Jina la Bwana wetu Yesu Kristo, libarikiwe. Nakukaribisha katika kuyatafakari maandiko.
Tunajua kuja kwa Yesu mara ya kwanza, kulibeba siri nyingi za kuja kwake mara ya pili, kwa mfano wakati ule kabla ya Herode, kutaka kumuua Yesu pindi alipozaliwa, kulitangulia kwanza sensa kubwa kwa watu wote wa ulimwengu, ambayo ilimlazimu kila mmoja aende kwenye mji wake aliozaliwa ili ahesabiwe huko..Na ndivyo itakavyokuja kuwa kipindi kifupi kabla ya Yesu kurudi mara ya pili duniani, mpinga-Kristo ataleta utaratibu mpya wa watu wote kuhakikiwa, mfumo huu mpya ndio ile inayojulikana kama chapa ya Mnyama ambao utamlazimu kila mmoja awe nayo, kama mtu hana basi hataweza kuuza au kununua au kufanya biashara, au kuajiriwa mahali popote..kwa urefu wa somo hilo tutumie ujumbe inbox tukutumie ..
Lakini pia kulikuwa na jambo lingine, ambalo lilichochea kwa haraka sana dhiki kutokea pale Yerusalemu pindi tu Yesu alipozaliwa. Na jambo lenyewe, lilikuwa kwa wale Mamajusi kutoka Mashariki.
Sasa ukiangalia pale, utagundua habari ya kuzaliwa kwa Yesu ilikuwa imeshajulikana hata kabla ya baadha ya watu pale Israeli kujua, utaona kulikuwa na wale wachungaji kule makondeni waliotokewa na malaika na kuambiwa wamfuate mtoto..Ni kweli walienda na kushuhudia waliyoambiwa, na pengine baaada ya pale walisambaza taarifa za kuzaliwa kwa watu wengi vijijini na mijini, lakini habari zao hazikuwa na nguvu sana, wala hazikuleta mabadiliko yoyote kwa Israeli au kwa Herode, Vivyo hivyo, walikuwepo wakina Simoni na Hana, ambao Mungu aliwashuhudia kuwa huyu ndiye mwokozi na mfalme, pengine nao walitangaza, lakini taarifa zao pia hazikufika mbali sana.
Walikuwepo wakina Zekaria kuhani na mke wake Elisabeti, ambao walitangaza habari za Yesu na Yohana, ambazo kwa habari ya Yohana biblia inasema zilijulikana katika mji wote ule lakini bado hazikuwa na mashiko sana..Lakini tunaona kulikuwa na kundi lingine la watu, toka mbali sana, lililoleta habari,..Hilo halikuwa la watu wa pale Israeli, bali lilitoka mbali sana, ndio wale mamajusi wa Mashariki, walioina nyota yake na kufunga safari mpaka Israeli, na walipofika moja kwa moja wakamuuliza mfalme Herode, yupo wapi mfalme wa Wayahudi aliyezaliwa..Sasa kwa taarifa hizo Biblia inatuambia sio tu Herode zilimfadhaisha, bali na Israeli nzima. Hapo ndipo pakawa mwanzo wa sura nyingine kwa taifa la Israeli.
Mathayo 2:1 “Yesu alipozaliwa katika Bethlehemu ya Uyahudi zamani za mfalme Herode, tazama, mamajusi wa mashariki walifika Yerusalemu, wakisema, 2 Yuko wapi yeye aliyezaliwa mfalme wa Wayahudi? Kwa maana tuliiona nyota yake mashariki, nasi tumekuja kumsujudia. 3 Basi mfalme Herode aliposikia hayo, alifadhaika, na Yerusalemu pia pamoja naye. 4 Akakusanya wakuu wa makuhani wote na waandishi wa watu, akatafuta habari kwao, Kristo azaliwa wapi”?
Mathayo 2:1 “Yesu alipozaliwa katika Bethlehemu ya Uyahudi zamani za mfalme Herode, tazama, mamajusi wa mashariki walifika Yerusalemu, wakisema,
2 Yuko wapi yeye aliyezaliwa mfalme wa Wayahudi? Kwa maana tuliiona nyota yake mashariki, nasi tumekuja kumsujudia.
3 Basi mfalme Herode aliposikia hayo, alifadhaika, na Yerusalemu pia pamoja naye.
4 Akakusanya wakuu wa makuhani wote na waandishi wa watu, akatafuta habari kwao, Kristo azaliwa wapi”?
Sasa kama tunavyoijua habari kilichofuata pale ni Herode kwenda kuwaua watoto wote waliokuwa Bethlehemu wakati ule (kukawa na kilio kikuu Bethlehemu).
Mathayo 2:18 “Sauti ilisikiwa Rama, Kilio, na maombolezo mengi, Raheli akiwalilia watoto wake, Asikubali kufarijiwa, kwa kuwa hawako”.
Lakini kabla ya kuwaua, Mama na mtoto walihamishwa, na kupelekwa Misri kuikwepa dhiki.
Sasa, katika siku za mwisho, mambo kama hayo hayo yataenda kujirudia,. Baada ya Unyakuo kupita, dunia itakuwa imebakiwa na miaka 7 tu mpaka iishe kabisa, katika kipindi hicho, Mungu atawanyanyua watu watu wawili ambao watawatenga kwa lengo moja tu, la kwenda kuwatolea Unabii Israeli, juu ya kurudi kwa Kristo ulimwenguni kutawala kama mfalme wa wafalme…ndio mfano wa wale mamajusi wa Mashariki. (Na Huo ndio utakuwa wakati wa neema kuhamia Israeli)
Watu hawa ndio wale mashahidi wawili tunaowasoma katika Ufunuo 11, Watahubiri pale Israeli, kwa kipindi cha miaka mitatu na nusu kama biblia inavyotuambia,..Na wakati huo mpinga-Kristo, atawasikia, na hiyo ndio itakuwa kama alert yake, kuwa mwisho umefika.Atakachofanya ni kufanya vita na hawa watu, na kuleta dhiki Israeli, na duniani kote, hiyo ndio ile dhiki kuu,
Ufunuo 11:3 “Nami nitawaruhusu mashahidi wangu wawili, nao watatoa unabii siku elfu na mia mbili na sitini, hali wamevikwa magunia. 4 Hao ndio ile mizeituni miwili na vile vinara viwili visimamavyo mbele za Bwana wa nchi. 5 Na mtu akitaka kuwadhuru, moto hutoka katika vinywa vyao na kuwala adui zao. Na mtu akitaka kuwadhuru, hivyo ndivyo impasavyo kuuawa. 6 Hao wana amri ya kuzifunga mbingu, ili mvua isinyeshe katika siku za unabii wao. Nao wana amri juu ya maji kuyageuza kuwa damu, na kuipiga nchi kwa kila pigo, kila watakapo. 7 Hata watakapoumaliza ushuhuda wao, yule mnyama atokaye katika kuzimu atafanya vita nao, naye atawashinda na kuwaua”.
Ufunuo 11:3 “Nami nitawaruhusu mashahidi wangu wawili, nao watatoa unabii siku elfu na mia mbili na sitini, hali wamevikwa magunia.
4 Hao ndio ile mizeituni miwili na vile vinara viwili visimamavyo mbele za Bwana wa nchi.
5 Na mtu akitaka kuwadhuru, moto hutoka katika vinywa vyao na kuwala adui zao. Na mtu akitaka kuwadhuru, hivyo ndivyo impasavyo kuuawa.
6 Hao wana amri ya kuzifunga mbingu, ili mvua isinyeshe katika siku za unabii wao. Nao wana amri juu ya maji kuyageuza kuwa damu, na kuipiga nchi kwa kila pigo, kila watakapo.
7 Hata watakapoumaliza ushuhuda wao, yule mnyama atokaye katika kuzimu atafanya vita nao, naye atawashinda na kuwaua”.
Lakini kabla hajafanikiwa, lipo kundi dogo ambalo litasikia injili ya wale mashahidi wawili, na kuondoshwa na kwenda kufichwa, ndio wale wayahudi 144,000, hao watafichwa na dhiki kuu haitawapata (Ufunuo 7&11).
Ufunuo 12:13 “Na joka yule alipoona ya kuwa ametupwa katika nchi, alimwudhi mwanamke yule aliyemzaa mtoto mwanamume. 14 Mwanamke yule akapewa mabawa mawili ya tai yule mkubwa, ili aruke, aende zake nyikani hata mahali pake, hapo alishwapo kwa wakati na nyakati na nusu ya wakati, mbali na nyoka huyo. 15 Nyoka akatoa katika kinywa chake, nyuma ya huyo mwanamke, maji kama mto, amfanye kuchukuliwa na mto ule. 16 Nchi ikamsaidia mwanamke; nchi ikafunua kinywa chake, ikaumeza mto ule alioutoa yule joka katika kinywa chake. 17 Joka akamkasirikia yule mwanamke, akaenda zake afanye vita juu ya wazao wake waliosalia, wazishikao amri za Mungu, na kuwa na ushuhuda wa Yesu; naye akasimama juu ya mchanga wa bahari”.
Ufunuo 12:13 “Na joka yule alipoona ya kuwa ametupwa katika nchi, alimwudhi mwanamke yule aliyemzaa mtoto mwanamume.
14 Mwanamke yule akapewa mabawa mawili ya tai yule mkubwa, ili aruke, aende zake nyikani hata mahali pake, hapo alishwapo kwa wakati na nyakati na nusu ya wakati, mbali na nyoka huyo.
15 Nyoka akatoa katika kinywa chake, nyuma ya huyo mwanamke, maji kama mto, amfanye kuchukuliwa na mto ule.
16 Nchi ikamsaidia mwanamke; nchi ikafunua kinywa chake, ikaumeza mto ule alioutoa yule joka katika kinywa chake.
17 Joka akamkasirikia yule mwanamke, akaenda zake afanye vita juu ya wazao wake waliosalia, wazishikao amri za Mungu, na kuwa na ushuhuda wa Yesu; naye akasimama juu ya mchanga wa bahari”.
Unaona, Lakini wayahudi wengine wote, waliosalia duniani, pamoja na wale watu ambao hawakuipokea chapa ya mnyama, Watapitia dhiki kubwa isiyokuwa na mfano tangu dunia kuumbwa.
Injili inayohubiriwa sasa hivi haiwezi kutikisa au kuleta matatizo duniani, ila kipindi cha injili za hawa manabii wawili watakaposimama, na kutoa unabii pale Israeli, na kwa yale mapigo yaliyoorodheshwa pale ndipo ulimwengu utakapojua rangi halisi ya mpinga-Kristo.
Hawa watu pengine tayari wapo duniani, kwasababu dalili zote zinaonyesha.. Lakini mpaka hayo yote yatokee sisi tuliookoka ambao tumejiweka tayari, tutakuwa siku nyingi tumeshakwenda utukufuni (kanisa halitashuhudia mambo hayo ya manabii wawili). Jiulize na wewe ndugu ikiwa unyakuo utapita leo, wewe utakuwa wapi? Utajisikiaje kuona wenzako wapo mbinguni, wanaona vitu ambavyo jicho halijawahi kuona, na wewe bado upo hapa duniani, kwenye dhiki za mpinga-Kristo, ukizingatia ulihubiriwa injili mara nyingi na hukutaka kusikia?..
Je! bado unadanganywa na manabii wa uongo? Je bado, unapumbazwa na ulimwengu huu unaopita, Je! bado unasita sita kwenye mawazo mawili. Tubu kama bado hujafanya hivyo, ukabatizwe, dunia hii ipo ukingoni. Hatuna muda mrefu sana.?.
Maran Atha.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Neno I.N.R.I kwenye msalaba wa Yesu maana yake ni nini?
VITA VYA KIFIKRA BAADA YA KUZALIWA MARA YA PILI
USHIRIKINA NA MADHARA YAKE.
AMEFANYIKA BORA KUPITA MALAIKA!
Biblia inamaana gani kusema;aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi?
Rudi Nyumbani:
Print this post
Mhubiri 7:17 “Usiwe mwovu kupita kiasi; Wala usiwe mpumbavu; Kwani ufe kabla ya wakati wako?
Mstari huo haumaanishi kuwa uwe mwovu kiasi, hapana, uovu ni uovu tu, na una hukumu, Uwe unatenda dhambi nyingi au chache, ukifa utahukumiwa na jehanum utaenda..
Lakini kinachomaanishwa, hapo ni kuwa upo uovu unaozidi ambao, unaweza kukusababishia uondoke hapa duniani kabla ya siku zako,..Na aina nyingine ya uovu huu ni ule unaendekezwa kwa muda mrefu, pale unapojua madhara yake lakini hutaki kuacha.
Tengeneza picha unafanya kazi ya ujambazi, wa kuua watu kisa mali, unategemea vipi usipigwe risasi siku moja na polisi?
Wale wahalifu waliosulibiwa na Yesu pale msalabani, walijua kabisa yale yamewapata kwasababu ya makosa yao ya uuaji na wizi, na ndio maana mmojawao akasema.
Luka 23:41 “Nayo ni haki kwetu sisi, kwa kuwa tunapokea malipo tuliyostahili kwa matendo yetu; bali huyu hakutenda lo lote lisilofaa”.
Au unasafirisha madawa ya kulevya, kimataifa, unategemea vipi usikamatwe na kunyongwa? Au unaiba mali za watu na umeonywa mara nyingi auche lakini husikii unategemea vipi usichomwe moto?
Au unamtukana Mungu unategemea vipi uhai wako usifupishwe? n.k n.k.
Au unauchukua utukufu wa Mungu kupita kiasi unategemea vipi Mungu asikuondoe, kwasababu yeye mwenyewe anasema, mimi ni Mungu mwenye wivu. Mtazame Herode alifanya jambo kama hilo, na Mungu anampiga saa ile ile na chango.
Matendo 12:21 “Basi siku moja iliyoazimiwa, Herode akajivika mavazi ya kifalme, akaketi katika kiti cha enzi, akatoa hotuba mbele yao. 22 Watu wakapiga kelele, wakisema, Ni sauti ya Mungu, si sauti ya mwanadamu. 23 Mara malaika wa Bwana akampiga, kwa sababu hakumpa Mungu utukufu; akaliwa na chango, akatokwa na roho”.
Matendo 12:21 “Basi siku moja iliyoazimiwa, Herode akajivika mavazi ya kifalme, akaketi katika kiti cha enzi, akatoa hotuba mbele yao.
22 Watu wakapiga kelele, wakisema, Ni sauti ya Mungu, si sauti ya mwanadamu.
23 Mara malaika wa Bwana akampiga, kwa sababu hakumpa Mungu utukufu; akaliwa na chango, akatokwa na roho”.
Huo ni mifano michache ya maovu yanavuka mipaka, au yanayoendekezwa kwa muda mrefu. Umekuwa mzinzi au uasherati, na unajua kabisa tabia hiyo haimpendezi Mungu lakini bado unaendelea kufanya hivyo, siku baada ya siku, hapo unajitafutia mwenyewe Mungu kukupiga na janga la Ukimwi, na kufa kabla ya siku zako.
Mhubiri 7:17 “Usiwe mwovu kupita kiasi; Wala usiwe mpumbavu; Kwani ufe kabla ya wakati wako”?
Hivyo lililo la msingi, ni kujiepusha na uovu kabisa, kwasababu ouvu wowote uwe hata kama huna adhabu hapa, lakini kule utakutana nayo. ambayo ni ziwa la moto.
Warumi 2:5 “Bali kwa kadiri ya ugumu wako, na kwa moyo wako usio na toba, wajiwekea akiba ya hasira kwa siku ile ya hasira na ufunuo wa hukumu ya haki ya Mungu”,
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
USIWE NA HAKI KUPITA KIASI.
Yuko mwenye haki apoteaye katika haki yake.
Huyu Azazeli ni nani tunayemsoma katika(Walawi 16:8)
Mungu aliposema Yesu ni mwanawe pekee, alimaanisha hakuwa na wengine?
Wenye kubatizwa kwa ajili ya wafu ni wakina nani?
UNYAKUO.
CHUKIZO LA UHARIBIFU
Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe.’
Kama unaishi, basi unayo kila sababu ya kumshukuru Mungu, hata kama huna shilingi 10 mfukoni mwako, unazo kila sababu za kumshukuru Mungu.
Kwasababu dakika hii tunayozungumza, wakati wewe unaumwa kichwa tu!..yupo mtu ICU, kapoteza fahamu, yupo mwingine kalazwa unaugua sana. Na wakati pengine wewe upo kitandani umelazwa, ukitafakari matatizo unayoyapitia, kuna mwingine sehemu nyingine ndio yupo katika hatua ya kukata roho.
Wakati wewe hujala tangu asubuhi, yupo mwingine tangu jana hajala kabisa. Wakati wewe unao wazazi na ndugu, yupo mwingine hana hao, yupo peke yake..
Wakati wewe macho yanakusumbua (unavaa miwani), yupo mwingine hana macho kabisa. Wakati unatembea kwa kuchechemea, yupo mwingine hata hiyo miguu hajawahi kuwa nayo.
Wakati wewe huna fedha wala mali, lakini unao uhuru wa kuamka asubuhi na kwenda unapotaka, wapo wengine sasahivi wamefungwa magerezani na tena kwa miaka mingi, hawana uhuru kama ulionao wewe, wanatamani wangeupata hata walau kwa siku moja tu, lakini hawana…
Wakati wewe leo siku yako imeenda vizuri, wapo wengine dakika hii hii wapo misibani, wameamka na taarifa za misiba, wanazika wapendwa wao, watu wao wa thamani na wa muhimu. Na sio kwamba wamemchukiza Mungu ndio maana yamewapata hayo hapana! wengine ni watumishi wa Mungu wa thamani kabisa mbele zake, lakini ni wagonjwa, wengine wamefungwa, wengine wametengwa, na wengine hata hawana chakula n.k Lakini wewe hupitii hayo mazito kama ya kwao..Tafakari mara mbili!!..Mshukuru Mungu wala usiwe mtu wa kulalamika kabisa!.
Kitendo cha wewe kuimaliza siku unaishi, huo tayari ni muujiza mkubwa sana. Hivyo katika hali yoyote ile uliyopo, maadamu unao uzima mshukuru Mungu. Siku zote usijilinganishe na yule aliyenacho, bali jilinganishe na yule asiyenacho, ndipo utakapokuwa na kila sababu za kumshukuru Mungu.
Tena mshukuru Mungu kwa kumwimbia, kumshangilia na kumtolea. Unapofanya hivyo, unaonyesha kumheshimu Mungu na kutambua uwepo wake katika maisha yako. Na pia ni mapenzi ya Mungu sisi tumshukuru yeye.
1Wathesalonike 5:17 “ombeni bila kukoma; shukuruni kwa kila jambo; maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu katika Kristo Yesu”.
Wakolosai 3:15 “…tena iweni watu wa shukrani”.
Siku hizi za kumalizia, shikilia imani kwa nguvu zaidi, kamwe usiruhusu, taabu za dunia kukukatisha tamaa, Mwisho upo karibu sana.
Bwana atubariki.
JIOKOE WEWE NA NYUMBA YAKO.
BWANA MUNGU NASHANGAA KABISA lyrics
YAKINI NA BOAZI.
BWANA SI MWEPESI WA HASIRA, LAKINI BWANA NI MWINGI WA HASIRA.
TAZAMA, NASIMAMA MLANGONI.
Mistari ya biblia kuhusu watoto
Jiunge na group la Whatsapp, ujifunze biblia na upate Neno la siku kila asubuhi. kwa link hii >>> https://chat.whatsapp.com/GRri9BATojl2FNGbOJpjC6
Tazama mistari hii, na chini kabisa utapata orodha ya masomo ya kujifunza kuhusu watoto, kwako wewe kama mzazi/mlezi.
Isaya 54:13 “Na watoto wako wote watafundishwa na Bwana; na amani ya watoto wako itakuwa nyingi”.
Mathayo 19:14 “Lakini Yesu akasema, Waacheni watoto wadogo waje kwangu; wala msiwazuie; kwa maana walio mfano wa hao, ufalme wa mbinguni ni wao”.
Wakolosai 3:20 “Ninyi watoto, watiini wazazi wenu katika mambo yote; maana jambo hili lapendeza katika Bwana”.
Mithali 1:8 “Mwanangu, yasikilize mafundisho ya baba yako, Wala usiiache sheria ya mama yako, 9 Kwa maana hayo yatakuwa kilemba cha neema kichwani pako, Na mikufu shingoni mwako”.
Mithali 1:8 “Mwanangu, yasikilize mafundisho ya baba yako, Wala usiiache sheria ya mama yako,
9 Kwa maana hayo yatakuwa kilemba cha neema kichwani pako, Na mikufu shingoni mwako”.
Waefeso 6:1 “Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika Bwana, maana hii ndiyo haki. 2 Waheshimu baba yako na mama yako; amri hii ndiyo amri ya kwanza yenye ahadi, 3 Upate heri, ukae siku nyingi katika dunia”.
Waefeso 6:1 “Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika Bwana, maana hii ndiyo haki.
2 Waheshimu baba yako na mama yako; amri hii ndiyo amri ya kwanza yenye ahadi,
3 Upate heri, ukae siku nyingi katika dunia”.
Luka 2:52 “Naye Yesu akazidi kuendelea katika hekima na kimo, akimpendeza Mungu na wanadamu”.
3Yohana 1:4 “Sina furaha iliyo kuu kuliko hii, kusikia ya kwamba watoto wangu wanakwenda katika kweli”.
Marko 10:15 “Amin, nawaambieni, Ye yote asiyeukubali ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo hatauingia kabisa. 16 Akawakumbatia, akaweka mikono yake juu yao, akawabarikia”.
Marko 10:15 “Amin, nawaambieni, Ye yote asiyeukubali ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo hatauingia kabisa.
16 Akawakumbatia, akaweka mikono yake juu yao, akawabarikia”.
1Timotheo 4:12 “Mtu awaye yote asiudharau ujana wako, bali uwe kielelezo kwao waaminio, katika usemi na mwenendo, na katika upendo na imani na usafi”.
Zaburi 127:3 “Tazama, wana ndio urithi wa Bwana, Uzao wa tumbo ni thawabu”.
Zaburi 34:11 “Njoni, enyi wana, mnisikilize, Nami nitawafundisha kumcha Bwana”.
Mithali 22:6 “Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee”.
Mithali 22:15 “Ujinga umefungwa ndani ya moyo wa mtoto; Lakini fimbo ya adhabu itaufukuzia mbali”.
Mithali 23:13 “Usimnyime mtoto wako mapigo; Maana ukimpiga kwa fimbo hatakufa. 14 Utampiga kwa fimbo, Na kumwokoa nafsi yake na Kuzimu”.
Mithali 23:13 “Usimnyime mtoto wako mapigo; Maana ukimpiga kwa fimbo hatakufa.
14 Utampiga kwa fimbo, Na kumwokoa nafsi yake na Kuzimu”.
Mithali 13:24 “Yeye asiyetumia fimbo yake humchukia mwanawe; Bali yeye ampendaye humrudi mapema”.
Mithali 19:18 “Mrudi mwanao, kwa maana liko tumaini; Wala usiikaze nafsi yako kwa kuangamia kwake”.
Waebrania 12:11 “Kila adhabu wakati wake haionekani kuwa kitu cha furaha, bali cha huzuni; lakini baadaye huwaletea wao waliozoezwa nayo matunda ya haki yenye amani”.
Mithali 29:17 “Mrudi mwanao naye atakustarehesha; Naam, atakufurahisha nafsi yako”.
Mithali 17:6 “Wana wa wana ndio taji ya wazee, Na utukufu wa watoto ni baba zao”.
Waefeso 6:4 “Nanyi, akina baba, msiwachokoze watoto wenu; bali waleeni katika adabu na maonyo ya Bwana”.
Mafundisho muhimu ya wazazi kwa watoto.
KILEMBA CHA NEEMA, JE! UMEMVIKA MWANAO?
LENGO LA SHETANI KWA WATOTO WA KIZAZI HIKI.
MALEZI YA MTOTO MCHANGA.
SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?
MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.
MKUMBUKE MKE WA LUTU.
Je! utapenda mafundisho ya Neno la Mungu ya kila siku yawe yanakufikia kwa njia ya whatsapp au email yako? Kama ndio, basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255789001312
SWALI: Bwana Yesu alimaanisha nini kusema “walakini, atakapokuja Mwana wa Adamu, je! Ataiona imani duniani?”
JIBU: Ili tupate picha kamili tuisome habari yake kuanzia juu kidogo, kwasababu Bwana alichokisema kinategemea hiyo habari iliyokuwa juu yake…
Luka 18 :1-8 “1 Akawaambia mfano, ya kwamba imewapasa kumwomba Mungu sikuzote, wala wasikate tamaa. 2 Akasema, Palikuwa na kadhi katika mji fulani, hamchi Mungu, wala hajali watu. 3 Na katika mji huo palikuwa na mwanamke mjane, aliyekuwa akimwendea-endea, akisema, Nipatie haki na adui wangu. 4 Naye kwa muda alikataa; halafu akasema moyoni mwake, Ijapokuwa simchi Mungu wala sijali watu, 5 lakini, kwa kuwa mjane huyu ananiudhi, nitampatia haki yake, asije akanichosha kwa kunijia daima. 6 Bwana akasema, Sikilizeni asemavyo yule kadhi dhalimu. 7 Na Mungu, je! Hatawapatia haki wateule wake wanaomlilia mchana na usiku, naye ni mvumilivu kwao? 8 Nawaambia, atawapatia haki upesi; walakini, atakapokuja Mwana wa Adamu, je! Ataiona imani duniani”?
Luka 18 :1-8
“1 Akawaambia mfano, ya kwamba imewapasa kumwomba Mungu sikuzote, wala wasikate tamaa.
2 Akasema, Palikuwa na kadhi katika mji fulani, hamchi Mungu, wala hajali watu.
3 Na katika mji huo palikuwa na mwanamke mjane, aliyekuwa akimwendea-endea, akisema, Nipatie haki na adui wangu.
4 Naye kwa muda alikataa; halafu akasema moyoni mwake, Ijapokuwa simchi Mungu wala sijali watu,
5 lakini, kwa kuwa mjane huyu ananiudhi, nitampatia haki yake, asije akanichosha kwa kunijia daima.
6 Bwana akasema, Sikilizeni asemavyo yule kadhi dhalimu.
7 Na Mungu, je! Hatawapatia haki wateule wake wanaomlilia mchana na usiku, naye ni mvumilivu kwao?
8 Nawaambia, atawapatia haki upesi; walakini, atakapokuja Mwana wa Adamu, je! Ataiona imani duniani”?
Kama tunavyosoma hapo alipomaliza tu kueleza hiyo habari ya huyo mjane ndipo akaongezea na hicho kipenge mwishoni.. “walakini, atakapokuja Mwana wa Adamu, je! Ataiona imani duniani”? Kumaanisha kuwa siku ya kuja kwake anatazamia kuona imani yenye mfano wa huyo mwanamke, kama kigezo cha mtu kunyakuliwa.
Huyo mwanamke, hakuvunjwa moyo, pale alipoona hakuna dalili yoyote ya kutendewa haki na Yule kadhi dhalimu, lakini aliendelea hivyo hivyo tu kila siku kama kipofu, akiamini siku moja atapatiwa haki yake, na mwisho wa siku akaipata, jaribu kujiweka wewe katika mazingira kama hayo, ni wazi utakata tamaa mapema pale unapoona mtu hata haoneshi dalili ya kukusikiliza, unaweza kusema anadharau, lakini kumbe hujui moyoni mwake unamtesa sana.
Vivyo hivyo, katika nyakati hizi za mwisho, nyakati za masumbufu ya maisha, nyakati ambazo watu wengi wamekata tamaa ya kumngojea Yesu, wengine wamerudi kwenye dunia, wengine wanadhihaki wanasema huyo Yesu mnayemsubiria yupo wapi? Kama biblia inavyosema katika..
2Petro 3:3 “Mkijua kwanza neno hili ya kwamba katika siku za mwisho watakuja na dhihaka zao watu wenye kudhihaki, wafuatao tamaa zao wenyewe, 4 na kusema, Iko wapi ahadi ile ya kuja kwake? Kwa maana, tangu hapo babu zetu walipolala, vitu vyote vinakaa hali iyo hiyo, tangu mwanzo wa kuumbwa”.
2Petro 3:3 “Mkijua kwanza neno hili ya kwamba katika siku za mwisho watakuja na dhihaka zao watu wenye kudhihaki, wafuatao tamaa zao wenyewe,
4 na kusema, Iko wapi ahadi ile ya kuja kwake? Kwa maana, tangu hapo babu zetu walipolala, vitu vyote vinakaa hali iyo hiyo, tangu mwanzo wa kuumbwa”.
Wengine watasema mnamwomba yeye ambaye hawajali..unaona?
Lakini siku atakapokuja Yesu, jambo la kwanza kama alivyosema ni kuwa ataangalia IMANI kwanza, ataaangalia wale waliokuwa na Imani kwake, ambao hawakukatishwa tamaa kuomba ufalme wake uje, (Mathayo 6:9), japokuwa alionekana kama amechelewa, watu ambao hawakuruhusu kurudi nyuma..hao ndio atakaowaangalia..Na hao ndio kitendo cha kufumba na kufumbua watatoweka duniani siku ile.
Wengine wote watabaki hapa duniani, na wale ambao walikuwa wameshakufa tayari, Jicho la Yesu nalo litatazama mpaka kule makaburini, kama mtu alikufa bila imani hiyo, atabakia pale pale makaburini, watakaofufuliwa ni wale tu ambao mpaka dakika ya mwisho ya maisha yao waliishi kama vile Yesu anarudi muda wao, hao ndio watakaosikia sauti yake mwana wa Adam una wataungana na wale walio hai kwa pamoja kwenda kwenye karama ya mwana-kondoo mbinguni.
Lakini swali ni Je! imani hiyo ipo ndani yetu au imeshakufa siku nyingi?..Jibu unalo. Tunachopaswa kufanya sasa, ni kutungeneza mahusiano yetu na Mungu vizuri katika hichi kipindi kifupi cha maisha tulichobakiwa nacho hapa duniani, tujue kalenda ya Mungu duniani sasa ni ipi?…Pale ulimwengu unapozidi kwenda mbali na Imani na kudhihaki sisi ndio tuzidi kuomba na kumlilia Mungu zaidi kama huyu mjane..
Na siku moja isiyokuwa na jina, kitendo cha kufumba na kufumbua, tutajiona pale mawingu na majeshi ya malaika wengi yamekuja kutulaki, na parapanda ya Mungu. Itakuwa ni raha isiyo na kifani, maneno ya kibinadamu hayawezi kuelezea. Hivyo tuishi kwa Imani Bwana atakapokuja aione ndani yetu.
Jina la Bwana libarikiwe Milele.
REKEBISHA YAFUATAYO ILI MAMBO YAENDE SAWA.
Uwanda wa dura ni nini?
JE UDHAIFU WANGU UNAWEZA KUZUIA INJILI?
MTI WA UZIMA NA MTI WA MAARIFA.
Mlima sinai upo nchi gani? Na Je unaijua Sinai yako ya rohoni?
WhatsApp
Jina la Bwana wetu Yesu Kristo lizidi kubarikiwa.
Karibu tujifunze Neno la Mungu wetu.
Kama ni msomaji mzuri wa Biblia utakuwa unayajua majaribu matatu ya Yesu aliyojaribiwa na Ibilisi kule jangwani. Jambo la ajabu ni kwamba shetani hakwenda kumjaribu Bwana Yesu kwa uchawi, au kwa magonjwa au kwa maneno yake, bali alikwenda kumjaribu kwa kutumia maandiko matakatifu.
Maana yake ni kwamba kitengo kikubwa cha Majaribu ya shetani kwa mkristo hakipo kwa wachawi, au kwa waganga wa kienyeji kama watu wengi wanavyofikiri, BALİ KİPO KATİKA NENO LA MUNGU. Na shetani hatumii nguvu nyingi kututumia majeshi ya wachawi wake kama unavyohubiriwa na watu, bali anatumia nguvu kubwa kuhakikisha kwamba hulielewi Neno la Mungu, na hapo akifanikiwa basi unakua umekwisha!.. Bwana wetu Yesu asingekuwa analijua Neno kweli kweli, basi asingemweza shetani kamwe..Lakini shetani hakumweza kwasababu yeye ndio aliyekuwa Neno mwenyewe.
Wengi wetu tunakosa shabaha hapo, Tukidhani uadui mkubwa wa shetani kwetu ni waganga wa kienyeji na wachawi wanaotuzunguka…jambo linalompelekea Mkristo kutwa kuchwa kupambana na wachawi katika maombi.. Na kusahau kuwa silaha yake kubwa ni Neno la Mungu (Ndio upanga) Waefeso 6:17. Na pasipo kujua kuwa asipokuwa na Neno la Mungu la kutosha ndani yake basi tayari anakuwa kalogwa na shetani siku nyingi (Wagalatia 3:1)..Hata kama atakuwa anasali na kupiga maombi ya vita kila siku.
Sasa hebu tusome kwa ufupi jinsi Bwana alivyomjibu shetani katika yale majaribu na kisha tutajifunza kitu cha muhimu sana. Usipite hata kama ulishasoma rudia tena.
Mathayo 4:1 “Kisha Yesu alipandishwa na Roho nyikani, ili ajaribiwe na Ibilisi. 2 Akafunga siku arobaini mchana na usiku, mwisho akaona njaa. 3 Mjaribu akamjia akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, amuru kwamba mawe haya yawe mikate. 4 Naye akajibu akasema, Imeandikwa, Mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu. 5 Kisha Ibilisi akamchukua mpaka mji mtakatifu, akamweka juu ya kinara cha hekalu 6 akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu jitupe chini; kwa maana imeandikwa, Atakuagizia malaika zake; Na mikononi mwao watakuchukua; Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe. 7 Yesu akamwambia, Tena imeandikwa, Usimjaribu Bwana Mungu wako. 8 Kisha Ibilisi akamchukua mpaka mlima mrefu mno, akamwonyesha milki zote za ulimwengu, na fahari yake, 9 akamwambia, Haya yote nitakupa, ukianguka kunisujudia. 10 Ndipo Yesu alipomwambia, Nenda zako, Shetani; kwa maana imeandikwa, Msujudie Bwana Mungu wako, umwabudu yeye peke yake. 11 Kisha Ibilisi akamwacha; na tazama, wakaja malaika wakamtumikia”
Mathayo 4:1 “Kisha Yesu alipandishwa na Roho nyikani, ili ajaribiwe na Ibilisi.
2 Akafunga siku arobaini mchana na usiku, mwisho akaona njaa.
3 Mjaribu akamjia akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, amuru kwamba mawe haya yawe mikate.
4 Naye akajibu akasema, Imeandikwa, Mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu.
5 Kisha Ibilisi akamchukua mpaka mji mtakatifu, akamweka juu ya kinara cha hekalu
6 akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu jitupe chini; kwa maana imeandikwa, Atakuagizia malaika zake; Na mikononi mwao watakuchukua; Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.
7 Yesu akamwambia, Tena imeandikwa, Usimjaribu Bwana Mungu wako.
8 Kisha Ibilisi akamchukua mpaka mlima mrefu mno, akamwonyesha milki zote za ulimwengu, na fahari yake,
9 akamwambia, Haya yote nitakupa, ukianguka kunisujudia.
10 Ndipo Yesu alipomwambia, Nenda zako, Shetani; kwa maana imeandikwa, Msujudie Bwana Mungu wako, umwabudu yeye peke yake.
11 Kisha Ibilisi akamwacha; na tazama, wakaja malaika wakamtumikia”
Kama tunavyojua maneno yote shetani aliyomwambia Bwana Yesu hapo , hayakuwa ya UONGO! Yote yalikuwa ya kweli na yapo katika biblia, yalikuwa ni maneno ya Mungu yenye pumzi ya uhai (hivyo upo ukweli unaopotosha)…na yote shetani aliyatoa katika biblia..Kwamfano hilo Neno “Atakuagizia malaika zake; Na mikononi mwao watakuchukua” Ni Neno la Zaburi 91:12.
Lakini shetani aliyapindisha yale maneno na kuyafanya yatumike mahali ambapo sio sahihi, na kwa wakati usio sahihi. Maneno ya Mungu yakitumika mahali ambapo sio sahihi na kwa wakati ambao sio sahihi yanakuwa ni sumu kubwa.
Kwamfano Neno la Mungu ni kweli linasema.. “waume waishi na wake zao kwa akili na kumpa mke heshima (1Petro 3:7)”..Sasa Neno hili linawahusu Wanaume waliooa ndoa halali ya kimaandiko…Na si mtu yeyote tu hata anayeishi na girlfriend wake. Nimewahi kukutana na watu wanaoishi pasipo kuonana na wanautumia huu mstari kwa madai kwamba Mungu amesema “tuishi na wake kwa akili”. Nimewahi kukutana na mwingine akiwashawishi wanawake kufanya nao uzinzi huku akitumia hichi kipengele cha maandiko.. 1Wakorintho 7:5 “Msinyimane isipokuwa mmepatana kwa muda, ili mpate faragha kwa kusali; mkajiane tena, Shetani asije akawajaribu kwa kutokuwa na kiasi kwenu”.
Hivyo mwanamke yeyote anayekutana naye anakimbilia kumwonyesha huu mstari, na kusema hata Mungu amesema “tusinyimane” na amefanikiwa kuwanasa mabinti wengi kwa andiko halo…Pasipo kufahamu kuwa hilo andiko linawahusu wana-ndoa tu!(watu ambao tayari wameoana) na sio kila mtu tu!.
Sasa shetani alimjia Yesu kwa njama hiyo hiyo, kuyaweka maneno ya Mungu mahali pasipopaswa na kwa wakati usiofaa.
Anamwambia Bwana ajitupe chini na Mungu atamwagizia malaika waje wamchukue asijikwae…Ni kweli hilo ni Neno la Mungu, lakini huo sio wakati wake..Neno hilo litafaa kutumika wakati ambao tumejikuta tumeingia majaribuni au hatarini pasipo hiari yetu, huo ndio wakati wa Bwana kuwaagiza malaika zake watuchukue. Lakini sio wakati ambao tupo salama halafu tunamjaribu Mungu tuone atafanya nini, tukifanya hivyo tunajitafutia laana badala ya baraka..
Na sisi tunapaswa tujifunze KULIGAWANYA VYEMA NENO LA MUNGU. Na hiyo inakuja kwa kulisoma Neno la Mungu kwa bidii. Ukisoma kijimstari kimoja tu na kwenda kulala! Ni rahisi kushindwa kuyagawanya Maneno ya Mungu ipasavyo..
Na pia usitumie nguvu kubwa kuchunguza mchawi wako ni nani?.. Tumia nguvu kubwa kuyachunguza maandiko!!…Je biblia inasema nini katika hali hiyo unayopitia?..Je katika biblia kuliwahi kutokea kisa kama hicho unachopitia na je kilitatuliwaje?.. Unapoona kuna kitu fulani hakipo sawa, tafuta kujua je! Biblia inasemaje kuhusu hiyo hali.. Usisubiri kufundishwa-fundishwa biblia, jifunze kuisoma mwenyewe..Utakutana na mambo mengi huko, ambayo hata mchungaji wako hawezi kukuhubiria, na pia utagundua ni vitu gani ulikuwa unapotoshwa na vitu gani ulikuwa unaambiwa ukweli.
Lakini ukisubiri tu kila somo unalokutana nalo mitandanoni, ni kulisoma tu, kwasababu mtumishi yule anaaminika na wengi!, au kila hubiri ni kusikiliza tu kwasababu mtumishi yule anasifiwa na wengi. Nataka nikuambie, utaishia kukosa mahali pa kusimamia, utakuwa ni mtu wa kupepesuka daima. Na kutufuta mchawi ni nani kwenye ukoo wako, kumbe uchawi ni kukosa kwako maarifa ya Neno la Mungu.
Hosea 4:6 “Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa;..”
Soma Biblia mwenyewe huo ndio uthibitisho wa kwanza wa kwamba umeamua kuanza safari ya kumjua Mungu.
Na Bwana akubariki
JINSI YA KUSOMA BIBLIA.
KWANINI TUNAPASWA TUJIZUIE?
UPONYAJI WA ASILI
MASOMO MBALIMBALI YA NENO LA MUNGU.
Je! Mwanamke anapaswa afunikwe kichwa anapokuwa ibadani?
Kwa namna ya kawaida fedha haina ubaya wowote, ni nyezo ambayo Mungu aliiruhusu iwepo na itumiwe ili kuendesha kushughuli zote za kijamii.
Mhubiri 19:19 “…Na fedha huleta jawabu la mambo yote”.
Lakini kitendo cha kupenda fedha, hicho ndicho Mungu amekikatazata, na katika biblia kimekemewa sana, ikiwa wewe ni mtoto wa Mungu, na roho ya kupenda fedha ipo ndani yako, basi upo hatarini sana, kuzama katika maovu mengi..biblia inasema hivyo..
1Timotheo 6:10 “Maana shina moja la mabaya ya kila namna ni kupenda fedha; ambayo wengine hali wakiitamani hiyo wamefarakana na Imani, na kujichoma kwa maumivu mengi.”
Ndio maana biblia inawaasa sana watoto wa Mungu na kuwaambia..
Waebrania 13:5 “Msiwe na tabia ya kupenda fedha; mwe radhi na vitu mlivyo navyo; kwa kuwa yeye mwenyewe amesema, Sitakupungukia kabisa, wala sitakuacha kabisa”.
Mungu ametoa ahadi ya kuwahudumia watoto wake, kiasi kwamba hawatapungukiwa kabisa, hawatakosa kabisa ikiwa tu watakuwa watulivu katika shughuli zao.
Mtu mwenye tabia ya kupenda fedha ni rahisi kuhonga, ili upate fursa Fulani,ni rahisi kufanya biashara haramu kisa tu ameona zinamwingizia fedha nyingi, mwingine atakuwa radhi hata kujiuza mwili wake kisa fedha, wengine wanakwenda kwa waganga, wengine wapo tayari kuikana imani,..n.k.n.k. hapo ndipo unajua ni kwanini biblia inasema kupenda fedha ni shina la mabaya yote ulimwenguni. Wengine wapo tayari hata kuua watu, ili walipwe au waibe.
Mithali 1:19 “Ndivyo zilivyo njia za kila mwenye tamaa ya mali; Huuondoa uhai wao walio nayo”.
Na dalili mojawapo ambayo biblia inasema itatutambulisha kuwa tunaishi katika siku za mwisho, ni kuibuka kwa wimbi kubwa la watu wanaopenda fedha.
2Timotheo 3:1 Lakini ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari. 2 Maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukana, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio safi,”
2Timotheo 3:1 Lakini ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari.
2 Maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukana, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio safi,”
Mpaka sasa, imefikia hatua huduma za rohoni kutolewa kwa fedha,
1Timotheo 6: 5 “na majadiliano ya watu walioharibika akili zao, walioikosa kweli, huku wakidhani ya kuwa utauwa ni njia ya kupata faida”.
Hiyo yote ni matokeo ya wanadamu kupenda fedha..Bwana Yesu alisema..
Mathayo 6:24 “Hakuna mtu awezaye kutumikia mabwana wawili; kwa maana atamchukia huyu, na kumpenda huyu; ama atashikamana na huyu, na kumdharau huyu. Hamwezi kumtumikia Mungu na mali”.
Shetani alijua hapa ndipo wanadamu wengi wanapoweza kunaswa, hivyo, akatumia njia hiyo hiyo kumjaribia pia Yesu, akamwambia nitakupa milki zote za ulimwenguni, nitakupa fedha zote na majumba yote ikiwa utanisujudia tu. Lakini Bwana Yesu alimkemea akamwambia utamsujudia Bwana Mungu wako tu.. Kwasababu alijua kupenda fedha ni kuupenda ulimwengu.
1Yohana 2:15 “Msiipende dunia, wala mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake”.
Kama hiyo haitoshi Wenye mali, bado biblia inawapa nafasi ndogo sana ya kuurithi ufalme wa mbinguni;
Mathayo 19:23 “Yesu akawaambia wanafunzi wake, Amin, nawaambieni, ya kwamba itakuwa shida tajiri kuingia katika ufalme wa mbinguni. 24 Nawaambia tena, Ni rahisi zaidi ngamia kupenya tundu ya sindano, kuliko tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu”.
Mathayo 19:23 “Yesu akawaambia wanafunzi wake, Amin, nawaambieni, ya kwamba itakuwa shida tajiri kuingia katika ufalme wa mbinguni.
24 Nawaambia tena, Ni rahisi zaidi ngamia kupenya tundu ya sindano, kuliko tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu”.
Vifungu vipo vingi sana kwenye biblia vinavyozungumzia hatari za kupenda fedha., hatuwezi kuviweka vyote hapa, lakini kwa hivyo vichache kama na wewe ni mmojawapo, basi geuka haraka sana, uridhike na vile Mungu anavyokupa, kwasababu biblia inasema..
Mhubiri 5:10 “Apendaye fedha hatashiba fedha, Wala apendaye wingi hatashiba maongeo. Hayo pia ni ubatili”.
Na pia inasema.
Zaburi 37:16 “Kidogo alicho nacho mwenye haki ni bora Kuliko wingi wa mali wa wasio haki wengi”.
Chuma kidogo kidogo utafanikiwa..
Mithali 13:11 “Mali iliyopatikana kwa haraka itapunguka; Bali yeye achumaye kidogo kidogo atazidishiwa”.
Lakini kama wewe hujaokoka, ukweli ni kwamba hii roho ya kupenda fedha haiwezi kuondoka ndani yako, hata iweje, itaondoka, ikiwa tu utamruhusu Bwana Yesu aingie ndani yako aibadilishe Nia yako..
Akishakubadilisha hapo ndipo Roho ya kuridhika na ya utulivu itaingia ndani yako, na hapo hapo Mungu ataanza kukufundisha njia sahihi na yenye Baraka ya kukusanya..mpaka mwisho wa siku atakufikisha pale anapotaka uwepo. Na zaidi ya yote utaurithi uzima wa milele.
Hivyo kama upo tayari leo hii kutubu dhambi zako, unahitaji kuokoka, uamuzi huo utakuwa ni wa busara sana basi, fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Bwana akubariki.
UNAWAFAHAMU MANABII WA UONGO?
USIPOWATAMBUA YANE NA YAMBRE, KATIKA KANISA LA KRISTO, UJUE UMEPOTEA.
YONA: Mlango 1
UTAWALA WA MIAKA 1000.
EPUKA MUHURI WA SHETANI
Luka 16:16 “Torati na manabii vilikuwapo mpaka Yohana; tangu wakati huo habari njema ya ufalme wa Mungu hutangazwa, na kila mtu hujiingiza kwa nguvu”.
Nataka uone hicho kifungu cha mwisho, “ Na kila mtu hujiingiza kwa nguvu”..
Bwana Yesu alipotoa habari hiyo, kulikuwa na sababu kubwa kwanini alianza kwanza na habari za agano la kale(Torati na manabii) kisha akaja kwenye agano jipya, na kumalizia kwa kusema, tangu huo wakati kila mtu atakawa anajiingiza kwa nguvu.
Alisema hivyo kuonesha kuwa hapo kabla, kulikuwa hakuhitaji bidii yoyote, au jasho lolote, au nguvu yoyote, kuijua torati, lakini kuanzia wakati wa Yohana, injili ya kweli ambayo inaleta ondoleo la dhambi, ilipoanza kuhubiriwa, injili ya kumfanya mtu awe na maarifa kamili kumuhusu Mungu ilipoanza kuhubiri, injili inayomfungua mtu kweli kweli, basi vipingamizi vikubwa sana vitanyanyuka kiasi kwamba, mpaka mtu aipate ni lazima atumie nguvu nyingi sana kuingia, tofauti na ilivyokuwa hapo mwanzo.
Kwamfano utaona wakati ule tu, kulikuwa na mafarisayo na waandishi, ambao wamesimama hapo, katikati kuhakikisha kuwa mtu yeyote atakayemkiri Yesu hadharani, moja kwa moja atatengwa na sinagogi, (Yohana 9:22)
Na kutengwa kwa zamani sio kama sasa, zamani ukitengwa na sinagogi ni jamii nzima ya Israeli imekutenga mpaka familia yako. Hata misaada ya kijamii ulikuwa hupati, Hivyo suala la kutengwa lilikuwa ni jambo zito sana.
Hivyo haikuwa ni rahisi, hata kidogo, ilibidi watu walazimishe, mambo kwa nguvu, wawe radhi kutengwa tu, wawe tayari kupoteza mahusiano yao tu, lakini wasiukose ufalme wa mbinguni.
Mambo hayo hayo hata sasa, yanaendelea, kuupata ufalme wa mbinguni, ni kujiingiza kwa nguvu nyingi, wapo viongozi wako wa dini wanakuzuia usiokoke, kisa tu imani yao haimini kile biblia inachosema, pengine Imani yao inafundisha kusujudia sanamu, haiamini katika karama za Roho, ndugu usiwaangalie hao, wewe jiingize kwa nguvu katika ufalme wa Mungu,.
Hao ni wale wana-sheria wa dini, ambao Bwana Yesu anasema, kazi yao ni kusimama pale mlango kushikilia funguo, kuwazuia watu wasiingie, na wao wenyewe hawauingii, wanataka mkae wote katika giza la milele pamoja..
Luka 11:52 “Ole wenu, enyi wana-sheria, kwa kuwa mmeuondoa ufunguo wa maarifa; wenyewe hamkuingia, na wale waliokuwa wakiingia mmewazuia”.
Hivyo usiwaangalie hao hata kidogo, achana na mapokeo ya dini, tubu dhambi uokoke, tafuta ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi (Yohana 3:23), na kwa jina la YESU KRISTO sawasawa na Matendo 2:38, na sio ule wa kunyunyiziwa ambao haupo katika maandiko.
Jiingize kwa nguvu, hata kama ndugu zako hawakuelewi, Jiingize kwa nguvu hata kama marafiki zako watakuona mshamba, jipenyeze kwa nguvu hata kama dunia itakuona umerukwa na akili..Iokoe roho yako, wakati huu jiepushe na mtu ambaye unaona kabisa anaizuia njia yako ya wokovu.
Wenyewe hawawezi kuona hilo, kwasababu bado wapo gizani, lakini wewe umeiona nuru, usijifananishe na wao, zidi jenga uhusiano wako binafsi ya Yesu. Hizi ni nyakati za mwisho na unyakuo upo karibu sana,
Mathayo 11:12 “Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatikana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka. 13 Kwa maana manabii wote na torati walitabiri mpaka wakati wa Yohana”.
Mathayo 11:12 “Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatikana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka.
13 Kwa maana manabii wote na torati walitabiri mpaka wakati wa Yohana”.
Isiishi kwa kuwapendezesha watu na huku umelisahau Neno, kwasababu kila mtu atalibeba furushi lake mwenyewe (Wagalatia 6:5). Dakika hizi za majeruhi, zinafananishwa na Sodoma na Gomora, ambazo tunajua ni watu 3 tu kati ya mamilioni waliokuwa katika miji ile ndio waliopona….Ndivyo itakavyokuwa siku hizi, litavuka kundi dogo tu, lililoweza kujiingiza kwa nguvu katika ufalme wa mbinguni bila kujali vizuizi vya mpito vya ibilisi.
Unadhani shetani, hajui kuwa mtu akiupata ufalme wa Mungu, amepata kitu cha thamani kubwa sana, anajua hilo, na ndio maana lazima akuletee ugumu ili usijaribu kuuingia, ubakie kwenye giza huko huko..Hivyo vitisho kutoka kwa viongozi wako wa dini na ndugu na marafiki, visikufanye usichukue uamuzi wa kumpokea Yesu.
Mathayo 10:34 “Msidhani ya kuwa nimekuja kuleta amani duniani; la! Sikuja kuleta amani, bali upanga. 35 Kwa maana nalikuja kumfitini mtu na babaye, na binti na mamaye, na mkwe na mkwe mtu; 36 na adui za mtu ni wale wa nyumbani mwake. 37 Apendaye baba au mama kuliko mimi, hanistahili; wala apendaye mwana au binti kuliko mimi, hanistahili. 38 Wala mtu asiyechukua msalaba wake akanifuata, hanistahili. 39 Mwenye kuiona nafsi yake ataipoteza; naye mwenye kuipoteza nafsi yake kwa ajili yangu ataiona”.
Mathayo 10:34 “Msidhani ya kuwa nimekuja kuleta amani duniani; la! Sikuja kuleta amani, bali upanga.
35 Kwa maana nalikuja kumfitini mtu na babaye, na binti na mamaye, na mkwe na mkwe mtu;
36 na adui za mtu ni wale wa nyumbani mwake.
37 Apendaye baba au mama kuliko mimi, hanistahili; wala apendaye mwana au binti kuliko mimi, hanistahili.
38 Wala mtu asiyechukua msalaba wake akanifuata, hanistahili.
39 Mwenye kuiona nafsi yake ataipoteza; naye mwenye kuipoteza nafsi yake kwa ajili yangu ataiona”.
Kama bado hujafanya uamuzi huo basi anza sasahivi, wokovu unapatikana bure, lakini si rahisi si rahisi lakini inahitaji nguvu kujiingiza kwa huo, hivyo jiingize kwa nguvu bila kujali, na huko huko Bwana Yesu atajifunua kwako kwa namna ambayo hukuwahi kumjua hapo kabla, ndipo utakapomjua Mungu, na ndipo atakapotembea na wewe.
USIUZE URITHI WAKO.
Je! Kiongozi wa dini anaouwezo wa kusamehe dhambi?
KANUNI RAHISI YA KUFANIKIWA.
JIHADHARI NA KUOSHWA MIGUU ISIVYOPASWA.
MWANANCHI WA UFALME WA MBINGUNI
USIISHI BILA KUIFANYA KAZI YA MUNGU KABISA..
Jukumu moja na kuu tulilonalo sisi ni KUMJUA SANA YESU KRISTO. Wengi wanalikwepa jukumu hili. Na Zaidi wanapenda sana kutafuta kuwajua watumishi wa Yesu kuliko ya Yesu mwenyewe.
Waefeso 4:13 “hata na sisi sote tutakapoufikia umoja wa imani NA KUMFAHAMU SANA MWANA WA MUNGU, hata kuwa mtu mkamilifu, hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo”.
Jitathmini ukiona kuna mahali unamjua mtumishi, zaidi ya Bwana wake mwenyewe ambaye ni Yesu, basi kuna tatizo mahali na pia una laana.(1Wakorintho 16:22)
Kama mtumishi wa Kristo akizungumziwa vibaya inakuuma Zaidi ya Yesu akifanyiwa mzaha, basi kuna tatizo katika uhusiano wako na Yesu.
Kama comedy za kumtania Mwokozi Yesu hazikuhuzunishi sana kama za kumtania mchungaji wako, au mwalimu wako, basi kuna tatizo mahali.
Kama unakuwa mkali dini yako inapozungumziwa vibaya, au dhehebu lako au mwalimu wako anayekufundisha Neno la Mungu kanisani, na wakati huo huo unakutana na comedy inayomkebehi Kristo waziwazi na wala haikuhumizi sana Zaidi inakuchekesha!, hebu jitafakari tena, inawezekana humjui kabisa Yesu, wala hayupo maishani mwako.
Kama Maisha yako ya binafsi ya siri, hujawahi kukaa ukazungumza na mwokozi wala kumshukuru, basi kuna shida.
Dada/kaka usitumie nguvu nyingi kutafuta kumpendeza mtumishi, wala usiwe mshabiki wa dini, wala usiwe mshabiki wa mtumishi wa Mungu.
Tafuta kumjua Yesu, na kumjua Yesu sio kuhama na kubadilisha kanisa…Ni hapo hapo ulipo tu!..Unachopaswa kukifanya baada ya kumpokea Kristo ni kukinunua kitabu kinachoitwa Biblia. Usitegemee ile ya ku-download kwenye simu yako.. Ya kudownload ni nzuri baada ya kuwa na ya KITABU chenye kurasa za karatasi.
Hivyo kinunue hichi kitabu kinachoitwa Biblia. Ukishakipata! Anza kukisoma mwenyewe!..Mungu kakupa macho, kakupa na uwezo wa kusoma, hawezi kukunyima uwezo wa kuelewa!..
Kinachosababisha wengi wasiielewe biblia ni kusoma kwa kutimiza wajibu tu!..na sio kwa kutoka ndani ya mioyo yao, wanasoma tu kwasababu wameambiwa wasome, au kwasababu tu wanahisi ndio wanampendeza Mungu, na anasoma kwa mwezi mara moja…Hivyo biblia inakuwa ni kitabu kigumu sana kwao kukielewa. Na pia wanasoma mstari mmoja kisha wanarukia mwingine…Hawapendi kusoma mwanzo wa kitabu hadi mwisho.
Hivyo soma biblia mwenyewe kwa macho yako mawili. Ukikutana na jambo gumu kuna nguvu Fulani ya asili ambayo Mungu kaiweka ndani yetu itakayokupeleka katika kuutafuta ukweli Zaidi, hapo ndipo kitakuja kitu cha kutafuta msaada Zaidi kwa mahubiri ya watumishi wa Mungu, utaona kuna kitu kinakusukuma kwenda sehemu Fulani labda kanisa Fulani, au kwenye semina Fulani, au katika mahubiri Fulani.. ambapo utaona utapata majibu ya maswali yako, au utakwenda kusoma jumbe Fulani ambazo utaona zitakufaidisha roho yako. Na kwa njia hiyo ndipo mafunuo ya Roho yanapokuja.
Lakini huwezi kusema naondoka kanisa hili nahamia lile kama hujapata sababu yoyote ya kimaandiko ya kufanya hivyo.. Wengi wanahama kanisa kwasababu tu wameambiwa ukweli..hivyo ule ukweli unawauma na kuishia kuhama, wengine kwasababu wamesikia wakisengenywa, wengine kwasababu wameona kanisani kumepungua watu hivyo na wao wanaondoka…mambo ambayo hayana mashiko kabisa!..Mtu wa namna hiyo hajaongozwa na Mungu, bali kafuata akili zake mwenyewe.
Lakini mtu wa kweli ambaye anaongozwa na Roho, huwa anaondoka sehemu moja hadi nyingine, ni kwasababu anatafuta uelewa wa maandiko Zaidi, anatamani kumjua Yesu zaidi na kukua kiroho.. huyo ndiye anayeongozwa na Roho. Anaona kuna umuhimu wa kutafuta kujifunza Neno Zaidi, kutafuta kufunga Zaidi na kusali. Na si kwasababu kasikia kasengenywa, au kasemwa, au kaudhiwa.
Hivyo siku zote usilisahau hili ndugu yangu mpendwa.. MJUE SANA YESU. Huyo ndio ndiye Mkuu wa Uzima, na ndiye mwenye funguo za Uzima, na ndiye aliyekabidhiwa mamlaka yote ya mbinguni na Duniani..Tunavyozungumza sasa yupo anaishi! Na atarudi tena kulichukua kanisa lake, Ana nguvu nyingi sana, yeye hadhihakiwi sio yule unayemwona kwenye picha, sio unayemwona kwenye Tv, Yesu ni Mungu, akijifunua kwetu kikamilifu, hata hapa duniani tunaweza tusitamani kuendelea kuishi, Hivyo tumjue yeye kila siku, tujinyenyekeze mbele zake, ajifunue kwetu zaidi na zaidi. Anatamani kujifunua kwetu sana, ni sisi tu.
Bwana atubariki sana.
Kuna haja gani ya kumwamini Yesu aliyezaliwa kama sisi?
WINGU KUBWA LA MASHAHIDI.
WANA JUHUDI KWA AJILI YA MUNGU, LAKINI SI KATIKA MAARIFA.
MWISHO WA HAO WAMSAHAUO MUNGU.
RUDIA, TENA NA TENA KUMWOMBA MUNGU USIKATE TAMAA.
Isaya 24:3 “Dunia hii itafanywa tupu kabisa, na kuharibiwa kabisa; maana Bwana amenena neno hilo. 4 Dunia inaomboleza, inazimia; ulimwengu unadhoofika, unazimia; watu wakuu wa dunia wanadhoofika. 5 Tena dunia imetiwa unajisi kwa watu wanaoikaa; kwa maana wameziasi sheria, wameibadili amri, wamelivunja agano la milele. 6 Ndiyo sababu laana imeila dunia hii, na hao wanaoikaa wameonekana kuwa na hatia, ndiyo sababu watu wanaoikaa dunia wameteketea, watu waliosalia wakawa wachache tu”.
Isaya 24:3 “Dunia hii itafanywa tupu kabisa, na kuharibiwa kabisa; maana Bwana amenena neno hilo.
4 Dunia inaomboleza, inazimia; ulimwengu unadhoofika, unazimia; watu wakuu wa dunia wanadhoofika.
5 Tena dunia imetiwa unajisi kwa watu wanaoikaa; kwa maana wameziasi sheria, wameibadili amri, wamelivunja agano la milele.
6 Ndiyo sababu laana imeila dunia hii, na hao wanaoikaa wameonekana kuwa na hatia, ndiyo sababu watu wanaoikaa dunia wameteketea, watu waliosalia wakawa wachache tu”.
Nabii Isaya alipotabiri juu ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo na bikira (Isaya 7:14), miaka 700 kabla ya Masihi kuja duniani, wapo watu pengine walioona kuwa hizo ni hadithi tu za kufikirikika… Alipotabiri tena juu ya mateso yake yatakayoompata (Isaya 53), nazo pia zikaonekana pengine ni habari tu, lakini wakati ulipofika, hayo yote kutimia kwa ufasaha wote, ndipo wakajua kuwa Neno la Mungu huwa halipiti.
Isaya huyo huyo aliyetabiri ujio wa Kristo kwa uvuvio wa Roho, ni huyu huyu alioonyeshwa pia hatma ya huu ulimwengu utakavyokuja kuwa siku za mwisho, na habari zake kaziandika sehemu nyingi sana kwenye kitabu hicho chenye sura 66, alionyeshwa jinsi hii dunia itakavyokwenda kuwa utupu, na kuharibiwa kabisa, jinsi jua litakavyotiwa giza, jinsi watu watakavyoadimika kama dhahabu duniani, na kibaya zaidi alionyeshwa fedha ya mtu wakati huo haitafanya kazi yoyote, umaarufu wa mtu utakuwa hauna maana, biashara za mtu zitakuwa ni kama takatakata, elimu ya mtu haitafanya kazi..tajiri na maskini wote watakuwa wakiomboleza sawa.
Na nyakati zenyewe ndio hizi tunazoishi mimi na wewe, kila mtu analijua hilo, hata ukimuuliza mtoto mdogo atakuambia, hizi ni nyakati za mwisho, watu wengi wanaposikia maneno haya wanapuuzia wakidhani hichi ni kama kile kipindi cha mitume..Ndugu hichi sio kipindi cha mitume.. Fuatilia mambo yanayoendelea duniani hata kupitia mitandao ndipo utakapojua kuwa tunaishi nyakati nyingine.
Bwana Yesu alisema hivi..
“Basi kwa mtini jifunzeni mfano; tawi lake likiisha kuchipuka na kuchanua majani, mwatambua ya kuwa wakati wa mavuno u karibu; 33 nanyi kadhalika, myaonapo hayo yote, tambueni ya kuwa yu karibu, milangoni. 34 Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia” (Mathayo 24:32).
“Basi kwa mtini jifunzeni mfano; tawi lake likiisha kuchipuka na kuchanua majani, mwatambua ya kuwa wakati wa mavuno u karibu;
33 nanyi kadhalika, myaonapo hayo yote, tambueni ya kuwa yu karibu, milangoni.
34 Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia” (Mathayo 24:32).
Sasa kama wewe ni msomaji wa Biblia utajua kuwa Mtini unafananishwa na Taifa la Israeli (Yeremia 24), na wakati ule Israeli ilikuwa bado haijachipua (yaani haijawa taifa), ilipitia miaka zaidi ya 2,500 tangu wachukuliwe utumwani Babiloni, na ulipofika mwaka 1948, Israeli ikachipuka tena na kuwa taifa kwa mara ya kwanza,..Na tunajua kabisa agenda ya Mungu ya wokovu itamalizia tena na Israeli pale Yerusalemu.
Hivyo tangu huo wakati Bwana alisema kizazi hiko, (yaani kilichoshuhudia Israeli kuchupuka tena), hakitapita mpaka hayo yote, kutimia,..Mambo yote aliyoyazungumzia katika Mathayo 24, hadi kurudi kwa pili kwake,..Na kizazi huwa hakizidigi miaka 120, sasa piga hesabu hapo, tunaishi katika wakati gani.. (Hatujui siku wala saa lakini tunayajua majira).
Sikuzote, kiwango chako cha maarifa kuhusu Mungu, ndio kinachoelezea maisha ya kiroho unayoishi sasa hivi, kama jicho lako bado halioni kuwa tunaishi katika majira ya unyakuo, na kwamba huu ndio ule wakati ambapo watu watadhanishia mbona ni amani, na salama, na kumbe ule uharibifu unakuja kwa ghafla (1Wathesalonike 5:3)..Kama ilivyokuja Corona kwa ghafulani pasipo ulimwengu kujiandaa…Ndicho kitakachoitokea dunia kipindi sio kirefu.
Sijui kama hilo unalijua ndugu yangu, kanisa hili linaitwa Laodikia, (Sio dhehebu linaloitwa Laodikia! Hapana!..Bali ni hali ya kanisa kwa ujumla inayofananishwa na Kanisa la Laodikia la Nyakati za kwanza, kasome Ufunuo 3:14), na ndio kanisa la mwisho la 7, na hakutakuwa na kanisa lingine baada ya hili, niambie ni dalili ipi ambayo haijatimia Yesu aliyoirodhesha kwenye Mathayo 24.
Internet imeweza kurahisisha mambo, siku hizi haihitaji mtu aende tena kwenye mikutano ya Injili asikie mahubiri, pale pale alipo hata kama ni kijijini akiwa chumbani mwake Injili inamfikia, utasema Injili haijahubiriwa dunia nzima leo?..
Shetani anataka watu waendelee kufikiria hivyo hivyo, kwamba bado sana, anataka watu waangalie upepo wa dunia unavyokwenda, lakini wasiangalie biblia inasema nini kuhusu siku hizi. Usipokuwa mvivu kusoma biblia ndipo utakapojua ni kwa jinsi gani tunaishi katika nyakati za hatari kushinda zote ambazo zilishawahi kupita katika historia.
Hivyo huu ni wakati wa kuamka usingizini..
Waefeso 5:14 “Hivyo husema, Amka, wewe usinziaye, Ufufuke katika wafu, Na Kristo atakuangaza”.
Kama bado hujaokoka, au umeokoka lakini bado mguu mmoja nje mwingine ndani, Embu anza, kuyaangalia upya maisha yako ya rohoni ndugu, Je! Yesu amekuokoa kweli kweli? Kama sio, basi huu ndio wakati, na sio kesho, unachopaswa kufanya ni kuamua kutubu dhambi zako kwa kumaanisha kuziacha na kutozifanya tena, na kisha kwenda kubatizwa katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji tele (Yohana 3:23), na kwa jina la YESU KRISTO sawasawa na Matendo 3:38,8:16 na 10:48 Upate ondoleo la dhambi zako.(Maagizo hayo ni muhimu sana!). Na Roho Mtakatifu atakuongoza katika kuyaelewa maandiko.
Na kuanzia hapo, anza kuishi maisha ya kama mtu unayemngojea Bwana Yesu kwasababu nyakati hizi, sio za kubembeelezewa wokovu tena, ni kubutuka haraka na kuishindania Imani.
KUOTA UNAKOJOA KITANDANI.
MAMBO MENGINE HAYATOKI ISIPOKUWA KWA KUFUNGA.
NI WAKATI WA KUJIPIMA, WEWE KAMA MTUMISHI WA MUNGU!
NA MTU MMOJA AKAVUTA UPINDE KWA KUBAHATISHA, AKAMPIGA MFALME
MISTARI YA BIBLIA YA UPONYAJI.
MANA ILIYOSHUSHWA KUTOKA MBINGUNI.