Uovu unapoongezeka sana na kufikia kiwango ambacho watu hawataki tena kubadilika..biblia inatuambia Mungu huwa anaachilia nguvu ya upotevu ili waendelee kuuamini UONGO. Ile nguvu ya kumfanya mtu aone njia anayoiendea sio sawa inaondoka ndani yake na inakuja nguvu nyingine mpya ya kumfanya aone na kuamini asilimia mia kwamba yupo katika njia sahihi.
Mstari huo tunausoma katika kitabu cha..
2Wathesalonike 2:10 “na katika madanganyo yote ya udhalimu kwa hao wanaopotea; kwa sababu hawakukubali kuipenda ile kweli, wapate kuokolewa. 11 Kwa hiyo Mungu awaletea nguvu ya upotevu, wauamini uongo; 12 ili wahukumiwe wote ambao hawakuiamini kweli, bali walikuwa wakijifurahisha katika udhalimu”.
2Wathesalonike 2:10 “na katika madanganyo yote ya udhalimu kwa hao wanaopotea; kwa sababu hawakukubali kuipenda ile kweli, wapate kuokolewa.
11 Kwa hiyo Mungu awaletea nguvu ya upotevu, wauamini uongo;
12 ili wahukumiwe wote ambao hawakuiamini kweli, bali walikuwa wakijifurahisha katika udhalimu”.
Leo tutaangalia mifano baadhi katika biblia ya watu ambao hawakutaka kudumu katika kweli na hivyo Mungu akawatumia nguvu ya kuamini uongo, ili wakaangamia katika huo.
Huyu ni mtu, Bwana alimuonya asiende kuwalaani Israeli lakini akawa hataki kusikiliza sauti ya Mungu, kinyume chake akawa analazimisha kwenda kuwalaani watu wa Mungu ili apate fedha na umaarufu kutoka kwa Mfalme wa Moabu..alionywa lakini hakusikia…matokeo yake Mungu akamwambia aende! Na yeye kudhani kwamba Mungu tayari kampa kibali alienda pasipo kujua kuwa tayari ile nguvu ya upotevu ya kuuamini uongo inampeleka pabaya…kama sio yule punda kumsaidia angeshakufa..(kasome kitabu cha Hesabu 22).
Huyu Mungu alimwonya mara nyingi sana juu ya uovu wake, ageuke atubu lakini hakusikia, mpaka ilipofika siku ambayo Mungu aliiachia nguvu ya upotevu ishuke juu yake, auamini uongo…Siku hiyo alitaka kwenda vitani na Mungu akatuma pepo la uongo liwaingie manabii wake ili wamwambie uongo…Kwani hao manabii wake kila siku walikuwa wanamwambia ukweli lakini siku hiyo waliingiwa na pepo pasipo wao kujua na kujikuta wanaona maono ya uongo, na kumpotosha mfalme..
1Wafalme 22: 20 “Bwana akasema, Ni nani atakayemdanganya Ahabu, ili akwee Ramoth-Gileadi akaanguke? Basi huyu akasema hivi; na huyu hivi. 21 Akatoka pepo, akasimama mbele za Bwana, akasema, MIMI NITAMDANGANYA. 22 Bwana akamwambia, Jinsi gani? Akasema, Nitaondoka, na kuwa pepo wa uongo kinywani mwa manabii wake wote. Akasema, Utamdanganya, na kudiriki pia; ondoka ukafanye hivyo. 23 Basi angalia, Bwana ametia pepo wa uongo kinywani mwa manabii wako hawa wote; naye Bwana amenena mabaya juu yako”.
1Wafalme 22: 20 “Bwana akasema, Ni nani atakayemdanganya Ahabu, ili akwee Ramoth-Gileadi akaanguke? Basi huyu akasema hivi; na huyu hivi.
21 Akatoka pepo, akasimama mbele za Bwana, akasema, MIMI NITAMDANGANYA.
22 Bwana akamwambia, Jinsi gani? Akasema, Nitaondoka, na kuwa pepo wa uongo kinywani mwa manabii wake wote. Akasema, Utamdanganya, na kudiriki pia; ondoka ukafanye hivyo.
23 Basi angalia, Bwana ametia pepo wa uongo kinywani mwa manabii wako hawa wote; naye Bwana amenena mabaya juu yako”.
Mfalme Ahabu akaenda kwenye vita, akiwa amedanganywa na pasipo kujua kuwa amedanganywa…na akafa!
Mfalme huyu naye njia zake hazikumpendeza Mungu..kwani aliwasumbua sana wana wa Israeli , na wakati ule ambao njaa ilipokuwa kubwa Samaria mpaka kufikia kiwango mavi ya njiwa na kichwa cha punda kuuzwa kwa bei kubwa mjini kutokana na njaa iliyosababishwa na mfalme huyu..Na ndiye aliyemdharau Mungu wa Israeli na kusema ni Mungu wa milimani na si wa nchi tambarare. Na japokuwa Mungu aliyanusuru Maisha yake mara nyingi ili atubu…lakini hakuwahi kutubu Zaidi ya yote alizidi kufanya vita na Israeli. Lakini ilifika siku moja akaugua sana, na akatuma watu wamwendee Elisha Nabii ili aulize kwa Mungu kama atapona au la!…Na kilichotokea ni nguvu ya upotevu kuachiliwa juu yake ili auamini Uongo..
Tusome..
2Wafalme 8:7 “Kisha, Elisha akaenda Dameski; na Ben-hadadi, mfalme wa Shamu, alikuwa hawezi; akaambiwa ya kwamba, Yule mtu wa Mungu amefika hapa 8 Mfalme akamwambia Hazaeli, Chukua zawadi mkononi mwako, ukaende ili kumlaki yule mtu wa Mungu, ukamwulize Bwana kwa kinywa chake, kusema, Je! Nitapona ugonjwa huu? 9 Basi Hazaeli akaenda kumlaki, akachukua zawadi mkononi mwake, za kila kitu chema kilichopatikana Dameski, kiasi cha mizigo ya ngamia arobaini, akaenda, akasimama mbele yake akasema, Mwana wako Ben-hadadi, mfalme wa Shamu, amenituma kwako, kusema, Je nitapona ugonjwa huu? 10 Elisha akamwambia, Enenda, ukamwambie, BILA SHAKA UTAPONA; LAKINI BWANA AMENIONYESHA YA KWAMBA BILA SHAKA ATAKUFA. …………..14 Ndipo akamwacha Elisha, akarudi kwa bwana wake; naye akamwambia, Elisha alikuambiaje? Akajibu, Aliniambia ya kuwa BILA SHAKA UTAPONA. 15 Ikawa siku ya pili yake, akatwaa tandiko la kitanda, akalichovya katika maji, akalitandaza juu ya uso wake, HATA AKAFA. Na Hazaeli akatawala badala yake”.
2Wafalme 8:7 “Kisha, Elisha akaenda Dameski; na Ben-hadadi, mfalme wa Shamu, alikuwa hawezi; akaambiwa ya kwamba, Yule mtu wa Mungu amefika hapa
8 Mfalme akamwambia Hazaeli, Chukua zawadi mkononi mwako, ukaende ili kumlaki yule mtu wa Mungu, ukamwulize Bwana kwa kinywa chake, kusema, Je! Nitapona ugonjwa huu?
9 Basi Hazaeli akaenda kumlaki, akachukua zawadi mkononi mwake, za kila kitu chema kilichopatikana Dameski, kiasi cha mizigo ya ngamia arobaini, akaenda, akasimama mbele yake akasema, Mwana wako Ben-hadadi, mfalme wa Shamu, amenituma kwako, kusema, Je nitapona ugonjwa huu?
10 Elisha akamwambia, Enenda, ukamwambie, BILA SHAKA UTAPONA; LAKINI BWANA AMENIONYESHA YA KWAMBA BILA SHAKA ATAKUFA.
…………..14 Ndipo akamwacha Elisha, akarudi kwa bwana wake; naye akamwambia, Elisha alikuambiaje? Akajibu, Aliniambia ya kuwa BILA SHAKA UTAPONA.
15 Ikawa siku ya pili yake, akatwaa tandiko la kitanda, akalichovya katika maji, akalitandaza juu ya uso wake, HATA AKAFA. Na Hazaeli akatawala badala yake”.
Umeona hapo?..Bwana alimwonyesha Elisha kuwa huyo mfalme atakufa lakini alimpa maagizo Elisha amdanganye Ben-hadadi kwamba atapona lakini kumbe atakufa!..
Hiyo ni baadhi ya mifano tu!, ndugu mpendwa saa tunazoishi ni za hatari sana….Tujitahidi sana tuupende na kuufuata ukweli ambao upo katika Neno la Mungu, ili Nguvu hii ya upotevu iliyoachiwa duniani sasa ya kuuamini uongo isije ikatumeza, na ghafla tukajikuta kwenye ziwa la Moto.
Hususani katika kipindi hichi cha siku za Mwisho, uongo umezagaa kila mahali…
Nimewahi kuona muhubiri maarufu akihubiri na kutetea dhambi madhabahuni, hali kadhalika nimeona mwingine akitumia maandiko kabisa kusapoti uvaaji wa suruali na vimini, na kama mtu huyajui maandiko vizuri anakuchukua!..kama ni wa kusoma tu mstari mmoja bila kujua mingine unakwenda na maji! Na maelfu tayari wamechukuliwa!. Hiyo ni mifano tu ya nguvu ya upotevu iliyoachiliwa nyakati hizi ili watu waamini uongo.
2Timotheo 3:13 “lakini watu wabaya na wadanganyaji wataendelea, na kuzidi kuwa waovu, wakidanganya na kudanganyika”.
Tutubu dhambi, na kujitenga na uovu kwa kadiri tuwezavyo..Bwana atusaidie, tukimwamini yeye, tukimtegemea yeye ni mwaminifu, hawezi kutuacha tukadanganyika au kuchukuliwa na hizo nguvu..Hivyo ni wajibu wetu kumpenda Mungu siku zote kwa nguvu zetu zote, kwa roho zetu zote na kwa akili zetu zote.
Bwana atubariki.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
UFALME WAKO UJE.
NGUVU YA MSAMAHA
PARAPANDA ITALIA.
NITAPOKEAJE NGUVU YA KUSHINDA DHAMBI?
Rudi Nyumbani:
Print this post
1 Wathesalonike 5:1 “Lakini, ndugu, kwa habari ya NYAKATI NA MAJIRA, hamna haja niwaandikie. 2 Maana ninyi wenyewe mnajua yakini ya kuwa SIKU YA BWANA yaja kama vile mwivi ajavyo usiku”.
1 Wathesalonike 5:1 “Lakini, ndugu, kwa habari ya NYAKATI NA MAJIRA, hamna haja niwaandikie.
2 Maana ninyi wenyewe mnajua yakini ya kuwa SIKU YA BWANA yaja kama vile mwivi ajavyo usiku”.
Shalom.
Katika mistari hiyo miwili, yapo mambo mawili pia ninataka uyaone. Jambo la kwanza ni “Nyakati na Majira” na Jambo la pili ni “Siku ya Bwana”..Mtume Paulo ameitenganisha hiyo mistari miwili, kwasababu inazungumziwa vitu viwili tofauti,
Kwamfano tukianzana na huo mstari wa Kwanza, unazungumzia Nyakati na Majira ya kurudi kwake Bwana, lakini huo wa pili unazunguzia siku yenyewe ya Bwana itakavyokuwa..
Sasa mpaka mtu anaposema kwa habari ya nyakati na majira sina haja ya kuwaandikia..anamaanisha kuwa suala la majira na nyakati ambayo Kristo atarudi ni jambo ambalo kila mtu anajua, sio siri lipo wazi!, limeshaelezwa kila mahali, sio jambo jipya..na ndio maana hawezi kuandika tena kuwakumbusha watu..
Nataka nikuambie ndugu yangu ikiwa wewe ni mkristo na mpaka sasa bado hujui majira na nyakati za kurudi kwa Yesu duniani kulinyakuwa kanisa lake, basi ujue kuwa kuna tatizo kubwa sana katika Imani yako tena sana ambalo utanatakiwa ulichukulie ‘seriously”…
Biblia imetuweka wazi kabisa na kutuambia tukishaona majira Fulani au nyakati zimebadilika basi tujue ndani ya hicho kipindi siku yoyote Kristo anarudi..Ili kuelewa vizuri tafakari mfano huu,
Leo hii labda unatafuta Kazi mahali fulani, kwenye shirika Fulani la utafiti wa kilimo, halafu ukapata, ukaitwa kwenye interview, ukafanikiwa kupita, lakini wakakwambia kazi yetu rasmi itaanza kipindi cha msimu wa masika, hivyo tutakupigia simu wakati huo ukifika hakikisha tu unakuwa hewani wakati wote, ili tusikukose pindi kazi zitakapoanza. Lakini ukiangalia wewe leo hii upo mwezi wa 9 na umeshajua masika huwa inaanza kuanzia mwezi wa 2-5 mwakani..
Sasa kwa namna ya kawaida hichi kipindi cha katikati utakuwa kawaida tu, lakini itakapofika mwakani kuanzia mwezi huo wa 2 hadi wa 5, utakuwa makini sana, utakuwa karibu na simu yako kwasababu unajua wakati wowote, utapigiwa simu ukaanze kazi,.Unaona hapo! hujapewa tarehe lakini umepewa majira na Nyakati..inaweza ikawa mwezi wa pili mwanzoni, au wa tatu mwishoni, au wa nne katikati hujui..bali utajiweka tayari muda wowote..
Vivyo hivyo na sisi wakristo, tumepewa majira ya kurudi kwa Bwana Yesu, lakini hatujapewa siku, wala saa. Na majira yenyewe ndio haya tunayoyaishi sasa.. Ndugu katika wakati ambao tungepaswa tuwe makini sana na wokovu wetu basi ni katika majira haya.. Kwasababu Bwana Yesu alituambia, mtakapoanza kuona milipuko ya magonjwa yenye mfano wa Tauni yanaipiga dunia (Corona) Luka 21:11 basi mjue yupo mlangoni, mtakapoona matetemeko ya nchi, basi mjue mpo ndani ya wakati huo, mtakapoona wimbi la manabii wa uongo wengi wakizuka duniani, mtakapoona watu wanapenda anasa kuliko kumpenda Mungu, watu wanapenda fedha, basi mjue hayo ndio majira yenyewe.
Mtakapoona maasi yanayongezeka kwa kasi (ushoga na uuajji), upendo wa watu wengi kupoa, kutokea kwa wimbi kubwa la watu wenye kudhihaki wakisema mbona huyo Yesu haji, dunia ipo vilevile wakati wote,(2Petro 3:3) basi tujue tupo katika hayo majira kabisa…
Na ndio pale sasa tukirudi katika ule mstari wa Pili anasema..
2 Maana ninyi wenyewe mnajua yakini ya kuwa SIKU YA BWANA yaja kama vile mwivi ajavyo usiku. 3 Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa.
2 Maana ninyi wenyewe mnajua yakini ya kuwa SIKU YA BWANA yaja kama vile mwivi ajavyo usiku.
3 Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa.
Tukiwa katikati ya majira hayo, ghafula wakati wowote, muda wowote, Bwana atatokea kama mwizi ajavyo usiku.. Kwa bahati mbaya kwa upande wao watasema mbona duniani tupo salama na kuna amani, Hapo ndipo Unyakuo unapita kwa ghafla sana na kwa haraka..wafu wanafufuliwa, na watakatifu wachache sana wanatoweka duniani..
Wakati baadhi ya watu wakipigwa butwaa kufikiri ni nini kimetokea mbona watu wachache hatuwaoni duniani..(wengi watajua ni kawaida watu kupotea potea na kuja kupatikana baada ya siku/miaka kadhaa hivyo watapuuzia) hapo ndipo mpinga-kristo ataanza kufanya kazi..wakati huo dunia haitakuwa na zaidi ya miaka 7, usitamani wakati huo ukukute kwasababu kutakuwa ni vilio na kusaga meno kwa watakaobaki.
Embu jiulize, ni kitu gani kinakufanya uishi maisha ya kubahatisha-bahatisha wakati huu wa siku za mwisho? Neema tuliyonayo haitakuwa hivi sikuzote, upo wakati utatamani ungerudi siku moja nyuma utengeneze mambo yako lakini haitawezekana, wakati huo wenzako wakiwa wanakula karamu ya mwana kondoo mbinguni wewe utakuwa umebaki halafu kibaya zaidi uliujua ukweli lakini hukuukubali kwa wakati.
Ndugu tubu dhambi zako, mgeukie mkuu wa uzima YESU KRISTO, azifute dhambi zako..Achana na mambo ya ulimwengu hayakufikishi popote, wala hayakupi faida yoyote wewe mwenyewe unajua. Hivyo fanya uamuzi mwema wa kugeuka na kumfuata Yesu ili uwe na amani katika kipindi cha maisha yako ulichobakiwa nacho hapa duniani.
Ni matumaini yangu utafanya hivyo. Na Kristo awe pamoja na wewe, na pamoja na sisi sote.
Maran Atha.
SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?
Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita..
MKUMBUKE MKE WA LUTU.
CHUKIZO LA UHARIBIFU
MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.
Waebrania 12:14 “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao”.
Ni agizo la Mungu kwamba tuwe na amani na watu wote..Ukijiona una shari na mtu au watu basi kuna tatizo mahali…Sio kila jambo ni la kupambana nalo, na njia ya kupambana na moto ni kuuzima na si kujitosa ndani ya moto. Hivyo tunapoudhiwa si wakati wa sisi kulipiza kisasi, ni wakati wa kuyazima hayo maudhi, kwa hekima na upole.Na mara nyingi kitu kinachowasha moto katika miasha yetu ni ULIMI.
Yakobo 3:5 “Vivyo hivyo ulimi nao ni kiungo kidogo, nao hujivuna majivuno makuu. Angalieni jinsi moto mdogo uwashavyo msitu mkubwa sana. 6 Nao ULIMI NI MOTO; ule ulimwengu wa uovu, ule ulimi, umewekwa katika viungo vyetu, nao ndio uutiao mwili wote unajisi, huuwasha moto mfulizo wa maumbile, nao huwashwa moto na jehanum”
Yakobo 3:5 “Vivyo hivyo ulimi nao ni kiungo kidogo, nao hujivuna majivuno makuu. Angalieni jinsi moto mdogo uwashavyo msitu mkubwa sana.
6 Nao ULIMI NI MOTO; ule ulimwengu wa uovu, ule ulimi, umewekwa katika viungo vyetu, nao ndio uutiao mwili wote unajisi, huuwasha moto mfulizo wa maumbile, nao huwashwa moto na jehanum”
Unaona hapo? Biblia inasema pia ukiweza kuuzuia ulimi wako hata SIKU YAKO ITAKUWA NJEMA…na ndivyo utakavyopata amani..
1Petro 3:10 “Kwa maana, Atakaye kupenda maisha, Na kuona siku njema, Auzuie ulimi wake usinene mabaya, Na midomo yake isiseme hila. 11 Na aache mabaya, atende mema; ATAFUTE AMANI, aifuate sana”
1Petro 3:10 “Kwa maana, Atakaye kupenda maisha, Na kuona siku njema, Auzuie ulimi wake usinene mabaya, Na midomo yake isiseme hila.
11 Na aache mabaya, atende mema; ATAFUTE AMANI, aifuate sana”
Hivyo mara zote tukijifunza kukaa kimya na kuwa wapole na wenye busara…basi ni lazima tu tutakuwa na amani na watu wote….Sisemi kwamba hautakuwa na watu wanaokuchukia kabisa,…hapana watu wanaokuchukia watakuwepo tu! lakini hawatakuwa na la kufanya kwako kwasababu muda wote watakuona ni mtu wa amani. Watatafuta maneno kwako lakini hawatayapata…hivyo mwisho wa siku wataachana na wewe, na kuendelea kufikiri mambo yao mengine.
Lakini ukiwa ni mtu wa kujibiza, kamwe vita kwako havitaisha..na hakuna siku utapata amani…kama mtu akikuudhi wewe nawe unajibu mashambulizi kwa kumrudishia maneno…nataka nikuambia hakuna siku utakuwa na amani, utakuwa ni mtu wa kugombana tu kila siku, na wa kukosa raha, na muda mwingine kuweka vinyongo tu…na pasipo kujua kuwa tatizo kubwa lipo upande wako.
Mithali 15:1 “Jawabu la upole hugeuza hasira; Bali neno liumizalo huchochea ghadhabu”.
Kila mahali jaribu kuwa mpole…hiyo ndiyo njia ya kupata Amani na watu wote…Na kuwa mpole sio “udhaifu”….Bwana wetu Yesu alikuwa ni mpole(Mathayo 11:28) na mtu mpole mara nyingi sio mtu wa kuzungumza sana, na sio mtu wa kuzungumza mambo ya wengine (msengenyaji).
Wafilipi 4:5 “Upole wenu na ujulikane na watu wote. Bwana yu karibu”.
Sisi kama wakristo tukiudhiwa kwa maneno sio lazima tujibu neno,.. ukiumizwa hupaswi na wewe kumuumiza..kila wakati tafuta namna ya kulitatua tatizo badala ya kulichochea…na kwa jinsi utakavyoonesha bidii ndivyo Mungu atakavyozidi kukupatanisha na wale ambao wanaonekana ni maadui zako wa kudumu..Na hivyo utazidi kuwa na amani.
Mithali 16:7 “Njia za mtu zikimpendeza Bwana, Hata adui zake huwapatanisha naye”.
Hivyo Bwana anavyotuambia tutafute kwa bidii (maana yake tufanye kila tuwezalo) tuwe na amani na kila mtu, kama vile tunavyofanya bidii kuutafuta utakatifu ambao hakuna atakayemwona Mungu asipokuwa nao.
KAMA UNAPENDA MAISHA, NA KUTAKA SIKU YAKO IWE NJEMA.
NI NINI TUNAJIFUNZA JUU YA MT. DENIS WA UFARANSA?
Mtu astahiliye hofu ni yupi?
FAHAMU ZA WATU HUWA ZINAONDOLEWA NA NINI?
DANIELI: Mlango wa 9
UPENDO NI NINI NA JE! KUNA AINA NGAPI ZA UPENDO?
Kwanini biblia inasema mtu wa rohoni huyatambua yote?
Ukisoma katika biblia utakuta kuna mahali Bwana alikuwa anasema maneno haya…
1Wafalme 16: 25 “Omri akafanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana, akatenda maovu kuliko wote waliomtangulia”
1Wafalme 16: 30 “Ahabu mwana wa Omri akafanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana kuliko wote waliomtangulia”.
Utaona hapo huyo Mfalme aliyeitwa Omri alifanya machukizo makubwa kuliko baba zake waliomtangulia…na anakuja kupata mtoto anayeitwa Ahabu na huyo mtoto anafanya naye mabaya kuliko yeye na wote waliomtangulia…Maana yake ni kwamba hali ya mtoto inakuwa ni mbaya kuliko ya mzazi, na ya mjukuu ni mbaya kuliko ya Baba na babu.
Sasa unaweza kujiuliza ni kwanini Bwana aweke hilo neno “ naye akafanya mabaya kuliko wote waliomtangulia”?..Jibu ni kwasababu matendo yetu yanapimwa yakilinganishwa na ya waliotutangulia..
Kama baba kaua mtu mmoja, na mtoto wake akaua wawili…basi maasi ya mtoto yamezidi yale ya Baba mara mbili…yaani kama yangewekwa katika mizani basi mzigo wa mtoto ni mkubwa kuliko wa Baba.
Kadhalika kama mtoto kafanya mema kuliko baba yake basi matendo yake kama yakiwekwa katika mizani yataonekana yamezidi ya Baba yake…na kama Baba yake amefanya mema kuliko yeye basi matendo ya Baba yake katika mizani ya kimbinguni ni mazito kuliko ya mtoto, na hivyo ya mtoto yataonekana yamepunguka…
Ndicho kilichomtokea Mfalme Belshaza wa Babeli…Mfalme huyu ijapokuwa alikuwa anayajua matendo ambayo Mungu wa Israeli alimfanyia Baba yake…lakini bado matendo yake yalikuwa maovu kuliko baba yake…Na mema yake yalionekana ni pungufu kuliko mema ya Baba yake katika mizani ya kimbinguni. Kwani Baba yake alimheshimu Mungu lakini yeye hakumweshimu na kwenda kuvichukua vyombo vitakatifu na kuvitumia kwa karamu zake za kiasherati.
Na Bwana akamwambia maneno haya..
Danieli 5:27 “TEKELI, umepimwa katika mizani nawe umeonekana kuwa umepunguka”.
Maana yake ni kwamba matendo mema aliyoyafanya baba yake yamezidi ya kwake…Bwana Mungu alitegemea matendo ambayo angeyafanya yazidi ya baba yake lakini kinyume chake yamepungua, na hivyo akamhukumu.
Biblia inasema….
2 Samweli 2:3 “Msizidi kunena kwa kutakabari hivyo; Majivuno yasitoke vinywani mwenu; Kwa kuwa Bwana ni Mungu wa maarifa, NA MATENDO HUPIMWA NA YEYE KWA MIZANI”.
Ndugu matendo yetu yanapimwa katika mizani kila siku yakilinganishwa na ya wengine kama sisi…kizazi chetu kinapimwa katika mizani kikilinganishwa na vizaza vilivyotangulia..
Mathayo 12:41 “Watu wa Ninawi watasimama siku ya hukumu pamoja na watu wa kizazi hiki, nao watawahukumu kuwa wamekosa; kwa sababu wao walitubu kwa mahubiri ya Yona; na hapa yupo aliye mkuu kuliko Yona”.
Mahali tunapoishi, tunapofanyia kazi tunapimwa…kila tunalolifanya linapimwa linalinganishwa na la wengine. Hata maisha tunayoishi sisi kama wakristo yanapimwa ndio maana Bwana Yesu alisema..
Mathayo 5:20 “Maana nawaambia ya kwamba, Haki yenu isipozidi hiyo haki ya waandishi na Mafarisayo, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni”.
Unapovaa suruali binti wa Mungu ambaye umezaliwa katika mazingira ya kikristo, pengine hata baba yako ni mchungaji…na unasema unakwenda mbinguni…ukumbuke kuna mwingine kama wewe mwenye umri kama wa kwako mahali fulani ambaye ni mzuri kuliko wewe na mwenye umbo zuri kuliko lako lakini havai hizo suruali wala vimini, ingawa mazingira yote yanamruhusu kufanya hivyo…yeye ameshinda katika mazingira magumu ya vishawishi vingi lakini wewe umeshindwa katika mazingira marahisi..Jua upendo wako kwa Mungu unapimwa!.
Unaposhindwa kumtafuta Mungu kwa kazi yako unayofanya masaa 8 tu kwa siku, na kusema upo bize sana…kumbuka kuna mwingine aliye bize kuliko wewe mwenye kufanya kazi masaa 10 mahali pengine lakini hakosi ibada, wala hakosi muda wa kusali na kuomba na kusoma Neno…ingawa anachoka kulko wewe…Fahamu kuwa upendo wako unapimwa!
Hivyo ndugu huu ni wakati wa kujipima kabla ya kupimwa!…na kujitathimini upya…
Kumbuka siku zote, usilisahau hili Neno utembeapo, uishipo…matendo yako yanapimwa katika mizani.
Ayubu 31: 5 “Kwamba nimetembea katika ubatili, Na mguu wangu umeukimbilia udanganyifu; 6 (Na nipimwe katika mizani iliyo sawasawa, Ili Mungu aujue uelekevu wangu);
Ayubu 31: 5 “Kwamba nimetembea katika ubatili, Na mguu wangu umeukimbilia udanganyifu;
6 (Na nipimwe katika mizani iliyo sawasawa, Ili Mungu aujue uelekevu wangu);
Bwana atubariki
Je! Mwanamke anapaswa afunikwe kichwa anapokuwa ibadani?
KISIMA CHA MAJI YA UZIMA NI KILE KILE CHA ZAMANI.
NINI TUNAJIFUNZA KWA MWANA MPOTEVU NA NDUGUYE?
ZIKIMBIE TAMAA ZA UJANANI! NA MTU YEYOTE ASIUDHARAU UJANA WAKO.
WhatsApp
Kuna hatua unafika Mungu anahitaji umuangilie sana yeye kuliko kujiangalia nafsi yako ili uweze kusonga mbele katika kumtumikia. Lipo tatizo kubwa ambalo lilishawahi kunikumba mimi, siku za mwanzoni nilipookoka, na naamini linawakumbuka watu wengi hata sasa waliookoka, Jambo hilo mtume Paulo alishaliona na kulitolea ufumbuzi wake kwa ufunuo wa Roho..
Kuna wakati unafika, unaona kila jambo unaloweza kujaribu kulifanya unaona pengine linaweza likawa linamkosea Mungu, au kama umefanya dhambi fulani ukatubu, unaona kama vile Mungu hajakusamehe vizuri, au amekukakasirikia, na hiyo inakufanya ujilaumu muda mwingi, Unajihukumu na kuhitimisha kuwa Mungu hawezi kuwa na mimi tena, Mungu hawezi kunitumia, Mungu ananiona mimi ni mchafu sana, Nimeuhuzunisha moyo wake sana hivyo ameshakata tamaa na mimi..
Paulo alisema hivi..
1 Wakorintho 4:1 “ Mtu na atuhesabu hivi, kuwa tu watumishi wa Kristo, na mawakili wa siri za Mungu. 2 Hapo tena inayohitajiwa katika mawakili, ndiyo mtu aonekane kuwa mwaminifu. 3 LAKINI, KWANGU MIMI, SI KITU KABISA NIHUKUMIWE NA NINYI, WALA KWA HUKUMU YA KIBINADAMU, WALA SIJIHUKUMU HATA NAFSI YANGU. 4 MAANA SIJUI SABABU YA KUJISHITAKI NAFSI YANGU, lakini sihesabiwi haki kwa ajili hiyo; ila anihukumuye mimi ni Bwana. 5 Basi ninyi msihukumu neno kabla ya wakati wake, hata ajapo Bwana; ambaye atayamulikisha yaliyositirika ya giza, na kuyadhihirisha mashauri ya mioyo; ndipo kila mtu atakapoipata sifa yake kwa Mungu”.
1 Wakorintho 4:1 “ Mtu na atuhesabu hivi, kuwa tu watumishi wa Kristo, na mawakili wa siri za Mungu.
2 Hapo tena inayohitajiwa katika mawakili, ndiyo mtu aonekane kuwa mwaminifu.
3 LAKINI, KWANGU MIMI, SI KITU KABISA NIHUKUMIWE NA NINYI, WALA KWA HUKUMU YA KIBINADAMU, WALA SIJIHUKUMU HATA NAFSI YANGU.
4 MAANA SIJUI SABABU YA KUJISHITAKI NAFSI YANGU, lakini sihesabiwi haki kwa ajili hiyo; ila anihukumuye mimi ni Bwana.
5 Basi ninyi msihukumu neno kabla ya wakati wake, hata ajapo Bwana; ambaye atayamulikisha yaliyositirika ya giza, na kuyadhihirisha mashauri ya mioyo; ndipo kila mtu atakapoipata sifa yake kwa Mungu”.
Kama tunavyojua Paulo ni mtu ambaye mawazo yake yote yalielekea kwa Mungu sana, alikuwa anajitahidi kwa kadiri awezavyo kumpendeza Mungu lakini pengine katika Nyanja fulani za Maisha yake ya huduma alishawahi kufanya makosa kadha wa kadha, au alishawahi kushindwa kufanikisha hiki au kile kwa ajili ya Mungu, kiasi kwamba hata yeye mwenyewe au watu wengine wangemwona kama ameshindwa kabisa, lakini hapa anasema..
“Lakini, kwangu mimi, si kitu kabisa nihukumiwe na ninyi, wala kwa hukumu ya kibinadamu, wala sijihukumu hata nafsi yangu. 4 Maana sijui sababu ya kujishitaki nafsi yangu”
“Lakini, kwangu mimi, si kitu kabisa nihukumiwe na ninyi, wala kwa hukumu ya kibinadamu, wala sijihukumu hata nafsi yangu.
4 Maana sijui sababu ya kujishitaki nafsi yangu”
Unaona madhaifu yake hayakuwa sababu ya yeye kujihukumu kuwa anafaa au hafai mbele za Mungu, japokuwa hilo halimthibitishii kuwa anafaa, lakini hakuruhusu ajihukumu kwasababu haoni sababu kwanini afanya vile, Pengine aliwaza Mungu hakuwahi kumwambia kuwa hampendi, Au Mungu hakuwahi kumuonyesha katika maono kuwa hamtaki tena? Kama sivyo, ni kwanini ajihukumu mwenyewe?
Hivyo Paulo aliamua kuendelea kuishi Maisha ya kumtegemea Kristo kuliko kuutegemea ukamilifu wake wote umsaidie katika huduma yake, na hiyo ilimfanya afike mbali, japokuwa alikutana na milima na mabonde,
Lakini kumbuka jambo kama hili halimuhusu mtu anayefanya dhambi za makusudi. Wewe kama mzinzi, Maisha yako yapo mbali na wokovu unafanya dhambi kwa makusudi, ndani yako hakuna hofu yoyote ya Mungu, ujue kuwa hata kama hutajihukumu, basi dhamira yako itakushuhudia ndani yako kuwa kuwa wewe ni mnafki na mwovu. Na utahukumiwa siku za mwisho…Na kumbuka mojawapo ya dhambi za makusudi kabisa, zisizo za madhaifu, ni dhambi ya uzinzi na uasherati. Mtu anayefanya uasherati baada ya kuokoka anafanya dhambi ya makusudi inayostahili hukumu. Hivyo kama unaifanya ndugu iache mara moja.
Lakini ikiwa upo ndani ya Kristo, na una kiu kweli ya kuzidi kumpendeza Mungu na unajitahidi kujizuia kwa kila kitu kiovu, basi kataa hukumu yoyote inayokuja ndani ya moyo wako inayokuambia wewe hufai, kataa mawazo yote yanayokuambia unachofanya kwa Mungu hakimpendezi hata kidogo, kataa hayo mawazo yanayokuambia Mungu hana mpango wa wewe, yakija yaulize mbona Mungu hajawahi kuniambia hilo jambo?. Endelea kumtumikia Mungu kwa karama aliyoiweka ndani yako..
Ikiwa ulifanya makosa Fulani madogo, basi rekekebisha makosa yako, kisha endelea kusonga mbele, mtazame Kristo, na yeye atakuwa na wewe siku baada ya siku, Vilevile usikubali hukumu kutoka kwa mtu yeyote ikutaabishe moyo,..yupo mtu anaweza kukuambia wewe bado hujaitwa na Mungu kwa kutazama maisha uliyokuwa unaishi huko nyuma?…na akakwambia Mungu hawezi kukutumia mtu kama wewe, muulize mbona Mungu hajawahi kunisemesha mambo kama hayo? Wengine wanaweza kukutamkia maneno ya laana hata kama yataonekana yana ukweli ndani yake lakini wewe yakatae matazame Kristo, endelea na safari…
JE! NI LAZIMA WATU WOTE WANENE KWA LUGHA?
Je! Ni kweli ubatizo wa maji hatuuhitaji tena?
JE KUNA UISLAMU KATIKA BIBLIA?
Ni uthibitisho upi unaoonyesha kuwa kuna MBINGUNI na KUZIMU?
Je ni kweli mtu akifa anakuwa hana dhambi tena kufuatia hili andiko Warumi 6:7 “kwa kuwa yeye aliyekufa amehesabiwa haki mbali na dhambi.”
JIBU: Bwana Yesu alisema haya maneno mahali Fulani…
Yohana 8:21 “Basi akawaambia tena, Mimi naondoka, nanyi mtanitafuta; nanyi MTAKUFA KATIKA DHAMBI yenu; mimi niendako ninyi hamwezi kuja……… 24 Kwa hiyo naliwaambieni ya kwamba MTAKUFA KATIKA DHAMBI ZENU; kwa sababu msiposadiki ya kuwa mimi ndiye, MTAKUFA KATIKA DHAMBI ZENU”.
Yohana 8:21 “Basi akawaambia tena, Mimi naondoka, nanyi mtanitafuta; nanyi MTAKUFA KATIKA DHAMBI yenu; mimi niendako ninyi hamwezi kuja………
24 Kwa hiyo naliwaambieni ya kwamba MTAKUFA KATIKA DHAMBI ZENU; kwa sababu msiposadiki ya kuwa mimi ndiye, MTAKUFA KATIKA DHAMBI ZENU”.
Bwana Yesu aliwaambia Waandishi na Mafarisayo maneno hayo..kuonyesha kuwa Kama mtu akikataa kutubu dhambi angali hai na kumwamini basi atakufa na hizo dhambi zake (maana yake hizo dhambi zake zitamfuata hata huko anakokwenda, na atahukumiwa kulingana na hizo).
Hilo utalithibitisha katika andiko hili..
1Timotheo 5:24 “Dhambi za watu wengine zi dhahiri, zatangulia kwenda hukumuni; wengine dhambi zao zawafuata”.
Kwasababu hiyo basi mstari huo wa Warumi 6:7, haumaanishi kuwa mtu mwenye dhambi anapokufa basi anakuwa hana dhambi tena…bali unamaanisha kuwa mtu “yeye aliyekufa Pamoja na Kristo, amehesabiwa haki mbali na dhambi”…Maana yake mtu aliye ndani ya Kristo hakuna hukumu ya adhabu juu yake kwasababu anakuwa amevuka kutoka mautini kuingia uzimani, ingawa bado anaishi ulimwenguni.
Ndio maana ukianzia mstari wa 6 na kuendelea kidogo mpaka wa 8 utaelewa vizuri..anasema..
Warumi 6: 6 “mkijua neno hili, ya kuwa utu wetu wa kale ulisulibishwa pamoja naye, ili mwili wa dhambi ubatilike, tusitumikie dhambi tena; 7 kwa kuwa yeye aliyekufa amehesabiwa haki mbali na dhambi. 8 Lakini tukiwa tulikufa pamoja na Kristo, twaamini ya kuwa tutaishi pamoja naye”
Warumi 6: 6 “mkijua neno hili, ya kuwa utu wetu wa kale ulisulibishwa pamoja naye, ili mwili wa dhambi ubatilike, tusitumikie dhambi tena;
7 kwa kuwa yeye aliyekufa amehesabiwa haki mbali na dhambi.
8 Lakini tukiwa tulikufa pamoja na Kristo, twaamini ya kuwa tutaishi pamoja naye”
Hivyo andiko hilo linatuhusu sisi sote…Hatuna budi kufa Pamoja na Kristo, kila mmoja wetu kwa kumwamini yeye na kutubu dhambi na kufufuka Pamoja naye kwa njia ya ubatizo wa maji na wa Roho Mtakatifu.
Warumi 6:3 “Hamfahamu ya kuwa sisi sote tuliobatizwa katika Kristo Yesu tulibatizwa katika mauti yake? 4 Basi tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika mauti yake, kusudi kama Kristo alivyofufuka katika wafu kwa njia ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo na sisi tuenende katika upya wa uzima”
Warumi 6:3 “Hamfahamu ya kuwa sisi sote tuliobatizwa katika Kristo Yesu tulibatizwa katika mauti yake?
4 Basi tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika mauti yake, kusudi kama Kristo alivyofufuka katika wafu kwa njia ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo na sisi tuenende katika upya wa uzima”
ROHO YA MPINGA KRISTO IKITENDA KAZI SIKU HIZI ZA MWISHO
USIFE NA DHAMBI ZAKO!
TUMAINI NI NINI?
NAMI NINAZO FUNGUO ZA MAUTI, NA ZA KUZIMU.
Wokovu huu ambao tumeupata bure, tusidhani yule aliyetugawia hakuingia gharama yoyote kuupata,..Halikuwa ni jambo la kukaa mbinguni tu na kusema niamnini mimi mtaokoka!..Hilo lisingewezekana kamwe, ili kuunda kitu kinachoitwa “wokovu” ilimpasa afuate kanuni Fulani..ilimpasa kwanza aache enzi na mamlaka yote mbinguni, awe hana kitu, kisha ashuke hapa duniani, aishi kama mwanadamu mwingine yoyote yule aliyezaliwa na mwanamke, aumwe wakati mwingine, audhiwe, apitie umaskini, kisha na yeye pia ajaribiwe na shetani, aonekane kama atashinda au la, ..Lakini kama tunavyosoma aliyashida yote kwa muda wa miaka 33 bila kutenda dhambi yoyote licha ya kupitia vipingamizi vyote vya kibinadamu..
Lakini sio hilo tu, ilimgharimu uhai pia, ili aweze sasa kukikamilisha hicho kitu kinachoitwa WOKOVU KWA MWANADAMU.. Ndio hapo akalazimika aende msalaba akapigwe afe, damu imwagike ili kusudi kwamba mimi na wewe tupokee huo wokovu kwa gharama alizoingia..
Lakini wengi wetu tunadhani mateso aliyoyapita yalikuwa ni ya kawaida tu, biblia inatuambia Bwana aliharibiwa uso wake, na mwili wake, Zaidi ya mwanadamu mwingine aliyewahi kuishi hapa duniani..
Soma..
Isaya 52:13 “Tazama, mtumishi wangu atatenda kwa busara, atatukuzwa, na kuinuliwa juu, naye atakuwa juu sana. 14 Kama vile wengi walivyokustaajabia, (USO WAKE ULIKUWA UMEHARIBIWA SANA ZAIDI YA MTU YE YOTE, NA UMBO LAKE ZAIDI YA WANADAMU), 15 ndivyo atakavyowasitusha mataifa mengi; wafalme watamfumbia vinywa vyao; maana mambo wasiyoambiwa watayaona; na mambo wasiyoyasikia watayafahamu”.
Isaya 52:13 “Tazama, mtumishi wangu atatenda kwa busara, atatukuzwa, na kuinuliwa juu, naye atakuwa juu sana.
14 Kama vile wengi walivyokustaajabia, (USO WAKE ULIKUWA UMEHARIBIWA SANA ZAIDI YA MTU YE YOTE, NA UMBO LAKE ZAIDI YA WANADAMU),
15 ndivyo atakavyowasitusha mataifa mengi; wafalme watamfumbia vinywa vyao; maana mambo wasiyoambiwa watayaona; na mambo wasiyoyasikia watayafahamu”.
Jaribu kuchua muda utafakari!, chukua muda utafakari hata dakika 15 au 20, fikiria huo uso uliwezekanikaje kuharibiwa Zaidi ya mtu yoyote hapa duniani, na mwili wake vivyo hivyo, ndipo utakapofahamu kuwa mapigo aliyopigwa Bwana hayakuwa ya mwanadamu wa kawaida, alikuwa kama nyama buchani, kile unachokifahamu kwenye filamu ni mfano mdogo wa jinsi Bwana alivyokuwa anaonekana, na hiyo yote ilimpasa apitie vinginevyo mimi na wewe tusingeupata wokovu..
biblia inasema..
“Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, NA KWA KUPIGWA KWAKE SISI TUMEPONA”.(Isaya 53:5)
Uso wake na mwili wake usingeharibiwa kwa mapigo mabaya kama yale ambayo mengine hata hayajaandikwa kwenye biblia, mimi na wewe leo hii tusingeufikia uponyaji wa roho zetu. Lakini jiulize wewe ndugu ambaye bado hujamwamini yeye licha ya kwamba umekusogezea wokovu huo bure mbele yako bila malipo yoyote..Jiulize, siku ya leo ukifa katika hali yako ya dhambi utawezaje kuokoka?
Kumbuka wokovu unapatikana bure, sasa bila gharama yoyote, usisubiri mpaka mlango wa neema ufungwe ndipo uje uutafute, hilo halitawezekana tena, wakati huo ukifika wewe utakuwa ni wa kusubiria tu kwenda jehanamu ya moto, lakini leo hii ukiyasalimisha Maisha yako kwake, licha tu ya kwamba unayo tiketi ya kwenda mbinguni, lakini pia ile damu yake ya thamani iliyomwagika pale msalabani wakati huo huo itaanza kukunenea mema juu ya Maisha yako angali ukiwa bado hapa duniani.
Hivyo tubu ndugu kama bado hujafanya hivyo..maadamu Bwana Yesu ni Rafiki yetu wa kweli, anayetupenda upeo.
Jina lake libarikiwe daima.
YATAFUTE YALIYO JUU SIKU ZOTE.
Kwanini Mungu alisema hakuna mtu awazaye kuuona uso wake akaishi?
KIFO CHA REINHARD BONKEY KINAACHA UJUMBE GANI KWETU?
NI KITU GANI PETRO NA YOHANA WALIKIGUNDUA KABURINI?
KANUNI RAHISI YA KUFANIKIWA.
Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!
JIBU: Vipo vyeo vitatu maalumu ambavyo vilimtambulisha Bwana Yesu Kristo…1) Mwana wa Mungu 2) Mwana wa Adamu 3) Mwana wa Daudi. Vyeo hivi kila kimoja kina maana yake..
Sasa kabla ya kuendelea mbele zaidi…ni muhimu kufahamu kuwa cheo cha “Mwana” ni cheo cha “urithi”…Maana yake ni kwamba mfano ukiwa na mtoto wako mmoja wa pekee huyo atarithi kila ulicho nacho…ikiwemo enzi yako yote, mali zako pamoja na hata jina lako…
Sasa katika biblia..mahali popote ambapo Neno Mwana linaanza kwa herufi kubwa…hilo linamzungumzia mtu mmoja tu maalumu ambaye ni Yesu Kristo…lakini ukiona neno “mwana” limeanza kwa herufi ndogo kama hivyo, basi fahamu ni mtu mwingine tofauti na Yesu anayezungumziwa hapo.. Kwa mantiki hiyo basi “wana wa Mungu” wapo wengi lakini “Mwana wa Mungu ni mmoja tu”…mimi na wewe tuliompokea Yesu ni wana wa Mungu….kadhalika wana wa Daudi wapo wengi..lakini “Mwana wa Daudi” ni mmoja tu ambaye ni Yesu…Sulemani alikuwa pia ni ‘mwana wa Daudi’, Hezekia, Yosia, Manase wote hao walikuwa ni wana wa Daudi….Hali kadhalika pia “wana wa Adamu wapo wengi”…mimi ni mwana wa Adamu(au kwa kifupi Mwanadamu)..wewe ni mwana wa Adamu lakini “Mwana wa Adamu” yupo mmoja tu ambaye ni Yesu…ni kama vile miungu wapo wengi lakini Mungu ni mmoja tu!.
Sasa tukirudi kwenye shabaha yetu ya msingi, ambapo tumeona kuwa Neno ‘mwana’ linazungumzia ‘urithi’
Hivyo basi vyeo hivyo vitatu tunaweza kuviweka katika mnyumbuliko ufuatao…1)Mrithi wa Mungu 2) Mrithi wa Adamu na 3) Mrithi wa Daudi.
Sasa unaweza kujiuliza Kristo alirithi nini kutoka kwa hawa watatu?
Kama mtu ataitwa Mwana wa Mungu maana yake ni kwamba ni Mrithi wa enzi yote ya Mungu na Ukuu …na huyo si mwingine zaidi ya Yesu Kristo, ambaye alirithishwa vyote.
Waebrania 1:1 “Mungu, ambaye alisema zamani na baba zetu katika manabii kwa sehemu nyingi na kwa njia nyingi, 2 mwisho wa siku hizi amesema na sisi katika MWANA, ALIYEMWEKA KUWA MRITHI WA YOTE, TENA KWA YEYE ALIUFANYA ULIMWENGU. 3 Yeye kwa kuwa ni mng’ao wa utukufu wake na chapa ya nafsi yake, akivichukua vyote kwa amri ya uweza wake, akiisha kufanya utakaso wa dhambi, aliketi mkono wa kuume wa Ukuu huko juu”
Waebrania 1:1 “Mungu, ambaye alisema zamani na baba zetu katika manabii kwa sehemu nyingi na kwa njia nyingi,
2 mwisho wa siku hizi amesema na sisi katika MWANA, ALIYEMWEKA KUWA MRITHI WA YOTE, TENA KWA YEYE ALIUFANYA ULIMWENGU.
3 Yeye kwa kuwa ni mng’ao wa utukufu wake na chapa ya nafsi yake, akivichukua vyote kwa amri ya uweza wake, akiisha kufanya utakaso wa dhambi, aliketi mkono wa kuume wa Ukuu huko juu”
Kwahiyo hiyo ndio sababu ya Kristo kujulikana kama MWANA WA MUNGU..Ni kwasababu amerithi milki zote za Mungu..
Mathayo 28:18 “Yesu akaja kwao, akasema nao, akawaambia, Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani”.
Cheo cha pili ni cheo cha MWANA WA DAUDI/Mrithi wa Daudi..Sasa ili kujua ni kwanini Kristo aliitwa mwana wa Daudi ni vizuri kumjua kwanza Daudi alikuwa ni nani…(kwa maelezo marefu unaweza kututumia ujumbe inbox tutakutumia somo lake)…lakini kwa ufupi ni kwamba Daudi alikuwa ni mfalme pekee aliyepata Hekima ya kufikiria kumjengea Mungu nyumba ya kifalme katika wa Yerusalemu…na hivyo kumfanya Mungu kuuchagua ule mji kuwa makao makuu yake ya kifalme Duniani (yaani Yerusalemu).
Kama sio Daudi basi mpaka leo pengine Mungu asingekuwa na mji wake maalumu duniani kati ya miji ya Israeli…(Tusingelisikia hili neno Yerusalemu au Sayuni likirudiwa rudiwa katika maandiko, kwani ungekuwa mji kama miji mingine tu, wala ile Yerusalemu mpya kwenye ufunuo pengine ingeitwa kwa jina lingine)…
Lakini Daudi ndiye aliyefanya Yerusalemu ikawa mji wa kifalme wa mwokozi..na Mungu alimwahidi hatakosa mtu wa kukaa katika kiti cha kifalme kutoka katika uzao wake…na katika uzao wake huo yupo mmoja ambaye ni mkuu sana alitabiriwa kutokea huko na huyo si mwingine zaidi ya YESU KRISTO mwenyewe(kasome Mathayo 1:1-17) ambaye atakuwa mfalme juu ya Dunia nzima! Na ndiye atakayeijenga Yerusalemu mpya ile itakayoshuka kutoka mbinguni…na kukaa na watu wake. Na ndio maana Kristo ilimpasa aitwe mwana wa Daudi kufuatana na yale Daudi aliyoyafanya na kukabidhiwa.
Na cheo cha Mwisho cha Yesu Kristo ni cheo cha MWANA WA ADAMU au Mwana wa mtu,…sasa kama tunavyomjua Adamu alikuwa ni mtu wa kwanza kuumbwa na kupewa Urithi wote na mamlaka yote duniani, kwamba atawale kila kitu, na kwamba viumbe vyote vitamwogopa!….lakini kama tunavyojua aliuuza na kuupoteza ule urithi wake aliopewa na Mungu kwa adui shetani…Hivyo ili urithi huo umrudie tena mwanadamu..basi hakuna budi aje kutokea Adamu mwingine wa pili, ambaye atakaribiana sana kufanana na Yule Adamu wa kwanza,…ambaye ataurithi ule urithi na enzi yote aliyopewa Adamu ya kwanza…
1Wakorintho 15:45 “Ndivyo ilivyoandikwa, Mtu wa kwanza, Adamu, akawa nafsi iliyo hai; Adamu wa mwisho ni roho yenye kuhuisha”.
Adamu wa pili atakuwa ni mwanamume kama Yule wa kwanza, naye atapewa mamlaka kama Yule wa Kwanza wa pale Edeni, na yeye ni lazima awe wa kwanza kuumbwa …na huyo si mwingine zaidi ya Yesu Kristo..ambaye ndiye limbuko letu rohoni na ndiye aliyekabidhiwa mamlaka yote ya duniani. Hiyo ndiyo sababu Yesu anaitwa Mwana wa Adamu…ni kwasababu amerithi mamlaka yote na enzi yote Yule Adamu wa kwanza aliyokuwa nayo (aliyopewa na Mungu)..
Mathayo 11:27 “Akasema, Nimekabidhiwa vyote na baba yangu; wala hakuna amjuaye Mwana, ila Baba; wala hakuna amjuaye Baba, ila Mwana, na ye yote ambaye Mwana apenda kumfunulia”.
Hivyo Yesu Kristo ndiye Mwanzo na Mwisho, Alfa na Omega…Ndiye mwanadamu kamili, ndiye aliye na mamlaka yote sasa, ndiye mwenye enzi ya kifalme, ndiye Mungu mwenyewe katika mwili. Na ndiye njia ya kufika mbinguni…Kama hujamwamini wala kumpokea…ni vyema ukafanya hivyo kwasababu hakuna njia nyingine yoyote unaweza kumfikia Mungu kama isipokuwa kwa kupitia yeye..
Ufunuo 22:12 “Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo. 13 MIMI NI ALFA NA OMEGA, MWANZO NA MWISHO, WA KWANZA NA WA MWISHO. 14 Heri wazifuao nguo zao, wawe na amri kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake”.
Ufunuo 22:12 “Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo.
13 MIMI NI ALFA NA OMEGA, MWANZO NA MWISHO, WA KWANZA NA WA MWISHO.
14 Heri wazifuao nguo zao, wawe na amri kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake”.
Bwana atubariki. Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
KWANINI YESU KRISTO NI WA MUHIMU KWETU SASA?
USIPOKUWA MWAMINIFU, NAFASI YAKO ITACHUKULIWA.
TAZAMA, MWISRAELI KWELI KWELI, HAMNA HILA NDANI YAKE!
Kuna ufufuo wa aina ngapi?
MAJESHI YA PEPO WABAYA.
Shalom,
Nakukaribisha tutafakari pamoja vifungu vifuatavyo vya maandiko, naamini lipo jambo utajifunza mwishoni mwa somo..
Matendo 16:6 “Wakapita katika nchi ya Frigia na Galatia, wakikatazwa na Roho Mtakatifu, wasilihubiri lile neno katika Asia. 7 Walipofika kukabili Misia wakajaribu kuenda Bithinia, lakini Roho wa Yesu hakuwapa ruhusa, 8 wakapita Misia wakatelemkia Troa. 9 Paulo akatokewa na maono usiku; alimwona mtu wa Makedonia amesimama, akimsihi, na kumwambia, Vuka, uje Makedonia utusaidie”.
Matendo 16:6 “Wakapita katika nchi ya Frigia na Galatia, wakikatazwa na Roho Mtakatifu, wasilihubiri lile neno katika Asia.
7 Walipofika kukabili Misia wakajaribu kuenda Bithinia, lakini Roho wa Yesu hakuwapa ruhusa,
8 wakapita Misia wakatelemkia Troa.
9 Paulo akatokewa na maono usiku; alimwona mtu wa Makedonia amesimama, akimsihi, na kumwambia, Vuka, uje Makedonia utusaidie”.
Wengi wetu tunafahamu vipingamizi pekee mtume Paulo alivyokuwa anapitia vya kuhubiri injili vilitoka kwa shetani, lakini hatujui kuwa kuna wakati mwingine Mungu mwenyewe alikuwa anamzuia Paulo asihubiri injili japokuwa alitamani kufanya hivyo,.
Mungu anafanya hivyo sio kwamba hataki watu wahubiriwe injili kama ilivyo kwa shetani, hapana, bali ni kawaida yake kuwapa vipaumbele vya kwanza wale ambao wanaonyesha kiu ya kutaka kumjua yeye.
Ili kutimiza haya maandiko.
Mathayo 5:6 “Heri wenye njaa na kiu ya haki; Maana hao watashibishwa”.
Na haya..
Mathayo 5:3 “Heri walio maskini wa roho; Maana ufalme wa mbinguni ni wao”.
Kama ukichunguza hiyo mistari utaona, Mungu hakumkataza Paulo kufika kabisa katika hiyo miji iliyotajwa hapo juu, lakini aliifikia na kuipita, kuonyesha kuwa kama kungekuwa na utayari wa wenyeji wa pale kutamani kumjua Mungu basi wangeanzwa kwanza wao, kisha ndio wafuate wale wengine..
Jaribu kufikiria anafika pale Frigia, anataka tu kuanza kuhubiri Mungu anamzuia, anaondoka anaenda mji unaofuata Galatia huko nako Mungu anamzuia anaondoka tena anafikiria labda ashuke kwenye miji mingine ya Asia (ambayo ndio kama Efeso, Smirna, Pergamo, Laodikia n.k. ) lakini huko nako Mungu anamwambia asihubiri chochote aondoke…
Haishii hapo anaondoka tena Asia anafika mji ulioitwa Misia ili aanze kuhubiri bado Mungu anamkataza, anafika Troa bado Mungu hampi kibali, wakati sasa akiwa hapo Troa ukingoni kabisa mwa mji ndipo Mungu anamwonyesha maono ambayo yalikuwa yanaonyesha jinsi watu wa kule Ng’ambo ya bahari Makedonia walivyokuwa wanahitaji msaada mkubwa sana wa kiroho..
Ndipo hapo utaona inamgharimu Paulo kuvuka bahari sasa asafiri, mpaka kwenye hiyo miji ya Makedonia ambayo, ilikuwa ni Filipi, Thesalonike, na Beroya.. Ili kuihubiri injili.. Si jambo rahisi
Ili kuelewa vizuri jaribu kutengeneza picha labda mtumishi wa Mungu anatoka nchi ya mbali Afrika Magharibi labda tuseme Ghana, anafika nchi za Afrika ya kati kama vile Congo n.k., Mungu anamwambia pita usihubiri, anafika mpaka nchi zetu za Afrika mashariki, Anaanzia Uganda anaambiwa pita, anafika Kenya anaambiwa pita, anafika hapa Tanzania, bado Mungu anamwambia usihubiri hapo, sasa akiwa ameshavuka kote toka kigoma, akiwa pale Daresalaam, Mungu anamwambia panda Meli nenda taifa la India wapo watu wangu kule wanahitaji msaada wa kunijua mimi..
Ndivyo ilivyokuwa kwa Mtume Paulo na wenzake, walienda Makedonia na kweli kule walikutana na watu ambao kwanza walikuwa ni maskini, lakini walikuwa tayari kumtolea Mungu kwa moyo wao wote..na zaidi ya yote walikuwa tayari kulipokea Neno la Mungu, mfano watu wa Beroya ndio wale ambao walikuwa wapo tayari kuchunguza maandiko ya kujua ufasaha wa yote,
2Wakorintho 8:1 “Tena ndugu zetu, twawaarifu habari ya neema ya Mungu, waliyopewa makanisa ya Makedonia; 2 maana walipokuwa wakijaribiwa kwa dhiki nyingi, wingi wa furaha yao na UMASKINI WAO uliokuwa mwingi uliwaongezea utajiri wa ukarimu wao. 3 Maana nawashuhudia kwamba, kwa uwezo wao, na zaidi ya uwezo wao, kwa hiari yao wenyewe walitoa vitu vyao;
2Wakorintho 8:1 “Tena ndugu zetu, twawaarifu habari ya neema ya Mungu, waliyopewa makanisa ya Makedonia;
2 maana walipokuwa wakijaribiwa kwa dhiki nyingi, wingi wa furaha yao na UMASKINI WAO uliokuwa mwingi uliwaongezea utajiri wa ukarimu wao.
3 Maana nawashuhudia kwamba, kwa uwezo wao, na zaidi ya uwezo wao, kwa hiari yao wenyewe walitoa vitu vyao;
Hivyo mimi na wewe tunajifunza nini?
Mungu ni yeye ule jana na leo na hata milele, kama mengi ya makanisa ya Asia hayakustahili kupewa neema ya wokovu kwanza, atafanya na kwetu vivyo hivyo kama hatutakuwa tayari kuipokea.
Tupaswa tujiulize je! mioyo yetu ni kweli ina kiu ya kumjua Mungu, kiasi kwamba mpaka rohoni Mungu anatufananisha na watu wa Makedonia?.. Vuka, uje Makedonia utusaidie?. Je! ni kweli tunaonyesha tunahitaji msaada kutoka kwa Mungu? Je tunastahili msaada?.. Kama ni kweli tunaonyesha tunahitaji msaada, basi hapo ndipo Mungu atakapofungua njia ya kutusaidia, kwa namna ya ajabu.
Na tunaonyesha tunahitaji msaada kwa namna gani?.. Tunaonyesha kwa bidii yetu sisi ya kutafuta yeye kwa nguvu zetu zote, kwa akili zetu zote, kwa mioyo yetu yote na kwa Roho zetu zote.
Bwana akubariki.
SAYUNI ni nini?
Mitume wote waliopita walikuwa ni watu weupe hata manabii wote waliopita hadi Ma-papa ni ngozi nyeupe. ni kweli ngozi nyeusi ililaaniwa ?
TABIA YA KIPEKEE USIYOIJUA KUHUSU NENO LA MUNGU.
Shalom mtu wa Mungu, karibu tuyatafakari maandiko…leo ni siku nzuri Bwana aliyotupa..hivyo ni vyema tukachukua nafasi hii kulitafakari Neno lake kwa ufupi..
Kumbuka siku zote kuwa baada ya kumpokea Kristo, kila mmoja wetu anawajibu wa kuifanya kazi ya Mungu kupitia karama Mungu aliyoiweka ndani yake. Kuna hatari kubwa sana ya kutoitumia karama Mungu aliyoiweka ndani yako kabisa….Na madhara makubwa yapo baada ya maisha haya…wakati ule ambapo watakatifu watapewa thawabu zao wewe hutakuwa na chochote…
Katika siku ile waliokuwa waaminifu kwa karama zao watapewa thawabu kubwa zaidi..na wale waliokuwa walegevu na kuleta faida ndogo katika ufalme wa mbinguni watalipwa kidogo, na wale ambao hawajafanya kitu kabisa hawatapewa chochote…
Lakini ni heri kufanya hata kama ni KIDOGO sana ukapata kitu kule kuliko kutofanya kabisa…
Hebu naomba usome mfano huu Bwana alioutoa…inawezekana ulishawahi kuusoma hapo kabla mara nyingi, na kuurudia rudia…. lakini hebu chukua muda tena sasa hivi kuusoma hadi mwisho taratibu, pasipo kuruka kipengele hata kimoja, kuna kitu cha kipekee sana nataka tujifunze leo.
Luka 19:11 “Waliposikia hayo, aliongeza kusema mfano, kwa sababu alikuwa karibu na Yerusalemu, na wao walidhani ya kuwa ufalme wa Mungu utaonekana mara. 12 Basi akasema, Mtu mmoja, kabaila, alisafiri kwenda nchi ya mbali, ili ajipatie ufalme na kurudi. 13 Akaita watu kumi katika watumwa wake, akawapa mafungu kumi ya fedha, akawaambia, FANYENI BIASHARA HATA NITAKAPOKUJA. 14 Lakini watu wa mji wake walimchukia, wakatuma wajumbe kumfuata na kusema, Hatumtaki huyu atutawale. 15 Ikawa aliporudi, ameupata ufalme wake, aliamuru waitwe wale watumwa aliowapa fedha, ili ajue faida aliyopata kila mtu kwa biashara yake. 16 Akaja wa kwanza, akasema, Bwana, fungu lako limeleta faida ya mafungu kumi zaidi. 17 Akamwambia, Vema, mtumwa mwema; kwa vile ulivyokuwa mwaminifu katika neno lililo dogo, uwe na mamlaka juu ya miji kumi. 18 Akaja wa pili, akasema, Bwana, fungu lako limeleta mafungu matano faida. 19 Akamwambia huyu naye, Wewe uwe juu ya miji mitano. 20 Akaja mwingine akasema, Bwana, hili ndilo fungu lako, ambalo nililiweka akiba katika leso. 21 Kwa maana nilikuogopa kwa kuwa u mtu mgumu; waondoa usichoweka, wavuna usichopanda. 22 Akamwambia, Nitakuhukumu kwa kinywa chako, mtumwa mwovu wewe. Ulinijua kuwa ni mtu mgumu, niondoaye nisichoweka, na kuvuna nisichopanda; 23 BASI, MBONA HUKUIWEKA FEDHA YANGU KWA WATOAO RIBA, ili nijapo niipate pamoja na faida yake? 24 Akawaambia waliosimama karibu, Mnyang’anyeni hilo fungu, mkampe yule mwenye mafungu kumi. 25 Wakamwambia, Bwana, anayo mafungu kumi. 26 Nawaambia, Kila aliye na kitu atapewa, bali yule asiye na kitu atanyang’anywa hata alicho nacho”.
Luka 19:11 “Waliposikia hayo, aliongeza kusema mfano, kwa sababu alikuwa karibu na Yerusalemu, na wao walidhani ya kuwa ufalme wa Mungu utaonekana mara.
12 Basi akasema, Mtu mmoja, kabaila, alisafiri kwenda nchi ya mbali, ili ajipatie ufalme na kurudi.
13 Akaita watu kumi katika watumwa wake, akawapa mafungu kumi ya fedha, akawaambia, FANYENI BIASHARA HATA NITAKAPOKUJA.
14 Lakini watu wa mji wake walimchukia, wakatuma wajumbe kumfuata na kusema, Hatumtaki huyu atutawale.
15 Ikawa aliporudi, ameupata ufalme wake, aliamuru waitwe wale watumwa aliowapa fedha, ili ajue faida aliyopata kila mtu kwa biashara yake.
16 Akaja wa kwanza, akasema, Bwana, fungu lako limeleta faida ya mafungu kumi zaidi.
17 Akamwambia, Vema, mtumwa mwema; kwa vile ulivyokuwa mwaminifu katika neno lililo dogo, uwe na mamlaka juu ya miji kumi.
18 Akaja wa pili, akasema, Bwana, fungu lako limeleta mafungu matano faida.
19 Akamwambia huyu naye, Wewe uwe juu ya miji mitano.
20 Akaja mwingine akasema, Bwana, hili ndilo fungu lako, ambalo nililiweka akiba katika leso.
21 Kwa maana nilikuogopa kwa kuwa u mtu mgumu; waondoa usichoweka, wavuna usichopanda.
22 Akamwambia, Nitakuhukumu kwa kinywa chako, mtumwa mwovu wewe. Ulinijua kuwa ni mtu mgumu, niondoaye nisichoweka, na kuvuna nisichopanda;
23 BASI, MBONA HUKUIWEKA FEDHA YANGU KWA WATOAO RIBA, ili nijapo niipate pamoja na faida yake?
24 Akawaambia waliosimama karibu, Mnyang’anyeni hilo fungu, mkampe yule mwenye mafungu kumi.
25 Wakamwambia, Bwana, anayo mafungu kumi.
26 Nawaambia, Kila aliye na kitu atapewa, bali yule asiye na kitu atanyang’anywa hata alicho nacho”.
Mfano huo unamhusu Bwana Yesu mwenyewe, yeye ndio mfano wa huyo mtu kabaila..ambaye aliondoka na kwenda nchi ya mbali(mbinguni) kutuandalia ufalme…na alipoondoka alitupatia vipawa (karama) akatuambia tukawafanye watu wote kuwa wanafunzi (maana yake kuwahubiria na kuwageuza wamwamini yeye kila mmoja kwa kipawa alichopewa)…Na siku moja atarudi kutoka huko nchi ya mbali(mbinguni)…alipokwenda kututengenezea ufalme…atarudi duniani kwaajili ya utawala wa miaka 1,000 (Ufunuo 20).. Na siku atakaporudi atawaangamiza wale wote ambao hawakumkubali (yaani watu waovu)..Na baada ya kuwaangamiza waovu wote ndipo atakapowakusanya watumishi wake waliompokea…na hapo kila mmoja ataketi na kutoa hesabu ya faida aliyoileta katika ufalme wa mbinguni..
Watasimama wachungaji, watasimama waimbaji, watasimama mitume, watasimama mashemasi, waalimu, manabii, maaskofu, wazee wa kanisa, waumini wote na kila mmoja atatoa hesabu jinsi alivyoitumia karama yake…waliofanya vizuri watapewa mamlaka makubwa na waliokuwa wavivu watakosa vyote…
Sasa katika kisa hicho tunasoma kuna mmoja alifukia talanta yake chini…kwa uvivu akijitumainisha kwamba Bwana huwa hasaidiwagi kazi…yeye anang’oa pando asilolipanda, kazi ambayo hajaifanya yeye anaiharibu!…kwahiyo akajifariji kwamba Mungu huwa hasaidiwi kazi…hatutegemei hata tusipokwenda kuhubiri walio wake watakuja tu!.. kwanza unaweza kwenda kuhubiri ukakosea kosea maneno ndio ukawa umemuudhi badala ya kumfurahisha……pia sio lazima sana kumtolea kwani hata tusipochangia chochote kwenye kazi yake yeye ni tajiri na sisi ni mavumbi hivyo atafanya njia tu kwa vyovyote vile(hasaidiwi kazi)……pia yeye hahitaji sana sifa zetu, tayari anao malaika wengi wanaomwimbia….. n.k
Kwahiyo kwa kujitumainisha huko na visingizio hivyo… mtu wa namna hii akawa hafanyi kazi ya Mungu akafananishwa na mtu aliyefukia fedha yak echini ya shimo…siku ile ikafika na Bwana akamhukumu kwa kinywa chake…
Ndugu mpendwa baada ya kuokoka…usikae ufikiri kwasababu Mungu ni mkuu basi hatutegemei sisi….Ni kweli hatutegemei anaweza kufanya asilimia mia pasipo sisi…lakini hataki tuwe wajinga!…Sio kwasababu kasema maneno haya…
Matendo 7:49 “Mbingu ni kiti changu cha enzi, Na nchi ni pa kuwekea miguu yangu; Ni nyumba gani mtakayonijengea? Asema Bwana, 50 Au ni mahali gani nitakapostarehe? Si mkono wangu uliofanya haya yote?”
Matendo 7:49 “Mbingu ni kiti changu cha enzi, Na nchi ni pa kuwekea miguu yangu; Ni nyumba gani mtakayonijengea? Asema Bwana,
50 Au ni mahali gani nitakapostarehe? Si mkono wangu uliofanya haya yote?”
Basi na sisi ndio tubweteke tusimjengee nyumba…kwasababu amesema yeye hakai kwenye nyumba zilizofanywa na mikono yetu…Ndugu Usikae ufikiri hivyo kamwe!.. Daudi aliujua vizuri huo mstari pamoja na Sulemani mwanawe lakini walimjengewa Bwana nyumba hivyo hivyo…na Mungu akapendezwa nao..Sikia maneno Sulemani aliyoyasema..
1Wafalme 8: 26 “Sasa, Ee Mungu wa Israeli, nakusihi, ulithibitishe neno lako, ulilomwambia mtumishi wako, Daudi, baba yangu. 27 LAKINI MUNGU JE? ATAKAA KWELI KWELI JUU YA NCHI? TAZAMA, MBINGU HAZIKUTOSHI, WALA MBINGU ZA MBINGU; SEMBUSE NYUMBA HII NILIYOIJENGA! 28 Walakini uyaelekee maombi ya mtumwa wako, na dua yake, Ee Bwana, Mungu wangu, uisikilize sauti na maombi ya mtumwa wako, aombayo mbele zako leo. 29 Macho yako yafumbuke na kuielekea NYUMBA HII usiku na mchana, mahali hapa ulipopataja, ukasema, Hapa ndipo litakapokuwapo jina langu; ili uyasikie maombi ya mtumwa wako aombapo akikabili mahali hapa”.
1Wafalme 8: 26 “Sasa, Ee Mungu wa Israeli, nakusihi, ulithibitishe neno lako, ulilomwambia mtumishi wako, Daudi, baba yangu.
27 LAKINI MUNGU JE? ATAKAA KWELI KWELI JUU YA NCHI? TAZAMA, MBINGU HAZIKUTOSHI, WALA MBINGU ZA MBINGU; SEMBUSE NYUMBA HII NILIYOIJENGA!
28 Walakini uyaelekee maombi ya mtumwa wako, na dua yake, Ee Bwana, Mungu wangu, uisikilize sauti na maombi ya mtumwa wako, aombayo mbele zako leo.
29 Macho yako yafumbuke na kuielekea NYUMBA HII usiku na mchana, mahali hapa ulipopataja, ukasema, Hapa ndipo litakapokuwapo jina langu; ili uyasikie maombi ya mtumwa wako aombapo akikabili mahali hapa”.
Walijua Mungu mbingu hazimtoshi na huku duniani ni mahali pa kuwekea miguu yake..lakini walilazimisha kumjengea Mungu duniani japokuwa waliyajua hayo maandiko…na mpaka leo Hekalu la Sulemani linajulikana.
Vivyo hivyo na wewe..usiseme Bwana ana malaika wengi…usiseme Bwana hahitaji fedha yangu kwani dhahabu zote na fedha zote ni za kwake… Usiseme sio lazima kujisumbua kuhubiri kwani Bwana anao watumishi wengi…usiseme sio lazima kujisumbua kuimarisha kazi ya Mungu kwasababu Mungu hahitaji msaada kutoka kwetu..ukifanya hivyo utakuwa umefukia talanta yako chini uliyopewa…
Na Mwisho kabisa Bwana alimwambia Yule mtu aliyefukia ile fedha chini maneno haya…” BASI, MBONA HUKUIWEKA FEDHA YANGU KWA WATOAO RIBA”… Mtu anayeweka fedha kwa watoa riba…maana yake haendi kuifanyia shughuli yoyote ile hela..ni kuiweka tu baada ya wakati Fulani inajizalisha…ni kama vile umemkopesha mtu hela…Sasa kazi ya kukopesha haitumii jasho lolote…ni kuwekeza tu hela na kusubiria faida basi!….Hata hiyo kazi nyepesi ambayo haihitaji jasho! Bwana angetegemea aione kwa huyu mtu lakini hakuiona..
Kadhalika na wewe…inawezekana huwezi kabisa kusimama mimbarani, au kwenda mitaani kuhubiri… basi angalau wekeza kwenye kazi ya Mungu kwa fedha zako au mali zako kwa uaminifu, nunua kinanda, nunua mifuko kadhaa ya cement, au nunua chochote kile uwezacho kipeleke nyumbani kwa Mungu…kwasababu unapomtolea Mungu, fedha au mali zile zinakwenda kutumika katika kuifanya kazi ya Mungu na hivyo unaleta faida katika ufalme wa Mbinguni… ukifanya hivyo angalau Bwana atakuheshimu siku ile utakuwa umeiweka talanta yako kwa watoa riba…
Bwana atusaidie sana katika hayo..
Kama bado hujampa Yesu maisha yako…tunaishi katika siku za mwisho, Kristo yupo mlangoni kurudi…hivyo tubu leo kwa kumaanisha kuacha dhambi zote unazozifanya kama ulevi, rushwa, anasa, uasherati, uuaji, ufiraji, ulawiti,ushoga, usagaji, utazamaji wa picha za ngono, kujichua na nyingine zinazofanana na hizo…Tubu leo kwa dhati na amua kuziacha…na baada ya kuomba rehema Bwana atukusamehe kama alivyoahidi…Na amini kashakusamehe kama umetubu kwa dhati!..Na baada ya hapo tafuta ubatizo sahihi ambao ni wa maji tele na kwa jina la Yesu ambalo ndio jina la Baba, Mwana na Roho Mtakatifu…na baada ya hapo Roho Mtakatifu ambaye tayari atakuwa ameshafika karibu yako atakupa uwezo wa kuzishinda hizo dhambi ulizoziacha..ili usizirudie tena…na mengine yaliyosalia atakuongoza kuyafanya.
Maran atha
USITUPE LULU ZAKO MBELE YA NGURUWE.
Ni rahisi zaidi ngamia kupenya tundu ya sindano.
MAOMBI YA VITA
FAIDA ZA MAOMBI.