Shalom.
Marko 8:23-26 Inatuambia Yesu alipokutana na Yule kipofu kule Bethsaida, Hakumponya palepale kama ilivyokuwa desturi yake ya kuponya watu wote wanaomfuata, bali biblia inatuambia alimchukua kwa kumshika mkono na kuanza kumtoa kwanza nje ya kijiji.
“22 Wakafika Bethsaida, wakamletea kipofu, wakamsihi amguse. 23 Akamshika mkono yule kipofu, akamchukua nje ya kijiji, akamwekea mikono yake, akamwuliza, Waona kitu? 24 Akatazama juu, akasema, Naona watu kama miti, inakwenda. 25 Ndipo akaweka tena mikono yake juu ya macho yake, naye akatazama sana; akawa mzima, akaona vyote waziwazi. 26 Akampeleka nyumbani kwake, akisema, Hata kijijini usiingie”.
“22 Wakafika Bethsaida, wakamletea kipofu, wakamsihi amguse.
23 Akamshika mkono yule kipofu, akamchukua nje ya kijiji, akamwekea mikono yake, akamwuliza, Waona kitu?
24 Akatazama juu, akasema, Naona watu kama miti, inakwenda.
25 Ndipo akaweka tena mikono yake juu ya macho yake, naye akatazama sana; akawa mzima, akaona vyote waziwazi.
26 Akampeleka nyumbani kwake, akisema, Hata kijijini usiingie”.
Jaribu kutengeneza picha, wewe ni kipofu, unapelekwa kwa daktari kwa ajili ya kupewa dawa uondoke, badala ya kukutibu anakuchukua anaondoka na wewe, bila maelekezo yoyote, na kibaya zaidi afadhali angekuwa anakupeleka hospitali nyingine badala yake anakupeleka mahali ambapo hata husikii tena sauti za watu, nje kabisa ya mji, ni rahisi kudhani huyu mtu hana nia nzuri na mimi.. Lakini tunaona huyu kipofu alitii, japokuwa hajui ni wapi anapelekwa, pengine alitembezwa na Yesu kilometa kadhaa, mpaka wanafikia mahali ambapo hamna makazi ya watu, ni mashamba tu, hata wale watu waliompeleka kwake walishamwacha, amebaki yeye tu na Yesu, na pengine na wanafunzi wake tu.
Akiwa sasa hana tumaini lolote, haelewi ni kitu gani kinaendelea hapo ndipo Yesu anamwekea mikono yake, na kumponya..Lakini utajiuliza tena, ni kwanini biblia inatuaeleza aliponywa mara ya kwanza na ya pili?..Ni kwasababu kuna jambo Yesu alitaka tujue kuhusu upofu wa Yule mtu..Ukiyatafakari vizuri maneno yake utagundua kuwa mtu Yule hakuwa kipofu tangu alipozaliwa, bali aliupata upofu wake wakati Fulani katika maisha yake. Kwasababu kama angekuwa ni kipofu wa kuzaliwa asingesema naona watu kama miti inakwenda..Mtu aliyezaliwa kipofu hawezi kutofautisha mti na mtu.
Hivyo upofu wake hakuzaliwa nao, aliupata sehemu Fulani, na huko si kwingine zaidi ya kule kijijini alipokuwepo. Na ndio maana utaona Bwana Yesu alimpomaliza kumponya akamwambia..Hata kijijini usiingie.
Hichi ndicho kinachoendelea sasahivi rohoni, ulimwengu huu umewapofusha watu wengi rohoni, masumbufu ya ulimwengu huu, anasa, mambo ya kidunia, hawaoni tena kuwa hizi ni siku za mwisho, hawaoni tena kuwa unyakuo upo karibu, hawaoni tena kuwa dunia hii imeshaoza, haijalishi watasikia injili ngumu kiasi gani bado wataona ni kawaida tu..
2Wakorintho 4:3 “Lakini ikiwa injili yetu imesitirika, imesitirika kwa hao wanaopotea; 4 AMBAO NDANI YAO MUNGU WA DUNIA HII AMEPOFUSHA FIKIRA ZAO WASIOAMINI, isiwazukie nuru ya injili ya utukufu wake Kristo aliye sura yake Mungu”.
2Wakorintho 4:3 “Lakini ikiwa injili yetu imesitirika, imesitirika kwa hao wanaopotea;
4 AMBAO NDANI YAO MUNGU WA DUNIA HII AMEPOFUSHA FIKIRA ZAO WASIOAMINI, isiwazukie nuru ya injili ya utukufu wake Kristo aliye sura yake Mungu”.
Lakini kama tunavyosoma hapo, mtu akitaka Yesu amfumbue macho, hakuna njia ya mkato vigezo ni sharti Yesu akuchukue nje ya kijiji..Ni lazima kwanza katika upofu wako ukubali Yesu akutoe katika ulimwengu, ni sharti ukubali kujitenga na anasa, lazima ukubali kuacha fashion na kuvaa mavazi ya kikahaba, ni lazima ukubali kuachana na marafiki wabaya, na mambo yote yasiyompendeza Mungu, yaani kwa ufupi ukubali kuipoteza nafsi yako kwenye mambo ya kidunia, na hapo ndipo Bwana YESU atakapokufumbua macho yako, na kuona mambo yote ya rohoni WAZI WAZI,
Kumwona shetani jinsi anavyofanya kazi katikati ya watu wa ulimwengu huu, kuona jinsi unyakuo ulivyo karibu, kuona jinsi ulivyokuwa hatarini kuelekea kuzimu.. Hapo ndipo utajijua kweli ulikuwa kipofu, lakini sasa hivi upo kwenye ulimwengu huwezi kujiona kwasababu tayari umepofushwa macho.
Ndugu pengine hii ni mara yako ya elfu kulisikia hili Neno kuwa hizi ni siku za mwisho, Hata kama Unyakuo hautakukuta, basi ujue hata siku zako za kuishi hapa duniani si nyingi, hujui kesho utaamkia wapi? Wanaokufa na kushuka kuzimu idadi yao haihesabiki, ukifa leo katika upofu ulio nao, hakuna tumaini tena la uzima baada ya hapo.
Kama wewe ni mkristo na unajua kuwa hili ndio kanisa la mwisho la 7 lijulikanalo kama Laodikia (Ufu.3:14) na kwamba hakutakuwa na kanisa lingine baada ya hili (Ufu.10:7), halafu bado huyathamini maisha yako ya rohoni, hiyo ni dalili kubwa kuwa umepofushwa macho na ulimwengu huu.
Huu ni wakati ambao tayari magugu na ngano vimeshajitenga, wale walio hapo katikati (yaani vuguvugu), upande wao ni wa shetani, kwasababu Bwana Yesu alishasema atawatapika..Ni heri utemwe, kuliko kutapikwa, matapishi hata kuyaangalia huwezi, sembuse kuliwa tena?.Usisibiri utapikwe, Tubu mtafute Bwana Yesu hichi kipindi cha kumalizia.
Maran Atha.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
SABATO TATU NI NINI?
Wanaowachukua wanawake wajinga mateka ni akina nani?
VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 8 (Kitabu cha Ezekieli)
JE TATIZO LA KULA KUCHA NI ISHARA YA KUWA NA MAPEPO?
MAMBO YATAKAYOTOKEA ISRAELI SIKU ZA HIVI KARIBUNI.
Rudi Nyumbani:
Print this post
Je udhaifu au ulemavu wangu unaweza kuzuia watu kumwamini Yesu?
Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze biblia.
Lipo swali moja muhimu sana linaloulizwa na wengi?..Je kama mimi nina tatizo fulani labla la kuona, au kusikia, au nina ulemavu fulani ambao unaonekana kabisa…Je hali kama hiyo nikienda kuhubiri/kushuhudia watu wataokoka kweli?..Si wataniuliza mbona huyo Mungu hajakuponya wewe kwanza atawezaje kutuponya sisi?.
Hii ni mojawapo ya silaha ya shetani anayoitumia kuhakikisha injili haihubiriwi!…Na silaha nyingine anayoitumia ni sauti inayosema “umemkufuru Roho Mtakatifu”..ukisikia sauti yoyote unakuambia hayo maneno mawili kwamba “huwezi kuhubiri kutokana na udhaifu wako” au “umeshamkufuru Roho Mtakatifu”.. Basi jua moja kwa moja hizo ni sauti za Adui shetani, hivyo zipuuzie!.
Sasa kabla ya kuendelea mbele ni vizuri tukafahamu mambo machache yafuatayo.
Kwanza Aliyepewa jukumu la kuhubiria wanadamu injili, ni Mwanadamu huyo huyo na si malaika. Hakuna mahali popote Mungu amewahi kumtuma malaika akahubiri injili. Na hakuna mwanadamu aliyeumbwa na Mungu asiye na kasoro kabisa!..Hata yule mhubiri maarufu na mashuhuri unayemfahamu na kumsikia anayo mapungufu yasiyohesabika. Kwahiyo Mungu anajua kabisa wanadamu wote wanayo mapungufu lakini akawapa hivyo hivyo jukumu la kubeba maneno yake na kuwasambazia wengine wasiyo nayo. Hivyo angekuwa anaangalia udhaifu kama ndio kigezo cha mtu kwenda kulihubiri neno lake, hakuna mwanadamu angestahili kuwa mhubiri…pengine Mungu angewatumia malaika wake walio watakatifu huko mbinguni na wala si wanadamu.
Kwahiyo kumbe kasoro zetu hazihusiani na sisi kukidhi vigezo vya kuhubiri Neno la Mungu!..maana yake ni kwamba uwe mrefu, uwe mfupi, uwe unajua kuongea au hujui kuongea vizuri, uwe na kigugumizi, uwe mzungu, uwe mwafrika, uwe albino, uwe kiziwi, uwe kipofu, uwe huna miguu, uwe huna mikono, uwe maskini, uwe tajiri, uwe hujui kusoma, uwe mtu mdogo kabisa katika jamii, uwe mtu mkubwa.. uwe yoyote yule uwazaye kuwa, maadamu unaitwa MWANADAMU!. Basi umeshafuzu kuwa na uwezo wa kulibeba Neno la Mungu na kuwapelekea wengine.
Kigezo cha kwanza cha wewe kuweza kuwapelekea wengine NENO la Mungu ni wewe kwanza uwe na hilo Neno la Mungu ndani yako. Hicho ndio kigezo cha kwanza na cha Muhimu, kwasababu hata katika hali ya kawaida, hakuna mwalimu anaweza kumfundisha mwanafunzi maarifa ambayo yeye mwenyewe hana!. Hivyo ni lazima Neno la Kristo likae ndani yako, na hiyo inakuja kwa kumpokea Mwokozi Yesu Kristo na kulisoma Neno lake na KULIISHI HILO NENO!.
Baada ya hapo! Unaweza kuhubiri Injili kwa mtu yeyote yule.. Usisubiri Uone maono, au utokewe na Yesu au Malaika.. Wengi wanaisubiri hii hatua na hawaifikii..Wanatamani wasikie sauti KWANZA ikiwaambia nenda kahubiri!.. “Ndugu usiisubirie hiyo sauti “ hutakaa uisikie milele..Ni kwanini hutakaa uisikie?..Ni kwasababu tayari alishasema katika neno lake… “ENENDENI MKAWAFANYE MATAIFA YOTE KUWA WANAFUNZI..(Mathayo 28:28)”. Usisubiri sauti nyingine..hutaisikia!!
Sasa Swali lingine…Ni nini kinachomgeuza Mtu kama sio Ukamilifu wetu wa kuongea na kusikia vizuri?
Tusome mstari ufuatao kisha tutajua..
Waebrania 4:12 “Maana Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili, tena lachoma hata kuzigawanya nafsi na roho, na viungo na mafuta yaliyomo ndani yake; tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo. 13 Wala hakuna kiumbe kisichokuwa wazi mbele zake, lakini vitu vyote vi utupu na kufunuliwa machoni pake yeye aliye na mambo yetu”
Waebrania 4:12 “Maana Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili, tena lachoma hata kuzigawanya nafsi na roho, na viungo na mafuta yaliyomo ndani yake; tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo.
13 Wala hakuna kiumbe kisichokuwa wazi mbele zake, lakini vitu vyote vi utupu na kufunuliwa machoni pake yeye aliye na mambo yetu”
Hapo anasema “NENO LA MUNGU” Sio maneno yaliyopangiliwa vizuri, wala sio midomo yetu inayoweza kuumba maneno mwanana, wala sio rangi za nyuso zetu, wala sio masikio yetu yanayosikia vizuri maneno tunayoulizwa na wale tunaowahubiria, wala macho yetu yanayotazama vyema watu tunaowahubiria wala ufupi wetu, wala urefu wetu, wala elimu yetu…Bali NENO LA MUNGU!..Hilo ndio lenye nguvu…linapotajwa na mwanadamu yeyote ambaye kalishika…basi linapenya mpaka ndani ya ule moyo wa anayelisikia..linamchana chana na kumgawanya moyo wake…linapenya na kumfunulia yule anayelisikia mambo yake ya siri anayoyafanya atoke katika hali yake ya kawaida. Wakati wewe unafikiri anasikiliza kigugumizi chako, au anazitafakari kasoro zako… kumbe mwenzio Roho Mtakatifu anateta naye huko, anaugulia ndani kwa ndani..
2Wakoritho 10:4 “(maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;) 5 tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; na tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo”
2Wakoritho 10:4 “(maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;)
5 tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; na tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo”
Kwahiyo usikubali kusikiliza uongo wa shetani ambao unakukatisha tamaa kwenda kuhubiri injili..Kama husikii vizuri, wewe hubiri hivyo hivyo, yule unayemhubiria akikuuliza swali sogea karibu msikilize tena na tena, ukiona bado humsikiI, wewe endelea mbele..usianze kuutafakari udhaifu wako…kwasababu hata yeye wakati huo atakuwa hautafakari udhaifu wako!… na pia hatakuchukia ila lile Neno utakalomwambia hata kama ni moja tayari ni Nguvu ya Mungu..na ni mbegu..
Tatizo kubwa la wengi ni kufikiri kwamba Injili ni maneno mengi… jambo ambalo sio kweli!…Mtu anayehubiri maneno mengi basi ni kaongozwa na Roho kufanya hivyo…Lakini Neno moja tu la MUNGU!..Linatosha kubadilisha moyo mgumu wa jiwe na kuwa mlaini.. Kwa neno moja tu la Mungu na iwe Nuru!..ndio iliumba jua hili ambalo mpaka leo tunalo vizazi na vizazi.. Hivyo usitafute sana ujuzi wala utaalamu katika kwenda kulitangaza Neno la Mungu…Wewe Tafuta Roho Mtakatifu. Kisha itumie karama yako Mungu aliyokupa.
Mwanamke mmoja mashuhuri anayeitwa Fanny Crosby alizaliwa akiwa mzima lakini baada ya wiki mbili akawa kipofu, aliishi duniani katika hali hiyo hiyo ya upofu kwa muda wa miaka 95, lakini hakuacha kutafuta mahali ambapo angemtumikia Mungu licha ya kuwa alikuwa kipofu, alifanikiwa kuandika nyimbo zaidi ya 8,000, katika kipindi hicho cha karne ya 19, akajulikana kwa jina la malkia wa nyimbo za injili, na mwimbaji kipofu, moja ya tenzi mbili muhimu ambazo mpaka leo hii unazijua na kuziimba “Usinipite Mwokozi” na “Ndio dhamana Yesu wangu” pengine ulikuwa hujui ziliimbwa na huyu mama kipofu, na kwa kupitia uimbaji wake, na kuwahubiria wengine alifanikiwa kuwavuta watu wengi kwa Kristo.
Hivyo na sisi, kila mmoja wetu amesimame na kile Mungu alichokiweka ndani yake kuhakikisha injili inawafikia wengi.
Bwana akubariki.
www wingulamshahidi org
USINIPITE MWOKOZI Lyrics
REKEBISHA YAFUATAYO ILI MAMBO YAENDE SAWA.
MAPAMBANO DHIDI YA SHETANI.
Mti wa MLOZI alioonyeshwa nabii Yeremia 1:12 tafsiri yake ni nini?
Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!
WALIPO WAWILI AU WATATU KWA JINA LANGU
Mto Frati upo nchi gani, na Umuhimu wake katika biblia ni upi, kwanini utajwe sana?
Mto Frati ni moja ya mito mikubwa na mirefu iliyopo Mashariki ya kati, Mto mwingine ukiwa ni Hidekeli (Tigris), mto huu unaanzia Uturuki na kutoka hapo unakatiza katika nchi ya Syria na Iraq na kwenda kumwaga maji yake katika Ghuba ya uajemi.
Tazama picha.
Mto Frati na Mto Hidekeli (Tigris) ni moja ya mito minne ambayo inatajawa kwenye biblia ilikuwa inatoa maji katika bustani ya Edeni.
Mwanzo 2:10 “Ukatoka mto katika Edeni wa kuitilia bustani maji, na kutokea hapo ukagawanyika kuwa vichwa vinne. 11 Jina la wa kwanza ni Pishoni; ndio unaozunguka nchi yote ya Havila, ambako kuna dhahabu; 12 na dhahabu ya nchi ile ni njema; huko kuna bedola, na vito shoham. 13 Na jina la mto wa pili ni Gihoni; ndio unaozunguka nchi yote ya Kushi. 14 Na jina la mto wa tatu ni Hidekeli; ndio unaopita mbele ya Ashuru. Na mto wa nne ni Frati”.
Mwanzo 2:10 “Ukatoka mto katika Edeni wa kuitilia bustani maji, na kutokea hapo ukagawanyika kuwa vichwa vinne.
11 Jina la wa kwanza ni Pishoni; ndio unaozunguka nchi yote ya Havila, ambako kuna dhahabu;
12 na dhahabu ya nchi ile ni njema; huko kuna bedola, na vito shoham. 13 Na jina la mto wa pili ni Gihoni; ndio unaozunguka nchi yote ya Kushi.
14 Na jina la mto wa tatu ni Hidekeli; ndio unaopita mbele ya Ashuru. Na mto wa nne ni Frati”.
Lakini kingine cha kushangaza juu ya mto Frati ni kuwa umetajwa pia kitabu cha Ufunuo, Kama tu vile Babeli ilivyotajwa tangu kwenye kitabu cha Mwanzo hadi Ufunuo. Kuonyesha kuwa kama vile ilivyo Babeli ya mwilini, hivyo hivyo pia ipo Babeli ya rohoni (Ufunuo 17 & 18). Halikadhalika na kwa mto Frati, sio tu ule unaouna pale Mashariki ya kati, hapana bali pia rohoni upo, na siku moja utakauka, na ukishakauka basi dunia itaingia katika vita kuu ya Tatu ya dunia
Ufunuo 9:14 ikimwambia yule malaika wa sita aliyekuwa na baragumu, Wafungue nao malaika wanne waliofungwa kwenye mto mkubwa Frati. 15 Wale malaika wanne wakafunguliwa, waliokuwa wamewekwa tayari kwa ile saa na siku na mwezi na mwaka, ili kwamba waue theluthi ya wanadamu. 16 Na hesabu ya majeshi ya wapanda farasi ilikuwa elfu ishirini mara elfu kumi; nilisikia hesabu yao. 17 Hiyo ndivyo nilivyowaona hao farasi katika maono yangu, nao waliokaa juu yao, wana dirii kifuani, kama za moto, na za samawi, na za kiberiti; na vichwa vya farasi hao ni kama vichwa vya simba, na katika vinywa vyao hutoka moto na moshi na kiberiti. 18 Theluthi ya wanadamu wakauawa kwa mapigo matatu hayo, kwa moto huo na moshi huo na kiberiti hicho, yaliyotoka katika vinywa vyao. 19 Kwa maana nguvu za hao farasi ni katika vinywa vyao, na katika mikia yao; maana mikia yao ni mfano wa nyoka, ina vichwa, nao wanadhuru kwa hivyo”.
Ufunuo 9:14 ikimwambia yule malaika wa sita aliyekuwa na baragumu, Wafungue nao malaika wanne waliofungwa kwenye mto mkubwa Frati.
15 Wale malaika wanne wakafunguliwa, waliokuwa wamewekwa tayari kwa ile saa na siku na mwezi na mwaka, ili kwamba waue theluthi ya wanadamu.
16 Na hesabu ya majeshi ya wapanda farasi ilikuwa elfu ishirini mara elfu kumi; nilisikia hesabu yao.
17 Hiyo ndivyo nilivyowaona hao farasi katika maono yangu, nao waliokaa juu yao, wana dirii kifuani, kama za moto, na za samawi, na za kiberiti; na vichwa vya farasi hao ni kama vichwa vya simba, na katika vinywa vyao hutoka moto na moshi na kiberiti.
18 Theluthi ya wanadamu wakauawa kwa mapigo matatu hayo, kwa moto huo na moshi huo na kiberiti hicho, yaliyotoka katika vinywa vyao.
19 Kwa maana nguvu za hao farasi ni katika vinywa vyao, na katika mikia yao; maana mikia yao ni mfano wa nyoka, ina vichwa, nao wanadhuru kwa hivyo”.
Unaona?. Watu wengi hawajui kuwa kipindi hicho kimekaribia sana,. Lakini kabla hilo halijatokea, kutatungulia kwanza Tukio la UNYAKUO, (kufahamu vizuri unyakuo utakuwaje kuwaje, tazama, masomo yaliyoorodheshwa chini).
Dalili zote zinaonyesha kizazi chetu kitaweza kushuhudia mambo hayo yote. Swali la kujiuliza Je! na wewe umejiwake tayari kwa tukio la kurudi kwa pili kwa Yesu Kristo? Je! Maisha yako yanauhakisi wokovu? Kama sivyo basi jitathimini sasa kwasababu ni kipindi kifupi cha neema tulichobakiwa nacho, Dunia hii inapumbaza kweli na wengi hawalijui hilo, Yesu atakuja kama mwivi usiku.
Hivyo kama upo tayari kumpa Yesu leo maisha yako, hilo jambo la muhimu sana, basi fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba.>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Ikiwa utapenda tuwe tunakutumia masomo ya Neno la Mungu kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Tazama chini vichwa vingine vya masomo.
MTO YORDANI UKO NCHI GANI KWA SASA?
UFUNUO: Mlango wa 9.
SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?
MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.
MAONO YA NABII AMOSI.
CHUKIZO LA UHARIBIFU
Mto Yordani uko nchi gani kwa sasa duniani?
Mto Yordani upo katika eneo la Mashariki ya kati, ni mto ambao unasimama kama mpaka wa mataifa mbalimbali, Ikiwemo Lebanoni, Syria, Israeli, na Yordani.
Ni kama vile ziwa Tanganyika lilivyo simama kama mpaka wa nchi 4, Congo, Burundi, Tanzania, na Zambia ndivyo ilivyo hata na kwa mto Yordani,
Nchi ya Yordani, unayoisikia leo hii pale mashariki ya kati, imechukua jina lake kutoka katika mto huu.
Mto huu chanzo chake ni kwenye chemchemi kadhaa zinazotiririka kutoka katika mlima Hermoni ulio mpakani mwa Lebanoni na Syria.Kisha kutoka hapo unateremsha maji yake mpaka Israeli kwenye bahari ya Galilaya/Tiberia/Genesareti. Na kutoka hapo unaibukia upande wa pili na kuendelea na safari yake moja kwa moja mpaka bahari ya Chumvi.
Tazama picha chini.
Mto huu, umekuwa kitovu katika historia ya Israeli kuanzia agano la kale mpaka agano jipya. Yoshua aliusimamisha mto huu na wana wa Israeli wakavuka kuelekea Yeriko.
Vilevile mto huu huu katika agano jipya ndio makutano mengi yalikuwa yanavuka kumwendea Yesu ili waponywe.(Mathayo 19:1-2), Na ni mto ambao Yesu mwenyewe alibatiziwa.
Kuonyesha kuwa ili nawe upate wokovu na ushindi dhidi ya maadui zako,na ili uponywe nafsi yako, ni lazima Uvuke Yordani yako ya Rohoni..Ili ukakutane na Yesu ng’ambo ya pili huna budi kuvuka Yordani, Na Unavukaje Yordani? Ni kwa kubatizwa, kama Yesu alivyobatizwa kwenye mto ule.
Hivyo na wewe sharti ukishamwamini Yesu moja kwa moja ukabatizwe, mahali popote penye maji tele kama ishara ya kuwa umeokoka kweli kweli. Na kuwa unakwenda kuwashinda maadui zako.
Marko 16:16 “Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa”.
Wengi wanapuuzia maagizo haya ya msingi, wanadhani kuamini tu inatosha, Ndugu kubatizwa ni tendo lenye maana kubwa sana kwako rohoni, aliyetupa maagizo hayo hakuwa amekosa cha kutuagiza bali alijua umuhimu wake.
Swali Nji wewe umebatizwa ipasavyo? Kama sivyo basi kafanye hivyo.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda masomo yetu yawe yanakufikia njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Israeli ipo bara gani?
Wafilisti ni watu gani.
MJUMBE WA AGANO.
Zile mbao mbili za mawe Musa alizoambiwa achonge zilikuwaje?
Mlima sinai upo nchi gani? Na Je unaijua Sinai yako ya rohoni?
MKUMBUKE MKE WA LUTU.
UNYAKUO.
SWALI: Neno “Korbani” linalozungumziwa katika Marko 7:11 lina maana gani?
JIBU: Ili tupate picha nzuri ya Neno hilo embu tusome sehemu zote mbili zinazozungumzia jambo hilo hilo moja.
Mathayo 15 :1-6
1 “Ndipo Mafarisayo na waandishi toka Yerusalemu walipomwendea Yesu wakisema, 2 Mbona wanafunzi wako huyahalifu mapokeo ya wazee, kwa maana hawanawi mikono walapo chakula. 3 Akajibu, akawaambia, Mbona ninyi nanyi huihalifu amri ya Mungu kwa ajili ya mapokeo yenu? 4 Kwa kuwa Mungu alisema, Mheshimu baba yako na mama yako, na Amtukanaye baba yake au mama yake kufa na afe. 5 Bali ninyi husema, Atakayemwambia babaye au mamaye, Cho chote kikupasacho kusaidiwa na mimi ni wakfu, 6 basi asimheshimu baba yake au mama yake. Mkalitangua neno la Mungu kwa ajili ya mapokeo yenu”.
1 “Ndipo Mafarisayo na waandishi toka Yerusalemu walipomwendea Yesu wakisema,
2 Mbona wanafunzi wako huyahalifu mapokeo ya wazee, kwa maana hawanawi mikono walapo chakula.
3 Akajibu, akawaambia, Mbona ninyi nanyi huihalifu amri ya Mungu kwa ajili ya mapokeo yenu?
4 Kwa kuwa Mungu alisema, Mheshimu baba yako na mama yako, na Amtukanaye baba yake au mama yake kufa na afe.
5 Bali ninyi husema, Atakayemwambia babaye au mamaye, Cho chote kikupasacho kusaidiwa na mimi ni wakfu,
6 basi asimheshimu baba yake au mama yake. Mkalitangua neno la Mungu kwa ajili ya mapokeo yenu”.
Marko 7:8-13
“8 Ninyi mwaiacha amri ya Mungu, na kuyashika mapokeo ya wanadamu. 9 Akawaambia, Vema! Mwaikataa amri ya Mungu mpate kuyashika mapokeo yenu. 10 Maana Musa alisema, Waheshimu baba yako na mama yako, na, Amtukanaye babaye au mamaye kufa na afe. 11 Bali ninyi husema, Mtu akimwambia babaye au mamaye, NI KORBANI, yaani, wakfu, kitu changu cho chote kikupasacho kufaidiwa nacho, huwa basi; 12 wala hammruhusu baada ya hayo kumtendea neno babaye au mamaye; 13 huku mkilitangua neno la Mungu kwa mapokeo yenu mliyopokeana; tena mwafanya mambo mengi yaliyo sawasawa na hayo.
“8 Ninyi mwaiacha amri ya Mungu, na kuyashika mapokeo ya wanadamu.
9 Akawaambia, Vema! Mwaikataa amri ya Mungu mpate kuyashika mapokeo yenu.
10 Maana Musa alisema, Waheshimu baba yako na mama yako, na, Amtukanaye babaye au mamaye kufa na afe.
11 Bali ninyi husema, Mtu akimwambia babaye au mamaye, NI KORBANI, yaani, wakfu, kitu changu cho chote kikupasacho kufaidiwa nacho, huwa basi;
12 wala hammruhusu baada ya hayo kumtendea neno babaye au mamaye;
13 huku mkilitangua neno la Mungu kwa mapokeo yenu mliyopokeana; tena mwafanya mambo mengi yaliyo sawasawa na hayo.
Kama tunavyosoma hapo, biblia imeshatoa tafsiri ya hilo Neno Korbani mbele kidogo kuwa linaamanisha WAKFU.
Kitu chochote kilichowekwa wakfu ina maana kuwa hakitumiwi kwa mtumizi mengine yoyote isipokuwa kwa Mungu tu. Sasa katika habari hiyo, utaona Bwana Yesu alikuwa anawelenga sana sana Mafarisayo na waandishi kwa unafki wao kwa kujifanya kuwa wanaishika torati yote, wakati yapo mambo mengine mengi ya torati walikuwa wanayakaidi.
Na ndio hapo Bwana Yesu akawatolea mfano mmojawapo, ambao ulihusu kuwaheshimu wazazi, kama mojawapo ya amri ambazo Mungu alizitoa zishikwe na watu wote. Na biblia iliposema kuwaheshimu wazazi, ilikuwa sio tu kuwaonyeshea heshima na utiifu, hapana ilikuwa ni zaidi ya hapo ikiwemo kuwahudumia kifedha, hususani wakiwa wazee.
Sasa hawa waandishi walikuwa wanayapindisha hayo maagizo, kwa kuwashurutisha watu, kuepuka majukumu yao ya kuwahudumia wazazi wao, kinyume chake walikuwa wanawaambia hayo wanayoyapata kwa ajili ya wazazi wanaweza tu kuyafanya kuwa wakfu(Korbani) mbele za Mungu, na ikawa ni sawa tu na kama wamewahudumia wazazi wao, isiwe dhambi mbele za Mungu.
Hivyo kama mtu alikuwa ametenga fedha yake kiasi kwa ajili ya matumizi ya baba yake au mama yake kule kijijini, basi walihimiziwa walizete Hekaluni kwa ajili ya Mungu kama wakfu..
Na mzazi akimuuliza, mbona huniletei matumizi, basi Yule kijana atasema, fedha hii au nafaka hii niliyoivuna ni wakfu kwa Mungu.
Hivyo watu wengi wakawa wanawaacha wazazi wao katika hali ya shida na umaskini wa hali ya juu. Jambo ambalo Mungu hakuliagiza.
Ndipo Yesu anawakemea hawa waandishi kwa kuyapindua maagizo ya Mungu, ya kutotimiza majukumu yao ya kuwahudumia wazazi kwa kanuni zao walizojitungia.
Nini tunajifunza?
Kumbuka biblia haifundishi watu wakimbie majukumu yao ya kifamilia kwa wazazi wao hususani pale wanapokuwa wazee kwa kisingizio kuwa wanamtolea Mungu.. Biblia inasema usipowahudumia watu wa nyumbani kwako, wewe ni kuliko hata mtu asiyeamini(1Timotheo 5:8).. Lakini pia biblia haifundishi kuwa watu waache kumtolea Mungu kwa kisingizio kuwa wanayo majukumu mengi ya kifamilia.
Lazima ujue kila utoaji una sehemu yake, na Baraka zake. Watu wa nyumbani kwako wana sehemu yao, maskini wana sehemu yao, na Mungu pia anayosehemu yake..Usipojua hilo utakuwa nawe pia unatangua torati kwa kufuata mawazo yako mwenyewe uliyojitungia. Kwasababu wapo watu wengi leo hii, wameacha kupeleka fedha zao kanisani, au kwenye huduma za Mungu, wanasema sitoi sadaka yangu, na ukiwauliza ni kwanini?, wanasema mbona hatuoni zikienda kuwahudumia maskini na wajane kama ilivyokuwa katika kanisa la kwanza la mitume…Lakini mtu huyo huyo hajui kuwa watakatifu wa kanisa la kwanza sio kama hawa wa sasahivi, wale walikuwa wapo tayari kuuza mashamba yao na viwanja vyao na kuleta kwa Mungu, hivyo kwa namna ya kawaida nishati ya kutosha ni lazima iwepo nyumbani kwa Mungu hata kuwahudumia mpaka wajane.
Lakini kama wewe unampelekea Mungu shilingi, wakati hiyo fedha hata gharama za umeme kanisani hazijitoshelezi, unapata wapi ujasiri wa kutaka kujua mfuko wa kanisa unatumikaje?? Fikiria tu. Je wewe unaweza kuuza shamba lako kule kijijini, umletee Mungu?
Bwana atusaidie,.
Je! Mwanamke anapaswa afunikwe kichwa anapokuwa ibadani?
WANA JUHUDI KWA AJILI YA MUNGU, LAKINI SI KATIKA MAARIFA.
MIJI YA MAKIMBILIO.
JE KUVAA PETE NI DHAMBI?
MAJONZI YA MTUME PAULO KWA NDUGU ZAKE.
YOTE NAMTOLEA YESU_Tenzi za Rohoni.
Je kualikwa kwenye sherehe za watu ambao si wakristo ni dhambi?
Historia ya wimbo wa tenzi – Ndio dhamana Yesu wangu. (Blessed assuarance)
Wimbo huu ulindikwa na mwanamke mmoja aliyeitwa Fanny Crosby, Mwanamke huyu japo aliishi kwa miaka 95 akiwa kipofu,lakini hakuacha kuitumia neema Mungu aliyompa kutangaza injili kwa njia ya Nyimbo zenye muundo wa Tenzi za rohoni na nyinginezo, katika maisha yake alifanikiwa kuandika nyimbo zaidi ya 8000, Na hii nyimbo “Ndio dhamana Yesu wangu” Ikiwa mojawapo, Nyingine inayojulikana sana mpaka leo ni “Usinipite mwokozi” yeye pia ndio aliyeiandika nyimbo hii alipokuwa amewatembelea wafungwa gerezani(angalia historia yake chini).
Phoebe Knapp
Sasa Siku moja alipokuwa amemtembelea rafiki yake nyumbani kwake aliyeitwa Phoebe Knapp, ambaye alikuwa ni mtunzi wa sauti za nyimbo, wakiwa nyumbani kwake Phoebe alianza kupiga mdundo wake aliokuwa ameutunga, kisha baada ya muda alimuuliza Fanny, Je unaweza kuniambia mdundo huu ni wa nyimbo gani?
Ndipo Fanny akamwambia “Ndio dhamana Yesu wangu”. Basi hapo ndio pakawa mwanzo wa mdundo na utunzi wa wimbo huo (1873).
Ndio dhamana Yesu wangu.
*****
Uimbapo wimbo huu kumbuka ni kipofu ndiye aliyeuandika, nawe pia unaposema “Ndio dhamana Yesu wangu” Basi awe kweli wokovu wako. Mpende yeye bila unafki na kumtumikia kwasababu ndiye aliyekufa kwa ajili yako.
Je! Umeokoka? Unajua kuwa Unyakuo upo karibu sana, kwasababu tunaishi katika kanisa la mwisho lijulikanalo kama Laodikia? Na kwamba hatutakuwa na kanisa lingine zaidi ya hili? Siku hizi zimekwisha, Hivyo kama upo tayari kumpa Yesu maisha yako leo ili wimbo huu uwe na maana kweli kwako. Basi fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba >>>KUONGOZWA SALA YA TOBA
Ikiwa utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
BWANA MUNGU NASHANGAA KABISA lyrics
CHA KUTUMAINI SINA lyrics
KUMTEGEMEA MWOKOZI Lyrics/Swahili.
MPINGA-KRISTO
UFUNUO: Mlango wa 1
Yote namtolea Yesu_tenzi za rohoni|Swahili hymn.
Wimbo huu uliandikwa na ndugu mmoja wa kimarekani aliyeitwa Judson W. Van DeVenter, Ndugu huyu alilelewa katika mazingira ya kikristo, aliokoka akiwa na miaka 17, kuanzia huo wakati wito wa kujitoa kikamilifu ulianza kuita ndani yake,lakini bado hakufanya uamuzi huo. DeVenter alifanikiwa kusoma mpaka chuo kikuu na kutunikiwa shahaba ya Sanaa, aliajiriwa kama mwalimu na mwongozaji katika shule za sanaa, hiyo ilimfanya aweze kusafiri sehemu nyingi mbalimbali katika bara la Ulaya kutokana na kazi yake ya sanaa.
Zaidi ya hilo alisomea pia na kufundisha elimu ya muziki, ilimchukua miaka 5 mpaka “Kumtolea yote Yesu”, Na hiyo ilikuwa ni baada ya marafiki zake kumshawishi sana, aingie katika kazi ya kumtumikia Mungu.
Mwaka 1896 Siku moja alipokuwa anafanya huduma ya muziki katika kanisani, hii ndio siku aliyoamua kuyasalimisha maisha yake ya ki-utumishi moja kwa moja kwa Kristo akiwa na miaka 41, aliamua kujitoa moja kwa moja kwa ajili ya kuifanya kazi ya unjilisti, na ndipo hapo huu wimbo “Yote namtolea Yesu” ulipozaliwa ndani ya moyo wake.
YOTE WA YESU.
Je! Na sisi tunapouimba wimbo huu tunaweza kumtolea Yote Yesu?. Je! mali zetu tunaweza kumpa yeye, nguvu zetu tunaweza kuzielekeza kwake?, akili zetu tunaweza kuzitumia ziitende kazi ya Mungu? Kama sivyo basi wimbo huu tutauimba kinafki.
Bwana atutupe kutambua hayo.
Je! Umeokoka? Ikiwa bado hujaokoka na unahitaji kuokoka leo, basi fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya toba >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Ikiwa utapenda tuwe tunakutumia masomo mbalimbali ya Neno la Mungu, kwa njia ya whatsapp yako, basi tutumie ujumbe kwa namba hii :+255 789001312
YESU KWETU NI RAFIKI
NI SALAMA ROHONI MWANGU Lyrics
DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.
Kuwa mwaminifu kwa maneno yako mwenyewe, ni muhimu sana!.
Jina la Bwana wetu Yesu libarikiwe. Karibu tujifunze biblia.
Mwinjilisti mmoja alichukuliwa katika maono mbinguni akakutana na Bwana Yesu, alionyeshwa mambo mengi yatakayotokea baada ya Maisha haya, kwa wema na waovu, lakini Pamoja na hayo kuna mambo mengine aliambiwa ambayo naamini leo tukiyatafakari yatatusaidia.
Na jambo mojawapo aliloambiwa lilikuwa ni kuhusu “uaminifu”…kulingana na maelezo yake, anasema Bwana Yesu alimwambia haya maneno;
“Neno langu ni nguvu inayoshikilia vitu vyote. Kwa kiwango ambacho unavyoamini Neno langu ni kweli, ndivyo unavyoweza kufanya vitu vyote. Wale ambao wanaamini kwamba maneno Yangu ni kweli, basi watakuwa pia wakweli kwa maneno yao wenyewe, Ni asili yangu kuwa kweli, na uumbaji huliamini Neno Langu kwa sababu mimi ni mwaminifu na kwake. Wale ambao ni kama mimi, pia huwa ni wakweli kwa maneno yao wenyewe. Neno lao ni hakika, na ahadi zao ni za kuaminika. ‘ndio’ yao inamaanisha ‘NDIO!’ na ‘hapana’ yao inamaanisha ‘HAPANA!’. Ikiwa maneno yako mwenyewe sio kweli, ni lazima pia utaanza kutilia shaka maneno Yangu, kwa sababu udanganyifu uko moyoni mwako. Ikiwa wewe sio mwaminifu kwa maneno yako mwenyewe, ni kwa sababu bado hujanijua kabisa mimi ni nani, mimi ni mwaminifu kwa maneno yangu. Ili kuwa na imani, lazima uwe mwaminifu kwa maneno yako. Nimekuita utembee kwa imani kwa sababu mimi ni mwaminifu. Hiyo ni asili yangu”.
“Neno langu ni nguvu inayoshikilia vitu vyote. Kwa kiwango ambacho unavyoamini Neno langu ni kweli, ndivyo unavyoweza kufanya vitu vyote. Wale ambao wanaamini kwamba maneno Yangu ni kweli, basi watakuwa pia wakweli kwa maneno yao wenyewe, Ni asili yangu kuwa kweli, na uumbaji huliamini Neno Langu kwa sababu mimi ni mwaminifu na kwake.
Wale ambao ni kama mimi, pia huwa ni wakweli kwa maneno yao wenyewe. Neno lao ni hakika, na ahadi zao ni za kuaminika. ‘ndio’ yao inamaanisha ‘NDIO!’ na ‘hapana’ yao inamaanisha ‘HAPANA!’. Ikiwa maneno yako mwenyewe sio kweli, ni lazima pia utaanza kutilia shaka maneno Yangu, kwa sababu udanganyifu uko moyoni mwako. Ikiwa wewe sio mwaminifu kwa maneno yako mwenyewe, ni kwa sababu bado hujanijua kabisa mimi ni nani, mimi ni mwaminifu kwa maneno yangu. Ili kuwa na imani, lazima uwe mwaminifu kwa maneno yako. Nimekuita utembee kwa imani kwa sababu mimi ni mwaminifu. Hiyo ni asili yangu”.
**mwisho**
Ndugu moja ya tatizo kubwa linalowakabili wakristo wengi wa sasa, ni kukosa UAMINIFU. Na uaminifu unaanza kwa mtu kukosa uaminifu kwa mambo yake mwenyewe kwanza. Kwamfano mtu baada ya kumpa Yesu Maisha yake, akaahidi kwamba hatasengenya tena, hatatukana, hataiba, hatafanya hichi au kile anaahidi pia atamtumikia Mungu, au atakuwa mtu wa kumtolea Mungu sana n.k..lakini baada ya muda kupita anaanza kwenda kinyume na kile alichokisema au alichokipanga. Ndugu hiyo ni hatari sana.
Maneno hayo ya mwinjilisti huyo aliyoambiwa na Bwana, nayaamini asilimia mia kuwa ni kweli. Hata katika hali ya kawaida kama huwezi kuwa mwaminifu kwa mali yako mwenyewe ni Dhahiri kuwa haiwezekani kuwa mwaminifu kwa mali ya mwingine. Kama kiatu chako mwenyewe hukitunzi wala hukijali utakijali vipi kiatu cha mwingine aliyekuazima ukivae kwa muda tu!. Uaminifu wa mtu unaanza kwa kile alichonacho yeye mwenyewe, ndipo aweze kuwa mwaminifu kwa kitu cha mwingine.
Kadhalika huwezi kuwa mwaminifu kwa Maneno ya Mungu, kama sio mwaminifu kwa maneno yako mwenyewe.
Katika Luka 16:10 Bwana Yesu alisema maneno haya..
“Aliye mwaminifu katika lililo dogo sana, huwa mwaminifu katika lililo kubwa pia; na aliye dhalimu katika lililo dogo, huwa dhalimu katika lililo kubwa pia”.
Hivyo tujifunze kuyashika maneno yetu wenyewe..Ndipo tutakapoona Neno la Mungu likiwa na nguvu juu ya maisha yetu… Ukisema sitaki hichi au kile!, au nataka hichi!..basi kishikilie hicho kweli kweli usiwe na mawazo mawili mawili… Hiyo nguvu ya Maamuzi ndio chanzo cha nguvu zako za kiroho. Hata likitokea jambo mbele yako, na ukanukuu mstari Fulani kwenye biblia kwa Imani, basi jambo lile ulilolitamka kufuatia mstari huo uliounukuu, litatimia kama ulivyolisema kwasababu wewe pia huwa ni mkweli katika maneno yako…Hivyo Mungu atahakikisha na yeye analifanya neno lake kuwa kweli juu yako. Lakini tusipokuwa wakweli kwenye maneno yetu, basi kuna uwezekano pia neno la Mungu lisiwe kweli juu yetu. Tunaweza tukalinukuu sana na tusiona matokeo yoyote.. kwasababu sisi wenyewe sio waaminifu.
Bwana atusaidie, na atubariki.
Maran atha!
Je! Ni ipi tarehe sahihi Evil-merodaki alimtoa Yekonia gerezani?
ZABURI 91, NI ZABURI YENYE NGUVU NYINGI.
Je! Mtume Paulo alikuwa ni Mrumi, Myahudi au raia wa Tarso?
JE! PAKA KULIA USIKU NI ISHARA YA UCHAWI?
NA UPEPO WA KUSI ULIPOANZA KUVUMA KIDOGO,
Hakuna mtu anenaye katika Roho,kusema Yesu amelaaniwa
Kwanini Amelaaniwa aangikwaye msalabani?
Kutundikwa msalaba au kwa jina lingine kutundikwa mtini, ilikuwa ni adhabu iliyotekelezwa kwa watu wenye makosa ya hali ya juu sana.
Adhabu hii ilikuwa sio tu ilikuwa inatekelezwa na watu wa mataifa mengine kama wengi wanavyodhani ni Warumi tu, hapana bali pia ilikuwa inatekelezwa na Israeli pia.
Ni adhabu yenye mateso mengi sana, na vilevile ni adhabu ya aibu. Waliokuwa wanatundikwa msabani walikuwa sana sana ni wauaji. Makosa ambayo yalikuwa yanathibitisha kuwa wamelaaniwa na Mungu.
Kumbukumbu 21:22 “Akiwa mtu ametenda dhambi ipasayo kufa, akauawa, nawe ukamtundika juu ya mti; 23 mzoga wake usikae usiku kucha juu ya mti; lazima utamzika siku iyo hiyo; kwani aliyetundikwa amelaaniwa na Mungu; usije ukatia unajisi katika nchi yako akupayo Bwana, Mungu wako, iwe urithi wako”.
Kumbukumbu 21:22 “Akiwa mtu ametenda dhambi ipasayo kufa, akauawa, nawe ukamtundika juu ya mti;
23 mzoga wake usikae usiku kucha juu ya mti; lazima utamzika siku iyo hiyo; kwani aliyetundikwa amelaaniwa na Mungu; usije ukatia unajisi katika nchi yako akupayo Bwana, Mungu wako, iwe urithi wako”.
Utasoma sehemu nyingi, katika biblia mifano ya watu waliangikwa msalabani. (Mwanzo 40:18-19, Esta 2:22-23, Esta 7:10)
Jambo hilo hilo tunaliona mpaka katika kipindi cha karibu na agano jipya, katika ule ufalme wa Rumi, wafungwa wote waliokuwa na kesi kubwa za mauaji au wizi, n.k. Adhabu yao ilikuwa ni kuangikwa/kutundikwa msalabani ukiwa hai.
Lakini cha ajabu ni kwamba, adhabu zilizokuwa zinawahusu watu waliolaaniwa, zilimkuta mtu ambaye hakuwahi kutenda dhambi hata moja..Na huyo si mwingine zaidi ya YESU KRISTO
Wagalatia 3:13 “Kristo alitukomboa katika laana ya torati, kwa kuwa alifanywa laana kwa ajili yetu; maana imeandikwa, AMELAANIWA KILA MTU AANGIKWAYE JUU YA MTI; 14 ili kwamba baraka ya Ibrahimu iwafikilie Mataifa katika Yesu Kristo, tupate kupokea ahadi ya Roho kwa njia ya imani”.
Wagalatia 3:13 “Kristo alitukomboa katika laana ya torati, kwa kuwa alifanywa laana kwa ajili yetu; maana imeandikwa, AMELAANIWA KILA MTU AANGIKWAYE JUU YA MTI;
14 ili kwamba baraka ya Ibrahimu iwafikilie Mataifa katika Yesu Kristo, tupate kupokea ahadi ya Roho kwa njia ya imani”.
Lakini ni kwanini yamkute hayo yote?
Je ni ilikuwa ni bahati mbaya tu? Au Mungu alishindwa kumzuia? Jibu ni la, ilitokea vile kwa makusudi kabisa, ili ile hati ya mashitaka ya waliolaaniwa ifutwe juu yetu, aliibeba yeye ile hati ya laana, na ndio maana pale ambapo Baraba muuaji alipopaswa auawe, Yesu aliuawa badala yake, pale ambapo wewe mzinzi ungepaswa uhukumiwe milele kwa makosa yako, Yesu aliichukua laana hiyo siku ile msalabani, pale ambapo wewe uliye na dhambi ambazo nyingine ni aibu kuzitaja, Yesu alizichukua, hatia zote kwako.
Lakini hizo haziwezi kufutika juu yako, hivi hivi tu, bali ni mpaka uende kuzisalimisha msalabani.
Na ndio maana unahitaji kumpokea Yesu maishani mwako, vinginevyo hati ya mashitaka ya dhambi zako zitaendelea kubakia juu yako hadi siku ya mwisho, na utahukumiwa kama mkosaji.
Lakini ikiwa leo upo tayari kumpokea Yesu maishani mwako, basi leo leo atazifuta dhambi zako bure kabisa, haijalishi wewe ni mwenye dhambi kiasi gani.
Isaya 53:4 “Hakika ameyachukua masikitiko yetu, Amejitwika huzuni zetu; Lakini tulimdhania ya kuwa amepigwa, Amepigwa na Mungu, na kuteswa. 5 Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona”.
Isaya 53:4 “Hakika ameyachukua masikitiko yetu, Amejitwika huzuni zetu; Lakini tulimdhania ya kuwa amepigwa, Amepigwa na Mungu, na kuteswa.
5 Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona”.
Hivyo kama upo tayari leo kumpa Yesu maisha yako, basi uamuzi huo ni wa busara, hivyo fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba >>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Tafadhali Share na wengine, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au katika namba hii hii +255 789001312
KWANINI YESU KRISTO NI WA MUHIMU KWETU SASA?
Nifanye nini ili niwe na uhakika nikifa naenda mbinguni?
MASOMO MBALIMBALI YA NENO LA MUNGU.
UTASIMAMA PEKE YAKO SIKU ILE.
Je! Watoto wa Ibrahimu/Wana wa Ibrahimu walikuwa ni wangapi?
Jumla ya wana wa Ibrahimu walikuwa ni nane (8). Kulingana na Biblia.
Mwana wa kwanza alikuwa ni Ishmaeli, ambaye alizaliwa na kijazi wa mke wake Sara aliyeitwa Hajiri (Mwanzo 16:1-4).
Mwana wa Pili, alikuwa ni Isaka,(Ndiye mwana wa Ahadi) ambaye alizaliwa miaka 14 baada ya Ishmaeli kuzaliwa.
Mwanzo 21:1 “Bwana akamjia Sara kama alivyonena, na Bwana akamfanyia kama alivyosema. 2 Sara akapata mimba akamzalia Ibrahimu mwana wa kiume katika uzee wake, kwa muhula alioambiwa na Mungu. 3 Ibrahimu akamwita jina lake Isaka, yule mwana aliyezaliwa, ambaye Sara alimzalia”.
Mwanzo 21:1 “Bwana akamjia Sara kama alivyonena, na Bwana akamfanyia kama alivyosema.
2 Sara akapata mimba akamzalia Ibrahimu mwana wa kiume katika uzee wake, kwa muhula alioambiwa na Mungu. 3 Ibrahimu akamwita jina lake Isaka, yule mwana aliyezaliwa, ambaye Sara alimzalia”.
Sara alipofariki, Ibrahimu akaoa mke mwingine, aliyeitwa Ketura. (Mwanzo 25:1-2)
Huyu Ketura ndiye aliyemzaliwa Ibrahimu wana wengine 6. Kufanya jumla ya watoto wote wa Ibrahimu kuwa 8, Biblia haielezi kuwa alikuwa na wana wengine wa kike.
Lakini katika wana hao wote, ni mmoja tu, aliyekuwa mrithi wa Ibrahimu, naye ni Isaka. Na siri moja ni kuwa wale wana wengine Ibrahimu aliwapa zawadi nyingi, lakini Isaka alipewa vyote, zawadi pamoja na urithi, kwasababu yeye ndiye aliyekuwa mwana wa Ahadi kutoka kwa Mungu.
Mwanzo 25:5 “Ibrahimu akampa Isaka yote aliyokuwa nayo. 6 Lakini wana wa masuria aliokuwa nao Ibrahimu, Ibrahimu akawapa zawadi, naye akawaondoa katika mahali alipokaa Isaka mwanawe, wakati wa uhai wake, waende pande za mashariki, mpaka nchi ya Kedemu”.
Mwanzo 25:5 “Ibrahimu akampa Isaka yote aliyokuwa nayo.
6 Lakini wana wa masuria aliokuwa nao Ibrahimu, Ibrahimu akawapa zawadi, naye akawaondoa katika mahali alipokaa Isaka mwanawe, wakati wa uhai wake, waende pande za mashariki, mpaka nchi ya Kedemu”.
Vivyo hivyo na sisi, tunaweza sote tukawa ni watu wa Mungu, tulioumbwa na Mungu, lakini si sote tukawa wana wa ahadi wa Mungu mfano wa Isaka. Wana wa ahadi ni wale waliozaliwa mara ya pili (yaani waliokoka). Na hao ndio Mungu kawaandalia vyote, thawabu pamoja na urithi wa ufalme wa mbinguni.
Ambapo Yesu alikwenda kuwaandalia waliompokea, Na siku atakaporudi, atawagawia urithi huo ambao alikuwa akiwaandalia kwa miaka 2000. Mambo ambayo jicho halijawahi kuoa wala sikio kusikia.
Swali la kujiuliza Ni je! na wewe ni mmojawapo wa wana wa Ahadi? Kama hujaokoka na kusimama, bado hujawa mwana wa ahadi, Lakini habari njema ni kuwa nafasi bado ipo lakini haitakuwepo siku zote ya wewe kufanyika hivyo.. Kama upo tayari leo hii kufanyika mtoto wa Mungu, na kuachana na dunia, na kutaka Yesu akuokoe, basi uaumuzi huo ni wa busara kwako, unachopaswa kufanya ni kufungua hapa ili upate maelekezo ya sala ya toba >>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Tazama chini kwa masomo mengine ya rohoni.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp yako mara kwa mara tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
WATOTO WA YESE KATIKA BIBLIA.
KUFUKIZA UVUMBA NDIO KUFANYAJE?
NENO NI LILE LILE, LAKINI UJUMBE NI TOFAUTI.
KIFO CHA MTAKATIFU PERPETUA NA FELISTA.