Category Archive Home

Kwa maana kahaba ni shimo refu; Na malaya ni rima jembamba.

SWALI: Nini maana ya huu mstari?

Mithali 23:27 “Kwa maana kahaba ni shimo refu; Na malaya ni rima jembamba.

28 Naam, huotea kama mnyang’anyi; Huwaongeza wenye hila katika wanadamu”.

JIBU: Kahaba ni mwanamke anayezini na mtu ambaye si mume wake, ni mwanamke mwenye mahusiano na wanaume wengi, akiwa na lengo la aidha kujiburudisha au kuharibu maisha ya wengine, huyu huwa hatafutwi bali yeye ndio anatafuta, kutimiza makusudi yake maalumu.

Lakini Malaya kibiblia ni mwanamke anayefanya uasherati kwa lengo la kujipatia fedha , au kupata upendeleo fulani, au kukubaliwa, mara nyingi huwa hajaolewa. Vilevile mwanamke yeyote anayejiamulia tu kufanya uasherati na mtu yeyote pale anapofuatwa, bila kujali chochote huyo pia ni Malaya.

Sasa Biblia inatuambia wote, ni hatari hakuna hata mmoja mwenye afadhali, ikiwa umenaswa nao.  Kwamfano ukizini na kahaba, rohoni ni kama unazama kwenye shimo. Na heri lingekuwa ni shimo tu, bali biblia inasema ni shimo refu, ikiwa na maana mtu akizama, hana matumaini tena ya kutoka huko. Ndio milele anapotea.

Vilevile anasema Malaya ni Rima jembamba. Rima ni shimo maalumu ambalo linachimbwa kwa ajili ya kunasa kitu, hususani wanyama. Zamani watu walipotaka kuwakamata wanyama wakali kama vile simba au dumu, walikuwa hawawapigi sindano za usingizi kama wanavyofanya sasa hivi,hapana, bali walikuwa wanachimba mashimo marefu sana, na membamba kisha, kwa juu wanayafunika na majani, kiasi kwamba mnyama akipita pale hawezi jua kama chini kuna shimo. Na akishasogea tu pale anatumbukia na kwenda chini sana, baadaye wanakuja kumkamata na kumtoa kirahisi.

Hivyo Malaya naye ndio vivyo hivyo, ukijiingiza kwenye mitego yao, unanasika na kutoka kamwe hutaweza. Soma.

Mithali 22: 14 “Kinywa cha malaya ni shimo refu; Anayechukiwa na Bwana atatumbukia ndani yake”.

Sasa tahadhari hii hawapewi wanaume tu, bali pia na wanawake..Kibiblia, kahaba na Malaya inamaanisha jinsia zote. Wewe ni kijana au binti, ikimbie zinaa kama vile biblia inavyosema katika 1Wakorintho 6:18… Kwasababu dhambi nyingine zote mtu unatenda nje ya mwili wako, lakini zinaa ni juu ya mwili wako mwenyewe.

Na ni dhambi inayowaangusha wengi sana, na inayoshusha viwango vya kiroho kwa kasi sana. Kiasi kwamba kitendo kimoja tu kama hicho kinaweza kukufanya uachwe na Mungu milele. Licha tu ya kuachwa na Mungu, pia yapo magonjwa hatari kama vile Ukimwi, jambo ambalo wengi hawafahamu, ni kuwa ukimwi ni PEPO, kwamfano inawezekana kabisa watu wawili wakakutana   wasiwe na maambukizi, lakini kwasababu kile kitendo kinahasisiwa na pepo la uzinzi, moja kwa moja linawavaa wote, na saa hiyo kila mmoja anapata UKIMWI, baadaye wakijiuliza  wametolea wapi, hawajui. Ndivyo ilivyokuwa kwa watu wa kwanza walioupata huo ugonjwa, hawakuambukizwa na mtu bali lilikuwa ni PEPO liliowavaa.

Hivyo kuwa makini sana, biblia inaposema ni Shimo refu na rima jembamba, inamaanisha kweli. Ukinasika usidhani ni rahisi kutoka. Hizo ni tahadhari kwetu. Lakini ukimpa Yesu maisha yako, atakupa uwezo wa kipekee wa kuweza kuvishinda vishawishi hivyo vyote. Uwezo huo hawezi kutoa mtu yeyote, zaidi ya Yesu Kristo tu peke yake. Watu wa ushauri nasaha, hawawezi kukufanya uushinde uzinzi, Madkatari hawawezi, Bali Yesu tu peke yake. Hivyo ukimwamini, utakusaidia.

Na kumwamini kunakuja kwa kutubu dhambi zako zote, kwa kumaanisha kabisa kuziacha, kisha kukubali kubatizwa katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa na kwa maji mengi, na yeye mwenyewe kuanzia huo wakati atakushushia kipawa chake cha Roho wake Mtakatifu kukusaidia kuweza kuyashinda majaribu yote, kama yeye alivyoweza kuyashinda.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

“Shinikizo” ni nini kibiblia, Na maana yake rohoni ni ipi?

Je! Daudi hakuwa mtoto wa ndoa wa Yese? (Zab 51:5)

Kama wakitenda mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu?

Kama wakitenda mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu?

Maana Ya Maneno Katika Biblia.

Rudi nyumbani

Print this post

Na hekima imejulikana kuwa ina haki kwa watoto wake wote.

SWALI: Kwanini Bwana Yesu alisema watu wa kizazi kile wamefanana na watoto walioketi masokoni na kuitana,? Mfano huo unaelewekaje?

Na pia alikuwa na maana gani kusema maneno haya?

Luka 7:35 “Na hekima imejulikana kuwa ina haki kwa watoto wake wote”


JIBU: Habari hizo utazisoma katika sehemu kuu mbili, ya kwanza ni Mathayo 11:16-20 na ya pili ni  Luka 7:31-35

Sasa tuisome hiyo ya Luka ndio yenye vifungu vya moja kwa moja vya swali lenyewe;

Luka  7:31 “Bwana akasema, Niwafananishe na nini watu wa kizazi hiki? Nao wamefanana na nini?

32 Wamefanana na watoto walioketi sokoni na kuitana, wakisema, Tuliwapigia filimbi wala hamkucheza; tuliomboleza, wala hamkulia.

33 Kwa kuwa Yohana Mbatizaji alikuja, hali mkate wala hanywi divai, nanyi mwasema, Ana pepo.

34 Mwana wa Adamu amekuja, anakula na kunywa; nanyi mwasema, Tazama, mlafi huyu, na mnywaji wa divai, rafiki wao watoza ushuru na wenye dhambi.

35 Na hekima imejulikana kuwa ina haki kwa watoto wake wote”.

Shalom.

Bwana Yesu alitoa mfano ambao ulikuwa ni wa kawaida na uliojulikana kwa wagalilaya wakati ule. Kwani ilikuwa ni desturi watoto wa aina mbalimbali  kukutana masokoni kwa ajili ya michezo kulingana na desturi zao, na walipokutana walikuwa wanaunda makundi mawili makubwa, lengo lao likiwa ni kuigiza mambo ambayo waliona watu wazima wakiyafanya aidha katika misiba au sherehe.

Sasa kundi la kwanza lilikuwa linaanza kwa kupiga filimbi za kwenye masherehe walizowahi kuzisikia mahali fulani zikipigwa huko nyuma, na lile kundi lingine kazi yake ilikuwa ni kuitikia kwa kucheza, kama watu wazima walivyofanya. ( Soma Luka 15:25)

Baadaye tena vivyo hivyo, wanarudia  kuigiza  nyimbo za misibani, wale wengine wanajifanya kama wanalia kwa kupiga piga vifua vyao. (Soma Mathayo 9:23).  Hivyo hata watu wazima walipowaona hawakuwazuia bali waliwaacha, kwani walikuwa wanaamini vitendo vile vinawajengea uzalendo wa kutambua tamaduni zao za kiyahudi.

Sasa kulingana na maneno ya Bwana Yesu ni kuwa, watoto hawa walipokusanyika, kundi lile la kwanza lilipopiga filimbi za masherehe, wale wengine hawakuonyesha mwitikio wowote walizira, pengine wakadhani wanataka za msiba, na walipowapigia wenzao za msiba, bado pia hawakujifanya kama wanaomboleza. Kitendo ambacho  pengine kiliwakasirisha wale waliojitoa.

Akifunua kuwa, Yohana alikuja kwa njia ya kujitenga sana na ulimwengu, hivyo pengine wangemwamini kwa maisha yake ya majangwani, na kutokula kula au kunywa, kama vile mtoto aliyewapigia filimbi za maombolezo, lakini hawakulia..Yaani mafarisayo na waandishi hawakuonyesha mwitikio wowote. Kinyume chake wakasema watu wenye mapepo, ndio wanaishi maisha ya namna hiyo, hakuna mtumishi mwenye akili timamu, akawa mchafu na mtu asiyejijali namna ile.

Labda hiyo ikaonekana kama ni njia ngumu kwao kuamini manabii wa Mungu, Hivyo Mungu akawapelekea mkuu wa uzima mwenyewe, Yesu Kristo, Bwana wetu, ambaye yeye alikuja kwa njia ya kula na kunywa, mtu wa watu, aketiye katikati ya wenye dhambi, hivyo mbele yao akafanana na wale watoto waliopiga filimbi, ili wenzao wacheze.. Lakini bado hawakuonyesha mwitikio wowote kwa injili ya Bwana, kinyume chake, wakamwita mlevi na mlafu. Hakuna mtumishi wa Mungu kweli anaweza kushinda bar muda wote na walevu kuwahubiria.

Kuonyesha kuwa hata sasa, Bado Mungu anaweza kutuma watumishi wake, katika wito tofauti tofauti, lakini bado watu wasiompenda Mungu wakapinga tu, wakadhihaki, wakakejeli, wakadharau. Akitumwa nabii wa Mungu anayehubiri injili ya kweli, ambaye pengine ni tajiri, na ana mali, watasema, tapeli huyu, anakula sadaka za waumini, wakipelekewa nabii ambaye muda wake wote anashinda sehemu za ibada, au milimani, mwenye nguo moja, asiye smati, hafanyi kazi yoyote isipokuwa kushinda uweponi mwa Mungu, watasema huyu mlokole maskini hatumtaki, kama Mungu wake ameshindwa kumfanya hata asivae viatu vilivyotoboka, atawezaji kunisaidia mimi?

Unaona?

Lakini sasa ukiendelea mistari inayofuata, Bwana Yesu ndio anasema..

Na hekima imejulikana kuwa ina haki kwa watoto wake wote”.. Ukisoma kwenye Mathayo 11:19 inasema “Na hekima imejulikana kuwa ina haki kwa kazi zake”. Hii ikiwa na maana Hekima ya Mungu ya kuokoa watu, imejulikana kuwa ni ya kweli kwa watoto wake ambao ni (Yohana na Yesu Kristo mwenyewe).. Kwamba kwa vyovyote vile, iwe ni katika utajiri au katika umaskini, au katika kujichanganya au kutojichanganya..kama ni ya Mungu, basi itathibitika tu kwa kazi zake,(matunda yake).

Hata leo hii, usimuhukumu mtumishi wa Mungu kisa ni tajiri, au ni maskini, au anakula au hali, vilevile usihukumu huduma yoyote kisa ni kubwa, au ni ndogo, au inamfumo huu au ule.. kwasababu Hekima ya Mungu haichagui mfumo wa kutembelea. Bali ihukumu hiyo huduma kwa kazi zake baada ya hapo.

Ikiwa matunda yake, ni yale ya Kristo, basi muheshimu mtumishi huyo au huduma hiyo, ikiwa watu wake, wanauelekea wokovu wa kweli na wanaishi maisha ya kumpendeza Mungu basi heshimu hata kama ipo kinyume na matazamio yako.

Vilevile ukiona mtumishi ni tajiri, au ni Yule maskini anayeishi milimani, na anachokifanya hakina matunda Kristo anayoyataka sawasawa na Neno lake. Yaani watu wake ndio wanakwenda mbali na wokovu na utakatifu, maisha yako ni ya kidunia, wanafuata tu kuponywa, basi lakini upendo na Kristo hawana.. achana naye, hata kama atajiona ni wa rohoni kiasi gani..au ni mtu wa kijamii namna gani, au mwenye ushawishi namna gani, achana naye. Hekima ya Mungu haipo hapo.

Kwasababu hekima ya kweli ya Mungu inathibitika kwa kazi zake. Kama ilivyothibitika kwa Bwana Yesu na kwa Yohana, japokuwa mapito yao yalikuwa ni tofauti lakini matunda yao yalikuwa ni thabiti.

Hiyo ndio sababu Bwana Yesu aliwaambia wale mafarisayo maneno hayo..

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Au bofya chini kujiunga na group la whatsapp moja kwa moja;

https://chat.whatsapp.com/GBX2lWIcoCq8zmlnXJgaWQ

https://chat.whatsapp.com/GBX2lWIcoCq8zmlnXJgaWQ

Mada Nyinginezo:

Hamjui ya kuwa mtawahukumu malaika? Ina maana gani?

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA WARAKA WA PILI WA YOHANA.

USIRUDI NYUMA KWA KUITUMAINIA HAKI YAKO.

MZAZI, JALI MAISHA YA KIROHO YA MTOTO WAKO.

SINA PESA SASA, YESU ATANISAIDIA NINI?

Rudi nyumbani

Print this post

PONGEZI NA MAONYO YA BWANA KWA WATAKATIFU.

Kama wewe ni mtoto wa Mungu kweli kweli na sio mwana-haramu, ni vema ukafahamu tabia za Mungu kwako zinavyokuwa hususani katika eneo la pongezi na maonyo, ili usije ukaishi maisha ya wasiwasi au maisha ya kujivuna sana.

Unapaswa ufahamu kuwa Mungu akikuonya haimaanishi kuwa wakati wote unamchukiza, na vilevile Mungu akikusifia haimaanishi kuwa wakati wote unampendeza.

Kwamfano embu tafakari ile habari tunayoisoma katika Mathayo 16 ambayo Bwana Yesu aliwauliza mitume wake, kwa habari yake, kuwa wao wanasema yeye ni nani? Utaona Petro alipotoa jibu fasaha wakati ule ule Bwana alimsifia kweli kweli, kwa jinsi alivyoupokea ufunuo mkubwa namna ile,mpaka akaambiwa kuwa juu ya ufunuo ule Kristo atalijenga kanisa lake na milango ya kuzimu haitalishinda,.Na pia atampa funguo za ufalme wa mbinguni..na lo lote atakalolifunga duniani, litakuwa limefungwa mbinguni; na lo lote atakalolifungua duniani, litakuwa limefunguliwa mbinguni..(Mathayo 16:13-20)

Ukiambiwa maneno kama haya, unaweza kujiona wewe ni spesheli sana, hakuna mtume mwingine zaidi yako wewe, wewe ni bora, wewe ni mwamba, Mungu amependezwa na wewe kuliko wengine wote, na ndio maana amekufunulia maono makubwa kama hiyo. Si ni kweli?

Lakini wakati Petro anafikiria vile, dakika chache mbeleni, wakati Bwana Yesu anawaeleza juu ya kifo chake, jinsi kitakavyokuwa, Petro huyo huyo akajitokeza tena na kuanza kumkemea Bwana na kumwambia kuwa hayatampata mabaya hayo mabaya yote. Akidhania kuwa na ufunuo wa namna hiyo amefunuliwa tena na Mungu mbinguni. Lakini majibu ya Bwana Yesu, yalikuwa ni ya tofauti kabisa, tusome..

Mathayo 16:21 “Tangu wakati huo Yesu alianza kuwaonya wanafunzi wake ya kwamba imempasa kwenda Yerusalemu, na kupata mateso mengi kwa wazee na wakuu wa makuhani, na waandishi, na kuuawa, na siku ya tatu kufufuka.

22 Petro akamchukua, akaanza kumkemea, akisema, Hasha, Bwana, hayo hayatakupata.

23 Akageuka, akamwambia Petro, Nenda nyuma yangu, Shetani; u kikwazo kwangu; maana huyawazi yaliyo ya Mungu, bali ya wanadamu”.

Tafakari, muda mfupi nyuma ameambiwa ufunuo ule wa kumjua Yesu ni nani alipewa na Mungu mwenyewe..Na muda huu tena Yesu haumwona kama ni Petro anayezungumza, ni heri ingekuwa hivyo, lakini anamwona Shetani kabisa, akizungumza kwenye kinywa cha Petro akinena.

Unaweza kujiuliza, Je!, Bwana hakuona, ni kitu gani Petro atakisema  mbele kidogo? Alijua vizuri lakini hilo halibatilishi kusifiwa kwa lile zuri alilolifikiri.

Ikiwa leo hii Mungu atakuambia habari zako njema, akakusifia, au akakupongeza, au akakuthaminisha, usidhani kuwa kwa kila kitu unachokifanya kwake ni sawa,..hapana usijipumbaze kwa namna hiyo bali zaidi jitahidi kumpendeza na kusimama katika njia zake..Vilevile Mungu akikuonya leo, kwa njia zako, haimaanishi kuwa anachukizwa na wewe kwa kila kitu unachokifanya, hapana, usifikirie hivyo utavunjika moyo hata kwa vile vizuri unavyovifanya, bali rekebisha hapo unapoonyewa, kwasababu, ndicho kikwazo anachokiona ndani yako kwa muda huo. Kwasababu vipo pia vizuri unavyomfanyia na anapendezwa na wewe.

Na wakati mwingine vyote viwili vinaweza kwenda sambamba, maonyo na pongezi.  Hivyo bado usichanganyikiwe, na kudhani kuwa moja ni la Mungu na lingine ni la shetani, hapana, bali vyote vinaweza vikawa ni vya Mungu. Vichukue vitendee kazi, kwasababu anayo mawazo mazuri na wewe.Ndicho alichokuwa anakifanya hata kwa yale makanisa 7 tunayoyasoma katika Ufunuo sura ya 2 & 3

Nikutakie maisha ya heri na ya Baraka tele katika safari yako ya kuelekea mbinguni.

SHALOM.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

HAKUNA MTU ANIONDOLEAYE, BALI MIMI NAUTOA MWENYEWE

NI VIZURI SISI KUWAPO HAPA.

Ni kweli Paulo alipuuzia maonyo aliyopewa ya kwenda Yerusalemu?

UFUNUO: Mlango wa 15

MILANGO YA KUZIMU.

NI LAZIMA KUISHIKILIA IMANI MPAKA MWISHO.

Rudi nyumbani

Print this post

Ni kweli Paulo alipuuzia maonyo aliyopewa ya kwenda Yerusalemu?

SWALI: Je Ni kweli Mtume Paulo alipuuzia, maonyo aliyoonyeshwa na Roho Mtakatifu kwa kinywa cha Agabo juu ya kwenda  Yerusalemu?


JIBU: Tusome habari yenyewe kwa faida ya watu wote;

Matendo 21:10 “Basi tulipokuwa tukikaa huko siku nyingi, nabii mmoja jina lake Agabo akashuka kutoka Uyahudi.

11 Alipotufikia akautwaa mshipi wa Paulo, akajifunga miguu na mikono, akasema, Roho Mtakatifu asema hivi, Hivyo ndivyo Wayahudi wa Yerusalemu watakavyomfunga mtu mwenye mshipi huu, nao watamtia katika mikono ya watu wa Mataifa.

12 Basi tuliposikia haya, sisi na watu wa mahali pale, tukamsihi asipande kwenda Yerusalemu.

13 Ndipo Paulo alipojibu, Mnafanya nini, kulia na kunivunja moyo? Kwa maana mimi, licha ya kufungwa, ni tayari hata kuuawa katika Yerusalemu kwa ajili ya jina lake Bwana Yesu.

14 Alipokataa shauri letu, tukanyamaza tukisema, Mapenzi ya Bwana na yatendeke.

15 Baada ya siku zile tukachukua vyombo vyetu tukapanda kwenda Yerusalemu.

Tofauti na wengi tunavyodhani kwamba mtume Paulo alipuuzia maono ya Mungu, na ndio maana akaenda kukumbana na matatizo makubwa kule Yerusalemu alipokwenda mambo ambayo hayakuwa na ulazima wa yeye kukutana nayo. Lakini si kweli, kama Paulo angekuwa ni mtu wa kupuuzia maono ya Mungu, asingeandika katika waraka wake mmoja “Msitweze unabii” (1Wathesalonike 5:20). Akimaanisha msipuuzie unabii.

Paulo alikuwa ni mtu aliyethamini sana maagizo ya Roho Mtakatifu, na kuyatekeleza wa wakati. Kuna wakati Mungu alimkataza asihubiri Neno Galatia na sehemu nyingine na akatii(mdo 16:6-9). Na wakati huo huo Mungu anamwonyesha maono avuke bahari aende Makedonia kuhubiri mahali ambapo hajawahi kufika hata siku moja. Na akatii

Hivyo kitendo cha kusema Paulo hakutii maagizo ya Roho Mtakatifu, ni kukosa shabaha.

Lakini swali linakuja kama sio kutii basi  ni kwanini aamue vile?

Jibu ni kuwa, ipo tofauti ya “mtu kupewa agizo” na “mtu kuelezwa uhalisia wa mambo / kupashwa habari”. Paulo hakupewa agizo na Roho Mtakatifu kuwa asipande Yerusalemu, kama alivyopewa maagizo sehemu nyingine. Hapana, bali alielezwa uhalisia wa mambo atakayokutana nayo huko mbeleni. Na ndio maana utaona kabla hata ya Agabo kumpa unabii ule, tayari Roho Mtakatifu alikuwa ameshamshuhudia mambo hayo kuwa atakutana nayo mbeleni. Soma.

Matendo 20:22 “Basi sasa, angalieni, nashika njia kwenda Yerusalemu hali nimefungwa rohoni, nisiyajue mambo yatakayonikuta huko;

23 isipokuwa Roho Mtakatifu mji kwa mji hunishuhudia akisema, ya kwamba vifungo na dhiki vyaningoja”.

Hivyo Paulo kwa kulitambua hilo, bado hakusita kukumbana na changamoto hizo, kwa ajili ya injili. Alifikiria sana akaona dhiki haziwezi kumfanya kondoo wa Mungu wasifikiwe na injili. Hivyo akajitia moyo na kwenda kama shujaa.

Jambo kama hilo utaona pia kwa mtume Petro, kipindi kile Bwana Yesu alimwambia wewe ni kijana, lakini ukiwa mzee watu watakuja kukufunga mikono yako na kukuchukua usipotaka, (Yohana 21:18). Kuonyesha kuwa vifungo na dhiki na vifo vinamsubiria mbeleni. Lakini lile halikuwa ni agizo kwamba Petro sasa akatafute namna ya kukwepa, dhiki hizo. Hapana.

Hata sasa ni kawaida ya Roho Mtakatifu kuzungumza nasi kwa namna zote mbili. Kuna wakati atatupa maagizo, na kuna wakati atatueleza uhalisia wa mambo. Sasa pale tunapopewa maagizo au tunapoonywa, ni sharti tutii, Mungu anapokuambia usihubiri mahali Fulani, ni kweli usiende kuhubiri, anapokuambia kahubiri mahali Fulani ni kweli nenda kahubiri.

Lakini kuna wakati utakuwa katika safari yako ya kumtumikia Mungu, na akakuonyesha, matunda, na changamoto zake, akakuonyesha hata, unapigwa mawe, au unafukuzwa, au unafungwa, au unazungumziwa vibaya. Moja kwa moja usikimbilie kusema Roho Mtakatifu ananionya nisiende kuhubiri, hapana, bali tazama pia upande wa pili wa matunda, Kwasababu dhiki kama hizo haziletwi na Mungu, bali ni shetani, ambaye anafanya hivyo ili akuzuie, usifanye kazi yake hilo tu. Lakini kumbe Mungu anatamani sana, ufike kule.

Kwahiyo usitafsiri kila ono, ni agizo ,  mengine Mungu anatuonyesha tu ili yatakapotokea tusifadhaike sana, kwasababu alishatutaarifu mapema.

Yohana 16:1 “Maneno hayo nimewaambia, msije mkachukizwa.

2 Watawatenga na masinagogi; naam, saa yaja atakapodhania kila mtu awauaye ya kuwa anamtolea Mungu ibada.

3 Na hayo watawatenda kwa sababu hawakumjua Baba wala mimi.

4 LAKINI NIMEWAAMBIA HAYO, ILI MAKUSUDI SAA ILE ITAKAPOKUJA MYAKUMBUKE YA KUWA MIMI NALIWAAMBIA. Sikuwaambia hayo tangu mwanzo, kwa sababu nalikuwapo pamoja nanyi”.

Hivyo Bwana atusaidie na sisi tujifunze kuyapambanua maono ya Mungu.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

VIFO VYA MITUME WA YESU/ JINSI MITUME WALIVYOKUFA.

Tofauti kati ya ufunuo, unabii na maono ni ipi?

PINDO LA VAZI LAKE SASA LIMEREFUSHWA.

BADO UPO YERUSALEMU TU..GALILAYA HUTAKI KWENDA?

LIPI TUNAJIFUNZA KWA WALIOMWONA YESU ALIYEFUFUKA?

Rudi nyumbani

Print this post

Ni kama machungwa katika vyano vya fedha.

SWALI: Nini maana ya huu mstari?

Mithali 25: 11 “Neno linenwalo wakati wa kufaa, Ni kama machungwa katika vyano vya fedha”.


JIBU: Vyano ni wingi wa neno “Chano”, lenye maana ya sinia. Hivyo hapo anaposema Neno linenwalo wakati wa kufaa, ni kama machungwa katika vyano vya fedha, anamaanisha kuwa ni kama machungwa katika masinia ya fedha.

Sasa kwanini afananishe Neno linalofaa na machungwa katika masinia ya fedha?. Si rahisi kuelewa kwa sisi watu ambao utamaduni wetu ni tofauti na ule wa watu wa mashariki. Kwasababu machungwa yanayozungumziwa hapo si kama ya jamii yetu hii tuliyonayo. Kule kuna aina ya machungwa, ambayo wanasema ni matamu kuliko jamii zote za machungwa duniani, juisi yake ina harufu nzuri sana, machungwa hayo huwezi kuyasafirisha nje ya nchi, kwasababu hayakai muda mrefu yanaharibika ni ya kule kule tu. Na kwa kawaida wanapoyachuma huwa wanayaweka kwenye vyombo vya masinia, na sio kwenye majaba au magunia.

Sasa machungwa haya yalikuwa ni mahususi, kwa ajili ya kupewa watu waliochoka, pale wanapokula, au wanapoinywa juisi yake, basi wanaburudika na kupunguza uchovu wao kwa sehemu kubwa sana. Ni sawa na leo hii labda mtu unapopewa soda ya baridi (Labda tuseme fanta orange) wakati jua kali na kiu. Itakuburudisha si ndio.. Na ndivyo ilivyokuwa kipindi hicho kwa watu wanaishi mashariki ya kati na baadhi ya sehemu za Asia.

Kufunua kuwa ni jinsi gani Neno zuri la kufajiri lilivyo na maana sana kwa mtu aliyekatika hali ya uchungu, au msiba, au Neno la kutia moyo lilivyo na thamani sana kwa aliyevunjika moyo, au Neno la kuhamasisha lilivyo na nguvu sana kwa walioishiwa nguvu, ni kama machungwa yaliyo kwenye masinia ya fedha, tayari kwa ajili ya waliochoka.

Na habari nzuri za kufajiri, za kujenga, za kuponya, za kuimarisha, hazitoki kwa mwingine zaidi ya Yesu Kristo pekee. Hivyo tunapowahubiria watu habari hizi njema za wokovu wa Yesu Kristo, zinaponya zaidi kuliko habari nyingine zozote tuzifahamuzo. Kwasababu yeye mwenyewe alisema alikuja kwa kazi hiyo..

Isaya 61:1 “Roho ya Bwana MUNGU i juu yangu; kwa sababu Bwana amenitia mafuta niwahubiri wanyenyekevu habari njema; amenituma ili kuwaganga waliovunjika moyo, kuwatangazia mateka uhuru wao, na hao waliofungwa habari za kufunguliwa kwao.

2 Kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa, na siku ya kisasi cha Mungu wetu; kuwafariji wote waliao;

3 kuwaagizia hao waliao katika Sayuni, wapewe taji ya maua badala ya majivu, mafuta ya furaha badala ya maombolezo, vazi la sifa badala ya roho nzito; wapate kuitwa miti ya haki, iliyopandwa na Bwana, ili atukuzwe”.

Umeona, hivyo tuwahubiri watu habari za Kristo, hizo zinatosha kutibu makundi yote ya watu. Ukimsaidia mtu kumpata Kristo, umemsaidia kutatua matatizo yake yote. Kwasababu ndani yake sio tu atapata wokovu bali, na furaha ya kweli na amani ya kweli.  Na kwa kufanya hivyo rohoni na sisi Mungu anatuona  kama wahudumu wake wa machungwa katika vyombo vya fedha.

Bwana atupe na sisi macho ya kuyatendea hayo kazi.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

ONDOA TAKATAKA KATIKA FEDHA, NA CHOMBO KITATOKEA KWA MTAKASAJI.

Naye aangukaye juu ya jiwe hilo atavunjika-vunjika..

APENDAYE FEDHA HASHIBI FEDHA.

Naomba kufahamu maana ya “sura ya kijiti” katika Marko 12:26.

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya Kuzumbua na kujitoja?

Nini maana ya kuzumbua na kujitoja? Katika biblia.(Walawi 6:3, Kumbukumbu 14:1, )

Jibu: Neno kuzumbua tunalisoma katika kitabu cha Mambo ya Walawi 6:3, na tafsiri ya neno hilo ni “kukipata kitu”, pengine ambacho kilikuwa kimepotea, au kimehamishwa mahali pake..

Walawi 6:1“ Bwana akanena na Musa, na kumwambia,

2 Mtu awaye yote akifanya dhambi, na kuasi juu ya Bwana, akamdanganya mwenziwe katika jambo la amana, au la mapatano, au la kunyang’anya, au kumwonea mwenziwe;

3 AU KUZUMBUA kitu kilichopotea na kutenda la uongo juu yake, na kuapa kwa uongo; katika mambo hayo yote mojawapo atakalolitenda mtu, na kufanya dhambi kwalo

4 ndipo itakapokuwa, akiwa amefanya dhambi, na kupata hatia, atarudisha hicho alichokipata kwa kunyang’anya, au kitu kile alichokipata kwa kuonea, au ile amana aliyowekewa, au kitu kile kilichopotea ALICHOKIZUMBUA yeye,”

Na hakuna mahali pengine katika biblia neno hili limeonekana tena.

Vile vile neno “kujitoja” tunalisoma katika kitabu cha Kumbukumbu la Torati 14:1, ambalo maana yake ni “kujikata”.. Mtu anayejikata kwa wembe au kisu katika mwili wake maana yake amejitoja kwa kitu hicho.

Kumbukumbu la Torati 14:1 “Ninyi mmekuwa wana wa Bwana, Mungu wenu; MSIJITOJE miili yenu, wala msifanye upaa katikati ya macho yenu kwa ajili ya aliyekufa”

Hakuna mahali pengine popote neno hili limeonekana katika biblia.

Katika maneno hayo mawili tunajifunza kuwa Mungu hapendezwi na dhuluma, maana yake kama ndugu yako kapoteza kitu na wewe ukakipata! (maana yake ukakizumbua), unapaswa umrudishie mwenyewe kitu hicho, hupaswi kubaki nacho wewe na kukificha kana kwamba ni chako na kumdanganya Yule aliyekipoteza.. jambo hilo halimpendezi Mungu kabisa.

Vile vile, biblia haijaturuhusu sisi kuitoja miili yetu, maana yake kuikata kata, kipagani… kama mfano wa wale manabii wa baali kipindi cha Nabii Eliya, walivyojikata..

1Wafalme 18: 28 “Wakapiga kelele, wakajikata-kata kwa visu na vyembe kama ilivyo desturi yao, hata damu ikawachuruzika”.

Hata leo, watu wanajikata katika matambiko yao ya kimila, na hata katika kuchanjwa chale, na wengine katika kujichora alama(tattoo). Namna zote hizi za kujikata ni machukizo mbele za Mungu, Kwasababu miili yetu ni hekalu la Roho Mtakatifu, maana yake Roho Mtakatifu anakaa ndani yetu, hivyo hatupaswi hata siku moja kufikiri kuiharibu nyumba yake hii.. kwasababu tukiiharibu na yeye amesema atatuharibu sisi. (1Wakoritho 3:17)

Bwana atubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

CHUKIZO LA UHARIBIFU

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 3

PALE UNAPOKUWA NA SABABU ZA KUMLAUMU MTU, UFANYE NINI?

NITAUPATAJE UPENDO WA KI-MUNGU NDANI YANGU?

Kwa jina lake Ubaba wote wa mbinguni na wa duniani unaitwa.

Rudi nyumbani

Print this post

SOMO no.02 (BINTI WA YEFTHA).

Karibu katika mwendelezo wa masomo yawahusuyo wanawake wa kwenye biblia,  Leo tutamtazama mwanamke mmoja/binti mmoja aliyekuwa mtoto wa pekee wa Mwamuzi wa Israeli.

Binti huyu alikuwa alikuwa ni mtoto wa pekee wa mtu aliyeitwa Yeftha, ambaye alikuwa ni Mwamuzi wa taifa la Israeli. Nafasi ya mwamuzi katika Israeli nyakati hizo, ilikuwa inakaribia sana kufanana na ile ya Mfalme, ingawa sio ya kifalme.  Hivyo mtu aliyekuwa mwamuzi katika Israeli katika nyakati hizo, alikuwa ni Mkuu sana, na mwenye kujilikana na kuheshimiwa katika nchi nzima.

Lakini tunasoma katika biblia alitokea Mwamuzi mmoja aliyeitwa Yeftha, ambaye huyu alikuwa ni shujaa sana..Na hakuwa na mwana wa kiume katika nyumba yake bali wa kike tu, tena mmoja. Lakini tunasoma wakati Fulani alipokwenda vitani, alimwekea Bwana nadhiri kubwa, kutokana na ukubwa wa vita iliyoko mbele yake, alitazama mbele yake akaona hiyo vita anayotaka kwenda kukumbana nayo, sio ndogo!, na endapo ikitokea kashinda basi ni muujiza wa Mungu tu umefanyika, na si kingine, kwasababu katika hali ya kawaida ni ngumu kushinda…kwasababu wanaokwenda kupigana nao ni wengi kuliko wao na wenye nguvu kuliko wao.

Kwahiyo ili kujihakikishia ushindi zaidi, alimwekea Mungu nadhiri, kwamba endapo Mungu atampa ushindi, basi kile cha kwanza, kitakachotoka kumlaki wakati anarudi vitani atakitoa kiwe sadaka ya kuteketezwa mbele za Bwana. Na katika mawazo  yake pengine alilenga mtumwa wake mmoja, au ndugu mmoja aliye katika nyumba yake, ndiye atakayekuja kumlaki (kwani nyumba yake ilikuwa na watu wengi, kwasababu yeye alikuwa ni Mkuu katika Israeli). Lakini cha kushtusha ni kwamba alitokea Binti yake wapekee kuja kumlaki, kinyume na matarajio yake. Na alipomwona akahuzunika sana, lakini akawa hana cha kufanya…(Hawezi kuitangua nadhiri yake)

Hebu tusome kidogo habari yenyewe kisha tusonge mbele..

Waamuzi 11:28 “Lakini mfalme wa wana wa Amoni hakuyasikiza hayo maneno ya Yeftha aliompelekea.

 29 Ndipo roho ya Bwana ikamjilia juu yake Yeftha, naye akapita katika Gileadi na Manase, akapita na katika Mispa ya Gileadi, na kutoka hapo Mispa ya Gileadi akapita kuwaendea wana wa Amoni.

30 NAYE YEFTHA AKAMWEKEA BWANA NADHIRI, AKASEMA, KWAMBA WEWE UTAWATIA WANA WA AMONI MKONONI MWANGU KWELI,

31 ndipo itakuwa ya kwamba, kile kitakachotoka katika milango ya nyumba yangu kunilaki, hapo nitakaporudi na amani kutoka kwa hao wana wa Amoni, kitu hicho kitakuwa ni cha Bwana, nami nitakisongeza kiwe sadaka ya kuteketezwa.

 32 Basi Yeftha akavuka kuwaendea wana wa Amoni ili kupigana nao; naye Bwana akawaua mkononi mwake.

33 Akawapiga kutoka Aroeri hata kufikilia Minithi, miji ishirini, na mpaka Abel-keramimu, akawapiga kwa machinjo makuu mno. Basi hivyo wana wa Amoni walishindwa mbele ya wana wa Israeli.

34 Kisha Yeftha akafika Mispa nyumbani kwake, na tazama, binti yake akamtokea kumlaki, na matari na machezo; naye alikuwa ni mwanawe pekee; hakuwa na mwingine, mwana wala binti, ila yeye.

35 Ikawa alipomwona akayararua mavazi yake, akasema, Ole wangu! Mwanangu, umenitweza sana, nawe u mmoja miongoni mwa hao wanisumbuao; kwa kuwa mimi nimemfunulia Bwana kinywa changu, nami siwezi kurejea nyuma.

36 BINTI YAKE AKAMWAMBIA, BABA YANGU, WEWE UMEMFUNULIA BWANA KINYWA CHAKO; BASI UNIFANYIE SAWASAWA NA HAYO YALIYOTOKA KINYWANI MWAKO; KWA KUWA YEYE BWANA AMEKULIPIA KISASI JUU YA ADUI ZAKO, HAO WANA WA AMONI.

  37 Kisha akamwambia baba yake, Basi na nifanyiwe neno hili; niache peke yangu muda wa miezi miwili, ili nipate kwenenda milimani, na kuombolea uanawali wangu, mimi na wenzangu.

  38 Akamwambia, Haya, enda. Akampeleka mbali muda wa miezi miwili; naye akaenda zake, yeye na wenziwe, akauombolea uanawali wake huko milimani.

 39 Basi ikawa mwisho wa hiyo miezi miwili, akarudi kwa babaye, aliyemtenda sawasawa na ile nadhiri yake aliyokuwa ameiweka; naye alikuwa hajamjua mtu mume. Kisha ikawa desturi katika Israeli,

 40 kwamba binti za Israeli waende mwaka baada ya mwaka ili kumkumbuka huyo mwana wa Yeftha, Mgileadi, siku nne katika mwaka”

Leo nimetamani tujifunze kuhusu huyu binti, Kwasababu alikuwa ana roho ya Ushujaa ndani yake!..

Dada/Mama/ binti siku zote kumbuka hili: ni vizuri kwanza kujifunza kwa wanawake waliopo katika biblia kabla ya kuwatafuta wanaume.

Wanawake wengi wanapenda sana kujifunza kwa Isaka!.. Jinsi alivyonusurika kifo!, cha kuchinjwa na kutolewa sadaka ya kuteketezwa, lakini hawajui kuwa Isaka alinusurika tu!!, hakuchinjwa, wala hakutolewa sadaka… Yupo Shujaa mmoja katika biblia ambaye Alikubali mwenyewe kuchinjwa na nyama yake kukatwa katwa vipande na kisha kutolewa kama sadaka ya kuteketezwa!.. Ambaye pengine tutakapofika mbinguni tutamkuta ni mkuu kuliko ISAKA!..Na tutajilaumu sana kwanini hatukujifunza kutoka kwake!

Na huyo si mwingine zaidi ya huyu binti wa Yeftha!!. Binti huyu baba yake alimwambia dhahiri kabisa kwamba atakwenda kutolewa sadaka ya kuteketezwa!.. Jambo ambalo kiuhalisia ni gumu sana mtu kukubaliana nalo, lakini Binti huyu baada ya kupewa hizo taarifa!, wala hazikumwazisha.. wala hakuogopa kufa!, wala hakuogopa makali ya visu katika mwili wake, wala moto.. badala yake alisema maneno haya..

“36 BINTI YAKE AKAMWAMBIA, BABA YANGU, WEWE UMEMFUNULIA BWANA KINYWA CHAKO; BASI UNIFANYIE SAWASAWA NA HAYO YALIYOTOKA KINYWANI MWAKO; KWA KUWA YEYE BWANA AMEKULIPIA KISASI JUU YA ADUI ZAKO, HAO WANA WA AMONI”.

Bila shaka maneno kama haya, Isaka mwana wa Ibrahimu asingeweza kusema, pale alipokuwa anapelekwa mlimani kuchinjwa! Na Baba yake. Si ajabu, Ibrahimu hakumwambia Isaka chochote, kwamba anakwenda kumchinja na kumtoa sadaka!..pengine ingekuwa kitimtimu pale!, pangekuwa hapatoshi!, pangetokea vurugu kubwa sana!…Ndio maana Ibrahimu alimficha, kwasababu alimwona pengine hana huo utayari wa kujitoa kufa!!.

Mwanzo 22: 6 “Basi Ibrahimu akazitwaa kuni za hiyo sadaka, akamtwika Isaka mwanawe; akatwaa moto na kisu mkononi mwake, wakaenda wote wawili pamoja.

 7 Isaka akasema na Ibrahimu baba yake, akinena, Babangu! Naye akasema, Mimi hapa, mwanangu. Akasema, Tazama! Moto upo, na kuni zipo, lakini yuko wapi mwana-kondoo kwa sadaka ya kuteketezwa?

 8 Ibrahimu akasema, Mungu atajipatia mwana-kondoo kwa hiyo sadaka, mwanangu. Basi wakaendelea wote wawili pamoja”.

Huyo ni Isaka anaulizia sadaka ya kuteketezwa ipo wapi!, maana yake yeye haimwingii akilini kujiweka katika hilo kundi!, kwamba yeye anaweza kuwa hiyo sadaka!.. Lakini alikuja kutokea Shujaa mmoja!, binti mdogo, ambaye taarifa za msiba si kitu kwake!, ambaye visu shingoni si kitu kwake, ambaye moto juu ya mwili wake si kitu kwake.. Zaidi ya yote alikuwa mtoto, tena ni binti, na tena ni BIKIRA!.. Lakini alikuwa na Imani kubwa kuliko ya Isaka!!. Huyu taarifa za kuchinjwa zilipomjia hakupepesuka wala hazikumshutua, alianza kuufikiria mambo mengine kabisa (Ubikira wake!!..na kwenda kuomboleza kwaajili ya huo, na alipomaliza kwa miezi miwili), kama vile kondoo apelekwavyo machinjoni, alikwenda mwenyewe na akachinjwa na kufa na kuteketezwa..

Labda inawezekana hujui vizuri!, sadaka ya kuteketezwa inakuwaje.

Sadaka ya kuteketezwa ambayo Mungu alimjaribu nayo Ibrahimu amtoe mwanawe , ilikuwa ni kwamba.. mtoto Yule anakamatwa, anafungwa kamba na kisha kisu kinapitishwa shingoni, anachinjwa kama ng’ombe, damu inachuruzika, na baada ya kuchinjwa, mwili wake unakatwa vipanda vipande, kisha vile vipande vinawekwa juu ya kuni, zilizopo juu ya mawe, na moto unawashwa na ile nyama inateketea kabisa mpaka inakuwa jivu!.. Hiyo ndiyo sadaka aliyokusudiwa Isaka!, ambayo Mungu alimwepusha nayo haikumpata, lakini ikatimia kwa shujaa huyu mmoja Binti wa Yeftha!, yeye alikubali mwenyewe kwenda kuchinjwa!.

Waebrania 11:35  “Wanawake walipokea wafu wao waliofufuliwa. Lakini wengine waliumizwa vibaya hata kuuawa, wasikubali ukombozi, ili wapate ufufuo ulio bora”

Isaka aliibeba picha ya Yesu tu!, lakini huyu binti alilibeba tukio zima la Yesu!.. alionja kile Bwana alichokipitia pale Kalvari.. Na baada yake hatuoni mtu mwingine, awe mwanaume au mwanamke aliyefanya jambo la kishujaa kama hilo!, wengine wote kwenye biblia waliingia kwenye dhiki bila idhini zao, walishikwa wakakatwa vichwa na kuchinjwa, lakini si kujipeleka wenyewe kuchinjwa!…

Jambo hilo tunaliona kwa watu wawili tu! Kwenye biblia nzima, wa kwanza ni MKUU WA UZIMA MWENYEWE, MWAMBA-YESU KRISTO..Na mwingine ni huyu “Binti wa Yeftha”.

Dada/Binti /mama umeona ni jinsi gani una mashindano makubwa mbele yako??… Siku ile utajitetea vipi, kwamba umeshindwa kujitoa kwake!, na kumtumikia  kwasababu tu wewe si mwanaume??..Leo hii unaogopwa kuchekwa!, wenzako walikufa kabisa!..jambo ambalo hata mwanaume hawakuweza kulifanya!.. Bado huoni tu! Siku ya hukumu binti wa Yeftha atasimama kuhukumu mabinti wengi??..Bado huoni tu hilo!..fahamu kuwa!..hukumu ya wanawake itakuwa ni kali kuliko ya wanaume.. kwasababu katika biblia wapo wanawake waliofanya makubwa kuliko wanaume.  Eliya alimkimbia Yezebeli, ili ayanusuru maisha yake, lakini huyu binti wa Yeftha, yeye anakifuata kifo mwenyewe!..jiulize kati ya hao wawili ni yupi mwenye imani kubwa!..Wanawake kama hawa pamoja na mfano wa Yule Malkia wa Sheba Bwana Yesu aliyemtaja, watasimama kuhukumu vizazi vyetu..

Mathayo 12:42 “Malkia wa kusini atasimama siku ya hukumu pamoja na watu wa kizazi hiki, naye atawahukumu kuwa wamekosa; kwa sababu yeye alikuja kutoka pande za mwisho za dunia ili asikie hekima ya Sulemani, na hapa yupo aliye mkuu kuliko Sulemani”.

Hivyo, wewe kama Mwanamke, simama itambue nafasi yako!.. kama Dada simama!, kama binti simama!.. usiogope kufa!, badala yake uwe tayari kufa hata kwaajili ya imani, usiogope kupitia dhiki,badala yake uwe tayari kukumbana nazo kwaajili ya imani yako, usiogopwe kuonwa mshamba unapoacha mambo yote ya kidunia, na fashion zote!..Badala yake uwe tayari kuonekana umerukwa na Akili, Fahamu kuwa thawabu yako ni kubwa mbinguni.. Kuanzia leo anza kupiga mbio, ukijifunza kwa wanawake mashujaa katika biblia..

Vile vile usiutamanie  udunia, ukasema ngoja uule ujana, ndio utamtumikia Mungu, siku ile huyu binti wa Yeftha atasimama kukuhukumu, kwasababu yeye alikufa katika ubikira wake bila mume, angeweza kumwambia baba yake amruhusu akaolewe kwanza miezi miwili ndipo, amtoe sadaka!..lakini hakufanya hivyo, aliuthamini ubikira wake, akafa hivyo hivyo..

Vile vile hakuwa mtoto wa maskini, labda tuseme amechoka maisha ndio maana kakubali kujitoa afe!.. hapana!, alikuwa ni mtoto wa Mwamuzi wa Israeli..Ni tajiri sana!, kwasababu waamuzi walikuwa ni kama wafalme, lakini hakuutumainia utajiri wake, wala ubikira wake, wala uzuri wake.. Alikubali kuondoka!, kwasababu alijua, anao mji unao mngojea huko mbele. Yeru salem mpya. Alijua ufufuo unakuja na atakuwa mkuu katika ufalme wa mbinguni.

Kumbuka Mungu aliwachagua tu wanaume kwenye biblia wawe kama mwonekano tu!.. ndio maana utaona kila mahali wanatajwa wanaume..kama Isaka, Yakobo, Eliya n.k Lakini hiyo haimaanishi kuwa wao ndio wa kwanza katika ufalme wa Mbinguni.. Kwaufupi ni kwamba Mbinguni watakuwepo wanawake watakaopata thawabu kubwa hata kuliko hata wakina Ibrahimu, Isaka na akina Eliya na Musa. Kwasababu Mungu siku zote hana upendeleo.

Hivyo unaposoma biblia, anza kutafuta matendo ya wanawake mashujaa, ujifunze kwao, na vile vile, jifunze kwa wale waliojiharibia njia zao pia, ili uchukue tahadhari.

Mwisho wa muhtasari huu kumhusu “binti wa Yeftha” shujaa wa Bwana. Usikose mwendelezo wa wanawake wanaofuta!.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Sadaka ya kuinuliwa ni sadaka ya namna gani?

FUNGUO WALIZOKUWA NAZO MABINTI WATANO WA SELOFEHADI!

TUJIFUNZE JAMBO KWA WANAWAKE HAWA WAWILI:

Maana Ya Maneno Katika Biblia.

Sadaka ya unga na sadaka ya kinywaji zilikuwaje?

Rudi nyumbani

Print this post

SIKU YA HOFU YANGU NITAKUTUMAINI WEWE.

Daudi alisema..

Zaburi 56:3 “Siku ya hofu yangu nitakutumaini Wewe;

4 Kwa msaada wa MUNGU nitalisifu neno lake. Nimemtumaini Mungu, sitaogopa; Mwenye mwili atanitenda nini”?

Maadamu tupo hapa duniani, haijalishi tutakuwa ni watakatifu au mkamilifu kiasi gani, lakini maadamu tunaishi chini ya jua, zipo siku ngumu tutapishana nazo katika safari yetu ya imani. Hizo ni  nyakati zenye masumbufu sana, zenye kuvunjika moyo kusikokuwa kwa kawaida, zenye huzuni nyingi sana, zenye machozi na majonzi, Daudi alizitambua nyakati hizo na kuziita  “SIKU ZA HOFU YANGU”.

Na hizi zinatofautiana kati ya mtu na mtu, mwingine Siku ya hofu yake, ni vipindi cha Misiba.  Pengine amefiwa na mpendwa/wapendwa wake wa karibu sana kwa ghafla, labda kwa ajali mbaya, hichi kipindi huwa ni kigumu sana isivyoelezeka. Mfano wa watu kama hawa kwenye biblia alikuwa ni Ayubu, aliyefiwa na watoto wake wote 10 kwa mkupuo.

Mwingine,  siku ya hofu yake ni siku za kuwindwa na maadui ili auawe, mfano wa watu hawa ndiye kama Daudi mwenyewe aliyeandika habari hiyo. Yeye ilifikia wakati serikali nzima inamwinda, imwangamize. Embu jiweke wewe katika hiyo nafasi, maisha yako yote, unajificha mapangoni tu, kwasababu umesikia kuwa raisi na watumishi wake wote wa usalama wametumwa nchi nzima kukuwinda ili wakuue. Si jambo jepesi.

Mwingine siku ya hofu yake ni siku za  magonjwa. Amepatwa na ugonjwa wa ghafla ambao pengine hakuwahi kudhani kama ungemfikia mtu kama yeye, labda Ukimwi, au Kansa, au amepata ajali, na ikamletea ulemavu wa kudumu, kama vile kiharusi, au ukiwete, au kalazwa ICU, kwa kwa kipindi kirefu, huo wakati unakuwa ni mgumu sana kuchukulika,. Mfano wa mtu kama huyu ni Eprafodito ambaye alikuwa  ni mtume aliyetenda kazi pamoja na akina Paulo, yeye  ilifikia wakati hali yake ikawa mbaya sana karibu na kufa kwa kuugua.(Wafilipi 2:25-27)

Mwingine siku ya hofu yake ni siku ya kusalitiwa.  Aidha Kusalitiwa na ndugu yake katika imani, au kusalitiwa na wazazi kisa ameokoka, au kusalitiwa na mke/mume, au kusalitiwa na marafiki.  Kama vile Bwana Yesu alivyosalitiwa na Yuda. Huu pia si wakati mwepesi, hauchukuliki kirahisi. Jambo kama hili linaweza kumpelekea mtu mwingine hata kujinyonga, au kuleta madhara yoyote kwa wengine.

Mwingine siku ya hofu yake, ni siku za kukumbana na hasara. Kupoteza kila kitu, kupoteza mali zake alizozisumbukia, au fedha, au mashamba, au mifugo, kama vile Ayubu kiasi kwamba habakiwi na chochote. Madeni yamemsonga,  bado familia inamwangalia, akiangalia mikopo anapaswa arudishe,na asiporudisha nyumba inauzwa, jambo ambalo hakutegemea kabisa kama lingemtokea kwa haraka hivyo.  Hichi kipindi huwa ni kigumu pia, sio cha kuchukulika kiwepesi.

Na vipindi vingine vyote vya namna kama hiyo..

Sasa ukijikuta katika siku kama hizo, na wewe umekoka, usiwe na haraka kumkatia tamaa Mungu, usiwe mwepesi wa kukimbilia kwa wanadamu, vilevile usitoe maneno ya kukufuru, au kupeleka manung’uniko  yote kwa Mungu. Bali zidi kumtumaini yeye, kama Daudi alivyosema “Siku ya hofu yangu nitakutumaini Wewe”.. Kuwa mtulivu kama Ayubu, utakumbuka hata wakati ambapo mke wake anamshauri amkufuru Mungu afe lakini yeye alimkemea  na kumwambia asiwaze kipumbavu kama wengine wafanyavyo,  Na wewe pia mtazame Mungu peke yake, usiwe na maneno mengi kwake katika siku kama hizo, na kuanza kusema kwanini hivi, kwanini vile, mtazame Mungu tu ndugu. Zipo sababu nyingine zilizo juu ya upeo wa ufahamu wako usizozijua.

Siku kama hizo , kifungu hichi kiwe faraja yako wakati wote..

Yeremia 29:11 “Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema Bwana, ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho”.

Mtazame mtu kama Ayubu jinsi mwisho wake ulivyokuwa wa faraja, kwani yote aliyoyapoteza Mungu alikuja kumrudishia mara mbili, hata watoto nao Mungu alimpa wengine wazuri kushinda hata wale wa kwanza, na hata siku ile ya ufufuo bado Mungu atamkutanisha na wale watoto wake wa kwanza aliowapoteza.

Yakobo 5:11 “Angalieni, twawaita heri wao waliosubiri. Mmesikia habari ya subira yake Ayubu, mmeuona mwisho wa Bwana ya kwamba Bwana ni mwingi wa rehema, mwenye huruma”.

Daudi naye, japokuwa alilemewa na maadui zake (Sauli), lakini bado hakuacha kumtumainia Mungu, mwisho wa siku Mungu akamlinda, na kumuhifadhi hai, na kumstarehesha katika ufalme wake.

Nawe vivyo hivyo fahamu tu, mwisho wako utakuja kuwa mzuri endapo utaendelea tu hivyo hivyo kushikamana na Bwana. Kwasababu yeye ni mwingi wa rehema na huruma, kumbuka anajishughulisha sana na mambo yetu, Na zaidi ya yote alishayachukua masikitiko na fadhaa zetu zamani sana(Isaya 53:4).

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

MLANGO MWINGINE WA ADUI KUTULETEA MAJARIBU.

Waoga ambao hawataurithi uzima wa milele ni watu wa namna gani?(Ufunuo 21:8).

Mungu anaposema “nitaliweka jina langu” ana maana gani?

KUWA MAKINI NA MITANDAO, NI SHIMO REFU.

NAWE UTAGEUZWA KUWA MTU MWINGINE.

Rudi nyumbani

Print this post

Kwanini Bwana aliwalenga mbwa na nguruwe tu katika Mathayo 7:6?

SWALI: Kwanini Bwana Yesu aliwalenga mbwa na nguruwe tu , na si wanyama wengine katika mfano wa Mathayo 7:6?

Mathayo 7:6 “Msiwape mbwa kilicho kitakatifu, wala msitupe lulu zenu mbele ya nguruwe, wasije wakazikanyaga chini ya miguu yao, wakageuka na kuwararua”.


JIBU: Alitumia mfano wa wanyama hao wawili, kwasababu ya tabia zilizopitiliza za kutokujali walizo nazo, kwamfano Mbwa, ni mnyama wa kufugwa lakini bado ni mnyama asiyejali ni kitu gani anakula tofauti na wengine kama vile paka.. Na ndio maana anaridhika na vyakula vya majalalani au   makombo yaliyosalia ya majumbani, kama vile Bwana Yesu alivyosema katika…

Mathayo 15:26 “Akajibu, akasema, Si vema kukitwaa chakula cha watoto na kuwatupia mbwa.

27 Akasema, Ndiyo, Bwana, lakini hata mbwa hula makombo yaangukayo mezani pa bwana zao”.

Vilevile ni heri ingekuwa anaishia kwenye makombo tu, lakini pia mbwa ni mnyama ambaye yupo tayari KUYALA MATAPISHI YAKE mwenyewe. Bila kujali kuwa ni uchafu ule. Sasa embu jiulize, kama hajali anachokula, atajali vipi, au atathamini vipi chakula kizuri unachompa?..Utadhani atakufurahia sana, kumbe mwenzako wala!!

Halikadhalika, na nguruwe naye. Ni mnyama wa kufugwa, lakini anapenda sana kukaa kwenye matope, jambo ambalo huwezi kuliona kwa kuku au mbuzi. Ni mnyama asiyethamini usafi hata kidogo. Sasa fikiria unaondoka, na kuchukua ile lulu yako ya thamani ambayo umeinunua kwa bei ghali, labda tuseme milioni 10, lulu ambayo unajua wanaovaa ni mamalkia tu au watu wenye uwezo, halafu unakwenda kumuogesha nguruwe wako vizuri na  kumvisha, lengo lako ni kutaka kumwona akipendeza.

Wewe unategemea nini kama sio kwenda kugaragara nayo kwenye matope,na kuikanyaga? Yaani ni heri hata ungemvisha punda, lakini sio nguruwe. Hivyo mbwa na nguruwe walitungiwa hata mithali yao tangu zamani, ambayo tunaisoma katika..

2Petro 2:22 “Lakini imetukia kwao sawasawa na ile mithali ya kweli, Mbwa ameyarudia matapiko yake mwenyewe, na nguruwe aliyeoshwa amerudi kugaa-gaa matopeni”.

Ikifunua kuwa hata leo hii, wapo watu wenye tabia za wanyama hawa, ambao hawapaswi hata kidogo kupewa vitu vitakatifu (ikiwa na maana hawapaswi kupewa mambo ya ndani kabisa yamuhusuyo Mungu). Watu kama hawa hata ujaribuje kuwaeleza habari za Mungu, na uzuri wake, mambo ambayo pengine wewe uliyapata kwa mateso, na ulipoyapata ukayafurahia, ukadhani itakuwa sawa na kwao, ndugu utaishia tu kudharauliwa, kuchekwa, kukejeliwa, kutukanwa, na wakati mwingine kupigwa na kuudhiwa.

Hivyo wewe kama mkristo unapaswa uwe na hekima unapokutana na makundi ya watu wa namna hii. Ukishaona mtu anabishana na wewe kuhusiana na habari za Kristo, au anadhihaki dhihaki, tu wala usihangaike naye kumuhadithia maneno mengi, achana naye, kuwa kama mjinga kwake, nenda kwa Yule mwingine aliyetayari kusikia.. Kwasababu ukizidi kubishana na huyu mwishowe wewe ndio utakayeumia.

Hiyo ndio maana ya hiyo mithali, Msiwape mbwa kilicho kitakatifu, wala msitupe lulu zenu mbele ya nguruwe, wasije wakazikanyaga chini ya miguu yao, wakageuka na kuwararua.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya Dirii, Chepeo na Utayari?

MTAWATUPIA MBWA NYAMA HIYO.

Nini maana ya “kila tendo lisilotoka katika imani ni dhambi?”

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 3

UFUNUO: Mlango wa 18

Rudi nyumbani

Print this post

Tofauti kati ya kuhukumu na kulaumu ni ipi?

SWALI: Bwana Yesu asifiwe,.Naomba kufahamu tofauti kati ya kuhukumu na kulaumu, maana nashindwa kuelewa, imesema tusihukumu. Je kwa mtu anayetenda dhambi kwa makusudi unapomlaumu ni sawa na kumuhukumu?

Luka 6:37 “Msihukumu, nanyi hamtahukumiwa; msilaumu, nanyi hamtalaumiwa; achilieni, nanyi mtaachiliwa”.


JIBU: Kuhukumu ni kitendo cha moja kwa moja kutoa/kuamua hatma ya mtu mwingine, Na hiyo inakuja pale mtu anapojiona yeye ni bora/mwema sana zaidi ya wale wengine, . Kwamfano mtu mmoja atamwona kahaba, au mlevi, au shoga barabarani na wakati huo huo atamwambia wewe ni ibilisi, mwana wa kuzimu, Au atakutana  na wapagani wanaabudu miungu yao mahali fulani, ataanza kuwanyooshea kidole na kuwaita makafiri wa motoni wale, bila hata kuwaambia kitu kingine chochote, kisa tu kawaona wanafanya matendo yasiyompendeza Mungu. Hapo tayari kashawahukumu.

Lakini Kulaumu ni kitendo cha kukosoa kila kitu, kwa lengo la kuonyesha kuwa  kitendo alichokifanya/anachokifanya Yule mwingine ni cha kupuuzi sikuzote, hakina maana. Na kwa kawaida watu wanaolaumu nao pia wanakuwa na fikra kwamba wao huwa hawakoseagi..Ingekuwa ni wamepewa fursa hiyo wangeitumia vizuri. (Wana tabia ya kujiona wao ni wakamilifu sikuzote)

Kwamfano lawama mara nyingi zinawakuta viongozi, Utakuta kiongozi, kafanya jambo fulani la kimaendeleo, lakini kwasababu mtu fulani anajiona yeye hawezi kukosea, ataanza kutoa kasoro, kwa kila kitu kilichofanywa hata kama ni kizuri, utasikia, kwanini zile pesa zisingetumiwa kwa hili au lile, kusingekuwa na matatizo haya na yale, hiyo ndio laumu. Kana kwamba yeye yupo sahihi wakati wote, hajawahi kufanya kitu akakosea.

Au mtu mwingine, labda mzazi wake ameshindwa kumtimizia haki yake ya msingi, pengine elimu, halafu amekuwa mtu mzima, akaona madhara ya kutopelekwa kwake shule. Sasa badala ajifunze “kuachilia” kama biblia inavyosema, achilieni, nanyi mtaachiliwa, yeye ataanza kuwalaumu wazazi  wake tangu ujana wake hadi uzee wake, kana kwamba walifanya makosa makubwa sana, Na kusahau kuwa yeye mwenyewe pia anayomakosa mengi, ambayo Mungu anayohaki ya kumlaumu kupitia hayo.

Vitendo vyote hivi Mungu havipendi. Kuhukumu pamoja na kulaumu, kwasababu na sisi Mungu atatufanyia hivyo hivyo siku ile ya hukumu, tusipobadilika, Na kwakweli Bwana atusaidie viondoke ndani yetu. Lakini pia tunapaswa tufahamu kuwa kuelezwa uhalisia wa mambo sio kuhukumiwa, jambo ambalo watu wengi wanatafsiri isivyosawa. Kwamfano mtu ni mlevi, halafu anaelezwa kuwa walevi wote biblia inasema wataenda jehanamu, akadhani hapo anahukumiwa.. Hapo haukumiwi, bali anaelezwa ukweli wa mambo. Kwamfano hata wewe ukimwona mtoto wako anacheza karibu na shimo, ukamwambia “watoto wanaocheza karibu na mashimo mwisho wao huwa ni kutumbukia na kufa”. Hapo hujahitimisha kuwa Yule mtoto ni wa kufa, lakini umemweleza uhalisia wa mambo. Hivyo na wewe unavyohubiriwa wazinzi wote watakwenda kuzimu, ujue kuwa hauhukumiwi, bali unaelezwa hatma ya maisha yako.

Unapoambiwa wanaojichubua miili yao wote na wanaovaa nguo za uchi uchi, hatma yao ni kwenye ziwa la moto. Hauhukumiwi wala haulaumiwi bali unahubiriwa hatma yako. Lengo la Yule mhubiri sio uende kwenye ziwa la moto bali utubu ili uikwepe hukumu.

Lakini mtu akikufuata na moja kwa moja akakwambia wewe ni ibilisi, au kafiri, au joka, au ajenti wa kuzimu, kana kwamba wewe huwezi kupokea neema yoyote kama ya kwake,. Huyo tayari ameshakuhukumu na biblia imekataza sana hilo, kwasababu anayejua hatma ya mtu ya mwisho ni Mungu na sio yeye. Lakini akikueleza matokeo ya ukafiri wako, hajakumukumu, zaidi kaonyesha upendo kwako.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

BASI, IWENI NA HURUMA, KAMA BABA YENU ALIVYO NA HURUMA(Luka 6:36)

Je Lutu alikwenda kuwahukumu watu wa Sodoma na Gomora? Kulingana na Mwanzo 19:9?

Tofauti kati ya uchafu wa mwilini na rohoni ni  ipi?

SI KWA UWEZA WALA KWA NGUVU BALI KWA ROHO YANGU, ASEMA BWANA.

Rudi nyumbani

Print this post