Title 2020

NAO WAKADHANI YA KUWA YUMO KATIKA MSAFARA;

Bwana wetu Yesu Kristo asifiwe ndugu yangu..

Nyakati hizi za mwisho tunazoishi sasa, ni nyakati ambazo zinakithiri kuwa na mseto wa watu wengi wanaojiita wakristo, leo hii ni rahisi kuona hata msanii wa kidunia anaimba nyimbo za Injili, ni rahisi kuona, mashoga wanatoa michango ya kujenga makanisa makubwa ulaya, wazinzi wanahudhuria kila jumapili ibadani, wengine mpaka wapo tayari kushiriki meza ya Bwana bila hofu nao wanaona ni kawaida tu. Ni kundi kubwa lenye mchanganyiko wa kila aina ya watu, wengine hawana hata mpango wa kufikiria maisha yao baada ya hapa, kinachowapeleka kwa Mungu tu, ni pengine waponywe waondoke, wengine wapate tu wachumba, wengine biashara zao ziende vizuri..basi hakuna cha zaidi baada ya hapo

Na wachache sana ndio wanaoutafuta wokovu wa kweli, ambao wapo tayari kumtii na kumfuata Yesu pale alipo yeye..

Embu leo kwa ufupi tuone habari moja ambayo, pengine unaijua sana, lakini tuiangalie kwa jicho lingine la ndani zaidi na naamini tutajifunza kitu kipya..

Na habari yenyewe ni ile ya Yesu akiwa bado kijana mdogo, alipokwenda na wazazi wake Yerusalemu kuila pasaka ya kila mwaka.. Lakini kama tunavyoijua habari baada ya sikukuu kuisha, ulipofika wakati wa kila mtu kurudi nyumbani kwake na katika taifa lake, wale waliotokea katika mikoa ya karibu kule Israeli walianza safari ya kurudi makwao, na wale waliotokea mataifa mengine ya mbali nao pia walianza kurejea makwao..

Lakini mambo yalikuwa tofauti kwa Bwana Yesu, yeye alibaki nyuma, wala hakuambata na makutano kurudi makwao, kama watu wengine walivyofanya, na kibaya zaidi hata wazazi wake hawakulijua hilo, wao wakakisia tu labda atakuwa katikati ya makutano wakirejea naye nyumbani…(Hilo ndio kosa linalofanywa na watoto wengi wa Mungu)

Luka 2:44 “Nao wakadhani ya kuwa yumo katika msafara; wakaenenda mwendo wa kutwa, wakawa wakimtafuta katika jamaa zao na wenzao;

45 na walipomkosa, wakarejea Yerusalemu, huku wakimtafuta.

46 Ikawa baada ya siku tatu wakamwona hekaluni, ameketi katikati ya waalimu, akiwasikiliza na kuwauliza maswali.

47 Nao wote waliomsikia walistaajabia fahamu zake na majibu yake.

48 Na walipomwona walishangaa, na mama yake akamwambia, Mwanangu, mbona umetutenda hivi? Tazama, baba yako na mimi tulikuwa tukikutafuta kwa huzuni.

49 Akawaambia, Kwani kunitafuta? Hamkujua ya kuwa imenipasa kuwamo katika nyumba ya Baba yangu”?

Kama tunavyoona hapo, ni wazazi wake tu pake yao, ndio waliokuwa walau wanamfikiria  Yesu katikati ya ndugu zao wengi walioambatana nao, na walipoona Kristo hayupo katikati ya makutano, katikati ya wingi wa watu, katikati ya ndugu, katikati ya marafiki, katikati ya majirani, katikati ya wageni wa mataifa mengine, ndipo ikiwapasa wageuke wajaribu kwenda kuanza kumtafutia kule walipompotezea Yerusalemu.. ndipo wakamkuta yupo hekaluni katikati ya WAALIMU..

Na ni kama bahati tu walipita hekaluni, lakini kama wasingeingia kule, kamwe wasingemwona daima, wangehangaika Yerusalemu nzima wasingempata kwa muda mrefu sana..

NI KIPI MUNGU ANATAKA TUJIFUNZE?

Wakristo wachache wa leo hawajui kuwa, wapo katikati ya kundi kubwa la wakristo vuguvugu, linaloondoka mbali na mafundisho ya kweli ya Neno la Mungu.. na ndio maana wanapojaribu kumtafuta Kristo katikati yao ni kama vile hawamuoni, lakini wao bado wanataka kuendelea kutembea nao tu, hawajui kuwa kwa jinsi wanavyozidi kukaa nao ndivyo wanavyozidi kumpoteza YESU wasimpate kabisa..

Ndugu geuka kama ni wewe,..angalia ulipotoka, kule mlipotoka ndipo Kristo yupo,..Na! ulipotoka ni wapi?? Ni katikati ya waalimu, kule Kristo alipo, na waalimu makao yao huwa ni wapi?..Makao yao ni darasani sikuzote, wakiwafundisha wanafunzi, na hapo ndipo makao ya Kristo yalipo siku zote..

Hutampata sehemu nyingine yoyote, hutampata, kwenye michezo, maombezi, hutampata kwenye matamasha, hutampata kwenye taasisi za kidini, wala hutampata kwenye dhehebu lolote, wala katikati ya ndugu zako, au rafiki zao, au majirani zako, huko kote utapotea, Kristo hatembei katikati ya misafara ya watu wanaosafiri mbali na yeye bali Kristo utamwona PALE NENO LAKE LINAPOFUNDISHWA BASI..

Ukiona hupendi tena kujifunza Neno la Mungu basi ujue, upo mbali sana na Kristo kwa mujibu wa biblia, ukiona huna muda wa kusoma biblia, usijidanganye utakaa umwone Kristo akijifunua kwako, ukiendelea kudhani Kristo yupo katika msafara unaouona leo hii, wimbi la watu wengi wanaosema tumeokoka, lakini Neno la Mungu hawalifuati, ni wavivu katika kutamani kumjua Mungu, ukiwauliza habari ya unyakuo kwao ni kama habari mpya za kuchosha, ukiwauliza, habari za kwenda mbinguni kwao ni kama hadithi za kizee, muda wote ni kujionyesha tu, na kujisifia wameokoka, lakini biblia ni kama kitabu cha ziada tu kwao basi ujue wamempoteza Kristo katikati yao..

Bwana atusaidie nyakati hizi za hatari tusimpoteze yeye aliye mwamba wa wokovu wetu..

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

NI NANI ALIYEWALOGA?

NI NANI ALIYEWAONYA KUIKIMBIA HASIRA ITAKAYOKUJA?

https://wingulamashahidi.org/mafundisho-ya-ndoa/

JE YESU ATARUDI TENA?

Biblia inamaana gani kusema;aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Kwanini yule mtu afe kwa kuliwa na simba?

Katika 1Wafalme 20:35-37, Kwanini yule mtu afe kwa kuliwa na simba baada ya kukataa kumpiga yule nabii?..je Mungu anaruhusu watu kupigana?

JIBU:Tusome

1Wafalme 20:35-37 “Basi, mtu mmoja wa wana wa manabii akamwambia mwenzake kwa neno la Bwana, Nipige, nakusihi. Akakataa yule kumpiga.

36 Akamwambia, Kwa sababu hukuisikiliza sauti ya Bwana, angalia, mara ukitoka kwangu simba atakuua. Na mara alipotoka kwake, simba alimwona, akamwua.

37 Ndipo akaona mtu mwingine, akasema, Nipige, nakusihi. Yule mtu akampiga, hata kumpiga na kumtia jeraha”

Kuna wakati Mungu anatumia ishara za mwilini kuzungumza na watu wake au kufikisha ujumbe mahali..Kwamfano utaona Nabii Hosea aliambiwa aoe mwanamke wa kizinzi,

Hosea 1:2 “Hapo kwanza Bwana aliponena kwa kinywa cha Hosea, Bwana alimwambia Hosea, Enenda ukatwae mke wa uzinzi, na watoto wa uzinzi; kwa maana nchi hii inafanya uzinzi mwingi, kwa kumwacha Bwana”.

Lengo la Mungu kumwambia Hosea akaoe mwanamke wa kizinzi sio kuhalalisha uzinzi kwa watu wake, hapana bali ni kuwaonyesha watu wake jinsi na wao wanavyofanya uzinzi mbele zake kinyume chake katika roho…Hosea hakuwa mzinzi lakini aliambiwa akamwoe mwanamke mzinifu, ambaye ni kahaba mwenye wanaume wengi, ambaye hatulii. Sasa nafasi ya Hosea ambaye hakuwa mzinifu ilimwakilisha Mungu na huyo mwanamke wa kizinzi ililiwakilisha taifa la Israeli, kwa jinsi yule mwanamke alivyokuwa ni kahaba baada hata ya kuolewa na Hosea ndivyo Taifa la Israeli lilivyofanya uzinzi katika roho na kumwacha Mungu wao ambaye ndiye mume wao kama Isaya 55:5 inavyosema “Kwa sababu Muumba wako ni MUME WAKO; Bwana wa majeshi ndilo jina lake; na Mtakatifu wa Israeli ndiye Mkombozi wako; Yeye ataitwa Mungu wa dunia yote”

Sasa endapo Nabii Hosea angekataa maagizo yale Mungu aliyompa ya kwenda kumwoa mwanamke kahaba…na kusema hapana Bwana mimi sitaki kumuoa mwanamke yule ambaye ni mzinzi na kahaba hata nikimuoa bado ataendelea kuwapenda hao mabwana wake…Ni Dhahiri kuwa Hosea angetenda dhambi kwasababu amekataa shauri la Bwana la yeye kufanyika ishara kwa Israeli. Na hivyo angewafanya Israeli wasitubu, lakini ishara ile iliwafanya Israeli wengi watubu..Kwasababu walipokwenda kumuuliza wewe Nabii wa Mungu mbona unaoa mwanamke ambaye anamabwana wengi na zaidi ya yote tunamwona mkeo huyo yupo na mabwana wengine, unajisikiaje kwa hilo?..Ndipo Hosea atawajibu ni mfano wa nyinyi mlivyomwacha Mungu wenu ambaye ni mume wenu na kuigeukia miungu mingine kuiabudu..Hivyo mrudieni Mungu wenu ambaye ni Mume wenu kwasababu amewakasirikia sana.

Halikadhalika kuna wakati Mungu alimwambia nabii mwingine amwambie mwenzake kwamba ampige mpaka apate majeraha…ili kwa kupitia yale majeraha aonekane kama alikuwa katika vita vikali na aende kwa mfalme wa Israeli akiwa na yale majeraha…Ili mfalme adanganyike na kuamini kuwa ni kweli alikuwa kwenye mapambano kwasababu ana majeraha..na ndipo ampe fumbo ambalo litamtega…Na kweli mfalme alipomwona mtu anakuja mwenye majeraha akasema bila shaka mtu huyu atakuwa ametoka vitani kwa majeraha yale..na alipopewa lile fumbo na yule nabii kumbe lilikuwa linamhusu mfalme mwenyewe..kwasababu alimwacha huru Benhadadi ambaye alipaswa kumuua kabisa..

Hivyo akaambiwa sehemu yake ataichukua yeye. Unaweza kuisoma vizuri habari hiyo katika 1Wafalme 20:35-43.

Lakini yule mtu alikataa maagizo yale ya Mungu..ingawa aliambiwa ni maagizo kutoka kwa Mungu lakini akakataa kumpiga..hakujua kuwa kwa kukataa kule kungemfanya mfalme wa Israeli asiyaamini maneno yale ya Mungu…Na ikasababisha dhambi kwake, na ndio mbeleni akaenda kuliwa na simba..lakini yule mwingine hakulichukulia lile jambo la kumpiga nabii wa Mungu kwamba ni jambo la kumuumiza..bali aliona mbele kwamba kwa ishara ile ya majeraha ya yule nabii, mfalme ataamini ujumbe kutoka kwa yule nabii sawasawa na Neno la Mungu na hivyo atakuwa ameyatenda mapenzi ya Mungu Zaidi.

Hivyo ni jambo la kawaida kabisa Mungu kuzungumza kwa ishara za mwili, alifanya hivyo kwa Hosea, Kwa Ezekieli, na kwa manabii wengine wengi.

Bwana atubariki

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

YEZEBELI ALIKUWA NANI

Kuna haja gani ya kumwamini Yesu aliyezaliwa kama sisi?

MAMBO MANNE,YANAYODHOOFISHA UOMBAJI WAKO.

KWANINI YESU KRISTO NI WA MUHIMU KWETU SASA?

MKARIBIE BWANA ZAIDI ILI UFANYIKE NGUZO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

JE WEWE NI LAZARO YUPI, WA KWANZA AU WA PILI?

Shalom jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe.

Kuna wakati Bwana Yesu aliwaambia mitume wake maneno haya..

Yohana 12:24 “ Amin, amin, nawaambia, Chembe ya ngano isipoanguka katika nchi, ikafa, hukaa hali iyo hiyo peke yake; bali ikifa, hutoa mazao mengi..”

Aliwaambia maneno haya, kwanza kutokana na wanafunzi wake kuona wingi wa watu waliokuwa wanamfuata ili waokolewe hususani wale waliotoka mpaka nchi za mbali kuja kumuona na pia alisema vile ili kuwafundisha wanafunzi wake, akijerea tendo, alilolifanya muda mfupi, au siku chache zilizopita,..

Na tendo lenyewe halikuwa lingine Zaidi ya lile la Lazaro..

Kama wengi wetu tunavyofahamu Lazaro alikuwa ni mtu aliyependwa na Yesu sana, alikuwa ni Rafiki wa Yesu tangu zamani, Lakini siku moja aliumwa sana, na taarifa zikamfikia Yesu, Lakini Yesu hakuchukua hatua yoyote, badala yake aliendelea kubaki kule kule mahali alipokuwepo, akamwacha aendelee kuugua mpaka afe,..

Na alipojua ameshakufa, bado hakufanya haraka kurudi siku hiyo hiyo kumuona, bali alingojea tena siku mbili, ndipo baadaye akashuka kwenda Bethania alipokuwa anaishi yeye na Dada zake..Kama tunavyosoma habari alipofika alimkuta ameshawekwa kaburini, anatoa harufu,.(Yohana 11 )

Unaweza ukajiuliza ni kwanini alimwacha mpaka aoze, ni kwasababu baadaye alikuwa anataka kuwafundisha wanafunzi wake kinadharia juu ya huo mstari tuliouona hapo juu, na madhara yake jinsi yatakavyokuwa..

Sasa Bwana Yesu alipofika na kumfufua Lazaro tena, na kumrudisha katika hali yake ya mwanzo tena katika afya Zaidi ya ile aliyokuwa nayo hapo mwanzo, biblia inatuonyesha tendo lile la kufufuka tu kwa Lazaro, lilikuwa ni tendo lililoutikisa ulimwengu wa giza… Yaani kwa ufupi ushuhuda ule wa Lazaro, uliwavuta watu wengi sana kwa Kristo, mpaka kufikia hatua ya wakuu wa Makuhani kutaka kumuua yeye naye (yaani Lazaro)…

Yohana 12:9 “Basi watu wengi katika Wayahudi walipata kujua ya kuwa yeye yuko huko, nao wakaja, si kwa ajili yake Yesu tu, ila wamwone na Lazaro, ambaye Yesu alimfufua katika wafu.

10 Nao wakuu wa makuhani wakafanya shauri la kumwua Lazaro naye;

11 maana kwa ajili yake wengi katika Wayahudi walijitenga, wakamwamini Yesu”.

Hiyo ni kuonyesha kuwa jinsi gani Lazaro aliyekufa akazikwa akaoza alivyokuwa na athari kubwa katika ulimwengu wa roho, kuliko yule ambaye hakuwahi kupitia hayo.

Jiulize hapo kwanza kwanini Lazaro, hakuwa vile?..Kwanini hakukuwa na mtu aliyemfuatilia, kwanini hakumvuta mtu yeyote kwa Kristo, japokuwa alikuwa ni Rafiki wa Karibu wa Bwana Yesu, tena aliyependwa.

Hata sasa haijalishi mtu anaweza akawa anasema Kristo ni Rafiki yangu kiasi gani, anaweza akawa anakujua kweli kama Lazaro wa kwanza.. lakini hakujui kama Lazaro ambaye alikufa akaoza akazikwa, kisha akafufua tena..

Na ndio maana sasa Bwana Yesu akawaambia wanafunzi wake baada ya tukio lile kipindi kifupi baadaye..

Yohana 12:24 “Amin, amin, nawaambia, Chembe ya ngano isipoanguka katika nchi, ikafa, hukaa hali iyo hiyo peke yake; bali ikifa, hutoa mazao mengi..”

Ndipo mstari huo ulipokuwa chimbuko lake..Akiurejea mfano wa Lazaro..

Ikiwa wewe ulishaokoka lakini hutaki kuwa tayari kufa, na kuoza kwa habari ya dhambi, hata wakati mwingine kuonekana kuwa ni mjinga, au umerukwa na akili kwasababu tu hutaki kufanya jambo Fulani kwa ajili tu ya Kristo, basi huwezi kuwa Lazaro wa pili.Wala huwezi kudai kuwa umezaliwa mara ya pili.. Ikiwa utakuwa unaogopa kuacha kuvaa vimini kisa tu ndugu zako au marafiki zako watakuonaje, watakuita wewe ni mshamba, basi bado huwezi kumletea Kristo mazao yoyote, haijalishi utasema umedumu katika wokovu muda gani..wapo waliodumu na Kristo Zaidi ya sisi mfano Yuda, lakini hakuwa na mazao yoyote kwa Bwana, na mwingine huyu Lazaro ambaye alipendwa pia lakini hakuwa na matunda yoyote kwa Bwana, kwasababu walikuwa bado hawajafa kwa habari ya dhambi.

Ikiwa utaogopa, kuacha Maisha ya uzinzi kisa unawaonea haya hao waasherati wenzako ulionao, na marafiki zako, unaogopa watakuita mlokole, na wewe hutaki kuitwa hivyo, basi ujue mpaka hapo bado hujafa ukaoza ukafufuliwa na Kristo na hautakuwa na matunda yoyote yakumfaa Kristo. Ndugu habari hizi unazisikia kila kukicha lakini bado unafanya moyo wako kuwa mgumu, unazidi kujitoa katika mstari wa neema kidogo kidogo…

Ikiwa kweli tunatamani tuwe na matunda ya rohoni, basi tuwe radhi pia kuiacha dunia moja kwa moja, hiyo ndio kanuni ya Kristo wala hakuna njia nyingine ya mkato.

Kumbuka tena hili Neno

“Amin, amin, nawaambia, Chembe ya ngano isipoanguka katika nchi, ikafa, hukaa hali iyo hiyo peke yake; bali ikifa, hutoa mazao mengi..””

Bwana atusaidie sote,

Ubarikiwe sana..

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

Kati ya Unyakuo,dhiki kuu, utawala wa miaka 1000 kipi kinaanza

Mstari huu unamaana gani? ″Walakini hautapotea hata Unywele mmoja wa Vichwa vyenu? (Luka21:18)

Ni kwa namna gani Yesu amewekwa kwa kuanguka na kuinuka?

MKARIBIE BWANA ZAIDI ILI UFANYIKE NGUZO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Ni wakati upi ambao vita vilipiganwa na shetani kutupwa chini?

SWALI: Katika Luka 10:18, tunasoma Bwana Yesu alimwona shetani akianguka kutoka mbinguni kama umeme..na katika Ufunuo 12:7-9 Biblia inasema kulikuwa na vita mbinguni na shetani akatupwa chini..Sasa ni wakati gani ambao shetani alitupwa chini? Kabla ya dunia kuumbwa au wakati wa Bwana Yesu akiwa duniani. Na je shetani sasa yupo kifungoni?.


JIBU: Katika Luka 10 tukianzia juu kidogo mstari wa 17 unasema…

“Ndipo wale sabini waliporudi kwa furaha, wakisema, Bwana, hata pepo wanatutii kwa jina lako.18 Akawaambia, Nilimwona Shetani, akianguka kutoka mbinguni kama umeme.”

Hivyo mstari huu hauzungumzii vita vilivyokuwa vinaendelea mbinguni kabla ya dunia kuumbwa..ambapo shetani alitaka kujiinua na kutaka kuwa kama Mungu, na hatimaye akafukuzwa mbinguni na kutupwa chini duniani..Bali unazungumzia habari za shetani kutoka katika nafasi ya juu aliyonayo juu ya watu wa Mungu na kushushwa chini..Ndio maana Bwana Yesu alizungumza maneno yale mara tu baada ya wanafunzi wake kutoka huko na huko kuhubiri injili na kutoa pepo wengi…Sasa kitendo hicho cha kwenda kufungua watu, na mateka kuwaacha huru, wale waliofungwa na nguvu za giza za shetani na mapepo yake hilo ndilo anguko la shetani kutoka juu mpaka chini, ambalo Bwana alikuwa analizungumzia hapo.

Hali kadhalika tukio tunalolisoma katika Ufunuo 12:7-9..Ndilo tukio la vita vilivyotokea mbinguni kabla ya dunia kuumbwa ambapo shetani alijiharibia nafasi aliyokuwepo ikasababishia kutupwa chini duniani.

Ufunuo 12:7 “Kulikuwa na vita mbinguni; Mikaeli na malaika zake wakapigana na yule joka, yule joka naye akapigana nao pamoja na malaika zake;
8 nao hawakushinda, wala mahali pao hapakuonekana tena mbinguni.
9 Yule joka akatupwa, yule mkubwa, nyoka wa zamani, aitwaye Ibilisi na Shetani, audanganyaye ulimwengu wote; akatupwa hata nchi, na malaika zake wakatupwa pamoja naye”.

Hivyo maanguko ya shetani yapo mawili…Lile la kwanza ambalo lilitokea kabla ya sisi wanadamu kuumbwa, ambalo lilimfanya asiwe na uwezo tena wa kurudi mbinguni. Na anguko la pili ni la hapa duniani ambalo tangu wakati wa Bwana Yesu mpaka sasa linaendelea… na litakamilika katika mwisho wa dunia ambapo wale wote waliokuwa wamekusudiwa uzima wa milele watakapomalizika kuingia ndani na mlango wa Neema kufungwa (Hiyo ndiyo siku ambayo shetani ataanguka kikabisa kabisa)..

Siku hiyo ni siku ambayo shetani hatakuwa na chembe hata moja ya ngano mkononi mwake, atakuwa na makapi tu ambayo yatakwenda kuteketezwa kwa moto(Mathayo 3:12). Siku hiyo ndio atakuwa ameshindwa mbinguni na duniani.

Hivyo hata wakati huu tunapokwenda kuhubiri injili,kutoa pepo, kufungua watu, kuwafariji, kuwajenga kiimani na kuwatoa sehemu moja hadi nyingine, kama Mitume hawa walivyofanya…katika ulimwengu wa roho ni tunamnyang’anya shetani mateka kwa kasi sana na hivyo tunakuwa tunamwangusha katika ile nafasi aliyonayo ya juu na kumshusha chini..kwasababu nguvu ya shetani ipo katika idadi ya watu wa Mungu anaowateka sasa..

Hivyo ni muhimu sana kuhubiri injili kwa watu wote..

Sasa utahubirije injili?..Kwa maisha yako utahubiri injili, kwa uvaaji wako utahubiri, kwa mwenendo wako, kwa uimbaji wako, kwa maombi yako na kwa mchango wako wowote ule wa kifedha katika kazi ya injili utakuwa umeihubiri injili.

Na shetani hajafungwa sasa, bado yupo anafanya kazi atakuja kufungwa miaka 1000 baada ya mwisho wa dunia.

Bwana akubariki.

Maran atha

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

Neno I.N.R.I kwenye msalaba wa Yesu maana yake ni nini?

Roho Mtakatifu ni nani?.

NILIMWONA SHETANI, AKIANGUKA KUTOKA MBINGUNI.

Je kupiga miayo ni ishara ya mapepo?

Je ni wakina nani ambao hawataonja mauti mpaka siku ya kuja Bwana?

Je! Shetani alitolea wapi uovu?

Rudi Nyumbani:

Print this post

ANGALIA UZURI WAKO, USIGEUKE KUWA KITANZI CHAKO.

Shalom, Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe daima..

Karibu tuzidi kujifunza maneno matakatifu ya Mungu, Na leo tutaona kwa ufupi habari ya mtu mmoja anayeitwa Absalomu mwana wa Daudi naamini lipo jambo utajifunza ndani yake..

Huyu Absalomu alikuwa ni mmojawapo wa wana wengi wa Daudi, isipokuwa yeye alikuwa anabeba kitu kingine cha ziada ambacho kilikuwa kinamtofautisha na wana wote wa Daudi waliokuwa katika enzi yake ya kifalme.

Biblia inatueleza Absalomu, alikuwa ni kijana mzuri sana (kwa lugha ya kiingereza labda tunaweza tukasema Handsome), sio tu katikati ya ndugu zake, bali pia katika Israeli nzima ndivyo walivyomwona, hakukuwa na kijana aliyekuwa mzuri kama yeye, kuanzia utosi wa kichwa chake, mpaka uwayo wa miguu yake, wanasema hakuna mwanadamu asiye na mapungufu, lakini huyu Absalomu yeye hakuwa na upungufu wowote katika mwili wake. Kila kiungo chake cha mwili kilionekana kizuri na cha kuvutia, na alisifiwa na kila mtu..

Na Zaidi ya yote, biblia imezitaja hizo nywele zake, inasema, alikuwa na nywele nzuri nzito, ambazo alikuwa hawezi kuziacha Zaidi ya mwaka mmoja bila kuzinyoa vinginevyo vitamlemea sana, embu tusome kidogo..

2Samweli 14:25 “Basi katika Israeli wote hapakuwa na mtu hata mmoja mwenye kusifiwa kwa uzuri wake kama huyo Absalomu; tangu nyayo za miguu yake hata utosi wa kichwa chake hapakuwa na ila kwake.

26 Naye aliponyoa kichwa, (basi mwisho wa kila mwaka hunyoa; na kwa sababu nywele zilikuwa nzito kwake, kwa hiyo akanyoa;) hupima nywele za kichwa chake shekeli mia mbili kwa uzani wa mfalme.”

Unaona, ukisoma hapo utaona nywele hizo alikuwa akishazinyoa zilikuwa zinakwenda kupimwa kwenye uzani wa mfalme, na inapatikana shekeli mia mbili ambayo ukiigeuza kwa vipimo vya kisasa ni Zaidi ya kilogramu 2.. Unaweza kutengeneza picha uzito wa kilo mbili ulikuwa unamlemea kichwani pake kama asipokata nywele zake baada ya mwaka mmoja..

Ili kuelewa vizuri, wanasema mtu wa kawaida ambaye amebahatika kuwa na nywele nyingi na zinazokuwa, akaziacha mwaka mzima, ili uzito wake uweze kufikia ule wa nywele za Absalomu kwa mwaka, basi itahitaji wachukuliwe watu kama yeye thelathini (30) kwa mwaka, kisha zichanganywe ndipo zitafikia uzito wa nywele za Absalomu ndani ya mwaka mmoja..

Hivyo unaweza kuona jinsi gani mtu huyu alipewa umbile la kipekee sana, na uzuri wa tofauti, nywele zenye utofauti sana lakini tunaposoma biblia tukumbuke kuwa siku zote biblia inapotaja umbile Fulani la mtu, basi tujue kuwa lina sehemu Fulani ya kusimamia katika habari husikia mbeleni,.. Hivyo kutajwa kwa sifa za nywele za Absalomu, ni wazi kuna mahali litatumika huko mbeleni..

Hivyo ukipata muda wako binafsi wa utulivu unaweza kuzisoma habari zake, kwa urefu na jinsi alivyokuwa, (2Samweli 13-18 )lakini kwa ufupi ni kuwa Absalomu, Japokuwa alikuwa na uzuri na umbile la kipekee na maneno ya kuvutia ambayo yaliweza kuifanya Israeli yote wampende mpaka kutaka kumfanya awe mfalme, lakini moyo wake ulikuwa ni tofauti na watu walivyokuwa wanamdhania..

Kwanza alikuwa na lengo la kuudondosha ufalme wa baba yake Daudi kinyume chake ili yeye atawale na Zaidi ya yote alikuwa anamtafuta baba yake ili amuue, pili alikuwa radhi hata kulala na Masuria 10 wa baba yake ili kuwaonyesha watu kuwa hampendi, japokuwa baba yake hakuwahi kumfanyia ubaya wowote..Na tatu alikuwa radhi kumuua ndugu yake, ambaye alilala na Dada yake, wala hakumsamehe..

Kwahiyo Absalomu, alikuwa ni mwovu, wala hakuwa mtu mwema, licha ya kuwa alikuwa ni mzuri na mwenye ushawishi wa maneno kwa watu.

Sasa ukizidi kusoma habari utaona alipokusudia kumwangamiza baba yake(Daudi), baada ya kumfukuza kwenye kiti cha enzi, aliondoka kwenda msituni yeye pamoja na jeshi kubwa la Israeli nyuma yake..Biblia inatuambia vita ilikuwa vikali sana katika msitu ule mkubwa sana.. Na unajua jinsi misitu ilivyo, vichaka vizito na miti ya Kamba Kamba za miiba inakuwa ni mingi sana, na inakuwa ni rahisi mtu kunaswa katika vichaka hivyo kama hutakuwa mwepesi..

Sasa kutokana na msitu ule kuwa mzito sana, biblia inasema watu waliokufa kwa uzito wa msitu ule, walikuwa ni wengi kuliko waliokufa kwa upanga.. Na huko huko lipo jambo ambalo Absalomu naye alikutana nalo embu tusome kwa ufupi..

2Samweli 18:6 “Hivyo watu wakatoka waende nyikani ili kupigana na Israeli; na vita vikatokea ndani ya msitu wa Efraimu.

7 Watu wa Israeli wakapigwa huko mbele ya watumishi wa Daudi, kukawa na maangamizo makuu huko siku ile, ya watu ishirini elfu.

8 Kwa maana vita vilienea huko juu ya uso wote wa nchi; na siku ile huo msitu ukala watu wengi kuliko wale walioliwa na upanga.

9 NA KWA BAHATI ABSALOMU AKAKUTANA NA WATUMISHI WA DAUDI. NAYE ABSALOMU ALIKUWA AMEPANDA NYUMBU WAKE, NA YULE NYUMBU AKAPITA CHINI YA MATAWI MANENE YA MWALONI MKUBWA, HATA KICHWA CHAKE KIKAKWAMA KATIKA MWALONI HUO, AKANYAKULIWA JUU KATI YA MBINGU NA NCHI; NA YULE NYUMBU ALIYEKUWA CHINI YAKE AKAENDA MBELE.

10 Basi mtu mmoja akaona hayo, akaenda akamwambia Yoabu, akasema, tazama, mimi nalimwona Absalomu ametundikwa katika mwaloni.

11 Naye Yoabu akamwambia mtu yule aliyempasha habari, Je! Wewe umeona haya; Mbona, basi, hukumpiga hata nchi papo hapo? Nami ningalikupa fedha kumi na mshipi.

12 Yule mtu akamwambia Yoabu, Kama ningalipata fedha elfu mkononi mwangu, hata hivyo singalinyosha mkono wangu juu ya mwana wa mfalme; kwa maana mfalme masikioni mwetu alikuagiza wewe, na Abishai na Itai, akisema, Angalieni sana mtu awaye yote asimguse yule kijana, Absalomu.

13 Na tena, kama ningaliitendea roho yake kwa hila; (wala hapana neno lo lote liwezalo kufichwa mbele ya mfalme); ndipo wewe mwenyewe ungalijitenga.

14 Ndipo Yoabu akasema, Siwezi kungoja na kusema nawe hivi. Akachukua vyemba vitatu mkononi mwake, akamchoma Absalomu moyoni, alipokuwa akali hai katikati ya ule mwaloni.

15 Kisha vijana kumi, waliomchukulia Yoabu silaha zake wakamzunguka, wakampiga Absalomu, na kumwua.

Utaona, hapo Absalomu, alipopita sehemu moja, biblia inasema kichwa chake kikakwama, kwenye mti mmojawapo, na yule farasi aliyekuwa chini yake akazidi kuendelea mbele, hivyo yeye akabakia pale pale amening’inia. Sasa, biblia inaposema kichwa inamaanisha eneo la nywele kwa ujumla wake, Ni kwamba zile nywele nyingi za Absalomu zilikwama kwenye vijiti vya miti, zikajisongorotesha pale, kwa namna ambayo asingeweza kuzifumua, akabakia tu anani’ngia nia tu pale kwa maumivu.. alikaa pale muda mrefu akijaribu lakini alishindwa kutoka mpaka mauti ilipomfika kwasababu ule uzuri wake ndio ulikuwa kitanzi chake..

Ndugu, hata sasa, watu wengi hawajui kuwa kile kinachowafanya wavutie, au wapendwe ndani yao ndio kitakuwa kitanzi chao baadaye ikiwa hawatasimama katika mstari wa wokovu.. Ikiwa ni mali zako zinakupa kiburi kumbuka yale maneno ya Bwana, Ni rahisi kwa ngamia kupenya katika tundu la sindano… Ikiwa ni urembo wako wewe binti, unajiona sasa huna haja ya Mungu bado wewe unavutia, una umbile zuri, kila mwanaume akikuangalia anakutamani, wakati utafika huo huo uzuri wako utakuwa kitanzi kwako, utanasa mahali ambapo hutatoka, na adui yako shetani atakumaliza kirahisi mbele ya macho yako ukiona kama ilivyokuwa kwa Absalomu, na ukajikuta katika lile ziwa la moto,..Vivyo hivyo na mambo mengine yote.

Huu ni wakati sasa wa kumtazama Kristo, na kuomba rehema kwake, kama na wewe umedanganywa na mojawapo ya hayo mambo, uzuri wako na utanashati wako. Tubu umgeukie Mungu, ili Mungu akurehemu na kukupa uzima wa milele. Nyosha njia yako kwa kuliamini na kulitii Neno la Mungu.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

UCHAWI WA BALAAMU.

USIPOWATAMBUA YANE NA YAMBRE, KATIKA KANISA LA KRISTO, UJUE UMEPOTEA.

USIPOWATAMBUA YANE NA YAMBRE, KATIKA KANISA LA KRISTO, UJUE UMEPOTEA.

KUTAKUWA NA MATETEMEKO YA NCHI, NJAA NA TAUNI.

 

NIMEOKOKA, ILA MUNGU NDIYE ANAYEJUA NITAKWENDA WAPI.

KWANINI YESU KRISTO NI WA MUHIMU KWETU SASA?

 

Rudi Nyumbani:

Print this post

Je! Bwana Yesu alibatiza akiwa hapa duniani?

Je! ni kweli Bwana Yesu alibatiza mtu akiwa hapa duniani?


JIBU: Bwana Yesu yeye mwenyewe hakubatiza bali wanafunzi wake ndio waliobatiza kwa agizo lake yeye. Hata leo mkuu wa nchi akitoa agizo la ujenzi wa jengo Fulani la serikali…Jengo lile litakapojengwa na kumalizika..jengo hilo litajulikana kama limejengwa na Mkuu huyo…lakini kiuhalisia sio yeye aliyelijenga waliolijenga ni wale vibarua na wafanyakazi wake…lakini kwasababu ni mkuu ndio katoa hiyo amri na fedha basi ni sahihi kabisa kusema ni Mkuu huyo ndiye kajenga jengo lile.

Kadhalika kuna mahali kwenye biblia paliposema Bwana Yesu alibatiza…lakini ukiendelea mbele kidogo utaona biblia imefafanua zaidi waliobatiza ni wakina nani…kwamba ni wanafunzi wake kwa amri yake na sio Bwana Yesu mwenyewe.

Tusome.

Yohana 4:1 “Kwa hiyo Bwana, alipofahamu ya kuwa Mafarisayo wamesikia ya kwamba, Yesu anafanya wanafunzi wengi kuliko Yohana, na kuwabatiza,

2 (lakini Yesu mwenyewe hakubatiza, bali wanafunzi wake,)

3 aliacha Uyahudi, akaenda zake tena mpaka Galilaya”.

Unaona hapo mstari wa pili unafafanua zaidi kwamba siye Bwana Yesu aliyebatiza bali ni wanafunzi wake.

Pamoja na hayo yote Jambo lingine la msingi hapo la kujifunza ni kwamba watu walianza kubatizwa kabla hata ya Bwana Yesu kusulubiwa, kufa na kufufuka ..kuonyesha ni jingi gani ubatizo ulivyokuwa wa muhimu…Ni agizo la awali kabisa pale mtu anapomwamini Yesu na kutubu dhambi zake.

Hivyo nasi tunajifunza kama hatujazingatia kwenda kubatizwa ubatizo sahihi tukidhani sio agizo la msingi, hapa tunaonyeshwa watu walianza kubatizwa kabla ya Kristo kwenda Golgotha, ..kuashiria umuhimu wa hicho kitu, na kumbuka pia ubatizo hautekelezwi kama mtu anavyoamua kwamba unaweza kuzamishwa kichwa tu kwenye maji na ukawa tayari umeshabatizwa, au unaweza kutumia mchanga badala ya maji, au unaweza kunyunyiziwa tu badala ya kuzama mwili mzima…hakuna njia mbadala ya ubatizo..Neno ubatizo maana yake ni KUZAMISHWA. Na kuzama maana yake ni kuzama hakuna maana nyingine ya neno hilo. Hivyo tunazamishwa katika maji mengi (kama Yohana 3:23 inavyosema), na kwa Jina la Bwana Yesu Kristo kama (Matendo 2:38,8:16, 10:48, 19:5 inavyosema).

Tuyazingatie hayo na Bwana atatukubali na kutubariki.

Shalom.

Muhtasari wa maelezo haya kwa njia ya video unaweza kuyapata hapa chini.

[embedyt] https://www.youtube.com/watch?v=68fHuz_icug[/embedyt]. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

MIILI YA UTUKUFU ITAKUWAJE?

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

LIVUNJENI HEKALU HILI, NAMI KATIKA SIKU TATU NITALISIMAMISHA.

MWACHE YESU, NDIO AWE WA  KWANZA KUKUHURUMIA.

LOLOTE ATAKALOWAAMBIA FANYENI.

RABI, UNAKAA WAPI?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Ni kwa namna gani Yesu amewekwa kwa kuanguka na kuinuka?

SWALI: mstari huu una maana gani? Luka 2:34 “Simeoni akawabariki, akamwambia Mariamu mama yake, Tazama, huyu amewekwa kwa kuanguka na kuinuka wengi walio katika Israeli, na kuwa ishara itakayonenewa”?


JIBU: Kwa faida yetu wote, ni vizuri tukaanzia mistari ya juu ili tupate ufahamu wa habari yote hiyo inamuhusu nani..

Luka 2:25 “Na tazama, pale Yerusalemu palikuwa na mtu, jina lake Simeoni, naye ni mtu mwenye haki, mcha Mungu, akiitarajia faraja ya Israeli; na Roho Mtakatifu alikuwa juu yake.

26 Naye alikuwa ameonywa na Roho Mtakatifu ya kwamba hataona mauti kabla ya kumwona Kristo wa Bwana.

27 Basi akaja hekaluni ameongozwa na Roho; na wale wazazi walipomleta mtoto Yesu ndani, ili wamfanyie kama ilivyokuwa desturi ya sheria,

28 yeye mwenyewe alimpokea mikononi mwake, akamshukuru Mungu, akisema,

29 Sasa, Bwana, wamruhusu mtumishi wako, Kwa amani, kama ulivyosema;

30 Kwa kuwa macho yangu yameuona wokovu wako,

31 Uliouweka tayari machoni pa watu wote;

32 Nuru ya kuwa mwangaza wa Mataifa, Na kuwa utukufu wa watu wako Israeli.

33 Na babaye na mamaye walikuwa wakiyastaajabia hayo yaliyonenwa juu yake.

34 Simeoni akawabariki, akamwambia Mariamu mama yake, TAZAMA, HUYU AMEWEKWA KWA KUANGUKA NA KUINUKA WENGI WALIO KATIKA ISRAELI, NA KUWA ISHARA ITAKAYONENEWA.”

Ukitazama hapo, kuna vipengele vitatu, 1) kuanguka, 2)Kuinuka kwa wengi 3) na kuwa ishara itakayonenewa.

Huyo ni Bwana wetu Yesu Kristo anayezungumziwa hapo na Simeoni akitolewa unabii juu ya mambo atakayokuja kuyatekeleza huko mbeleni kwamba atawekwa kwa ajili ya kutumiza makusudi hayo matatu, yaani kuanguka na kuinuka kwa watu wengi walio katika Israeli na kuwa ishara itakayonenewa.

Tuanze kwa kutazama kwa ufupi kipengele kimoja kimoja..

  1. Kuanguka: Hii ni kazi mojawapo ambayo Kristo alikuja kuitimiza hapa duniani licha ya kuwa alikuwa ni mwokozi wa Ulimwengu aliyekuja kuokoa, lakini pia wale waliompinga na kuyakataa maneno yake, mambo yalikuwa ni tofauti badala ya kubakia kama walivyokuwa baada ya kumpinga kinyume chake ndio walianguka chini kabisa..

na unabii huo ulishatolewa tangu zamani..

Isaya 8:14 “Naye atakuwa ni mahali patakatifu; bali ni jiwe la kujikwaza na mwamba wa kujikwaa kwa nyumba za Israeli zote mbili, na mtego na tanzi kwa wenyeji wa Yerusalemu.

15 Na wengi watajikwaa juu yake, na kuanguka na kuvunjika, na kunaswa na kukamatwa”.

Jambo hilo tuliliona kwa mafarisayo, waandishi na masadukayo, na Taifa la Israeli kwa ujumla wale wote waliompinga Kristo na kumkataa, walitiwa upofu..

Yohana 9:39 “Yesu akasema, Mimi nimekuja ulimwenguni humu kwa hukumu, ili wao wasioona waone, nao wanaoona wawe vipofu.

40 Baadhi ya Mafarisayo waliokuwapo pamoja naye wakasikia hayo, wakamwambia, Je! Sisi nasi tu vipofu?”

Neema hiyo ya wokovu iliondolewa kwao, na kuletwa kwetu sisi watu wa mataifa, na kilichobakia kwao hakikuwa kingine Zaidi ya , taifa la Israeli kuja kuangamizwa na Warumi mwaka 70 WK, Ili kutimiza ule unabii Kristo aliozungumza juu yao kuhusu uharibifu wa Yerusalemu na Watoto wao (Soma Luka 19:41-44)

  1. KUINUKA KWA WENGI: Lakini kinyume chake wale waliompokea, walipewa uzima wa milele, Ikiwemo waisraeli wachache na watu wengi wa mataifa, (Ambao ni mimi na wewe). Ukisoma matendo ya Mitume utaona jinsi Mungu alivyokuwa akilizidisha kanisa kwa kasi, na watu wengi walikuwa wanamjua Mungu, na kupata uzima wa milele.
  2. KUWA ISHARA ITAKAYONENEWA: Hilo Neno “itayakayonenewa” maana yake ni itakayozungumziwa kinyume..

Ukisoma tafsiri nyingine hususani zile za kiingereza utaelewa vizuri, mstari huo unasema..” and for a sign which shall be spoken against;”(kjv).. Ishara ambayo haitapokelewa/haitakubaliwa na wengi..

Licha ya kuwa Kristo alijidhihirisha kwao kwa ishara nyingi, na miujiza mingi, akitimiza maandiko mengi yamuhusuyo masihi, lakini wayahudi wengi walimpinga, walitazamia pengine masihi wao angetokea kwenye majumba ya kifalme, lakini walipomuona amezaliwa katika familia ya kimaskini wakajikwaa kabisa.

Hata sasa, Kristo anatimiza, unabii huo, yaliyotokea wakati ule, ndio yanayotokea wakati huu, wakati wengine wanaokolewa, na kunyanyuka, na kupokea uzima wa milele, wapo wengine saa hii wanajikwaa kwa Kristo na kuanguka na kupoteza neema ya wokovu moja kwa moja…Na wanaanguka kwa jinsi gani?.. Ni Pale mtu anapoona Kristo anaokoa na kwamba yeye ndio mwokozi wa ulimwengu halafu hataki kumwamini apokee uzima wa milele, kama ilivyokuwa kwa wale mafarisayo na waandishi, kinyume chake haonyeshi kuthamini jambo hilo, au anadhihaki, basi mtu huyo Kristo anabadilika hawi tena mwokozi kwake bali anakuwa jiwe la kukwaza.. Inamaana kuwa akiendelea hivyo kuna wakati utafika Yule Roho wa Kristo wa neema anayemlilia kila siku atubu, ataondoka ndani yake, kitakachobakia kwake ni kuendelea tu kuupinga wokovu na kudhihaki watu wa Mungu mpaka siku anaondoka duniani.

Watu kama hao wapo kila mahali, utajiuliza hawamwogopi hata Mungu, kulitamka jina la YESU ovyo ovyo tu mitaani, hawaogopi kuufanyia mzaha wokovu na msalaba.

Hivyo na sisi Bwana atusaidie, tuitii injili ili iwe na manufaa kwetu ya rohoni, tusije tukaanguka kwa injili hiyo hiyo. Neno la Mungu ni upanga ukatao kuwili.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

Biblia inakataza kuapa kabisa, lakini kwanini watu wanaapa mahakamani na katika vifungo vya ndoa?

Kwanini Mungu aliikubali sadaka ya Yeftha ya kumtoa binti yake kafara?

KWANINI DAUDI ALIKUWA NI MTU ALIYEUPENDEZA MOYO WA MUNGU?

Je! Shetani alitolea wapi uovu?

Ikiwa sisi tuliumbwa na Mungu,Je! Mungu aliumbwa na nani?

JE MOYO WAKO NI MNYOFU MBELE ZA MUNGU

Rudi Nyumbani:

Print this post

IKIMBIE DHAMBI KWA GHARAMA ZOZOTE ZILE!

Ikimbie dhambi.


Shalom.

Karibu tujifunze biblia, na kujikumbusha yale ambayo tumeshajifunza. Kitu pekee ambacho watu wa Mungu tunapaswa tukiogope kuliko vyote kwa nyakati zetu hizi sasa ni dhambi…Wala hatupaswi kuogopa mapepo wala wachawi wala shetani mwenyewe. Tunachopaswa kukiogopa cha kwanza ni dhambi.

Kwasababu dhambi ndio mlango wa mambo hayo mengine yote.

Hivyo kwa nguvu zote na kwa jitihada zote tunapaswa tujiepushe na dhambi..Na tunajiepusha na dhambi kwa kuikimbia dhambi..maana yake unaiacha kwa gharama zozote zile..Roho Mtakatifu biblia inamwita MSAIDIZI, (Yohana 14:16), unaelewa maana ya msaidizi?..Msaidizi ni mtu anayekusaidia wewe kufanya jambo Fulani ambalo tayari umeshachukua hatua ya kulifanya…yeye sio mfanyaji..bali ni mwongezeaji nguvu kile ambacho umeshaanza kukifanya…

Hivyo tunapookoka na kumpokea Roho Mtakatifu ndani yetu…kazi yake sio KUTUZUIA KWA NGUVU TUSIFANYE DHAMBI!..Hapana hiyo sio kazi yake hata kidogo…Kazi yake ni kutusaidia namna ya kuishinda dhambi!..anatupa mashauri, anatupa kila sababu kwanini sasa hatupaswi kufanya jambo hili baya na tufanye hili jema..Hivyo tunapomtii mashauri yake ndani yetu ile kiu ya kufanya dhambi inakufa ghafla, ndipo hapo tunajikuta tunakaa bila kutenda dhambi. Na kwa jinsi unavyozidi kujizoeza kumtii ndani yako ndivyo zile dhambi zinazidi kufa ndani yako. Ni kawaida kitu usipokifanyia mazoezi muda mrefu unakisahau na unapoteza uzoefu wa hicho kitu (kitendo cha kupoteza uzoefu wa kile ulichokuwa unakifanya ndio kufa katika hicho kitu)…kadhalika unapopoteza uzoefu katika kutenda dhambi ambazo ulikuwa unazitenda hapo kwanza, unapomtii Roho Mtakatifu ndani yako..ule uzoefu unapungua na hatimaye unaisha kabisa na unakuwa UMEKUFA KWA HABARI YA DHAMBI!…Unakuwa hata iweje huwezi kufanya uasherati, huwezi kutukana, huwezi kuiba, huwezi kula rushwa, huwezi kumchukia mtu n.k

Sasa tatizo kubwa linalokuja kwa wengi wetu ni kutoelewa kazi ya Roho Mtakatifu ndani yetu, na hivyo tunadhani Roho anapokuja ndani yetu kama dikteta, ambaye ataziharibu na kutuzia kwa nguvu tusifanye dhambi. Na kutokana na watu kufikiria hivyo wanajikuta wanapopokea Roho na kujiachia ndipo wanajikuta wanashindwa na dhambi na hivyo kuendelea na maisha ya dhambi..na kujiuliza wengine wanawezaje na wao wanashindwa.

Nataka nikuambie ukishaamua kumfuata Bwana Yesu kwa kutubu dhambi zako, ambazo Roho kakushuhudia ndani yako kwamba umepotea kwa hizo na hivyo uziache..Hatua inayofuata baada ya hapo ni kumtii. Na humtii kwa kusema maneno tu mdomoni kwamba “NIMEKUTII BWANA”. Hapana huo ni mwanzo tu wa kutii..Unapaswa umtii kwa VITENDO. Maana yake ni kwamba kama ulikuwa unafanya dhambi Fulani UNAIACHA kwa lazima!…Hutafuti ushauri kwa yeyote Yule, unaiacha kwa kutumia akili zako zote, nguvu zako zote, na roho yako yote. Wala hapo huhitaji kuombewa..

Kwamfano tuchukue mfano mmoja namna ya kuiacha dhambi ya uasherati kisha tutahitimisha. Dhambi ya uasherati ambayo ndani yake inajumuisha uzinzi, ulawiti, ufiraji, na usagaji na hata utazamaji wa picha cha ngono na kujichua, na masturbation…Dhambi hii haimtoki mtu kwa Kuombewa!!..Usimfuate mtumishi wa Mungu na kumwambia niombee niache dhambi hii au dhambi ile..Hakuna maombi ya namna hiyo!..Nakuambia hivyo kwasababu na sisi wengine tulikuwa namna hiyo hiyo..tukadhani kuombewa ndio suluhisho..tukafunga muda mrefu na kujiombea na hakuna kilichobadilika ndani yetu, mpaka tulipoyasoma maandiko, tukaifahamu kweli nayo hiyo kweli ikatuweka huru. Hivyo ndugu mpendwa usipoteze muda kufanya utafiti ambao tayari umeshasaidiwa kuufanya utazunguka na kuzunguka na mwisho wa siku utarudi pale pale.

Suluhisho la kuacha dhambi ya uasherati ni KUUKIMBIA!..Kuukimbia maana yake ni kuondoka bila HIARI ya huo uasherati. Maana yake ni kwamba kama ulikuwa unaishi na mwanamke/mwanamume ambaye mnafanya naye uasherati ni KUMKIMBIA GHAFLA! Na Kukata mazoea!…Akikutafuta kwenye simu mwambie mara moja tu kwamba umeokoka na hivyo tunapaswa tutubu kwa yote tuliyokuwa tunayatenda na kumrudia Mungu. Ukiona hakuelewi wewe jiokoe nafsi yako usitazame nyuma wala usiwe na huruma, usipokee simu zake, …Usianze kushauriana naye huku bado mnakutana kutana na kuzungumza zungumza, akikutafuta kwenye simu usijibu meseji yake hata moja, hata akilia kwa machozi ya damu kwamba mrudiane usiwe na huruma jiokoe nafsi yako na yake, kwa kuukimbia uasherati ikiwezekana block hiyo namba …Usizungumze naye hata kidogo. Mfano wa Yusufu. Mke wa Potifa alimtamani na Yusufu baada ya kulijua hilo, aliacha kuongea na mke wa Potifa..

Mwanzo 39:10 “Akawa akizidi kusema na Yusufu siku baada ya siku, lakini hakumsikia alale naye, wala aongee naye”.

Utasemaje unataka kuacha uzinzi na bado unaongea na unajibu meseji za watu unaozini nao?..utasemaje unataka kuacha uasherati na huku unamazoea zoea na wanawake wa mtaani na wanaume wa mtaani?, na huku bado unafuatilia vitamthilia na vi-movie vya kipepo vyenye maudhui ya kizinzi ndani yake kwenye Tv yako vinavyochochea uzinzi tu na wala si kitu kingine?..utasemaje unataka kuacha kutazama picha za ngono na huku kwenye simu yako bado zipo?, bado umejiunga whatsapp na facebook makundi ya mambo hayo?, utasemaje unatamani kuacha pombe na wakati kuna chupa za bia ndani mwako, na bado unakula meza moja na kampani zako za walevi?. Na dhambi nyingine zote ni hivyo hivyo…dawa ya kuziacha ni KUZIKIMBIA!!…Ondoka! Dhambi nyingine ili uweze kuziepuka zinakugharimu kuhama hata hapo ulipo, hama hata mtaa..hamia mwingine..Hizo ndio gharama za kuacha dhambi!..Hizo ndizo gharama za kumtii Roho Mtakatifu.

Usipotaka kuzikimbia namna hiyo na kutafuta kuombewa, au kuwekewa mikono, kirahisi rahisi tu hivyo…Utajikuta unaombewa na kila mtu na hata kuwekewa maroho mengine mabaya hata kuliko hayo uliyonayo sasa. Hali yako kila siku itazidi kuwa mbaya kwasababu umekosa maarifa ya kutosha!.

Ndugu umeyasikia/umeyasoma haya..hutasema siku ile hukuambiwa…kama hutamtii Roho Mtakatifu leo, basi yeye mwenyewe atahakikisha anakusaidia kuyatimiza maazimio yako..lakini pia kama hutatii uamuzi ni wako. Lakini natumaini utatii, na Bwana akusaidie. Hivyo kama hujaokoka au kama wewe ni vuguvugu, upo hatarini kutapikwa hivyo kabla hujatapikwa hebu fanya mageuzi haraka..Mtii leo Roho Mtakatifu kwa kuacha dhambi kwa Lazima.. baada ya kuziacha, nenda katafute ubatizo sahihi wa kuzama mwili wote katika maji na kwa jina la Bwana Yesu kulingana na Matendo 2:38, na Yule Roho Mtakatifu ambaye aliishaianza kazi njema moyoni mwako atakusaidia kufanya yale ambayo peke yako ilikuwa ni ngumu kuyatimiza, na dhambi kwako itakuwa sio kitu kigumu kukishinda kwasababu Nira ya Kristo siku zote ni laini na utapata furaha, na amani isiyoelezeka, na utaona siku zote ulikuwa wapi kuingia ndani ya Kristo…kwa raha utakayoipata na furaha..wala dhambi haitakuwa ni kitu kinachokusisimua hata kidogo.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

KWANINI AWE PUNDA NA SI MNYAMA MWINGINE?

Nini tofauti kati ya Amri, sheria na Hukumu?

TOBA IGUSAYO MOYO WA BWANA.

KWANINI UNAPASWA UJIWEKE TAYARI SASA, KABLA YA ULE WAKATI KUFIKA?.

NAO WALIOKUWA WAMEKUSUDIWA UZIMA WA MILELE WAKAAMINI.

MAMBO MANNE,YANAYODHOOFISHA UOMBAJI WAKO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Chapa zake Yesu ni zipi hizo?

SWALI: Chapa zake Yesu ni nini? Kama tunavyosoma katika Wagalatia 6:17?


JIBU:

Wagalatia 6:17 “Tangu sasa mtu asinitaabishe; kwa maana ninachukua mwilini mwangu chapa zake Yesu.”

Kuna mambo machache ya kuzingatia hapo. 1) jambo la kwanza ni chapa 2) mahali Inapochukuliwa.

Chapa ni alama..Chochote kilichopigwa chapa maana yake kimewekwa alama inayokitambulisha kitu hicho kuwa ni milki ya kitu kingine. Kila bidhaa inayouzwa lazima ina chapa ya kampuni husika, au anayeizalisha. Sasa katika mstari huu Mtume Paulo anasema “tangu sasa mtu asinitaabishe; kwa maana ninachukua mwilini mwangu chapa zake Yesu.”..Maana yake ni kwamba “anachukua alama za Yesu katika mwili wake”..zingatia hilo Neno “mwilini mwake”..maana yake alama alizokuwa nazo Yesu na yeye anazichukua..kama uthibitisho wa kuwa milki ya Yesu.

Sasa kwanini Mtume Paulo alizungumza Sentensi hiyo kwamba TANGU SASA MTU ASINITAABISHE?

Ukianza kusoma kuanzia juu kidogo mstari wa 12 wa kitabu hicho cha Wagalatia utaona kuwa Mtume Paulo alikuwa anawazungumzia wayahudi ambao walikuwa wanawafundisha watu kuwa KUTAHIRIWA ndio uthibitisho au alama ya ki-Mungu…Kwamba alama au chapa pekee katika mwili ya kuonyesha kwamba wewe ni mtu wa Mungu ni KUWA UMETAHIRIWA, kama hujatahiriwa basi wewe huna chapa ya kiMungu au alama ya kiMungu. Hivyo wakawa wanawahubiria watu wengi mafundisho hayo potofu na hivyo kuwataabisha watu wengi hususani watu wa Mataifa. Sasa Paulo ndio akawa analisahihisha hilo na kusema, watu hao nia yao ni kutafuta kuona fahari au kupata wafuasi juu ya watu ambao watatahiriwa, lakini mioyoni mwao hata hawana mpango na Mungu..Na hapo ndio Paulo akasema mpaka sasa “tangu sasa mtu asinitaabishe kwa maana ninachukua katika mwili wangu chapa zake Kristo”..maana yake alama za Kristo kama uthibitisho wa kuwa Mkristo..

Sasa alama katika mwili wa Yesu ni zipi?..si nyingine Zaidi ya zile za Mateso, makovu ya misumari katika mwili wake, makovu ya viboko katika mgongo wake, uso uliotemewa mate, msalaba juu ya mwili wake n.k. Hizo ndizo alama au chapa za Yesu. Na hapa Mtume Paulo anasema naye pia anazichukua katika mwili wake…maana yake hizo ndizo zitakazomthibitisha kwamba yeye ni milki ya Yesu. Na sio KUTAHIRIWA.

Ndio maana utaona Paulo alijikana nafsi katika viwango vikubwa sana. Kama Bwana Yesu alivyochapwa viboko vingi, Paulo naye alichapwa idadi ya viboko 39 mara 5..

2Wakorintho 11:23 “Wao ni wahudumu wa Kristo? (Nanena kiwazimu), mimi ni zaidi; katika taabu kuzidi sana; katika vifungo kuzidi sana; katika mapigo kupita kiasi; katika mauti mara nyingi.

24 Kwa Wayahudi mara tano nalipata mapigo arobaini kasoro moja.

25 Mara tatu nalipigwa kwa bakora; mara moja nalipigwa kwa mawe; mara tatu nalivunjikiwa jahazi; kuchwa kucha nimepata kukaa kilindini;

26 katika kusafiri mara nyingi; hatari za mito; hatari za wanyang’anyi; hatari kwa taifa langu; hatari kwa mataifa mengine; hatari za mjini; hatari za jangwani; hatari za baharini; hatari kwa ndugu za uongo;

27 katika taabu na masumbufu; katika kukesha mara nyingi; katika njaa na kiu; katika kufunga mara nyingi; katika baridi na kuwa uchi”.

2Wakorintho 4:8 “Pande zote twadhikika, bali hatusongwi; twaona shaka, bali hatukati tamaa;

9 twaudhiwa, bali hatuachwi; twatupwa chini, bali hatuangamizwi;

10 siku zote twachukua katika mwili kuuawa kwake Yesu, ILI UZIMA WA YESU NAO UDHIHIRISHWE KATIKA MIILI YETU.

11 Kwa maana sisi tulio hai, siku zote twatolewa tufe kwa ajili ya Yesu, ili uzima wa Yesu nao udhihirishwe katika miili yetu ipatikanayo na mauti”

Hizo ndizo chapa za Yesu ambazo Mtume Paulo na mitume wengine walizozichukua katika miili yao. Hawakujisifia kutahiriwa kama wayahudi, wala hawakujisifia mavazi marefu na meupe katika miili yao kama alama ya kuwa watu wa Mungu, wala vyakula bali mateso katika Imani ndio iliyokuwa alama yao kuwa wao ni watu wa Mungu.

Je ni wao tu waliopaswa kuzichukua chapa za Yesu katika miili yao au pia ni kwa watu wote?

Jibu ni kwamba kila mtu aliyeokoka ni lazima azitwae chapa hizi..wengi hatupendi kusikia hivi kwasababu tunafikiri Ukristo ni kupata tu raha na burudani katika haya Maisha…Bwana Yesu alisema mtu yoyote akitaka kunifuata sharti ajitwike msalaba wake na ajikane nafsi yake ndipo amfuate…Maana yake huo msalaba atakaojitwika ndio utakaompeleka msalabani… msalaba alioubeba Bwana ulimpeleka kufa pale Kalvari kifo cha mateso…wewe na mimi ni misalaba gani tunayoibeba ambayo mwisho wa siku itatupekea kuifia Imani, au kuteswa kwa ajili ya Imani?..Misalaba unayovaa shingoni ni urembo tu.

Soma maandiko machache yafuatayo..ambayo yatakusaidia kujua kuwa Ni wajibu wetu wote kubeba chapa zake Yesu katika miili yetu..

Wafilipi 1:29 “Maana mmepewa kwa ajili ya Kristo, si kumwamini tu, ila na kuteswa kwa ajili yake; 30 mkiwa na mashindano yale yale mliyoyaona kwangu, na kusikia kwamba ninayo hata sasa.”

1Wathesalonike 3: 3 “mtu asifadhaishwe na dhiki hizi; maana ninyi wenyewe mnajua ya kuwa twawekewa hizo”.

Warumi 5: 3 “Wala si hivyo tu, ila na mfurahi katika dhiki pia; mkijua ya kuwa dhiki, kazi yake ni kuleta saburi;”

2Wathesalonike 1:4 “Hata na sisi wenyewe twaona fahari juu yenu katika makanisa ya Mungu kwa ajili ya saburi yenu, na imani mliyo nayo katika adha zenu zote na dhiki mnazostahimili.

5 Ndiyo ishara hasa ya hukumu iliyo haki ya Mungu, ili mhesabiwe kuwa mwastahili kuuingia ufalme wa Mungu, ambao kwa ajili yake mnateswa”

Je umebeba msalaba wako na kumfuata Yesu?..kumbuka kubeba msalaba sio kuvaa mkufu wa msalaba shingoni bali ni kuukataa ulimwengu kama Yesu, kuishikilia Imani bila kuangalia ni nani anakubaliana na wewe au hakualiani na wewe…Kwa ufupi kama tukio lile lile lililotokea kwa Bwana nasi pia linapaswa lijirudie katika Maisha yetu.

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

HERI NINYI MLIAO SASA, KWA SABABU MTACHEKA.

WAKAMTUKANA MUNGU, WALA HAWAKUTUBU.

UKADHANI YA KUWA MIMI NI KAMA WEWE.

MKARIBIE BWANA ZAIDI ILI UFANYIKE NGUZO.

NIMEOKOKA, ILA MUNGU NDIYE ANAYEJUA NITAKWENDA WAPI.

Kwanini Ibrahimu analitaja jina la YEHOVA wakati Musa anasema hakujifunua kwa jina hilo kwao?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Je kupiga miayo ni ishara ya mapepo?

Shalom, Naomba kufahamu kitendo cha kupiga miayo mara kwa mara hususani wakati wa maombi, Je! Ishara ya kuwa na mapepo au nguvu za giza?.

JIBU: Kwa namna ya kawaida kupiga miayo ni ishara ya mambo mawili makuu katika mwili, 1) Ya kwanza ni njaa, 2) Ya pili ni usingizi.

Hivyo tukirudi katika masuala ya maombi mkristo hapaswi kufikiria kuwa kupiga miayo ni kitendo cha mapepo au nguvu za giza, hapana bali ni mwitikio wa mwili wake mwenyewe, ukimwambia kuwa huu sasa ni wakati wa kwenda kupumzika umechoka, sio wakati wa kusali..Na ndio maana utagundua ni wakati tu wa kusali, au wa kusikiliza Neno watu ndio wanasikia uchovu wa hali ya juu, lakini wakitoka hapo hiyo hali inapotea yenyewe, utajiuliza ni kwa nini?

Ni kwasababu Biblia inatufundisha kuwa mwili ni adui wa mambo ya rohoni sikuzote, wakati roho yako ipo tayari hata kuzama muda mrefu kwenye maombi mwili wako utaanza kutoa sababu nyingi, mara umechoka, unapaswa ukapumzike, utakuletea mpaka hivyo viashiria vya miayo mingi, ili tu kukuthibitishia, na tena kama utakuwa unafikiria chakula muda wa maombi ndio kabisa utakuletea mpaka miayo ya njaa, mpaka utatetemeka wakati ni muda mfupi tu nyuma hapo ulitoka kula.

Wagalatia 5:17 “Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka’’.

Hivyo, hali kama hiyo ikikujia, hupaswi kukemea mapepo, bali ni wakati kushindana na mwili wako mpaka ukutii wenyewe, na habari njema ni kuwa kwa jinsi utakavyozidi kuzama katika maombi, ndivyo hiyo hali itakavyokuwa inatoweka yenyewe ndani yako kidogo kidogo, mpaka mwishoni utajikuta unaweza kwenda muda mrefu mpaka utajiuliza ule usingizi mwanzoni ulitokea wapi.

Kwahiyo njia rahisi ni kuhakikisha wakati unaposali, peleka mawazo yako yote na fikra zako zote kwenye maombi na sio katika mambo mengine, ndivyo utakavyoweza kuushinda mwili kirahisi, na kama ni usiku unasali toka katika mazingira ya kitanda.

Mwisho, fahamu kuwa kama mkristo huwezi kuishi bila maombi.

Kwahiyo shindana na mwili wako mpaka uushinde, vinginevyo hutadumu muda mrefu katika imani au kama utaendelea kuwepo basi ujue maisha yako yatakuwa ni ya majaribu kila kukicha ambayo yangeweza kuepukika tu kwa maombi..

Mathayo 26:41 “ Kesheni, mwombe, msije mkaingia majaribuni; roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu”.

Ubarikiwe.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

USIISHIE KUTAZAMA JUU, ENDELEA MBELE.

JE MOYO WAKO NI MNYOFU MBELE ZA MUNGU

JE WAKRISTO TUNARUHUSIWA KUSHEHEREKEA VALENTINE’S DAY?

PASAKA NI NINI? NA JE TUNARUHUSIWA KUSHEHEREKEA PASAKA?

Je! Ni dhambi kwa kijana aliyeokoka kuvaa suruali za kubana (model), kunyoa mitindo (mfano kiduku), ?

Je! Ni sahihi kwa mkristo kuoa/kuolewa na mtu wa imani nyingine?

ROHO ZILIZO CHINI YA MADHABAHU:

Rudi Nyumbani:

Print this post