Kama watu wamefunga ndoa ya serikali na wakaachana, wanaweza kuoa au kuolewa tena na watu wengine?
JIBU: Shalom, Ndoa iliyofungwa kiserikali, au kwa namna yoyote ile…ambayo imehusisha makubaliano ya pande zote mbili na taratibu zote ikiwemo mahari na kutangazwa mbele ya jamii kuwa watu hao wawili wamekuwa mume na mke…kwa namna yoyote ndoa hiyo haipaswi kuvunjwa kwasababu imetangazwa tayari mbele ya mashahidi, hivyo hiyo tayari ni ndoa (ingawa sio ya kikristo)..
Na endapo ikitokea wawili hao wamefunga ndoa hiyo ya kiserikali na wakaachana, basi mbele za Mungu watakuwa na hatia…(Na kumbuka ndoa ya kiserikali hawafungi na wakristo, yaani maana yake mtu ambaye tayari ameshamjua Yesu Kristo na kumwamini, hawezi kwenda kufungishwa ndoa ya kiserikali, mkristo anayefunga ndoa ya kiserikali ni mwasherati), wanaofungishwa ndoa hizo za kiserikali ni wale ambao bado hawajamjua au kumwamini Yesu Kristo, au kwa namna nyingine wapagani, mfano wa ndoa hizo ni kama ile ya Herodia ambayo alimwacha mumewe aliyeitwa Filipo na kwenda kuolewa na ndugu ya mume wake, sasa ndoa hiyo ya Herodia na Filipo haikuwa ya kikristo, pengine ilikuwa ya kiserikali au ya kitamaduni za taifa lao au ya kidini yao lakini maadamu ilikuwa imeshahalalishwa na jamii yao au serikali yao basi ilikuwa ni dhambi kwa Herodia kumwacha mume wake huyo na kwenda kuolewa na ndugu ya mume wake (kasome kisa hicho katika Marko 6:17-18).
Lakini ikitokea mmoja wa waliofungishwa ndoa ya namna hiyo /kiserikali kaamini na kuwa mkristo na mwenzake hataki kuishi naye kwasababu tu kawa mkristo na akaamua kumuacha..hapo huyu aliyeachwa kwasababu ya Imani yake ya kikristo atakuwa huru kuolewa/kuoa na mtu mwingine ambaye ni mkristo mwenzake tu, lakini kama hata baada ya kuokoka kwake mwenziye ambaye anaishi naye hataki kuokoka lakini bado anataka kuendelea kuishi naye..huyu hana budi kuendelea kuishi naye hata kama hajaokoka..na endapo akimwacha kwasababu tu hataki kuokoka atakuwaa na hatia mbele za Mungu..Na akimwacha na kwenda kuoa/kuolewa na mwingine atakuwa anazini.
Sasa wapo watu huko nyuma kabla ya kuokoka walifunga ndoa ya kiserikali, na baada ya kuokoka wanapojaribu kuwashawishi wake zao/waume zao nao pia waokoke kama wao, wanapowaona wanakataa basi wanakusudia kuwaacha..ingawa bado wanapedwa na hao wenza wao na hawajaachwa..lakini wao kwasababu wameokoka hawataki tena kuishi na wale waume zao/wake zao ambao hawajaokoka..Ndugu usifanye hivyo ni dhambi kubwa sana!..Mume wako/mke wako uliyefunga naye ndoa hata kama ni mlevi lakini hataki kukuacha, basi hupaswi kumuacha…na hiyo ni kulingana na Biblia kasome..1Wakorintho 7:10-15.
Na pia ikitokea wote wawili hapo kwanza walikuwa wamefunga ndoa ya kiserikali na sasa wameokoka na kuifahamu neema ya Kristo, Hawa wote wawili wanapaswa kwenda kanisani kuifanya ndoa yao iwe ya kikristo. Kwasababu ilipofungwa kiserikali haikumhusisha Kristo wala maagizo yake, Wanapaswa kwenda kuahidiana upya mbele za Mungu na wanadamu kwamba wataishi kwa uaminifu pasipo kuachana, na kifo ndicho kitakachowatenganisha, na kwamba watakuwa kielelezo kwa watakatifu wengine wowote kwa kuishi katika ndoa ya kikristo ya mume mmoja na mke mmoja, na mambo mengine ambayo watayaahidi mbele ya kanisa la Mungu na mbele ya Kristo mwenyewe. Baada ya hapo ndoa yao itabarikiwa na Mungu, na kuwa ya kikristo na zile baraka zote za wanandoa zitafuatana nao.
Sasa kuna kundi lingine ambalo linajiita ni wanandoa…Hili ni lile ambalo walikutana tu na kuamua kuishi Pamoja, pasipo utaratibu wowote…ni ile watu wawili wamekutana tu kijana na binti na kuwekana ndani, hakuna cha mahari, hakuna imani. Hawa kibiblia wanafanya uasherati (NI WAASHERATI).
Na endapo ikitokea mmoja kaamini katika hali hiyo waliyopo ya kukaa Pamoja (maana yake katubu na kuwa Mkristo). Moja kwa moja yule aliyeamini anapaswa avunje hayo mahusiano, kwasababu ni uasherati ndio aliokuwa anaufanya..Anapaswa avunje hayo mahusiano hata kama wameshazaa Watoto, arudi kwa wazazi wake, au akaishi peke yake kwa kujitegemea na wanawe… mpaka huyo mwenzake naye atakapotubu kama yeye na kuwa mkristo na kwenda kufunga ndoa kanisani. Lakini endapo huyo mwingine kakataa kutubu katakata na kujisalimisha kwa Yesu Kristo, basi huyu aliyetubu yupo huru kuolewa/kuoa mtu mwingine lakini aliye mkristo kama yeye tu!…(hapaswi kwenda kuoa/kuolewa na mtu ambaye sio mkristo)
Kumbuka tena mtu ambaye ameshamjua Yesu Kristo, na kufahamu kuwa ndoa halali ni ile ya kikristo (mfano wa mimi na wewe ambao tumeshajua sasa) na ameshafahamu kuwa inapaswa ifungwe mbele ya kusanyiko la Kristo, akienda kufunga ndoa yoyote ile kinyume na hiyo, akaenda kufunga ndoa aidha ya kimila au ya kiserikali au akijichukulia tu mke/mume na kuishi naye ndani…pasipo kwenda kuifungisha ndoa yake kanisani BASI ANAFANYA UASHERATI!!…Na waasherati wote biblia inasema hawataurithi ufalme wa mbinguni (1Wakoritho 6:9).
Na pia maana halisi ya neno ndoa ni Muunganiko wa MUME na MKE na sio muunganiko wa mume na mume au mke na mke…Hivyo hicho kinachoitwa ndoa ya jinsia moja hakipaswi kiitwe hivyo…kinapaswa kiitwe “uasherati wa jinsia moja”…na sio “ndoa ya jinsia moja”..Hivyo serikali inayohalalisha “uasherati wa jinsia moja” Huo Mungu kaukataa na ni machukizo makubwa mbele za Mungu..kasome Walawi 20:13.
Je umemwamini Yesu Kristo?, kama bado unasubiri nini?, hizi ni siku za mwisho na Kristo yupo karibuni kulichukua kanisa lake, je utakuwa miongoni mwa watakaonyakuliwa, Unafahamu kuwa kanisa hili tunaloishi ndio kanisa la mwisho, hakutakuwa na kanisa lingine baada ya hapa?
Bwana atubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
Je! Ni sahihi kwa mkristo kuoa/kuolewa na mtu wa imani nyingine?
Kama kuna majira ambayo si ya kufanya mchezo na masuala ya wokovu wetu hata kidogo basi ni haya. Kwani moja ya hizi siku tutashuhudia mabadiliko makubwa sana na ya ghafla katika kanisa la Kristo,..wakati ambao Bwana Yesu anakwenda kuchukua hatua ambayo hakuwahi kuichukua tangu aondoke hapa duniani.. Na hatua yenyewe ni Kuingia na kuufunga mlango wa hekalu lake.
Hayo mambo pengine utayashuhudia kwa macho yako siku si nyingi,..Kumbuka biblia inalifananisha kanisa la Kristo na hekalu lake (Waefeso 2:19-22)..Sasa ukisoma kitabu cha Ezekieli utaona anaonyeshwa matukio yanayoambata na hakalu la Mungu, Na utaona akionyeshwa malango mengi ya hekalu yakiwa wazi, lakini ukisoma ile sura ya 44 utaona Ezekieli anaonyeshwa ghafla lango la mashariki likiwa limefungwa..Na anaambiwa halitafunguliwa tena, wala mtu awaye yote hataingia kwa kupitia lango hilo.
Ndipo Ezekieli akaambiwa sababu ya lango hilo kufungwa, na sababu yenyewe ilikuwa ni hii..tusome..
Ezekieli 44:1 “Kisha akanirudisha kwa njia ya lango lile la nje, la mahali patakatifu lililoelekea upande wa mashariki; nalo lilikuwa limefungwa.
2 Bwana akaniambia, Lango hili litafungwa, halitafunguliwa, wala mtu awaye yote hataingia kwa lango hili, kwa maana Bwana, Mungu wa Israeli, ameingia kwa hilo; basi kwa sababu hiyo litafungwa”.
Unaona, sababu ni kuwa Bwana, Mungu wa Israeli (KRISTO), ameingia kwa lango hilo.. Hii ni kuonyesha kuwa mlango huo uliwekwa mahususi kwa ajili yake na si mwingine, yeye ndiye aliyekuwa amewekewa wazi mlango huo mpaka atakapofika,. Hivyo wale waliokuwa wanaingia kabla ya hapo ni neema tu, lakini haukuwekwa wazi kwa ajili yao..
Hivyo Habari hiyo jambo kwa sehemu limetimia lakini ni unabii wa siku za mwisho, wakati ambao Mlango wa Neema utafungwa.
Ndugu, huu mlango ambao tunauita wa neema tulio nao leo hii, Mungu kauacha wazi si kwasababu yetu, bali kwasababu ya Yesu Kristo, Ni mlango wa Kristo Yesu mwenyewe na sio wetu, na moja ya siku hizi, hivi karibuni atasimama, kisha ataupita, na akishaingia, basi utafungwa na ukishafungwa, Habari imeishia hapo hautafunguliwa tena milele..
Mambo yatakayokuwa yanaendelea humo ndani ni siri yake na wale watakaokuwa humo.. Kwahiyo usione unahubiriwa injili, usione unapigiwa kilele utubu dhambi ukadhani Mungu anakuangalia wewe sana, hilo jambo halipo! Mungu anamtazama Kristo tu!, achukue hatua yake, na akishaichukua, hapo ndipo kutakuwa na kilio na kusaga meno kama alivyosema, hakutania alimaanisha kweli wapo watu watalia kweli kweli wakitamani hata nusu saa nyuma lirudi watengeneze mambo yao lakini watakuwa wameshachelewa.
Luka 13:24 “Jitahidini kuingia katika mlango ulio mwembamba, kwa maana nawaambia ya kwamba wengi watataka kuingia, wasiweze.
25 Wakati mwenye nyumba atakaposimama na kuufunga mlango, nanyi mkaanza kusimama nje na kuubisha mlango, mkisema, Ee Bwana, tufungulie; yeye atajibu na kuwaambia, Siwajui mtokako;
26 ndipo mtakapoanza kusema, Tulikula na kunywa mbele yako, nawe ulifundisha katika njia zetu. 27 Naye atasema, Nawaambia, Siwajui mtokako; ondokeni kwangu ninyi nyote mlio wafanyaji wa udhalimu.
28 Ndipo kutakapokuwa na kilio na kusaga meno…”
Kumbuka hatua hiyo sio ya unyakuo, hapo unyakuo bado, mambo hayo yatatendeka hapa hapa duniani, kwasababu wakati huo utatamani umjue Kristo, lakini hutaweza tena, kwasababu anayewavuta watu kwa Kristo sasa ni Roho Mtakatifu na sio mtu mwenyewe..Hivyo Roho Mtakatifu akishaondoka juu yako huwezi tena kumfuata Mungu hata iweje..(Yohana 6:44)
Sasa muda mfupi baada ya huo wakati, Unyakuo ndio utapita, na wewe ambaye humtaki Kristo sasa…utaendelea kubaki hapa hapa duniani ambacho kitakachofuata ni dhiki kuu kabla hujafa na kuingia katika jehanamu ya moto. Kama tunavyoona mambo yalivyo sasa, ni tunaishi katika muda wa nyiongeza tu.., hii dunia ingepaswa iwe imeshaisha tangu zamani kulingana na unabii wa kibiblia, lakini dalili zote zinaonyesha sasa wakati wowote, mambo yatabadilika kwa ghafla sana. Na Mlango utafungwa na watu watatamani kuingia watashindwa..
Soma Habari hii kulithibitisha hilo tena..uone jinsi wanawali wale wapumbavu waliporudi na kukuta mlango umefungwa, ufananishe na hali itakavyokuwa wa wakristo wengi vuguvugu waliopo leo duniani..
Mathayo 25 : 1-13 “Ndipo ufalme wa mbinguni utakapofanana na wanawali kumi, waliotwaa taa zao, wakatoka kwenda kumlaki bwana arusi.
2 Watano wao walikuwa wapumbavu, na watano wenye busara.
3 Wale waliokuwa wapumbavu walizitwaa taa zao, wasitwae na mafuta pamoja nao; 4 bali wale wenye busara walitwaa mafuta katika vyombo vyao pamoja na taa zao.
5 Hata bwana arusi alipokawia, wote wakasinzia wakalala usingizi.
6 Lakini usiku wa manane, pakawa na kelele, Haya, bwana arusi; tokeni mwende kumlaki.
7 Mara wakaondoka wanawali wale wote, wakazitengeneza taa zao.
8 Wale wapumbavu wakawaambia wenye busara, Tupeni mafuta yenu kidogo; maana taa zetu zinazimika. 9 Lakini wale wenye busara wakawajibu, wakisema, Sivyo; hayatatutosha sisi na ninyi; afadhali shikeni njia mwende kwa wauzao, mkajinunulie.
10 Na hao walipokuwa wakienda kununua, bwana arusi akaja, nao waliokuwa tayari wakaingia pamoja naye arusini; mlango ukafungwa.
11 Halafu wakaja na wale wanawali wengine, wakasema, Bwana, Bwana, utufungulie.
12 Akajibu akasema, Amin, nawaambia, siwajui ninyi.
13 Basi kesheni, kwa sababu hamwijui siku wala saa”.
Je! Na wewe bado nje ya mlango huo hujaingia tu ndani mpaka sasa?..Kumbuka tena jambo hili lango hilo likishafungwa mara moja, halitafunguliwa tena milele..(Na Yesu ndiye lango) Ni heri ukatubu dhambi zako leo ikiwa hujafanya hivyo..Ili Mungu atakusamehe na kukupa uzima wa milele bure.
Ufunuo 22:17 “Naye mwenye kiu na aje; na yeye atakaye, na ayatwae maji ya uzima bure.”
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
Je! Adamu aliwasaliana na Mungu kwa lugha ipi pale bustanini?
Katika maisha kila mwanadamu ambaye ameumbwa na Mungu mkuu, ni lazima ameumbiwa kitu kinachoitwa huzuni ndani yake. Maana yake ni kwamba ni lazima atapitia vipindi vya huzuni na vile vile atapitia vipindi vya furaha. Kila mwanadamu hata kama ni mtumishi wa Mungu ni lazima atapitia hivyo vipindi..Bwana wetu Yesu Kristo ambaye alikuwa ni mkamilifu asilimia zote alivipitia si zaidi sisi tusiokuwa wakamilifu?..Ni lazima tuvipitie. Na huzuni ni kama ugonjwa ukiwekwa katika mazingira Fulani inazidi na pia ikiwekwa katika mazingira Fulani unapungua.
Na huzuni inaweza kuja aidha kutokana na kupata taarifa mbaya, au umepatwa na jambo baya..au unakwenda kupatwa na jambo baya…au wakati mwingine inakuja pale linapotokea jambo ambalo hukulitegemea au hukulipanga, au hukutamani liwe hivyo lilivyo.
Mtu anapofikia hali kama hiyo anajikuta anazama katika dimbwi kubwa la mawazo, na kukosa hamu ya kufanya jambo lolote lile..hata hamu ya kula inatoweka, wakati mwingine hata hamu ya kuishi.
Siku ile ambayo Bwana ndio alikuwa anakwenda kusulibiwa, Huzuni kubwa iliwaingia wanafunzi wake, baada ya kuwaambia kwamba muda si mrefu atakwenda kusulibiwa, na ataondoka atakwenda zake kwa Baba..
Yohana 16:5 “Lakini sasa mimi naenda zangu kwake yeye aliyenipeleka, wala hakuna mmoja wenu aniulizaye, Unakwendapi?
6 Ila kwa sababu nimewaambia HAYO HUZUNI IMEJAA MIOYONI MWENU.
7 Lakini mimi nawaambia iliyo kweli; yawafaa ninyi mimi niondoke, kwa maana mimi nisipoondoka, huyo Msaidizi hatakuja kwenu; bali mimi nikienda zangu, nitampeleka kwenu”.
Na zaidi ya yote walipoambiwa kwamba mmoja wao atamsaliti..Ndio kabisa moto wote ukakata ndani yao..Wakati wanadhani kwamba Kristo atazidi kuendelea kuwepo, yeye anawapa taarifa za msiba, kwamba anakwenda kusulibiwa..wakawa wanawaza kwanini hayo yote yampate Bwana wao, sasa maisha yatakuwaje baada ya yeye kuondoka.
Na hata Bwana alipowachukua usiku ule kwenda kusali naye hata nguvu zilikuwa zimewaisha kabisa, hawakusali sana wakalala kwasababu ya huzuni nyingi..Tusome..
Luka 22:45 “Alipoondoka katika kuomba kwake, akawajia wanafunzi wake, AKAWAKUTA WAMELALA USINGIZI KWA HUZUNI.
46 Akawaambia, Mbona mmelala usingizi? Ondokeni, mkaombe, msije mkaingia majaribuni”.
Lakini katika hali kama hiyo, Bwana aliuona udhaifu wa mioyo yao kwamba wamechoka na wanahuzuni nyingi. Lakini aliwaambia waamke waombe..kwasababu roho i radhi lakini mwili ni dhaifu…Hivyo wanapaswa waishinde hali hiyo ya huzuni..kwasababu wana huzuni, lakini siku chache baadaye watakuwa na furaha. Hivyo alijaribu kuwaasa kwamba wajaribu kuishinda huzuni ambayo ilipelekea udhaifu wa mwili wasimame waombe kwasababu majaribu hayo ni ya siku chache tu..siku mbili baadaye watakuwa na furaha isiyo na kifani. Kwasababu aliwaambia bado kitambo kifupi hawamwoni (yaani atakufa na kuzikwa)..na tena bado kitambo kidogo watamwona tena (yaani siku atakapofufuka)..wataendelea kumwona mpaka Pentekoste na watakuwa na furaha kuu.(Soma Yohana 20:20).
Katika wakati huu unaoitwa wa pasaka miongoni mwa mambo mengi tunayojifunza basi ni muhimu kulijua hili pia…USIHUZUNIKE..Pengine umepitia shida Fulani, au umepata usumbufu Fulani, au huzuni Fulani, au tabu Fulani, au taarifa Fulani, au jambo lolote lile ambalo limekuletea huzuni kubwa moyoni hata umekata tamaa ya kila kitu na ya kuendelea mbele katika imani…Huo sio wakati wa kuzidi kuipalilia huzuni kwa kukata tamaa na kuiacha Imani, sio wakati wa kulala usingizi kwa huzuni..Bali ni wakati wa kusimama na KUOMBA kwa nguvu…ni wakati wa kuzidi kuendelea mbele kwasababu huzuni hiyo ni ya kitambo tu!. Baada ya siku chache itaondoka na furaha itakurudia kama mwanzo na utajuta kwanini siku chache nyuma ulikuwa unahuzunika…utajuta kwanini ule muda ambao ulikuwa na huzuni usingeutumia hata kuomba au kumsifu Mungu.
Hivyo simama sasa mtu wa Mungu, huu sio wakati wa kupalilia huzuni bali ni wakati wa kuomba..Mitume wa Yesu huzuni yao iligeuka furaha pale walipomwona Bwana kafufuka…nawe pale utakapoona kile kilichokuwa kimekufa kimefufuka, siku sio nyingi furaha yako itarudi. Hivyo usihuzunike..simama uombe, simama uendelee mbele kwasababu hatua zilizobakia mbele yako ni chache kuliko ulizoziacha nyuma. Hivyo sio wakati wa kunyongonyea ni wakati wa kuomba.
Bwana akubariki
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312.
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
Bwana wetu Yesu Kristo asifiwe ndugu yangu..
Nyakati hizi za mwisho tunazoishi sasa, ni nyakati ambazo zinakithiri kuwa na mseto wa watu wengi wanaojiita wakristo, leo hii ni rahisi kuona hata msanii wa kidunia anaimba nyimbo za Injili, ni rahisi kuona, mashoga wanatoa michango ya kujenga makanisa makubwa ulaya, wazinzi wanahudhuria kila jumapili ibadani, wengine mpaka wapo tayari kushiriki meza ya Bwana bila hofu nao wanaona ni kawaida tu. Ni kundi kubwa lenye mchanganyiko wa kila aina ya watu, wengine hawana hata mpango wa kufikiria maisha yao baada ya hapa, kinachowapeleka kwa Mungu tu, ni pengine waponywe waondoke, wengine wapate tu wachumba, wengine biashara zao ziende vizuri..basi hakuna cha zaidi baada ya hapo
Na wachache sana ndio wanaoutafuta wokovu wa kweli, ambao wapo tayari kumtii na kumfuata Yesu pale alipo yeye..
Embu leo kwa ufupi tuone habari moja ambayo, pengine unaijua sana, lakini tuiangalie kwa jicho lingine la ndani zaidi na naamini tutajifunza kitu kipya..
Na habari yenyewe ni ile ya Yesu akiwa bado kijana mdogo, alipokwenda na wazazi wake Yerusalemu kuila pasaka ya kila mwaka.. Lakini kama tunavyoijua habari baada ya sikukuu kuisha, ulipofika wakati wa kila mtu kurudi nyumbani kwake na katika taifa lake, wale waliotokea katika mikoa ya karibu kule Israeli walianza safari ya kurudi makwao, na wale waliotokea mataifa mengine ya mbali nao pia walianza kurejea makwao..
Lakini mambo yalikuwa tofauti kwa Bwana Yesu, yeye alibaki nyuma, wala hakuambata na makutano kurudi makwao, kama watu wengine walivyofanya, na kibaya zaidi hata wazazi wake hawakulijua hilo, wao wakakisia tu labda atakuwa katikati ya makutano wakirejea naye nyumbani…(Hilo ndio kosa linalofanywa na watoto wengi wa Mungu)
Luka 2:44 “Nao wakadhani ya kuwa yumo katika msafara; wakaenenda mwendo wa kutwa, wakawa wakimtafuta katika jamaa zao na wenzao;
45 na walipomkosa, wakarejea Yerusalemu, huku wakimtafuta.
46 Ikawa baada ya siku tatu wakamwona hekaluni, ameketi katikati ya waalimu, akiwasikiliza na kuwauliza maswali.
47 Nao wote waliomsikia walistaajabia fahamu zake na majibu yake.
48 Na walipomwona walishangaa, na mama yake akamwambia, Mwanangu, mbona umetutenda hivi? Tazama, baba yako na mimi tulikuwa tukikutafuta kwa huzuni.
49 Akawaambia, Kwani kunitafuta? Hamkujua ya kuwa imenipasa kuwamo katika nyumba ya Baba yangu”?
Kama tunavyoona hapo, ni wazazi wake tu pake yao, ndio waliokuwa walau wanamfikiria Yesu katikati ya ndugu zao wengi walioambatana nao, na walipoona Kristo hayupo katikati ya makutano, katikati ya wingi wa watu, katikati ya ndugu, katikati ya marafiki, katikati ya majirani, katikati ya wageni wa mataifa mengine, ndipo ikiwapasa wageuke wajaribu kwenda kuanza kumtafutia kule walipompotezea Yerusalemu.. ndipo wakamkuta yupo hekaluni katikati ya WAALIMU..
Na ni kama bahati tu walipita hekaluni, lakini kama wasingeingia kule, kamwe wasingemwona daima, wangehangaika Yerusalemu nzima wasingempata kwa muda mrefu sana..
NI KIPI MUNGU ANATAKA TUJIFUNZE?
Wakristo wachache wa leo hawajui kuwa, wapo katikati ya kundi kubwa la wakristo vuguvugu, linaloondoka mbali na mafundisho ya kweli ya Neno la Mungu.. na ndio maana wanapojaribu kumtafuta Kristo katikati yao ni kama vile hawamuoni, lakini wao bado wanataka kuendelea kutembea nao tu, hawajui kuwa kwa jinsi wanavyozidi kukaa nao ndivyo wanavyozidi kumpoteza YESU wasimpate kabisa..
Ndugu geuka kama ni wewe,..angalia ulipotoka, kule mlipotoka ndipo Kristo yupo,..Na! ulipotoka ni wapi?? Ni katikati ya waalimu, kule Kristo alipo, na waalimu makao yao huwa ni wapi?..Makao yao ni darasani sikuzote, wakiwafundisha wanafunzi, na hapo ndipo makao ya Kristo yalipo siku zote..
Hutampata sehemu nyingine yoyote, hutampata, kwenye michezo, maombezi, hutampata kwenye matamasha, hutampata kwenye taasisi za kidini, wala hutampata kwenye dhehebu lolote, wala katikati ya ndugu zako, au rafiki zao, au majirani zako, huko kote utapotea, Kristo hatembei katikati ya misafara ya watu wanaosafiri mbali na yeye bali Kristo utamwona PALE NENO LAKE LINAPOFUNDISHWA BASI..
Ukiona hupendi tena kujifunza Neno la Mungu basi ujue, upo mbali sana na Kristo kwa mujibu wa biblia, ukiona huna muda wa kusoma biblia, usijidanganye utakaa umwone Kristo akijifunua kwako, ukiendelea kudhani Kristo yupo katika msafara unaouona leo hii, wimbi la watu wengi wanaosema tumeokoka, lakini Neno la Mungu hawalifuati, ni wavivu katika kutamani kumjua Mungu, ukiwauliza habari ya unyakuo kwao ni kama habari mpya za kuchosha, ukiwauliza, habari za kwenda mbinguni kwao ni kama hadithi za kizee, muda wote ni kujionyesha tu, na kujisifia wameokoka, lakini biblia ni kama kitabu cha ziada tu kwao basi ujue wamempoteza Kristo katikati yao..
Bwana atusaidie nyakati hizi za hatari tusimpoteze yeye aliye mwamba wa wokovu wetu..
Maran Atha.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
https://wingulamashahidi.org/mafundisho-ya-ndoa/
Biblia inamaana gani kusema;aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi?
Katika 1Wafalme 20:35-37, Kwanini yule mtu afe kwa kuliwa na simba baada ya kukataa kumpiga yule nabii?..je Mungu anaruhusu watu kupigana?
JIBU:Tusome
1Wafalme 20:35-37 “Basi, mtu mmoja wa wana wa manabii akamwambia mwenzake kwa neno la Bwana, Nipige, nakusihi. Akakataa yule kumpiga.
36 Akamwambia, Kwa sababu hukuisikiliza sauti ya Bwana, angalia, mara ukitoka kwangu simba atakuua. Na mara alipotoka kwake, simba alimwona, akamwua.
37 Ndipo akaona mtu mwingine, akasema, Nipige, nakusihi. Yule mtu akampiga, hata kumpiga na kumtia jeraha”
Kuna wakati Mungu anatumia ishara za mwilini kuzungumza na watu wake au kufikisha ujumbe mahali..Kwamfano utaona Nabii Hosea aliambiwa aoe mwanamke wa kizinzi,
Hosea 1:2 “Hapo kwanza Bwana aliponena kwa kinywa cha Hosea, Bwana alimwambia Hosea, Enenda ukatwae mke wa uzinzi, na watoto wa uzinzi; kwa maana nchi hii inafanya uzinzi mwingi, kwa kumwacha Bwana”.
Lengo la Mungu kumwambia Hosea akaoe mwanamke wa kizinzi sio kuhalalisha uzinzi kwa watu wake, hapana bali ni kuwaonyesha watu wake jinsi na wao wanavyofanya uzinzi mbele zake kinyume chake katika roho…Hosea hakuwa mzinzi lakini aliambiwa akamwoe mwanamke mzinifu, ambaye ni kahaba mwenye wanaume wengi, ambaye hatulii. Sasa nafasi ya Hosea ambaye hakuwa mzinifu ilimwakilisha Mungu na huyo mwanamke wa kizinzi ililiwakilisha taifa la Israeli, kwa jinsi yule mwanamke alivyokuwa ni kahaba baada hata ya kuolewa na Hosea ndivyo Taifa la Israeli lilivyofanya uzinzi katika roho na kumwacha Mungu wao ambaye ndiye mume wao kama Isaya 55:5 inavyosema “Kwa sababu Muumba wako ni MUME WAKO; Bwana wa majeshi ndilo jina lake; na Mtakatifu wa Israeli ndiye Mkombozi wako; Yeye ataitwa Mungu wa dunia yote”
Sasa endapo Nabii Hosea angekataa maagizo yale Mungu aliyompa ya kwenda kumwoa mwanamke kahaba…na kusema hapana Bwana mimi sitaki kumuoa mwanamke yule ambaye ni mzinzi na kahaba hata nikimuoa bado ataendelea kuwapenda hao mabwana wake…Ni Dhahiri kuwa Hosea angetenda dhambi kwasababu amekataa shauri la Bwana la yeye kufanyika ishara kwa Israeli. Na hivyo angewafanya Israeli wasitubu, lakini ishara ile iliwafanya Israeli wengi watubu..Kwasababu walipokwenda kumuuliza wewe Nabii wa Mungu mbona unaoa mwanamke ambaye anamabwana wengi na zaidi ya yote tunamwona mkeo huyo yupo na mabwana wengine, unajisikiaje kwa hilo?..Ndipo Hosea atawajibu ni mfano wa nyinyi mlivyomwacha Mungu wenu ambaye ni mume wenu na kuigeukia miungu mingine kuiabudu..Hivyo mrudieni Mungu wenu ambaye ni Mume wenu kwasababu amewakasirikia sana.
Halikadhalika kuna wakati Mungu alimwambia nabii mwingine amwambie mwenzake kwamba ampige mpaka apate majeraha…ili kwa kupitia yale majeraha aonekane kama alikuwa katika vita vikali na aende kwa mfalme wa Israeli akiwa na yale majeraha…Ili mfalme adanganyike na kuamini kuwa ni kweli alikuwa kwenye mapambano kwasababu ana majeraha..na ndipo ampe fumbo ambalo litamtega…Na kweli mfalme alipomwona mtu anakuja mwenye majeraha akasema bila shaka mtu huyu atakuwa ametoka vitani kwa majeraha yale..na alipopewa lile fumbo na yule nabii kumbe lilikuwa linamhusu mfalme mwenyewe..kwasababu alimwacha huru Benhadadi ambaye alipaswa kumuua kabisa..
Hivyo akaambiwa sehemu yake ataichukua yeye. Unaweza kuisoma vizuri habari hiyo katika 1Wafalme 20:35-43.
Lakini yule mtu alikataa maagizo yale ya Mungu..ingawa aliambiwa ni maagizo kutoka kwa Mungu lakini akakataa kumpiga..hakujua kuwa kwa kukataa kule kungemfanya mfalme wa Israeli asiyaamini maneno yale ya Mungu…Na ikasababisha dhambi kwake, na ndio mbeleni akaenda kuliwa na simba..lakini yule mwingine hakulichukulia lile jambo la kumpiga nabii wa Mungu kwamba ni jambo la kumuumiza..bali aliona mbele kwamba kwa ishara ile ya majeraha ya yule nabii, mfalme ataamini ujumbe kutoka kwa yule nabii sawasawa na Neno la Mungu na hivyo atakuwa ameyatenda mapenzi ya Mungu Zaidi.
Hivyo ni jambo la kawaida kabisa Mungu kuzungumza kwa ishara za mwili, alifanya hivyo kwa Hosea, Kwa Ezekieli, na kwa manabii wengine wengi.
Bwana atubariki
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
Shalom jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe.
Kuna wakati Bwana Yesu aliwaambia mitume wake maneno haya..
Yohana 12:24 “ Amin, amin, nawaambia, Chembe ya ngano isipoanguka katika nchi, ikafa, hukaa hali iyo hiyo peke yake; bali ikifa, hutoa mazao mengi..”
Aliwaambia maneno haya, kwanza kutokana na wanafunzi wake kuona wingi wa watu waliokuwa wanamfuata ili waokolewe hususani wale waliotoka mpaka nchi za mbali kuja kumuona na pia alisema vile ili kuwafundisha wanafunzi wake, akijerea tendo, alilolifanya muda mfupi, au siku chache zilizopita,..
Na tendo lenyewe halikuwa lingine Zaidi ya lile la Lazaro..
Kama wengi wetu tunavyofahamu Lazaro alikuwa ni mtu aliyependwa na Yesu sana, alikuwa ni Rafiki wa Yesu tangu zamani, Lakini siku moja aliumwa sana, na taarifa zikamfikia Yesu, Lakini Yesu hakuchukua hatua yoyote, badala yake aliendelea kubaki kule kule mahali alipokuwepo, akamwacha aendelee kuugua mpaka afe,..
Na alipojua ameshakufa, bado hakufanya haraka kurudi siku hiyo hiyo kumuona, bali alingojea tena siku mbili, ndipo baadaye akashuka kwenda Bethania alipokuwa anaishi yeye na Dada zake..Kama tunavyosoma habari alipofika alimkuta ameshawekwa kaburini, anatoa harufu,.(Yohana 11 )
Unaweza ukajiuliza ni kwanini alimwacha mpaka aoze, ni kwasababu baadaye alikuwa anataka kuwafundisha wanafunzi wake kinadharia juu ya huo mstari tuliouona hapo juu, na madhara yake jinsi yatakavyokuwa..
Sasa Bwana Yesu alipofika na kumfufua Lazaro tena, na kumrudisha katika hali yake ya mwanzo tena katika afya Zaidi ya ile aliyokuwa nayo hapo mwanzo, biblia inatuonyesha tendo lile la kufufuka tu kwa Lazaro, lilikuwa ni tendo lililoutikisa ulimwengu wa giza… Yaani kwa ufupi ushuhuda ule wa Lazaro, uliwavuta watu wengi sana kwa Kristo, mpaka kufikia hatua ya wakuu wa Makuhani kutaka kumuua yeye naye (yaani Lazaro)…
Yohana 12:9 “Basi watu wengi katika Wayahudi walipata kujua ya kuwa yeye yuko huko, nao wakaja, si kwa ajili yake Yesu tu, ila wamwone na Lazaro, ambaye Yesu alimfufua katika wafu.
10 Nao wakuu wa makuhani wakafanya shauri la kumwua Lazaro naye;
11 maana kwa ajili yake wengi katika Wayahudi walijitenga, wakamwamini Yesu”.
Hiyo ni kuonyesha kuwa jinsi gani Lazaro aliyekufa akazikwa akaoza alivyokuwa na athari kubwa katika ulimwengu wa roho, kuliko yule ambaye hakuwahi kupitia hayo.
Jiulize hapo kwanza kwanini Lazaro, hakuwa vile?..Kwanini hakukuwa na mtu aliyemfuatilia, kwanini hakumvuta mtu yeyote kwa Kristo, japokuwa alikuwa ni Rafiki wa Karibu wa Bwana Yesu, tena aliyependwa.
Hata sasa haijalishi mtu anaweza akawa anasema Kristo ni Rafiki yangu kiasi gani, anaweza akawa anakujua kweli kama Lazaro wa kwanza.. lakini hakujui kama Lazaro ambaye alikufa akaoza akazikwa, kisha akafufua tena..
Na ndio maana sasa Bwana Yesu akawaambia wanafunzi wake baada ya tukio lile kipindi kifupi baadaye..
Yohana 12:24 “Amin, amin, nawaambia, Chembe ya ngano isipoanguka katika nchi, ikafa, hukaa hali iyo hiyo peke yake; bali ikifa, hutoa mazao mengi..”
Ndipo mstari huo ulipokuwa chimbuko lake..Akiurejea mfano wa Lazaro..
Ikiwa wewe ulishaokoka lakini hutaki kuwa tayari kufa, na kuoza kwa habari ya dhambi, hata wakati mwingine kuonekana kuwa ni mjinga, au umerukwa na akili kwasababu tu hutaki kufanya jambo Fulani kwa ajili tu ya Kristo, basi huwezi kuwa Lazaro wa pili.Wala huwezi kudai kuwa umezaliwa mara ya pili.. Ikiwa utakuwa unaogopa kuacha kuvaa vimini kisa tu ndugu zako au marafiki zako watakuonaje, watakuita wewe ni mshamba, basi bado huwezi kumletea Kristo mazao yoyote, haijalishi utasema umedumu katika wokovu muda gani..wapo waliodumu na Kristo Zaidi ya sisi mfano Yuda, lakini hakuwa na mazao yoyote kwa Bwana, na mwingine huyu Lazaro ambaye alipendwa pia lakini hakuwa na matunda yoyote kwa Bwana, kwasababu walikuwa bado hawajafa kwa habari ya dhambi.
Ikiwa utaogopa, kuacha Maisha ya uzinzi kisa unawaonea haya hao waasherati wenzako ulionao, na marafiki zako, unaogopa watakuita mlokole, na wewe hutaki kuitwa hivyo, basi ujue mpaka hapo bado hujafa ukaoza ukafufuliwa na Kristo na hautakuwa na matunda yoyote yakumfaa Kristo. Ndugu habari hizi unazisikia kila kukicha lakini bado unafanya moyo wako kuwa mgumu, unazidi kujitoa katika mstari wa neema kidogo kidogo…
Ikiwa kweli tunatamani tuwe na matunda ya rohoni, basi tuwe radhi pia kuiacha dunia moja kwa moja, hiyo ndio kanuni ya Kristo wala hakuna njia nyingine ya mkato.
Kumbuka tena hili Neno
“Amin, amin, nawaambia, Chembe ya ngano isipoanguka katika nchi, ikafa, hukaa hali iyo hiyo peke yake; bali ikifa, hutoa mazao mengi..””
Bwana atusaidie sote,
Ubarikiwe sana..
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?
Kati ya Unyakuo,dhiki kuu, utawala wa miaka 1000 kipi kinaanza
Mstari huu unamaana gani? ″Walakini hautapotea hata Unywele mmoja wa Vichwa vyenu? (Luka21:18)
Ni kwa namna gani Yesu amewekwa kwa kuanguka na kuinuka?
MKARIBIE BWANA ZAIDI ILI UFANYIKE NGUZO.
SWALI: Katika Luka 10:18, tunasoma Bwana Yesu alimwona shetani akianguka kutoka mbinguni kama umeme..na katika Ufunuo 12:7-9 Biblia inasema kulikuwa na vita mbinguni na shetani akatupwa chini..Sasa ni wakati gani ambao shetani alitupwa chini? Kabla ya dunia kuumbwa au wakati wa Bwana Yesu akiwa duniani. Na je shetani sasa yupo kifungoni?.
JIBU: Katika Luka 10 tukianzia juu kidogo mstari wa 17 unasema…
“Ndipo wale sabini waliporudi kwa furaha, wakisema, Bwana, hata pepo wanatutii kwa jina lako.18 Akawaambia, Nilimwona Shetani, akianguka kutoka mbinguni kama umeme.”
Hivyo mstari huu hauzungumzii vita vilivyokuwa vinaendelea mbinguni kabla ya dunia kuumbwa..ambapo shetani alitaka kujiinua na kutaka kuwa kama Mungu, na hatimaye akafukuzwa mbinguni na kutupwa chini duniani..Bali unazungumzia habari za shetani kutoka katika nafasi ya juu aliyonayo juu ya watu wa Mungu na kushushwa chini..Ndio maana Bwana Yesu alizungumza maneno yale mara tu baada ya wanafunzi wake kutoka huko na huko kuhubiri injili na kutoa pepo wengi…Sasa kitendo hicho cha kwenda kufungua watu, na mateka kuwaacha huru, wale waliofungwa na nguvu za giza za shetani na mapepo yake hilo ndilo anguko la shetani kutoka juu mpaka chini, ambalo Bwana alikuwa analizungumzia hapo.
Hali kadhalika tukio tunalolisoma katika Ufunuo 12:7-9..Ndilo tukio la vita vilivyotokea mbinguni kabla ya dunia kuumbwa ambapo shetani alijiharibia nafasi aliyokuwepo ikasababishia kutupwa chini duniani.
Ufunuo 12:7 “Kulikuwa na vita mbinguni; Mikaeli na malaika zake wakapigana na yule joka, yule joka naye akapigana nao pamoja na malaika zake;
8 nao hawakushinda, wala mahali pao hapakuonekana tena mbinguni.
9 Yule joka akatupwa, yule mkubwa, nyoka wa zamani, aitwaye Ibilisi na Shetani, audanganyaye ulimwengu wote; akatupwa hata nchi, na malaika zake wakatupwa pamoja naye”.
Hivyo maanguko ya shetani yapo mawili…Lile la kwanza ambalo lilitokea kabla ya sisi wanadamu kuumbwa, ambalo lilimfanya asiwe na uwezo tena wa kurudi mbinguni. Na anguko la pili ni la hapa duniani ambalo tangu wakati wa Bwana Yesu mpaka sasa linaendelea… na litakamilika katika mwisho wa dunia ambapo wale wote waliokuwa wamekusudiwa uzima wa milele watakapomalizika kuingia ndani na mlango wa Neema kufungwa (Hiyo ndiyo siku ambayo shetani ataanguka kikabisa kabisa)..
Siku hiyo ni siku ambayo shetani hatakuwa na chembe hata moja ya ngano mkononi mwake, atakuwa na makapi tu ambayo yatakwenda kuteketezwa kwa moto(Mathayo 3:12). Siku hiyo ndio atakuwa ameshindwa mbinguni na duniani.
Hivyo hata wakati huu tunapokwenda kuhubiri injili,kutoa pepo, kufungua watu, kuwafariji, kuwajenga kiimani na kuwatoa sehemu moja hadi nyingine, kama Mitume hawa walivyofanya…katika ulimwengu wa roho ni tunamnyang’anya shetani mateka kwa kasi sana na hivyo tunakuwa tunamwangusha katika ile nafasi aliyonayo ya juu na kumshusha chini..kwasababu nguvu ya shetani ipo katika idadi ya watu wa Mungu anaowateka sasa..
Hivyo ni muhimu sana kuhubiri injili kwa watu wote..
Sasa utahubirije injili?..Kwa maisha yako utahubiri injili, kwa uvaaji wako utahubiri, kwa mwenendo wako, kwa uimbaji wako, kwa maombi yako na kwa mchango wako wowote ule wa kifedha katika kazi ya injili utakuwa umeihubiri injili.
Na shetani hajafungwa sasa, bado yupo anafanya kazi atakuja kufungwa miaka 1000 baada ya mwisho wa dunia.
Bwana akubariki.
Maran atha
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
Neno I.N.R.I kwenye msalaba wa Yesu maana yake ni nini?
Roho Mtakatifu ni nani?.
NILIMWONA SHETANI, AKIANGUKA KUTOKA MBINGUNI.
Je kupiga miayo ni ishara ya mapepo?
Je ni wakina nani ambao hawataonja mauti mpaka siku ya kuja Bwana?
Je! Shetani alitolea wapi uovu?
Shalom, Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe daima..
Karibu tuzidi kujifunza maneno matakatifu ya Mungu, Na leo tutaona kwa ufupi habari ya mtu mmoja anayeitwa Absalomu mwana wa Daudi naamini lipo jambo utajifunza ndani yake..
Huyu Absalomu alikuwa ni mmojawapo wa wana wengi wa Daudi, isipokuwa yeye alikuwa anabeba kitu kingine cha ziada ambacho kilikuwa kinamtofautisha na wana wote wa Daudi waliokuwa katika enzi yake ya kifalme.
Biblia inatueleza Absalomu, alikuwa ni kijana mzuri sana (kwa lugha ya kiingereza labda tunaweza tukasema Handsome), sio tu katikati ya ndugu zake, bali pia katika Israeli nzima ndivyo walivyomwona, hakukuwa na kijana aliyekuwa mzuri kama yeye, kuanzia utosi wa kichwa chake, mpaka uwayo wa miguu yake, wanasema hakuna mwanadamu asiye na mapungufu, lakini huyu Absalomu yeye hakuwa na upungufu wowote katika mwili wake. Kila kiungo chake cha mwili kilionekana kizuri na cha kuvutia, na alisifiwa na kila mtu..
Na Zaidi ya yote, biblia imezitaja hizo nywele zake, inasema, alikuwa na nywele nzuri nzito, ambazo alikuwa hawezi kuziacha Zaidi ya mwaka mmoja bila kuzinyoa vinginevyo vitamlemea sana, embu tusome kidogo..
2Samweli 14:25 “Basi katika Israeli wote hapakuwa na mtu hata mmoja mwenye kusifiwa kwa uzuri wake kama huyo Absalomu; tangu nyayo za miguu yake hata utosi wa kichwa chake hapakuwa na ila kwake.
26 Naye aliponyoa kichwa, (basi mwisho wa kila mwaka hunyoa; na kwa sababu nywele zilikuwa nzito kwake, kwa hiyo akanyoa;) hupima nywele za kichwa chake shekeli mia mbili kwa uzani wa mfalme.”
Unaona, ukisoma hapo utaona nywele hizo alikuwa akishazinyoa zilikuwa zinakwenda kupimwa kwenye uzani wa mfalme, na inapatikana shekeli mia mbili ambayo ukiigeuza kwa vipimo vya kisasa ni Zaidi ya kilogramu 2.. Unaweza kutengeneza picha uzito wa kilo mbili ulikuwa unamlemea kichwani pake kama asipokata nywele zake baada ya mwaka mmoja..
Ili kuelewa vizuri, wanasema mtu wa kawaida ambaye amebahatika kuwa na nywele nyingi na zinazokuwa, akaziacha mwaka mzima, ili uzito wake uweze kufikia ule wa nywele za Absalomu kwa mwaka, basi itahitaji wachukuliwe watu kama yeye thelathini (30) kwa mwaka, kisha zichanganywe ndipo zitafikia uzito wa nywele za Absalomu ndani ya mwaka mmoja..
Hivyo unaweza kuona jinsi gani mtu huyu alipewa umbile la kipekee sana, na uzuri wa tofauti, nywele zenye utofauti sana lakini tunaposoma biblia tukumbuke kuwa siku zote biblia inapotaja umbile Fulani la mtu, basi tujue kuwa lina sehemu Fulani ya kusimamia katika habari husikia mbeleni,.. Hivyo kutajwa kwa sifa za nywele za Absalomu, ni wazi kuna mahali litatumika huko mbeleni..
Hivyo ukipata muda wako binafsi wa utulivu unaweza kuzisoma habari zake, kwa urefu na jinsi alivyokuwa, (2Samweli 13-18 )lakini kwa ufupi ni kuwa Absalomu, Japokuwa alikuwa na uzuri na umbile la kipekee na maneno ya kuvutia ambayo yaliweza kuifanya Israeli yote wampende mpaka kutaka kumfanya awe mfalme, lakini moyo wake ulikuwa ni tofauti na watu walivyokuwa wanamdhania..
Kwanza alikuwa na lengo la kuudondosha ufalme wa baba yake Daudi kinyume chake ili yeye atawale na Zaidi ya yote alikuwa anamtafuta baba yake ili amuue, pili alikuwa radhi hata kulala na Masuria 10 wa baba yake ili kuwaonyesha watu kuwa hampendi, japokuwa baba yake hakuwahi kumfanyia ubaya wowote..Na tatu alikuwa radhi kumuua ndugu yake, ambaye alilala na Dada yake, wala hakumsamehe..
Kwahiyo Absalomu, alikuwa ni mwovu, wala hakuwa mtu mwema, licha ya kuwa alikuwa ni mzuri na mwenye ushawishi wa maneno kwa watu.
Sasa ukizidi kusoma habari utaona alipokusudia kumwangamiza baba yake(Daudi), baada ya kumfukuza kwenye kiti cha enzi, aliondoka kwenda msituni yeye pamoja na jeshi kubwa la Israeli nyuma yake..Biblia inatuambia vita ilikuwa vikali sana katika msitu ule mkubwa sana.. Na unajua jinsi misitu ilivyo, vichaka vizito na miti ya Kamba Kamba za miiba inakuwa ni mingi sana, na inakuwa ni rahisi mtu kunaswa katika vichaka hivyo kama hutakuwa mwepesi..
Sasa kutokana na msitu ule kuwa mzito sana, biblia inasema watu waliokufa kwa uzito wa msitu ule, walikuwa ni wengi kuliko waliokufa kwa upanga.. Na huko huko lipo jambo ambalo Absalomu naye alikutana nalo embu tusome kwa ufupi..
2Samweli 18:6 “Hivyo watu wakatoka waende nyikani ili kupigana na Israeli; na vita vikatokea ndani ya msitu wa Efraimu.
7 Watu wa Israeli wakapigwa huko mbele ya watumishi wa Daudi, kukawa na maangamizo makuu huko siku ile, ya watu ishirini elfu.
8 Kwa maana vita vilienea huko juu ya uso wote wa nchi; na siku ile huo msitu ukala watu wengi kuliko wale walioliwa na upanga.
9 NA KWA BAHATI ABSALOMU AKAKUTANA NA WATUMISHI WA DAUDI. NAYE ABSALOMU ALIKUWA AMEPANDA NYUMBU WAKE, NA YULE NYUMBU AKAPITA CHINI YA MATAWI MANENE YA MWALONI MKUBWA, HATA KICHWA CHAKE KIKAKWAMA KATIKA MWALONI HUO, AKANYAKULIWA JUU KATI YA MBINGU NA NCHI; NA YULE NYUMBU ALIYEKUWA CHINI YAKE AKAENDA MBELE.
10 Basi mtu mmoja akaona hayo, akaenda akamwambia Yoabu, akasema, tazama, mimi nalimwona Absalomu ametundikwa katika mwaloni.
11 Naye Yoabu akamwambia mtu yule aliyempasha habari, Je! Wewe umeona haya; Mbona, basi, hukumpiga hata nchi papo hapo? Nami ningalikupa fedha kumi na mshipi.
12 Yule mtu akamwambia Yoabu, Kama ningalipata fedha elfu mkononi mwangu, hata hivyo singalinyosha mkono wangu juu ya mwana wa mfalme; kwa maana mfalme masikioni mwetu alikuagiza wewe, na Abishai na Itai, akisema, Angalieni sana mtu awaye yote asimguse yule kijana, Absalomu.
13 Na tena, kama ningaliitendea roho yake kwa hila; (wala hapana neno lo lote liwezalo kufichwa mbele ya mfalme); ndipo wewe mwenyewe ungalijitenga.
14 Ndipo Yoabu akasema, Siwezi kungoja na kusema nawe hivi. Akachukua vyemba vitatu mkononi mwake, akamchoma Absalomu moyoni, alipokuwa akali hai katikati ya ule mwaloni.
15 Kisha vijana kumi, waliomchukulia Yoabu silaha zake wakamzunguka, wakampiga Absalomu, na kumwua.
Utaona, hapo Absalomu, alipopita sehemu moja, biblia inasema kichwa chake kikakwama, kwenye mti mmojawapo, na yule farasi aliyekuwa chini yake akazidi kuendelea mbele, hivyo yeye akabakia pale pale amening’inia. Sasa, biblia inaposema kichwa inamaanisha eneo la nywele kwa ujumla wake, Ni kwamba zile nywele nyingi za Absalomu zilikwama kwenye vijiti vya miti, zikajisongorotesha pale, kwa namna ambayo asingeweza kuzifumua, akabakia tu anani’ngia nia tu pale kwa maumivu.. alikaa pale muda mrefu akijaribu lakini alishindwa kutoka mpaka mauti ilipomfika kwasababu ule uzuri wake ndio ulikuwa kitanzi chake..
Ndugu, hata sasa, watu wengi hawajui kuwa kile kinachowafanya wavutie, au wapendwe ndani yao ndio kitakuwa kitanzi chao baadaye ikiwa hawatasimama katika mstari wa wokovu.. Ikiwa ni mali zako zinakupa kiburi kumbuka yale maneno ya Bwana, Ni rahisi kwa ngamia kupenya katika tundu la sindano… Ikiwa ni urembo wako wewe binti, unajiona sasa huna haja ya Mungu bado wewe unavutia, una umbile zuri, kila mwanaume akikuangalia anakutamani, wakati utafika huo huo uzuri wako utakuwa kitanzi kwako, utanasa mahali ambapo hutatoka, na adui yako shetani atakumaliza kirahisi mbele ya macho yako ukiona kama ilivyokuwa kwa Absalomu, na ukajikuta katika lile ziwa la moto,..Vivyo hivyo na mambo mengine yote.
Huu ni wakati sasa wa kumtazama Kristo, na kuomba rehema kwake, kama na wewe umedanganywa na mojawapo ya hayo mambo, uzuri wako na utanashati wako. Tubu umgeukie Mungu, ili Mungu akurehemu na kukupa uzima wa milele. Nyosha njia yako kwa kuliamini na kulitii Neno la Mungu.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
UCHAWI WA BALAAMU.
USIPOWATAMBUA YANE NA YAMBRE, KATIKA KANISA LA KRISTO, UJUE UMEPOTEA.
USIPOWATAMBUA YANE NA YAMBRE, KATIKA KANISA LA KRISTO, UJUE UMEPOTEA.
KUTAKUWA NA MATETEMEKO YA NCHI, NJAA NA TAUNI.
NIMEOKOKA, ILA MUNGU NDIYE ANAYEJUA NITAKWENDA WAPI.
KWANINI YESU KRISTO NI WA MUHIMU KWETU SASA?
Je! ni kweli Bwana Yesu alibatiza mtu akiwa hapa duniani?
JIBU: Bwana Yesu yeye mwenyewe hakubatiza bali wanafunzi wake ndio waliobatiza kwa agizo lake yeye. Hata leo mkuu wa nchi akitoa agizo la ujenzi wa jengo Fulani la serikali…Jengo lile litakapojengwa na kumalizika..jengo hilo litajulikana kama limejengwa na Mkuu huyo…lakini kiuhalisia sio yeye aliyelijenga waliolijenga ni wale vibarua na wafanyakazi wake…lakini kwasababu ni mkuu ndio katoa hiyo amri na fedha basi ni sahihi kabisa kusema ni Mkuu huyo ndiye kajenga jengo lile.
Kadhalika kuna mahali kwenye biblia paliposema Bwana Yesu alibatiza…lakini ukiendelea mbele kidogo utaona biblia imefafanua zaidi waliobatiza ni wakina nani…kwamba ni wanafunzi wake kwa amri yake na sio Bwana Yesu mwenyewe.
Tusome.
Yohana 4:1 “Kwa hiyo Bwana, alipofahamu ya kuwa Mafarisayo wamesikia ya kwamba, Yesu anafanya wanafunzi wengi kuliko Yohana, na kuwabatiza,
2 (lakini Yesu mwenyewe hakubatiza, bali wanafunzi wake,)
3 aliacha Uyahudi, akaenda zake tena mpaka Galilaya”.
Unaona hapo mstari wa pili unafafanua zaidi kwamba siye Bwana Yesu aliyebatiza bali ni wanafunzi wake.
Pamoja na hayo yote Jambo lingine la msingi hapo la kujifunza ni kwamba watu walianza kubatizwa kabla hata ya Bwana Yesu kusulubiwa, kufa na kufufuka ..kuonyesha ni jingi gani ubatizo ulivyokuwa wa muhimu…Ni agizo la awali kabisa pale mtu anapomwamini Yesu na kutubu dhambi zake.
Hivyo nasi tunajifunza kama hatujazingatia kwenda kubatizwa ubatizo sahihi tukidhani sio agizo la msingi, hapa tunaonyeshwa watu walianza kubatizwa kabla ya Kristo kwenda Golgotha, ..kuashiria umuhimu wa hicho kitu, na kumbuka pia ubatizo hautekelezwi kama mtu anavyoamua kwamba unaweza kuzamishwa kichwa tu kwenye maji na ukawa tayari umeshabatizwa, au unaweza kutumia mchanga badala ya maji, au unaweza kunyunyiziwa tu badala ya kuzama mwili mzima…hakuna njia mbadala ya ubatizo..Neno ubatizo maana yake ni KUZAMISHWA. Na kuzama maana yake ni kuzama hakuna maana nyingine ya neno hilo. Hivyo tunazamishwa katika maji mengi (kama Yohana 3:23 inavyosema), na kwa Jina la Bwana Yesu Kristo kama (Matendo 2:38,8:16, 10:48, 19:5 inavyosema).
Tuyazingatie hayo na Bwana atatukubali na kutubariki.
Shalom.
Muhtasari wa maelezo haya kwa njia ya video unaweza kuyapata hapa chini.
[embedyt] https://www.youtube.com/watch?v=68fHuz_icug[/embedyt]. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
LIVUNJENI HEKALU HILI, NAMI KATIKA SIKU TATU NITALISIMAMISHA.
SWALI: mstari huu una maana gani? Luka 2:34 “Simeoni akawabariki, akamwambia Mariamu mama yake, Tazama, huyu amewekwa kwa kuanguka na kuinuka wengi walio katika Israeli, na kuwa ishara itakayonenewa”?
JIBU: Kwa faida yetu wote, ni vizuri tukaanzia mistari ya juu ili tupate ufahamu wa habari yote hiyo inamuhusu nani..
Luka 2:25 “Na tazama, pale Yerusalemu palikuwa na mtu, jina lake Simeoni, naye ni mtu mwenye haki, mcha Mungu, akiitarajia faraja ya Israeli; na Roho Mtakatifu alikuwa juu yake.
26 Naye alikuwa ameonywa na Roho Mtakatifu ya kwamba hataona mauti kabla ya kumwona Kristo wa Bwana.
27 Basi akaja hekaluni ameongozwa na Roho; na wale wazazi walipomleta mtoto Yesu ndani, ili wamfanyie kama ilivyokuwa desturi ya sheria,
28 yeye mwenyewe alimpokea mikononi mwake, akamshukuru Mungu, akisema,
29 Sasa, Bwana, wamruhusu mtumishi wako, Kwa amani, kama ulivyosema;
30 Kwa kuwa macho yangu yameuona wokovu wako,
31 Uliouweka tayari machoni pa watu wote;
32 Nuru ya kuwa mwangaza wa Mataifa, Na kuwa utukufu wa watu wako Israeli.
33 Na babaye na mamaye walikuwa wakiyastaajabia hayo yaliyonenwa juu yake.
34 Simeoni akawabariki, akamwambia Mariamu mama yake, TAZAMA, HUYU AMEWEKWA KWA KUANGUKA NA KUINUKA WENGI WALIO KATIKA ISRAELI, NA KUWA ISHARA ITAKAYONENEWA.”
Ukitazama hapo, kuna vipengele vitatu, 1) kuanguka, 2)Kuinuka kwa wengi 3) na kuwa ishara itakayonenewa.
Huyo ni Bwana wetu Yesu Kristo anayezungumziwa hapo na Simeoni akitolewa unabii juu ya mambo atakayokuja kuyatekeleza huko mbeleni kwamba atawekwa kwa ajili ya kutumiza makusudi hayo matatu, yaani kuanguka na kuinuka kwa watu wengi walio katika Israeli na kuwa ishara itakayonenewa.
Tuanze kwa kutazama kwa ufupi kipengele kimoja kimoja..
na unabii huo ulishatolewa tangu zamani..
Isaya 8:14 “Naye atakuwa ni mahali patakatifu; bali ni jiwe la kujikwaza na mwamba wa kujikwaa kwa nyumba za Israeli zote mbili, na mtego na tanzi kwa wenyeji wa Yerusalemu.
15 Na wengi watajikwaa juu yake, na kuanguka na kuvunjika, na kunaswa na kukamatwa”.
Jambo hilo tuliliona kwa mafarisayo, waandishi na masadukayo, na Taifa la Israeli kwa ujumla wale wote waliompinga Kristo na kumkataa, walitiwa upofu..
Yohana 9:39 “Yesu akasema, Mimi nimekuja ulimwenguni humu kwa hukumu, ili wao wasioona waone, nao wanaoona wawe vipofu.
40 Baadhi ya Mafarisayo waliokuwapo pamoja naye wakasikia hayo, wakamwambia, Je! Sisi nasi tu vipofu?”
Neema hiyo ya wokovu iliondolewa kwao, na kuletwa kwetu sisi watu wa mataifa, na kilichobakia kwao hakikuwa kingine Zaidi ya , taifa la Israeli kuja kuangamizwa na Warumi mwaka 70 WK, Ili kutimiza ule unabii Kristo aliozungumza juu yao kuhusu uharibifu wa Yerusalemu na Watoto wao (Soma Luka 19:41-44)
Ukisoma tafsiri nyingine hususani zile za kiingereza utaelewa vizuri, mstari huo unasema..” and for a sign which shall be spoken against;”(kjv).. Ishara ambayo haitapokelewa/haitakubaliwa na wengi..
Licha ya kuwa Kristo alijidhihirisha kwao kwa ishara nyingi, na miujiza mingi, akitimiza maandiko mengi yamuhusuyo masihi, lakini wayahudi wengi walimpinga, walitazamia pengine masihi wao angetokea kwenye majumba ya kifalme, lakini walipomuona amezaliwa katika familia ya kimaskini wakajikwaa kabisa.
Hata sasa, Kristo anatimiza, unabii huo, yaliyotokea wakati ule, ndio yanayotokea wakati huu, wakati wengine wanaokolewa, na kunyanyuka, na kupokea uzima wa milele, wapo wengine saa hii wanajikwaa kwa Kristo na kuanguka na kupoteza neema ya wokovu moja kwa moja…Na wanaanguka kwa jinsi gani?.. Ni Pale mtu anapoona Kristo anaokoa na kwamba yeye ndio mwokozi wa ulimwengu halafu hataki kumwamini apokee uzima wa milele, kama ilivyokuwa kwa wale mafarisayo na waandishi, kinyume chake haonyeshi kuthamini jambo hilo, au anadhihaki, basi mtu huyo Kristo anabadilika hawi tena mwokozi kwake bali anakuwa jiwe la kukwaza.. Inamaana kuwa akiendelea hivyo kuna wakati utafika Yule Roho wa Kristo wa neema anayemlilia kila siku atubu, ataondoka ndani yake, kitakachobakia kwake ni kuendelea tu kuupinga wokovu na kudhihaki watu wa Mungu mpaka siku anaondoka duniani.
Watu kama hao wapo kila mahali, utajiuliza hawamwogopi hata Mungu, kulitamka jina la YESU ovyo ovyo tu mitaani, hawaogopi kuufanyia mzaha wokovu na msalaba.
Hivyo na sisi Bwana atusaidie, tuitii injili ili iwe na manufaa kwetu ya rohoni, tusije tukaanguka kwa injili hiyo hiyo. Neno la Mungu ni upanga ukatao kuwili.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
Biblia inakataza kuapa kabisa, lakini kwanini watu wanaapa mahakamani na katika vifungo vya ndoa?
Kwanini Mungu aliikubali sadaka ya Yeftha ya kumtoa binti yake kafara?
KWANINI DAUDI ALIKUWA NI MTU ALIYEUPENDEZA MOYO WA MUNGU?
Je! Shetani alitolea wapi uovu?
Ikiwa sisi tuliumbwa na Mungu,Je! Mungu aliumbwa na nani?
JE MOYO WAKO NI MNYOFU MBELE ZA MUNGU