Mkuu wa anga ni nani?
Shalom karibu tuongeze maarifa ya kumjua Mungu wetu..na sio tu kumjua Mungu wetu bali hata kumjua adui yetu…Hata wanyama wa porini wasio na akili huwa wanajifunza kuwatambua marafiki zao na kadhalika maadui zao…Nyumbu atakakula nyasi pamoja na pundamilia na swala, lakini akimwona tu simba kwa mbali basi atakimbia kuyanusuru maisha yake..kwanini? ni kwasababu huko nyuma tayari alishajifunza kumjua adui yake ni nani…na rafiki yake ni nani. Na sisi wakristo tunapaswa tuwe hivyo hivyo…
Leo tutajifunza kwa ufupi juu ya wakuu wa anga…Sasa wapo wakuu wa giza na kadhalika wakuu wa anga..hizo ni roho mbili tofauti. Wakuu wa giza wapo saba…na wakuu wa anga wapo wengi.
Mkuu wa giza aliyepo sasahivi ni wa saba na wa mwisho. Huyu ndiye Pepo mwenye nguvu kuliko wale sita waliotangulia..na kazi zake rasmi zilianza kudhihirishwa mwanzoni mwa karne ya 20 na mpaka leo bado anaendelea kutenda kazi. Kazi yake kubwa huyu ni kuchochea giza Nene duniani..kwa kuwafanya watu wawe vuguvugu, ndiyo jukumu kubwa alilokabidhiwa na shetani.
Shetani anajua tunaishi katika siku za mwisho na muda wake umekaribia kuisha sana..hivyo anachokifanya ni kuwafanya watu wawe vuguvugu sana, na tageti yake sio mtu asiyeamini hapana, tageti yake ni mtu anayeiona kuwa ni mkristo…Anamfanya mtu awe nusu mshirikina nusu mwungwana..Nusu mwombaji nusu mzinzi, nusu mwimbaji wa nyimbo za kumsifu Mungu nusu mshabiki wa mambo na nyimbo za kidunia…Nusu mchungaji nusu mzinzi n.k Hataki kuwafanya watu wawe wazinzi moja kwa moja kwasababu anajua wakiwa baridi kabisa ni rahisi kushtuka usingizini na kutubu…anataka wawe vuguvugu ili iwe rahisi wao kujihesabia haki, na mwisho wa siku watakapokufa wajikute jehanamu badala ya mbinguni…
Ndio maana leo hii..utamwona mtu kavaa kikahaba, na ukijaribu kumwuliza umeokoka atakuambia ndio mimi nimeokoka na jana tu nilikuwa kanisani…huyo huyo ukiiangalia simu yake anaboyfriend ambaye anatembea naye..na ukijaribu kumwambia usipotubu utakwenda hukumuni atakwambia unamhukumu…na atakufunulia maandiko baadhi tu ilimradi ajionyeshe yeye yupo sawa…Sasa hilo ndio lengo kuu la shetani.
Lakini ukimfuata kahaba ambaye hana mpango kabisa na Mungu wala hajui habari za Mungu..ukimwambia tu kidogo habari za dhambi anazozifanya na kwamba asipogeuka atapotea..jambo la kwanza atakiri kuwa yeye ni mwenye dhambi, na hiyo inamfanya iwe rahisi kwake kutubu hata kwa kulia …Sasa shetani ndio kitu ambacho hakitaki hicho…anajua watu baridi kabisa ni rahisi kuigeukia injili…hivyo anafanya juu chini watu wawe vuguvugu. Ili iwe ngumu kumgeukia Mungu wao…
Na faida nyingine shetani anayoipata pindi watu wanapokuwa vuguvugu ni kutapikwa na Mungu…Anajua Mungu hapendezwi na watu vuguvugu..anasema ni heri mtu angekuwa baridi kabisa..yaani angekuwa mwasherati moja kwamoja au kahaba au muabudu sanamu moja kwa moja kuliko kuwa vuguvugu..amesema atamtapika.
Ufunuo 3:15 “Nayajua matendo yako, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri kama ungekuwa baridi au moto. 16 Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu. 17 Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi”.
Ufunuo 3:15 “Nayajua matendo yako, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri kama ungekuwa baridi au moto.
16 Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu.
17 Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi”.
Hiyo ndiyo kazi ya mkuu wa giza hili..Sasa chini yake wapo wapo wakuu wa anga…hawa kazi yao ni kukusanya taarifa za watu na kushinikiza kueneza uvuguvugu duniani kote..Ni kama Raisi alivyo na wakuu wake wa mikoa…ambao kazi yao ni kuifanya kazi ile ile ya Raisi katika mikoa waliyopo..ni kama wawakilishi wa Raisi huko katika majimbo yao.
Wakuu wa anga wanatumia anga kuleta madhara yao..Kama vile sisi wanadamu tutumiavyo anga kuharakisha maendeleo yetu..kwamba tunatumia anga kusafiri haraka kwa chombo kama ndege..tunatumia anga kurusha wawimbi yetu ya redio na tv pamoja na internet..kiasi kwamba mtu yupo Ulaya unaweza kumwangalia mtu mwingine hapa Tanzania mubashara dakika hiyo hiyo…Kadhalika tunatumia anga kuhifadhi vyombo vyetu kama satellite..ambayo hiyo inatusaidia kutabiri hali ya hewa, mabadiliko ya tabia ya nchi..kufuatilia maeneo tuliyopo..kwa kutumia tu simu yenye program ya satelaiti tunaweza kujiona mahali tulipo..mahali tunapokwenda hata tunaweza kuona mabati ya nyumba zetu…mbali na hayo hata vita vya siku hizi vikuu ni vya angani n.k
Sasa wakuu wa anga nao wanafanya mambo kama hayo kwa kutumia elimu zao za giza…wao hawatumii sayansi..lakini wanatumia elimu yao ambapo wanauwezo wa kujua kiwango cha uvuguvugu uliopo duniani..wanauwezo wa kumjua mtu mmoja mmoja..wana uwezo wa kujua wanadamu wanaomcha Mungu na wasiomcha Mungu..
Sasa mambo yote hayo wanaweza kuyajua kwa kutumia anga..ndio maana wanaitwa wakuu wa anga..Na lengo lao kubwa ni lile lile kuifanya dunia iwe vuguvugu..
Wanafanya vita na wakristo waliookoka na waliosimama kweli kweli…wanatafuta kila njia ya kumwangusha..ili awe vuguvugu!..watamtumia watu ili kumshawishi afanye uasherati…na maroho ambayo yatamwamshawishi na kumwambia mbona Daudi alifanya na akasamehewa?..Na wewe nenda kafanye uasherati utatubu tu!..Na mtu akishaingia huko kufanya dhambi za makusudi kama hizo baada ya kuujua ukweli Mungu anamtapika…Na siku zote hakuna mtu anayeweza kurudia matapishi yake..
Kadhalika mtu ni mlevi..shetani atamwambia usiwe mlevi siku zote hivyo..angalau toa toa sadaka…Na Yule mtu kwa kusikiliza ushawishi huo badala ya kutubu kabisa na kuacha ulevi ndipo akamtolee Mungu wake….yeye atakwenda kujifunza kumtolea Mungu sadaka na hali yake ya ulevi ile ile..akiamini kuwa moyoni Mungu anapendezwa na yeye…Na ukijaribu kumwambie atubu anasema yeye ni mkristo na ni mtoaji…ukiendelea zaidi anakwambia usimhukumu..Mtu wa namna hiyo tayari kashatimiza lengo la mkuu wa giza hili…(Soma Mhubiri 5:1) soma tena Mithali 15:8 “Sadaka ya mtu mbaya ni chukizo kwa Bwana; Bali maombi ya mtu mnyofu ni furaha yake”.
Mwambie mtu mizaha na matusi ni dhambi..usengenyaji ni dhambi, rushwa ni dhambi..atakwambia mimi naendaga kanisani na naijua biblia yote na natoa fungu la 10..Hicho ndicho kiburi shetani anachopambana kila siku kukiingiza ndani ya watu.
Bwana atusaidie sana shetani asitupate kwa njia hizo..Je! bado unamtii mkuu wa anga hili kwa kuendelea kuwa vuguvugu?..Au umesimama na kuwa moto?..bado unaendelea kuvaa vimini na huku unahudhuria kanisani?..bado unaendelea kupaka wanja, na kuvaa mawigi na unakwenda kanisani na unajiona upo sawa na Mungu…Yesu anakuambia..unajiona u utajiri lakini ni maskini, na mnyonge na mwenye mashaka…Lakini ametoa shauri kwamba utubu nawe utakuwa tajiri.
Waefeso 2:1 “Nanyi mlikuwa wafu kwa sababu ya makosa na dhambi zenu; 2 ambazo mliziendea zamani kwa kuifuata kawaida ya ulimwengu huu, na kwa kumfuata mfalme wa uwezo wa anga, roho yule atendaye kazi sasa katika wana wa kuasi; 3 ambao zamani, sisi sote nasi tulienenda kati yao, katika tamaa za miili yetu, tulipoyatimiza mapenzi ya mwili na ya nia, tukawa kwa tabia yetu watoto wa hasira kama na hao wengine”.
Waefeso 2:1 “Nanyi mlikuwa wafu kwa sababu ya makosa na dhambi zenu;
2 ambazo mliziendea zamani kwa kuifuata kawaida ya ulimwengu huu, na kwa kumfuata mfalme wa uwezo wa anga, roho yule atendaye kazi sasa katika wana wa kuasi;
3 ambao zamani, sisi sote nasi tulienenda kati yao, katika tamaa za miili yetu, tulipoyatimiza mapenzi ya mwili na ya nia, tukawa kwa tabia yetu watoto wa hasira kama na hao wengine”.
Na kumbuka Mkuu wa anga hili na mkuu wa giza hili hatuwashindi kwa kuingia kwenye maombi ya mfungo..wala kwa kurusha mishale ya moto angani…Tunamshinda tu kwa kuamua kubadilika na kumgeukia Kristo kikamilifu..kwa kuzikataa kazi za shetani zote…kama ulikuwa ni mwasherati unaamua kugeuka, ulikuwa mlevi unageuka na kuacha ulevi kwa imani…Na baada ya kugeuka, unatubu na kwenda kubatizwa..kisha Roho Mtakatifu ndani yako atakuongoza na kukutia katika kweli yote ya kimaandiko.
Na silaha nyingine ya kumshinda wakuu hao ni kulifahamu Neno, ambalo hiyo inatokana na kujifunza kusoma biblia mwenyewe na kujifunza sehemu nyingine tofauti tofauti..Ndani ya Biblia utajifunza kuhesabiwa haki kwa Imani..utajifunza kuukulia wokovu na kusimama thabiti..pamoja na kujua nguvu iliyopo katika jina la Yesu na damu ya Yesu.
Waefeso 6:12 “Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho. 13 Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama. 14 Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani, 15 na kufungiwa miguu utayari tupatao kwa Injili ya amani; 16 zaidi ya yote mkiitwaa ngao ya imani, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu. 17 Tena ipokeeni chapeo ya wokovu, na upanga wa Roho ambao ni neno la Mungu;”
Waefeso 6:12 “Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.
13 Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama.
14 Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani,
15 na kufungiwa miguu utayari tupatao kwa Injili ya amani;
16 zaidi ya yote mkiitwaa ngao ya imani, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu.
17 Tena ipokeeni chapeo ya wokovu, na upanga wa Roho ambao ni neno la Mungu;”
Bwana akubariki sana. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
MKUU WA GIZA.
JE VIBWENGO NI KWELI VIPO?
NGUVU ILIYOPO KATIKA MAAMUZI.
ASKOFU MKUU NA MCHUNGAJI MKUU NI NANI?
MTINI, WENYE MAJANI.
Rudi Nyumbani:
Print this post
SWALI: Shalom Naomba kuuliza Je, ni halali kwa mimi kumuoa binti ambaye alishazaa na mtu mwingine bila kuishi nae Je, naweza kufunga naye ndoa ya kikristo na ikawa halali?
JIBU: Hapo yapo mambo mawili. Ikiwa binti huyo alikuwa ameshaolewa, halafu akaachika kwa sababu yoyote ile, labda pengine amekosana na mume wake, au amefumaniwa katika uzinifu na hivyo ameachwa, au sababu nyingine yoyote tofauti na kifo cha mumewe tu! Au kwasababu ya kufukuzwa kwa ukristo wake..Mtu huyu hapaswa kuolewa na mwanamume yeyote Yule.. Maana akifanya hivyo biblia inasema anazidi, na Yule pia aliyemuoa biblia inasema naye pia azini.
Marko 10:11 “Akawaambia, Kila mtu atakayemwacha mkewe na kuoa mwingine azini juu yake; 12 na mke, akimwacha mumewe na kuolewa na mtu mwingine, azini”.
Marko 10:11 “Akawaambia, Kila mtu atakayemwacha mkewe na kuoa mwingine azini juu yake;
12 na mke, akimwacha mumewe na kuolewa na mtu mwingine, azini”.
Luka 16:18 Kila amwachaye mkewe na kumwoa mke mwingine azini; naye amwoaye yeye aliyeachwa na mumewe azini.
Hivyo ili uwe katika mkono salama, usiangukie hukumu, ikiwa umegundua mwanamke huyo yupo katika hali hiyo unapaswa umuache mara moja..hata kama ulishazaa naye watoto.
Lakini kama mwanamke huyo, alipata tu mimba akiwa katika dhambi, kwa uasherati, Hivyo na baadaye akaja akatubu na kumgeukie Mungu wake. Na sasa anataka kwenda kuolewa basi hapo ni uchaguzi wako mwenyewe wewe unayetaka kuoa, ukiridhia kuwa naye katika hali hiyo akiwa na watoto, ni sawa hakuna shida yeyote ukimuoa, kwasababu hapo mwanzo alikuwa hajaolewa. Lakini kama hajaridhia hafanyi dhambi pia kutokumuoa, ukitafuata ambaye hana watoto.
Na hiyo inalenga pande zote mbili, hata na kwa mwanaume pia..Ikiwa ameacha ndoa yake akaenda kuoa tena, biblia inasema azini, na Yule aliyeolewa naye vilevile azini..Lakini kama alikuwa hajaoa, lakini kazaa katika uzinzi na sasa amemgeukia Mungu katubu na amekuwa mkristo, anaweza akaoa, na isiwe anafanya dhambi mbele za Mungu.
Hizi ndio sababu pekee zinazoweza kumfanya mtu iwe halali kwake kuoa/kuolewa na mtu ambaye tayari anao watoto.
Ubarikiwe.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
NDOA NA HARUSI TAKATIFU.
Je! ni halali kutoa cheti kwa wakristo wanaooa?
NDOA NA TALAKA:
Yeshuruni ni nani katika biblia?
Nini Tofauti kati ya uzinzi na uasherati ?
Shalom, Ni siku nyingine Bwana ametupa kuiona kwa neema zake, hivyo nakukaribisha tuzidi kuyatafakari maneno ya uzima..
Leo tutajifunza juu ya wazazi wa mitume wawili wa Yesu, (Yohana na Yakobo)..Na tutaona pia ni jinsi gani wazazi wanavyoweza kuyaathiri maisha ya watoto wao ya rohoni kwa kiasi kikubwa. Kama tulivyotangulia kuona katika masomo yaliyopita, kwamba mzazi akimlea mtoto wake, na kumfundisha kumuheshimu, Basi Mungu anaamvika kilemba cha neema kichwani pake. Na neema hiyo si nyingine Zaidi ya ile ya kumjua Kristo kwa mapana yake na marefu yake(Mithali 1:8-9) na kuja kuwa msaada kwa wengine.
Na tutaona pia mwitikio wa wazazi jinsi unavyopaswa uwe kwa watoto wao pale wanapochukua uamuzi wa kumfuata Yesu. Tutajifunza kwa kuziangalia tabia za wazazi wa Yohana na Yakobo. Lakini awali ya yote,nataka utafakari jambo hili, Ulishawahi kujiuliza kwanini miongoni wa wale mitume 12 ni watatu tu ndio waliokuwa karibu sana na Yesu?.
Na miongoni mwa hao watatu, wawili walikuwa ndugu, na huyo mwingine ni Petro. Na mtume ambaye alipendwa na Yesu kuliko wote, ambaye kila wakati alikuwa akiegema kifuani mwa Yesu alikuwa ni mmojawapo wa hao wawili..Ni kwanini? Je! Mitume wengine walikuwa na mapungufu mengi? Jibu ni Hapana…Lakini kwanini Yesu aliwapenda hao wawili mpaka akawapa jina lao spesheli, akawaitwa Boanerge yaani wana wa ngurumo..(Soma Marko 3:17).
Yote hayo si kwa bidii zao tu peke yake lakini pia juhudi za wazazi zilichangia,..Embu tuwatazame kwa ufupi wazazi hawa tukianzana na Baba yao..tusome.
Mathayo 4:18 “Naye alipokuwa akitembea kando ya bahari ya Galilaya, aliona ndugu wawili, Simoni aitwaye Petro, na Andrea nduguye, wakitupa jarife baharini; kwa maana walikuwa wavuvi. 19 Akawaambia, Nifuateni, nami nitawafanya kuwa wavuvi wa watu. 20 Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata. 21 Akaendelea mbele, akaona ndugu wengine wawili, Yakobo wa Zebedayo, na Yohana nduguye, ambao walikuwamo chomboni pamoja na Zebedayo baba yao, wakizitengeneza nyavu zao; akawaita. 22 Mara wakakiacha chombo na baba yao, wakamfuata”.
Mathayo 4:18 “Naye alipokuwa akitembea kando ya bahari ya Galilaya, aliona ndugu wawili, Simoni aitwaye Petro, na Andrea nduguye, wakitupa jarife baharini; kwa maana walikuwa wavuvi.
19 Akawaambia, Nifuateni, nami nitawafanya kuwa wavuvi wa watu.
20 Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata.
21 Akaendelea mbele, akaona ndugu wengine wawili, Yakobo wa Zebedayo, na Yohana nduguye, ambao walikuwamo chomboni pamoja na Zebedayo baba yao, wakizitengeneza nyavu zao; akawaita.
22 Mara wakakiacha chombo na baba yao, wakamfuata”.
Mwanzoni kabisa mwa wito, Yesu alipowaona vijana hawa wawili kuwa wanamfaa kwa kazi yake ya utume..Moja kwa moja alikwenda na kuwaita wakiwa katikati ya baba yao..katikati ya biashara ya baba yao waliyokuwa wanaifanya..Lakini Utaona baba yao hakuleta ukinzani wowote katika jambo hilo,..Aliwaachilia Watoto wake waende kwa moyo wote, afadhali ingekuwa ni mmoja, bali aliwaacha wote wawili wamfuate Yesu..
Jambo ambalo, si rahisi kwa mzazi yeyote wa kawaida wa leo kufanya hivyo, kuwaachilia Watoto wake wamtumikie Kristo,..Lakini kwake ilikuwa tofuati hakuona shida aachiwe vyombo vyake vya kazi, aitende kazi ile peke yake,pamoja na watu wa mshahara na uzee wake ilimradi tu wanawe waupate wokovu..
Tukimwangalia mama tena..
Mathayo 20:20 “Ndipo mama yao wana wa Zebedayo akamwendea pamoja na wanawe, akamsujudia, na kumwomba neno. 21 Akamwambia, Wataka nini? Akamwambia, Agiza kwamba hawa wanangu wawili waketi mmoja mkono wako wa kuume, na mmoja mkono wako wa kushoto, katika ufalme wako. 22 Yesu akajibu akasema, Hamjui mnaloliomba. Je! Mwaweza kunywea kikombe nitakachonywea mimi? Wakamwambia, Twaweza. 23 Akawaambia, Hakika mtakinywea kikombe changu; lakini kuketi mkono wangu wa kuume na mkono wangu wa kushoto, sina amri kuwapa, bali watapewa waliowekewa tayari na Baba yangu.
Mathayo 20:20 “Ndipo mama yao wana wa Zebedayo akamwendea pamoja na wanawe, akamsujudia, na kumwomba neno.
21 Akamwambia, Wataka nini? Akamwambia, Agiza kwamba hawa wanangu wawili waketi mmoja mkono wako wa kuume, na mmoja mkono wako wa kushoto, katika ufalme wako.
22 Yesu akajibu akasema, Hamjui mnaloliomba. Je! Mwaweza kunywea kikombe nitakachonywea mimi? Wakamwambia, Twaweza.
23 Akawaambia, Hakika mtakinywea kikombe changu; lakini kuketi mkono wangu wa kuume na mkono wangu wa kushoto, sina amri kuwapa, bali watapewa waliowekewa tayari na Baba yangu.
Embu jaribu kutafari mama huyu alivyokuwa anawatakia mema Watoto wake, aliona kufuatana na Yesu tu haitoshi hapa duniani haitoshi, bali pia wawe karibu na Yesu hata katika huo ulimwengu unaokuja. Alikuwa anawatafutia tu fursa nzuri Watoto wake huko mbeleni.. Wewe unadhani Watoto hao..wataachaje kupendwa na YESU, na kuwa vinara kwa Kristo. Kwasababu hawamtumikii Kristo kwa presha, bali kwa sapoti yote kutoka hata kwa wazazi wao.
Unadhani, wazazi wa mitume wengine walikuwa hawajui kuwa Watoto wao wanatumika na Bwana?. Walikuwa wanajua sana, lakini hakuna hata mmoja mzazi wake anaorodheshwa katika huduma za Yesu isipokuwa wazazi wa hawa vijana wawili.
Pengine walikuwa hawaoni umuhimu wowote, wa wao kuongozana na Yesu..Wameacha shughuli zao, fedha zao, biashara zao, ya nini tena kuwasapoti..hawakuwa na muda..Lakini wazazi wa mitume hawa wawili walikuwa bega kwa bega na Watoto wao, hadi hatua ya mwisho kuhakikisha kuwa hawamkosi Yesu..Na mwishowe wakawa miongoni mwa wale watatu waliopendwa na Yesu.
Hata leo hii, ikiwa wewe ni mzazi, au unajiandaa kuwa mzazi..Utakapomwona mtoto wako anaonyesha uelekeo wa kumpenda Mungu, unapaswa uwe wa kwanza kumsapoti. Kama unaweza kuwa wa kwanza kumsapoti kumnunulia kitabu cha shuleni, kwanini usimsapoti kumnunulia biblia, na vitabu vyenye mafundisho ya Neno la Mungu. Kwanini usimweke chini wa wachungaji wako wamfundishe Neno la Mungu?..Unajuaje kuwa kwa bidii yako hiyo utamkuza Samweli, au Yakobo, au Yohana?.
Bwana atusaidie tunapojifunza mifano ya wazazi hawa ili na sisi tuwe na mioyo kama hiyo hiyo kwa Watoto wetu.
Ubarikiwe sana. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
VIGEZO VYA KUWA KARIBU NA YESU KRISTO KATIKA ULIMWENGU UJAO.
Roho, Nafsi, na Mwili vina utofauti gani?
KUTOKUIHUBIRI INJILI,KUNA MADHARA GANI?
Ni sahihi kumuita Mariamu mama wa Mungu?
Je! ni sahihi kwa Mkristo kusherekea siku yake ya kuzaliwa.[Birth day]?
Lakini haitakuwa hivyo kwenu.
Shalom, Karibu tuzidi tujifunze Neno la Mungu.
Mathayo 20: 24 “Na wale kumi waliposikia, waliwakasirikia wale ndugu wawili. 25 Lakini Yesu akawaita, akasema, Mwajua ya kuwa wakuu wa Mataifa huwatawala kwa nguvu, na wakubwa wao huwatumikisha. 26 Lakini haitakuwa hivyo kwenu; bali mtu ye yote anayetaka kuwa mkubwa kwenu, na awe mtumishi wenu; 27 na mtu ye yote anayetaka kuwa wa kwanza kwenu na awe mtumwa wenu; 28 kama vile Mwana wa Adamu asivyokuja kutumikiwa, bali kutumika, na kutoa nafsi yake iwe fidia ya wengi”.
Mathayo 20: 24 “Na wale kumi waliposikia, waliwakasirikia wale ndugu wawili.
25 Lakini Yesu akawaita, akasema, Mwajua ya kuwa wakuu wa Mataifa huwatawala kwa nguvu, na wakubwa wao huwatumikisha.
26 Lakini haitakuwa hivyo kwenu; bali mtu ye yote anayetaka kuwa mkubwa kwenu, na awe mtumishi wenu;
27 na mtu ye yote anayetaka kuwa wa kwanza kwenu na awe mtumwa wenu;
28 kama vile Mwana wa Adamu asivyokuja kutumikiwa, bali kutumika, na kutoa nafsi yake iwe fidia ya wengi”.
Jinsi dunia inavyoenenda ni tofauti kabisa na wakristo wanavyopaswa kuenenda…Kama Bwana Yesu alivyosema hapo juu, watu wa mataifa huwatawala kwa nguvu na mkubwa wao huwatumikisha…lakini haitakuwa hivyo kwenu..Ikifunua kuwa hekima ya dunia hii ni kinyume na hekima ya Mungu…Hekima ya dunia hii, mdogo anamtumikia Mkubwa…lakini Hekima ya kimbinguni mkubwa ndiye anayemtumikia mdogo….
Hekima ya kidunia inasema ukimbilie ukubwa ili usiwe mtumwa…lakini hekima ya kimbinguni inasema ukimbilie udogo ili uwe mkubwa…
Hekima tena ya kidunia inasema…Mpende akupendaye na umchukie anayekuchukia…lakini hekima ya kimbinguni inasema “mpende adui yako mwombee yeye anayekuudhi”..adui yako akiwa na njaa mlishe, akiwa na kiu mnyweshe…(Soma Mathayo 5:44 na Warumi 12:20).
Hekima ya dunia hii inasema ukiipatia nafsi yako kila kitu chema cha ulimwengu huu ndio maana ya maisha…lakini hekima ya Mungu inasema “aipataye nafsi yake ataipoteza na aipotezaye kwa ajili ya Kristo ataipata”…Kwahiyo karibia mambo yote ya ulimwengu yanakwenda kinyume na hekima ya Mungu…Ndio maana inakuwa ni ngumu mtu wa kidunia kumwambia kwamba kuna siku hii dunia tunayoishi itafikia mwisho na kwamba mwisho huo umekaribia sana na siku moja hili jua tunaloliona litatiwa giza…atakuona ni mtu wa ajabu kwasababu yeye anaona dunia mbona bado ni mahali salama?..itawezekanikaje jambo hilo..kwamba eti siku moja jua litiwe giza?..Atakuona kuna kau-pumbavu Fulani kapo kichwani mwako..
Ndio maana biblia ikasema…
katika 1 Wakorintho 1:18 “Kwa sababu neno la msalaba kwao wanaopotea ni upuzi, bali kwetu sisi tunaookolewa ni nguvu ya Mungu.
19 Kwa kuwa imeandikwa, Nitaiharibu hekima yao wenye hekima, Na akili zao wenye akili nitazikataa.
20 Yu wapi mwenye hekima? Yu wapi mwandishi? Yu wapi mlete hoja wa zamani hizi? Je! Mungu hakuifanya hekima ya dunia kuwa ni upumbavu?
21 Kwa maana katika hekima ya Mungu, dunia isipopata kumjua Mungu kwa hekima yake, Mungu alipenda kuwaokoa waaminio kwa upuzi wa lile neno linalohubiriwa.”
Unaona?..Hebu leo hii itafute hii hekima ya Mungu..ambayo imekataliwa na watu wengi…kama wewe ni mkristo na ulikuwa hujui kwamba unapaswa uwapende wanaokuchukia anza kufanya hivyo leo…Usiisikilize hekima ya dunia ambayo kwa nje inaonekana ni tamu, lakini mwisho wake ni upotevu…inayokuambia usimwache adui yako kuishi…na mbaya Zaidi hekima hiyo ya kidunia imeshaanza kuhubiriwa hata mpaka makanisani kana kwamba ni hekima ya ki-Mungu.
Kama ulikuwa hujui kwamba ili uwe mkubwa kuliko wote ni sharti uwe mdogo kuliko wote..anza kufanya hivyo leo…Kama wewe ni boss mahali ulipo tumika kana kwamba wewe sio boss tumika kuliko hata wale uliowaajiri…kuwa mpole kuliko yule mfanyakazi wa chini kabisa uliomwajiri…Ndivyo mbele za Mungu utakavyoonekana Mkubwa…Na ndivyo Mungu atakavyozidi kukupandisha juu. Mungu anasema Musa alikuwa ni mtu aliyekuwa mpole kuliko wote ulimwenguni, lakini kwa kupitia upole wake Mungu alimfanya kuwa kichwa cha wana wa Israeli.(Hesabu 12:3).
Bwana Yesu alikuwa ni mkubwa kuliko wote lakini aliwaosha miguu wanafunzi wake ambao wengine hata walimsaliti na kumkana..Na pamoja na kujua kuwa atasalitiwa na kukanwa lakini aliwaosha miguu hivyo hivyo na kuendelea kula nao na kunywa nao kwa upendo wote…Je wewe unaweza kufanya hivyo kwa watu waliopo chini yako?..ambao unajua kabisa wamekufanyia hiki au kile?..Kama huwezi basi tambua una hekima ya ulimwengu huu lakini hauna hekima ya ki-Mungu.
Na mambo mengine yote ni vivyo hivyo..Hekima hii inaingia ndani ya mtu kwa kujifunza Neno la Mungu…kuna tofauti kati ya kusoma na kujifunza…
Kujifunza Maana yake unajiingiza mwenyewe kwenye darasa ambalo utausoma mstari na kuutafakari kwa kina na kwa msaada wa Roho kupata ufunuo kutoka katika huo mstari..Na hauhusomi wakati kichwa chako kimevurugika na mambo mengine ya ulimwengu…hakikisha unapata utulivu wa kutosha…katika hali ya utulivu ndipo sauti ya Mungu inasikika..Roho Mtakatifu ataanza kukufundisha jambo moja baada ya lingine..na utaona mwenyewe kwa jinsi gani dunia ipo mbali na hekima ya Mungu…na hata wewe binafsi ulivyokuwa mbali na hekima ya Mungu.
Vilevile kama tutaipuuzia hii hekima ya Mungu na kujiona tunajua Zaidi ya Neno lake..Basi tufahamu kuwa Hekima hiyo mbele za Mungu ni upuuzi..
1Wakorintho 3:18 Mtu asijidanganye mwenyewe; kama mtu akijiona kuwa mwenye hekima miongoni mwenu katika dunia hii, na awe mpumbavu, ili apate kuwa mwenye hekima. 19 Maana hekima ya dunia hii ni upuzi mbele za Mungu. Kwa maana imeandikwa, Yeye ndiye awanasaye wenye hekima katika hila yao. 3.20 Na tena, Bwana anayafahamu mawazo ya wenye hekima ya kwamba ni ya ubatili.
1Wakorintho 3:18 Mtu asijidanganye mwenyewe; kama mtu akijiona kuwa mwenye hekima miongoni mwenu katika dunia hii, na awe mpumbavu, ili apate kuwa mwenye hekima.
19 Maana hekima ya dunia hii ni upuzi mbele za Mungu. Kwa maana imeandikwa, Yeye ndiye awanasaye wenye hekima katika hila yao.
3.20 Na tena, Bwana anayafahamu mawazo ya wenye hekima ya kwamba ni ya ubatili.
Bwana akubariki. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
MAOMBI KWA WENYE MAMLAKA.
JE SALA YA ROZARI TAKATIFU NI YA KIMAANDIKO?
Kwanini yule mtu hakukutwa na vazi la arusi wakati alialikwa?
KUVUNJA MAAGANO YA UKOO.
Je ni wakina nani ambao hawataonja mauti mpaka siku ya kuja Bwana?
Moja ya maswali yanayoulizwa na wengi ni kutaka kujua juu ya Historia ya Israeli/Taifa la Israeli/Wana wa Israeli..Lakini kiuhalisia historia ya Israeli ipo kwenye biblia. Ukisoma kitabu cha Mwanzo, Kutoka, Mambo ya Walawi, Kumbukumbu la Torati, hesabu, Yoshua, waamuzi pamoja na vitabu vya wafalme..vimeelezea vizuri sana kuhusu Taifa la Israeli/wana wa Israeli…
Hakuna mahali popote ambapo pameelezea vizuri historia ya Israeli kama kwenye Biblia takatifu..Hata kurasa kama Wikipedia na kamusi nyingine zote..zinatoa taarifa zao kuhusu Taifa la Israeli kwa kunukuu kutoka kwenye Biblia..Hivyo hakuna mahali pengine historia ya Taifa hilo inaweza kupatikana isipokuwa katika Biblia takatifu. Tatizo kubwa tulilonalo wengi wetu hatupendi kusoma Biblia, badala yake tunapenda kutafuta kusimuliwa au kufupishiwa habari fulani na watu ambao tayari wameshaisoma.
Hivyo hakuna tabia nzuri kama tabia ya kusoma Neno la Mungu..Matokeo ya kutolisoma Neno la Mungu (yaani Biblia) na kusubiriwa kutafsiriwa..Ni mwishowe kudondokea katika mikono ya mawakala wa shetani..ambao kazi yao ni kuipotosha kweli na kuingiza uongo katikati ya kweli. Na mtu akishadanganywa hawezi kujua kama kadanganywa au la..kwasababu hasomi biblia mwenywe.
Hivyo leo tuitazame kwa ufupi Historia ya Israeli.
Taifa la Israeli lilianza kwa ahadi…Yaani mtu mmoja aliyeitwa Ibrahimu alimpendeza Mungu, Hivyo Mungu akamwahidi kuwa atakuwa Taifa kubwa.
Mwanzo 12:1 “Bwana akamwambia Abramu, Toka wewe katika nchi yako, na jamaa zako, na nyumba ya baba yako, uende mpaka nchi nitakayokuonyesha; 2 nami nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, na kukubariki, na kulikuza jina lako; nawe uwe baraka; 3 nami nitawabariki wakubarikio, naye akulaaniye nitamlaani; na katika wewe jamaa zote za dunia watabarikiwa”
Mwanzo 12:1 “Bwana akamwambia Abramu, Toka wewe katika nchi yako, na jamaa zako, na nyumba ya baba yako, uende mpaka nchi nitakayokuonyesha;
2 nami nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, na kukubariki, na kulikuza jina lako; nawe uwe baraka;
3 nami nitawabariki wakubarikio, naye akulaaniye nitamlaani; na katika wewe jamaa zote za dunia watabarikiwa”
Ahadi hiyo ilianza kutimia baada ya Ibrahimu kupata mtoto wa kwanza wa kiume..ambaye alimwita Isaka (Alikuwa na mwingine aliyemwita Ishmaeli lakini Ishmaeli hakuwa mwana wa Ahadi kwasababu alizaliwa na mwanamke mwingine)..Baadaye Isaka akamzaa Yakobo..Na Yakobo ambaye ni mjukuu wa Ibrahimu akazaa watoto 12. Hawa watoto 12 wa kiume waliozaliwa na Yakobo…waliitwa wana wa Yakobo…au watoto wa Yakobo…
Lakini ulipofika wakati fulani Yakobo jina lake lilibadilishwa na kuwa ISRAELI…Tafsiri ya jina Israeli ni “MSHINDI”. Hivyo kama jina lake limebadilika kadhalika na watoto wake hawakuitwa tena wana wa Yakobo bali wana wa ISRAELI. Na majina yao yalikuwa ni RUBENI, LAWI, ZABULONI, ISAKARI, NAFTALI, DANI, YUDA, SIMEONI, GADI, ASHERI, YUSUFU, na BENYAMINI.
Hawa wana 12, walioa wake na kuzaa watoto wengi..na watoto wao nao pia wakaoa na kuzaa watoto na wajukuu na vitukuu..Hatimaye Taifa likaanza kuwa kubwa na kufikia watu elfu 10, elfu 20, laki mpaka milioni..Kila kizazi kilichokuwa kinatokea kilirekodiwa asili ya Baba yake wa kwanza…kama ni Rubeni, au Lawi, au Gadi au mwingine yoyote alijulikana asili yake…Hivyo majina ya Baba zao yakageuzwa na kuwa MAKABILA YAO. Hivyo kila mtu alikuwa na kabila lake miongoni mwa yale 12.
Sasa Kuna mambo waliyafanya wana wa Israeli yakawapeleka Misri, ambapo waliingia kwa amani lakini wakatoka kwa ushindani mkali. Baada ya kutolewa Misri na mkono wa Mungu mwenyewe…walianza safari ya kuelekea nchi ya Ahadi. Ijulikanayo kama KAANANI. Iliwachukua miaka 40 kukamilisha safari yao mpaka kufikia nchi ya Ahadi…Wakiwa njiani ndio huko huko Mungu akawa anazungumza nao na kuwapa AMRI za kuzishika na SHERIA ili wakafanikiwe wanapoiendea hiyo nchi ya Ahadi. Amri hizo zikiwemo kumtumikia na kumsujudia Mungu wao mmoja tu yeye peke yake aliyewatoa katika nchi Misri, nyumba ya utumwa…nyingine ni kuwaheshimu wazazi, kutokuiba, kutokuzini n.k
Walipoingia nchi ya Ahadi waligawanyiwa nchi hiyo kulingana na makabila yao.. kabila lenye watu wengi lilipewa sehemu kubwa ya ardhi, kadhalika lenye watu wachache lilipewa urithi mdogo.
Wana wa Israeli walipitia vipindi virefu vya kumsahau Mungu na kumrudia..Kizazi kilichofanya mabaya zaidi kiliadhibiwa na Mungu..na kile kilichofanya vizuri katika kuzishika amri na sheria za Mungu kilibarikiwa na kufanikiwa. Hivyo Mungu aliwafikisha katika nchi hiyo na kuwafanya kuwa wengi sana mamilioni..Na kutimiza Ahadi Mungu aliyemwahidia Ibrahimu.
Ilipofika wakati wa Ahadi ya Mungu kuuokoa ulimwengu..alimtuma mwanawe mpendwa ambaye alizaliwa katika Taifa hilo la Israeli…katika mnyororo wa kabila la YUDA. Yesu alizaliwa Maskini lakini alikuwa Mfalme..alikufa kifo cha aibu lakini alipofufuka alipata heshima…Yesu alifanyika kuwa wokovu kwa waisraeli wenyewe pamoja na watu wa mataifa.
Watu wa Mataifa ni watu wa mataifa mengine yote tofauti na taifa la Israeli. Waisraeli jina lingine wanaitwa WAYAHUDI..Wayahudi ndio hao hao waisraeli..hivyo uonapo mahali popote wanataja wayahudi basi fahamu kuwa ni hao hao waisraeli…sehemu nyingine wanatajwa kama Waebrania.
Taifa la Israeli lilijulikana kama Taifa teule la Mungu kwasababu ndio Taifa pekee duniani kote ambalo lilikuwa linamuabudu Mungu wa kweli YEHOVA. Aliyeumba mbingu na nchi…Mataifa mengine yaliyosalia yalikuwa yanaabudu sanamu, mizimu, miti na wanadamu. Ni Israeli pekee ndilo lililokuwa linamwabudu Mungu wa kweli..Ndio maana likaitwa Taifa Teule.
Mpaka leo Taifa hili bado lipo…na bado ni kipenzi cha Mungu…Ingawa wayahudi sasa hawamwamini Yesu kama Masihi.. lakini biblia imetabiri katika siku za mwisho watamwagiwa roho ya Neema na watamkubali Kristo.
Kijeografia, Taifa hili lipo katika Bara la ASIA, Eneo linalojulikana kama mashariki ya kati…Waisraeli kimwonekano wanakaribia kufanana na waarabu lakini si waarabu, wapo wayahudi pia wanaoishi mataifa mengine ya nje….Na nchi ya Israeli ni ndogo tu kama Mkoa wa Njombe wa Tanzania, lakini ina utajiri mwingi japokuwa asilimia kubwa ni jangwa…Na kwa sehemu watu wake wamejaliwa kuwa na uwezo wa ubunifu na uvumbuzi.
Idadi ya waisraeli waliopo Israeli sasahivi inakadiriwa kuwa Milioni 9. Nchi ya Israeli ndiyo nchi pekee duniani yenye idadi kubwa ya maadui kuliko nchi nyingine zote..Kwani imezungukwa na nchi za kiarabu pande zote ambazo zinalipinga vikali Taifa hilo.
Pamoja na maadui wote hao lakini bado Mungu anawashindania. Kwasababu anakusudi nao katika siku za mwisho. Kwani baada ya unyakuo wa kanisa kupita Mungu atalirudia tena Taifahilo kwa nguvu na kuwapa watu wake moyo wa Toba…Wayahudi wote watatubu kwa machozi na maombolezo kwa uchafu wote wanaoufanya na kwasababu walimsulibisha Masihi wao…na Bwana atawaasamehe na kuanza kuwashindania tena kama nyakati za kale…na mataifa yote yatapanga vita dhidi ya Taifa hilo na Mungu atalishindia yote..
Hatuwezi kuandika mambo yote hapa kuhusu Taifa hilo…lakini kwa urefu kasome binafsi biblia hususani vile vitabu vitano vya Musa, ukihitaji kujua kama Israeli ilikuwa na mfalme au la kasome kitabu cha Wafalme..Ukitaka kujua kama Israeli ilishawahi kwenda utumwani tena kwa mara nyingine kasome kitabu cha Mambo ya nyakati..Ukitaka kujua kuhusu Hekalu la Mungu lililokuwepo Israeli kasome kitabu cha Wafalme…Ukitaka kujua Makuhani walikuwa ni wakina nani, na majukumu yao, na mavazi na kwa jinsi gani sadaka zilikuwa zinatolewa katikakati ya wana wa Israeli kasome kitabu cha mambo ya walawi…
Ukitaka kujua kwa urefu safari ya wana wa Israeli..mambo yaliyowakuta njiani wakati wanakwenda kaanani kasome kitabu cha Hesabu..Ukitaka kujua ni kwa namna gani walishindana vita na kutwaa urithi wao wakati wanaingia kaanani kasome kitabu cha Yoshua.
Ukitaka kujua sheria walizopewa, na hukumu pamoja na ahadi na aina ya vyakula walivyoamuriwa wale na vile walivyoambiwa wasile kasome kitabu cha kumbukumbu la Torati..Na ukitaka kujua ni kwa jinsi gani watarudiwa katika siku hizi za mwisho kasome kitabu cha Warumi.
Na mengine baadhi fungua masomo mengine mwisho wa somo hili..
Je umeokoka?..una uhakika wa kwenda mbinguni?..Kumbuka yeye ajaye anakuja upesi wala hatakawia.
WAISRAELI WENGI SANA WANARUDI KWAO SASA.
NG’OMBE MWEKUNDU ALIYEZALIWA ISRAELI, ANAFUNUA NINI?
MAMBO YATAKAYOTOKEA ISRAELI SIKU ZA HIVI KARIBUNI.
BONDE LA KUKATA MANENO.
NITAFANYA YERUSALEMU KUWA JIWE LA KUWALEMEA .
MPAKA UTIMILIFU WA MATAIFA UTAKAPOWASILI.
Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!
WhatsApp
Mithali 11:24 “Kuna atawanyaye, lakini huongezewa zaidi; Kuna azuiaye isivyo haki, lakini huelekea uhitaji”.
Shalom, Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe. Karibu tena tuyatafakari maandiko.
Kuna kanuni Mungu kaziweka katika maisha ambazo ni vizuri tukazielewa ili tusije tukajikuta tunaangamia kwa kukosa maarifa, na kukosa maarifa ni pamoja na kuhangaika huku na huko kutafuta maombezi wakati misingi ya Neno la Mungu iliyo imara tumeiacha nyuma..
Kwamfano mtu anaweza akawa anasumbuliwa na tatizo Fulani labda tuseme, na nguvu za giza,.. lakini kwa kukosa tu maarifa ya kujua kwamba damu ya Yesu Kristo ndiyo inayoondoa mizizi yote ya nguvu za giza ndani ya mtu, pale anapoamua tu kuokoka kwa kumaanisha na kubatizwa..Sasa mtu huyo kwa kutolizingatia hilo anataka mambo hayo yaondolewe kwa njia ya maombezi na huku bado yupo katika dhambi, bado ni mzinzi, bado anaishi na mke/mume ambaye si wake, bado ni mlevi, bado anavaa mavazi yake ya kikahaba, na wakati huo huo anataka kuombewa mapepo yamtoke.
Sasa Kwa namna ya kawaida mapepo hayo hayamwacha yamesoge pembeni tu. Atajiona kama amepata tu unafuu, lakini baada ya muda tena hali yake itamrudia, na itakuwa mbaya zaidi kuliko hata ilivyokuwa hapo mwanzo.
Hiyo yote ni kutokana na kukosa maarifa sahihi ya kulitatua tatizo lake.
Jambo lingine ambalo tunapaswa tujifunze pia, Ni katika suala la utoaji. Kwa hali ya kibinadamu kutoa huwa ni kugumu kuliko kupokea..Licha ya kuwa utoaji ni nguzo muhimu kwa mtu yeyote Yule (awe mwenye dhambi asiwe mwenye dhambi )…
Lakini linapuuziwa na wengi hata na kwa watu waliookoka.
Lakini fahamu kuwa ukitaka uwe mtoaji mzuri, unapaswa uishinde hali yako ya sasa.. “Hali zetu ni adui mkubwa wa matoleo yetu”…Siku zote ukiangalia hali yako ilivyo, ukianza kupiga gharama hujafanya hiki, hujafanya kile, hata kama wewe ni bilionea utoaji wako bado utakuwa ni mgumu tu, ..kwasababu Utawaza sijawekeza kwenye hichi au kwenye kile. Vivyo vivyo hata na kwa Yule aliye na kipato cha kawaida naye akishaanza kujifikiria tu hali yake ilivyo, sijanunua, tv, sijanunua simu, sijanunua viatu, n.k. basi utoaji wake naye ndipo unapopitia ukinzani.
Kwasababu kile alichonacho hakitamtosha kukidhi matakwa yake, na huku tena afikirie kumsaidia mtu mwingine bado itakuwa ngumu, au kutoa sadaka hapo hapo kwake yeye vilevile itakuwa ngumu. Nataka nikumbie kila siku tutakuwa na uhitaji tu, hatutakoma kuwa na mahitaji hata tufanikiwe vipi, kikubwa ni kuzishinda hali zetu.
Lakini kanuni za Mungu ni tofauti, kama tukiweza kuzishinda hali zetu, au bajeti zetu, na kusema ngoja nifungue mkono wangu kwa hiki au kile, kumsaidia huyu mwenye uhitaji au Yule, au kutoa sadaka, na kuisapoti kazi ya Mungu isonge mbele, kawapa mayatima kitu kidogo, tukinyoosha mikono yetu katika mambo kama hayo ..Basi tujue kuwa huo ndio utakuwa mwanzo wa Baraka zetu, lile wingu la utukufu wa Mungu litatembea na sisi wakati wote.
Na andiko hili litatimia juu yetu;
“Kuna atawanyaye, lakini huongezewa zaidi; Kuna azuiaye isivyo haki, lakini huelekea uhitaji”.
Kwa jicho la kibinadamu utaonekana kama ni mtu usiyekuwa na malengo, au mtu usiyekuwa na bajeti ya maisha, lakini Mungu hatakuacha..Siku zitakuja siku zitakwenda, ipo milango ambayo Mungu atahakikisha anakufungulia ki-miujiza miujiza, utashangaa, umewezaje kuvuka hapa au pale, Utashangaa kile ulichokipoteza Mungu anakurudishia na zaidi, na utakuwa umepata faida mara mbili..kujiwekea hazina mbinguni, na hapa duniani.
Luka 6:38 “Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa; kipimo cha kujaa na kushindiliwa, na kusukwa-sukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa vifuani mwenu. Kwa kuwa kipimo kile kile mpimacho ndicho mtakachopimiwa”.
Lakini kama kila kitu tunachokipata tunasema hichi ni cha kwetu tu,.tuna malengo mengi ya kufanya, mwaka huu nataka nifanye hivi au vile hivyo kwasasa sina fedha ya kwenda nje ya bajeti yangu..Siwezi kumsaidia ndugu yangu huyu mwenye shida hii, siwezi kuwasidia yatima wale, siwezi kumtolea Mungu…nataka nikuambie tutajiona kama tunakusanya, na fedha zetu hazipotei bure,zipo katika bajeti, lakini tutabakia katika hali hiyo hiyo miaka nenda miaka rudi, na mwisho wa siku tutajikuta malengo yetu kuyafikia bado yapo mbali na sisi..
Na hivyo Neno hili nalo pia linatimia juu yetu: “Kuna azuiaye isivyo haki, lakini huelekea uhitaji”.
Tutaelekea uhitaji ikiwa tutazuia matoleo yetu,..Hivyo utoaji ni jambo la muhimu sana, katika kuvuta Baraka za Mungu katika maisha yetu. Tendo moja la utoaji lina nguvu hata mara elfu kumi zaidi ya Maneno tunayomuomba Mungu kila siku atubariki katika sala. Lakini pia kumbuka katika kumtolea Mungu madhabahuni au katika kazi yake..zingatia kuwa msafi kwasababu Mungu wetu hapedezwi tunapomtolea sadaka na wakati ndani ya mioyo yetu tupo mbali naye…
Na ili tuwe watoaji wazuri, tupunguze msisitizo katika kuzitazama hali zetu za sasa. Na Bwana atatubariki, kama alivyoahidi katika Neno lake, kwasababu yeye si mwongo.
HERI NINYI MLIAO SASA, KWA SABABU MTACHEKA.
DHAMBI INAZAA KIFO.
UPAKO NI NINI?
Mauti ya pili ni nini?.. Ni mauti inayofuata baada ya hii mauti ya kwanza…Mauti ya kwanza ni pale roho ya Uhai inapoutoka mwili..Yaani pale tu Roho inapotengana na mwili hiyo ndiyo mauti ya kwanza. Lakini mauti ya pili ni roho kujitenga na nafsi.
Mauti ya kwanza inaweza kusababishwa na mambo mbali mbali..Inaweza kusababishwa na aidha ugonjwa fulani, au ajali fulani ambayo mtu anaweza kuipata…Lakini pia inaweza isisababishwe na ajali wala ugonjwa ikasababishwa na jambo lingine…
Hivyo mtu anapokufa katika hii mauti ya kwanza..(Yaani roho inapotengana na mwili)..Mtu huyo mwili wake unakwenda kuzikwa kaburini, unaoza na kuliwa na funza na kuwa mavumbi…lakini nafsi yake na roho yake zinakuwa hazijafa hivyo zinakwenda mahali pa wafu…
Mahali pa wafu nako kumegawanyika katika sehemu mbili..Sehemu ya kwanza ni mahali ambapo wafu waliokufa katika Kristo wanahifadhiwa..ambapo kwa lugha nyingine panaitwa peponi au paradiso..ni mahali pa raha sana na hapana mateso…
Na sehemu ya pili ni mahali panapojulikana kama KUZIMU au Jehanamu..ni mahali ambapo roho za wanadamu wote waliokufa katika dhambi zinahifadhiwa kwa muda..ni sehemu ya mateso mabaya sana.
Siku ya unyakuo itakapofika roho zilizohifadhiwa paradiso zitafufuliwa na kupewa miili ya utukufu na kwenda mawinguni na Bwana Yesu…lakini zilizosalia ambazo zipo kuzimu..siku ya hukumu zitafufuliwa nazo na kuhukumiwa kila mmoja sawasawa na matendo yake.
Yohana 5:28 “Msistaajabie maneno hayo; kwa maana saa yaja, ambayo watu wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake. 29 Nao watatoka; wale waliofanya mema kwa ufufuo wa uzima, na wale waliotenda mabaya kwa ufufuo wa hukumu”.
Yohana 5:28 “Msistaajabie maneno hayo; kwa maana saa yaja, ambayo watu wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake.
29 Nao watatoka; wale waliofanya mema kwa ufufuo wa uzima, na wale waliotenda mabaya kwa ufufuo wa hukumu”.
Sasa roho hizi ambazo zilikuwa zipo jehanamu/kuzimu baada ya kuhukumiwa….zitakusanywa zote na kutupwa katika ziwa la moto..Ziwa la moto ni tofauti na jehanamu…Na zitaungua huko kwa muda mrefu sana…Zilizofanya maovu sana kuliko nyingine zitaungua kwa muda mrefu…na zilizofanya machache zitaungua kwa muda pungufu kidogo wa hizo nyingine…
Baada ya kipindi kirefu sana kisichoelezeka cha mateso ndani ya ziwa la moto hatimaye roho zote zilizotupwa katika ziwa la moto zitakufa..Atakayekufa wa mwisho katika jehanamu ya moto atakuwa ni shetani huyo ndiye mwenye adhabu kubwa kuliko wote..wakifuatiwa na mapepo wake, wakifuatiwa na wachungaji na waaalimu wa uongo na manabii wa uongo..na mwisho watu wengine waovu waliosalia kila mmoja kulingana na uovu alioufanya..Hiyo ndio itakuwa MAUTI YA PILI, yaani kifo katika ziwa la moto..Roho kutenganishwa na nafsi.
Ufunuo 20:12 “Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa na matendo yao. 13 Bahari ikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake; na Mauti na Kuzimu zikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake. Wakahukumiwa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake. 14 Mauti na Kuzimu zikatupwa katika lile ziwa la moto. Hii ndiyo mauti ya pili, yaani, hilo ziwa la moto. 15 Na iwapo mtu ye yote hakuonekana ameandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika lile ziwa la moto”.
Ufunuo 20:12 “Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa na matendo yao.
13 Bahari ikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake; na Mauti na Kuzimu zikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake. Wakahukumiwa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake.
14 Mauti na Kuzimu zikatupwa katika lile ziwa la moto. Hii ndiyo mauti ya pili, yaani, hilo ziwa la moto.
15 Na iwapo mtu ye yote hakuonekana ameandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika lile ziwa la moto”.
Inajulikana na wengi kwamba ziwa la moto ni la milele lakini kiuhalisia sio la milele…Milele ilivyotumika katika kitabu cha ufunuo ni Everlasting…Yaani maana yake “kudumu muda mrefu” na si “eternal” ambayo maana yake ni milele…
Sasa kama mtu atakuwepo kuzimu milele tayari maana yake anao uzima wa milele…kitu ambacho sio kweli…Mwenye uzima wa milele ni Mungu tu..Na wana wa Mungu waliookolewa hao ndio watakaopata uzima wa milele..(yaani wataishi milele) Lakini roho zote zilizoasi zitakufa!. Biblia inasema hivyo..hata shetani naye pia atakufa…hana uzima wa milele.
Hivyo tofauti na wengi wanadhani kwamba adhabu kuu atakayoipata mwanadamu aliyeasi ni kuchomwa moto kuzimu…La! Hiyo sio adhabu…Adhabu kubwa au pigo kubwa hasa ni kuupoteza uzima wa milele..Yaani kufa na kutoweka kana kwamba hujawahi kuwepo kabisa…Na kifo hicho ni katika ziwa la moto. Hebu tafakari unakuwa haupo!
Hivyo Uzima sio kitu cha kufanyia mchezo kabisa…Tukose kila kitu lakini si uzima wa milele. Na uzima huu unapatikana kwa Yesu Kristo mwenyewe…Hivyo kama hujaokoka..mlango upo wazi sasa ila hautakuwa hivi siku zote..Tubu kwa kudhamiria kuacha kabisa dhambi, na kisha kabatizwe katika ubatizo sahihi ambao ni wa maji mengi na kwa jina la Yesu kama hujabatizwa. Na Roho Mtakatifu atakuongoza katika kweli yote na kukusaidia katika kuishi maisha masafi yanayompendeza Mungu.
Lakini kama usipotubu na kuipenda dunia..na kuendelea kuwa mlevi, mzinzi, mwasherati, mwizi, msengenyaji, mwongo, muuaji, mchawi, mla rushwa na mtoaji mimba…Biblia imeweka wazi sehemu ya watu wa namna hiyo ni ziwa la moto (Hivyo mauti ya pili ni nini?)
unapozungumzia ziwa la moto maana yake ni mauti ya pili.
Ufunuo 21:8 “Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili”.
Bwana atusaidie. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Tafadhali share na wengine na Bwana azidi kukubairiki.
Jehanamu ni nini?
KARAMA YA MUNGU NI UZIMA WA MILELE.
HATARI YA KUHUBIRI INJILI TOFAUTI NA ILIYOANDIKWA KWENYE BIBLIA.
KITABU CHA UZIMA
PENGINE MUNGU ALISHASEMA NAWE KWA NJIA HII.
Nguvu iliyopo katika maamuzi.
Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe. Karibu tujikumbushe Biblia…
Leo kwa Neema za Bwana tutajikumbusha mambo ambayo tulishawahi kujifunza huko nyuma..Kwasababu biblia inatufundisha hivyo katika 2Petro 1:12-13, 2Petro 3:1-2, na 1Wakorintho 4:17.
Na leo tutajikumbusha jambo muhimu sana ambalo linatutatiza wengi…Na hilo si lingine Zaidi ya nguvu iliyopo katika maamuzi.
Nguvu za Mungu haziwezi kuzidi maamuzi yetu sisi…Tunapomtumikia Mungu hatumtumikii kama maroboti kwamba maroboti yanakuwa hayajitambui lakini yanapelekwa tu mahali ambapo yule anayetaka kuyapeleka yawepo…Maroboti hayana maamuzi
Lakini sisi Mungu wetu hakutuumba hivyo wala hatutumikishi hivyo…Ametuumbia jambo linaloitwa maamuzi, na hivyo yeye au kiumbe chochote hakiwezi kuingilia maamuzi yetu…hata shetani hawezi!!…Sio kwamba hawezi kutufanya kuwa kama maroboti hapana uwezo huo anao…lakini hajapenda kutufanya hivyo..
Kwahiyo Mungu anapomvuta mtu kwake, ambaye amemkusudia uzima wa milele..anachofanya ni kumshawishi kwa kumpa kila sababu ya yeye kutubu…Anamfumbua macho na kuona hali aliyopo kwamba anakwenda kupotea kama asipochukua hatua hii au ile..Ni kama mtu mwingine wa pili yupo pembeni yake..anamshawishi afanye maamuzi Fulani…na endapo akikubali anakuwa anajiungamanisha na yule mtu…Lakini Roho Mtakatifu hafikii hatua ya kumteka mtu na kumfanya mateka..
Wengi wanaomba Mungu awazuie wasifanye uasherati kwa lazima…Hicho kitu hakipo!..Roho Mtakatifu ni msaidizi sio mfanyaji…Wafanyaji ni sisi, yeye ni msaidizi tu…Unapomfuata Kristo unatakiwa kwanza wewe binafsi kuutii ushauri wa Roho Mtakatifu wa kuacha uasherati…Ukishaamua wewe kutii kwa kuacha yeye anakuja hapo kukusaidia…Kwahiyo ukichukua maamuzi yako ukajumlisha na msaada wake..Hapo kamwe uasherati hautakushinda….
Kadhalika huwezi kumwomba Mungu akuachishe pombe au sigara kwa lazima…Kwamba utokee tu umeacha sigara au umeacha pombe…Nataka nikuambie Roho Mtakatifu hatendi kazi namna hiyo…Kama unataka kuacha pombe ambazo zimekufanya mtumwa kwa muda mrefu…Hatua ya kwanza ni wewe kumtii Roho Mtakatifu ambaye yupo pembeni yako anayekuambia uache pombe….hivyo mtii kwa kwenda kuvunja hizo chupa za bia zilizopo nyumbani kwako…kwa kuacha kwenda Bar, kwa kuacha kutembea na kampani za wanywaji pombe na kwa kuacha kabisa kunywa pombe…Ukishaamua kwa vitendo kama hivyo…
Basi yule msaidizi aliyeko pembeni yako, anakusaidia kushinda tamaa ya kunywa tena pombe anakuongezea nguvu …Lakini usipoamua…Miaka na miaka itapita utabakia hivyo hivyo,..utahudhuria kanisani, utawekewa mikono na kila aina ya mtumishi, lakini hakuna kitakachotokea.
Ni kwanini?..Ni kwasababu Nguvu za Roho Mtakatifu haziwezi zikazidi nguvu za maamuzi yako.
Na ndio maana Bwana Yesu anajulikana pia kama Mshauri wa Ajabu..
Isaya 9:6 “Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani”.
Mshauri ni mtu ambaye haingilii maamuzi yako lakini yupo karibu sana na mawazo yako kuyaboresha.
Kadhalika na uongo mwingine uliozagaa kila mahali ni wa watu kutenda dhambi na kusema ni shetani kawapitia…Ndugu usidanganyike hata kidogo kwa uongo huo!
Mtu anayekwenda kuzini..shetani hajampitia….kilichofanyika katika ulimwengu wa roho ni roho za mashetani zilitumwa kwa huyo mtu kumshawishi na kumpa kila sababu ya yeye kwenda kufanya uasherati…Ni kama mtu mwingine wa pembeni tena anamshawishi akafanye uasherati..atamkumbusha picha za ngono alizowahi kuziangalia, atamkumbusha uasherati wa mwisho aliowahi kuufanya na yule mtu atajaa tamaa na hivyo kwa maamuzi yake mwenyewe atanyanyuka na kwenda kutafuta kufanya kile kitendo…
Sasa huyo mtu hajashikwa na kufungwa na kupelekwa kwa lazima kufanya uasherati..la! bali kutokana na nguvu ya ushawishi iliyomshawishi na kuitii kwa hiari yake mwenyewe kaenda kufanya alichokifanya…Sasa huyu anaweza kujifariji ni shetani lakini hajui kwamba ni yeye ndiye kaamua kwenda kufanya..laiti angekataa kile kitu katika mawazo yake kamwe shetani asingeweza kumlazimisha…Kwasababu hakuna kiumbe chochote kilichoumbwa kinachoweza kuzidi maamuzi ya mtu!.nguvu iliyopo katika maamuzi ni kubwa sana.
Hivyo ndugu kama ulikuwa umekaa kwa muda mrefu huwezi kuacha kufanya masturbation..na ulikuwa unaamini kwamba ipo siku moja tu itatokea miujiza Mungu atakushukia na utaacha…nataka nikuambie ukweli…utasubiri hiyo siku miaka na miaka na haitafika!!!…Unachotakiwa kufanya ni leo leo kuamua kusema ninatubu dhambi zangu na kusema NIMEACHA!..na unaambatanisha vitendo juu yake kama dalili ya Imani yako…unafuta picha zote za ngono kwenye simu yako..unayazuia mawazo ya uasherati yajapo kichwani unayakataa..unakaa mbali na kitu chochote ambacho unajua ukikaa nacho dakika chache kitakupeleka katika mawazo ya uasherati…
Makala za kizinzi unaacha kuzisoma…magroup ya kizinzi unajiondoa, na ukikutana hata na post yoyote yenye maudhui ya kiuasherati unairuka huisomi…Vitabu na magazeti ya kiasherati unaacha kuyasoma…kuna magazeti ambayo kwa nje yanaonekana ni magazeti ya kimaadili ya kupunguza zinaa lakini ndani yake ndiyo yanayochochea zinaa kwa kasi kubwa…yana roho za usherati! Hivyo sio ya kusoma kabisa..mada mada na vikao vya mizaha unajitenga navyo…hata ukizungumza na mtu ukiona anaanza kwenda kwenye mada hizo unazikatisha…Lakini ukijiachia na kuendelea kusoma hayo magazeti, na Makala, na posti za mapenzi na magroup ya kiuasherati…pamoja na movie na matamthilia ya kidunia yenye maudhui ya mapenzi…na huku unaamini kwamba siku moja nguvu za Roho Mtakatifu zitakushukia na kukuteka na utajikuta tu umeacha kwa lazima…nataka nikuambie usiangamie kwa kukosa maarifa!!..hiyo siku haitafika.
Walioacha hawakuacha kwa njia hiyo…walimtii Mungu kwanza ambaye anaugua ndani yao kuhusu dhambi zao..na baada ya kumtii wakaamua kuacha kwa vitendo..ikiwemo kujitenga na vishawishi vyote vya kiuasherati…Huko ndiko kujikana nafsi…Na mambo mengine yote ni hivyo hivyo..ukitaka kuacha usengenyaji ni hivyo hivyo, ukitaka kuacha wizi ni hivyo hivyo…ukitaka kuacha uchawi ni hivyo hivyo…unaamua kwanza binafsi kuacha na unakwenda kuchoma vibuyu vyote ulivyonavyo..na kufuta namba za waganga wa kienyeji..na kampani za marafiki wanaohudhuria huko.
Na baada ya kufanya hayo yote…Hakikisha unakwenda kukamilisha hatua za wokovu ikiwemo kubatizwa, kufanya ushirika na waaminio wenzako, na kudumu katika kujifunza Neno la Mungu kila siku.
Bwana akubariki sana.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789 001 312 jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?
SIKUJA KULETA AMANI DUNIANI, BALI MAFARAKANO.
ROHO HUTUOMBEA KWA KUUGUA KUSIKOWEZA KUTAMKWA!
Ubatizo wa moto ni upi?
Roho, Nafsi, na Mwili, Je! vina tofauti gani?
JIBU: Mwanadamu ameumbwa katika pande kuu mbili, Upande wa kwanza unajulikana kama utu wa ndani, na upande wa pili unajulikana kama utu wa nje.
Utu wa nje ndio huu mwili wetu, ambao unaona, unahisi, unasikia, unatembea, unalala, unakula, unatamani n.k. Yaani kwa ufupi utu huu wa nje (yaani miili yetu) imeumbwa kwa lengo la kutimiza matakwa yote ya hapa duniani.
Lakini utu wa ndani, kidogo ni mpana kuulewa tofauti na huu wa nje, kwani wenyewe haujaumbwa na kitu kimoja, bali umeumbwa na mambo makuu mawili, la kwanza ni nafsi na la pili ni roho.. Hapa ndipo watu wengi wanapochanganyikiwa namna ya kuvitofautisha vitu hivi viwili.
Ukweli ni kwamba vitu hivi viwili vimeshikana sana, kiasi kwamba hata katika biblia sehemu nyingi, inataja nafsi na sehemu nyingine roho, unashindwa kuelewa ni kipi kinacholengwa hasaa hapo?.
Tunapaswa tujue kuwa Mungu amevishikamanisha hivi vitu viwili kwa pamoja kwa makusudi kabisa kiasi kwamba vionekane kama ni kitu kimoja, lakini kiuhalisi nafsi na roho ni vitu viwili tofauti..Ni sawa na mtu achukie rangi ya blue, kisha aichanganye na rangi ya njano..Matokeo yake hapo kama wewe ulishawahi kufanya stadi za kazi unaelewa ni nini kinatokea, hapo kinachozaliwa ni rangi ya Kijani..
Sasa mtu akikuambia uchukue rangi ya kijani halafu utoe rangu ya blue ndani yake, au rangi ya njano ndani yake, ni jambo ambalo haliwezekani, au kama linawekezana basi ni gumu sana kulifanya.
Ndivyo ilivyo kwa nafsi na roho, vimeshikamanishwa pamoja, kiasi kwamba hakuna mtu awezaye kuvitenganisha isipokuwa Neno la Mungu peke yake, mwanadamu hawezi, shetani hawezi, wala kiumbe kingine chochote..
Webrania 4:12 “Maana Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili, tena lachoma hata kuzigawanya nafsi na roho, na viungo na mafuta yaliyomo ndani yake; tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo. 13 Wala hakuna kiumbe kisichokuwa wazi mbele zake, lakini vitu vyote vi utupu na kufunuliwa machoni pake yeye aliye na mambo yetu”.
Webrania 4:12 “Maana Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili, tena lachoma hata kuzigawanya nafsi na roho, na viungo na mafuta yaliyomo ndani yake; tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo.
13 Wala hakuna kiumbe kisichokuwa wazi mbele zake, lakini vitu vyote vi utupu na kufunuliwa machoni pake yeye aliye na mambo yetu”.
Unaona hapo? Biblia inasema Neno la Mungu pekee, ndio linaloweza kuchoma hata kuzigawa nafsi na roho..Upo ufunuo mkubwa sana hapo? .Usitamani siku ile nafsi yako nafsi yako itengwe na roho yako,..ni maumivu makali sana ndani utakayoyasikia, ukitambua kuwa ndio mwisho wako umefika, kwamba hutakaa uwepo milele..
Mwanadamu au shetani au kiumbe chochote kinaouwezo wa kuutenganisha “utu” wa mtu wa nje, na ule wa ndani, kwa kufanya jambo jepesi la kumuua tu!, .lakini kuutenganisha ule utu wa ndani yaani nafsi yake na roho yake.. hakuna mtu yeyote anayeweza kufanya hivyo isipokuwa ni Mungu peke yake..
Mathayo 10:28 “Msiwaogope wauuao mwili, wasiweze kuiua na roho; afadhali mwogopeni yule awezaye kuangamiza mwili na roho pia katika jehanum”.
Tukisoma, Mwanzo pale anasema:
Mwanzo 2:7 “Bwana Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai”
Jiulize ni kwanini haijasema,.. “mtu akawa mwili hai” badala yake ikasema mtu akawa nafsi hai?. Hiyo ni kuonyesha kuwa pumzi ya uhai iliyotoka kwa Mungu iliingia ndani ya nafsi ambayo ilikuwa tayari imeshaumbwa ukisoma Mwanzo 1:27 utaona hilo …Ilipopokea pumzi hiyo ndipo ikawa nafsi hai.
Sasa pumzi ya uhai inayozungumziwa hapo ndio roho yenyewe..Ambayo inatoka kwa Mungu. Hivyo Roho ya uhai inayotoka kwa Mungu ikikutana na nafsi ambayo Mungu aliumba inamtengeneza mtu wa ndani aliye hai.
Ni sawa na unavyochanganya zile rangi mbili, ya blue na njano, kama tulivyoona hapo juu kutengeneza kijani..Sasa hichi kijani chenyewe ndio mtu wa Ndani.
Hivyo unaposoma biblia sehemu nyingine utaona inazungumzia roho, sehemu nyingine inasema, nafsi, sehemu nyingine inasema moyo, usichanganyikiwe..Fahamu kuwa inazungumzia kitu kile kile kimoja kinachomlenga huyu mtu wa Ndani. Japo ni vitu viwili tofuati.
Kwahiyo hii nafsi ndio mtu mwenyewe na ndio imebeba taarifa zote Mungu alizomuumbia mwanadamu ndani yake, kwa mfano wa Mungu, yaani upendo, furaha, sifa, wivu, ibada, utu wema n.k.. vyote hivyo vinatoka ndani ya nafsi ya mtu.
Kwahiyo ili vyote viweze kufanya kazi vilihitaji uhai ndani yake..na uhai huo ndio roho ya mtu..Ni sawa na balbu..ili iweze kuwaka na kutoa mwanga, inahitaji umeme ndani yake..Hivyo nafsi pia ili iwe hai na kuonyesha tabia zote za ki-Mungu ndani yake ilihitaji roho yenye pumzi ya Mungu ndani yake.
Hiyo ndio tofauti kati ya Roho Nafsi na Mwili..
Hivyo uulinde sana moyo wako kuliko kitu kingine chochote kama biblia inavyosema kwasababu huko ndipo zinapotoka chemchemi za maji ya uzima (Mithali 4:23).
Mhubiri 12:1 ‘Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, Kabla hazijaja siku zilizo mbaya, Wala haijakaribia miaka utakaposema, Mimi sina furaha katika hiyo…’
6 Kabla haijakatika kamba ya fedha; Au kuvunjwa bakuli la dhahabu; Au mtungi kuvunjika kisimani; Au gurudumu kuvunjika birikani; 7 Nayo mavumbi kuirudia nchi kama yalivyokuwa, NAYO ROHO KUMRUDIA MUNGU ALIYEITOA’.
6 Kabla haijakatika kamba ya fedha; Au kuvunjwa bakuli la dhahabu; Au mtungi kuvunjika kisimani; Au gurudumu kuvunjika birikani;
7 Nayo mavumbi kuirudia nchi kama yalivyokuwa, NAYO ROHO KUMRUDIA MUNGU ALIYEITOA’.
Tubu dhambi zako kama hujatubu umgukie muumba wako aliyekupa roho ya uhai bure angali muda upo..Utafika wakati kwa maumivu makali pumzi ya uhai itaondolewa kwenye nafsi yako katika ziwa la moto na kupata mauti ya pili kama inavyozungumziwa katika kitabu cha Ufunuo 2:11 na Ufunuo 22:6 na 20:14.
Ubarikiwe. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Muhtasari wa maelezo haya kwa njia ya video unaweza kuyapata hapa chini.
[embedyt] https://www.youtube.com/watch?v=hiXs2a7Im2A[/embedyt]
Roho Nafsi na Mwili, humkamilisha mwanadamu.
JE! MTUMISHI KUTOKUWA NA FEDHA NI ISHARA KUWA KUNA TATIZO KATIKA IMANI YAKE?
KILEMBA CHA NEEMA, JE! UMEMVIKA MWANAO?
NAMNA YA KUITAMBUA SAUTI YA MUNGU INAPOZUNGUMZA NA WEWE
USIPOLITENDEA KAZI NENO LA MUNGU.
Je Kwa mwanaume ni sahihi kuoa mtu uliyemzidi umri?..Na kwa upande wa mwanamke ni sahihi kuolewa na mwanaume uliyemzidi umri? (kuolewa na wanaume vijana)..Je ndoa za jinsia moja ni ishara ya nini? je watu watakuwa wakioa na kuolewa katika siku za mwisho inamaanisha nini?
JIBU: Biblia haijaweka katazo lolote kwa mwanaume kuoa mwanamke aliyemzidi umri au kwa mwanamke kuolewa na mwanaume uliyemzidi umri. Lakini kilichokataza ni tamaa.
Katika hizi siku za mwisho..Biblia imetabiri kuongezeka kwa maasi..na moja ya maasi hayo ni kuongezeka kwa Tamaa..Na Tamaa kubwa inayoikabili ulimwenguni ni tama ya uasherati…nyingine ni tamaa ya mali na umaarufu. Lakini namba moja ni tamaa ya uasherati na ya mali inashika nafasi ya pili.
Nyakati hizi za mwisho biblia imetabiri kuwa watu watakuwa wakioa na kuolewa.
Luka 17:26 ”Na kama ilivyokuwa siku za Nuhu, ndivyo itakavyokuwa katika siku zake Mwana wa Adamu. 27 Walikuwa wakila na kunywa, walikuwa wakioa na kuolewa, hata siku ile Nuhu aliyoingia katika safina, gharika ikashuka ikawaangamiza wote”
Luka 17:26 ”Na kama ilivyokuwa siku za Nuhu, ndivyo itakavyokuwa katika siku zake Mwana wa Adamu.
27 Walikuwa wakila na kunywa, walikuwa wakioa na kuolewa, hata siku ile Nuhu aliyoingia katika safina, gharika ikashuka ikawaangamiza wote”
Sasa kuoa au kuolewa sio kubaya…Lakini kuoa na kuolewa kunakozungumziwa hapo ambako ni kubaya na kwamba kutakuja kutokea katika siku za mwisho ni NDOA ZA JINSIA MOJA pamoja na NDOA ZA TAMAA ZA WATU KUOANA WALIOZIDIANA UMRI.
Siku hizi za mwisho ndoa za jinsia moja zinaongezeka kwa kasi hususani katika mataifa ya Magharibi hakuna tena hofu…
Kadhalika ndoa baina ya vijana wa kiume na wanawake wazee zinaongezeka kwa kasi kutokana na tamaa…wazee wanawatamani vijana na vijana wanawatamani wazee..Na hiyo ni kutokana na wanaume wazee kuwachoka wake zao walio wazee kama wao na kutamani mabinti vijana na hivyo kuwaacha wake zao na kwenda kutafuta mabinti vijana wa kuwaoa..ili watimize haja zao za tamaa za uasherati.
Vivyo hivyo wanawake wazee wanawachoka waume zao ambao ni wazee kama wao..na hivyo kuwaacha na kwenda kutafuta kuolewa na wanaume vijana kutimiza matakwa yao ya uasherati.
Kadhalika wanawake vijana wanatafuta kuolewa na wanaume wazee kwaajili ya kupata mali…Na vivyo hivyo vijana wa kiume wanatafuta kuoa wanawake wazee kwasababu ya kupata mali vile vile…Sasa machafuko kama haya ndiyo yasiyompendeza Mungu na ndiyo yaliyosababisha hata dunia ya kwanza ya akina Nuhu kugharikishwa na maji.
Hivyo kwa mtu yoyote anayetafuta kuoa au kuolewa na mtu aliyemzidi au aliye chini ya umri wake…kwa namna hiyo hapo juu..mtu huyo anafanya dhambi…Na hivyo anaangukia katika kundi la watu waovu waliotabiriwa kutokea katika siku za mwisho kwamba ‘watakuwa wakioa na kuolewa’.
Lakini kama si kwasababu hizo hapo juu bali ni kwasababu ya upendo basi sio dhambi kuoa au kuolewa na mtu aliyekuzidi umri au aliyepungufu ya umri wako..
La Muhimu na la kuzingatia ni kwamba huyo unayekwenda kumwoa au kuolewa naye..angalau asiwe rika la mwanao au la mzazi wako…Kwasababu ni ngumu sana kutokea mwanamume akampenda mtu wa rika la mama yake au bibi kizee..Wengi ni tamaa tu!..inakuwa ni roho nyingine inawasukuma kufanya hivyo..
Pia awe hana mume kabisa (yaani hajaolewa) au hajaoa..Kama alishaoa na ameachana na mwenziwe huyo hapaswi kuoa wala kuolewa..anapaswa arudiane na mkewe au mumewe. Pia awe ni mkristo, kwasababu ndoa yoyote inayohusisha watu wa imani mbili tofauti hiyo sio ndoa ya kimaandiko kabisa.
Tafadhali ‘share’ na wengine.
JE NI HALALI KUOA WAKE WENGI, AU KUTOA TALAKA?
Naomba kujua watakaoenda mbinguni je! ni wengi au wachache?
HATUTAACHA KUJIFUNZA NENO KILA INAPOITWA LEO.
Dini ya kweli ni ipi?