SWALI: Kwanini Bwana Yesu aliitaja Tiro na Sidoni, kwamba kama ingeliona miujiza ile aliyoifanya kule Bethsaida ingalitubu kwa kuvaa magunia na majivu. Kwani miji hii ilikuwa ni ya namna gani, na ilifanya kosa gani?
JIBU: Tusome..
Mathayo 11:21 “Ole wako, Korazini! Ole wako, Bethsaida! Kwa kuwa kama miujiza iliyofanyika kwenu ingalifanyika katika Tiro na Sidoni, wangalitubu zamani kwa kuvaa magunia na majivu.
22 Walakini nawaambieni, itakuwa rahisi Tiro na Sidoni kustahimili adhabu zao siku ya hukumu kuliko ninyi.
23 Nawe Kapernaumu, je! Utakuzwa mpaka mbinguni? Utashushwa mpaka kuzimu; kwa kuwa kama miujiza iliyofanyika kwako ingalifanyika katika Sodoma, ungalikuwapo mji huo hata leo”.
Ukitazama kwa karibu utaona Bwana Yesu aliiona miji hiyo miwili (yaani Tiro na Sidoni), ilifanana na Sodoma na Gomora kwa tabia zake.
Kumbuka Sodoma na Gomora iliangamizwa kwa maovu yaliyopindukia, Vivyo hivyo Tiro na Sidoni ziliangamizwa, lakini wengi wetu hatufahamu iliangamizwaje? Na Kwa kosa gani..Na hiyo ni kutokana na kwamba habari zao hazipo wazi sana katika biblia kama vile zilivyokuwa za Sodoma na Gomora.
Jaribu kufikiria mpaka biblia inamfananisha mfalme wa Tiro na Shetani mwenyewe..Ujue kuwa ilikuwa inamwangaza shetani mwenyewe duniani kwa tabia zake..Tutakuja kuona huko mbele..
Sasa ukisoma agano la kale, utagundua kuwa mji huu ulikuwa ni mkubwa sana kibiashara hususani ule wa TIRO, Ujenzi wa Hekalu la Mfalme Sulemani kwa sehemu kubwa ulitegemea njenzo na vifaa kutoka katika nchi hizi mbili (Soma 1Nyakati 22:4)..
Hivyo enzi zile za wafalme, mataifa haya mawili yalitajirika kwa haraka sana, japokuwa mataifa kama Babeli na Ashuru yalikuwa bado yapo juu yao, lakini mataifa haya mawili yalikuwa na nguvu kubwa sana kiuchumi, ni sawa leo tuyaite CHINA, huku Babeli na Ashuru yabakie kuwa , Marekani na Urusi. Jinsi leo hii China ilivyochangamka kibiashara ndivyo ilivyokuwa miji hiyo miwili.
Sasa ukipata muda unaweza kusoma kitabu cha Ezekieli kuanzia sura ya 26 mpaka ya 28, Ujione jinsi mataifa haya yalivyosifiwa na Mungu kuwa imara kibiashara na kiuchumi, Na jinsi Mungu alivyoyatamkia maangamizo yao, siku moja, ambayo yatatelekezwa na mfalme wa Babeli Nebukadreza..
Ukisoma pale utaona inasema..
nchi hiyo kwa jinsi ilivyokuwa nzuri mpaka ikajiita “Ukamilifu wa Uzuri” hakuna wa kufananishwa nayo. Jinsi Ilivyokuwa kiini cha biashara cha mataifa yote, mpaka Nchi ya Tarshishi ile Yona aliyoikimbilia, ilitegemea kufanya biashara na Tiro, watu wasomi na wenye akili walikuwa wanaishi humo (TIRO).. kila aina ya biashara ya madini na mawe, biashara ya wanyama, na vifaa vya kivita zilifanyika humo. Biashara za nguo na urembo wa kila namna, biashara ya vyakula na matunda. walikuwa na jeshi kubwa la kutosha, mpaka wakawa wanawauzia silaha mataifa mengine.
Hiyo ndio ikampa kiburi mkuu wao mpaka afikie hatua ya kujilinganisha na Mungu, kutokana na Hekima na utajiri aliokuwa nao na fedha nyingi..Na Yezebeli Yule tunayemsoma kwenye biblia alitokea huko(Ndiye aliyemwingiza mungu baali Israeli)..Hivyo Mungu akapanga siku ya maangamizo yao..(Ezekieli 28:1-10)
Biblia inasema Wafalme wa kila mahali watatetemeza kwa jinsi anguko lake litakavyokuwa(Tiro), wakisema wewe uliyekuwa mwenye nguvu imekuaje umeanguka ghafla hivi, kirahisi,
Ezekieli 27:32 “Na katika kulia kwao watakufanyia maombolezo, na kukuombolezea, wakisema, Ni nani aliye kama Tiro, kama yeye aliyenyamazishwa kati ya bahari?
33 Bidhaa zako zilipotoka katika bahari, uliwajaza watu wa kabila nyingi; uliwatajirisha wafalme wa dunia, kwa wingi wa mali zako, na kwa utajiri wako”.
Ezekieli 26: 1 “Ikawa katika mwaka wa kumi na mmoja, siku ya kwanza ya mwezi, neno la Bwana likanijia, kusema,
2 Mwanadamu, Kwa sababu Tiro amesema juu ya Yerusalemu, Aha! Yeye amevunjika aliyekuwa lango la kabila za watu; amenigeukia; nitajazwa kwa kuwa sasa ameharibika;
3 basi Bwana MUNGU asema hivi; Tazama, mimi ni juu yako, Ee Tiro, nami nitaleta mataifa mengi kupigana nawe, kama bahari iinuavyo mawimbi yake.
4 Nao wataziharibu kuta za Tiro, na kuibomoa minara yake; tena nitakwangua hata mavumbi yake yamtoke, na kumfanya kuwa jabali tupu”.
Ukiendelea sasa kusema Ezekieli 28:11-19 utaona Mungu akitoa unabii wa shetani, na jinsi anguko lake lilivyokuwa kule mbinguni kwa kivuli hichi hichi cha mfalme wa Tiro.
Vivyo hivyo na Sidoni naye alikuwa pacha wake, soma habari iliyosalia utaona hilo. Kama vile tu Gomora alivyokuwa pacha wa Sodoma.
Sasa watu wa miji hiyo walitiwa kiburi kwa mali na fedha, wakamsahau Mungu muumba wa mbingu na nchi, wakawa wanaishi maisha ya dhambi, wanawaza tu mambo ya kidunia hadi siku moja Mungu alipoleta uharibifu wao kwa mkono wa Nebukadneza.
Lakini tunaona pale Bwana Yesu anasema.. Laiti ingeliona miujiza iliyokuwa inafanywa na yeye, basi miji hiyo miwili ambayo imefananishwa na utawala wa shetani kwa kujiinua..Watu hao wangalitubu tena kwa kuvaa nguo za magunia na majivu. Mpaka na mfalme wao angetubu.
Tengeneza picha, ni sawa na leo hii, kila mahali tunasikia shuhuda nyingi, tunaona miujiza mingi Kristo akiifanya, mpaka wafu wanafufuliwa mbele ya macho yetu lakini bado tunaupuuzia wokovu, tunaona kama ni habari za kale.
Tujiulize Je siku ile tutastahimili vipi adhabu ya hukumu?.
Ni wazi kuwa kama ziwa la moto litakuwa kali sana, basi kwa vizazi vyetu litakuwa limechochewa mara 7 zaidi,.Bwana atusaidie tusiupuuzie wokovu, Kristo alilipa gharama kubwa sana kwa ajili yetu..kwahiyo tusiudharau wokovu hata kidogo.
Bwana akubariki.
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
JINSI SODOMA NA GOMORA ILIVYOKUWA INAVUTIA SANA..
MAHALI UNAPOPASWA USIMVUMILIE SHETANI HATA KIDOGO.
MTANGO WA YONA.
FAHAMU JINSI KRISTO ANAVYOPONYA WATU ROHO.
Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!
CHUKIZO LA UHARIBIFU
Sanamu ni kitu chochote kile kinachotengenezwa chenye umbile aidha la malaika wa mbinguni, mwanadamu, mnyama, au mimea…Mwanadamu yoyote anayetengeneza kitu chochote chenye mifano ya hivyo vitu tayari kashatengeneza sanamu.
Sasa sio dhambi kutengeneza sanamu…ikiwa ina lengo lisilo la kiibada…kwamfano sanamu zilizopo makumbusho, hizo lengo lake ni la kumbukumbu, pia sanamu za Wanyama kama tembo, samaki,swala,watu n.k zilizopo sehemu za makumbusho au sehemu za maonyesho, au ambazo zinawekwa mahali kama nembo ya nchi au urembo wa mji sio dhambi…
Tatizo kubwa ni pale zinapotengenezwa kwa lengo la Ibada!…kwamba inapofikia hatua ya mtu kuamini kwamba sanamu ile ya tembo ina UUNGU ndani yake na hivyo inahitajika kuogopwa au kusujudiwa, kwamba Sanamu ya mtu yule ambaye alikuwa shujaa wa Taifa letu ina Uungu ndani yake, sanamu ile ya Mtakatifu aliyewahi kuishi Ina Uungu ndani yake, na hivyo inastahili kusujudiwa, na kupewa heshima fulani na hata kutukuzwa..Hilo ndio tatizo.
Sasa kuzitumikia na kuzisujudia sanamu kwa namna hiyo ndiko kunakoitwa IBADA ZA SANAMU. Na hizi ibada za sanamu zilianzia kwa wapagani, na shetani ameziingiza mpaka kwenye kanisa..na amewapofusha watu macho na kuwafanya wasione kabisa ukweli kuwa wanaabudu sanamu..
Kwamfano utaona sanamu ya mtakatifu fulani wa kwenye biblia labda tuseme Petro, au Paulo au Hana…imewekwa pale na inapewa heshima kana kwamba ni Paulo mwenyewe yupo ndani ya ile sanamu, inapewa heshima kana kama ni Petro mwenyewe yupo ndani ya ile sanamu kiasi kwamba mtu anaogopa hata kuikanyaga kwa bahati mbaya..kwasababu anahisi kabisa yule pale ni Petro, au Paulo amesimama…
Unakuta imewekwa sanamu ya Bwana Yesu pale, mtu anaogopa hata kuitazama usoni akihisi ni Bwana Yesu Mwenyewe yupo pale anamtazama,…hivyo inamfanya aende kwa adabu na staha na moyo wa ibada mbele ya ile sanamu, hatimaye kujinyenyekeza chini yake na hata kutaka kubarikiwa chini ya ile sanamu…HAYO NDIYO MACHUKIZO MBELE ZA MUNGU…Hiyo ndiyo sababu Bwana amesema Kwamba tusizichonge kabisa kama zitatupeleka katika kuzisujudia na kuzitumikia kwasababu zinamtia Mungu WIVU…Maana yake ni kwamba badala moyo wako uwe mbinguni Mungu aliko, na akili yako uipeleke mbinguni, na mawazo yako uyapeleke mbinguni mahali alipo…wewe unayapeleka kwenye ile sanamu iliyopo mbele yako, unayapeleka katika picha iliyopo mbele yako, hicho ndicho kinachomtia Mungu wivu.
Na inafika mbali Zaidi hadi wengine wanaziundia sala maalumu za kuombea, yaani wanafanya sanamu hizo kama nyezo au daraja la kuwasiliana na Mungu.
Kutoka 20:4 “Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia.
5 Usivisujudie wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi, Bwana, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao,
6 nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao, na kuzishika amri zangu”.
Mungu wetu anataka tumwabudu katika roho na kweli…na si katika sanamu…
Yohana 4:20 “Baba zetu waliabudu katika mlima huu, nanyi husema ya kwamba huko Yerusalemu ni mahali patupasapo kuabudia
21 Yesu akamwambia, Mama, unisadiki, saa inakuja ambayo hamtamwabudu Baba katika mlima huu, wala kule Yerusalemu.
22 Ninyi mnaabudu msichokijua; sisi tunaabudu tukijuacho; kwa kuwa wokovu watoka kwa Wayahudi.
23 Lakini saa inakuja, nayo sasa ipo, ambayo waabuduo halisi watamwabudu Baba katika ROHO NA KWELI. Kwa maana Baba awatafuta watu kama hao wamwabudu.
24 Mungu ni Roho, nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli”
Umeona Mungu aabudiwi kupitia sanamu fulani, wala kilima fulani wala mtu fulani wala malaika fulani..yeye anaabudiwa katika roho na kweli…Laiti kama angekuwa anapenda tumwabudu kwa kumuuona…asingekuwa kama alivyo leo…angejidhihirisha duniani kote na wote tungeijua sura yake, na picha yake ingezagaa kila mahali, tungeiabudu na kuisujudia na wote tungekuwa na nakala ya picha hiyo…tungeiweka mpaka kama nembo ya Hela yetu..lakini hajayaruhusu hayo kwasababu anataka sisi tusimwabudu kupitia picha yake..anataka tumwabudu katika ROHO NA KWELI.
Hatumwoni lakini tunaamini yupo…Na hiyo Imani ya kwamba hatumwoni lakini tunaamini yupo, ndiyo ya thamani kwake…na ndiyo anayotaka tumwabudu nayo…
Kama ni picha ya Bwana Yesu au mtakatifu yoyote iwepo tu kama “lugha ya picha” na si chombo cha ibada wala kichukuacho sehemu ya hisia za mtu kana kwamba ndio kitu chenyewe halisi….Bwana anataka tukiweka sanamu/picha ya mtakatifu fulani tuichukulie ile picha kama vile tunavyoichukulia picha/sanamu ya mnyama iliyopo makumbusho…Hakuna mtu anayeweza kwenda mbele ya sanamu tembo na kuiogopa na kuipa heshima kana kwamba ni tembo halisi yupo pale, hakuna mtu anayeweza kuona sanamu ya simba akatetemeka na kukimbia, hakuna mtu anaweza kuona sanamu ya ng’ombe akaenda kukamua maziwa chini yake…Na sisi hatupaswi kwenda kukamua baraka kutoka kwenye sanamu ya mtakatifu Mariamu tulioitengeneza sisi au ya Bwana mwenyewe.
Shetani ameshalijua hilo, Hivyo alichokifanya ni kwenda kujipachika nyuma ya sanamu hizo, ili mumwabudu kisirisiri. Hivyo unapojihusisha na mojawapo ya ibada hizo ujue kabisa unamwabudu shetani.
2Wakorintho 6:16 “Tena pana mapatano gani kati ya hekalu la Mungu na sanamu? Kwa maana sisi tu hekalu la Mungu aliye hai; kama Mungu alivyosema, ya kwamba, Nitakaa ndani yao, na kati yao nitatembea, nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.
17 Kwa hiyo, Tokeni kati yao, Mkatengwe nao, asema Bwana, Msiguse kitu kilicho kichafu, Nami nitawakaribisha.
18 Nitakuwa Baba kwenu, Nanyi mtakuwa kwangu wanangu wa kiume na wa kike,
Bwana atubariki na kutusaidia.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
MAFUNDISHO YA MASHETANI
DANIELI: Mlango wa 3
Sabato halisi ni lini, Je! ni Jumapili au Jumamosi?, Ni siku gani itupasayo kuabudu?
Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!
CHUKIZO LA UHARIBIFU
UNYAKUO.
1.Naomba kuelezewa maana ya huu mstari tafadhali, unaosema; Mfalme wa Israel akajibu, akasema, Mwambieni ” Avaaye asijisifu kama avuaye ” huyu mfalme alikuwa anamaanisha nimi kusema hivyo? (1Wafalme 20:11)
JIBU: Hiyo ni mithali iliyokuwa inatumika wakati huo, kama leo watu wanavyosema “usitukane mamba kabla hujavuka mto”..Na hapo ni hivyo hivyo…hapo huyu Benhadadi alikuwa ameshajitangazia ushindi dhidi ya Israeli kabla hata ya vita…(Ni kama vile anameshawadharau anaokwenda kupigana nao kabla hata hajapigana nao), Ndio Mfalme Ahabu akamwambia avaaye asijisifu kama avuaye…maana yake avaaye mavazi ya vita ambaye ndio kwanza anakwenda vitani asijisifu kama yule mtu ambaye tayari ameshavimaliza vita na kashinda! na hivyo sasa anavua mavazi yake na kusherehekea ushindi..Hiyo ndio maana yake huo mstari.
Na ukifuatilia Habari hiyo utaona jinsi Mungu alivyowapigania Israeli kutokana na kiburi hicho cha mfalme wa Shamu, kuwadharau Israeli Pamoja na Mungu wao.
1Wafalme 20: 10 “Ndipo Ben-hadadi akatuma kwake, akasema, Miungu wanifanyie hivi na kuzidi, yakiwa mavumbi ya Samaria yatatosha makonzi ya watu wote walio miguuni pangu.
11 Mfalme wa Israeli akajibu, akasema, Mwambieni, Avaaye asijisifu kama avuaye.
12 Ikawa, Ben-hadadi alipolisikia neno hilo, naye alikuwa akinywa, yeye na wafalme, mabandani, aliwaambia watumwa wake, Jipangeni. Wakajipanga juu ya mji.
13 Na tazama, nabii akamjia Ahabu mfalme wa Israeli, akasema, Bwana asema hivi, Je! Umeona makutano haya yote walio wengi? Angalia, nitawatia leo mkononi mwako; nawe utajua ya kuwa ndimi Bwana”.
Shalom.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
NA MTU MMOJA AKAVUTA UPINDE KWA KUBAHATISHA, AKAMPIGA MFALME
Katika injili utaona zipo sehemu kuu mbili ambazo Bwana alimfukuza shetani waziwazi.. sehemu ya kwanza ni pale shetani alipotaka amsujudie kwa mapatano kuwa atampa milki zote za ulimwengu.Na sehemu ya pili ni pale Shetani alipomfariji kuwa hatapitia mabaya yaliyo mbele yake..
Tusome..
Mathayo 4:8 “Kisha Ibilisi akamchukua mpaka mlima mrefu mno, akamwonyesha milki zote za ulimwengu, na fahari yake,
9 akamwambia, Haya yote nitakupa, ukianguka kunisujudia.
10 Ndipo Yesu alipomwambia, NENDA ZAKO, SHETANI; kwa maana imeandikwa, Msujudie Bwana Mungu wako, umwabudu yeye peke yake”.
Na mahali pengine ni..
Mathayo 16:21 “Tangu wakati huo Yesu alianza kuwaonya wanafunzi wake ya kwamba imempasa kwenda Yerusalemu, na kupata mateso mengi kwa wazee na wakuu wa makuhani, na waandishi, na kuuawa, na siku ya tatu kufufuka.
22 Petro akamchukua, akaanza kumkemea, akisema, Hasha, Bwana, hayo hayatakupata.
23 Akageuka, akamwambia Petro, NENDA NYUMA YANGU, SHETANI; u kikwazo kwangu; maana huyawazi yaliyo ya Mungu, bali ya wanadamu”.
Bwana aliona ipo mipaka ambayo mtu yeyote au kiumbe chochote hakipaswi kuvuka, Na kwamba yeyote atakayejaribu kufanya hivyo si tu kukemewa bali ni kufukuzwa kabisa.. Na shetani alifukuzwa na Bwana katika vitu hivi viwili..Kwanza ni pale alipotaka asujudiwe hilo tayari lilikuwa ni kosa kubwa machoni pa Bwana haijalishi ni ahadi ngapi nzuri zilifuata mbele yake..
Leo hii watu wengi wapo tayari, kumwabudu shetani kisa mali, wapo tayari kubadili imani kisa wanawake/wanaume, wapo tayari kula rushwa kisa wanaahidiwa pesa nzuri, wapo tayari kuua na kutoa kafara ili wawe matajiri, wapo tayari kujiuza ili wapate kipato, wapo tayari kupiga ramli wawaridhishe wazee wa ukoo, wapo tayari kufanya lolote lile haijalishi ni kinyume na mapenzi ya Mungu kiasi gani ili wapate faida Fulani au unafuu Fulani..
Ndugu hatua kama hiyo ukifikia ikiwa wewe ni mkristo Usimwangalie shetani mara mbili, usimvumilie shetani hata kidogo!, mfukuze kwa kishindo chote, haijalishi leo hii unapitia katika hali ngumu kiasi gani..Kumbuka hata wakati shetani anamletea Kristo majaribu kama haya ya kuahidiwa ulimwengu mzima na milki zote, alikuwa katika hali ya njaa, hajala siku 40, hana kibanda, wala biashara wala nini..Lakini alimwambia ondoka, hapa, kwa namna nyingine tunaweza kusema nisikuone eneo hili tena.
Sehemu nyingine ambayo unapaswa usimvumilie shetani ni pale, Mungu anapokuonyesha mafanikio Fulani makubwa mbeleni lakini sharti kwanza upitie mateso Fulani au dhiki Fulani kabla ya kuyapata, lakini shetani anatokea na kukwambia usihofu hutapitia..Hapo hupaswi kusikiliza, ni kumfukuza tu..
Embu jaribu kufiria mfano Bwana angeyasikiliza yale maneno ya shetani yaliyokuwa ndani ya kinywa cha Petro, mambo yangekuwaje leo hii? ni wazi kuwa hadi leo hii mimi na wewe tusingepata neema ya wokovu, kwasababu Kristo asingesulibiwa..Damu isingepatikana kwa ajili ya ondoleo la dhambi zetu… Lakini aliona wimbi kubwa la wanadamu linakwenda kuokolewa na ibilisi hataki hilo litendeke..akajaribu kumbunia njia za kulikwepa.
Hata Mtume Paulo, kuna wakati alijua kabisa kuwa vifungo na dhiki vinamngoja huko mbeleni, lakini hakukubali kukatishwa tamaa na watu, kwamba abaki asiende Yerusalemu. Watu wanadhani Roho Mtakatifu kumwambia Paulo vile, ilikuwa ni kumzuia asiende hapana, bali alikuwa anampa taarifa ya mambo yatakayomkuta huko mbeleni, kwasababu ni kawaida ya Mungu kuwapata watu wake taarifa kabla mabaya hayajawakuta.. Lakini Ni wale watu waliokuwa naye ndio waliomwambia asiende, lakini yeye hakukubali, akawaambia..
Matendo 21:12 “Basi tuliposikia haya, sisi na watu wa mahali pale, tukamsihi asipande kwenda Yerusalemu.
13 Ndipo Paulo alipojibu, Mnafanya nini, kulia na kunivunja moyo? Kwa maana mimi, licha ya kufungwa, ni tayari hata kuuawa katika Yerusalemu kwa ajili ya jina lake Bwana Yesu”.
Alifanya hivyo kwasababu aliona wingi wa matunda atakayoyaleta kwa Mungu ni mengi akifananishwa na dhiki fupi za kitambo, zitakazoletwa na shetani.
Hivyo na sisi wakristo, tusiruhusu mambo hayo mawili shetani ayalete mbele yetu..kwanza tusiruhusu tamaa za ulimwengu kutufarakanisa na Mungu wetu, Pia tusiruhusu dhiki za kitambo zikatukosesha Baraka Mungu alizotuchumia huko mbeleni…
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
Je kuweka mapambo kama mikufu, vikuku na kutoboa pua ni dhambi?
Ni dhambi kuota unafanya kitu kiovu kama uzinzi, uuaji, wizi, uasherati, au ulevi?
JIBU: Ndoto huja pasipo hiari ya mtu..hakuna mtu anayeweza kupanga aote nini leo au kesho…Zinakuja tu zenyewe pasipo mtu kupanga….Lakini ndoto nyingi ni MATOKEO ya kitu Fulani ambacho kinaendelea katika maisha ya mtu.
Kwamfano umelala na njaa..usiku utajikuta unaota unakula!,(Isaya 29:8) umeshinda ukifanya shughuli Fulani siku nzima ukilala utajiona unaendelea kufanya vile vitu katika ndoto…kabla ya kulala ulikuwa unatazama kitu Fulani kwenye luninga au mtandaoni ambacho kimegusa hisia zako…utakapolala ni rahisi sana kukiota kile kitu
Vivyo hivyo..umekuwa karibu na mtu Fulani kwa muda mrefu katika maisha yako ghafla akaondoka au akafariki..Ni lazima utakuwa unamwota ota mara kwa mara. Kwahiyo ndoto nyingi ni matokeo ya kitu Fulani ambacho kinaendelea katika maisha ya mtu..Ndio maana biblia imeweka wazi jambo hilo katika..
Mhubiri 5:3 “Kwa maana ndoto huja kwa sababu ya shughuli nyingi; na sauti ya mpumbavu kwa njia ya wingi wa maneno”.
Kwahiyo ukiota unaiba na ndoto inajirudia rudia ni matokeo ya kitu ambacho kinaendelea katika maisha yako… “Hiyo ndoto uliyoiota sio dhambi”…lakini ni ujumbe kwamba katika maisha yako kuna uwezekano bado kuna vimelea vya wizi…hivyo zidi kuyachunguza kwa undani maisha yako na kuyatakasa…Ukiona unafanya uasherati, ni hivyo hivyo…chunguza mtindo wa maisha yako unayoishi, labda bado unatabia ndogo ndogo pengine unaridhia picha chafu au video chafu ambazo unapishana nazo kwenye mitandao, au bado unayaendekeza mawazo machafu ya zinaa yanapokujia kichwani mwako..kwahiyo ndio maana zinaendelea mpaka kwenye kichwa chako unapolala..
Na jambo muhimu la kufahamu ni kwamba kama ulikuwa umetoka kwenye dunia moja kwa moja ukaokoka…Bwana anakuwa amekusamehe maisha yako na dhambi zako, lakini madhara ya dhambi katika maisha yako hayataondoka siku ile ile unapookoka..yataondoka kidogo kidogo mpaka mwisho wake kuisha kabisa…yaani kama ulikuwa ni mzinzi wa kupindukia kabla ya kuokoka…
Siku ile unapookoka Roho Mtakatifu anaiondoa ile tabia ndani yako…lakini utaendelea kuvuna matokeo ya uzinzi wako kwa kipindi Fulani, ndio hapo hayo mandoto ya mambo uliokuwa unayafanya nyuma yanaweza kuendelea kwenye kichwa chako kwa kipindi kadhaa (Hayo ndio madhara ya dhambi)…
Lakini yajapo hayo baada ya kumwamini na kupokea Roho Mtakatifu usiogope!.. unapoota unafanya hayo mambo katika ndoto baada ya kumwamini Yesu, na ilihali hayo mambo katika maisha yako halisi umeshayaacha kitambo…unachotakiwa kufanya ni kuikataa hiyo hali…na kusema mimi sio huyo!!!..usiruhusu kuikubali hiyo hali kwamba ni wewe…Ikatae!, usikubali kukata tamaa wala kuwa mdhaifu…na itafika kipindi Fulani hayo mandoto yatakwisha kabisa….
Wengi wanapofikia hatua kama hii, wamemwamini Yesu, wamekwenda kubatizwa na wamepokea Roho Mtakatifu lakini wanapojikuta baada ya siku kadhaa wanaota wanafanya mambo ambayo wameshayatubia, wengi wanarudi nyuma na kuvunjika moyo na kuhisi hawakutubu vizuri…Na hapo shetani anachukua nafasi ya kuwarudisha tena katika mambo waliyokuwa wanayafanya, na mtu anasimama kurudia rudia kuokoka hata mara 100 katika maisha yako..
Na jambo lingine ambalo litakusaidia kuepukana kwa haraka na ndoto za namna hiyo, ni kuwa mwombaji na mtafakariji wa Neno, walau Sali kila siku lisaa limoja, kama Bwana Yesu alivyotuagiza, lakini kama utakuwa maisha yako ya kuomba, hali hizo zitaendelea kukurudia rudia bila kikomo..Maombi ni ngao ya majaribu ya shetani. Ukisema umeokoka halafu maombi yanakushinda, basi bado hujaokoka.
Hivyo kwa ujumla dhambi ni mbaya na ina madhara! Na inatesa hata baada ya kuiacha!…Ukiingia mkataba na shetani, hutatoka kirahisi. Ni sawa na gari lililokuwa kwenye mwendo likapiga breki ghafla..Matairi yatasimama, injini itasimama lakini gari litazidi kuendelea mbele kidogo…na dhambi ni hivyo hivyo..utaacha uasherati, ulevi, na kila kitu siku ile unaokoka lakini mambo hayo yataendelea katika ulimwengu wako wa ndoto, lakini ukizingatia hayo tuliyoyasema utaepukana na hizo hali kwa haraka sana.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
Mwanzo 13:14 Bwana aliongea na Abramu Alipotengana na Lutu na kumpa nchi. Sasa ni kwanini aongee naye baada tu ya wao kutengana?. inamana uwepo wa Lutu ulimzuia Mungu kumpa nchi Abramu?.
JIBU: Tatizo halikuwa kwa Mungu, bali kwa Ibrahimu. Yale mazingira aliyokuwa nayo Ibrahimu ndiyo yaliyokuwa kikwazo cha Mungu kuzungumza naye kwa wakati.
Jambo hilo halikuanzia hapo, utaona tangu Mungu alipomwambia atoke kule Uru ya ulkaldayo, Badala atoke yeye peke yake alitoka na baba yake ambaye alikuwa ni mpagani-mwabudu miungu, na hiyo ikamfanya akae sehemu moja iliyoitwa Harani kwa muda mrefu bila Mungu kuzungumza naye.. Na siku tu baba yake alipokufa ndipo Mungu akazungumza naye tena na kumwambia aondoke pale aende katika nchi ya Kaanani..Jambo ambalo lingepaswa liwe ni la safari ya moja kwa moja, lakini lilimfanya awe mtu wa vituo vituo kwa muda mrefu. Ni wazi kuwa baba yake alimpinga vikali sana, kwa mambo mengi.
Matendo 7:3 “akamwambia, Toka katika nchi yako na katika jamaa zako, ukaende hata nchi nitakayokuonyesha.
4 Ndipo alipotoka katika nchi ya Wakaldayo, akakaa Harani, akatoka huko baada ya kufa babaye, Mungu akamhamisha mpaka nchi hii mnayokaa ninyi sasa”.
Lakini hakuondoka peke yake tena kule Harani bali aliondoka na mjomba wake Lutu..Na walipofika huku, Mungu hakujifunua kikamilifu kwake mpaka walipotengana tena, ndipo baadaye Mungu alipoona utulivu wake sasa kazungumza naye tena.
Hiyo ni desturi ya Mungu tangu zamani. Akikuita unapaswa uondoke wewe kama wewe na kumfuata, kwasababu ukienda na mtu mwingine ambaye hana Habari na Mungu, ni wazi kuwa atakuja kuwa kikwazo kikubwa kwako huko mbeleni, unaweza wewe kutamani hivi, yeye atatamani kile, wewe ukiwaza muda huu nikasali, au nikashuhudie yeye akafikiri vile mkafanye biashara, na hiyo inakuwa kikwanzo kikubwa sana cha Mungu kuyatimiliza yale maono aliyoyaweka ndani yako.
Na ndio maana Bwana Yesu alisema, nimekuja kuleta upanga duniani….
Mathayo 10:34 “Msidhani ya kuwa nimekuja kuleta amani duniani; la! Sikuja kuleta amani, bali upanga.
35 Kwa maana nalikuja kumfitini mtu na babaye, na binti na mamaye, na mkwe na mkwe mtu;
36 na adui za mtu ni wale wa nyumbani mwake.
37 Apendaye baba au mama kuliko mimi, hanistahili; wala apendaye mwana au binti kuliko mimi, hanistahili”.
Hivyo tukitaka tufike mbali, au tukitaka Mungu atutumie ipasavyo hatuna budikuweka mbali vitu au kujitenga na watu ambao tunaona kabisa wanaweza kuathiri mwito wetu kiuwepesi.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
Je! Ule mwiba uliokuwa katika mwili wa Paulo ulikuwa ni nini?
Je! Ule mwiba uliokuwa katika mwili wa Paulo ulikuwa ni nini?
NINI NI KILICHOMFANYA IBRAHIMU AKUBALI KUMTOA MWANAWE SADAKA?
Kwanini Mungu aliikubali sadaka ya Yeftha ya kumtoa binti yake kafara?
Utukufu na Heshima.
Mungu wetu ndiye anayestahili utukufu na heshima yote..biblia inatuambia hivyo katika..
Ufunuo 4:11 “Umestahili wewe, Bwana wetu na Mungu wetu, kuupokea UTUKUFU NA HESHIMA na uweza; kwa kuwa wewe ndiwe uliyeviumba vitu vyote, na kwa sababu ya mapenzi yako vilikuwako, navyo vikaumbwa”.
Lakini Pamoja na hayo Mungu wetu sio mchoyo, yupo tayari kumvika utukufu na heshima kila mtu ambaye atakuwa tayari kumpokea, na kuishi Maisha matakatifu na kuyashinda Maisha ya ulimwengu biblia inatuambia..
Warumi 2:10 “bali utukufu na heshima na amani kwa kila mtu atendaye mema, Myahudi kwanza na Myunani pia; 11 kwa maana hakuna upendeleo kwa Mungu”.
Unaona?. Kuna mambo mazuri sana, Mungu aliyotuandalia mbinguni, mambo ambayo jicho halijawahi kuona wala sikio kusikia, wala hayajawahi kuingia katika moyo wa mwanadamu. Tutavikwa mataji ya utukufu na heshima, tutang’aa kama jua, tutaishi Maisha ya raha na furaha milele, tutasahau yote tuliyopitia nyuma. Tutapewa miili ya utukufu isiyougua milele, isiyozeeka, isiyo chakaa, isiyo minyonge, isiyo na ulemavu. Na Zaidi ya yote Tutatawala la Mungu, tuyafurahia Maisha kwa miaka isiyokuwa na mwisho,.. Ni raha iliyoje? Ni heri tukose kila kitu duniani lakini tusikose, heshima hiyo Mungu aliyotuandalia kule ng’ambo.
Lakini, ni kinyume chake ni kwamba wale ambao leo hii duniani hawataki kuutafuta huu utukufu na heshima idumuo, utokao kwa Mungu, siku ile ya hukumu watapata hasira na ghadhabu ya milele.
Warumi 2:7 wale ambao kwa saburi katika kutenda mema wanatafuta utukufu na heshima na kutokuharibika, watapewa uzima wa milele;
8 na wale wenye fitina, wasioitii kweli, bali wakubalio dhuluma, watapata hasira na ghadhabu;
9 Utukufu na Heshima ya mwanadamu atendaye uovu, Myahudi kwanza na Myunani pia.
Tunaishi katika siku ambazo unyakuo, unaweza kutokea siku yoyote. Na watakatifu kunyakuliwa mbinguni. Dalili zote zinathibitisha hilo, na dalili mojawapo kuu ni hilo la kuzuka kwa magonjwa yasiyokuwa na tiba ambayo biblia imeyafananisha na TAUNI..Leo hii duniani tunaona magonjwa kama CORONA, yanatimiliza unabii wazi wazi mbele ya macho yetu…Tuseme nini tena?
Je wewe nawe bado upo nje ya Kristo? Ingia ndugu yake ndugu yangu, Kristo ayabadilishe Maisha yako. Ukiamua leo kwa dhati kutubu dhambi zako Kristo atakupa utukufu na heshima isiyoharibika kwako. Haijalishi ulikuwa mlevi kiasi gani, umetoa mimba nyingi namna gani, umeua watu wengi kiasi gani, umeloga sana watu namna gani, umezini mara nyingi namna gani..Kristo yupo tayari kukusamehe leo hii ikiwa kwa moyo wako wa dhati utakubali..
Kama upo tayari kufanya hivyo..
Basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.
EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.
ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.
AMEN.
Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako.
Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.
Ubarikiwe sana.
Utukufu na Heshima, zina Mungu wetu daima.
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
UNYAKUO.
CHUKIZO LA UHARIBIFU
Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!
MAONO YA NABII AMOSI.
MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.
Mungu ni Mungu tu!.
Watu wengi tunadhani, tunaweza kumuudhi Mungu au kumkomoa Mungu kiasi cha kumgharimu kupoteza kitu fulani, pale tunapofanya jambo lisilompendeza..
Biblia inasema hivi..
Ayubu 35:6 Ikiwa umefanya dhambi, umefanya nini juu yake? Yakiwa makosa yako yameongezeka, wamfanyia nini yeye?
7 Ikiwa u mwenye haki, wampa kitu gani? Au yeye hupokea nini mkononi mwako?
8 Uovu wako waweza kumwumiza mtu kama wewe; Na haki yako yaweza kumfaa mwanadamu.
Unaona, Kumbe hata haki zetu, au matendo yetu mazuri, hayamwongezi Mungu kitu chochote, hayamwongezei umri wa kuishi, kwa yeye tayari ni wa milele, hayamwongezei afya, wala chochote kile kizuri kwasababu vitu vyote vinatoka kwake.
Warumi 11:36 “Kwa kuwa vitu vyote vyatoka kwake, viko kwa uweza wake, tena vinarejea kwake. Utukufu una yeye milele. Amina”.
Tukisema, tujiue, hakumbadilishi yeye kuwa Mungu, tukisema hatumpendi bado hakumfanyi yeye kutokuwa Mungu, hata tukisema hayupo, ndio kabisa hakuubadilishi uungu wake. Ndege wataendelea kumsifu, jua litaendelea kuangaza majira yake, anga litaendelea kuwa la blue.
Hivyo tunachopaswa kufanya ni kujinyenyekeza mbele zake tu, haijalishi leo hii tunapitia magumu mengi kiasi gani, au mazuri mengi kiasi gani, tukiwa wanyenyekevu mbele zake, wakati wake ukifika tutauna wema aliotuwekea sisi tunaomtumainia ..Kuzielewa njia zote za Mungu hiyo haiwezekani, hata tupambane vipi, lakini tunachojua tu ni kuwa anatuwazia mawazo mazuri siku zote,
Yeremia 29:11 Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema Bwana, ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho.
Hivyo ndugu yangu unausoma ujumbe huu pengine, bado hujaokoka, wakati uliokubalika ndio sasa, usiache leo ipite bila kuyasalimisha maisha yako kwa Kristo. Ukimaanisha na kudhamiria kweli kutubu, hapo ulipo haijalishi upo sehemu gani, Kristo atayageuza maisha yako mara moja, na kukupa badiliko la ajabu ambalo litakufanya ulistaajabie maisha yako yote..
Kama upo tayari kufanya hivyo basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.
EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, . NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.
ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.
AMEN.
Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, kuanzia huu wakati, Kwasababu Mungu ameshaipokea toba yako . Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako sawasawa na Matendo 2:38.
Mungu ni Mungu tu!
Ubarikiwe sana.
Mada Nyinginezo:
SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?
CHUKIZO LA UHARIBIFU
UTENDAJI KAZI WA MPINGA-KRISTO.
Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!
JINSI SODOMA NA GOMORA ILIVYOKUWA INAVUTIA SANA..
Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe.
Kama wengi wetu tujuavyo, Ndoa ya kwanza ilifungishwa pale Edeni na Mungu mwenyewe. Na ilikuwa ndoa takatifu, iliyobeba msingi na dira ya ndoa nyingine zote zitakazofuata jinsi zinavyopaswa ziwe.
Katika ndoa ile ilihusisha Mtu mume mmoja (Adamu) na mtu mke mmoja (Hawa)..Kwa kupitia wazazi wetu hawa wawili ndio sisi sote tumetokea…ikiwa na maana kuwa ndoa kamili na takatifu inahusisha mume mmoja na mke mmoja…na si Zaidi. Hicho ni kigezo cha kwanza na cha muhimu.
Pia kabla ya ndoa ile kufungishwa, Maisha yalianza na Adamu kwanza, Mungu alimpa Adamu mimea, mashamba ya kulima, makazi na kila kitu, hapo kabla Hawa hajatokea…na Adamu akaanza majukumu yake ya shughuli pale Edeni kabla ya Hawa kutokea…Na Hawa alipotokea alikuwa kama msaidizi tu wa kazi ambayo tayari ilikuwa imeshaanza. Ikiwa na maana kuwa Mwanamume yoyote kabla hajadhamiria kuoa ni lazima angalau awe na mahali pa kujishikiza ili aweze kumhudumia huyo mkewe anayekuja kumwoa…
Na kumbuka Mungu hakumleta Hawa kwaajili ya tamaa za mwili za Adamu, hapana bali alimleta ili awe msaidizi kwake, kwa namna zote, kifikra, na hata katika kazi zake za kimaendeleo Adamu alizokuwa anazifanya…Ikiwa na maana kuwa lengo la kwanza la ndoa sio kukutana kimwili kama inavyochukuliwa sasa na wachache wasio na maarifa ya kutosha.
Hivyo mwanamke jukumu lake kubwa katika ndoa ni kushirikiana na mume wake, na kuyafanya majukumu yote ambayo mume wake angepaswa ayafanye, ikiwemo ya kihuduma na ya kiuchumi, Hawa hakupelekwa kwa Adamu kumtoa Adamu pesa!..bali awe msaidizi….Maana yake kitu ambacho hakijakaa sawa au hakijakamilika mikononi mwa mwanaume, mwanamke anakiweka sawa na kukimalizia.
Na jukumu kubwa Zaidi mwanamume na mwanamke walilopewa ni kujiepusha na Uovu…Na shetani huwa anawatumia wanawake wengi kuharibu ndoa kuliko wanaume..Kama Hawa mzazi wetu wa kwanza angekaa katika nafasi yake na kujiepusha na uovu, leo hii duniani kungekuwa ni paradiso, lakini kwa kuacha majukumu yake ya USAIDIZI na kwenda kula matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya ambayo Mungu hakumwagiza matokeo yake ndio yakawa yale…Na hata sasa mwanamke akiacha majukumu yake na kujikita katika ulimwengu huu, katika usengenyaji, umbea, katika kutoa siri za mume wake nje, katika kutomheshimu mume wake, kumdharau, kumdhalilisha, kumwaibisha, kuvaa kikahaba, kuwa mhuni, mlevi,mtu mwenye mizaha na kila aina ya udunia, anajiharibia mwenyewe na anaibomoa nyumba yake kwa mikono yake mwenyewe..
Na Ndoa takatifu ni lazima ihusishe watu wawili wenye Imani moja..Ni kinyume na maandiko kuoa/kuolewa na mtu asiyeamini baada ya wewe kuamini, Kama umeshamwamini Yesu Kristo na uweza wake hupaswi hata kidogo kutafuta kuoa/kuolewa na mtu asiye mkristo. Na ndoa yoyote ya kikristo lazima iwasilishwe na kubarikiwa mbele ya kanisa la Kristo. Sio sahihi kabisa kufunga ndoa za kimila wala za kiserikali baada ya kumwamini Yesu Kristo.
Na ni lazima kulipa mahari kwa ndugu wa mwanamke kabla ya kumwoa, kama huo ndio utaratibu wa familia ya mwanamke, Adamu hakulipa mahari kwasababu mkewe Hawa ,chimbuko lake lilikuwa ubavuni mwake, hakuwa na wazazi wala ndugu…lakini sasa kila mwanamke anao wazazi/ndugu/walezi…Huko ndiko alikolelewa, hakulelewa ubavuni mwako,…kwahiyo ni wajibu kumtoa kwa wazazi wake kwa utaratibu huo maalumu wa kulipa mahari…
Hata Hawa alipotolewa ubavuni mwa Adamu, Bwana Mungu aliparudishia nyama pale palipotolewa ili Maisha ya Adamu yaweze kuendelea, hakuacha shimo pale wala kidonda!…Na hali kadhalika unapomtoa mwanamke kwa wazazi wake ni lazima uzibe pengo uliloliacha pale, na hilo unaliziba angalau kwa mahari, sio unamwiba na kuacha huzuni kule na malalamiko na laana na maumivu.
kama utashindwa kulipa mahari ya kiasi hicho kidogo cha fedha utawezaje kuitunza na kuihudumia familia yako inayokuja huko mbele, ambayo pengine itahitaji matunzo ya gharama nyingi kuliko hizo za mahari??…kama hutaki kutoa mahari, maana yake bado hujaelewa maana ya kuoa, hivyo unapaswa ungoje mpaka utakapoelewa vyema maana ya ndoa ndipo uoe.
Na mwisho biblia inatuambia kuwa wakati tuliobakiwa nao ni mchache sana…wale ambao wameoa na wawe kama hawajaoa…ili muda mwingi tuutumie katika kuutafuta Zaidi ufalme wake na haki yake kwasababu unyakuo upo karibuni, na mbinguni tuendako hakutakuwa na kuoa wala kuolewa, yatakuwa ni mambo mapya huko ambayo ni ya muhimu Zaidi kuliko haya.
1Wakorintho 7:28 “Lakini, kama ukioa, huna hatia; wala mwanamwali akiolewa, hana hatia; lakini watu kama hao watakuwa na dhiki katika mwili nami nataka kuwazuilia hayo.
29 Lakini, ndugu, nasema hivi, muda ubakio si mwingi; basi tokea sasa wale walio na wake na wawe kama hawana;
30 na wale waliao kama hawalii; na wale wafurahio kama hawafurahi; na wale wanunuao, kama hawana kitu.
31 Na wale wautumiao ulimwengu huu, kama hawautumii sana; kwa maana mambo ya ulimwengu huu yanapita.
32 Lakini nataka msiwe na masumbufu. Yeye asiyeoa hujishughulisha na mambo ya Bwana, ampendezeje Bwana;
33 bali yeye aliyeoa hujishughulisha na mambo ya dunia hii, jinsi atakavyompendeza mkewe”
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Mti wa MLOZI alioonyeshwa nabii Yeremia 1:12 tafsiri yake ni nini?
Ilikuwa ni mwaka wa 320, wakati wa utawala wa mfalme Licinius wa Rumi, Kumbuka zamani hizo Rumi ndiyo iliyokuwa inatawala karibu dunia nzima wakati huo na ndio iliyokuwa kichwa cha mbele kuwatesa na kuwaua wakristo ulimwenguni kote, Sasa huyu alikuwa ni mpagani, ambaye hakutaka kusikia Imani yoyote ya Kikristo.
Lakini upande wa pili kulikuwa na askari wa kirumi katika mji mmoja ulioitwa Sebaste (Kwasasa ni maeneo ya Uturuki) ambao jumla yao 40, waliotoka katika nchi mbalimbali walimwamini Kristo, na kuikiri Imani bila uwoga wowote,.Sasa alipopata habari alitoa amri kali ya kuzuia mtu yeyote kuabudu miungu mingine tofauti na yake, hivyo mfalme alichokifanya ni kutoa agizo, kwa mtu yeyote atakayeonekana anafanya hivyo atateswa vikali na kuuawa.
Lakini hawa askari, historia inatuambia wote hawa mashahidi 40 walikataa kusalimu amri, hivyo wakachukuliwa na kupelekwa kando kando ya ziwa la maji ya baridi (wakati huo ulikuwa ni msimu wa kipindi cha baridi kali huko Asia), ili wapigwe na baridi mpaka kuganda na kufa.
Na wakati huo huo Mfalme alitoa amri pembeni pawekwe bwawa la maji ya moto, na chakula kizuri, kwa yeyote atayesalimu amri atolewe na kuingizwa kwenye hilo bwana la moto apate moto, kisha alishwe vizuri.
Lakini katikati ya mateso hayo makali ambayo yaliwafanya wakae siku tatu usiku na mchana, mmoja wa wale 40 kweli alisalimu amri na kutoka kwenye maji yale ya baridi, hivyo wakabakia 39, lakini mmoja tena kati ya wale askari waliokuwa wanawasimamia akachomwa moyo sana, na usiku mmoja alipokuwa amelala kando kando ya moto kwenye barafu aliota ndoto, malaika ameshuka mbinguni, pale kwenye ziwa kisha akawavika wale askari mataji, anasema, aliyahesabu yalikuwa 39..
Alipoamka asubuhi akakata shauri, akavua silaha zake, akamkiri Kristo na saa hiyo hiyo akavua nguo zake za ki-askari, akaingia majini kuungana na wale 39 ili kutimiza idadi ya watu 40..
Na ilipofika siku ya nne asubuhi, wengi wao walikuwa wamekufa, lakini wale waliosalia hoi, waliuliwa, na miili yao ikachomwa moto, kisha, majivu yao yakaenda kutupwa kwenye mto.
Hivyo ndivyo walivyoishindania Imani mpaka kufa mashujaa hawa..
Biblia inatuambia..
Mathayo 16:25 “Kwa kuwa mtu atakaye kuiokoa nafsi yake, ataipoteza; na mtu atakayepoteza nafsi yake kwa ajili yangu, ataiona”.
Sisi tunaweza tusifikie huko kwenye kuchagua kifo au uzima kwa ajili ya Kristo, lakini kama tutashindwa kuchagua jambo jepesi la “kufa kwa Habari ya ulimwengu” kwa ajili ya Kristo , tusitazamie kamwe tutauona ufalme wa mbinguni.. sehemu nyingi biblia imetuonya kwa kutumia neno hili “MSIDANGANYIKE”..Ikiwa na maana, tunaweza kudanganyika, tukadhani kuwa kwa kuendelea kuwa walezi, siku moja tunaweza kuingia mbinguni, kwa kuendelea kuzini mara moja moja, kwa kutoa mimba, kwa kusagana, kwa kuvaa vimini na nguo za kikahaba, kwa kula rushwa, kwa kutazama picha za ngono mitandaoni, bado tukawa na nafasi ya kuingia mbinguni siku ya mwisho.
1Wakorintho 6:9 “Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti,
10 wala wevi, wala watamanio, wala walevi, wala watukanaji, wala wanyang’anyi”.
Biblia inatuambia tusidanganyike, njia ile imesonga sana, na wanaoyoiona ni wachache. Kama hatutakubali kufa kwa Habari ya ulimwengu mpaka tukaonekana sisi si kama wao, tusahau kuiona mbingu..
Kama kuacha kuvaa vimini, kuvaa suruali(wanawake), kunyoa viduku na kusuka rasta(wanaume),kuacha kampani za watu waovu, kuacha kusikiliza nyimbo za kidunia, kuacha kwenda disko, kuacha kula rushwa, kuacha kutazama picha za ngono, ni Ngumu basi, ni uzima wa milele ni wa watu wengine si wako! ….ni sawa na huyo askari mmoja aliyejaribu kuingia kwenye hayo maji ya baridi lakini uzalendo ukamshinda na kutoka kurudi kwenye mambo ya kidunia.
Ikiwa Mambo ya kujikana nafsi tu, yatatushinda, utawezaje kuutoa uhai wako kwa ajili ya Kristo, siku ile Je! tutawezaje kufananishwa na hili wingu kubwa la mashahidi wa Imani ambao walikuwa tayari kuyatoa Maisha yao (tena kwa kifo cha mateso) kwa ajili ya Kristo? (Waebrania 12:1)
Utasema mimi mazingira yanayonizunguka yananifanya nishindwe kuwa mkristo..Wenzako walikuwa ni wanajeshi wanatumika katika kazi ngumu za kidunia kushinda wewe lakini walikuwa tayari kumtanguliza Kristo kwanza.
Huu ni wakati wa kuvuta soksi zetu juu, na kuanza kuyatengeneza Maisha upya, nyakati hizi za mwisho si nyakati tena za kuvutwa vutwa tena katika wokovu, zama hizo zilishakwisha, kwasababu injili kila mahali anasikika sasa, huu ndio ule wakati Bwana Yesu alisema..
Mwenye kudhulumu na azidi kudhulumu; na mwenye uchafu na azidi kuwa mchafu; na mwenye haki na azidi kufanya haki; na mtakatifu na azidi kutakaswa (Ufunuo 22:11).
Hivyo kama wewe ni mtakatifu, pambana binafsi kuzidi kujitakasa, zidi kuogopa kuwa hapo katikati (vuguvugu), kwasababu biblia inasema walio hapo watatapikwa (Ufunuo 3:16 ). Hivyo ikiwa unajitahidi kufanya hivyo, kumbuka Bwana anakutia moyo na kukwambia, “Safari aliyoianzisha yeye moyoni mwako ataitimiza mpaka siku ile ya mwisho”.
Umeamua kuukataa ulimwengu, zidi kupiga hatua nyingine katika UTAKATIFU, haijalishi utaonekana umepotea kiasi gani, haijalishi utaonekana ni mjinga, endelea mbeleni.. lakini mwisho wako utakapofika utajikuta umetokea kwenye mji wa furaha…
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
CHUKUA MZIGO WA MWINGINE.
Chapa zake Yesu ni zipi hizo?
KUMBUKUMBU LA DHAMBI.
OLE WAO WANAOJITAHIDI KUMFICHA BWANA MASHAURI YAO.
KABLA YA MAANGAMIZI, KRISTO HUWA ANAONYESHA KWANZA NJIA YA KUTOROKEA.
USIMWOGOPE YEZEBELI.