Bwana alimaanisha nini kusema “Hamtaimaliza miji ya Israeli hata ajapo mwana wa Adamu”
Tusome;
Mathayo 10:23 “Lakini watakapowafukuza katika mji huu, kimbilieni mwingine; kwa maana ni kweli nawaambia HAMTAIMALIZA MIJI YA ISRAELI HATA AJAPO MWANA WA ADAMU”
JIBU: Ukiusoma mstari huo kuanzia juu kabisa, yaani kuanzia mstari wa kwanza…Utaona ni Habari inayohusu tendo la Bwana Yesu kuwatuma wanafunzi wake kwenda kuhubiri injili katika miji ya Israeli…Na utaona alipowaagiza wakahubiri aliwapa na baadhi ya maagizo au masharti, kwamba wasichukue chochote na pia wawe wavumilivu kwa watakayoyapitia huko..Lakini mwishoni kabisa mwa maagizo tunaona Bwana anawaambia…“hamtaimaliza miji ya Israeli hata ajapo mwana wa Adamu”..
Sasa swali linalojitengeneza kwenye vichwa vyetu hapo ni kwamba…mbona Bwana Mitume walikuwa wameshaimaliza hiyo miji na Yesu bado alikuwa hajarudi?..ina maana mpaka leo injili haijasambaa kwenye miji yote ya Israeli ndio maana Bwana hajarudi mpaka leo?.
Jibu rahisi la swali hili tunaweza kulipata kwenye Habari kama hii hii katika kitabu cha Luka…Tusome,
Luka 10:1 “Basi, baada ya hayo Bwana aliweka na wengine, sabini, akawatuma wawili wawili wamtangulie kwenda kila mji na kila mahali alipokusudia kwenda mwenyewe. 2 Akawaambia, Mavuno ni mengi, lakini watenda kazi ni wachache; basi mwombeni Bwana wa mavuno apeleke watenda kazi katika mavuno yake. 3 Enendeni, angalieni, nawatuma kama wana kondoo kati ya mbwa-mwitu. 4 Msichukue mfuko, wala mkoba, wala viatu; wala msimwamkie mtu njia”
Luka 10:1 “Basi, baada ya hayo Bwana aliweka na wengine, sabini, akawatuma wawili wawili wamtangulie kwenda kila mji na kila mahali alipokusudia kwenda mwenyewe.
2 Akawaambia, Mavuno ni mengi, lakini watenda kazi ni wachache; basi mwombeni Bwana wa mavuno apeleke watenda kazi katika mavuno yake.
3 Enendeni, angalieni, nawatuma kama wana kondoo kati ya mbwa-mwitu.
4 Msichukue mfuko, wala mkoba, wala viatu; wala msimwamkie mtu njia”
Tuvichunguze baadhi ya vipengele katika mstari huo wa kwanza ambavyo ndivyo vitakavyotupa dira ya kuelewa Habari nzima….katika mstari wa kwanza biblia inasema… “Bwana aliweka na wengine, sabini, AKAWATUMA WAWILI WAWILI WAMTANGULIE kwenda kila mji na kila mahali alipokusudia kwenda mwenyewe”…Zingatia hilo neno “WAMTANGULIE”..Kama wewe ni mswahili mzuri utaelewa maana ya neno “kutangulia” ni nini…kutangulia maana yake ni mtu anakwenda mahali kisha wewe unafuata baadaye…yaani anawahi kufika kule kabla wewe kufika…hiyo ndiyo maana ya kutangulia…
Hivyo mstari huo una maana kuwa “hao wanafunzi sabini na wale 12 Bwana aliokuwa anawatuma kwenda huko katika miji ya Israeli hakuwatuma tu…huko wenyewe…bali Bwana aliwaahidi kwamba atawafuata, hivyo aliwatuma tu kama wamtangulie.”
Ili kuelewa vizuri tafakari tena kamfano haka… “Umemwagiza mfanyakazi wako atangulie asubuhi na mapema sehemu ya kazi kuendelea na kazi, na ukamwambia hatamaliza kazi zote kabla ya wewe kufika hapo ofisini, maana yake utafika kabla hata hajamaliza kazi zote”.. Ndicho Bwana alichowaambia wanafunzi wake, kwamba huko wanakwenda naye pia atakuja kabla hawajaimaliza miji yote ya Israeli (Hilo ni neno la Faraja)…Na kweli aliiungana nao baadaye hakuwaacha yatima…
Sasa kuna jambo moja la kujifunza hapo…Kwamba Desturi ya Bwana ilikuwa hafiki mahali kabla ya kutuma kwanza wajumbe wake wakamtengenezee njia…Maana yake kabla ya yeye kuja mahali anatuma kwanza watumishi wake wakahubiri injili..Ndivyo alivyofanya kwa Yohana Mbatizaji…yeye alitumwa kumtengenezea Bwana njia na kuiandaa mioyo ya watu kabla Bwana mwenyewe hajaanza kuhubiri..ili atakapoanza kuhubiri vile Bwana atakavyohubiri visiwe ni vitu vigeni sana kwa watu wake.(kasome Yohana 10:41-42, na Luka 1:17).
Utaona sehemu zote kabla Bwana hajaenda mahali huwa anatuma wanafunzi wake kwanza na baadaye anaungana nao.. (kasome Luka 9:52-54, Marko 14:12-18, Marko 11:1-4)..
Ndugu Mpendwa hata sasa, Bwana bado anatuma watu wake kuitengeneza njia yake…Umesikia injili mara ngapi?, kila mahali upitapo, mtaani, kwenye magari, mashuleni, unapofanyia kazi?..lakini unadharau kwasababu labda anayekuhubiria umemzidi kipato, au umemzidi elimu, au umri?..Lakini lisikie hili neno ambalo Bwana Yesu alilisema..
Marko 9:37 “Mtu akimpokea mtoto mmoja wa namna hii kwa jina langu, anipokea mimi; na mtu akinipokea mimi, humpokea, si mimi, bali yeye aliyenituma”
Hako katoto unakokadharau sasa, huyo uliyemzidi elimu, pengine na kipato…huyo ambaye hata maandiko hawezi kuyatamka vizuri na anakuhubiria utubu umgeukie Mungu lakini unamchukulia unavyojua wewe…Bwana Yesu ambaye sasa hivi yupo mbingu za mbingu anamheshimu, siku ile tutaonyeshwa tumemkataa yeye Dhahiri.
Bwana atusaidie.
Kama bado hujampa Yesu Kristo Maisha yako, tupo ukingoni sana mwa siku za mwisho, ambapo ghafla tu unyakuo utapita na watakatifu watatoweka….waliobaki hawatasikia tena usumbufu wa mahubiri wanayohubiriwa sasa..watakuwa wamefungua jalada lingine la maisha..na watakatifu vivyo hivyo..Kwahiyo sio wakati wa kukaa nje..Mlango wa Safina unakaribia kufungwa, waasherati,walevi, wezi, watukanaji, watazamaji picha chafu mitandaoni, wanaokula rushwa, na wanaofanya kila aina ya machafuko biblia inasema sehemu yao itakuwa ni katika lile ziwa la moto. Ingia leo ndani ya Safina ya Yesu, wokovu unapatikana bure.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
Wewe u nabii yule akajibu la!..swali huyu ‘nabii yule’ ni nani?
JE! WEWE NI MWAKILISHI MWEMA?
Kwanini Bwana alisema Hakuna aliye mwema ila mmoja?
Habari ile ya Pilato kuchanganya zile damu za wayahudi na pamoja na dhabihu zao,(Luka 13) ilihusu nini?
Rudi Nyumbani:
Print this post
Waefeso 5:15 “Basi angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si kama watu wasio na hekima bali kama watu wenye hekima; 16 mkiukomboa wakati kwa maana zamani hizi ni za uovu. 17 Kwa sababu hiyo msiwe wajinga, bali mfahamu ni nini yaliyo mapenzi ya Bwana. 18 Tena msilewe kwa mvinyo, ambamo mna ufisadi; BALI MJAZWE ROHO”;
Waefeso 5:15 “Basi angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si kama watu wasio na hekima bali kama watu wenye hekima;
16 mkiukomboa wakati kwa maana zamani hizi ni za uovu.
17 Kwa sababu hiyo msiwe wajinga, bali mfahamu ni nini yaliyo mapenzi ya Bwana.
18 Tena msilewe kwa mvinyo, ambamo mna ufisadi; BALI MJAZWE ROHO”;
Mwishoni mwa mstari huo wa 18 biblia inatuambia ‘”bali mjazwe Roho”.. Hili Ni neno endelevu, Sasa kumbuka Mtume Paulo alipokuwa anazungumza na kanisa hili la Efeso Alijua kabisa walishapokea Roho Mtakatifu tangu zamani walipoamini, na ndio maana likawa kanisa kubwa lilolitwa Efeso, Lakini hiyo haikumfanya mtume Paulo aone wamefika, bali aliwaasa siku baada ya siku wajazwe Roho, kwasababu alijua kuwa Roho anaweza kuzimishwa ndani ya mtu, hali kadhalika pia anaweza kujaa na kupungua kwa jinsi mtu atakavyokuwa makini au mzembe katika wokovu wake.
Hata sisi wakristo wa zama hizi ambazo uovu wetu ni mkubwa kuliko ule wa kanisa la Efeso, kusema tu, tumeokoka, au tumepokea Roho Mtakatifu, na huku bado uhusiano wetu na Mungu haueleweki haitoshi kutufikisha mbinguni, bali tunapaswa tujazwe Roho Mtakatifu siku baada ya siku mpaka siku ile ya Unyakuo itakapotukuta..
Kwasababu tukipuuzia jambo hilo, tutafananishwa na wale wanawali wapumbavu tunaowasoma katika Mathayo 25 ambao walikuwa wanamngojea Bwana wao lakini hawakuwa na mafuta ya kutosha ya kuwafikisha hadi ule wakati wa kumlaki Bwana wao.. matokeo yake saa ile ilipofika ya Bwana wao kutokea, ndio wakajishtukia kuwa taa zao zinakwenda kuzima…Sasa wakati wanakwenda kununua huku nyuma tayari Bwana arusi ameshawasili na kuwachukua wale aliowakuta wapo tayari na kuingia nao karamuni..Na wale wengine waliokwenda kuchukua mafuta waliporudi wakajikuta wameshachelewa.. Hasara ikawa ni kwao na taabu yao yote ya kumngojea Bwana ikiwa ni bure.. Japokuwa nao pia walikuwa ni wanawali (mabikira) yaani wameokoka, ambao wanamngojea tu Bwana wao kwa saburi kama wale wengine.. Lakini kwasababu ya kupuuzia jambo la msingi la mafuta katika chupa zao ikawafanya wakose karamu..
Siku zote mafuta yanafananishwa na Roho Mtakatifu..Tunapompokea Roho Mtakatifu siku zile za kwanza tulipookoka, tulipokea mafuta ya kuwasha tu vyombo vyetu vya usafari..Lakini tukiridhika na yale tu, hatutafika mbali. Ndugu ili kukivuka hichi kipindi cha Uovu uliokirithiri duniani sasa..Tunapaswa tuendelee kujazwa Roho..
Pengine utauliza nifanye nini ili nijazwe Roho Mtakatifu?
Roho Mtakatifu anaweza kuendelea kujaa ndani yetu, kwa walau mambo makuu manne.
Biblia inasema, Luka 13:13 “Basi, ikiwa ninyi mlio waovu mnajua kuwapa watoto wenu vipawa vyema, je! Baba aliye mbinguni hatazidi sana kuwapa Roho Mtakatifu hao wamwombao?”
Ukiwa mtu wa kuomba, na kukataa uvivu kwa kutokusali walau saa moja kwa siku, ndivyo utavyojiongezea mafuta yako ya rohoni na hivyo Roho Mtakatifu atapata wigo mpana wa kuyatawala maisha yako siku baada ya siku.
2. Kwa kujifunza kwa bidii Neno la Mungu..; Neno ndio chakula cha uzima wa mtu. Usipojibidiisha kujifunza Neno la Mungu, kutafuta habari za uzima, usidhani kuwa Roho Mtakatifu atapata nafasi ya kukufundisha kitu chochote ndani yako. Kwasababu Mungu yupo katika Neno lake(Sauti ya Mungu ni Neno lake). Ukiwa umeokoka, halafu unaona uvivu kujifunza Biblia basi ujue Roho wa Mungu ameshazimika ndani yako kitambo..Na hivyo hata wakati wa unyakuo utakapofika utafananishwa na wale wanawali wapumbavu.
3. Kaa mbali na uovu; Siku zote dhambi inavutia, lakini mwisho wake ni mbaya..Tunapoivumilia dhambi katika maisha yetu ndivyo Mungu anavyouficha uso wake. Na matokeo yake Roho Mtakatifu anazimika, au anaondoka kabisa ndani yetu.(Isaya 59:2)
4. Tangaza habari njema: Ukiwafundisha wengine, na wewe hapo hapo Roho wa Mungu anakufundisha, ukiwafungulia wengine hazina ya maneno ya uzima, Roho Mtakatifu anapata nafasi ya kukufunulia wewe Zaidi na kukutumia, ili kuwaokoa watu wake..Na hivyo ni sharti atakaujaza tu Roho wake, kwasababu siku zote unafanya kazi yake..Na hapo utakuwa na nafasi nyingine ya kuwa karibu na yeye.
Hivyo tusiridhike tu, na hali za kiroho tulizopo, tukajificha nyuma ya kivuli cha Neno nimeokoka..Tunapaswa tujiulize Je! Mafuta tuliyonayo yanatutosha mpaka wakati wa kuja kwa Bwana? Kama sivyo basi huu ndio wakati wa kuzitengeneza upya taa zetu..kwa kuhakikisha kuwa kila siku Roho Mtakatifu anapata nafasi maishani mwetu..Ili ile siku ambayo hatujui ni lini itakapotujilia kwa ghafla basi tuwe na uhakika kuwa UNYAKUO hautatupita.
Ubarikiwe.
JINSI ROHO MTAKATIFU ANAVYOWAFUNULIA WATU MAANDIKO.
Je! hizi roho saba za Mungu ni zipi? na je zinatofautiana na Roho Mtakatifu?
RABI, UNAKAA WAPI?
NA MTU MMOJA AKAVUTA UPINDE KWA KUBAHATISHA, AKAMPIGA MFALME
KUTUBU SIO KUOMBA REHEMA.
MATUNDA 9 YA ROHO MTAKATIFU
Pakanga ni mmea fulani mchungu uliokuwa unajulikana enzi za kale za biblia, ulikuwa ni mmea unaoota sehemu kame na ulikuwa ni mchungu sana..Hivyo kutokana na sifa ya mmea huo, chochote kile ambacho kingeleta uchungu mkali zamani kiliitwa jina la pakanga Kwa mfano kwenye biblia tunaona neno hilo likitumika sehemu mbali mbali…
Yeremia 23:15 “Basi Bwana wa majeshi asema hivi, katika habari ya manabii, Tazama, nitawalisha pakanga, nitawanywesha maji ya uchungu; kwa kuwa kutoka kwa manabii hao wa Yerusalemu kukufuru kumeingia katika nchi yote”.
Soma tena..
Mithali 5:3 “Maana midomo ya malaya hudondoza asali, Na kinywa chake ni laini kuliko mafuta; 4 Lakini mwisho wake ni mchungu kuliko pakanga; Ni mkali kama upanga wa makali kuwili”.
Yeremia 9:14 “bali wameenenda katika ushupavu wa mioyo yao wenyewe, na kuandamana na Mabaali, kama walivyofundishwa na baba zao. 15 Basi, Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Tazama, nitawalisha pakanga, naam, watu hawa, nami nitawapa maji ya uchungu wayanywe. 16 Nami nitawatawanya kati ya mataifa, ambao wao hawakuwajua; wala baba zao, nami nitatuma upanga nyuma yao, hata nitakapowaangamiza kabisa”
Yeremia 9:14 “bali wameenenda katika ushupavu wa mioyo yao wenyewe, na kuandamana na Mabaali, kama walivyofundishwa na baba zao.
15 Basi, Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Tazama, nitawalisha pakanga, naam, watu hawa, nami nitawapa maji ya uchungu wayanywe.
16 Nami nitawatawanya kati ya mataifa, ambao wao hawakuwajua; wala baba zao, nami nitatuma upanga nyuma yao, hata nitakapowaangamiza kabisa”
Ufunuo 8:10 “Malaika wa tatu akapiga baragumu, nyota kubwa ikaanguka kutoka mbinguni, iliyokuwa ikiwaka kama taa, ikaanguka juu ya theluthi ya mito, na juu ya chemchemi za maji. 11 Na jina lake ile nyota yaitwa Pakanga; theluthi ya maji ikawa pakanga, na wanadamu wengi wakafa kwa maji hayo, kwa kuwa yalitiwa uchungu”.
Soma pia (Maombolezo 3:15,19), (Amosi 6:12), utaliona Neno hilo..
Hivyo biblia inapotumia hili Neno pakanga, inamaanisha uchungu mkali usio wa kawaida utakaowapata watu wanaotenda dhambi.. kama vile uasherati, uabuduji sanamu, utoaji wa unabii wa uongo n.k..
Hata leo Maisha yetu Mungu anaweza kuyatia pakanga, ikiwa tutaendelea kuishi Maisha ya kutokujali..Tuombe Bwana atuepushe na hayo mambo, huku tukikaa mbali na dhambi..Magonjwa haya tuyaonayo leo hii ni sehemu tu ndogo ya Pakanga, Ukilishangaisha ni hiyo itakayokuja kuachiliwa siku za mwisho ambapo watu watasaga ndimi, wakitamani vifo viwafikie, lakini mauti itawakimbia.. mambo hayo yatakuja baada ya unyakuo kupita.
Shalom.
NI WAPI MAHALI SAHIHI PA KULIPA ZAKA?
Neno I.N.R.I kwenye msalaba wa Yesu maana yake ni nini?
Utii ni nini? na ni nani tunayepaswa kumtii au kutokumtii?
NDUGU,TUOMBEENI.
Bwana aliposema kuwa yeye ni “Mungu wa miungu” alikuwa na maana gani?..je! yeye ni Mungu wa sanamu?
TIMAZI NI NINI
Tunapotenda Mema ni kwa faida yetu na si ya Mungu..kadhalika tunapofanya maovu ni kwa hasara yetu sisi na si hasara ya Mungu. Kwa mfano mtu anayezini biblia inasema anatenda dhambi juu ya mwili wake mwenyewe anafanya jambo litakalomwangamiza yeye mwenyewe.. maana yake anakuwa hana tofauti na mtu anayejiua…
Mithali 6:32 “Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa; Afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake.33 Atapata jeraha na kuvunjiwa heshima; Wala fedheha yake haitafutika”
Kadhalika mtu anayeiba au anayeua, HAMKOMOI MUNGU..bali anafanya jambo ambalo litawaumiza wanadamu wenzake na hali kadhalika litakalomwaribu yeye mwenyewe baadaye. Na dhambi nyingine zote ni hivyo hivyo…zina madhara kwetu na si kwa Mungu…Vivyo hivyo tunapotenda mema, mema hayo tunapoyafanya si kwa faida ya Mungu bali kwa faida yetu sisi wenyewe..Bwana anapotuasa na kututaka tutende mema si kwaajili yake yeye, bali kwaajili yetu sisi..ni sawa na mtu anayekizuia kisu katika shingo ya mtu anayetaka kujiua..Ndivyo anavyofanya kwetu pale anapotuzuia tusifanye dhambi..ni kwa faida yetu si yake…endapo akituacha tu basi tutajimaliza na hakuna kitakachosalia…
Kwamfano Biblia inasema wapeni watu vitu nanyi mtapewa…(Luka 6:38) kipimo cha kujaa, na kushindiliwa hata kusukwa sukwa ndivyo watu watakavyowapa vifuani mwenu…kwamaana kipimo kile tupimacho ndicho tutakachopimiwa…Maana yake ni kwamba sio kwamba Mungu anatupa sheria ngumu ili yeye ajifurahishe moyo wake anapotuona tunamtii..hapana anafanya vile ili sisi tupate faida..yeye hatumwongezei chochote kwa wema wetu tunaoufanya…
Hivyo ukitenda mema na kuwapa watu vitu na wewe utapewa vitu siku moja kwa kiwango kile kile ulichowapa wengine…Kwahiyo mema ni kwa faida yetu sisi na si ya Mungu.
Kwahiyo Biblia inapotuonya tusizini, au tusifanye uasherati, au tusiibe, au tusiue, au tuwaheshimu wazazi wetu n.k ni kwafaida yetu ili tupate mema katika ulimwengu huu na ule unayokuja..Na si kwa sababu Mungu anapenda kutuangalia kama kwenye Tv huku duniani tukitenda mema, kwamba ndio chakula chake yeye..Ukifikiri/tukifikiri hivyo..tutakuwa bado hatujamwelewa huyu Mungu tunayemwabudu…
Soma maandiko haya:
Ayubu 35: 5 “Ziangalie mbingu ukaone; Na mawingu yaangalie, yaliyo juu kuliko wewe. 6 Ikiwa umefanya dhambi, umefanya nini juu yake? Yakiwa makosa yako yameongezeka, wamfanyia nini yeye? 7 Ikiwa u mwenye haki, wampa kitu gani? Au yeye hupokea nini mkononi mwako? 8 Uovu wako waweza kumwumiza mtu kama wewe; Na haki yako yaweza kumfaa mwanadamu”.
Ayubu 35: 5 “Ziangalie mbingu ukaone; Na mawingu yaangalie, yaliyo juu kuliko wewe.
6 Ikiwa umefanya dhambi, umefanya nini juu yake? Yakiwa makosa yako yameongezeka, wamfanyia nini yeye?
7 Ikiwa u mwenye haki, wampa kitu gani? Au yeye hupokea nini mkononi mwako?
8 Uovu wako waweza kumwumiza mtu kama wewe; Na haki yako yaweza kumfaa mwanadamu”.
Umeona? Unapovaa vimini na suruali na kuonywa usivae kikahaba ni kwa faida yako mwanamke….Unapoua kwa kutoa mimba ni kwa hasara yako wewe na yule uliyemuua, …Unapojiongezea maasi juu ya maasi na dhambi juu ya dhambi, humpunguzii kitu Mungu kwasababu yeye haishi kwa dhambi zetu wala kwa haki yetu…Hivyo dhambi zako unazojiongezea juu kila siku ni sawa unasikia njaa na kukata kiungo chako kimoja kimoja kila siku ili ukile upunguze njaa..(hapo unajimaliza mwenyewe).
Unasikia mahubiri kila kona, ni kwasababu Mungu anakupenda na anataka upate faida wewe na si yeye..anataka usipate hasara wewe na si yeye..
Hili neno “hizi ni siku za mwisho” pengine umeshalisikia sasa hii ni mara ya elfu, na limeshakuchosha…lakini kipindi si kirefu hutalisikia tena kwasababu siku zenyewe zitakuwa zimeshatimia…Kristo atachukua walio wake na kila mtu atavuna alichokipanda akiwa hapa duniani. Na watakatifu watanyakuliwa..na dhiki kuu itaanza na siku ya Bwana itashuka ulimwenguni, wakati huo disko unazohudhuria sasa hazitakuwepo tena, bar unazokwenda kulewea hazitakuwepo tena, madili haramu na rushwa unazokula sasa hazitakuwepo tena…viwanda vinavyotengeneza mavazi yako ya kikahaba havitakuwepo tena, hakutakuwa na kurudi nyumbani kulala kutandani, wala kuangalia tv, wala kuingia internet..siku hizo zitahitimisha mambo hayo yote..Na baada ya hayo ziwa la moto litafunguliwa shetani na malaika zake watatupwa kwanza kwa maana lilitengenezwa kwaajili yao.
Kisha wote walio nje ya Kristo watafuata. Walio nje ya Kristo sio wale unaowategemea kwamba ni watu wa dini fulani..bali hata wewe uliye vuguvugu umbaye mguu mmoja upo nje mwingine ndani…ambaye ni mlevi lakini bado una jina la kikristo, ni mwasherani na mtembeaji uchi barabarani lakini bado unasali..wewe ndio mfano wa watakaoachwa wakati huo, na hiyo ni kulingana na maandiko na si mapokeo au mafundisho ya mtu binafsi aliyejiamulia tu kuzungumza.
Siku ya kunyakuliwa leo imekaribia sana kuliko jana na juzi…mwaka huu tumeukaribia unyakuo sana kuliko miaka ya nyuma..Hivyo huu ndio wakati wa kuongeza umakini wetu kuliko vipindi vya nyuma.
MKARIBIE BWANA ZAIDI ILI UFANYIKE NGUZO.
NIMEOKOKA, ILA MUNGU NDIYE ANAYEJUA NITAKWENDA WAPI.
Chapa zake Yesu ni zipi hizo?
MUNGU WETU, JINSI LILIVYO TUKUFU JINA LAKO DUNIANI MWOTE!
KUTAKUWA NA MATETEMEKO YA NCHI, NJAA NA TAUNI.
KWANINI YESU KRISTO NI WA MUHIMU KWETU SASA?
SWALI: Je! Mtume Paulo alikuwa anamwabudu malaika wake aliyekuwa anatembea naye kama tunavyosoma katika Matendo 27:23?
JIBU: Tuusome huo mstari..
Matendo 27:23 “Kwa maana usiku huu wa leo malaika wa Mungu yule ambaye mimi ni wake, naye ndiye nimwabuduye, alisimama karibu nami,”
Mstari huu ukisomwa kwa haraka haraka ni rahisi kutafsiri kwamba Mtume Paulo alimaanisha kusema kwamba anamwabudu Malaika wake..Lakini ukiurudia tena taratibu utaona kwamba hapo Mtume Paulo hakumaanisha kuwa anamwabudu Malaika bali ni Mungu..
Sasa tunaweza kuiweka vizuri sentensi hiyo kama ifuatavyo; “Kwa maana usiku wa leo Malaika wa Mungu alinijia”…..sasa swali ni Mungu yupi?…ndio anaendelea kusema…Mungu yule ambaye mimi ni wake, naye ndiye nimwabuduye…
Hivyo ukirudia kusoma kwa namna hiyo huo mstari utapata tafsiri kamili.
Hivyo Pamoja na hayo tunazidi kujifunza kwamba tunapaswa kuzidi kuyachunguza maandiko, ili tupate kulielewa Neno la Mungu kama yeye Mungu wetu anavyotaka tulielewe..kwasababu ipo mistari mingi na Habari nyingi katika maandiko matakatifu ambazo wakati mwingine ni ngumu kuzielewa lakini tunapokaa chini na kutaka kumwuliza Roho Mtakatifu yeye ni mwaminifu na atatufulia, kwasababu tusipopata tafsiri kamili kwa msaada wa Roho Mtakatifu shetani anaweza kuitumia mistari hiyo hiyo kutukosesha na kutuhalalisha uovu wake…kama alivyoitumia baadhi ya mistari kuwadanganya watu kuhalalisha ulevi, zinaa, ndoa za mitara na hata ameshautumia mstari huu kwa baadhi ya watu kuhalalisha ibada za kuabudu malaika na ibada za sanamu.
Bwana atusaidie na kutubariki.
Je! Bwana Yesu alibatiza akiwa hapa duniani?
Je! Shetani alitolea wapi uovu?
Je ni wakina nani ambao hawataonja mauti mpaka siku ya kuja Bwana?
Ulinzi wa daima (eternal security) Je! ni neno la kimaandiko?
Kwanini Musa alipewa mbao mbili za mawe na sio moja au zaidi
Chukua tahadhari juu ya neema ya Mungu.
Hakuna ulinzi mkubwa ambao mwanadamu anaweza kuupata kama ulinzi wa kuwa ndani ya Yesu..Kama wengi wetu tunavyojua au tulivyosikia kwamba watu wote waliompokea Yesu Kristo uhai wao unakuwa umefichwa pamoja na Kristo.(Wakolosai 3:3). Kiasi kwamba tunalindwa dhidi ya nguvu za giza na mipango yote ya Ibilisi.
Wengi wetu tunaifurahia neema hii na kutamani kuingia ndani yake lakini hatujui kuwa ikichukiliwa isivyopaswa ina madhara makubwa kuliko kitu kingine chochote tunachoweza kukijua.
Neema ya Mungu inafananishwa na nyumba ya karamu, yenye mlango…Mathayo 7:13. Sasa kama tujuavyo nyumba yoyote ile ya muhimu kama Ikulu au ukumbi wa sherehe ya muhimu sana ina mlango na vile vile ina uzio…na mara nyingi kuta zake zinakuwa zimezungushiwa uzio mwingine ambao ni wa umeme..Na kama ni nyumba yenye umuhimu mkubwa zaidi ya hayo inakuwa na walinzi wanaotembea tembea wenye silaha kuizunguka, lengo ni kuzuia watu wa wasiruke ukuta na kuingia ndani…Na ikitokea mtu akijaribu kukiuka na kuusogelea ukuta kutaka kuruka aingie ndani ndipo anaweza akajikuta kapigwa risasi au kapigwa shoti ya umeme, na hivyo hata kuweza kujisababishia kifo…Lakini ulinzi huo haujawekwa kwaajili ya kuangamiza watu, bali kulinda usalama.
Na Neema ya Mungu ni hivyo hivyo…Ipo nguvu ya ziada iwalindao wale watu walioingia ndani ya Neema ya Kristo..Nguvu hiyo ndiyo inayotulinda dhidi ya nguvu zote za giza, dhidi ya shetani na majeshi yake (mapepo na wachawi) na kila mpango mwovu wa Ibilisi..Hivyo yoyote anayejaribu kuingia kutaka kuwaharibu watu wa Mungu walio chini ya neema ya Mungu basi atakuwa anajitafutia matatizo yeye mwenyewe..
Lakini jambo lingine la kuogopesha ni kwamba ikitokea mtu aliyeko ndani ambaye tayari kashaingia ndani ya jengo hilo, akatoka na kwenda kupanda ukuta na kurukia zile nyaya za umeme zilizouzunguka ukuta, yeye naye atajeruhiwa vile vile kama sio kufa kabisa. Maumivu yale yale atakayoyasikia Yule anayetaka kuruka ukuta na kuingia ndani ndio hayo hayo atayapata Yule anayetaka kuruka na kutoka nje.
Madhara atakayoyapata mchawi anayetaka kuwadhuru watu wa Mungu, ndio hayo hayo atakayoyapata mkristo anayeuacha wokovu na kuurudia ulimwengu. Mkristo ambaye ameshaonja kipawa cha Mungu na kuburudika na neema ya Mungu, na ghafla anarudia uasherati wake, anarudia wizi wake, anarudia matusi yake, anarudia mauaji yake, usagaji wake, utoaji mimba wake, mambo ambayo alikuwa ameshayaacha machafu anayarudia tena…akidhani kwamba mkono wa Mungu ni kinyume cha wale waliopo nje pasipo kujua hata waliopo ndani ambao wanataka kutoka vile vile mkono wa Mungu upo kinyume chao.
Wengi wetu hatupendi kusikia mambo kama haya kwasababu hatupendi kuumizwa mioyo, hatupendi kusikia habari mbaya, lakini fahamu kuwa tahadhari siku zote sio habari njema, lakini zina umuhimu sana katika maisha hususani katika siku za baadaye…hata vidonge tupewacho na wataalamu wa afya ambavyo vinatumika kwa tiba, bado vina tahadhari zake…lengo la tahadhari zile sio kuwatisha watumiaji wala kuwakatisha tamaa bali kuwanufaisha zaidi.
Vivyo hivyo Neema ya Kristo inayo tahadhari…Na ni lazima kila mtu aijue tahadhari hiyo, wahubiri wengi hawaifundishi kwasababu watakosa waumini, na wao bado wanatafuta waumini…Lakini sikia leo hii mtu wa Mungu tahadhari, ili baadaye tusije kujuta, na tahadhari hii haikuhusu wewe unayesoma tu, hapana hata mimi ninayeandika inanihusu. Biblia inasema.. Waebrania 10:26 “Maana, kama tukifanya dhambi kusudi baada ya kuupokea ujuzi wa ile kweli, haibaki tena dhabihu kwa ajili ya dhambi; 27 bali kuna kuitazamia hukumu yenye kutisha, na ukali wa moto ulio tayari kuwala wao wapingao. 28 Mtu aliyeidharau sheria ya Musa hufa pasipo huruma, kwa neno la mashahidi wawili au watatu. 29 Mwaonaje? Haikumpasa adhabu iliyo kubwa zaidi mtu yule aliyemkanyaga Mwana wa Mungu, na kuihesabu damu ya agano aliyotakaswa kwayo kuwa ni kitu ovyo, na kumfanyia jeuri Roho wa neema?”
Vivyo hivyo Neema ya Kristo inayo tahadhari…Na ni lazima kila mtu aijue tahadhari hiyo, wahubiri wengi hawaifundishi kwasababu watakosa waumini, na wao bado wanatafuta waumini…Lakini sikia leo hii mtu wa Mungu tahadhari, ili baadaye tusije kujuta, na tahadhari hii haikuhusu wewe unayesoma tu, hapana hata mimi ninayeandika inanihusu. Biblia inasema..
Waebrania 10:26 “Maana, kama tukifanya dhambi kusudi baada ya kuupokea ujuzi wa ile kweli, haibaki tena dhabihu kwa ajili ya dhambi;
27 bali kuna kuitazamia hukumu yenye kutisha, na ukali wa moto ulio tayari kuwala wao wapingao.
28 Mtu aliyeidharau sheria ya Musa hufa pasipo huruma, kwa neno la mashahidi wawili au watatu.
29 Mwaonaje? Haikumpasa adhabu iliyo kubwa zaidi mtu yule aliyemkanyaga Mwana wa Mungu, na kuihesabu damu ya agano aliyotakaswa kwayo kuwa ni kitu ovyo, na kumfanyia jeuri Roho wa neema?”
Kama umeamua kumfuata Yesu basi umfuate kweli kweli..usiusogelee kabisa ukuta wa Neema..uwe ndani au nje ni upanga ukatao kuwili..Neno la Mungu linasema usizini…hizo ni kuta!..neno linasema usiibe, usiue hizo ni kuta..ukipanda na kuzivuka nguvu ya Mungu utakumaliza..ambayo hiyo Mungu hakuiweka kwaajili ya kuua watu, bali kwaajili ya kuwalinda watu wake.
Bwana akubariki.
JE KUPONYWA NI UTHIBITISHO WA MUNGU KUWA NA WEWE?
USITUPE LULU ZAKO MBELE YA NGURUWE.
MWISHO WA DUNIA UTAKUJAJE?
NAO WALIOKUWA WAMEKUSUDIWA UZIMA WA MILELE WAKAAMINI.
Je kupiga miayo ni ishara ya mapepo?
Shalom jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe.
Kuna wakati Bwana Yesu aliwaambia mitume wake maneno haya..
Yohana 12:24 “ Amin, amin, nawaambia, Chembe ya ngano isipoanguka katika nchi, ikafa, hukaa hali iyo hiyo peke yake; bali ikifa, hutoa mazao mengi..”
Aliwaambia maneno haya, kwanza kutokana na wanafunzi wake kuona wingi wa watu waliokuwa wanamfuata ili waokolewe hususani wale waliotoka mpaka nchi za mbali kuja kumuona na pia alisema vile ili kuwafundisha wanafunzi wake, akijerea tendo, alilolifanya muda mfupi, au siku chache zilizopita,..
Na tendo lenyewe halikuwa lingine Zaidi ya lile la Lazaro..
Kama wengi wetu tunavyofahamu Lazaro alikuwa ni mtu aliyependwa na Yesu sana, alikuwa ni Rafiki wa Yesu tangu zamani, Lakini siku moja aliumwa sana, na taarifa zikamfikia Yesu, Lakini Yesu hakuchukua hatua yoyote, badala yake aliendelea kubaki kule kule mahali alipokuwepo, akamwacha aendelee kuugua mpaka afe,..
Na alipojua ameshakufa, bado hakufanya haraka kurudi siku hiyo hiyo kumuona, bali alingojea tena siku mbili, ndipo baadaye akashuka kwenda Bethania alipokuwa anaishi yeye na Dada zake..Kama tunavyosoma habari alipofika alimkuta ameshawekwa kaburini, anatoa harufu,.(Yohana 11 )
Unaweza ukajiuliza ni kwanini alimwacha mpaka aoze, ni kwasababu baadaye alikuwa anataka kuwafundisha wanafunzi wake kinadharia juu ya huo mstari tuliouona hapo juu, na madhara yake jinsi yatakavyokuwa..
Sasa Bwana Yesu alipofika na kumfufua Lazaro tena, na kumrudisha katika hali yake ya mwanzo tena katika afya Zaidi ya ile aliyokuwa nayo hapo mwanzo, biblia inatuonyesha tendo lile la kufufuka tu kwa Lazaro, lilikuwa ni tendo lililoutikisa ulimwengu wa giza… Yaani kwa ufupi ushuhuda ule wa Lazaro, uliwavuta watu wengi sana kwa Kristo, mpaka kufikia hatua ya wakuu wa Makuhani kutaka kumuua yeye naye (yaani Lazaro)…
Yohana 12:9 “Basi watu wengi katika Wayahudi walipata kujua ya kuwa yeye yuko huko, nao wakaja, si kwa ajili yake Yesu tu, ila wamwone na Lazaro, ambaye Yesu alimfufua katika wafu. 10 Nao wakuu wa makuhani wakafanya shauri la kumwua Lazaro naye; 11 maana kwa ajili yake wengi katika Wayahudi walijitenga, wakamwamini Yesu”.
Yohana 12:9 “Basi watu wengi katika Wayahudi walipata kujua ya kuwa yeye yuko huko, nao wakaja, si kwa ajili yake Yesu tu, ila wamwone na Lazaro, ambaye Yesu alimfufua katika wafu.
10 Nao wakuu wa makuhani wakafanya shauri la kumwua Lazaro naye;
11 maana kwa ajili yake wengi katika Wayahudi walijitenga, wakamwamini Yesu”.
Hiyo ni kuonyesha kuwa jinsi gani Lazaro aliyekufa akazikwa akaoza alivyokuwa na athari kubwa katika ulimwengu wa roho, kuliko yule ambaye hakuwahi kupitia hayo.
Jiulize hapo kwanza kwanini Lazaro, hakuwa vile?..Kwanini hakukuwa na mtu aliyemfuatilia, kwanini hakumvuta mtu yeyote kwa Kristo, japokuwa alikuwa ni Rafiki wa Karibu wa Bwana Yesu, tena aliyependwa.
Hata sasa haijalishi mtu anaweza akawa anasema Kristo ni Rafiki yangu kiasi gani, anaweza akawa anakujua kweli kama Lazaro wa kwanza.. lakini hakujui kama Lazaro ambaye alikufa akaoza akazikwa, kisha akafufua tena..
Na ndio maana sasa Bwana Yesu akawaambia wanafunzi wake baada ya tukio lile kipindi kifupi baadaye..
Yohana 12:24 “Amin, amin, nawaambia, Chembe ya ngano isipoanguka katika nchi, ikafa, hukaa hali iyo hiyo peke yake; bali ikifa, hutoa mazao mengi..”
Ndipo mstari huo ulipokuwa chimbuko lake..Akiurejea mfano wa Lazaro..
Ikiwa wewe ulishaokoka lakini hutaki kuwa tayari kufa, na kuoza kwa habari ya dhambi, hata wakati mwingine kuonekana kuwa ni mjinga, au umerukwa na akili kwasababu tu hutaki kufanya jambo Fulani kwa ajili tu ya Kristo, basi huwezi kuwa Lazaro wa pili.Wala huwezi kudai kuwa umezaliwa mara ya pili.. Ikiwa utakuwa unaogopa kuacha kuvaa vimini kisa tu ndugu zako au marafiki zako watakuonaje, watakuita wewe ni mshamba, basi bado huwezi kumletea Kristo mazao yoyote, haijalishi utasema umedumu katika wokovu muda gani..wapo waliodumu na Kristo Zaidi ya sisi mfano Yuda, lakini hakuwa na mazao yoyote kwa Bwana, na mwingine huyu Lazaro ambaye alipendwa pia lakini hakuwa na matunda yoyote kwa Bwana, kwasababu walikuwa bado hawajafa kwa habari ya dhambi.
Ikiwa utaogopa, kuacha Maisha ya uzinzi kisa unawaonea haya hao waasherati wenzako ulionao, na marafiki zako, unaogopa watakuita mlokole, na wewe hutaki kuitwa hivyo, basi ujue mpaka hapo bado hujafa ukaoza ukafufuliwa na Kristo na hautakuwa na matunda yoyote yakumfaa Kristo. Ndugu habari hizi unazisikia kila kukicha lakini bado unafanya moyo wako kuwa mgumu, unazidi kujitoa katika mstari wa neema kidogo kidogo…
Ikiwa kweli tunatamani tuwe na matunda ya rohoni, basi tuwe radhi pia kuiacha dunia moja kwa moja, hiyo ndio kanuni ya Kristo wala hakuna njia nyingine ya mkato.
Kumbuka tena hili Neno
“Amin, amin, nawaambia, Chembe ya ngano isipoanguka katika nchi, ikafa, hukaa hali iyo hiyo peke yake; bali ikifa, hutoa mazao mengi..””
Bwana atusaidie sote,
Ubarikiwe sana..
SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?
Kati ya Unyakuo,dhiki kuu, utawala wa miaka 1000 kipi kinaanza
Mstari huu unamaana gani? ″Walakini hautapotea hata Unywele mmoja wa Vichwa vyenu? (Luka21:18)
Ni kwa namna gani Yesu amewekwa kwa kuanguka na kuinuka?
SWALI: Katika Luka 10:18, tunasoma Bwana Yesu alimwona shetani akianguka kutoka mbinguni kama umeme..na katika Ufunuo 12:7-9 Biblia inasema kulikuwa na vita mbinguni na shetani akatupwa chini..Sasa ni wakati gani ambao shetani alitupwa chini? Kabla ya dunia kuumbwa au wakati wa Bwana Yesu akiwa duniani. Na je shetani sasa yupo kifungoni?.
JIBU: Katika Luka 10 tukianzia juu kidogo mstari wa 17 unasema…
“Ndipo wale sabini waliporudi kwa furaha, wakisema, Bwana, hata pepo wanatutii kwa jina lako.18 Akawaambia, Nilimwona Shetani, akianguka kutoka mbinguni kama umeme.”
Hivyo mstari huu hauzungumzii vita vilivyokuwa vinaendelea mbinguni kabla ya dunia kuumbwa..ambapo shetani alitaka kujiinua na kutaka kuwa kama Mungu, na hatimaye akafukuzwa mbinguni na kutupwa chini duniani..Bali unazungumzia habari za shetani kutoka katika nafasi ya juu aliyonayo juu ya watu wa Mungu na kushushwa chini..Ndio maana Bwana Yesu alizungumza maneno yale mara tu baada ya wanafunzi wake kutoka huko na huko kuhubiri injili na kutoa pepo wengi…Sasa kitendo hicho cha kwenda kufungua watu, na mateka kuwaacha huru, wale waliofungwa na nguvu za giza za shetani na mapepo yake hilo ndilo anguko la shetani kutoka juu mpaka chini, ambalo Bwana alikuwa analizungumzia hapo.
Hali kadhalika tukio tunalolisoma katika Ufunuo 12:7-9..Ndilo tukio la vita vilivyotokea mbinguni kabla ya dunia kuumbwa ambapo shetani alijiharibia nafasi aliyokuwepo ikasababishia kutupwa chini duniani.
Ufunuo 12:7 “Kulikuwa na vita mbinguni; Mikaeli na malaika zake wakapigana na yule joka, yule joka naye akapigana nao pamoja na malaika zake;8 nao hawakushinda, wala mahali pao hapakuonekana tena mbinguni.9 Yule joka akatupwa, yule mkubwa, nyoka wa zamani, aitwaye Ibilisi na Shetani, audanganyaye ulimwengu wote; akatupwa hata nchi, na malaika zake wakatupwa pamoja naye”.
Hivyo maanguko ya shetani yapo mawili…Lile la kwanza ambalo lilitokea kabla ya sisi wanadamu kuumbwa, ambalo lilimfanya asiwe na uwezo tena wa kurudi mbinguni. Na anguko la pili ni la hapa duniani ambalo tangu wakati wa Bwana Yesu mpaka sasa linaendelea… na litakamilika katika mwisho wa dunia ambapo wale wote waliokuwa wamekusudiwa uzima wa milele watakapomalizika kuingia ndani na mlango wa Neema kufungwa (Hiyo ndiyo siku ambayo shetani ataanguka kikabisa kabisa)..
Siku hiyo ni siku ambayo shetani hatakuwa na chembe hata moja ya ngano mkononi mwake, atakuwa na makapi tu ambayo yatakwenda kuteketezwa kwa moto(Mathayo 3:12). Siku hiyo ndio atakuwa ameshindwa mbinguni na duniani.
Hivyo hata wakati huu tunapokwenda kuhubiri injili,kutoa pepo, kufungua watu, kuwafariji, kuwajenga kiimani na kuwatoa sehemu moja hadi nyingine, kama Mitume hawa walivyofanya…katika ulimwengu wa roho ni tunamnyang’anya shetani mateka kwa kasi sana na hivyo tunakuwa tunamwangusha katika ile nafasi aliyonayo ya juu na kumshusha chini..kwasababu nguvu ya shetani ipo katika idadi ya watu wa Mungu anaowateka sasa..
Hivyo ni muhimu sana kuhubiri injili kwa watu wote..
Sasa utahubirije injili?..Kwa maisha yako utahubiri injili, kwa uvaaji wako utahubiri, kwa mwenendo wako, kwa uimbaji wako, kwa maombi yako na kwa mchango wako wowote ule wa kifedha katika kazi ya injili utakuwa umeihubiri injili.
Na shetani hajafungwa sasa, bado yupo anafanya kazi atakuja kufungwa miaka 1000 baada ya mwisho wa dunia.
Maran atha
Roho Mtakatifu ni nani?.
NILIMWONA SHETANI, AKIANGUKA KUTOKA MBINGUNI.
Shalom, Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe daima..
Karibu tuzidi kujifunza maneno matakatifu ya Mungu, Na leo tutaona kwa ufupi habari ya mtu mmoja anayeitwa Absalomu mwana wa Daudi naamini lipo jambo utajifunza ndani yake..
Huyu Absalomu alikuwa ni mmojawapo wa wana wengi wa Daudi, isipokuwa yeye alikuwa anabeba kitu kingine cha ziada ambacho kilikuwa kinamtofautisha na wana wote wa Daudi waliokuwa katika enzi yake ya kifalme.
Biblia inatueleza Absalomu, alikuwa ni kijana mzuri sana (kwa lugha ya kiingereza labda tunaweza tukasema Handsome), sio tu katikati ya ndugu zake, bali pia katika Israeli nzima ndivyo walivyomwona, hakukuwa na kijana aliyekuwa mzuri kama yeye, kuanzia utosi wa kichwa chake, mpaka uwayo wa miguu yake, wanasema hakuna mwanadamu asiye na mapungufu, lakini huyu Absalomu yeye hakuwa na upungufu wowote katika mwili wake. Kila kiungo chake cha mwili kilionekana kizuri na cha kuvutia, na alisifiwa na kila mtu..
Na Zaidi ya yote, biblia imezitaja hizo nywele zake, inasema, alikuwa na nywele nzuri nzito, ambazo alikuwa hawezi kuziacha Zaidi ya mwaka mmoja bila kuzinyoa vinginevyo vitamlemea sana, embu tusome kidogo..
2Samweli 14:25 “Basi katika Israeli wote hapakuwa na mtu hata mmoja mwenye kusifiwa kwa uzuri wake kama huyo Absalomu; tangu nyayo za miguu yake hata utosi wa kichwa chake hapakuwa na ila kwake. 26 Naye aliponyoa kichwa, (basi mwisho wa kila mwaka hunyoa; na kwa sababu nywele zilikuwa nzito kwake, kwa hiyo akanyoa;) hupima nywele za kichwa chake shekeli mia mbili kwa uzani wa mfalme.”
2Samweli 14:25 “Basi katika Israeli wote hapakuwa na mtu hata mmoja mwenye kusifiwa kwa uzuri wake kama huyo Absalomu; tangu nyayo za miguu yake hata utosi wa kichwa chake hapakuwa na ila kwake.
26 Naye aliponyoa kichwa, (basi mwisho wa kila mwaka hunyoa; na kwa sababu nywele zilikuwa nzito kwake, kwa hiyo akanyoa;) hupima nywele za kichwa chake shekeli mia mbili kwa uzani wa mfalme.”
Unaona, ukisoma hapo utaona nywele hizo alikuwa akishazinyoa zilikuwa zinakwenda kupimwa kwenye uzani wa mfalme, na inapatikana shekeli mia mbili ambayo ukiigeuza kwa vipimo vya kisasa ni Zaidi ya kilogramu 2.. Unaweza kutengeneza picha uzito wa kilo mbili ulikuwa unamlemea kichwani pake kama asipokata nywele zake baada ya mwaka mmoja..
Ili kuelewa vizuri, wanasema mtu wa kawaida ambaye amebahatika kuwa na nywele nyingi na zinazokuwa, akaziacha mwaka mzima, ili uzito wake uweze kufikia ule wa nywele za Absalomu kwa mwaka, basi itahitaji wachukuliwe watu kama yeye thelathini (30) kwa mwaka, kisha zichanganywe ndipo zitafikia uzito wa nywele za Absalomu ndani ya mwaka mmoja..
Hivyo unaweza kuona jinsi gani mtu huyu alipewa umbile la kipekee sana, na uzuri wa tofauti, nywele zenye utofauti sana lakini tunaposoma biblia tukumbuke kuwa siku zote biblia inapotaja umbile Fulani la mtu, basi tujue kuwa lina sehemu Fulani ya kusimamia katika habari husikia mbeleni,.. Hivyo kutajwa kwa sifa za nywele za Absalomu, ni wazi kuna mahali litatumika huko mbeleni..
Hivyo ukipata muda wako binafsi wa utulivu unaweza kuzisoma habari zake, kwa urefu na jinsi alivyokuwa, (2Samweli 13-18 )lakini kwa ufupi ni kuwa Absalomu, Japokuwa alikuwa na uzuri na umbile la kipekee na maneno ya kuvutia ambayo yaliweza kuifanya Israeli yote wampende mpaka kutaka kumfanya awe mfalme, lakini moyo wake ulikuwa ni tofauti na watu walivyokuwa wanamdhania..
Kwanza alikuwa na lengo la kuudondosha ufalme wa baba yake Daudi kinyume chake ili yeye atawale na Zaidi ya yote alikuwa anamtafuta baba yake ili amuue, pili alikuwa radhi hata kulala na Masuria 10 wa baba yake ili kuwaonyesha watu kuwa hampendi, japokuwa baba yake hakuwahi kumfanyia ubaya wowote..Na tatu alikuwa radhi kumuua ndugu yake, ambaye alilala na Dada yake, wala hakumsamehe..
Kwahiyo Absalomu, alikuwa ni mwovu, wala hakuwa mtu mwema, licha ya kuwa alikuwa ni mzuri na mwenye ushawishi wa maneno kwa watu.
Sasa ukizidi kusoma habari utaona alipokusudia kumwangamiza baba yake(Daudi), baada ya kumfukuza kwenye kiti cha enzi, aliondoka kwenda msituni yeye pamoja na jeshi kubwa la Israeli nyuma yake..Biblia inatuambia vita ilikuwa vikali sana katika msitu ule mkubwa sana.. Na unajua jinsi misitu ilivyo, vichaka vizito na miti ya Kamba Kamba za miiba inakuwa ni mingi sana, na inakuwa ni rahisi mtu kunaswa katika vichaka hivyo kama hutakuwa mwepesi..
Sasa kutokana na msitu ule kuwa mzito sana, biblia inasema watu waliokufa kwa uzito wa msitu ule, walikuwa ni wengi kuliko waliokufa kwa upanga.. Na huko huko lipo jambo ambalo Absalomu naye alikutana nalo embu tusome kwa ufupi..
2Samweli 18:6 “Hivyo watu wakatoka waende nyikani ili kupigana na Israeli; na vita vikatokea ndani ya msitu wa Efraimu. 7 Watu wa Israeli wakapigwa huko mbele ya watumishi wa Daudi, kukawa na maangamizo makuu huko siku ile, ya watu ishirini elfu. 8 Kwa maana vita vilienea huko juu ya uso wote wa nchi; na siku ile huo msitu ukala watu wengi kuliko wale walioliwa na upanga. 9 NA KWA BAHATI ABSALOMU AKAKUTANA NA WATUMISHI WA DAUDI. NAYE ABSALOMU ALIKUWA AMEPANDA NYUMBU WAKE, NA YULE NYUMBU AKAPITA CHINI YA MATAWI MANENE YA MWALONI MKUBWA, HATA KICHWA CHAKE KIKAKWAMA KATIKA MWALONI HUO, AKANYAKULIWA JUU KATI YA MBINGU NA NCHI; NA YULE NYUMBU ALIYEKUWA CHINI YAKE AKAENDA MBELE. 10 Basi mtu mmoja akaona hayo, akaenda akamwambia Yoabu, akasema, tazama, mimi nalimwona Absalomu ametundikwa katika mwaloni. 11 Naye Yoabu akamwambia mtu yule aliyempasha habari, Je! Wewe umeona haya; Mbona, basi, hukumpiga hata nchi papo hapo? Nami ningalikupa fedha kumi na mshipi. 12 Yule mtu akamwambia Yoabu, Kama ningalipata fedha elfu mkononi mwangu, hata hivyo singalinyosha mkono wangu juu ya mwana wa mfalme; kwa maana mfalme masikioni mwetu alikuagiza wewe, na Abishai na Itai, akisema, Angalieni sana mtu awaye yote asimguse yule kijana, Absalomu. 13 Na tena, kama ningaliitendea roho yake kwa hila; (wala hapana neno lo lote liwezalo kufichwa mbele ya mfalme); ndipo wewe mwenyewe ungalijitenga. 14 Ndipo Yoabu akasema, Siwezi kungoja na kusema nawe hivi. Akachukua vyemba vitatu mkononi mwake, akamchoma Absalomu moyoni, alipokuwa akali hai katikati ya ule mwaloni. 15 Kisha vijana kumi, waliomchukulia Yoabu silaha zake wakamzunguka, wakampiga Absalomu, na kumwua.
2Samweli 18:6 “Hivyo watu wakatoka waende nyikani ili kupigana na Israeli; na vita vikatokea ndani ya msitu wa Efraimu.
7 Watu wa Israeli wakapigwa huko mbele ya watumishi wa Daudi, kukawa na maangamizo makuu huko siku ile, ya watu ishirini elfu.
8 Kwa maana vita vilienea huko juu ya uso wote wa nchi; na siku ile huo msitu ukala watu wengi kuliko wale walioliwa na upanga.
9 NA KWA BAHATI ABSALOMU AKAKUTANA NA WATUMISHI WA DAUDI. NAYE ABSALOMU ALIKUWA AMEPANDA NYUMBU WAKE, NA YULE NYUMBU AKAPITA CHINI YA MATAWI MANENE YA MWALONI MKUBWA, HATA KICHWA CHAKE KIKAKWAMA KATIKA MWALONI HUO, AKANYAKULIWA JUU KATI YA MBINGU NA NCHI; NA YULE NYUMBU ALIYEKUWA CHINI YAKE AKAENDA MBELE.
10 Basi mtu mmoja akaona hayo, akaenda akamwambia Yoabu, akasema, tazama, mimi nalimwona Absalomu ametundikwa katika mwaloni.
11 Naye Yoabu akamwambia mtu yule aliyempasha habari, Je! Wewe umeona haya; Mbona, basi, hukumpiga hata nchi papo hapo? Nami ningalikupa fedha kumi na mshipi.
12 Yule mtu akamwambia Yoabu, Kama ningalipata fedha elfu mkononi mwangu, hata hivyo singalinyosha mkono wangu juu ya mwana wa mfalme; kwa maana mfalme masikioni mwetu alikuagiza wewe, na Abishai na Itai, akisema, Angalieni sana mtu awaye yote asimguse yule kijana, Absalomu.
13 Na tena, kama ningaliitendea roho yake kwa hila; (wala hapana neno lo lote liwezalo kufichwa mbele ya mfalme); ndipo wewe mwenyewe ungalijitenga.
14 Ndipo Yoabu akasema, Siwezi kungoja na kusema nawe hivi. Akachukua vyemba vitatu mkononi mwake, akamchoma Absalomu moyoni, alipokuwa akali hai katikati ya ule mwaloni.
15 Kisha vijana kumi, waliomchukulia Yoabu silaha zake wakamzunguka, wakampiga Absalomu, na kumwua.
Utaona, hapo Absalomu, alipopita sehemu moja, biblia inasema kichwa chake kikakwama, kwenye mti mmojawapo, na yule farasi aliyekuwa chini yake akazidi kuendelea mbele, hivyo yeye akabakia pale pale amening’inia. Sasa, biblia inaposema kichwa inamaanisha eneo la nywele kwa ujumla wake, Ni kwamba zile nywele nyingi za Absalomu zilikwama kwenye vijiti vya miti, zikajisongorotesha pale, kwa namna ambayo asingeweza kuzifumua, akabakia tu anani’ngia nia tu pale kwa maumivu.. alikaa pale muda mrefu akijaribu lakini alishindwa kutoka mpaka mauti ilipomfika kwasababu ule uzuri wake ndio ulikuwa kitanzi chake..
Ndugu, hata sasa, watu wengi hawajui kuwa kile kinachowafanya wavutie, au wapendwe ndani yao ndio kitakuwa kitanzi chao baadaye ikiwa hawatasimama katika mstari wa wokovu.. Ikiwa ni mali zako zinakupa kiburi kumbuka yale maneno ya Bwana, Ni rahisi kwa ngamia kupenya katika tundu la sindano… Ikiwa ni urembo wako wewe binti, unajiona sasa huna haja ya Mungu bado wewe unavutia, una umbile zuri, kila mwanaume akikuangalia anakutamani, wakati utafika huo huo uzuri wako utakuwa kitanzi kwako, utanasa mahali ambapo hutatoka, na adui yako shetani atakumaliza kirahisi mbele ya macho yako ukiona kama ilivyokuwa kwa Absalomu, na ukajikuta katika lile ziwa la moto,..Vivyo hivyo na mambo mengine yote.
Huu ni wakati sasa wa kumtazama Kristo, na kuomba rehema kwake, kama na wewe umedanganywa na mojawapo ya hayo mambo, uzuri wako na utanashati wako. Tubu umgeukie Mungu, ili Mungu akurehemu na kukupa uzima wa milele. Nyosha njia yako kwa kuliamini na kulitii Neno la Mungu.
UCHAWI WA BALAAMU.
USIPOWATAMBUA YANE NA YAMBRE, KATIKA KANISA LA KRISTO, UJUE UMEPOTEA.
Je! ni kweli Bwana Yesu alibatiza mtu akiwa hapa duniani?
JIBU: Bwana Yesu yeye mwenyewe hakubatiza bali wanafunzi wake ndio waliobatiza kwa agizo lake yeye. Hata leo mkuu wa nchi akitoa agizo la ujenzi wa jengo Fulani la serikali…Jengo lile litakapojengwa na kumalizika..jengo hilo litajulikana kama limejengwa na Mkuu huyo…lakini kiuhalisia sio yeye aliyelijenga waliolijenga ni wale vibarua na wafanyakazi wake…lakini kwasababu ni mkuu ndio katoa hiyo amri na fedha basi ni sahihi kabisa kusema ni Mkuu huyo ndiye kajenga jengo lile.
Kadhalika kuna mahali kwenye biblia paliposema Bwana Yesu alibatiza…lakini ukiendelea mbele kidogo utaona biblia imefafanua zaidi waliobatiza ni wakina nani…kwamba ni wanafunzi wake kwa amri yake na sio Bwana Yesu mwenyewe.
Tusome.
Yohana 4:1 “Kwa hiyo Bwana, alipofahamu ya kuwa Mafarisayo wamesikia ya kwamba, Yesu anafanya wanafunzi wengi kuliko Yohana, na kuwabatiza, 2 (lakini Yesu mwenyewe hakubatiza, bali wanafunzi wake,) 3 aliacha Uyahudi, akaenda zake tena mpaka Galilaya”.
Yohana 4:1 “Kwa hiyo Bwana, alipofahamu ya kuwa Mafarisayo wamesikia ya kwamba, Yesu anafanya wanafunzi wengi kuliko Yohana, na kuwabatiza,
2 (lakini Yesu mwenyewe hakubatiza, bali wanafunzi wake,)
3 aliacha Uyahudi, akaenda zake tena mpaka Galilaya”.
Unaona hapo mstari wa pili unafafanua zaidi kwamba siye Bwana Yesu aliyebatiza bali ni wanafunzi wake.
Pamoja na hayo yote Jambo lingine la msingi hapo la kujifunza ni kwamba watu walianza kubatizwa kabla hata ya Bwana Yesu kusulubiwa, kufa na kufufuka ..kuonyesha ni jingi gani ubatizo ulivyokuwa wa muhimu…Ni agizo la awali kabisa pale mtu anapomwamini Yesu na kutubu dhambi zake.
Hivyo nasi tunajifunza kama hatujazingatia kwenda kubatizwa ubatizo sahihi tukidhani sio agizo la msingi, hapa tunaonyeshwa watu walianza kubatizwa kabla ya Kristo kwenda Golgotha, ..kuashiria umuhimu wa hicho kitu, na kumbuka pia ubatizo hautekelezwi kama mtu anavyoamua kwamba unaweza kuzamishwa kichwa tu kwenye maji na ukawa tayari umeshabatizwa, au unaweza kutumia mchanga badala ya maji, au unaweza kunyunyiziwa tu badala ya kuzama mwili mzima…hakuna njia mbadala ya ubatizo..Neno ubatizo maana yake ni KUZAMISHWA. Na kuzama maana yake ni kuzama hakuna maana nyingine ya neno hilo. Hivyo tunazamishwa katika maji mengi (kama Yohana 3:23 inavyosema), na kwa Jina la Bwana Yesu Kristo kama (Matendo 2:38,8:16, 10:48, 19:5 inavyosema).
Tuyazingatie hayo na Bwana atatukubali na kutubariki.
Muhtasari wa maelezo haya kwa njia ya video unaweza kuyapata hapa chini.
[embedyt] https://www.youtube.com/watch?v=68fHuz_icug[/embedyt]. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
MIILI YA UTUKUFU ITAKUWAJE?
DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.
LIVUNJENI HEKALU HILI, NAMI KATIKA SIKU TATU NITALISIMAMISHA.
MWACHE YESU, NDIO AWE WA KWANZA KUKUHURUMIA.
LOLOTE ATAKALOWAAMBIA FANYENI.
WhatsApp