Tunamtumikia Mungu kwa karama tulizopewa, na karama ndizo zinazozaa Huduma..Na Karama za Roho Mtakatifu zimefananishwa na viungo katika miili yetu. Maana yake tukijifunza kwa kina jinsi viungo vya miili yetu vinavyofanya kazi basi tutakuwa tumeelewa vyema pia jinsi karama za Roho zinavyotenda kazi.
Warumi 12:4 “Kwa kuwa kama vile katika mwili mmoja tuna viungo vingi, wala viungo vyote havitendi kazi moja. 5 Vivyo hivyo na sisi tulio wengi tu mwili mmoja katika Kristo, na viungo, kila mmoja kwa mwenzake”
Warumi 12:4 “Kwa kuwa kama vile katika mwili mmoja tuna viungo vingi, wala viungo vyote havitendi kazi moja.
5 Vivyo hivyo na sisi tulio wengi tu mwili mmoja katika Kristo, na viungo, kila mmoja kwa mwenzake”
Tabia moja ya kipekee ya viungo vya mwili ni kwamba kila kiungo kipo kwaajili ya kuvisaidia viungo vingine…Kwamfano Miguu utaona ipo kwa kazi ya kuubeba mwili, haipo kwa kazi ya kujibeba yenyewe..Mikono ni hivyo hivyo, ipo kwa kazi ya kuhudumia mwili sehemu mbalimbali kama kupeleka chakula mdomoni, kuosha mwili, kuchana nywele n.k..
Vile vile macho yapo si kwaajili ya kujiangalia yenyewe, bali kwaajili ya kutazama mambo yanayoendelea katika mwili na nje ya mwili na hivyo kupeleka taarifa kwenye ubongo. Masikio hayapo kwaajili ya kujisikia yenyewe, wala ngozi haipo kwaajili ya kujifunika yenyewe, bali kuufunika mwili na viungo vya ndani.
Moyo haudundi kujifurahisha, au kujipa burudani, bali unafanya vile kuhakikisha unasukuma damu katika viungo vyote vya mwili. Na viungo vingine vyote ni hivyo hivyo, vipo kwaajili ya kusaidia viungo vyenzake.
Na karama za rohoni zinatenda kazi kwa namna hiyo hiyo. Ukiona mahali hakuna kusaidiana basi hapo kuna kasoro, Roho wa Mungu hayupo hapo, lakini mahali ambapo Roho Mtakatifu yupo ni lazima viungo vyote visaidiane.
Ukiona ndani yako huna msaada wowote katika mwili wa Kristo, au huhitaji msaada wowote basi huo ni uthibitisho kwamba wewe ni kiungo kilichokufa na tena kimezikwa.. Kwasababua hata mkono uliokufa haufanyi chochote, na kama umekufa muda mrefu basi maana yake ni kwamba umeshaoza na kilichobakia ni mifupa tu..
Vivyo hivyo kama huna msaada wowote katika Mwili wa Kristo wewe ni mifupa katika roho, na usifurahie kuwa katika hiyo hali, ni afadhali ukafufuka leo!.
Utasema mimi siijui karama yangu! Hivyo nasubiri Mungu anifunulie kwanza.
Ndugu hakuna kitu kinakuja kwa kukaa tu na kukisubiri…Wengi wanakaa tu wakisubiri Mungu awafunulie karama zao, (Wengine wanafanya hivyo kwasababu hawajui na wengine ni wavivu). Nataka nikuambie mtu wa Mungu kama ulikuwa unakaa kusubiri kwasababu hujui basi nataka nikuambie usiendelee kusubiri kwasababu utakaa sana, na wala hutaona chochote…kila siku utabaki ukikisia tu labda ni hii, au ile.. utabaki ukihuzunika unapoona wengine wanafanya kazi ya Mungu na wewe hufanyi chochote..Hivyo usibaki kusubiri!. (Kasome hichi kisa 2Wafalme 7:1-15 )
Kuifahamu karama yako hakuji kwa namna hiyo (ya kusubiri), kunakuja kwa wewe kujiingiza kwenye kazi yoyote au huduma yoyote ya Mungu ambayo inaona inafunguka mbele yako, na huko huko utaona kuna mahali umefit vizuri!..utaona kuna mahali unafanya vizuri na kwa furaha zaidi ya wengine na tena unafanya kwa ubora na pasipo kusukumwa..Utaona Mungu anaanza kukufungulia milango na kukupa akili na uwezo wa kutumika katika hilo eneo siku baada ya siku. Ukiona umefikia hiyo hatua, basi hapo huenda ndio mahali huduma yako ilipo, usianze kunia Makuu na kutamani makubwa, anza na hicho hicho chako kwasababu ni muhimu sana katika Mwili wa Kristo kwaajili ya kuwahudumia watu wake, na siku zinavyozidi kwenda Kristo atazidi kukistawisha.
Usisubiri maono wala kuoteshwa ndoto wala kutokewa na Bwana au malaika!..Je siku ulipokwenda kutafuta kazi ulisubiri maono au ndoto?. Vivyo hivyo katika kuifanya kazi ya Mungu hatuenendi kwa kuona bali kwa IMANI. (2Wakorintho 5:7).
Sasa utaanzaje safari ya kuilelekea huduma yako Mungu aliyoikusudia?
Kwanza kabisa, jichanganye na watakatifu mahali unapoabudu na mahali unapoishi, au popote pale unapoweza kukutana nao (Usijitenge wala usijione bora).. Shiriki nao katika kazi wanazozifanya za kanisa au za kihuduma, popote pale ambapo unaona unaweza kuchangia mawazo yako, au ujuzi wako, au chochote kile, wewe changia!. Utaona pale ulipochangia pengine mawazo yako yamekuwa bora mara nyingi kuliko ya wengine, au pale ulipotumia ujuzi wako au elimu yako pameleta matokeo makubwa sana, na hivyo pakafanya uwepo wako uwe wa muhimu sana..n.k
Kwamfano unaweza kuingia kwenye kundi, katikati huko ukasikia kuna mtu fulani alipatwa na matatizo haya na yale hivyo sasahivi yupo katika masononeko makubwa, wameenda watu kumfariji lakini wapi!..na hata kashafikia hatua ya kukata tamaa na kurudi nyuma, sasa wewe kama karama yako ni faraja, utaona kuna kitu kitakuchoma ndani..na kujisikia huruma mara mbili zaidi ya wenzako, na kutafuta kwenda kumsaidia yule mtu, na utashangaa umemrudisha na amerudia katika hali yake, na watu wote wanashangaa umewezaje! ..ukishaanza kuona hizo hali za kuweza kufanya kitu ambacho ni kigumu kwa wengine kukifanya lakini wewe umeweza tena kwa ufasaha!, basi huo ni uthibitisho kuwa haupo mbali na huduma yako. Ukifikia hiyo hatua utaona Bwana ataanza kukusafishia njia zaidi ya kuliendea kusudi alilokuitia utaona hekima inazidi kuongezeka juu yako siku baada ya siku, na utaona majukumu ya wewe kuifanya hiyo kazi ya Mungu yanazidi kuongezeka, utaona mzigo unazidi kuongezeka ndani yako..Na mwisho wa siku Mungu ataweka ndani yako UZIO.
Uzio ni hali fulani ambayo inawatokea watumishi wa Mungu, ambao ikipita siku au masaa hawajafanya kazi ya Mungu, wanasikia hali moja mbaya sana, hata kufikia KUUMWA! au kuishiwa nguvu za Mwili. Ndio kama ile hali ya Bwana aliyosema katika Yohana 4:34 “Yesu akawaambia, Chakula changu ndicho hiki, niyatende mapenzi yake aliyenipeleka, nikaimalize kazi yake”.
Kazi ya Mungu inakuwa kama ni chakula kwao!. Hivyo hiyo hali ni kama ishara ya kumsaidia mtu wa Mungu asitoke nje ya mstari. Hivyo ikitokea amemaliza siku moja au mbili hajatumika kabisa katika kazi yake hiyo, hali ya mwili wake inaanza kumbadilikia na hivyo inamfanya siku zote aifanye kazi ya Mungu kama vile ni chakula chake.
Sasa kumbuka kama tulivyotangulia kusema..Karama na huduma ni kwaajili ya masaidiano na si kwaajili ya kujisaidia mwenyewe.. Kwahiyo ukiona umeingia kwenye huduma fulani katikati ya watakatifu na moyo wako unaelekea kupata pesa, au kupata umaarufu wako binafsi na si wa Kristo, au kupata jina au cheo, au umaarufu..basi jua hiyo ni roho nyingine ya Adui ipo ndani yako, ambayo shetani kakupandikizia, na lengo la roho hiyo ni kwenda kuliharibu kundi la Mungu
Lakini ukiona ni kwenda kusaidia watakatifu na watu wengine, basi zidi kufanya mbele ya safari Bwana atakufungulia milango zaidi.
Ndugu kama ulikuwa unasubiria maono ndipo uanze kuifanya kazi ya Mungu, leo umejua…usisubiri, jiunganishe na wanaofanya kazi za Mungu na huko huko Bwana atakusafishia njia..Lakini pia kabla ya kwenda huko kama hujaokoka! Ni vyema ukafanya hivyo leo, kwasababu huwezi kwenda kufanya kazi ya mtu ambaye hampatani. Hivyo ni lazima umkubali ndipo ukafanya kazi zake, hivyo mpokee leo Kristo moyoni mwako, na kisha katafute kubatizwa na Roho Mtakatifu atakuongoza katika njia unayoiendea.
Tafuta kwa bidii kuifanya kazi ya Mungu, na Mungu atakuheshimu.
Bwana akubariki!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
USIPOKUWA MWAMINIFU, NAFASI YAKO ITACHUKULIWA.
MTU ASIYE PAMOJA NAMI YU KINYUME CHANGU.
Je Mungu anawapenda watu wote au ana chuki?
JE NI LAZIMA MKRISTO AOE/AOLEWE?
LOLOTE ATAKALOWAAMBIA FANYENI.
Rudi Nyumbani:
Print this post
Shalom, nakukaribisha tuyatafakari Pamoja maneno ya uzima.
Katika hichi kipindi cha mwisho, kuna mwitikio mmoja tu, ambao utamtambulisha bibi-arusi wa kweli wa Kristo ni nani..
Kumbuka bibi-arusi ni tofauti na Suria, Sulemani alikuwa na Masuria 700 lakini wake au (bibia-arusi) walikuwa ni 300 tu. Tofauti ya mke na suria ni kuwa mke anauhalali wa vyote ikiwemo urithi na mali, lakini suria yeye anaweza kupewa vyote lakini sio urithi au jina..Jambo hilo utaliona kwa Ibrahimu, ambaye mbali na Isaka alikuwa pia na watoto wengine 7, lakini wao walipewa zawadi tu, mashamba, majumba n.k..Lakini Isaka peke yake ndiye aliyepewa vyote, zawadi pamoja na urithi na jina,..Na ndio maana mpaka leo, tunamtambua Isaka, na sio wale wengine..Hiyo ni kwasababu walikuwa ni wana wa Masuria na sio wana wa mke halali kama ilivyokuwa kwa Sara. (Kasome Mwanzo 25:5-6)
Ndivyo hivyo hata wakati huu wa mwisho, haya makundi mawili yapo, hivyo usifurahie tu, Mungu kukubariki, usifurahie tu Mungu kukupa hiki au kile..furahia pale unapokuwa na uhakika kuwa wewe ni mrithi wa ahadi za milele za Mungu baada ya Maisha haya..
Kwasababu Masuria sikuzote ni wengi kushinda wake.
Sasa tukirudi katika kitabu cha ufunuo, utaona sehemu nyingi, Bwana Yesu alianza kulitamka hili Neno “tazama, naja upesi”;.. Utasoma..
Ufunuo 22:7 “Na tazama, naja upesi; heri yeye ayashikaye maneno ya unabii wa kitabu hiki…. 12 “Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo”.
Ufunuo 22:7 “Na tazama, naja upesi; heri yeye ayashikaye maneno ya unabii wa kitabu hiki….
12 “Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo”.
Hiyo ni kuonyesha kuwa wakati wake wa kurudi duniani umekaribia sana..
Lakini ukishuka chini kidogo utaona, wanaorodheshwa wawili walioitikia mwito huo, nao ni Roho Mtakatifu na bibi-arusi.
22:17 “NA ROHO NA BIBI-ARUSI WASEMA, NJOO! Naye asikiaye na aseme, Njoo! Naye mwenye kiu na aje; na yeye atakaye, na ayatwae maji ya uzima bure”.
Ni kwasababu gani bibi-arusi alikuwa na ujasiri wa kuitikia mwito huo “Njo Bwana Yesu”? Ni kwasababu, alijua urithi wake halisi upo karibu, ni kwasababu alikuwa na ajasiri wa Imani yake, kwa Yule Roho Mtakatifu aliye ndani yake.
Na ndio maana hata Mtume Yohana, aliposikia Bwana akiyarudia maneno hayo tena chini kidogo, naye pia aliitikia kwa ujasiri mkubwa na kusema amina na uje Bwana Yesu..
Ufunuo 22:20 “Yeye mwenye kuyashuhudia haya asema, Naam; naja upesi. Amina; na uje, Bwana Yesu”.
Maneno haya bibi-arusi tu peke yake aliyejazwa Roho Mtakatifu ndio atakayekuwa na ujasiri wa kuyasema wakati huu wa mwisho..
Swali la kujiuliza ni je! mimi na wewe tunaweza kuyasema maneno hayo? kumbuka Jibu halipo katika vinywa vyetu bali katika mioyo yetu. Kama hatuna ujasiri huo basi sisi sio bibi-arusi, haijalishi tutasema tumeokoka kiasi gani, sisi tutakuwa ni Masuria tu. Na siku ya unyakuo itakapofikia tutabaki hapa dunia, hatutanyakuliwa Pamoja na bibiarusi wa kweli.
Masuria kwa jina lingine ndio wale wanawali wapumbavu ambao walichukua taa zao, lakini hawakuwa na mafuta ya ziada katika vyombo vyao, Na Bwana arusi alipokuja walikutwa hawana mafuta ya kutosha (Mathayo 25)
Kwahiyo ndugu tusifurahie tu, kusema sisi ni wakristo, bali tufurahie kusema sisi ni bibi-arusi, tuliojazwa Roho Mtakatifu.. Kumbuka lile neno la Bwana “Waitwao ni wengi, ila wateule ni wachache”
Kama tulishaokoka, lakini bado tulikuwa tunaishi maisha ya uvuguvugu, basi huu ni muda wetu sasa, kuzitengeneza taa zetu katika hichi kipindi kifupi tulichobakiwa nacho.
Na Mungu atatujalia tufikie mwisho mwema kwa neema zake.
Maran Atha.
NAMI NINAZO FUNGUO ZA MAUTI, NA ZA KUZIMU.
AMELAANIWA AANGIKWAYE MSALABANI.
Je! Shetani alitolea wapi uovu?
KARAMU YA MWANA-KONDOO.
MAWE YALIYOKWISHA KUCHONGWA MACHIMBONI.
Jina La Bwana wetu Yesu libarikiwe. Karibu tuyatafakari maandiko tena siku ya leo.
Kuna mtafaruku mkubwa sana katika ukristo kuhusu vyakula, wapo wanaoamini kuwa vipo vyakula najisi na wapo wanaoamini kuwa vyakula vyote ni halali kuliwa. Na hivyo kusababisha mashindano yasiyoisha.
Kama tukiyasoma maandiko tutaona kuwa vyakula haviwezi kumtia mtu unajisi. Ingawa hatuwezi kusema kwamba vyote vinafaa, hapana si vyote..huwezi kula mbao, au chuma, au sumu au pombe na kusema vinafaa…hapana hivyo havifai kwasababu vinauharibu mwili badala ya kuujenga.
1Wakorintho 10:23 “Vitu vyote ni halali; bali si vitu vyote vifaavyo. Vitu vyote ni halali; bali si vitu vyote vijengavyo”.
Kwahiyo kama umehakiki hicho ulacho hakina madhara katika mwili wako, basi kula! Si dhambi..lakini kama umehakiki kwamba kina madhara basi usile. Na pia kama unawasiwasi na mashaka kwamba hicho ulacho kinaweza kuwa na madhara basi usile kabisa. Kwasababu hata usipokula hutendi dhambi!!
Warumi 14:22 “ Ile imani uliyo nayo uwe nayo nafsini mwako mbele za Mungu. Heri mtu yule asiyejihukumu nafsi yake katika neno lile analolikubali. 23 Lakini aliye na shaka, kama akila, amehukumiwa kuwa ana hatia, kwa maana hakula kwa imani. Na kila tendo lisilotoka katika imani ni dhambi”.
Warumi 14:22 “ Ile imani uliyo nayo uwe nayo nafsini mwako mbele za Mungu. Heri mtu yule asiyejihukumu nafsi yake katika neno lile analolikubali.
23 Lakini aliye na shaka, kama akila, amehukumiwa kuwa ana hatia, kwa maana hakula kwa imani. Na kila tendo lisilotoka katika imani ni dhambi”.
Sasa leo hatutaingia sana kujifunza juu ya vyakula, kama utahitaji somo juu ya hilo, basi utatujuza inbox..Lakini tutajifunza namna ya kuepukana na unajisi, kwa kupitia maandiko yafuatayo ambayo ni maarufu sana.
Tusome…
Marko 7:5 “Basi wale Mafarisayo na waandishi wakamwuliza, Mbona wanafunzi wako hawaendi kwa kuyafuata mapokeo ya wazee, bali hula chakula kwa mikono najisi?…………………………….. 14 Akawaita makutano tena, akawaambia, Nisikieni nyote na kufahamu. 15 Hakuna kitu kilicho nje ya mtu ambacho kikimwingia chaweza kumtia unajisi, bali vile vimtokavyo, ndivyo vimtiavyo unajisi yule mtu. 16 Mtu akiwa na masikio ya kusikilia, na asikie.]”
Marko 7:5 “Basi wale Mafarisayo na waandishi wakamwuliza, Mbona wanafunzi wako hawaendi kwa kuyafuata mapokeo ya wazee, bali hula chakula kwa mikono najisi?……………………………..
14 Akawaita makutano tena, akawaambia, Nisikieni nyote na kufahamu.
15 Hakuna kitu kilicho nje ya mtu ambacho kikimwingia chaweza kumtia unajisi, bali vile vimtokavyo, ndivyo vimtiavyo unajisi yule mtu.
16 Mtu akiwa na masikio ya kusikilia, na asikie.]”
Sasa maneno haya Bwana wetu Yesu aliwaambia makutano, ambao pengine idadi yao ilikuwa ni mamia au maelfu, na ndani ya mkutano huo walikuwepo pia wanafunzi wake wale 12, Na kwa Pamoja wakasikia maneno hayo…kwamba hakuna kimwingiacho mtu kimtiacho unajisi bali kimtokacho..sasa baada ya maneno hayo kama umefuatilia kwa makini Bwana hakuendelea kuongea zaidi. Hivyo kila mmoja akatoka na tafsiri yake kichwani…naamini wengi walifiki kwamba ni kimwingiacho mtu ni chakula na kimtokacho ni matapishi au kinyesi na mkojo..na kwamba hivyo ndivyo vimtiavyo mtu unajisi..Lakini ule mkutano wote ulitawanyika ukidhani umemwelewa Bwana vizuri kumbe hawakumwelewa hata kidogo..
Baadaye ndipo wanafunzi wake wakahisi kuna kitu hawakukielewa na hivyo wakaamua kumfuata wakiwa peke yao kumwomba awafafanulie zaidi..
Tusome..
“17 Hata alipoingia nyumbani, ameuacha mkutano, wanafunzi wake wakamwuliza habari za ule mfano. 18 Akawaambia, Hivi hata ninyi hamna akili? Hamfahamu ya kwamba kila kitu kilicho nje ya mtu, kikimwingia, hakiwezi kumtia unajisi; 19 kwa sababu hakimwingii moyoni, ila tumboni tu; kisha chatoka kwenda chooni? Kwa kusema hivi alivitakasa vyakula vyote. 20 Akasema, Kimtokacho mtu ndicho kimtiacho unajisi. 21 Kwa maana ndani ya mioyo ya watu hutoka mawazo mabaya, uasherati, 22 wivi, uuaji, uzinzi, tamaa mbaya, ukorofi, hila, ufisadi, kijicho, matukano, kiburi, upumbavu. 23 Haya yote yaliyo maovu yatoka ndani, nayo yamtia mtu unajisi”.
“17 Hata alipoingia nyumbani, ameuacha mkutano, wanafunzi wake wakamwuliza habari za ule mfano. 18 Akawaambia, Hivi hata ninyi hamna akili? Hamfahamu ya kwamba kila kitu kilicho nje ya mtu, kikimwingia, hakiwezi kumtia unajisi;
19 kwa sababu hakimwingii moyoni, ila tumboni tu; kisha chatoka kwenda chooni? Kwa kusema hivi alivitakasa vyakula vyote.
20 Akasema, Kimtokacho mtu ndicho kimtiacho unajisi.
21 Kwa maana ndani ya mioyo ya watu hutoka mawazo mabaya, uasherati,
22 wivi, uuaji, uzinzi, tamaa mbaya, ukorofi, hila, ufisadi, kijicho, matukano, kiburi, upumbavu.
23 Haya yote yaliyo maovu yatoka ndani, nayo yamtia mtu unajisi”.
Umeona hapo?. Wanafunzi wamepata ufafanuzi vizuri, lakini makutano hawakupata!..Makutano wameondoka wakidhani unajisi ni majasho, matapishi, haja kubwa na haja ndogo…Kumbe sivyo!. Vitu najisi ni vile vinavyotoka moyoni na si mwilini…
Unapopita barabarani na kwa bahati mbaya ukasikia matusi yakitukanwa… yale yanaingia moyoni mwako, na kwenda kwenye hazina ya kumbukumbu zako, (hapo hakuna unajisi)..lakini unapopitia hali ya kuudhiwa siku za mbeleni na kwenda kuifungua ile hazina na kisha kuyatumia yale matusi uliyoyasikia huko nyuma na kumtukana mwingine hapo ndipo unapokuwa najisi.
Unapoona mauaji yamefanyika ambayo sio wewe umeyafanya kwamfano mauaji ya utoaji mimba..Jambo lile linakwenda kwenye hazina ya moyo wako, hapo hujawa najisi, lakini siku moja ukapata ujauzito na ukaenda kuutoa au mwingine akapata ujauzito na ukamshauri akaitoe, hapo tayari umekuwa najisi. Na mambo mengine yote ni hivyo hivyo.
Na mtu najisi mbele za Mungu ni mtu mchafu..Katika agano la kale mtu najisi alikuwa haruhusiwi hata kuingia katika kusanyiko la Mungu, anatengwa mpaka atakaposafishika…Na hata sasa bado unajisi upo!..Ukiwa mlevi tayari umejitia unajisi, ukiwa mwasherati, mzinzi, muuaji, mtukanaji, mlawiti, mtazamaji picha za tupu, msengenyaji n.k tayari wewe ni najisi mbele za Mungu, hustahili kuwepo katika kundi la Mungu, haijalishi umeshakuwa mkristo kwa miaka mingapi, bado ni najisi mbele za Mungu, kwamba unahitaji kutubu..Na kujitenga na hayo mambo.
Tito 1:15 “Vitu vyote ni safi kwa hao walio safi; lakini hakuna kilicho safi kwao walio wanajisi, wasioamini; bali akili zao zimekuwa najisi, na nia zao pia. Wanakiri ya kwamba wanamjua Mungu, bali kwa matendo yao wanamkana; ni wenye machukizo, waasi, wala kwa kila tendo jema hawafai”.
Kama hujaokoka! Kristo anakupenda na alikufa kwa ajili yetu..Wokovu unapatikana bure leo, unachopaswa kufanya hapo ulipo ni kupiga magoti binafsi, na kutubu mbele zake kwa dhati kabisa..Kama umemaanisha kweli pale utakaposema tu Amen, basi tayari ameshakusikia na kukusamehe..na utaona amani ya ajabu imeingia moyoni mwako, baada ya hapo nenda katafute ubatizo sahihi wa kimaandiko, ambao ni ule wa maji tele (Yohana 3:23) na kwa jina la Mwokozi wetu Yesu Kristo, ambalo ndio jina la Baba, Mwana na Roho Mtakatifu (Mathayo 28:19, Matendo 2:38)..Kwa kuyatii maagizo hayo machache na mepesi utakuwa utakuwa umeihakikishia mbingu kuwa kweli umeanza umegeuka na hivyo Mungu atakuheshimu zaidi. Na utakaso halisi wa Kristo utakuja ndani yako.
Bwana akubariki.
Kama umeokoka usisahau kuliombea Kanisa Pamoja na wakristo wote na watumishi wa Mungu kila siku..
Maran atha!
Je kualikwa kwenye sherehe za watu ambao si wakristo ni dhambi?
LAKINI USIKU WA MANANE, PAKAWA NA KELELE.
KWA VILE ALIVYOKUWA MTU WA HAKI.
MAMBO MANNE,YANAYODHOOFISHA UOMBAJI WAKO.
Mkatale ni nini katika biblia? (Matendo 16:24)
JINA LAKE KWA KIEBRANIA NI ABADONI, NA KWA KIYUNANI NI APOLIONI.
Hazama ni nini?
Hazama ni pete ya puani.
Neno hilo utalisoma katika vifungu hivi;
Mwanzo 24:47, Kutoka 35:22,
Na pia ukisoma Ezekieli sura ya 16 yote utaona jinsi Mungu anavyolilinganisha taifa la Israeli na msichana ambaye alipozaliwa tu alitelekezwa porini na wazazi wake akiwa hata hajakatwa kitovu chake. Na Bwana alipokuwa anapita (hapa akijifananisha na mwanaume fulani), alimwona na kumuhurumia, akamchukua na kwenda kumtunza, akamkuza, akafanya naye maagano kuwa atakuwa wake, akamkuza vizuri sana, akawa mrembo sana, akamvisha mavazi mazuri, na kumpamba kwa kila aina ya mapambo ikiwemo hazama na vikuku, lakini baadaye alipokuja kuwa mtu mzima alikengeuka na kuanza kuzini na wanaume wengi, na kuwa kahaba wa kipindukia, ..
Ezekieli 16:11 “Nikakupamba kwa mapambo pia, nikatia vikuku mikononi mwako, na mkufu shingoni mwako. 12 NIKATIA HAZAMA PUANI MWAKO, na pete masikioni mwako, na taji nzuri juu ya kichwa chako. 13 Hivyo ulipambwa kwa dhahabu na fedha; na mavazi yako yalikuwa ya kitani safi, na hariri, na kazi ya taraza; ulikula unga mzuri, na asali, na mafuta; nawe ulikuwa mzuri mno, ukafanikiwa hata kufikilia hali ya kifalme. 14 Sifa zako zikaenea kati ya mataifa kwa sababu ya uzuri wako; kwa maana ulikuwa mkamilifu, kwa sababu ya utukufu wangu niliokutia, asema Bwana MUNGU”.
Ezekieli 16:11 “Nikakupamba kwa mapambo pia, nikatia vikuku mikononi mwako, na mkufu shingoni mwako.
12 NIKATIA HAZAMA PUANI MWAKO, na pete masikioni mwako, na taji nzuri juu ya kichwa chako.
13 Hivyo ulipambwa kwa dhahabu na fedha; na mavazi yako yalikuwa ya kitani safi, na hariri, na kazi ya taraza; ulikula unga mzuri, na asali, na mafuta; nawe ulikuwa mzuri mno, ukafanikiwa hata kufikilia hali ya kifalme.
14 Sifa zako zikaenea kati ya mataifa kwa sababu ya uzuri wako; kwa maana ulikuwa mkamilifu, kwa sababu ya utukufu wangu niliokutia, asema Bwana MUNGU”.
Lakini sasa mfano huo haumaanishi kuwa wanawake wa ki-kristo wanaruhusiwa kujipamba hapana, kumbuka huo ni mfano tu ambao Mungu aliutoa kuonyesha ni jinsi gani Israeli taifa lake alilolipamba rohoni kwa utukufu wake, tangu zamani, baadaye likaja kukengeuka kuabudu miungu mingine tofauti nay eye.
Biblia inasema..
1Petro 3:1 “Kadhalika ninyi wake, watiini waume zenu; kusudi, ikiwa wako wasioliamini Neno, wavutwe kwa mwenendo wa wake zao, pasipo lile Neno; 2 wakiutazama mwenendo wenu safi, na wa hofu. 3 Kujipamba kwenu, kusiwe kujipamba kwa nje, yaani, kusuka nywele; na kujitia dhahabu, na kuvalia mavazi; 4 bali kuwe utu wa moyoni usioonekana, katika mapambo yasiyoharibika; yaani, roho ya upole na utulivu, iliyo ya thamani kuu mbele za Mungu”.
1Petro 3:1 “Kadhalika ninyi wake, watiini waume zenu; kusudi, ikiwa wako wasioliamini Neno, wavutwe kwa mwenendo wa wake zao, pasipo lile Neno;
2 wakiutazama mwenendo wenu safi, na wa hofu.
3 Kujipamba kwenu, kusiwe kujipamba kwa nje, yaani, kusuka nywele; na kujitia dhahabu, na kuvalia mavazi;
4 bali kuwe utu wa moyoni usioonekana, katika mapambo yasiyoharibika; yaani, roho ya upole na utulivu, iliyo ya thamani kuu mbele za Mungu”.
Umeona, mwanamke wa kikristo hapaswi kuweka hazama, au vikuku, au lipstick, au wanja, au mikufu, au hereni mwilini mwake, badala yake mapambo haya anapaswa ayahamishie rohoni, kwa matendo mema. Ndivyo biblia inavyoagiza.
Kwahiyo kama wewe ulikuwa unaweza hazama au vipini puani mwako, ni vyema ukaacha. Ishi sasa maisha ya kama wanawake wacha Mungu walivyoyaishi. Mapambo yasikusababishe uikose mbingu.
Shalom.
Tazama tafsiri ya maneno mengine chini.
MASERAFI NI NANI?
Jabari ni nini, kama linavyotumika kwenye biblia?
Pomboo ni nini katika biblia?(Kutoka 25:5, Ezekieli 16:10)
Naomba kujua nini maana ya kuteguka uvungu wa paja?
WINGU KUBWA LA MASHAHIDI.
NJONI, NUNUENI MLE NA MNYWE.
Katika biblia shetani amepewa majina tofauti tofauti na hiyo ni kutokana na aina ya kazi anazozifanya hapa duniani, kwamfano biblia inapomwita shetani/ibilisi ni kwasababu ni mpinzani na mshitaki wa roho zetu kwa Mungu ndio tafsiri ya jina hilo,.
Vilevile sehemu nyingine inapomwita Joka (Ufunuo 12), ni kwasababu ni mwongo kama alivyokuwa nyoka, na anameza roho za watu kama majoka yafanyavyo kumeza wanyama,..
Bado sehemu nyingine inamwita, mkuu wa ulimwengu huu, (Yohana 12:31,2Wakorintho 4:4), kwasababu mambo yote yaliyotukuka ulimwenguni sasa yanashikiliwa na yeye, yeye ndiye kiongozi wa hayo ..
Pia inamwita mfalme wa uweza wa anga (Waefeso 2:2) kwasababu nguvu zote za giza katika ulimwengu wa roho anazishikilia yeye, baba wa mapepo na wachawi duniani.
Vilevile sehemu nyingine inamwita mjaribu (Mathayo 4:3,1Wathesalonike 3:5), kwasababu, yeye ndio chanzo cha majaribu yote kwa mkristo..Na ndio maana Bwana Yesu alituambia kesheni mwombe msije ingia majaribuni..Kwasababu tusipoomba huyu atapata nafasi kubwa ya kutuletea majaribu ili kutuangusha.
Lakini zaidi ya yote biblia inatuonyesha kuwa atakuja kuwa na jina lingine, lijulikanalo kama Abadoni au Apolioni,.. Tafsiri ya jina hili ni MHARIBIFU…Ikiwa na maana atakuja kuwa na kazi ya kufanya uharibifu tu.
Kama leo hii unamwona shetani ni mharibifu, basi bado haujajua vizuri uharibifu wake upoje.
Tukisoma kitabu cha ufunuo, kama tunavyojua mara baada ya unyakuo wa kanisa kupita, kutafuata matukio ambayo hayaelezeki kwa namna ya kawaida. Tukiachana na yale mapigo ya vile vitasa 7 na ile siku ya Bwana mwenyewe ambayo jua hili litaondolewa, kutatangulia kwanza mapigo ya baragumu 7,..Sasa hatuwezi kuyachambua yote hapa, ikiwa utahitaji somo lake utuambia inbox tukutumie..
Lakini leo tutatazama, baragumu la tano, ambalo ndio kiini cha somo letu la Leo. Baragumu hilo litakapopigwa, biblia inatuambia, Shimo la kuzimu litafunguliwa na humo watatoka nzige wabaya sana..tusome;
Ufunuo 9:1 “Malaika wa tano akapiga baragumu, nikaona nyota iliyotoka mbinguni, imeanguka juu ya nchi; naye akapewa ufunguo wa shimo la kuzimu. 2 Akalifungua shimo la kuzimu; moshi ukapanda kutoka mle shimoni kama moshi wa tanuru kubwa; jua na anga vikatiwa giza kwa sababu ya ule moshi wa shimoni. 3 Nzige wakatoka katika ule moshi, wakaenda juu ya nchi, wakapewa nguvu kama nguvu waliyo nayo nge wa nchi. 4 Wakaambiwa wasiyadhuru majani ya nchi, wala kitu cho chote kilicho kibichi, wala mti wo wote, ila wale watu wasio na muhuri ya Mungu katika vipaji vya nyuso zao. 5 Wakapewa amri kwamba wasiwaue, bali wateswe miezi mitano. Na maumivu yao yalikuwa kama kuumwa na nge, aumapo mwanadamu. 6 Na siku zile wanadamu watatafuta mauti, wala hawataiona kamwe. Nao watatamani kufa, nayo mauti itawakimbia. 7 Na maumbo ya hao nzige yalikuwa kama farasi waliowekwa tayari kwa vita, na juu ya vichwa vyao kama taji, mfano wa dhahabu, na nyuso zao zilikuwa kama nyuso za wanadamu. 8 Nao walikuwa na nywele kama nywele za wanawake. Na meno yao yalikuwa kama meno ya simba. 9 Nao walikuwa na dirii kifuani kama dirii za chuma. Na sauti ya mabawa yao ilikuwa kama sauti ya magari, ya farasi wengi waendao kasi vitani. 10 Nao wana mikia kama ya nge, na miiba; na nguvu yao ya kuwadhuru wanadamu miezi mitano ilikuwa katika mikia yao. 11 Na juu yao wanaye mfalme, naye ni malaika wa kuzimu, jina lake kwa Kiebrania ni ABADONI, na kwa Kiyunani analo jina lake APOLIONI.
Ufunuo 9:1 “Malaika wa tano akapiga baragumu, nikaona nyota iliyotoka mbinguni, imeanguka juu ya nchi; naye akapewa ufunguo wa shimo la kuzimu.
2 Akalifungua shimo la kuzimu; moshi ukapanda kutoka mle shimoni kama moshi wa tanuru kubwa; jua na anga vikatiwa giza kwa sababu ya ule moshi wa shimoni.
3 Nzige wakatoka katika ule moshi, wakaenda juu ya nchi, wakapewa nguvu kama nguvu waliyo nayo nge wa nchi.
4 Wakaambiwa wasiyadhuru majani ya nchi, wala kitu cho chote kilicho kibichi, wala mti wo wote, ila wale watu wasio na muhuri ya Mungu katika vipaji vya nyuso zao.
5 Wakapewa amri kwamba wasiwaue, bali wateswe miezi mitano. Na maumivu yao yalikuwa kama kuumwa na nge, aumapo mwanadamu.
6 Na siku zile wanadamu watatafuta mauti, wala hawataiona kamwe. Nao watatamani kufa, nayo mauti itawakimbia.
7 Na maumbo ya hao nzige yalikuwa kama farasi waliowekwa tayari kwa vita, na juu ya vichwa vyao kama taji, mfano wa dhahabu, na nyuso zao zilikuwa kama nyuso za wanadamu.
8 Nao walikuwa na nywele kama nywele za wanawake. Na meno yao yalikuwa kama meno ya simba.
9 Nao walikuwa na dirii kifuani kama dirii za chuma. Na sauti ya mabawa yao ilikuwa kama sauti ya magari, ya farasi wengi waendao kasi vitani.
10 Nao wana mikia kama ya nge, na miiba; na nguvu yao ya kuwadhuru wanadamu miezi mitano ilikuwa katika mikia yao.
11 Na juu yao wanaye mfalme, naye ni malaika wa kuzimu, jina lake kwa Kiebrania ni ABADONI, na kwa Kiyunani analo jina lake APOLIONI.
Sasa hapa biblia imetumia tu lugha ya mfano ili upate halisi ya jinsi mambo yatakavyokuwa.. Hapo anasema wakatoka nzige..Sasa hao sio nzige halisi bali hayo ni Mapepo (maroho) ambayo kwasasa yapo kifunguni..Kumbuka si idadi yote ya mapepo yafayanyayo kazi sasa, yapo mengine mengine yapo kifungoni, biblia inasema hivyo katika kitabu cha Yuda.
Sasa mapepo hayo Yamefananishwa na wale Nzige waharibifu wa mazao, na ulimwengu umefananishwa na shamba lenye mazao (Mathayo 13:38) Na kama unavyojua nzige wakipita mahali kwenye mazao ya kijani, kitendo cha masaa machache tu, hilo shamba linageuka na kuwa vijiti tu.. Ni tishio kubwa sana duniani hata sasa, fuatilia tu habari ya nzige wa jangwani walipopita Afrika Mashariki kipindi cha hivi karibu uone uharibifu wao ulivyokuwa tishio.
Sasa tunajuaje kama haya ni mapepo na si nzige halisi, ni kwasababu hayajapewa kudhuru nchi, bali wanadamu ambao hawana muhuri wa Mungu duniani. Kazi hiyo huwa inafanywa na shetani mwenyewe na malaika zake, Soma Ufunuo 7 utaona hao ambao watakuwa wameitiwa muhuri ni wakina nani. Lakini kama ikitokea unyakuo leo hii umekupita, ujue kuwa mambo hayo yatakukuta tu..
Mapepo haya yatakayoachiliwa kutoka kuzimu na moja kwa moja yatapokea oda kutoka kwa kiongozi wao mkuu shetani/Apolioni/Abadoni, kwa lengo la KUWAHARIBU wanadamu tu. Kama jinsi atakavyojulikana kwa jina hilo.
Mapepo haya yatawaingia watu, bila kizuizi chochote, mengine yatawafanya watu kuwa vichaa, na kuwatesa tu kama yalivyomtesa Yule bwana aliyekutana na Yesu kule makaburini, mengine yatawafanya watu wawe wakatili kupita kiasi, kuchukiana kitaongezeka mara nyingi zaidi, kugombana, kuumizana, na kuuana n.k. mengine yatawafanya watu wapate ajali lakini si za kuwaua, bali za kuwaumiza tu vibaya..
Mengine yatawaletea watu magonjwa yasiyo ya kawaida lakini hakuna kifo, kama vile wakati wa Ayubu, siku hiyo kama hukwenda kwenye unyakuo utakaa kwenye majivu ya kila namna kujipoza lakini wapi, utatamani kufa lakini kifo kitakukimbia, yaani kwa ufupi duniani kutakuwa na watu ambao si watu, maroho hayo yatafanya uharibifu usio kuwa wakawaida.
Mioyo ya wanadamu itaharibiwa kwa kiwango cha juu sana, na kama vile yanavyofananishwa na nzige maana yake ni kuwa mpaka hicho kipindi chao kiishe, watu watakuwa kama makapi tu, wamechoka sana..
Huo wakati ndugu yangu, si wa kuwepo, ukisikia hizi ni siku za mwisho, usidhani unyakuo ukishapita mambo yatakuwa kama unavyoyaona leo.. Ni Roho Mtakatifu ndani ya kanisa lake ndiye anayezuia hayo mambo kwasasa. Lakini kuna wakati utafika, ataondolewa, na akiondolewa anaondoka na kanisa lake takatifu (Ndio unyakuo wenyewe).Kitakachosalia duniani ni vilio tu na kusaga meno (Mathayo 25:30).
2Wathesalonike 2:5 “Je! Hamkumbuki ya kuwa wakati nilipokuwapo pamoja nanyi naliwaambieni hayo? 6 Na sasa lizuialo mwalijua, yule apate kufunuliwa wakati wake. 7 Maana ile siri ya kuasi hivi sasa inatenda kazi; LAKINI YUKO AZUIAYE SASA, HATA ATAKAPOONDOLEWA”.
2Wathesalonike 2:5 “Je! Hamkumbuki ya kuwa wakati nilipokuwapo pamoja nanyi naliwaambieni hayo?
6 Na sasa lizuialo mwalijua, yule apate kufunuliwa wakati wake.
7 Maana ile siri ya kuasi hivi sasa inatenda kazi; LAKINI YUKO AZUIAYE SASA, HATA ATAKAPOONDOLEWA”.
Swali la kujiuliza, Je! Bado tunaudharau wokovu wa Yesu?.
Je! Bado tunaishi maisha ya kutokujali, mpaka haya mambo yote yatukute? Kama ndivyo ni heri tuyakabidhi maisha yetu kwa Bwana leo, ayaokoe. Vilevile tukabatizwe katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na Kwa jina la YESU KRISTO tupate ondoleo la dhambi zetu. Bwana wetu ni mwingi wa huruma, anatuonya mbele kabla ya mambo hayajatokea kwa ghafla. Hivyo mpokee Kristo leo na atakufanya kiumbe kipya, ulimwengu unapita na mambo yake yote, lakini Kristo na Neno lake wanadumu milele. Na yeye anatuambia itatufaidia nini kuupata ulimwengu mzima na kupata hasara za nafsi zetu?
Bwana atusaidie, Bwana atubariki sote.
UFUNUO: Mlango wa 10.
https://wingulamashahidi.org/2019/09/01/nini-maana-ya-maneno-haya-ya-bwana-nami-nikiinuliwa-juu-ya-nchinitawavuta-wote-kwanguyohana1232/
Areopago ni nini? Kwanini mtume Paulo walimpeleka huko?
VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 8 (Kitabu cha Ezekieli)
WhatsApp
Mavu ni nini?
Mavu ni wadudu jamii ya nyuki, kwa jina maarufu ni NYIGU. Maumbile yao ni makubwa zaidi ya nyuki wa kawaida, Na mauvimu yao ni kama tu yale ya nyuki..
Wametajwa mara kadha wa kadha katika biblia, na hivi ni baadhi ya vifungu vinavyowaelezea;
Kutoka 23:27 “Nitatuma utisho wangu utangulie mbele yako, nami nitawafadhaisha watu wote utakaowafikilia, nami nitawafanya hao adui zako wote wakuonyeshe maungo yao. 28 NAMI NITAPELEKA MAVU MBELE YAKO, watakaomfukuza Mhivi, na Mkanaani, na Mhiti, watoke mbele yako. 29 Sitawafukuza mbele yako katika mwaka mmoja; nchi isiwe ukiwa, na wanyama wa bara wakaongezeka kukusumbua”.
Kutoka 23:27 “Nitatuma utisho wangu utangulie mbele yako, nami nitawafadhaisha watu wote utakaowafikilia, nami nitawafanya hao adui zako wote wakuonyeshe maungo yao.
28 NAMI NITAPELEKA MAVU MBELE YAKO, watakaomfukuza Mhivi, na Mkanaani, na Mhiti, watoke mbele yako.
29 Sitawafukuza mbele yako katika mwaka mmoja; nchi isiwe ukiwa, na wanyama wa bara wakaongezeka kukusumbua”.
Kumbukumbu 7:19 “uyakumbuke hayo majaribu makuu yaliyoyaona macho yako, na hizo ishara, na maajabu, na mkono wa nguvu, na mkono ulionyoka, aliokutolea nje Bwana, Mungu wako; ndivyo atakavyowafanya Bwana, Mungu wako, mataifa yote unaowaogopa. 20 Tena Bwana, Mungu wako, ATAMPELEKA MAVU KATI YAO, hata hao watakaosalia, hao wajifichao, waangamie mbele zako. 21 Usiingiwe na kicho kwa sababu yao; kwa kuwa Bwana, Mungu wako, yu katikati yako, Mungu mkuu, mwenye utisho”.
Kumbukumbu 7:19 “uyakumbuke hayo majaribu makuu yaliyoyaona macho yako, na hizo ishara, na maajabu, na mkono wa nguvu, na mkono ulionyoka, aliokutolea nje Bwana, Mungu wako; ndivyo atakavyowafanya Bwana, Mungu wako, mataifa yote unaowaogopa.
20 Tena Bwana, Mungu wako, ATAMPELEKA MAVU KATI YAO, hata hao watakaosalia, hao wajifichao, waangamie mbele zako.
21 Usiingiwe na kicho kwa sababu yao; kwa kuwa Bwana, Mungu wako, yu katikati yako, Mungu mkuu, mwenye utisho”.
Yoshua 24:11 “Nanyi mliuvuka Yordani, mkafika Yeriko; nao watu wa Yeriko wakapigana nanyi, Mwamori, na Mperizi, na Mkanaani, na Mhiti, na Mgirgashi, na Mhivi, na Myebusi; nami nikawatia mikononi mwenu. 12 NIKATUMA MAVU MBELE YENU, waliowafukuza mbele yenu hao wafalme wawili wa Waamori, si kwa upanga wako, wala kwa upinde wako”.
Yoshua 24:11 “Nanyi mliuvuka Yordani, mkafika Yeriko; nao watu wa Yeriko wakapigana nanyi, Mwamori, na Mperizi, na Mkanaani, na Mhiti, na Mgirgashi, na Mhivi, na Myebusi; nami nikawatia mikononi mwenu.
12 NIKATUMA MAVU MBELE YENU, waliowafukuza mbele yenu hao wafalme wawili wa Waamori, si kwa upanga wako, wala kwa upinde wako”.
Katika mistari hiyo tunaona Mungu alivyowatumia wadudu hawa mavu kama silaha ya kuwafukuza maadui wa Israeli. Kufunua kuwa wapo mavu wa rohoni, ambao Mungu huwa anawatuma kuwafukuza maadui wa watakatifu duniani sasa.
Na mavu wenyewe ni malaika wa Bwana, na maadui wa watakatifu ni majeshi ya mapepo.. Mtakatifu yeyote rohoni huwa analindwa na kundi la malaika wa Bwana, hivyo shetani na mapepoo yake hawezi kumgusa kwa namna yoyote.
Lakini ikiwa mtu yupo nje ya Kristo, ibilisi ni lazima awe na mamlaka juu ya mwili wako. Na mapepo pia ni lazima yatajiamulia kufanya chochote yapendacho ndani yako, kwasababu hawapo mavu wa kukulinda wewe.
Kama hujaokoka na unahitaji kuokoka leo, basi fungua hapa kwa ajili ya sala ya Toba, >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Kumbuka Ni kwa Yesu tu unaweza kuwa salama pengine pote unapotea.
Tazama na tafsiri ya maneno mengine ya biblia chini.
Neno beramu lina maana gani katika biblia?
MUNGU HANA MBARAKA MMOJA TU!..MWAMINI.
DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.
CHUKIZO LA UHARIBIFU
Pomboo ni nini?
Pomboo ni aina ya samaki jamii ya nyangumi anayeishi baharini, Anajulikana kwa jina maarufu la DOLPHIN, Ni samaki anayezaa, pia ananyonyesha, lakini zaidi ya yote anasifa ya kuwa mnyama mwenye akili nyingi kuliko wote ulimwenguni baada ya mwanadamu. Na kuwa na tabia ya uokozi. Tazama picha juu.
Samaki huyu ni rahisi kufundishika, na ni rahisi kuishi na wanadamu.
Katika biblia pomboo(Dolphin) ametajwa sehemu nyingi, hususani katika matumizi ya ngozi yake, ambayo ilitumika katika kutekengeza hema ya kukutania, pamoja na vitu vingine vitengenezwayo kwa ngozi, kama vile viatu vya thamani.
Hivi ni baadhi ya vifungu katika biblia vinavyomtaja Pomboo.
Kutoka 25:3 “Sadaka utakayopokea mikononi mwao ni hii; dhahabu, na fedha, na shaba, 4 na nyuzi za rangi ya samawi, na za rangi ya zambarau, na za rangi nyekundu, na nguo za kitani safi, na singa za mbuzi; 5 na ngozi za kondoo waume zilizotiwa rangi nyekundu, na NGOZI ZA POMBOO, na miti ya mshita, 6 na mafuta ya ile taa, na viungo vya manukato kwa yale mafuta ya kupaka, na kwa ule uvumba wenye harufu nzuri”;
Kutoka 25:3 “Sadaka utakayopokea mikononi mwao ni hii; dhahabu, na fedha, na shaba,
4 na nyuzi za rangi ya samawi, na za rangi ya zambarau, na za rangi nyekundu, na nguo za kitani safi, na singa za mbuzi;
5 na ngozi za kondoo waume zilizotiwa rangi nyekundu, na NGOZI ZA POMBOO, na miti ya mshita,
6 na mafuta ya ile taa, na viungo vya manukato kwa yale mafuta ya kupaka, na kwa ule uvumba wenye harufu nzuri”;
Kutoka 26:14 “Nawe fanya kifuniko cha ile hema, cha ngozi za kondoo waume zilizotiwa rangi nyekundu, na juu yake KIFUNIKO CHA NGOZI ZA POMBOO. 15 Nawe fanya hizo mbao za maskani za mti wa mshita, zenye kusimama”.
Kutoka 26:14 “Nawe fanya kifuniko cha ile hema, cha ngozi za kondoo waume zilizotiwa rangi nyekundu, na juu yake KIFUNIKO CHA NGOZI ZA POMBOO.
15 Nawe fanya hizo mbao za maskani za mti wa mshita, zenye kusimama”.
Kutoka 35:5 “Katwaeni kati yenu matoleo kwa Bwana; mtu awaye yote aliye na moyo wa kupenda, ayalete matoleo; dhahabu na fedha na shaba; 6 na nyuzi za rangi ya samawi, na za rangi ya zambarau, na za rangi nyekundu, na kitani nzuri, na singa za mbuzi; 7 na ngozi za kondoo waume zilizotiwa rangi nyekundu, na NGOZI ZA POMBOO, na mbao za mshita”;
Kutoka 35:5 “Katwaeni kati yenu matoleo kwa Bwana; mtu awaye yote aliye na moyo wa kupenda, ayalete matoleo; dhahabu na fedha na shaba;
6 na nyuzi za rangi ya samawi, na za rangi ya zambarau, na za rangi nyekundu, na kitani nzuri, na singa za mbuzi;
7 na ngozi za kondoo waume zilizotiwa rangi nyekundu, na NGOZI ZA POMBOO, na mbao za mshita”;
Ezekieli 16:9 “Kisha nikakuosha kwa maji; naam, nalikuosha kabisa damu yako, nikakupaka mafuta; 10 nikakuvika nguo ya taraza, nikakupa VIATU VYA NGOZI YA POMBOO, nikakufunga nguo ya kitani safi kiunoni mwako, nikakufunika kwa Hariri”.
Ezekieli 16:9 “Kisha nikakuosha kwa maji; naam, nalikuosha kabisa damu yako, nikakupaka mafuta;
10 nikakuvika nguo ya taraza, nikakupa VIATU VYA NGOZI YA POMBOO, nikakufunga nguo ya kitani safi kiunoni mwako, nikakufunika kwa Hariri”.
Mistari mingine ni kama hii;
(Kutoka 35:23, 36:19, 39:34, Hesabu 4:6,8,10,11,12,)
Ni kwanini Mungu aliruhusu hema ya kukutania ifunikwe na ngozi ya samaki hodari (pomboo)?
Kumbuka, wana wa Israeli, waliwashinda maadui zao kabisa kabisa, kwa njia ya habari tu,.pale walipojaribu kuvuka kama wao waligharikishwa,.Hivyo ni kama samaki hodari Mungu aliwavusha baharini pasipo wao kuzama..
Hiyo ni kuwakumbuksha kuwa kila watakapokusanyika mbele ya Hema, na kuitazama hiyo hema iliyofunikwa kwa ngozi ya pomboo, wakumbuke wema wa Mungu aliowafanyia wakati wanaivuka bahari ambayo kwa namna ya kawaida haiwezekani mwanadamu yeyote kuivuka isipokuwa samaki tu peke yake..
Hivyo wamtukuze yeye, na kumpa shukrani zote peke yake.
Tazama maana maneno mengine ya biblia chini;
Yeshuruni ni nani katika biblia?
Kitabu cha YASHARI kinachozungumziwa katika 2Samweli 1:17-18, ni kitabu gani?
Kamsa ni nini kwenye biblia? (Sefania 1:16, Wimbo 3:8)
MPINGA-KRISTO
Kupokea chanjo ni dhambi kibiblia?
Chanjo ni “ugonjwa dhaifu” unaoingizwa ndani ya mwili wa mtu, ambao mwili una uwezo wa kuudhibiti, na hivyo kuuachia mwili kumbukumbu ya ugonjwa huo pindi utakapokuja tena katika ukamilifu wote siku za mbeleni.
Ili kuelewa zaidi tafakari mfano huu “Mfanya biashara mmoja aliyefanikiwa katika biashara zake, alikuwa akihifadhi fedha zake nyumbani, na nyumba yake hiyo haukuwa na uzio zaidi ya mlango wake mmoja tu wa kuingilia ndani. Siku moja wahalifu walimvamia usiku na kujaribu kuvunja mlango wake, lakini kutokana na kwamba mlango wake ule ulikuwa imara sana na wahalifu wale hawakuwa na zana za kutosha walishindwa kuuvunja mlango ule, wakaondoka…hivyo tukio lile lilimtafakarisha sana yule mfanya biashara, na hivyo akatafuta suluhisho ili tukio kama lile lisijirudie tena, kwamba wasije wahalifu wengine wenye nguvu kuliko wale wa kwanza na kufanikiwa kuvunja mlango na kumwibia na kumdhuru, hivyo kulizuia hilo, kulipopambazuka aliita mafundi wakatengeneza uzio mkubwa kuizunguka nyumba yake yote, na pamoja na hayo akaweka na mlinzi getini pamoja na mbwa”.
Sasa ukilitafakari tukio hilo utagundua kwamba…kwa lile tukio la kwanza lililomtokea la wezi wasio na nguvu za kutosha kujaribu kuvunja mlango wake ni kama limemfungua akili mfanya biashara yule na kugundua kuwa kumbe yupo katika hatari na hivyo anapaswa kujilinda zaidi.
Sasa katika ulimwengu wa sayansi ya tiba, hao wezi dhaifu ndio wanafananishwa na “chanjo” wanapowekwa ndani ya mwili, lengo ni kuupa mwili taarifa za hatari iliyopo na hivyo kujitengenezea kinga madhubuti kwa hatari itakayokuja kutokea mbeleni iliyo mfano wa hiyo.
Kwahiyo matabibu (madaktari) wakati mtoto anapozaliwa, ili kumnusuru wanamweka mtoto chanjo hizo mbalimbali za magonjwa tofauti tofauti..lengo ni ili ule mwili wa mtoto upate taarifa na ujitengenezee kinga mapema kabla huo ugonjwa haujaja kwa nguvu siku za mbeleni. Sasa hilo ndio lengo la kwanza la Chanjo. Na kwa lengo hilo basi sio dhambi kumpa mtoto chanjo, au mtu kupokea chanjo.
Lakini pia sio lazima, kwasababu viwango vya Imani vinatofuatiana. Wapo wengine waliopewa neema ya kumwamini Mungu, na hivyo huweza kuishi bila hivyo vitu, na wasipatikane na madhara yoyote. Hao ni wachache, na wanafanya vizuri zaidi. Lakini pia sio wote wenye imani hiyo, kwahiyo nao pia sio dhambi wakipokea chanjo.
Warumi 14: 1 “Yeye aliye dhaifu wa imani, mkaribisheni, walakini msimhukumu mawazo yake. 2 Mtu mmoja anayo imani, anakula vyote; lakini yeye aliye dhaifu hula mboga. 3 Yeye alaye asimdharau huyo asiyekula, wala yeye asiyekula asimhukumu huyo alaye; kwa maana Mungu amemkubali”.
Warumi 14: 1 “Yeye aliye dhaifu wa imani, mkaribisheni, walakini msimhukumu mawazo yake.
2 Mtu mmoja anayo imani, anakula vyote; lakini yeye aliye dhaifu hula mboga.
3 Yeye alaye asimdharau huyo asiyekula, wala yeye asiyekula asimhukumu huyo alaye; kwa maana Mungu amemkubali”.
Hivyo sio dhambi kupokea chanjo!.Na hata kama unayo Imani ya kutokupokea hiyo, hupaswi kuwafanyia hivyo watoto wako, wala kuwahukumu wale wanaopokea…Ni vizuri ukawapeleka watoto wako kwenye chanjo, wewe baki na imani yako..watakapokuwa watu wazima watachagua..
Pia kuna jambo la kuzingatia. Sio kila chanjo ni lazima kupokea au kumpa mwanao, Zipo chanjo za msingi kabisa, ambazo zinajulikana katika mahospitalini, ambazo ni chache sana. Chanjo chache ni vizuri zaidi kwasababu anayetupa afya ni Mungu, na si wanadamu, KİLA KİTU TUNAPASWA TUKİFANYE KWA KİASİ. Na si kuweka tegemeo letu huko asilimia 100, kwamba ndio uhai wetu na ulinzi wetu upo huko. Tukiweka mategemeo yetu huko asilimia 100, hiyo ni dalili tosha kwamba hatuna Imani kwa Mungu hata kidogo. Jambo ambalo ni dhambi na linamtia Mungu wetu wivu na huzuni kwasababu hizo ni sawa na ibada za sanamu.
Hivyo kwa hitimisho: Kupokea Chanjo sio dhambi, wala kumpa mwanao chanjo sio dhambi…Wala kuipa mifugo yako chanjo sio dhambi. Isipokuwa inapaswa itumike kwa kiasi, kwa mimi nionavyo chanjo 3 zinatosha zikizidi sana 4. Mengine tumwamini Mungu atupaye afya na uzima, na atuponyaye. (Zaburi 107:20).
Na chanjo tunayoizungumzia hapa ni ile ya HOSPITALINI na si ya kwa waganga wa kienyeji. Chanjo za waganga wa kienyeji ambazo zinahusisha “kuchanjwa chale” ni za kishirikina, ambazo ni machukizo makubwa kwa Mungu wetu, hizo zinahusiana na ibada za sanamu na Mungu kazikataza..(Soma Walawi 19:28)
Je Kutoa Mimba ni dhambi?
NJIA MOJAWAPO YA KUPATA MSAADA KUTOKA KWA MUNGU.
NAYE HERI AWAYE YOTE ASIYECHUKIZWA NAMI.
Shalom, karibu tujifunze Biblia.
Katika kitabu cha Mwanzo tunasoma kuhusu uumbaji..Tunasoma Mungu alimwumba Mtu kutoka katika mavumbi ya nchi, lakini Zaidi ya hayo tunaona aliumba na vitu vingine vinavyoonekana kama miti, Wanyama, samaki n.k.
Sasa kama umekisoma vizuri kitabu hicho utagundua kuwa vimetajwa tu vitu na viumbe vinavyoonekana kwa macho, lakini vile visivyoonekana kwa macho havijatajwa. Kwamfano hutaona viumbe kama bakteria wametajwa hapo katika uumbaji..ingawa ni wengi kuliko idadi ya viumbe vyote vinavyoonekana kwa macho, na tena kuna aina nyingi za bakteria na virusi, hutaona pia Mungu kazitaja chembe chembe hai za damu zilizopo ndani ya mwili wa Adamu zinazoishi ndani yake na kumlinda dhidi ya maadui wa mwili wake..hali kadhalika utaona Mungu kataja mavumbi katika kitabu cha mwanzo…lakini hajataja elementi nyingine zilizo ndogo sana na nyingi kuliko mavumbi yote ya dunia na mchanga zinazoitwa protoni na elektoni, zilizopo ndani ya huo mchanga na ndani ya kila kitu.
Kwahiyo hiyo ina maana kuwa Uumbaji wa Mungu sio tu huu wa vitu tunavyoviona kwa macho, bali pia kuna vitu na viumbe vingine vingi visivyoonekana kwa macho ambavyo Mungu kaviumba pia vinavyoishi katikati yetu..Hii tunayoiona ni kama tu “summary” ya vitu vilivyoumbwa.
Na kama umegundua matatizo mengi na mafanikio mengi yanatokana na hivi vitu tusivyoviona…Kwamfano matatizo ya magonjwa yote ni kutokana na hawa bakteria au virusi. Hawaonekani lakini wanaweza kusababisha madhara makubwa, hata kifo, virusi vya korona havionekani kwa macho lakini leo hii vinausumbua ulimwengu.
Vivyo hivyo mafanikio mengi yanatokana na vitu visivyoonekana..kwamfano unaweza kushangaa inawezekanikaje kioo chenye waya waya tu kinaweza kuonyesha sura ya mtu na matukio yake..(kumbe ukifuatilia nyuma yake ni hivyo vitu vidogo sana visivyoonekana protoni na elecroni vinatumika), na umeme ni hivyo hivyo, unajiuliza ule waya mwembamba vile unawezaje kupitisha nguvu kubwa vile ya kuwezesha mashine kusukuma vyuma Na hata kusaga nafaka na kuzifanya unga, au unawezaje kupitisha moto mwingi kiasi kile cha kuchemsha maji kwa dakika tano na yakatokota kabisa. Kumbe nguvu ile inatokana na sayansi ya vitu visivyoonekana (protoni na electroni).
Kwa mantiki hiyo basi, hakuna sababu za kusema kwamba shetani hayupo kwasababu tu hatumwoni, au hakuna sababu ya kusema kwamba mapepo hayapo kwasababu hatuyaoni kwa macho, wala hatuna sababu za kusema kwamba Malaika hawapo..kwasababu tu hatuwaoni.
Matukio mengi yanayoendelea sasa duniani, yanaanzia rohoni. Hata hii dunia tu yenyewe imeumbwa kutoka katika vitu visivyoonekana..kasome Waebrania 11:3.
Kwahiyo vitu vile visivyoonekana ndio vya kuvizingatia Zaidi kuliko vile vinavyoonekana.
2Wakorintho 4:18 “tusiviangalie vinavyoonekana, bali visivyoonekana. Kwa maana vinavyoonekana ni vya muda tu; bali visivyoonekana ni vya milele”.
Na pia vipo vitu vingine ambavyo hata kwa kutumia hizo hadubini havionekani lakini vipo..na tunaamini kuwa vipo..Kwamfano Ile “nguvu ya uvutano ya sumaki” haionekani kwa njia yoyote ile. Mpaka leo hakuna mtu wala mwanasayansi aliyegundua kifaa cha kuiona..Imebakia fumbo mpaka leo.
Vivyo hivyo ndugu, ulimwengu wa roho upo, huo hauonekani kwa macho, vipo viumbe vya rohoni pia navyo havionekani kwa macho, lakini madhara yake ni makubwa katika Maisha yetu.
Kama unakiogopa kirusi cha ukimwi usichokiona kisiingie mwilini mwako kwa kujitenga na uasherati.. Basi kuna viumbe vingine vibaya kuliko hivyo virusi ambavyo vinaweza kuingia mwilini mwako kwa njia hiyo hiyo ya uasherati,(mapepo) vitakavyokuletea madhara kwenye Maisha yako moja kwa moja. Pepo mmoja tu anayeweza kuingia katika Maisha yako kwa njia ya tendo moja tu la uasherati na ana uwezo wa kukuharibia Maisha yako moja kwa moja.
Kama unaogopa kupigwa shoti usiyoiona kwa kushika nyaya za umeme bila uangalifu, basi iogope dhambi kwasababu vipo vitu katika ulimwengu wa roho vibaya kuliko kuliko umeme.. ambavyo havionekani, vyenye uwezo wa kukusababishia hata kupoteza Maisha yako ghafla utakapovisogelea tu.
Biblia ndio “hadubini yetu”. Unaposoma Neno ni rahisi kuzigundua roho hizi na jinsi zinavyotenda kazi..na namna ya kujihadhari nazo. Kwamfano biblia inasema katika Mithali…
Mithali 6:32 “Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa; Afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake”
Hivyo mtu akilijua hili Neno na akaenda kinyume nalo, anakuwa amefungua mlango wa mapepo kuingia katika Maisha yake.. hataona kwa macho, lakini baada ya kipindi Fulani kupita ndipo atakapoona madhara yake. Madhara ya uasherati wengi wanafikiri ni yale ya kupata HIV tu basi!.. lakini hawajui kuwa mtu anaweza kutoka kufanya usherati leo na akaanguka ghafla tu na kupoteza Maisha, au akafa tu ghafla kifo kisichoeleweka, au akapata ajali au akapoteza tu ghafla kitu cha muhimu katika Maisha yake kama kazi, au heshima.
Bwana atusaidie kuyajua Zaidi mambo ya rohoni kuliko ya mwilini, na kutupa Imani Zaidi.. Nasema hivyo kwasababu siku chache tu nyuma nimekutana na pepo, kwa macho haya ya mwilini barabarani, ndipo Mungu akanipa somo kuwa hizi roho zinazurura huku duniani kutafuta watu kwa nguvu kuwaangamiza, na yanaongeza bidii siku hizi za mwisho kwasababu yanajua muda wao ni mchache, hivyo wanawinda watu kwa nguvu, ili kuwaangamiza.
Hivyo kuwa makini sana. Mambo rohoni sio kama unavyoyasikia. Ingia ndani ya Kristo uwe salama.
KITABU CHA UZIMA
MAFUNDISHO YA MASHETANI
MIHURI SABA
MTUMAINIE YESU ASIYEISHA MATUKIO.
UFUNUO: Mlango wa 6
Mavyaa ni nani?
Neno hilo tunalipata katika mstari huu kwenye biblia;.
Mika 7:6 “Kwa maana mwana humwaibisha babaye, na binti huondoka ashindane na mamaye; na mwanamke aliyeolewa hushindana na MAVYAAYE; adui za mtu ni watu wa nyumbani mwake mwenyewe. 7 Lakini mimi, nitamtazamia Bwana; nitamngojea Mungu wa wokovu wangu; Mungu wangu atanisikia”.
Mika 7:6 “Kwa maana mwana humwaibisha babaye, na binti huondoka ashindane na mamaye; na mwanamke aliyeolewa hushindana na MAVYAAYE; adui za mtu ni watu wa nyumbani mwake mwenyewe.
7 Lakini mimi, nitamtazamia Bwana; nitamngojea Mungu wa wokovu wangu; Mungu wangu atanisikia”.
Mavyaa ni Neno la kiswahili linalomaanisha mama-mkwe, – Yaani mama wa mke/mume wako.
Na kwa upande wa Baba-mkwe ni hivyo hivyo linabadilika na kuwa Bavyaa– Yaani baba wa mke/mume wako.
Hivyo kwenye mstari huo, tunapewa picha ya jinsi audui unavyoanza…Kwamba hauanzii mbali, labda kwa watu wasiotujua hapana, bali uadui wa kwanza sikuzote huanzia kwa watu nyumbani mwetu wenyewe, Lakini uadui hauji hivi hivi bali ni lazima uwe na sababu yake. Na ndio maana mstari ambao Bwana Yesu aliurejea alipokuwa anazungumzia habari za mtu kujikana nafsi yake pale anapotaka kumfuata yeye, ulikuwa ni huu, na alisema maneno haya:
Mathayo 10:34 “Msidhani ya kuwa nimekuja kuleta amani duniani; la! Sikuja kuleta amani, bali upanga. 35 Kwa maana nalikuja kumfitini mtu na babaye, na binti na mamaye, na mkwe na mkwe mtu; 36 na adui za mtu ni wale wa nyumbani mwake. 37 Apendaye baba au mama kuliko mimi, hanistahili; wala apendaye mwana au binti kuliko mimi, hanistahili. 38 Wala mtu asiyechukua msalaba wake akanifuata, hanistahili. 39 Mwenye kuiona nafsi yake ataipoteza; naye mwenye kuipoteza nafsi yake kwa ajili yangu ataiona”.
Mathayo 10:34 “Msidhani ya kuwa nimekuja kuleta amani duniani; la! Sikuja kuleta amani, bali upanga.
35 Kwa maana nalikuja kumfitini mtu na babaye, na binti na mamaye, na mkwe na mkwe mtu;
36 na adui za mtu ni wale wa nyumbani mwake.
37 Apendaye baba au mama kuliko mimi, hanistahili; wala apendaye mwana au binti kuliko mimi, hanistahili.
38 Wala mtu asiyechukua msalaba wake akanifuata, hanistahili.
39 Mwenye kuiona nafsi yake ataipoteza; naye mwenye kuipoteza nafsi yake kwa ajili yangu ataiona”.
Hivyo, katika wewe safari yako ya imani, (yaani umeokoka), ni lazima uweke akilini kuwa adui za kwanza kukupinga watakuwa ni watu wa nyumbani mwako, aidha watoto wako, au binti zako, au mavyaako, au bavyaako, au kaka zako, au wajomba zako au binamu zako n.k. Usitazamie vita vikubwa kutokea mbali.
Kwasababu adui za mtu ni watu wa nyumbani mwake mwenyewe. Hivyo ukikutana nayo ushingae, songa mbele, ishinde vita, Na Bwana atakuwa pamoja na wewe.
Tazama tafsiri ya maneno mengine ya biblia chini.
Daawa ni nini kama tunavyosoma katika biblia?
Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!
SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?
MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.
UTAWALA WA MIAKA 1000.