Mistari ya biblia kuhusu kifo.
Kifo ni jambo lisilozoeleka kwa mtu yeyote, Lakini pamoja na hayo lipo tumaini la uzima tena, kwa wale waliomwamini Bwana Yesu Kristo. Na ndio maana mtume Petro aliwatia moyo waaminio wote wa wakati ule, akiwaambia wasistaajabie sana, msiba huo utakapowapata kwa ghafla kama jaribu la moto, kinyume chake wafurahie kwasababu lipo tumaini tena la uzima siku ile ya ufufuo..Kwasababu watafufuliwa tena, na kuwaona wapendwa wao.
1Petro 4:12 “Wapenzi, msione kuwa ni ajabu ule msiba ulio kati yenu, unaowapata kama moto ili kuwajaribu, kana kwamba ni kitu kigeni kiwapatacho.
13 Lakini kama mnavyoyashiriki mateso ya Kristo, furahini; ili na katika ufunuo wa utukufu wake mfurahi kwa shangwe”.
Hivyo na wewe unapoipitia mistari hii naomba uitafakari kwa utulivu, itakuponya sehemu Fulani.
Kwababu biblia inasema tena..
Mhubiri 7:2 “Heri kuiendea nyumba ya matanga, Kuliko kuiendea nyumba ya karamu. Kwa maana huo ndio mwisho wa wanadamu wote, naye aliye hai atautia moyoni mwake.
3 Huzuni ni afadhali kuliko kicheko, Maana simanzi ya uso ni faida ya moyo”.
Na pia Bwana Yesu alisema…
Mathayo 5:4 “Heri wenye huzuni; Maana hao watafarijika”.
Na bado biblia inaendelea kusisitiza na kusema..
Mhubiri 7: 1 “Heri sifa njema kuliko marhamu nzuri; Na siku ya kufa kuliko siku ya kuzaliwa”.
1Wathesalonike 4:13 “Lakini, ndugu, hatutaki msijue habari zao waliolala mauti, msije mkahuzunika kama na wengine wasio na matumaini.
14 Maana, ikiwa twaamini ya kwamba Yesu alikufa akafufuka, vivyo hivyo na hao waliolala katika Yesu, Mungu atawaleta pamoja naye.
15 Kwa kuwa twawaambieni haya kwa neno la Bwana, kwamba sisi tulio hai, tutakaosalia hata wakati wa kuja kwake Bwana, hakika hatutawatangulia wao waliokwisha kulala mauti.
16 Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza.
17 Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana hewani; na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele.
18 Basi, farijianeni kwa maneno hayo.”.
Zaburi 23:4 “Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, Gongo lako na fimbo yako vyanifariji”.
Warumi 14:8 “Kwa maana kama tukiishi, twaishi kwa Bwana, au kama tukifa, twafa kwa Bwana. Basi kama tukiishi au kama tukifa, tu mali ya Bwana”.
Luka 23:43 “Yesu akamwambia, Amin, nakuambia, leo hivi utakuwa pamoja nami peponi”.
Yohana 11:26 “naye kila aishiye na kuniamini hatakufa kabisa hata milele. Je! Unayasadiki hayo”?
Yohana 14:1 “Msifadhaike mioyoni mwenu; mnamwamini Mungu, niaminini na mimi.
2 Nyumbani mwa Baba yangu mna makao mengi; kama sivyo, ningaliwaambia; maana naenda kuwaandalia mahali.
3 Basi mimi nikienda na kuwaandalia mahali, nitakuja tena niwakaribishe kwangu; ili nilipo mimi, nanyi mwepo.
4 Nami niendako mwaijua njia”.
Zaburi 116:15 “Ina thamani machoni pa Bwana Mauti ya wacha Mungu wake”.
Ufunuo 14:13 “Nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, Andika, Heri wafu wafao katika Bwana tangu sasa. Naam, asema Roho, wapate kupumzika baada ya taabu zao; kwa kuwa matendo yao yafuatana nao”.
Mhubiri 3:1 “Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.
2 Wakati wa kuzaliwa, na wakati wa kufa; Wakati wa kupanda, na wakati wa kung’oa yaliyopandwa;
3 Wakati wa kuua, na wakati wa kupoza; Wakati wa kubomoa, na wakati wa kujenga;
4 Wakati wa kulia, na wakati wa kucheka; Wakati wa kuomboleza, na wakati wa kucheza”;
1Wakorintho 15:26 “Adui wa mwisho atakayebatilishwa ni mauti”.
Ufunuo 21:4 “Naye atafuta kila chozi katika macho yao, wala mauti haitakuwapo tena; wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu hayatakuwapo tena; kwa kuwa mambo ya kwanza yamekwisha kupita”.
2Wakorintho 5:1 “Kwa maana twajua ya kuwa nyumba ya maskani yetu iliyo ya dunia hii ikiharibiwa, tunalo jengo litokalo kwa Mungu, nyumba isiyofanywa kwa mikono, iliyo ya milele mbinguni”.
Wafilipi 3:20 “Kwa maana sisi, wenyeji wetu uko mbinguni; kutoka huko tena tunamtazamia Mwokozi, Bwana Yesu Kristo;
21 atakayeubadili mwili wetu wa unyonge, upate kufanana na mwili wake wa utukufu, kwa uweza ule ambao kwa huo aweza hata kuvitiisha vitu vyote viwe chini yake.
2Wakorintho 12:9 “Naye akaniambia, Neema yangu yakutosha; maana uweza wangu hutimilika katika udhaifu. Basi nitajisifia udhaifu wangu kwa furaha nyingi, ili uweza wa Kristo ukae juu yangu.
10 Kwa hiyo napendezwa na udhaifu, na ufidhuli, na misiba, na adha, na shida, kwa ajili ya Kristo. Maana niwapo dhaifu ndipo nilipo na nguvu”.
Warumi 5:12 “Kwa hiyo, kama kwa mtu mmoja dhambi iliingia ulimwenguni, na kwa dhambi hiyo mauti; na hivyo mauti ikawafikia watu wote kwa sababu wote wamefanya dhambi”
Lakini tukishafahamu hayo, tukishafahamu kuwa haya maisha ni ya kitambo tu, yanayeyuka kama mvuke, swali linakuja je! Wewe umejiwekaje kipindi hichi kifupi ulichobakiwa nacho duniani?
Yakobo 4:14 “walakini hamjui yatakayokuwako kesho. Uzima wenu ni nini? Maana ninyi ni mvuke uonekanao kwa kitambo, kisha hutoweka”.
Jiulize ukifa na wewe leo ghafla, utakuwa upande gani?.Ukiona moyoni mwako huna jibu la uhakika ni wazi kuwa ukifa huwezi kwenda mbinguni..Kwasababu wanaokwenda mbinguni Yesu Kristo anauweka uhakika huo moyoni mwao. Lakini kama wewe ni mwenye dhambi, biblia inasema, mauti ya pili inakuongojea huko mbeleni, hata baada ya kifo hichi cha kawaida.
Warumi 6:23 “Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu”
Embu yatafakari vizuri maisha yako, hata ukipata kila kitu, na pesa zote duniani ujue ipo siku isiyokuwa na jina utakuwa ni vumbi tu..
Mhubiri 12:7 “Nayo mavumbi kuirudia nchi kama yalivyokuwa, Nayo roho kumrudia Mungu aliyeitoa”.
Mhubiri 9: 5 “kwa sababu walio hai wanajua ya kwamba watakufa; lakini wafu hawajui neno lo lote, wala hawana ijara tena; maana kumbukumbu lao limesahauliwa”.
Zaburi 146: 4 “Pumzi yake hutoka, huurudia udongo wake, Siku hiyo mawazo yake yapotea”.
Ndio kifo kitakukuta, lakini Bwana hapendi ufe katika hali ya dhambi, kwasababu hutakuwa na tumaini tena la maisha baada ya hapo.
Ezekieli 18:32 “Maana mimi sikufurahii kufa kwake afaye, asema Bwana MUNGU; basi ghairini, mkaishi”.
Inawezekana upo katika msiba wa mtu wako wa karabu, fahamu kuwa wakati mwingine Bwana anaruhusu uyapitie hayo, au uyaone hayo ili kukumbusha jambo la muhimu unalotakiwa kulifikiria kwanza.
Mhubiri 7: 14 “Siku ya kufanikiwa ufurahi, Na siku ya mabaya ufikiri. Mungu ameifanya hiyo moja kwenda sambamba na hiyo ya pili, ili mwanadamu asipate kulijua neno lo lote litakalofuata baada yake”.
Unaona?
Lakini ukimpa leo Yesu maisha yako, atakupa tumaini la kweli, atakuondolea hofu la mauti, atakuponya roho yako na wewe utakuwa na amani wakati wote, hata ikitokea umekufa leo, unaouhakika wa kwenda mbinguni.. anasema..
Mathayo 11:28 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha”.
Wokovu ni bure, kwa wakati wote, na unapatikana wakati wowote mtu anapoufungua moyo wake. Kwanini usimkaribishe Yesu mwokozi maishani mwako?
Yohana 3:16 “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele”.
Hivyo ikiwa leo umeguswa ndani yako na unasema sitaki tena kuishi maisha ya kubahatisha, sitaki kuishi maisha ya mguu mmoja ndani mwingine nje, nataka kuwa upande wa Yesu moja kwa moja. Basi uamuzi huo ni wa busara sana kwako, Kwasababu yeye anasema wote wajao kwangu sitawatupa nje kamwe.. Hivyo fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba na Bwana akubariki. >>>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Maran Atha.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
NINI KINATOKEA BAADA YA KIFO?
USIUZE URITHI WAKO.
VIFUNGO VYA GIZA VYA MILELE.
UNYAKUO.
Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!
MIHURI SABA
Naomba kufahamu Nyama zilizosongolewa ni zipi?Je kunywa damu ni dhambi kwa Mkristo?
Nyama zilizosongolewa ni nyama za wanyama ambao hawajachinjwa, na damu yao kumwagika chini.
Kipindi kabla hata ya agano la kwanza(Kale) , Mungu tayari alikuwa ameshampa Nuhu maagizo kuwa asile nyama ya mnyama yoyote pamoja na damu yake ndani yake.
Mwanzo 9:4 “Bali nyama pamoja na uhai, yaani, damu yake, msile”.
Tunaona miaka mingi baadaye Mungu anakuja kumwambia tena Musa jangwani maneno hayo hayo:
Kumbukumbu 12:23 “Ila ujihadhari kwamba usile damu, kwani ile damu ndiyo uhai; na uhai usile pamoja na nyama. 24 Usiile; imwage juu ya nchi kama maji”.
Walawi 17:10 “Kisha mtu awaye yote wa nyumba ya Israeli, au miongoni mwa hao wageni wakaao kati yao, atakayekula damu, ya aina yo yote, nitakunja uso wangu juu ya mtu huyo alaye damu, nami nitamkatilia mbali na watu wake.
11 Kwa kuwa uhai wa mwili u katika hiyo damu; nami nimewapa ninyi hiyo damu juu ya madhabahu, ili kufanya upatanisho kwa ajili ya nafsi zenu; kwani ni hiyo damu ifanyayo upatanisho kwa sababu ya nafsi.
12 Kwa hiyo naliwaambia wana wa Israeli, Hapana mtu miongoni mwenu aliye na ruhusa kula damu, wala mgeni aketiye kati yenu asile damu”.
Lakini tukirudi tena katika agano letu jipya, tunaona moja ya maagizo ambayo mitume wanalipa kanisa la mataifa(yaani sisi) Ni kutokula nyama zilizongolewa( yaani nyama ambazo hazijachinjwa na damu kumwagika)..
Matendo 15:19 “Kwa sababu hiyo mimi naamua hivi; Tusiwataabishe wale waliomgeukia Mungu katika Mataifa;
20 bali tuwaandikie kwamba wajiepushe na unajisi wa sanamu, na uasherati, na nyama zilizosongolewa, na damu.
21 Kwa maana tangu zamani za kale Musa anao watu wahubirio mambo yake; katika kila mji husomwa kila sabato katika masinagogi”.
Sasa swali linakuja Je kwa mantiki hiyo wakristo haturuhusiwi kabisa kula nyama zilizongolewa au kunywa damu?
Ukweli ni kwamba kulingana na mazingira ya wakati ule kwa watu wa mataifa, na ya sasa, ni ngumu kuishi bila kukutana na nyama za namna hiyo.. Kwasababu nyama nyingi siku hizi, hazichinjiwi nyumbani, unazikuta mabuchani, au supermarket, na kule hujui zimechinjwaje chinjwaje.. Hivyo huwezi kuuliza hii nyama iliandiliwaje, vinginevyo hutakaa ule nyama kabisa…Sasa Bwana Yesu kwa kulijua hilo akawaagiza mitume wake, kuwa watakachokutana nacho mbele yao kila mahali mnapokaribishwa wale (Luka 10:8),
Mtume Paulo naye aliliweka wazi hilo kwa wakorintho na kuwaambia..
1Wakorintho 10:25 “Kila kitu kiuzwacho sokoni kuleni, bila kuuliza-uliza, kwa ajili ya dhamiri;
26 maana, Dunia ni mali ya Bwana na vyote viijazavyo”.
Kwamfano Soseji nyingine zinatengenezwa na damu ndani yake, na nyingine hazitengenezwi na damu, Hivyo ukipewa kula bila kuuliza uliza, ukikuta zinauzwa dukani nunua ule bila kuuliza uliza.
Kwasababu sisi agano letu halipo katika vyakula, bali lipo rohoni..vyakula havitubadilishi kitu. Lakini pale inapotokea unachinja mbuzi wako, au kuku wako, au ng’ombe wako nyumbani ni vema ukaimwaga damu ya mnyama huyo chini, usinywe kisusio..Si vema kufanya hivyo, kwasababu tumeshapewa maagizo hayo.
Zaidi ya yote amani ya Kristo iamue ndani yako.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
DAMU YA YESU INANENAJE MEMA KULIKO YA HABILI?
MUNGU AKIKUPITA LEO, HAIMAANISHI KUWA HAJAKUCHAGUA.
USITAFUTE FAIDA YAKO MWENYEWE BALI YA WENGINE.
MAJONZI YA MTUME PAULO KWA NDUGU ZAKE.
HUDUMA YA WALE MASHAHIDI WAWILI.
UNYAKUO.
SWALI: Je tunaruhusiwa kujipaka mafuta au kujipulizia marashi/manukato (perfumes)?
JIBU: Sio vibaya kujipaka mafuta usoni au mwilini, ili kuondoa ule mpauko wa asili, mafuta hususani yale ya asili ni mazuri kwa ngozi, lakini pia sio amri kwamba lazima tujipake mafuta, hata hivyo ngozi zetu huwa zinatoa zenyewe mafuta yake ya asili.
Lakini yapo mafuta ya kuchubua ngozi, na yenye marashi makali, hayo ni kinyume na maandiko kuyatumia kwasababu lengo lake ni kubadilisha maumbile, ambayo maudhui yake ni Udunia!..Biblia inasema miili yetu ni hekalu la Roho Mtakatifu na pia miili yetu sio mali yetu wenyewe, ni mali ya Mungu, hivyo hatupaswi kuibadilisha kutoka katika hali yake ya asili na kuifanya tutakavyo sisi (1Wakorintho 6:19).
Sasa unaweza kuuliza ni wapi katika agano jipya tumepewa ruhusa ya kutumia mafuta?
Mathayo 6: 16 “Tena mfungapo, msiwe kama wanafiki wenye uso wa kukunjamana; maana hujiumbua nyuso zao, ili waonekane na watu kuwa wanafunga. Amin, nawaambia, wamekwisha kupata thawabu yao.
17 Bali wewe ufungapo, JİPAKE MAFUTA KİCHWANİ, UNAWE USO;
18 ili usionekane na watu kuwa unafunga, ila na Baba yako aliye sirini; na Baba yako aonaye sirini atakujazi”
Hayo ni maneno yaliyozungumzwa na Bwana Yesu mwenyewe.
Swali lingine ni je! Ni mafuta gani yanayofaa?..Hakuna orodha maalum ya mafuta yanayofaa, kikubwa mafuta yoyote yale yawe ya kiwandani au ya asili ambayo hayana kemikali nyingi na hayana marashi makali yanafaa kutumika.
Na Marashi ni hivyo hivyo, yapo marashi ya nguo..ambayo lengo lake ni kudhibiti nguo isitoe harufu mbaya aidha ya jasho au ya kitu kingine kisichofaa. (Katika mazingira fulani)
Nayo pia sio vibaya kuyatumia, ilimradi tu yasiwe na maudhui ya kishetani. Marashi yanayotumika mengi siku hizi yana maudhui ya kidunia, marashi mtu anayotumia ambapo mtu aliyesimama mita 2 mbele yake au nyuma yake anasikia harufu yake, tayari lengo la marashi hayo sio kudhibiti harufu bali kuvuta hisia kutoka kwa mwingine…jambo ambalo sio sawa.
Kiwango cha marashi kinapaswa kiwe kidogo sana)..kiasi kwamba mpaka pua ifike karibu na nguo ndipo isikike..(na hiyo ni kama kuna ulazima wa kuyatumia kutokana na mazingira, lakini kama hakuna ulazim hayapaswi kutumika kabisa).
Na zaidi sana, mafuta mengi tunayotumia au sabuni zina kiwango tosha cha marashi ambayo hatuhitaji kuongeza mengine juu yake.
Katika biblia marashi yametafsiriwa sehemu kadha wa kadha kama “Marhamu” au “Manukato”. Unaweza kupitia mistari ifuatayo binafsi (Mathayo 26:7-13, Marko 14:3, Marko 16:1).
Lakini zaidi sana Marashi yetu yanayompendeza Mungu ni Maombi yetu kwake, na utakatifu wetu.
Ufunuo 5:8 “Hata alipokitwaa kile kitabu, hao wenye uhai wanne na wale wazee ishirini na wanne wakaanguka mbele za Mwana-Kondoo, kila mmoja wao ana kinubi, na vitasa vya dhahabu vilivyojaa MANUKATO, AMBAYO Nİ MAOMBİ YA WATAKATİFU”.
2Wakorintho 2:14 “Ila Mungu ashukuriwe, anayetushangiliza daima katika Kristo, na kuidhihirisha harufu ya kumjua yeye kila mahali kwa kazi yetu.
15 Kwa maana sisi tu manukato ya Kristo, mbele za Mungu, katika wao wanaookolewa, na katika wao wanaopotea;
16 katika hao wa pili harufu ya mauti iletayo mauti; katika hao wa kwanza harufu ya uzima iletayo uzima. Naye ni nani atoshaye kwa mambo hayo”
Hivyo tukiwa maridadi wa mwilini, tukanukia vizuri na huku rohoni tunatoa harufu mbaya, hatusali, hatufungi, hatuombi, hatuishi maisha ya kumpendeza yeye..basi mbele za Mungu tunapeleka harufu mbaya.
Lakini tukiwa waombaji, tukimwomba Mungu rehema, na neema..pamoja na tukiwaombea na wengine na kuliombea kanisa, na tukiishi maisha masafi, basi tutakuwa ni lulu mbele za Mungu.
Mungu atasaidie katika hilo.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
SWALI: Ni jeshi gani la Mbinguni ambalo Mungu aliwaacha wana wa Israeli waliabudu katika Matendo 7:42? Je ni Malaika au?
JIBU: Matendo 7: 41 “Wakafanya ndama siku zile, wakaleta dhabihu kwa sanamu ile, wakafurahia kazi za mikono yao.
42 Basi Mungu akaghairi, akawaacha ili waliabudu jeshi la mbinguni, kama ilivyoandikwa katika chuo cha manabii, Je! Mlinitolea mimi dhabihu na sadaka Miaka arobaini katika jangwa, enyi nyumba ya Israeli?”
Habari hii inawazungumzia wana wa Israeli wakati wanatoka Misri. Wakiwa jangwani biblia inasema walikuwa wakikengeuka mara kadhaa, walikuwa wakimwacha Mungu na kugeukia kuchonga sanamu, na wakati mwingine kumjaribu Mungu (Kutoka 17:2).
Lakini kuna jambo lingine tunaliona walilokuwa wanalifanya ambalo lilikuwa ni machukizo kwa Mungu, na hilo si lingine zaidi ya KULIABUDU JESHI LA MBINGUNI.
Sasa swali la msingi hapo ni je! Hilo jeshi ni lipi?, ni malaika au ni nini?.
Jibu ni kwamba si Malaika, bali ni miungu ya kipagani.
Si kila mahali kwenye biblia palipoandikwa neno “mungu” panamaanisha “Mungu wa mbingu na nchi”, vivyo hivyo sio kila mahali katika biblia palipoandikwa neno “bwana” panamaanisha “Bwana Mungu wa mbingu na nchi”…hali kadhalika sio kila mahali katika biblia palipoandikwa neno “mbingu” au “mbinguni”, panamaanisha “Mbinguni malaika watakatifu walipo”..
Dini karibia zote zinaamini kwamba kuna mbingu..kwamba kuna mahali huko juu ambapo kuna viumbe watakatifu wanaishi,..Na nyingine zinaamini huko mbinguni kuna miungu mingi, kuna jeshi kubwa la miungu, ambayo yote inastahili kuabudiwa. Kwamfano dini ya kihindu tu peke yake ina zaidi ya miungu milioni 330.
Sasa ikatokea kwa mtu ambaye ni mkristo, ambaye ameshajua ukweli wote kwamba Mungu ni mmoja tu aliyeko mbinguni ambaye anaabudiwa katika roho na kweli.. akaiacha hiyo imani na kisha akaenda kujiunga na imani nyingine(kama hiyo ya kihundu) inayoamini kwamba mbinguni kuna miungu mingi, na akaenda kuiabudu hiyo miungu yao. Hapo ni sawa na kusema “AMEKWENDA KULİSUJUDİA JESHİ LA MBİNGUNİ”..na si mbingu ile ambayo malaika watakatifu wapo bali ni mbingu ya kihindu, ambayo kiuhalisia haipo! ni uongo uliotengenezwa na shetani tu kuwadanganya watu kuwa kuna mbingu yenye miungu mingi!,
Ni agenda ya shetani na mapepo yake Kutafuta kuabudiwa na kuwapotosha watu wa Mungu. Hiyo idadi yote ya miungu wanayoiabudu ni mapepo yanayojiguza na kuchukua sura ya hivyo wanavyoviabudu. (zingatia: wengi wanaoabudu hiyo miungu, sio watu wabaya na wala si maadui zetu, wengi wao ni watu wazuri, wanafanya hayo kwasababu bado hawajaujua ukweli, au macho ya mioyo yao bado hayajafumbuliwa, kwahiyo wanaabudu vitu wasivyovijua, hivyo ni jukumu letu wewe na mimi kuwapelekea injili na kuwaombea!, ili macho yao yafumbuliwe wapate kuona na kuokolewa Matendo 17:29-31).
Kwahiyo Jeshi la mbinguni linalozungumziwa hapo sio Malaika waliopo mbinguni, bali ni miungu iliyopo mbinguni huko angani, ambayo kiuhalisia ni shetani na mapepo yake.
Na malkia wa mbinguni aliyezungumziwa pia katika Yeremia 7:18, 44:17-25 sio Bikira Mariamu wala sio Malaika fulani wa kike aliyeko mbinguni bali ni mungu fulani wa kipagani, wanayedai kwamba yupo mbinguni (kwa maelezo marefu utatutumia ujumbe inbox), ambaye ni Pepo!.
Mwisho ni muhimu kuchukua tahadhari!.. pale tunapoonywa mara nyingi!…Hapo kwenye matendo 7:42, biblia inasema “ Basi MUNGU AKAGHAİRİ, AKAWAACHA ili waliabudu jeshi la mbinguni,”.
Litazame hilo neno kwa makini!..Mungu akaghairi!, akawaacha!! İli waliabudu jeshi la mbinguni…Ni jambo la kuogopesha sana pale Mungu anapoghairi juu yako, na kukuacha uendelee kufanya unayoyafanya!…hilo ni jambo la kuogopesha sana!..Anaabudu masanamu unayodhani ni watakatifu Fulani wa mbinguni, na umeonywa mara nyingi husikii, hapo unamfanya Mungu aghairi juu yako.
Warumi 1:28 “Na kama walivyokataa kuwa na Mungu katika fahamu zao, Mungu aliwaacha wafuate akili zao zisizofaa, wayafanye yasiyowapasa”
2Wathesalonike 2:10 “na katika madanganyo yote ya udhalimu kwa hao wanaopotea; kwa sababu hawakukubali kuipenda ile kweli, wapate kuokolewa. Kwa hiyo Mungu awaletea nguvu ya upotevu, wauamini uongo”.
Jiupeshe na ibada za sanamu ni dhambi, jiepushe na mambo yote maovu na mwisho soma neno kwa bidii..
Bwana atubariki.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
AINA YA MAADUI UTAKAOKUTANA NAO KATIKA SAFARI YAKO YA WOKOVU.
AINA YA MAADUI UTAKAOKUTANA NAO KATIKA SAFARI YAKO YA WOKOVU.
CHUKIZO LA UHARIBIFU
MUNGU WANGU,MBONA UMENIACHA?.
Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!
2Wakorintho 13:14 “Neema ya Bwana Yesu Kristo, na pendo la Mungu, na ushirika wa Roho Mtakatifu ukae nanyi nyote”.
Hii ni salamu ya kumalizia ambayo mtume Paulo aliwaandikia wakorintho, na watu wote watakaousoma waraka huo (ikiwemo mimi na wewe).
Maneno haya, yamegusa Nyanja zote tatu za Kusudi la Mungu kwetu sisi wanadamu.
> Paulo anaanza kwa kusema, Neema ya Bwana Yesu Kristo, ikae nasi; Akiwa na maana kuwa mpaka sisi tukamilike, mpaka sisi tushinde, tunaihitaji hii neema ya Yesu Kristo wakati wote itembee na sisi, tukipungukiwa neema, basi ni ngumu kuweza kuushinda ulimwengu. Na neema hii inaanza kutembea juu ya mtu kwa mara ya kwanza pale anapookoka.
> Anasema tena, Pendo la Mungu likae nasi: Ni kwa njia ya upendo Mungu alitukuomboa (Yohana 3:16). Hivyo na sisi tukiukosa Upendo, haijalishi tutakuwa washirika wazuri kiasi gani, haijalishi tutafanya miujiza mingi kiasi gani, tutanena kwa lugha za malaika nyingi kiasi gani, bado sisi tutabakia kuwa si kitu. Hivyo Pendo la Mungu linapokaa ndani yetu basi Mungu anakuwa karibu na sisi. Na pendo la Mungu ndio lile linalozungumziwa katika 1Wakorintho 11:1-8
Na ndio huo Paulo alikuwa analiombea kanisa ukae ndani yao.
> Anamalizia na kusema pia Ushirika wa Roho Mtakatifu ukae nanyi nyote; Hii ikiwa na maana palipo na Roho Mtakatifu pana ushirika.. Sisi kama wakristo tuliookoka ni jukumu letu kuutunza ushirika wa Roho tukinia mamoja, tukiifanya kazi ya Mungu..
Waefeso 4:3 “na kujitahidi kuuhifadhi umoja wa Roho katika kifungo cha amani.
4 Mwili mmoja, na Roho mmoja, kama na mlivyoitwa katika tumaini moja la wito wenu.
5 Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja.
6 Mungu mmoja, naye ni Baba wa wote, aliye juu ya yote na katika yote na ndani ya yote”.
Mambo haya matatu yakienda pamoja na sisi, basi Mungu naye ataenda pamoja na sisi, lakini tukipungukiwa kimoja wapo, aidha neema, au Upendo, au Ushirika, ni ngumu kusimama kama Kanisa.
Hivyo mimi na wewe tujitathmini ni wapi, hatujakamilisha, kisha tukamilishe, Na Bwana atusaidie.
Shalom.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
UNYAKUO.
KWANINI MUNGU ALIMTUMIA MUSA KWA VIWANGO VILE?
UPONYAJI WA ASILI
JE UDHAIFU WANGU UNAWEZA KUZUIA INJILI?
ADAM NA EVA.
Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!
Kibanzi Na Boriti, kwenye biblia vinamaanisha nini?
Boriti ni kipande kikubwa sana cha mbao, kinaweza kikawa ni ki-gogo, au nguzo, au mbao yoyote pana..
Lakini kibanzi, ni kichembe kidogo sana cha mbao, kama mchanga, hata wakati mwingine kufikia kuwa kama vumbi la mbao ambalo ni ngumu sana kuliona. Hicho ndicho kibanzi.
Sasa Bwana Yesu alitoa mfano huo, wa picha ili kuweka msisitizo kile alichotaka kukisema, yaani katika hali ya kawaida, kama wewe huwezi kuona nguzo iliyosimama mbele ya macho yako inayokuzuia usione kabisa, utaona vipi vumbi la mbao lililo katika jicho la mwenzako?..Umeona moja kwa moja huo ni unafki..
Vivyo hivyo na sisi kabla hatujawahukumu watu, tuyachunguze maisha yetu Je! hayo wanayoyafanya Je, hayapo ndani yetu na sisi? Kabla hujamwambia Fulani acha usengenyaji, Je! na wewe si msengenyaji? Kama sivyo basi ni heri ukae tu kimya, kwasababu mistari ya juu yake inasema, kipimo kile kile tuhukumucho ndicho tutakachokuhumiwa na sisi.
Mathayo 7:1 “Msihukumu, msije mkahukumiwa ninyi.
2 Kwa kuwa hukumu ile mhukumuyo, ndiyo mtakayohukumiwa; na kipimo kile mpimiacho, ndicho mtakachopimiwa.
3 Basi, mbona wakitazama kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako, na boriti iliyo ndani ya jicho lako mwenyewe huiangalii?
4 Au utamwambiaje nduguyo, Niache nikitoe kibanzi katika jicho lako; na kumbe! Mna boriti ndani ya jicho lako mwenyewe?
5 Mnafiki wewe, itoe kwanza ile boriti katika jicho lako mwenyewe; ndipo utakapoona vema kukitoa kile kibanzi katika jicho la ndugu yako.
Bwana atusaidie sote tuyashinde hayo.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
https://wingulamashahidi.org/ikabodi-maana-yake-ni-nini/
KAMA MMOJA TU NDIO HIVI! SI ZAIDI 153?
UNYAKUO.
MKUMBUKE MKE WA LUTU.
CHUKIZO LA UHARIBIFU
Israeli ipo bara gani?
Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!
Jiunge na channel yetu ya Whatsapp, ujifunze biblia na upate Neno la siku kila asubuhi. kwa link hii >>> https://chat.whatsapp.com/GWxBOH2GXncIc0pwVIhnch
Mistari ya biblia ya faraja.
Unaweza ukawa unapitia katika wakati mgumu, wakati wa mateso, wakati wa majaribu, wakati wa jangwa, wakati wa shida wewe kama mkristo kwa ajili ya imani yako,. Lakini nachoweza kukwambia ni kuwa biblia peke yake, ndiyo inayoweza kukupa faraja ya kweli.. Haijalishi utaambiwa maneno elfu kumi ya faraja na wanadamu, lakini ni biblia pekee ndiyo inayoweza kukupa faraja ya kweli.
Hivyo itafakari mistari ifuatayo, ni lipo jambo ambalo litakutia nguvu katika safari yako ya Imani..
Unlock the Power of crystals: Elevate Your Space with Feng Shui Essentials! Discover the Magic of Crystals for a Harmonious Home. Our store offers a curated selection of premium feng shui products, including exquisite crystals that bring positive energy and balance to your surroundings. Embrace the beauty and serenity that crystals can bring into your life. Enhance your living space with the timeless allure of crystals today!
Wafilipi 4:13 “Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu”.
Isaya 41:10 “usiogope, kwa maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia, naam, nitakushika kwa mkono wa kuume wa haki yangu”.
Isaya 40:31 “bali wao wamngojeao Bwana watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia”.
Kumbukumbu 31: 6 “Iweni hodari na moyo wa ushujaa, msiogope wala msiwahofu; kwa maana Bwana, Mungu wako, yeye ndiye anayekwenda pamoja nawe, hatakupungukia wala kukuacha”.
Isaya 40:29 “Huwapa nguvu wazimiao, humwongezea nguvu yeye asiyekuwa na uwezo”.
1Wakorintho 10:13 “Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu; ila Mungu ni mwaminifu; ambaye hatawaacha mjaribiwe kupita mwezavyo; lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea, ili mweze kustahimili”.
Kutoka 15:2 “Bwana ni nguvu zangu, na wimbo wangu; Naye amekuwa wokovu wangu. Yeye ni Mungu wangu, nami nitamsifu; Ni Mungu wa baba yangu, nami nitamtukuza”.
Kumbukumbu 20: 4 “kwa maana Bwana, Mungu wenu, ndiye awaandamaye kwenda kuwapigania juu ya adui zenu, ili kuwaokoa ninyi”.
2Wakorintho 12:9 “Naye akaniambia, Neema yangu yakutosha; maana uweza wangu hutimilika katika udhaifu. Basi nitajisifia udhaifu wangu kwa furaha nyingi, ili uweza wa Kristo ukae juu yangu”.
Tembelea washirika wetu, https://www.swisswatch.is/product-category/richard-mille/ – viongozi katika viatu vya mtindo!
Isaya 12:2 “Tazama, Mungu ndiye wokovu wangu; Nitatumaini wala sitaogopa; Maana Bwana YEHOVA ni nguvu zangu na wimbo wangu; Naye amekuwa wokovu wangu”.
Mathayo 6:34 “Basi msisumbukie ya kesho; kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe. Yatosha kwa siku maovu yake”.
Zaburi 27:1 “Bwana ni nuru yangu na wokovu wangu, Nimwogope nani? Bwana ni ngome ya uzima wangu, Nimhofu nani”?
Zaburi 31: 24 “Iweni hodari, mpige moyo konde, Ninyi nyote mnaomngoja Bwana”.
Zaburi 73:26 “Mwili wangu na moyo wangu hupunguka, Bali Mungu ni mwamba wa moyo wangu Na sehemu yangu milele”.
Zaburi 29: 11 “Bwana atawapa watu wake nguvu; Bwana atawabariki watu wake kwa amani”.
Zaburi 23:4 “Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, Gongo lako na fimbo yako vyanifariji”.
Zaburi 118:14 “Bwana ni nguvu zangu na wimbo wangu, Naye amekuwa wokovu wangu”.
Habakuki 3:19 “YEHOVA, aliye Bwana, ni nguvu zangu, Yeye huifanya miguu yangu kuwa kama ya kulungu, Naye ataniendesha katika mahali pangu palipoinuka”.
Yohana 16:33 “Hayo nimewaambieni mpate kuwa na amani ndani yangu. Ulimwenguni mnayo dhiki; lakini jipeni moyo; mimi nimeushinda ulimwengu”.
2Wathesalonike 3:3 “Lakini Bwana ni mwaminifu, atakayewafanya imara na kuwalinda na yule mwovu”.
Luka 1:37 “kwa kuwa hakuna neno lisilowezekana kwa Mungu”.
Yeremia 29:11 “Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema Bwana, ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho”.
Wafilipi 1:6 “Nami niliaminilo ndilo hili, ya kwamba yeye aliyeanza kazi njema mioyoni mwenu ataimaliza hata siku ya Kristo Yesu”;
Zaburi 34:8 “Onjeni mwone ya kuwa Bwana yu mwema; Heri mtu yule anayemtumaini”.
Mathayo 11:28 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha”.
Jiunge na Forum ya Neno la Mungu hapa ya mada zaidi zihusuzo Faraja >> FARAJA FORUMS
Inawezekana pia hujaokoka, lakini leo hii unataka Yesu asikupite bila kuyaokoa maisha yako. Unasema mimi na dunia sasa basi, mimi na dhambi basi..Hivyo Kama umeamua leo kumgeukia Mungu kwa moyo wako wote, yeye mwenyewe anasema, “kila ajaye kwangu sitamtupa Nje kamwe”..Kwahiyo Leo hii Yesu ataingia ndani ya maisha yako kama umeamua kweli kumfuata…hivyo kama upo tayari fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba..>>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Bwana akubariki.
Ikiwa utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu, kwa njia ya email, au whatsapp yako basi tutumie ujumbe kwenye namba hii tukuweke : +255789001312
Mada Nyinginezo:
Tukiachilia mbali, Eneo linaloitwa Arabuni ambalo limetajwa sana katika biblia, .
Kama tunavyosoma katika vifungu vifuatavyo..
2Nyakati 9:14 “mbali na ile waliyoileta wachuuzi na wafanya biashara; tena wafalme wote wa Arabuni, na maliwali wa nchi wakamletea Sulemani dhahabu na fedha”.
Isaya 21:13 “Ufunuo juu ya Arabuni. Ndani ya msitu wa Arabuni mtalala, Enyi misafara ya Wadedani”.
Yeremia 25: 13 “Ufunuo juu ya Arabuni. Ndani ya msitu wa Arabuni mtalala, Enyi misafara ya Wadedani”.
Wagalatia 1:17 “wala sikupanda kwenda Yerusalemu kwa hao waliokuwa mitume kabla yangu; bali nalikwenda zangu Arabuni, kisha nikarudi tena Dameski”.
Wagalatia 4:25 “Maana Hajiri ni kama mlima Sinai ulioko Arabuni, umelingana na Yerusalemu wa sasa; kwa kuwa anatumika pamoja na watoto”.
Eneo ambalo walikuwa wanaishi jamii ya watu wa kiarabu.. Au kwa jina lingine linaitwa Arabia.Tazama picha juu.
Lakini Neno hili limetajwa kwa namna nyingine, katika biblia kama tunavyosoma katika vifungu vifuatavyo
2Wakorintho 1:22 “naye ndiye aliyetutia muhuri akatupa arabuni ya Roho mioyoni mwetu”.
2Wakorintho 5:5 “Basi yeye aliyetufanya kwa ajili ya neno lilo hilo ni Mungu, aliyetupa arabuni ya Roho”.
Waefeso 1:3 “Nanyi pia katika huyo mmekwisha kulisikia neno la kweli, habari njema za wokovu wenu; tena mmekwisha kumwamini yeye, na kutiwa muhuri na Roho yule wa ahadi aliye Mtakatifu.
14 Ndiye aliye arabuni ya urithi wetu, ili kuleta ukombozi wa milki yake, kuwa sifa ya utukufu wake”.
Sasa Mungu alipotugawia ahadi zake za uzima wa milele na nyinginezo, hakutaka kutupa mikono mitupu tu hivi hivi bila uthibitisho wowote, Hivyo ili kututhibitishia kuwa ahadi zake ni kweli alitupa uhakika huo kwa kutugawia Roho Mtakatifu, kama garantii au tunaweza kusema, kuponi, ya kuwa ahadi zake tutafikia, au atatutimizia.. Sasa hiyo garantii/kuponi ndio inayoitwa arabuni.
Ukipokea Roho Mtakatifu basi unayo arabuni ya uzima wa milele, kama alivyowaahidia wale waliomwamini.
Ukipokea Roho Mtakatifu basi una uhakika kuwa wewe ni mbarikiwa wa Mungu, hakuna laana yoyote inayoweza kukaa juu yako.
Ukipokea Roho Mtakatifu basi maombi yako ni hakika kuwa yanasikiwa na kujibiwa mbinguni, sawasawa na ahadi za Yesu kwa wote waliomwamini.
Lakini ukiwa huna Roho Mtakatifu, na unasema umeokoka, bado mbinguni hutaenda..Kama vile maandiko yanavyosema..
Warumi 8:9 “…Lakini mtu awaye yote asipokuwa na Roho wa Kristo, huyo si wake”.
Hivyo kama na wewe unataka upate hii arabuni(garantii) ya urithi wa ahadi za Mungu zote za mwilini na rohoni,, basi ni sharti umpokee Roho Mtakatifu. Na mtu anampokea Roho Mtakatifu kwa kuzaliwa mara ya pili.
Mtu anazaliwaje mara ya pili?
Pale unapotubu dhambi zako kwa kumaanisha kabisa kuziacha, , na baada ya kutubu ukawa tayari kwenda kubatizwa katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo, sawasawa na Mdo 2:38, hapo utakuwa tayari umeshazaliwa mara ya pili.
Na moja kuwa moja, kuanzia huo wakati na kuendelea Roho anashuka ndani yako..Na unakuwa tayari umeshapokea garantii hiyo(arabuni) ya kuwa wewe ni mwana wa ahadi… Hivyo kama hutarudi nyuma utaendelea tu kuishi katika maisha matakatifu ya wokovu ya kumpendeza Mungu na kudumu katika ushirika wa Mungu..Ni uhakika kuwa hata ukifa usiku huo huo, wewe ni wa mbinguni tu mrithi wa ahadi zote za Mungu..
Hivyo kama hujaokoka, basi anza sasa kufuata hatua hizo kwa moyo wako wote..Kama unahitaji leo kumpa Yesu maisha yako basi fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba.>>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Na ikiwa utahitaji kubatizwa usisite kuwasiliana nasi kwa namba hizi +255789001312: Ubatizo ni bure, na unafanyika pindi tu mtu anapotubu dhambi zake..Hakuna madarasa ya kupitia, wala hakuna kutoa fedha, kwasababu biblia haitufundishi kanuni hizo..
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Yuko azuiaye sasa hata atakapoondolewa! ni nani huyo?
USIFIKIRI FIKIRI.
KILA MMOJA WENU AJUE KUUWEZA MWILI WAKE.
https://wingulamashahidi.org/ikabodi-maana-yake-ni-nini/
AMELAANIWA AANGIKWAYE MSALABANI.
UNYAKUO.
SWALI: Biblia inamaanisha nini inaposema “Usimtokose mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.”
JIBU: Huu ni msemo ambao umeonekana ukipachikwa katikati ya vifungu kadha wa kadha kwenye biblia..
Kwa mfano utaona.. pale kwenye Kutoka 23:18-19 inasema..
18 Usisongeze damu ya dhabihu zangu pamoja na mkate uliotiwa chachu, wala mafuta ya sikukuu yangu usiyaache kusalia hata asubuhi.
19 Ya kwanza ya malimbuko ya nchi yako utayaleta na kuyatia ndani ya nyumba ya Bwana, Mungu wako. Usimtokose mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.
Ukisoma tena..Kutoka 34:25-26, utaona inasema hivi..
“25 Usisongeze damu ya sadaka yangu pamoja na mkate uliotiwa chachu; wala hiyo sadaka ya sikukuu ya pasaka haitasazwa hata asubuhi.
26 Vitu vya kwanza vya malimbuko ya nchi yako utavileta na kuvitia ndani ya nyumba ya Bwana Mungu wako. Usimtokose mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake”.
Ukirudi tena kwenye Kumbukumbu 14:21 nayo pia utaona ikisema.
“Msile nyamafu yo yote; waweza kumpa mgeni aliye ndani ya malango yako, ili apate kula; au kumliza mtu wa mataifa; kwa kuwa wewe u taifa takatifu kwa Bwana, Mungu wako. Usimtokose mwana-mbuzi katika maziwa ya mamaye”.
Sasa pale anaposema, usimtokose mwana-mbuzi, katika maziwa ya mama yake, anamaanisha kumchemsha mtoto wa mbuzi, kwa maziwa ya mama yake, yaani badala ya kumchemsha kwenye maji, wewe unachukua yale maziwa anayoyanyonya kutoka kwa mama yake na kumchemshia nayo..
Kwa namna ya kawaida ni kitendo kisicho cha kiungwana chenye ukakasi kidogo, hata kwako wewe unayesikia eti?..Utajiuliza ni kwanini ufanye hivyo? Kwani hakuna maji ya kumchemshia, au kitu kingine mpaka utumie maziwa, tena yale yale ya mama yake? Ni sawa na nguruwe aliyezaa mtoto, halafu unampa mtoto wake mwenyewe amle kama chakula chake..sasa hiyo ndio picha iliyopo hapo.
Ni kitendo kinachoonyesha unyama si unyama, ukosefu wa nidhamu..?
Ni utaratibu na mfumo wa kipagani ambao ulikuwa unafanyika na watu wa mataifa wasiomjua Mungu, walikuwa wanafanya hivyo kwa sababu za kishirikina, ni kama mila zinazoendelea siku hizi, hivyo Mungu aliwaonya wana wa Israeli wasifanye mambo kama hayo, kwasababu ni machukizo mbele zake, ni Utaratibu ambao hauna tofauti na ule wa kuwapitisha watoto kwenye moto, (soma 2Wafalme 21:6, 2Wafalme 16:3).
Hata sasa, wengi wetu tunafanya kafara kama hizo rohoni?.
Tunamtolea Mungu dhabihu zilizochanganyikana na mambo ambayo Mungu ameyakataza, tunafanya mambo kama watu wa mataifa. Tunamsifu Mungu na huku vinywa vyetu vimejaa matusi, na masengenyo, chuki na visasi, tunamtolea Mungu na huku biashara zetu ni haramu, tunahudhuria kanisani lakini tunaendelea kudumisha mila zetu za kishirikina, hali kadhalika tumeokoka lakini heshima kwa mzazi haipo, na heshima kwa Watoto wetu haipo (hiyo yote katika roho ni sawa na kumtokosa mwanambuzi katika maziwa yake) N.k.
Bwana atusaidie, tuzishike amri zake na tumpendeze yeye.
Bwana atuokoe na kutubariki..
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Imani ya mitume (Apostle’s creed), inapatikana wapi kwenye biblia?
Imani ya mitume ambayo unaisikia mara kwa mara ikikiriwa katika baadhi ya madhehebu hususani Katoliki, Lutherani, na Anglikana, haipo mahali popote katika maandiko, na wala haikuwahi kukikiriwa na mitume wa Kristo sehemu yoyote.
Imani hii, ilikuja kuaandikwa miaka mingi mbeleni(zaidi ya miaka 300),baada ya mitume kuondoka, waliiandika wakizingatia kiini cha wazo kuu la mitume walichokuwa wanaamini katika maandiko.
Na kimsingi imani hii ipo kimaandiko. Hivyo mtu kuikiri hakuna shida, kwasababu haimpotezi katika misingi ya imani ya biblia.
Inasema hivi.
Namwamini Mungu Baba mwenyezi, muumba wa mbingu na nchi, na Yesu Kristo, mwana wake wa pekee, Bwana wetu.
Aliyechukuliwa mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu. Akazaliwa na bikira Mariamu. Akateswa zamani za Pontio Pilato. Akasulubiwa. Akafa. Akazikwa.
Akashuka mahali pa wafu. Siku ya tatu akafufuka. Akapaa mbinguni. Ameketi mkono wa kuume wa Mungu Baba mwenyezi. Kutoka huko atakuja kuwahukumu walio hai na wafu.
Namwamini Roho Mtakatifu, kanisa takatifu lililo moja, ushirika wa watakatifu, ondoleo la dhambi, ufufuo wa wafu na uzima wa milele.
Amina.
Jambo la kuzingatia ni kuwa, ukiikiri/usipoikiri sio tiketi ya wewe ni mkristo, au utakwenda mbinguni, huu ni utaratibu tu au mapokeo tu ya baadhi ya wakristo. kitachokufa wewe uwe mkristo, ni kuamini, kutubu na kuoshwa dhambi zako kwa damu ya YESU Kristo, kwa njia ya ubatizo( sawasawa na Matendo 2:38).
Na ubatizo sahihi wa kimaandiko ni ule wa kuzamwishwa katika maji mengi,(Yohana 3:23) na kwa jina la Yesu Kristo.
Hivyo kama utahitaji upate ubatizo huu sahihi. Na Kama utapenda tuwe tunakutumia masomo ya biblia kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Je! Ni sahihi kutumia maji ya upako,katika kufanya maombezi?
Je mtu akifa anakuwa hana dhambi tena?
KWA KUWA NGUVU ZA MBINGUNI ZITATIKISIKA.
FANYIKA SIPORA WA KRISTO, UNYAKUO UPO KARIBU.
MKUMBUKE MKE WA LUTU.
CHUKIZO LA UHARIBIFU
MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.