Category Archive Uncategorized @sw-tz

UKIOKOKA, JIANDAE KUPITISHWA USIPOPATAZAMIA.

Kama leo hii Mungu akikutoa katika utumwa wa dhambi (Yaani kuokoka), basi weka akilini kuwa unapopelekwa kutakuwa ni nje ya matarajio yako, na pengine pasiwe ni pa kuvutia kabisa katika macho yako. Ni vizuri tukafahamu njia za Mungu, ili pale tunapokutana nazo tusiwe ni watu wa  kulaumu laumu, au kuuliza uliza ni kwanini hivi, kwanini vile?

Kipindi kile Mungu alipowatoa wana wa Israeli katika nchi ya Misri, walitazamia kupitishwa  katika NJIA kuu ya mataifa yote, iliyojulikana kama  njia ya wafilisti. Njia hiyo ilikuwa ni ya haraka na ya chap chap, kiasi kwamba kama wangeipitia hiyo, ingewachukua wiki kadhaa tu wangeshafika Kaanani. Lakini Mungu alikuwa na sababu ya wao kutowapitisha njia ile..Tusome..

Kutoka 13:17 “Ilikuwa hapo Farao alipokwisha kuwaacha watu hao waende zao, Mungu hakuwaongoza kwa njia ya nchi ya Wafilisti, ijapokuwa ilikuwa ni ya karibu; maana Mungu alisema, Wasije wakaghairi watu hawa hapo watakapokutana na vita, na kurudi Misri;

18 lakini Mungu akawazungusha hao watu kwa njia ya bara kando ya Bahari ya Shamu; wana wa Israeli wakakwea kutoka nchi ya Misri hali wamevaa silaha”.

Unaona wana wa Israeli walipitishwa katika njia ngeni kabisa machoni pao, njia yenye ukingo wa mbeleni ya bahari, njia ya vichakani, isiyopitwa na watu, njia ya upweke..Mpaka biblia inatuambia hicho ndicho kilichomvutia Farao, kuwafuatilia tena ili wawateke nyara wawarudishe Misri. Lakini hawakujua kuwa Mungu yupo kule kuwatetea.

Kutoka 14:1 “Bwana akasema na Musa, akamwambia,

2 Waambie wana wa Israeli, kwamba warudi na kupiga kambi yao mbele ya Pi-hahirothi, kati ya Migdoli na bahari, kukabili Baal-sefoni; mtapanga mbele yake karibu na bahari.

3 Naye Farao atasema katika habari za wana wa Israeli, Wametatanishwa katika nchi, ile jangwa imewazuia wasitoke.

4 Nami nitaufanya uwe mgumu moyo wa Farao, naye atafuata nyuma yao; nami nitajipatia utukufu kwa Farao, na kwa jeshi lake lote; na Wamisri watajua ya kuwa mimi ndimi Bwana. Basi wakafanya hivyo.

5 Mfalme wa Misri aliambiwa ya kuwa wale watu wamekwisha kimbia; na moyo wa Farao, na mioyo ya watumishi wake, iligeuzwa iwe kinyume cha hao watu, nao wakasema, Ni nini jambo hili tulilotenda, kwa kuwaacha Waisraeli waende zao wasitutumikie tena?

6 Akaandalia gari lake, akawachukua watu wake pamoja naye;”

Hata sasa, wapo watu wanapookoka, na ghafla kuona mambo yanakwenda kinyume na matazamio yao, wanapolazimika kuishi staili nyingine ya maisha, wanageuka na kurudi nyuma na kuuacha wokovu. Na tena pale wanapoona, kuna ukigo mzito mbele yao na kwamba wakiendelea na njia hiyo ya wokovu watakwama ndio kabisa  wanakimbia kwa miguu yote miwili, na kusema huyu si Mungu.

Pengine mwingine atapitia shida kidogo, au dhiki kutoka kwa ndugu, au kupungukiwa, jambo ambalo ni kinyume na matarajio yake, wakati hapo mwanzo yeye alidhani akimpokea Kristo siku hiyo hiyo mambo yataanza kuwa safi, sasa anapoona kumetokea mitikisiko Fulani katika maisha, anamwacha Mungu anasema huyu sio Mungu.

Ndugu ikiwa kweli umetubu dhambi zako, na umejitwika msalaba wako kumfuata Kristo, umesema mimi na ulimwengu ndio kwaheri, kamwe usitazame nyuma, pale unapoona mambo yanakuja kinyume na matarajio yako, wewe songa mbele. Ni Mungu ndiye kakusudia kukupitisha hapo, usianze kulaumu laumu au kunung’unika, na kusema kwanini mimi, maadamu Kristo yupo ndani ya moyo wako, songa mbele. Unapoona njia hiyo imekuwa ndefu sana, kama vile huielewi itaisha lini? Bado usiwe mwepesi wa kutazama nyuma. Wewe endelea mbele maadamu unamwona Kristo kila siku katika maisha yako. Kumbuka iliwachukua miaka 40 wana wa Israeli kuifikia Kaanani yao.

Nawe pia upo wakati Bwana aliouweka atakufikisha katika Kaanani yako ya hapa duniani na mbinguni. Ni wewe tu, kutambua kuwa njia za Mungu sio njia zetu. Jambo ambalo wengi wetu hatulijua pale tunaposema tumemfuata Kristo, na huku tunamtaka Mungu atatupitisha kwa njia ya wengi.

Kamwe tuondoe hayo mawazo. Yeye ana njia zake, na wanadamu wana njia zao. Hilo tulifahamu. Na pia tukumbuke mtoto yoyote wa Mungu, atapitishwa tu kwenye njia hizo, haijalishi ni mjanja, au hodari, au tajiri au maskini kiasi gani, ni lazima atakutana tu na njia hizi zisizoeleweka za Mungu, kwasababu madarasa ya Mungu hayarukwi. Na tabia ya hizi njia ni kuwa zinaambatana ni miujiza mingi ya Mungu, ikiwa na maana mtu anaweza kufikia mahali anaona amekwama, ghafla anashangaa amepitaje pitaje mazingira hayo, huo ndio uthitibisho kuwa yupo katika njia hiyo ya Mungu.

Lakini kama akistahimili, basi ajue, licha tu ya kuupokea uzima lakini mwisho wako atakuwa ni wa mafanikio na wa Baraka sana hapa duniani.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengin

Mada Nyinginezo:

NJIA YA ‘UTAJIRI MKUU’ KWA KIJANA.

BIBLIA INAITAJA NJIA KUU YA MFALME, NJIA HII NI IPI?

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 2

NJIA YA KUPATA WOKOVU.

MUNGU HATAZAMI MOTO WA KIGENI,KUWA MAKINI!

Rudi nyumbani

Print this post

MAVUNO YAMESHAKWISHA  SHAMBANI.

Mathayo 24:14 “Tena habari njema ya ufalme itahubiriwa katika ulimwengu wote, kuwa ushuhuda kwa mataifa yote; hapo ndipo ule mwisho utakapokuja”.

Bwana Yesu asifiwe ndugu mpendwa..

Ukitaka kujua kuwa mambo yote sasa yameshakamilika, kinachongojewa ni UNYAKUO tu, angalia hali ya mavuno shambani mwa Bwana. Embu fananisha watu waliokuwa wanamjia Kristo kipindi cha mitume, na watu wanaookoka sasa  katika kipindi chetu hichi.

Kipindi kile injili ilipokwenda kuhuburiwa mahali kwa mara ya kwanza, mwitikio wa watu  wa kumgeukia Kristo ulikuwa ni wa kustaajabisha sana, utakumbuka baada ya Pentekoste tu, kanisa lilikuwa likijiongeza  kwa idadi ya maelfu, kwa injili ndogo sana. Na ndio maana kwa kipindi kifupi sana, ukristo ulienea ulimwenguni kote, na sio kuenea tu, badi kuhubiriwa (Wakolosai 1:6, 1Wathesalonike 1:8).Hiyo ni kuonyesha kuwa kweli ule ulikuwa ni wakati wa mavuno.

Lakini angalia sasa,  mambo ni tofauti hakuna mtu asiyeifahamu injili, au kuzijua habari za Kristo, wote tunazifahamu, lakini jiulize kwanini, watu hawataki kuokoka, kinyume chake ndio wanakwenda mbali kabisa na Ukristo..Hiyo ni kuonyesha kuwa mavuno yameshakwisha shambani, kilichobaki ni magugu tu.

Na hiyo imepelekea sasa injili kubadilika sio tena ya kuwavuta watu, bali ni ya ushuhuda. Unapoona, injili imekufikia hapo ulipo kitandani kwako ukiwa umeishika simu yako na kusoma, ujue hiyo sio ya kukuvuta wewe, hiyo ni ya ushuhuda tu, ukiona injili imekufikia hapo sebuleni kwako unapotazama tv na familia yako, injili inakufikia kwenye hivyo vipeperushi unavyovisoma huko mitaani. Unapewa biblia bure ya kwenye simu yako, mambo ambayo hata zamani hayakuwepo. Basi ujue hiyo sio injili ya kukuvuta tena kwa Kristo ndugu. Ni injili ya USHUHUDA Tu. Ili utakapokufa katika dhambi zako, usiwe na sababu ya kusema sikuwahi kusikia, au kuona, au kuambiwa.

Wewe jiulize tu, ni kwanini pamoja na mahubiri yote hayo uliyohubiriwa na kuyasikia siku zote za maisha yako, na bado huna badiliko lolote ndani yako. Unadhani ni jambo la kawaida? Hapana, kwa kawaida Neno moja tu lingetosha kukufanya uwe mtakatifu sawasawa na Waebrania 4:12.  Lakini hujageuka kwasababu  wewe sio Ngano bali ni gugu tu.

Kilichosalia sasa hivi ni Mungu anatazama walau kama yatakuwepo masalia salia machache ayaokoe. Lakini nataka nikuambie, moja ya hizi siku ambazo zinahesabika, tutashuhudia mabadiliko makubwa sana duniani. Tutashuhudia tendo kuu la Unyakuo wa kanisa.

Ndio yale maneno ambayo Bwana Yesu alisema, .(Mathayo 24:40-42) yatatimia hapo. Usiku huo wawili watakuwa wamelala mmoja atatwaliwa, mmoja ataachwa. Wanawake wawili watakuwa wanasaga(ikimaanisha watakuwa katika biashara zao), mmoja atatwaliwa mmoja ataachwa. Wale watakaoachwa, huku duniani kitakachokuwa kinaendelea ni vilio na kusaga meno. Wakijuta kwanini kipindi kile hawakuitii sauti ya Mungu, ilipokuwa inawavuta kwake kwa upole. Watalia na kuomboleza, kweli kweli, ndugu usiwe mmojawapo.

Lakini watakaokuwa wamenyakuliwa, moja kwa moja wataelekea mbinguni wakiwa na miili yao ya utukufu, katika ile karamu ya mwana-kondoo.  Kwenye raha isiyokuwa na kifani. Wakifutwa machozi kwa taabu zao walizokuwa wanapitia huku duniani kwa ajili ya Kristo.

Ndugu mambo haya unaweza kuona kama ni hadithi, au mambo yatakayotokea miaka elfu 5 mbeleni, usijidanganye. Yesu aliposema TUBUNI, kwa maana ufalme wa mbinguni UMEKARIBIA. Alikuwa hasemi uongo. Ni kweli ufalme wa mbinguni  ulikuwa umekaribia, jiulize  sisi wa sasa hivi tusemeje?.

Maanisha kugeuka, unaposikia injili kwa wakati huu.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

UNYAKUO.

KUMBE MUNGU ANAWEZA KUKULIPA KWA USICHOSTAHILI!

MWANZO WA INJILI YA YESU KRISTO.

UFUNUO: Mlango wa 14

Kuwiwa maana yake nini katika biblia?

Je watu ambao hawajasikia kabisa injili watahukumiwa?

Rudi nyumbani

Print this post

NI SAHIHI KABISA, HUU SI WAKATI WA TINI!

Katika ukristo ogopa sana ile kauli ya kusema “Huu si wakati”… “Bado kidogo”…. “Wakati wake utafika tu siku moja”… Ogopa sana kauli kama hizo, tena ziogope kuliko  ukoma.

Kwanini ninakuambia hivyo? Ni kwasababu wakati ambapo unafikiria majira yake bado, huo ndio wakati Kristo anatazamia kuona matunda kwako. Jambo ambalo ni kinyume kabisa na asili. Hana tabia ya kutafuta matunda wakati wa msimu. Haongozwi na misimu.

Embu kitafakari vizuri kitendo alichokifanya siku ile alipokuwa anakwenda Yerusalemu kutokea Bethania, alipokutana na ule mtini njiani, alifanya nini!. Utaona alikwenda moja kwa moja na kutafuta matunda juu yake, Na alipokosa akaulaani na kunyauka saa ile ile , pasipo kujali kuwa ule haukuwa hata msimu wake wa kuzaa..

Marko 11:12 “Hata asubuhi yake walipotoka Bethania aliona njaa.

13 Akaona kwa mbali mtini wenye majani, akaenda ili labda aone kitu juu yake; na alipoufikilia hakuona kitu ila majani; MAANA SI WAKATI WA TINI.

14 Akajibu, akauambia, Tangu leo hata milele mtu asile matunda kwako. Wanafunzi wake wakasikia”.

Hili ni jambo ambalo watu wengi hawalifahamu, wanapoangalia mazingira Fulani, wanaona kama vile wakati wake bado, pale mtu unapomuambia biblia inasema “saa ya wokovu ni sasa, na wakati uliokubalika kuokoka ni leo (2Wakorintho 6:2 )” yeye atasema, ngoja kwanza, siku moja nitaokoka tu!, ngoja nimalize chuo, ngoja nioe kwanza, ngoja nipate kazi, ngoja nitoke kwanza kwa wazazi wangu..Ngoja nijenge nyumba yangu kwanza..

Huku akitazamia kweli siku moja akishavipata hivyo vitu  ndio atatulia afikirie sasa kumtumikia Mungu. Lakini hajui wakati amekaa akiungojea huo wakati  ufike Kristo anatokea ghafla kwenye maisha yake, kutafuta matunda, anayakosa, hatua inayofuata kwake ni KULAANIWA MILELE.

Maana yake ni kuwa kamwe asahau WOKOVU katika maisha yako, na ndio maana watu kama hao ambao wana tabia ya kusubiri, subiri, kujivuta vuta, mwisho wa siku unawakuta mpaka wanakufa hawajaokoka haijalishi kuwa wameshapata kila kitu. Sio kwamba kulikuwa na ugumu wowote. Hapana lakini kwasababu walishalaaniwa na Yesu tangu zamani, walipotazamiwa wamzalie Kristo matunda wakashindwa.

Hivyo ndugu, tambua kuwa jicho lako sio jicho la Yesu. Wewe unatazama misimu, Yesu hajui msimu. Wewe unatazama nyakati, Kristo hajui nyakati. Wakati wowote anataka ajapo akukute, ukiwa na matunda. Akukute unamzalia matunda ya Roho. Lakini ukiwa ni mtu wa kusubiria siku Fulani ifike ndio ufanye maamuzi. Upo katika hatari kubwa sana ya kulaaniwa.

Wana wa Israeli, kuna wakati nao pia walijibunia utaratibu kama huo, wakati ambapo Mungu alishawapa tamko la kwenda kumjengea nyumba, Lakini walipopokea vitisho kutoka kwa mfalme aliyefuata kwamba waache ujenzi, wao nao wakasikiliza sauti yake kweli wakaacha. Ukisoma pale utagundua kuwa Kilichofuata ni Mungu kuwalaani, akawapiga kwa umaskini na shida zisizokuwa za kawaida. Mpaka siku walipogundua kosa lao, na kwenda kumjengea tena Mungu nyumba, walijutia mawazo yao.

Hagai 1:2 “Bwana wa majeshi asema hivi, ya kwamba, Watu hawa husema, Huu sio wakati utupasao kuja, huu sio wakati wa kujenga nyumba ya Bwana.

3 Ndipo neno la Bwana lilikuja kwa kinywa cha nabii Hagai, kusema,

4 Je! Huu ndio wakati wa ninyi kukaa katika nyumba zenye mapambo ya mbao, iwapo nyumba hii inakaa hali ya kuharibika”?

Leo hii, mtu akishazuiwa na wazazi wake, au boss wake, au mume wake, basi hiyo ndio inakuwa tiketi ya yeye kuukimbia kabisa wokovu au utumishi wa Mungu, akijitetea kuwa pengine haukuwa wakati sahihi na ndio maana vikwazo kama hivyo vimetokea. Nataka nikuambie, ondoa hayo mawazo kuanzia leo, kwasababu hata kwa Yesu hayapo, utalaaniwa.

Upokee wokovu leo, tubu dhambi zako leo, kuwa tayari kubatizwa katika ubatizo sahihi  leo, anza kuishi maisha matakatifu yampendezayo Mungu, bila kujali mazingira, watu, hali, au msimu,..Na baada ya hapo yeye mwenyewe atakupokea na kukujalia kuzaa matunda wakati huu huu, unaoonekana kama haufai kwako.

Kumbuka hizi ni siku za mwisho, wakati wa mavuno umekaribia sana, dalili zote zinaonyesha kizazi chetu tunachoishi kitashuhudia tukio halisi la kurudi kwa Bwana Yesu duniani mara ya pili, kulinyakua kanisa lake. Jiulize Ikiwa atarudi leo usiku utakuwa na lipi la kujitetea, ikiwa hukumpa maisha yako? Au ukifa leo utamweleza nini huko uendako kama Yesu si mwokozi wa maisha yako.

Usizifiche dhambi zako, ikiwa upo tayari kuokoka leo, basi uamuzi huo utakuwa ni wa busara sana kwako. Basi popote pale kama utahitaji msaada huo wasiliana nasi kwa namba hizo hapo chini, au tafuta kanisa la kiroho lililo karibu na wewe, wakusaidie kupokea wokovu.

Kisha hakikisha unatafuta ubatizo sahihi wa kuzamishwa kwenye maji mengi, na kwa jina la YESU KRISTO (Zingatia sana hilo), kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako. Na yeye mwenyewe atakupa kipawa cha Roho Mtakatifu.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita..

AINA TATU ZA WAKRISTO.

UFUNUO: Mlango wa 22

JE UNAYAFANYA MAPENZI YA MUNGU?

Mlima wa Mizeituni  unaumuhimu gani kwetu?

VAZI LA YESU HALIGAWANYWI.

Rudi nyumbani

Print this post

UKIOKOKA,HIZI FIKRA ZIKIJA NDANI YAKO, ZIKATAE.

Kuna silaha ambazo nataka ufahamu shetani anazozitumia kwa watu ambao wanakaribia kuokoka, au waliookoka lakini bado ni wachanga katika imani. Silaha hizo, zimewafanya watu wengi waishi katika hofu, na misongo mikubwa ya mawazo, mimi nikiwa mmojawapo kabla sijaokoka.

Nataka nikuambie mawazo haya yakikujia, yakatae kwa nguvu zako zote, kwasababu ni vita vya kifikra ambavyo shetani na majeshi yake ya mapepo wanavyoleta ili kukuangusha uiche imani, au usisonge mbele. Narudia tena usiruhusu hata kidogo mawazo hayo yakutawale;

     1)  Umemkufuru Roho Mtakatifu:

Hii ndiyo silaha ya ibilisi ya kwanza ; Anakuletea mawazo kuwa wewe huwezi kusamehewa, kwani dhambi yako ni ya kumkufuru Roho Mtakatifu. Na anaweza kukurushia mpaka hayo mawazo ya namna hiyo ili ujione wewe tayari dhambi yako imeandikwa kwa kalamu ya chuma.

Nataka nikuambie, huo ni uongo tu, dhambi ya kumkufuru Roho Mtakatifu haiji hivyo. Na kamwe mtu aliyemkufuru Roho hata hofu na Mungu hana ndani yake, ni mfano wa mafarisayo na masadukayo ambao walikuwa wanazipinga kazi za Roho Mtakatifu wazi wazi na kuzishuhudia hadharani kuwa ni za mapepo wakati wanaujua kabisa ukweli kwamba na Roho Mtakatifu ndiye aliyekuwa anafanya kazi zile (Mathayo 12:24-32).

Sasa jiulize wewe ni lini ulishawahi kwenda kuzipinga kazi za Roho Mtakatifu huku ukajua kabisa ndio yeye, halafu ukatoa maneno ya kufuru  na kusema zile ni kazi ya mapepo..Ulishawahi kufanya jambo kama hilo mbele ya kadamnasi? Ni wazi kuwa hujawahi kufanya.. Sasa hayo mawazo ya wewe umemkufuru Roho Mtakatifu yametoka wapi kama sio kwa shetani?

Watu wengi, nimewasiliana nao, wamekuwa wakisumbuliwa na mawazo mkandamizo kama hayo, Lakini leo nataka nikuambie Usiogope, hiyo ni ishara kuwa Mungu yupo karibu na wewe sana, unachopaswa kujua ni kufahamu ile kweli, ili ikuweke huru kweli kweli.

   2) Bado hujaokoka: 

Unaweza ukawa umetubu kweli dhambi zako kwa kudhamiria kuziacha, na ukabatizwa katika ubatizo sahihi, na baada ya hapo ukaanza kuishi maisha yanayompendeza Mungu, Lakini kipindi fulani kikapita shetani akakuletea mawazo kwamba bado hujaokoka, wanaookoka hawawi kama wewe. Mawazo kama haya, yakatae, Bwana Yesu alisema, “Hakuna mtu anayeweza kwenda kwake, kama Baba yake hajamvuta kwake (Yohana 6:44)” Hivyo mpaka wewe umefikia hatua ya kutubu, na kubatizwa na kuanza kuonyesha bidii ya kuishi sawasawa na mapenzi yake, haikuwa kwa akili zako, bali ni Yesu mwenyewe alikuvuta.

Hivyo songa mbele, zidi kujitakasa siku baada ya siku, mpaka kuufikia ukamilifu kwasababu Yesu yupo pamoja na wewe.

  3) Umeshachelewa:

Hili ni jambo lingine ambalo, limewadhoofisha wengi. Wanadhani elimu ya kidunia ni sawa na elimu ya ufalme wa mbinguni. Elimu ya kidunia, ukishakuwa mtu uzima na hujaenda shule, unaweza ukaonekana kama umeshachelewa. Duniani ukifikisha umri fulani hujaolewa, au hujapata kitu fulani umeshachelewa. Lakini kwa Mungu haiendi hivyo, maadamu pumzi ya uhai ipo ndani yako bado hujachelewa kumtumikia yeye.

Mungu anakutazama, ufanye vizuri isipokuwa tu uonyeshe bidii, ili ufanye vizuri kuliko hata wale ambao walikuwepo tangu zamani. Embu mkumbuke mtume Paulo, hakuwa miongoni mwa wale 12, wala siku ile ya Pentekoste hakuwepo. Lakini alikuja kufanya kazi kubwa kuliko wote waliomtangulia.

Ukumbuke pia ule mfano wa mwajiri na waajiriwa ambao Bwana Yesu aliutoa, akasema kulikuwa na wengine ambao walikutwa jioni kabisa hawana kazi yoyote, wakaambiwa waende shambani, na kule shambani walipomaliza shughuli yao, wakalipwa sawa sawa na wale wengine, ambao walikuwa tangu asubuhi shambani.(Mathayo 20:1-16). Na ndio maana Bwana Yesu akamalizia na kusema “wapo walio wa mwisho watakuwa wa kwanza, na wale wa kwanza watakuwa wa mwisho”.

Vivyo hivyo na wewe, ikiwa umeitwa kwenye miaka ya 20, au 30 au 40 au 50 au 80. Hujachelewa  popote pale. Mtumikie Bwana kwa moyo wako wote na kwa uaminifu. Na thawabu yako inaweza kuwa kubwa kama tu ile ya mitume.

   4) Mungu hawezi kupendezwa na wewe:

Haya mawazo yanakuja hususani pale ambapo pengine hukutumiza wajibu wako fulani uliloambiwa na Mungu ufanye, au ulifanya dhambi fulani ambayo ilikuwa ni ya makusudi kabisa kwa Mungu, pengine ulivunja viapo vya ndoa yako ukaenda kuzini, au uliua mtu, au uliiba n.k..

Nataka nikuambie kama umetubu tayari kwa kumaanisha kutoka katika moyo wako. Basi usiruhusu tena hayo mawazo yawe ndani yako, kukutawala. Mrudie Mungu wako, mtumikie kwa bidii, kwani kumpendeza tena kunawezekana, na akawa rafiki yako, zaidi hata ya pale mwanzo kama utatii. Daudi alizini ni mke wa Uria, lakini alitubu, hata baada ya kuadhibiwa na Mungu, aliendelea kumtafuta Mungu wake, na mwisho wa siku bado akawa mtu ambaye ameupendeza moyo wa Mungu.

    5) Fulani ni bora kuliko wewe mbele za Mungu:

Haya ni mawazo mengine ya ibilisi, kukukandamizi tu usipige hatua, kwamba fulani ni zaidi yako wewe mbele za Mungu. Hilo jambo halipo, Mungu hana utaratibu huo wa kulinganisha watu.Yeye huwa anasimama katika utaratibu wake. Ni sawa na mwalimu anayesahihisha mitihani, hasahishi kwasababu fulani ni machachari kuliko wengine, hapana, bali kwasababu amejibu sawasawa na alichotaka.

Ndivyo ilivyo kwa Mungu, hana habari na sura ya mtu, ikiwa wewe utatembea katika njia zake, basi atakuwa rafiki kwako, wala hakulinganishi na mtu mwingine aliye juu yako au aliye chini yako, na Yule mwingine hamlinganishi na wewe, bali wote anawalinganisha na Neno lake, kila mmoja kivyake.

Hivyo na wewe tembea katika njia yako, na Mungu wako, acha kujilinganisha na fulani, jilinganishe na biblia. Vinginevyo shetani atakuletea mikandamizo ya mawazo ukashindwa kumtumikia Mungu kwa ufanisi, kwa kumwona fulani tayari ni mtiwa mafuta wa Bwana, wewe huwezi kumfikia yeye.

Mawazo kama hayo yakatae.

Kumbuka, kuingia katika wokovu ni kurahisi sana, lakini kudumu kunakuwa kugumu, na hiyo yote inasababishwa na shetani na mapepo yake, Na dawa ya shetani sio tu kuomba, bali pia kulijua NENO. Nikisema Neno, sio kukariri vifungu vya biblia hapana, bali kupata ufunuo wa Neno la Mungu katika maisha yako ya kila siku.

Bwana Yesu alimshinda shetani kwa Neno kule jangwani, vivyo hivyo na wewe. Mungu anaweza akawa ameshakupa uhuru, lakini kama hutakuwa na maarifa ya kutosha ya kuupigania uhuru wako, bado ibilisi atakusumbua hata kama umeokoka. Maombi ya kufunguliwa pekee hayawezi kukufanya kuwa huru.. Kama ni hivyo Bwana Yesu asingesema..Mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru” (Yohana 8:32)Umeona kinachokamilisha uhuru wa mtu ni KWELI, na KWELI ni Neno la Mungu. (Yohana 17:17)

Hivyo jitahidi sana, uwe mtafakariji wa Neno. Ili ujue nafasi yako kwa Mungu ni ipi, wakati huu ni wakati wa vile VITA vikali ambavyo, Danieli alionyeshwa, katika (Danieli 10:1). Si vita tena vya kimwili, bali vita vya kifikra vinavyoletwa na ibilisi na mapepo yake.

Kama hujatubu, nafasi bado unayo. Tubu sasa mgeukie muumba wako, kisha ukabatizwe katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako, ikiwa hukufanya hivyo. Na baada ya hapo Mungu atakupa Roho wake Mtakatifu atakayekusaidi kuifahamu kweli yote ili uwe huru (Yohana 16:13).

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya kumwabudu Mungu katika Roho na kweli?

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

ZIFAHAMU KAZI TATU ZA ROHO MTAKATIFU KATIKA ULIMWENGU.

NAMNA YA KUITAMBUA SAUTI YA MUNGU INAPOZUNGUMZA NA WEWE

SI KWA UWEZA WALA KWA NGUVU BALI KWA ROHO YANGU, ASEMA BWANA.

Rudi nyumbani

Print this post

VAZI LA YESU HALIGAWANYWI.

Nakusalimu katika jina kuu sana la mwokozi wetu Yesu Kristo. Karibu tuyatafakari maandiko maadamu siku ile inakaribia.

Tukitazama matukio yaliyokuwa yanaendelea pale msalabani yapo mambo kadha wa kadha tunaweza kujifunza. Kwamfano siku ile utaona walimvua  nguo zake zote, wakazigawanya mafungu manne, kila askari fungu lake. Hii ikiwa na maana kuwa Bwana Yesu alisulibiwa akiwa uchi kabisa, hakutuonea haya sisi, iweje sisi tumwonee haya  yeye?

Lakini wale askari walipofika kwenye Kanzu yake nayo, kwasababu ilikuwa ni ya Tano, na wenyewe walikuwa ni wanne, na kila mmoja alitaka apate sehemu ya vazi lile..Wakaona njia rahisi ni kuligawanywa, walau kila mtu apate kipande chake.

Lakini lile vazi lilikuwa ni la kitofauti sana, lilikuwa halijashonwa kwa kuunganishwa vipande mbalimbali hapana.Bali Lote tokea juu hadi chini lilikuwa ni vazi moja, kiasi kwamba kulikuwa hakuna sehemu lilikuwa na kipande kilichojitegemea kikaunganishwa nalo hapana. Unaweza kutazama mfano wa vazi hilo kwenye picha juu.

Hivyo wale askari walipotafuta walau, maungio ya vazi lile ili wawezi kukata wagawane kila mtu kipande chake hawakuona. Pengine walitafuti kwenye mikono hawakuona, kwenye kola hawakuona, kwenye mfuko hawakuona. Mwishoni wakaona ni heri walipigie tu kura, ili liwe la mmojawapo.

Yohana 19:23 “Nao askari walipomsulibisha Yesu, waliyatwaa mavazi yake, wakafanya mafungu manne, kwa kila askari fungu lake; na kanzu nayo. Basi kanzu ile haikushonwa, ilikuwa imefumwa yote pia tangu juu.

24 Basi wakaambiana, Tusiipasue, lakini tuipigie kura, iwe ya nani. Ili litimie andiko lile linenalo, Waligawanya nguo zangu, Na vazi langu wakalipigia kura. Basi ndivyo walivyofanya wale askari”.

Lakini tunaposoma habari hiyo ni jambo gani Mungu anataka tujue? Je! Ni mambo ya mavazi yake tu kupigiwa kura tu au ni nini?

Ujumbe mkuu Mungu anataka tuone hapo  ni  kwamba VAZI LA YESU HALIGAWANYI.. Kwasababu halija ungwaungwa, kama mengine yalivyo. Kama utalihitaji ni sharti ulichukue lote, au uliharibu kabisa, hakuna namna..

Hata sasa, mtu yeyote anayeamua kuwa mkristo, hana budi alivae vazi hili. Ambalo haliungwi ungwi.. Ndilo linalojulikana kama VAZI LA WOKOVU, Tunalolisoma katika

Isaya 61:10 “Nitafurahi sana katika Bwana, nafsi yangu itashangilia katika Mungu wangu; maana AMENIVIKA MAVAZI YA WOKOVU, AMENIFUNIKA VAZI LA HAKI, kama bwana arusi ajipambavyo kwa kilemba cha maua, na kama bibi arusi ajipambavyo kwa vyombo vya dhahabu.

Unapolivaa vazi hili ni  lazima UUISHI wokovu wote, huwezi kuyakwepa maisha ya utakatifu.. Wakristo wengi wanatafuta kuligawanya vazi la wokovu wawe nalo kwa sehemu tu, hawataki kujitoa kikamilifu kwa Mungu pale wanapookoka. Wanataka waitwe wanakwaya, lakini bado waendelee na uzinzi kwa chini chini, wanataka waitwe vijana waliokoka, lakini waendelee kwenda disco, wavae vimini, na milegezo, na viduku, Wanadhani, hilo jambo linawezekana katika wokovu. Ni kweli litawezekana kwenye dini zao, na madhehebu yao, lakini kwa KWA YESU hilo jambo halipo.

Ndugu, watakaokwenda kwenye UNYAKUO, watakuwa wale tu walio tayari kulichukua vazi lote la Yesu, hao ndio wanaojulikana kama BIBI-ARUSI wa Kristo. Lakini tukijidanganya kuwa tumeokoka, halafu bado tupo nusu nusu, hatueleweki sisi ni wa upande upi, ipo wazi kuwa wakati ule tatabaki tu hapa duniani kwenye dhiki kuu ya mpinga-Kristo, na kama hutakuwa hai, basi utaendelea kubakia makaburini mpaka siku ile ya ufufuo itakapofika uhukumiwe uende motoni.

Ufunuo 19:7 “Na tufurahi, tukashangilie, tukampe utukufu wake; kwa kuwa arusi ya Mwana-Kondoo imekuja, na mkewe amejiweka tayari.

8 Naye amepewa kuvikwa kitani nzuri, ing’arayo, safi; KWA MAANA KITANI NZURI HIYO NI MATENDO YA HAKI YA WATAKATIFU”.

Naamini utakuwa unatambua kuwa tunaishi katika kanisa la Laodikia, na uvuguvugu na tabia ya kanisa hili ni kuwa lipo Vuguvugu, tofauti na  yale mengine. Hivyo Bwana atuepushe na uvuguvugu huu uliopo duniani leo.

Maran atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

PINDO LA VAZI LAKE SASA LIMEREFUSHWA.

Nini maana ya “mkilichukia hata vazi lililotiwa uchafu na mwili”?

kwanini yule kijana aliitupa ile nguo ya kitani chini na kukimbia uchi?

WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.

Rudi nyumbani

Print this post

Biblia inamaana gani kusema “vipo sita, naam saba”?

SWALI: Biblia inamaana gani kusema “vipo sita, naam saba”. Kwanini isingesema tu mara moja saba, mpaka ianze sita,halafu tena saba?


JIBU: Ni lugha ya zamani, iliyotumika kuwekea msisitizo kitu hususani kile cha mwisho, yaani, kama inadhaniwa ni sita, basi kipo na cha saba ambacho ndio zaidi.

Kwa mfano ukisoma ile Mithali 6:16  inayozungumzia mambo sita ambayo Mungu anayachukia utaona anaongezea na kingine cha saba, ambacho  ni “kupanda mbegu ya fitina katika ya ndugu” ikiwa na maana hicho ndio kibaya zaidi..

Mithali 6:16 “Kuna vitu sita anavyovichukia Bwana; Naam, viko saba vilivyo chukizo kwake.

17 Macho ya kiburi, ulimi wa uongo, Na mikono imwagayo damu isiyo na hatia;

18 Moyo uwazao mawazo mabaya; Miguu iliyo myepesi kukimbilia maovu;

19 Shahidi wa uongo asemaye uongo; Naye apandaye mbegu za fitina kati ya ndugu”.

Ukisoma pia  Mithali 30:18 “utaona Sulemani anasema tena kati ya mambo ambayo yanamshangaza mienendo yao, yapo matatu lakini lile la nne ndio zaidi, ambalo ni mwendo wa kijana pamoja na msichana.

Mithali 30:18 “Kuna mambo matatu yaliyo ya ajabu kwangu, Naam, kuna manne nisiyoyafahamu.

19 Mwendo wa tai katika hewa; Na mwendo wa nyoka juu ya mwamba; Mwendo wa merikebu katikati ya bahari; Na mwendo wa mtu pamoja na msichana”.

Vivyo hivyo, ukisoma Mithali 30:29, Sulemani anasema pia vipo vitu vitatu vyenye mwendo wa kupendeza lakini akakiongezea na cha nne chenye mwendo wa kupendeza zaidi nacho ni mfalme asiyehasika.

Mithali 30:29 “Kuna watatu wenye mwendo wa kupendeza, Naam, wanne walio na mwendo mzuri.

30 Simba aliye hodari kupita wanyama wote; Wala hajiepushi na aliye yote;

31 Jimbi aendaye tambo; na beberu; Na mfalme ambaye haasiki”.

Soma, pia vifungu hivi;

Mithali 30:15 “Mruba anao binti wawili, Waliao, Nipe! Nipe! Kuna vitu vitatu visivyoshiba kamwe, Naam, vinne visivyosema, Basi!

16 Kuzimu; na tumbo lisilozaa; Nchi isiyoshiba maji; na moto usiosema, Basi!”

Ayubu 5:19 “Yeye atakuokoa na mateso sita; Naam, hata katika saba hapana uovu utakaokugusa.

Amosi 1:3 “Haya ndiyo asemayo Bwana; Kwa makosa matatu ya Dameski, naam, kwa manne, sitaizuia adhabu yake isimpate; kwa sababu wameipura Gileadi kwa vyombo vya kupuria vya chuma”;

Soma pia Amosi 1:4.

Na hata sasa, katika mambo saba(7) ambayo  biblia inasema yanamkamilisha mwanadamu, lipo la nane(8) ambalo ndio kuu zaidi linaloitwa UPENDO.

Tusome.

2Petro 1:5 “Naam, na kwa sababu iyo hiyo mkijitahidi sana kwa upande wenu, katika imani yenu tieni na wema, na katika wema wenu maarifa,

6 na katika maarifa yenu kiasi, na katika kiasi chenu saburi, na katika saburi yenu utauwa,

7 na katika utauwa wenu upendano wa ndugu, na katika upendano wa ndugu, UPENDO.

8 Maana mambo hayo yakiwa kwenu na kujaa tele, yawafanya ninyi kuwa si wavivu wala si watu wasio na matunda, kwa kumjua Bwana wetu Yesu Kristo.

Ni vizuri tukawa na hayo mengine yote, lakini tukikosa upendo wa Ki-Mungu, basi bado hatujakamilishwa.

Je! Upendo wa AGAPE upo ndani yako?

Ili kufahamu tunaupate upendo wa namna hii, fungua link hii>>

https://wingulamashahidi.org/2020/12/21/nitaupataje-upendo-wa-ki-mungu-ndani-yangu/ 

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

UPENDO NI NINI NA JE! KUNA AINA NGAPI ZA UPENDO?

NI NINI KITAKACHOTUFANYA TUPIGE MBIO BILA KUPUNGUZA MWENDO?

UFUNUO: Mlango wa 1

Je! kuna madhara kuchukiwa na kila mtu kwasababu huna mali?. Kama biblia inavyosema katika Mithali 14:20?.

Mpumbavu ni nani katika biblia? (Zaburi 14:1, Mithali 10:14)

Rudi nyumbani

Print this post

Ni yupi aliyekuwa mkwe wa Musa kati ya Reueli na Yethro?

JIBU: Ukisoma katika kitabu cha Kutoka, utaona kuna habari kama inajichanganya kuhusiana na baba-mkwe halisi wa Musa, Kwamfano Kutoka 2:18 Inasema aliitwa Reueli, lakini sehemu nyingine zote zilizosalia kama vile Kutoka 3:1,4:18, inamtaja kama ni Yethro. Je  kuna makosa ya kiuandishi?

Embu tusome baadhi ya vifungu hivyo;

Kutoka 2:15 “Basi Farao alipopata habari, akataka kumwua Musa; lakini Musa akakimbia mbele ya Farao, akakaa katika nchi ya Midiani; akaketi karibu na kisima.

16 Basi kuhani wa Midiani alikuwa na binti saba, nao wakaja wakateka maji, wakazijaza birika maji, wapate kunywesha kundi la baba yao.

17 Wachungaji wakaja wakawafukuza; lakini Musa akasimama, akawasaidia, akalinywesha kundi lao.

18 Walipofika kwa Reueli baba yao, akasema, Imekuwaje hata mkarejea mapema leo?

19 Wakasema, Mmisri mmoja alituokoa katika mikono ya wachungaji, tena zaidi ya hayo, akatutekea maji, akalinywesha kundi.

20 Akawaambia binti zake, Yuko wapi basi? Mbona mmemwacha mtu huyo? Mwiteni, ale chakula.

21 Musa akawa radhi kukaa kwake mtu yule, naye akampa Musa binti yake, Sipora.

Kutoka 3:1 “Basi huyo Musa alikuwa akilichunga kundi la Yethro mkwewe, kuhani wa Midiani; akaliongoza kundi nyuma ya jangwa, akafika mpaka mlima wa Mungu, hata Horebu”.

Jibu ni kuwa hakuna hitilafu, yoyote ya kiuandishi isipokuwa zamani ilikuwa ni jambo la kawaida mtu mmoja kuwa na jina zaidi ya moja, Kwamfano tukimtazama Yakobo, Mungu alimwambia utaitwa Israeli, Hivyo majina yake yote mawili utayakuta yakiandikwa sehemu mbalimbali katika biblia Lakini mtu ni Yule Yule mmoja.

Vivyo hivyo na Yethro mkwewe Musa, aliitwa pia Reueli, na kwasababu alikuwa ni kuhani, hatushangai kuona akiwa na majina mawili, moja la kwake la asili na lingine la kikuhani.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine

Mada Nyinginezo:

UTAJI ULIOKUWA JUU YA USO WA MUSA.

Je Musa yupo anawashitaki watu..kulingana na Yohana 5:45?

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

NJIA YA KUPATA WOKOVU.

Je Musa kumwoa Sipora, Mkushi alifanya dhambi?

USIKATE TAMAA UNAPOPITIA MAGONJWA.

Rudi nyumbani

Print this post

TABIA ZA WATAKAOMKARIBIA SANA MUNGU SIKU ILE.

Kwa mara ya kwanza Yohana alionyeshwa maono ya jinsi mbinguni kulivyo, na mfumo wake mzima wa utawala ulivyojiunda.

Tukisoma mambo yale tusidhani, Mungu alikuwa anamuonyesha Yohana sinema tu ya mbinguni jinsi kulivyo, Hapana zipo siri kubwa sana zinazotuhusu sisi, endapo tutazitambua.

Leo kwa ufupi tutazama ngazi hizo, na ni jinsi gani zilivyoficha siri za sisi kumkaribia Mungu..

Ukisoma kile kitabu cha Ufunuo, sura ya 4 yote, utaona Yohana alionyeshwa mbingu zikifunga. Na moja kwa moja macho yake yakakiona kile kiti cha Enzi cha Mungu kilichojaa utukufu mwingi.

Lakini kiti hichi hakikusimama peke yake, bali alionyeshwa pia viti 24 ambavyo vimekizunguka kile kiti cha enzi ambavyo vimekaliwa na wale wazee 24, na katikati ya vile viti 24 aliona pia wenye uhai 4 ambao wamesimama mbele ya kile kiti cha enzi. Na nyuma ya wale wazee 24 kulikuwa maelfu kwa maelfu ya malaika mbinguni  wamemzunguka Mungu, wakimsifu na kumtukuza. Soma Ufunuo sura ya 4 yote.

Embu tusome baadhi ya vifungu kidogo; Tafadhali soma kwa utulivu,usiviruke.

Ufunuo 4:1 “Baada ya hayo naliona, na tazama, mlango ukafunguka mbinguni, na sauti ile ya kwanza niliyoisikia kama sauti ya baragumu ikinena nami, ikisema, Panda hata huku, nami nitakuonyesha mambo ambayo hayana budi kuwako baada ya hayo.

2 Na mara nalikuwa katika Roho; na tazama, kiti cha enzi kimewekwa mbinguni na mmoja ameketi juu ya kile kiti;

3 na yeye aliyeketi alionekana mithili ya jiwe la yaspi na akiki, na upinde wa mvua ulikizunguka kile kiti cha enzi, ukionekana mithili ya zumaridi.

4 Na viti ishirini na vinne vilikizunguka kile kiti cha enzi, na juu ya vile viti naliona wazee ishirini na wanne, wameketi, wamevikwa mavazi meupe; na juu ya vichwa vyao walikuwa na taji za dhahabu.

5 Na katika kile kiti cha enzi kunatoka umeme na sauti na ngurumo. Na taa saba za moto zilikiwaka mbele ya kile kiti cha enzi, ndizo Roho saba za Mungu.

6 Na mbele ya kile kiti cha enzi kulikuwa na mfano wa bahari ya kioo, kama bilauri; na katikati ya kile kiti cha enzi, na pande zote za kile kiti, walikuwako wenye uhai wanne, wamejaa macho mbele na nyuma”.

Ufunuo 5:11 “Nikaona nikasikia sauti ya malaika wengi pande zote za kile kiti cha enzi, na za wale wenye uhai, na za wale wazee, na hesabu yao ilikuwa elfu kumi mara elfu kumi na elfu mara elfu,

12 wakisema kwa sauti kuu, Astahili Mwana-Kondoo aliyechinjwa, kuupokea uweza na utajiri na hekima na nguvu na heshima na utukufu na baraka.

13 Na kila kiumbe kilichoko mbinguni na juu ya nchi na chini ya nchi ya juu ya bahari, na vitu vyote vilivyomo ndani yake, nalivisikia, vikisema, Baraka na heshima na utukufu na uweza una yeye aketiye juu ya kiti cha enzi, na yeye Mwana-Kondoo, hata milele na milele.

14 Na wale wenye uhai wanne wakasema, Amina. Na wale wazee wakaanguka, wakasujudu.

Sasa ni vizuri ukajiuliza kwanini walivyozidi kumkaribia Mungu, walionekana na maumbile tofauti tofauti. Ikumbukwe kuwa hao wote wanaozungumziwa hapo ni malaika, hakuna mwanadamu hata mmoja. Jiulize ni kwanini wawe ni wazee, na si vijana, na vilevile kwanini wale wenye Uhai wanne wawe na maumbile kama yale na si vinginevyo.?

Hiyo ni kufunua kuwa rohoni, na sisi tukitaka kumkaribia sana Mungu, basi hatuna budi kupitia hatua kama za wale wanaoonekana wapo karibu sana na Mungu.

Kwamfano tukiwatazama wale wazee 24, wanafunua kuwa ili mtu aweze kumkaribia Mungu sana, ni lazima awe ni mzee rohoni, awe amekomaa siku za wokovu ndani yake. Awe kama Ibrahimu, awe kama Henoko aliyetembea na Mungu kwa miaka 300 bila kumwacha, awe kama Eliya aliyemtumikia Mungu mpaka uzee wake, awe kama Ayubu, Hana, na Simoni, Zekaria na Elizabeti. Ambao hao walitembea katika haki yote na Mungu wao bila kumwacha. Watu wa namna hiyo, wanapomaliza siku zao hapa duniani, na wametembea na Mungu tangu ujana wao, mpaka kufa kwao, basi ni wazee rohoni. Na hivyo watakapovuka kule ng’ambo watakuwa karibu sana na Mungu.

Kwasababu Mungu naye, anajitambulisha kama mzee wa siku (Danieli 7:9). Hivyo na wale watakaomkaribia ni lazima wawe wameshiba siku za wokovu, Lakini ikiwa wewe unataka kuwa mkristo tu wa kufa ili uende mbinguni, hutaki kutenda mapenzi ya Mungu angali ukiwa hapa duniani, hutaki kukua kiroho, ujue kuwa ukifa leo hii, kamwe hutakaa umkaribie Mungu kule mbinguni, utakuwa mtu baki tu, haijalishi umeikwepa hukumu

Kwa urefu wa somo hilo fungua link hii>>

https://wingulamashahidi.org/2021/02/22/tutamkaribia-mungu-kwa-idadi-ya-mvi-zetu-rohoni/

Sasa tupige hatua mbele kidogo, kumbuka hawa malaika 24 ambao walifanana sana na wanadamu wazee 24 ni kweli walikuwa karibu na sana na Mungu, lakini wapo waliokuwa karibu zaidi ya Mungu kuliko wao. Na hao si wengine zaidi ya wale wenye uhai 4.

Wenye Uhai 4 walisimama moja kwa moja mbele ya kiti cha enzi cha Mungu, mbele ya wale wazee 24, Ndio makerubi wa Mungu. Hawa walikuwa na nyuso 4 kila mmoja. Uso wa kwanza upande wa kulia ulikuwa ni wa simba, upande wa kushoto ulikuwa ni wa ndama, upande wa nyuma ulikuwa ni wa Tai, na upande wa  mbele ulikuwa ni kama wa binadamu. Ndivyo Ezekieli alivyoonyesha kwa uwazi wote viumbe hai hao  jinsi walivyo (Ezekieli 1:1-26)

Japokuwa Yohana alionyeshwa upande mmoja mmoja wa kila kiumbe hai huyo kwasababu kulikuwa na sababu ya yeye kuonyeshwa vile, Lakini wote hao walikuwa na sura 4 kila mmoja wao (Soma Ufunuo 4).

Sasa kama tulivyotangulia kusema, haikuwa sinema tu, kwamba Mungu anataka kutuonyesha viumbe hao jinsi walivyo wa ajabu hapana. Bali alikuwa anatuonyesha kuwa na sisi tukitaka kumkaribia zaidi yeye. Ni lazima tuwe kama wao Rohoni, kwamba ni lazima uwe na sura hizo nne, ili ukidhi vigezo vya kuwa karibu sana na Mungu. hivyo tu.

Na leo kwa ufupi tutatazama kila uso wa hao makerubi, unawakilisha nini kwa leo. Tukianzana na ule..

USO WA SIMBA:

Kama tunavyojua simba ni mnyama jasiri asiye na woga,

Mithali 30:29 “Kuna watatu wenye mwendo wa kupendeza, Naam, wanne walio na mwendo mzuri.

30 Simba aliye hodari kupita wanyama wote; Wala hajiepushi na aliye yote;”

Kuonyesha kuwa kama mkristo, ni lazima uvae sura ya ujasiri kwa ajili ya imani yako na injili, kama Yesu Kristo alivyokuwa, na ndio maana anaitwa Simba wa Yuda (Ufunuo 5:6). Yeye hakuogopa mwanadamu yoyote, ilipofika suala la wokovu hata Herode alipotaka kumkamata, aliwaambiwa wale watu akisema “mwambieni Yule MBWEHA”!.. kuonyesha kuwa yeye hababaishwi na mwanadamu yoyote kuhubiri injili.

Vilevile na sisi ni lazima tuwe kama simba tukiwa hapa duniani kwasababu shetani naye hatufuati kama kondoo, bali kama Simba, biblia inasema hivyo katika 1Petro 5:8, Unategemea vipi na sisi tumwendee kwa upole katika kuuharibu ufalme wake?

USO WA NDAMA:

Upande wa kushoto wa vile viumbe walikuwa na uso wa ndama. Kama tunavyojua ndama ni wanyama wa kafara, wa kuchinjwa, wa kuchukua  dhambi za watu n.k. Hivyo hiyo ni kuonyesha kuwa unapokuwa mkristo ni lazima uso wa ndama/mwana kondoo, uwe nao pia. Yaani ukubali kuteseka kila siku kwa ajili ya manufaa ya wengine, na si yako tu peke yako. Ukubali hata kujinyima kwa ajili ya injili,

Paulo alisema..”Ninakufa kila siku”.. 1Wakor 15:31. Hata Bwana wetu Yesu Kristo alikuwa tayari kuutoa uhai wake kwa ajili yetu, ili sisi tupate ondoleo la dhambi. Vivyo hivyo na sisi kama wakristo, tunapaswa tuwe na uso huu wa ndama ndani yetu. Tuwe tayari kufa kila siku kwa ajili ya injili ya Kristo. Kujitoa ikiwemo na mali zetu  na nguvu zetu kwa ajili ya injili., kama alivyofanya Kristo na mitume wake.

USO WA TAI:

Wenye uhai 4 walikuwa na uso wa Tai kwa nyuma. Tai ni ndege anayeiona mbali sana, Jicho lake linaweza kuona chakula kutokea mbali sana, mahali ambapo wewe huwezi hata kumuona juu. Na sio tu chakula, bali pia maadui.

Na ndio maana Bwana Yesu alisema katika siku za mwisho, ni Tai tu ndio watakaoweza kuona chakula cha kweli cha roho kilipo. Wengine wote watakuwa kama kuku, wakisikia Kristo yupo huku wanakimbilia, yupo kule wanakimbilia, manabii wa uongo na imani potofu zikiwachanganya, wanabahatisha kwasababu macho yao hayawezi kuona mbali.

Luka 17:37 “Wakajibu, wakamwuliza, Wapi, Bwana? Akawaambia, Ulipo mzoga, ndipo watakapokutanika tai”.

USO WA MWANADAMU:

Wenye uhai 4 hawa walikuwa pia na nyuso wa binadamu kwa mbele.

Kumbuka mwanadamu, ndiye aliyejuu ya zaidi ya wanyama wote ambao Mungu alishawahi kuwaumba. Mwanadamu anao ujuzi, hekima, utashi, fikra, elimu, ujuzi, maarifa. Kwa kutumia tu utashi aliopewa na Mungu anaweza kubuni na kuvumbua mambo makubwa sana, ambayo yanaweza kumletea matokeo chanya au matokeo hasi. Inategemea na dhima yake ni nini.

Hivyo, Na sisi pia ni lazima tutumie utashi wetu tuliopewa na Mungu, kumpendeza Mungu. Sio kila mahali, tutatumia maombi tu peke yake hapana. Wakati ule Mungu anampa Musa maagizo ya kutengeneza vitu vya hemani, alimwambia akamtafute mtu aliyeitwa Bazaleli, ambaye Mungu atampa  ujuzi na utashi wa uchongaji wa vitu hivyo.

Kutoka 31:1 “Bwana akanena na Musa, na kumwambia,

2 Angalia, nimemwita kwa jina lake Bezaleli mwana wa Uri, mwana wa Huri, wa kabila ya Yuda;

3 nami nimemjaza roho ya Mungu, katika hekima, na maarifa, na ujuzi, na mambo ya kazi ya kila aina,

4 ili abuni kazi za ustadi, kuwa fundi wa dhahabu, na wa fedha, na wa shaba”,

Tujiulize je! Sisi tulishawahi kumbunia nini Mungu?  Watu wa ulimwengu wanatushinda, wao kila siku wanambunia mungu wao shetani, mambo mapya kila siku, mengi ya kuwavutia wao, wanamtungia kila aina ya nyimbo za miundo tofauti tofauti, lakini sisi kama wakristo, ujuzi wetu tuliopewa na Mungu tumeuweka kapuni, tukimwimbia Mungu badala tufikirie ni jinsi gani nyimbo zetu zitakuwa zimejaa Roho, sisi tunawaiga wale wa kidunia staili zao.

Bwana atusaidie sana.

Hivyo Bwana atusaidie sana. Nyuso zote hizo 4 tuwe nazo. Yaani tuwe jasiri kama Simba, tuwe wa kujitoa kama ndama, tuwe na jicho la kuona mbali chakula chetu kilipo kama Tai, na pia tuwe na hekima na ujuzi kama mwanadamu.

Tukiweza hayo, basi tujue kuwa tutakuwa karibu sana Mungu, kuliko tunavyodhani, kwasababu shetani anakuwa hana upenyo wa kutuingilia. Kwasababu kila upande kuna uso tunamwona.

Mwisho, kabisa, upako wa wenye uhai hawa wanne ulitembea pia katika nyakati saba za kanisa. Hivyo kama utapenda kufahamu kwa urefu juu ya nyakati hizo na jinsi mihuri ile ilivyofunguliwa basi fungua link hii utakutana na mfufulilizo wa maelezo hayo.

https://wingulamashahidi.org/2018/07/19/mihuri-saba/

Bwana akubariki sana.

Je! Umeokoka ndugu? Je! Una habari kuwa tunaishi katika kipindi ambacho tutashuhudia tukio la kurudi kwa pili kwa Kristo duniani?  Unalifahamu hilo? Kwasababu hakuna dalili hata moja Kristo aliyoizungumzia haijatimia. Ni heri ukayasalimisha maisha yako leo kwake, ili siku ile isikukute pabaya.

Tubu kwa kumaanisha kabisa, kisha kabatizwe katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo upate ondoleo la dhambi zako.

Jina la Bwana libarikiwe.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine

Mada Nyinginezo:

UNYAKUO.

UFUNUO: Mlango wa 4

PINDO LA VAZI LAKE SASA LIMEREFUSHWA.

IFAHAMU HUZUNI NA FURAHA YA MALAIKA.

KAMA MKRISTO FAHAMU ZIPO HATUA UTAPIGISHWA NA MUNGU.

NYAKATI SABA ZA KANISA NA WAJUMBE WAKE.

Rudi nyumbani

Print this post

WALIYATWAA MAVAZI YAKE, WAKAFANYA MAFUNGU MANNE,

Yohana 19:23 “Nao askari walipomsulibisha Yesu, waliyatwaa mavazi yake, wakafanya mafungu manne, kwa kila askari fungu lake; na kanzu nayo. Basi kanzu ile haikushonwa, ilikuwa imefumwa yote pia tangu juu.

24 Basi wakaambiana, Tusiipasue, lakini tuipigie kura, iwe ya nani. Ili litimie andiko lile linenalo, Waligawanya nguo zangu, Na vazi langu wakalipigia kura. Basi ndivyo walivyofanya wale askari”.

Ulishawahi kujiuliza ni kwanini biblia haijakaa kimya kuhusiana na mavazi ya Yesu pale Goligotha, na jinsi yalivyopigiwa kura? Mpaka kufikia hatua ya kugawanywa katika mafungu manne (4) kwa wale askari wanne waliokuwa pale msalabani.? Na lile moja la 5 ambalo ni kanzu yake kupigiwa kura?. Haikuandikwa kutengeneza stori tu, kwamba Yesu alikuwa na mavazi matano, bali kulikuwa na maana nzito nyuma yake.

Hiyo ni kuonyesha kuwa hakubakiwa na nguo hata moja muda ule alipotundikwa  pale msalabani. Alisulibiwa akiwa uchi kabisa wa mnyama. Ni jambo ambalo haliwezekani kwamba nguo nyingine zipigiwe kura, na kugawanya, halafu nyingine abakiwe nazo kutundikiwa msalabani, Maandiko hayatuonyeshi hivyo. Kile tunachokiona kwenye misalaba ya kuchonga au kwenye muvi  kwamba Bwana Yesu alisulibiwa akiwa na kipande cha nguo cha kumsitiri, si kweli. Ukweli ni kwamba alisulibiwa akiwa uchi kabisa wa mnyama. Hata hivyo wakati ule wa Rumi wahalifu wote waliouliwa kwa kusulibiwa ilikuwa ni lazima wasulibiwe uchi, ili kwamba sio tu wafe kwa mateso bali pia wafe kwa aibu.

Je! ulishawahi kutafakari kwa utulivu kwanini Kristo aruhusu hayo yote yampitie, wakati alikuwa na uwezo kabisa wa kuyaepuka? Unadhani hakikuwa kitendo cha aibu kile? Kilikuwa ni kitendo kikubwa sana cha aibu, ambacho ninauhakika hata wewe ungekuwepo wakati ule usingedhubutu hata kumwangalia pale msalabani akiwa katika hali ile. Lakini yeye hakuona aibu, kuwekwa uchi, ilimradi tu mimi na wewe tu tuokoke. Huko ni kujitoa kulikopitiliza.

Hakunionea haya mimi, vilevile hakukuonea haya wewe, kinyume chake biblia inatuambia aliidharau aibu,

Waebrania 12:2 “tukimtazama Yesu, mwenye kuanzisha na mwenye kutimiza imani yetu; ambaye kwa ajili ya furaha iliyowekwa mbele yake aliustahimili msalaba NA KUIDHARAU AIBU, naye ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Mungu”.

Unaona, ukitafakari hilo vizuri, ndugu yangu, hutaona sababu ya wewe kumwonea aibu Bwana wako, katika dunia hii mbovu. Hutaona aibu kuitwa mshamba, kwa ajili yake, hutaona sababu  kuogopa kuitangaza injili yake.

Paulo alisema..

Warumi 1:16 “Kwa maana siionei haya Injili; kwa sababu ni uweza wa Mungu uuletao wokovu, kwa kila aaminiye, kwa Myahudi kwanza, na kwa Myunani pia”.

Alimwambia pia Timotheo maneno hayo hayo;

2Timotheo 1:8a “Basi usiuonee haya ushuhuda wa Bwana wetu, ..;”

Huu si wakati wa kufikiria Fulani atanionaje, au marafiki watanichukuliaje, au majirani watanizungumziaje ikiwa nitampa Kristo Maisha yangu. Kumbuka Yesu hakukuonea haya wewe, aliposulibiwa uchi mbele ya kadamnasi, mbele ya maelfu ya watu waliokuwa pale Goligota, kwanini wewe umwonee haya yeye wakati hujafikia hata hatua ya kutembezwa uchi barabarani kwa ajili yake?.

Ukimkataa leo wakati utafika atakukataa na wewe.

Marko 8:38 “Maana kila mtu atakayenionea haya mimi, na maneno yangu, katika kizazi hiki cha uzinzi na dhambi, Mwana wa Adamu atamwonea haya mtu huyo, atakapokuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika watakatifu”.

Tengeneza picha unasimama mbele ya mamilioni kwa mamilioni ya malaika, halafu Kristo anakuonea aibu mbele yao, utajisikiaje? Hali Fulani mbaya,

Hivyo chukua msalaba wako ujitwike umfate Kristo. Hizi ni siku za mwisho, yupo mlangoni kurudi. Kama bado hujatubu basi huu ndio wakati wako, mwamini yeye ukabatizwe katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO, upate ondoleo la dhambi zako na yeye mwenyewe atakupa Roho wake Mtakatifu atakayekuongoza katika kweli yote.

Ikiwa utahitaji kuokoka, basi wasiliana nasi kwa namba hizi hapo chini, Nasi tutakusaidia katika hilo.

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine:

Mada Nyinginezo:

VAZI KUU AMBALO MUNGU AMETUANDALIA KILA MMOJA WETU.

kwanini yule kijana aliitupa ile nguo ya kitani chini na kukimbia uchi?

Kutahayari ni nini katika biblia?(2Timotheo 2:15)

MARINDA KATIKA BIBLIA NI KITU GANI?

Nguo za magunia katika biblia ni zipi?

Rudi nyumbani

Print this post

Kama tunaokolewa kwa neema kwanini wokovu tuupate kwa nguvu?

SWALI: Je! kuna mchango wowote sisi tunaweza kuuweka ili tupate wokovu wetu? Na  kama sio kwanini basi maandiko yanasema, ufalme wa mbinguni unapatikana kwa nguvu nao wenye nguvu ndio wanaouteka (Mathayo 11:12)?


JIBU: Kuhusu mchango wetu katika Neema ya wokovu, maandiko yapo wazi ni kuwa HAUPO.

Waefeso 2:8 “Kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani; ambayo hiyo haikutokana na nafsi zenu, ni kipawa cha Mungu;

9 wala si kwa matendo, mtu awaye yote asije akajisifu”.

Lakini swali linakuja kama ni hivyo basi kwanini, maandiko yanasema..

Mathayo 11:12 “Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatikana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka”.

Jibu ni kuwa adui yetu tupo naye ni shetani, huyo ndiye anayeifanya njia ya wokovu ionekane ni ya jitahada kidogo. Hivyo inahitaji nguvu ya ziada kuiona na vilevile kuiendea kwasababu ni nyembamba sana na imesonga.

Mathayo 7:13 “Ingieni kwa kupitia mlango ulio mwembamba; maana mlango ni mpana, na njia ni pana iendayo upotevuni, nao ni wengi waingiao kwa mlango huo.

14 Bali mlango ni mwembamba, na njia imesonga iendayo uzimani, nao waionao ni wachache”.

Kwamfano leo hii, shetani anaweza kukuzuia usimfanyie Kristo ibada, kisa tu wazazi wako wamekataa, au kazi yako imekusonga, au mazingira si rafiki hakuna mtu atakayekuelewa, unadhani ukiiruhusu hiyo hali, ataurithi uzima wa milele?. Haiwezekani, inahitaji kulazimisha mambo, kutumia nguvu, kukubali kuchukiwa, au wakati mwingine kupoteza hata kile ulichonacho, ili mradi tu usiopoteze wokovu wako.

Hapo ndipo neno ufalme wa mbinguni unapatikana  kwa nguvu, nao wenye nguvu ndio wanauteka.

Kwamfano, Kristo alituambia tukeshe tuombe, lengo la kusema vile lilikuwa ni kusudi tusiingie majaribuni(Mathayo 26:41), kwasababu adui yetu shetani anaishi kutuwinda. Sasa kama wewe husali, ili kuulinda wokovu wako uliopewa bure na Kristo bila kuusumbukia, unaona uvivu, ufahamu kuwa shetani atakesha kwa ajili yako, na siku ya siku ikifika atakuletea majaribu mazito, kama alivyowaletea wakina Petro usiku ule mpaka kufikia hatua ya kumkana Bwana na wengine kumtoroka uchi, unadhani walipenda? Hapana hiyo yote ni kutokana na kupuuzia kwao maagizo ambayo Yesu aliwapa muda mchache kabla kwamba wakeshe waombe, wao wakalala.

Vivyo hivyo, na wewe usipokuwa mwombaji, usipojitesa kufunga wakati mwingine, hata kutumika kwa ajili ya Kristo, ni ngumu  sana kuutunza wokovu wako kama sio kuupoteza kabisa.

Hivyo, hatumwamini Yesu na kubakia hivyo hivyo tu, hapana hiyo ni hatua moja, hatua ya pili ni lazima tushindane na tupambane, tupigane vita, na tuumie ili kuulinda wokovu wetu kwasababu adui yetu shetani yupo kuuwinda wokovu wetu usiku na mchana.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengi

Mada Nyinginezo:

Neema ni nini?

Kwanini Yakobo alimshinda Mungu, Je! Mungu huwa anashindwa na wanadamu?

NJIA YA KUPATA WOKOVU.

YEYE ALIYEUWASHA HUO MOTO LAZIMA ATALIPA.

Nini maana ya siku moja kwa Bwana ni kama miaka elfu, na miaka elfu ni kama siku moja? (2Petro 3:8)

Rudi nyumbani

Print this post