KUOTA UNAANGUKA .

KUOTA UNAANGUKA .

Kuota unaanguka chini maana yake ni nini?


Ndoto hii huwa inachukua maumbile tofautitofauti, wengine wanaota wanaanguka kutoka kwenye ghorofa refu sana, wengine kutoka kwenye mti mrefu, wengine kwenye shimo lisilokuwa na mwisho, wengine wanaota wanaanguka kutoka angani. Wengine wanaangukia kwenye maji n.k.

Maadamu kiini cha ndoto ni Kuanguka kutoka sehemu fulani, basi ujue ndoto hiyo ni tahadhari kubwa  kwako kutoka kwa Mungu, kwani Biblia inasema..

Ayubu 33:14 “Kwa kuwa Mungu hunena mara moja, Naam, hata mara ya pili, ajapokuwa mtu hajali. 

15 Katika ndoto, katika maono ya usiku, Usingizi mzito uwajiliapo watu, Katika usingizi kitandani; 

16 Ndipo huyafunua masikio ya watu, Na kuyatia muhuri mafundisho yao, 

17 Ili amwondoe mtu katika makusudio yake, Na kumfichia mtu kiburi; 

18 YEYE HUIZUIA NAFSI YAKE ISIENDE SHIMONI, Na uhai wake usiangamie kwa upanga. 

19 Yeye hutiwa adabu kwa maumivu kitandani mwake, Na kwa mashindano yaendeleayo daima mifupani mwake”;

Unaona huo mstari wa 15 unasema  Mungu kumbe anaweza kuzungumza na mtu mara moja, katika ndoto na asipojali atazungumza naye hata mara mbili..ili tu amzuie nafsi yake isiende shimoni. Hivyo fahamu kuwa ndoto hiyo ni Mungu anazungumza na wewe kukuonya.

Ni vizuri kujua katika biblia inapozungumza kuanguka inamlenga  ibilisi mwenyewe kwasababu yeye peke yake ndio anayetajwa akianguka kutoka mbinguni..Bwana Yesu alisema..

 “…Nilimwona Shetani, akianguka kutoka mbinguni kama umeme(Luka 10:18)..

Sasa inaposema alimwona shetani akianguka inamaanisha kuwa hapo mwanzo alikuwa sehemu sahihi lakini kuna wakati ulifika alifanya mambo fulani yasiyofaa ndio yakamfanya atoke katika ile sehemu yake na aanguke chini kwa kasi sana kama umeme.. na hicho si kingine Zaidi ya dhambi ya uasi..

Hivyo tendo la kuanguka ni tendo linalofunua uasi.. Shetani alipoasi ndipo alipoanguka chini, Vivyo hivyo na mtu yeyote leo hii anapomuasi Mungu, ni ishara kuwa anaanguka kutoka katika uwepo wa Mungu na mwisho wake unaenda kuwa mbaya  kama ulivyokuwa kwa shetani.

Kwahiyo ikiwa unaota unaanguka chini, tena mahali ambapo hufiki, basi ujue hiyo ni tahadhari kwako, kuwa unaanguka kutoka katika neema ya Mungu, mrudie Mungu wako kabla mlango wa neema haujafungwa.. Yaangalie Maisha yako, na matendo yako, unaona kabisa hayaendani na njia ya wokovu..unaona kabisa hata Kristo akirudi leo hii utaachwa kutokana na njia zako na mienendo yako.

Kwa kuwa Mungu anakupenda na anaona mwisho wako utakavyokuwa kama wa shetani, ndio maana anakuonyesha ndoto kama hiyo, anachotaka kwako ni  utubu dhambi zako, umgeukie yeye. Ukitubu leo kwa kumaanisha atakuokoa, na kukusafisha kabisa..Anachohitaji kwako ni moyo wa kumaanisha, kabisa, Hivyo kama kweli umemaanisha kufanya hivyo leo basi ujue uamuzi unaoufanya ni mzuri..Usijiangalie wewe ni muislamu, au mkristo ikiwa Kristo hajaumbika ndani ya Maisha yako, haijalishi wewe ni nani, umepotea tu na hata ukifa leo huwezi kwenda mbinguni..

Hivyo kama unapenda Yesu leo awe mwokozi wako, na kiongozi wa Maisha yako basi

Basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Biblia inasema saa ya wokovu ni sasa, hivyo usingojee Kesho, haitakuwa yako..

Sasa ukishajitenga sehemu yako mwenye, piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU  MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo,

Sasa Mungu akishaona umegeuka kabisa kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.

Ubarikiwe sana

Unaweza pia kujiunga na kundi letu la mafundisho Whatsapp, au kuwasiliana nasi kwa link hii

Group la whatsapp Kwa mgawanyo bora wa masomo download App hapa>> App wingu la mashahidi

Mada Nyinginezo:

NIFANYE NINI ILI NILITIMIZE KUSUDI LA MUNGU.

NINI TUNAJIFUNZA KWA MWANA MPOTEVU NA NDUGUYE?

CHAGUA NI JIWE LIPI LITAKALO KUFAA KWA UJENZI.

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

NI NANI ALIYEWAONYA KUIKIMBIA HASIRA ITAKAYOKUJA?

Shalom. Jina kuu la Mwokozi wetu Yesu Kristo, libarikiwe.

Karibu tujifunze biblia.

Mathayo 3:5 “Ndipo walipomwendea Yerusalemu, na Uyahudi wote, na nchi zote za kandokando ya Yordani;

6 naye akawabatiza katika mto wa Yordani, huku wakiziungama dhambi zao.

7 Hata alipoona wengi miongoni mwa Mafarisayo na Masadukayo wakiujia ubatizo wake, aliwaambia, Enyi wazao wa nyoka, ni nani aliyewaonya ninyi kuikimbia hasira itakayokuja?

8 Basi zaeni matunda yapasayo toba;

9 wala msiwaze mioyoni mwenu kwamba, Tunaye baba, ndiye Ibrahimu; kwa maana nawaambia ya kwamba Mungu aweza katika mawe haya kumwinulia Ibrahimu watoto.

10 Na shoka limekwisha kuwekwa penye mashina ya miti; basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni”

Soma tena mstari wa 7 “Hata alipoona wengi miongoni mwa Mafarisayo na Masadukayo wakiujia ubatizo wake, aliwaambia, Enyi wazao wa nyoka, ni nani aliyewaonya ninyi kuikimbia hasira itakayokuja? ”

Tunaweza kuiweka vizuri hiyo sentensi kwa namna hii “Enyi wazao wa nyoka ni nani aliyewadanganya(maana yake ni nani aliyewaonya) kwamba mtaiepuka hukumu inayokuja kwa njia hiyo mnayoitaka nyie?”..Njia gani?…Njia hiyo ya kuja kutaka kubatizwa na huku bado hamtaki kuacha dhambi zenu…Ni nani aliyewahubiria kuwa mtaikwepa hukumu kwa namna hiyo?…Maana yake mnafikiri kuwa kwa kuja kubatizwa tu hiyo inatosha kuikwepa hukumu itakayokuja….Mnajidanganya!…ZAENI MATUNDA YAPATANAYO NA TOBA!…Maana yake ni kwamba baada ya kutubu ishini kulingana na kutubu kwenu..Kama ulikuwa ni mwasherati, tubu na UACHE UASHERATI! Usiufanye tena, kama ulikuwa na kiburi tu na uache kuwa mwenye kiburi tena, kama ulikuwa mlevi unatubu na kuachana na ulevi wako, n.k..Huu ubatizo hautakuwa na msaada wowote kwenu kama mtakuja tu kubatizwa na huku bado hamjaacha matendo yenu mabaya. Huo ndio ujumbe Yohana Mbatizaji alikuwa anataka kuwapa wale Mafarisayo na Masadukayo.

Mafarisayo walisikia injili ya Yohana, wakaogopa, lakini wakasema aah ngoja tukabatizwe na sisi ili pengine tutaokoka huko mbeleni, lakini mioyoni mwao walikuwa hawana mpango wa kubadilika haka kidogo,..Walitaka kuugeuza ubatizo wa Yohana kama dini tu!..kama ni Liturujia mpya tu ya kufuata, kama katekisimo tu!..lakini walikuwa hawajui lengo kuu la ule ubatizo ni nini.. Lengo lake kuu lilikuwa ni kutubu na KUACHA DHAMBI!..sio kwenda kulowekwa kwenye maji na kurudi kuendelea na Maisha yako ya dhambi kama kawaida, na jina lako liwe limeshaandikwa mbinguni. Sio hivyo kabisa.

Vivyo hivyo na leo, ubatizo sio dini, na wala sio lebo ya kwamba Mungu anataka watu waliobatizwa ndio wawe wamepata tiketi ya kuingia mbinguni haijalishi wanaishije, yeye anataka tu watu wabatizwe.. hapana! Mungu anataka watu waliotubu na KUACHA DHAMBI. Hao ndio mbele za Mungu ubatizo wao una maana lakini kama mtu hujatubu kwa KUACHA DHAMBI, mtu huyo anamdhihaki Mungu.

Ukimuuliza mtu je umeokoka anakujibu, mimi nimebatizwa!..ukimuuliza tena je una uhakika wa kwenda mbinguni anakujibu ndio nilishabatizwa. Ubatizo hauna uhusiano wowote na kwenda mbinguni kama hujatubu kwa kuacha dhambi..Ndicho mafarisayo walichokuwa wanaenda kufanya kwa Yohana.

Umesema tu umetubu lakini bado unaendelea kuvuta sigara, bado unaendelea na uasherati, unaendelea na ulevi na ulawiti na usagaji, na pornography, halafu unasema umebatizwa au unakwenda KUTAFUTA UBATIZO, Ukidhani ndio unampendeza Mungu, na kwamba ndio utakwenda mbinguni..nataka nikuambie hapo unakwenda kujitafutia tu Laana badala ya Baraka.

Kutubu maana yake ni kugeuka na kuacha kile ulichokuwa unakifanya, na sio kusema tu mdomoni nimeacha na ilihali Maisha yako bado yapo vile vile. Ikiwa haupo tayari kuokoka, basi ni heri usiugize wokovu, wala usijiite hivyo, kwasababu ndivyo unavyomtia Mungu wivu kwa mienendo yako.

Watu wa Ninawi Mungu aliwasamehe kwasababu Aliona matendo yao kwamba wamegueka, wameacha mambo maovu waliyokuwa wanayafanya, hiyo ndiyo ikawafanya Waepukane na hukumu ile ambayo ilikuwa inawajia, na Mungu hakuona midomo yao kwamba wametubu kwa midomo ndipo awasamehe, hapana! bali matendo yao ndiyo yaliyosababisha wao kusamehewa.

Yona 3:10 “Mungu akaona MATENDO YAO, ya kuwa wameiacha njia yao mbaya. Basi Mungu akalighairi neno lile baya, ambalo alisema atawatenda; asilitende”

Hali kadhalika, usifanyike kuwa mzao wa nyoka, kwa kutafuta kutimiza maagizo ya Mungu na huku moyoni huna mpango wa kutenda mapenzi yake. Hizo ni tabia za Nyoka kibiblia. Mafarisayo wanamwendea Yohana kubatizwa na huku mioyoni mwao ni wale wale watu wenye viburi, wanaopenda utukufu, wenye wivu, wenye chuki, …maana japokuwa walikuwa wanamwendea Yohana kubatizwa lakini mioyoni mwao walikuwa wanamchukia n.k

Kama umeamua kumfuata Yesu leo, basi kubali pia kubeba na msalaba wako, kabla ya kwenda kubatizwa piga gharama kabisa kwamba unakwenda kuacha dhambi moja kwa moja, kwamba dunia ndio umeipa mgongo hivyo, msalaba mbele, ulimwengu umeuacha nyuma..Na kwa kufanya hivyo ndipo utaona nguvu za Mungu katika Maisha yako zikikusaidia na kukuongoza na ndivyo Mungu atakavyokukaribia Zaidi na kukupenda. Na kukubariki.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

MATUNDA YAPATANAYO NA TOBA!

JE! UMEFANYIKA KUWA MWANAFUNZI WA BWANA?

HISTORIA YA ISRAELI.

INJILI YA KRISTO HAITANGAZWI KWA HATI MILIKI.

KWANINI NAYAWEZA MAMBO YOTE KATIKA YEYE ANITIAYE NGUVU?

AINA YA MAADUI UTAKAOKUTANA NAO KATIKA SAFARI YAKO YA WOKOVU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

التنين القديم

التنين القديم

لماذا الشيطان هو التنين القديم / التنين القديم؟

شالوم ، بنعمة إلهنا رأينا الشمس مرة أخرى اليوم. مرحبا بكم في دراسة كلمة الله التي هي غذاء لأرواحنا.

يقول الكتاب المقدس في ..

    رؤيا يوحنا 20: 1 “ورأيت ملاكا ينزل من السماء ، وله مفتاح الحفرة القاع وسلسلة كبيرة في يده.

    2 وأمسك التنين ، الذي عانى الشيطان والشيطان ، وقيده بألف سنة ، ”

يُعرف الشيطان باسم الثعبان القديم أو التنين القديم … وهذا يعني أنه عاش منذ فترة طويلة ، وقد عاش مثل التنين / الثعبان القديم منذ ذلك الحين … وإذا كنت تعرف أي شيء موجود منذ فترة طويلة ، فيجب أن يكون تجارب كافية عن الحياة ، على سبيل المثال ، يجب أن يعرف الرجل العجوز الكثير من الشباب. كبار السن هم أكثر دراية من المراهقين.

نظرًا لأنهم مروا بأشياء كثيرة في حياتهم وتعلموا الكثير ، فقد تعلموا من أخطائهم ومن أخطاء الآخرين … لذلك لا يمكن مقارنتهم مطلقًا بالأطفال حديثي الولادة أو المراهقين.

وبالمثل ، يُعرف الشيطان أيضًا باسم التنين القديم / التنين القديم …

هذا يعني أنه يعرف الكثير عن الإنسان … إنه موجود منذ عدن ، ويعرف آدم في وجهه وشكله وشخصيته التي لم ينسها ، ويعرف حواء أيضًا … إنه يعرف نوح ، وكان يشهد كيف دمر العالم عند الطوفان … كان ينظر … وما زال يتذكر صورة إبراهيم وسارة … يتذكر المكان الذي أزعجوه فيه في حياتهم. إنه يتذكر موسى … وما زال يعرف كل شخصيته ويعرف نقاط ضعفه. لديه وجه دانيال ونبوخذ نصر ، وإيليا ويتذكر سلوكهما … كما يعرف رئيس الحياة ، يسوع المسيح ، يتذكر جميع الأحداث من ولادته حتى أنه كان هناك في البرية لإغراءه ، وعندما توفي وقام ، يعرف قوته والقوة التي لديه الآن … إلخ

لذلك فإن الشيطان يعرف الناس جيدًا ، ويعرف الناس وسلوكهم ، ويعرف ما يحبه ، وما لا يعجبهم … لقد رأى كل الأجيال من آدم حتى الآن …

ما عليك سوى أن تسأل نفسك حتى الآن عن عمر 70 عامًا على الأرجح ، ومع ذلك يمكنك تصنيف سلوك بعض الأشخاص وبعض القبائل لدرجة أنك ربما تعرف سلوك شخص ما حتى لو لم يكن يتكلم كلمة واحدة .. يمكنك تجميعه / لها حتى قبل أن تذهب بعيدًا … الآن إذا كنت ممن تقل أعمارهم عن 60 عامًا تعرف بالفعل المجتمعات وعاداتها … إلى أي مدى تعتقد أن الشيطان سيعرف الناس؟ لأنه من عدن إلى هذا اليوم.

أريد أن أخبرك أنه يعرف البشر جيدًا … إنه يعرف مكان احتجاز الأطفال الأسرى ، كبارًا وصغارًا على حد سواء … لأن الرجل هو نفسه … لعدة أشخاص في الأجيال الماضية ونجح … إنه يعرف كيفية إسقاط الأطفال. عبيد الله … لأنه جرب في الماضي ونجح للآخرين بحيث يطبق نفس التجربة على الناس من جميع الأعمار. إنه (التنين القديم) يعرف كيفية إبعاد الناس عن الصلاة ، ويعرف كيف يؤثر عليهم ليس للبحث عن الله ، لأنه حاول بهذه الطريقة في الماضي ونجح. لديه خبرة كافية.

ما لم تحصل على حق في يسوع ، فلن تهزم الشيطان بأي شكل من الأشكال ، لديه معرفة أكثر منك وأنت ،

إذا كنت لا تريد الرب يسوع وأنك تستطيع أن تمنع نفسك من ارتكاب الزنا دون أن تكون في المسيح ، فأنا أريد أن أخبرك بالحقيقة أنك تضيع وقتك! في يوم من الأيام سوف ترتكبها … أشخاص مثلك حاولوا ذلك في الماضي وكان (الشيطان) قد قبض عليهم ، لذا فأنت لست أول من يفكر في ذلك أو يجربه.

مرة أخرى ، إذا قلت إن بإمكانك فعل أشياء جيدة أو بدون أن تكون في يسوع … أخت! لقد سعى الشيطان بالفعل إلى حل لأشخاص مثلك على الأرجح منذ أكثر من 2000 عام … قد تعتقد أنك أول من جرب ذلك ، لكن ربما يكون لدى الشيطان 10 ملايين قائمة من الأشخاص في الأجيال الماضية حاولوا أن يتصرفوا مثلك من السيد المسيح وقد تغلب عليهم جميعا.

لذلك أنت الذي ولدت هذه الأيام لا يمكنك أن تتفوق على حكمة الشخص الذي كان موجودا قبل سنوات عديدة … (ألا تعرف لماذا يسمى الشيطان إله هذا العالم؟ لأنه يعرف الشؤون الإنسانية أكثر من أي إنسان آخر).

لهذا أخبره الرب يسوع أنه يفكر دائمًا في ما يخص البشر وليس لله. لأنه لا يدرس الله بل يدرس الرجال وكيف يحكمه. اذهب واقرأ (متى 16:23).

لذلك سوف تسأل إذا كان الشيطان يعرف الكثير عن الشؤون الإنسانية ، فمن ذا الذي يستطيع الهروب؟ وتغلب عليه؟

الجواب هو هذا ؛ بالإضافة إلى كل عظمة الوعي الإنساني الذي لديه في حكمته ، هناك شخص أكبر منه سناً. هذا هو المعروف باسم قديم من الأيام.

دانيال 7:13 -14 “رأيت في رؤى ليلية ، واذا جاء واحد مثل ابن الإنسان مع غيوم السماء ، وجاء إلى قديم الأيام ، واقتادوه بالقرب منه.

    ١٤ وكان قد أُعطي له سلطانًا ومجدًا ومملكةً لكي تخدمه جميع الشعوب والأمم واللغات: سلطانه هو سلطان أبدي لا يموت ، ومملكته التي لا يجوز تدميرها ”

أبانا يعرفنا أكثر مما يعرفنا الشيطان. يتمتع الشيطان بالتجربة لإسقاطنا ، لكن الحكمة التي لدى الله لديها القدرة على معرفة أفكاره ونواياه وخططه ، وإسقاط أفكاره … كل ما يريد أن يفكر فيه ، نحن في المسيح بالفعل. لدينا القدرة على معرفة كل الفخاخ له. تخترقنا الحكمة الإلهية التي تعطينا القدرة على إدراك كل الأفكار الشيطانية والتغلب عليها.

 لكن هذه الحكمة تُمنح فقط لأولئك الذين يؤمنون بابنه الحبيب ، يسوع المسيح.

لن يتمكن الآخرون خارج المسيح من هزيمة التنين القديم الذي هو الشيطان. سيتم توجيههم إلى الشيطان حيث يريدهم أن يذهبوا ، وهذا هو السبب في أن الشخص الذي لم ينقذ لن يكون له سلام ولن يتغلب أبدًا على الخطيئة أو إرادة العالم. هذا هو ما يفعله … في بعض الأحيان يخطط للقيام بهذا أو ذاك ، ولكن في النهاية ينتهي الأمر إلى أن يكون شيئًا آخر … لماذا؟ ذلك لأنه يريد أن يوجه نفسه ويعتقد أنه قادر على النجاح بقوته وعقله.

لذلك إذا لم يتم خلاصك ، ومع ذلك فإن الأمل في التغلب على التنين القديم لا يزال متاحًا حتى اليوم ، فإن حكمة الله الإلهية تريد أن تدخل فيك اليوم … لا تستمع إلى الشيطان الذي يخبرك في ذهنك الآن أنه لا يمكن إنقاذك أن لديك الكثير من الخطايا وأن الله لن يغفر لك … إنه يستخدم تكتيكاته القديمة فقط ، لذلك لا تستمع إليه … لكنك تنكره اليوم وتأكد من حرمانك من العمل … قرر اليوم أن تتوقف عن الخطيئة والتوبة والتوقف عن الذهاب إلى النوادي الليلية وتقرر إيقاف ثرثرة وتقرر إيقاف السكر. والزنا والرب أحبك … والحكمة الرائعة من قديم الأيام. (الرب) إلهنا ، سوف يأتي إليك ، قد يعرف ماكره وحيله ..

     الأمثال 2: 6 “لأن الرب يعطي الحكمة: من فمه يأتي المعرفة والفهم.

    7 وضع حكمة سليمة للأبرار: هو دجل لهؤلاء الذين يمشون منتصبين.

    8 يحفظ طرق الدين ويحفظ طريق قديسيه.

    9 حينئذ تفهم البر والحكم والعدالة. نعم ، كل طريق جيد.

    10 عندما تدخل الحكمة الى قلبك وتكون المعرفة ممتعة لنفسك.

الرب يباركك.

يرجى مشاركتها مع الآخرين.

Print this post

JE KUHUDUMU KWA NYIMBO ZA INJILI KUKOJE?

Nyimbo za Injili ni zipi?, waimbaji wanapaswa waitendeje huduma hiyo?..

Shalom. Karibu tuongeze maarifa kuhusu Neno la Mungu..Tukilijua Neno la Mungu vyema, tutayajua mapenzi ya Mungu na hivyo tutaishi kulingana na yeye anavyopenda na tutabarikiwa.

Moja ya karama ya muhimu sana katika Mwili wa Kristo ni karama ya uimbaji. Sasa ni wazi kuwa mtu yoyote anaweza kuimba, awe mwanamume au mwanamke..Lakini yupo ambaye akiimba nyimbo au akiimbisha basi kunaambatana na nguvu fulani za kipekee za Roho Mtakatifu. Sasa nguvu hizo sio za kuwafanya watu waanguke au walie..Hapana bali nguvu hizo ni zile zinazomfanya mtu apate badiliko fulani la rohoni, ageuke kutoka kuwa mwenye dhambi mpaka kuwa mtakatifu.

Mwimbaji huyu anapoimba au anapoimbisha, basi Roho yule yule anayeshuka juu ya watu wakati Mchungaji anahubiri ndio huyo huyo anayeshuka juu  ya watu wakati anaimbisha.

Sasa huduma ya uimbaji sio huduma ya kutafuta fedha, kama vile huduma nyingine yoyote katika mwili wa Kristo isivyo ya lengo la kutafuta fedha wala umaarufu. Mchungaji au Mwalimu anapohubiri katika kanisa lake, na anapoalikwa mahali pengine au Taifa lingine kwenda kuihubiri Injili, hapaswi kwenda kule kwa lengo la kutafuta fedha. Biblia inasema tumepewa bure tutoe bure..Hivyo atakwenda kule alikoalikwa na atahubiri bure..Ndio wale waliomwalika watamgharimia nauli, pamoja na malazi na makazi kwa huo wakati, lakini hapaswi kwenda kwa lengo la kutafuta malipo/mshahara. Kama waliomwalika watakuwa na moyo mwingine na kusema hatutapenda mtumishi huyu aondoke mikono mitupu, hivyo kwa kuguswa kwao wakampatia chochote kile iwe fedha, au mali..hapo sio dhambi kupokea..lakini Mchungaji, au mwalimu au mtu yoyote yule hapaswi kuomba chochote, wala kuonyesha dalili ya kuwa mhitaji.

Mungu anajua kuwahudumia watu wake, haihitaji yeye kusaidiwa, hivyo aliposema…”Tumepewa bure tutoe bure alimaanisha kabisa”..kwamba kwa namna yoyote ile atawafungulia watumishi wake mlango wa kula na kunywa hata njia hiyo.

Vivyo hivyo na uimbaji wa nyimbo za injili. Mtu yeyote aliyepewa karama hiyo hapaswi kuwa kama wasanii wa nyimbo za ulimwengu ambao wapo kwa lengo la kutafuta fedha kwa sanaa zao hizo. Mtu mwenye karama ya uimbaji atafanya kazi ya Mungu bure pasipo malipo..akifika mahali kaalikwa kwenda kuongoza nyimbo za kumsifu Mungu na kumwabudu, hapaswi kutazamia malipo kwa namna yoyote ile. Anapaswa afanye kazi yake ya uimbaji kwa uaminifu kama ya mchungaji aliyealikwa…aimbe nyimbo za injili na kuhakikisha neema ya Mungu imeshuka juu ya watu, hiyo ndio inapaswa iwe furaha yake ya kwanza, na lengo lake kuu la kwenda pale.

Hali kadhalika hapaswi kubadilika kimavazi na kufanana na wasanii wa kidunia..Kazi ya Mungu sio ya kuonyesha uanamitindo…kwamba leo umevaa hiki, kesho unavaa kile, ili watu wakuone jinsi unavyojua kuvaa…Vaa nguo za heshima, kama ni mwanamke vaa gauni refu haijalishi ni la gharama au sio la gharama, lakini lazima liwe la kujisitiri, hupaswi kwenda kufanya huduma huku umevaa suruali, huku mgongo upo wazi, huku umejichubua uso, huku umeweka make up mfano wa Mwanamke Yezebeli wa kwenye biblia..hali kadhalika mwanaume hupaswi kwenda kufanya huduma huku umenyoa kidunia, huku umevaa nguo za kubana, huku umejipamba mpaka unakaribia kufanana na wanawake.

Ukifanya hivyo na kwenda kufanya huduma na mambo hayo machafu utakuwa bado hujaelewa nini maana ya kumtumikia Mungu, utakuwa unamdharau Mungu na madhabahu yake, na utakapoambiwa ukweli utaona kama unaonewa WIVU, hakuna wivu hapo unaoonewa, ni kwa faida yako binafsi..Unakwenda kuzitafutia laana badala ya baraka ndugu…..Unapoacha kusimama katika Neno la Mungu na kujilinganisha na wasanii wa kidunia, ni sawa na mchungaji aliyeacha majukumu yake madhabahuni na kujilinganisha na wanasiasa waliopo bungeni.

Ndugu yangu, uliyejaliwa karama ya uimbaji..Utumie kwa utukufu wa Mungu, kama wachungaji ambao wamealikwa kutembea dunia yote kuhubiri hawabweteki na kwanini wewe unabweteka na kujiharibia huduma yako kwa kuwaiga hao wasanii wa kidunia au hata baadhi ya wanaojiita wasanii wa injili ambao hawajaelewa maana ya kumtumikia Mungu?

Sasa utauliza je! Sitakiwi kabisa kwenda kurekodi nyimbo zangu studio?

Hapana unapaswa ukazirekodi kabisa tena kwa bidii nyingi, kwa uongozo thabiti wa Roho Mtakatifu, ili injili ienee kwa wengi, na kuwa msaada na baraka kwa wengi..Lakini katika hiyo usiigeuze kuwa ndio sehemu ya kupatia fedha na utajiri. Weka bei ya bidhaa hiyo ambayo inalingana na gharama ulizoingia, na faida kidogo kwaajili ya msingi wa kazi zitakazofuata kama hizo na si kwaajili ya kupata fedha, wala kwaajili ya kujiandaa kuwa msanii maarufu. Na hupaswi kukasirika unaposikia watu wanabarikiwa kwa nyimbo ulizoimba, au wanaziimba nyimbo zilizotungwa na wewe pasipo kukutaja wewe wala kukupa malipo…Hupaswi kukasirika, zaidi ya yote unapaswa ufurahi kwasababu injili ya Kristo inakwenda mbele.

Kwasababu hata wachungaji ndio hivyo hivyo, wanapotengeneza kitabu..na mafunuo waliyoyapata na kuyaandika ndani ya kile kitabu yatakwenda kufundishwa huko na huko, kila mahali na hata kumrudia yeye mwenyewe…na wala hawasemi wala kuchukia kwamba ule ufunuo ni wa kwao na kwamba wana hati miliki nao, mtu mwingine hapaswi kuhubiri bila idhini yao. Kama yupo Mtumishi wa namna hiyo, basi huyo naye bado hajaelewa nini maana ya kuwa mtumishi,  kwasababu injili ya Kristo haihubiriwi kwa hati miliki. Lakini kama hujawahi kuona kwanini wewe muimbaji uchukie na kukwazika kuona mtu anaimba nyimbo uliyoiimba wewe bila hata kukutaja au kukutambua?.

Ukiona unasikia huo wivu basi fahamu kuwa bado kuna kasoro ndani yako, upo kutafuta umaarufu na faida kupitia kazi ya Mungu, na haupo kwa lengo la kuisambaza injili. Huna tofauti na Yuda Iskariote.

Hivyo zingatia hayo machache mtu wa Mungu, na Bwana atakusaidia, kama una huduma yoyote ndani yako ya kuhudumu kwa nyimbo za injili, tenga muda uilinganishe na huduma nyingine katika mwili wa Kristo jinsi zinavyofanya kazi, ili upate hekima na ufahamu jinsi ya kuitenda kazi ya Mungu katika shamba lake.

Bwaan akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

SIKU YA HUKUMU ITAKUWAJE?

NINI TUNAJIFUNZA KWA MWANA MPOTEVU NA NDUGUYE?

KILEMBA CHA NEEMA, JE! UMEMVIKA MWANAO?

https://wingulamashahidi.org/2019/09/01/maana-ya-huu-mstari-ni-ipi-mithali-144-zizi-ni-safi-ambapo-hapana-ngombebali-nguvu-za-ngombe-zaleta-faida-nyingi/

MATUMIZI YA DIVAI.

JE KUNA UISLAMU KATIKA BIBLIA?

KITABU CHA UZIMA

Rudi Nyumbani:

Print this post

USIPOWATAMBUA YANE NA YAMBRE, KATIKA KANISA LA KRISTO, UJUE UMEPOTEA.

Ukisoma ule waraka wa pili ambao Paulo alimwandikia Timotheo kuanzia ile sura ya tatu mstari wa 1-9, utaona jinsi Paulo alivyoanza kumweleza Timotheo juu ya mambo yatakayotokea siku za mwisho..Lakini alianza kwa kumwambia neno hili “siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari”.. Jiulize ni kwa nini alimwambia hivyo?. Alimwambia hivyo kwasababu aliona jinsi wimbi kubwa la watu wenye mfano wa utauwa (wanaonekana kama  ni watu wa Mungu), lakini wakizikana nguvu zake, watakavyonyanyuka na kuwapoteza wengi.

Hao watu hawakuwepo wakati mwingine wowote isipokuwa tu watatokea katika siku za mwisho, yaani watu wanaoonekana ni watumishi wa Mungu, wanaoonekana wanawaongoza watu katika njia za kweli, lakini kumbe nyuma ya mgongo wanazikana nguvu za Mungu..

Sasa hizi nguvu za Mungu ni zipi?..

Biblia inatueleza “Neno la msalaba” ndio nguvu ya Mungu..

1Wakorintho 1:18  “Kwa sababu neno la msalaba kwao wanaopotea ni upuzi, bali kwetu sisi tunaookolewa ni nguvu ya Mungu”.

Sehemu nyingine inaiita injili kama “uweza wa Mungu (POWER)” Warumi 1:16.

Unaona Injili inayolenga ukombozi wa msalaba,  inayowafanya watu wautazame msalabani, watubu dhambi , wakapate msamaha na ondoleo la dhambi zao, hapo ndipo nguvu za Mungu zilipo..

Hakuna mahali popote biblia inasema nguvu za Mungu zipo katika mali, au biashara na majumba..Hayo hayawezi kumfanya mtu apate uzima wa milele…Sasa watu wa namna hii ndio watanyanyuka sana katikati ya kanisa la Mungu, ambao watakuwa wanajifanya ni wanatangaza habari za wokovu, kumbe wanahubiri mambo yao mengine, hawana habari na injili ya toba, wala hata haiwavutii,  wala hawajali kwamba mtu wanayemchunga na kuchukua sadaka zake anaweza kufa leo na kwenda kuzimu kutokana na dhambi zake, hilo hawalijali wao wapo radhi kuwasisitizia tu mafanikio ya miili yao, lakini si roho zao.

Wengine wapo radhi, kuwakaririsha mapokeo ya dini zao, ili watu wawe tu wa kidini, wajue litrujia, wasome rozari, na sala zote za marehemu, lakini hao hao watu ukiwauliza je umeokoka, watakauambia mimi si mlokole, ukiwauliza, Je! Unajua kuwa kuna kitu kinachoitwa Unyakuo, watakauambia..sijui unazungumzia kitu gani!!..Sasa embu fikiria mtu wa namna hiyo mbinguni atakwendaje?..Lakini hayo yote ni kiongozi wake hajawahi kumwambia hayo mambo, ni kiongozi ambaye anao mfano wa utauwa lakini anazikana nguvu za Mungu..

Sasa Paulo aliwafananisha watu hawa na Yane na Yambre ambao walinyanyuka wakati wa Musa..Jinsi walivyokuwa wanapingana naye..

2Timotheo 3:8  “Na kama vile Yane na Yambre walivyopingana na Musa, vivyo hivyo na hawa wanapingana na ile kweli; ni watu walioharibika akili zao, wamekataliwa kwa mambo ya imani.

9  Lakini hawataendelea sana; maana upumbavu wao utakuwa dhahiri kwa watu wote, kama vile na upumbavu wa hao ulivyokuwa Dhahiri”.

Sasa kama uwafahamu Yane na Yambre ni wakina nani…

Walikuwa ni wale wachawi wa Farao ambao Musa alipokuwa anafanya miujiza na wao walikuwa wanafanya ili tu kumpinga Musa.

Unaona? Jambo pekee ambalo lilikuwa linawatofautisha hawa wachawi wawili (Yane na Yambre) na Musa, halikuwa miujiza..hapana, hata wao kwa sehemu fulani walipewa kufanya miujiza, jambo pekee lililowatofautisha na Musa, ni UJUMBE waliobeba.. Musa alikuja na ishara lakini alikuwa na Ujumbe nyuma ya ishara zile..Nao ndio huu “Bwana asema hivi! Waache watu wangu huru,waende kunitumikia”..Lakini Yane na Yambre hawakuwa na ujumbe wowote isipokuwa kupinga tu, na kuwaburudisha na kuwatumainisha wamisri kwa miujiza yao,..Ni wana-mazingaombwe tu!..Mtu anayefanya mazingaumbwe siku zote hana ujumbe wowote kwa mazingaombwe yake, anafanya tu kuburudisha watu, na wala wakati mwingine anaweza asiongee kuanzia anaanza mazingaombwe yake mpaka anamaliza. Na wakina Yane walikuwa hivyo hivyo.

Musa alikuwa na ujumbe wa ukombozi, wa kuwatangazia watu uhuru watoke katika utumwa mgumu wa Farao, Ambao kwa sasa sisi tuliookolewa tunafananishwa na wana wa Israeli pale tunapomwamini Kristo, tunaokolewa kutoka katika utumwa wa dhambi wa Ibilisi.

Sasa ukiona, mtu anakujia na miujiza na ishara hizi au zile, lakini hana ujumbe wowote wa kukutoa Misri (kukutoa kwenye utumwa wa dhambi), Basi ujue kuwa unaongozwa na Yane na Yambre(wana mazingaombwe), watumishi wa shetani.. Haijalishi watashika biblia, haijilishi watakuombea upone kiasi gani, Yane na Yambre waliweza kuyafanya hayo yote, haijalishi watafanya miujiza mingi vipi, kama hawana ujumbe wa kukurudisha msalabani upate ukombozi wa roho yako, Ujue hao ni Yane na Yambre tu wanakuongoza…

 Ndio hao sasa mtume Paulo anaowazungumzia kuwa  “wenye mfano wa utauwa, lakini wakikana nguvu zake”…..Hizi ndio nyakati zenyewe za hatari zinazozungumziwa hapo. Mahali popote unapoongozwa embu jipime nafsi yako, je tangu umekuwa hapo ni kitu gani kimeongezeka katika Maisha yako ya rohoni kwa ujumla, Je! Mahusiano yako na Mungu yameongezeka au yapo pale pale?, Kama sivyo basi ujue upo chini ya Yane na Yambre wa siku za mwisho.

Na kibaya Zaidi kama hujui, watu waliochangia kuufanya moyo wa Farao kuwa mgumu ni hawa wachawi wawili..Kama sio wao basi pengine Farao angeshatubu zamani..(Ingawa ni Mungu mwenyewe ndiye aliyeruhsu). Vivyo hivyo leo hutaki kumgeukia Kristo na kutaka kutubu dhambi zako na kutafuta utakatifu kwasababu tayari wapo akina Yane na Yambre wanaokupumbaza na miujiza, ukikumbushwa habari ya utakatifu na kwenda mbinguni, unasema nabii wetu/kiongozi wetu wa kidini mbona hajawahi kutufundisha hayo, na miujiza mbona inafanyika mingi tu..

Ndugu siku ukifa na kujikuta upo kuzimu, hutakuwa na  la kujitetea, kwasababu biblia inatuambia..mtu akifa matendo yake yanafuatana naye (Ufunuo 14:13)..Haisema majumba yake, au magari yake, au bishara yake, au dhehebu lake, inasema matendo yake..Sasa kama nabii wako au mchungaji wako, anakutumaisha na mambo ya ulimwengu huu na wewe unaona raha, nataka nikuambie siku ile vyote pamoja na mali zako, pamoja na huyo kiongozi wako wa imani, aliyekuwa anakufundisha kujiwekea hazina duniani badala ya mbinguni, wote watakuaga pale makaburini, utakuwa umebakia wewe mwenyewe, utashangaa ni  matendo yako tu yapo na wewe..hayo ndiyo yatakayoeleza hatma yako ni nini..

 kwasababu biblia imeshatuonya jinsi ya kuendana na watu wa namna hii, hivyo ni wajibu wako wewe binafsi kutumia akili, kwa kuutafuta uhusiano wako binafsi na Mungu wako…Kuupima wokovu wako kama upo sawasawa au la, na kama haupo! Basi ndio ufanye bidii kumtafuta Kristo kwa moyo wako wote na kwa nguvu zako zote, katika hichi kipindi kifupi tulichobakiwa nacho, maadamu muda unao..

2Wakorintho 13:5 “Jijaribuni wenyewe kwamba mmekuwa katika imani; jithibitisheni wenyewe. Au hamjijui wenyewe, kwamba Yesu Kristo yu ndani yenu? Isipokuwa mmekataliwa”

Usisubiri ufe ndipo ujue kuwa ulikuwa kwenye njia isiyo sahihi, amka usingizi, anza kuyatengeneza Maisha yako.

Waefeso 5:14 “Hivyo husema, Amka, wewe usinziaye, Ufufuke katika wafu, Na Kristo atakuangaza”.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group


Mada Nyinginezo:

Rudi Nyumbani:

Print this post

JIHADHARI NA DHAMBI YA WIVU/HUSUDA.

Jiepusha na dhambi ya wivu/husuda ambayo mwisho wake ni mauaji.

Silaha moja kubwa shetani anayoitumia kuwadhuru watu ni wivu…mtu mwenye wivu ni rahisi kutumiwa na shetani kwa viwango vikubwa sana… Mauaji mengi yanasababishwa na wivu, uchawi mwingi unatokana na wivu, hila nyingi zinatokana na wivu..na mambo yote mabaya yanatokana na wivu.

Hivyo ni muhimu kujifunza kutokuwa na wivu ili tusiwe kifaa cha kutumiwa na shetani kuwadhuru wengine.

 Roho ya wivu ndiyo iliyowafanya  Mafarisayo na Masadukayo wamchukie Bwana, pale walipoona Bwana anatenda miujiza ambayo wao hawawezi kuitenda, pale walipoona Bwana anawarejeza watu wengi kwa Mungu kuliko wao…Na mioyoni Roho Mtakatifu alikuwa akiwashuhudia kabisa kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu…na walikuwa wanajua kabisa katumwa na Mungu lakini kwasababu ya wivu..wakawa wanajitoa ufahamu na kumkufuru.. Soma..

Mathayo 22:15 “Ndipo Mafarisayo wakaenda zao, wakafanya shauri, jinsi ya kumtega kwa maneno.

16 Wakatuma kwake wanafunzi wao pamoja na Maherodi, wakasema, Mwalimu, twajua ya kuwa wewe u mtu wa kweli, na njia ya Mungu waifundisha katika kweli, wala hujali cheo cha mtu awaye yote, kwa maana hutazami sura za watu”.

Unaona, walijua kabisa Kristo alikuwa mtu wa kweli aliyetumwa na Mungu..

Soma tena.. Yohana  3:1-3 utalithibitisha hilo…

Yohana 3:1 “Basi palikuwa na mtu mmoja wa Mafarisayo, jina lake Nikodemo, mkuu wa Wayahudi.

2 Huyo alimjia usiku, akamwambia, Rabi, twajua ya kuwa u mwalimu, umetoka kwa Mungu; kwa maana hakuna mtu awezaye kuzifanya ishara hizi uzifanyazo wewe, isipokuwa Mungu yu pamoja naye”.

Lakini pamoja na hayo yote nguvu ya wivu ilikuwa kubwa ndani yao ikazidi nguvu ya kumpenda..na hatimaye wakafanya hila mpaka za kutaka kwenda kumsulubisha mfalme wao..Walimsulubisha moyoni wakijua kabisa huyu ni mwana wa Mungu aliyetumwa kutoka mbinguni…Hilo halikuwa na shaka mioyoni mwao. Walijua kabisa ndiye mfalme aliyetabiriwa kuja ulimwenguni.

Na hata walipompeleka kwa Pilato..Haraka sana Pilato ambaye hakuwa Myahudi akajua kuwa hakukuwa na kosa lolote alilolifanya Bwana Yesu ambalo linastahili yeye kusulubiwa lakini ni kwasababu tu ya wivu…Hawa wayahudi wamesikia tu wivu alivyojiita yeye ni mwana wa Mungu..Hilo tu! Wala hakuna lingine…walimwonea wivu kwa miujiza aliyokuwa anaitenda ambayo wao walishindwa kuitenda na wala hakuna lingine, na jinsi anavyowajalia watu wengi kupata wokovu…Kwahiyo hata Pilato aliliona hilo kama biblia inavyosema katika..

Marko 15:9 “Pilato akawajibu, akisema, Je! Mnataka niwafungulie mfalme wa Wayahudi?

10 Kwa maana alitambua ya kuwa wakuu wa makuhani wamemtoa kwa HUSUDA.

11 Lakini wakuu wa makuhani wakawataharakisha makutano, kwamba afadhali awafungulie Baraba”.

Sasa neno ‘HUSUDA’ maana yake ni ‘WIVU’ soma tena (Mathayo 27:17-18)..Kwahiyo unaona Pilato alishawajua kabisa hawa watu ni wivu ndio uliowafanya watake kumwua Yesu na wala hakuna lingine..alijua kabisa mioyoni mwako wanamwamini Yesu na kwamba “Yesu katoka kwa Mungu, na ni mfalme wao” lakini kwa kuwa wamemwonea wivu ndio maana wanataka afe…Ndio maana Pilato alikuwa akiwauliza kwa kurudia rudia.. “kama kweli wamemaanisha kumuua mfalme wao”

Yohana 19:13 “Basi Pilato, aliposikia maneno hayo, akamleta Yesu nje, akaketi juu ya kiti cha hukumu, mahali paitwapo Sakafu ya Mawe, au kwa Kiebrania, Gabatha.

14 Nayo ilikuwa Maandalio ya pasaka, yapata saa sita. Akawaambia Wayahudi, TAZAMA, MFALME WENU!

15 Basi wale wakapiga kelele, Mwondoshe! Mwondoshe! Msulibishe! Pilato akawaambia, JE! NIMSULIBISHE MFALME WENU! Wakuu wa makuhani wakamjibu, Sisi hatuna mfalme ila Kaisari”.

Wivu ni mbaya sana unakufanya umkane Mtu, hata kama unamwamini na kumpenda…

Na ndio maana mwishoni kabisa baada ya kusulubishwa Bwana Yesu, Pilato aliandika anwani juu ya msalaba wa Bwana Yesu kwa lazima.. “Yesu Mnazareti, Mfalme wa Wayahudi”

Yohana 19:19 “Naye Pilato akaandika anwani, akaiweka juu ya msalaba, imeandikwa, YESU MNAZARETI, MFALME WA WAYAHUDI.

20 Basi anwani hiyo waliisoma wengi katika Wayahudi; maana mahali pale aliposulibiwa Yesu palikuwa karibu na mji; nayo iliandikwa kwa Kiebrania, na Kirumi, na Kiyunani.

21 Basi wakuu wa makuhani na Wayahudi wakamwambia Pilato, Usiandike, Mfalme wa Wayahudi; bali ya kwamba yule alisema, Mimi ni mfalme wa Wayahudi.

22 PILATO AKAJIBU, NILIYOANDIKA NIMEYAANDIKA”.

Unaona hapo?..Pilato aling’ang’ania kuandika anwani ile kwa lazima?…kwanini?..ni kwasababu anaujua unafiki wa mafarisayo..mioyoni mwao walimwamini lakini mdomoni walimkana na kumtukana na kumsulubisha na hiyo yote ni kwasababu ya wivu tu!. Na ndio maana Pilato akaandika anwani ile.

Yohana 12:42 “Walakini hata katika wakuu walikuwamo wengi waliomwamini; lakini kwa sababu ya Mafarisayo hawakumkiri, wasije wakatengwa na sinagogi”.

Sasa sio wote kabisa waliomwamini, Bwana Yesu…wapo ambao ni kweli hawakumwamini kabisa pamoja na ishara zote zile alizozifanya…lakini asilimia kubwa ya mafarisayo na wakuu wa makuhani walimwamini Bwana mioyoni mwao lakini WIVU ukawasababisha kumsulubisha Bwana, na sio Bwana tu bali hata mitume wake walisumbuliwa na mafarisayo hao hao..na yote hiyo ni kutokana na wivu tu.

Matendo 5:16 “Nayo makutano ya watu wa miji iliyoko kandokando ya Yerusalemu wakakutanika, wakileta wagonjwa, nao walioudhiwa na pepo wachafu; nao wote wakaponywa.

17 Akaondoka Kuhani Mkuu na wote waliokuwa pamoja naye, (hao ndio walio wa madhehebu ya Masadukayo), WAMEJAA WIVU,

18 wakawakamata mitume wakawaweka ndani ya gereza;”

Hiyo ndiyo silaha shetani aliyotumia kumpeleka Bwana msalabani…Na silaha hiyo hiyo anaitumia leo kuangamiza watu..Je! na wewe una wivu?…kama unaingiwa na wivu ndugu yako akipata jambo Fulani ambalo wewe huna ujue unakaribia kufanyika chombo cha shetani kumwangamiza, kama unasikia wivu jambo Fulani zuri ndugu yako, au jamii yako, au rafiki yako analolifanya, kama unasikia wivu, mwingine anapooa, au anapoolewa au anapofanya hiki au kile..au anapotoka hatua moja mpaka  nyingine…kuna hatari kubwa ya kufanyika chombo cha shetani. Na wivu ukizidi sana unakuwa huna tena huruma..unakuwa unatamani kifo kwa huyo ndugu yako kama vile Kaini, alivyomwonea wivu ndugu yake mpaka akaenda kumwua.

Hivyo ni kwa namna gani utashinda Wivu?

Kwanza ni kwa kumpa Yesu Kristo maisha yako?..Unapookoka Bwana anakufanya kuwa kiumbe kipya, na ya kale yote yanakuwa yamepita, unakuwa umefanyika kiumbe kipya…Ule utu wa zamani, Bwana anauzika, Nia yako Bwana anaigueza kutoka kutazama vitu vya ulimwengu huu vinavyopita na kutazama mambo ya ulimwengu ujao ya milele yasiyoharibika..Hivyo kunakuwa hakuna shughuli yoyote ya kidunia ambayo itaweza kukupa wivu ndani ya moyo wako kwasababu nia yako imeshageuzwa na kuutazama ulimwengu ujao ambao utajiri wake na hazina yako hauna mwisho.

Pili baada ya kuokoka unapaswa uanze kujiwekea hazina yako mbinguni, Biblia inasema hazina yako ilipo ndipo na moyo wako utakapokuwepo…Hazina yako ikiwa kubwa katika mambo ya ulimwengu huu na moyo wako lazima utakuwa huko huko, hilo haliepukiki, kama ndoto zako kubwa kuliko zote ni wewe kupata mali nyingi sana ili hatimaye watu wote waje kukuona na kukuangukia na kukuheshimu, hapo roho ya wivu hauwezi kuiepuka, kwasababu atakapotokea mtu kakuzidi kidogo tu au unamwona ananyanyuka utamwonea wivu. Ndicho kilichowakuta mafarisayo na masadukayo, walikuwa na ndoto kubwa za wao waonekane wapo juu ya watu wote, na alipotokea mwingine mwenye nguvu kuliko wao wakaishia kumwonea wivu.

Lakini kama hazina yako ipo mbinguni, kwamba ndoto yako kubwa ni siku ile uirithi mbingu kwa daraja la kwanza, na kuwa na thawabu kubwa kule, kamwe hutakaa umwonee mtu wivu kwa vitu vya kidunia vinavyopita…Hazina yako inapoongezeka mbinguni, mawazo yako, akili yako, na moyo wako wote unakuwa kule, unakuwa kila siku unatafakari utukufu na thawabu zinazokungoja kule, na hivyo habari ya kuanza kuona wivu kwa vitu vya kidunia unakuwa huna..

Na hazina ya mbinguni unaitengeneza kwa kumpendeza Mungu na kwa kuifanya kazi yake…Na kazi yake sio kuhubiri tu, bali hata ile ya kuosha choo cha nyumba ya Mungu ni kazi yake yenye thawabu kubwa kule, hata ile ya kuwaombea watakatifu ni kazi yake yenye thawabu kubwa sana…n.k Unapofanya hayo bila ulegevu Roho Mtakatifu kila siku atakuwa anakushuhudia ndani yako kwamba thawabu yako ni kubwa mbinguni, na inazidi kuongezeka siku baada ya siku, hivyo kamwe huwezi kumwonea wivu mtu aliyeoa/ kuolewa na wewe hujaolewa, au jirani yako ambaye ni bilionea..

Ufunuo 2:17 “Yeye ashindaye nitampa baadhi ya ile mana iliyofichwa, nami nitampa jiwe jeupe, na juu ya jiwe hilo limeandikwa jina jipya asilolijua mtu ila yeye anayelipokea………

26 Na yeye ashindaye, na kuyatunza matendo yangu hata mwisho, nitampa mamlaka juu ya mataifa,

27 naye atawachunga kwa fimbo ya chuma, kama vyombo vya mfinyanzi vipondwavyo, kama mimi nami nilivyopokea kwa Baba yangu”……

Ufunuo 3:5 “Yeye ashindaye atavikwa hivyo mavazi meupe, wala sitalifuta kamwe jina lake katika kitabu cha uzima, nami nitalikiri jina lake mbele za Baba yangu, na mbele ya malaika zake”………..

12 Yeye ashindaye, nitamfanya kuwa nguzo katika hekalu la Mungu wangu, wala hatatoka humo tena kabisa, nami nitaandika juu yake jina la Mungu wangu, na jina la mji wa Mungu wangu, huo Yerusalemu mpya, ushukao kutoka mbinguni kwa Mungu wangu, na jina langu mwenyewe, lile jipya…….

21 Yeye ashindaye, nitampa kuketi pamoja nami katika kiti changu cha enzi, kama mimi nilivyoshinda nikaketi pamoja na Baba yangu katika kiti chake cha enzi”.N.k

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

NI NANI ALIYEWALOGA?

JE NI DHAMBI KUWA NA MAHUSIANO KABLA YA NDOA?

Kwanini kila nikitaka kusali naingiwa na uvivu?

NINI TOFAUTI KATI YA KARAMA, UTENDAJI KAZI NA HUDUMA.

MSIJISUMBUE KWA NENO LOLOTE.

TOA SADAKA ISIYO NA KASORO KWA BWANA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

JINI MAHABA NI NINI?

Jini Mahaba yupo kibiblia?, Mtu mwenye jini mahaba anakuwaje?

Moja ya elimu inayowachanganya wengi na inayopotoshwa ni Elimu juu ya mapepo..

Mapepo kwa lugha nyingine wanaiwa majini…Ni kitu kimoja kinachojulikana kwa majina mawili tofauti, ni kama MWANADAMU na MTU. Hayo ni majina mawili tofauti lakini yanaelezea kitu kimoja.

Sasa mapepo ni roho za malaika walioasi mbinguni, ambao walitupwa chini pamoja na kiongozi wao mkuu shetani. Baada ya kutupwa chini ndio yakaitwa mapepo.

  • MAPEPO YANAPOMWINGIA MTU YANAMFANYA AWEJE?

Mapepo hayo yanaweza kumwingia mtu na kumfanya awe na tabia yoyote ile wanayotaka wao. Mapepo haya yanaweza kumwingia mtu na kumfanya awe mwizi, mengine yanaweza kumfanya mtu awe mlevi, mengine yanaweza kumfanya mtu awe mzinifu au mwenye tabia ya zinaa.

  • JINI MAHABA.

Sasa mapepo ambayo yanawafanya watu wabadilike tabia na kuwa wazinifu au kuhisi wanafanya mapenzi na watu wakati wa kulala ndio hayo WATU wanayoyaita MAJINI MAHABA. Lakini kiuhalisia mapepo hayo hayana jinsia yoyote kwasababu ni roho. Na haya yanapomwingia mtu yoyote ambaye hajaokoka.(yaani ambaye hajampokea Yesu Kristo kama Bwana na mwokozi wa maisha yake) yanamfanya anakuwa mtumwa wa dhambi hiyo ya zinaa katika ndoto au katika maisha yake ya kawaida..Kwa mtu wa kawaida huwa hayamtokei kwa wazi lakini kwa wale ambao wamekufa kabisa kiroho na wamejiuza kwa shetani huwa yanaweza kujidhihirisha kwa macho kabisa..

Lakini kumbuka shetani siku zote ni mwongo pamoja na mapepo yake yote, biblia inasema shetani  anao uwezo wa kujigeuza na kuwa hata malaika wa Nuru (Kasome 2Wakoritho 11:14), hivyo sio ajabu kuweza kujigeuza na kuwa hata mwanamke mzuri au mwanamume mzuri wa kuvutia, lakini ndani yake ni pepo mbaya na mchafu. Watu wengi wanadanganyia na kufikiri kuna mapepo ya kike..Ndugu usidanganyike hakuna kitu kama hicho…hayo ni maroho tu hayana jinsi, shetani ni baba wa uongo siku zote.

  • JE MTU ANAINGILIWAJE NA HIZI ROHO?

Kwa asili roho hizi za mapepo huwa hazimtokei mtu kwa wazi kama tulivyotangulia kujifunza hapo juu, isipokuwa kwa mtu ambaye tayari amejiuza kwa shetani moja kwa moja, hususani kama mtu ni mshirikina, au mganga au mchawi kabisa, huyu anaweza kuziona kwa macho..Lakini kwa wengine ambao wapo nusunusu, vuguvugu..roho hizi zinawaendesha katika ndoto tu na katika tabia zao. Katika ndoto wanakuwa wanaota wanafanya zinaa na katika tabia wanakuwa wanatabia zilizokithiri za uasherati mpaka wengine kuwafanya kuwa mashoga au wasagaji, au walawiti au wafiraji.

Na zifuatazo ni njia mapepo haya yanayozitumia kuingia ndani ya watu.

  1. Kufanya zinaa nje ya ndoa
  2. Kutazama picha/video za ngono/Pornograph
  3. Mazungumzo machafu yahusuyo zinaa na uasherati
  4. Kuvaa mavazi ya kikahaba, kama kuvaa suruali kwa wanawake, na vitop pamoja na vimini
  5. Matumizi ya vipodozi na urembo..ikiwemo kujichubua, kuchonga nyusi, kusuka mitindo mitindo na kujipulizia marashi kupindukia.
  6. Kusoma hadithi na Majarida ya mambo yanayozungumzia zinaa, pamoja na kutazama filamu na movie za maudhui hayo.
  • JE KUJITAZAMA KWENYE KIOO KUNAMLETA JINI MAHABA?

Kujitazama kwenye kioo hakuna uhusiano wowote na kuingiwa na roho hizo..Isipokuwa mtu mwenye tabia ya kujipamba, na kujichubua, kusuka suka, kuchonga nyusi anakuwa na tabia ya kujiangalia kwenye kioo mara kwa mara..hivyo hiyo tabia ya kujipamba na kuchonga nyusi ndio mlango wa mapepo hayo kuingia lakini sio kujitazama kwenye kioo.

  • JE MTU MWENYE MAPEPO/JINI MAHABA ATAKWENDA MOTONI?

Biblia inasema katika..

Ufunuo 21:27 “Na ndani yake hakitaingia kamwe cho chote kilicho kinyonge, wala yeye afanyaye machukizo na uongo, bali wale walioandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo”.

Kilicho kinyonge kinachozungumziwa hapo ndio hicho chenye roho ya mapepo ndani yake..Kwasababu mtu mwenye roho ya mapepo atakuwa na tabia tu fulani chafu ambazo watu wenye tabia hizo biblia inasema hawataurithi uzima wa milele. Mtu mwenye pepo la zinaa/jini mahaba ni lazima atakuwa mzinifu na mbinguni hawataingia wazinifu..Mtu mwenye pepo la ulevi ni lazima atakuwa tu mlevi na mbinguni hawataingia walevi.

Ufunuo 21:8 “Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili..”

Mbinguni wataingia tu watu wenye Roho Mtakatifu..ambao ni watakatifu.

Waebrania 12:14 “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao; “

  • NI NAMNA GANI PEPO LA ZINAA/JINI MAHABA LITAKUTOKA?

Kwanza ni kwa kumpa Yesu Kristo maisha yako, unatubu kwa kudhamiria kabisa kuacha dhambi na kisha unajiepusha na milango kujitenga na milango hiyo sita hapo juu tuliyoiona ambayo ndio mlango ya kuingiwa na roho hizo chafu. Na roho hizo zitakuacha kabisa na utakuwa huru.

Bwana akubariki

Group la whatsapp Kwa mgawanyo bora wa masomo download App hapa>> App wingu la mashahidi

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Rudi Nyumbani:

Print this post

JE NI KWELI SAMAKI NGUVA YUPO?

Je ni kweli kuna samaki nguva?..Je kwenye  biblia nguva katajwa?

Jibu: Ukweli ni kwamba hakuna mahali popote katika biblia palipotajwa uwepo wa samaki aina ya nguva. Maana yake ni kwamba hakuna kiumbe cha namna hiyo kilichoumbwa na Mwenyezi Mungu.

Lakini utauliza je! hicho wanachokiona watu ni nini? ambacho kimaumbile kinaonekana nusu mtu nusu samaki?

Jibu ni kwamba vinavyoonekana na watu vyenye umbo kama hilo ni roho za mapepo. Kumbuka biblia inasema shetani anao uwezo wa kujigeuza na kuwa hata Malaika wa Nuru (Kasome 2Wakorintho 11:14), sasa si zaidi kujigeuza na kuwa kiumbe kiumbe kingine chochote chenye umbo la ajabu?. Anao huo uwezo, anaweza kujiguza na kuwa kama nusu mtu nusu mbuzi, anaweza kujigeuza na kuwa nusu mtu nusu nyoka, vivyo hivyo anao uwezo wa kujigeuza na kuwa nusu mtu nusu samaki (ambao ndio hao wanaojulikana kama nguva).

Sasa shetani na mapepo yake wote wanao huo uwezo wa kujigueza na kuwa hivyo viumbe vya ajabu..Na lengo lao ni lile lile moja..Kuwapoteza wanadamu na kuwaweka mbali na kweli ya Mungu, na hatimaye wafe katika dhambi zao na kuingia Jehanamu ya moto, wala hana lingine. Hivyo shetani kila siku anabuni njia mpya za kuwafanya watu wawe wabaya zaidi na kuzidi kuuamini uongo wake.

Sasa haya mapepo ambayo yanajigeuza maumbile..huwa hayawatokei wala hayawaingii watu waliookoka (Yaani waliomwamini Yesu Kristo na kuoshwa dhambi zao kwa damu yake). Huwa yanawatokea na kuwaingia watu ambao katika roho wapo dhaifu sana, na hao ni wale wote ambao wapo nje ya Neema ya Yesu Kristo. Huwa yanawajia katika ndoto, kuwahimiza kufanya jambo fulani lililo kinyume na neno la Mungu au kuwapa hisia ambayo ni kinyume na Neno la Mungu..

Na hisi kubwa na ya kwanza yanayopeleka kwa mtu ni hisia ya ZINAA na UASHERATI. Kwasababu hiyo ndio dhambi ya kwanza ambayo shetani anatumia kumwangusha nayo mwanadamu na ndio Dhambi ya asili.

Hisia ya pili ni.. kutenda mabaya, aidha kuabudu sanamu, au miungu, kuwa mshirikina, au wakati mwingine yanamletea mtu hisia za kuwa na chuki na jamii ya watu fulani, au mtu fulani na kumpeleka hata kutamani kuua, au kuiba au kudhuru. Hiyo ndio kazi ya mapepo hayo yanapomwingia mtu ndani yake…na haya yana majina mengi (wengine wanayaita majini, wengine vibwengo n.k)..lakini ndio hayo hayo mapepo…

Mapepo haya yakiwemo hayo yanayojigeza na kuwa huo mfano wa nguvu, huwa hayamtokea mtu kwa macho, yanakuwa ni roho ambazo zinamwingia mtu au zinatembea na mtu, na mtu anaweza kuziona tu katika ndoto..lakini si katika macho ya asili..Lakini pia kama mtu huyo hali yake ya roho ipo chini sana yanaweza kumtokea kabisa na akayaona dhahiri, wengi wa wanaoyaona hayo ni wale ambao ni wachawi au waganga, au washirikina…ambao wameshajiuza kwa shetani kikabisa.

Kwahiyo nguva si kiumbe kilichoumbwa ambacho kinaishi baharini, bali ni roho za mapepo, kama umewahi kuota upo na nguva au umewahi kumwona..Basi tambua kuwa hali yako katika roho ipo chini sana na ni hatari.

Hivyo suluhisho ni kumpa Yesu maisha yako, unapoamua kugeuka na kutubu kwa kumaanisha kuacha dhambi na maisha ya machafu uliyokuwa unaishi huko nyuma, na kwenda kubatizwa katika ubatizo sahihi, roho hizo zitakuacha hata pasipo kwenda kuwekewa mikono na mtu yoyote na utakuwa huru mbali na utumwa wa roho za mapepo.

Bwana akubariki sana.

Group la whatsapp Kwa mgawanyo bora wa masomo download App hapa>> App wingu la mashahidi

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Rudi Nyumbani:

Print this post

KWA HIYO NDUGU, VUMILIENI, HATA KUJA KWAKE BWANA.

Yakobo 5:7 “Kwa hiyo ndugu, vumilieni, hata kuja kwake Bwana. Tazama, mkulima hungoja mazao ya nchi yaliyo ya thamani, huvumilia kwa ajili yake hata yatakapopata mvua ya kwanza na ya mwisho.

8 Nanyi vumilieni, mthibitishe mioyo yenu, kwa maana kuja kwake Bwana kunakaribia”.

Kwanini mtume huyu alifananisha kumngojea Bwana na uvumilivu na wa mkulima anayengojea mazao ya nchi, mpaka atakapopata mvua ya kwanza na ya mwisho.?

Hii Mvua ya kwanza na mvua ya mwisho ni ipi?

Mvua ya kwanza kwa jina lingine ni mvua ya masika, na mvua ya mwisho ni mvua ya vuli..Israeli tangu zamani hadi sasa ni nchi ya jangwa, sio kama huku kwetu kwenye ukanda wa kitropiki, ardhi ina unyevunyevu wakati wowote, kiasi kwamba hata ukitaka kuchimba kisima popote unakutana maji chini..Jambo hilo huwezi kulikuta katika nchi za jangwa kama vile Israeli..

Hivyo wakulima walikuwa wanategemea sana misimu ya mvua ili kulima na kupanda, wakati mwingine wowote ilikuwa haiwezakani kutokana na kwamba ardhi kuwa kame na ngumu.

Hivyo wakulima ilikuwa inawapasa wangojee wakati wa mvua tu, ndipo wafanye kazi za ukulima, Kwasababu hata mito haikuwepo, na hata kama ipo basi haijitoshelezi yote kwa kilimo cha umwagiliaji..Na hiyo ilikuwa inawafanya wasubirie tu wakati wa mvua, na utakapofika huwa basi wanafanya kazi kama vichaa kwa uvumilivu wote na kwa subira yote kwasababu wanajua upo wakati ambao hawataweza kufanya kazi tena.. Sasa kulingana na Jeografia ya Israeli, mvua ya masika kwao ilikuwa inaanza mwezi wa 10-11, na vuli mwezi 3-4, tofauti na huku kwetu ambapo ni kinyume chake.

Sasa masika ilikuwa ikishaanza tu wakulima wote wanatoka wanaingia mashambani na kuanza kuandaa mashamba na kupanda mbegu zao, na kuzipalilia…Mpaka itakapoisha, Lakini baadaye tena mvua nyingine ndogo ndogo zilikuwa zinaendelea si kali kama zile za Masika ndio hizo za Vuli, ili kustawisha tu mazao, na kuifanya ardhi isipoteze unyevu wake, mpaka misimu yote ya mvua itakapoisha moja kwa moja

Sasa ndio hapa Mtume Yakobo anafanisha kumngojea kwetu Bwana kama mkulima aliye katika msimu wa kilimo chake anavyovumilia mpaka mazao yake yatakapopata mvua zote mbili yaani ya kwanza na ya mwisho… Na akishamaliza basi huvuna na kuyaweka ghalani, jasho lake, na taabu yake sasa inakuwa imekwisha..

HIVYO,MVUA YA KWANZA, NA YA MWISHO ROHONI INAFUNUA NINI?

Vivyo hivyo na sisi tunaomgonjea Bwana, Tulishanyeshewa mvua ya kwanza, siku ile ya Pentekoste takribani miaka 2000 iliyopita, Kazi ikaanza..sasa kuanzia huo wakati tumekuwa tukilima, na kupanda, na kupalilia shamba la Bwana..Lakini pia iliahidiwa mvua nyingine itakayokuja huko mbeleni ambayo itakayokamilisha taabu yetu ya ulimaji..

Ndugu kama hujui ni kuwa tayari tumeshaingia katika kipindi cha msimu wa mwisho wa mvua ambayo ndio ile mvua ya mwisho ya vuli (rohoni), Na mvua hii ilianza mwaka wa 1906, Huu ni wakati ambapo kwa mara nyingine tena Mungu aliijilia dunia kwa vipawa na karama za roho, na kazi zile zile zilikuwa zinatendeka wakati ule wa Pentekoste ya mitume miaka 2000 iliyopita, mambo ambayo hapo katikati yalikuwa hayafanyiki, wala hayaonekani.. Hivyo kuanzia wakati huo ndio, Karama zile zote za rohoni zilianza kurejeshwa katika kanisa tena upya, vilevile Mungu akanyanyua watumishi wake wengi waaminifu kulithibitisha hilo kuwa wakati huo umeanza watu hao ikiwemo (William Seymor, baadaye William marrion Branham, Billy Granham, Oral Roberts, TL Osborn na wengineo wengi)

Tangu huu wakati injili ilianza kuhubiriwa kwa nguvu na ujumbe ulikuwa ni huu…WAKATI WA MAVUNO UMEKARIBIA!! BWANA ANAKARIBIA KULICHUKUA KANISA LAKE..

Wote hawa walikuwa na ujumbe huo, wote walijua tupo katika wakati ule wa MVUA YA MWISHO, wa mvua ya vuli..Na mpaka sasa ndipo mvua hiyo inakaribia kufika ukingoni kabisa… kwenda kugota..Na ikishagota, basi hakutakuwa ni mvua nyingine tena milele..

Ndugu hii neema unayoiona, unapoona unahubiriwa injili kirahisi hivi, Neno la Mungu limezagaa kila mahali, lakini unalipuuzia usidhani ilikuwa hivyo kipindi cha karne ya 19 kushuka huko chini..Hii miujiza unayoina na karama za rohoni unazoziona usidhani zilikuwepo muda wowote wa kanisa… Wewe Mungu amekupa neema ya kuishi katika msimu huu wa mvua ya Vuli rohoni, ambayo ipo karibuni kuisha..Lakini unaichezea hii nafasi..Upo wakati utaitamani lakini mlango wa neema utakuwa umeshafungwa..

Kipindi si kirefu, kanisa litanyakuliwa, wala hakuna mtu atakayesema mimi sikuambiwa wala sikujua, wakati huo Bwana atakusanya mavuno yake na kuyaweka ghalani na magugu kuyatupa motoni..Wote tunafahamu, hali ilivyo sasa, magonjwa ya kutisha yanavyozidi kuzuka, tetesi za vita, matetemeko,manabii wa uongo, watu kupenda fedha, watu kupenda anasa kuliko kumpenda Mungu, ushoga kama ilivyokuwa katika siku za Lutu, n.k. yote hayo yaliandikwa na tukaambiwa hizo ndio zitakuwa dalili kuu zitakazotutambulisha kuwa Kristo yupo mlangoni kurudi..

Lakini sisi tuliompokea tumeambiwa, tuyaonapo hayo..Basi ndio tunyanyue vichwa vyetu juu, kwasababu ukombozi wetu umekaribia..

Mvua hii ya neema ipo ukingoni, mkaribishe Bwana moyoni mwako kabla haijakoma kabisa moyoni mwako..Sisi sio wa kuambiwa tena tuvumilie kwasababu sisi tupo tayari wakati wa mavuno, waliokuwa wanapaswa wavulie ni wale wa makanisa mengine lakini sio sisi wa kanisa la mwisho la LAODIKIA.

Shalom.

Tafadhali “Share” Ujumbe huu na kwa wengine. Pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email, au Whatsapp au inbox yako ya faceboook, basi utujuze inbox nasi tutafanya hivyo. Vilevile usiache kutembelea website yetu hii (www wingulamashahidi org) kwa mafunzo zaidi.

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Sabato halisi ni lini, Je! ni Jumapili au Jumamosi?, Ni siku gani itupasayo kuabudu?

BARAGUMU NI NINI?

KUOTA NYOKA.

USIJARIBU KUMGEUZA MUNGU MGANGA WA KIENYEJI,UTAKUFA.

KUSUDI LA MIMI KUWEPO DUNIANI NI LIPI?

Kwanini wakristo wengi ni maskini?.

Rudi Nyumbani:

Print this post