SWALI: Kwanini Mungu aliufananisha uzuri wa Kaanani na kama nchi ibubujikayo maziwa na asali? Kwanini isiwe kitu kingine chochote, labda dhahabu na nafaka?
Kutoka 3:8 “nami nimeshuka ili niwaokoe na mikono ya Wamisri, niwapandishe kutoka nchi ile, hata nchi njema, kisha pana; nchi ijaayo maziwa na asali; hata mahali pa Mkanaani, na Mhiti, na Mwamori, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi”.
JIBU: Mungu aliposema Kaanani ni nchi ibubujikayo maziwa na asali, hakumaanisha kuwa kuna mito ya maziwa, au mabomba ya asali, kila mahali hapana. Bali alitumia lugha hiyo ya picha kuonyesha uzuri wa nchi ile jinsi ulivyo.
Kama tunavyojua maziwa yanatolewa na mifugo, kama ng’ombe,. Na ng’ombe ili atoe maziwa mengi na ya kutosha, anategemea sana mazingira yenye malisho mazuri ya kijani na chemchemi nzuri za maji. Hivyo Hapo ni Mungu alikuwa anawaonyesha wana wa Israeli kuwa nchi waiendeayo si nchi kame, bali ni nchi yenye rutuba nyingi sana, ambayo mboga mboga na malisho mazuri vinastawi, kiasi kwamba tukisema ni maziwa basi mifugo yao itamwaga maziwa mengi sana, hadi yasiwatoshe kwa wingi wa malisho yaliyopo huko.
Vilevile aliposema asali, aliwalenga nyuki. Na nyuki ni wadudu wanaotegemea sana, aina mbalimbali za mimea na maua ili kutengeneza asali yao, Kama tunavyojua mahali ambapo pana jamii chache za miti na mimea, inawachukua muda mrefu sana kuunda asali kidogo, kwani inawagharimu kutembea umbali mrefu sana, kutafuta virutubisho hivyo.
Lakini kama wapo eneo lenye misitu, na jamii tofauti tofauti za miti na mimea, huwa inawachukua muda mfupi sana. Hivyo Mungu aliposema hiyo nchi ibubujikayo asali, alimaanisha kuwa ni nchi yenye aina mbalimbali ya miti ya vyakula na matunda, Kama tukisema ni nyuki watengeneze asali, basi asali itakuwa ni ya kumwagika sana.tofauti na hiyo nchi ya ukame waliyotoka.
Na ndio maana wale wapepelezi waliotumwa na Musa kwenda kuipeleleza Kaanani, aliporudi na kichala kikubwa cha mzabibu na tini na mkomamanga, waliwaambia wana wa Israeli maneno haya;
Hesabu 13:27 “Wakamwambia wakasema, Tulifika nchi ile uliyotutuma, na hakika yake, ni nchi yenye wingi wa maziwa na asali, na haya ndiyo matunda yake”
Unaona, kwa yale waliyoyakutana nayo huko walithibitisha maneno ya Mungu kuwa ni kweli, kuwa nchi hiyo ni ya maziwa na asali.
Hata sasa, Mungu ana mpango huo kwa watoto wake , kuwafikisha katika nchi hii, lakini ni lazima kwanza, awafundishe kanuni zake, na jinsi ya kuishi ndani yake. Vinginevyo wakiifikia na huku maisha yao bado hajabadilishwa, nchi hiyo itawatapika kama ilivyowatapika wenyeji wa Kaanani. Na kanuni zenyewe ni kuishi sawasawa na amri za Mungu (Neno lake).
Walawi 18:26 “Kwa hiyo mtazishika amri zangu na hukumu zangu, wala msifanye machukizo hayo mojawapo; yeye aliye mzalia, wala mgeni aketiye kati yenu; 27 (kwa kuwa hao watu wa nchi wameyafanya machukizo haya yote, hao waliotangulia mbele zenu, na hiyo nchi imekuwa najisi;) 28 ILI KWAMBA HIYO NCHI ISIWATAPIKE NA NINYI PIA, hapo mtakapoitia unajisi, kama ilivyoitapika hiyo taifa iliyotangulia mbele yenu”.
Walawi 18:26 “Kwa hiyo mtazishika amri zangu na hukumu zangu, wala msifanye machukizo hayo mojawapo; yeye aliye mzalia, wala mgeni aketiye kati yenu;
27 (kwa kuwa hao watu wa nchi wameyafanya machukizo haya yote, hao waliotangulia mbele zenu, na hiyo nchi imekuwa najisi;)
28 ILI KWAMBA HIYO NCHI ISIWATAPIKE NA NINYI PIA, hapo mtakapoitia unajisi, kama ilivyoitapika hiyo taifa iliyotangulia mbele yenu”.
Lakini tukiishi sawasawa na Neno lake, wakati huo utafika na Bwana atatuingiza katika nchi hiyo kama alivyofanya kwa wana wa Israeli walipozitii amri zake.
Hesabu 14:8 “Ikiwa Bwana anatufurahia, atatuingiza katika nchi hii atupe iwe yetu, nayo ni nchi yenye wingi wa maziwa na asali”.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali. Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
UNYAKUO.
Maziwa yasiyoghoshiwa ni nini? Kwanini biblia inatumia mfano huo?
UFUNUO: Mlango wa 18
Kuota upo nchi nyingine.
ESTA: Mlango wa 4
Rudi nyumbani
Print this post
Daudi ni mfalme ambaye alikuwa amezungukwa na mashujaa hodari sana, na mashujaa hao aliowachagua walikuwa wamegawanyika katika makundi makuu matatu, Kundi la kwanza kabisa ambalo lilikuwa ndio la juu kabisa zaidi ya yote liliundwa na maaskari watatu, na lile pili yake liliunda na wawili, na lile la tatu liliundwa na mashujaa 37.
Sasa ukitaka kujua kwa urefu ushujaa wao, na mashujaa wenyewe walikuwa ni wakina nani fungua link hii usome zaidi…
Lakini leo tutaona kwa ufupi, ni nini kilimtokea mmojawapo kati ya wale mashujaa watatu wa kwanza, Na ni ujumbe gani Kristo anataka tuupate kupitia ushujaa wake.
shujaa huyu aliitwa Eleazari, yeye kuna wakati walikutana na jeshi kubwa la wafilisti, wakati huo alikuwa peke yake tu, Israeli yote ilikuwa imeondoka, hata wale mashujaa wenzake hawakuwepo.. Lakini hakuogopa vita bali alinyanyuka na kuushikilia upanga wake mmoja.. akaanza kupigana na wafilisti yeye peke yake kama vile Samsoni, aliushikilia upanga wake kwa nguvu sana kiasi kwamba haikuwa rahisi kuuondoa mkononi mwake.
Lakini kwasababu maadui walikuwa wengi,kuna muda ulifika alilemewa sana, na ile nguvu ya kuendelea kuushikilia upanga ikamwishia, akataka kuuachilia ule upanga kwasababu alichoka sana, lakini biblia inatuambia upanga ule hakuwezi kutoka katika mkono wake, ikiwa na maana ulijiganda kama gundi katika mkono wake. Pale alipojaribu kurusha mkono, upanga haukuchomoka mkononi mwake, bali ulikwenda naye Hivyo akaendelea kupigana na wafilisti mpaka akawamaliza wote. Baadaye Israeli walipokuja kazi yao ikawa ni kuteka nyara tu huko nyuma, kwa kipigo cha jeshi la mtu mmoja.
2Samweli 23:9 “Na baada yake kulikuwa na Eleazari, mwana wa Dodai, Mwahohi, mmojawapo wa wale mashujaa watatu waliokuwa pamoja na Daudi; walipowatukana Wafilisti waliokuwa wamekusanyika huko ili kupigana, na watu wa Israeli walikuwa wamekwenda zao; 10 huyo aliinuka, akawapiga Wafilisti hata mkono wake ukachoka, na mkono wake ukaambatana na upanga; naye Bwana akafanya wokovu mkuu siku ile; nao watu wakarudi nyuma yake ili kuteka nyara tu”.
2Samweli 23:9 “Na baada yake kulikuwa na Eleazari, mwana wa Dodai, Mwahohi, mmojawapo wa wale mashujaa watatu waliokuwa pamoja na Daudi; walipowatukana Wafilisti waliokuwa wamekusanyika huko ili kupigana, na watu wa Israeli walikuwa wamekwenda zao;
10 huyo aliinuka, akawapiga Wafilisti hata mkono wake ukachoka, na mkono wake ukaambatana na upanga; naye Bwana akafanya wokovu mkuu siku ile; nao watu wakarudi nyuma yake ili kuteka nyara tu”.
Hiyo ni kuonyesha jinsi gani, mtu anapotaka kung’ang’ana na kusudi la Mungu, kusudi nalo litang’ang’ana naye, ili kutimiza lile lengo.
Leo hii ukiling’ang’ania kusudi la Bwana kwa moyo wako wote na kwa bidii, lile kusudi nalo litang’ang’ana na wewe tu, hamna namna, kwasababu hiyo ni kanuni ya ki-Mungu, hata kama utafikia wakati umechoka, bado litaendelea kukung’ang’ania tu. Na ndio maana unaona ni kwanini watumishi wa Mungu wa kweli, hawachoki kumtumikia Mungu, japokuwa hawafanyi kazi ya mshahara, sio kwamba hawachoki, au hawapitii magumu, au hawapungukiwi nguvu..wanachoka, lakini wakati wanakaribia kuanguka, lile kusudi la Mungu linang’ang’ana nao, hivyo wanajikuta bado wanaendelea mbele na safari.
Isaya 40:29 “Huwapa nguvu wazimiao, humwongezea nguvu yeye asiyekuwa na uwezo. 30 Hata vijana watazimia na kuchoka, na wanaume vijana wataanguka; 31 bali wao wamngojeao Bwana watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia”.
Isaya 40:29 “Huwapa nguvu wazimiao, humwongezea nguvu yeye asiyekuwa na uwezo.
30 Hata vijana watazimia na kuchoka, na wanaume vijana wataanguka;
31 bali wao wamngojeao Bwana watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia”.
Hata sisi sote, tunapodhamiria kweli kwa mioyo yetu yote, kutembea na Mungu, kamwe Mungu hawezi kutuachia katikati tuaibishwe na shetani, tunakuwa mfano wa Eleazari, nguvu za Mungu zitaambatana na sisi kuhakikisha kuwa lile kusudi la Mungu linatimia kwa gharama zozote zile.
Lakini tukiwa watu vuguvugu, leo tupo na Mungu kesho shetani, hatujajikana nafsi zetu na kusema kuanzia leo mambo ya ulimwengu basi, tunakwenda na Kristo. Kamwe nguvu ya Mungu haiwezi kushikamana na sisi kama alivyokusudia, pale tunapoishiwa nguvu au tunapokumbana na majaribu. Na ndio hapo utaona mkristo anakuwa moto na Mungu siku za mwanzoni mwanzoni, tu ikifika baadaye, anapoa, mpaka anauacha wokovu kabisa..ukimuuliza ni kwanini atasema, hali ya maisha ilikuwa ngumu, mwingine nilipitiwa na ujana, mwingine nilikuwa katika mazingira yasiyo rafiki,..Sasa tatizo halipo kwa Mungu bali kwa huyu mtu.
Kwasababu Mungu akishaianzisha safari ndani ya maisha ya mtu huwa haikatishi katikati, Kwasababu Mungu huwa hashindwi , anaelewa kabisa kuwa yapo majira mbalimbali tutapitia hapa duniani kama wakristo, hivyo anatuhakikishia nguvu ya ziada kutoka kwake, lakini hiyo inakuja endapo tu tutakuwa na nia ile ile ya kutembea naye.
Paulo alisema
Wafilipi 1:6 “Nami niliaminilo ndilo hili, ya kwamba yeye aliyeanza kazi njema mioyoni mwenu ataimaliza hata siku ya Kristo Yesu;”
Hivyo ishi maisha ya kumaanisha mbele zake, ishi ndani ya kusudi la Mungu, ili Mungu awe nawe nyakati za taabu. Swali ni Je umemaanisha kweli kumfuata Kristo? Kama bado basi leo ndio wakati wako wa kudhamiria kutoka katika moyo wako kutubu na kuacha dhambi zako zote, Fanya hivyo kisha baada ya hapo nenda kabatizwe katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO ikiwa hukubatizwa hapo kabla, Na Mungu mwenyewe atakupa Roho wake Mtakatifu, akutie nguvu hadi siku ukombozi wako.
Zingatia: Waliokombolewa na Mungu hawashindwi na ulimwengu.
Ikiwa utapenda upate huduma ya ubatizo sahihi, basi utawasiliana na sisi kwa namba hizi 0693036618, tukusaidie.
Shalom.
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo .jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
LIPO LA KUJIFUNZA KWA WALE MASHUJAA 37 WA DAUDI.
NA VIUNGO VYETU VISIVYO NA UZURI VINA UZURI ZAIDI SANA.
Tofauti kati ya ufalme wa mbinguni na ufalme wa Mungu ni ipi?
LISHIKILIE SANA LILE AGIZO LA KWANZA.
WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.
Nakusalimu katika jina kuu sana la Bwana wetu Yesu Kristo. Karibu tuyatafakari maandiko. Sisi kama wakristo, ili tuweze kukua kutoka utukufu hadi utukufu, na imani hadi imani, hatuna budi kuyatafakari maneno ya Mungu sana kwa kadiri tuwezavyo.
Leo tutajifunza tabia za kipekee walizokuwa nazo watu wa Makedonia nyakati zile za mitume.
Makedonia iliundwa na makanisa makuu matatu, (Kanisa la Wathesalonike, Wafilipi, na Waberoya). Hawa watu walikuwa ni wa kipekee sana, Kwamfano watu wa Beroya, tabia yao ya kupenda kuchunguza maandiko pengine iliwasaidia kutambua jukumu kubwa sana ambalo walipaswa walitimize katika utakatifu wao. Na jukumu lenyewe lilikuwa ni katika suala la UTOAJI.
Sasa kwa ufupi tutatazama waliwezaje kulitimiza hilo jukumu katika mazingira magumu waliyokuwa nayo. Naamini na sisi lipo la kujifunza kwa watu hawa, ili tusijikute tunakwamishwa na jambo lolote katika kuuelekea ukamilifu wetu. Embu tuzisome tabia zao ambao zinazungumziwa katika kitabu cha 2Wakorintho 8:1-15
Lakini hawakusahau kumtolea Mungu, katika umaskini wao, kiasi kwamba wao ndio wakaongoza katika kuitimiza huduma hiyo kuliko makanisa mengine yote .
2Wakorintho 8:1 “Tena ndugu zetu, twawaarifu habari ya neema ya Mungu, waliyopewa makanisa ya Makedonia; 2 maana walipokuwa wakijaribiwa kwa dhiki nyingi, wingi wa furaha yao na umaskini wao uliokuwa mwingi uliwaongezea utajiri wa ukarimu wao.
2Wakorintho 8:1 “Tena ndugu zetu, twawaarifu habari ya neema ya Mungu, waliyopewa makanisa ya Makedonia;
2 maana walipokuwa wakijaribiwa kwa dhiki nyingi, wingi wa furaha yao na umaskini wao uliokuwa mwingi uliwaongezea utajiri wa ukarimu wao.
Mfano mzuri wa kuiga, kumbe umaskini wetu, hauwezi kuwa kikwazo katika kumtolea Mungu.. Mtume Paulo anatuthibitishia kuwa maskini ndio walioongoza kumtolea Mungu miongoni mwa makanisa yote aliyoyahudumu mataifa mbalimbali.
2) Licha ya kuwa katika umaskini mwingi, lakini bado walikuwa tayari kutoa hata zaidi ya uwezo wao.
2Wakor 8:3 “Maana nawashuhudia kwamba, kwa uwezo wao, na zaidi ya uwezo wao, kwa hiari yao wenyewe walitoa vitu vyao;”
Embu tutengeneze picha, maskini pengine anayo sh.100 tu lakini anaona hiyo bado haistahili kuipeleka kwa Mungu, anakwenda kuuza hata ile baiskeli yake, anayoitegemea kwenda nayo shambani kila siku, ili tu apate kiasi kingi kidogo cha pesa akamtolee Mungu, awe radhi kutumia miguu yake kwenda shambani, kuliko kupeleka kiwango kidogo kwa Mungu wake. Unadhani huko tukuiteje, kama sio kutoa zaidi ya uwezo wako.
Sasa mambo kama haya, yalikuwa ni kawaida kwa watakatifu wa Makedonia.
Tujipime na sisi wakristo wa leo hii, pengine Mungu amekubariki gari, tuachilie mbali kwenda kuliuza na kumletea Mungu thamani yake je! Tunaweza kupanda daladala wiki 2 mfululizo, halafu hiyo pesa ambayo tungetumia katika kununua mafuta kila siku tukaipeleka kanisani? Je hilo linawezakana? Au utampelekea Mungu elfu 1, na huku wiki nzima umetumia elfu 50 ya mafuta?. Je tunaweza kuwafikia watakatifu hawa, ambao walijitoa kwa Mungu zaidi ya uwezo wao?
3) Walifurahia kumtolea Mungu, kwa moyo wa furaha, licha ya kuwa walikuwa ni maskini, na walitoa zaidi.. 2Wakor 8:3
Tabia nyingine ni hii, walifurahia kufanya hivyo. Hawakuwa wanung’unikaji, walipomtolea Mungu, ndivyo walivyopata amani mioyoni mwao, lakini ni rahisi sana kuona mtakatifu wa leo anatoa malalamiko kwa kila anachokitoa, utasikia, Yule mchungaji anakula sadaka zetu, mbona hatuoni matumizi ya pesa zetu kanisani. Na kwa kawaida ukiangalia hao wanaonung’unika hivyo, asilimia kubwa huwa si watoaji.
4) Wao wenyewe waliomba na kusihi katika kutoa.
8:4 “Wakituomba sana pamoja na kutusihi kwa habari ya neema hii, na shirika hili la kuwahudumia watakatifu”.
Unaona? Waliwasihi mitume, waitimize huduma hiyo, kana kwamba wanachokifanya ni kwa faida yao,. Embu fikiria wewe leo, mtu anakuja kukuomba akupe pesa tena kwa kukusihi, Unaweza kudhani ni tajiri sana, au ana pesa za mchezo, lakini kumbe sio, hawa watu walikuwa maskini kama tunavyosoma, lakini walijua wajibu wao kwa Bwana.
Na sisi je! Tutamsubiri mpaka mchungaji wetu atukumbushe, kwa habari za zaka? Atukumbushe kuwa kuna kazi ya injili inahitaji fedha? Hapana, ni wajibu wetu kukumbuka, na kumtolea Bwana, pale anapotuamrisha.
5) Pia Utoaji wao ulianza kwanza na kujitoa kwa Bwana.
2Wakor 8:5 “Tena walitenda hivi si kama tulivyotumaini tu, bali kwanza walijitoa nafsi zao kwa Bwana; na kwetu pia, kwa mapenzi ya Mungu”.
Kuonyesha kuwa, tabia ya utoaji, huwa chanzo chake ni kujitoa kwanza kwa Bwana.. Hawa watu walikubali kujibidiisha na mambo yote ya Mungu. Na ndio maana hawakuona ugumu wowote na kutoa hata zaidi ya uwezo wao kwa Mungu.
Hivyo mwisho kabisa mtume Paulo alipoona mwenendo wa watakatifu hawa wa Makedonia alitaka na makanisa mengine yote yaige mfano wao, hususani kanisa la Korintho, litimize karama hiyo pia, “ili auone unyofu wa upendo wao”.
2Wakor 8:8 “Sineni ili kuwaamuru, bali kwa bidii ya watu wengine nijaribu unyofu wa upendo wenu”.
Hata leo, wapo watakatifu ambao katika roho wapo Makedonia, watu kama hao utawaona tu, kazi ya Mungu, hawaichukulii kama kazi-baki, bali kama ni kazi ya kuthaminiwa sana, wanaelewa kuwa ina gharama zake na mahitaji yake, Hivyo hata kama wapo katika umaskini, hawana kazi, au wana kazi, wanakuwa na moyo kweli kwa kuijali kazi ya Mungu kwa vyovyote vile Mungu anavyowabariki, na wengine wanajitoa hata zaidi ya uwezo wao, ukidhania kuwa ni matajiri sana kumbe, hata kesho hawajui watakula nini, ni moyo wao tu wa upendo kwa Mungu.. Mungu azidi kuwabariki sana watu kama hawa.
Lakini wapo watakatifu wengine ambao kiroho wapo Korintho, ambao utoaji kwao ni jambo lisilo la umuhimu sana. Watakuwa tayari kusikiliza injili, na kulishwa vya rohoni kanisani, kufundishwa miaka nenda rudi, lakini wasijitoe hata kwa lolote kwa Mungu. Kisingizio chao kikubwa ni sina kazi, au ninapitia shida hii au ile, au nina madeni, nina mikopo nahitaji kurejesha..Ni kweli kama utakuwa unafikiria hilo, basi usiwasahau pia na watu wa Makedonia. Ambao walikuwa katika majaribu makubwa na umaskini wa kupindukia, pengine kuliko wewe, lakini hawakuzihusisha shida zao na kumtolea Mungu wao aliyewaumba.
Kumtolea Bwana, si kuchangia mabilioni, lakini kumtolea kinono kwa kile anachokujalia ndicho anachothamini, mfano wa Yule mwanamke mjane aliyemtolea Bwana senti mbili. Unaona> Kama Mungu anakujalia sh. 100 kwa siku, ukimtolea Mungu hata 50, Mungu anathamini sana. Kushinda Yule anayejaliwa bilioni 1 halafu anamtolea Mungu milioni 1 tu..
Hivyo tujitahidi sana, tufanane na watakatifu wa Makedonia.
Bwana akubariki sana.
Nini maana ya.. “Utoapo sadaka mkono wako wa kuume usijue ufanyalo mkono wako wa kushoto”
MADHARA YA KUFUATA MAMBO YAKO TU!
UYATIE MACHOZI YANGU KATIKA CHUPA YAKO EE! BWANA.
HALI ZETU JINSI ZINAVYOWEZA KUATHIRI UTOAJI WETU.
SWALI: Kwanini Bwana Yesu alisema watu wa kizazi kile wamefanana na watoto walioketi masokoni na kuitana,? Mfano huo unaelewekaje?
Na pia alikuwa na maana gani kusema maneno haya?
Luka 7:35 “Na hekima imejulikana kuwa ina haki kwa watoto wake wote”
JIBU: Habari hizo utazisoma katika sehemu kuu mbili, ya kwanza ni Mathayo 11:16-20 na ya pili ni Luka 7:31-35
Sasa tuisome hiyo ya Luka ndio yenye vifungu vya moja kwa moja vya swali lenyewe;
Luka 7:31 “Bwana akasema, Niwafananishe na nini watu wa kizazi hiki? Nao wamefanana na nini? 32 Wamefanana na watoto walioketi sokoni na kuitana, wakisema, Tuliwapigia filimbi wala hamkucheza; tuliomboleza, wala hamkulia. 33 Kwa kuwa Yohana Mbatizaji alikuja, hali mkate wala hanywi divai, nanyi mwasema, Ana pepo. 34 Mwana wa Adamu amekuja, anakula na kunywa; nanyi mwasema, Tazama, mlafi huyu, na mnywaji wa divai, rafiki wao watoza ushuru na wenye dhambi. 35 Na hekima imejulikana kuwa ina haki kwa watoto wake wote”.
Luka 7:31 “Bwana akasema, Niwafananishe na nini watu wa kizazi hiki? Nao wamefanana na nini?
32 Wamefanana na watoto walioketi sokoni na kuitana, wakisema, Tuliwapigia filimbi wala hamkucheza; tuliomboleza, wala hamkulia.
33 Kwa kuwa Yohana Mbatizaji alikuja, hali mkate wala hanywi divai, nanyi mwasema, Ana pepo.
34 Mwana wa Adamu amekuja, anakula na kunywa; nanyi mwasema, Tazama, mlafi huyu, na mnywaji wa divai, rafiki wao watoza ushuru na wenye dhambi.
35 Na hekima imejulikana kuwa ina haki kwa watoto wake wote”.
Bwana Yesu alitoa mfano ambao ulikuwa ni wa kawaida na uliojulikana kwa wagalilaya wakati ule. Kwani ilikuwa ni desturi watoto wa aina mbalimbali kukutana masokoni kwa ajili ya michezo kulingana na desturi zao, na walipokutana walikuwa wanaunda makundi mawili makubwa, lengo lao likiwa ni kuigiza mambo ambayo waliona watu wazima wakiyafanya aidha katika misiba au sherehe.
Sasa kundi la kwanza lilikuwa linaanza kwa kupiga filimbi za kwenye masherehe walizowahi kuzisikia mahali fulani zikipigwa huko nyuma, na lile kundi lingine kazi yake ilikuwa ni kuitikia kwa kucheza, kama watu wazima walivyofanya. ( Soma Luka 15:25)
Baadaye tena vivyo hivyo, wanarudia kuigiza nyimbo za misibani, wale wengine wanajifanya kama wanalia kwa kupiga piga vifua vyao. (Soma Mathayo 9:23). Hivyo hata watu wazima walipowaona hawakuwazuia bali waliwaacha, kwani walikuwa wanaamini vitendo vile vinawajengea uzalendo wa kutambua tamaduni zao za kiyahudi.
Sasa kulingana na maneno ya Bwana Yesu ni kuwa, watoto hawa walipokusanyika, kundi lile la kwanza lilipopiga filimbi za masherehe, wale wengine hawakuonyesha mwitikio wowote walizira, pengine wakadhani wanataka za msiba, na walipowapigia wenzao za msiba, bado pia hawakujifanya kama wanaomboleza. Kitendo ambacho pengine kiliwakasirisha wale waliojitoa.
Akifunua kuwa, Yohana alikuja kwa njia ya kujitenga sana na ulimwengu, hivyo pengine wangemwamini kwa maisha yake ya majangwani, na kutokula kula au kunywa, kama vile mtoto aliyewapigia filimbi za maombolezo, lakini hawakulia..Yaani mafarisayo na waandishi hawakuonyesha mwitikio wowote. Kinyume chake wakasema watu wenye mapepo, ndio wanaishi maisha ya namna hiyo, hakuna mtumishi mwenye akili timamu, akawa mchafu na mtu asiyejijali namna ile.
Labda hiyo ikaonekana kama ni njia ngumu kwao kuamini manabii wa Mungu, Hivyo Mungu akawapelekea mkuu wa uzima mwenyewe, Yesu Kristo, Bwana wetu, ambaye yeye alikuja kwa njia ya kula na kunywa, mtu wa watu, aketiye katikati ya wenye dhambi, hivyo mbele yao akafanana na wale watoto waliopiga filimbi, ili wenzao wacheze.. Lakini bado hawakuonyesha mwitikio wowote kwa injili ya Bwana, kinyume chake, wakamwita mlevi na mlafu. Hakuna mtumishi wa Mungu kweli anaweza kushinda bar muda wote na walevu kuwahubiria.
Kuonyesha kuwa hata sasa, Bado Mungu anaweza kutuma watumishi wake, katika wito tofauti tofauti, lakini bado watu wasiompenda Mungu wakapinga tu, wakadhihaki, wakakejeli, wakadharau. Akitumwa nabii wa Mungu anayehubiri injili ya kweli, ambaye pengine ni tajiri, na ana mali, watasema, tapeli huyu, anakula sadaka za waumini, wakipelekewa nabii ambaye muda wake wote anashinda sehemu za ibada, au milimani, mwenye nguo moja, asiye smati, hafanyi kazi yoyote isipokuwa kushinda uweponi mwa Mungu, watasema huyu mlokole maskini hatumtaki, kama Mungu wake ameshindwa kumfanya hata asivae viatu vilivyotoboka, atawezaji kunisaidia mimi?
Unaona?
Lakini sasa ukiendelea mistari inayofuata, Bwana Yesu ndio anasema..
“Na hekima imejulikana kuwa ina haki kwa watoto wake wote”.. Ukisoma kwenye Mathayo 11:19 inasema “Na hekima imejulikana kuwa ina haki kwa kazi zake”. Hii ikiwa na maana Hekima ya Mungu ya kuokoa watu, imejulikana kuwa ni ya kweli kwa watoto wake ambao ni (Yohana na Yesu Kristo mwenyewe).. Kwamba kwa vyovyote vile, iwe ni katika utajiri au katika umaskini, au katika kujichanganya au kutojichanganya..kama ni ya Mungu, basi itathibitika tu kwa kazi zake,(matunda yake).
Hata leo hii, usimuhukumu mtumishi wa Mungu kisa ni tajiri, au ni maskini, au anakula au hali, vilevile usihukumu huduma yoyote kisa ni kubwa, au ni ndogo, au inamfumo huu au ule.. kwasababu Hekima ya Mungu haichagui mfumo wa kutembelea. Bali ihukumu hiyo huduma kwa kazi zake baada ya hapo.
Ikiwa matunda yake, ni yale ya Kristo, basi muheshimu mtumishi huyo au huduma hiyo, ikiwa watu wake, wanauelekea wokovu wa kweli na wanaishi maisha ya kumpendeza Mungu basi heshimu hata kama ipo kinyume na matazamio yako.
Vilevile ukiona mtumishi ni tajiri, au ni Yule maskini anayeishi milimani, na anachokifanya hakina matunda Kristo anayoyataka sawasawa na Neno lake. Yaani watu wake ndio wanakwenda mbali na wokovu na utakatifu, maisha yako ni ya kidunia, wanafuata tu kuponywa, basi lakini upendo na Kristo hawana.. achana naye, hata kama atajiona ni wa rohoni kiasi gani..au ni mtu wa kijamii namna gani, au mwenye ushawishi namna gani, achana naye. Hekima ya Mungu haipo hapo.
Kwasababu hekima ya kweli ya Mungu inathibitika kwa kazi zake. Kama ilivyothibitika kwa Bwana Yesu na kwa Yohana, japokuwa mapito yao yalikuwa ni tofauti lakini matunda yao yalikuwa ni thabiti.
Hiyo ndio sababu Bwana Yesu aliwaambia wale mafarisayo maneno hayo..
Au bofya chini kujiunga na group la whatsapp moja kwa moja;
Hamjui ya kuwa mtawahukumu malaika? Ina maana gani?
MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA WARAKA WA PILI WA YOHANA.
USIRUDI NYUMA KWA KUITUMAINIA HAKI YAKO.
MZAZI, JALI MAISHA YA KIROHO YA MTOTO WAKO.
SINA PESA SASA, YESU ATANISAIDIA NINI?
WhatsApp
SWALI: Je Ni kweli Mtume Paulo alipuuzia, maonyo aliyoonyeshwa na Roho Mtakatifu kwa kinywa cha Agabo juu ya kwenda Yerusalemu?
JIBU: Tusome habari yenyewe kwa faida ya watu wote;
Matendo 21:10 “Basi tulipokuwa tukikaa huko siku nyingi, nabii mmoja jina lake Agabo akashuka kutoka Uyahudi. 11 Alipotufikia akautwaa mshipi wa Paulo, akajifunga miguu na mikono, akasema, Roho Mtakatifu asema hivi, Hivyo ndivyo Wayahudi wa Yerusalemu watakavyomfunga mtu mwenye mshipi huu, nao watamtia katika mikono ya watu wa Mataifa. 12 Basi tuliposikia haya, sisi na watu wa mahali pale, tukamsihi asipande kwenda Yerusalemu. 13 Ndipo Paulo alipojibu, Mnafanya nini, kulia na kunivunja moyo? Kwa maana mimi, licha ya kufungwa, ni tayari hata kuuawa katika Yerusalemu kwa ajili ya jina lake Bwana Yesu. 14 Alipokataa shauri letu, tukanyamaza tukisema, Mapenzi ya Bwana na yatendeke. 15 Baada ya siku zile tukachukua vyombo vyetu tukapanda kwenda Yerusalemu.
Matendo 21:10 “Basi tulipokuwa tukikaa huko siku nyingi, nabii mmoja jina lake Agabo akashuka kutoka Uyahudi.
11 Alipotufikia akautwaa mshipi wa Paulo, akajifunga miguu na mikono, akasema, Roho Mtakatifu asema hivi, Hivyo ndivyo Wayahudi wa Yerusalemu watakavyomfunga mtu mwenye mshipi huu, nao watamtia katika mikono ya watu wa Mataifa.
12 Basi tuliposikia haya, sisi na watu wa mahali pale, tukamsihi asipande kwenda Yerusalemu.
13 Ndipo Paulo alipojibu, Mnafanya nini, kulia na kunivunja moyo? Kwa maana mimi, licha ya kufungwa, ni tayari hata kuuawa katika Yerusalemu kwa ajili ya jina lake Bwana Yesu.
14 Alipokataa shauri letu, tukanyamaza tukisema, Mapenzi ya Bwana na yatendeke.
15 Baada ya siku zile tukachukua vyombo vyetu tukapanda kwenda Yerusalemu.
Tofauti na wengi tunavyodhani kwamba mtume Paulo alipuuzia maono ya Mungu, na ndio maana akaenda kukumbana na matatizo makubwa kule Yerusalemu alipokwenda mambo ambayo hayakuwa na ulazima wa yeye kukutana nayo. Lakini si kweli, kama Paulo angekuwa ni mtu wa kupuuzia maono ya Mungu, asingeandika katika waraka wake mmoja “Msitweze unabii” (1Wathesalonike 5:20). Akimaanisha msipuuzie unabii.
Paulo alikuwa ni mtu aliyethamini sana maagizo ya Roho Mtakatifu, na kuyatekeleza wa wakati. Kuna wakati Mungu alimkataza asihubiri Neno Galatia na sehemu nyingine na akatii(mdo 16:6-9). Na wakati huo huo Mungu anamwonyesha maono avuke bahari aende Makedonia kuhubiri mahali ambapo hajawahi kufika hata siku moja. Na akatii
Hivyo kitendo cha kusema Paulo hakutii maagizo ya Roho Mtakatifu, ni kukosa shabaha.
Lakini swali linakuja kama sio kutii basi ni kwanini aamue vile?
Jibu ni kuwa, ipo tofauti ya “mtu kupewa agizo” na “mtu kuelezwa uhalisia wa mambo / kupashwa habari”. Paulo hakupewa agizo na Roho Mtakatifu kuwa asipande Yerusalemu, kama alivyopewa maagizo sehemu nyingine. Hapana, bali alielezwa uhalisia wa mambo atakayokutana nayo huko mbeleni. Na ndio maana utaona kabla hata ya Agabo kumpa unabii ule, tayari Roho Mtakatifu alikuwa ameshamshuhudia mambo hayo kuwa atakutana nayo mbeleni. Soma.
Matendo 20:22 “Basi sasa, angalieni, nashika njia kwenda Yerusalemu hali nimefungwa rohoni, nisiyajue mambo yatakayonikuta huko; 23 isipokuwa Roho Mtakatifu mji kwa mji hunishuhudia akisema, ya kwamba vifungo na dhiki vyaningoja”.
Matendo 20:22 “Basi sasa, angalieni, nashika njia kwenda Yerusalemu hali nimefungwa rohoni, nisiyajue mambo yatakayonikuta huko;
23 isipokuwa Roho Mtakatifu mji kwa mji hunishuhudia akisema, ya kwamba vifungo na dhiki vyaningoja”.
Hivyo Paulo kwa kulitambua hilo, bado hakusita kukumbana na changamoto hizo, kwa ajili ya injili. Alifikiria sana akaona dhiki haziwezi kumfanya kondoo wa Mungu wasifikiwe na injili. Hivyo akajitia moyo na kwenda kama shujaa.
Jambo kama hilo utaona pia kwa mtume Petro, kipindi kile Bwana Yesu alimwambia wewe ni kijana, lakini ukiwa mzee watu watakuja kukufunga mikono yako na kukuchukua usipotaka, (Yohana 21:18). Kuonyesha kuwa vifungo na dhiki na vifo vinamsubiria mbeleni. Lakini lile halikuwa ni agizo kwamba Petro sasa akatafute namna ya kukwepa, dhiki hizo. Hapana.
Hata sasa ni kawaida ya Roho Mtakatifu kuzungumza nasi kwa namna zote mbili. Kuna wakati atatupa maagizo, na kuna wakati atatueleza uhalisia wa mambo. Sasa pale tunapopewa maagizo au tunapoonywa, ni sharti tutii, Mungu anapokuambia usihubiri mahali Fulani, ni kweli usiende kuhubiri, anapokuambia kahubiri mahali Fulani ni kweli nenda kahubiri.
Lakini kuna wakati utakuwa katika safari yako ya kumtumikia Mungu, na akakuonyesha, matunda, na changamoto zake, akakuonyesha hata, unapigwa mawe, au unafukuzwa, au unafungwa, au unazungumziwa vibaya. Moja kwa moja usikimbilie kusema Roho Mtakatifu ananionya nisiende kuhubiri, hapana, bali tazama pia upande wa pili wa matunda, Kwasababu dhiki kama hizo haziletwi na Mungu, bali ni shetani, ambaye anafanya hivyo ili akuzuie, usifanye kazi yake hilo tu. Lakini kumbe Mungu anatamani sana, ufike kule.
Kwahiyo usitafsiri kila ono, ni agizo , mengine Mungu anatuonyesha tu ili yatakapotokea tusifadhaike sana, kwasababu alishatutaarifu mapema.
Yohana 16:1 “Maneno hayo nimewaambia, msije mkachukizwa. 2 Watawatenga na masinagogi; naam, saa yaja atakapodhania kila mtu awauaye ya kuwa anamtolea Mungu ibada. 3 Na hayo watawatenda kwa sababu hawakumjua Baba wala mimi. 4 LAKINI NIMEWAAMBIA HAYO, ILI MAKUSUDI SAA ILE ITAKAPOKUJA MYAKUMBUKE YA KUWA MIMI NALIWAAMBIA. Sikuwaambia hayo tangu mwanzo, kwa sababu nalikuwapo pamoja nanyi”.
Yohana 16:1 “Maneno hayo nimewaambia, msije mkachukizwa.
2 Watawatenga na masinagogi; naam, saa yaja atakapodhania kila mtu awauaye ya kuwa anamtolea Mungu ibada.
3 Na hayo watawatenda kwa sababu hawakumjua Baba wala mimi.
4 LAKINI NIMEWAAMBIA HAYO, ILI MAKUSUDI SAA ILE ITAKAPOKUJA MYAKUMBUKE YA KUWA MIMI NALIWAAMBIA. Sikuwaambia hayo tangu mwanzo, kwa sababu nalikuwapo pamoja nanyi”.
Hivyo Bwana atusaidie na sisi tujifunze kuyapambanua maono ya Mungu.
Maran Atha.
VIFO VYA MITUME WA YESU/ JINSI MITUME WALIVYOKUFA.
Tofauti kati ya ufunuo, unabii na maono ni ipi?
PINDO LA VAZI LAKE SASA LIMEREFUSHWA.
BADO UPO YERUSALEMU TU..GALILAYA HUTAKI KWENDA?
LIPI TUNAJIFUNZA KWA WALIOMWONA YESU ALIYEFUFUKA?
SWALI: Bwana Yesu asifiwe,.Naomba kufahamu tofauti kati ya kuhukumu na kulaumu, maana nashindwa kuelewa, imesema tusihukumu. Je kwa mtu anayetenda dhambi kwa makusudi unapomlaumu ni sawa na kumuhukumu?
Luka 6:37 “Msihukumu, nanyi hamtahukumiwa; msilaumu, nanyi hamtalaumiwa; achilieni, nanyi mtaachiliwa”.
JIBU: Kuhukumu ni kitendo cha moja kwa moja kutoa/kuamua hatma ya mtu mwingine, Na hiyo inakuja pale mtu anapojiona yeye ni bora/mwema sana zaidi ya wale wengine, . Kwamfano mtu mmoja atamwona kahaba, au mlevi, au shoga barabarani na wakati huo huo atamwambia wewe ni ibilisi, mwana wa kuzimu, Au atakutana na wapagani wanaabudu miungu yao mahali fulani, ataanza kuwanyooshea kidole na kuwaita makafiri wa motoni wale, bila hata kuwaambia kitu kingine chochote, kisa tu kawaona wanafanya matendo yasiyompendeza Mungu. Hapo tayari kashawahukumu.
Lakini Kulaumu ni kitendo cha kukosoa kila kitu, kwa lengo la kuonyesha kuwa kitendo alichokifanya/anachokifanya Yule mwingine ni cha kupuuzi sikuzote, hakina maana. Na kwa kawaida watu wanaolaumu nao pia wanakuwa na fikra kwamba wao huwa hawakoseagi..Ingekuwa ni wamepewa fursa hiyo wangeitumia vizuri. (Wana tabia ya kujiona wao ni wakamilifu sikuzote)
Kwamfano lawama mara nyingi zinawakuta viongozi, Utakuta kiongozi, kafanya jambo fulani la kimaendeleo, lakini kwasababu mtu fulani anajiona yeye hawezi kukosea, ataanza kutoa kasoro, kwa kila kitu kilichofanywa hata kama ni kizuri, utasikia, kwanini zile pesa zisingetumiwa kwa hili au lile, kusingekuwa na matatizo haya na yale, hiyo ndio laumu. Kana kwamba yeye yupo sahihi wakati wote, hajawahi kufanya kitu akakosea.
Au mtu mwingine, labda mzazi wake ameshindwa kumtimizia haki yake ya msingi, pengine elimu, halafu amekuwa mtu mzima, akaona madhara ya kutopelekwa kwake shule. Sasa badala ajifunze “kuachilia” kama biblia inavyosema, achilieni, nanyi mtaachiliwa, yeye ataanza kuwalaumu wazazi wake tangu ujana wake hadi uzee wake, kana kwamba walifanya makosa makubwa sana, Na kusahau kuwa yeye mwenyewe pia anayomakosa mengi, ambayo Mungu anayohaki ya kumlaumu kupitia hayo.
Vitendo vyote hivi Mungu havipendi. Kuhukumu pamoja na kulaumu, kwasababu na sisi Mungu atatufanyia hivyo hivyo siku ile ya hukumu, tusipobadilika, Na kwakweli Bwana atusaidie viondoke ndani yetu. Lakini pia tunapaswa tufahamu kuwa kuelezwa uhalisia wa mambo sio kuhukumiwa, jambo ambalo watu wengi wanatafsiri isivyosawa. Kwamfano mtu ni mlevi, halafu anaelezwa kuwa walevi wote biblia inasema wataenda jehanamu, akadhani hapo anahukumiwa.. Hapo haukumiwi, bali anaelezwa ukweli wa mambo. Kwamfano hata wewe ukimwona mtoto wako anacheza karibu na shimo, ukamwambia “watoto wanaocheza karibu na mashimo mwisho wao huwa ni kutumbukia na kufa”. Hapo hujahitimisha kuwa Yule mtoto ni wa kufa, lakini umemweleza uhalisia wa mambo. Hivyo na wewe unavyohubiriwa wazinzi wote watakwenda kuzimu, ujue kuwa hauhukumiwi, bali unaelezwa hatma ya maisha yako.
Unapoambiwa wanaojichubua miili yao wote na wanaovaa nguo za uchi uchi, hatma yao ni kwenye ziwa la moto. Hauhukumiwi wala haulaumiwi bali unahubiriwa hatma yako. Lengo la Yule mhubiri sio uende kwenye ziwa la moto bali utubu ili uikwepe hukumu.
Lakini mtu akikufuata na moja kwa moja akakwambia wewe ni ibilisi, au kafiri, au joka, au ajenti wa kuzimu, kana kwamba wewe huwezi kupokea neema yoyote kama ya kwake,. Huyo tayari ameshakuhukumu na biblia imekataza sana hilo, kwasababu anayejua hatma ya mtu ya mwisho ni Mungu na sio yeye. Lakini akikueleza matokeo ya ukafiri wako, hajakumukumu, zaidi kaonyesha upendo kwako.
BASI, IWENI NA HURUMA, KAMA BABA YENU ALIVYO NA HURUMA(Luka 6:36)
Je Lutu alikwenda kuwahukumu watu wa Sodoma na Gomora? Kulingana na Mwanzo 19:9?
Tofauti kati ya uchafu wa mwilini na rohoni ni ipi?
SI KWA UWEZA WALA KWA NGUVU BALI KWA ROHO YANGU, ASEMA BWANA.
Huruma ni nguzo muhimu sana ambayo tunapaswa tuwe nayo sisi tuliompokea Kristo maishani mwetu.
Ni kwanini tuwe na huruma? Ni kwasababu Baba yetu naye ni mtu mwenye huruma.
Luka 6:36 “Basi, iweni na huruma, kama Baba yenu alivyo na huruma”.
Lakini wengi wetu bado hatujafahamu vema huruma hasaa ni nini. Kuna tofauti kati ya huruma na Rehema(wafilipi 2:1). Rehema ni neno pana linalomaanisha kusamehe au kusaidia hata kama mtu huyo hastahili kupewa fadhili hizo, lakini huruma ni kitendo cha kuonyesha kusamehe/kusaidia/kujali kwa mtu ambaye anaonekana anahitaji msaada huo hata kama hatosema,au kuonyesha.
Kwa mfano mwanajeshi vitani anapomkamata adui yake (ambaye ni mwanajeshi kama yeye). Na ikatokea adui huyo akajisalimisha kwa magoti akiomba asiuliwe,..Na yule mwanajeshi akamsaheme, kwa kuomba kule, basi hapo kaonyesha kitendo cha huruma.
Lakini ikitokea, Yule adui amekamatwa lakini bado analeta ubishi, bado ni mkaidi, anataka kuleta madhara, na wakati huo huo Yule mwanajeshi bado akayahifadhi tu maisha yake..Hiyo sio huruma bali ni rehema.
Mfano mwingine wa rehema ni pale raisi anapowaachilia wafungwa, sio kwamba wale watu walimwomba watoke, au wamejirekebisha kwa tabia zao mbaya, au ni wema sana hapana bali ni pengine raisi anatimiza tu wajibu wake wa kisheria kama raisi, wa kusamehe wafungwa kila muhula kwake.
Mfano mwingine wa huruma ni pale Baba anapomtimizia mtoto wake mahitaji yake ya chakula au mavazi,huwezi kusema anaonyesha kitendo cha rehema, hapana, bali huruma, kwasababu anajua sikuzote mtoto ni dhaifu, hana uwezo wa kujiamulia mambo yake mwenyewe.
Hivyo rehemu na huruma vyote vinahitajika sana kwetu. Lakini leo tutajikita sana katika upande wa huruma, na tayari tumeshapata msingi wa maana halisi ya huruma, kwamba huwa unaenda moja kwa moja kwenye kundi la watu wanaoonyesha kuhitaji msaada fulani. Basi biblia inatufundisha sisi kama wakristo, tuonyeshe huruma zetu, kwa makundi kama hayo; kwasababu Baba yetu wa mbinguni naye anaonyesha huruma zake kwetu sisi tunapomlilia, usiku na mchana.
Kibiblia ni makundi gani tunapaswa tuyaonyeshee huruma zetu?
1) HURUMA KWA WENYE MAGONJWA.
Utaona katika maandiko Bwana Yesu aliwaponya wagonjwa wengi sana kwasababu aliwahurumia, hakuwaacha tu waende zao,bali alijitahidi kuchukuliana nao, na kuwaponya.
Marko 1:40 “Akaja kwake mtu mwenye ukoma, akamsihi na kumpigia magoti, na kumwambia, Ukitaka, waweza kunitakasa. 41 NAYE AKAMHURUMIA, akanyosha mkono wake, akamgusa, akamwambia, Nataka, takasika. 42 Na mara ukoma wake ukamtoka, akatakasika.
Marko 1:40 “Akaja kwake mtu mwenye ukoma, akamsihi na kumpigia magoti, na kumwambia, Ukitaka, waweza kunitakasa.
41 NAYE AKAMHURUMIA, akanyosha mkono wake, akamgusa, akamwambia, Nataka, takasika.
42 Na mara ukoma wake ukamtoka, akatakasika.
Unaona? nasi vivyo hivyo, tunapoona wengine wanataseka na magonjwa, wanaumwa, hatupaswi kuwaacha hivi hivi, tuwe nao karibu tuwaombee, tujiweke na sisi katika nafasi zao, Jiulize je! Kama na wewe ungekuwa unaumwa kansa, au kisukari, au ukimwi kama Yule, halafu unaona watu hawakujali hata kukuombea, utajisikiaje?.
Tazama tena kisa hiki kingine..
Luka 7:12 “Na alipolikaribia lango la mji, hapo palikuwa na maiti anachukuliwa nje, ni mwana pekee wa mamaye ambaye ni mjane, na watu wa mjini wengi walikuwa pamoja naye. 13 Bwana alipomwona ALIMWONEA HURUMA, akamwambia, Usilie. 14 Akakaribia, akaligusa jeneza; wale waliokuwa wakilichukua wakasimama. Akasema, Kijana, nakuambia, Inuka”.
Luka 7:12 “Na alipolikaribia lango la mji, hapo palikuwa na maiti anachukuliwa nje, ni mwana pekee wa mamaye ambaye ni mjane, na watu wa mjini wengi walikuwa pamoja naye.
13 Bwana alipomwona ALIMWONEA HURUMA, akamwambia, Usilie.
14 Akakaribia, akaligusa jeneza; wale waliokuwa wakilichukua wakasimama. Akasema, Kijana, nakuambia, Inuka”.
2) HURUMA KWA WENYE UHITAJI.
Kuna wakati jirani yako atakuwa amepungukiwa na kitu fulani aidha mboga kidogo, au sabuni, au pesa kidogo za matumizi, na pengine hilo lipo ndani ya uwezo wako, hupaswi kumuacha tu hivi hivi, bali uonyeshe huruma zako, kwasababu hivyo ndivyo Mungu anataka..
1Yohana 3:17 “Lakini mtu akiwa na riziki ya dunia, kisha akamwona ndugu yake ni mhitaji, akamzuilia HURUMA ZAKE, je! Upendo wa Mungu wakaaje ndani yake huyo? 18 Watoto wadogo, tusipende kwa neno, wala kwa ulimi, bali kwa tendo na kweli”.
1Yohana 3:17 “Lakini mtu akiwa na riziki ya dunia, kisha akamwona ndugu yake ni mhitaji, akamzuilia HURUMA ZAKE, je! Upendo wa Mungu wakaaje ndani yake huyo?
18 Watoto wadogo, tusipende kwa neno, wala kwa ulimi, bali kwa tendo na kweli”.
3) HURUMA KWA WALIOKUMBWA NA MATATIZO:
Kuna muda ambao, mtu fulani atahitaji msaada wa haraka kutoka kwako, labda mgonjwa wake kazidiwa anaomba msaada wako,wa kumfikisha hospitali, na wewe pekee ndio upo hapo wa kuweza kumsaidia, wakati kama huo, usijione kuwa upo buzy sana, au unawahi ibadani, zingatia kumsaidia kwanza, kwasababu biblia inatufundisha hivyo kwa ule mfano wa msamaria mwema;
Luka 10:30 “Yesu akajibu akasema, Mtu mmoja alishuka toka Yerusalemu kwenda Yeriko, akaangukia kati ya wanyang’anyi; wakamvua nguo, wakamtia jeraha, wakaenda zao, wakimwacha karibu ya kufa. 31 Kwa nasibu kuhani mmoja alishuka kwa njia ile; na alipomwona alipita kando. 32 Na Mlawi vivyo hivyo, alipofika pale akamwona, akapita kando. 33 Lakini, Msamaria mmoja katika kusafiri kwake alifika hapo alipo; na alipomwona ALIMHURUMIA, 34 akakaribia, akamfunga jeraha zake, akizitia mafuta na divai; akampandisha juu ya mnyama wake, akampeleka mpaka nyumba ya wageni, akamtunza”.
Luka 10:30 “Yesu akajibu akasema, Mtu mmoja alishuka toka Yerusalemu kwenda Yeriko, akaangukia kati ya wanyang’anyi; wakamvua nguo, wakamtia jeraha, wakaenda zao, wakimwacha karibu ya kufa.
31 Kwa nasibu kuhani mmoja alishuka kwa njia ile; na alipomwona alipita kando.
32 Na Mlawi vivyo hivyo, alipofika pale akamwona, akapita kando.
33 Lakini, Msamaria mmoja katika kusafiri kwake alifika hapo alipo; na alipomwona ALIMHURUMIA,
34 akakaribia, akamfunga jeraha zake, akizitia mafuta na divai; akampandisha juu ya mnyama wake, akampeleka mpaka nyumba ya wageni, akamtunza”.
4) HURUMA KWA WAKRISTO WALIORUDI NYUMA:
Hapa ni mahali pengine ambapo tunapaswa kupazingatia sana. Kuna wakati ndugu mwenzako katika imani anaweza kurudi nyuma, pengine akauacha wokovu kabisa, lakini akawa anatamani kurudi tena kwa Mungu, wewe kama mkristo, ni lazima uonyeshe huruma zako kwa mtu kama huyo kumsaidia, tutalisoma hilo katika ule mfano wa mwana mpotevu, utaona baada ya kuasi nyumbani na maisha kuwa magumu huko alipokwenda alizingatia kurudi nyumbani. Na aliporudi alimwambia baba yake maneno haya; Lakini utasoma babaye hakumfukuza bali alimuhurumia.
Luka 15:19 “sistahili kuitwa mwana wako tena; nifanye kama mmoja wa watumishi wako. 20 Akaondoka, akaenda kwa babaye. Alipokuwa angali mbali, baba yake alimwona, AKAMWONEA HURUMA, akaenda mbio akamwangukia shingoni, akambusu sana. 21 Yule mwana akamwambia, Baba, nimekosa juu ya mbingu na mbele yako; sistahili kuitwa mwana wako tena. 22 Lakini baba aliwaambia watumwa wake, Lileteni upesi vazi lililo bora, mkamvike; mtieni na pete kidoleni, na viatu miguuni; 23 mleteni ndama yule aliyenona mkamchinje; nasi tule na kufurahi; 24 kwa kuwa huyu mwanangu alikuwa amekufa, naye amefufuka; alikuwa amepotea, naye ameonekana. Wakaanza kushangilia”.
Luka 15:19 “sistahili kuitwa mwana wako tena; nifanye kama mmoja wa watumishi wako.
20 Akaondoka, akaenda kwa babaye. Alipokuwa angali mbali, baba yake alimwona, AKAMWONEA HURUMA, akaenda mbio akamwangukia shingoni, akambusu sana.
21 Yule mwana akamwambia, Baba, nimekosa juu ya mbingu na mbele yako; sistahili kuitwa mwana wako tena.
22 Lakini baba aliwaambia watumwa wake, Lileteni upesi vazi lililo bora, mkamvike; mtieni na pete kidoleni, na viatu miguuni;
23 mleteni ndama yule aliyenona mkamchinje; nasi tule na kufurahi;
24 kwa kuwa huyu mwanangu alikuwa amekufa, naye amefufuka; alikuwa amepotea, naye ameonekana. Wakaanza kushangilia”.
Vivyo hivyo na sisi tuwahurumie wale ambao wanarudi kwa moyo wa dhati kwa Mungu.
5) HURUMA KATIKATI YA WAAMINIO.
Vilevile sisi kama waaminio, tuliokoka, kanisa la Kristo, ni lazima tujue kuwa kila kiungo kinamuhitaji mwenzake, unapoona kiungo kimoja kimeumia, au kimefadhaika huna budi kukitibu, unapoona kimepungukiwa huna budi kukijali, kinapokukosea huna budi kikisamehe. Ndivyo Bwana anavyotaka.
Waefeso 4:32 “tena iweni wafadhili ninyi kwa ninyi, wenye huruma, mkasameheane kama na Mungu katika Kristo alivyowasamehe ninyi”.
Bwana atusaidie tuyazingatie hayo, ili na sisi tufanane na Baba yetu wa mbinguni, ambaye anatuhurumia kila wakati.
UPENDO WA MUNGU.
JE! NI WAPI UTAPOKEA HISIA ZA KWELI ZA KI-MUNGU?
TUMEFANYIKA KUWA WANA WA MUNGU!
Kwa jina lake Ubaba wote wa mbinguni na wa duniani unaitwa.
Je! Mfalme Abiya na Mfalme Asa walikuwa ni ndugu?
Kati ya watoto ambao Daudi aliwapenda sana na wakati huo huo wakamsumbua sana, ni Absalomu. Absalomu alikuwa ni kijana mzuri wa umbo, na vilevile alikuwa ni kijana aliyetumia mbinu za kipekee sana katika kutimiza malengo yake.
Absalomu, alileta taharuki kuu mbili Israeli, Taharuki ya kwanza, ni ile ya kumuua ndugu yake, aliyeitwa Amnoni, mwana wa mfalme, na ya pili ni ile ya jaribio lake la kuupindua ufalme wa Baba yake (Daudi).
Kama wewe ni msomaji wa biblia, kitabu cha 2Samweli sura ile ya 13-19, utakutana na habari hizo, utakumbuka kuwa huyu Absalomu alikuwa ni dada yake wa tumbo moja aliyeitwa Tamari, lakini ikatokea siku moja ndugu yake wa mama mwingine aliyeitwa Amnoni, akamtamani, na mwisho wa siku akamwingilia kwa nguvu, bila kufuata utaratibu, hivyo akamletea aibu kubwa binti Yule, pamoja na ndugu yake. Sasa huyu Absalomu, ambaye ni kaka wa mama mmoja na Tamari, alipopata habari akaudhika sana kwa kitendo kile, akamchukia Amnoni kupindukia.
Lakini tabia moja ya Absalomu,ilikuwa si ya kuchukua maamuzi ya muda huo huo, na ndio maana utasoma, hakuzungumza naye neno lolote lile liwe la heri au la shari, bali alitulia kimya tu. Sio kwamba moyoni alikuwa hawaki.
2Samweli 13:22 “Ila Absalomu hakusema na Amnoni wala kwa heri wala kwa shari; kwa maana Absalomu alimchukia Amnoni kwa kumtenza nguvu umbu lake Tamari”.
Akaanza chini chini kupanga mipango yake, ambayo ilikuja kutimia MIAKA MIWILI MBELE. Na mipango hiyo ilikuwa ni ya kumwangamiza ndugu yake.
Ukisoma utaona alianza kazi ya ukataji manyoya, na alipofanikiwa baada ya miaka miwili mizima akamwalika baba yake na ndugu zake waje washereheke pamoja naye, hivyo akatumia sasa fursa ile kumwomba baba yake yule ndugu yake aliyembaka dada yake, awepo, akakubali, na alipoenda, akamvizia saa amelewa, akatuma watumishi wake wamuue. Lengo lake likawa limetimia hapo hapo. Amnoni akafa. Kirahisi hivyo. Unaweza kujiuliza ni kwanini, Absalomu hakuchukua hatua za haraka tangu mwanzoni? Jibu ni kuwa ipo tabia ambayo Mungu anataka tujifunze kwa mtu huyu, jinsi alivyokuwa mtu wa mikakati.
Baadaye, baba yake alipopata taarifa akataka kumuua, lakini Absalomu akakimbilia taifa lingine akakaa huku muda wa miaka mitatu mizima.Sasa, kwa muda wako fuatilia kisa hicho katika biblia, lakini nataka tuone jinsi tabia yake ile ile ya uvumilivu na malengo ilivyomletea mafanikio mengine makubwa mbeleni.
Ukisoma biblia utaona, ulifika wakati akarudi Israeli, na kwenda kuonana na baba yake, Lakii akiwa kama mgeni alidhamiria ndani ya moyo kuwa mfalme wa Israeli. Kama ilivyo kawaida yake alijua njia pekee sio kuanza kukurupuka na kuleta mapinduzi kwa haraka hapana, hatafanikiwa bali, alijua uvumilivu na bidii, ni nguzo muhimu sana za kutimiza malengo yake.
Hivyo akaanza mikakati yake, biblia inatuambia, akawa anaamka kila siku asubuhi sana na mapema, labda saa 10 alfajiri, anakwenda kusimama, karibu la lango la kuelekea kwa mfalme, ili kukutana na watu wenye shida zao,ambao wanahitaji kutatuliwa. Alipokutana nao, kila mmoja kabla ya kufika kwa mfalme alimbusu, akajinyenyekeza kwake, akamsikiliza shida zake, akamjibu kwa upole, ikawa kila mtu aliyetoka pale alimpenda sana, na mwisho akawa anawaambia, maneno ya uongo, kuwa hakuna mtu anayewajili, kama wakimfanya yeye kuwa mfalme awatafanyia mema mengi..
2Samweli 15:1 “Ikawa baada ya hayo, Absalomu akajiwekea tayari gari na farasi, na watu hamsini wa kupiga mbio mbele yake. 2 Tena Absalomu huondoka asubuhi na mapema, na kusimama kando ya njia ya lango; kisha ikawa, mtu ye yote aliyekuwa na neno, lililokuwa halina budi kufika kwa mfalme ili kuhukumiwa, Absalomu humwita mtu huyo kwake, na kumwuliza, Wewe u mtu wa mji gani? Naye akasema, Mtumwa wako ni mtu wa kabila fulani ya Israeli. 3 Naye Absalomu humwambia, Tazama, maneno yako ni mema yenye haki; lakini hapana mtu aliyeagizwa na mfalme kukusikiliza. 4 Tena Absalomu husema, Laiti mimi ningewekwa kuwa mwamuzi katika nchi hii, ili kila mtu mwenye neno au daawa aje kwangu, nimpatie haki yake! 5 Tena ikawa hapo alipokaribia mtu ye yote kumsujudia, hunyosha mkono wake, na kumshika, na kumbusu. 6 Hivyo ndivyo Absalomu alivyowatendea Israeli wote, waliomwendea mfalme ili wapate hukumu; na hivyo Absalomu akawadanganya watu wa Israeli. 7 Hata ikawa mwisho wa miaka minne, Absalomu akamwambia mfalme Tafadhali uniache niende nikaondoe nadhiri yangu, niliyomwekea Bwana huko Hebroni”.
2Samweli 15:1 “Ikawa baada ya hayo, Absalomu akajiwekea tayari gari na farasi, na watu hamsini wa kupiga mbio mbele yake.
2 Tena Absalomu huondoka asubuhi na mapema, na kusimama kando ya njia ya lango; kisha ikawa, mtu ye yote aliyekuwa na neno, lililokuwa halina budi kufika kwa mfalme ili kuhukumiwa, Absalomu humwita mtu huyo kwake, na kumwuliza, Wewe u mtu wa mji gani? Naye akasema, Mtumwa wako ni mtu wa kabila fulani ya Israeli.
3 Naye Absalomu humwambia, Tazama, maneno yako ni mema yenye haki; lakini hapana mtu aliyeagizwa na mfalme kukusikiliza.
4 Tena Absalomu husema, Laiti mimi ningewekwa kuwa mwamuzi katika nchi hii, ili kila mtu mwenye neno au daawa aje kwangu, nimpatie haki yake!
5 Tena ikawa hapo alipokaribia mtu ye yote kumsujudia, hunyosha mkono wake, na kumshika, na kumbusu.
6 Hivyo ndivyo Absalomu alivyowatendea Israeli wote, waliomwendea mfalme ili wapate hukumu; na hivyo Absalomu akawadanganya watu wa Israeli.
7 Hata ikawa mwisho wa miaka minne, Absalomu akamwambia mfalme Tafadhali uniache niende nikaondoe nadhiri yangu, niliyomwekea Bwana huko Hebroni”.
Aliendelea hivyo kwa muda wa MIAKA MINEE (4), Mfululizo, akiamka asubuhi, kwa ajili ya kukutana na shida zao hao watu.. Ndipo watu wote, wakamtambua, wakampenda sana, kwa unyenyekevu wake, na kujali kwake, wakamsikiliza hata kwa uongo wake, Absalomu akafanikiwa kujikusanyia wimbi kubwa la watu waliompenda..akapata nguvu, huku baba yake hajui chochote.
Ndipo siku ya siku ilipofika, ghafla, Daudi akasikia mtoto wake Absalomu, amekusanya majeshi ya watu, yanataka kuja kumpindua. Daudi kuona vile ikampasa akimbilie msituni kuokoa maisha yake. Na kama sio Bwana alikuwa upande wake, ule ufalme ulikuwa ni wa Absalomu. Kwasababu watu wengi sana waliandamana naye. Na vita vilivyopiganwa Israeli kipindi hicho vilikuwa ni vikubwa sana, hatuna nafasi ya kueleza habari yote, lakini kwa muda wako soma kwenye biblia utajionea.
Mpaka wakati ambapo Absalomu anakufa, Mfalme Daudi alikuwa ameshapata somo kubwa sana.
Ni nini tunajifunza?
Kumbuka hadithi zote tunazozisoma katika agano lake, zimebeba funzo kubwa kwetu, haijalishi ni za mtu mwovu au mwema. Leo sisi kama watoto wa Mungu, tumekuwa watu wa kutazamia mapinduzi ya wakati huo huo. Tunataka yote tunayoyatazamia yatokee ndani ya usiku mmoja. Kumbe hiyo siyo kanuni, ili tuteke, wakati mwingine tunahitaji uvumilivu na bidii. Itakupasa uhubiri injili kila siku kwa muda wa miaka kadhaa, bila kuona chochote, ndipo baadaye sana uanze kuvuna matunda ya kusumbuka kwako.
Itakugharimu ufanye mazoezi mengi sana ya kuimba, utunge nyimbo nyingi tu, ndipo baada ya kipindi fulani pengine miaka kadhaa, Bwana ndio azifanye nyimbo zako kuwa Baraka kwa watu wengi. Kama unataka karama ya uponyaji itende kazi ndani yako, itakugharimu uwe mvumilivu wa kuchukuliana na matatizo ya watu wengi, kuwaombea kwa bidii, hata kama hutaona lolote katika siku za kwanza kwanza, itakubidi uendelee hivyo hivyo, hata kwa miaka kadhaa pengine, lakini mwisho wake Bwana atakujalia kipawa hicho kwa viwango vingine. Uvumilivu na bidii, inapaswa iwe sehemu ya maisha yetu.
Absalomu, hakuwa mtu wa papo kwa papo, lakini uvumilivu wake na mikakati yake ilimsaidia sana baadaye, kuitikisa Israeli. Hivyo usikate tamaa, unapoona chochote unachomfanyia Mungu sasa, hakizai kama vile unavyotazamia.. Kamwe usife moyo, kinyume chake ongeza bidii. Na wakati utafika utaona matunda ya taabu zako.
UKIOKOKA, JIANDAE KUPITISHWA USIPOPATAZAMIA.
Nini maana ya siku moja kwa Bwana ni kama miaka elfu, na miaka elfu ni kama siku moja? (2Petro 3:8)
VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 3
USIMLAANI KIZIWI, WALA USITIE KWAZO MBELE YA KIPOFU.
Walawi 19:14 “Usimlaani kiziwi, wala usitie kwazo mbele ya kipofu, bali umche Mungu wako; Mimi ndimi Bwana”.
Vifungu hivyo vinatuonyesha, tabia ya watu ambao wanatumia udhaifu wa watu wengine kuwaletea madhara au matatizo zaidi badala ya kuwasaidia.
Kibinadamu ukikutana na kipofu njiani, na anataka asaidiwe kuvuka barabara, bila shaka utamwonea huruma na kwenda kumshika mkono umvushe, huwezi kwenda kumvizia wakati gari linapita ndio umsogeze barabarani agongwe afe, afe huo sio utu.
Lakini cha ajabu ni kwamba hao watu wapo. Kwa mfano utakuta mtu anataka kununua bidhaa fulani, lakini kwa bahati mbaya mteja huyo hajui sana ubora wa bidhaa hizo, labda tuseme simu. Sasa muuzaji badala atumie busara kumwelekeza bidhaa bora, kinyume chake anatumia fursa ile, kwenda kumletea feki, na kumuuzia kwa bei ile ile ya orijino, kisa tu haijui orijino ipoje. Na mwisho wa siku mnunuzi anaitumie siku mbili tatu, imeharibika, anaitupa, anakuwa amepata hasara. Sasa huo ndio ukwazo Bwana anaouzungumzia hapo mtu anaomwekea kipofu.
Hilo jambo linamkasirisha sana Mungu, Na kwa bahati mbaya wafanyabiashara wengi sana wanayo tabia hii. Ni tabia ya shetani, ambayo alikuwa nayo tangu zamani, Utakumbuka pale Edeni alipoona Hawa ni kipofu, hajui mema na mabaya, akatumia udhaifu huo kumdanganya, badala ya kumwelekeza kuyashika maagizo ya Mungu, na mwisho wake ukawa ni Hawa kutumbukia shimoni. Sasa wapo baadhi ya wanadamu waliokosa UTU namna hii, wanatumia udhaifu wa watu wengine kujitafutia faida zao.
Au utakuta ni mama ntilie, anaona akipika chakula bora hapati faida ya kutosha, anachowaza ni kwenda kutia hamira kwenye ubwabwa wake, ili uvimbe awauzie wateja wengi zaidi, kwasababu anajua wateja wanapenda chakula kingi, Na amekuwa akifanya hivyo kwa muda mrefu, Hiyo yote ni kisa tu haonekani kwa wateja, wakati mwingine anapikia na mafuta ya trasfoma.. Hiyo ni dhambi inayomchukiza sana Mungu.
Mwingine ni mtumishi wa Mungu, anakutana na mtu mwenye matatizo fulani, pengine ya kiafya, au ya kifamilia, au ya kiroho sasa yeye badala amuhudumie kama mtumishi wa Bwana,anatumia nafasi hiyo ya udhaifu wake, kumtisha, na kumpa shuhuda za uongo, lengo tu ni atumie fursa hiyo kuchukua pesa zake. Watu kama hawa nimeshakutana nao sana. Huko ndio kutia kwazo mbele ya kipofu, na kumlaani kiziwi.
Tunapaswa tuwe kama Ayubu, ambaye alisema..
Ayubu 29:15 “Nalikuwa macho kwa kipofu, Nalikuwa miguu kwa aliyechechemea”.
Tuwasaidie wale ambao wanahitaji msaada, vilevile tuwaongoze mahali sahihi wale ambao wanahitaji kusaidiwa. Tumche Bwana wetu, Tupate siku nyingi na za heri za kuishi katika dunia yake.
Ni nani aliye kipofu, ila mtumishi wangu?
UFUNUO: Mlango wa 15
USIPOTEZWE NA MANENO YA MANABII WA UONGO.