Category Archive Uncategorized @sw-tz

Je! Shetani anao uwezo wa kuumba, kama Mungu?

SWALI 1: Je! Shetani anaweza kuumba, kama Mungu? Kama sio Mbona kipindi cha Farao, tunaona wale waganga waliweza kuleta vyura na nyoka, kama alivyofanya Musa. Je wale vyura aliwaumbaje, uhai alitolea wapi kama sio Mungu?


JIBU:  Bwana Yesu anasema; Shetani ni mwongo, na sio tu mwongo, bali ni Baba wa huo;

Yohana 8:44 “..wala hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake. Asemapo uongo, husema yaliyo yake mwenyewe; kwa sababu yeye ni mwongo, na baba wa huo”.

Maana yake ni kwamba ufalme wake ameujenga juu ya misingi ya uongo. Alitumia uongo kumnyang’anya Adamu nafasi yake ya umiliki. Vivyo hivyo hadi sasa anatumia uongo kuwadanganya watu wasiutambue ukweli  wote kuhusu yeye.

Anataka kuwadanganya watu, wadhani kuwa yeye ana nguvu za kuweza kukaribiana hata na Mungu au anao uwezo wa kuumba kama Mungu. Lakini ukweli ni kwamba, shetani au kiumbe chochote kile hakiwezi kuumba hata sisimizi. Uwezo huo anao Mungu tu, peke yake.

Kama ni hivyo, ni nini alikifanya kipindi cha Farao?

Alichokifanya kipindi cha Farao, si kingine zaidi ya uongo. Kutokana na maarifa aliyokuwa nayo kipindi kile ambayo anayo hadi sasa, shetani anaweza kubaliki kitu fulani kionekane ni kitu kingine mbele tu ya macho ya watu, au hata kujibadilisha yeye, aonekane ni malaika wa kweli, kumbe ndani ni yeye Yule yule shetani..Biblia inatuambia uwezo huo anao..

2Wakorintho 11:14 “Wala si ajabu. Maana Shetani mwenyewe hujigeuza awe mfano wa malaika wa nuru”.

Hivyo tabia hiyo anayo.. kipindi kile hakuumba nyoka wenye pumzi ya uhai, kama nyoka wengine, au vyura wapya..bali alifanya kazi yake hiyo ya kubadilisha maumbile ya vitu mbele ya macho ya watu.. Kwa lugha ya sasa wanaita “kiini-macho” au “mazingaumbwe”, na ndio maana nyoka wa Musa, hakuwaona wale kama ni nyoka wenzake, wanaohitaji mapambano, bali aliona kama ni chakula tu, akala.

Ni sawa na mwanadamu ambaye amefikia maarifa ya kutoa ‘photocopy’ kitu orijino, Shetani naye hapo amepafikia.Lakini hana uwezo wa kutengeneza orijino.

Kama shetani angekuwa na uwezo wa kuumba chura, hata mbwa angeweza, hata ng’ombe pia angeweza, na  sokwe nao. Na matokeo yake dunia, ingejawa na vitu vilivyoumbwa na Mungu, na vilivyoumbwa na shetani, leo hii tungesikia wale nguruwe si wa Mungu bali ni wa shetani, usiwaguse. Lakini hadi sasa hakuna rekodi ya kitu chochote kilichoumbwa na shetani, zaidi sana rekodi aliyonayo ni kuumba uovu na uasi duniani.

Pia tazama..

1 Jehanamu ni wapi?
2 Nini kinatokea baada ya kifo?
3 Freemason ni nini?
4 Siku ya unyakuo itakuwaje?
5 Upendo ni nini, je kuna aina ngapi za upendo?
6 Je! umepokea Kweli Roho Mtakatifu?
7 Mauti ya pili ni nini?
8 Faida za maombi
9 Jinsi ya kusoma biblia.
10 Je! kuna aina ngapi za malaika?

SWALI 2 : Je! Jini au pepo ni roho tu au pia wana miili inayoonekana, kiasi kwamba tunaweza kuwashika? Kama ndivyo Mbona Bwana Yesu alisema.

Luka 24:39 “Nishikenishikeni, mwone; kwa kuwa roho haina mwili na mifupa kama mnavyoniona mimi kuwa nayo”.

JIBU: Ni kweli sawasawa na maneno ya Bwana Yesu, hakuna jini au pepo, au kiumbe chochote cha rohoni, chenye mwili, na kikaweza kuishi hapa duniani kama sisi.. Hakuna.

Kumbuka, Bwana Yesu alisema..

Mathayo 12:43 “Pepo mchafu, amtokapo mtu, hupitia mahali pasipo maji, akitafuta mahali pa kupumzika, asipate.

44 Halafu husema, Nitarudi nyumbani kwangu nilikotoka; hata akija, aiona tupu, imefagiwa, na kupambwa.

45 Mara huenda, akachukua pamoja naye pepo wengine saba walio waovu kuliko yeye mwenyewe, nao huingia na kukaa humo; na mtu yule hali yake ya mwisho huwa mbaya kuliko ya kwanza. Ndivyo itakavyokuwa kwa kizazi hiki kilicho kibaya”.

SWALI 2 : Je! Jini au pepo ni roho tu au pia wana miili inayoonekana, kiasi kwamba tunaweza kuwashika? Kama ndivyo Mbona Bwana Yesu alisema.

Maandiko hayo ni kutuonyesha kuwa, mapepo, hayana miili yao wenyewe ya kuishia hapa duniani, yanategemea watu,au wanyama,ili kutembea duniani, kama wakati ule yalivyomwomba Bwana yawaingie wale nguruwe. Lakini yenyewe kama yenyewe, hayawezi kusimama na kuwa kama wanadamu kutembea duniani.

Lakini Je! Wale wanaoshuhudia kwamba mapepo yanawatokewa, na pengine kuzuni nao, ni nini vile?

Mapepo yanaouwezo wa kujidhihirisha mbele ya mtu kwa taswira ya kitu fulani, aidha ya mtu, au kitu, kukutisha au kukufanya uogope,  (Mathayo 14:26), au kukutokea katika ndoto,au maono.. lakini zaidi ya hapo yasiweza,  kuendelea na kuchukua maumbile na kuwa kama mwanadamu mwingine na kuishi hapa duniani, kama vile kula, kunywa, kufanyabiashara, kuoa, au kuolewa n.k. huo uwezo hawana kwasababu hawana miili. Pepo haliwezi kuzaa na wewe.

Vinginevyo, shetani angeshajidhihirisha siku nyingi na kuwa mfalme wa dunia. Lakini mpaka sasa ni roho tu, na atabakia kuwa roho, mpaka atakapotupwa kwenye ziwa la moto na mapepo yake.

Lakini kumbuka ukiwa ni mtu wa kujishughulisha na mambo ya ushirikina, aidha wewe ni mganga, au mchawi, au ulishawahi kwenda huko, ukafanyiwa matambiko, au kufanyiwa mazindiko ya kipepo, au ukala vitu vyao, Huo nao ni mlango unaoongeza wigo mkubwa sana, wa shetani au mapepo yake, kujidhihirisha kwako, kwasababu umeingizwa katika mtandao wao wa kiroho, hivyo inakuwa rahisi sana kwao kujidhihirisha kwako, na pengine kuchukua umbile ya kitu chochote kukuletea madhara mwilini. Tofauti na mtu ambaye  yupo mbali na mambo hayo.

Hivyo dawa pekee, ya kumfukuza shetani na majini yake, yasikutokee tokee au yasikufuate fuate ni kumkabidhi Yesu maisha yako. Kwa kumaanisha kabisa kuacha maisha ya dhambi, na baada ya hapo, ukazingatia kusoma NENO..

Kwasababu kuokoka ni sehemu ya kwanza, ya kuwekwa huru.. Ili kuukamilisha uhuru wako ni lazima Neno la Mungu likae ndani yako kwa wingi ili uweze kumshinda kabisa kabisa shetani.

Biblia inasema.

Yohana 8:32 “tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru”.

Bwana Yesu, alikuwa ni mtakatifu wa Mungu, ambaye hakutenda dhambi, lakini hilo halikumzuia shetani asimjie, na kuzungumza naye. Lakini utaona alimshinda kwa Neno la Mungu lililokuwa ndani yake, na si kitu kingine.

Vivyo hivyo na wewe, ikiwa tayari umeshaokoka, Jifunze sana Neno, ujue mamlaka, na haki uliyonayo katika Msalaba wa YESU KRISTO. Hiyo itakufanya usiishi maisha ya woga,wala wasiwasi wa nguvu zozote za giza, kwasababu utakuwa tayari umeshajua uwezo uliopewa jinsi ulivyo mkubwa kuliko wa ibilisi

Lakini ukiwa ni mkristo, mvivu, Neno husomi ujue kabisa shetani ataendelea kukusumbua tu, haijalishi utakuwa ni mwombaji kiasi gani.

Hivyo zingatia hayo mambo mawili.

  1. Wokovu
  2. Neno

Ikiwa bado hujaokoka na upo tayari leo, kumpa Yesu maisha yako, ili akusamehe na kukupa wokovu, na kuyafukuza maroho yote machafu yaliyokuvamia. Basi uamuzi huo ni wa busara sana kwako, ambao hautakaa uujutie milele.

Hivyo fungua hapa, kwa mwongozo wa sala hiyo>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

Je shetani ana uwezo wa kujua mawazo ya mtu?

Mjoli ni nani katika biblia?

Gombo ni nini?

WANA-NDOA: Baba Mkwe, Na mama Mkwe.

Rudi nyumbani

Print this post

TATIZO LA VISIGINO KUUMA KIBIBLIA

Tatizo la visigino kuuma ni ishara ya nini kibiblia?..Au visigino kuwaka moto?.

1) Visigino kuuma.

Kama unafanya shughuli yenye kuhusisha miguu, kwamfano kulima au kutembea umbali mrefu, au michezo..basi ni jambo la kawaida visigino kuuma, au visigino kuwaka moto.

Suluhisho la tatizo hilo ni kupunguza shughuli hizo zinazohusisha miguu, na miguu itarudia hali yake.

Lakini kama huna shughuli zozote unazozifanya na umeenda hospitali na hujapata suluhisho, na hujui sababu, na pengine umeshafanyiwa hata na maombezi, na tatizo bado lipo palepale..

Basi suluhisho la tatizo hilo,linaweza kuwa la kimaandiko,na maandiko yafuatayo yatakufungua…

Yeremia 13:22 “Nawe ukisema moyoni mwako, Mbona mambo haya yamenipata mimi? Ni kwa sababu ya WINGI WA UOVU WAKO, marinda yako yamefunuliwa, na visigino vya miguu yako vimeumia”.

Jiangalie maisha yako ni wapi hapako sawa na Mungu..tubu makosa yako kwa Mungu kwa kumaanisha kuyaacha.

Angalia mahali unapofanyia kazi, au mahali unapoishi, jinsi unavyoenenda, tafakari mawazo ya mioyo yako, je yanampendeza Mungu?..

Je unao upendo?, Wewe ni mvumilivu, ni mtu wa kusamehe au wa vinyongo?, Je ni mtu unayemcha Mungu na kumwogopa?.

Kama sio basi hiyo ndio sababu kwanini visigino vyako vinauma, au vinawaka moto, na umekosa ufumbuzi kila mahali.

Litafakari sana hilo na Mungu akusaidie, yeye ni mwaminifu tukiungama dhambi zetu kwa lengo la kuziacha kabisa, anatusamehe na kuponya magonjwa yetu na majeraha yetu, kwasababu lengo lake sio sisi tuteseke, bali tuwe na furaha na tupate mema, ndio maana saa nyingine anaruhusu vitu fulani vitutokee ili tutubu, na mwishoni atubariki zaidi.

Maran atha!.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

JE TATIZO LA KULA KUCHA NI ISHARA YA KUWA NA MAPEPO?

EE MUNGU, MUNGU WANGU, NITAKUTAFUTA MAPEMA:

TATIZO LA NDANI LINALOWASUMBUA VIJANA, WALIOOKOKA.

WITO WA MUNGU

Kulabu ni nini katika biblia?(2Wafalme 19:27)

Rudi nyumbani

Print this post

Je Malaika Mikaeli ndiye Yesu mwenyewe?

JIBU: Hakuna mahali popote katika biblia inamtaja Mikaeli kuwa ndiye Bwana Yesu. Kinyume chake, maandiko yanamtofautisha Yesu na Malaika hata kwa asili aliyoitwaa,  Biblia inasema.

Waebrania 2:16 “Maana ni hakika, hatwai asili ya malaika, ila atwaa asili ya mzao wa Ibrahimu”.

Ikiwa na maana, kudhihirishwa kwa Bwana Yesu kwa mara ya kwanza, kulikuwa ni katika asili ya mwanadamu na sio Malaika. Na ndio maana utaona, Malaika nao, walimwona na kumtambua kwa mara ya kwanza, siku ile alipozaliwa katika mwili.

1Timotheo 3:16 “Na bila shaka siri ya utauwa ni kuu. Mungu alidhihirishwa katika mwili, Akajulika kuwa na haki katika roho, Akaonekana na malaika, Akahubiriwa katika mataifa, Akaaminiwa katika ulimwengu, Akachukuliwa juu katika utukufu”.

Ni kweli Mikaeli ni mmoja wa Malaika wakuu mbinguni,na pengine Zaidi ya wote, Lakini hana sifa yoyote ya kudhaniwa kuwa yeye ndiye Kristo, kwani  biblia inatuambia kuwa Kristo anaabudiwa sio tu na wanadamu, bali pia na malaika wote mbinguni(Waebrania 1:6), Lakini  hakuna Malaika yoyote anayeabudiwa.

Pia Kristo alikuwa na mamlaka ya kusamehe dhambi, Pamoja na kukemea pepo kwa uweza wake,lakini Malaika (akiwemo Mikaeli), hawana uwezo huo, wanajiona hawastahili mpaka wanasema Bwana mwenyewe na awakemee mashetani (Yuda 1:9)..

Na mwisho biblia inasema, hakuna mahali popote, Mungu alimwita Malaika yoyote “Mwanangu”, bali hao ni watumishi wake, watumikao kuwahudumia watakatifu, lakini kwa Bwana Yesu, Mungu alimwita mwana, kumtofautisha yeye na Malaika zake.

Waebrania 1:5 “Kwa maana alimwambia malaika yupi wakati wo wote, Ndiwe mwanangu, Mimi leo nimekuzaa? Na tena, Mimi nitakuwa kwake baba, Na yeye atakuwa kwangu mwana?

Hivyo, Mikaaeli ni Malaika wa Bwana na atabakia kuwa hivyo. Lakini ikiwa utatamani kujua Zaidi aina za Malaika wa Mungu, na kazi zao na idadi zao, Fungua hapa >> Je! Kuna malaika wangapi mbinguni?

Swali Je! Unatambua kuwa Mungu ameshawaweka tayari Malaika zake kwa ajili ya mapigo ya siku hizi za mwisho? Una Habari kuwa unyakuo upo karibuni sana kutokea, kuliko unavyoweza kudhani?

Kumbuka paraparanda ya Mungu ikilia leo, basi, Malaika hao wa mapigo, Mungu atawaachilia ulimwenguni mwote, wataipiga dunia kwa kwa zile baragumu saba, na vitasa saba. Wakati huo kutakuwa ni nyakati za shida sana ulimwenguni. Soma Ufunuo 8 &16, ujionee mpendwa. Ni Malaika mahususi wa kuleta mabaya duniani.

Zaburi 78:49 “Akawapelekea ukali wa hasira yake, Ghadhabu, na uchungu, na taabu, Kundi la malaika waletao mabaya”.

Usitamani uwepo wakati huo ndugu yangu, Ni heri leo ukatubu na kumrudia muumba wako. Upokee uhakika wa kuurithi uzima wa milele. Ikiwa utataka kusoma juu ya mapigo hayo, fungua link hii>>

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

Neno Saumu lina maana gani katika biblia?

UNYAKUO.

Ninawi ni nchi gani kwasasa?

AINA SABA (7) ZA UNAFIKI, AMBAZO UNAPASWA UJIEPUSHE NAZO.

Rudi nyumbani

Print this post

Tofauti kati ya mbinguni, peponi, Kuzimu, Jehanamu, na Paradiso ni ipi?

SWALI: Naomba kuelewa kwa undani Tofauti kati ya mbinguni, peponi, Kuzimu, Jehanamu, na Paradiso ni ipi?


JIBU:

Mbinguni,

Sehemu nyingi Biblia inaposema mbinguni, huwa inamaanisha moja kwa moja kule Mungu alipo Pamoja Malaika zake, Kule ambako Bwana Yesu alikwenda kutuandalia makao. Mahali ambapo sisi kama watakatifu bado hatujafika hata mmoja.

Ndio mbingu ya Tatu, ambayo Mtume Paulo alinyakuliwa kuonyeshwa baadhi ya vitu vilivyopo kule vipo kule ambavyo havielezeki kibinadamu, kwasababu upeo wetu ni mdogo. (2Wakorintho 12:1-4)

Ni juu sana, ambako, hatuna maelezo ya kutosha kupaelezea, mpaka tutakapofika.

2Nyakati 6:18 “Lakini Mungu je! Yamkini atakaa na watu duniani? Tazama, mbingu na mbingu za mbingu za mbingu hazikutoshi; siuze nyumba hii niliyoijenga!”

Peponi/Paradiso:

Ni mbingu ya mangojeo, ambayo sio makazi yetu ya kudumu. Mtakatifu anayekufa sasa hivi anakwenda mahali panapoitwa Peponi/Paradiso, akisubiria, siku ya unyakuo ifike, arudi kaburini achukue mwili wake, kisha aungane Pamoja na wale watakatifu watakaokuwa hai wakati huo, na moja kwa moja safari ya kwenda mbinguni ianze, kule Bwana Yesu alipo.

Yule mwizi pale msalabani, Bwana alimwambia maneno hayo;

Luka 23:42 “Kisha akasema, Ee Yesu, nikumbuke utakapoingia katika ufalme wako.

43 Yesu akamwambia, Amin, nakuambia, leo hivi utakuwa pamoja nami peponi”.

Wengine wanaiita mbingu ya pili, lakini vyovyote vile iitwavyo, bado ni mahali pa mangojeo pa watakatifu, Ndio kifuani pa Ibrahimu, yule maskini Lazaro alikwenda (Luka 16:19-31), ndio kule ambazo zile Roho zilizo chini ya madhahabu zilikuwa zinalia, zikiomba zilipiziwe kisasi kwa watesi wao.

Ufunuo 6:9 “Na alipoifungua muhuri ya tano, nikaona chini ya madhabahu roho zao waliochinjwa kwa ajili ya neno la Mungu, na kwa ajili ya ushuhuda waliokuwa nao.

10 Wakalia kwa sauti kuu, wakisema, Ee Mola, Mtakatifu, Mwenye kweli, hata lini kutokuhukumu, wala kuipatia haki damu yetu kwa hao wakaao juu ya nchi?

11 Nao wakapewa kila mmoja nguo ndefu, nyeupe, wakaambiwa wastarehe bado muda mchache, hata itakapotimia hesabu ya wajoli wao na ndugu zao, watakaouawa vile vile kama wao”.

Vilevile huku ndio kule wale wafu waliofufuka na Bwana Yesu walipoelekea kwa mara ya kwanza. (Mathayo 27:52-53)

Hivyo leo, hii ukifa katika Kristo, basi unakwenda katika eneo hili la mbingu, ambalo ni lizuri sana. Ukisubiri ufufuo wa mwisho.

Kuzimu:

Kuzimu kibiblia ni Neno lililomaanisha makao ya wafu  Au kaburini. Ambapo, waovu na wema walikuwa wanakwenda kabla ya Kristo kuja duniani, kuwatenganisha moja kwa moja kimakao,

Ayubu anasema

Ayubu 14:13 “Laiti ungenificha kuzimuni, Ukanilinda kwa siri, hata ghadhabu zako zitakapopita, Na kuniandikia muda ulioamriwa, na kunikumbuka!”

Daudi pia alipazungumzia, (Zaburi 16:10), kwamba Bwana hatomwacha huko milele.

Lakini baada ya Bwana Yesu kuja, wakatifu walitoka huko  makaburini, na kwenda peponi/ Paradiso. Mahali pa raha Zaidi pa juu na si makaburini tena. Hivyo wanaobakia makaburini au kuzimu ni waovu.

Jehanamu:

Ni mahali pa mangojeo pa waovu, ni mahali pa mateso, kama vile Paradiso palivyo mahali pa raha pa mangojeo kwa watakatifu, vivyo hivyo jehanamu nako, ni mahali pa mangojeo pa watu waovu wanaokufa sasa. Wanaadhibiwa huko, wakingojea siku ile ya hukumu ya mwisho ifike. Ili wapewe hukumu yao, katika hukumu ya kile kiti cheupe cha enzi cha mwanakondoo, kisha wakatupwe kwenye lile ziwa la moto, ambalo ndio mauti ya pili ilipo.

Ni sawa na mhalifu anayekamatwa sasa hivi, kabla ya kuhukumiwa kifungo, huwa anawekwa kwanza mahabusu, akisubiria siku ya kupandishwa kizimbani ifike, ahukumiwe kisha akatumikie kifungo chake Jela, Ndivyo ilivyo kwa watu waovu wanaokufa sasa, na waliokufa zamani. Wanakwenda katika sehemu hii ya mateso, ambayo si ya kawaida.

Bwana Yesu alisema..

Marko 9:45 “Na mguu wako ukikukosesha, ukate; ni afadhali kuingia katika uzima, u kiwete, kuliko kuwa na miguu miwili, na kutupwa katika jehanum; [

46 ambamo humo funza wao hafi, wala moto hauzimiki.]”

Je! Wewe ni wa makao yapi?

Swali, la kujiuliza ni Je! Tukifa leo, au Unyakuo ukitukuta leo, mimi na wewe tutakuwa wa upande upi? Katika mambo ambayo hupaswi kuyachukulia juu juu tu, basi ni mambo ya Maisha yako ya milele. Kwasababu ukishakufa hakuna nafasi ya pili tena. Kama umestahili Jehanamu basi utaendelea kuishi humo milele.

Ni heri ukamgeukie Kristo, maadamu muda mchache bado unao. Acha kutazama, mambo ya ulimwengu, kwani huwa yanapumbaza sana, kukufanya usione kama kuna mabaya yanakuja mbele, Moja ya hizi siku utajutia Maisha yako, uliishije endapo hukumpa Kristo Maisha yako leo.

Tubu dhambi zako, maanisha kumfuata Yesu.

Bwana atusaidie, kuyafahamu haya.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

Je! kuna maombi yoyote ya kumtoa mtu aliyekufa kwenye mateso ya kuzimu?

MILANGO YA KUZIMU.

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 1)

Rudi nyumbani

Print this post

HUJAPEWA MBAWA ZA KUKIMBIA MATATIZO

Ni kawaida mwanadamu anapopitia matatizo mengi au shida nyingi, huwa anatamani hata  afanane na mnyama asiyejua shida, anatamani angekuwa kama ndege apae zake aende mbali na makao ya watu akaishi humo.

Ndivyo Daudi alivyosema..kipindi ambacho anafukuzwa na Sauli huko majangwani, alisema..

Zaburi 55:5-8
[5]Hofu na tetemeko limenijia,
Na hofu kubwa imenifunikiza.
[6]Nikasema, Ningekuwa na mbawa kama njiwa,
Ningerukia mbali na kustarehe.
[7]Ningekwenda zangu mbali, 
Ningetua jangwani.
[8]Ningefanya haraka kuzikimbia
Dhoruba na tufani.

Lakini jinsi Mungu alivyotuumba, kamwe hatuwezi kuzitoroka dhoruba na tufani za maisha…fahamu kuwa watu wanaokuudhi ndio hao hao utaendelea kuishi nao, na kama hutaishi nao nyumba moja, basi kuna kipindi mtakutana tu katika nukta fulani ya maisha..

Maadui zako, watesi wako, pamoja na wachawi hakuna siku Mungu atakutenga nao akupeleke katika dunia yako mwenyewe uishi huko kwa starehe, hicho kipindi hutakaa ukifikie haijalishi wewe ni mtakatifu kiasi gani.

Mungu anachokifanya kwetu ni kutulinda na kutuepusha tu na madhara yao, yasitufikie. Lakini kuishi katikati yao ni jambo endelevu mpaka mwisho.
Bwana Yesu alisema;

Yohana 17:15
[15]Mimi siombi kwamba uwatoe katika ulimwengu; bali uwalinde na yule mwovu.

Wakati mwingine, Mungu anapotaka kukupa rizki, anatumia hata njia ya hao hao, unakula katikati yao wakikuona..

Zaburi 23:5
[5]Waandaa meza mbele yangu,
Machoni pa watesi wangu.
Umenipaka mafuta kichwani pangu,
Na kikombe changu kinafurika.

Hivyo ndugu uliyeokoka, acha kutaabika kwa ajili ya wanadamu, wala usipeleke akili zako mbali sana, ukidhania kuwa hao watu walio na wewe kama mwiba kuna siku watatoweshwa milele, uishi peke yako kwa starehe..Kanuni hiyo Mungu hajaichagua japo tunaitamani.

Zaidi sana jifunze kuyatimiza mapenzi ya Mungu katikati yao. Utakuwa na furaha katika maisha.
Kumbuka Mbawa kama za njiwa hatujapewa wanadamu.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

Kwanini wakristo wengi ni maskini?.

ALAMA KATIKA VIPAJI VYA NYUSO.

KWANINI MTINI KATIKATI YA MIZABIBU?

Swali: Kurushwa upesi kunakozungumziwa katika Danieli 9:21 ndio kupi?

Rudi nyumbani

Print this post

Wokovu wa kweli ni upi?

Je unaposema umeokoka, ni nini kinakupa uhakika huo?

Fahamu ni nini Bwana anataka kuona kwako, pindi tu unapookoka.

Ni kweli katika Warumi 10:9 biblia inasema;

“Ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka”.

Lakini kukiri kunakozungumziwa hapo, sio sawa na inavyotafsiriwa sasa. Zamani, kukiri kulimaanisha kutangaza vita na ulimwengu, Pamoja na kuhatarisha Maisha yako pia . Kwani ukristo ulijulikana kama ni dini asi, dhidi ya Imani za kipagani.

Soma,

Yohana 9:22 “.. kwa maana Wayahudi walikuwa wamekwisha kuafikiana kwamba mtu akimkiri kuwa ni Kristo, atatengwa na sinagogi”.

Hivyo watu wengi walikuwa wanauliwa, wengine wanafukuzwa mbali na jamii, kwa jambo hilo tu moja, la kumkiri Yesu hadharani. Kwahiyo mtu yeyote kabla ya kwenda kumtangaza  Yesu hadharani kuwa ndiye mwokozi wake, alijifikiria mara mbili kwanza.

Sasa jambo kama hili linatokea kweli sehemu baadhi ulimwenguni, lakini  sio kote. Kwani sisi tuliopo katika mazingira mchanganyiko kama haya. Neno kukiri tu kwa kinywa, sio kipimo tosha kwamba wewe umemfuata Yesu, kwasababu mtu yeyote anaweza kufanya hivyo hata mpagani, kwasababu hakuna hatari yoyote inaweza kumtokea kama akifanya hivyo. Kwasababu anakuwa ni kama tu kaongea.

Na ndio maana leo hii kuna idadi kubwa sana ya watu wanajiita wakristo wanasema wameokoka. Ukiwauliza wameokokaje watakuambia, kwasababu walimkiri Yesu kwa vinywa vyao, hilo tu.Na huku ukiangalia Maisha yao, hayana tofauti na watu wa kidunia.

Ndugu usidanganyike, wokovu wetu ili ufanane na ule wa watu wa zamani, hatuna budi tumkiri Yesu KWA MATENDO YETU. Tunaukataa ulimwengu na mambo yake yote, kivitendo.

Bwana Yesu alitabiri kuwa siku za mwisho, wengi watamwita ‘Bwana, Bwana’, kwa midomo tu, lakini matendo yao yapo mbali naye, lakini anasema atawafukuza Dhahiri.

Mathayo 7:21 “Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.

22 Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?

23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu.

Umeona? Ikiwa hao atakaowafukuza wanafanya miujiza mikubwa, na kutoa ishara nyingi, jiulize wewe ambaye hutendi lolote, na bado unatenda dhambi, unadhani utamwonga Mungu, kisa uliongozwa sala ya toba?

Ndugu, ni kuwa makini sana nyakati hizi, Ukisema umeokoka, uthibitishe wokovu wako kwa matendo kwamba umeuacha ulimwengu kweli kweli. Unaacha hivyo vimini, hizo suruali uvaazo binti,Uzinzi, anasa, punyeto, picha za ngono utazamazo mitandaoni.

Kuongozwa sala ya toba mara nyingi, sio tiketi ya kwenda mbinguni, bali badiliko lako ndilo litakalokuoa.

Bwana atufumbue macho yetu tulione hilo.

Print this post

MUNGU ALIVICHAGUA VITU AMBAVYO HAVIKO.

Nakusalimu katika jina kuu la Bwana wetu Yesu Kristo, ukuu na uweza vina yeye milele na milele. Amina.

Mtume Paulo aliandika, ANGALIENI MWITO WENU, Akiwa na maana, kwamba tunapaswa tuwe na ufahamu tosha juu ya wito wa Mungu katika Maisha yetu jinsi unavyokuja. Tofauti na tunavyodhani kuwa Mungu akikuuita, ni mpaka uwe shupavu au hodari Fulani. Mpaka uwe na miguu miwili, mpaka uwe na digrii Fulani ya dini, mpaka uwe na kipato Fulani au familia nzuri, mpaka uwe na kipaji Fulani cha kitofauti, Hapana..

Bali yeye huwa anakwenda kinyume chake..Tunalithibitisha hilo katika vifungu hivi;

1Wakorintho 1:26 “Maana, ndugu zangu, angalieni mwito wenu, ya kwamba si wengi wenye hekima ya mwilini, si wengi wenye nguvu, si wengi wenye cheo walioitwa;

27 bali Mungu aliyachagua mambo mapumbavu ya dunia awaaibishe wenye hekima; tena Mungu alivichagua vitu dhaifu vya dunia ili aviaibishe vyenye nguvu;

28 tena Mungu alivichagua vitu vinyonge vya dunia na vilivyodharauliwa, naam, VITU AMBAVYO HAVIKO, ili avibatilishe vile vilivyoko;

29 mwenye mwili awaye yote asije akajisifu mbele za Mungu”.

Bwana anasema, anavichagua vitu ambavyo haviko, akiwa na maana sio kwamba haviko kabisa ulimwenguni, hapana, bali uwepo wake, ni kama tu vile haviko. Kwamfano nikija na kukutajia nchi kama “Marekani” au “Ufaransa” ni wazi kuwa ulishawahi kuzisikia mahali Fulani nchi hizi, kwasababu kila siku zinatajwa aidha katika vyombo vya Habari au midomoni mwa watu, Lakini nikikutajia nchi kama “Tuvalu” au “Kiribati” pengine leo ndio inaweza ikawa mara yako ya kwanza kuzisikia hizi nchi, Ni kama vile hazipo duniani sio ndio!. Lakini ni nchi ambazo zipo, na zinamfumo huru unaojiendesha kama tu vile nchi yako.

Vivyo hivyo, wito wa Mungu, unachagua, watu ambao “hawapo” yaani wasiojulikana, wasiosikika hata katika masikio ya watu, waliosahaulika zamani, kama vile Daudi, alivyoitwa hao akiwa huko maporini, ndio jicho la Mungu linawatazama sana, ili awatumie.

Pengine umekata tamaa, au unajidharau, au unajiona wewe si kitu, huna elimu yoyote, huna uzuri, huna ujuzi, upo upo tu, huna marafiki wengi, huwezi kujichanganya sana, pengine ni mlemavu, au ni mzito wa kutenda,.

Nataka nikuambie, wito wa Mungu upo karibu sana na wewe kuliko unavyodhani, kuliko kwa watu wenye nguvu, ikiwa tu, utakubali kujisogeza karibu na yeye. Wengi wa Mitume wa Kristo walikuwa hawana elimu yoyote biblia inasema hivyo katika ( Matendo 4:13), walikuwa ni wavuvi tu, lakini walipoitwa na Mungu, walitii na kumfuata kwa ukamilifu wote, bila kuwa na mawazo mawili mawili. Na ndio hao Mungu aliwatumia kwa viwango vya juu mpaka, tunawaita mababa wa Imani.

Na sisi pia, tusione madhaifu yetu, au unyonge wetu, kama ndio sababu ya kutomtumikia Mungu, kinyume chake, ndio tumtafute kwa bidii kwasababu katika hali hizo wito wake ndio mkubwa kushinda pale tunapokuwa na nguvu.

Udhaifu wowote, tuunaona ndani yetu, ndio uweza wa Mungu unapotimilikia hapo.

2Wakorintho 12:9 “Naye akaniambia, Neema yangu yakutosha; maana uweza wangu hutimilika katika udhaifu. Basi nitajisifia udhaifu wangu kwa furaha nyingi, ili uweza wa Kristo ukae juu yangu.

10 Kwa hiyo napendezwa na udhaifu, na ufidhuli, na misiba, na adha, na shida, kwa ajili ya Kristo. Maana niwapo dhaifu ndipo nilipo na nguvu”.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

Amri zilizo ndogo alizozizungumzia Yesu ni zipi?

Chuo cha vita vya Bwana ni kipi?(Hesabu 21:14)

JE WEWE NI LAZARO YUPI, WA KWANZA AU WA PILI?

Rudi nyumbani

Print this post

Na ulimi laini huvunja mfupa.(Mithali 25:15)

SWALI: Biblia ina maana gani kusema “Na ulimi laini huvunja mfupa”? (Mithali 25:15)

Mithali 25:15 “Kwa uvumilivu mwingi mkuu husadikishwa; Na ulimi laini huvunja mfupa”.


JIBU: Ulimi ni kiungo kilaini kuliko vyote katika mwili. Lakini biblia inatupa ufunuo wake, kuwa kinauwezo  wa kuvunja mifupa?

Je kinavunjaje mifupa?

Hiyo ni lugha ya ki-mithali tu, kuonyesha kwamba ulimi unaweza kuleta matokeo au madhara makubwa ya nje, kuliko hata kinavyoweza kudhaniwa.

  1. Ulimi ukitumika vyema unaweza kuleta suluhu ya matatizo makubwa yaliyoshindikana…

    2.  Vilevile ukitumika isivyopasa unaweza kuleta, matatizo makubwa kupita kiasi.

Tutazame kwenye biblia mfano wa pale ulimi ulipotumika vibaya:

Mtoto wa Sulemani, alilisababishia taifa la Israeli kugawanyika mara mbili, kwasababu  tu ya ulimi wake, usiokuwa na busara, kwa wana wa Israeli. Na hilo alilisema kutokana na malalamika ya baadhi ya wayahudi ambao waliomba wapunguziwe utumwa ambao baba yake Sulemani aliwatwisha.. Lakini yeye badala ya kusikiliza mashauri ya wazee, akasikiliza mashauri ya vijana wanzake, Na kibaya Zaidi badala awapooze kwa maneno mazuri akawaambia, utumwa wangu utakuwa ni Zaidi hata ya ule utumwa wa baba yangu.

Hivyo maneno hayo yakawakasirisha sana wayahudi wengi, mpaka, wakakataa kutawaliwa na uzao Daudi wakajitenga, ndio hapo pakawa mwanzo wa mataifa mawili kuundwa ndani ya nchi moja (yaani Israeli na Yuda), kwa miaka mingi sana.

1Wafalme 12:13 “Mfalme akawajibu watu wale kwa ukali, akaliacha shauri lile wazee walilompa;

14 akawajibu kama vile walivyomshauri vijana, akasema, Baba yangu alilifanya zito kongwa lenu, bali mimi nitaongeza kongwa lenu; baba yangu aliwapiga kwa mijeledi, bali mimi nitawapigeni kwa nge.

15 Basi mfalme hakuwasikia wale watu; maana jambo hili lilitoka kwa Bwana, ili alitimize neno lake, Bwana alilomwambia Yeroboamu mwana wa Nebati kwa kinywa cha Ahiya Mshiloni.

16 Basi Israeli wote walipoona ya kuwa mfalme hakuwasikia, hao watu walimjibu mfalme, wakasema, Tuna sehemu gani katika Daudi? Wala hatuna urithi katika mwana wa Yese. Haya! Nendeni zenu hemani kwenu, enyi Israeli; sasa itunze nyumba yako mwenyewe, Ee Daudi. Hivyo Israeli wakaenda zao hemani kwao”.

Huo ni mfano wa mahali ambapo ulimi ulitimika vibaya;

Mahali pengine ambapo ulimi ulitumika vizuri, na ukabatilisha mashauri mabaya;

Ni pale Daudi alipoonyesha fadhila zake nyingi kwa mtu mmoja aliyeitwa Nabali, lakini pale naye alipotaka chakula, Nabali alimjibu kwa maneno ya kukasirisha na kashfa, hivyo Daudi akaapa kuwa atakwenda kuwaangamiza watu wote wa nyumbani mwake, japokuwa aliwasaidia hapo kabla. Lakini alipokuwa njiani, mke wa Nabali alipata taarifa hizo kuwa Daudi na jeshi lake wanakuja kuwaangamiza, hivyo akamwendea Daudi, kwa kujinyenyekeza na kumpa maneno malaini ya kutuliza hasira. Ndipo Daudi akaghahiri uuaje wake aliokusudia, kwa ukoo mzima wa Nabali.

1Samweli 25:21 “Basi Daudi alikuwa amesema, Hakika ni bure nilivyokuwa nikilinda nyikani yote aliyo nayo mtu huyu, asipotewe na kitu cho chote cha mali yake yote; naye amenilipa mabaya badala ya mema.

22 Mungu naye awafanyie hivyo adui za Daudi, na kuzidi, nikimwachia katika wote walio wake hata mtoto mume mmoja, kutakapopambazuka asubuhi.

23 Ndipo hapo Abigaili alipomwona Daudi, alifanya haraka kushuka juu ya punda wake, akamwangukia Daudi kifulifuli, akainama mpaka nchi.

24 Akamwangukia miguuni pake, akasema, Juu yangu, bwana wangu, juu yangu mimi na uwe uovu; tafadhali mjakazi wako na anene masikioni mwako, nawe uyasikilize maneno ya mjakazi wako.

25 Nakusihi, bwana wangu, wewe usimwangalie huyu mtu asiyefaa, yaani, Nabali; kwa maana kama lilivyo jina lake ndivyo alivyo yeye; jina lake ndilo Nabali, na upumbavu anao; lakini mimi, mjakazi wako, sikuwaona hao vijana wa bwana wangu aliowatuma.

26 Basi sasa, bwana wangu, aishivyo Bwana, na iishivyo nafsi yako, kwa kuwa Bwana amekuzuia usimwage damu, tena usijilipize kisasi mkono wako mwenyewe, basi sasa adui zako, na hao wamtakiao bwana wangu mabaya, wawe kama Nabali.

27 Na sasa zawadi hii, mjakazi wako aliyomletea bwana wangu, na wapewe vijana wamfuatao bwana wangu.

28 Nakuomba ulisamehe kosa lake mjakazi wako, kwa kuwa hakika Bwana atamfanyia bwana wangu nyumba iliyo imara, kwa sababu bwana wangu anavipiga vita vya Bwana; tena uovu hautaonekana ndani yako siku zako zote.

29 Na hata ijapokuwa binadamu angeinuka akuwinde, na kuitafuta nafsi yako, hiyo nafsi ya bwana wangu itafungwa katika furushi ya uhai pamoja na Bwana, Mungu wako; na nafsi za adui zako ndizo atakazozitupa nje, kama kutoka kati ya teo.

30 Tena itakuwa, hapo Bwana atakapokuwa amemtendea bwana wangu sawasawa na mema yote aliyoyanena juu yako, na kukutawaza juu ya Israeli;

31 hili halitakuwa kwazo, wala chukizo la moyoni kwa bwana wangu, ama ya kuwa umemwaga damu bure, ama ya kuwa bwana wangu amejilipiza kisasi mwenyewe; tena hapo Bwana atakapokuwa amemtendea bwana wangu mema, ndipo umkumbuke mjakazi wako.

32 Naye Daudi akamwambia Abigaili, Na ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, ambaye amekuleta hivi leo kunilaki;

33 na ibarikiwe busara yako, na ubarikiwe wewe, uliyenizuia hivi leo nisimwage damu, wala kujilipiza kisasi kwa mkono wangu mwenyewe.

34 Kwa kuwa ni kweli, aishivyo Bwana, Mungu wa Israeli, aliyenizuia nisikudhuru, kwamba hungefanya haraka kuja kunilaki, hakika huyu Nabali asingaliachiwa hata mtoto mume mmoja, kutakapopambazuka asubuhi.

35 Basi Daudi akapokea mkononi mwake vitu vile alivyomletea; akamwambia, Haya! Kwea kwa amani kwenda nyumbani kwako; tazama, nimeisikiliza sauti yako, nami nimeukubali uso wako”.

Ndio maana Biblia inamalizia kwa kusema..

Yakobo 3:5 “Vivyo hivyo ulimi nao ni kiungo kidogo, nao hujivuna majivuno makuu. Angalieni jinsi moto mdogo uwashavyo msitu mkubwa sana.

6 Nao ulimi ni moto; ule ulimwengu wa uovu, ule ulimi, umewekwa katika viungo vyetu, nao ndio uutiao mwili wote unajisi, huuwasha moto mfulizo wa maumbile, nao huwashwa moto na jehanum.

7 Maana kila aina ya wanyama, na ya ndege, na ya vitambaavyo, na ya vitu vilivyomo baharini, vinafugika, navyo vimekwisha kufugwa na wanadamu.

8 Bali ulimi hakuna awezaye kuufuga; ni uovu usiotulia, umejaa sumu iletayo mauti.

9 Kwa huo twamhimidi Mungu Baba yetu, na kwa huo twawalaani wanadamu waliofanywa kwa mfano wa Mungu”.

Hivyo tujifunze kutumia ndimi zetu vizuri. Kwasababu kwa hizi tutajibariki wenyewe na kwa hizi tutajiangamiza wenyewe.

Kumbuka; ulimi laini huvunja mfupa.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya kilichotarajiwa kikikawia kuja moyo huugua (Mithali 13:12)?.

DORKASI AITWAYE PAA.

CHANGIA SASA.

UTAONA MAMBO MAKUBWA KULIKO HAYA.

MKAMCHUKUE SALAMA.

Rudi nyumbani

Print this post

NDIPO HUENDA AKACHUKUA PEPO WENGINE SABA.

Luka 11:24 “Pepo mchafu amtokapo mtu, hupitia mahali pasipo maji, akitafuta mahali pa kupumzika; asipoona, husema,

25 Nitairudia nyumba yangu niliyotoka.

26 Hata afikapo, akaiona imefagiwa na kupambwa, ndipo huenda akachukua pepo wengine saba, walio waovu kuliko yeye mwenyewe, wakaingia na kukaa humo; na mtu yule hali yake ya mwisho huwa mbaya kuliko ya kwanza”.

Ukitafakari vifungu hivyo, utagundua tabia kadha wa kadha za mapepo;

  1. Jambo la kwanza huwa linatabia ya kwenda kuishi mahali pasipokuwa na maji;

Ni adui wa maji; Sasa ni lazima ujue sehemu isiyokuwa na maji ni ipi kiroho? Ni moyo mkavu, usiokuwa na chemchemi ibubujikayo maji ya uzima ndani yake, yaani Roho Mtakatifu..

Yohana 4:14 “walakini ye yote atakayekunywa maji yale nitakayompa mimi hataona kiu milele; bali yale maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji, yakibubujikia uzima wa milele”.

Mtu yeyote asiyekuwa na Kristo ndani yake, tayari kwa namna moja au nyingine ndani yake  kuna  mapepo, kwasababu ni kukame. Kwa urefu wa  habari hiyo , tutumie ujumbe inbox tukutumie somo lake;

    2) Tabia ya pili ni kwamba, yapo mapepo mengi ambayo hayana makao, yanasubiria tu, kualikwa.

Ndio maana ukisoma hapo anasema, likirudi na kukuta nyumba yake imefagiliwa, linakwenda kutafuta mengine saba yaliyo maovu kuliko yeye.

Jiulize linakwenda kutafutia wapi,? Hiyo ni kuonyesha kuwa yapo mahali fulani yanangojea kuitwa, na kwanini lisitafute limoja tu, bali saba? Ni kuonyesha kuwa yapo mengi, na kwanini lisitafute la saizi yake, bali yenye nguvu kuliko yeye. Ni kuonyesha kuwa na yenyewe huwa yanafanya uchaguzi, ni nani wa kukaa nao. Hiyo yote ni kujihakikishia ulinzi wake ili atakaporudi asibugudhiwe kwa lolote.

Kulithibitisha hilo, Soma ile habari ya Mariamu Magdalena, ambaye Bwana Yesu alimponya kwa kuyatoa mapepo saba ndani yake; Kuonyesha kuwa hapo kabla alikuwa ni mtu vuguvugu, yaani Mungu kidogo shetani kidogo, ndio maana yakamuingia yote yale kwa mpigo.

Marko 16:9 “Naye alipofufuka alfajiri siku ya kwanza ya juma, alimtokea kwanza Mariamu Magdalene, ambaye kwamba alimtoa pepo saba”.

Kuwa makini sana, unaposhiriki ibada yoyote ya Ki-Mungu, na ilihali maisha yako ni ya kipepo (yaani ya dhambi). Unazini, unalewa, unakwenda kwa waganga, unafanya anasa n.k. na wakati huo huo unakwenda kanisani kushiriki meza ya Bwana au kumwabudu Mungu, na kutoa sadaka.

Watu wengi leo hii hawajijui kuwa wanajiongezea tu idadi kubwa ya mapepo, kwasababu ibada yoyote uifanyayo kwa Mungu ni adui wa mapepo, hivyo yanapoona hali fulani ya hatari katika nyumba zao imetokea, Ni lazima yajihakikishie ulinzi kwa kuyaalika mengine saba yenye nguvu kuliko yenyewe.

Ndio hapo hali yako ya mwisho inakuwa mbaya kuliko ya mwanzo. Unakwenda kanisani, Neno limekuchoma, uache uasherati,  badala uache mambo hayo, unatoka kuendeleza tabia hizo, ujue kuwa utakuwa mzinzi mbaya kuliko hata ulivyokuwa pale mwanzo.

Ni heri ukatubu dhambi zako leo, Na kumfuata Bwana Yesu kwa kumaanisha kweli kweli, ufalme wa Mungu unapatikana kwa nguvu, biblia inasema hivyo, kwasababu shetani anajua kuwa muda wake ni mchache, hivyo anafanya kazi kwa bidii sana akishirikiana na mapepo yake, kuwaangusha watu.

Ndio maana siku hizi za mwisho hushangai kuona, maovu yamekithiri duniani, hata aibu tena hamna, hizo zote ni kazi za mapepo wachafu, ambazo  zimewavaa na kuwaendesha.

Hata wewe au mimi, tukiwa ni watu vuguvugu, hatueleweki tupo upande upi, tujue kuwa tupo kwenye hatari kubwa sana ya kuwa na mapepo wengi. Hivyo kwa haya machache ikiwa unataka, Kristo aanze na wewe upya katika maisha yako, na ayafukuze haya mapepo moja kwa moja.

Basi fuatisha sala hii;

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU  MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuwa na uhalali kwa kuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Na kufukuza mapepo yote, yaliyokuwa yameweka mzizi ndani yako.

Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

NUNUA MAJI YA UZIMA.

SI MAPEPO YOTE NI YA KULIPUKA.

ONDOKA YESU, TUACHIE MAPEPO.

NUNUA MAJI YA UZIMA.

Je! Wana wenu huwatoa kwa nani? maana yake ni nini?

Rudi nyumbani

Print this post

Ninyi mnaoimba nyimbo za upuzi pamoja na sauti ya vinanda.

SWALI: Bwana alimaanisha nini katika mstari huu;

Amosi 6:5 “ninyi mnaoimba nyimbo za upuzi pamoja na sauti ya vinanda, na kujifanyizia vinanda vya namna nyingi, kama vile Daudi”

Je! alimkosa Daudi, kwa namna alivyokuwa anamsifu?


JIBU: Jibu ni la! Mstari huo haumaanishi kuwa Mungu anachukizwa na watu wanaomsifu kwa ala, na vyombo vingi vya muziki, hapana, kinyume chake anasisitiza sana tufanye hivyo, tena hiyo pia ilikuwa ni sababu nyingine iliyomfanya Mungu ampende Daudi..

Daudi kwa uvuvio wa Roho aliandika maneno haya;

Zaburi 150:3 “Msifuni kwa mvumo wa baragumu; Msifuni kwa kinanda na kinubi;

4 Msifuni kwa matari na kucheza; Msifuni kwa zeze na filimbi;

5 Msifuni kwa matoazi yaliayo; Msifuni kwa matoazi yavumayo sana.

6 Kila mwenye pumzi na amsifu Bwana. Haleluya”.

Umeona? Kuonyesha kuwa Mungu anapendezwa sana na kufisiwa kwa ala na midundo mbalimbali ya miziki.

Lakini sasa kwanini kwenye mstari huyo wa Amosi, anaonekana kama anawakemea watu wanaofanya hivyo?

Kumbuka hapo, anasema ninyi “mnaoimba nyimbo za upuzi”. Ikiwa na maana, wanachokiimba  hakimtukuzi Mungu, kinamfano wa ki-Mungu lakini ni cha kidunia, na pia hawamuiimbi Mungu katika Roho na Kweli, yaani, matendo yao, yapo mbali na Mungu halafu wanajifanya wanamwimbia yeye katika ustadi wa ala mbalimbali..

Ndicho walichokifanya wana Israeli hicho kipindi, walikuwa wanafanya maasi mengi, lakini wanajifanya wanajua kumtukuza Mungu kwa nguvu kama Daudi..Matokeo yake, Mungu akawazira kwa sifa zao za kinafki, akawapa adhabu ya kuchukuliwa utumwani Babeli..

Ukisoma mistari ya mbele kidogo Bwana anasema;

Amosi 6:8 “Bwana MUNGU ameapa kwa nafsi yake, asema Bwana, Mungu wa majeshi; Naizira fahari ya Yakobo, nachukizwa na majumba yake; kwa sababu hiyo nitautoa huo mji, pamoja na wote waliomo ndani yake.

9 Hata itakuwa, wakisalia wanaume kumi katika nyumba moja, watakufa”.

Umeona, mfano wa Kanisa la Kristo lililopo sasa.

Tuna vyombo vingi vya kisasa vya kumsifu Mungu, tuna magitaa, tuna maspika yenye nguvu, tuna mapiano, vinanda vya kisasa, matarumbeta n.k. jambo ambalo ni zuri kumsifu Mungu kwa namna hiyo. Lakini angalia kinachoimbwa sasa, na staili za uchezaji, ni ‘upuuzi’ sawasawa na maneno ya Bwana. Huwezi tofautisha nyimbo ya ki-Mungu na nyimbo za wasanii wa kidunia.

Na hata kama tutaimba maneno ya kumsifu Mungu, lakini angalia matendo yetu nyuma ya pazia, yapo mbali kabisa na wokovu na utakatifu.

Hivyo unabii huo unatuhusu sisi, tunapaswa tujirekebishe, ili Bwana asituzire kwa kutupa adhabu kama alivyowapa wana wa Israeli kwa kuwapeleka utumwani Babeli.

Biblia inasema tumwabudu Mungu katika uzuri wa utakatifu, Na Sio katika vinywa tu, na midundo, Ili tupokee baraka alizozikusudia katika kufanya hivyo.

1Nyakati 16:29 “Mpeni Bwana utukufu wa jina lake;…. Mwabuduni Bwana kwa uzuri wa utakatifu”;

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

Matoazi na Matari ni nini? (Kutoka 15:20)

Kinubi ni nini katika biblia? (1Samweli 16:16, 23)

Zaburi maana yake nini, katika Biblia?

Amwimbiaye nyimbo mtu mwenye moyo mzito.

Rudi nyumbani

Print this post