Category Archive Home

JE! HAMPOTEI KWA SABABU HII?

Jina la Bwana wetu Yesu libarikiwe daima. Karibu tuyatafakari maandiko pamoja ndugu yangu.

Wakati ule masadukayo walimfuata Bwana Yesu, na kumuuliza maswali ambayo, ndio yaliyowafanya waamue kuwa  masadukayo kama walivyo wasioamini  kuwa kuna kitu kinachoitwa ufufuo wa wafu. Na swali lenyewe lilikuwa ni kuhusu ndoa baada ya kifo..Walikuwa na sababu nzuri kabisa za kufikirika kwa akili za kibinadamu, kwamba kama kiyama ipo basi Musa asingeruhusu mtu kuoa mke wa mtu baada ya kufa, ili huko ng’ambo kusiwe na migongano ya kindoa,.Lakini kama aliruhusu kuoa mke wa marehemu, ni wazi kuwa mambo yote ni ya hapa hapa duniani, hakuna kufufuliwa wafu.

Embu Tusome kwa ufupi habari yenyewe na pale mwishoni lipo jambo ambalo Bwana atatufundisha siku ya leo..

Anasema..

Marko 12:18 “Kisha Masadukayo, watu wasemao ya kwamba hakuna kiyama, wakamwendea, wakamwuliza na kusema,

19 Mwalimu, Musa alituandikia ya kwamba ndugu ya mtu akifa, akamwacha mkewe wala hana mtoto, ndugu yake amtwae yule mkewe akampatie ndugu yake mzao.

20 Basi kulikuwa na ndugu saba, wa kwanza akatwaa mke, akafa, asiache mzao.

21 Wa pili naye akamtwaa akafa, wala yeye hakuacha mzao. Na wa tatu kadhalika;

22 hata na wote saba, wasiache mzao. Mwisho wa wote yule mwanamke akafa naye.

23 Basi, katika kiyama atakuwa mke wa yupi katika hao? Maana wote saba walikuwa naye.

24 Yesu akajibu, akawaambia, JE! HAMPOTEI KWA SABABU HII, KWA KUWA HAMYAJUI MAANDIKO WALA UWEZA WA MUNGU?

Kama tunavyosoma hapo kulingana na maneno ya Bwana Yesu, aliona watu hao wamepotea, na kupotea kwako kulichangiwa na sababu mbili kubwa, ya kwanza 1) Walikuwa hawayajui maandiko 2) Walikuwa hawaujui uweza wa Mungu.

Hizi ni sababu kuu ambazo zinaweza kumfanya mtu apotee hata leo hii, aidha katika Dini za uongo kama hawa Au arudi nyuma katika ulimwengu kabisa aseme, haya mambo hayawezekani.

  1. Tukianzana na kutokuujua uweza wa Mungu

Hawa mafarisayo, waliishi kwa fikra za kibinadamu na sio kwa fikra za Ki-Mungu, hawakukaa kujiuliza hao malaika wanaishije ishije huko mbinguni, bila kuoana au kuzaliana lakini bado wanaishi kwa furaha mbele za Mungu. Hata leo hii, Hawakujua kuwa Mungu pia anao uwezo wa kuwafanya kama Malaika. Akaondoa katika miili yao tamaa za mwili, wakawa ni miili ya utukufu isiyokuwa na mapungufu, isiyosinzia, isiyoumwa, isiyochoka kama wao..Hilo hawakuliwaza, kwasababu hawakuujua uweza wa Mungu kuwa unaweza kufanya na hilo pia.

Imani kama hizo hata leo zipo katika baadhi ya dini, wakidhani kuwa mtu akifa atakwenda kupewa wake 70 huko mbinguni. Hiyo yote ni kwasababu hatuujui uweza wa Mungu.

Kukosa kuujua uweza wa Mungu hata sasa, kunawafanya watu wengi, wapotee sana, wakidhani pia Mungu hawezi kuwaokoa wanadamu wakiwa hapa duniani..kwa kuwafanya wawe watakatifu..Na hiyo inawapelekea wajidanganye hivyo hivyo kwamba hakuna mtu anayeweza kushinda dhambi akiwa duniani, na matokeo yake wanakufa katika dhambi zao, na mwisho wa siku wanajikuta wapo kuzimu.

Kumbe hawajua uweza huo wa kufanywa wakamilifu hautoki kwa mwanadamu bali kwa Mungu pale mtu anapomwamini na kumpokea. Alisema..

Yohana 1:12 “Bali wote waliompokea ALIWAPA UWEZO wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake;”

Mtu akimwamini Kristo, na kumtii yeye, kitu kinachotokea kwake ni kupokea uwezo mpya, wa kufanyika mwana wake wa kushinda dhambi. Ukishindwa kuyajua hayo, basi ni rahisi sana kupotea..

2) Sababu ya pili ni: Ni kutojua Maandiko.

Tukirudi kwenye lile swali lao walilomuuliza tunaona mbele kidogo Bwana akiwauliza, HAMJASOMA?. Akitazamia kuwa kama wangekuwa wamesoma vema wasingekuwa na swali kama hilo..

Marko 12:26 “Na kwa habari ya wafu ya kwamba wafufuliwa, hamjasoma katika kitabu cha Musa, Sura ya Kijiti, jinsi Mungu alivyomwambia, akisema, Mimi ni Mungu wa Ibrahimu, na Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo?

27 Yeye si Mungu wa wafu, bali wa walio hai. HIVYO MWAPOTEA SANA”.

Unaona? Dini ambayo ilikuwa imeshakita mizizi yenye wafuasi wengi, kama baadhi ya dini nyingi leo hii duniani lakini kumbe ilikuwa imeshapotea kwa kutoyajua tu maandiko.

Leo hii watu wengi wamepotoshwa kwa kutoyafahamu maandiko, ukiona unaabudu sanamu, Ukiona unashikilia sabato na kusema huo ndio muhuri wa Mungu, wakati biblia inasema muhuri wa Mungu ni Roho Mtakatifu (Waefeso 4:30) ujue umepotoshwa na dini, ukiona unaabudu sanamu na kudhani kuwa zile ni viunganishi au vipatanishi na Mungu basi ujue umepotoshwa.

Hivyo sote kwa pamoja ni sharti tuufahamu uweza wa Mungu, kwamba hapa duniani wokovu upo, na watakatifu pia wapo, na kwamba pasipo utakatifu hakuna mtu atakayemwona Mungu asipokuwa nao sawasawa na (Waebrania 12:14) vilevile tuyasome maandiko, tuyatafakari sana, kila siku ili tusije tukazama katika madanganyo ya dini au madhehebu, au upotofu wa kidunia uliopo leo hii duniani.

Tukizingatia hayo mawili kama Bwana Yesu alivyosema, tusahau kupotea.

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Tofauti kati ya ufunuo, unabii na maono ni ipi?

KUMBE MUNGU ANAWEZA KUKULIPA KWA USICHOSTAHILI!

Neema ni nini?

Je! Ni dhambi kumpiga au kumuua mnyama bila sababu yoyote?

CHANGIA SASA.

MAPEPO YANATAFUTA HIFADHI NDANI YAKO KWA BIDII SANA.

Rudi nyumbani

Print this post

Tofauti kati ya ufunuo, unabii na maono ni ipi?

  1. UFUNUO

Ufunuo ni jambo ambalo hapo kabla lilikuwa limesitirika au limefungwa lakini sasa limefunuliwa. Kwa mfano katika biblia, utaona, Watu wengi walishindwa kumtambua Yesu ni nani, wengine walidhani ni Yeremia, wengine, mmojawapo wa manabii wa kale, wengine ni Yohana mbatizaji, Lakini Yesu alipowauliza mitume wake, Petro akasema, wewe ndiye Kristo mwana wa Mungu aliye hai. Yesu kusikia vile tunaona akamwambia maneno haya;

Mathayo 16:17 “Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu HAVIKUKUFUNULIA HILI, bali Baba yangu aliye mbinguni.

18 Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda”.

Unaona, Petro alifunuliwa, siri ambayo ilikuwa haijulikani na watu hapo kabla.

Vivyo hivyo na sisi tunahitaji ufunuo wa Roho Mtakatifu kuyaelewa  maandiko vinginevyo tutakuwa tunakisia tu au hatuyaelewi pale tunapoyasoma.

2) MAONO.

Ni taarifa ya rohoni ambayo mtu anapokea kutoka kwa Mungu,aidha anapokuwa usingizini, au akiwa macho. Anajikuta anaona vitu ambavyo hakupanga kuviona, na taarifa hizo zinaweza kuwa kwa mafumbo, au kwa uwazi, na zinaweza kueleza matukio yaliyopita au ya hapo hapo, au yale yatakayokuja baadaye.

Katika biblia tunaona watu wengi sana wakionyeshwa Maono..

Matendo 10:1 “Palikuwa na mtu Kaisaria, jina lake Kornelio, akida wa kikosi kilichoitwa Kiitalia,

2 mtu mtauwa, mchaji wa Mungu, yeye na nyumba yake yote, naye alikuwa akiwapa watu sadaka nyingi, na kumwomba Mungu daima.

3 Akaona katika maono waziwazi, kama saa tisa ya mchana, malaika wa Mungu, akimjia na kumwambia, Kornelio!

4 Akamtazama sana, akaogopa akasema, Kuna nini, Bwana? Akamwambia, Sala zako na sadaka zako zimefika juu na kuwa ukumbusho mbele za Mungu.

5 Sasa basi, peleka watu Yafa, ukamwite Simoni, aitwaye Petro”.

3) UNABII

Ni taarifa ya wakati ujao, (utabiri wa rohoni), ambayo Mungu anautoa moja kwa moja, hiyo inaweza kuwa katika maneno ya mtu anayozungumza bila yeye kujua, mfano utasoma mstari huu kuhani mkuu alitoa unabii pasipokujua kama yeye aliutoa.

Yohana 11:51 “Na neno hilo yeye hakulisema kwa nafsi yake; bali kwa kuwa alikuwa Kuhani Mkuu mwaka ule, alitabiri ya kwamba Yesu atakufa kwa ajili ya taifa hilo”.

au kwa njia ya kuambiwa au kuhubiriwa,

Ufunuo 11:3 “Nami nitawaruhusu mashahidi wangu wawili, nao watatoa unabii siku elfu na mia mbili na sitini, hali wamevikwa magunia”.

Hii ikiwa na maana kuwa katikati ya mafundisho, au mahubiri, Mungu huwa anatoa unabii wa mambo yajayo ndani yake.

1Timotheo 1:18 “Mwanangu Timotheo, nakukabidhi agizo hilo liwe akiba, kwa ajili ya maneno ya unabii yaliyotangulia juu yako, ili katika hayo uvipige vile vita vizuri”;

Kwa njia ya kuonyeshwa au kwa maono.

Yuda 1:14 “Na Henoko, mtu wa saba baada ya Adamu, alitoa maneno ya unabii juu ya hao, akisema, Angalia, Bwana alikuja na watakatifu wake, maelfu maelfu”,

Pia  kitabu chote cha Ufunuo ni kitabu kitabu cha unabii, ambacho Yohana alionyeshwa kwa njia ya maono.

Ufunuo 22:6 “Kisha akaniambia, Maneno haya ni amini na kweli. Naye Bwana, Mungu wa roho za manabii, alimtuma malaika wake kuwaonyesha watumwa wake mambo ambayo hayana budi kuwako upesi.

7 Na tazama, naja upesi; heri yeye ayashikaye maneno ya unabii wa kitabu hiki”.

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Mafundisho

UFUNUO: Mlango wa 1

Tofauti kati ya ndoto na Maono ni ipi?

THAWABU YA UAMINIFU.

Rudi nyumbani

Print this post

THAWABU YA UAMINIFU.

Kwa kawaida Mungu huwa hatoi karama zake zote kwa mkupuo, bali huwa anakupa kwanza kidogo kisha anaupima auminifu wako au uadilifu wako katika hicho, kisha akishaona umekithaminisha ndipo baadaye anakumwagia vyote vilivyobakia kwa wingi.

Leo tutaitazama mifano miwili ya watu walioambiwa maneno hayo naamini kwa kuisoma itakuongeza nguvu katika eneo hili la uaminifu,, wa kwanza tutauona kutoka katika maandiko na wa pili katika shuhuda za watu walitutangulia kwenye Imani.

Katika biblia, tunaona mtu mmoja aliyeitwa Yoshua, kuhani mkuu, ambaye Mungu alimwambia maneno haya;

Zekaria 3:6 “Kisha malaika wa Bwana akamshuhudia Yoshua, akisema,

7 Bwana wa majeshi asema hivi, Kama ukienda katika njia zangu, na kama ukishika maagizo yangu, ndipo utakapoihukumu nyumba yangu, nawe utazilinda nyua zangu, NAMI NITAKUPA NAFASI YA KUNIKARIBIA KATI YAO WASIMAMAO KARIBU”.

Huyu Yoshua alichaguliwa na Mungu kuwa kuhani mkuu wakati ule ambapo wana wa Israeli wanaondolewa tena Babeli, kumbuka huyu si yule Yoshua aliyewavusha wana wa Israeli Yordani, kutoka jangawani hapana, bali ni mwingine kabisa.

Sasa wakati akiwa Yerusalemu, Mungu akamchagua na kumtakasa, akamtia mafuta, awe kuhani wake, kuwapatanisha wayahudi wote.. Lakini tunasoma ahadi nyingine hakuzipokea palepale, bali zilitegemea kwanza uaminifu wake, ndipo Mungu ampatie ahadi hizo baadaye..

Mungu alimwahidi kuwa ikiwa atakuwa mwaminifu, ndipo ataihukumu nyumba yake, na vilevile atampa nafasi ya kumkaribia yeye, kati ya hao wasimamao karibu yake. Ulishawahi kujiuliza ni wakina nani hao wasimamao karibu na Mungu?.. Hapa duniani sio watu wote watakuja kusimama karibu na Mungu tutakapofika kule ng’ambo hata kama watakuwa wameokoka.

Ni sawa na leo hii, si watu wote wanaweza kusimama karibu na raisi wa nchi, kama hawajaalikwa na yeye, au kama hawana nafasi yoyote au cheo chochote katika serikali. Utagundua ni mawaziri tu, na watu wakubwa wakubwa wa serikalini, au familia yake tu ndio wanaoweza kumkaribia yeye. Lakini wengine wote mtakuwa mkimtazama kwenye Tv, au majukwaani.

Na vivyo hivyo kwa Mungu, wapo watu tayari ambao wameshawekwa karibu na Mungu,kutokana na uaminifu wao wa juu walipokuwa hapa duniani, katika maandiko tunawafahamu baadhi, wa kwanza ni Ibrahimu,

Mathayo 8:11 “Nami nawaambieni, ya kwamba wengi watakuja kutoka mashariki na magharibi, nao wataketi pamoja na Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo katika ufalme wa mbinguni;”

Wengine wakiwemo, akina Musa na Eliya, Wakina Danieli, watu waliopendwa na Mungu, wengine ni Ayubu, Samweli, akina Daudi aliyeupendeza moyo wa Mungu, Henoko, Mitume 12 wa Yesu, ambao Bwana aliwaahidia wataketi katika viti 12 wakiyahukumu makabila 12 ya Israeli, Yohana mbatizaji ambaye katika uzao wa wanawake hakuna aliyewahi kuwa mkuu Zaidi yake, wengine ni kama Mtume Paulo ambaye alitenda kazi kuliko wakristo wote wa wakati ule. Na pia wale mashahidi wawili ambao tunawasoma katika  ufunuo ambao wanafananishwa na ile mizeituni miwili,N.k.

Ufunuo 11:4 “Hao ndio ile mizeituni miwili na vile vinara viwili visimamavyo mbele za Bwana wa nchi”.

Sasa hawa wote, ni watu ambapo wanasimama karibu sana na Mungu.. Hivyo Yoshua naye kama kuhani mkuu aliahidiwa ofa hiyo, kwamba kama akiwa mwaminifu, na yeye pia ataingizwa katika kundi  hilo dogo la watu watakaosimama karibu na Mungu, tengeneza picha unasimama karibu na Mungu muumba wa Mbingu na nchi na malaika..si jambo dogo hilo. Na sisi pia tutamani nafasi hizo.

Vivyo hivyo, leo tutamtazama mtu mwingine ambaye alitokea katika kizazi chetu aliyeitwa WILLIAM BRANHAM.

Ikiwa hujawahi kumfahamu mtu huyu, ushuhuda wake ulikuwa ni wa kipekee sana, hatuwezi eleza habari yake yote hapa,  lakini, kwa ufupi ni kuwa alizaliwa mwaka 1909, huko Marekani, katika familia ya kimaskini sana, elimu yake iliishia darasa la saba tu, lakini tangu akiwa mdogo Mungu alianza kumuonyesha maono mengi, ambayo mengine hakujua tafsiri yake ni nini, mengine aliyaona yakitimia muda mfupi baadaye,..Lakini alipokuwa mtu mzima, akiwa kama mchungaji wa kanisa dogo la kibaptisti baada ya kupitia shida nyingi, ikiwemo kufiwa na mke na mtoto wake, hakuacha kumtafuta Mungu kwa bidii.

Siku moja usiku wakati anasali kama saa 9 hivi, kumuuliza Mungu ni nini maana kusudi lake duniani, alitembelewa na Malaika wa Bwana, akamwambia, nimetumwa kutoka uweponi mwa Mungu, kukuambiwa kuwa maisha yako ya kutokueleweka, ni kukuonyesha kuwa Mungu amekuchagua kulibeba kusudi lake kwa watu..Akaambiwa atapewa karama ya uponyaji, na kama akiwa mwaminifu utafika wakati utakuwa na uwezo wa kujua hata siri za mioyo ya watu, na hukuna ugonjwa wowote utakaoisimama mbele yako hata saratani yenyewe..(Kwa kipindi hicho ugonjwa wa saratani ndio uliokuwa tishio duniani)

Ni kweli mtu huyu baada ya hapo alionyesha uaminifu wake kwa Mungu, na yote aliyoahidiwa yalikuja kutimia muda mfupi sana katika huduma yake .. alianza kufahamu siri za mioyo ya watu, wote waliosimama mbele yake katika mstari kuombwa, Na Zaidi ya hayo Mungu akamzidishia na ishara za ajabu, ilifikia wakati nguzo ya Moto ilitokea na kutua Juu yake, mbele ya kanisa akiwa anahubiri, na ikapigwa picha na kuwekwa katika makumbusho za kihistoria huko Marekani, baada ya kuthibitishwa na FBI, kuwa picha hiyo ni ya kimiujiza, ndio hiyo hapo unayoina katika katika ujumbe huu.

Si hilo tu wakati Fulani akiwa anawabatiza watu katika mto mmoja huko Marekani mwaka 1933, ghafla kulitokea nuru kubwa kama nyota na kutua juu yake, watu wote waliokuwepo pale waliiona, habari hizo zilishapishwa katika magazeti mengi maarufu huko Marekani..Na wakati alipokuwa akiwabatiza watu anasema alisikia sauti ikimwambia kama vile Yohana mbatizaji alivyotumwa kutangulia kuja kwa kwanza kwa Kristo, vivyo hivyo na ujumbe wako utatangulia kuja kwa pili kwa Kristo.

William Branham mpaka sasa, ni mwinjilisti ambaye wanazuoni na wanatheolojia wa dini wanamkumbuka kwa ishara na maajabu yaliyokuwa yanafuata naye katika huduma yake. Ya kuhubiri injili ulimwenguni kote.

Ikiwa utapenda kupata historia yake ndefu..tutumie ujumbe inbox ..

Lakini hiyo yote ni kutokana na uaminifu aliokuwa nao kwa Bwana.. Hakuhubiri udhehebu, kinyume chake, aliikemea roho za kidhehebu ambazo zinawafunga wakristo wasimtambue Mungu, na hiyo ikampelekea kuchukiwa sana na watu wa dini. Injili yake iliegemea katika kuwaelekeza watu kwa Yesu, na sio kwake, au kwa mtu Fulani, alikemea dhambi, hususani katika uvaaji mbaya wa wanawake.. Na matokeo yake Bwana akamtukuza na yeye. Mafundisho yake yaliegemea katika Misingi ya Neno tu.

Hivyo Ujumbe wake umekuwa kama MBIU kwa kanisa la mwisho la Laodikia ambalo ndio sisi tunaoishi, kwamba tutoke huko kwenye Kamba za udini na udhehebu tumwabudu Mungu katika Roho na Kweli.William ni mjumbe wa kanisa la letu la Laodikia.

Sasa kwa mifano hiyo miwili ,nataka  uone ni jinsi gani, Mungu anauthamini uaminifu wa mtu. Hata Musa kule jangwani aliuthamini kwanza muujiza wa kijiti kuteketea moto, ndipo Mungu akampa na mingine kikubwa Zaidi.  Kila mmoja wetu anapaswa awe mwaminifu katika kitu alichopewa na Mungu. Leo hii utaona Mungu kampa mchungaji kanisa, na kwa neema zake limeanza kukua kidogo, lakini itapita miaka miwili, mitatu, utasikia amefumaniwa katika uzinzi, mwingine amejilimbikizia mali zote za kanisa.. huko ni kukosa uaminifu kwa kile ulichopewa na Mungu.

Mungu anaweza kukupa karama Fulani katika kanisa, lakini baada ya kipindi Fulani unaanza kujiona wewe ni wewe, unaanza kuonyesha kiburi, huko ni kukosa uaminifu kwa kile kidogo ulichopewa. Unabadilika kama Yeroboamu unasahau kuwa ni Mungu ndiye aliyekupa,.. Kila mmoja wetu alieyokoka, kuna kitu Mungu amempa lakini tukishindwa kuwa waamifu navyo, tukavidharau, tukawa hatuvitendei kazi, kamwe tusitazamie kuwa Mungu atakaa atupe ahadi nyingine za juu zaidi ambazo alikuwa amekusudia kutupa.

Hivyo kuanzia leo mimi na wewe tuanze kujenga uaminifu kwa vile vichache Bwana alivyotupa.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

HISTORIA YA WILLIAM BRANHAM

KAMA MKRISTO FAHAMU ZIPO HATUA UTAPIGISHWA NA MUNGU.

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 1

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

UFUNUO: Mlango wa 19

Rudi nyumbani

Print this post

Je! ni sahihi kwa mkristo kujifukiza?

SWALI: Nina swali mtumishi. Je mkristo aweza kujifukiza katika kipindi hiki cha changamoto za kupumua. Biblia inasema nini juu ya hili. Je, neno hili kwenye Ayubu 5:3 inazuia kujifukizia?

Ayubu 5:3 “Nimewaona wapumbavu wakishusha mizizi; Lakini mara niliyalaani maskani yake”.

JIBU: Kujifukiza ni tiba mojawapo kama zilivyo tiba nyingine. Mtu mmoja anaweza kuumwa na akaenda kumeza dawa za hospitalini, na mwingine akaenda kuchemsha mwarobaini akanywa. Na wote wakawa wazima.

Jambo ambalo si sahihi, ni pale tiba hiyo inapotolewa “sadaka kwa sanamu” nikiwa na maana kuwa pale inapohusianishwa na uganga au Imani potofu ambazo mara nyingi zinaambatanisha na masharti Fulani ambayo hata hayana uhusiano wowote na hiyo dawa kwamfano labda utaambiwa unywapo sema maneno Fulani, au nenda kainywee makaburini, au usinywe mbele ya watoto wako, au unyapo hakikisha upo uchi n.k… Sasa hizo ndio Mungu amekataza kwasababu ni ibada za sanamu.

Lakini tukirudi kwenye huo Mstari wa Ayubu 5:3 haizungumzii mizizi hii tunayoifahamu kama dawa, hapana, bali habari hiyo inazungumzia jambo lingine kabisa jinsi wenye dhambi wanavyoweza kujiimarisha kiasi cha kukita mizizi chini, wakijiwekea hazina nyingi, na kujijengea maboma makubwa, lakini hata hivyo, Mungu atawalaani na kuziangamiza maskani zao. Ukianzia kusoma tokea mistari ya juu utapata picha kamili ya habari hiyo.

Hivyo, kwa mkristo kujivukiza, si makosa, lakini pia ni vizuri tukajua sababu ya magonjwa haya kulipuka ni nini. Mungu hajayaleta ili tuyatafutie tiba hapana, Bali haya ni mapigo kutoka kwa Mungu na hilo lipo wazi yanayotutambulisha kuwa sisi kama dunia tumemsahau yeye, na pia  tunaishi katika siku za mwisho sawasawa na maneno ya Yesu katika , (Luka 21:11).

Swali ni je! Umeokoka? Je Yesu yupo ndani yako? Kama jibu ni hapana, basi ujue upo katika wakati wa hatari sana. Na wewe upo ndani ya hiyo hiyo ghadhabu ya Mungu iliyoachiliwa wakati huu tunaoishi, Hivyo fanya uamuzi wa busara, mkaribishe Yesu maishani mwako katika dakika hizi za majeruhi tunazoishi, Kabla mabaya hayajakufikia.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

https://wingulamashahidi.org/2019/09/01/je-ni-vema-kwa-mkristo-kwenda-hospitali-au-kutumia-miti-shamba-anapougua/

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya “Ulipo mzoga, ndipo watakapokutanika tai?

SWALI: Shalom naomba kufahamu maana ya huu mstari..

Luka 17:37 “Wakajibu, wakamwuliza, Wapi, Bwana? Akawaambia, Ulipo mzoga, ndipo watakapokutanika tai”.


JIBU: Kabla ya wanafunzi wa Yesu kumuuliza Bwana hilo swali “WAPI?”..Kuna maneno ambayo yalitangulia juu kidogo, ambayo tukiyasoma yatatusaidia kuelewa vizuri huo mstari ulimaanisha nini, embu tusome kidogo.

Luka 17:22 “Akawaambia wanafunzi, Siku zitakuja mtakapotamani kuona siku moja katika siku zake Mwana wa Adamu, msiione.

23 Tena watawaambia, Tazama, kule! Tazama, huku! Msiondoke mahali mlipo, wala msiwafuate”;

Ukisoma kwenye Mathayo imeeleza kwa undani zaidi, inasema..

Mathayo 24:23 “Wakati huo mtu akiwaambia, Tazama, Kristo yupo hapa, au yuko kule msisadiki.

24 Kwa maana watatokea makristo wa uongo, na manabii wa uongo, nao watatoa ishara kubwa na maajabu; wapate kuwapoteza, kama yamkini, hata walio wateule.

25 Tazama, nimekwisha kuwaonya mbele.

26 Basi wakiwaambia, Yuko jangwani, msitoke; yumo nyumbani, msisadiki”.

Maneno hayo Yesu aliyatanguliza kama angalizo la nyakati za hatari zitakazotokea siku za mwisho, akiwaonya kwamba wengi watakuja wakiwavuta watu kwao wakiwaambia Kristo yupo huku au kule, kwa maneno yao ya ushawishi, wakijinadi, tuna hichi au kile, sisi tuna miujiza mikubwa, sisi tuna upako wa mafuta mabichi, sisi ni wataalumu wa tiba za kiroho, sisi tuna makanisa makubwa kuliko yote duniani n.k.

Hivyo Yesu kwa kulijua hilo kwamba litakuja kutokea akawapa tahadhari wanafunzi wake kwamba wasitoke kuwafuata, wasiwe wepesi kuwaendea, wabaki mahali walipo, wasiende popote, kwasababu watawapotosha..

Sasa katika mazingira hayo ya kutokwenda mahali popote ndipo wanafunzi wake mwishoni wakamuuliza swali, NI WAPI sasa patakuwa sahihi pa kwenda..au tutakwenda wapi?

Ndipo Yesu akawaambia palipo na mzoga ndipo watakaposanyika Tai.. Ikiwa na maana mahali palipo na chakula cha Tai ndipo watakapokuja hapo na kukusanyika..

Na kama tunavyojua ndege aina ya tai wanaouwezo wa kuona mbali sana, leo hii kama kuna mnyama kafa porini na angani hakuna ndege yoyote, ukikaa baada ya muda mfupi utawaona tai wengi wamekusanyika hapo.. utajiuliza wametokea wapi na wakati anga lilikuwa jeupe halina ndege hata mmoja? Ni kwasababu jicho la Tai huwa linaona chakula kutokea mbali sana. Tai anaona mahali ambapo wewe huwezi kumwona.

Ni kama tu vile, mahali Fulani pawe na kinyesi cha mnyama au mtu, dakika si nyingi utaona nzi wengi wamekusanyika, na utajiuliza wametoka wapi wadudu hao na mahali hapo ni porini..Jibu ni kwamba, Mungu kawaumbia uwezo mkubwa wa kunusa vitu vya asili yao, tokea mbali, na ndio maana utawaona hata kama eneo hilo limejificha namna gani, wataenda tu.

Vivyo hivyo na wana tai wa Mungu, Kristo kawawekea uwezo Fulani wa kujua chakula chao halisi kilipo haijalishi ni wapi walipo watakipata tu. Tai si kama kuku, ambaye anaona vya hapo chini tu, bali Tai anaona vya mbali sana. Vivyo hivyo na sisi kama ni wanatai, ni lazima tuwe wa kufuata kile chakula kilicho chetu tu..Si kila chakula cha kukikurupukia kisa kipo karibu na sisi, au kinavutia..

Bali tuwe na macho ya tai ya kujua chakula chetu kipo wapi..

Hizi siku za mwisho, usiwe wa kukurupukia kila aina ya mafundisho, au imani. Kristo ameshatuonya..

Tafuta chakula cha wakati wako unaoishi.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo:

Rudi nyumbani

Print this post

Kwanini Yesu aliwakataza mitume wake kumdhihirisha?

SWALI: Shalom ndugu wapendwa! Naomba kuuliza kwa nini Yesu awakataze akina Petro wasiseme kwa watu kwamba yeye ni KRISTO kama ilivyo kwenye Mathayo 16:20

JIBU:

Kwa faida ya wengi tusome habari yote inayoelezea hilo tukio..

Mathayo 16:13 “Basi Yesu akaenda pande za Kaisaria-Filipi, akawauliza wanafunzi wake akasema, Watu hunena Mwana wa Adamu kuwa ni nani?

14 Wakasema, Wengine hunena u Yohana Mbatizaji, wengine Eliya, wengine Yeremia au mmojawapo wa manabii.

15 Akawaambia, Nanyi mwaninena mimi kuwa ni nani?

16 Simoni Petro akajibu akasema, Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai.

17 Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni.

18 Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda.

19 Nami nitakupa wewe funguo za ufalme wa mbinguni; na lo lote utakalolifunga duniani, litakuwa limefungwa mbinguni; na lo lote utakalolifungua duniani, litakuwa limefunguliwa mbinguni.

20 NDIPO ALIPOWAKATAZA SANA WANAFUNZI WAKE WASIMWAMBIE MTU YE YOTE ya kwamba yeye ndiye Kristo”.

Sasa ukisoma vitabu vyote vya injili utagundua sio tu katika tukio hilo aliwakataza wanafunzi wake wasimdhihirishe, bali pia yapo matukio mengine mbalimbali aliwakataza watu wasimdhihirishe, utaona kuna wakati aliwazuia makutano aliowaponya wasimtangaze..(Mathayo 8:4) Wakati mwingine aliyazuia pia  mapepo aliyoyatoa yasimtangaze,

Marko 3:11 “Na pepo wachafu, kila walipomwona, walianguka mbele yake, wakalia wakisema, Wewe ndiwe Mwana wa Mungu. 12 Akawakataza sana, wasimdhihirishe”.

na pia utaona kuna wakati Bwana alipojidhihirisha kwa mitume wake, wale 3 kule mlimani kwa mavazi ya kumeta-meta aliwaambia maneno hayo hayo.

Lakini kwanini awazuie watu kumdhihirisha?

Sio kwamba aliogopa, au alikuwa hataki kujulikana hapana, lakini aliwazuia kwasababu Ushuhuda wake ulikuwa bado haujakamilika. Ilimpasa kwanza ayatimize yote aliyoandikiwa kama mkombozi wa huu ulimwengu, kisha yakishakamilika, ndipo sasa habari hizo zihubiriwe rasmi kwa watu wote, Na ndio maana utaona sehemu nyingine anasema, subirini mpaka nitakapofufuka kutoka katika wafu ndipo mhubiri habari zangu, myasimulie haya.

Mathayo 17:5 “Alipokuwa katika kusema, tazama, wingu jeupe likawatia uvuli; na tazama, sauti ikatoka katika lile wingu, ikasema, Huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, ninayependezwa naye; msikieni yeye.

6 Na wale wanafunzi waliposikia, walianguka kifulifuli, wakaogopa sana.

7 Yesu akaja, akawagusa, akasema, Inukeni, wala msiogope.

8 Wakainua macho yao, wasione mtu ila Yesu peke yake.

9 Na walipokuwa wakishuka mlimani, Yesu aliwaagiza, akasema, MSIMWAMBIE MTU YE YOTE HABARI YA MAONO HAYO, HATA MWANA WA ADAMU ATAKAPOFUFUKA KATIKA WAFU.

Hapo ndio lile Neno la Yesu alilolisema katika Mathayo 10:27 lilipokuja kutimia..

Mathayo 10:27 “Niwaambialo ninyi katika giza, lisemeni katika nuru; na msikialo kwa siri, lihubirini juu ya nyumba”.

Ni jambo la kawaida hata sasa  kitu chochote ambacho kitatumiwa na uma, huwa kinajaribiwa kwanza na watu wachache, kisha kikishathibitishwa, au kukamilishwa ndipo kinapoachiwa kwa uma mzima kutumiwa.

Hivyo, sababu ya yeye kuzuia mambo yake mengi yasidhihirishwe kwa wakati ule ni kwasababu ushuhuda wake ulikuwa haujamilika bado. Lakini sasa umeshakamilika na ndio maana tunazitangaza habari za Yesu wazi wazi kwa wote bila kumficha mtu chochote.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

NI VIZURI SISI KUWAPO HAPA.

Nini maana ya “Tumejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii”?

TUMEFANYIKA KUWA WANA WA MUNGU!

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

Kwanini  vizazi vya ukoo wa Yesu vinajipinga katika Mathayo na Luka.

Kiango na Pishi ni nini (Mathayo 5:15)?

Rudi nyumbani

Print this post

NI VIZURI SISI KUWAPO HAPA.

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe daima, Ni siku nyingine tena Mungu ametupa neema ya kujifunza, hivyo nakukaribisha tuyatafakari pamoja maneno ya uzima maadamu siku ile inazidi kujongea.

Lipo jambo alilizungumza Petro, wakati ule ambao Bwana Yesu aliwachukua yeye pamoja na Yakobo na Yohana juu ya ule mlima mrefu.. Tukilisoma naamini litatupwa mwanga wa jinsi ya kutembea  vema katika safari yetu hii ya wokovu, Tusome habari yenyewe kwa ufupi na mbeleni kuna jambo kubwa ambalo Mungu atatufundisha siku ya leo.

Luka 9:28 “Baada ya maneno hayo yapata siku nane, aliwatwaa Petro na Yohana na Yakobo, akapanda mlimani ili kuomba.

29 Ikawa katika kusali kwake sura ya uso wake ikageuka, mavazi yake yakawa meupe, yakimeta-meta.

30 Na tazama, watu wawili walikuwa wakizungumza naye, nao ni Musa na Eliya;

31 walioonekana katika utukufu, wakanena habari za kufariki kwake atakakotimiza Yerusalemu.

32 Petro na wale waliokuwa pamoja naye walikuwa wamelemewa na usingizi; lakini walipokwisha amka waliuona utukufu wake, na wale wawili waliosimama pamoja naye.

33 Ikawa hao walipokuwa wakijitenga naye, PETRO ALIMWAMBIA YESU, BWANA MKUBWA, NI VIZURI SISI KUWAPO HAPA; NA TUFANYE VIBANDA VITATU; KIMOJA CHAKO WEWE, NA KIMOJA CHA MUSA, NA KIMOJA CHA ELIYA; HALI HAJUI ASEMALO.

34 Alipokuwa akisema hayo, lilitokea wingu likawatia uvuli, wakaogopa walipoingia katika wingu hilo.

35 Sauti ikatoka katika wingu, ikisema, Huyu ni Mwanangu, mteule wangu, msikieni yeye.

36 Na sauti hiyo ilipokwisha, Yesu alionekana yu peke yake. Nao wakanyamaza, wasitangaze kwa mtu siku zile lo lote katika hayo waliyoyaona”.

Katika mazingira hayo utaona, wakati Yesu akiwa uweponi mwa Mungu, ghafla Musa na Eliya walitokea wakaanza kuzungumza naye.. Mazungumzo hayo inaelekea yalikuwa ni marefu kidogo, kwasababu hawakuja kama malaika kuleta ujumbe tu na kuondoka hapana, bali walikuja kama wageni, kuzungumza naye, na mada kuu ilikuwa ni kuhusu kifo chake, jinsi atakavyoteswa na kukataliwa na watu kule Yerusalemu.

Kumbuka wakati huo mitume walikuwa wamelala, lakini walipoamka ghafla, wakamwona Yesu waliyemzoea akiwa katika mwonekano mwingine kabisa, na pembeni yake walikuwa watu wengine wawili wamesimama, na cha kushangaza walikuwa wakiongea naye kama vile wanajuana.

Hivyo Petro kuona tukio kama lile Bwana akiwa na wageni wa kimbinguni, huku akitazama na mazingira ya pale mlimani, hakuna hata chochote CHA KUWATIA UVULI, akaona si vema, asikae tu hivi hivi akimtazama Bwana akizungumza na wageni wake kwenye jua.

Ghafla akajikuta tu anazungumza, na kumwambia Bwana, Ni vizuri sisi kuwapo hapa.. akiwa na maana ni kama vile bahati wao kupanda naye kule mlimani kwasababu, walau wanaweza kumsaidia kufanya kitu.. Ndipo Petro akasema wacha tuwatengenezee vibanda vitatu, kimoja chako wewe, kimoja cha Eliya na kingine cha Musa.. Ili walau mpate uvuli juu ya mlima huu mrefu, mwendelee kuzungumza kwa utulivu zaidi.. hivyo wacha sisi tushuke chini tukachukue vifito tuanze kazi..

Embu tengeneza picha, Petro alijua Bwana amepatwa na ugeni wa kimbinguni, alijua wale watu hawana haja ya kukaa kwenye vibanda,, lakini kutokana na mazungumzo yao kuwa eneo tupu la wazi kama lile hakuona aibu kuonyesha kujali kwake kwao… Kama vile Ibrahimu wakati ule alipotembelewa na wale watu watatu, alipowaalika na kuwanjia ndama.

Na biblia inatuambia mara baada ya Petro kuzungumza maneno yale.. saa hiyo hiyo, wingu kubwa jeupe, likashuka mahali pale, likawatia UVULI wote, walipoona vile waliogopa sana, kukaribia kuzimia kwasababu jambo kama hilo hawajawahi kuliona katika maisha yao yote, na saa hiyo hiyo, sauti ikatoka KATIKATI ya lile wingu ikisema..

“Huyu ni mwanangu mpendwa wangu msikieni yeye”…Maneno kama hayo kuyasikia ilihitaji mbingu ikupasukie kwanza, walioweza kusikia sauti ya Mungu moja kwa moja kutoka mbinguni ikimshuhudia Yesu ni hawa watatu, pamoja na Yohana mbatizaji Ambaye yeye wakati anambatiza Yesu, mbingu zilimpasukia na kusikia maneno hayo hayo.(Mathayo 3:16-17)

Lakini hiyo yote, ilikuwa ni kwasababu gani?

Ni kwasababu alifikiria kwanza kumwekea Bwana uvuli kwa vile vibanda walivyokuwa wanataka kumjengea yeye. Ndipo Mungu akawatia UVULI halisi wa Mbinguni kwa wingu lake yeye mwenyewe.

Tengeneza picha mfano wasingejaribu kufikiria vile kwa ajili ya Bwana wao.. Ni wazi kuwa wasingeshukiwa na wingu lolote na wala wasingekaa waisikie sauti ya Mungu moja kwa moja ikuzungumza nao. Ushuhuda ambao wangebakiwa nao ni ule wa kumwona Eliya na Musa, na Yesu kuwa na mavazi meupe basi. Hakuna Zaidi.

Vivyo hivyo na sisi leo, Je, tunamtazama Kristo akihudumu katika hali gani? Na sisi tutakuwa  ni watu wa kutazama tu, au wa kusikiliza tu, au tutasema kama Petro, NI VEMA SISI KUWAPO MAHALI HAPA. Tukifikiria hata kwa uchache Mungu aliotujalia, au alivyotupa hivyo vinatosha kwa Mungu, ahitaji wingi wako, anahitaji nia yako, na moyo wako wa dhati.. Kama wafuasi wa Kristo hatupaswi kukaa kuangalia injili inahubiriwa katika hali ya taabu. Ni kweli utukufu wa Mungu utaendelea kuonekana, lakini zipo faida ambazo tutazikosa kama hatutakuwa na mawazo  kama ya Petro, alivyosema NI VEMA MIMI KUWEPO HAPA, wacha nikachukue fito nimwekee Bwana kivuli, sihitaji niwe na matofauti kwanza.

Wakati mwingine tunashindwa kumsikia Mungu kipekee kwasababu ya sisi kutoelewa kanuni za utendaji kazi wake.

Kumbuka Neno la Mungu (BIBLIA) ndiyo dira ya safari yetu hapa duniani. Siri zote za Mungu na njia zote za  kumfikia yeye utazipata huko tu, na sio kwa mwanadamu yoyote, au kwa mwanazuoni yeyote, au msomi yoyote, au kwenye kitabu kingine chochote.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

CHANGIA SASA.

PATANA NA MSHITAKI WAKO KWANZA.

ESTA: Mlango wa 8, 9 & 10. (SIKU KUU YA PURIMU)

UFUNUO: Mlango wa 19

TUMTOLEE MUNGU VILE VINAVYOTUGHARIMU ZAIDI.

Nini maana ya ombeni kukimbia kwenu kusiwe wakati wa baridi wala siku ya sabato?.

Rudi nyumbani

Print this post

Fuawe ni nini? Kama tunavyosoma katika Isaya 41:7

Isaya 41:7 “Seremala akamtia moyo mfua dhahabu, na yeye alainishaye kwa nyundo AKAMHIMIZA YULE APIGAYE FUAWE, akiisifu kazi ya kuunga, akisema, ni kazi njema; naye akaikaza kwa misumari isitikisike. ”.


JIBU: Fuawe ni chuma kizito, zilichotengenezwa na wafuaji kwa ajili ya kazi ya kuchonga au kukarabati vitu vyenye asili ya chuma, kama fedha, dhahabu, shaba, n.k. kwa kuviponda ponda  juu ya chuma hicho ili vitokee katika  maumbile waliyoyatazamia Tazama picha chini.

Ilikuwa kama wanataka kuunda umbile Fulani la chuma au shaba au fedha, walikiingiza kwanza kwenye moto kiyeyuke ili kiwe kirahisi kupondwa.. Ndipo kikishatolewa kililetwa kwenye hii fuawe sasa kwa ajili ya kugongwa kwa lengo la kukipa umbile lake.

Hivyo tukirudi katika mstari huo, anasema seremala akamtia moyo mfua dhahabu, hapa alikuwa anamzungumzia mtengeneza vinyago, vya mbao, ambaye baada ya kuvichonga sasa alikuwa tayari kuvipeleka vinyago vyake kwa walainishao yaani wafuaji, ili wawandalie dhahabu au fedha ya  kuvifunika vinyago vyake na huyo mfua fedha, aishaiweka dhahabu aliipeleka  sasa kwa huyu mpiga fuawe, mchongaji wa mwisho wa kinyago, ili kuleta umbo kamili la kinyago kile, Soma pia (Isaya 40:19)

chuma kizito fuawe

Lakini Mungu hapo alikuwa anaonyesha taabu zao, na gharama zao nyingi wanazoingia kwa mambo yasiyokuwa na faida, Kwa kujiundia vinyago visivyoweza kuzungumza wala kusikia, wala kuokoa, wala kutoa ahadi za ulinzi baadaye.. Lakini tunaona hapo mistari iliyofuata Mungu akiwaahidia watu wake Israeli ahadi nono, ambazo vinyago haviwezi kutoa, akiwaambia..

Isaya 41:8 “Nawe, Israeli, mtumishi wangu; Yakobo, niliyekuchagua; mzao wa Ibrahimu, rafiki yangu;

9 wewe niliyekushika toka miisho ya dunia, na kukuita toka pembe zake, nikikuambia, Wewe u mtumishi wangu; nimekuchagua wala sikukutupa;

10 usiogope, kwa maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia, naam, nitakushika kwa mkono wa kuume wa haki yangu”.

11 Tazama, wote walioona hasira juu yako watatahayarika na kufadhaika; watu washindanao nawe watakuwa si kitu, na kuangamia.

12 Utawatafuta wala hutawaona wale wapiganao nawe; watakuwa si kitu; watakuwa kama kitu kisichokuwa, wale waliofanya vita juu yako.

13 Kwa maana mimi, Bwana, Mungu wako, nitakushika mkono wako wa kuume, nikikuambia, Usiogope; mimi nitakusaidia.

14 Usiogope, Yakobo uliye mdudu, nanyi watu wa Israeli; mimi nitakusaidia, asema Bwana, na mkombozi wako ni Mtakatifu wa Israeli.

15 Tazama, nitakufanya kuwa chombo kikali kipya cha kupuria, chenye meno; utaifikicha milima, na kuisaga; nawe utafanya vilima kuwa kama makapi.

16 Utawapepeta, na upepo utawapeperusha; upepo wa kisulisuli utawatawanya; nawe utamfurahia Bwana, utajitukuza katika Mtakatifu wa Israeli.

17 Maskini na wahitaji wanatafuta maji, wala hapana; ndimi zao zimekauka kwa kiu; mimi, Bwana, nitawasikia, mimi, Mungu wa Israeli, sitawaacha.

18 Nitafunua vijito vya maji juu ya vilima, na chemchemi katikati ya mabonde; nitageuza jangwa kuwa ziwa la maji, na mahali pakavu kuwa vijito vya maji.

19 Nitapanda katika jangwa mwerezi, mshita, mhadasi, na mbono; nitatia katika nyika mberoshi, mtidhari, na mteashuri pamoja;”

Na sisi je, tunaweza kuweka kando ibada zote za sanamu za rohoni na mwilini, mpaka ifikie hatua ya Mungu kutuahidia ulinzi mnono kama huo aliowaahidia wana wa Israeli?

Jibu tunalo,

Je umeokoka? Je, unatambua kuwa nyakati hizi ni za mwisho?.. Na kanisa tunaloishi ndio kanisa la mwisho lijulikanalo kama Laodikia? Kama unayatambua hayo sasa Unangoja nini usimkaribishe Kristo leo maishani mwako. Ikiwa upo tayari kufanya hivyo leo. Basi fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

kwanini Yakobo amefananishwa na mdudu?(Isa 42:14)

Kwanini biblia inaitaja mara kwa mara dhahabu ya Ofiri?

Nini maana ya ombeni kukimbia kwenu kusiwe wakati wa baridi wala siku ya sabato?.

Njuga ni nini (Isaya 3:16, Zekaria 14:20)?

Bwana Yesu alimaanisha nini kusema “Saa yangu haijawadia?”

Ni nani aliyesema “Nitume mimi”? katika (Isaya 6:8)

Rudi nyumbani

Print this post

Je kwa mkristo aliyeokoka, ni dhambi kunyoa ndevu zake?

SWALI: Je kwa mkristo aliyeokoka, ni dhambi kunyoa ndevu zake kulingana na huu mstari?

Walawi 19:26 “Msile kitu cho chote pamoja na damu yake; wala msifanye kuloga, wala kutumia utambuzi.

27 MSINYOE DENGE PEMBE ZA VICHWANI, WALA MSIHARIBU PEMBE ZA NDEVU ZENU.

28 Msichanje chale yo yote katika nyama ya miili yenu kwa ajili ya wafu, wala msiandike alama miilini mwenu; mimi ndimi Bwana.

29 Usimnajisi binti yako, ili kumfanya awe kahaba; isiwe hiyo nchi kuuandama ukahaba, na nchi kujawa na uovu mkuu”.

JIBU: Wana wa Israeli wakiwa jangwani Mungu aliwapa maagizo hayo, ya kutokunyoa ndege(para) kwenye pembe za vichwa vyao, na wala wasichonge ndevu (kwa pembeni) wanyoapo.

Sasa Mungu kuwapa maagizo hayo, haikuwa kwasababu wataonekana na mwonekano tofauti, hapana bali mitindo hiyo ilikuwa ni inamaana kubwa Zaidi kwa watu wale, kwani ziliwakilisha ibada za miungu yao ya kipagani na ushirikina.  Wakati ule wamisri na waarabu waliokuwa wanaishi majangwani, walikuwa wananyolewa nywele zote za pembeni na kuachwa na KIDUKU cha mvuringo hapo juu, na wengine walikuwa wananyoa para kabisa,(Isaya 15:2, Yeremia 48:37) walifanya hivyo  kwa heshima ya miungu yao. Vilevile na kuchongwa kwa pembe za ndevu zao, kwa lengo hilo hilo.

Sasa Ili Mungu kuwatofautisha watu wake na mionekano ya kipagani, akawazuia wasifanye vile kama wao. Mungu alilichagua taifa la Israeli liwe takatifu, lijulikane kama ni taifa la Yehova, sio taifa ambalo watu akilitazama waone desturi za miungu ya kipagani ndani yao. Na ndio maana utaona mpaka “chale” alikataza wasichanjwe, mpaka michoro ya mwilini (Tatoo) wasichore, kwasababu zote hizo zilikuwa ni desturi za wachawi na miungu ya kipagani.

Kama vile wafanyavyo wachina leo hii, utawaona wamenyoa vichwa vyao vyote, na kuacha kifuniko kidogo cha nywele hapo juu, sio kwamba ni fashion hapana, bali ni wanatangaza desturi za miungu yao.

Hata leo hii, Ni ajabu sana kumuona mkristo ananyoa KIDUKU, wala hata hajui asili yake ni nini au anatangaza nini.. Na hata kama hana nia ya kutangaza upagani, lakini pia hajui kuwa Mungu ametuita kujitofautisha na watu wa ulimwenguni, kama alivyofanya kwa waisraeli.

kunyoa kiduku

Unaponyoa kiduku, halafu ni mkristo, unatoa nuru gani kwa jamii inayokuzunguka.  Ni wazi kuwa unatangaza usanii wa wanamiziki, unapovaa nguo iliyochanika chanika magotini, unatangaza nini?.. Unapofuga rasta, unamtangaza Mungu gani hapo, wewe kama mkristo unatangaza nini..? Kumbuka sisi ni barua tunayosomwa na watu wote.

Pia upo unyoaji wa ndevu wa kisasa ambao unaweza ukawa hauna maana ya ibada ya kipagani, lakini staili ya unyoaji wake zikakutambulisha wewe ni nani, kama utanyoa ndevu kwengine kote  halafu hapo katikati  unaziacha zirefuke ziwe kama za mbuzi, au unanyoa kisha unaziwekea mitindo mitindo uonekane kama msanii Fulani kwenye tv, wewe kama mkristo unapaswa ujue bado ni rafiki wa dunia. Na sio wa Mungu.

Hivyo kama wewe ni mnyoaji wa viduku, au wa hizo staili ni heri ukaacha, kwasababu Mungu hapendezwi ni mkristo wa namna hiyo.

Warumi 12:1 “Basi, ndugu zangu, nawasihi, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, ya kumpendeza Mungu, ndiyo ibada yenu yenye maana.

2 Wala msiifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu”.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Je kuweka mapambo kama mikufu, vikuku na kutoboa pua ni dhambi?

Kikuku/vikuku ni nini katika biblia?

Nini maana ya ombeni kukimbia kwenu kusiwe wakati wa baridi wala siku ya sabato?.

UFUNUO: Mlango wa 15

Swali: Je Ni sahihi kwa Mkristo kupeleka kesi mahakamani?

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 9 (Kitabu cha Ayubu).

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya ombeni kukimbia kwenu kusiwe wakati wa baridi wala siku ya sabato?.

Jibu: Ili tupate kuelewa vizuri, tutaisoma habari hii hii katika vitabu vitatu tofauti vya Injili. Tukianza na kitabu cha Mathayo, biblia inasema…

Mathayo 24:15  “Basi hapo mtakapoliona chukizo la uharibifu, lile lililonenwa na nabii Danieli, limesimama katika patakatifu (asomaye na afahamu),

16  ndipo walio katika Uyahudi na wakimbilie milimani;

17  naye aliye juu ya dari asishuke kuvichukua vitu vilivyomo nyumbani mwake;

18  wala aliye shambani asirudi nyuma kuichukua nguo yake.

19  Ole wao wenye mimba na wanyonyeshao siku hizo!

20  OMBENI, ILI KUKIMBIA KWENU KUSIWE WAKATI WA BARIDI, WALA SIKU YA SABATO.

21  KWA KUWA WAKATI HUO KUTAKUWAPO DHIKI KUBWA, AMBAYO HAIJATOKEA NAMNA YAKE TANGU MWANZO WA ULIMWENGU HATA SASA, WALA HAITAKUWAPO KAMWE.

22  Na kama siku hizo zisingalifupizwa, asingeokoka mtu ye yote; lakini kwa ajili ya wateule zitafupizwa siku hizo”.

Habari hii inazungumzia unabii wa Kuanguka kwa mji wa Yerusalemu, Baada ya wayahudi kumkataa Bwana Yesu. Yesu mwenyewe aliwaambia, kuwa utafika wakati, ambao Mungu atawaadhibu kwa kuikataa hiyo neema, tena akawaambia siku hizo zipo karibu kutokea ambapo, maadui zao (Yaani Warumi ambao wanawatawala sasa), watakapowazunguka pande zote na kuubomoa mji wao pamoja na hekalu, na kuwatawanya baadhi yao huko na huko, kama wakati wa uhamisho wa Babeli, na hayo yote ni kutokana na wao kumkataa Masihi, hivyo ile neema ya ulinzi kutoka kwa Mungu itaondoka juu yao, na adui atawavamia na kuwaharibu…

Habari hiyo tunaisoma katika kitabu cha Luka..

Luka 19:41  “Alipofika karibu aliuona mji, akaulilia,

42  akisema, Laiti ungalijua, hata wewe katika siku hii, yapasayo amani! Lakini sasa yamefichwa machoni pako.

43  Kwa kuwa siku zitakuja, adui zako watakapokujengea boma, likuzunguke; watakuzingira na kukuhusuru pande zote;

44  watakuangusha chini wewe na watoto wako ndani yako, wasikuachie jiwe juu ya jiwe, kwa sababu hukutambua majira ya kujiliwa kwako”.

Sasa Bwana alipoutoa huo unabii, watu waliokuwa wanamdharau na kumkataa hususani viongozi wa dini, Mafarisayo na Masadukayo, waliyapuuzia maneno hayo, na kumwona kama amerukwa na akili. Lakini wanafunzi wa Yesu walijua kabisa kuwa maneno ya Yesu hayatapita, jambo hilo lazima litimie, ndipo wakamfuata wakamwuliza ni lini hayo mambo yatatokea?. Ndipo Bwana akawaambia…

Luka 21:20 “… hapo mtakapoona mji wa Yerusalemu umezungukwa na majeshi, ndipo jueni ya kwamba uharibifu wake umekaribia.

21  Ndipo walio katika Uyahudi na wakimbilie milimani, na walio katikati yake wakimbilie nje, na walio katika mashamba wasiuingie.

22  Kwa kuwa siku hizo ndizo za mapatilizo, ili yatimizwe yote yaliyoandikwa.

23  Ole wao wenye mimba na wanaonyonyesha katika siku hizo! Kwa kuwa kutakuwa na shida nyingi katika nchi, na hasira juu ya taifa hili.

24  Wataanguka kwa ukali wa upanga, nao watatekwa nyara na kuchukuliwa katika mataifa yote; na Yerusalemu utakanyagwa na Mataifa, hata majira ya Mataifa yatakapotimia”.

Hapo sasa Bwana Yesu anazungumza na wanafunzi wake  tu, na si watu wote..hapana! bali wanafunzi wake tu, anawaambia jinsi mambo yatakavyokuwa na anawaambia jinsi ya kuepukana na hiyo siku ya mapatilizo.. Anawaambia watakapoona tu mji wa Yerusalemu umezungukwa na Majeshi..basi watambue kwamba ile ule unabii aliowaambia ya kwamba Yerusalemu itateketezwa umekaribi kutimia…

Sasa anaendelea kuwaambia wanafunzi kwamba watakapoona hayo majeshi, wasingoje chochote, waondoke mji wa Yerusalemu wasije na wao wakaangamia huko kwasababu ni siku ya kisasi cha Mungu. Hivyo waondoke wasafiri waende mji mwingine..wakakae huko..

Na pia waombe kuwa siku hizo za kuondoka zisitokee msimu wa Baridi wala siku ya Sabato..

Sasa kwanini siku ya Baridi na sabato?

Maeneo ya Yerusalemu miezi ya Machi na Aprili, kunakuwa na baridi sana, wakati mwingine mpaka kutengeneza barafu, sasa kwa ufahamu wa kawaida tu, kusafiri na punda kwenye barafu au wakati wa joto ipi bora?..bila shaka ni heri kusafiri kipindi cha joto kuliko cha barafu.. Hiyo ndio maana Bwana Yesu akasema waombe hayo yasitokee msimu wa baridi.

Lakini sio hilo tu! Akawaambia pia waombe yasitokee siku ya Sabato?

Sasa kwanini siku ya sabato?…Je Bwana Yesu alikuwa anamaanisha watu waishike sabato?. Jibu ni la.. Kumbuka wayahudi walikuwa wanashika sheria ya Musa, na pia siku ya sabato watu walikuwa hawaruhusiwi kufanya kazi, wala kutembea umbali mrefu…kulikuwa ni kipimo kidogo tu cha mwendo kwa siku, ambacho mtu hapaswi kukizidisha hicho katika siku ya sabato. Kipimo hicho kilikuwa kinaitwa “MWENDO WA SABATO”.

Matendo 1:12 “Kisha wakarudi kwenda Yerusalemu kutoka mlima ulioitwa wa Mizeituni, ulio karibu na Yerusalemu, wapata mwendo wa sabato”.

Ulikuwa ni mita kadhaa tu, Hivyo haikuruhusiwa mtu yeyote kutoka kusafiri, au kwenda kuzurula zurura. Na ilikuwa ni sheria mtu yeyote akionekana anafanya kazi siku hiyo au anatembea tembea hovyo ilikuwa ni kifo. (Unaweza kusoma sheria hiyo ya kutembe vizuri katika kile kitabu cha Kutoka 16:25-30) /www wingulamashahidi org/

Sasa hebu jiulize katika mazingira kama hayo, (yaani siku ya sabato), ndio majeshi yamezunguka Yerusalemu, ambapo ndio wakati wa kuondoka…utawezaje kuondoka?? Maana nchi hairuhusu mtu kusafiri, maana yake utajikuta unakaa huko huko mjini mpaka maangamizi yanakukuta. Ndio maana Bwana akawaambia “waombe kwamba siku hizo za kukimbia zisitokee msimu wa baridi, wala siku ya sabato”. Kwasababu kama zikitokea katika mojawapo ya mazingira hayo, basi dhiki yake itakuwa ni kubwa sana, ambayo haina mfano wake. Na watakaoathirika wa kwanza ni wanawake, tena hususani wale wenye mimba, au wanaonyonyesha…Hebu jiulize tena, mwanamke mjamzito au mwenye kichanga mkononi, ambacho muda wote kinahitaji malezi na joto la mama,  atakimbiaje kwenye baridi na katika mazingira ya mji kuzuiliwa watu kusafiri??..umeona jinsi ilivyo ngumu, ndio maana Bwana akawaambia ole wao wenye mimba, na wanyonyeshao.

Sasa baada ya Bwana Yesu kuwaambia maneno hayo ya unabii, pamoja na maneno mengine mengi…Bwana Yesu siku za kupaa kwake zilifika na aliondoka, lakini wanafunzi wakabaki na ufahamu vichwani mwao, kwamba siku si nyingi Yerusalemu itakuja kuzungukwa na majeshi, na huo ndio wakati wa sisi kuondoka..tusingoje..

Miaka 37 baada ya Bwana Yesu kuondoka, Unabii huo ulitimia.. yaani mwaka AD 70, Wakati ambapo Yerusalemu kunaonekana kuna amani, majeshi ya Warumi yalianza kuizunguka Yerusalemu wakiwa na silaha, watu wakajua ni jambo la kawaida tu, suluhisho la amani kwa mazungumzo litapatikana, pengine wakatokea watu wa kutabiri kutakuwa na amani, hakuna shida, hakuna haja ya hofu, kwasababu wakati huo Rumi ndio uliyokuwa inatawala dunia.

Lakini Mitume wa Yesu baadhi ambao bado walikuwa wanaishi, waliowaonya wakristo juu ya unabii huo wa Bwana, hivyo miongoni mwa wakristo, tukio hilo lilipotokea hawakusubiri wala kupoteza muda.. Wengi wao waliondoka Yerusalemu.. Na kukimbilia nchi za kando kando…waliyakumbuka yale maneno ya Bwana aliyosema.. “hapo mtakapoona mji wa Yerusalemu umezungukwa na majeshi, ndipo jueni ya kwamba uharibifu wake umekaribia  Ndipo walio katika Uyahudi na wakimbilie milimani, na walio katikati yake wakimbilie nje, na walio katika mashamba wasiuingie”. Hivyo wakristo waliokuwa na shughuli zao, huko waliziacha na kuondoka Yerusalemu kipindi hicho hicho, ingawa walionekana wendawazimu.

Lakini hao wengine wasioujua unabii  waliendelea kubaki wakijua hayo majeshi yataondoka tu…wengine wakawa wanaendelea na shughuli zao za kiuchumi, huku mazungumzo ya amani yanaendelea…siku chache mbele, mambo yakabadilika, yale majeshi yaliyokuwa yametulia tu mipakani, yakaingia Yerusalemu kama maji, yakaua watu wengi, na yakaangusha majengo yote ikiwemo hekalu, wala halikubakia jiwe juu ya jiwe, kama Bwana Yesu alivyotabiri, waliosalimika ni wale walioondoka tu. Na hayo yote biblia inasema yaliwapata kwasababu hawakutambua majira ya kujiliwa kwao.

Ndugu huo ni mfano wa dhiki kuu halisi ambayo inakuja huko mbeleni, Dhiki kuu yenyewe ipo karibu kutokea, itaanza ghafla tu, wakati kama huu ambao watu wanasema kuna amani na utulivu…ambapo baada ya unyakuo kupita watakatifu watakapoondolewa duniani, wale waliobaki, ambao wataikataa ile chapa, watateswa kwa mateso yasiyo ya kawaida, na baada ya kuteswa kwa miaka kadhaa bila kuruhusiwa kufa ndipo watakufa..

Hivyo unyakuo sio wa kukosa kabisa… na maneno ya Bwana Yesu kamwe hayapiti. Alisema Yerusalemu itazungukwa na maadui na hakuna jiwe litasalia juu ya jiwe..jambo hilo limetimia… Na maneno mengine yote aliyoyasema ni lazima yatatimia, hakuna ambalo halitatimia.

Marko 13:31 “Mbingu na nchi zitapita; lakini maneno yangu hayatapita kamwe”

Je umempokea Kristo?..Je una uhakika hata parapanda ikilia leo utanyakuliwa?..Kama huna uhakika basi huo tayari ni uthibitisho kwamba hutaenda, kwahiyo ni vyema ukatafuta uhakika kuanzia leo kwa kuyatengeneza maisha yako katika Yesu.

Bwana akubariki

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

IMESALIA RAHA YA SABATO KWA WATU WA MUNGU.

NYAYO TUNAZOPASWA KUZIFUATA.

NITAFANYA YERUSALEMU KUWA JIWE LA KUWALEMEA .

CHUKIZO LA UHARIBIFU

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

Rudi nyumbani

Print this post