii ni orodha ya vitabu vya agano la kale:

  1. Mwanzo
  2. Kutoka
  3. Mambo ya walawi
  4. Hesabu
  5. Kumbukumbu la Torati
  6. Yoshua
  7. Waamuzi
  8. Ruthu
  9. 1 Samweli
  10. 2 Samweli
  11. 1 Wafalme
  12. 2 Wafalme
  13. 1 Mambo ya Nyakati
  14. 2 Mambo ya Nyakati
  15. Ezra
  16. Nehemia
  17. Esta
  18. Ayubu
  19. Zaburi
  20. Mithali
  21. Mhubiri
  22. Wimbo ulio bora
  23. Isaya
  24. Yeremia
  25. Maombolezo
  26. Ezekieli
  27. Danieli
  28. Hosea
  29. Yoeli
  30. Amosi
  31. Obadia
  32. Yona
  33. Mika
  34. Nahumu
  35. Habakuki
  36. Sefania
  37. Hagai
  38. Zekaria
  39. Malaki

Ifuatayo ni orodha ya vitabu vya agano jipya:

  1. Mathayo
  2. Marko
  3. Luka
  4. Yohana
  5. Matendo
  6. Warumi
  7. 1 Wakorintho
  8. 2 Wakorintho
  9. Wagalatia
  10. Waefeso
  11. Wafilipi
  12. Wakolosai
  13. 1 Wathesalonike
  14. 2 Wathesalonike
  15. 1 Timotheo
  16. 2 Timotheo
  17. Tito
  18. Filemoni
  19. Waebrania
  20. Yakobo
  21. 1 Petro
  22. 2 Petro
  23. 1 Yohana
  24. 2 Yohana
  25. 3 Yohana
  26. Yuda
  27. Ufunuo

Zipo zinazosemekanakuwa ni biblia, ambazo zina vitabu 72 na nyingine zaidi. Na zinatumiwa na baadhi ya madhehebu ya kikristo kama vile Katoliki na Othrodoksi.  Vitabu hivyo vilivyoongezwa havijathibitishwa kuwa vimevuviwa na Roho Mtakatifu hivyo hatupaswi kuviamini.

Biblia tunayopaswa kuiamini ni ile yenye vitabu hivyo 66 vilivyoorodheshwa hapo juu.

Shalom.

Je! utapenda uwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp? kama ndivyo basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Biblia ni nini?

Watoto wa Ibrahimu/Wana wa Ibrahimu walikuwa ni wangapi?

JIFUNZE KULIGAWANYA VYEMA NENO LA MUNGU.

JINSI YA KUSOMA BIBLIA.

WINGU KUBWA LA MASHAHIDI.

Rudi Nyumbani:

Print this post