Title December 2021

Kuhusuru ni nini kibiblia? (Luka 19:43)

Kuhusuru ni kuzinga kitu, pande zote  kisiwe na upenyo wa kutoroka au kupita.

 Mbinu hii yalitumia majeshi ya zamani katika vita..kabla ya kwenda kupigana na adui zao waliwazingira kwanza kuhakikisha hakuna upenyo wowote wa wao kutoka..na hiyo inaweza kuchukua hata miezi kadhaa.. Mpaka pale chakula kitakapoisha ndani..Sasa kwa hali kama hiyo maudui, wao wenyewe tu  watalazimika aidha kuiomba amani..au watoke wapigane..na kwa kawaida huwezi pigana na adui yako ukiwa na njaa.. Utapigwa tu.

Neno hili utalisoma sehemu nyingi sana katika biblia..kwamfano hivi ni baadhi ya vifungu ambavyo utakutana na Neno hilo..

2 Wafalme 6:24-25

[24]Ikawa baada ya hayo, Ben-hadadi mfalme wa Shamu akakusanya majeshi yake yote, akakwea akauhusuru Samaria.

[25]Njaa ikawa kuu huko Samaria; na tazama, wakauhusuru, hata kichwa cha punda kikapata kuuzwa kwa vipande themanini vya fedha, na kibaba cha mavi ya njiwa kwa vipande vitano vya fedha.

1 Samweli 23:8

[8]Basi Sauli akawaita watu wote waende vitani, ili waishukie Keila, na kumhusuru Daudi na watu wake.

1 Wafalme 8:37

[37]Ikiwa nchi imeingia njaa, au tauni, au ukosefu wa mvua, au ukungu, au nzige, au panzi; ikiwa adui wamewahusuru katika nchi ya miji yao; au ukiwapo msiba wo wote, au uele wo wote;

Luka 19:43

[43]Kwa kuwa siku zitakuja, adui zako watakapokujengea boma, likuzunguke; watakuzingira na kukuhusuru pande zote;

Soma pia Kumbukumbu 20:12, 19, 2Wafalme 24:11, Isaya 29:4

Ni picha gani tunaipata katika Roho?

Ndivyo anavyofanya shetani sasa katika roho..akitaka kuwaangusha watu hususani wale ambao anajua ni ngumu kuwaangusha..atakimbilia kuhusuru sehemu mbalimbali ambazo anajua wanazitegemea kuendeshea maisha yao, halafu baada ya hapo akishafanikiwa anamlazimisha ufanye dhambi fulani..

Labda anakunyima kazi..halafu anakuambia ukitaka hii kazi zini na mimi..ukiona hivyo usidhubutu..bali mpinge, kabisa kabisa..

Alipomwona Bwana Yesu anayo njaa kule jangwani..ndipo akamletea mkate..Lakini Bwana hakukubali ushawishi wake..akamwambia mtu hataishi kwa mkate, bali kwa kila Neno linalotoka katika kinywa cha Bwana.

Na wewe mwambie shetani hutaishi kwa hilo tu analoliwazia..bali kwa kila Neno linalotoka katika kinywa cha Bwana. Mungu atakupasulia mlango kwingine..

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Maji ya Zamzam yapo kibiblia?

Mintarafu ni nini?

Wanefili walikuwa ni watu gani?

HISIA YA MUNGU ILIYO MBAYA KULIKO ZOTE.

KUWA RAFIKI WA DUNIA NI KUWA ADUI WA MUNGU.

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya kilichotarajiwa kikikawia kuja moyo huugua (Mithali 13:12)?.

Jibu: Tusome,

Maandiko yanasema..

Mithali 13:12 “Kilichotarajiwa kikikawia kuja, moyo huugua. Bali haja ya mtu ikipatikana, ni mti wa uzima”.

Ni kawaida siku zote kuugua pale unapokuwa katika hali ya kusubiria jambo kwa muda mrefu.

Mtu anayemngojea mwenzake aliyekawia kwa dakika 10, yule anayemngoja ataona kakawia kama lisaa hivi, ingawa ni dakika 10 tu zimepia.

Hiyo ni kwasababu, ya kile kinachotarajiwa kimekawia, moyo wa mtu huwa unaugua.
Lakini maandiko yanazidi kusema kuwa mtu anapopata haja yake ni Mti wa Uzima.
Sasa swali hapo ni kwanini mtu anapopata haja yake anafanishwa na mti wa Uzima.

Siku zote miti unafananishwa na watu.

Marko 8:24 “Akatazama juu, akasema, Naona watu kama miti, inakwenda”.

Pia Bwana sehemu nyingine alisema “mti hutambulika kwa matunda yake”..maana yake watu wanafananishwa na miti.

Luka 6:44 “kwa kuwa kila mti hutambulikana kwa matunda yake; maana, katika miiba hawachumi tini, wala katika michongoma hawachumi zabibu.

45 Mtu mwema katika hazina njema ya moyo wake hutoa yaliyo mema, na mtu mwovu katika hazina mbovu ya moyo wake hutoa yaliyo maovu; kwa kuwa mtu, kinywa chake hunena yale yaujazayo moyo wake”.

Maana yake ni kwamba, kama mtu ndani yake ni mwema, ni mtakatifu, ana uzima..Basi mtu huyo ni MTI WA UZIMA.

Matunda atakayoyatoa yatawapa wengine uzima.

Sasa ni kwa namna gani, mtu anayepata haja yake anafananishwa na mti wa uzima?.

Ni kwasababu ya ile furaha atakayoipata, itawafaidia wengi, ni kwasababu ya ile neema atakayoiachia baada ya pale.

Siku zote watazame watu waliofanikiwa kupata jambo fulani,waliokuwa wanalitafuta utaona wanakuwa wakarimu ghafla, utaona wanatoa maneno mazuri mdomoni mwao.

Mithali 15:4 “Ulimi safi ni mti wa uzima;
Bali ukorofi wa ulimi huvunja moyo”.

Lakini kinyume chake, mtu ambaye hajapata anachokitafuta anakuwa mkali. Huwezi kutegemea kupata chochote chema kutoka kwake, hiyo ni kwasababu bado hajakipata anachokitafuta.

Hivyo hizo ni hekima tu ambazo Sulemani aliziona na kuzitoa kwa watu.

Na sisi tunapompokea Yesu maishani, Roho Mtakatifu anatupa haja ya mioyo yetu, anakata kiu yote, hivyo tunajikuta nasi pia tunakuwa wazuri ghafla, tunatoa matunda ya Uzima, hivyo tunakuwa Mti wa Uzima kwa wengine.

Ndivyo maandiko yanavyosema..

Mithali 3:13 “Heri mtu yule aonaye hekima, Na mtu yule apataye ufahamu.

14 Maana biashara yake ni bora kuliko biashara ya fedha, Na faida yake ni nyingi kuliko dhahabu safi.

15 Yeye ana thamani kuliko marijani, Wala vyote uvitamanivyo havilingani naye.

16 Ana wingi wa siku katika mkono wake wa kuume, Utajiri na heshima katika mkono wake wa kushoto.

17 Njia zake ni njia za kupendeza sana, Na mapito yake yote ni amani.

18 Yeye ni mti wa uzima kwao wamshikao sana; Ana heri kila mtu ashikamanaye naye”.

Je na wewe ni Mti wa Uzima?, Kwa wengine?. Au ni mti wa Mauti?.

Ni HAJA moja tu maishani itakayokufanya uwe Mti wa uzima duniani. Na hiyo ni kumwamini Yesu na kupokea Roho Mtakatifu.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Kama wakitenda mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu?

Nini maana ya ‘Maandalio ya moyo ni ya mwanadamu’ ?

JINSI YA KUEPUKA KUUMIZWA MOYO KUSIKOKUWA NA SABABU.

HATARI YA KUTOKUITAFAKARI BIBLIA VIZURI?

MTI WA UZIMA NA MTI WA MAARIFA.

Rudi nyumbani

Print this post

KWANINI MTINI KATIKATI YA MIZABIBU?

Kuna baadhi ya watu Mungu anawapanda katika kanisa, kwa namna ya kitofauti na kipekee sana..

Na pengine wenyewe hawalijui hilo..hivyo wanaishi maisha ya kimaficho ficho tu..au ya juu juu tu, kwa kisingizio kuwa wao si kama wengine.. wakidhani kuwa Kristo, amewaweka hapo bure, kwasababu hiyo..

Ulishawahi kuitafakari vizuri hii habari..

Luka 13:6-9
[6]Akanena mfano huu; Mtu mmoja alikuwa na mtini umepandwa katika shamba lake la mizabibu; akaenda akitafuta matunda juu yake, asipate.
[7]Akamwambia mtunzaji wa shamba la mizabibu, Tazama, miaka mitatu hii naja nikitafuta matunda juu ya mtini huu, nisipate kitu; uukate, mbona hata nchi unaiharibu?
[8]Akajibu akamwambia, Bwana, uuache mwaka huu nao, hata niupalilie, niutilie samadi;
[9]nao ukizaa matunda baadaye, vema! La, usipozaa, ndipo uukate.

Fikiria hilo ni shamba la Mizabibu..pengine ekari elfu moja, limeandaliwa mahususi kwa ajili ya kutoa zabibu za kibishara..lakini mwenye shamba tunaona bado katikati ya shamba hilo kubwa alipanda mti mwingine wa matunda ujulikanao kama “mtini”..

Kumbuka lengo lake halikuwa apate matunda ya biashara kutoka katika mti huo..bali pengine ya kula tu, na ndio maana mtini wenyewe ulikuwa ni mmoja tu. Lakini bado hakutaka ukae bila matunda..akaupa muda ili uzae..

Kuna watu Mungu kawapanda katika kanisa lake, ambao wanaweza kuonekana ni tofauti sana na watakatifu wengine pengine kilugha, labda hawajui kiswahili vizuri, au kimazingira, labda wapo mbali, au kinafasi, ni viongozi wakubwa n.k.na hivyo hawawezi moja kwa moja kutumika kama hawa wengine..kwa vikwazo hivyo.

Lakini wengi wa hawa huwa wanaishi maisha ya kujificha, wakidhani pengine sio sehemu ya kanisa la Kristo.

Nataka nikuambie, vyovyote vile ujionavyo..Kristo anatazamia matunda kutoka kwako. Anataka aone ukristo wako ukiangaza kwa wengine..anataka kuona unafanya kitu kwa ajili ya ufalme wa mbinguni..anataka kuona shamba lake alilokuweka wewe ndani yake pamoja na hao wengine hulikalii bure…na wewe pia kwa nafasi yako uhakikishe unazaa matunda..

Hizi ni siku za mwisho ndugu yangu..Kristo anasema Naja upesi, na ujira wangu, upo mkononi mwangu kumlipa kila mtu..sawasawa na kazi yake ilivyo..

Ufunuo wa Yohana 22:12
[12]Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo.

Utalipwa nini siku ile..ikiwa miaka nenda rudi, wewe ni msikiaji tu wa injili, miaka nenda rudi upo tu mafichoni, hutaki ijulikane..jiulize Ni nini umemfanyia Bwana basi..mpaka akupe ufalme siku ile?

Bwana atutie nguvu, tutambue kuwa sote tupo shambani mwake..na sio jukumu la askofu fulani au shemasi. Na kwamba Bwana atamvumilia mtakatifu yoyote katika shamba lake asiyemzalia matunda.

Tafadhali shea na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo:

Rudi nyumbani

Print this post

Maji ya Zamzam yapo kibiblia?

Naomba kujua kama Maji ya Zamzam yapo kibiblia na kama tunaweza kuyanunua na kutumia.

Jina kuu la Mwokozi wetu Yesu libarikiwe.

Maji ya Zamzam ni maji yanayoaminika kutoka katika kisima kimoja kilichopo Saudi Arabia kujulikanacho kwa jina hilo Zamzam.

Baadhi ya waarabu wanaamini kisima hicho ndicho kile kisima ambacho Hajiri aliyekuwa kijakazi wa Sara, mke wa Ibrahimua alioneshwa na yule malaika katika Mwanzo 21.

Mwanzo 21:17 “Mungu akasikia sauti ya kijana. Malaika wa Mungu akamwita Hajiri kutoka mbinguni, akamwambia, Una nini, Hajiri? Usiogope, maana Mungu amesikia sauti ya kijana huko aliko.

18 Ondoka, ukamwinue kijana, ukamshike mkononi mwako, kwa kuwa nitamfanya kuwa taifa kubwa.

19 Mungu akamfumbua macho, naye akaona kisima cha maji; akaenda akakijaza kiriba maji, akamnywesha kijana.

20 Mungu akawa pamoja na huyo kijana, naye akakua, akakaa katika jangwa, akawa mpiga upinde.

21 Akakaa katika jangwa la Parani; mama yake akamtwalia mke katika nchi ya Misri.

Lakini je! Kuna ukweli katika hayo?

Jibu ni la! Hakuna ukweli katika hayo, Kisima Hajiri alichooneshwa na Malaika hakikuwepo katika nchi ya Saudia, bali katika jagwa la Parani, ambalo lipo maeneo karibia na jangwa la Sinai, mbali kabisa na Saudia.

Kadhalika biblia haijarekodi popote kuwa kisima hicho kilikuwa kinaitwa Zamzam, wala haijarekodi kuwa baada ya hapo maji yake yalikuwa ni matakatifu. Kilikuwa ni kisima tu kama kisima kingine ambacho Mungu alikitumia kumwokoa Ishmaeli pamoja na mamaye, hakikuwa cha kimiujiza, wala hakikubeba nguvu zozote za kiungu baada ya hapo.

Imekuwa ni kawaida watu kufanya ziara sehemu ambazo kulionekana uweza wa kiMungu.

Kwamfano utaona leo hii watu wanakwenda mlima Sinai, na kwenda kuadhimisha au kufanya ibada, mahali pale Musa alipoona kijiti kikiteketea, vile vile utaona wengine leo hii wanakwenda kuchukua maji ya mto Yordani, mahali ambapo Bwana Yesu alibatiziwa na Yohana Mbatizaji, wengine watachukua udogo kutoka Yerusalemu .nk. wakiamini kuwa vitu hivyo vina uungu wa kipekee na wakitofauti.

Pasipo kujua kuwa wamedanganyika, yule Adui shetani kawapofusha macho yao, wakifikiri wanamwabudu Mungu kupitia vitu hivyo kama wanamwabudu yeye.

Bwana Yesu alisema maneno haya.

Yohana 4:21 “Yesu akamwambia, Mama, unisadiki, saa inakuja ambayo hamtamwabudu Baba katika mlima huu, wala kule Yerusalemu.

22 Ninyi mnaabudu msichokijua; sisi tunaabudu tukijuacho; kwa kuwa wokovu watoka kwa Wayahudi.

23 Lakini saa inakuja, nayo sasa ipo, ambayo waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli. Kwa maana Baba awatafuta watu kama hao wamwabudu.

24 Mungu ni Roho, nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.

Umeona?. Nyakati hizi Mungu haabudiwi tena katika milima, wala katika udongo wala katika maji..bali anaabudiwa katika Roho na Kweli..

Hivyo mtu anayetumia kitu chochote kwa imani kuwa kinamsogeza kwa Mungu zaidi, au kinampatia uponyaji..basi mtu huyo kadanganyika na uongo wa adui.

Kama unapitia ugonjwa au tatizo, tumepewa jina la Yesu, ambalo hilo tukitamka mara moja tu kwa Imani, kazi zote za shetani zinavunjika.

Je! Umemwamini na kumpokea Yesu, wewe unayesoma ujumbe huu?. Kama bado unasubiri nini?..mpokee leo na akuoshe dhambi zako nawe utapata uzima wa milele.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.

Kisima cha joka na lango la jaa ni nini?(Nehemia 2:13)

“Shinikizo” ni nini kibiblia, Na maana yake rohoni ni ipi?

BIRIKA LA SILOAMU.

Je! Ni sahihi mtu kubatizwa kwenye maji ya KISIMANI?

Rudi nyumbani

Print this post

DONT LEAVE YOUR CLOTHES AND GO NAKED!

There is a place tha Lord said these words…

Revelation 16:15 “Behold, I come as a thief. Blessed is he that watcheth, and keepeth his garments, lest he walk naked, and they see his shame.

Have you ever ask yourself why Lord said ” blessed is he that watcheth and keepeth his garments, lest he walk naked”?

In normal circumstance one cannot come out naked and go somewhere naked maybe a person with mental disorder, but a person with sound mind it’s impossible to walk out naked while people see his or her naked.

But when Lord said that, he meant it’s very possible for a person to walk out naked and people see his shame, if the person will be at a certain environment. Let’s read this story in the bible

Mark 14:48-52

48 And Jesus answered and said unto them, Are ye come out, as against a thief, with swords and with staves to take me?

49 I was daily with you in the temple teaching, and ye took me not: but the scriptures must be fulfilled.

50 And they all forsook him, and fled.

51 And there followed him a certain young man, having a linen cloth cast about his naked body; and the young men laid hold on him:

52 And he left the linen cloth, and fled from them naked.

You see in this context?..The boy was among Jesus’ disciples, but when he saw a difficult situation that he is going to die with Jesus and he has been arrested, he left his linen cloth there and Fled from them naked and people saw his shame.

The same issue continues in our spirit nowdays..

When we decide to be disciples of Jesus we are being clothed with the Lord ” THE FINE LINEN CLOTH” , whereby the meaning of that cloth is “holiness” and we are proving it from…

Revelation 19:8 “And to her was granted that she should be arrayed in fine linen, clean and white: for the fine linen is the righteousness of saints”.

When we decide to follow Jesus and be his disciples, we have to deny ourselves and bear our crosses, together with our fine linen clothes. And be ready to die with Jesus. But if we deny Lord let’s us know that we cannot run while having the fine linen clothes (righteousness of saints).

We have to leave the linen cloth before running and people will be able to see our shame.

Have you leave behind your linen clothes and run away? Just because you have go through difficult situations with your faith, isolation from parents, being hated by relatives, your boss doesn’t want you to pray, so because of these all you have decided to leave your linen clothes to Jesus( your righteousness ) and run away naked ( repeating the filth of the World). Remember God said this..

Revelation 16:15 “Behold, I come as a thief. Blessed is he that watcheth, and keepeth his garments, lest he walk naked, and they see his shame”.

Are you taking care of your linen clothes?… dont leave them to Jesus and run away naked because of troubles. Before you decide to follow Jesus remember to deny yourself, and know that you will face some troubles that can risk your life, in all these you dont need to take off your linen cloth, so that you can save your flesh.

Mark 8:35 “For whosoever will save his life shall lose it; but whosoever shall lose his life for my sake and the gospel’s, the same shall save it”.

May the Lord help us and Bless us

He comes as a thief!

Maranatha!


Related Articles:

Is a woman allowed going to the altar when she is in her menstruation?

JESUS WILL PASS SOMEDAY AND PEOPLE SHALL NOT KNOW IT.

UNDERSTAND HOW CHRIST HEALS PEOPLE’S SOULS.

Home:

Print this post

JE UPANGA UMEINGIA MOYONI MWAKO?.

Maandiko yanasema, Neno la Mungu ni kama Upanga unaokata kuwili, (yaani una makali pande mbili,mfano wa sime). Na lina uwezo wa kuzigawanya Nafsi na Roho.

Mtu aliyejikana Nafsi yake, na kuyakataa mapenzi yake kwajili ya Mungu, maana yake ni kwamba Neno la Mungu kama Upanga limeingia ndani yake na kuitenganisha Roho yake na Nafsi yake, ndio maana mtu huyo haishi tena kwa nafsi yake, bali kwa roho yake tu, ambayo hiyo ndio inayotenda mapenzi ya Mungu!

Waebrania 4:12 “Maana Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili, tena lachoma hata KUZIGAWANYA NAFSI NA ROHO, na viungo na mafuta yaliyomo ndani yake; tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo.

13 Wala hakuna kiumbe kisichokuwa wazi mbele zake, lakini vitu vyote vi utupu na kufunuliwa machoni pake yeye aliye na mambo yetu”.

Umeona?, hakuna kitu kingine chochote kinachoweza kumtenga mtu na nafsi yake, isipokuwa Neno la Mungu tu!.. Hakuna mtu anayeweza kusema ameukataa ulimwengu, amejikana nafsi yake na huku upanga haujapita moyoni mwake.

Upanga wa Mungu yaani Neno lake, ndio unaoweza kututenga sisi na mambo ambayo tumeshindwa sisi kutengana nayo kwa nguvu zetu, huwezi kujitenga na hasira kama huu upanga hujapita ndani yako,kukutenga wewe na hiyo hasira, huwezi kujitenga na vinyongo na visasi kama huu upanga hujaingia ndani yako, kuna vitu unaweza kujitenga navyo, lakini kuna vingine vinahitaji upanga wa Roho (Neno la Mungu), ili vikuachie.. kwasababu vimejishonanisha na roho yako, au nafsi yako.

Ni lazima uruhusu upanga uingie ndani yako ili uweze kuvitenganisha vitu hivyo.

Sasa utaruhusu vipi huu upanga uingie ndani yako?

Maandiko yanasema Bwana Yesu ndiye Neno la Mungu,

Ufunuo 19:13 “Naye amevikwa vazi lililochovywa katika damu, na jina lake aitwa, Neno la Mungu.

14 Na majeshi yaliyo mbinguni wakamfuata, wamepanda farasi weupe na kuvikwa kitani nzuri, nyeupe, safi”.

Unaweza kusoma pia Yohana 1:1, utaliona jambo hilo hilo,

Hivyo kama Kristo ndiye NENO LA MUNGU, maana yake yeye ndiye UPANGA, ambapo anapoingia moyoni anatenganisha roho yako na nafsi yako, hakuna chochote kilichopo ndani yako kilichojificha asikijue, atayasafisha mawazo yako yote na kutenganisha uovu na wema ndani yako. Na kukuweka katika hali salama ya kuyatenda mapenzi ya Baba tu.

Kumbuka tena maandiko yanasema..

Waebrania 4:12 “Maana Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili, tena lachoma hata KUZIGAWANYA NAFSI NA ROHO, na viungo na mafuta yaliyomo ndani yake; tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo.

13 Wala hakuna kiumbe kisichokuwa wazi mbele zake, lakini vitu vyote vi utupu na kufunuliwa machoni pake yeye aliye na mambo yetu”.

Hivyo kama tunataka kuwa wakamilifu, kama tunataka kuwa huru rohoni, kama tunataka kuyatenda mapenzi ya Mungu, BASI TUNAMHITAJI YESU SANA MIOYONI MWETU.

Wengi leo wanaye YESU katika biashara zao, wanaye Yesu katika watoto wao, wanaye Yesu katika viungo vyao, lakini hawana Yesu MIOYONI MWAO. Upanga umepita katika shughuli zao, upanga umepita katika biashara zao hata wameona shetani kawekwa mbali nao, kadhalikaupanga umepita katika miili yao hata wameona wametengwa mbali na magonjwa yaliyokuwa yanawasumbua lakini UPANGA BADO HAUJAINGIA MIOYONI MWAO.

Mariamu aliyekuwa mamaye Yesu, ijapokuwa alikuwa na Yesu katika tumbo lake, lakini wakati ule bado alikuwa hajampata Yesu moyoni..Ndio maana Simoni, Yule nabii mzee alimwambia maneno haya..

Luka 2:34 “Simeoni akawabariki, akamwambia Mariamu mama yake, Tazama, huyu amewekwa kwa kuanguka na kuinuka wengi walio katika Israeli, na kuwa ishara itakayonenewa.

35 NAWE MWENYEWE, UPANGA UTAINGIA MOYONI MWAKO, ili yafunuliwe mawazo ya mioyo mingi”.

Kuna tofauti kubwa ya Yesu kuwepo tumboni mwa Mariamu na Yesu kuwepo moyoni mwa Mariamu..Ulifika wakati Mariamu alikuwa hana budi kumwamini Yesu kama mwokozi wake na Bwana wake, na si kama “mtoto wake”. Nafasi ya Mariamu kama mama wa Yesu, iliwahi kuisha mapema sana, kabla hata ya Bwana Yesu kusulubishwa, Mariamu alishaacha kitambo sana kumwona Bwana kama mwanawe, ilifika wakati alianza kumjua kama Bwana na Mwokozi, na kuyaamini maneno yake na kwenda kubatizwa na kupokea Roho Mtakatifu. (Huo ni wakati ambapo upanga uliingia ndani yake na yeye pia).

Swali la kujiuliza ni je! Na wewe Upanga umeingia moyoni mwako?, au upo tu! Nje kwenye biashara yako?. Upanga ukiingia ndani yako kule kuupenda ulimwengu kunakufa, kule kujikana nafsi kunaingia ndani yako, kiasi kwamba hata ndugu wakuchukie, hata marafiki wajitenge nawe, hata ukose kila kitu lakini huwezi kuacha kuyafanya mapenzi ya Baba.

Dunia nzima inaweza kukuona umerukwa na akili, lakini wewe unajitambua unazo akili timamu katika Kristo. Mageuzi kama hayo katika maisha yako ndio uthibitisho kuwa Upanga umeingia ndani yako.

Mathayo 10:34 “Msidhani ya kuwa nimekuja kuleta amani duniani; LA! SIKUJA KULETA AMANI, BALI UPANGA.

35 Kwa maana nalikuja kumfitini mtu na babaye, na binti na mamaye, na mkwe na mkwe mtu;

36 na adui za mtu ni wale wa nyumbani mwake.

37 Apendaye baba au mama kuliko mimi, hanistahili; wala apendaye mwana au binti kuliko mimi, hanistahili.

38 Wala mtu asiyechukua msalaba wake akanifuata, hanistahili.

39 MWENYE KUIONA NAFSI YAKE ATAIPOTEZA; NAYE MWENYE KUIPOTEZA NAFSI YAKE KWA AJILI YANGU ATAIONA.

Kama bado hujampokea Yesu maishani mwako, basi mtafute mtumishi yoyote wa Mungu wa kweli, na mweleze kuwa unahitaji kumpokea Yesu, atakusaidia katika kukuongoza sala ya kumpokea Yesu, au wasiliana nasi kwa namba hizi hapa chini.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

NA VIUNGO VYETU VISIVYO NA UZURI VINA UZURI ZAIDI SANA.

Kwanini Bwana Yesu aliwaagiza wanafunzi wake wakanunue upanga?

Roho, Nafsi, na Mwili vina utofauti gani?

KUNA NGUVU YA ZIADA KATIKA KULING’ANG’ANIA KUSUDI LA MUNGU.

Je! Bwana Yesu alibatiza akiwa hapa duniani?

Rudi nyumbani

Print this post

Na alaaniwe ampigaye mwenzake kwa siri.

SWALI: Nini maana ya huu mstari

Kumbukumbu 27: 24 “Na alaaniwe ampigaye mwenzake kwa siri. Na watu wote waseme Amina”.


SWALI: Kulingana na sheria ya wayahudi, kosa lolotela kumdhuru mwenzako, liwe ni dogo au kubwa, lilipoonekana, adhabu yake ilitolewa palepale kulingana na kosa lenyewe.. kwamfano ukimng’oa mwenzako jino, na wewe pia uling’olewa la kwako, ukimtoa jicho, na lako pia linatolewa, ukiua na wewe pia uliuliwa,..hapo ndipo uovu ulipoweza kuondoka juu ya mtu.

Lakini kulikuwa na makosa mengine watu waliyafanya kwa siri, ambayo hayakuwa rahisi kugundulika kwa wazi, wanashangaa tu labda mtu kafa, wakidhani ni siku yake tu imefika, kumbe aliwekewa sumu siku nyingi ambayo ilikuwa inamuua kwa taratibu..

Sasa watu kama hawa, biblia inasema, wamelaaniwa, kwasababu wanawapiga wenzao kwa siri, wakidhani kuwa hata mbele za Mungu hawataonekana.

Mfano wa watu kama hawa katika biblia ni Yezebeli. Yeye alikwenda kumuua Nabothi Myezreeli, ili tu alipate shamba lake, akawaajiri watu wa kushuhudia uwongo waseme wamemsikia Nabothi amemtukana Mungu na mfalme, ili watu wampige mawe afe, na kweli akafanikiwa adhma yake, na watu hawakujua lolote.

Lakini Mungu alijua, ndipo akamtuma nabii Eliya kumtolea hukumu yake. Na kumwambia mbwa watamla maiti yake. Na kweli ndivyo ilivyokuja kuwa (1Wafalme 21).

Mwingine ni mfalme wa Daudi, yeye alimuua askari wake aliyeitwa Uria kwa siri akidhani kuwa Mungu hatamwona. Alichofanya ni kumwambia mkuu wake wa majeshi amweke, Uria mahali penye vita vikali, kisha wamuache mwenyewe, ili azidiwe na majeshi ya adui auliwe, na kweli, njama zake zilifanikiwa, lakini Mungu akamrudia Daudi na kumpa adhabu kali sana, na doa ambalo mpaka leo hii sisi tunalisoma (2Samweli 11).

Hata leo, watu wanawapiga wenzao kwa siri, kwa kuwawekea vikwazo mbalimbali, lakini kwa nje wanajifanya wapo Pamoja na wao kuwasaidia, tukiwa watu wa hivi Mungu atatulaani. Halikadhalika Wachawi wote wapo chini ya hii laana, kwasababu mchana wanacheka na wenzao kinafki, lakini usiku wanazunguka huku na huko kuwanga, na kuwasababishia wenzao madhara, na kuvuruga mipango ya watu wanaotaka kumtafuta Mungu.

Hivyo tuwe makini sana, ni heri uadhibiwe na mwanadamu, kuliko kuangukia katika laana za Mungu mwenyewe. Kwasababu yeye ndiye anayeichunguza mioyo ya watu. Ili tuweze kuishinda hii hali, hatuna budi kumaanisha kumfuata Kristo kweli kweli katika Maisha yetu. Hapo ndipo tutakapoweza kuishi Maisha ya upendo na wengine.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Mlima Gerizimu na Ebali ni ipi, na umuhimu wao rohoni ni upi?

Nini maana ya mstari huu: (Mtu ambarikiye mwenzake kwa sauti kuu asubuhi na mapema; Itahesabiwa kuwa ni laana kwake.Mithali 27:14 )?

MAAGIZO AMBAYO HAYAJAAGIZWA!

Ni SIRI gani Paulo aliyokuwa anaimaanisha katika Waefeso 5:32?

Kuwaogopa wanadamu huleta mtego,(Mithali 29:25)

Rudi nyumbani

Print this post

Sadaka ya kutikiswa ilikuwaje?

Katika Agano la kale zilikuwepo aina za sadaka mbali mbali, ambazo Mungu aliwaagiza wana wa Israeli wazitoe, ilikuwepo sadaka ya Amani, sadaka ya dhambi, sadaka ya kuinuliwa, kadhalika ilikuwepo sadaka ya kutikiswa na nyingine nyingi. Leo tutaitazama hii sadaka ya kutikiswa kwa ufupi na ujumbe wake katika roho.

Awali ya yote ikumbukwe kuwa makuhani peke yao ndio waliopewa dhamana na Mungu ya kutumika katika nyumba yake, na ndio waliopewa dhamana ya kufanya shughuli zote za kikuhani, ikiwemo kupokea sadaka kutoka kwa watu, walizomletea Bwana. Sadaka hizo zilikuwa za aina tofauti tofauti, zilikuwepo za wanyama, zilikuwepo  za ndege kama njiwa, zilikuwepo pia  za nafaka kama ngano, unga na nafaka nyingine.

Endapo Mtu akileta sadaka yake ya mnyama kama kondoo, basi alimleta kwa kuhani, kisha kuhani atamchinja Yule kondoo na kuichukua damu yako, ambayo hiyo ndiyo itakuwa kwaajili ya upatanisho wa Yule mtu, kisha viungo baadhi atavichoma juu ya madhabahu ndani ya Hema au hekalu mbele za Bwana, na sehemu ya nyama iliyobakia ambayo haijachomwa, Mungu aliruhusu Kuhani huyo iwe yake yeye na familia yake (Ndio mshahara wake). Makuhani walikuwepo wengi wanaofanya kazi hizo, na walikuwa wanafanya kazi hizo kwa zamu.

Na sadaka ya unga, ilikuwa ni hivyo hivyo, kiwango kidogo kilichomwa juu ya madhabahu mbele za Bwana na kiwango kilichobakia kilikuwa ni kwaajili ya Makuhani waliohudumu katika nyumba ya Bwana, Sadaka zote za dhambi na hatia ndio zilikuwa zinatolewa kwa utaratibu huo.

Sasa sadaka ya Kutikiswa ilikuwa ni tofauti kidogo, Kwani baada ya sadaka kupokelewa na Kuhani, kama ni Nafaka au Mnyama. Basi kuhani alichukua kwanza sehemu ndogo ya sadaka hiyo na kuinyanyua juu na kisha KUIPUNGA HEWANI MBELE ZA BWANA, kwa mfumo wa KUITIKISA TIKISA, Kisha baada ya hapo ataishusha chini, na kuendelea na hatua nyingine za kutekekeza baadhi ya viungo juu ya madhabahu, na sehemu iliyobakia ni riziki yao.

Sadaka ya kutikishwa ilihusisha aina zote za sadaka, yaani za Wanyama, ndege pamoja na Nafaka.  Sasa sio kila sadaka wana wa Israeli walizokuwa wanazileta zilitikiswa namna hiyo mbele za Bwana, la! Bali ni baadhi tu!.

Walawi 7:28 “Bwana akanena na Musa, na kumwambia,

29 Nena na wana wa Israeli uwaambie, Yeye asongezaye dhabihu yake ya sadaka za amani kwa Bwana, atamletea Bwana matoleo yake, kutoka katika ile dhabihu ya sadaka zake za amani;

30 mikono yake mwenyewe itamletea hizo sadaka za kusongezwa kwa moto; mafuta yake pamoja na kidari atayaleta, ili kwamba hicho kidari kitikiswe kuwa SADAKA YA KUTIKISWA MBELE YA BWANA.

31 Kuhani atayateketeza hayo mafuta juu ya madhabahu; lakini hicho kidari kitakuwa cha Haruni na cha wanawe.

32 Mguu wa nyuma wa upande wa kuume mtampa kuhani kuwa sadaka ya kuinuliwa kutoka katika hizo sadaka zenu za amani.

33 Katika wana wa Haruni, huyo atakayeisongeza damu ya sadaka za amani, na mafuta yake, yeye atapata mguu wa nyuma wa upande wa kuume kuwa sehemu yake.

34 Kwa maana, HICHO KIDARI CHA KUTIKISWA, na huo mguu wa kuinuliwa, nimevitwaa kwa wana wa Israeli, katika dhabihu zao za sadaka za amani, nami nimempa Haruni kuhani na wanawe, kuwa haki yao ya milele kutoka kwa wana wa Israeli.”.

Mistari mingine inayozungumziwa sadaka hiyo ya kutikiswa ni Kutoka 29:27,Walawi 8:27, Walawi 9:21, Walawi 10:14, Hesabu 6:20, Hesabu 8:11, na Hesabu 8:18.

Sadaka hiyo imebeba ujumbe gani kwetu?

Mungu aliruhusu baadhi za sadaka zitolewe kwa  njia ya kawaida na nyingine zitolewe kwa njia hiyo ya kunyanyuliwa juu na kutikiswa tikiswa, (yaani kuipungia hewani)

Kutufundisha kuwa na sisi hatuna budi kuzitofautisha sadaka zetu, Sadaka ya kumshukuru Mungu kwa matendo aliyokufanyia mwaka mzima, au mwezi mzima, au jinsi alivyokuokoa na majaribu makuu haiwezi kuwa sawa na sadaka ya kawaida unayomtolea siku zote, Ya shukrani ni lazima iwe ya juu kidogo, na uitangaze mbele zake, kwasababu ya matendo makuu aliyokufanyia, ni  lazima iambatane na kuinyanyua mikono yako juu na kumwimbia kwa kumshukuru, na kumtukuza, Sadaka ya namna hiyo inapendeza zaidi mbele za Mungu wetu..

Bwana atubariki.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Rudi nyumbani

Print this post

UDHURU NI NINI KIBIBLIA?

Shalom, karibu tujifunze na tujikumbushe wajibu wetu sisi kama watakatifu katika safari yetu ya Imani hapa duniani.

Kuna mambo ambayo tunaweza tukashindwa kumfanyia Mungu, tukadhani kuwa “Mungu anaelewa”, kumbe yanatafsirika kama Ni UDHURU mbele zake.

Tofauti na sisi tunavyoweza kutafsiri Neno udhuru. Kwamba ni kutoa sababu za uongo, ili tu kuepuka jukumu au wajibu Fulani, kwamfano, labda mtu kakuambia naomba ukanipakilie mzigo wangu kwenye gari pale stendi unitumie.. Sasa pengine wewe hutaki kwenda, ili kupindua hiyo safari, saa hiyo hiyo unaunda safari yako ya uongo na kumwambia, hapana sitaweza kwenda, kwani ninamgeni wangu natarajia baadaye, nikamchukue hotelini sijui atatoka muda gani..Lakini unajua kabisa, jambo kama hilo hukuwa na mpango nalo, huo ndio udhuru tunaoufahamu sisi.

Lakini kwa Mungu udhuru, ni kutoa sababu za kweli tena  zenye maana na mashiko kabisa.. ambazo wakati mwingine ni kweli kabisa zinastahili kufanywa.. Ili kuelewa vizuri Embu tusome tena Habari hii kwa utulivu, naamini umeshaipitia mara kadhaa, lakini isome tena, na tena, uone ni nini Mungu analenga, na ujiangalie na wewe katika nafasi yako, Je! Mambo kama hayo yapo?,,Tusome..

Luka 14:16 “Akamwambia, Mtu mmoja alifanya karamu kubwa akaalika watu wengi,

17 akamtuma mtumwa wake saa ya chakula awaambie wale walioalikwa, Njoni, kwa kuwa vitu vyote vimekwisha kuwekwa tayari.

18 Wakaanza wote kutoa udhuru kwa nia moja. Wa kwanza alimwambia, Nimenunua shamba, sharti niende nikalitazame; tafadhali unisamehe.

19 Mwingine akasema, Nimenunua ng’ombe jozi tano, ninakwenda kuwajaribu; tafadhali unisamehe.

20 Mwingine akasema, Nimeoa mke, na kwa sababu hiyo siwezi kuja.

21 Yule mtumwa akaenda, akampa bwana wake habari ya mambo hayo. Basi, yule mwenye nyumba akakasirika, akamwambia mtumwa wake, Toka upesi, uende katika njia kuu na vichochoro vya mji, ukawalete hapa maskini, na vilema, na vipofu, na viwete.

22 Mtumwa akasema, Bwana, hayo uliyoagiza yamekwisha tendeka, na hata sasa ingaliko nafasi.

23 Bwana akamwambia mtumwa, Toka nje uende barabarani na mipakani, ukawashurutishe kuingia ndani, nyumba yangu ipate kujaa.

24 Maana nawaambia ya kwamba katika wale walioalikwa, hapana hata mmoja atakayeionja karamu yangu.

Embu zitafakari hizo sababu, uone kama hakuna hata moja isiyo na mashiko, ni kweli, sherehe tu, huwezi ifananisha na mke mpya..mwingine kanunua ng’ombe, wengi, hivyo ni lazima siku hiyo akawajaribu kwanza, vinginevyo wakiwa sio bora na siku imeshapita hawezi tena kuwarudisha,tayari ni hasara, mwingine kanunua shamba tayari, lakini bado hajaliona, hivyo ni lazima akalihakiki, kama ni lenyewe au kama ameuziwa dimbwi, na siku yenyewe ndio hiyo hiyo ya karamu aliyoalikwa hawezi kuacha kwenda?

Umeona, zote hizo zilikuwa ni sababu, lakini mwenye karamu anazitafsiri kama ni Udhuru. Kwasababu gani? Kwasababu wameyathamini mambo yao, Zaidi ya ile karamu yake kubwa.

Leo hii,watu wengi hata jumapili wameacha kwenda kanisani kabisa, wanasema, boss wangu hataki, wanazitetea kazi zao, ili wasifukuzwe..halafu kwenye vichwa vyao wanasema BWANA ANAELEWA!…Kama ingekuwa sio huyu boss wangu kunizuia, mimi nisingekosa kanisani hata siku moja..

Ndugu kwa Mungu huo ni udhuru..Kama unaweza kuitumikia kampuni yako, kwa siku 6 za wiki, hadi siku ya Mungu unaiiba, fahamu tu, Mungu hawezi kukuelewa, anautafsiri kama Udhuru. Haiwezekani wiki nzima, usijiwekee ratiba kwa Mungu wako ya kumwabudu yeye, hata siku moja.

Danieli hakuruhusu udhuru, hata alipokatazwa na mfalme wa dunia yote,(kumbuka Sio boss wa ka-kampuni fulani) kuabudu Mungu wake, na vitisho vyao vya kuwatupa katika tundu la simba wote watakaokaidi. kinyume chake Danieli ndio alifungua madirisha yake, akawa anamwabudu Mungu, wakati wengine, wanasema Mungu anaelewa, hali halisi ya sasa, tumekatazwa na mfalme, sisi ni nani tupinge..

Na walipomkamata na kumtupa katika tundu la Simba, Tunaona Mungu alikuwa naye..

Vivyo hivyo na akina Shedraka, Meshaki, na Abednego, walikataa udhuru wa Nebukadreza wa kuabudu sanamu, wakati wengine wanasema, Mungu anaelewa..wenyewe wakakataa kumvunjia Mungu heshima, ndipo walipotupwa katika tanuru la moto..Bwana aliwapigania na kuwaokoa.

Lakini ikiwa sisi kila jambo tutazama, hali zetu, tusijidanganye kuwa Mungu anaelewa! Hizo zote ni udhuru. Usiruhusu kazi ile muda wa Mungu wako, usiruhusu, familia, mihangaiko, mali zitafune muda wa Mungu wako. Wengine wanasema jumapili ndio faida ninapata, ndugu ziache hizo faida zipite, Ni nani kakuambia Mungu hatakupa hizo siku nyingine? epuka udhuru..

Na ndio maana mwishoni kabisa mwa ile Habari, Bwana anasema…

“Maana nawaambia ya kwamba katika wale walioalikwa, hapana hata mmoja atakayeionja karamu yangu”.

Watu wanaotanguliza mambo yao mbele Zaidi ya Mungu katika kipindi hichi cha siku za mwisho, kwenye Unyakuo, kwenye karamu ya mwanakondoo mbinguni hawataenda. Swali je! Na wewe ni mtu wa udhuru kwa Bwana? Jibu unalo.

Maran atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Maswali na Majibu

UFUNUO: Mlango wa 19

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 3

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

KWASABABU MUDA TULIOBAKIWA NAO SI MWINGI.

Rudi nyumbani

Print this post

Hapo ndipo, atakapompa Mungu Baba ufalme wake.

SWALI: Kulingana na Danieli 7:14 inatabiri kuwa Ufalme wa Bwana Yesu utakuwa ni wa milele, Lakini tukirudi katika 1Wakorintho 15:24 anasema mwishoni atampa Baba yake ufalme wake,

Je hapo inamaana gani , Bwana Yesu ataurejesha ufalme kwa Baba yake au?


JIBU: Tusome vifungu vyote..

Danieli 7:13 “Nikaona katika njozi za usiku, na tazama, mmoja aliye mfano wa mwanadamu akaja pamoja na mawingu ya mbingu akamkaribia huyo mzee wa siku, wakamleta karibu naye.

14 Naye akapewa mamlaka, na utukufu, na ufalme, ili watu wa kabila zote, na taifa zote, na lugha zote, wamtumikie; mamlaka yake ni mamlaka ya milele, ambayo hayatapita kamwe, na ufalme wake ni ufalme usioweza kuangamizwa”.

Pia..

1Wakoritho 15:24 “Hapo ndipo mwisho, atakapompa Mungu Baba ufalme wake; atakapobatilisha utawala wote, na mamlaka yote, na nguvu.

25 Maana sharti amiliki yeye, hata awaweke maadui wake wote chini ya miguu yake.

26 Adui wa mwisho atakayebatilishwa ni mauti”.

Ni vema tukumbuke kuwa Mungu na Yesu, sio watu wawili tofauti, wenye falme mbili tofauti.. Hapana, “SIRI ya uungu” ni kubwa sana, kama vile mtume Paulo alivyoandika katika 1Timotheo 3:16, Ikiwa na maana mtu usipofumbuliwa macho na kuielewa sehemu ya siri hii, anaweza kudhani Bwana Yesu na Baba yake, ni watu wawili tofauti kabisa…

Ukweli ni kwamba, ufalme Yesu, ndio ufalme wa Baba yake, na Ufalme wa Baba yake ndio ufalme wa Yesu, hivyo akimrudishia Baba ufalme, hakufanyi badiliko lolote, kwasababu yeye na Baba ni kitu kimoja. Ni kama anavyopenda tu yeye mwenyewe atawalie katika ofisi ipi!! Je ya Baba au ya Mwana.. hivyo tu..

Kwahiyo Ufalme huo, kwasasa unatawala rohoni, lakini utadhihirika rasmi, tunapoingia katika ule utawala wa miaka1000, ambapo Mungu (Ndani ya Kristo), atatawala kwa miaka hiyo elfu mpaka atakapohakikisha kila kitu kiovu kimefikia mwisho wake, Kisha baada ya hapo, atatawala sasa kama Baba (Yehova), milele na milele.

Na ndio maana ufalme wake ni wa milele na milele na milele.. Ambao hauwezi kuhasika na kwenda kwa adui, au kwa Malaika yoyote, au kwa kiumbe chochote, utabaki kwake milele na milele na milele. Utukufu na shukrani vimrudie yeye daima.

Amen.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

YESU NI NANI?

Tofauti kati ya ufalme wa mbinguni na ufalme wa Mungu ni ipi?

DANIELI: Mlango wa 11

TUMEFANYIKA KUWA WANA WA MUNGU!

UNYAKUO.

Rudi nyumbani

Print this post