Atakapokuja Mwana wa Adamu, je! Ataiona imani duniani? Maana yake nini?

Atakapokuja Mwana wa Adamu, je! Ataiona imani duniani? Maana yake nini?

SWALI: Bwana Yesu alimaanisha nini kusema “walakini, atakapokuja Mwana wa Adamu, je! Ataiona imani duniani?”


JIBU: Ili tupate picha kamili tuisome habari yake kuanzia juu kidogo, kwasababu Bwana alichokisema kinategemea hiyo habari iliyokuwa juu yake…

Luka 18 :1-8

“1 Akawaambia mfano, ya kwamba imewapasa kumwomba Mungu sikuzote, wala wasikate tamaa.

2 Akasema, Palikuwa na kadhi katika mji fulani, hamchi Mungu, wala hajali watu.

3 Na katika mji huo palikuwa na mwanamke mjane, aliyekuwa akimwendea-endea, akisema, Nipatie haki na adui wangu.

4 Naye kwa muda alikataa; halafu akasema moyoni mwake, Ijapokuwa simchi Mungu wala sijali watu,

5 lakini, kwa kuwa mjane huyu ananiudhi, nitampatia haki yake, asije akanichosha kwa kunijia daima.

6 Bwana akasema, Sikilizeni asemavyo yule kadhi dhalimu.

7 Na Mungu, je! Hatawapatia haki wateule wake wanaomlilia mchana na usiku, naye ni mvumilivu kwao?

8 Nawaambia, atawapatia haki upesi; walakini, atakapokuja Mwana wa Adamu, je! Ataiona imani duniani”?

Kama tunavyosoma hapo alipomaliza tu kueleza hiyo habari ya huyo mjane ndipo akaongezea na hicho kipenge mwishoni.. “walakini, atakapokuja Mwana wa Adamu, je! Ataiona imani duniani”? Kumaanisha kuwa siku ya kuja kwake anatazamia kuona imani yenye mfano wa huyo mwanamke, kama kigezo cha mtu kunyakuliwa.

Huyo mwanamke, hakuvunjwa moyo, pale alipoona hakuna dalili yoyote ya kutendewa haki na Yule kadhi dhalimu, lakini aliendelea hivyo hivyo tu kila siku kama kipofu, akiamini siku moja atapatiwa haki yake, na mwisho wa siku akaipata, jaribu kujiweka wewe katika mazingira kama hayo, ni wazi utakata tamaa mapema pale unapoona mtu hata haoneshi dalili ya kukusikiliza, unaweza kusema anadharau, lakini kumbe hujui moyoni mwake unamtesa sana.

Vivyo hivyo, katika nyakati hizi za mwisho, nyakati za masumbufu ya maisha, nyakati ambazo watu wengi wamekata tamaa ya kumngojea Yesu, wengine wamerudi kwenye dunia, wengine wanadhihaki wanasema huyo Yesu mnayemsubiria yupo wapi? Kama biblia inavyosema katika..

2Petro 3:3 “Mkijua kwanza neno hili ya kwamba katika siku za mwisho watakuja na dhihaka zao watu wenye kudhihaki, wafuatao tamaa zao wenyewe,

4 na kusema, Iko wapi ahadi ile ya kuja kwake? Kwa maana, tangu hapo babu zetu walipolala, vitu vyote vinakaa hali iyo hiyo, tangu mwanzo wa kuumbwa”.

Wengine watasema mnamwomba yeye ambaye hawajali..unaona?

Lakini siku atakapokuja Yesu, jambo la kwanza kama alivyosema ni kuwa ataangalia IMANI kwanza, ataaangalia wale waliokuwa na Imani kwake, ambao hawakukatishwa tamaa kuomba ufalme wake uje, (Mathayo 6:9), japokuwa alionekana kama amechelewa, watu ambao hawakuruhusu kurudi nyuma..hao ndio atakaowaangalia..Na hao ndio kitendo cha kufumba na kufumbua watatoweka duniani siku ile.

Wengine wote watabaki hapa duniani, na wale ambao walikuwa wameshakufa tayari, Jicho la Yesu nalo litatazama mpaka kule makaburini, kama mtu alikufa bila imani hiyo, atabakia pale pale makaburini, watakaofufuliwa ni wale tu ambao mpaka dakika ya mwisho ya maisha yao waliishi kama vile Yesu anarudi muda wao, hao ndio watakaosikia sauti yake mwana wa Adam una wataungana na wale walio hai kwa pamoja kwenda kwenye karama ya mwana-kondoo mbinguni.

Lakini swali ni Je! imani hiyo ipo ndani yetu au imeshakufa siku nyingi?..Jibu unalo. Tunachopaswa kufanya sasa, ni kutungeneza mahusiano yetu na Mungu vizuri katika hichi kipindi kifupi cha maisha tulichobakiwa nacho hapa duniani, tujue kalenda ya Mungu duniani sasa ni ipi?…Pale ulimwengu unapozidi kwenda mbali na Imani na kudhihaki sisi ndio tuzidi kuomba na kumlilia Mungu zaidi kama huyu mjane..

Na siku moja isiyokuwa na jina, kitendo cha kufumba na kufumbua, tutajiona pale mawingu na majeshi ya malaika wengi yamekuja kutulaki, na parapanda ya Mungu. Itakuwa ni raha isiyo na kifani, maneno ya kibinadamu hayawezi kuelezea. Hivyo tuishi kwa Imani Bwana atakapokuja aione ndani yetu.

Jina la Bwana libarikiwe Milele.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

REKEBISHA YAFUATAYO ILI MAMBO YAENDE SAWA.

Uwanda wa dura ni nini?

JE UDHAIFU WANGU UNAWEZA KUZUIA INJILI?

MTI WA UZIMA NA MTI WA MAARIFA.

Mlima sinai upo nchi gani? Na Je unaijua Sinai yako ya rohoni?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Nifanye nini ili niishi maisha ya ushindi siku zote?

Maisha ya ushindi


Shalom,

Awali ya yote ni lazima ufahamu kuwa kupita katika majaribu, kupita katika dhiki, kupita katika mateso, haimaanishi kuwa umeshindwa, hapana hivyo vyote vinaitwa vita,..Kushindwa ni pale, vita hivyo vinapokuzidi nguvu na hatimaye kukuangusha kabisa..hapo ndio umeshindwa.

Kwasababu kama ingekuwa kila anayepitia majaribu au dhiki au shida, au bonde la mauti ni kushindwa, basi Daudi angekuwa wa kwanza, kwasababu yeye, kila kukicha alikuwa anapita katika hali ya kukimbizwa na maadui zake na hatari za kufa, mpaka wakati mwingine anakwenda kuomba msaada kutoka kwa maadui zake wengine ili tu wampe hifadhi kwa muda. Lakini katika yote alikuwa na uhakika kuwa maisha yake ni ya ushindi tu..mpaka akaandika katika Zaburi 23 “Bwana ndiye mchungaji wangu, Sitapungukiwa na kitu…. Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, Gongo lako na fimbo yako vyanifariji”. (Zab 23)

Na kweli kama tunavyojua mwisho wa siku aliibuka mshindi, na kuwa mfalme wa Israeli, na mpaka sasa habari zake tunazisoma,

Hata Bwana wetu Yesu,vivyo hivyo alijaribiwa kama sisi tulivyojaribiwa, hata zaidi ya sisi lakini katika majaribu yake yote, hakuwahi kushindwa na hata moja, wala hakuwahi kutenda dhambi.. Na ndio maana akatuambia..

Yohana 16:33 “Hayo nimewaambieni mpate kuwa na amani ndani yangu. Ulimwenguni mnayo dhiki; lakini jipeni moyo; mimi nimeushinda ulimwengu”.

Unaona? Na watakatifu wengine wote kwenye biblia hivyo hivyo..

Lakini siri ya ushindi wao ilikuwa ni nini?

Je ni nguvu zao? Au bidii zao? Au ni nini.. Biblia imeshatoa jibu na kusema, mtu anayeweza kuushinda ulimwengu,(kuishi maisha ya ushindi) ni mtu Yule ambaye amezaliwa na Mungu tu.

1Yohana 5:4 “Kwa maana kila kitu kilichozaliwa na Mungu huushinda ulimwengu; na huku ndiko kushinda kuushindako ulimwengu, hiyo imani yetu”.

Unaona?, Ni mtu tu aliyezaliwa na Mungu ndio anapokea uwezo huo wa kuushinda ulimwengu, si mtu mwingine yeyote, nguvu za mtu binafsi haziwezi, bidii za mtu haziwezi, fedha ya mtu haiwezi, wala kipaji cha mtu hakiwezi kuushinda ulimwengu.

Huwezi kumshinda shetani atakapokuletea majaribu kama hujazaliwa na Mungu (yaani hujazaliwa mara ya pili), haiwezekani kuushinda uzinzi, haiwezekani kuishinda dhambi ile inayokusumbua, ni ngumu kuwashinda wachawi na mapepo, vilevile ni ngumu kuishi maisha ya amani na furaha hapa duniani.

Kwasababu Mungu anakuwa hayupo upande wako kukutia nguvu..Lakini wale ambao Mungu yupo ndani yao..biblia inasema hivi.

Warumi 8:31 “Basi, tuseme nini juu ya hayo? Mungu akiwapo upande wetu, ni nani aliye juu yetu?

32 Yeye asiyemwachilia Mwana wake mwenyewe, bali alimtoa kwa ajili yetu sisi sote, atakosaje kutukirimia na mambo yote pamoja naye?

33 Ni nani atakayewashitaki wateule wa Mungu? Mungu ndiye mwenye kuwahesabia haki.

34 Ni nani atakayewahukumia adhabu? Kristo Yesu ndiye aliyekufa; naam, na zaidi ya hayo, amefufuka katika wafu, naye yuko mkono wa kuume wa Mungu; tena ndiye anayetuombea.

35 Ni nani atakayetutenga na upendo wa Kristo? Je! Ni dhiki au shida, au adha, au njaa, au uchi, au hatari, au upanga”?

Kwa mtu aliyezaliwa mara ya pili kunakuwa na nguvu Fulani ya ajabu kutoka kwa Mungu inayomlinda asitetereke pindi unapopitia majaribu mazito ulimwenguni.

Hivyo ukiwa kama hujaokoka, au ulikuwa upo nusu nusu, (yaani mguu mmoja nje,mwingine ndani) na ndio maana maisha yako yamekuwa ni ya kushindwa kudumu katika wokovu, ya kushindwa kusimama, ya kushindwa kuwa na mahusiano mazuri na Mungu. Basi leo hii fanya uamuzi thabiti wa kumpa Yesu maisha yako upya kwa kumaanisha kabisa.

1Yohana 1:9 “Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote”.

Kama upo tayari kumruhusu Yesu ayaunde upya maisha yako, basi uamuzi huo ni wa busara, sana, fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba. Na pia kama unahitaji kubatizwa pia usisite kuwasiliana nasi .>>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Ikiwa umefungua na kufuata hayo maelekezo hapo juu, basi mpaka hapo tayari ushindi wa kwanza umepata wa mauti..

1Wakorintho 15:55 “Ku wapi, Ewe mauti, kushinda kwako? U wapi, Ewe mauti, uchungu wako?

Vilevile wachawi na mapepo hawatakuweza, kwa lolote..

Kuanzia huo  wakati utakapobatizwa na kuendelea utaanza kuona mabadiliko ya tofauti katika maisha yako,.Sina mengi ya kusema, wewe mwenyewe utayashuhudia.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye  namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

HIZI NI NYAKATI ZA KUJIINGIZA KWA NGUVU.

OLE WAO WANAOJITAHIDI KUMFICHA BWANA MASHAURI YAO.

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

NINI KINATOKEA BAADA YA KIFO?

KUZIMU NI WAPI

Rudi Nyumbani:

Print this post

JIFUNZE KULIGAWANYA VYEMA NENO LA MUNGU.

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo lizidi kubarikiwa.

Karibu tujifunze Neno la Mungu wetu.

Kama ni msomaji mzuri wa Biblia utakuwa unayajua majaribu matatu ya Yesu aliyojaribiwa na Ibilisi kule jangwani. Jambo la ajabu ni kwamba shetani hakwenda kumjaribu Bwana Yesu kwa uchawi, au kwa magonjwa au kwa maneno yake, bali alikwenda kumjaribu kwa kutumia maandiko matakatifu.

 Maana yake ni kwamba kitengo kikubwa cha Majaribu ya shetani kwa mkristo hakipo kwa wachawi, au kwa waganga wa kienyeji kama watu wengi wanavyofikiri,  BALİ KİPO KATİKA NENO LA MUNGU. Na shetani hatumii nguvu nyingi kututumia majeshi ya wachawi wake kama unavyohubiriwa na watu, bali anatumia nguvu kubwa kuhakikisha kwamba hulielewi Neno la Mungu, na hapo akifanikiwa basi unakua umekwisha!.. Bwana wetu Yesu asingekuwa analijua Neno kweli kweli, basi asingemweza shetani kamwe..Lakini shetani hakumweza kwasababu yeye ndio aliyekuwa Neno mwenyewe.

Wengi wetu tunakosa shabaha hapo, Tukidhani uadui mkubwa wa shetani kwetu ni waganga wa kienyeji na wachawi wanaotuzunguka…jambo linalompelekea Mkristo kutwa kuchwa kupambana na wachawi katika maombi.. Na kusahau kuwa silaha yake kubwa ni Neno la Mungu (Ndio upanga) Waefeso 6:17. Na pasipo kujua kuwa asipokuwa na Neno la Mungu la kutosha ndani yake basi tayari anakuwa kalogwa na shetani siku nyingi (Wagalatia 3:1)..Hata kama atakuwa anasali na kupiga maombi ya vita kila siku.

Sasa hebu tusome kwa ufupi jinsi Bwana alivyomjibu shetani katika yale majaribu na kisha tutajifunza kitu cha muhimu sana. Usipite hata kama ulishasoma rudia tena.

Mathayo 4:1  “Kisha Yesu alipandishwa na Roho nyikani, ili ajaribiwe na Ibilisi. 

2  Akafunga siku arobaini mchana na usiku, mwisho akaona njaa. 

3  Mjaribu akamjia akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, amuru kwamba mawe haya yawe mikate. 

4  Naye akajibu akasema, Imeandikwa, Mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu. 

5  Kisha Ibilisi akamchukua mpaka mji mtakatifu, akamweka juu ya kinara cha hekalu

6  akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu jitupe chini; kwa maana imeandikwa, Atakuagizia malaika zake; Na mikononi mwao watakuchukua; Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe. 

7  Yesu akamwambia, Tena imeandikwa, Usimjaribu Bwana Mungu wako. 

8  Kisha Ibilisi akamchukua mpaka mlima mrefu mno, akamwonyesha milki zote za ulimwengu, na fahari yake, 

9  akamwambia, Haya yote nitakupa, ukianguka kunisujudia. 

10  Ndipo Yesu alipomwambia, Nenda zako, Shetani; kwa maana imeandikwa, Msujudie Bwana Mungu wako, umwabudu yeye peke yake. 

11  Kisha Ibilisi akamwacha; na tazama, wakaja malaika wakamtumikia”

Kama tunavyojua maneno yote shetani aliyomwambia Bwana Yesu hapo , hayakuwa ya UONGO! Yote yalikuwa ya kweli na yapo katika biblia, yalikuwa ni maneno ya Mungu yenye pumzi ya uhai (hivyo upo ukweli unaopotosha)…na yote shetani aliyatoa katika biblia..Kwamfano hilo Neno “Atakuagizia malaika zake; Na mikononi mwao watakuchukua” Ni Neno la Zaburi 91:12.

Lakini shetani aliyapindisha yale maneno na kuyafanya yatumike mahali ambapo sio sahihi, na kwa wakati usio sahihi. Maneno ya Mungu yakitumika mahali ambapo sio sahihi na kwa wakati ambao sio sahihi yanakuwa ni sumu kubwa.

Kwamfano Neno la Mungu ni kweli linasema.. “waume waishi na wake zao kwa akili na kumpa mke heshima (1Petro 3:7)”..Sasa Neno hili linawahusu Wanaume waliooa ndoa halali ya kimaandiko…Na si mtu yeyote tu hata anayeishi na girlfriend wake. Nimewahi kukutana na watu wanaoishi pasipo kuonana na wanautumia huu mstari kwa madai kwamba Mungu amesema “tuishi na wake kwa akili”. Nimewahi kukutana na mwingine akiwashawishi wanawake kufanya nao uzinzi huku akitumia hichi kipengele cha maandiko.. 1Wakorintho 7:5 “Msinyimane isipokuwa mmepatana kwa muda, ili mpate faragha kwa kusali; mkajiane tena, Shetani asije akawajaribu kwa kutokuwa na kiasi kwenu”.

Hivyo mwanamke yeyote anayekutana naye anakimbilia kumwonyesha huu mstari, na kusema hata Mungu amesema “tusinyimane” na amefanikiwa kuwanasa mabinti wengi kwa andiko halo…Pasipo kufahamu kuwa hilo andiko linawahusu wana-ndoa tu!(watu ambao tayari wameoana) na sio kila mtu tu!.

Sasa shetani alimjia Yesu kwa njama hiyo hiyo, kuyaweka maneno ya Mungu mahali pasipopaswa na kwa wakati usiofaa.

Anamwambia Bwana ajitupe chini na Mungu atamwagizia malaika waje wamchukue asijikwae…Ni kweli hilo ni Neno la Mungu, lakini huo sio wakati wake..Neno hilo litafaa kutumika wakati ambao tumejikuta tumeingia majaribuni au hatarini pasipo hiari yetu, huo ndio wakati wa Bwana kuwaagiza malaika zake watuchukue. Lakini sio wakati ambao tupo salama halafu tunamjaribu Mungu tuone atafanya nini, tukifanya hivyo tunajitafutia laana badala ya baraka..

Na sisi tunapaswa tujifunze KULIGAWANYA VYEMA NENO LA MUNGU. Na hiyo inakuja kwa kulisoma Neno la Mungu kwa bidii. Ukisoma kijimstari kimoja tu na kwenda kulala! Ni rahisi kushindwa kuyagawanya Maneno ya Mungu ipasavyo..

Na pia usitumie nguvu kubwa kuchunguza mchawi wako ni nani?.. Tumia nguvu kubwa kuyachunguza maandiko!!…Je biblia inasema nini katika hali hiyo unayopitia?..Je katika biblia kuliwahi kutokea kisa kama hicho unachopitia na je kilitatuliwaje?.. Unapoona kuna kitu fulani hakipo sawa, tafuta kujua je! Biblia inasemaje kuhusu hiyo hali.. Usisubiri kufundishwa-fundishwa biblia, jifunze kuisoma mwenyewe..Utakutana na mambo mengi huko, ambayo hata mchungaji wako hawezi kukuhubiria, na pia utagundua ni vitu gani ulikuwa unapotoshwa na vitu gani ulikuwa unaambiwa ukweli.

Lakini ukisubiri tu kila somo unalokutana nalo mitandanoni, ni kulisoma tu, kwasababu mtumishi yule anaaminika na wengi!, au kila hubiri ni kusikiliza tu kwasababu mtumishi yule anasifiwa na wengi. Nataka nikuambie, utaishia kukosa mahali pa kusimamia, utakuwa ni mtu wa kupepesuka daima. Na kutufuta mchawi ni nani kwenye ukoo wako, kumbe uchawi ni kukosa kwako maarifa ya Neno la Mungu.

Hosea 4:6 “Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa;..”

Soma Biblia mwenyewe huo ndio uthibitisho wa kwanza wa kwamba umeamua kuanza safari ya kumjua Mungu.

Na Bwana akubariki

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

JINSI YA KUSOMA BIBLIA.

KWANINI TUNAPASWA TUJIZUIE?

UPONYAJI WA ASILI

JIOKOE WEWE NA NYUMBA YAKO.

MASOMO MBALIMBALI YA NENO LA MUNGU (2026).

Je! Mwanamke anapaswa afunikwe kichwa anapokuwa ibadani?

UNYAKUO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Jiepushe na tamaa ya Mali/kupenda fedha.

Kwa namna ya kawaida fedha haina ubaya wowote, ni nyezo ambayo Mungu aliiruhusu iwepo na itumiwe ili kuendesha kushughuli zote za kijamii.

Mhubiri 19:19 “…Na fedha huleta jawabu la mambo yote”.

Lakini kitendo cha kupenda fedha, hicho ndicho Mungu amekikatazata, na katika biblia kimekemewa sana, ikiwa wewe ni mtoto wa Mungu, na roho ya kupenda fedha ipo ndani yako, basi upo hatarini sana, kuzama katika maovu mengi..biblia inasema hivyo..

1Timotheo 6:10 “Maana shina moja la mabaya ya kila namna ni kupenda fedha; ambayo wengine hali wakiitamani hiyo wamefarakana na Imani, na kujichoma kwa maumivu mengi.”

Ndio maana biblia inawaasa sana watoto wa Mungu na kuwaambia..

Waebrania 13:5 “Msiwe na tabia ya kupenda fedha; mwe radhi na vitu mlivyo navyo; kwa kuwa yeye mwenyewe amesema, Sitakupungukia kabisa, wala sitakuacha kabisa”.

Mungu ametoa ahadi ya kuwahudumia watoto wake, kiasi kwamba hawatapungukiwa kabisa, hawatakosa kabisa ikiwa tu watakuwa watulivu katika shughuli zao.

Mtu mwenye tabia ya  kupenda fedha ni rahisi kuhonga, ili upate fursa Fulani,ni rahisi kufanya biashara haramu kisa tu ameona  zinamwingizia  fedha nyingi, mwingine atakuwa radhi hata kujiuza mwili wake kisa fedha, wengine wanakwenda kwa waganga, wengine wapo tayari kuikana imani,..n.k.n.k. hapo ndipo unajua ni kwanini biblia inasema kupenda fedha ni shina la mabaya yote ulimwenguni. Wengine wapo tayari hata kuua watu, ili walipwe au waibe.

Mithali 1:19 “Ndivyo zilivyo njia za kila mwenye tamaa ya mali; Huuondoa uhai wao walio nayo”.

Na dalili mojawapo ambayo biblia inasema itatutambulisha kuwa tunaishi katika siku za mwisho, ni kuibuka kwa wimbi kubwa la watu wanaopenda fedha.

2Timotheo 3:1 Lakini ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari.

2 Maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukana, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio safi,”

Mpaka sasa, imefikia hatua huduma za rohoni kutolewa kwa fedha,

1Timotheo 6: 5 “na majadiliano ya watu walioharibika akili zao, walioikosa kweli, huku wakidhani ya kuwa utauwa ni njia ya kupata faida”.

Hiyo yote ni matokeo ya wanadamu kupenda fedha..Bwana Yesu alisema..

Mathayo 6:24 “Hakuna mtu awezaye kutumikia mabwana wawili; kwa maana atamchukia huyu, na kumpenda huyu; ama atashikamana na huyu, na kumdharau huyu. Hamwezi kumtumikia Mungu na mali”.

Shetani alijua hapa ndipo wanadamu wengi wanapoweza kunaswa, hivyo, akatumia  njia hiyo hiyo kumjaribia pia Yesu, akamwambia nitakupa milki zote za ulimwenguni, nitakupa fedha zote na majumba yote ikiwa utanisujudia tu. Lakini Bwana Yesu alimkemea akamwambia utamsujudia Bwana Mungu wako tu.. Kwasababu alijua kupenda fedha ni kuupenda ulimwengu.

1Yohana 2:15 “Msiipende dunia, wala mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake”.

Kama hiyo haitoshi Wenye mali, bado biblia inawapa nafasi ndogo sana ya kuurithi ufalme wa mbinguni;

Mathayo 19:23 “Yesu akawaambia wanafunzi wake, Amin, nawaambieni, ya kwamba itakuwa shida tajiri kuingia katika ufalme wa mbinguni.

24 Nawaambia tena, Ni rahisi zaidi ngamia kupenya tundu ya sindano, kuliko tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu”.

Vifungu vipo vingi sana kwenye biblia vinavyozungumzia hatari za kupenda fedha., hatuwezi kuviweka vyote hapa, lakini kwa hivyo vichache  kama na wewe ni mmojawapo, basi geuka haraka sana, uridhike na vile Mungu anavyokupa, kwasababu biblia inasema..

Mhubiri 5:10 “Apendaye fedha hatashiba fedha, Wala apendaye wingi hatashiba maongeo. Hayo pia ni ubatili”.

Na pia inasema.

Zaburi 37:16 “Kidogo alicho nacho mwenye haki ni bora Kuliko wingi wa mali wa wasio haki wengi”.

Chuma kidogo kidogo utafanikiwa..

Mithali 13:11 “Mali iliyopatikana kwa haraka itapunguka; Bali yeye achumaye kidogo kidogo atazidishiwa”.

Lakini kama wewe hujaokoka, ukweli ni kwamba hii roho ya kupenda fedha haiwezi kuondoka ndani yako, hata iweje,  itaondoka, ikiwa tu utamruhusu Bwana Yesu aingie ndani yako aibadilishe Nia yako..

Akishakubadilisha hapo ndipo  Roho ya kuridhika na ya utulivu itaingia ndani yako, na hapo hapo Mungu ataanza kukufundisha njia sahihi na yenye Baraka ya kukusanya..mpaka mwisho wa siku atakufikisha pale anapotaka uwepo. Na zaidi ya yote utaurithi uzima wa milele.

Hivyo kama upo tayari leo hii kutubu dhambi zako, unahitaji kuokoka, uamuzi huo utakuwa ni wa busara sana basi, fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

UNAWAFAHAMU MANABII WA UONGO?

USIPOWATAMBUA YANE NA YAMBRE, KATIKA KANISA LA KRISTO, UJUE UMEPOTEA.

YONA: Mlango 1

UNYAKUO.

UTAWALA WA MIAKA 1000.

EPUKA MUHURI WA SHETANI

Rudi Nyumbani:

Print this post

Mshulami ni msichana gani?

Mshulami ni jina Sulemani alilompa msichana ambaye alikuwa naye katika mahusiano kama tunavyosoma katika kitabu cha wimbo ulio bora, alimwita hivyo kutokana na kuwa eneo alilotokea lilitwa  Shulami,

Wimbo 6:13 “Rudi, rudi, Mshulami, Rudi, rudi, ili sisi tukutazame. Kwani mnataka kumtazama Mshulami, kama kutazama ngoma ya Mahanaimu?


Fahamu zaidi:

Je unajua ni kwa nini Mariamu aliitwa Mariamu magdalene? >>> Mariamu Magdalene

Mlima Sinai upo nchi gani? >> Mlima sinai

Mti wa mlozi ni mti gani>>>> Fimbo ya haruni -mti wa mlozi

Kwanini Yesu alisema wacheni wafu wazike wafu wao? >>> Wafu wazike wafu wao

Amin, Amin, nawaambia kizazi hiki hakitapita >>> Kizazi hiki hakitapita,

Mitume wa Yesu walikufaje >>> Vifo vya mitume wa Yesu

Rudi Nyumbani:

Print this post

HIZI NI NYAKATI ZA KUJIINGIZA KWA NGUVU.

Luka 16:16 “Torati na manabii vilikuwapo mpaka Yohana; tangu wakati huo habari njema ya ufalme wa Mungu hutangazwa, na kila mtu hujiingiza kwa nguvu”.

Nataka uone hicho kifungu cha mwisho, “ Na kila mtu hujiingiza kwa nguvu”..

Bwana Yesu alipotoa habari hiyo, kulikuwa na sababu kubwa kwanini alianza kwanza na habari za agano la kale(Torati na manabii) kisha akaja kwenye agano jipya, na kumalizia kwa kusema, tangu huo wakati kila mtu atakawa anajiingiza kwa nguvu.

Alisema hivyo kuonesha kuwa hapo kabla, kulikuwa hakuhitaji bidii yoyote, au jasho lolote, au nguvu yoyote, kuijua torati, lakini kuanzia wakati wa Yohana, injili ya kweli ambayo inaleta ondoleo la dhambi, ilipoanza kuhubiriwa, injili ya kumfanya mtu awe na maarifa kamili kumuhusu Mungu ilipoanza kuhubiri, injili inayomfungua mtu kweli kweli, basi vipingamizi vikubwa sana vitanyanyuka kiasi kwamba, mpaka mtu aipate ni lazima atumie nguvu nyingi sana kuingia, tofauti na ilivyokuwa hapo mwanzo.

Kwamfano utaona wakati ule tu, kulikuwa na mafarisayo na waandishi, ambao wamesimama hapo, katikati kuhakikisha kuwa mtu yeyote atakayemkiri Yesu hadharani, moja kwa moja atatengwa na sinagogi, (Yohana 9:22)

Na kutengwa kwa zamani sio kama sasa, zamani ukitengwa na sinagogi ni jamii nzima ya Israeli imekutenga mpaka familia yako. Hata misaada ya kijamii ulikuwa hupati, Hivyo suala la kutengwa lilikuwa ni jambo zito sana.

Hivyo haikuwa ni rahisi, hata kidogo, ilibidi watu walazimishe, mambo kwa nguvu, wawe radhi kutengwa tu, wawe tayari kupoteza mahusiano yao tu, lakini wasiukose ufalme wa mbinguni.

Mambo hayo hayo hata sasa, yanaendelea, kuupata ufalme wa mbinguni, ni kujiingiza kwa nguvu nyingi, wapo viongozi wako wa dini wanakuzuia usiokoke, kisa tu imani yao haimini kile biblia inachosema, pengine Imani yao inafundisha kusujudia sanamu, haiamini katika karama za Roho, ndugu usiwaangalie hao, wewe jiingize kwa nguvu katika ufalme wa Mungu,.

Hao ni wale wana-sheria wa dini, ambao Bwana Yesu anasema, kazi yao ni kusimama pale mlango kushikilia funguo, kuwazuia watu wasiingie, na wao wenyewe hawauingii, wanataka mkae wote katika giza la milele pamoja..

Luka 11:52 “Ole wenu, enyi wana-sheria, kwa kuwa mmeuondoa ufunguo wa maarifa; wenyewe hamkuingia, na wale waliokuwa wakiingia mmewazuia”.

Hivyo usiwaangalie hao hata kidogo, achana na mapokeo ya dini, tubu dhambi uokoke, tafuta ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi (Yohana 3:23), na kwa jina la YESU KRISTO sawasawa na Matendo 2:38, na sio ule wa kunyunyiziwa ambao haupo katika maandiko.

Jiingize kwa nguvu, hata kama ndugu zako hawakuelewi, Jiingize kwa nguvu hata kama marafiki zako watakuona mshamba, jipenyeze kwa nguvu hata kama dunia itakuona umerukwa na akili..Iokoe roho yako, wakati huu jiepushe na mtu ambaye unaona kabisa anaizuia njia yako ya wokovu.

Wenyewe hawawezi kuona hilo, kwasababu bado wapo gizani, lakini wewe umeiona nuru, usijifananishe na wao, zidi jenga uhusiano wako binafsi ya Yesu. Hizi ni nyakati za mwisho na unyakuo upo karibu sana,

Mathayo 11:12 “Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatikana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka.

13 Kwa maana manabii wote na torati walitabiri mpaka wakati wa Yohana”.

Isiishi kwa kuwapendezesha watu na huku umelisahau Neno, kwasababu kila mtu atalibeba furushi lake mwenyewe (Wagalatia 6:5). Dakika hizi za majeruhi, zinafananishwa na Sodoma na Gomora, ambazo tunajua ni watu 3 tu kati ya mamilioni waliokuwa katika miji ile ndio waliopona….Ndivyo itakavyokuwa siku hizi, litavuka kundi dogo tu, lililoweza kujiingiza kwa nguvu katika ufalme wa mbinguni bila kujali vizuizi vya mpito vya ibilisi.

Unadhani shetani, hajui kuwa mtu akiupata ufalme wa Mungu, amepata kitu cha thamani kubwa sana, anajua hilo, na ndio maana lazima akuletee ugumu ili usijaribu kuuingia, ubakie kwenye giza huko huko..Hivyo vitisho kutoka kwa viongozi wako wa dini na ndugu na marafiki, visikufanye usichukue uamuzi wa kumpokea Yesu.

Mathayo 10:34 “Msidhani ya kuwa nimekuja kuleta amani duniani; la! Sikuja kuleta amani, bali upanga.

35 Kwa maana nalikuja kumfitini mtu na babaye, na binti na mamaye, na mkwe na mkwe mtu;

36 na adui za mtu ni wale wa nyumbani mwake.

37 Apendaye baba au mama kuliko mimi, hanistahili; wala apendaye mwana au binti kuliko mimi, hanistahili.

38 Wala mtu asiyechukua msalaba wake akanifuata, hanistahili.

39 Mwenye kuiona nafsi yake ataipoteza; naye mwenye kuipoteza nafsi yake kwa ajili yangu ataiona”.

Kama bado hujafanya uamuzi huo basi anza sasahivi, wokovu unapatikana bure, lakini si rahisi si rahisi lakini inahitaji nguvu kujiingiza kwa huo, hivyo jiingize kwa nguvu bila kujali, na huko huko Bwana Yesu atajifunua kwako kwa namna ambayo hukuwahi kumjua hapo kabla, ndipo utakapomjua Mungu, na ndipo atakapotembea na wewe.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

USIUZE URITHI WAKO.

Je! Kiongozi wa dini anaouwezo wa kusamehe dhambi?

KANUNI RAHISI YA KUFANIKIWA.

JIHADHARI NA KUOSHWA MIGUU ISIVYOPASWA.

MWANANCHI WA UFALME WA MBINGUNI

USIISHI BILA KUIFANYA KAZI YA MUNGU KABISA..

Rudi Nyumbani:

Print this post

JUKUMU LA MUHIMU LINALOKWEPWA NA WENGI.

Jukumu moja na kuu tulilonalo sisi ni KUMJUA SANA YESU KRISTO. Wengi wanalikwepa jukumu hili. Na Zaidi wanapenda sana kutafuta kuwajua watumishi wa Yesu kuliko ya Yesu mwenyewe.

Waefeso 4:13 “hata na sisi sote tutakapoufikia umoja wa imani NA KUMFAHAMU SANA MWANA WA MUNGU, hata kuwa mtu mkamilifu, hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo”.

Jitathmini ukiona kuna mahali unamjua mtumishi, zaidi ya Bwana wake mwenyewe ambaye ni Yesu, basi kuna tatizo mahali na pia una laana.(1Wakorintho 16:22)

Kama mtumishi wa Kristo akizungumziwa vibaya inakuuma Zaidi ya Yesu akifanyiwa mzaha, basi kuna tatizo katika uhusiano wako na Yesu.

Kama comedy za kumtania Mwokozi Yesu hazikuhuzunishi sana kama za kumtania  mchungaji wako, au mwalimu wako, basi kuna tatizo mahali.

Kama unakuwa mkali dini yako inapozungumziwa vibaya, au dhehebu lako au mwalimu wako anayekufundisha Neno la Mungu kanisani, na wakati huo huo unakutana na comedy inayomkebehi Kristo waziwazi na wala haikuhumizi  sana Zaidi inakuchekesha!, hebu jitafakari tena, inawezekana humjui kabisa Yesu, wala hayupo maishani mwako.

Kama Maisha yako ya binafsi ya siri, hujawahi kukaa ukazungumza  na mwokozi wala kumshukuru, basi kuna shida.

Dada/kaka usitumie nguvu nyingi kutafuta kumpendeza mtumishi, wala usiwe mshabiki wa dini, wala usiwe mshabiki wa mtumishi wa Mungu.

Tafuta kumjua Yesu, na kumjua Yesu sio kuhama na kubadilisha kanisa…Ni hapo hapo ulipo tu!..Unachopaswa kukifanya baada ya kumpokea Kristo ni kukinunua kitabu kinachoitwa Biblia. Usitegemee ile ya ku-download kwenye simu yako.. Ya kudownload ni nzuri baada ya kuwa na ya KITABU chenye kurasa za karatasi.

Hivyo kinunue hichi kitabu kinachoitwa Biblia. Ukishakipata! Anza kukisoma mwenyewe!..Mungu kakupa macho, kakupa na uwezo wa kusoma, hawezi kukunyima uwezo wa kuelewa!..

Kinachosababisha wengi wasiielewe biblia ni kusoma kwa kutimiza wajibu tu!..na sio kwa kutoka ndani ya mioyo yao, wanasoma tu kwasababu wameambiwa wasome, au kwasababu tu wanahisi ndio wanampendeza Mungu, na anasoma kwa mwezi mara moja…Hivyo biblia inakuwa ni kitabu kigumu sana kwao kukielewa. Na pia wanasoma mstari mmoja kisha wanarukia mwingine…Hawapendi kusoma mwanzo wa kitabu hadi mwisho.

Hivyo soma biblia mwenyewe kwa macho yako mawili. Ukikutana na jambo gumu kuna nguvu Fulani ya asili ambayo Mungu kaiweka ndani yetu itakayokupeleka katika kuutafuta ukweli Zaidi, hapo ndipo kitakuja kitu cha kutafuta msaada Zaidi kwa mahubiri ya watumishi wa Mungu, utaona kuna kitu kinakusukuma kwenda sehemu Fulani labda kanisa Fulani, au kwenye semina Fulani, au katika mahubiri Fulani.. ambapo utaona utapata majibu ya maswali yako, au utakwenda kusoma jumbe Fulani ambazo utaona zitakufaidisha roho  yako. Na kwa njia hiyo ndipo mafunuo ya Roho yanapokuja.

Lakini huwezi kusema naondoka kanisa hili nihamia lile kama hujapata sababu yoyote ya kimaandiko ya kufanya hivyo.. Wengi wanahama kanisa kwasababu tu wameambiwa ukweli..hivyo ule ukweli unawauma na kuishia kuhama, wengine kwasababu wamesikia wakisengenywa, wengine kwasababu wameona kanisani kumepungua watu hivyo na wao wanaondoka…mambo ambayo hayana mashiko kabisa!..Mtu wa namna hiyo hajaongozwa na Mungu, bali kafuata akili zake mwenyewe.

Lakini mtu wa kweli ambaye anaongozwa na Roho, huwa anaondoka sehemu moja hadi nyingine, ni kwasababu anatafuta uelewa wa maandiko Zaidi, anatamani kumjua Yesu zaidi na kukua kiroho.. huyo ndiye anayeongozwa na Roho. Anaona kuna umuhimu wa kutafuta kujifunza Neno Zaidi, kutafuta kufunga Zaidi na kusali. Na si kwasababu kasikia kasengenywa, au kasemwa, au kaudhiwa.

Hivyo siku zote usilisahau hili ndugu yangu mpendwa.. MJUE SANA YESU. Huyo ndiye Mkuu wa Uzima, na ndiye mwenye funguo za Uzima,  na ndiye aliyekabidhiwa mamlaka yote ya mbinguni na Duniani.. Tunavyozungumza sasa yupo anaishi! Na atarudi tena kulichukua kanisa lake, Ana nguvu nyingi sana, yeye hadhihakiwi sio yule unayemwona kwenye picha, sio unayemwona kwenye Tv, Yesu ni Mungu, akijifunua kwetu kikamilifu, hata hapa duniani tunaweza tusitamani kuendelea kuishi, Hivyo tumjue yeye kila siku, tujinyenyekeze mbele zake, ajifunue kwetu zaidi na zaidi. Anatamani kujifunua kwetu sana, ni sisi tu.

Bwana atubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

JE UDHAIFU WANGU UNAWEZA KUZUIA INJILI?

Kuna haja gani ya kumwamini Yesu aliyezaliwa kama sisi?

WINGU KUBWA LA MASHAHIDI.

WANA JUHUDI KWA AJILI YA MUNGU, LAKINI SI KATIKA MAARIFA.

MWISHO WA HAO WAMSAHAUO MUNGU.

RUDIA, TENA NA TENA KUMWOMBA MUNGU USIKATE TAMAA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

KUZALIWA KWA YESU.

kuzaliwa kwa Yesu kulikuwaje?


Mathayo 1:18 “Kuzaliwa kwake Yesu Kristo kulikuwa hivi. Mariamu mama yake alipokuwa ameposwa na Yusufu, kabla hawajakaribiana, alionekana ana mimba kwa uweza wa Roho Mtakatifu.

19 Naye Yusufu, mumewe, kwa vile alivyokuwa mtu wa haki, asitake kumwaibisha, aliazimu kumwacha kwa siri.

20 Basi alipokuwa akifikiri hayo, tazama, malaika wa Bwana alimtokea katika ndoto, akisema, Yusufu, mwana wa Daudi, usihofu kumchukua Mariamu mkeo, maana mimba yake ni kwa uweza wa Roho Mtakatifu.

21 Naye atazaa mwana, nawe utamwita jina lake Yesu, maana, yeye ndiye atakayewaokoa watu wake na dhambi zao.

22 Hayo yote yamekuwa, ili litimie neno lililonenwa na Bwana kwa ujumbe wa nabii akisema,

23 Tazama, bikira atachukua mimba, Naye atazaa mwana; Nao watamwita jina lake Imanueli; Yaani, Mungu pamoja nasi.

24 Naye Yusufu alipoamka katika usingizi, alifanya kama malaika wa Bwana alivyomwagiza; akamchukua mkewe;

25 asimjue kamwe hata alipomzaa mwanawe; akamwita jina lake YESU”.

Yesu mwokozi, kama si kuzaliwa kwake ulimwenguni, leo hii tungekuwa wapi? Kama sio kuimwaga neema yake duniani, tungepatia wapi ondoleo la dhambi?

Mamajusi walitoka nchi ya mbali, kwa furaha tu ya kumwona mwokozi wa Ulimwengu, ambaye hata hakuzaliwa katika nchi yao..lakini kwa kuiona tu nyota yake, hawakusubiri, wahadithiwe, walianza safari..

Lakini Swali la kujiuliza Je! Na wewe amezaliwa moyoni mwako?

Bwana Yesu lipoanza kuitenda kazi ambayo Baba yake amemtumia alisimama na kusema maneno haya..

Luka 4:18 “Roho wa Bwana yu juu yangu, Kwa maana amenitia mafuta kuwahubiri maskini habari njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao, Na vipofu kupata kuona tena, Kuwaacha huru waliosetwa,

19 Na kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa”.

Hiyo ni kazi kubwa ambayo ilimleta duniani, na ndio maana mwishoni kabisa mwa kitabu cha Ufunuo alisema hivi..

Ufunuo 21:6 “Mimi ni Alfa na Omega, Mwanzo na Mwisho. Mimi nitampa yeye mwenye kiu, ya chemchemi ya maji ya uzima, bure”.

Hivyo mpe leo Yesu maisha yako, ayaokoe, akufanye kuwa kiumbe kipya. Hizi ni siku za mwisho, Yesu yupo mlangoni kurudi.Dalili zote zinaonyesha, kuwa mimi na wewe tunaweza kushuhudia tukio la Unyakuo.

Bwana atusaidie sana.

Shalom.

Ikiwa utapenda mafundisho ya biblia yawe yanakufikia kwa njia ya whatsapp, basi tutumie ujumbe kwa namba hii: +255789001312

Mada Nyinginezo:

KWANINI YESU KRISTO ALIKUJA DUNIANI?

JIFUNZE NENO LA MUNGU KWA BIDII ZOTE.

EPUKA MUHURI WA SHETANI

https://wingulamashahidi.org/2018/07/19/nyakati-saba-za-kanisa-na-wajumbe-wake/

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Kuhutubu ni nini?

Rudi Nyumbani:

Print this post

USHIRIKINA NA MADHARA YAKE.

Ushirikina na madhara yake, rohoni ni yapi?


Ushirikina ni kitendo cha kwenda kutafuta msaada wa kiroho au wa kimwili katika mamlaka ya giza. Nikisema mamlaka ya giza namaanisha kwa shetani na mapepo na majini yake yote yanayofanya kazi kupitia watu wanaoitwa waganga au wachawi.

Sasa unapoumwa, halafu badala ya kwenda kuwa Mungu upate msaada, wewe unakimbilia kwa waganga wa kienyeji ili upate msaada ya kiganga, hapo moja kwa moja tayari umeshashirikiana na mashetani katika ulimwengu wa roho.

Au unapopitia matatizo Fulani aidha ya kifamilia, au ya kikazi, au unahaja ya jambo Fulani pengine masomo, au ndoa, au cheo, halafu wewe moja kwa moja unakimbilia kwa mganga akusaidie kutatua tatizo lako, ujue kuwa tayari umeshaingizwa katika mtandao wa Mashetani.

Jambo ambalo wengi hawajui ni kuwa, walau kwa mtu wa kawaida yeyote, kunakuwa na ka-ulinzi Fulani kutoka kwa Mungu, ambacho anazaliwa nacho hicho kanamfanya shetani asiweze kujiamulia tu jambo lolote atakalo juu ya huyo mtu, vinginevyo ungekuwa shetani kashawamaliza watu wote duniani, kwa kuwaua, Ndio ni kweli ataweza baadhi  lakini sio yote. Sasa pale mtu anapokwenda kwa shetani mwenyewe kumwomba msaada, maana yake ni  kuwa anasaini naye mkataba rasmi kuwa kuanzia sasa, huy mtu ni wangu na naweza kufanya jambo lolote juu yake.

Haya ndio madhara ya moja kwa moja ya ushirikina.

  1. Unaingiliwa na mapepo:

Angalia vizuri utaona asilimia kubwa ya watu wanaoudhuria kwa waganga wanakuwa wanasumbuliwa na nguvu za giza, au wengine wanapata ulemavu Fulani ambao hapo kabla hawakuwa nao, au ugonjwa Fulani, ambao hauponi, hiyo yote ni kutokana na mtu kujishughulisha na ushirikina.

  1. Unakuwa hatarini kufa:

Kutokana na kuwa tayari umeshajihalalisha kwa shetani, basi shetani kazi yake kubwa iliyobakiwa nayo kwako ni kukuua,..Kwasababu ndio dhumuni lake hapa duniani, kuua biblia inasema hivyo…

Yohana 8:44 “Ninyi ni wa baba yenu, Ibilisi, na tamaa za baba yenu ndizo mpendazo kuzitenda. Yeye alikuwa mwuaji tangu mwanzo; wala hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake”.

  1. Chochote unachokifanya hutafanikiwa:

Hata kama kitaonekana kukuletea matokeo mazuri kiasi gani mwanzoni, kumbuka hiyo ni gia tu ya shetani kukuvuta kwake, ili usimwache, lakini katika kipindi cha muda mrefu, hakitakufikisha popote, kama ulikuwa umekwenda kutafuta mali, hizo mali zitapotea tu baada ya kipindi Fulani, kama ulikuwa umekwenda kutafuta kazi, hiyo kama unaweza usiipate, na hata ukiipata haitadumu, utakuwa ni mtu ambaye anafanya jambo lakini baada ya muda mrefu haoni faida ya jambo hilo, au haoni maendeleo yoyote. Na mwisho wa siku unajikuta ni heri usingeenda.

Mithali 11:21 “Hakika, mtu mwovu hatakosa adhabu; Bali wazao wa wenye haki wataokoka”.

Ayubu  21:13 “Siku zao hutumia katika kufanikiwa, Kisha hushuka kuzimuni ghafula”.

  1. Unapoteza Utu na uwezo wa kupambanua mambo ya rohoni:

Kumbuka pale unapokwenda kwa waganga, ni unaonyesha kuwa humuhitaji Roho Mtakatifu kukusaidia, na kazi ya Roho Mtakatifu ni kuwavuta watu kwa Mungu, na kuwapa macho ya rohoni, Hivyo unapojihusisha na ushirikina na uchawi, ni kuwa unapoteza huo uwezo, na matokeo yake unakufa kiroho.. Hapo ndipo unaanza kufanya hata yale mambo ambayo mwanadamu wa kawaida hawezi kufanya,..Hayo unaweza usiyaone leo, lakini kwa jinsi siku zitakavyozidi kwenda mabadiliko hayo utayaona, kwasababu nguvu za giza wakati huo zitakuwa zinakutawala.

2Wakorintho 4:4 “ambao ndani yao mungu wa dunia hii amepofusha fikira zao wasioamini, isiwazukie nuru ya injili ya utukufu wake Kristo aliye sura yake Mungu”.

 

  1. Ukifa unakwenda motoni.

Washirikina wote, wachawi wote, biblia inasema sehemu yao ni katika lile ziwa la moto. Ukifa leo na upo katika hali hiyo , basi ni moto wa milele unakuongoja.

Ufunuo 21:8 “Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili”.

 

Sasa kwanini hayo yote yakukute?

Lakini Habari njema ni kuwa, hata kama umeingia huko, bado unayo nafasi ya kutengenezwa upya. Na anayeweza kufanya hivyo, si mwingine zaidi ya YESU KRISTO tu peke yake..Huyo ndiye aliyetiwa mafuta na Mungu, ili kuwatoa watu katika vifungo vya giza, mwingine yeyote hawezi….

Isaya 61:1 Roho ya Bwana MUNGU i juu yangu; kwa sababu Bwana amenitia mafuta niwahubiri wanyenyekevu habari njema; amenituma ili kuwaganga waliovunjika moyo, kuwatangazia mateka uhuru wao, na hao waliofungwa habari za kufunguliwa kwao.

Hivyo kama ulishaingia humo, au bado hujaingia, lakini Kristo bado hayupo ndani yako, basi leo hii fanya uamuzi huo, wa kumkaribisha ndani yako ayaokoe maisha yako moja kwa moja, haijalishi wewe ni muislamu, Yesu anawaokoa wote, wanaomkimbilia yeye kwa moyo wa dhati.

Akikuweka huru, amekuweka huru kweli kweli, haachi hata alama ya uovu ndani yako, akikusamehe amekusamehe kweli kweli, kana kwamba hukuwahi kumkosea, kwa lolote. Atakufungua kutoka katika malango hayo ya mauti ya ibilisi yaliyokufunga, na kukuletea katika ufalme wa wana wa Mungu. Roho Mtakatifu akiingia ndani yako, hakuna pepo lolote litakaloweza kukaa ndani yako, Ukimkaribisha leo hii atakufanya huru, na kuna amani itaingia ndani mwako, ambayo utashangaa imetoka wapi..Huyo ndio Yesu mwokozi.

Hivyo kama upo tayari leo hii kutubu dhambi zako kwa kumaanisha kabisa kuacha, na kusema kuanzia sasa namfuata Yesu, sitaki ushirikina, sitaki dhambi, Namfanya Yesu kuwa kiongozi wa maisha yangu basi uamuzi huo ni mzuri na wa busara, basi, fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala fupi ya Toba..>>>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Ubarikiwe sana.

Mada Nyinginezo:

NINI KINATOKEA BAADA YA KIFO?

EPUKA MUHURI WA SHETANI

JINSI WATU WANAVYOZAMA KATIKA USHIRIKINA NA UCHAWI.

NIKUPE WEWE URITHI WA BABA ZANGU?

MAONO YA NABII AMOSI.

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

DUNIA HII ITAHARIBIWA KABISA.

Isaya 24:3 “Dunia hii itafanywa tupu kabisa, na kuharibiwa kabisa; maana Bwana amenena neno hilo.

4 Dunia inaomboleza, inazimia; ulimwengu unadhoofika, unazimia; watu wakuu wa dunia wanadhoofika.

5 Tena dunia imetiwa unajisi kwa watu wanaoikaa; kwa maana wameziasi sheria, wameibadili amri, wamelivunja agano la milele.

6 Ndiyo sababu laana imeila dunia hii, na hao wanaoikaa wameonekana kuwa na hatia, ndiyo sababu watu wanaoikaa dunia wameteketea, watu waliosalia wakawa wachache tu”.

Nabii Isaya alipotabiri juu ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo na bikira (Isaya 7:14), miaka 700 kabla ya Masihi kuja duniani, wapo watu pengine walioona kuwa hizo ni hadithi tu za kufikirikika… Alipotabiri tena juu ya mateso yake yatakayoompata (Isaya 53), nazo pia zikaonekana pengine ni habari tu, lakini wakati ulipofika, hayo yote kutimia kwa ufasaha wote, ndipo wakajua kuwa Neno la Mungu huwa halipiti.

Isaya huyo huyo aliyetabiri ujio wa Kristo kwa uvuvio wa Roho, ni huyu huyu alioonyeshwa pia hatma ya huu ulimwengu utakavyokuja kuwa siku za mwisho, na habari zake kaziandika sehemu nyingi sana kwenye kitabu hicho chenye sura 66, alionyeshwa jinsi hii dunia itakavyokwenda kuwa utupu, na kuharibiwa kabisa, jinsi jua litakavyotiwa giza, jinsi watu watakavyoadimika kama dhahabu duniani, na kibaya zaidi alionyeshwa fedha ya mtu wakati huo haitafanya kazi yoyote, umaarufu wa mtu utakuwa hauna maana, biashara za mtu zitakuwa ni kama takatakata, elimu ya mtu haitafanya kazi..tajiri na maskini wote watakuwa wakiomboleza sawa.

Na nyakati zenyewe ndio hizi tunazoishi mimi na wewe, kila mtu analijua hilo, hata ukimuuliza mtoto mdogo atakuambia, hizi ni nyakati za mwisho, watu wengi wanaposikia maneno haya wanapuuzia wakidhani hichi ni kama kile kipindi cha mitume..Ndugu hichi sio kipindi cha mitume.. Fuatilia mambo yanayoendelea duniani hata kupitia mitandao ndipo utakapojua kuwa tunaishi nyakati nyingine.

Bwana Yesu alisema hivi..

“Basi kwa mtini jifunzeni mfano; tawi lake likiisha kuchipuka na kuchanua majani, mwatambua ya kuwa wakati wa mavuno u karibu;

33 nanyi kadhalika, myaonapo hayo yote, tambueni ya kuwa yu karibu, milangoni.

34 Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia” (Mathayo 24:32).

Sasa kama wewe ni msomaji wa Biblia utajua kuwa Mtini unafananishwa na Taifa la Israeli (Yeremia 24), na wakati ule Israeli ilikuwa bado haijachipua (yaani haijawa taifa), ilipitia miaka zaidi ya 2,500 tangu wachukuliwe utumwani Babiloni, na ulipofika mwaka 1948, Israeli ikachipuka tena na kuwa taifa kwa mara ya kwanza,..Na tunajua kabisa agenda ya Mungu ya wokovu itamalizia tena na Israeli pale Yerusalemu.

Hivyo tangu huo wakati Bwana alisema kizazi hiko, (yaani kilichoshuhudia Israeli kuchupuka tena), hakitapita mpaka hayo yote, kutimia,..Mambo yote aliyoyazungumzia katika Mathayo 24, hadi kurudi kwa pili kwake,..Na kizazi huwa hakizidigi miaka 120, sasa piga hesabu hapo, tunaishi katika wakati gani.. (Hatujui siku wala saa lakini tunayajua majira).

Sikuzote, kiwango chako cha maarifa kuhusu Mungu, ndio kinachoelezea maisha ya kiroho unayoishi sasa hivi, kama jicho lako bado halioni kuwa tunaishi katika majira ya unyakuo, na kwamba huu ndio ule wakati ambapo watu watadhanishia mbona ni amani, na salama, na kumbe ule uharibifu unakuja kwa ghafla (1Wathesalonike 5:3)..Kama ilivyokuja Corona kwa ghafulani pasipo ulimwengu kujiandaa…Ndicho kitakachoitokea dunia kipindi sio kirefu.

Sijui kama hilo unalijua ndugu yangu, kanisa hili linaitwa Laodikia, (Sio dhehebu linaloitwa Laodikia! Hapana!..Bali ni hali ya kanisa kwa ujumla inayofananishwa na Kanisa la Laodikia la Nyakati za kwanza, kasome Ufunuo 3:14), na ndio kanisa la mwisho la 7, na hakutakuwa na kanisa lingine baada ya hili, niambie ni dalili ipi ambayo haijatimia Yesu aliyoirodhesha kwenye Mathayo 24.

Internet imeweza kurahisisha mambo, siku hizi haihitaji mtu aende tena kwenye mikutano ya Injili asikie mahubiri, pale pale alipo hata kama ni kijijini akiwa chumbani mwake Injili inamfikia, utasema Injili haijahubiriwa dunia nzima leo?..

Shetani anataka watu waendelee kufikiria hivyo hivyo, kwamba bado sana, anataka watu waangalie upepo wa dunia unavyokwenda, lakini wasiangalie biblia inasema nini kuhusu siku hizi. Usipokuwa mvivu kusoma biblia ndipo utakapojua ni kwa jinsi gani tunaishi katika nyakati za hatari kushinda zote ambazo zilishawahi kupita katika historia.

Hivyo huu ni wakati wa kuamka usingizini..

Waefeso 5:14 “Hivyo husema, Amka, wewe usinziaye, Ufufuke katika wafu, Na Kristo atakuangaza”.

Kama bado hujaokoka, au umeokoka lakini bado mguu mmoja nje mwingine ndani, Embu anza, kuyaangalia upya maisha yako ya rohoni ndugu, Je! Yesu amekuokoa kweli kweli? Kama sio, basi huu ndio wakati, na sio kesho, unachopaswa kufanya ni kuamua kutubu dhambi zako kwa kumaanisha kuziacha na kutozifanya tena, na kisha kwenda kubatizwa katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji tele (Yohana 3:23), na kwa jina la YESU KRISTO sawasawa na Matendo 3:38,8:16 na 10:48 Upate ondoleo la dhambi zako.(Maagizo hayo ni muhimu sana!). Na Roho Mtakatifu atakuongoza katika kuyaelewa maandiko.

Na kuanzia hapo, anza kuishi maisha ya kama mtu unayemngojea Bwana Yesu kwasababu nyakati hizi, sio za kubembeelezewa wokovu tena, ni kubutuka haraka na kuishindania Imani.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

KUOTA UNAKOJOA KITANDANI.

MAMBO MENGINE HAYATOKI ISIPOKUWA KWA KUFUNGA.

NI WAKATI WA KUJIPIMA, WEWE KAMA MTUMISHI WA MUNGU!

NA MTU MMOJA AKAVUTA UPINDE KWA KUBAHATISHA, AKAMPIGA MFALME

MISTARI YA BIBLIA YA UPONYAJI.

MANA ILIYOSHUSHWA KUTOKA MBINGUNI.

Rudi Nyumbani:

Print this post