Category Archive Uncategorized @sw-tz

Arabuni maana yake ni nini?

Tukiachilia mbali, Eneo linaloitwa Arabuni ambalo limetajwa sana katika biblia,  .

Kama tunavyosoma katika vifungu vifuatavyo..

2Nyakati 9:14 “mbali na ile waliyoileta wachuuzi na wafanya biashara; tena wafalme wote wa Arabuni, na maliwali wa nchi wakamletea Sulemani dhahabu na fedha”.

 

Isaya 21:13 “Ufunuo juu ya Arabuni. Ndani ya msitu wa Arabuni mtalala, Enyi misafara ya Wadedani”.

 

Yeremia 25: 13 “Ufunuo juu ya Arabuni. Ndani ya msitu wa Arabuni mtalala, Enyi misafara ya Wadedani”.

 

Wagalatia 1:17 “wala sikupanda kwenda Yerusalemu kwa hao waliokuwa mitume kabla yangu; bali nalikwenda zangu Arabuni, kisha nikarudi tena Dameski”.

 

Wagalatia 4:25 “Maana Hajiri ni kama mlima Sinai ulioko Arabuni, umelingana na Yerusalemu wa sasa; kwa kuwa anatumika pamoja na watoto”.

Eneo ambalo walikuwa wanaishi jamii ya watu wa kiarabu.. Au kwa jina lingine linaitwa Arabia.Tazama picha juu.


Lakini Neno hili limetajwa kwa namna nyingine, katika biblia kama tunavyosoma katika vifungu vifuatavyo

2Wakorintho 1:22 “naye ndiye aliyetutia muhuri akatupa arabuni ya Roho mioyoni mwetu”.

 

2Wakorintho 5:5 “Basi yeye aliyetufanya kwa ajili ya neno lilo hilo ni Mungu, aliyetupa arabuni ya Roho”.

 

Waefeso 1:3 “Nanyi pia katika huyo mmekwisha kulisikia neno la kweli, habari njema za wokovu wenu; tena mmekwisha kumwamini yeye, na kutiwa muhuri na Roho yule wa ahadi aliye Mtakatifu.

14 Ndiye aliye arabuni ya urithi wetu, ili kuleta ukombozi wa milki yake, kuwa sifa ya utukufu wake”.

Sasa Mungu alipotugawia ahadi zake za uzima wa milele na nyinginezo, hakutaka kutupa mikono mitupu tu hivi hivi bila uthibitisho wowote, Hivyo ili kututhibitishia kuwa ahadi zake ni kweli alitupa uhakika huo kwa kutugawia Roho Mtakatifu,  kama garantii au tunaweza kusema, kuponi, ya kuwa ahadi zake tutafikia, au atatutimizia.. Sasa hiyo garantii/kuponi  ndio inayoitwa arabuni.

Ukipokea Roho Mtakatifu basi unayo arabuni ya uzima wa milele, kama alivyowaahidia wale waliomwamini.

Ukipokea Roho Mtakatifu basi una uhakika kuwa wewe ni mbarikiwa wa Mungu, hakuna laana yoyote inayoweza kukaa juu yako.

Ukipokea Roho Mtakatifu basi maombi yako ni hakika kuwa yanasikiwa na kujibiwa mbinguni, sawasawa na ahadi za Yesu kwa wote waliomwamini.

Lakini ukiwa huna Roho Mtakatifu, na unasema umeokoka, bado mbinguni hutaenda..Kama vile maandiko yanavyosema..

Warumi 8:9 “…Lakini mtu awaye yote asipokuwa na Roho wa Kristo, huyo si wake”.

Hivyo kama na wewe unataka upate hii arabuni(garantii) ya urithi wa ahadi za Mungu zote za mwilini na rohoni,, basi ni sharti umpokee Roho Mtakatifu. Na mtu anampokea Roho Mtakatifu kwa kuzaliwa mara ya pili.

Mtu anazaliwaje mara ya pili?

Pale unapotubu dhambi zako kwa kumaanisha kabisa kuziacha, , na baada ya kutubu  ukawa tayari kwenda kubatizwa katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo, sawasawa na Mdo 2:38, hapo utakuwa tayari umeshazaliwa mara ya pili.

Na moja kuwa moja, kuanzia huo wakati na kuendelea Roho anashuka ndani yako..Na unakuwa tayari umeshapokea garantii hiyo(arabuni) ya kuwa wewe ni mwana wa ahadi… Hivyo kama hutarudi nyuma utaendelea tu kuishi katika maisha matakatifu ya wokovu ya kumpendeza Mungu na kudumu katika ushirika wa Mungu..Ni uhakika kuwa hata ukifa usiku huo huo, wewe ni wa mbinguni tu mrithi wa ahadi zote za Mungu..

Hivyo kama hujaokoka, basi anza sasa kufuata hatua hizo kwa moyo wako wote..Kama unahitaji leo kumpa Yesu maisha yako basi fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba.>>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Na ikiwa utahitaji kubatizwa usisite kuwasiliana nasi kwa namba hizi +255789001312: Ubatizo ni bure, na unafanyika pindi tu mtu anapotubu dhambi zake..Hakuna madarasa ya kupitia, wala hakuna kutoa fedha, kwasababu biblia haitufundishi kanuni hizo..

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Yuko azuiaye sasa hata atakapoondolewa! ni nani huyo?

USIFIKIRI FIKIRI.

KILA MMOJA WENU AJUE KUUWEZA MWILI WAKE.

https://wingulamashahidi.org/ikabodi-maana-yake-ni-nini/

AMELAANIWA AANGIKWAYE MSALABANI.

UNYAKUO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Nini maana ya “Usimtokose mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake?”

SWALI: Biblia inamaanisha nini inaposema “Usimtokose mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.”


JIBU: Huu ni msemo ambao umeonekana ukipachikwa katikati ya vifungu kadha wa kadha kwenye biblia..

Kwa mfano utaona.. pale kwenye Kutoka 23:18-19 inasema..

18 Usisongeze damu ya dhabihu zangu pamoja na mkate uliotiwa chachu, wala mafuta ya sikukuu yangu usiyaache kusalia hata asubuhi.

19 Ya kwanza ya malimbuko ya nchi yako utayaleta na kuyatia ndani ya nyumba ya Bwana, Mungu wako. Usimtokose mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.

Ukisoma tena..Kutoka 34:25-26, utaona inasema hivi..

“25 Usisongeze damu ya sadaka yangu pamoja na mkate uliotiwa chachu; wala hiyo sadaka ya sikukuu ya pasaka haitasazwa hata asubuhi.

26 Vitu vya kwanza vya malimbuko ya nchi yako utavileta na kuvitia ndani ya nyumba ya Bwana Mungu wako. Usimtokose mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake”.

Ukirudi tena kwenye Kumbukumbu 14:21 nayo pia utaona ikisema.

“Msile nyamafu yo yote; waweza kumpa mgeni aliye ndani ya malango yako, ili apate kula; au kumliza mtu wa mataifa; kwa kuwa wewe u taifa takatifu kwa Bwana, Mungu wako. Usimtokose mwana-mbuzi katika maziwa ya mamaye”.

Sasa pale anaposema, usimtokose mwana-mbuzi, katika maziwa ya mama yake, anamaanisha kumchemsha mtoto wa mbuzi, kwa maziwa ya mama yake, yaani badala ya kumchemsha kwenye maji, wewe unachukua yale maziwa anayoyanyonya kutoka kwa mama yake na kumchemshia nayo..

Kwa namna ya kawaida ni kitendo kisicho cha kiungwana chenye ukakasi kidogo, hata kwako wewe unayesikia eti?..Utajiuliza ni kwanini ufanye hivyo? Kwani hakuna maji ya kumchemshia, au kitu kingine mpaka utumie maziwa, tena yale yale ya mama yake? Ni sawa na nguruwe aliyezaa mtoto, halafu unampa mtoto wake mwenyewe amle kama chakula chake..sasa hiyo ndio picha iliyopo hapo.

Ni kitendo kinachoonyesha unyama si unyama, ukosefu wa nidhamu..?

Ni utaratibu na mfumo wa kipagani ambao ulikuwa unafanyika na watu wa mataifa wasiomjua Mungu, walikuwa wanafanya hivyo kwa sababu za kishirikina, ni kama mila zinazoendelea siku hizi, hivyo Mungu aliwaonya wana wa Israeli wasifanye mambo kama hayo, kwasababu ni machukizo mbele zake, ni Utaratibu ambao hauna tofauti na ule wa kuwapitisha watoto kwenye moto, (soma 2Wafalme 21:6, 2Wafalme 16:3).

Hata sasa, wengi wetu tunafanya kafara kama hizo rohoni?.

Tunamtolea Mungu dhabihu zilizochanganyikana na mambo ambayo Mungu ameyakataza, tunafanya mambo kama watu wa mataifa. Tunamsifu Mungu na huku vinywa vyetu vimejaa matusi, na masengenyo, chuki na visasi, tunamtolea Mungu na huku biashara zetu ni haramu, tunahudhuria kanisani lakini tunaendelea kudumisha mila zetu za kishirikina, hali kadhalika tumeokoka lakini heshima kwa mzazi haipo, na heshima kwa Watoto wetu haipo (hiyo yote katika roho ni sawa na kumtokosa mwanambuzi katika maziwa yake) N.k.

Bwana atusaidie, tuzishike amri zake na tumpendeze yeye.

Bwana atuokoe na kutubariki..

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

USITUMAINISHWE NA MANENO YA UONGO.

YESU KWETU NI RAFIKI

Bali wajane walio vijana ukatae kuwaandika hao.

ZIFAHAMU HUDUMA KUU (10) ZA SHETANI DUNIANI.

CHOCHOTE UMFANYIACHO KRISTO KINA THAMANI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

AINA ZA MAJINI, MAJINA YAO, KAZI ZAO, NA TIBA ZAKE.

Ndugu Msomaji, nakukaribisha katika ukurasa huu kupata maarifa ya rohoni, Awali ya yote nakutahadharisha kuwa mitandaoni kuna elimu nyingi za uongo, Hivyo uisamini kila kitu mtu anachokuambia, kwasababu wengine, hawana nia njema wapo kwa ajili ya kutangazama biashara zao, na hawana lolote la kukusaidia kiroho.

 Sasa turudi katika kutazama majini, na kazi zao.

Nataka ufahamu kuwa ufalme wa Roho, upo katika pande kuu mbili tu!

  1. Upande wa Mungu.
  2. Upande wa Shetani.

Hakuna upande wa hapo katikati..

Upande wa Mungu yupo Mungu mwenyewe pamoja na malaika zake watakatifu. Na upande wa Shetani, Yupo shetani na malaika zake(Mapepo), Haya mapepo ndio wale malaika walioasi mbinguni, na kwa jina lingine wanaitwa MAJINI.

Usidanganywe na mwanadamu yeyote chini ya jua kukwambia kuwa kuna majini wazuri..Huo ni uongo mkubwa sana. Hakuna majini wazuri, majini wote ni roho za mashetani zinazofanya kazi duniani  kuangamiza roho wa watu, na lengo lao kubwa ni kuwapeleka  watu kuzimu..Na ndio maana nakuambia chukua tahadhari mpendwa. Mafundisho ya mashetani yalitabiriwa kutokea sana katika siku hizi za mwisho

1Timotheo 4:1 “Basi Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani;

Pengine ulishawahi kukutana na watu wakikueleza juu ya majini wazuri, na wabaya akakutajia mmojawapo kati ya hawa..

  • Jini subiani,
  • Jini Maimuna,
  • Jini Makata,
  • Jini Ruhani,
  • Jini Kabula,
  • Jini Kajadu,
  • Jini Sharifu,
  • Jini Jabari,
  • Jini bahari,
  • Jini Bedui,
  • Jini Zuhura,
  • Jini Zohari,
  • Jini Zamda n.k. n.k.

Haya yote ni mapepo ya kuzimu, na mbali ya kuwapeleka watu kuzimu huwa yanafanya na kazi nyingine pia za kuiharibu dunia na jamii,

  • mengine yanawafanya watu wawe vichaa na kutembea uchi ..

Mathayo 8:28 “Naye alipofika ng’ambo, katika nchi ya Wagerasi, watu wawili wenye pepo walikutana naye, wanatoka makaburini, wakali mno, hata mtu asiweze kuipitia njia ile”.

  • Mengine yawanawafanya watu wawe na ulemavu wa kudumu.

Luka 13:11 “Na tazama, palikuwa na mwanamke aliyekuwa na pepo wa udhaifu muda wa miaka kumi na minane, naye amepindana, hawezi kujinyosha kabisa.

12 Yesu alipomwona alimwita, akamwambia, Mama, umefunguliwa katika udhaifu wako.

  • Wawe mabubu, na vipofu, na viziwi..

Luka 11:14 “Naye alikuwa akitoa pepo bubu; ikawa pepo alipotoka, yule bubu akanena, makutano wakastaajabu”.

  • Mengine yanawafanya watu wasimpende Mungu, pale wanapotakana kusoma biblia, au kusikia mahubiri wanachukia na kuleta vurugu na kutaka kuondoka maeneo hayo.

Luka 8:2 “na wanawake kadha wa kadha ambao walikuwa na pepo wabaya na magonjwa wakaponywa; nao ni Mariamu aitwaye Magdalene aliyetokwa na pepo saba”,

  • Mengine yanawafanya watu wasifanikiwe, katika mambo yao; Ndoa, biashara, elimu, n.k. n.k.k

Sasa, watu wanawadanganya watu na kuambiwa , jini(Pepo) ukitaka kulituma au  likikuingia, fauta taratibu Fulani za asili kulitoa, labda aidha chukua majivu changanya na hiki au na kile, au andika maneno kwenye karatasi jeupe fanya hivi au vile, au ukilala angalia juu, au chukua udongo wa makaburini uchanganye na maji ya bahari na hiki au kile…Mambo kibao, Na ukifanya hivyo basi utaweza kulitoa jini hilo, au kulituma kufanya kazi Fulani.

Ndugu kama ulishawahi kufanya hivyo, ujue kuwa hukulitoa wala hukulituma, bali ndio umelikaribisha ndani ya maisha yako kukuharibu.

Idadi ya mapepo ulimwenguni ni kubwa sana, na yapo yanazunguka zunguka duniani kila mahali (Ayubu 1:7), hivyo kwa namna moja au nyingine ikiwa hujafahamu njia ya kufanya yasikukurabie basi utateswa sana. Na wengi wanadhani mpaka yawepo ndani yako, ni mpaka yatakapojidhihirisha..Hilo jambo si kweli, Mapepo ni roho, na yanafanya kazi kwa njia nyingi, mtu anaweza kuwa ni jini ndani yake lakini lisijidhirishe hata kidogo, lakini utamjua tu huyo mtu kwa tabia ya kitofauti aliyonayo.

NIFANYE NINI ILI MAJINI YASINIFUATE?

Lakini habari njema ni kuwa, yupo mmoja tu, anayeweza kumtoa mtu Mapepo/Majini kabisa kabisa, Na NI mmoja TU anayeweza kumzuia mtu asisogelewa na hayo maroho ya mashetani ndani yake kabisa kabisa, na huyo mtu si mwingine zaidi ya YESU KRISTO.

Ikiwa wewe ni Mkristo/muislamu, huna haja ya kuzunguka kwa waganga, au kwa watu wanaojiita mataalamu wakuondolee,au wakufukuzie mapepo katika maisha yako, hao wanakudanganya tu..unamuhitaji YESU..

Yeye pekee yake ndiye aliyeweza kuyatoa majini kama aliweza kuyatoa majini (zaidi ya 82,000) kwa wakati mmoja, kwa mtu ambaye alishindikana katika mji mzima yeye akayatoa .Na saa ile ile Yule kichaa akawa mzima..

Mathayo 8:28 “Naye alipofika ng’ambo, katika nchi ya Wagerasi, watu wawili wenye pepo walikutana naye, wanatoka makaburini, wakali mno, hata mtu asiweze kuipitia njia ile.

29 Na tazama, wakapiga kelele, wakisema, Tuna nini nawe, Mwana wa Mungu? Je! Umekuja kututesa kabla ya muhula wetu?

30 Basi, kulikuwako mbali nao kundi la nguruwe wengi wakilisha.

31 Wale pepo wakamsihi, wakisema, Ukitutoa, tuache twende, tukaingie katika lile kundi la nguruwe.

32 Akawaambia, Nendeni. Wakatoka, wakaingia katika nguruwe; na kumbe! Kundi lote wakatelemka kwa kasi gengeni hata baharini, wakafa majini”.

Na wewe hivyo hivyo, ukimpokea Yesu leo katika maisha yako, atakufanya kuwa huru..Biblia inasema hivyo katika Yohana 8:36..

Je! Unataka leo Yesu akuokoe?..Kumbuka wokovu sio dini, wokovu sio fedha..Wokovu ni bure kwa watu wote watakaompokea Yesu, Hivyo, kama upo tayari leo akubadilishe, unachopaswa kwanza kufanya ni kukubali kuacha dhambi zako zote,  Kisha unatubu, na baada ya hapo Yesu atayabadilisha maisha yako.

Sasa kabla sijakwenda kukuombea neema ya Yesu, ikuponye hapo hapo ulipo..Fuatisha kwanza hii sala ya Toba, kwa kumaanisha kabisa..

Hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha sema maneno haya kwa Imani,

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU  MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuwa na uhalali kwa kuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako.

Sasa upo tayari kuombewa..

Bwana Yesu, wewe ni yeye Yule jana na leo na hata milele, uliwaponya wale, ukaniponya mimi, utamponya na huyu ndugu aliyetubu leo hii.. Nakuomba Bwana Yesu unyooshe mkono wako umguse, roho yake, uyaguse maisha yako, uuguse mwili wako. Chunguza kiungo kimoja hadi kingine, uone ni wapi, pana kasoro umponye Bwana Yesu kama ulivyomponya Yule kichaa. Nguvu zote za giza zinazomsumbua mwili wake, au familia yake, au biashara yake, au ajira yake, leo hii nazitangazia mwisho wake kwa jina lako YESU KRISTO. Natuma moto wa Roho Mtakatifu ukayafunike maisha yake kama ulivyofunika Ayubu kuanzia leo na hata milele.

Asante Bwana Yesu kwa kumponya. Amen.

Sasa ikiwa umefuatisha maelekezo yote, kuanzia hichi kipindi utaanza kuona jinsi Yesu atakavyotembea na wewe maishani mwako. Hivyo usiache kujifunza Neno la Mungu lililo hai. Mwisho kabisa wa somo hili kuna masomo mengine ya kiroho, anza kuyapitia ujifunze ukue kimaarifa.

Pia kama utahitaji msaada zaidi, wa kupata mafundisho ya mara kwa mara kwa njia ya email. Au whatsapp yako, na ubatizo, basi wasiliana nasi kwa namba hizi : +255789001312

Bwana akubariki sana. Na hongera kwa wokovu.

Group la whatsapp Kwa mgawanyo bora wa masomo download App hapa>> App wingu la mashahidi

Mada Nyinginezo:

MAJINI WAZURI WAPO?

SI MAPEPO YOTE NI YA KULIPUKA.

NDIPO HUENDA AKACHUKUA PEPO WENGINE SABA.

Je! Wana wenu huwatoa kwa nani? maana yake ni nini?

MAPEPO YANATAFUTA HIFADHI NDANI YAKO KWA BIDII SANA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Nifanye nini ili niishi maisha ya ushindi siku zote?

Maisha ya ushindi


Shalom,

Awali ya yote ni lazima ufahamu kuwa kupita katika majaribu, kupita katika dhiki, kupita katika mateso, haimaanishi kuwa umeshindwa, hapana hivyo vyote vinaitwa vita,..Kushindwa ni pale, vita hivyo vinapokuzidi nguvu na hatimaye kukuangusha kabisa..hapo ndio umeshindwa.

Kwasababu kama ingekuwa kila anayepitia majaribu au dhiki au shida, au bonde la mauti ni kushindwa, basi Daudi angekuwa wa kwanza, kwasababu yeye, kila kukicha alikuwa anapita katika hali ya kukimbizwa na maadui zake na hatari za kufa, mpaka wakati mwingine anakwenda kuomba msaada kutoka kwa maadui zake wengine ili tu wampe hifadhi kwa muda. Lakini katika yote alikuwa na uhakika kuwa maisha yake ni ya ushindi tu..mpaka akaandika katika Zaburi 23 “Bwana ndiye mchungaji wangu, Sitapungukiwa na kitu…. Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, Gongo lako na fimbo yako vyanifariji”. (Zab 23)

Na kweli kama tunavyojua mwisho wa siku aliibuka mshindi, na kuwa mfalme wa Israeli, na mpaka sasa habari zake tunazisoma,

Hata Bwana wetu Yesu,vivyo hivyo alijaribiwa kama sisi tulivyojaribiwa, hata zaidi ya sisi lakini katika majaribu yake yote, hakuwahi kushindwa na hata moja, wala hakuwahi kutenda dhambi.. Na ndio maana akatuambia..

Yohana 16:33 “Hayo nimewaambieni mpate kuwa na amani ndani yangu. Ulimwenguni mnayo dhiki; lakini jipeni moyo; mimi nimeushinda ulimwengu”.

Unaona? Na watakatifu wengine wote kwenye biblia hivyo hivyo..

Lakini siri ya ushindi wao ilikuwa ni nini?

Je ni nguvu zao? Au bidii zao? Au ni nini.. Biblia imeshatoa jibu na kusema, mtu anayeweza kuushinda ulimwengu,(kuishi maisha ya ushindi) ni mtu Yule ambaye amezaliwa na Mungu tu.

1Yohana 5:4 “Kwa maana kila kitu kilichozaliwa na Mungu huushinda ulimwengu; na huku ndiko kushinda kuushindako ulimwengu, hiyo imani yetu”.

Unaona?, Ni mtu tu aliyezaliwa na Mungu ndio anapokea uwezo huo wa kuushinda ulimwengu, si mtu mwingine yeyote, nguvu za mtu binafsi haziwezi, bidii za mtu haziwezi, fedha ya mtu haiwezi, wala kipaji cha mtu hakiwezi kuushinda ulimwengu.

Huwezi kumshinda shetani atakapokuletea majaribu kama hujazaliwa na Mungu (yaani hujazaliwa mara ya pili), haiwezekani kuushinda uzinzi, haiwezekani kuishinda dhambi ile inayokusumbua, ni ngumu kuwashinda wachawi na mapepo, vilevile ni ngumu kuishi maisha ya amani na furaha hapa duniani.

Kwasababu Mungu anakuwa hayupo upande wako kukutia nguvu..Lakini wale ambao Mungu yupo ndani yao..biblia inasema hivi.

Warumi 8:31 “Basi, tuseme nini juu ya hayo? Mungu akiwapo upande wetu, ni nani aliye juu yetu?

32 Yeye asiyemwachilia Mwana wake mwenyewe, bali alimtoa kwa ajili yetu sisi sote, atakosaje kutukirimia na mambo yote pamoja naye?

33 Ni nani atakayewashitaki wateule wa Mungu? Mungu ndiye mwenye kuwahesabia haki.

34 Ni nani atakayewahukumia adhabu? Kristo Yesu ndiye aliyekufa; naam, na zaidi ya hayo, amefufuka katika wafu, naye yuko mkono wa kuume wa Mungu; tena ndiye anayetuombea.

35 Ni nani atakayetutenga na upendo wa Kristo? Je! Ni dhiki au shida, au adha, au njaa, au uchi, au hatari, au upanga”?

Kwa mtu aliyezaliwa mara ya pili kunakuwa na nguvu Fulani ya ajabu kutoka kwa Mungu inayomlinda asitetereke pindi unapopitia majaribu mazito ulimwenguni.

Hivyo ukiwa kama hujaokoka, au ulikuwa upo nusu nusu, (yaani mguu mmoja nje,mwingine ndani) na ndio maana maisha yako yamekuwa ni ya kushindwa kudumu katika wokovu, ya kushindwa kusimama, ya kushindwa kuwa na mahusiano mazuri na Mungu. Basi leo hii fanya uamuzi thabiti wa kumpa Yesu maisha yako upya kwa kumaanisha kabisa.

1Yohana 1:9 “Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote”.

Kama upo tayari kumruhusu Yesu ayaunde upya maisha yako, basi uamuzi huo ni wa busara, sana, fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba. Na pia kama unahitaji kubatizwa pia usisite kuwasiliana nasi .>>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Ikiwa umefungua na kufuata hayo maelekezo hapo juu, basi mpaka hapo tayari ushindi wa kwanza umepata wa mauti..

1Wakorintho 15:55 “Ku wapi, Ewe mauti, kushinda kwako? U wapi, Ewe mauti, uchungu wako?

Vilevile wachawi na mapepo hawatakuweza, kwa lolote..

Kuanzia huo  wakati utakapobatizwa na kuendelea utaanza kuona mabadiliko ya tofauti katika maisha yako,.Sina mengi ya kusema, wewe mwenyewe utayashuhudia.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye  namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

HIZI NI NYAKATI ZA KUJIINGIZA KWA NGUVU.

OLE WAO WANAOJITAHIDI KUMFICHA BWANA MASHAURI YAO.

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

NINI KINATOKEA BAADA YA KIFO?

KUZIMU NI WAPI

Rudi Nyumbani:

Print this post

Mshulami ni msichana gani?

Mshulami ni jina Sulemani alilompa msichana ambaye alikuwa naye katika mahusiano kama tunavyosoma katika kitabu cha wimbo ulio bora, alimwita hivyo kutokana na kuwa eneo alilotokea lilitwa  Shulami,

Wimbo 6:13 “Rudi, rudi, Mshulami, Rudi, rudi, ili sisi tukutazame. Kwani mnataka kumtazama Mshulami, kama kutazama ngoma ya Mahanaimu?


Fahamu zaidi:

Je unajua ni kwa nini Mariamu aliitwa Mariamu magdalene? >>> Mariamu Magdalene

Mlima Sinai upo nchi gani? >> Mlima sinai

Mti wa mlozi ni mti gani>>>> Fimbo ya haruni -mti wa mlozi

Kwanini Yesu alisema wacheni wafu wazike wafu wao? >>> Wafu wazike wafu wao

Amin, Amin, nawaambia kizazi hiki hakitapita >>> Kizazi hiki hakitapita,

Mitume wa Yesu walikufaje >>> Vifo vya mitume wa Yesu

Rudi Nyumbani:

Print this post

KUZALIWA KWA YESU.

kuzaliwa kwa Yesu kulikuwaje?


Mathayo 1:18 “Kuzaliwa kwake Yesu Kristo kulikuwa hivi. Mariamu mama yake alipokuwa ameposwa na Yusufu, kabla hawajakaribiana, alionekana ana mimba kwa uweza wa Roho Mtakatifu.

19 Naye Yusufu, mumewe, kwa vile alivyokuwa mtu wa haki, asitake kumwaibisha, aliazimu kumwacha kwa siri.

20 Basi alipokuwa akifikiri hayo, tazama, malaika wa Bwana alimtokea katika ndoto, akisema, Yusufu, mwana wa Daudi, usihofu kumchukua Mariamu mkeo, maana mimba yake ni kwa uweza wa Roho Mtakatifu.

21 Naye atazaa mwana, nawe utamwita jina lake Yesu, maana, yeye ndiye atakayewaokoa watu wake na dhambi zao.

22 Hayo yote yamekuwa, ili litimie neno lililonenwa na Bwana kwa ujumbe wa nabii akisema,

23 Tazama, bikira atachukua mimba, Naye atazaa mwana; Nao watamwita jina lake Imanueli; Yaani, Mungu pamoja nasi.

24 Naye Yusufu alipoamka katika usingizi, alifanya kama malaika wa Bwana alivyomwagiza; akamchukua mkewe;

25 asimjue kamwe hata alipomzaa mwanawe; akamwita jina lake YESU”.

Yesu mwokozi, kama si kuzaliwa kwake ulimwenguni, leo hii tungekuwa wapi? Kama sio kuimwaga neema yake duniani, tungepatia wapi ondoleo la dhambi?

Mamajusi walitoka nchi ya mbali, kwa furaha tu ya kumwona mwokozi wa Ulimwengu, ambaye hata hakuzaliwa katika nchi yao..lakini kwa kuiona tu nyota yake, hawakusubiri, wahadithiwe, walianza safari..

Lakini Swali la kujiuliza Je! Na wewe amezaliwa moyoni mwako?

Bwana Yesu lipoanza kuitenda kazi ambayo Baba yake amemtumia alisimama na kusema maneno haya..

Luka 4:18 “Roho wa Bwana yu juu yangu, Kwa maana amenitia mafuta kuwahubiri maskini habari njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao, Na vipofu kupata kuona tena, Kuwaacha huru waliosetwa,

19 Na kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa”.

Hiyo ni kazi kubwa ambayo ilimleta duniani, na ndio maana mwishoni kabisa mwa kitabu cha Ufunuo alisema hivi..

Ufunuo 21:6 “Mimi ni Alfa na Omega, Mwanzo na Mwisho. Mimi nitampa yeye mwenye kiu, ya chemchemi ya maji ya uzima, bure”.

Hivyo mpe leo Yesu maisha yako, ayaokoe, akufanye kuwa kiumbe kipya. Hizi ni siku za mwisho, Yesu yupo mlangoni kurudi.Dalili zote zinaonyesha, kuwa mimi na wewe tunaweza kushuhudia tukio la Unyakuo.

Bwana atusaidie sana.

Shalom.

Ikiwa utapenda mafundisho ya biblia yawe yanakufikia kwa njia ya whatsapp, basi tutumie ujumbe kwa namba hii: +255789001312

Mada Nyinginezo:

KWANINI YESU KRISTO ALIKUJA DUNIANI?

JIFUNZE NENO LA MUNGU KWA BIDII ZOTE.

EPUKA MUHURI WA SHETANI

https://wingulamashahidi.org/2018/07/19/nyakati-saba-za-kanisa-na-wajumbe-wake/

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Kuhutubu ni nini?

Rudi Nyumbani:

Print this post

USHIRIKINA NA MADHARA YAKE.

Ushirikina na madhara yake, rohoni ni yapi?


Ushirikina ni kitendo cha kwenda kutafuta msaada wa kiroho au wa kimwili katika mamlaka ya giza. Nikisema mamlaka ya giza namaanisha kwa shetani na mapepo na majini yake yote yanayofanya kazi kupitia watu wanaoitwa waganga au wachawi.

Sasa unapoumwa, halafu badala ya kwenda kuwa Mungu upate msaada, wewe unakimbilia kwa waganga wa kienyeji ili upate msaada ya kiganga, hapo moja kwa moja tayari umeshashirikiana na mashetani katika ulimwengu wa roho.

Au unapopitia matatizo Fulani aidha ya kifamilia, au ya kikazi, au unahaja ya jambo Fulani pengine masomo, au ndoa, au cheo, halafu wewe moja kwa moja unakimbilia kwa mganga akusaidie kutatua tatizo lako, ujue kuwa tayari umeshaingizwa katika mtandao wa Mashetani.

Jambo ambalo wengi hawajui ni kuwa, walau kwa mtu wa kawaida yeyote, kunakuwa na ka-ulinzi Fulani kutoka kwa Mungu, ambacho anazaliwa nacho hicho kanamfanya shetani asiweze kujiamulia tu jambo lolote atakalo juu ya huyo mtu, vinginevyo ungekuwa shetani kashawamaliza watu wote duniani, kwa kuwaua, Ndio ni kweli ataweza baadhi  lakini sio yote. Sasa pale mtu anapokwenda kwa shetani mwenyewe kumwomba msaada, maana yake ni  kuwa anasaini naye mkataba rasmi kuwa kuanzia sasa, huy mtu ni wangu na naweza kufanya jambo lolote juu yake.

Haya ndio madhara ya moja kwa moja ya ushirikina.

  1. Unaingiliwa na mapepo:

Angalia vizuri utaona asilimia kubwa ya watu wanaoudhuria kwa waganga wanakuwa wanasumbuliwa na nguvu za giza, au wengine wanapata ulemavu Fulani ambao hapo kabla hawakuwa nao, au ugonjwa Fulani, ambao hauponi, hiyo yote ni kutokana na mtu kujishughulisha na ushirikina.

  1. Unakuwa hatarini kufa:

Kutokana na kuwa tayari umeshajihalalisha kwa shetani, basi shetani kazi yake kubwa iliyobakiwa nayo kwako ni kukuua,..Kwasababu ndio dhumuni lake hapa duniani, kuua biblia inasema hivyo…

Yohana 8:44 “Ninyi ni wa baba yenu, Ibilisi, na tamaa za baba yenu ndizo mpendazo kuzitenda. Yeye alikuwa mwuaji tangu mwanzo; wala hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake”.

  1. Chochote unachokifanya hutafanikiwa:

Hata kama kitaonekana kukuletea matokeo mazuri kiasi gani mwanzoni, kumbuka hiyo ni gia tu ya shetani kukuvuta kwake, ili usimwache, lakini katika kipindi cha muda mrefu, hakitakufikisha popote, kama ulikuwa umekwenda kutafuta mali, hizo mali zitapotea tu baada ya kipindi Fulani, kama ulikuwa umekwenda kutafuta kazi, hiyo kama unaweza usiipate, na hata ukiipata haitadumu, utakuwa ni mtu ambaye anafanya jambo lakini baada ya muda mrefu haoni faida ya jambo hilo, au haoni maendeleo yoyote. Na mwisho wa siku unajikuta ni heri usingeenda.

Mithali 11:21 “Hakika, mtu mwovu hatakosa adhabu; Bali wazao wa wenye haki wataokoka”.

Ayubu  21:13 “Siku zao hutumia katika kufanikiwa, Kisha hushuka kuzimuni ghafula”.

  1. Unapoteza Utu na uwezo wa kupambanua mambo ya rohoni:

Kumbuka pale unapokwenda kwa waganga, ni unaonyesha kuwa humuhitaji Roho Mtakatifu kukusaidia, na kazi ya Roho Mtakatifu ni kuwavuta watu kwa Mungu, na kuwapa macho ya rohoni, Hivyo unapojihusisha na ushirikina na uchawi, ni kuwa unapoteza huo uwezo, na matokeo yake unakufa kiroho.. Hapo ndipo unaanza kufanya hata yale mambo ambayo mwanadamu wa kawaida hawezi kufanya,..Hayo unaweza usiyaone leo, lakini kwa jinsi siku zitakavyozidi kwenda mabadiliko hayo utayaona, kwasababu nguvu za giza wakati huo zitakuwa zinakutawala.

2Wakorintho 4:4 “ambao ndani yao mungu wa dunia hii amepofusha fikira zao wasioamini, isiwazukie nuru ya injili ya utukufu wake Kristo aliye sura yake Mungu”.

 

  1. Ukifa unakwenda motoni.

Washirikina wote, wachawi wote, biblia inasema sehemu yao ni katika lile ziwa la moto. Ukifa leo na upo katika hali hiyo , basi ni moto wa milele unakuongoja.

Ufunuo 21:8 “Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili”.

 

Sasa kwanini hayo yote yakukute?

Lakini Habari njema ni kuwa, hata kama umeingia huko, bado unayo nafasi ya kutengenezwa upya. Na anayeweza kufanya hivyo, si mwingine zaidi ya YESU KRISTO tu peke yake..Huyo ndiye aliyetiwa mafuta na Mungu, ili kuwatoa watu katika vifungo vya giza, mwingine yeyote hawezi….

Isaya 61:1 Roho ya Bwana MUNGU i juu yangu; kwa sababu Bwana amenitia mafuta niwahubiri wanyenyekevu habari njema; amenituma ili kuwaganga waliovunjika moyo, kuwatangazia mateka uhuru wao, na hao waliofungwa habari za kufunguliwa kwao.

Hivyo kama ulishaingia humo, au bado hujaingia, lakini Kristo bado hayupo ndani yako, basi leo hii fanya uamuzi huo, wa kumkaribisha ndani yako ayaokoe maisha yako moja kwa moja, haijalishi wewe ni muislamu, Yesu anawaokoa wote, wanaomkimbilia yeye kwa moyo wa dhati.

Akikuweka huru, amekuweka huru kweli kweli, haachi hata alama ya uovu ndani yako, akikusamehe amekusamehe kweli kweli, kana kwamba hukuwahi kumkosea, kwa lolote. Atakufungua kutoka katika malango hayo ya mauti ya ibilisi yaliyokufunga, na kukuletea katika ufalme wa wana wa Mungu. Roho Mtakatifu akiingia ndani yako, hakuna pepo lolote litakaloweza kukaa ndani yako, Ukimkaribisha leo hii atakufanya huru, na kuna amani itaingia ndani mwako, ambayo utashangaa imetoka wapi..Huyo ndio Yesu mwokozi.

Hivyo kama upo tayari leo hii kutubu dhambi zako kwa kumaanisha kabisa kuacha, na kusema kuanzia sasa namfuata Yesu, sitaki ushirikina, sitaki dhambi, Namfanya Yesu kuwa kiongozi wa maisha yangu basi uamuzi huo ni mzuri na wa busara, basi, fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala fupi ya Toba..>>>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Ubarikiwe sana.

Mada Nyinginezo:

NINI KINATOKEA BAADA YA KIFO?

EPUKA MUHURI WA SHETANI

JINSI WATU WANAVYOZAMA KATIKA USHIRIKINA NA UCHAWI.

JE NI KWELI MTU ANAWEZA KUTOKA NJE YA MWILI WAKE?.

MAONO YA NABII AMOSI.

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

WATASHINDANA LAKINI HAWATAKUSHINDA

Watapigana nawe lakini hawatakushinda maana yake ni nini?


Yeremia 1:18 “Maana, tazama, nimekufanya leo kuwa mji wenye boma, na nguzo ya chuma, na kuta za shaba, juu ya nchi yote; juu ya wafalme wa Yuda, na juu ya wakuu wake, na juu ya makuhani wake, na juu ya watu wa nchi hii.

19 Nao watapigana nawe; lakini hawatakushinda; maana mimi nipo pamoja nawe, asema Bwana, ili nikuokoe”.

Haya ni maneno ambayo alipewa Yeremia baada ya kuitwa na Mungu katika huduma. Lakini kwa hofu ya labda atakapokwenda kuwaeleza  watu juu ya hukumu za Mungu, watakasirika na kumletea madhara ya ghafla labda watampiga mawe, hapo ndipo hapo Mungu akamuhakikishia kuwa ni kweli watakuja kupigana na yeye, lakini hawatamshinda, kwasababu yeye yupo pamoja naye.

Hata sasa adui hawezi kuja kupigana na mtu kama huna huduma ya  Mungu mkononi mwake, mstari huu unapendwa kutamkwa na watu wengi kirahisi rahisi hata watu ambao wapo katika dhambi, wanajidanganya wakisema..

watashindana lakini hawatakushinda

Huo ni uongo, shetani hashindani na watu waovu,hata mara moja, kwasababu tayari alishawashinda siku nyingi. Hivyo ukijiona unapitia vita visivyokuwa na maana angali wewe ni mwenye dhambi ujue hayo sio mapambano.

Lakini ili Neno hili liwe na nguvu ndani yako, ni sharti kwanza, uokoke, umkabidhi Yesu maisha yako kweli kweli, kisha uwe na kazi ya kufanya katika injili yake, ndipo hapo hata shetani akinyanyuka na majeshi yake yote kutaka kukuangusha wewe ni sawa na kazi bure, kwasababu Mungu yupo pamoja na wewe daima.

Wakati huo hata ulimwengu mzima uungane vipi kutaka kukupindua usisonge mbele, watakuwa ni kama wanapoteza Muda kwasababu Mungu yupo upande wako.

Hivyo kama upo tayari leo kuokoka, ili maneno haya yawe na nguvu kwako, basi uamuzi huo ni wa busara, fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Shalom.

Mada Nyinginezo

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA WARAKA WA TATU WA YOHANA.

Historia ya wimbo wa tenzi – Ndio dhamana Yesu wangu

KWANINI TUNAOMBA KWA JINA LA YESU?

NAO WATAKAOUAWA NA BWANA WATAKUWA WENGI.

YEREMIA

Rudi Nyumbani:

Print this post

WAMWENDEA YESU KWA KUSAFIWA lyrics na historia

WAMWENDEA YESU KWA KUSAFIWA lyrics (Are you washed in the Blood?)


Wimbo huu uliandikwa na ndugu mmoja aliyeitwa Elisha Hoffman mwaka 1878, huko Ohio Marekani. Baada ya kuhitimu katika chuo cha biblia alisimikwa na kuwa mchungaji na kutumika kwa miaka mingi katika huduma hiyo, katika maisha yake yote ya huduma alifanikiwa kuandika nyimbo za kikristo zaidi ya 2000. Na huu “Wamwendea Yesu kwa kusafiwa,

” Ulikuwa ni mmojawapo.

 Wimbo huu umechukia maudhui yake kutoka katika sehemu nyingi za biblia ikiwemo;

Ufunuo 7:14 “Nikamwambia, Bwana wangu, wajua wewe. Akaniambia, Hao ndio wanatoka katika dhiki ile iliyo kuu, nao wamefua mavazi yao, na kuyafanya meupe katika damu ya Mwana-Kondoo”.

Wamwendea Yesu kwa kusafiwa.

****

Wamwendea Yesu kwa kusafiwa,
Na kuoshwa kwa damu ya kondoo?
Je, neema yake umemwagiwa?
Umeoshwa kwa damu ya kondoo?
 
Kuoshwa, kwa damu,
Itutakasayo ya kondoo;
Ziwe safi nguo nyeupe mno;
Umeoshwa kwa damu ya kondoo?
 
Wamwandama daima Mkombozi,
Na kuoshwa kwa damu ya kondoo?
Yako kwa Msulubiwa makazi,
Umeoshwa kwa damu ya kondoo?
 
Kuoshwa, kwa damu,
Itutakasayo ya kondoo;
Ziwe safi nguo nyeupe mno;
Umeoshwa kwa damu ya kondoo?
 
Atakapokuja Bwana-arusi,
Uwe safi kwa damu ya kondoo!
Yafae kwenda mbinguni mavazi,
Yafuliwe kwa damu ya kondoo.
 
Kuoshwa, kwa damu,
Itutakasayo ya kondoo;
Ziwe safi nguo nyeupe mno;
Umeoshwa kwa damu ya kondoo?
 
Yatupwe yalipo na takataka,
Na uoshwe kwa damu ya kondoo,
Huoni kijito chatiririka,
Na uoshwe kwa damu ya kondoo?
 
Kuoshwa, kwa damu,
Itutakasayo ya kondoo;
Ziwe safi nguo nyeupe mno;
Umeoshwa kwa damu ya kondoo?
 

****

Je na wewe uimbapo wimbo huu, maisha yako kweli yameshwa kwa damu ya mwana-kondoo (Yesu Kristo), Je unajua kuwa hukumu haikwepeki kwako ikiwa bado upon je ya Kristo. Hivyo kama hujatubu ni heri ufanye hivyo sasa, Bwana akusafishe uwe safi.

Shalom.

Tazama historia ya tenzi nyingine chini.

Mada Nyinginezo:

NI SALAMA ROHONI MWANGU Lyrics

YESU KWETU NI RAFIKI

USINIPITE MWOKOZI Lyrics

 

UNYAKUO.

EPUKA MUHURI WA SHETANI

Rudi Nyumbani:

Print this post

KUOTA UPO MAKABURINI.

Kuota upo makaburini kuna maanisha nini kibiblia?

Makaburini sikuzote ni mahali wanapolazwa wafu, ikiwa unaota ndoto hii mara kwa mara upo makaburini ni ishara kuwa hali yako ya rohoni ni mfu. Upo mfano mmoja katika biblia wa mtu ambaye makao yake yalikuwa ni makaburini tu maisha yake yote haondoki pale.. Na biblia inatoa sababu kwamba ni nguvu za giza za mapepo zilikuwa zimemfunga..Na mapepo yale yalikuwa hayana lengo lingine zaidi ya kumuua..

Utasema umejuaje hilo? Tumejua hilo pale tulipoona baada ya kukemewa na Yesu, yalimpotoka na kuwaingia wale nguruwe, na moja kwa moja yale mapepo yakawakimbiza wale nguruwe kwenye maji kuwaangamiza..Hiyo yote ni kuonyesha kuwa lengo lao lilikuwa kuua tu na si kingine..Embu tusome kidogo..

Marko 5 :1-15

“1 Wakafika ng’ambo ya bahari mpaka nchi ya Wagerasi.

2 Na alipokwisha kushuka chomboni, mara alikutana na mtu, ambaye ametoka makaburini, mwenye pepo mchafu;

3 makao yake yalikuwa pale makaburini; wala hakuna mtu ye yote aliyeweza kumfunga tena, hata kwa minyororo;

4 kwa sababu alikuwa amefungwa mara nyingi kwa pingu na minyororo, akaikata ile minyororo, na kuzivunja-vunja zile pingu; wala hakuna mtu aliyekuwa na nguvu za kumshinda.

5 Na sikuzote, usiku na mchana, alikuwako makaburini na milimani, akipiga kelele na kujikata-kata kwa mawe.

6 Na alipomwona Yesu kwa mbali, alipiga mbio, akamsujudia;

7 akapiga kelele kwa sauti kuu, akasema, Nina nini nawe, Yesu, Mwana wa Mungu aliye juu? Nakuapisha kwa Mungu usinitese.

8 Kwa sababu amemwambia, Ewe pepo mchafu, mtoke mtu huyu.

9 Akamwuliza, Jina lako nani? Akamjibu, Jina langu ni Legioni, kwa kuwa tu wengi.

10 Akamsihi sana asiwapeleke nje ya nchi ile.

11 Na hapo milimani palikuwa na kundi kubwa la nguruwe, wakilisha.

12 Pepo wote wakamsihi, wakisema, Tupeleke katika nguruwe, tupate kuwaingia wao.

13 Akawapa ruhusa. Wale pepo wachafu wakatoka, wakaingia katika wale nguruwe; nalo kundi lote likatelemka kwa kasi gengeni, wakaingia baharini, wapata elfu mbili; wakafa baharini.

14 Wachungaji wao wakakimbia, wakaieneza habari mjini na mashambani. Watu wakatoka walione lililotokea.

15 Wakamwendea Yesu, wakamwona yule mwenye pepo, ameketi, amevaa nguo, ana akili zake, naye ndiye aliyekuwa na lile jeshi; wakaogopa”.

Unaona, Vivyo hivyo ikiwa unaota upo makaburini ni ishara kuwa hali yako ya kiroho ni mbaya sana, Lakini habari njema ni kuwa YESU Yule Yule wa zamani ndio huyo huyo wa leo.

Siwezi jua maisha yako upo katika hali gani sasahivi kiroho, pengine upo katika vifungo vya dhambi, au vyovyote vile, lakini Nataka nikuambie ni Yesu pekee tu, ndiye anayeweza kukupa raha maishani mwako, haijalishi wewe ni muislamu au nani, ni Yesu peke yake ndio anayeweza kukupa tumaini la maisha mema, ya hapa duniani na mbinguni.

Yeye (Bwana Yesu) mwenyewe alisema..

Mathayo 11:28 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.

29 Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu”;

Unachopaswa kufanya ikiwa unahitaji kumkaribisha Yesu leo maishani mwako, akutengeneze upya, basi uamuzi huo utakuwa ni wa busara sana kwako, Kumbuka sio hilo tu, yapo na mengine usiyoyajua wewe, Yesu anataka kuyarekebisha katika maisha yako, ni wewe tu kuufungua moyo wako,. Hivyo kama upo tayari leo kutubu, dhambi zako kwa kumaanisha kabisa, na kusema kuanzia leo nitamfuata Yesu, basi ni uhakika kuwa leo leo, atakuja ndani yako na kukuokoa, na utaanza kuona mabadiliko makubwa sana kwenye maisha yako ya rohoni na mwilini..

Ikiwa upo tayari sasa kufanya hivyo basi, na kuanza safari mpya ya wokovu, basi fungua hapa, kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba >>>>KUONGOZWA SALA YA TOBA

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo

TAZAMA, NASIMAMA MLANGONI.

BWANA SI MWEPESI WA HASIRA, LAKINI BWANA NI MWINGI WA HASIRA.

UNYAKUO.

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

YESU MPONYAJI.

Rudi Nyumbani

Print this post