Category Archive Home

Mbinguni ni sehemu gani?

JIBU: Ili tusichanganyikiwe jambo la muhimu  tulinalopaswa kujua ni kuwa Katika biblia Neno “mbinguni” limetumika kuwakilisha sehemu tofauti tofauti tatu.

Sehemu ya kwanza ni anga hili ambalo lipo juu yetu: Ambalo ndilo hili tunaloliona lenye nyota, mawingu, mwezi jua na sayari, ambalo ndege wote wa angani wanaruka na kufurahia, biblia imelitaja kama mbingu..Tunasoma..

Isaya 55:10 “Maana kama vile mvua ishukavyo, na theluji, kutoka mbinguni, wala hairudi huko; bali huinywesha ardhi, na kuizalisha na kuichipuza, ikampa mtu apandaye mbegu, na mtu alaye chakula;

11 ndivyo litakavyokuwa neno langu, litokalo katika kinywa changu; halitanirudia bure, bali litatimiza mapenzi yangu, nalo litafanikiwa katika mambo yale niliyolituma.”

Luka 17:24 “kwa kuwa, kama vile umeme umulikavyo toka upande huu chini ya mbingu hata upande huu chini ya mbingu, ndivyo atakavyokuwa Mwana wa Adamu katika siku yake”.

Sehemu ya Pili ya mbingu ni makao ya Mungu yalipo: Na hii ipo katika Roho, sehemu ambayo Mungu na malaika zake wanaishi, hatuwezi kuiona kwa jicho la kibinadamu wala hatuwezi kufika huko kwa kifaa chochote cha kibinadamu, lakini ni mahali halisi kabisa. Tiketi ya pekee ya kufika huko biblia inatuambia ni Yesu Kristo tu, Na hii mbingu ni pana sana ndio imejumuisha ile mbingu mpya na nchi mpya ambayo itakuja kuwa ni makao ya watakatifu baadaye, pamoja na ile paradiso (peponi) kule ambapo wale wote waliokufa zamani na wanaokufa sasa hivi katika Kristo wanahifadhiwa kwa muda wakisubiria ufufuo siku ile ya Unyakuo ili kwa pamoja waingie katika makao ya Mungu mwenyewe yaliyo juu sana na ndio maana utaona mtume Paulo alinyakuliwa mpaka mbingu ya Tatu, mbingu hii ya tatu ni hiyo ya makao ya Mungu mwenyewe,  akaonyeshwa sehemu ya maono ya huko, na kusema mambo yaliyo huko hayajuzu hata mwanadamu kuyatamka,(2Wakorintho 12:2-4). na ndiko watakatifu waliokombolewa watakapokwenda siku ile ya Unyakuo itakapofika, ni mahali patakatifu na pasafi ambapo mtu yeyote mchafu hataingia..

1Wafalme 8:27 “Lakini Mungu je? Atakaa kweli kweli juu ya nchi? Tazama, mbingu hazikutoshi, wala mbingu za mbingu; sembuse nyumba hii niliyoijenga!”

1Timotheo 6:16 “ambaye yeye peke yake hapatikani na mauti, amekaa katika nuru isiyoweza kukaribiwa; wala hakuna mwanadamu aliyemwona, wala awezaye kumwona. Heshima na uweza una yeye hata milele. Amina.”

Na sehemu ya tatu biblia inapataja kama mbinguni ni mahali pa juu sana, makao ya juu sana: Mahali ambapo Mungu pekee ndiye anayestahili kuwepo, jambo ambalo hata hapa duniani linaweza kufikiwa,

Watu walio ndani ya Yesu, ambao wameokoka kikamilifu kwa kumwamini Yesu na kubatizwa, katika ulimwengu wa roho, ni sawa na wameketi pamoja na Kristo mbinguni..

Waefeso 2:5 “hata wakati ule tulipokuwa wafu kwa sababu ya makosa yetu; alituhuisha pamoja na Kristo; yaani, tumeokolewa kwa neema.

6  Akatufufua pamoja naye, akatuketisha pamoja naye katika ulimwengu wa roho, katika Kristo Yesu;”

Kadhalika pia, Ufalme wowote au mtu yeyote anayetafuta kuinuliwa ziadi ya vitu vingine vyote huyo katika roho anaonekana anakipandia cheo cha Mungu kilipo, na Mungu yupo mbinguni, hivyo anaonekana kama amefika mbinguni.

Danieli 4:19 “Ndipo Danieli, aliyeitwa jina lake Belteshaza, akashangaa kwa muda, na fikira zake zikamfadhaisha. Mfalme akajibu akasema, Ee Belteshaza, ndoto ile isikufadhaishe wala tafsiri yake. Belteshaza akajibu, akasema, Bwana wangu, ndoto hii iwapate wao wakuchukiao, na tafsiri yake iwapate adui zako.

20 Ule mti uliouona, uliokua, ukawa na nguvu, urefu wake ukafika mpaka mbinguni, na kuonekana kwake mpaka dunia yote;

21 ambao majani yake yalikuwa mazuri, na matunda yake mengi, na ndani yake chakula cha kuwatosha wote; ambao chini yake wanyama wa kondeni walikaa, na ndege wa angani walikuwa na makao yao katika matawi yake;

22 ni wewe, Ee mfalme, uliyekua, na kupata nguvu; maana ukuu wako umekua na kufika mpaka mbinguni, na mamlaka yako yamefika mpaka mwisho wa dunia.

Mathayo 11:23 “Nawe Kapernaumu, je! Utakuzwa mpaka mbinguni? Utashushwa mpaka kuzimu; kwa kuwa kama miujiza iliyofanyika kwako ingalifanyika katika Sodoma, ungalikuwapo mji huo hata leo.”

Isaya 14:12 “Jinsi ulivyoanguka kutoka mbinguni, Ewe nyota ya alfajiri, mwana wa asubuhi! Jinsi ulivyokatwa kabisa, Ewe uliyewaangusha mataifa!

13 Nawe ulisema moyoni mwako, Nitapanda mpaka mbinguni, Nitakiinua kiti changu juu kuliko nyota za Mungu; Nami nitaketi juu ya mlima wa mkutano, Katika pande za mwisho za kaskazini.

14 Nitapaa kupita vimo vya mawingu, Nitafanana na yeye Aliye juu.

15 Lakini utashushwa mpaka kuzimu; Mpaka pande za mwisho za shimo”.

Hivyo kwa vyovyote vile, tunapaswa tujitahidi ili tufike huko, si kwa kujiinua tukiyatumainia haya Maisha, bali kwa kupitia Yesu Kristo, kwasababu biblia inasema mambo tuliyoandaliwa huko, jicho halijawahi kuona wala sikio kusikia.

Ubarikiwe.


Mada Nyinginezo:

JE! NI KWELI DUNIA ILIUMBWA TAKRIBANI MIAKA 6000 ILIYOPITA? NA JE! SHETANI ALIKUWEPO DUNIANI WAKATI DUNIA INAUMBWA?

TUMEAMBIWA TUNAPOSALI TUSIPAYUKE-PAYUKE, JE! HUKO KUPAYUKA PAYAUKA NDIO KUPI?

JE! KUNA DHAMBI KUBWA NA NDOGO?

NI NANI ANAYETAWALA DUNIA KATI YA MUNGU NA SHETANI?.


Rudi Nyumbani:

Print this post

JE BIKIRA MARIAMU ALIZAA WATOTO WENGINE?

Biblia imeweka wazi kuwa Mariamu, mama yake Yesu alikuwa na watoto wengine..

Mathayo 13:53 “Ikawa Yesu alipoimaliza mifano hiyo, alitoka akaenda zake.

54 Na alipofika nchi yake, akawafundisha katika sinagogi lao, hata wakashangaa, wakasema, Huyu amepata wapi hekima hii na miujiza hii?

55 Huyu si mwana wa seremala? Mamaye si yeye aitwaye Mariamu? Na nduguze si Yakobo, na Yusufu, na Simoni, na Yuda?

56 Na maumbu yake wote hawapo hapa petu? Basi huyu amepata wapi haya yote?

57 Wakachukizwa naye. Yesu akawaambia, Nabii hakosi kupata heshima, isipokuwa katika nchi yake, na nyumbani mwake mwenyewe”. 

Maumbu kama inavyosomeka kwenye mstari wa 56, maana yake ni ndugu wa ‘KIKE’ (madada)..Kwahiyo Mariamu alikuwa ana watoto wengine wakiume na wakike.


Mada Nyinginezo:

SAYUNI NI NINI?

NI HALALI KUBATIZA WATOTO WADOGO?

KUNA HUKUMU ZA AINA NGAPI?

SABATO HALISI NI LINI, JE! NI JUMAPILI AU JUMAMOSI?, NI SIKU GANI ITUPASAYO KUABUDU?

MUNGU ALIKUWA ANAONGEA NA NANI ALIPOSEMA NA “TUMFANYE MTU KWA MFANO WETU”,(MWANZO 1:26)?


Rudi Nyumbani:

Print this post

JE BIKIRA MARIAMU ALIKUFA?

Hakuna mahali popote Biblia imerekodi kifo cha Mariamu, wala  hakuna  mahali popote Biblia imerekodi kifo cha Mtume Petro, wala Yusufu mume wake Mariamu, wala Mtume Paulo, wala Mtume Adrea wala Tomaso, Nathanieli, n.k…manabii wengi sana na mitume vifo vyao havijarekodiwa kwenye Biblia takatifu..

Na ni kwanini biblia havijarekodi vifo vya hawa watu, ni kwasababu sio vitu vya muhimu sana kuvijua kwetu sisi…Inatusaidia nini sisi kujua Petro alikufa mwaka gani? au mwezi gani?.. unaona haitusaidii chochote! Lakini tunajua kuwa Petro alikufa, Paulo alikufa, Yusufu alikufa…kadhalika na Bikira Mariamu alikufa vile vile.

Mariamu hakuwa mtu wa tofauti sana na watu wengine…Eliya ambaye hakufa bali  alipaa, Biblia inamtaja kuwa mtu wa mwenye tabia sawa na sisi, (soma Yakobo 5:17) itakuwaje Mariamu ambaye hakupaa?..Ni mmoja tu ndiye aliyekuwa wa kipekee ambaye biblia inasema alikufa na kufufuka na akapaa mbinguni, na huyo ni Yesu Pekee yake, ndio maana wokovu upo kwake. Kulikuwa hakuna haja ya kuja Bwana Yesu kama Mariamu alikuwa na wokovu .

Hivyo kwa hitimisho ni kwamba Mariamu alikufa kama watu wengine.


Mada Nyinginezo:

JE MARIAMU NI NANI?

JE! NI SAHIHI KUMUITA MARIA MAMA WA MUNGU?

JE! BIKIRA MARIA NI MALKIA WA MBINGUNI?

KWANINI MUNGU AWACHOME WATU KWENYE ZIWA LA MOTO NA HALI YEYE NDIYE ALIYEWAUMBA?


Rudi Nyumbani:

Print this post

JE NI KWELI BWANA YESU SIKU YA KURUDI ATAFIKIA ISRAEL

Jambo moja linalowachanga watu wengi wa Mungu, ni kutokujua Ujio wa Yesu utakuwaje.

Ujio wa Bwana Yesu umegawanyika katika sehemu kuu 3. nazo ni UJIO WA KWANZA, UJIO WA PILI na UJIO WA TATU.

UJIO WA KWANZA: Ni wakati Bwana Yesu alipozaliwa na Bikira Mariamu, na kuifanya kazi yake kwa miaka mitatu na nusu, na kufa, na kufufuka, kisha kurudi mbinguni alikotoka. Huo ulikuwa ni ujio wa kwanza.

UJIO WA PILI: Utakuwa ni wakati wa unyakuo…Ujio huu hautahusisha Bwana kushuka kabisa duniani, bali Bwana atakuja na ataishia mawinguni, sisi tulio hai tutaungana pamoja na wale waliokufa katika Kristo, kwa pamoja tutanyakuliwa kwenda kumlaki mawinguni, na kwenda mbinguni kwenye karamu yake aliyotuandalia, (1 Wathesalonike 4) ambapo huko tutakaa kwa muda wa miaka 7…

UJIO WA TATU: Utahusisha Bwana kurudi  tena na watakatifu wake duniani walionyakuliwa, atakuja duniani kwa ajili ya Hukumu ya Mataifa,  Vita ya Harmagedon, pamoja na kuanzisha utawala mpya duniani wa Amani utakaodumu kwa miaka 1000. Ujio huu ndio kila jicho litamwona akija wa majeshi ya mbinguni..Na atashukia Israeli. Hapo ndio yatakuwa makao yake makuu kipindi cha utawala wake duniani.

Kwa urefu wa ujio huo pitia somo hapa chini linalosema UTAWALA WA MIAKA 1000.


Mada Nyinginezo:

UTAWALA WA MIAKA 1000.

KATI YA UNYAKUO WA KANISA, DHIKI KUU, VITA VYA HAR-MAGEDONI, UTAWALA WA MIAKA 1000, VITA YA GOGU NA MAGOGU, HUKUMU YA KITI CHA ENZI CHEUPE. JE, NI KIPI KINAANZA NA KINGINE KUFUATA?

NAMNA YA KUITAMBUA SAUTI YA MUNGU INAPOZUNGUMZA NA WEWE


Rudi Nyumbani:

Print this post

Jehanamu ni nini?

Jehanamu au Jehanum ni Neno lenye chimbuko la  kiyunani Gehenna, ambalo limetafsiriwa kutoka katika lugha ya kiyahudi ge-hinnom Ikiwa na maana bonde la mwana wa Hinomu.. Hili ni eneo lililokuwa kusini mwa mji wa Yerusalemu, lililojulikana kama Tofethi ambao watu wasiokuwa wanamcha Bwana  walikuwa wanalitumia kuwatolea watoto wao kafara kwa kuwapitisha motoni kwa miungu waliyoikuta huko Kaanani. Jambo ambalo lilikuwa ni chukizo kubwa sana kwa Mungu, ambalo nalo pia lilikuwa ni mojawapo  ya mambo yaliyowafanya wachukuliwe utumwani Babeli.

JEHANUM NDANI YA BIBLIA

Tunasoma hayo katika..

Jeremia 7:30 “Maana wana wa Yuda wametenda yaliyo maovu machoni pangu, asema Bwana; wameweka machukizo yao ndani ya nyumba hiyo, iitwayo kwa jina langu, hata kuitia unajisi.

31 Nao wamepajenga mahali palipoinuka pa Tofethi, palipo katika bonde la mwana wa Hinomu, ili kuwateketeza wana wao na binti zao motoni; jambo ambalo mimi sikuliagiza, wala halikuingia moyoni mwangu.”

Yeremia 19:1 “Bwana akasema hivi, Enenda ukanunue gudulia la mfinyanzi, ukachukue pamoja nawe baadhi ya wazee wa watu, na baadhi ya wazee wa makuhani;

2 ukatoke uende mpaka bonde la mwana wa Hinomu lililo karibu na mahali pa kuingia kwa lango la vigae, ukahubiri huko maneno nitakayokuambia,

3 ukisema, Lisikieni neno la Bwana, enyi wafalme wa Yuda, na wenyeji wa Yerusalemu; Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli asema hivi, Angalieni, nitaleta mabaya juu ya mahali hapa, ambayo mtu ye yote akisikia habari yake, masikio yake yatawaka.

4 Kwa sababu wameniacha mimi, nao wamepafanya mahali hapa kuwa mahali pageni, nao hapa wamewafukizia uvumba miungu mingine wasiowajua, wala wao, wala baba zao, wala wafalme wa Yuda; nao wamepajaza mahali hapa damu ya wasio na hatia;

5 nao wamemjengea Baali mahali pake palipo juu, ili kuwachoma moto wana wao, wawe sadaka za kuteketezwa kwa Baali; tendo nisiloliamuru mimi, wala kulinena, wala halikuingia moyoni mwangu;

6 basi, angalieni, siku zinakuja, asema Bwana, ambazo katika siku hizo mahali hapa hapataitwa tena Tofethi, wala Bonde la mwana wa Hinomu, bali, Bonde la Machinjo.”

Lakini baadaye tunaona Mfalme Yosia alikuja kulinajisi eneo hilo , likawa halitumiki tena kufanya mambo yao ya kichawi,

2Wafalme 23:10 “Naye akainajisi Tofethi, iliyomo katika bonde la wana wa Hinomu, ili mtu asipitishe mwana wake au binti yake motoni kwa Moleki.”

 likabakia kutumika kama dampo la jiji, na bonde la kutupia miili ya watu waovu, pamoja na wanyawa waliokufa pamoja na kuchoma takataka na kila aina ya uchafu wote uliotoka mjini..Na hiyo ilipelekea bonde hilo kuwa la kinyaa sana na wakati wote kuwa linawaka moto, na moshi mkubwa unaopanda juu pamoja na harufu kali sana, kutokana na kwamba kila wakati uchafu ulikuwa unaingia..

FUNZA WA JEHANAMU

Sasa zile sehemu ambazo moto ulikuwa haufiki vizuri, kulikuwa na funza wengi sana, ambao walipita katikati ya mizoga ile iliyokuwa imetupwa, ni eneo ambalo hakuna mtu angeweza kukaa hata dakika mbili au kusogea karibu na ukawa sawa. Kama ulishawahi kuona jalala kuu la manispaa au jiji basi fahamu kuwa huo ni mfano mdogo sana ukilinganisha na GEHENA ilivyokuwa..bonde hilo lilikuwa linatisha sana. Funza wa jehanamu walikuwa ni wagumu kufa kwasababu walikuwa ni tofauti na funza wengine.

Na ndio maana Bwana YESU alitumia mfano huo, kueleza picha halisi ya kuzimu ilivyo kwa wale ambao watakufa katika dhambi zao. Alisema..

Marko 9:43 “Na mkono wako ukikukosesha, ukate; ni afadhali kuingia katika uzima u kigutu, kuliko kuwa na mikono miwili, na kwenda zako jehanum, kwenye moto usiozimika;

44 ambamo humo funza wao hafi, wala moto hauzimiki.] 9.45 Na mguu wako ukikukosesha, ukate; ni afadhali kuingia katika uzima, u kiwete, kuliko kuwa na miguu miwili, na kutupwa katika jehanum; [

46 ambamo humo funza wao hafi, wala moto hauzimiki.]

47 Na jicho lako likikukosesha, ling’oe, ulitupe; ni afadhali kuingia katika ufalme wa Mungu, una chongo, kuliko kuwa na macho mawili, na kutupwa katika jehanum;

48 ambamo humo funza wao hafi, wala moto hauzimiki.”

Ni wazi kuwa hakuna mtu anayependa kuwepo sehemu yeyote chafu, basi hiyo inatupa chachu pia tujiepusha na kuzimu kwasababu kuzimu ipo kweli na si mahali pazuri hata kidogo huko hakuna raha, ukishajikuta kule, utakuwa katika mateso siku zote ukisubiria hukumu ya siku za mwisho kabla ya kutupwa katika lile ziwa la moto..

JE UPO NJE YA KRISTO AU NDANI YA KRISTO?

Kama upo nje ya Kristo, wakati ndio huu, tubu sasa, mpe Bwana maisha yako naye atakupokea..Na kukusamehe kabisa, kwasababu mbingu amekuandalia wewe, hivyo daima hataki nafasi yako ipotee.

Ubarikiwe.

 
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

BWANA ALIMAANISHA NINI KUSEMA “WAACHE WAFU WAZIKE WAFU WAO?.

MADHARA YA KUKOSA MAJI YA UZIMA BAADA YA KIFO.

NOTI YA UFALME WA MBINGUNI.

KUNA UFUFUO WA AINA NGAPI?

CHANZO CHA MAMBO.

NGUVU YA UPOTEVU.


Rudi Nyumbani:

Print this post

KANISA NI NINI?

Kanisa ni nini?..kanisa la Mungu ni kitu gani?

hili ni swali linalowachanganya watu wengi ikidhaniwa kuwa Kanisa ni  jengo. Lakini hiyo sio maana halisi ya kanisa. Neno kanisa limetokana na Neno la kiyunani EKKLESIA, ikimaanisha “walioitwa”, Enzi za Agano jipya kasanyiko lolote la wakristo(yaani hao walioitwa) lilijulikana kama kanisa..Na kusanyiko hilo liliweza  kuanzia watu wawili au watu, kufuatana na maneno ya Yesu Kristo mwenyewe aliyosema katika..

Mathayo 18:20 “Kwa kuwa walipo wawili watatu wamekusanyika kwa jina langu, nami nipo papo hapo katikati yao.”

Hivyo ilifahamika kuwa mahali popote walipokusanyika watu waliomwamini Kristo  iwe ni nyumbani, au hekaluni, au kwenye sinagogi, au popote pale kwa jina lake kutokujali mazingira yazungukayo basi hilo tayari ni kanisa.

Wagalatia 1:13 “Maana mmesikia habari za mwenendo wangu zamani katika dini ya Kiyahudi, kwamba naliliudhi kanisa la Mungu kupita kiasi, nikaliharibu”

Umeona?..Sentensi hiyo haioneshi kanisa kama jengo bali “wakristo” Paulo ndio aliowaudhi na kuwaharibu..Kwahiyo kanisa ni nini? Ni mkusanyiko wa watu walioitwa (au kwa lugha rahisi wakristo)

Hivyo kwa ufupi, mkusanyiko wowote usio wa kikristo, yaani usio usiomtambua Kristo kama kichwa cha kusanyiko hilo haijalishi ni mkubwa kiasi gani, haijalishi upo kwenye jengo lenye misalaba mingi kiasi gani, haijalishi linafuata utaratibu mzuri kiasi gani, hilo sio kanisa kibiblia. Ni sawa na mwili ambao hauna kichwa, ni mfu, vivyo hivyo na mkusanyiko wowote  usio na Kristo hauwezi kuwa ni Kanisa.

Waefeso1:20 “aliotenda katika Kristo alipomfufua katika wafu, akamweka mkono wake wa kuume katika ulimwengu wa roho;

21 juu sana kuliko ufalme wote, na mamlaka, na nguvu, na usultani, na kila jina litajwalo, wala si ulimwenguni humu tu, bali katika ule ujao pia;

22 akavitia vitu vyote chini ya miguu yake, akamweka awe kichwa juu ya vitu vyote kwa ajili ya kanisa; ambalo

23 ndilo mwili wake, ukamilifu wake anayekamilika kwa vyote katika vyote.”

AMEN.

Kwa Maswali, Maombezi, Ushauri, au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba hizi

+225693036618/ +225789001312

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

WALIPO WAWILI AU WATATU KWA JINA LANGU.

NYAKATI SABA ZA KANISA NA WAJUMBE WAKE.

AGENDA KUBWA YA SHETANI KWA KANISA HILI LA LAODIKIA.

SIRI YA KUASI KATIKA KANISA LA MUNGU.

MADHARA YA KUKOSA MAJI YA UZIMA BAADA YA KIFO.

UNYAKUO.

JE KUJIUA NI DHAMBI?

Rudi Nyumbani:

Print this post

JE! UNAYO NAFASI MBINGUNI?

Umewahi kujiuliza kwanini Bwana Yesu alisema, Anakwenda kutuandalia makao? (Yohana 14:2), Na kwanini mbinguni kunafananishwa na karamuni?…Ni dhahiri kuwa utaratibu wa maandalizi ya karamu unafanana sana na utaratibu wa kuingia mbinguni. Kwahiyo tukizijua tabia za karamu ndio tutajua mbinguni kutakuwaje!

Kwanza Karamu ni lazima iandaliwe, siku gani itafanyika na wapi itafanyikia, na ni lazima iandaliwe kwa kupambwa vizuri, ni lazima pia iwe na vyakula na vinywaji, na ni lazima iwe na ndugu waalikwa…sherehe isiyokuwa na watu hiyo sio sherehe….

Na karamu kama Harusi sio ruhusa kila mtu kuingia, isipokuwa walioalikwa tu! Na ni kwanini sio watu wote wanaruhusiwa kuingia karamuni?..Ni kwasababu ya bajeti!…Waliochangia mara nyingi ndio wanaopewa kadi ya mwaliko. Na sherehe nyingi siku chache kabla ya tukio lenyewe, kadi zote zinakuwa zimeshagawiwa kwa wahusika, na hivyo hakuna nafasi tena ya mtu mwingine kuingia, Idadi ya viti imehesabiwa na Idadi ya watu imeshajulikana, mwingine yeyote akitaka kujichomeka kwenye karamu ile, siku ya Harusi atazuiliwa mlangoni…Na sababu ya kuzuiliwa mlangoni sio kwamba ni kwasababu anachukiwa, au kwasababu ni mtu mbaya sana hapana! Sababu pekee ni kwasababu nafasi yake haipo kwenye karamu hiyo, na hiyo inatokana na pengine hakuchangia, na hivyo akakosa kadi, na hata akiingia nafasi ya kiti hatapata humo ndani kwasababu Kila kitu kipo kwenye mahesabu, hivyo ataishia kuvuruga tu karamu badala ya kuipendezesha.

Kwasababu uwepo wa hiyo karamu ni kutokana na michango ya waalikwa..Gharama zote zimetokana na michango ya waalikwa.

Na katika ufalme wa Mbinguni ni hivyo hivyo… Ufalme wa Mbinguni unajengwa na michango ya Watakatifu. Bwana alipokwenda mbinguni yeye ni kama Mwana-kamati Mkuu, na Mkuu wa Sherehe..Gharama zote za maandalizi, zinatokana na Maisha ya watakatifu huku ulimwenguni…Kila atakayechangia gharama hizo, ndivyo anavyojiwekea nafasi nzuri ya kuwepo ndani ya ile karamu Mbinguni. Ndio maana Bwana Yesu mwenyewe alisema…

Mathayo 11: 12 “Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatikana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka”. Kwahiyo kama tunasubiri unyakuo wa ghafla, na hakuna chochote tunafanya kwa ajili ya ufalme wa mbinguni, hicho kitu tuondoe kwenye akili..Watakaonyakuliwa ni wale tu watakaoalikwa, na walioalikwa ni wale waliochangia kitu katika ufalme wa Mbinguni.

Sasa tutachangiaje katika Ufalme wa Mbinguni ili tuweze kuuingia?

Biblia inasema katika kitabu cha Luka..

Luka 10:25 “Na tazama, mwana-sheria mmoja alisimama amjaribu; akisema, Mwalimu, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?

26 Akamwambia, Imeandikwa nini katika torati? Wasomaje?

27 AKAJIBU AKASEMA, MPENDE BWANA MUNGU WAKO KWA MOYO WAKO WOTE, NA KWA ROHO YAKO YOTE, NA KWA NGUVU ZAKO ZOTE, NA KWA AKILI ZAKO ZOTE; NA JIRANI YAKO KAMA NAFSI YAKO.

28 Akamwambia, Umejibu vema; fanya hivi nawe utaishi”

Kwahiyo Mchango mkubwa unaohitajika ili kujitengenezea nafasi katika Ufalme wa Mbinguni NI UPENDO WA MUNGU NA WA NDUGU..HIZO NDIZO TIKETI!.

Kumpenda Mungu kwa Nguvu zetu zote maana yake unatumia nguvu zako za mwilini na rohoni kutimiza mapenzi ya Mungu..Nguvu zako za ujana ambazo ungepeleka kutatufa mambo ya ulimwengu huu, unazitumia kumtafuta Mungu, Nguvu zako zote unazipeleka katika kuhubiria wengine injili, nguvu zako za kuimba, za kucheza, za kusoma..unazitumia kumwimbia Mungu, kumchezea Mungu, kusoma Neno la Mungu….. wakati huu ambao unaweza kutembea, kukimbia..Ndio wakati wa kukimbia kwenda kuihubiri Injili, wakati huu ambao mwili wako una nguvu na afya, ndio wakati wa kufunga, na kuomba katika kumtafuta Mungu.

Na inaposema Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, maana yake unampenda pasipo unafiki, Unapompenda mtu kwa moyo, huwezi kumuumiza, utajitoa kwake kwa kila kitu, huwezi kufanya jambo ukitazamia malipo, na unapofanya jambo kwa moyo siku zote huwezi kufanya kwa kulazimishwa kwasababu unafanya kwa moyo…. kadhalika tunapaswa tumpende Mungu kwa moyo, ikiwa na maana kuwa hatupaswi kumtafuta kwa kulazimishwa lazimishwa, wala hatutakiwi kufanya kazi yake kwa kusukumwasukumwa..walata hatutakiwi tumtafute kwasababu tunataka fedha kutoka kwake, au tunataka utajiri kutoka kwake, tunamtafuta kwasababu tunampenda kutoka moyoni, kwasababu yeye ni Mungu wetu, na tukimpenda kwa Namna hiyo atahakikisha anatutimizia mahitaji yetu pasipo hata sisi kumwomba kwani anajua tunayohitaji kabla hata hatujamwomba..

Tatu, tunapaswa tumpende Mungu kwa Akili zetu zote, Maana ya kumpenda Mungu kwa akili maana yake ni kutumia akili katika kumtafuta na kumtumikia Mungu..Na akili hiyo inatokana na kulinganisha mambo, unajifunza kuweka mambo mawili kwenye mizani na kuchagua moja lililo na uzito..Kwamfano kununua kiatu cha laki moja na huku huna biblia mkononi, huko ni kutotumia akili, kutokusoma Neno kwasababu huna Biblia na huku una smartphone mkononi mwako, huko pia ni kutokumia akili, kwasababu ungeweza kusoma kwa kutumia hata hiyo hiyo simu yako ya mkononi.. Kushindwa kumjua Mungu kwasababu tu hujakutana na mhubiri wa kukuhubiria barabarani, huko pia ni kutokutumia akili, kwasababu ungeweza kutumia simu yako hiyo hiyo kupata mafundisho yoyote yamhusuyo Kristo katika Mtandao. Kwahiyo kwa ulegevu kama huo unaweza kusababisha kukosa nafasi katika karamu ile.

Na tiketi ya nne ni kumpenda Mungu kwa roho yako yote. Kumpenda kwa roho ni Zaidi ya kumpenda kwa moyo, kwa roho maana yake unampenda mtu kwa utu wa ndani kabisa, (Utu wa Ndani unahusisha Ibada), ukimpenda mtu kwa moyo unakuwa humwabudu, lakini ukimpenda kwa roho ni unafikia kiwango cha kumwabudu….unakuwa tayari kufa hata kwaajili yake na kwaajili ya Injili, unakuwa na shauku ya kumwona Mungu, unakuwa na shauku ya kumwabudu na unakuwa pia na shauku ya kumaliza kazi ya Mungu kwa gharama yoyote ile ili ukamwone uso kwa uso. Kila siku unafikiria namna ya kuimaliza kazi ya Mungu kama alivyokuwa Bwana.

Na mwisho kabisa ni kuwapenda majirani zetu kama nafsi zetu..kama vile unavyojipenda wewe, hakuna hata siku moja umefikiria kujilipizia kisasi au kujisengenya mbele ya mwingine, au kujiangamiza mwenyewe vivyo hivyo tunapaswa tuwapende wale wanaotuzunguka kwa upendo wa viwango hivyo hivyo.

Vigezo hivyo vitano ndivyo vinavyotumika kuandaa nafasi za Wateule karamuni, mambo hayo 5 ndio kadi ya mwaliko…Kila mmoja, haijalishi ni Mtume,mchungaji, mwalimu, mwinjilisti, mwimba kwaya,Nabii, mpiga gitaa kanisani, au msafisha choo cha kanisa, au mtunza bustani wa kanisa…ni Lazima afanye mambo hayo ili aurithi uzima wa milele, ili aingie karamuni…Vigezo hivyo vitano ndio vinavyotumika kutengeneza kadi ya mwaliko wa kuingia kwenye mji ule.

Ndio maana Bwana Tangu wakati ule mpaka leo bado anaandaa makao…kila kizazi watu watu wajiingiza kwa nguvu, wanatengeneza tiketi zao na kujitwalia nafasi. Kila kizazi watu wanajiingiza kwa nguvu…Hakuna nafasi za watu wasiojishughulisha na ufalme wa Mbinguni.

Luka 16:16 “Torati na manabii vilikuwapo mpaka Yohana; tangu wakati huo habari njema ya ufalme wa Mungu hutangazwa, na kila mtu hujiingiza kwa nguvu”.

Je! Na wewe umealikwa?..Unayo Kadi yako mkononi? Unayo nafasi katika ufalme wa Mbinguni? Umeingia kwa nguvu? Au unaendelea na matendo mabaya ya giza na huku unasubiria unyakuliwe?.. Biblia inasema pia waovu wana sehemu yao katika lile ziwa la moto, ikiwa na maana kuwa, hata kuzimu nako watu wanajitengenezea nafasi zao kule kuanzia sasa.

Ufunuo 21:8 “ Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili”.

Kama hujampa Kristo masha yako, mlango upo wazi sasa, Lakini upo karibuni kufungwa, karamu inakaribia kuanza, fanya hima upate kadi ya mwaliko, kwa kutubu dhambi zako zote, kubatizwa na kuishi kwa vigezo hivyo vitano hapo juu.

Bwana akubariki sana.

Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group


Mada Nyinginezo:

TAZAMA, NASIMAMA MLANGONI.

RUDIA, TENA NA TENA KUMWOMBA MUNGU USIKATE TAMAA.

MATUNDA YAPATANAYO NA TOBA!

JE! ADAMU ALIWASALIANA NA MUNGU KWA LUGHA IPI PALE BUSTANINI?

JE! KUCHORA TATTOO NI DHAMBI?


Rudi Nyumbani:

Print this post

NI KWANINI MUNGU HAONEKANI?

(Kwanini Mungu hatumuoni?)….Hili ni swali ambalo karibu kila mtu anajiuliza au alishawahi kujiuliza pengine kipindi Fulani nyuma, kwanini Mungu hajidhihirishi wazi wazi tukamwona kama tunavyoonana sisi kwa sisi?, au kwanini Mungu hatumsikii kama tunavyosikilizana sisi tunavyoongea?….Watu wanasema Ni rahisi kumwona Mungu kwa kazi zake lakini yeye mwenyewe ni ngumu sana ni kwanini kaamua kuwa hivyo? Na hiyo imewafanya watu wengi kuishia kutoamini kabisa kama kuna Mungu na wengine wameishia kusema Mungu amekufa..

Lakini Je! kutokumwamini Ndio kutaleta suluhisho la yeye kutokuonekana?, Jibu ni hapana, yeye atabakia kuwa Mungu tu haijalishi tunamfikiriaje au tunamzungumziaje,..Jambo la pekee tunaweza kufanya ni kujiuliza ni kwanini Mungu aonyeshe tabia kama hiyo

Ukweli ni kuwa Mungu hayupo hivyo wakati wote, upo wakati biblia inatuambia tutamwona, uso kwa uso, upo wakati tutakaa naye, upo wakati tutazungumza naye uso kwa uso, (Mathayo 5:8, 1Wakorintho 13:11-12), Ufunuo 21:3 inasema..

“Nikasikia sauti kubwa kutoka katika kile kiti cha enzi ikisema, Tazama, maskani ya Mungu ni pamoja na wanadamu, naye atafanya maskani yake pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Naye Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao.”

Lakini kwasasa yeye ametuweka tuishi katika hali hii ya kutomwona tujifunze kitu, Na siku tukilifahamu vizuri hilo wazo la Mungu, hatutafikiri kitoto tena..Embu jaribu kufikiria, wewe ulipokuwa mtoto, au kijana ambaye upo chini ya wazazi wako, jaribu kuwaza ingekuwa mzazi wako kila mahali ulipo au unapokwenda yupo nyuma yako kukufuatilia, ukienda kula mgahawani yupo hapo anakuangalia ni chakula gani unakula, ukienda shule yupo hapo nyuma yako anakuangalia, ukiingia darasani yupo pale nyuma ya darasa na yeye anakuangalia kuakikisha ni kitu gani unasoma au unaandika, ukiwa unazungumza na marafiki zako yupo hapo anakusikiliza mazungumzo yako na kukuambia zungumza nao hivi, au usizungumze nao vile, ukiwa upo kwenye michezo yupo pembeni yako kukuchunga usiumie, ukienda uwani, yupo hapo nje anakusubiria utoke,..kila kitu unachokifanya yupo hapo pembeni yako anakuangalia, anasema ni kwasababu anakupenda na anakujali na ndio maana hataki akae mbali na wewe hata sekunde moja..anataka kila wakati umuone na yeye akuone..

Sasa jiulize wewe kama mtoto utajisikiaje, cha kwanza ni kuwa japo mzazi wako anakupenda sana na kukujali sana, lakini kule kuwa na wewe kila sekunde kila dakika kunakufanya upoteze uhuru Fulani wa kufanya mambo yako hata yale ya msingi.., pili kunakufanya uboreke kwa sehemu Fulani, haijalishi nia ya mzazi ni nzuri kiasi gani..Kuna mahali utahijitaji uhuru wako sehemu Fulani ili ufanye mambo yako kwa ufasaha zaidi.

Na kwa Mungu ndivyo ilivyo, tunasema Ee Mungu naomba kila saa nikuone, naomba kila saa nisikie sauti yako, naomba kila saa unitokee, tunasema hivyo ni kwa vile tu hutujui tunachokiomba,..Wewe unaweza kuona ni jambo jema na zuri kumwona Mungu au kusikia kila dakika anasema na wewe, lakini katika upande wa pili utakuwa unamtumikia Mungu kwa presha na bila UHURU ambao Mungu anataka utembee nao, na hilo ndilo jambo ambalo Mungu hapendi.

Wengi tunatamani Mungu akishatuokoa tu, basi saa hiyo hiyo tuanze kumsikia akizungumza ndani yetu na kutupa maelekezo karibu ya kila kitu cha kufanya..hata tukitaka kupiga hatua tunataka tumsikie Mungu akituambia piga hatua tano kisha kunja mbili kulia, fanya hivi, fanye vile, sema hiki, usiseme kile..kama vile GPS, ambayo hiyo inakuongoza kama vile Roboti kugeuka kulia na kushoto ili kufika pale ulipoelekezwa…

Mungu hayupo hivyo, yeye anachofanya ni kutugawia sisi ramani mkononi, ambayo inatuonyesha mwanzo hadi mwisho wa safari yetu, na katika ramani hiyo hiyo anatuonesha na mwisho wa njia mbaya zote, na katika ramani hiyo hiyo ndani yake kaweka mashauri ya njia sahihi ya kuiendea, Hivyo hapo ni wewe kuchagua njia ipi inayokufaa, kama utachagua njia ya uzima hapo ni wewe, kama utachagua njia ya mauti hapo ni wewe mwenyewe, lakini ramani inaelekeza kila kitu na ramani yenyewe ni BIBLIA TAKATIFU.

Lakini leo hii ukimpa Kristo maisha yako na ukaufahamu ukweli usitazamie utasikia sauti inakuambia usiende disko, au usizini au usiibe, au usiabudu sanamu, au kula hichi au usile kile, au ukaanza kutokewa na Mungu kila siku, kwenye ndoto, ikitokea jambo kama hilo basi ufahamu kuwa ni Mungu anataka kukufundisha kitu lakini usidhani itakuwa ni jambo la sikuzote. Ni wajibu wako wewe kuishi kulingana na njia za uzima inavyoelekeza ili ufikie mwisho mwema, na ndivyo utakavyoishi kwa uhuru ambao Mungu anataka auone kwetu..Ni sawa na mwanamke mwerevu aliyeolewa, ambaye akishaingia tu ndani ya nyumba ya mumewe hasubirii kusikia mumewe akimwambia nipikie chai, au nenda sokoni, yeye mwenyewe tu atajua majukumu yake kama mwanamke na kuanza kujitumia sawasawa na alivyoitiwa vivyo hivyo na mwanamume mwenye akili ambaye ameona, hatangojea siku mkewe amwambie mume wangu nenda katafute ugali wa nyumbani, yeye mwenyewe tu atatoka na kwenda kupambana ili kuakikisha kuwa familia yake inakula na kufurahi.

Hivyo ikiwa wewe ni mkristo, usisibiri Bwana akupe maagizo Fulani ya kufanya, utafunga sana, utaomba sana na usipate majibu yoyote, lakini tambua majukumu yako kama mkristo na uishi kulingana na ramani uliyopewa mkonono mwako yaani biblia!, na huko huko mbele ya safari ikiwa kuna kitu cha kuongezea au kina mapungufu ndipo Bwana atakuambia rekebisha hapa au rekebisha pale.

Kwamfano kama mkristo unajua kabisa tunapaswa kumzalia Mungu matunda ya aina zote (yaani ya haki na ya kazi), sasa tusisubirie kumngojea Mungu atuambie tukawashuhudie wengine waje kwake Hilo hutakaa ulisikie, Kwasababu Mungu anataka tuifanye kazi yake kwa uhuru..Hivyo tumia uhuru uliopewa kuifanya kazi ya Mungu pale ulipo kabla siku zako hazijaisha hapa duniani…Wapo wengi wanahitaji kumjua Mungu kama wewe ulivyo, lakini ukisubiria uone maono, hutafika popote.

2Wakorintho 3:17 Basi ‘Bwana’ ndiye Roho; walakini alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru.

Hizi ni siku za mwisho, Bwana wetu yupo mlangoni kurudi, hivyo tuzidi kuongeza nguvu katika kumtafuta yeye.

Bwana akubariki.


Mada Nyinginezo:

HATARI YA KUTOKUITAFAKARI BIBLIA VIZURI?

EPUKA KUTOA UDHURU.

DAMU YA ZAKARI BIN BARAKIA.

KWANINI BWANA YESU ALISEMA PALE MSALABANI NAONA KIU?

BIBLIA INAMAANA GANI KUSEMA “VILIVYOTAKASWA NA MUNGU, USIVIITE WEWE NAJISI”?


Rudi Nyumbani:

Print this post

KWANINI YESU KRISTO NI MWANA WA DAUDI?

Shalom, Mtu wa Mungu, karibu tujifunze biblia, Jukumu kubwa tulilopewa miongoni mwa mengi ni jukumu la kumfahamu sana YESU KRISTO, Na lengo kuu la kumfahamu sio kwasababu yeye anauhitaji sana wa Utukufu, au uhitaji sana wa kutafuta ajulikane, hapana! Hilo sio lengo…kwasababu pale tu alipo tayari anajulikana…Lakini bado anatuasa tunapaswa tumfahamu sana yeye…Hivyo hiyo ikimaanisha kuwa kwa jinsi tunavyomfahamu yeye ni tofauti na yeye anavyotaka sisi tumfahamu…

Kwasasa Mtu maarufu kuliko wote duniani kwa wakati wote ni YESU KRISTO, hakuna mwanadamu yeyote aliyewahi kufikia kiwango cha umaarufu alionao Bwana Yesu Kristo, ukienda kwa wachina, wahindu, wabudha wote wanamjua Yesu Kristo…Hata watu ambao sio wakristo kwa namna moja au nyingine walishawahi kumsikia Yesu Kristo katika Maisha yao..kwahiyo yeye ni maarufu tayari.

Biblia inasema katika…Waefeso 4: 13 “ …hata na sisi sote tutakapoufikia umoja wa imani na KUMFAHAMU SANA MWANA WA MUNGU, hata kuwa mtu mkamilifu, hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo;

14 ili tusiwe tena watoto wachanga, tukitupwa huku na huku, na kuchukuliwa na kila upepo wa elimu, kwa hila ya watu, kwa ujanja, tukizifuata njia za udanganyifu”

Na kwanini anataka sisi tumfahamu sana yeye? Mstari wa 14, hapo juu umetupa majibu… Ni ili tusiendelee kuwa Watoto wachanga, tukitupwa huku na huko, tukidanganywa na kila upepo wa elimu, na kuishia kuzifuata njia za udanganyifu.

Kwahiyo hakuna Elimu nyingine itakayoweza kutufanya tusiweze kudanganyika na elimu ya mashetani, isipokuwa Elimu ya kumfahamu Yesu Kristo, hakuna namna yoyote utakayoweza kuifahamu na kuidhibiti noti bandia pasipo kwanza kuijua noti halali ilivyo, ukishaifahamu noti halali ilivyo na tabia zake ndivyo utakavyoweza kuijua noti bandia..Kadhalika tunajukumu kubwa sana la kumfahamu Yesu Kristo kwa undani ili tuweze kuyadhibiti mafundisho ya mashetani na wapinga Kristo.

Leo tutajifunza kwanini Yesu Kristo, anajulikana kama Mwana wa Daudi na kwanini ni MFALME.

Sasa ni Dhahiri kabisa tunajua kuwa Yesu hakuwa na Baba wa kimwili, lakini kuna mahali kwenye maandiko kajitambulisha kuwa Mwana wa Daudi.. Sasa kwanini alijiita hivyo?

Sababu pekee ya Bwana Yesu kujulikana kama mwana wa Daudi, ni kutokana na Baraka Daudi alizozibeba, lakini si kutokana na undugu wa kidamu..Wewe unaitwa mwana wa Baba yako kutokana na uhusiano wa kidamu..lakini unaweza ukaitwa mwana wa Raisi wako, ila si kwa uhusiano wa kidamu bali wa pengine wa kiitikadi fulani….

Kwamfano pia sisi wakristo tunaitwa Wana wa Mungu, si kwasababu tumezaliwa familia moja na Muumba wetu,hapana au kwamba tuna damu moja na Mungu, hapana ni kutokana na Baraka za kimbinguni zinavyohusiana na sisi ndio maana tunaitwa wana wa Mungu.

Vivyo hivyo tunajulikana kwamba ni wana wa Ibrahimu , sio kwasababu sisi tuna damu moja na Ibrahimu, hapana bali ni kwasababu ni warithi wa Ahadi zile zile alizopewa Ibarahimu na Mungu, ndio maana na sisi tunajulikana kama wana wa Ibrahimu, Na Bwana Yesu ndio hivyo hivyo, Baraka alizopewa Daudi na mnyororo wa ukoo wake wote zilimhusu pia Bwana wetu Yesu Kristo…Daudi alikusudia kumjengea Mungu, Nyumba na hivyo Mungu akambarikia yeye na uzao wake kuwa uzao wa kifalme milele.(soma 2 Samweli 7:1-12)

kwasababu alizaliwa katika nyumba ya Yusufu ambaye alikuwa ni wa ukoo wa Daudi uliobarikiwa (ukoo wa kifalme),..Moja ya Baraka za ukoo wa Daudi ni kwamba utakuwa ni ukoo wa kifalme, kwamba wazao wote wa Kwanza wa Daudi walipakwa Mafuta na Mungu wawe wafalme soma (2 Wafalme 8:19,). Na ndio maana Bwana Yesu alipozaliwa katika nyumba ya Yusufu kama mzaliwa wa kwanza, roho ya kifalme ilikuwa juu yake. Kwahiyo kwa namna yoyote ile ni lazima angekuja tu kuwa Mfalme..

Je! Unajua kuwa Yusufu baba yake Yesu angepaswa awe mfalme wa Israeli kwa kipindi kile, kulingana na ahadi Mungu aliyomahidia Daudi?…Lakini kutokana na dhambi zao, Taifa la Israeli lilikatwa na uzao wa Daudi wa kifalme ukasimamishwa katika kutawala na ulisimamishwa kipindi gani?..

Kama ukisoma kitabu cha Wafalme, baada ya Daudi kufa, akafuata mwanawe Sulemani akawa mfalme kweli kulingana na ile Ahadi lakini naye pia akafa, na ikaendelea hivyo hivyo, kwa wajukuu na vitukuu vya Daudi, mpaka mfalme wa mwisho aliyetawala Yuda aliyeitwa Sedekia, ambaye alikuwa ni kitukuu cha 20 cha Daudi, huyu ndiye mfalme wa Mwisho kutawala Yuda, baada yake yeye, ndio Watu wakapelekwa Utumwani Babeli, hiyo ndiyo siku waliokatwa na waliporudi kukawa hakuna mfalme tena katika Israeli…vitukuu vya Daudi vilivyozaliwa baada ya Sedekia Mfalme wa Mwisho kufa, wakawa ni watu tu wa kawaida, kama watu wengine…

Ndio maana Yusufu baba yake Yesu alikuwa ni mtu wa kawaida tu maskini, ingawa alikuwa ni mwana wa kifalme…(Kwa urefu fuatilia ukoo huu wa Yesu kwenye kitabu cha Mathayo 1:1-17), laiti Israeli asingeasi na kupelekwa utumwani, Yusufu baba yake Yesu angekuwa mfalme wa Yuda, na Kristo angezaliwa huko…

Hivyo Israeli iliendelea kuwa kama mti uliokatwa baada ya kutoka Babeli…Wayahudi wakakaa mamia ya miaka bila mfalme….kukawa hakuna dalili yoyote ya Mfalme kunyanyuka katika uzao wa Daudi,..kwani Utawala wa Rumi ulikuwa umekamata dunia nzima, na Warumi waliwaweka watu wao kwenye makoloni yao yote, mpaka Israeli ilikuwa ni koloni la Warumi..Hivyo mtawala aliyetawala koloni la Israeli alikuwa ni Mrumi…jambo hilo liliendelea kwa miaka mingi…lakini Biblia ilitabiri katika Isaya Mlango wa 11 kuwa litatoka chipukizi katika shina la Yese….Kumbuka Yese alikuwa ni Baba yake Daudi, kwahiyo ni sawa na kusema litatoka chipukizi katika shina la Daudi au katika uzao wa Daudi. Tunasoma hayo katika…

Isaya11:1 “ Basi litatoka chipukizi katika shina la Yese, na tawi litakalotoka katika mizizi yake litazaa matunda.

2 Na roho ya Bwana atakaa juu yake, roho ya hekima na ufahamu, roho ya shauri na uweza, roho ya maarifa na ya kumcha Bwana”.

Kama ni msomaji mzuri wa maandiko utagundua kuwa…hilo shina linalozungumziwa hapo si lingine Zaidi ya BWANA YESU KRISTO mwenyewe…Biblia inasema litatoka shina, ikiwa na maana kuwa ni kutoka katika mti uliokatwa, nalo litazaa sana matunda… Kama ulishawahi kuona mti mkubwa uliokatiwa chini kabisa..linakuwa linabaki tu kama gogo…halafu baada ya kipindi fulani unaona kitawi kidogo cha kijani kinajitokeza ubavuni mwa lile gogo, na kama hakitakatwa na chenyewe, baada ya kipindi fulani kitakuwa kikubwa na hatimaye kuwa tena mti mkubwa kama ulivyokuwa mwanzo…

Ndicho kilichotokea baada ya uzao wa Daudi kukatwa na kupelekwa Babeli…ni sawa na mti uliokatwa…lakini chipukizi likatoka, katika uzao huo huo wa Daudi..

Bwana Yesu, Mwana wa Daudi, mzao wa kifalme, mwenye ahadi ya kifalme juu yake, alizaliwa huko Bethlehemu, alikuwa ni mfalme aliyetoka katika shina lililokatwa ndio maana utaona alizaliwa katika zizi la ng’ombe, familia ya kimaskini, laiti Yusufu baba yeke angekuwa mfalme basi naye pia angezaliwa katika familia ya kifalme..Lakini kinyume chake alizaliwa katika ufalme uliokatwa…

Lakini maandiko yanatabiri, huyo atakuja kuwa mti mkubwa na utazaa sana matunda, na ufalme wake utaenea duniani kote…kipindi alichokuja miaka 2000 iliyopita, roho ya Bwana ilikuwa juu yake, roho ya hekima na ufahamu, roho ya shauri na uweza, roho ya maarifa na ya kumcha Bwana” Kwa hekima, na maarifa aliyoyabeba alituletea sisi Wokovu…ambao mpaka sasa tunanufaika nao…., Lakini katika utawala wa miaka 1000 ijayo, ndio tutamwona vizuri kama Mfalme, aliyeketi katika kiti cha Kifalme…katika wakati huo, yeye pamoja na sisi ambao sasa tumemwamini, tutatawala naye, sisi tutakuwa wafalme nay eye atakuwa kama Mfalme wa wafalme.

Wakati huo Mamlaka yote ya kifalme atakuwa nayo yeye, utakuwa sio wakati wa wokovu tena bali wakati wa utawala, sasa hivi ndio tupo wakati wa wokovu, nyakati hizo zitakuwa ni nyakati za utawala mkuu wa Yesu Kristo. Dunia yote itajawa na kumcha Bwana, kutakuwa hakuna vurugu, kutakuwa na Amani isiyo ya kawaida..simba na kondoo watakaa pamoja na hawatadhuriana, mtoto atacheza na nyoka, na hakutakuwa na madhara yoyote.

Tusome tena Isaya hii 11 Mpaka mwisho..

“1 Basi litatoka chipukizi katika shina la Yese, na tawi litakalotoka katika mizizi yake litazaa matunda.

2 Na roho ya Bwana atakaa juu yake, roho ya hekima na ufahamu, roho ya shauri na uweza, roho ya maarifa na ya kumcha Bwana;

3 na furaha yake itakuwa katika kumcha Bwana; wala hatahukumu kwa kuyafuata ayaonayo kwa macho yake, wala hataonya kwa kuyafuata ayasikiayo kwa masikio yake;

4 bali kwa haki atawahukumu maskini, naye atawaonya wanyenyekevu wa dunia kwa adili; naye ataipiga dunia kwa fimbo ya kinywa chake, na kwa pumzi ya midomo yake atawaua wabaya.

5 Na haki itakuwa mshipi wa viuno vyake, na uaminifu mshipi wa kujifungia.

6 Mbwa-mwitu atakaa pamoja na mwana-kondoo, na chui atalala pamoja na mwana-mbuzi; ndama na mwana-simba na kinono watakuwa pamoja, na mtoto mdogo atawaongoza.

7 Ng’ombe na dubu watalisha pamoja; watoto wao watalala pamoja; na simba atakula majani kama ng’ombe.

8 Na mtoto anyonyaye atacheza penye tundu la nyoka, na mtoto aliyeachishwa atatia mkono wake katika pango la fira.

9 Hawatadhuru wala hawataharibu katika mlima wangu wote mtakatifu; maana dunia itajawa na kumjua Bwana, kama vile maji yanavyoifunika bahari.

10 Na itakuwa katika siku hiyo, shina la Yese lisimamalo kuwa ishara kwa kabila za watu, yeye ndiye ambaye mataifa watamtafuta; na mahali pake pa kupumzikia patakuwa na utukufu”.

Ufunuo 3:20 “Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami.

21 YEYE ASHINDAYE, NITAMPA KUKETI PAMOJA NAMI KATIKA KITI CHANGU CHA ENZI, KAMA MIMI NILIVYOSHINDA NIKAKETI PAMOJA NA BABA YANGU KATIKA KITI CHAKE CHA ENZI.

22 Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa”

Na pia alisema..

Ufunuo 22:12 “Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo.

13 Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, wa kwanza na wa mwisho.

14 Heri wazifuao nguo zao, wawe na amri kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake.

15 Huko nje wako mbwa, na wachawi, na wazinzi, na wauaji, na hao waabuduo sanamu, na kila mtu apendaye uongo na kuufanya.

16 Mimi Yesu nimemtuma malaika wangu kuwashuhudia ninyi mambo hayo katika makanisa. Mimi ndimi niliye Shina na Mzao wa Daudi, ile nyota yenye kung’aa ya asubuhi.

17 Na Roho na Bibi-arusi wasema, Njoo! Naye asikiaye na aseme, Njoo! Naye mwenye kiu na aje; na yeye atakaye, na ayatwae maji ya uzima bure”

Kama hujampa Yesu Kristo Maisha yako, jua umechelewa sana, lakini mlango bado hujafungwa ingia kabla mlango hujafungwa..mwisho wa mambo yote umekaribia, na Kristo yupo Mlangoni kurudi, atakaporudi nyakati hii ya mwisho atakuja kama mfalme na mtawala mkuu hatakuja tena kama mwokozi.

Bwana akubariki.

Tafadhali share kwa wengine


Mada Nyinginezo:

MWANA WA MUNGU.

ANGUKO LA UFALME WA SHETANI:

JIWE LA KUSAGIA

HUDUMA YA MALAIKA WATAKATIFU.

JE! MTU KUSIKIA SAUTI ZA WATU WALIO MBALI, KUNAWEZA TOKANA NA MUNGU?

BWANA ALIMAANISHA NINI KUSEMA “HERI WALIOTASA, NA MATUMBO YASIYOZAA, NA MAZIWA YASIYONYONYESHA”?


Rudi Nyumbani:

Print this post

MWAKA WA BWANA ULIOKUBALIWA.

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe, Leo ni siku nyingine Bwana ametupa neema  mimi na wewe kuiona, hivyo ni wajibu wetu kiutimia vizuri siku yetu kwa kujifunza maneno yake ambayo ndio nuru yetu na uzima wetu hapa duniani kila siku.

Leo kwa neema za Bwana tutajifunza juu ya huu mwaka wa Bwana uliokubaliwa ni upi ambao Bwana Yesu aliuzungumzia katika…

Luka 4:18 “Roho wa Bwana yu juu yangu, Kwa maana amenitia mafuta kuwahubiri maskini habari njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao, Na vipofu kupata kuona tena, Kuwaacha huru waliosetwa,

19 Na kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa”.

Sasa ni vizuri kufahamu kuwa biblia inaposema mwaka sio kila mahali inamaanisha kuwa ni mwaka Fulani mahususi labda 2018 au 2019 hapana, bali inamaanisha kipindi Fulani cha wakati kilichotengwa mahususi kukamilisha lengo Fulani chenye mwanzo wake na mwisho wake ambacho kimefananishwa na mwaka..

Hivyo hapo ni sawa na kusema “kuutangaza wakati wa Bwana uliokubaliwa”..Ikiwa na maana kuwa kama huo ndio wakati uliokubaliwa, basi pia  zilikuwepo nyakati nyingine ambazo hazikukubaliwa…. Na pia tunapaswa kufahamu ulikubaliwa kwa kusudi lipi?

Katika agano la kale kila mwaka wa 50 uliitwa Yubilee, mwaka huu ulikuwa ni mwaka wa maachilio, haikuruhusiwi kulima wala kupanda, ardhi ilikuwa inastarehe, ni mwaka ulioitwa mwaka wa maachilio ya watumwa, na kusamehe watu madeni yao (Walawi 25:11),

Na ndicho Bwana Yesu alichokuja kukifanya katika agano jipya, kuleta maachilio ya vifungo vyote, vya rohoni na mwilini, vile vile alikuja kuutangaza huo mwaka Bwana uliokubalika, yaani wakati wa Mungu kumkubali mwanadamu, kumwokoa na kumfunulia uso wake na mapenzi yake amjue yeye..Hiyo ililetwa na Bwana YESU tu peke yake, kumbuka  hapo kabla Mungu alikuwa hampokei Mwanadamu yeyote haijalishi ni kuhani au nabii au rabi kiasi gani, hakukuwa na mwanadamu yeyote ambaye aliwahi kumkaribia  Mungu na kutoa hoja zake pasipo kuwa na deni la dhambi ndani yake, na ndio maana ilimpasa kuhani mkuu peke yake aingie patakatifu pa patakatifu mara moja tu kwa mwaka afanye upatanisho wa dhambi za watu, pamoja na dhambi zake mwenyewe ambazo kimsingi zilikuwa haziondolewa bali zinafunikwa, baada ya hapo shughuli imeishia hakuna mashauri wala mahojiano, unaondoka mbele ya madhabahu ya Mungu ambayo ilikuwa duniani na wala sio mbinguni..

Lakini Bwana Yesu alipokuja yeye alisimama kama kuhani mkuu, na hivyo sasahivi sio tu tumepata ondoleo la dhambi na  maombi yetu kusikiwa bali pia tunaketi na kula na kunywa na Mungu katika ulimwengu wa Roho kama vile Baba na mtoto wake wa pekee ampendaye.. Haleluya!.

Kwahiyo tunaishi bado katika kipindi cha Mwaka wa Bwana uliokubalika…Lakini huu wakati hautadumu milele, mwaka Bwana uliokubalika hautadumu milele, kuna wakati Bwana Yesu kama kuhani mkuu atasimama kutoka katika kiti chake cha ukuhani, na kuanzia huo wakati na kuendelea hakutakuwa na rehema tena, na wala Mungu  hatakuwa na nafasi ya kuwatazama waasi, kinachobakia tu ni ghadhabu ya Mungu kumiminwa juu ya waovu wote..Na huo wakati upo karibu sana ndugu, Unyakuo ukishapita tu basi fahamu kuwa kiti cha rehema kilishaondolewa..

Luka 13.24 “Jitahidini kuingia katika mlango ulio mwembamba, kwa maana nawaambia ya kwamba wengi watataka kuingia, wasiweze.

25 Wakati mwenye nyumba ATAKAPOSIMAMA na kuufunga mlango, nanyi mkaanza kusimama nje na kuubisha mlango, mkisema, Ee Bwana, tufungulie; yeye atajibu na kuwaambia, Siwajui mtokako;

26 ndipo mtakapoanza kusema, Tulikula na kunywa mbele yako, nawe ulifundisha katika njia zetu.

27 Naye atasema, Nawaambia, Siwajui mtokako; ondokeni kwangu ninyi nyote mlio wafanyaji wa udhalimu.

28 Ndipo kutakapokuwa na kilio na kusaga meno, mtakapomwona Ibrahimu na Isaka na Yakobo na manabii wote katika ufalme wa Mungu, nanyi wenyewe mmetupwa nje”.

Na ndio maana biblia inasema wakati uliokubalika ndio sasa, ndio huu tulionao mimi na wewe,  yaani leo kwasababu kesho hatujui itakuwaje….

2 Wakorintho  6:2 “(Kwa maana asema, Wakati uliokubalika nalikusikia, Siku ya wokovu nalikusaidia;tazama,wakati uliokubalika ndiyo sasa; tazama siku ya wokovu ni sasa)”..

Usisubirie wakati ambao haukubaliki ndio umkumbuke Mungu, utakuwa umeshachelewa ndugu. Ikiwa bado upo mbali na Kristo wakati ndio huu wa sasa tubu dhambi zako, jitwike msalaba wako umfuate YESU, atakusamehe dhambi zako, kisha hakikisha baada ya kutubu kwako unabatizwa  kisha yeye mwenyewe atakupa kipawa cha Roho wake Mtakatifu bure kama alivyoahidi katika (Matendo 2:38)…

Bwana akubariki sana.


Mada Nyinginezo:

NINI MAANA YA KUISHI KWA KUUKOMBOA WAKATI?

CHANZO CHA MAMBO.

WATAMTAZAMA YEYE AMBAYE WALIMCHOMA.

JE! TARATIBU ZA KUFUNGA NDOA [YAANI HARUSI] NI AGIZO LA MUNGU AU NI MAPOKEO TU YA KIBINADAMU?

KUNENA KWA LUGHA KUKOJE?


Rudi Nyumbani:

Print this post